Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Jamani Kibamia Kitamu Asikwambie Mtu Looh!!!

$
0
0
Habari zenu wapendwa, 
Hapa nilipo niko nje ya bongo safari flani hv ya kizushi, na safari hiyo niko huku tangu mei mosi, saa bana ile ninefika tuu hotelini si mnajua mambo yetu yale, daaah nikanasa tundu bovu. Sass ile kufika ground play looh!!! Kila mtu kavaa jezi za game heee kumbe mwenzangu yeye mkulima wa bamia bana daah!! Nikataka kitoka nje ya ground play na kujisemea bora kukutana na mkulima wa mihogo kuliko bamia. Ila nataka kunyanyu mguu nitoke ulingoni si akanikamata bega, akaniwekea ulingoni bamia ya chukuchuku akachanganya na nyanya chungu, japo nyanya chungu ni chungu ila ziliongeza utamu kwenye bamia. Sasa basi sijakaa sawa akaniwwkea bamia la rosti lililochanganywa na bilinganya viazi ulaya pilipili hoho vitunguu maji na saumu karoti daaah wakati nakula poshi hilo la tatu nikamuuliza umeoa? Upishi huu wa bamia umeutoa wapi? Alinijibu kwa poshi la nne ambapo aliweka kunde bamia la kukatakata slices akachanganya na maharage mabichi na akaunga na karanga nilipomaliza kula pishi la nne sikuongea zaidi ya kulala kwa kuvimbiwa.
Jamani nawaasa msipendw kuhukumu kitu kwa kukiangalia kwa nje tuu angalia utendaji maana mie hapa tangu mei mosi nakula bamia kila siku na wala halinikinai. Play ground swadakta!!!!

Wanawake Hufurahishwa na Vitu Vidogo Vidogo Sana Hakuna Haja ya Gharama

$
0
0
kawaida mtu kutumia pesa nyingi labda kumpeleka mpenzi wake kwenye mahotel makubwa au kumnunulia vitu vya thamani ili kumuonyesha mapenzi, ila ukweli ni kwamba unaweza ukafanya hayo yote ukajiingiza kwenye gharama kubwa na matumizi usiyotarajia  bila mafaniko. Mwanamke haitaji vyote hivyo mwanamke anahitaji muda, tumia muda mwingi kuwa nae, muonyeshe unamjali, tatizo lake chukua liwe lako. Mpe kidogo ulicho nacho na kitoke moyoni, Usilazimishe mambo utamboa, fanya ajiamini ukiwa nae, kuwa na misimamo yako usiyumbe yumbe katika maamuzi, Usiogope kumwambia hisia zako kwake, kwani wanawake wanapenda mtu anayejiamini. Fanya hayo utaona matokeo yake..!! 

Je, Unadhani ni Kwanini Wanaume Wengi Hawawaridhishi Wanawake wao Katika Mapenzi?

$
0
0
Je, unadhani ni kwanini wanaume wengi wamekuwa wakishindwa kuwaridhisha wanawake wao katika mapenzi?

Nay wa Mitego Aongea Kuhusu Kusambaa kwa Picha ya Mchumba wake Akivishwa Pete na ‘Pedeshee’

$
0
0
Hatimaye Nay wa Mitego amezungumzia scandal iliyokuwa ikimhusu mchumba wake aitwaye Siwema ambaye mwezi uliopita ilisambaa video na picha kwenye mtandao wa Instagram inayomuonesha akivishwa pete na pedeshee.

Maelezo kuhusu video/picha hizi yalisema:

Siwema demu wa Nay Wa Mitego amevalishwa pete ya uchumba na jibaba ( pedeshee ) linalomuweka mjini na ndilo lililomnunulia magari mwanzo aina ya Verosa na baadaye Kluger halafu Verosa akampa Nay wa Mitego, sasa hivi kamnunulia Lexus harrier… Inasemekana Nay pia analelewa na huyo dingi maana amekubalije amegewe demu na kuhongwa gari alilohongwa demu wake.”

Pia kupitia mtandao huo, picha za msichana huyo zinazomuonesha akiwa nusu utupu zilisambaa.

