Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live

BAADA ya Taarifa Kuwa Nyingi Juu ya Kujiunga na Simba..Ngoma Aibuka na Kufunguka Haya..!!!

0
0

Mshambuliaji nyota wa Yanga, Donald Ngoma ambaye sasa ni majeruhi amesema kuwa hana mpango wa kujiunga na klabu ya Simba mara mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa mwezi ujao.

Ngoma alisema hayo baada ya kuwepo uvumi jijini Dar es Salaam na kwenye mitandao kuwa kutoonekana katika kikosi cha timu hiyo kumetokana na mkakati wake wa kujiunga na wapinzani wa jadi wa klabu yake ya sasa.

Alisema kuwa kuwapo kwake nje kumetokana na kuumia na si vinginevyo na wala hana mgomo wa kuichezea timu hiyo kama inavyosambazwa na watu mbalimbali.

“Yapo mengi yamesemwa kuhusu mimi, mengi siyo kweli, kazi yangu ni mpira na mchezaji yeyote huwa anapenda kucheza na wala si kukaa benchi.

“Naomba nisihusishwe na Simba au timu yoyote, bado ni mchezaji halali wa Yanga, naheshimu mkataba,” alisema Ngoma.

Alifafanua kuwa uongozi wa klabu hiyo (Yanga) umempa ruhusa ya kupumzika na wala hajatoroka kwenda Afrika Kusini kutafuta timu zaidi ya kufuata matibabu ya kisasa.

Mchezaji huyo kutoka Zimbabwe alisema kuwa hadi sasa hajasaini mkataba mpya na klabu hiyo pamoja na kuwa tayari kufanya hivyo endapo watakubaliana na masharti yake.

“Siwezi kusema kama nitaondoka au la, itategemea uamuzi ya wakati huo na hasa ule wa uongozi, kwa sasa nimepata nafuu na nitaanza mazoezi karibuni,” alisema.     

MECK Sadick Afunguka Mengine Juu ya Kujiuzulu Kwake..Adai Huwa Hapendi Kukwamisha Katika Kazi Zake..!!!

0
0

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Meck Sadick ambaye jana Rais Magufuli amekubali ombi lake la kujiuzulu katika nafasi yake hiyo amefunguka na kusema katika maisha yake anaumizwa sana pale anapotaka kufanya jambo lakini akakwamishwa na mtu.

Meck Sadick anasema hawezi kuweka wazi sababu kubwa iliyopelekea yeye kuomba kuacha kazi hiyo kwani tayari alishazisema kwa Rais Magufuli ambaye ameamua kukubaliana naye na sasa anasema haitaji kuajiriwa na mtu bali atarudi kwao Usukumani kulima. 

"Sababu za kuacha kazi anazijua Rais niliyemuomba, siwezi kumtangazia kila mtu hili, ila changamoto kubwa ni pale unapotaka kitu fulani kifanyike na hakifanyiki kwa hiyo hiki ni kitu kinachotuumiza sana viongozi kwa mfano utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi na wananchi wana matarajio kwamba itakapofika 2020 serikali ya CCM itakuwa imefanya moja, mbili, tatu nne sasa yasipofikia hayo ni changamoto kwa kweli kubwa kwa hiyo ndiyo changamoto naweza kusema zinakwamisha maendeleo yetu" alisema Meck Sadick 

Mbali na hilo Meck Sadick anasema saizi anarudi Usukumani kulima

"Mimi kazi nayoifahamu ni kilimo ukiachilia mbali hii kazi ya Utawala na kilimo tu kwa hiyo saizi mimi narudi usukumani kwenda kulima, sitegemei kuajiriwa na mtu tena mimi nakwenda kufanya shughuli za kilimo sababu ndiyo nina uzoefu nayo" alisema Meck Sadick 

UTATA Watawala Majaji na Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro Kujiuzulu..Lissu Afunguka Mazito Juu ya Sakata Hilo..!!!

0
0

WAKATI Rais John Magufuli jana akitangaza kuridhia maombi ya kuacha kazi kwa majaji wawili na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Meck Sadiki, wadau wa sheria wamesema huenda kashfa ya Escrow na dawa za kulevya vinahusika na uamuzi huo.

Ikulu kupitia taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi ilitoa taarifa jana asubuhi ikieleza kuwa pamoja na Sadiki, Rais aliridhia maombi ya kuacha kazi kwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria, Aloysius Mujulizi na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Upendo Msuya, kuanzia Mei 15.

Baada ya habari za kuacha kazi kwa viongozi hao, mijadala ilitawala katika mitandao ya kijamii huku baadhi yao ikihusisha kuacha kazi kwa Jaji Mujulizi kuwa ni kutokana na kuhusishwa na sakata la Escrow ambapo alitajwa miongoni mwa majaji walionufaika kwa kupata mgao.

Kwa mujibu wa ripoti ya Bunge kuhusu sakata la Escrow, Jaji huyo alitajwa kupokea rushwa kwa mmoja wa wamiliki wa kampuni ya IPTL inayoliuzia umeme Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco).

Wengine waliohusishwa na kashfa hiyo ya kupokea rushwa ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Profesa Eudes Ruhangisa, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka.

Wengine ni aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema, na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi Tanesco na waliokuwa wenyeviti watatu wa kamati za kudumu za Bunge, ambao ni Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, Victor Mwambalaswa, Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala, William Ngeleja na Kamati ya Bajeti, Andrew Chenge.

Bunge lilitoa maazimio manane yaliyosomwa bungeni na aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe.

Zitto alisema mabilioni ya fedha yaliyotolewa kwenye akaunti ya Tegeta Escrow yalitumika kuwapa kinachoonekana kuwa ni rushwa.

“Vitendo vilivyofanywa na watu hawa vinaashiria uzembe na makosa mbalimbali ya jinai kama vile wizi, ubadhirifu kutakatisha fedha haramu, matumizi mabaya ya madaraka, rushwa na kupokea mali ya wizi,” alisema.

Alitaja azimio la kwanza la Bunge, ni kulitaka Jeshi la Polisi na vyombo vingine husika vya ulinzi na usalama vichukue hatua stahiki kwa mujibu wa sheria za nchi yetu.

Zitto alisema watu wote waliotajwa na taarifa maalumu ya Kamati kuhusika na vitendo vyote vya kijinai kuhusu miamala ya Akaunti ya Escrow na watu wengine watakaogundulika baada ya uchunguzi unaoendelea kuhusika katika vitendo hivyo vya jinai, watachukuliwa hatua stahiki kwa mujibu wa sheria.

Azimio la tatu ni kuzitaka kamati husika za kudumu za Bunge, zichukue hatua za haraka na kwa vyovyote vile kabla ya mkutano wa 18 wa Bunge kuwavua nyadhifa zao za uenyeviti wa kamati husika za Bunge.

Zitto alitaja azimio la nne kuwa ni la kumwomba Rais aunde Tume ya Kijaji kuchunguza tuhuma za utovu wa maadili dhidi ya Jaji Mujulizi na Jaji Profesa Eudes Ruhangisa wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Kwa upande wa Jaji Msuya uchunguzi wa JAMBO LEO, kutoka vyanzo mbalimbali unaonesha huenda uamuzi wa kuacha kazi kwake unatokana na kuhusishwa na uamuzi wa kesi zake za dawa za kulevya, ingawa taarifa nyingine zinaonesha ugonjwa ndiyo sababu ya hatua hiyo.

