Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

BAADA ya Waandishi wa Habari Kukamatwa na Kuachiwa na Polisi Jana Mkoani Arusha..Nape Nnauye Ametoa Lake la Moyoni..!!!

0
0

Mbunge wa Jimbo la Mtama Mh. Nape Nnauye ameshauri vyombo vya usalama nchini vitimize majukumu yao pasipo kutumia nguvu sehemu ambayo mazungumzo yanaweza kuwa na tija ili kuendelea kulinda nchi katika namna nzuri ya kushirikiana. 

Mh. Nape amesema kuwa vyombo vya dola vimekuwa ni vyombo vya wananchi

"Ni vizuri vyombo vya dola vikatimiza wajibu wao na ni vizuri tukalinda nchi yetu katika mazingira ambayo tumekuwa tukihusiana kwa muda mrefu, vyombo hivi vya dola hivi vimekuwa ni vyombo vya wananchi na ndio maana jeshi letu linaitwa jeshi la Wananchi wa Tanzania, si vizuri kutumia nguvu kubwa pale ambapo hapahitajiki kutumia nguvu kubwa. Na mimi nimeendelea kushauri nchi yetu bado tumeendelea kufanya mambo yetu kwa mazungumzo kwa kuelewana" alisema Nape Nnauye 

Mbali na hilo Nape Nnauye anasema mambo haya ya polisi kutumia nguvu sehemu isipohitajika nguvu yanajenga chuki kati ya wananchi na serikali yao. 

"Nchi yetu hatukuzoea hayo, nchi yetu hatukuzoea mabavu, kwanza matendo haya yanajenga chuki kati ya serikali na wananchi, yatajenga chuki kati ya Rais na wananchi, yatajenga chuki kati ya CCM na wananchi kwa sababu itafika mahali wananchi hawakuzoea mambo haya watajenga chuki tu kuona nchi yetu haiendi sawasawa" alisisitiza Nape Nnauye 

MAUJI ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani Yamfanya Zitto Kabwe Kufunguka Haya Mengine..!!!

0
0

Mbunge wa jimbo la Kigoma Mjini, Zitto Zuberi Kabwe amefungukia juu ya Mauaji yanayoendelea mkoani Pwani na kudai maeneo matatu ya Mkuranga, Kibiti na Rufiji hatajawahi kupatiwa majibu ikiwa ni mtu wa 31 akiwa ameuawa usiku wa kuamkia leo.

Zitto amefunguka hayo baada ya Taarifa za kifo cha Mwenyekiti wa CCM Tawi la Njia Nne katika Kijiji cha Muyuyu Wilayani Kibiti, Iddy Kirungi,  kuthibitishwa kwa mwenyekiti huyo ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana.

"Eneo la #MKIRU ( Mkuranga, Kibiti, Rufiji) halijapata jawabu la kudumu, Huyu mtu wa 31 kuuwawa eneo Hilo"

 Akithibitisha kutokea kwa mauaji hayo Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kibiti, Juma Njwayo,ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Rufiji na kusema  kwamba, marehemu alipigwa risasi akiwa nyumbani kwake wakati akijaribu kukimbia.

Bw. Njwayo amesema, kabla ya kuuawa kwa Mwenyekiti huyo, pia wauaji hao walianza kumjeruhi kwa kumpiga risasi ya tumboni mtoto wa marehemu aliyetajwa kwa jina la Nurdin Iddy Kirungi.

Mganga wa zamu katika kituo cha afya Ikwiriri, Dk. Rashid Omar, amesema, walimpokea Nurdin akiwa na jeraha kubwa tumboni mwake ambalo halikutokeza upande wa pili, majeruhi huyo walimpatia rufaa kwenda Hospital ya Mchukwi kutokana na kuwa anavuja damu nyingi sana.

GWAJIMA Aanika Uislamu Wake ..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 19/5/2017..!!!

Mrembo Wema Sepetu Kushiriki Mazishi ya Aliyekuwa Team Wema Damu Instagram

0
0


Wema Sepetu amepata msiba wa mmoja wa followers wake damu kwenye mtandao wa Instagram, Japo hawajawahi onana lakini amefunguka haya:

By @wemasepetu .
Imeniuma kuskia Umetutoka lakini Imeniuma zaidi nilipogundua kuwa You were One of Team Wema Damu kabisa.... And after goin thru your page nikaona jinsi ilivyojaa picha zangu ndo nimezidi kuumia.... Ni njia yetu sote my love... Pumzika kwa amani kipenzi.... Dah... My Condolences to ndugu, jamaa na marafiki... Tulikupenda lakini Allah amekupenda zaidi.... RIP mamy.... @mwajuma_pesa @mwajuma_pesa @mwajuma_pesa @mwajuma_pesa .... Dah... Inshallah ntakuepo kwenye mazishi... Innah lillahy wa innah illahy rajiun...🙏🏼🙏🏼😊...
.
HAKIKA ALICHOAMUA KUFANYA WEMA NI MFANO WA KUIGWA HATA KWA WASANII /WATU WENGINE... TUSHIRIKI KATIKA MATATIZO YA MASHABIKI ZETU... SI LAZIMA MISIBA.
.
.
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MWAJUMA MAHALA PEMA PEPONI.... WOTE TUSEME "AMEN "

JESHI la Polisi Latoa Ufafanuzi Sakata la Vyeti Feki kwa Askari Wake..!!!