Akiongea kwenye kipindi cha So So Fresh cha Clouds FM Ijumaa hii, Nay alisema ni kweli Siwema alimkosea lakini amemsamehe.

Mimi Siwema ni mwanamke ambaye nampenda kila mtu anafahamu maybe ndio maana ilikuja kuwa tatizo. Kuna vitu vilitokea mimi nilikuwa sifahamu kama nilivyosema kuna watu wakanifuata wenye nia zao sielewi mtu alikuwa na nia gani wakiviweka Instagram na kwenye mtandao. Mimi mwanamke wangu najua alinikosea. Sikujua kilichokuwa kinaendelea lakini hakuweka wazi. Ni kitu ambacho kilitokea kabla ya mimi kuwa naye lakini hakuwahi kuniambia kwamba kilitokea mpaka wakafikia hatua ya design hiyo, hilo ni kosa ambalo alinikosea. Tuliyamaliza, mimi ni gangster ambaye na nina mwanamke ambaye nampenda. Huwezi kumwacha mwanamke kwasababu ya kitu ambacho ni cha historia, sidhani kama ni fair. Pia ni mwanamke ambaye mimi nipo naye kwasababu tunapendana halafu ni mwanamke ambaye ananielewa na tunaelewana na ndio maana niliamua kumweka wazi kila mtu anamfahamu. Hata kama itakuwa vyovyote vile, siwezi kumwacha hata siku moja. Kweli ni kosa kubwa ambalo linahitaji moyo kwaajili ya kumsamehe mtu lakini naamini nimefunzwa kusamehe kwenye mahusiano, hili ni la kwanza acha lipite mwenyezi Mungu atusaidie tuendelee kudumu. Mimi nipo bado na Wema na maisha yanaendelea.”

Dida’s Fashion,Aliyekuwa Mke wa Ndoa wa Q Chillah Aelezea Sababu ya Kuachana Naye

$
0
0
Mwanadada Hadija Seif (Dida’s Fashion) aliyekuwa mke wa ndoa wa msanii wa muziki Q Chillah amefunguka kisa kilicho afanya waachane pamoja na jitihada alizozifanya kumnusuru msanii huyo na wimbi la matumizi ya madawa ya kulevya.

Akizungumza katika kipindi cha Mboni Show, akiwa nchini Uingereza, Dida alisema Q Chillah ndiye aliyemtumia ujumbe wa kumwacha.

“Nilimpigia simu akaniambia ‘najua wewe haupo Uingereza unanidanganya’ ,nikamwambia ‘nipo UK’,'akaniambia upo UK’? Hii code namba ya nchi gani?’, ‘nikamwambia kwani vipi?’Kuna muda kadi huwa zinatokea hivyo akakasirika akaniambia ‘upo kwa bwana yako’,nikamwambia ‘mimi siko huko’, nikawasiliana na baba yake mzee Katwila nikamwambia ‘baba, Q Chillah ananimbia hii namba siyo sahihi nifanyeje?’, baba yake mzee Katwila akaniambia ‘usiwe na wasiwasi mimi nitayamaliza’. Ile hasira yake akampigia mama yangu kwakuwa yeye anapatana sana mama yangu. Kwahiyo akaenda akamlilia mama yangu, akamwambia mimi nimetoka nimeenda kwa wanaume sijui kitu gani wakati mimi nilienda kumtafutia vitu kwajili ya show na vitu vyake mwenyewe. Kwahiyo akampigia simu mama ‘oooh mimi anifanyia dharau sijui nini mimi namuacha’ Mama yangu akamwambia ‘mbona unachukua jukumu la nani, kwasasa hujui mwenzako anafanya nini huko’. Akanitumia message sijui ‘mhuni unatoka UK sijui unaenda wapi bila kuniambia’, nikakubali kosa ‘nisamehe ila ongea na mzee akufahamishe vizuri’, akiniambia ‘sitaki tuongee na baba sitaki kufanya nini na wewe’ mwenyewe sitaki kukusikia’,basi hivyo ndivyo ilivyotokea,” alisema Dida.

Hata hivyo Dida amesema kwasasa hamwitaji tena kimapenzi Q Chillah ila anammiss kimazoea kwakuwa waliishi pamoja na kuzoeana.