Taarifa zinaonesha kwamba Juni 6, 2011 Jaji Msuya alitoa uamuzi wa kuwapa dhamana watuhumiwa wa dawa za kulevya, kwa maelezo kwamba upande wa mashitaka ulishindwa kuthibitisha sababu za kuwanyima dhamana, baada ya kukiri kutowasilisha nyaraka muhimu za kutetea hoja zao.

Mwaka 2013, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ilitoa amri ya kukamatwa kwa wadhamini wawili wa raia wa Pakistani waliokabiliwa na kesi ya dawa za kulevya kukamatwa.

Uamuzi huo huenda una msukumo wa Jaji Msuya kujiuzulu hasa ikizingatiwa kuwa Rais Magufuli alipata kuzungumzia tabia za baadhi ya watendaji wa Mahakama kuwaachia watuhumiwa wa kesi za dawa za kulevya, hivyo kuzorotesha vita hivyo.

Ikumbukwe, kuwa muda mfupi baada ya Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana Dawa za Kulevya, Rogers Siyanga kuapishwa na Rais Magufuli Ikulu, Dar es Salaam, alisema wapo majaji wanaotoa hukumu kwa kupendelea watuhumiwa hali inayoweka viashiria vya rushwa hivyo kukwamisha mapambano.

“Kazi uliyonipa ni ngumu, kwani mapambano haya yanahusu watu wenye uwezo. Wakati mwingine wanaharibu kesi, ila nakuahidi tutahakikisha tunapambana nao wote wanaohusika,” alisema.

Mawakili

Akizungumzia tukio hilo, Wakili wa Mahakamu Kuu ya Rufaa, Profesa Abdallah Safari alisema ingawa uamuzi huo si wa mara ya kwanza kufanyika, lakini kwa siku za karibuni unaweza kuonekana ni mpya.

Safari alisema mfumo wa majaji unataka kuwepo kwa tume ya kuwaondoa ambao unashirikisha nchi za Jumuiya ya Madola, hivyo inawezekana kulikuwa na fununu ya kufanyika hivyo na wahusika wakaona waondoke kwa heshima kabla ya hatua ya kuwaondoa kuchukuliwa.

“Ninavyowajua, hao majaji bado ni vijana, wana nafasi ya kutumikia Mahakama hivyo kwa hayo ambayo yanasemwa kuwa nyuma yao, yanaweza ndio yamewasukuma kufanya hivyo ili kulinda heshima zao na huko nyuma wengine walishafanya, sitawataja,” alisema.

Kuhusu uwezekano wa majaji hao kushitakiwa kama watakuwa wameachia ngazi kwa misingi ya kashfa, alisema kwa mujibu wa sheria za Mahakama, mtu akifikia sifa ya ujaji analindwa, hivyo hakuna uwezekano huo.

Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Tundu Lissu alisema jambo hilo ni la kushangaza: “Hili ni jambo jipya nchini. Huyu Jaji Mujulizi alitajwa kuchota mgawo wa fedha akaunti ya Tegeta Escrow.

“Alitajwa kuchukua fedha katika akaunti hiyo. Kwa nini ameacha kazi sijui! Ila kwa vyovyote vile kitendo cha majaji kuacha kazi licha ya kuwa kinaruhusiwa kikatiba, si cha kawaida sana. Ni vizuri tukapewa taarifa zaidi juu ya sababu za kuacha kazi,” alisema Lissu.

Kuhusu Jaji Msuya, alisema hawezi kumzungumzia kwa kina huku akibainisha kuwa kuacha kazi kwa Meck Sadiki kuna kitu ndani yake.

Lissu alihusisha uamuzi wa Rais Magufuli kumhamishia Kilimanjaro kutoka Dar es Salaam, huku nafasi yake ikichukuliwa na mteule mwingine wa Rais ambaye awali alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni.

Lissu alibainisha kuwa TLS itatoa taarifa rasmi ya kuacha kazi kwa majaji hao baada ya kusoma taarifa ya Ikulu na kufanya uchambuzi wa kina.

Wakili wa kujitegemea, Kaloli Mluge alisema hajui ni sababu gani ambayo imefanya majaji hao waache kazi, lakini yeye anadhani maslahi yamepungua na pia ajira serikalini imekuwa ngumu, tofauti na kipindi cha nyuma.

Mluge alisema hivi sasa watu wamechoka kufanya kazi kwa kuburuzwa, kila mtu anafahamu taaluma yake inamtaka afanye nini, kwa hiyo hakuna sababu ya kuanza kumfundisha kazi wakati anajua majukumu yake.

“Ni ngumu kuusemea moyo, lakini mzee kabana sana, maisha yamekuwa magumu serikalini hakuna mtu anayetamani kufanya kazi naye, kutokana na mfumo anaotumia wa kuwafundisha watu wafanye nini,” alisema Mluge.

Wakili Emmanuel Muga alisema njia waliyotumia majaji hao kuacha kazi ni sahihi na pia si jambo la ajabu.

Alisema kila mtu ana uhuru wa kuacha kazi pasipo kuulizwa maswali mengi, kwa sababu hawana makosa na kama wameamua kufanya hivyo ni sawa. Inawezekana wameamua kufanya kazi ya uwakili, ambalo ni jambo zuri tu.

Wakili Abubakar Salim alisema si mara ya kwanza majaji kuacha kazi, watu wamehamaki kwa sababu huko nyuma kulikuwa hakutolewi taarifa ndiyo maana limeonekana kama suala geni.

“Wapo waliokuwa wakiacha kazi kwa uamuzi wao wa kupumzika na kuendelea na maisha mengine. Hii ya leo imeleta maswali mengi kwa sababu tu watu wameona ni tukio jipya, lakini mambo hayo yapo, sema yalikuwa hayatolewi taarifa,” alisema.

Wakili Jamhuri Johnson alisema si jambo geni na kuwa ugeni wake ni kutangazwa katika vyombo vya habari, kitu ambacho huko nyuma hakikufanyika ila sababu za kuacha hawa hatujui.

“Hapa upya ni kutangazwa, lakini majaji wengi wameacha kazi kwa mfano Jaji Chingwile alikuwa Kilimanjaro aliacha kazi, Jaji Kalegea wa Mahakama ya Rufaa aliacha kazi, tatizo ni kutangaza ndicho naona,” alisema.

TANZANIA Yaanza Kung’ara Sekta ya Viwanda..Miradi 393 ya Viwanda Kujengwa Nchini..!!!

0
0

SEKTA ya viwanda imeanza kukua tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani na jumla ya miradi 393 yenye thamani ya Sh trilioni 5.198 inayotarajiwa kuzalisha ajira 38,862 imesajiliwa nchini.

Pia katika Bajeti ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa fedha 2017/18 iliyowasilishwa bungeni jana, imeongezwa katika eneo la fedha za maendeleo na kufikia Sh bilioni 80 kutoka Sh bilioni 40 mwaka 2016/17.

Pamoja na hayo, katika kipindi cha Julai mwaka jana hadi Machi mwaka huu, Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kilifanikiwa kusajili jumla ya miradi 242 ya sekta mbalimbali ikiwemo miradi ya viwanda 170 yenye thamani ya dola za Marekani milioni 2,079 inayotarajiwa kutoa ajira mpya 17,285.

Hayo yalibainishwa na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2017/18.

