Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Soma Nafasi za Ajira zilizotangazwa Siku ya Leo


SAKATA la Matumizi Mabaya ya Fedha ya Rambirambi za Wafiwa wa Wanafunzi 32 wa Shule ya Lucky Vincent Latinga Bungeni..!!

$
0
0

SAKATA la matumizi ya fedha ya rambirambi iliyochangwa kwa lengo la kuwafariji wafiwa wa wanafunzi 32 na wafanyakazi watatu wa Shule ya Lucky Vincent ya jijini Arusha, limetinga bungeni baada ya watunga sheria kutaka maelezo kwa nini fedha hiyo imeelekezwa kwenye matumizi ya serikali.

Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema), ndiye aliyelifikisha suala hilo bungeni mjini hapa jana aliposimama na kuomba mwongozo wa Kiti cha Spika kuhusu matumizi ya fedha hizo mara tu baada ya kumalizika kwa kipindi cha 'Maswali na Majibu'.

Katika kujenga hoja yake, mbunge huyo alisema amepata taarifa kupitia vyombo vya habari kwamba, fedha ya rambirambi imeelekezwa katika ukarabati wa Hospitali ya Mount Meru jijini Arusha.

"Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba mwongozo wako kwa kutumia Kanuni ya 68(7) kinachohusu jambo lilijitokeza mapema bungeni. Nilikuwa hapo nje, nimeangalia magazeti yanaelezea matumizi ya fedha zilizotolewa kwa ajili ya rambirambi na kuwafariji wafiwa wa watu waliofariki katika ajali ya basi la Shule ya Lucky Vincent zimetumika kinyume cha malengo yake," alisema.

“Madaktari wamelipwa kama posho na fedha zingine zinakarabati Hospitali ya Mount Meru, tofauti na ilivyokusudiwa. Katika hili, Bunge linahusika kwa maana tulikatwa posho hapa ili kusaidia familia za wafiwa, ilikuwa misaada kwa wahusika. Sasa hii tabia imekuwa ikijirudia."

Alisema wananchi wamekuwa wakichanga kwa lengo la kusaidia waathirika lakini serikali imekuwa haifikishi fedha hizo kwa walengwa.

"Tabia hii imekuwa ikijirudia mara kwa mara, jambo ambalo si zuri kwani watu wataacha kuchanga wakijua kwamba fedha hazisaidii walengwa," alisema na kufafanua zaidi:

"Tabia hii inanikera hata mimi mwenyewe, kama tutakuwa tunachanga fedha za rambirambi halafu inabadilishwa matumizi juu kwa juu bila hata wahusika kupelekewa.

"Kama ni hivyo, ni vyema kila chama kikakusanya fedha za michango chenyewe au kada zingine zifanye hivyo kwa lengo la kuwafikishia wahusika wenyewe ili kuepuka ulaji wa fedha za michango."

Hata hivyo, Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge, akimjibu mbunge huyo, alisema chombo hicho cha kutunga sheria hakiwezi kufanyia kazi kupitia taarifa za vyombo vya habari.

Chenge pia alisema: “Kwa mila na desturi za kiafrika, ukishatoa mchango wako wa rambirambi unawaachia familia ile au chombo kile... sijatoa mwongozo haya ni maoni yangu."

"Naomba tusiendeleze jambo hilo, serikali ipo, Bunge lipo, unategemea mrejesho ili siku nyingine mkiombwa iwe rahisi kutoa lakini kuleta tuhuma tu, siyo.

“Ila kwa mwongozo wangu, swala lako halijatokea mapema bungeni leo (jana). Kwa hiyo, sina cha kulijibia, hatuendeshwi na magazeti humu bungeni."

Bunge lilichangia Sh. milioni 100 (wabunge Sh. milioni 86 na Ofisi ya Bunge Sh. milioni 14) kwa lengo la kuwafariji wafiwa.

Michango iliyotolewa na wadau ni zaidi ya Sh. milioni 300, Sh. milioni 133 zikitolewa kwa familia za wafiwa (kila familia ilipata Sh. milioni 3.8).

Wanafunzi 32, walimu wawili na dereva walifariki katika ajali ya barabarani baada ya basi dogo walilokuwa wakisafiria kutoka mjini Arusha kwenda Karatu kufanya mitihani ya ujirani mwema, kudaiwa kupinduka na kuingia kwenye korongo.

KIMENUKAA..Sumaye Afunguka Mazito Juu ya Serikali ya Mkoa wa Arusha Kutumia Vibaya Fedha za Wafiwa..!!!

$
0
0

Waziri Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye ameitaka Serikali kuacha kutumia michango inayotolewa kwa wahanga wa majanga, kwa matumizi yake.

Sumaye, ambaye ni Waziri Mkuu wa kwanza kushika nafasi hiyo kwa miaka kumi mfululizo, alisema hayo akitoa mfano kwa wahanga wa tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera pamoja na ajali iliyoua watu 35 wa Shule ya Lucky Vicent ya jijini Arusha Mei 6.

