Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Serengeti Boy aliyeifunga Angola kachunguzwa kama anatumia dawa za kuongeza nguvu

$
0
0

Vichwa vya habari jana na leo ni kuhusu Tanzania kuishinda Angola kwenye michuano ya soka la wenye umri chini ya miaka 17 huko Gabon na nyingine ni kuhusu Mchezaji wa Serengeti Boys baada ya hiyo mechi kudaiwa kupimwa na CAF kama alitumia dawa za kuongeza nguvu.
Abdul Hamis Selemani aliyeifungia Serengeti Boys goli la pili ambae pia alitajwa kuwa Mchezaji bora wa mechi ndio aliripotiwa kuwa alichukuliwa kwenda kupimwa kwa kushukiwa kuwa alitumia dawa za kuongeza nguvu kutokana na uwezo wake mkubwa aliouonyesha kwenye hiyo game vs Angola licha ya kutoka majeruhi.


Afisa habari wa TFF Alfred Lucas amesema “Niwatoe shaka Watanzania kwamba kuchukuliwa vipimo kujua kama Mchezaji katumia dawa za kusisimua misuli au la ni utaratibu wa kawaida“ 


‘Daktari husika wa mchezo anaesimamia ni lazima kila mwisho wa mchezo achukue vijana wawili wa kila timu akawapime ili ajiridhishe kwenye kuandika ripoti yake kama ambavyo Mwamuzi na Wasimamizi wengine wanavyoandika ripoti zao

UKWELI Mchungu..Wadada Mliozaliwa 80's na Hujaolewa Huu Sio Muda wa Kuchagua Tena..!!!

$
0
0

Kama kichwa kinavyojieleza wadada mliozaliwa 80's kama bado hujaolewa huu tena sio muda wa kuchagua wa kukuoa.

Kama ni mechi wanasema fungulia mbwa...yani sagula sagula..ngoma nagwaaa..jua lishakuchwaa...we olewa tu mengine yatajulikana mbele ya safari. Sasa we jitie yes no nyingi.. Utazeeka na kujipaka miwanja ya usoni kwa staili ya "mwenzenu sina mume".

Kwa wasiojua staili ya wanja ya "mwenzenu sina mume "ni ile staili ya wadada kunyoa nyusi zoote halafu unapaka wanja juu kidogo ya mstari wa nyusi.

MAMBO 5 ya Kuzingatia Wakati wa Kumlisha Mtoto..!!!

$
0
0

Ukweli ni kwamba familia nyingi kwa sasa zimekuwa zikiishi na kinadada wa kazi (house girl) ambao ndio kwa kiasi kikubwa wamekuwa wakishiriki katika kuwatunza watoto nyumbani na kuhakikisha wanakula vizuri na kushinda katika hali ya usalama.

Hivyo ninayofuraha kukumbusha wewe mzazi pamoja na dada wa nyumbani au mlezi mambo haya machache ya kuzingatia katika kuhakikisha usalama wa mtoto wakati wa kula;

1. Jambo la kwanza hakikisha haumuachi mtoto mdogo na chakula au kinywaji bila uangalizi hata kama ni maziwa ya chupa, kama utasahau na kumuacha mtoto katika hali hiyo huweza kusababisha mtoto akapaliwa.

2. Pia usimpe mtoto chakula au maziwa akiwa amelala, analia au anacheka huweza kusababisha mtoto kupaliwa.


3. Epuka kumpa chakula ambacho kinaweza kumkaba au kumpalia hususani karanga, mahindi, zabibu n.k


4. Kabla ya kumpa mtoto chakula hakikisha umekiangalia joto lake usije ukamuunguza mdomo.


5. Mbali na hayo yote, pia usafi wa mtayarishaji, mlishaji na mlishwaji (mtoto) ni muhimu sana katika afya ya mtoto.

HIZI Hapa Faida za Kula Ndizi Kila Siku Kama Unataka Kuwa Mwanaume wa Ukweli..!!!

$
0
0

Ndizi ni mojawapo ya tunda lenye ladha nzuri na limekuwa likipendwa na watu kutokana na ladha yake hiyo.

Aidha ndizi imekuwa likisifika sana kwa faida zake za kiafya, japokuwa si wengi wanazifahamu kwani wengi hulichukulia kama tunda la kawaida tu.