0
0

Jeshi la Polisi nchini limekanusha taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikiwahusisha askari wake kuwepo katika majina ya vyeti feki na kusema taarifa hizo ni za uongo na wala hazijatolewa na Jeshi hilo.

Hayo yamebainishwa na taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, ACP Advera Bulimba na kusema wanaendelea kumtafuta mtu aliyesambaza taarifa hiyo kwa lengo la kupotosha umma ili hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yake na kuwa fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.

"Jeshi la Polisi nchini, linaujulisha umma kwamba, orodha ya majina ambayo yamekuwa yakisambazwa kwenye mitandao ya kijamii yakidai kuwa ni majina ya askari wa jeshi la polisi wenye vyeti feki ni ya uongo na wala taarifa hiyo haijatolewa na jeshi la polisi". Ilisema taarifa hiyo

MASIKINI..Hivi Ndivyo Dogo Mfaume Alivyopigania Uhai Wake ..Rafiki Yake Agunguka A - Z Siku Chache Kabla Hajafariki Ilivyokuwa..!!!

0
0

Kibabu Fleva rafiki wa karibu wa marehemu Dogo Mfaume amefunguka na kusema msanii huyo alipooza upande mmoja na katika hatua za mwisho alikuwa amepoteza kabisa kumbukumbu.

Kibabu Fleva anadai Dogo Mfaume alikuwa afanyiwe upasuaji wa kichwa lakini kabla ya hatua kufanyika akapoteza maisha. Mazishi ya Dogo Mfaume yanatarajia kufanyika leo Ijumaa maeneo ya Gongolamboto.  

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Nchini Yatahadharisha Mvua Kubwa Zaidi Kuendelea Kunyesha Nchini..!!!

0
0

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imesema wakati msimu wa mvua za masika ukielekea ukingoni, wananchi wanatakiwa kufuatilia taarifa zinazoendelea kutolewa ili kuchukua tahadhari dhidi ya mvua kubwa zinazoweza kutokea.

Msimu wa mvua za masika ulianza Machi na zitamalizika Mei mwaka huu,  katika maeneo ya Ukanda wa Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manaya , Kaskazini, Pwani ya Kaskazini  katika mikoa ya  Morogoro, Pwani, Dar es Salaam, Tanga na visiwa vya Unguja na Pemba.

Mkurugenzi wa Utafiti na Matumizi ya Hali ya Hewa wa TMA, Dk. Ladislaus Chang’a, alilieleza Nipashe jana kuwa mvua hizo zimeendelea kupungua wakati zikifikia ukingoni.

“Mvua zinaendelea kupungua, lakini matukio machache ya mvua kubwa yanaweza kuwatokea, hivyo wananchi wanatakiwa kutufuatilia taarifa tunazotoa ili kuchukua tahadhari ingawa zimepungua lakini hatuwezi kusema zimeisha hadi msimu umalizike,” alisema.

Alisema katika maeneo hayo  na yale ya kuzunguka Ziwa Victoria wanapata mvua mara mbili kwa mwaka ambazo ni mvua za vuli na masika na kwamba kwa mwaka huu zilikuwa kubwa.

Alisisitiza kuwa msimu wa mvua bado unaendelea, ingawa zinaelekea ukingoni na kwamba zinaendelea kupungua kabla ya kumalizika kabisa.

KABURU: Yanga Wanashangilia Ubingwa Hewa..!!!

0
0

Makamu wa rais wa timu ya Simba, Geoffrey Nyange Kaburu amesema kuwa watani zao Yanga wanashangilia ubingwa hewa kwani ligi bado haijamalizika.

Amesema kuwa katika ligi yoyote duniani hakuna mtu anayeweza kutangaza ubingwa wakati mechi bado na kuna uwezekano wa timu yoyote kuuchukua ubingwa.

Aidha, Simba wanatakiwa kushinda zaidi ya mabao nane katika mechi yao ya mwisho ya Ligi Kuu huku wakiomba Yanga ifungwe zaidi ya mabao matano na Mbao FC mjini Mwanza ili wao wawe mabingwa.

Hali hiyo imeonekana kutowakatisha tamaa Simba na hawataki kusikia Yanga wakitangazwa kuwa mabingwa kabla ya mechi yao ya mwisho wao wakiwavaa Mwadui FC jijini Dar es Salaam.

“Sisi tunajua bingwa bado hajapatikana na tutaona hadi katika mechi ya mwisho. tutapambana hadi tone la mwisho.

“Hatuwezi kukata tamaa, huu ni mpira na vijana wako vizuri kabisa,” amesema Kaburu.

Hata hivyo, endapo mechi ya mwisho Yanga atakubali kufungwa atakuwa na pointi 68 sawa na Simba ambao viongozi bado wanaamini kuwa pointi tatu walizopokonywa dhidi ya Kagera Sugar zitarudishwa kwani wanataka kwenda FIFA kudai pointi zao na watakuwa na pointi 71.

MHASIBU wa Takukuru Aliyejilimbikizia Mali za Bilioni 3.5 Kupandishwa Mahakamani Muda Wowote Kuanzia Sasa..!!!

0
0

ALIYEKUWA Mhasibu Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Godfrey Gugai, ambaye anadaiwa kukutwa na mali za thamani zaidi ya Sh. bilioni 3.5 sasa anaweza kufikishwa mahakamani wakati wowote.