Fedha za misaada ya wahanga wa tetemeko la ardhi, takriban Sh7.5 bilioni zilitumiwa kukarabati miundombinu iliyoharibika, wakati za ajali ya basi la Lucky Vicent zimetumika kwa shughuli mbalimbali za kuaga maiti na mazishi na hivyo kuibua lawama kuwa baadhi ya matumizi hayakutakiwa kugharimiwa na fedha hizo.

Ajali ya Lucky Vicent iliua wanafunzi 32, walimu wawili na dereva mmoja. wanafunzi watatu walionusurika, wamesafirishwa kwa msaada kwenda Marekani kwa matibabu zaidi, wakiwa pamoja na daktari, muuguzi na mzazi mmoja kila mwanafunzi.

“Tujuavyo, huwa tunachangia kuwasaidia waliopatwa na tatizo. Huu utaratibu mpya wa kuichangia Serikali kupitia misiba au majanga umeanza lini na ni chombo gani kimeupitisha?” alihoji Sumaye.

Kutokana na matukio hayo mawili na kilichofanywa na Serikali, Sumaye alisema utaratibu huo si sahihi kwa sababu unawadhulumu wale waliotakiwa kusaidiwa na kuwavunja moyo wachangiaji.

 “Ni aibu kubwa sana kwa Serikali kufanya hivyo. Serikali iache kutumia mabavu kuchukua michango ya watu na kuitumia kinyume na watoaji walivyodhamiria,” alisema.

Licha ya mabadiliko ya matumizi yaliyofanywa katika rambirambi, mkuu wa mkoa wa Arusha aliagiza kukamatwa kwa watu waliojitokeza kwenda kutoa pole zao katika shule hiyo na kuzuia Sh18 milioni walizotaka kuikabidhi Lucky Vicent.

“Watanzania wapenda amani na wapenda haki lazima tulaani kwa nguvu zetu zote kitendo hicho cha uonevu, ukatili na uvunjifu wa haki za binadamu,” alisema Sumaye.

“Mtindo wa kutesa watu wasio na hatia kwa sababu za kisiasa ni chachu ya machafuko katika nchi na amani hii tuliyonayo ikitoweka, hakuna atakayepona.”

UKWELI Mchungu..Mrisho Gambo Afafanue Zaidi Rambirambi..!!!

$
0
0

Mwishoni mwa wiki iliyopita Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo alitoa kauli tata aliposema amesitisha uchangishaji wa fedha za rambirambi kwa ajili ya msiba mkubwa ulioikumba Shule ya Msingi ya Lucky Vincent.

Wanafunzi 32, walimu wawili na dereva wa shule hiyo walifariki katika ajali ya basi iliyotokea Mei 6.

Mkuu huyo wa mkoa hakufafanua kama alisitisha michango inayopitia ofisi yake au hata ndugu, jamaa na marafiki walioshindwa kutoa pole mapema shuleni na kwa familia za wanafunzi waliofariki.

Tunasema ni kauli tata kwa kuwa Ijumaa iliyopita alitoa amri polisi wakamate na kuwasweka mahabusu watu waliokuwa katika msafara wa meya uliokuwa kwenye shule hiyo kutoa pole. Meya aliongoza msafara wa viongozi wa dini na wa Chama cha Wamiliki wa Shule na vyuo Binafsi Tanzania (Tamongsco) ambao Shule ya Lucky Vincent ni mwanachama wao.

Polisi walisema walipewa amri na mkuu huyo wa mkoa kwa kuwa mkusanyiko huo haukuwa halali na Sh18 milioni walizokuwa wamebeba zilichukuliwa na askari hao na wao wakaswekwa mahabusu. Baada ya meya na wenzake kusota kwa siku mbili mahabusu, ndipo mkuu wa mkoa akatoa tamko la kusitisha uchangishaji rambirambi.

Tunajua wanafunzi hao, walimu pamoja na dereva walifariki dunia njiani baada ya basi walilokuwa wanasafiria kutumbukia kwenye korongo refu. Wanafunzi watatu waliojeruhiwa vibaya wako Marekani kwa matibabu.

Kutokana na idadi hiyo kupotea ghafla kwa wakati mmoja, ulichukuliwa kuwa msiba wa Taifa. Hiyo ndiyo sababu mkuu wa mkoa ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati ya Maafa ya Mkoa alichukua jukumu la kusimamia msiba huo ambao Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan aliongoza wananchi katika kuaga miili ya waliopoteza maisha.

Baadhi ya watu, taasisi, idara na kampuni walipeleka rambirambi zao ofisi ya mkuu wa mkoa, lakini wapo waliopenda kuipa pole shule hiyo moja kwa moja na wengine walikwenda na tunadhani wanaendelea kwenda kuzipa pole familia kwa kuzingatia udugu, ujirani na urafiki.