Hata hivyo ni vyema ikafahamika kuwa tunda hili ni nzuri sana kwa wanaume kutokana na kuwa na uwezo mzuri wa kuboresha masuala ya uzazi kwa jinsia hiyo.

Ndizi ni nzuri sana katika kuboresha mbegu za kiume na kuongeza uwezo wa kufanya tendo hilo vizuri na kwa muda, hivyo ni vizuri kujenga utaratibu wa kula tunda hili mara kwa mara ili kupata faida zaidi.

Ndani ya ndizi kuna virutubisho muhimu kama 'potassium' ambayo husaidia sana kuongeza kiwango cha mbegu kwa wanaume.

Pamoja na hayo ikiwa utaona unamuda mrefu kwenye ndoa na hujafanikiwa kupata mtoto ni vizuri ukafanya utaratibu wa kuwaona wataalam kwa ushauri zaidi

HIZI Hapa Faida za Mwanaume Kula Parachichi Kila Siku..!!

$
0
0

Wanaume wengi wamekuwa wakisumbuliwa na tatizo la kutokwa na vipele mara tu baada ya kunyoa ndevu zao.

Mbaya zaidi asilimia kubwa ya wanaume wamekuwa wakishindwa kujua nini cha kufanya ili kuondoa tatizo hilo ambalo pia huharibu muonekanano wa mhusika.

Hapa napenda kukueleza kuwa tunda la parachichi nalo huweza kuondoa tatizo hilo au kupunguza madhara kwa mtu mwenye shida hiyo.

Jambo la kufanya ni kupata tunda hili fresh kisha limenye na baadaye kulisaga halafu utalitumia mara tu baada ya kunyoa ndevu zako kwa kupaka rojorojo hilo la parachichi sehemu zote za kidevu yaani hii unaweza kuiita 'after shave ya asili'.

Tunda hili la parachichi linauwezo wa kuondoa tatizo hilikutokana na kuwa mafuta mazuri kwa ngozi ambayo pia husaidia kufanya ngozi kuteleza na kuwa laini na yenye afya.

BAADA ya Ben pol Kusambaza Picha Zake za Utupu Mitandaoni..Fid Q Aibuka na Kauli Hizi..!!!

$
0
0

Msanii mkongwe wa muziki wa hip hop Fid Q ambaye anadaiwa kuwa mshauri mkuu wa Ben Pol katika shughuli za muziki amefunguka kuzungumzia ishu ya muimbaji huyo kupiga picha za utupu na kusambaza mtandaoni.

Mapema jana mkali huyo wa wimbo ‘Phone’, kupitia mtandao wa Instagram alipost picha zikimuonyesha sehemu zake za mwili ambazo hazipaswi kuonekana wazi.

Akiongea Ijumaa hii katika kipindi cha U-Heard cha Clouds FM, Fid Q amedai hajashauriana na Ben Pol kuhusu picha hizo zinazosambaa mtandaoni na hajui chochote kinachoendelea.

“Sijajua anataka kuongelea nini kwenye ile cover na mimi nasubiria kuangalia nini kitatokea, siwezi kusema ni kitu kibaya au kizuri kwa sababu sijajua nini anataka kufanya” alisema Fid Q.

Aliongeza, “Kwahiyo hata mimi sijui ana maana gani ndio maana nikasema tusubirie tuona ana kitu gani anakuja nacho ndipo tuanze kuzungumza kwamba ni ishu mbaya au nzuri,”

Pia rapa huyo amewataka wasanii kufuata maadili ya kazi zao kwa kuwa wasanii wakongwe waliweza kufanya muziki mzuri na kuwashawishi wazee kuamini muziki sio uhuni.

“Nijaribu kuwakumbusha wasanii kwamba muziki sio uhuni, tumeweza kuwashawishi wazee wetu kuamini muziki wetu sio uhuni ndiyo maana mpaka leo umeweza kufika hapa. Kwahiyo mimi ningesema wasanii wanatakiwa kufanya kazi nzuri ambazo zitaweza kuwafanya wao kufanya vizuri zaidi,”

Wadau mbalimbali katika mitandao ya kijamii wamepinga tukio hilo huku wakidai muimbaji huyo sio msanii na matukio hayo.