Alisema katika bajeti ya wizara hiyo imetengewa jumla ya Sh bilioni 122.2 kwa matumizi ya kawaida na ya maendeleo. Kati ya fedha hizo matumizi ya kawaida ni Sh bilioni 42 na matumizi ya maendeleo ni Sh bilioni 80.1.

Tofauti na mwaka wa fedha unaoishia wa 2016/17, kiwango cha fedha kilichotengwa kwa wizara hiyo kilikuwa ni Sh bilioni 81.8 za matumizi ya kawaida na maeneo, kati ya hizo Sh bilioni 41.8 zilitengwa kwa matumizi ya kawaida na Sh bilioni 40 kwa ajili ya fedha za matumizi ya maendeleo.

Waziri huyo alisema miradi hiyo mikubwa 393 kwa sasa ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji na mingine iko katika hatua za miwsho za kuanza uzalishaji. “Kati ya miradi hiyo TIC imesajili midair 224, Mamlaka ya EPZ miradi 41 na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imesajili miradi 128.

Pia Shirika la Kuhudumia Viwanda vidogo (SIDO) limeratibu uanzishwaji wa viwanda vidogo 1,843,” alisema. Alieleza kuwa kwa miradi 242 iliyosajiliwa na TIC pamoja na kuwepo kwa miradi hiyo 170 ya viwanda, miradi 54 ipo katika hatua ya ujenzi na miradi 17 imeanza uzalishaji.

Alisema kwa mujibu wa takwimu za mwaka jana shughuli za uzalishaji viwandani zilikuwa kwa asilimia 7.8 ikilinganishwa na asilimia 6.5 mwaka 2015 na ukuaji huo ulitokana na ongezeko la uzalishaji wa bidhaa za vyakula, vinywaji na bidhaa za tumbaku.

“Ukuaji wa sekta ya viwanda wa asilimia 7.8 ni juu ya wastani wa ukuaji wa pato la taifa wa asilimia saba kwa mwaka jana. Pia mchango wa sekta ya viwanda umekuwa na kufikia asilimia 5.2 ikilinganishwa na asilimia 5.2 mwaka 2015,” alifafanua.

Waziri Mwijage alisema kwa mwaka jana pekee sekta ya viwanda imetoa ajira 146,892 ikilinganishwa na ajira 139,895 zilizotolewa mwaka 2015, ikiwa ni ongezeko la asilimia 7.1.

Alisema kutokana na sensa ya mwaka 2013, Tanzania ina jumla ya viwanda 49,243 ambayo asilimia 85.13 ni viwanda vidogo sana, asilimia 14.02 ni viwanda vidogo, asilimia 0.35 ni viwanda vya kati na asilimia 0.5 ni viwanda viwanda vikubwa.

“Hali hii si ya kushangaza kwa kuwa taswira ya Tanzania kuwa na viwanda vidogo sana vingi inajitokeza pia katika nchi karibia zote duniani kwa mfano, Japan viwanda vidogo na vya kati vinachukua takribani asilimia 99 ya sekta viwanda, Kenya asilimia 98, Ujerumani asilimia 99, Malaysia asilimia 97.3 na Canada asilimia 98,” alisema.

Alitaja baadhi ya viwanda ambavyo vimeanzishwa katika kipindi cha mwaka 2016/17 kuwa ni viwanda vya uzalishaji chuma, viwanda vya saruji, vigae, nguo na mavazi, ngozi na bidhaa za ngozi, kusindika nyama, vyakula, mbogamboga na matunda, maziwa na mafuta ya kula ambavyo vyote vina fursa kubwa ya kutoa ajira kwa Watanzania.

Alifafanua kuwa katika kuhamasisha mikoa kutenga maeneo ya uwekezaji wa viwanda, jumla ya mikoa 13 imetoa taarifa ya kutenga maeneo hayo, ambapo baadhi ya mikoa hiyo ni Kigoma imetenga jumla ya ekari 451.46, Kilimanjaro ekari 53,033.16, Simiyu ekari 807.06, Shinyanga ekari 33,637.63 na Tanga ekari 33,788.62.

Bei ya vyakula Akizungumzia bei za mazao makuu ya chakula, alibainisha wazi kuwa bei ya mazao ya chakula kama vle mahindi, maharage, mchele, ngano, uwele, ulezi na mtama zimeongezeka kwa kiwango tofautitofauti.

Kwa upande wa mahindi gunia la kilo 100 bei yake imeongezeka kutoka Sh 59,873 msimu wa mwaka 2015/16 hadi kufikia Sh 99,527 sawa na asilimia 66.23. Bei ya mchele kwa gunia la kilo 100 iliongezeka kutoka wastani wa Sh 177,340 msimu wa mwaka 2015/16 hadi kufikia Sh 191,289 msimu wa 2016/17, bei ya gunia la maharage la kilo 100 limeongezeka kutoka Sh 162,383 msimu wa 2015/16 hadi kufikia 178,101 sawa na ongezeko la asilimia 9.68.

Alisema kupanda kwa bei hiyo ya mzao kumetokana na kushuka kwa ugavi kutokana na uhaba wa mvua msimu wa kilimo wa 2016/17. Viwanda vilivyobinafsishwa Katika mwaka wa fedha wa 2016/17 jumla ya viwanda 30 vilivyobinafsishwa vilifuatiliwa kati ya hivyo 18 vinafanya vizuri, vitatu vinafanya kazi kwa kusuasua na tisa vimefungwa.

Kufuatiliwa kwa viwanda hivyo kunafanya jumla ya viwanda kwa mwaka wa fedha 2015/16 hadi 2016/17 vilivyofuatiliwa kufikia 110. “Juhudi mbalimbali zimefanyika kushawishi wamiliki kufufua viwanda vilivyofungwa baadhi vimefanikiwa kuwa katika mchakato wa kufufuliwa na vingine bado wamiliki wake wanatafutwa.

Hata hivyo, kuna changamoto ya madeni makubwa ya mikopo ya benki inayowakabili baadhi ya wamiliki wa viwanda hivyo, wizara inaendelea kutatua changamoto hizo,” alisema.

KUTANA NA SHEKH SHARIFU SIMBA Mtabibu wa Nyota na Tiba za Asili Tanzania na Duniani Kote

0
0

KUTANA NA SHEKH SHARIFU SIMBA mtabibu wa nyota Tanzania na duniani kote,

✨SHEKH SHARIFU SIMBA anatoa shukrani kwa wote mnaopiga simu mlioko ndani na nje ya Tanzania, wanatoa shukrani na wale wenye matatizo, pia anawashukuru wote wanaomshirikisha na kutoa shuhuda jinsi tiba zake zinavyo wasaidia.
✨Bado ujachelewa piga simu na uweze kusaidiwa, SHEKH SHARIFU SIMBA yupo kwaajili ya kutatua matatizo yote yanayo wakabiki wanadamu,

🦅SHEKH SHARIFU SIMBA ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili anatumia kitabu cha QUR'AN, dawa za asili, dawa za kiarabu na majini,

✨je umeachwa na Mme/ mke, mchumba au umpenzi wako? SHEKH SHARIFU SIMBA anauwezo wa kurejesha mahusiano yako ndani ya masaa (72)
✨je umahangaika kupata mtoto bila mafanikio?
✨je mikosi inakuandama na umekuwa mtu wa kilia kila siku bila kupata msaada wowote?
✨je madeni yanakuandama?
✨je umesimamishwa kazi au kushushwa cheo bila sababu? SHEKH SHARIFU SIMBA anatoa kisomo na kusafisha NYOTA na kung'arisha, ili ung'ae upya kwa kila mtu na mahali popote,
💍SHEKH SHARIFU SIMBA anatoa Pete za bahati zilizoambatana na jini Mali,
✨Anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume chango kwa kina mama, ngizi na n.k, pia anatibu miguu kuuma na kufa ganzi, tumbo kujaa gesi na kuunguruma na magongwa mengine ya siri,
🇺🇸pia anatibu kwa njia ya simu kwa wale walioko mbali au nje ya nchi,
📞SHEKH SHARIFU SIMBA anapatikana BAGAMOYO, kwa wale walio nje ya nchi tumia WhatsApp no +255 719361792, kwa wale wa ndani ya nchi piga simu no: 0719-361792 au 0689-476132 na 0745-281712.