Amedai alijitahidi sana kutuma pesa kwa Q Chillah ili zimsaidie kuachana na matumizi ya madawa wa kulevya. “Kuna watu nilikuwa nawapa pesa ili wampe Q Chillah aachane na matumizi ya madawa ya kulevya,ila sikutaka watu wamwambie kama nimetuma mimi, pia kuna watu wanadai eti mimi ndio nimesababisha Q Chillah atumie madawa,” alisema Dida ambaye kwa sasa anamiliki kampuni ya Dida Entertainment.

Ndoto "mpya" ya kakobe yaitesa ukawa!

$
0
0
 Kama ilivyo kawaida kwa askofu Kakobe kuota ndoto mbalimbali kuhusu mambo yanayohusu mstakabali wa taifa letu. Askofu Kakobe ameota ndoto nyingine ambayo inawahusu UKAWA na harakati zao za kudai katiba ya wananchi.

Katika ndoto hiyo ya askofu Kakobe ambayo ameitoa leo katika ibada ya jumapili kwenye kanisa lake, amesema kuwa, kutokana na hali ya ubaguzi uliokithiri kwenye upinzani kupitia umoja wao huo wa UKAWA, haoni kama kutakuwa na mafanikio yoyote ya malengo ya wana UKAWA.

Askofu Kakobe katika kufafanua alieleza kwamba, viongozi wa UKAWA hasa mhe Mbowe hakuwa sahihi katika maamuzi yake ya kuwatenga waasisi wa upinzani nchini, akimaanisha mhe Mrema. Hivyo, kitendo hicho cha ubaguzi kitaondoa baraka iliyokuwa imepandikizwa awali kwenye umoja huo.

My take,

Ni vyema sasa mhe Mbowe akachukua onyo hili na kufanya maamuzi sahihi ya kumuunganisha mhe Mrema na UKAWA. Kwa kuwa wote tunajua nguvu ya kiutabiri aliyonayo nabii Kakobe.

Wema aache umaarufu wa kubebwa na scandal.

$
0
0
MWENYEKITI wa Klabu ya Bongo Movie Unity,
Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ ameibuka na
kumuonya Wema Sepetu kupiga kazi na kuepuka
umaarufu bila kazi.
Nyerere amemtaka Wema aachane na skendo za
kila kukicha kwani hazina maana kama kazi ya
sanaa aliyoichagua kama njia ya kumuingizia
kipato.
“Kwanza nampongeza sana Diamond kwa tuzo
zote alizopata kwa kuwa alistahili lakini Wema
naye anapaswa kuiga mfano, vinginevyo atakuwa
maarufu bila ya heshima,” alisema Steve
Nyerere.

Stevie Nyerere Analazimisha Ustaa?

$
0
0
Huyu Stevie Nyerere mbona mwenzenu simuelewi,namuona tu na kimbelembele chake na kujikwezakweza aonekane na yeye yumo.Hivi anafanya kazi gani ya kuonekana inayomfanya ajione yumo kiasi hicho au fans wake ni kina nani?Naona kama muonekano wake unamkataza kabisa kuwa Celebrity ila yeye kama analazimisha hivi au?.

Binti Mrembo wa 1992 Akiri Kuwa na Mahusiano ya Kisagaji na Star wa Bongo Movies

$
0
0
Siwezi kumwacha, nikimwacha ntakufa” ni maneno makali kutoka kwa binti mdogo wa 1992 ambae amekiri kua yuko kwenye mahusiano sasa na binti mwenzake.
Chanzo cha habari kutoka ndani ya familia ya binti huyu (ambae jina tunalo) mkazi wa Arusha kinasema kua amekua akiaga nyumbani anakuja Dar Es Salaam kwa dada yake na kumbe anaishia kuwekwa kinyumba na msanii maarufu wa bongo movie ambae ameshutumiwa mara kadhaa na vyombo vya habari kua ni msagaji lakini hupinga swala hilo kwa macho makavu yasiyo na aibu.

Manchester City Win Premier League Title

$
0
0
Manchester City have won the Barclays Premier League title with a 2-0 defeat over West Ham United at home.

Goals either side of half-time from Samir Nasri and Vincent Kompany saw City capture the title with an easy victory.