SIKU Chcahe Baada ya Wema Kuonekana na Diamond Kwenye Party..Zari Aibuka na Hili Juu ya Mahusiano Yake na Diamond..!!!

$
0
0

Ikiwa imepita wiki kwa sumbaa picha zikimuonesha wema na Diamond wapo kwenye party ya Meneja wa Diamond, Zari akapost picha ya kutaka tumuombee ex- wake Ivan apone kwani anaumwa na amelazwa katika hospital moja huko Afrika Kusini

Hatimaye leo Zari ameamua kuweka wazi kuwa yeye na mpenzi wake Diamond mambo kwao ni safi tu. Zari amepost picha akiwa na baby daddy wake huyo kupitia Instagram zikiwa ni throwback ya picha za arobaini ya mtoto wao wa pili Nillan.

Siku chache zilizopita Wema Sepetu Naye alimjibu shabiki yake kuwa yeye na Diamond hakuna kitu na kwamba watu wamuombee apate mume bora na sio bora mume.

MARAIS wa Nchi za Afrika Mashariki Kukutana Leo Ikulu Dar Es Salaam..!!!

$
0
0

Wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wanatarajia kufanya mazungumzo ya pamoja katika  mkutano wa kawaida wa  18 utakaofanyika leo (Jumamosi), Ikulu jijini hapa. 

Mkutano huo unatarajiwa kupokea  ripoti ya usuluhishi ya kamati inayoongozwa na Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa kuhusu mgogoro wa Burundi.

 Mambo mengine yatakayozungumzwa katika mkutano huo ni pamoja na taarifa na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa katika mkutano wa 17 wa wakuu wa nchi za Jumuiya hiyo.

 Masuala hayo ni pamoja na namna ya kuwezesha uundaji wa magari katika   Jumuiya ya Afrika Mashariki na kupunguza uagizaji wa magari yaliyotumika kutoka nje ya Jumuiya, mapitio kuhusu sekta ya nguo na ngozi.

Masuala mengine ni pamoja na  kuzuia ama kuondoa uagizaji wa nguo na viatu vya mtumba kutoka nje.

Wakuu hao wa Nchi pia wanatarajia kujadili namna endelevu ya uchangiaji wa bajeti ya Jumuiya hiyo kwa nchi wananchama.

MAYANGA Aita Kikosi cha Stars kwa Mchezo Dhidi la Lesotho wa Kuwania Kufuzu Afcon..!!

$
0
0

Kocha mkuu wa timu ya Taifa Stars, Salum Mayanga ametangaza kikosi chake kwa ajili ya mechi ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi ya Lesotho mwezi ujao June 10 – 2017.

Taifa Stars itaendelea kuongozwa na nahodha wake Mbwana Samatta ambaye anakipiga nchini Ubelgiji katika klabu ya KRC Genk.

Makipa;
Aishi Manula (Azam), Benno Kakolanya (Yanga) na Said Mohammed (Mtibwa Sugar).

Mabeki;
Shomari Kapombe (Azam), Hassan Kessy (Yanga), Mohammed Hussein ‘Zimbwe Jr’ (Simba), Mwinyi Haji, Salim Mbonde (Mtibwa Sugar), Abdi Banda (Simba) na Erasto Nyoni (Azam ).

Viungo;
Himid Mao (Azam), Jonas Mkude (Simba), Said Ndemla (Simba), Muzamiru Yassin (Simba), Simon Msuva (Yanga), Shiza Kichuya (Simba), Farid Mussa (Tennerife, Hispania) na Abubakar Salum ( Azam)

Washambuliaji;
Mbwana Samatta (KRC Genk, Ubelgiji), Thomas Ulimwengu (AFC Eskilstuna, Sweden), Ibrahim Ajibu (Simba), Mbarak Yussuf (Kagera Sugar) na Abdulrahman Mussa (Ruvu Shooting),

LINAH Kama Diamond..Makampuni Yajitokeza Kumdhamini Mtoto Wake ..!!!

$
0
0

Wakati watoto wa mwanamuziki Diamond Platnumz wakiwa mabalozi wa maduka ya nguo za watoto, mwanamuziki  Linah Sanga anayetarajia kujifungua hivi karibuni amepata ubalozi wa duka la nguo za watoto.