UGONJWA wa Ivan Wamtesa Zari Hassan, Watu Waliomuona Kabla ya Kulazwa Wanasema Alikuwa Amezoofu Sana

0
0
KAMPALA: Habari mbaya zilizolifikia Amani zinadai kuwa, aliyekuwa mume wa staa wa Uganda, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, Tycoon Ivan Ssemwanga yu hoi bin taaban akisumbuliwa na maradhi ya shambulio la moyo (Coronary Artery Disease).

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari vya jijini Kampala, Uganda ambako ndiko maskani yake yalipo maeneo ya Munyonyo, pamoja na kwamba ana makazi Pretoria, Afrika Kusini, Ivan alionekana hadharani kwa mara ya mwisho akiwa amedhoofu na rangi ya ngozi kupauka, tofauti na alivyozoeleka kuwa na rangi nyeusi yenye mng’aro alipotinga kwenye Pati ya Blankets and Wine iliyofanyika Kampala hivi karibuni.



Chanzo kilichomshuhudia Ivan kilitonya: “Sisi wenyewe tulipomuona kwenye Blankets and Wine Party akiwa na rafiki yake, Ed Cheune, kwanza hatukumtambua, lakini tulipomuangalia vizuri ndipo tukamjua ni yeye. Ukweli tulishtuka sana na tulijua anaumwa. “Tofauti na alivyozoeleka kuwa ni mtu wa bata, lakini siku hiyo alikuwa mpole sana. Alikuwa hanywi pombe kali na za bei mbaya kama alivyozoeleka.

Badala yake alikuwa anakula samaki na kushushia na soda, tofauti na wadhifa wake unavyojulikana. Ivan linapokuja suala la starehe, huwa hana utani kwa sababu anajua kujiachia. “Nakumbuka tukio hilo lilikuwa Mei 11 (mwaka huu) na tangu siku hiyo hajawahi kurudi kwenye hali yake ya kawaida hadi tuliposikia amelazwa akisumbuliwa na maradhi ya moyo,” kilikaririwa chanzo kimoja na mitandao ya Uganda.



Hata hivyo, Amani lilizungumza na mtu wa ndani ya familia ya Zari kwa Bongo ambaye alibumburua kwamba, kufuatia ishu hiyo, Zari amekuwa akiangua kilio kumlilia mumewe huku akiwataka watu kumuombea ‘eksi’ wake huyo kwa Mungu ili apone haraka.“Bi mkubwa hana raha kabisa, unaambiwa Ivan anamliza maana si unajua ni baba wa watoto wake watatu? ‘So’ na yeye kama binadamu lazima roho imuume kusikia mzazi mwenzake anaumwa,” alisema mtu huyo kwa ombi la kutotajwa gazetini.

Juzi Jumanne, Zari kupitia ukurasa wake wa Snapchat aliandika: “Siku mbili kwangu zimekuwa ngumu, nawaomba tumuombee Ivan.” Baadaye mama huyo wa watoto watano alitupia picha akiwa amekwenda kumjulia hali Ivan katika Hospitali ya Steve Biko Academic huko Pretoria, Afrika Kusini ambapo jamaa huyo alionekana kuwa katika hali mbaya kiafya. Ndugu, jamaa, marafiki na watoto wake watatu aliozaa na Zari wamekuwa wakimuombea ili kurejea katika uzima wake.

GPL

KISA Ajali ya Wanafunzi Arusha…‘School Bus’ Sasa Zawahenyesha Wazazi

0
0
DAR ES SALAAM: Baadhi ya wazazi wenye watoto wanaosoma shule za jijini Dar zinazotumia magari maalum ya kuwapeleka watoto shule (School Bus) wamejikuta wakihenyeka kufuatia magari mengi kuzuiwa kufanya shughuli zao kutokana na kuwa na matatizo mbalimbali. Mengi ya magari hayo yamepigwa ‘stop’ baada ya kutokea kwa ile ajali kule Arusha, wilayani Karatu iliyosababisha vifo vya watu 35 wakiwemo wanafunzi 32 kisha kubainika kuwa, gari walilokuwa wamepanda halikuwa na sifa za kufanya safari.



Kufuatia ajali hiyo, katika Jiji la Dar magari mengi mabovu yaliyokuwa yakisafirisha wanafunzi yamekuwa yakikamatwa, hali iliyosababisha wazazi na walezi wengi kuchukua jukumu la kuwapeleka watoto wao shule na kuwarudisha nyumbani. Amani juzi kwa nyakati tofauti lilishuhudia baadhi ya wazazi wakitembea umbali mrefu wakiwa na watoto wao na wengine kutumia usafiri wa daladala, Bajaj na bodaboda kuhakikisha watoto wao wanakwenda kupata elimu wakati siku za nyuma walikuwa wakitumia magari maalum.

Akizungumza na gazeti hili, mmoja wa wazazi aliyejitambulisha kwa jina la mama Sonia wa Sinza jijini Dar alisema, yeye alikuwa akitumia School Bus ya kampuni binafsi lakini hivi karibuni alitumiwa meseji kuwa, magari yao yamekamatwa hivyo wanasitisha huduma kwa muda. “Kwa kweli nahenyeka sana na huyu mwanangu, naamka saa 11 asubuhi, napanda gari hadi Faya, nashuka kisha naanza kutembea hadi Shule ya Msingi Olympio, kila siku na jioni naenda kumfuata.

“Na hili siyo mimi tu, wazazi wengi wanakiona cha mtemakuni, imebainika magari mengi yanayobeba wanafunzi ni mabovu na hicho ndicho kinaleta hili tatizo. Wenyewe tulizoea asubuhi mwanao anapitiwa nyumbani, anapelekwa na kurudishwa, sasa hivi baadhi ya wazazi ndiyo wanafanya kazi hiyo,” alisema mzazi huyo.

Kuhusiana na hilo la kukamatwa kwa magari mengi yanayosafirisha wanafunzi, Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, DCP Mohammed Mpinga aliliambia Amani kuwa, ni kweli polisi wamekuwa wakikagua
magari yote yakiwemo hayo ya wanafunzi ili kuhakikisha usalama kwa wanaotumia. “Nisisitize; Siyo mabasi tu, ni magari yote tunakagua. Nawaomba wote wanaoona magari yao hayafai kuwa barabarani kwa ubovu, wasingoje kukamatwa, watii sheria bila shuruti kwa kutoyaingiza barabarani,” alisisitiza Kamanda Mpinga.

Article 1

0
0

Mwenyekiti wa CCM tawi la Njia nne Iddy Kirungi liliopo katika kijiji cha Muyuyu kata ya Mtunda wilayani  Kibiti ameuawa kwa kupigwa risasi akiwa kwake.