Manuel Pellegrini's side led second-place Liverpool by only two points in the league heading into the match.

But their sizeable goal difference meant a draw against West Ham at Etihad Stadium would be enough to take the title

The title is Man City's second in three seasons.

For Liverpool, only victory over Newcastle United and a shock West Ham win could have seen them finish the season on top.

Liverpool trailed after an early own goal from Martin Skrtel, however two goals in the second half - from Daniel Agger and Daniel Sturridge - secured second place in the league.

Man City received a boost for their final match with the return of Argentine striker Sergio Aguero from a groin injury.

Aguero's return was the only change from the City side which beat Aston Villa 4-0 mid-week.

But it was Nasri who broke through West Ham's defences six minutes before the interval, taking aim from 20 yards with a powerful shot which went in off the post.

The goal was followed by another four minutes into the second half when Kompany struck home from six yards after Edin Dzeko won the ball from a corner.

Aguero had two chances to extend City's lead, but his header sailed wide at the near post and he later failed to score before an open goal from a Zabaleta cross.

In other key matches, Norwich City's relegation was confirmed after a 2-0 defeat to Arsenal.

Cardiff City also bowed out of the Premier League after a 2-1 defeat at the hands of Chelsea.

Tottenham secured a place in the Europa League for next season with a 3-0 win over Aston Villa.

Mwili wa Mtu Asiyejulikana Umeokotwa Mto Mzinga Kongowe

$
0
0
Kamera yetu leo hii imenasa mwili wa mtu mmoja ambaye hakufahamika jina lake ukielea ndani ya Mto Mzinga maeneo ya Kongowe jijini Dar es Salaam.

Mwili wa mtu huyo ulipatikana baada ya wakazi wa eneo hilo kudai kuwa harufu kali ilikuwa ikitoka eneo hilo na ndipo waligundua maiti hiyo ambayo waliikuta ikiwa imeharibika kwa kiasi kikubwa.

(Picha: Chande Abdallah/GPL)

Chris Brown Aongezewa siku 131 za Kukaa Jela

$
0
0
Uhuru wa Chris Brown kwa sasa bado ni ndoto sababu Ijumaa iliyopita (May 9) jaji wa mahakama ya Los Angeles alimhukumu mwimbaji huyo kifungo cha mwaka mmoja jela (siku 365), baada ya kukiri kuvunja masharti ya kesi yake ya kumpiga aliyekuwa mpenzi wake Rihanna mwaka 2009.

Jaji anayeisikiliza kesi hiyo, James R. Brandlin alimuondolea siku 234 za kifungo hicho ambazo tayari amezitumikia kwa kukaa rehab na jela, hivyo anatakiwa kumalizia siku 131 zilizobaki.

Breezy aliwekwa jela toka katikati ya March baada ya kuvunja sheria za rehab huko Malibu, alipoamriwa kukaa kwaajili ya matibabu ya kukabiliana na hasira.

Kesi zinazomkabili mwimbaji huyo wa R&B kwa kiasi flani zimeathiri muziki wake japo management yake inajitahidi kuendelea kutoa nyimbo mpya akiwa jela. Mwezi March aliachia video ya version ya tatu ya wimbo wake ‘Loyal’ aliyowashirikisha Lil Wayne na Tyga, na mwezi uliofuata (April 15) aliachia video ya moja ya nyimbo zitakazokuwepo katika album yake ya ‘X’, “Don’t Be Gone Too Long” aliomshirikisha Ariana Grande.

Mwezi February mwaka huu Brown alitangaza tarehe mpya ya album yake kutoka (May 5) ambayo imemkuta jela. Album hiyo imeahirishwa mara kwa mara toka mwaka jana kutokana na sababu mbalimbali.

“”X” is by far my best album yet…. Setting the date for MAY 5” hii ilikuwa tweet ya Breezy mwezi wa pili.

Mke kanisusia nyumba, kaniacha na house girl Huyu

$
0
0
Kaondoka siku tatu sasa zimepita. Simu hapokei wala hajibu sms, kaenda Kigamboni kwa rafiki yake.
Nimeongea na rafiki yake anasema mke wangu kaenda kubadilisha upepo.