Linah ambaye ni mwanamziki wa nyimbo za kizazi kipya amepata dili hilo la kuwa balozi wa duka la nguo za watoto la Kids City Shopping (KCS), zikiwa zimebaki wiki chache kabla ya kujifungua mtoto wake wa kwanza.

Linah ambaye mapema wiki hii alitambulisha herufi ya mwanzo ya jina la mtoto anayemtarajia baada ya kuweka picha ya ujauzito kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuandika ‘Baby T on the way’,anakuwa miongoni mwa mastaa ambao watoto wao wamepata bahati ya kuwa mabalozi.

“Kwa mara ya kwanza nitazungumza na mashabiki wangu mwishoni mwa wiki hii kwa niaba ya KCS ambao ni  wauzaji wa bidhaa mbalimbali za watoto na akinamama wajawazito,” amesema Linah.

Hivi karibuni Linah alizindua wimbo wake mpya ‘Upweke’ na kupita katika vituo mbalimbali vya redio, televisheni na magazeti kwa ajili ya kuutangaza wimbo wake huo mpya.

Mwanadada huyo ambaye hivi karibuni alimtangaza mpenzi wake anayetarajia kuwa baba wa mtoto wake aitwaye Shabani ambaye pia ni bosi wake, Linah amedai kuwa anafuraha kuwa mjamzito kwa kuwa ni kitu ambacho alikuwa akitamani kwa muda mrefu.

“Ninafuraha kubwa kwa sababu ni kitu ambacho kama mwanamke nilikuwa nakitamani siku zote kwamba na mimi nije niitwe mama, nafuraha nimepata mtu sahihi wa kuwa mzazi mwenzangu ambaye nitalea naye watoto,”amesema.

Mzazi mwenzake ambaye pia ni mkurugenzi wa Kampuni Drops Up Entertainment ambayo inamsimamia Linah, amesema wamejipanga kuhakikisha Linah anafika mbali zaidi kimziki.


BASHITE Avutiwa Pumzi...Hbari Vichwa vya Magazeti y Leo Jumamosi 20/5/2017..!!!

CAG Mstaafu Afunguka Mazito Kuhusu Ripoti Zake za Zamani...Aitupia Lawama Serikali ya JPM..!!!

$
0
0

Aliyekuwa Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh amesema mapendekezo yanayotolewa na CAG katika ripoti yake ya ukaguzi hayatekelezwi kikamilifu na watendaji wa serikali, jambo linalosababisha makosa hayo kujirudia na kusababisha upotevu mkubwa wa fedha za umma.

Utouh ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Uwajibikaji wa Umma ya Wajibu (WIPA), amesema kwa mamlaka za serikali za mitaa pekee, CAG alitoa mapendekezo 79, kati ya hayo ni matatu tu sawa na asilimia 4 ndiyo yalitekelezwa wakati asilimia 44 yalikuwa kwenye utekelezaji na asilimia 52 hayakutekelezwa kabisa.

Utouh amesema watendaji wa Serikali wamekuwa wakipuuzia mapendekezo hayo kwa sababu hawawajibishwi kwa makosa yao.

Mkurugenzi huyo amesema hata miongozo inayotolewa na Kamati za Bunge za Hesabu za Serikali (PAC) na Serikali za Mitaa (LAAC) haitekelezwi hata pale kunapobainika makosa ya wazi.

"Mwaka wa fedha uliopita, kamati ya LAAC ilitoa miongozo 1,094 kwa mamlaka za serikali za mitaa, miongozo 438 sawa na asilimia 40 yalitekelezwa, 230 sawa na asilimia 21 yalikuwa katika hatua za utekelezaji na 427 sawa na asilimia 39 hayakutekelezwa kabisa," amesema Profesa Utouh

RAIS Mpya wa Ufaransa Atangaza Vita Nchini Mali..Aaapa Kutorudi Nyuma Hadi Kieleweke..!!!

$
0
0

Rais Emmanuel Macron amefanya ziara ya kwanza katika bara la Afrika kwa kuitembelea Mali ambako amesema Ufaransa haitarudi nyuma katika vita dhidi ya magaidi na wapiganaji wengine wa kijihadi katika nchi hiyo na eneo la Sahel.