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Juma Njwayo,ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Rufiji amethibitisha kutokea mauaji hayo.

Amesema marehemu alipigwa risasi akiwa kwake wakati akijaribu kukimbia.

Njwayo amesema kabla ya kuuawa kwa mwenyekiti huyo, pia wauaji hao walianza kumjeruhi kwa kumpiga risasi ya tumboni mtoto wa marehemu aliyetajwa kwa jina la Nurdin Iddy Kirungi.

Mganga wa zamu katika kituo cha afya Ikwiriri, Dk Rashid Omar alisema walimpokea Nurdin akiwa na jeraha kubwa tumboni mwake ambalo halikutokeza upande wa pili.

Alisema majeruhi huyo walimpatia rufaa kwenda Hospital ya Mchukwi kutokana na kuwa anavuja damu nyingi sana.


Aliyempa vyeti Paul Makonda atoweka

0
0

Taasisi ya kuzuia na kupambana Rushwa mkoani Tabora inamsaka Mwandishi na mtangazaji wa kituo cha redio cha Sauti ya Tabora (Voice Of Tabora) Paul Christiani kwa siku kadhaa bila mafanikio.

MANGE Kimambi Ampigia Magoti Rais Magufuli...Amuomba Ampe Ukuu wa Mkoa

0
0

By @mangekimambi_ .
Naomba mnisadie kumfikishia ujumbe huu Mh. Rais, Nilikuwa naomba anifikirie kwenye nafasi ya ukuu wa Mkoa huko Moshi, sitomuangusha, nitapiga kazi Bashite nyuma......kwenye mkoa wangu kila mtu atakuwa CCM la sivyo ntamfukuza kwenye Mkoa wangu na atakosa wa kumtetea...Yani wachaga wajipange!!
.
.
Mwambieni Mzee Siasa sio uadui, tusameheane tusahau yaliyopita.....
.
.
.Mwambieni he needs someone like me in his team, I can imagine how strong we are going to be, me him and Bashite! Hakika tutawanyooosha! .
.
.

I know im over qualified for the job since I can do more than read and write, I hold a masters degree! Lakini niko tayari kuchukua kazi ambayo iko beneathe me...
.
.
Naomba mniombee 🙏.
.
JE MANGE ATAWEZA???? .
TOA MAONI YAKO HAPA

UNDANI wa Kifo cha Dogo Mfaume na Ugonjwa Uliomuua...Uswahilini Simanzi tupu

0
0
DAR ES SALAAM: Rest In Peace Dogo! Haya ndiyo maneno tunayoweza kusema baada ya kupata taarifa za kushtusha za kifo cha msanii maarufu wa nyimbo za Mchiriku na Mnanda, Dogo Mfaume aliyefariki dunia jana mchana wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Amani lina data za kutosha. Kwa mujibu wa taarifa hizo, Dogo Mfaume alikuwa akisumbuliwa na uvimbe kichwani na kwamba kesho, alikuwa katika ratiba ya kufanyiwa upasuaji baada ya tatizo hilo kumsumbua kwa miezi kadhaa.

KUTOKA SOBER HOUSE, KIGAMBONI

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Pilli Missanah Foundation, Pilli Missanah, Dogo Mfaume ambaye kwa muda mrefu alikuwa katika kituo hicho akipatiwa matibabu ya kuachana na utumiaji wa madawa ya kulevya, alikimbizwa hospitalini baada ya afya yake kuzidi kuzorota. “Dogo Mfaume alikuwa na matatizo ya uvimbe kichwani kwa muda mrefu, ingawa pia alikuwa akisumbuliwa na magonjwa mengine kiasi kwamba alifikia wakati akashindwa hata kuongea. “Ugonjwa wake ulimsumbua kwa muda wa miezi mitatu, baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya tukalazimika kumpeleka Muhimbili kwa matibabu zaidi na kesho (Ijumaa) alikuwa afanyiwe upasuaji huo,” alisema Pili.




DOGO MFAUME NI NANI?

Wakati vijana wenzake wakitamba na Muziki wa Kizazi Kipya maarufu kama Bongo Fleva, Dogo Mfaume aliibuka katikati ya miaka ya 2000 akiimba muziki wa mitaani, ambao ulionekana kama wa kihuni zaidi, wa Mchiriku na
Mnanda, ambako alifanikiwa kujitengenezea jina kubwa baada ya nyimbo zake mbili, Hereni na Kazi yangu ya Dukani kumfikisha kileleni. Mwaka 2009 akiwa katika ubora wake, Dogo Mfaume alitwaa Tuzo ya Msanii Bora wa Muziki Asilia kupitia kibao chake hicho cha Kazi Yangu ya Dukani.

INTERVIEW YA MWISHO NA GLOBAL TV

Miezi michache iliyopita, Dogo Mfaume alifanya mahojiano na Global TV Online, akiwa katika kituo cha kusaidia kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya, Kigamboni jijini Dar es Salaam, ambapo alizungumza mambo mbalimbali kuhusiana na safari yake ya matumizi ya madawa ya
kulevya.


JINSI ALIVYOANZA ‘KULA UNGA’

“Mimi nilikuwa navuta bangi tu, sasa siku moja nilikuwa nimekwenda kujiweni nikamkuta mshkaji anavuta, nikamgongea nikijua ni bangi tu ya kawaida. Sasa yule jamaa hakutaka kuniambia ukweli, aliogopa pengine ninaweza kwenda kumtangazia kwa watu na asingeweza kuninyima maana nisingemwelewa. “Kwa hiyo akanipa, nikapiga pafu tatu akaninyang’anya, akavuta tena mara kadhaa akanipa, nikavuta tena, nilipomaliza, nikaona raha f’lani ambayo sijawahi kuiona tangu nianze kuvuta bangi. Nikaanza kama kusinzia hivi kitu ambacho siyo kawaida.”

ATOA UJUMBE MZITO

“Kusema kweli ile raha ilinifanya kesho yake nimtafute yule mshkaji nikamuuliza vipi ile kitu ya jana, akaniambia ili tuipate, inatakiwa buku (shilingi elfu moja) nikampa mia tano na yeye akatoa mia tano, akaenda kuchukua, tukavuta. “Hivyo ndivyo nilivyoanza kuvuta, hii kitu ukianza siyo rahisi kuacha, ndivyo hivyo ilivyokuwa.”

NIMETESEKA MIAKA SABA

“Nimetumia madawa ya kulevya kwa muda wa miaka saba, mwanzo nilikuwa najifichaficha watu wasinione, lakini hali ilivyozidi nikajikuta sioni aibu tena, badala ya kwenda kununuliwa nikawa naenda mwenyewe.”