Kama Ulikuwa Hujui Unaambiwa Ugomvi ni Afya kwenye Mapenzi..Soma Hapa

$
0
0
Ukimuuliza binti yeyote akutajie mambo 10 asiyopenda kusikia au kuyaona katika ndoa yake, mojawapo litakuwa ni ugomvi. Ugomvi unaumiza, kiakili na kimwili. Ugomvi si ustaarabu, zaidi sana ugomvi si haki !! Kuna ugomvi wa hoja, kuna ugomvi wa ngumi mbili tatu mambo yawe sawa, kuna ugomvi wa ukimya! Vyovyote uwavyo, ugomvi si neno jema, halina ladha kwa wapendanao!!!
....
Kama ulikuwa ukifikiria kuwa ugomvi katika mahusiano ni jambo baya basi umekosea sana! Kama ukikutana na wanandoa wakakuambia hawakuwahi kugombana au kutofautiana katika ndoa yao, ama wanakutania tu au wape pole! Ugomvi katika mahusiano una maana zifuatazo;
....
UGOMVI UNA MAANA MNAPENDANA
Wanasaikolojia Bruce na John katika kitabu chao cha Language of love, wanasema, kama wawili wanapendana kweli, lazima wagombane! Wanagombana kwa sababu kila mmoja anatetea sehemu ya pili isiende pengine, anailinda, anaionea wivu. Hivyo kugombana na pengine kugombezwa ni ushahidi kuwa ndani yenu mnahitajiana na mnapendana kwa hiari.
....
UGOMVI HUTIBU MATATIZO YA HISIA (HEALTHIER EMOTIONS)
Wanandoa/Wachumba wasiotofautiana na kugombana mara kadhaa basi ni wazi hisia za kimapenzi baina yao zinaumwa! Hapo kuna misongo ya mawazo, kuna kulimbikiza maudhi sio upole huo, kuna hasira inayosubiri kulipuka.. Upendo wenye afya huonekana kwa hisia za wazi.
....
KUGOMBANA NI KUONESHA KUJALI (CARE)
Hapa ntatofautiana wengi wanaofikiri kuwa kumjali mwenza ni kumtoa out, kumpa maua, kumnyoshea shati, kumpa zawadi, surprise n.k Kugombana ni zawadi ambayo wanandoa vijana wengi hawaijui uzuri wake. Kuwa na mahusiano yaliyopoa kabisa kuna gharama zake, wengi hushituka mambo yalishaharibika. Mwanasaikolojia George R. Bach na Peter Wyden katika kitabu chao cha 'How to fight fair in love' wanasema '...we have discovered that couples who fight together are couples who stay together- provided they know how to fight properly..." 
....
Ugomvi wa wachumba huhusu zaidi mavazi, simu, mwonekano, hitaji la watoto,namna ya kutumia starehe n.k 
Ugomvi wa wanandoa wengi huhusu zaidi pesa, watoto, wakwe, ndugu, majukumu, tendo la ndoa n.k
Ugomvi wa wanandoa wazee huhusu wajukuu, watoto wao wakubwa, ibaada n.k
....
TAHADHARI
Sijaruhusu kupigana makonde, unaweza kupigana na mwenza kwa kutumia akili nyingi pasipo kutumia nguvu nyingi. Ugomvi mzuri ni ule unaoleta suluhu mapema na usipigane kuwapa wengine faida.
Be brave!

Nisha Afunguka Sababu ya Kuachana na Ney wa Mitego Japo Alipenda Kuolewa Naye

$
0
0
Msanii wa maigizo Salama Jabu maarafu kama Nisha amefunguka na kueleza sababu kubwa iliyomfanya kusitisha penzi lake na mwanabongo flava Nay wa Mitego. Akiongea  Nisha alisema" Unajua Nay ndiye mwanaume pekee aliyefanikiwa kuuteka mtima wangu hadi leo hii sipata mwanaume anaejua mapenzi kama yeye lakini sasa nilikuwa napata shida sana kwake" Alisema Nisha Msanii huyo aliendelea kusema kuwa
" Unajua Nay kwenye maapenzi ni balaa anajua sana yani sikuamini kama ningekuja kuachana nae lakini kutokana na mazingira ya yule mtu sikuwa na jinsi nikaamua kumpigia chini" Alisema Hata hivyo Nisha alizitaja sababu kubwa  zilizopelekea kuchukua uamuzi huo ni pamoja na ukorofi wa mwanamuziki huyo pamoja na matusi matusi ndiyo maana alichukua maamuzi hayo magumu.