Chanzo cha uhakika kimeiambia Nipashe kuwa mojawapo ya kosa litakalompeleka mahakamani kigogo huyo wa zamani wa Takukuru, ni kosa la kujilimbikizia mali kinyume cha maadili ya utumishi wa umma. Pia mali hizo zinahusishwa na tuhuma za rushwa.

Kwa mujibu wa tangazo la Takukuru jana, mali za mhasibu huyo wa zamani ni pamoja na nyumba saba za maghorofa zilizopo katika maeneo ya Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam; nyumba tisa za kawaida zikiwamo zilizopo kwenye maeneo mbalimbali ya majiji ya Dar es Salaam na Mwanza na pia Musoma mkoani Mara; viwanja 37 vikiwamo vya kwenye maeneo ya karibu mwa bahari ya Bagamoyo, Ununio, Mbweni na Kigamboni; magari matano na pikipiki moja ambavyo kwa pamoja, thamani yake inakadiriwa kuwa zaidi ya Sh. bilioni 3.5.

Chanzo hicho ndani ya Takukuru kiliiambia Nipashe jana kuwa taratibu zinakamilishwa na mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani kujibu mashtaka yake wakati wowote kuanzia sasa.

“Yuko mbioni kushtakiwa. Na ndiyo maana lile tangazo limetolewa kwenye magazeti… ukiona tangazo kama lile ujue huyo mtu karibu anashtakiwa,” alisema mtoa taarifa huyo kwa sharti la kutotajwa jina.

“Siwezi kusema ni lini hasa atafikishwa mahakamani. Lakini naweza kukuthibitishia kuwa siku si nyingi… ni suala la kusubiri tu,” chanzo kilisema na kuongeza:

“Mahakama haiwezi kutoa oda ya kuzua mali ya mtu kama hujaishawishi. Lazima uishawishi mahakama kwamba mtu unayemtuhumu yuko mbioni kushtakiwa na ndipo wanakupa oda ya kuzuia mali zake. Kwa hiyo hilo ndilo lililopo kwa sasa. ”

Mei 9 mwaka huu, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilitoa amri ya zuio la mali za Gugai ambaye anakabiliwa na tuhuma za limbikizo la mali kinyume cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Namba 11 ya mwaka 2007.

Amri ya zuio la mali za Gugai imetolewa na mahakama hiyo kufuatia ombi la Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) chini ya kifungu namba 38(1)(a) na (b) cha sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya mwaka 2007 katika shauri namba 13 la 2017.

Kufuatia maombi ya DPP, mahakama imeamuru mali zilizotajwa kuwa za Gugai ziwe chini ya zuio la mahakama.

Pia mawakala wake na watu wengine wote wanaomwakilisha wamezuiwa kuuza au kuhamisha umiliki au kuweka dhamana mali zote zilizowekewa zuio.
Aidha, msajili wa hati ameagizwa kusajili zuio hilo kama kizuizi dhidi ya mali zote zilizotajwa.

Pia Msajili Msaidizi wa magari ameagizwa asiruhusu uhamishaji wa umiliki wa vyombo vya moto vilivyowekewa zuio mpaka mahakama itakapoelekeza.

MALI ZENYEWE
Orodha ya mali zilizowekewa zuio la mahakama ni pamoja na nyumba nne za ghorofa moja zilizoko kiwanja na 64 Kitalu B, Ununio, Kinondoni; nyumba tatu za ghorofa moja zilizoko kiwanja na 150 Kitalu 8 Bunju, Kinondoni na nyumba nne zilizoko kiwanja namba 225 kitalu 6, Mbweni JKT, Kinondoni.

Nyingine ni nyumba zilizoko kwenye kiwanja namba 62 na 63 kitalu C, Kinondoni; nyumba iliyoko kiwanja namba 29 kitalu L, Majita, Musoma mkoani Mara; nyumba namba 713 PPF Kiseke, Mwanza na nyumba iliyoko kwenye kiwaja namba 438 kitalu D, Nyegezi, Mwanza.

Aidha, viwanja ni pamoja na kiwanja namba 14 kitalu J, Bunju, Kinondoni; kiwanja namba 47 kitalu B, Mwongozo, Kigamboni; kiwanja namba 184 kitalu B, Buyuni,Temeke; kiwanja namba 103 kitalu L, Kaole, Bagamoyo; kiwanja namba 104 kitalu L, Kaole, Bagamoyo na kiwanja namba 209 kitalu B, Kibaha.

Vingine ni kiwanja namba 195 kitalu 3, Kihonda, Morogoro; kiwanja namba 993 kitalu L, Kiegeya, Morogoro; kiwanja namba 868 kitalu Q, Lukobe, Morogoro; kiwanja namba 34 kitalu K, Kisasa B, Dodoma; kiwanja namba 32 kitalu N, Itega, Dodoma; kiwanja namba 39 kitalu M, Itega, Dodoma; kiwanja namba 24 kitalu B, Chidachi, Dodoma; kiwanja namba 64 Nzuguni, Dodoma; kiwanja namba 230 kitalu B, Nyegezi, Mwanza na kiwanja namba 439 kitalu D, Nyegezi, Mwanza.