Wakati mamia ya mashabiki wa Mchiriku nchini wakiamini kuwa Kibao cha Kazi Yangu ya Dukani, kilimpa mafanikio makubwa msanii huyo kimuziki na kimaisha, ukweli kutoka mdomoni mwake ni kuwa wimbo huo ndiyo ulichangia kwa kiasi kikubwa kuporomoka na hatimaye kuharibika kabisa kwa maisha yake.
“Nilikuwa nimeshaanza kutumia unga wakati natoa kile Kibao cha Kazi Yangu ya Dukani, kusema ukweli wimbo ule ndiyo ulichangia sana kuniangamiza, kwa sababu nilikutana na watu wengi na pia nilipata pesa nyingi, nilikuwa sina mke, sina majukumu, kwa hiyo kadiri nilivyopata pesa ndiyo kasi ya kubwia ilivyozidi


“Kuna siku tulikuwa tumealikwa kwenye shoo sehemu, ilipofika zamu yangu nikaitwa kupanda jukwaani, sasa nilivyoshika mic tu, mtu mmoja aliyekuwa karibu akaanza kupayuka kwa sauti, toa teja hilooo, toa teja hilooo, tumetoa hela yetu hatutaki mateja sisi…Dah! Jamaa alinitoa kabisa kwenye reli, sitakisahau kile kitendo. “Nilimuona jamaa kama ndiyo ananitangazia kwa sababu wakati anasema, alikuwa akisikika katika spika, nikajua Tanzania nzima watajua kama nakula unga maana hadi wakati huo nilitam
bua kuwa hakuna mtu aliyekuwa anajua,” alisema Dogo Mfaume.

Hadi Amani linakwenda mitamboni kulikuwa hakuna taarifa zozote kutoka kwa familia yake, kuhusu msiba na shughuli za mazishi, lakini baadhi ya wasanii wenzake, kupitia mitandao ya kijamii, walizungumzia kifo hicho cha mmoja wa wasanii walioacha alama katika Mchiriku. Wasanii ambao walikuwa wameposti kuhusiana na msiba huo ni pamoja na Mr. Blue, Mheshimiwa Temba, Chegge Chigunda, Nay wa Mitego na Dulla Makabila walionesha kumlilia. Aidha, mitaani hasa uswahili ambako alikuwa na mashabiki wengi kufuatia aina ya muziki aliokuwa akifanya, simanzi imetawala hasa kufuatia taarifa kuwa, ilikuwa arejee kwenye game baada ya afya yake kutengemaa. Mungu ailaze mahali pema roho ya marehemu, Amina. Kwa habari kuhusiana na maisha ya Dogo Mfaume kabla ya kufikwa na mauti.

GPL

NAFASI za Kazi Zilizotangazwa Leo

SABABU za Malima Kukamatwa Zaanikwa..!!!

0
0

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limetaja sababu tatu za kumkamata aliyekuwa Naibu Waziri wa Fedha na Mbunge wa Mkuranga, Adam Malima, katika tukio lililombatana na kufyatua risasi tatu angani.

Mtuhumiwa huyo jana alifikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kujibu tuhuma zinazomkabili na kutetewa na Wakili Peter Kibatala.

Hatua hiyo imekuja baada ya kusambaa mitandaoni picha za video zikionesha gari aina ya Toyota Land Cruiser namba T 296 ATW, ambalo liliegeshwa pembeni karibu na hoteli ya Double Tree, Masaki, Dar es Salaam, wakashuka askari wawili – mmoja wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) na mwingine polisi wa kawaida.

Akizungumzia suala hilo jana, Kamanda wa Kanda hiyo, Simon Sirro alisema tukio hilo lilitokea juzi saa sita mchana Masaki karibu na ofisi za Ubalozi wa Canada, ambapo mfanyakazi wa kampuni ya Priscane Business Enterprises, alikuta gari la Malima limeegeshwa sehemu isiyotakiwa, huku akisisitiza dereva wa gari alipotakiwa alipeleke gari hilo yadi alikaidi na kulirudisha kwa nguvu lilipokuwa.

“Mfanyakazi wa Priscane alilikuta gari la Malima likiwa na dereva aliyeambiwa ameegesha sehemu isiyoruhusiwa, lakini cha kushangaza alikaidi ndipo mvutano ukaanza kati yake na mfanyakazi huyo na kulazimu polisi kuingilia kati,” alisema Kamanda Sirro.

Katika video ya tukio hilo, askari wa FFU baada ya kushuka kwenye gari hilo alionekana akinyanyua bunduki na kufyatua risasi angani, kabla mwenzake kumfuata na kumshika kifuani na kutaka kumrudisha kwenye gari.

Tukio liliendelea kwa askari aliyemfuata mwenzake kumfuata Malima na kuzungumza naye, lakini wakati wakiendelea na mazungumzo, yule askari aliyefyatua risasi pia alimfuata na kumsukuma mara mbili waziri huyo wa zamani, kisha kuinua juu bunduki na kusikika akitamka:

“Kwa nini hamheshimu Serikali nyie, mzee heshimu Serikali, mimi nimewekwa kuitumikia Serikali, siwezi kudharaulika.”

Katika video hiyo pia ilisikika sauti ya mtu ambaye hakuonekana akitamka:  “Huna mamlaka, huna mamlaka ya kutishia.”

Wakati hayo yakiendelea, Malima alionekana kujibizana na askari hao akiwa ameweka mikono mfukoni mwa suruali yake, huku mmoja wa askari hao aliyeonekana akimsihi mwenzake aende kwenye gari akitamka: “Poti, Poti, Poti ee!”

Katika mkutano wake na wanahabari, Kamanda Sirro alisema Malima alipotoka nje ya Ubalozi huo, askari walimwambia gari lake linatakiwa liende yadi kwa sababu lilikiuka sheria za maegesho, lakini alionekana kukaidi hali iliyolamzimu askari huyo kufyatua risasi tatu angani.

Alisema licha ya amri ya askari, Malima aliendelea kukaidi huku akitamka kuwa yeye amefanya kazi na viongozi wakubwa, hali iliyomlazimu askari kufyatua risasi nyingine.

Sirro alisema: “Kelele za watu waliokuwa wakizomea, zilichangia askari kutumia busara kupiga risasi hizo angani ili kuwatawanya na endapo   wangewaacha Malima na dereva wake, ingechangia kuwaaminisha wananchi kuwa polisi wameshindwa kufanya kazi yao.”

Alitaja sababu nyingine kuwa ni mazingira hatarishi yaliyomlazimu askari huyo kufyatua risasi, kulingana na wakati na kwamba askari wangeondoka eneo la tukio bila kuwakamata, wangeshitakiwa kwa woga.

Aidha, alisema waziri huyo wa zamani alifikishwa mahakamani kujibu mashitaka yanayomkabili yakiwamo ya kuzuia polisi kufanya kazi zao, kujeruhi na kukaidi amri.

Mahakamani

Malima na dereva wake, Ramadhani Kingwande walipandishwa kizimbani kujibu mashitaka ya kuzuia polisi kufanya kazi yake na kujeruhi.

Kesi hiyo inawakutanisha Wakili Kibatala na Wakili wa Serikali, Mwanaamina Kombakono.

Wakili Mwanaamina alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicious Mwijage kuwa Malima ambaye alikuwa Mbunge wa Mkuranga  na dereva wake wabnakabiliwa na mashitaka mawili.

Ilidaiwa kuwa washitakiwa hao walitenda makosa hayo Mei 15 Masaki Kinondoni, Dar es Salaam.

Wakili huyo alidai kuwa Kingwande kwa nia ya kukataa kukamatwa kutokana na kuegesha vibaya gari lake namba T 587 DDL, alimjeruhi Mwita Joseph ambaye ni Ofisa Operesheni wa kampuni ya Priscane Business Enterprises na kumsababishia maumivu makali.

Wakili huyo alidai kuwa Malima alitenda kosa la shambulio, Mei 15     Masaki, wakati akimzuia dereva wake kukamatwa baada ya kutuhumiwa kutenda kosa  barabarani.