Macron alitoa kauli hiyo jana baada ya kuwatembelea wanajeshi wa Ufaransa katika kambi yao ya Gao, kaskazini mwa nchi hiyo, ambako wanaisaidia Mali kurejesha hali ya utulivu na amani. Ufaransa imewatuma wanajeshi wake 1,600 kaskazini mwa Mali kupambana na magaidi.

Huku akiwa na mwenyeji wake Rais Ibrahim Boubacar Keita, Macron alisema mbali ya Ufaransa, Ujerumani pia itaendelea kuhakikisha kuwa magaidi hao wanashindwa. “Ujerumani wapo nasi katika operesheni hizi,” alisema.

Aidha, amesema kuwa ushirikiano wa Ufaransa na Ujerumani ni muhimu sana barani Ulaya katika masuala ya usalama lakini pia kulisaidia bara la Afrika.

GAMBO: Mnaotaka Kutoa Rambirambi Mfuate Utaratibu..!!!

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amewataka wananchi na taasisi zinazoendelea kutoa rambirambi kwa familia za wanafunzi waliofariki katika ajali ya basi la wanafunzi wa Shule ya Lucky Vincent kufuata taratibu zilizowekwa ili kuepusha migongano isiyo ya lazima.

Kauli hiyo imekuja wakati jeshi la polisi mkoani Arusha likiendelea kuwahoji Meya wa jiji la Arusha Kalst Lazaro na watu wengine wanne kuhusiana na tuhuma za kutengeneza mkusanyiko usio na kibali serikali wakati wa kwenda kutoa rambirambi katika shule hiyo.

Gambo amesema masuala ya fedha yana changamoto na yasiposimamiwa vizuri lengo tarajiwa haliwezi kutimia, na kwamba serikali itaendelea kuwadhibiti wote watakaotaka kuingiza siasa kwenye majanga likiwemo la vifo vya wanafunzi.

RAIS Magufuli Kumkabidhi Museveni Uenyekiti EAC Leo Hii..!!!

$
0
0

Rais John Magufuli  leo Jumamosi ya Mei 20, 2017 katika mkutano wa 18 wa Wakuu wa Nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)anatarajiwa kumkabidhi kijiti cha uenyekiti wa jumuiya hiyo Rais wa Uganda, Yoweli Museveni baada ya Tanzania kuingoza EAC kwa vipindi viwili mfululizo.

Hayo yamesemwa jana Mei, 19 na Waziri wa Mambo ya Nje, Balozi Augustine Mahiga katika Mkutano wa 34 wa Baraza la Mawaziri la EAC, ambapo alieleza mafanikio yaliyopatikana katika kipindi ambacho Tanzania iliiongoza jumuiya hiyo, ikiwemo kuridhia maombi ya muda mrefu ya uanachama, ya nchi ya Jamhuri ya Sudan Kusini na kuipatia uanachama kamili wa jumuiya hiyo.

“Tanzania tumemaliza muda wetu baada ya kuiongoza vipindi viwili mfululizo, Rais Magufuli Jumamosi atamkabidhi uenyekiti Rais Museveni wa Uganda,” alisema.

Alieleza kuwa, pamoja na Rais Magufuli kukabidhi kijiti hicho kwa Museveni, Rais Mstaafu Benjamin Mkapa anatarajiwa pia katika mkutano huo kuwasilisha ripoti ya mazungumzo ya pamoja ya kuleta amani, ikiwa ni utekelezaji wa agizo la wakuu wa nchi wa EAC lililotolewa mwezi Januari,2017.  

Kuhusu mkutano wa Baraza la Mawaziri wa EAC uliofanyika jana Mei 18, 2017, alisema wajumbe wa baraza hilo watajadili ushirikiano wa masuala mbalimbali yanayohusu jumuiya hiyo, ikiwemo ushirikiano kibiashara, uwekezaji, elimu pamoja na huduma mbalimbali za kuendesha nchi wanachama hasa ujenzi wa miundombinu na uchukuzi.

“Kwanza Tanzania itatoa ripoti ya ushirikiano kwa kipindi cha miaka miwili iliyoiongoza EAC ikiwemo ya ushirikiano kibiashara, kielimu na huduma za kuendesha nchi,” alisema.