Viwanja vingine ni kiwanja namba 275 Kitalu 2, Nyamhongolo, Mwanza; kiwanja namba 277 kitalu 2 Nyamhongolo, Mwanza; kiwanja namba 296 kitalu 2, Nyamhongolo, Mwanza; kiwanja namba 297 kitalu 2, Nyamhongolo, Mwanza; kiwanja namba 286 kitalu G, Nyamagana, Mwanza, kiwanja namba 287 kitalu G, Nyamagana, Mwanza; kiwanja namba 90 kitalu 5, Bugarika, Mwanza; kiwanja namba 126 kitalu A, Makoko, Musoma; kiwanja namba 622 kitalu A, Gomba, Arusha; kiwanja namba 621 na 623, kitalu A, Gomba, Arusha; kiwanja namba 737 kitalu C, Mwambani, Tanga; Kiwanja namba 1,2 na 3 kitalu J,

Mwambani,Tanga; kiwanja namba 4 kitalu J Mwambani, Tanga; kiwanja namba 5 kitalu J, Mwambani Tanga; kiwanja namba 18 kitalu J, Mwambani, Tanga; kiwanja namba 79 kitalu J, Mwakidila, Tanga; na kiwanja namba 11 13 kitalu J, Mwakidila, Tanga.

Magari yaliyozuiwa ni matano, ambayo ni gari namba T 180 DBQ, Mitsubish Canter; gari namba T 581 BQU, Toyota Hillux; gari namba T 814 CSC , Nissan Murrano; gari namba T 679 ASD Toyota RAV 4; gari namba T 913 DHE Suzuki na pikipiki namba MC 837BCL.

Credit - Nipashe

VIDEO:Kijana Mwingine Ajitokeza na Kudai Yeye na Harmorapa ni Ndugu...Amekuja Dar Kumtafuta

0
0
Kijana mmoja aliyesema anaitwa Frank Omary amesafiri kutoka Iringa kuja Dar kumtafuta Harmorappa mna kudai yeye ni ndugu yake mama yake amemwambi ni wa baba mmoja, ameacha na namba zake akitaka Harmorapa amtafute akiona ujumbe wake mtandaoni

Tazama Video:

JE, Dada Unapenda Kuwa Mrembo na Kaka Kuwa Mtanashati na Kurudisha Heshima ya Ndoa?

0
0

JE, DADA UNAPENDA KUWA MREMBO? NA KAKA UNAPENDA KUWA MTANASHATI NA KURUDISHA HESHIMA YA NDOA? Tumia Bidhaa halisi za MARKSON kwa mafanikio ya uhakika na bila madhara.
Zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kuthibitishwa kiafya.
🍉🌿🍓🍒🎄🍍🍀🍓🍉
Pata hizi 👇👇👇👇👇👇

1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @120,000/=
2. Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa (a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200,000/=
(b)Vidonge @180,000/=
3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @120,000/=
(11)Vidonge @150,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-
(a) Gely ya kupaka @130,000/=
(b) Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu hata kwa wenye kisukari @130,000/= (c)Handsome up original @200,000/=
6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @120,000/=
7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula @120,000/=
8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a) Dawa ya kunywa au kupaka @120,000/=
(b) Mkanda wa kawaida @100,000/=
(c) micro-computer belt unaovaibret @250,000/=
9 .Kupunguza maziwa na kuyasimamisha @120,000/=
10. Kushepu miguu na kuwa minene na kuondoa migimbi @120,000/=
11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @100,000/=
12. kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @120,000/=

NB: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
Wasiliana nasi :-
(+255) 0767447444 na
0714335378
Follow us on instagram @Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr

Dr Slaa: Sina Mpango wa Kurudi Tanzania Ng'oo

0
0
Aliyekuwa katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dkt. Willbroad Slaa amesema hana mpango wa kurudi Tanzania kwa sasa na kwamba taarifa zinazosambazwa hazina ukweli wowote.

Slaa alijiuzulu ukatibu mkuu wa CHADEMA na siasa za vyama baada ya CDM kumpokea Edward Lowassa na kumpa nafasi ya kuwakilisha chama hicho katika uchaguzi wa urais 2015

Ndani ya Mkutano Lucky Vicent Arusha Kabla ya Polisi Kuvamia (Video Fupi)

0
0
Jana May 18 kwenye shule ya Lucky Vicent Arusha, Polisi walivamia mkutano ulioongozwa na Meya wa jiji hilo akiambatana na viongozi wa dini, Madiwani na Waandishi wa habari ambao Meya alidai lengo lake ni kukabidhi rambirambi walizozichanga wao kutokana na msiba wa ajali ya Wanafunzi wa shule ya Lucky Vicent.

Wakati viongozi hao wakiendelea kuhojiwa na Polisi Arusha, millardayo.com na AyoTVzinakukutanisha na video ya sehemu ya vilivyokua vinazungumzwa ndani ya mkutano huo kabla ya Polisi kuvamia.

Hii video hapa chini Katibu wa chama cha Wamiliki wa Shule binafsi mkoa wa Arusha Leonard Mao alikua anaongea

“Nilitangaza kwa niaba ya Watanzania siku ya kuaga ile miili 35 kwamba tutaendelea kuchanga rambirambi zetu na kwenda kuwaona wale wazazi mmoja baada ya mwingine“

“Hakuna hata senti ya mtu itakwenda pembeni…. hatumpi mtu hata kwenye shule ya Vicent, ni waliofiwa wenyewe mkono kwa mkono

’ FULL VIDEO NDIO HII HAPA CHINI UNAWEZA KUPLAY UKAJIONEZA ZAIDI:



My take, ni uhuni uliopindukia kuvamia na kuharibu shughuli ya uwasilishwaji wa rambirambi zilitolewa kwa wapendwa wetu waliotangulia mbele za haki laana iwe juu ya yeyote aliyehusika na uhuni huu.