Haiwezekani Nataka Kupima DNA Nimestuka!! Wanangu Hawajafanana na Mimi

$
0
0
Mwenzenu jamani nahisi nmechakachuliwa,nina mke wangu tumezaa watoto wawili mmoja yuko na miaka mitano na wa pili miwili,kati yetu mimi na mke wangu nahisi kuna kitu kinaendelea na nimefanya uchunguzi wa kina na kuishia kwa majibu ambayo hayaniingii aklini na pili vilevile hawa watoto wanafanana exactly na watu ninao wahisi
Nkijaribu kurudisha hisia nyuma naona matukio yanafanana na mke wangu pia alikuwa amejipatia ujauzito kwenye mazingira ya kutatanisha,Huyu wa kwanza anafanana sana na boyfriend wake wa zamani ambaye mimi namjua!kipindi yuko mjamzito nilishawahi kumfuma na meseji kibao za mahapa na njemba hilo!
Huyu wa pili anafanana sana na Babu mmoja hapa mtaani kwetu anashona viatu
Huyu mara nyingi nmeshawahi kumkuta home anajisingizie kuja kuchukua viatu,mbaya zaidi hata huyu mtoto huyu mwwanamke anajitahidi sana kumjengea mazoea nae
Sasa naombeni ushauri jamani mm nifanye nini?

Staa wa Kike Bongo Atupia Mtandaoni Picha ya Utata..Je waweza Mtambua ni Nani?

$
0
0

NI STAA GANI HUYU?
Katika hali isiyokuwa ya kawaida na kushtua staa mmoja wa kike nchini anaejihusisha na ugizaji wa filamu za kibongo ameachia picha kimitego mtandai na kuzusha mjadala mzito. Habari za uhaika zilizoifikia mtandao huu zinasema kuwa picha hii imevujishwa makusudi mtandaoni ili wadau wapande dau, hata hivyo licha ya mtandao huu kuchunguza kwa kina ili kumtambua staa huyu lakini mambo yamekuwa magumu kutokana na kuficha uso wake.

Mrema Aiombea heri Ndoa ya Chadema, CUF, NCCR

$
0
0
MBUNGE wa Vunjo, Augustine Mrema (TLP ) ametaja ushirikiano wa vyama vitatu vinavyounda kambi rasmi ya upinzani bungeni kwamba ni ndoa ambayo kama wahusika wangekuwa na nia njema, ungeanza siku nyingi tangu Chadema kilipounda baraza lake mwaka 2010.

Mwanasiasa huyo ambaye ameunga mkono kauli ya Spika Anne Makinda, kwamba kambi hiyo rasmi ya upinzani imekumbuka shuka kunakucha, amekiri kwamba haelekei na wala hapatani na wana Ukawa; lakini yeye ni mpinzani na mzalendo wa kweli nchini.

Mrema alisema hayo juzi mjini hapa akizungumza na mwandishi wa habari hizi.

Alimjibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani, Freeman Mbowe ambaye katika kutangaza Baraza Kivuli la Mawaziri juzi, alisema mbunge huyo hana dhamira ya kuwa mshirika wa Ukawa na alishaweka wazi kuwa mshirika wa CCM.

Alitaja ushirikiano huo wa Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi, kuwa ni ‘ndoa’ anayoiombea kila la heri na hawezi kuibashiria mabaya, isipokuwa anachoona ni kwamba kama wangekuwa na nia njema, ndoa hiyo ingeanza siku nyingi tangu Chadema ilipounda baraza mwaka 2010.

“Ushirikiano huu ni jambo lao, wanafikiri litawasaidia. Lakini kwani hatujui walivyokuwa (CUF na Chadema) wakitukanana? Siwezi kuwabashiria mabaya. Wangelikuwa wema, hiyo ndoa ingeanza siku nyingi,” alisema Mrema.