Alisema wajumbe hao watajadili namna ya kuondoa na au kupunguza vikwazo visivyo vya kisheria hasa vinavyokwamisha biashara ikiwemo ushuru wa forodha, vizuizi vya magari, aina za biashara, na kwamba watajadili namna ya kuanzisha soko imara la pamoja.

“Kuna vikwazo visivyo vya lazima vinavyokwamisha biashara kwa nchi wananchama, mfano Tanzania tuna vyombo viwili vinavyopima ubora wa bidhaa, TBS na TFDA ambapo wenzetu wanasema ngazi hizi mbili zinazuia biashara zao, kwa hiyo tutazungumzia suala hili. Pia tutajadili namna ya kutekeleza lengo letu la kuzuia uingizwaji wa nguo za mitumba kutoka nchi za nje ya jumuiya hii,” alisema.

Kwa upande wa elimu, Balozi Mahiga alisema wajumbe hao watajadili namna ya kuanzisha mfumo wa elimu ambao utasaidia kuondoa tofauti ya upatikanaji elimu katika vyuo vya EAC ikiwemo wanafunzi wa jumuiya hiyo kupata elimu kwa malipo na vigezo vinavyo fanana na kwamba kusiwepo na vikwazo.

“Tulikuwa na chuo kimoja tu cha jumuiya, lakini sasa tuna vyuo tanzu katika nchi ya Tanzania, Kenya na Uganda kwa hiyo kuna umuhimu wa kuwa na mfumo wa elimu kwa wanafunzi kupata elimu kwa malipo na vigezo vinavyofanana. Mwanafunzi wa Tanzania akienda Kenya asome kwa vigezo na gharama ileile anayolipa mwanafunzi wa Kenya,” alisema.

KUTANA NA SHEKH SHARIFU SIMBA Mtabibu wa Nyota na Tiba za Asili Tanzania na Duniani Kote

$
0
0

KUTANA NA SHEKH SHARIFU SIMBA mtabibu wa nyota Tanzania na duniani kote,

✨SHEKH SHARIFU SIMBA anatoa shukrani kwa wote mnaopiga simu mlioko ndani na nje ya Tanzania, wanatoa shukrani na wale wenye matatizo, pia anawashukuru wote wanaomshirikisha na kutoa shuhuda jinsi tiba zake zinavyo wasaidia.
✨Bado ujachelewa piga simu na uweze kusaidiwa, SHEKH SHARIFU SIMBA yupo kwaajili ya kutatua matatizo yote yanayo wakabiki wanadamu,

🦅SHEKH SHARIFU SIMBA ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili anatumia kitabu cha QUR'AN, dawa za asili, dawa za kiarabu na majini,

✨je umeachwa na Mme/ mke, mchumba au umpenzi wako? SHEKH SHARIFU SIMBA anauwezo wa kurejesha mahusiano yako ndani ya masaa (72)
✨je umahangaika kupata mtoto bila mafanikio?
✨je mikosi inakuandama na umekuwa mtu wa kilia kila siku bila kupata msaada wowote?
✨je madeni yanakuandama?
✨je umesimamishwa kazi au kushushwa cheo bila sababu? SHEKH SHARIFU SIMBA anatoa kisomo na kusafisha NYOTA na kung'arisha, ili ung'ae upya kwa kila mtu na mahali popote,
💍SHEKH SHARIFU SIMBA anatoa Pete za bahati zilizoambatana na jini Mali,
✨Anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume chango kwa kina mama, ngizi na n.k, pia anatibu miguu kuuma na kufa ganzi, tumbo kujaa gesi na kuunguruma na magongwa mengine ya siri,
🇺🇸pia anatibu kwa njia ya simu kwa wale walioko mbali au nje ya nchi,
📞SHEKH SHARIFU SIMBA anapatikana BAGAMOYO, kwa wale walio nje ya nchi tumia WhatsApp no +255 719361792, kwa wale wa ndani ya nchi piga simu no: 0719-361792 au 0689-476132 na 0745-281712.

MREMA: Tusiangaike na Mateja, Tukamate Mapapa..!!!