Red Bull Ni Kinywaji Hatari Sana Kwa Afya Yako

0
0
RED BULL Huuzwa katika maduka makubwa (Supermarkets) na madogo (Retail Shops) katika nchi ya Tanzania, watu wazima na watoto wengi wana mazoea ya kunywa kinywaji hiki ambacho kinaweza kusababisha kifo. Kemikali zinazopatikana katika kinywaji cha RED BULL zilitengenezwa maalum katika maabara za kijeshi za Marekani kwa ajili ya kutuliza mzuka wa maaskari wao wakati wakitekeleza mauaji ya kikatili sana dhidi ya wananchi wa Vietnam miaka ya sitini na sabini. Kemikali hizo zilitumika pia kama dawa ya kuwazindua watu waliozirai (“stress coma”).

Hazikukusudiwa kutumiwa kama kinywaji au kilevi cha kawaida! Duniani kinywaji hiki
(RED BULL) huuzwa kama kitu cha kuleta msismko (Energizer Drink) na matangazo
yake yanataja sifa zake kama ifwatavyo. “Ni kinywaji kinachompa mtu nguvu ya kustahimili na umakini. Humpa mtu kasi ya vitendo” na kadhalika.

RED BULL imesambaa katika nchi 100 kwa mpigo (nchi masikini!). Na matangazo yake huwalenga vijana na watoto, hasa wanamichezo. Hawa ni rahisi kushabikia kinywaji hiki kibaya na kudhurika kiafya baadaye. Katika hali yake ya matumizi ya sasa kinywaji hiki kiligunduliwa na Mjerumani Dietrich Mateschitz ambaye alikikuta huko Hong Kong kikiwa ni mojawapo ya madawa yaliyotumika katika kutengeneza dawa ya mswaki wa meno.
Dawa hiyo ilitengenezwa kwa kemikali ambazo zina kafeni na taurini (“caffeine and “taurine).

Mjerumani huyo aliona vijana wajinga wa huko wakishabikia unywaji wake akaona mwanya wa kufanya biashara na akafanikiwa kukileta ulaya. ATHARI ZA KUNYWA RED BULL Kinywaji kinachotengenezwa na kusambazwa leo hii kina kemikali mbaya iitwayo “Glucuronolactone”, kemikali hatari ambayo ilitengenezwa na idara ya jeshi la Marekani wakati wa vita na Vietnam kwa ajili ya kutuliza mvurugiko wa mawazo wa maaskari wake uliotokana na mauaji ya kinyama waliokuwa wanafanya huko Vietnam.

Kwa sababu ya madhara makubwa ya kinywaji hiki nchi za FRANCE na DENMARK zimepiga marufuku kinywaji hiki na kibatiza jina la “MKOROGO WA UMAUTI”. Katika nchi hizi, utafiti uligundua kuwa maaskari wa Marekani waliotumia kinywaji chenye
kemikali ya “GLUCURONOLACTONE” waliishia kupata madhara ya maumivu makali ya kichwa, uvimbe wa ubongo na hata ugonjwa wa ini (Migraines, Cerebral tumours and liver diseases).

Na kwa sababu hiyo wamarekani waliacha kuwapa maaskari wao hicho kinywaji katika miaka ya sitini na sabini. Jambo la kushangaza ni kuwa lebo ya RED BULL inaonyesha wazi kuwa kinwaji hiki kimetengenezwa kwa kemikali hatari ya “GLUCURONOLACTONE”! Ni kwa sababu hiyo serikali za Denmark na Ufaransa nazo zikapiga marufuku unywaji wa RED BULL. Pamoja na wauzaji wa RED BULL kuweka bayana kuwa ndani mwake mna hiyo kemikali hatari ya “GLUCURONOLACTONE” lebo ya RED BULL hailezi madhara makubwa yanayoletwa na kemikali hiyo.

Madhara ambayo hayakuwekwa bayana kwa mnywaji ni kama yafuatayo:

1. Ni hatari kwa mtu ambaye hafanyi kazi au mazoezi mazito sana kukitumia kwani kina tabia ya kuongeza msukumo wa damu na kasi ya mapigo ya moyo kiasi kwamba mtumiaji anaweza kupatwa na ugonjwa wa moyo.

2. Mtumiaji anaweza kupatwa na ugonjwa wa damu kuvuja ubongoni kwani RED BULL ina kemikali zinazoifanya damu iwe nyembamba ili moyo upate kusukuma damu nyingi bila kutumia nguvu nyingi.

3. Ni hatari kuchanganya RED BULL na pombe ya aina yoyote kwani mchanganyiko wake huwa ni sumu (“Deadly Bomb”) inayoathiri musuli za ini la mtumiaji na kuiacha katika hali ambayo haitapona kamwe.

4. RED BULL Ina vitamini B12 kwa wingi, vitamini ambayo hutumiwa kama dawa ya kuwazindua wagonjwa mahututi. Matumizi ya vitamini hii katika watu wazima ina athari za kuleta shinikizo la damu na humfanya mtu ajisikie kama mlevi.