Alisema yeye ni mpinzani ambaye kamwe hawezi kushiriki katika mambo ya kubomoa nchi.

“Kwanza mimi sijaomba huo uwaziri kivuli. Hawa watu ni wa ajabu sana... Mbona Maalim Seif (Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF), yuko kwenye Serikali ya Umoja wa kitaifa Zanzibar. Mbona CUF hawaambiwi ni CCM? “Kwanza ukinilinganisha na wao, naona wananionea wivu. Nimeshika madaraka ambayo hawajawahi kuyashika. Mbowe hana sifa za kuniteua. Ana sifa ipi sasa?.”

Mrema alitamba kuhusu nafasi za uongozi serikalini alizowahi kushika, ikiwemo ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Waziri wa Kazi na Maendeleo ya Vijana na Naibu Waziri Mkuu.

Alisema licha ya kuwa miongoni mwa watumishi waliotukuka, katika uchaguzi mkuu wa mwaka 1995 akiwa NCCR Mageuzi, alipata kura milioni 1.8 ambazo kwa mujibu wake, hakuna mpinzani anayeweza kuzipata.

“Na nilikuwa NCCR Mageuzi. Si watu wangenikataa kuwa mimi ni CCM…Nani amewahi kuvunja rekodi hii ya kura?” Alihoji.

Akiendelea kutamba kwamba hatishiwi na cheo chochote, alisema aliamua kuachana na kile alichoita ‘biashara ya jumla’ akimaanisha kugombea urais na badala yake, akaingia kwenye ‘biashara ya reja reja’ kwa maana ya ubunge.

Ngorongoro Heroes Yapigwa Kipigo cha Mbwa Mwizi

$
0
0
TIMU ya taifa ya soka ya vijana wa chini ya miaka 20, Ngorongoro Heroes, jana walianza vibaya kampeni ya kuwania kufuzu kwa Fainali za Afrika kwa umri huo baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Nigeria kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mchezo ulianza kwa kasi huku wageni wakionekana kujiamini, ingawa iliwachukua dakika tano tu Ngorongoro kulifikia lango la Nigeria ‘Flying Eagles’, ambapo Saad Kipanga alikosa bao akishindwa kumalizia kazi ya Kelvin Friday aliyemimina krosi toka winga ya kulia.

Dakika ya 11, mlinda mlango wa Ngorongoro, Aishi Manula, alifanya kazi ya ziada kuhakikisha nyavu zake hazitikiswi, ambapo alimzuia Mathew Ifeanyi, tukio ambalo lilimsababishia kuumia na kulazimka kutibiwa mara tatu katika dakika 45 za kwanza.

Kupitia shambulizi hilo, Manula alikuwa katika hatari ya kufungwa ama kusababisha penalti kama angemkabili vibaya Ifeanyi, lakini kwa ustadi mkubwa alilala kwa umakini na kuokoa hatari, ambayo ilimfanya aendelee kucheza na maumivu kabla ya kutolewa wakati wa mapumziko.

Hadi filimbi ya mapumziko ya mwamuzi Jean Ndala Ngabo wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), si Ngorongoro Heroes wala Flying Eagles iliyofumania nyavu za mwenzake.

Kipindi cha pili kilianza kwa Ngorongoro kufanya mabadiliko mawili kwa kuwatoa Aishi Manula na nafasi yake kuchukuliwa na Manyika Peter, na Gadiel Michael ambaye nafasi yake ilijazwa na Juma Liuzio. Nigeria nao wakafanya mabadiliko kwa kumtoa Abdullahi Alhassan na kumuingiza Iheanacho Promise.

Katika dakika ya 49, Flying Eagles walijipatia bao la kwanza, likiwekwa kimiani kirahisi kwa shuti dhaifu la karibu la Yahaya Musa, akiunganisha krosi maridadi ya Mohammed Mussa.

Kuingia kwa bao hilo kuliwachanganya Ngorongoro, ambao walijikuta wakishambuliwa mfululizo na kama si umakini wa Manyika Peter langoni, wangeweza kufungwa bao la pili, lakini yoso huyo anayefuata nyayo za baba yake Peter Manyika, aliokoa mchomo wa mbali na kuwa kona tasa dakika ya 54.