$
0
0

Mwenyekiti wa bodi ya Parole Taifa, Augustino Mrema ameliomba Jeshi la Polisi nchini kuacha kuhangaika na watumiaji wa madawa ya kulevya (mateja) wasiojiweza na kuwapeleka magereza bali wasaidiwe kwa kupelekwa vituo vya kuwasaidia waathirika wa dawa za kulevya.

Mrema aliyazungumza hayo leo katika kipindi cha East Africa Breakfast cha EA radio na kusisitiza, jeshi la polisi linapaswa kuhakikisha wanaowapeleka magereza wawe mapapa wa dawa za kulevya ambao ni chanzo cha mateja nchini.

Alisema kuwa kuwakamata na kuwapeleka Magereza mateja ni sababu moja wapo ya msongamano wa wafungwa pamoja na wanachi kupenda kesi na visasi kwa kushindwa kumalizana mitaani.

"Wananchi wamekuwa sababu ya misongamano magerezani kwani kesi nyingine ni ndogo za kuweza kumalizana nyumbani lakini wanaamua kukomoana kwa kupelekana polisi hadi kufikia kufungana," Alisema Mrema.

Watoto wa Mgombea Ubunge Eldoret-Kenya Watekwa na Kuuawa Kenya

$
0
0
Watoto 3 wa mgombea ubunge huko Eldoret Kenya ambao walikuwa wamepotea wamekutwa wameuawa na maiti zao kutupwa kwenye mto Nzoia. Watoto hao walipotea toka jumamosi iliyopita wakati wakitoka kanisani (Eldovil SDA Church).

Mgombea huyo ambaye watoto wake wameuawa anaitwa jina James Ratemo wa Jubilee.
Na mgombea Udiwani huko Machakos Thomas Minito amekutwa ameuawa na maiti take kutupwa Athi River huko machakos.

Ben Pol ni Shujaa Kupiga Picha Uchi - Dogo Janja

$
0
0
Baada ya msanii Ben Pol kupiga picha zenye ukakasi na kuzipost kwenye ukurasa wake wa Instgram rapa Dogo Janja ameibuka na kusema kuwa kitendo alichokifanya Ben Pol ni kitendo cha kishujaa sana kwani wengi hata yeye asingeweza kufanya jambo hilo.

Dogo Janja amesema hayo leo alipokuwa kwenye kipindi cha 5Selekt na kusema jambo hilo alilofanya Ben Pol linahitaji moyo na kusema inawezekana kwa sasa likawa na faida kwa msanii huyo ila athari ya kitendo hicho atakuja kuiona baadaye.

"Labda brother alijiuliza akivaaje atapendeza akaamua asivae kitu tu mbona freshi, lakini mimi sidhani kama nitaweza kufanya jambo kama lile kuwaonyesha watu 'Too much' hapana aisee, vitu kama vile vinaishi milele. unaweza kufanya leo ukapata maslahi lakini kesho kikawa na athari katika maisha yako" alisema Ben Pol

Siwezi Kumshauri Magufuli - Jay Moe

$
0
0
Rapa Jay Moe anasema kama akipata nafasi ya kukutana na Rais wa awamu ya tano Dkt. John Pombe Magufuli hataweza kumshauri jambo lolote kwa kuwa yule ni Rais wa nchi bali yeye atamuomba awafikirie wasanii na kuona umuhimu wao.

Jay Moe amesema hayo na kusisitiza wasanii walikuwa na mchango mkubwa katika uchaguzi uliopita ambao umesaidia viongozi wengi kuingia madarakani

"Nitamuomba Magufuli maana siwezi kumshauri yule ni Mh. Rais wa nchi bali nitamuomba atufikirie na aone umuhimu wetu, kwa sababu mchango wetu umetumika sana katika uchaguzi uliopita, tumeweza kwenda 'endorse' kuithinisha wagombea na vitu kama hivyo kwa hiyo waone kwamba imefika muda na wao kutoa shukrani kwa kile ambacho sisi tulikifanya kwa kufanikiwa kwao kushinda, matatizo yetu sisi wasanii yanajulikana tuna mfumo mbovu sana wa masoko, mzuki wetu mzuri lakini haujulikani utauzwa wapi nadhani kupitia serikali na idara zake kama COSOTA, BASATA, Waziri wanaweza wakakomaa wakaweka nguvu fulani" alisema Jay Moe  
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images