5. Unywaji wa RED BULL mara kwa mara huvuruga mfumo ya neva za fahamu na husababisha maradhi mithili ya mfadhaiko wa akili usioponyeka.

HITIMISHO:
RED BULL ni kinywaji HATARI SANA ambacho hapana budi kipigwe marufuku katika nchi zote zinazoendelea kwani ni dhahiri kimetengenezwa na kusambazwa ili kiathiri afya za wananchi wasiojiweza wa nchi hizi masikini. Kwa kuwa wengi katika nchi hizi hutumia pombe za kila aina ni wazi kuwa kinywaji hiki kinalenga kuwamaliza watu watu wetu– kana kwamba ukimwi uliobuniwa na hao wabaya wetu hautoshi!

Nimeona Utupu wa Mke wa Mtu..Sasa Imekuwa tabu!! Ushauri

0
0
Ilikuwa wiki moja iliyopita.Wakati wa asubuhi naingia bafuni kuoga kumbe kulikuwa na mke wa jirani yangu ambaye pengine hakusikia ujio wangu nami sikujua kama yumo.

Ile anataka kutoka tu pale mlangoni,kanga yake ikaanguka na akabaki mtupu Macho hayana pazia niliona utupu wake nae aliona kuwa nimeona.Ile tu anajizoazoa kujisitiri akateleza akaanguka ikabidi nimsaidie kumuinua , nikamwinua huku akiwa uchi wa myama na kuhakikisha hajaumia popote ...then nikamfunika na kumwambia pole nikaondoka kiistaarabu.
Ila sasa naona ustaarabu wangu uliniponza sasa naona ananifanyia vituko Mwanzo nilifikiri yameisha,alianza kwa kukwepesha macho na mimi,,mara akajenga mazoea na mimi.Na sasa vituko vimezidi,mara sms za ajab,wakati wote anataka kujua niko wapi na nafanya nini, siku ingine ananiletea chakula alichopika nile..

Kwa tabia na msimamo wangu naheshimu sana ndoa za watu.Nishaurini nifanye nini kumuepuka ? Nimepanga chumba hapa na nimelipa kodi ya mwaka mzima,ni jirani tu chumba cha nne toka kwangu

KUTANA NA SHEKH SHARIFU SIMBA Mtabibu wa Nyota na Tiba za Asili Tanzania na Duniani Kote

0
0

KUTANA NA SHEKH SHARIFU SIMBA mtabibu wa nyota Tanzania na duniani kote,

✨SHEKH SHARIFU SIMBA anatoa shukrani kwa wote mnaopiga simu mlioko ndani na nje ya Tanzania, wanatoa shukrani na wale wenye matatizo, pia anawashukuru wote wanaomshirikisha na kutoa shuhuda jinsi tiba zake zinavyo wasaidia.
✨Bado ujachelewa piga simu na uweze kusaidiwa, SHEKH SHARIFU SIMBA yupo kwaajili ya kutatua matatizo yote yanayo wakabiki wanadamu,

🦅SHEKH SHARIFU SIMBA ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili anatumia kitabu cha QUR'AN, dawa za asili, dawa za kiarabu na majini,

✨je umeachwa na Mme/ mke, mchumba au umpenzi wako? SHEKH SHARIFU SIMBA anauwezo wa kurejesha mahusiano yako ndani ya masaa (72)
✨je umahangaika kupata mtoto bila mafanikio?
✨je mikosi inakuandama na umekuwa mtu wa kilia kila siku bila kupata msaada wowote?
✨je madeni yanakuandama?
✨je umesimamishwa kazi au kushushwa cheo bila sababu? SHEKH SHARIFU SIMBA anatoa kisomo na kusafisha NYOTA na kung'arisha, ili ung'ae upya kwa kila mtu na mahali popote,
💍SHEKH SHARIFU SIMBA anatoa Pete za bahati zilizoambatana na jini Mali,
✨Anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume chango kwa kina mama, ngizi na n.k, pia anatibu miguu kuuma na kufa ganzi, tumbo kujaa gesi na kuunguruma na magongwa mengine ya siri,
🇺🇸pia anatibu kwa njia ya simu kwa wale walioko mbali au nje ya nchi,
📞SHEKH SHARIFU SIMBA anapatikana BAGAMOYO, kwa wale walio nje ya nchi tumia WhatsApp no +255 719361792, kwa wale wa ndani ya nchi piga simu no: 0719-361792 au 0689-476132 na 0745-281712.

Zitto Kabwe Adai Serikali inaua Viwanda

0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe ameitaka serikali kusimamia ipasavyo sekta ya viwanda ili kuhakikisha kinachozalishwa nchini kinakuwa na maana kwa faida ya Watanzania,


Amehimiza serikali kuvilinda viwanda vya ndani dhidi ya kuvurugwa na bidhaa za nje ambazo zinaingizwa kinyemela, vinginevyo ikubali kuwa inaviua makusudi.

Zitto ambaye ni kiongozi mkuu wa Chama cha ACT –Wazalendo, alisema serikali imekuwa ikishindwa kusimamia ushauri inaopewa na wabunge, akitolea mfano wa alichokieleza bungeni wakati wa mkutano wa bajeti mwaka jana kuhusu umuhimu wa kulindwa viwanda vya ndani.