Saad Kipanga aliikosesha Ngorongoro bao la kusawazisha katika dakika ya 60, baada ya kumiminiwa majalo safi na Friday, lakini kichwa chake kikapaa juu ya lango la Flying Eagles.

Dakika ya 82, Awoniyi Taiwo aliipatia Nigeria bao la pili kwa shuti la karibu na kuzima matumaini ya Ngorongoro. Kwa matokeo hayo, Tanzania itahitaji ushindi wa mabao 3-0 ugenini ili kusonga mbele.

Ngorongoro: Aishi Manula/Manyika Peter, Swalehe Mohamed/Mohamed Ibrahim, Mohamed Hussein, Pato Ngonyani, Abdullahi Kheri, Abdi Banda, Ally Nassoro, Kelvin Friday, Saad Kipanga, Idd Selemani na Gadiel Michael/Juma Liuzio.

Nigeria: Enaholo Joshua, Muhamed Mussa, Mustapha Abdullahi, Idowu Akinjide, Ndidi Onyinye, Omego Izuchukwu, Alfa Abdullahi, Abdullahi Alhassan/Iheanacho Promise, Awoniyi Taiwo, Mathew Ifeanyi na Yahaya Mussa/Nwakali Chidiebere.

Lugola: Serikali ya CCM Inaendeshwa Kisanii

$
0
0
Mbunge machachari wa Mwibara, Alphaxard Kangi Lugola, amedai kuwa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambayo yeye ni mbunge wake, inaendeshwa kisanii.

Lugola ambaye katika Bunge lililopita aliwaongoza wabunge wenzake kuichachafya Serikali hadi mawaziri wanne kujiuzulu nyadhifa zao, jana aligeuka tena mwiba kwa Serikali ya CCM.

Akichangia hotuba ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Lugola alisema anashangaa Waziri mwenye dhamana, Christopher Chizza kuendelea kuwa waziri wakati hotuba yake imejaa blabla.

Pia alimgeukia naibu wa wizara hiyo, Godfrey Zambi na kumwambia kuwa amejisahau kwamba naye alikuwa akikaa kiti cha nyuma bungeni akipaza sauti, lakini baada ya kupata madaraka amewageuka na kushirikiana na waziri.

Akichangia kwa hisia kali, Lugola alihoji inakuwaje wakulima wanapelekewa pembejeo feki, dawa feki na skimu za umwagiliaji zinachakachuliwa na bado Chizza anaendelea kubaki ofisini kama Waziri.

“Waziri huyuhuyu ndiye anayezindua mbegu aina ya Chutoni ambayo haioti, bado ni Waziri. Waziri huyu huyu analipa ruzuku mbegu ya pamba isiyoota bado ni Waziri,” alisema Lugola.

Lugola alihoji kama Mchina aliyekuwa akijenga daraja la Kilombero alijiua kwa sababu tu ya kuhofia kupigwa risasi atakaporudi kwao, hata Waziri Chizza alipaswa awe ameiacha kazi hiyo.

“Simshauri waziri ajiue, lakini kwa vitendo vyote hivi waziri huyu angekuwa ameacha wizara hii na kupumzika na kufanya kazi nyingine mbadala,” alisema Lugola huku akipigiwa makofi.

Lugola alikumbushia Chizza alikuwa ni miongoni mwa mawaziri waliotajwa kuwa ni mizigo na kusema mambo yanayofanywa na wizara hiyo yatakigharimu Chama Cha Mapinduzi.

Mbunge huyo alibainisha kuwa, katika hotuba yake mwaka jana, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisema Serikali iko kwenye mchakato wa kuanzisha mfuko wa kinga ya pamba ili kuwasaidia wakulima.

Hata hivyo, alisema katika hotuba ya Waziri Mkuu juzi, hakuna sehemu aliyozungumzia mfuko huo wala Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika katika hotuba yake ya mwaka huu, naye hajazungumzia mfuko huo.

“Hivi nchi hii tunaiendesha kwa usanii mpaka lini? Usanii juu ya usanii… Hatuwezi kuwadanganya wananchi kwa kiwango hiki. Itakuwaje mimi mbunge niunge mkono bajeti ya namna hii?” alihoji.
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>