Ilidaiwa kuwa siku hiyo, Malima alimzuia askari Polisi namba H 7818 Konstebo Abdu kufanya kazi halali ya kumkamata Kingwande aliyefanya makosa ya kumshambilia Joseph.

Washitakiwa walikana mashitaka hayo na upande wa mashitaka ulidai kuwa upelelezi wa kesi haujakamilika na hawana pingamizi la dhamana.

Wakili Kibatala aliiomba Mahakama kutoa masharti nafuu ya dhamana kutokana na asili ya mashitaka hayo.

Pia alidai Malima ambaye ni mshitakiwa wa pili katika kesi hiyo ni mtu anayetambulika katika jamii kwa kuwa alikuwa Mbunge na Naibu Waziri.

Hakimu Mwijage aliwataka washitakiwa kila mmoja kuwa na mdhamini mmoja atakayesaini dhamana ya Sh milioni tano. Washitakiwa hao waliachwa huru baada ya kutimiza masharti ya dhamana. Kesi iliahirishwa hadi Juni 15.

Hata hivyo, Wakili Kibatala alidai mahakamani hapo kuwa katika tarehe ijayo atawasilisha pingamizi kwamba mashitaka ya pili yanayomkabili Malima hayaendani na maelezo yake. 

UPASUAJI Majeruhi wa wa Ajali ya Basi la Wanafunzi wa Shule ya Lucky Vincent ya Arusha Wafanikiwa Marekan..!!!!

0
0

HALI za wanafunzi majeruhi wa shule ya Lucy Vincent ya mkoani Arusha, waliopelekwa hospitali ya Mercy jijini Sioux katika jimbo la IOWA nchini Marekani kwa matibabu inaendelea vizuri na tayari wote watatu wamefanyiwa upasuaji.

Majeruhi Sadya Awadh na Wilson Tarimo wote walifanyiwa upasuaji jana wakati Doren Mshana alifanyiwa juzi. Mtu wa Karibu anayefuatilia afya za watoto hao na Mbunge wa Singida Kaskazini na rafiki wa karibu wa watalii madaktari waliowaokoa majeruhi na kuopoa maiti siku ya ajali Mei 6, mwaka huu.

Ajali hiyo ilitokea katika eneo la kilima cha Rhotia, Karatu na kusababisha vifo wanafunzi 32 wakiwemo walimu wawili wanafunzi na dereva, aliandika hayo katika ukurasa wake wa Facebook jana.

Nyalandu alisema: “Kila mtoto amewekwa kwenye chumba chake peke yake, na mama mzazi na muuguzi mmoja wanakuwa naye wakati wote.” Mbunge huyo alisema Sadya amefanyiwa upasuaji maeneo matatu yaliovunjika ikiwemo mkono wa kulia lakini shingo haikufanyiwa upasuaji na badala yake aliwekewa kifaa cha kunyoosha (Brace) atakayokaa nayo wiki sita kuanzia sasa.

“Wote wanaendelea na mapumziko katika hospitali ya Mercy, Sioux City. Mungu ni mwema sana,” aliandika Nyalandu. Katika hatua nyingine, kutokana na ajali hiyo, Polisi wa mkoani humo limetangaza kiama kwa kuyakamata magari yote mabovu yasiyokidhi viwango vya kusafirisha wanafunzi yanayotumiwa na wamiliki wa shule za watu binafsi Jijini hapa.

HUZUNI: Hili Neno "KATA" la Mheshimiwa Rais Limezua na Linazua Hali Mbaya Sana Nchini..!!!

0
0

Siwezi kumuita Rais wetu Mh. J.P Magufuli kama Dikteta au mwenye Ukatili na asiyewajali watu wake ila kuna kauli zake zimekuwa zikisababisha mateso makubwa sana kwa wananchi wake.

Ukiacha zile za wakati wa Njaa na Tetemeko la ardhi.

Mfano mkubwa mzuri ni hili neno alilotoa kuhusu ukataji wa umeme kuwa endapo mwananchi yeyote wa mahali popote atakuwa/watakuwa hawajalipia umeme basi TANESCO wasihoji chochote bali wakate umeme. 

Amekuwa akisema kuwa hata kama ni Ikulu haijalipia umeme (kitu ambacho kamwe hakiwezekani) basi wakate ilihali umeme haukatiki huko asilani.

KINACHOUMIZA ZAIDI, leo Mbunge wa Morogoro kupitia CHADEMA ameelezea hali inayosikitisha na kuhuzunisha sana kuwa Wafungwa (Wanaume, Wanawake na Watoto) wa magereza ZOTE za mkoani morogoro wanaishi katika giza tororo kisa Umeme umekatwa huko.

Hali hiyo imekuwa ikisababisha hata wafungwa watoto kubakwa na kulawitiwa, wanawake kubakwa na kupata mimba kiholela.

Na isitoshe mazingira ya magereza ni magumu sanaa kwa binadamu yeyote kuishi.

Hivi sio serikali inayopaswa kulipia umeme wa magereza? Au ni hao wafungwa?

Ni kwanini Mh. Rais asifute hii kauli yake kwa sehemu kama hizi?

Je wananchi wa maeneo haya wanamchukuliaje Mh. Rais?


MBUNGE Susan Lyimo: Kama Kweli Hostel za UDSM Zimejengwa kwa Mil 500, Nitatoa Hela Zijengwe Zingine..!!!

0
0

“Naomba CAG afanye ukaguzi maalum katika hostel mpya UDSM na kama kweli jengo moja linalochukua wanafunzi takribani 390 linagharimu Milioni 500 basi mimi nitatoa Milioni 500 serikali ijenge jengo lingine la ghorofa tatu ili tuweke vijana wengine”. - Susan Lyimo (Mbunge-Chadema) 

Toa maoni yako

SIMBA Waipigia Saluti Yanga..Wakubali Kushindwa Ligi Kuu!!!!

0
0

MAKAMU wa Rais wa Klabu ya Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ amewapongeza mahasimu wao Yanga, kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, na kusema wanajipanga kwa msimu ujao.

Simba imeshindwa kumaliza vizuri ligi ya msimu huu, baada ya kuongoza kwa tofauti ya pointi nane kwa muda mrefu hadi ilipokuja kuenguliwa kileleni kufuatia kipigo cha mabao 2-1, kutoka kwa Kagera Sugar.

Akizungumza  jana, Kaburu alisema wanajisikia vibaya kuukosa ubingwa wa msimu huu, lakini hawana budi kuwapongeza Yanga kutokana na kufanikiwa kutetea taji hilo kwa bahati dakika za mwisho.

“Yanga ni wapinzani wetu kwenye ligi ya Tanzania, tunawapongeza kwa taji hilo lakini ni bahati ndiyo imewabeba kwa sababu karibu msimu mzima sisi ndiyo tumeongoza ligi lakini mwishoni tuliharibu na wenzetu kupata nafasi,” alisema Kaburu.

Kiongozi huyo alisema baada ya kupoteza taji hilo nguvu zao kwa sasa wamezielekeza kwenye mchezo wa fainali ya Kombe la FA, dhidi ya Mbao FC utakaopigwa kwenye Uwanja wa Jamhuri Dodoma Mei 28 mwaka huu.

Yanga inaongoza msimamo ikiwa na pointi 63 na Simba ina pointi 65 huku kila mmoja akibakiwa na mechi moja. Ili Simba itwae ubingwa inahitaji kuomba Mbao iifunge Yanga mabao 5-0 katika mechi ya mwisho huku yenyewe ikiifunga Mwadui mabao 8-0 jambo ambalo kwa mwenendo wa ligi ulivyo halitawezekana.