Alikuwa akichangia hoja ya makadirio ya bajeti ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji iliyowasilishwa bungeni jana na Waziri Charles Mwijage.

“Wito wangu kwenye hili bado ni uleule, naamini ni muhimu mno kuhakikisha tunaweka utaratibu wa kisera na kisheria wa kulinda bidhaa zetu za ndan. Bado nasisitiza kuwa Serikali iendelee na juhudi za kuhakikisha kuwa tunaongeza uzalishaji wa mafuta ya kula nchini,” alisema.

Amesema amekuwa akihimiza viwanda vilivyopo nchini kulindwa na njia nzuri zaidi ya kutekeleza hilo, hususan kwa viwanda vya mafuta ya kula, ni kuzuia uagizaji wa mafuta ya kula kutoka nje ya nchi. “Uzuiaji huu utasisimua uzalishaji wa ndani wa mafuta ya kula, hasa mafuta ya mawese na alizeti,” amesema.

“Kasi ya kulinda viwanda vyetu hivi, inapaswa iwe kubwa na ya haraka sana, bado kuna maeneo yamefichika sana, tukiyakalia kimya kwa sasa madhara yake kwa nchi ni makubwa. Mfano mzuri ni bidhaa ya betri. Kuna smuggling (uingizaji wa bila kulipa kodi/magendo) kubwa ya betri kutoka nje na kuathiri kabisa hata mauzo ya ndani ya viwanda vya betri vilivyopo nchini,” amesema Zitto.

Amegusia kiwanda cha betri cha Panasonic alichosema kimeathiriwa mno na uingizwaji wa betri kutoka nchi za Asia wakati betri hizo hazilipiwi kodi hivyo bei yake kuwa ndogo kuliko betri zinazozalishwa nchini.

Mwenendo huo umesababisha kiwanda cha Panasonic kuwa hatarini kufungwa, hatua itakayolazimu Watanzania wanaofanya kazi hapo kukosa ajira, bali pia na serikali itakosa mapato ya kodi yaliyokuwa yakipatikana kutokana na kiwanda hicho kuzalisha.

“Kwa mujibu wa takwimu kutoka Ofisi ya Takwimu ya China, mwaka 2016 jumla ya betri zenye thamani ya Dola milioni 36.5 (zaidi ya Sh. milioni 81) zililetwa Tanzania. Lakini kwa upande wa Tanzania, takwimu za TRA na TBS zinaonesha Tanzania iliagiza betri za thamani ya Dola milioni 5.3 tu (wastani wa Sh. bilioni 11) kutoka China,” amesema.

Zitto amesema mtindo huo unamaana kwamba zaidi ya asilimia 80 ya betri zinazoingizwa kutoka nchini China haziingizi kodi. Kwa upande mwingine, ina maana serikali inaruhusu bidhaa za ndani ya nchi kunyimwa fursa ya ushindani wa haki na bidhaa zinazotoka nje ambazo hazilipiwi kodi.

“Jambo hili lina athari kubwa sana kwa Taifa, hasa kwenye mapato ya kodi yanayopotea. Lakini wanaoathirika zaidi ni wazalishaji wa ndani wa betri. Maana bei za bidhaa za magendo ni pungufu zaidi, na hivyo huleta ushindani zaidi kwenye soko,” amesema Zitto ambaye amehimiza ujenzi wa viwanda vipya kwa vile vilivyojengwa zamani haviendesheki mpaka kwanza mifumo yake ya uzalishaji ibadilishwe kutokana na teknnolojia ya sasa.

Nape Nnauye Afunguka Kuhusu Ukimya wa Kinana, Mwenendo wa Shughuli za Bunge Pamoja Polisi Kutumia Nguvu Kubwa

0
0
Na Regina Mkonde
Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye amefunguka kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo, ukimya wa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, muenendo wa shughuli za Bunge pamoja na tukio lililotokea hivi karibuni la Askari Polisi mmoja wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kufyatua risasi hewani mbele ya aliyekuwa Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima baada ya kutokea majibizano yaliyosababishwa na dereva wa Malima kuegesha gari vibaya.

Nape amefunguka hayo jana  jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na wanahabari ambapo alisema, Kinana ambaye baadhi ya watu wanadai kuwa ukimya wake umetokana na kujiuzulu, yuko katika wadhifa wake wa ukatibu mkuu na anaendelea kufanya kazi za chama.

“Mimi sio msemaji wa chama, lakini Katibu Mkuu yupo na anafanya kazi yake kama kawaida…., mimi bado ni mwanachama na muumini mzuri wa CCM inayopenda haki, na nina amini hiki ndicho chama pekee bora kitakachoweza kuwakomboa watanzania pamoja na kuamiwa ikiwa kitatekeleza mkataba wake na wananchi ambao ni wa kutimiza ahadi zake ilizo ziahidi,” alisema.

Kuhusu tukio la Askari Polisi kufyatua risasi hewani, ambalo Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamanda Simon Sirro alisema ulikuwa uamuzi wa busara wa kuondoa taharuki katika tukio hilo, na mbinu ya kuwatia nguvuni watuhumiwa.

Nape alishauri vyombo vya dola kutotumia nguvu kwani kitendo hicho kitajenga hofu na chuki baina ya serikali na wananchi na hata kwa chama tawala CCM, huku akiisihi serikali kuondoa vitendo vinavyotia hofu wananchi.

“Ni vizuri vyombo vya dola vikatimiza majukumu yake kwa kuwa ni vyombo vya wananchi, si vizuri vikitumia nguvu kubwa pale isipostahili. Ifikie hatua raia asiye na silaha Polisi wasitumie nguvu kushughulika naye kwa kutumia silaha. Nimeona ile video ikionyesha Malima alikuwa anauliza chanzo cha tatizo,” alisema na kuongeza.

“Kuna nchi tamaduni zake ni kutumia mabavu na nyingine zinatumia demokrasia, nchi yetu utamaduni wake si wa kutumia nguvu, tumezoea kuelewana kwa mazungumzo. Vyombo vya dola visitumie nguvu kwa kuwa tunajenga usugu usio na maana. Na kama kuna mazingira hatarishi basi nguvu itumike.”

Kuhusu mienendo ya shughuli za Wabunge Bungeni, aliwataka wabunge kutekeleza majukumu yao ikiwemo kuwawakilisha na kusimamia vema masilahi ya wananchi wanaowawakilisha, pamoja na kuisimamia serikali kutekeleza vizuri majukumu yake.

“Bunge ni mkutano wa wananchi, na wabunge wapo kwa niaba ya wananchi katika kupitisha na kushauri mipango ya serikali. Ni vizuri wasimame katika maeneo yao, wasiwe wapiga makofi, pale serikali inapofanya vizuri ipongezwe na inapofanya vibaya ikosolewe,” alisema.

Kuhusu Uhuru wa Vyombo vya Habari, alisema ifikie hatua wananasiasa wawe na ngozi ngumu ya kuvumilia kukosolewa  na watu kupitia vyombo vya habari. Pia ameshauri wananchi wanaotaka maonesho ya vikao vya bunge moja kwa moja, kuuomba mhimili huo kubadilisha sheria zake ambazo zimeipa mamlaka ya kuamua namna ya kuendesha shughuli zake.

“Naamini uamuzi wa siku ile wa kuzuia shughuli za bunge live ulikuwa sahihi sababu sheria zinasema Bunge litaendeshwa kwa sheria zake. Wananchi wanaozungumzia Bunge live, waliombe libadilishe sheria zake ili lianze kuonyeshwa live,” alisema

Nimekuta Chupi ya Mke Wangu Chumbani Kwa Mdogo Wangu wa Kiume

0
0
Jamani Leo ni Siku ya saba tangia nikute chupi ya mke wangu chumbani kwa mdogo wangu wa kiume,nimekaa nalo moyoni naona niwashikirikishe wenzangu nione mnishauri nini
Ni hivi Ninaishi na mke wangu,mwaka wa NNE sasa,tuna mtoto mmoja,nina Mdogo wangu,anaishi hapa tangia January niliponunua bajaj ili awe anaendesha ili kusaidia wazazi wetu nyumbani kijijini,sasa jumapili iliyopita Wife aliwahi sana asubuhi kwenda kanisani pamoja na mtoto, Mimi nilibaki nimejilaza mpaka kama SAA moja na nusu Hivi, nilivyokumbuka kuwa nilikuwa na Ahadi Fulani, katika kufanya maandalizi sikiweza kuiona pass, so nikaenda straight chumbani kwa dogo katika kuitafuta ndo nilipo kutana na chupi ya mke wangu, ambayo Mimi mwenyewe nilimununulia so imechoka choka kiasi chake,nilishikwa na butwaa kwani namwamini sana wife, dogo mwenyewe heshima kwa sana, nilichukua simu na kupiga picha kadha na kuzificha kwenye private vault, ile chupi nikaaicha palepale, wife hajasema chochote mpaka sasa, nawaza namna ya kuanza kumuulizia japo ameshahisi kuwa siko normal,coz nikimuona usoni nakuata hasira imepnada sana,kwa kifupi naogopa ukweli kuwa mke wangu amenisaliti kwa mdogo wangu,mpaka sasa simuoni kama mke wangu tena, namuona kama bundi kajificha chumbani kwangu, naomba mnishauri kwani Mimi kwa haraka haraka naona nimwite kaka yake aje amchukue kabla sijamfanya kitu mbaya, tatizo hasira zangu hupanda pole pole sana, kuzishusha ni kazi sana

By Shonkoso

Lulu Amber Agoma Katu Katu Kufuta Tatuu ya Young D

0
0

VIDEO Queen anayesumbua Bongo, Lulu Augen ‘Amber Lulu’ ameweka wazi kuwa, pamoja na kwamba kwa sasa msanii wa Bongo Fleva, David Genzi ‘Young D’ hana mpango naye, hatafuta tatuu yake kwa kuwa inabaki kama kumbukumbu maishani kwake.

Akizungumza na Story Mix, Amber anayefanya pia Muziki wa Bongo Fleva akiwa na Ngoma ya Watakoma alisema, tatuu hiyo yenye jina la Young D iliopo upande wake wa kushoto ni kumbukumbu tosha ya maisha yake. “Sina mpango wa kuifuta tatuu ya mwanaume niliyempenda, hata mwanaume ajaye atalazimika kulifahamu hilo, siwezi kuifuta eti kisa hanitaki, hii itabaki mwilini mwangu daima,” alisema Amber Lulu.

Na Ally Katalambula/GPL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images