Kaburu alisema wamepanga timu yao kuipeleka Zanzibar kupiga kambi ya wiki moja kujiandaa na mchezo huo wa fainali lengo ni kuhakikisha wanashinda ili kushiriki na michuano ya kimataifa.

Alisema, baada ya mchezo wao wa mwisho wa ligi dhidi ya Mwadui keshokutwa, kikosi chao kitaondoka Dar es Salaam Jumapili kwa ajili ya kambi hiyo ambayo wanaamini itakuwa na mafanikio kutokana na ari waliyokuwa nayo wachezaji na viongozi.

Huu ni msimu wa nne mfululizo Simba inalikosa taji hilo, na kuwaachia wapinzani wao Yanga wakilitwaa moja kwa moja baada ya kulichukua mara tatu mfululizo

Shilole: Sipendi Wanaume wafupi

0
0

Msanii Shilole amefunguka na kuweka wazi kigezo kimoja wapo anachoangalia katika kumkubali mtu au kumtokea kuwa kuwa naye katika mahusiano na kusema kimo cha mtu kwake ni kigezo moja wapo.


Shilole alisema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha KIKAANGONI kinachofanyika kupitia ukurasa wa facebook wa EATV, wiki mbili zilizopita na kudai saizi yeye kutoka kimapenzi na mtu mfupi ni jambo gumu kwani anavutiwa zaidi na watu warefu wenye kimo cha kutosha na si wanaume wafupi.

"Mimi napenda mwanaume yoyote yule ilimradi anajitambua basi, suala la muonekano hilo linatengenezwa ila kiukweli kabisa mimi napenda mwanaume mrefu, mwanaume mfupi kwangu hapana, Barnaba yeye ni mfupi na kila mmoja ameumbwa na Mungu tofauti, ila sasa hivi vigezo na masharti kuzingatiwa" alisema Shilole

Mbali na hilo Shilole anasema anapenda sana kuolewa ili na yeye awe na heshima yake kama mke
"Napenda kuolewa na mimi niwe na heshima yangu, niwe na mume wangu basi hamna mtu asiyependa kuolewa, ndoa ni heshima ndiyo maana unasikia watu wanasema mke wa fulani yule, muwe wa fulani yule lakini siyo aah yule si mwanamke tu kwa hiyo ndoa ni heshima" alisisitiza Shilole

Matibabu Kwanza PF3 Baadaye: Mwigulu

0
0

Waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Mwigulu Lameck Nchemba amesema kuanzia sasa mtu yoyote atayeweza kupata majeraha yasiyokuwa na utata wapewe matibabu kwanza hospitali bila ya kuwa na kibali kutoka kwa Jeshi la Polisi (PF3) kama ilivyozoeleka.

Mwigulu ametoa kauli hiyo kupitia ukurasa wake wa kijamii Facebook kwa kusema utaratibu huo unajicho la karibu kutoka kwenye vyombo vya usalama ili kubaini ukweli wa jeraha la muhusika.

“Tumeamua majeruhi, mahututi asiyeweza kutoroka na mtu mwenye majeraha yasiyo na utata wapewe matibabu kwanza bila PF3..Hatua za kufuata PF3 zianze mara moja wakati akiendelea kupewa matibabu, hii tunalengea kuokoa maisha yao kwanza, utaratibu huu unajicho la karibu kutoka kwenye vyombo vyetu vya usalama ili kubaini ukweli jeraha la mhusika”. Ameandika Mwigulu.

Mwigulu amesema hayo baada ya Jeshi la Polisi kutupiwa lawama nyingi kutoka kwa wananchi walipatwa na matatizo kushindwa kupewa huduma hospitali kwa haraka mpaka wapitie kituo cha Polisi kupatiwa cheti cha PF3 ili aende kupata huduma.

WATUMISHI 700 wa Umma Wahakikiwa Vyeti Upya..!!

0
0

TAKRIBANI vyeti 700 vya watumishi wa umma viko kwenye hatua za mwisho za mchakato wa kuhakikiwa upya, kutokana na rufaa zilizokatwa na watumishi hao baada ya Serikali kuruhusu kufanya hivyo.

Taarifa kutoka Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) zinaonesha kwamba watumishi wengi waliowasilisha rufani zao ni wenye vyeti vyenye utata visivyokamilika maelezo.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa NECTA, John Nchimbi alisema mchakato wa uhakiki wa vyeti hivyo kwa mujibu wa agizo la Rais John Magufuli umemalizika.

Alisema watumishi wengi walijitokeza kukata rufaa na kwamba baada ya kuwasilisha malalamiko hayo, sasa yanayafanyiwa kazi kisha majibu yatapelekwa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Alisema wanajitahidi kuhakikisha rufani na malalamiko ya watumishi hao kuhusu vyeti vyao yanafanyiwa kazi haraka, ili kutoa majibu kwa hatua zaidi za kiutendaji.

“Mwanzoni walikuwa wengi, siwezi kusema kundi kubwa ni akina nani, lakini wengi walioleta ni wa vyeti vyenye utata vinavyotumiwa na watu wengi, pia ambao havijakamilika, lakini wa kughushi ni wachache,” alisema Nchimbi.

Aliongeza kuwa siku ya mwisho iliyowekwa na Rais ilikuwa Mei 15 na kama kuongeza ataongeza mwenyewe na kazi ya Necta ni kutekeleza, hivyo kama kuna fursa basi itatolewa na Rais Magufuli.

Mei 4, Serikali ilitaka watumishi wa umma walioorodheshwa kwenye orodha ya watumishi wa umma wenye vyeti bandia, wakati hawakutakiwa kuwekwa, wakate rufaa.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk Laurean Ndumbaro, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Uhakiki wa vyeti bandia kwa watumishi wa umma, ulihusisha vyeti vya kidato cha nne, cha sita, ualimu na taaluma zingine.

Baada ya uhakiki huo, iliagizwa kuwa watumishi 9,932 waliokuwa na vyeti bandia waondolewe kwenye ajira, watumishi 1,538 wenye vyeti vyenye utata kwa maana kwamba vinatumiwa na watu zaidi ya mmoja, wathibitishe vyeti vyao kabla ya Mei 15 na mishahara yao isimamishwe hadi uhakiki utakapokamilika.

Watumishi 11,596 waliogundulika kuwa na vyeti pungufu, walitakiwa kuwasilisha vyeti vyao vikaguliwe kabla ya Mei 15, vinginevyo wangechukuliwa hatua.

Aliwataka wanaodai kwamba wamewekwa kwenye orodha ya wenye vyeti bandia wakati hawakutakiwa kuwa huko, kuandika barua za kukata rufaa kwa Katibu Mkuu Utumishi kupitia kwa waajiri wao.

Hata hivyo waajiri hao, walitakiwa kuwasilisha vyeti hivyo Necta kwa ajili ya uhakiki zaidi kabla ya Mei 15.

“Pamoja na hayo, ieleweke kwamba baadhi ya watumishi wakati wanaajiriwa, waliwasilisha vyeti vya matokeo mengine ya sekondari na wakati wa uhakiki, walionesha vyeti vingine.

“Lakini, naomba ieleweke, kwamba hakuna mtumishi wa umma mwenye cheti halali atakayeondolewa katika utumishi wa umma,” alisema.
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live




Latest Images