Misiba, kwa mila na desturi za Tanzania, waombolezaji huchukua siku tatu. Lakini baadhi ya makabila, ikiwa aliyekufa ni mzee mashuhuri katika familia au jamii, huweza kuomboleza mwezi mzima, lengo likiwa kutoa fursa kwa ndugu na jamaa waishio mbali, hata wakifika kuhani baada ya siku tatu za maombolezo wakute watu muhimu hawajatawanyika.

Na ingawa siku tatu za maombolezo kwa msiba wa wanafunzi wa Lucky Vincent zimeisha na wanafunzi ambao hawakuhusika katika ajali wamerejea masomoni, bado kwa utamaduni wa Kiafrika, watu wanaweza kwenda kutoa pole shuleni.

Kwa hiyo, kama tamko hilo linalenga michango inayopitia ofisini kwake atakuwa sahihi. Lakini atakuwa amejitwisha majukumu yasiyo yake kuzuia michango ya watu binafsi, vikundi, wanafunzi wa shule nyingine kwenda kuhani msiba ule.

Tunadhani kwamba hatua yake ya kuwazuia viongozi wa Tamongsco na wadau wengine si sahihi.

Tunamsihi afikirie nje la boksi la siasa na aondokane na dhana potofu kwamba fedha zikipita kwa watu wengine ni ufisadi. Pia atoe ufafanuzi wa kauli hiyo na aeleze ni kiasi gani kilichangwa kupitia ofisi yake na zilitumikaje? Kwa nini posho ya daktari na nesi walioandamana na watoto wagonjwa nchini Marekani wanalipwa kwa fedha za rambirambi badala ya posho za Serikali wakati watumishi hao wako kazini?

Credit Mwananchi

MIILI ya Wanafunzi Waliozama Ziwa Victoria Yapatikana ..!!!

$
0
0

Wanafunzi watatu kati ya 24 wa shule ya msingi Butwa,  waliozama katika ziwa Victoria, kisiwa cha Butwa, wamefariki dunia.

 Awali wanafunzi 21 waliokolewa na watatu hawakuonekana lakini saa chache baadaye, miili mitatu iliopolewa. Ajali hiyo ilitokea jana saa 10 alasiri.

 Mkuu wa Wilaya ya  Geita, Herman Kapufi amesema wanafunzi hao walikuwa kwenye mtumbwi waliotumia kuvuka wakitoka shuleni.

OMOG Ala Kiapo Kuisambaratisha Mbao Jumamosi..Adai Inyeshe Mvua Au Liwake Jua Lazima Wazikate Mbao..!!!

$
0
0

MECHI ya fainali ya Kombe la FA kati ya Simba na Mbao FC itakayopigwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Jamhuri Dodoma, ni muhimu kuliko mechi nyingine zilizotangulia kwa sababu itaamua hatima ya klabu, wachezaji na benchi la ufundi, imeelezwa.

Mshindi wa mechi hiyo atakuwa mwakilishi wa Tanzania Bara katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika wakati mabingwa wa Ligi Kuu Bara, Yanga wao watashiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika hapo mwakani.

Akizungumza  jana, Kocha Mkuu wa Simba, Joseph Omog, alisema kuwa katika kujiandaa na mchezo huo, kikosi chake kitaweka kambi ya siku mbili mkoani Morogoro na baadaye Alhamisi kitaelekea Dodoma tayari kwa mchezo huo.

Omog alisema ushindi ndiyo utawapa furaha na kuwafuta machozi Wanasimba wote ambao malengo yao ya kwanza yalikuwa ni kumaliza wakiwa mabingwa wa Ligi Kuu Bara kabla ya msimu kumalizika.

"Ni mechi muhimu sana, tunahitaji ushindi, ushindi katika mchezo huo wa fainali ni muhimu kuliko kitu chochote kwetu, tunajua haitakuwa kazi rahisi kwa sababu hatutacheza peke yetu," alisema Omog.

Kocha huyo wa zamani wa Azam FC alisema wanaiheshimu Mbao na wataingia uwanjani wakijua wanakutana na moja ya timu zilizotoa ushindani na kuleta mabadiliko kwenye soka msimu huu.

Simba ilitinga fainali kwa mara ya kwanza baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Azam FC katika mechi ya hatua ya nusu fainali wakati Mbao FC iliyoshiriki Ligi Kuu Bara msimu huu, yenyewe iliwavua ubingwa Yanga kutokana na kupata ushindi kama huo kupitia kwa beki wa Wanajangwani hao, Andrew Vicent 'Dante' aliyejifunga wakati akijitahidi kuokoa.

Wakati huo huo, Makamu wa Rais wa Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu' alisema kuwa tayari rufaa yao imeshafika katika makao makuu ya Shirikisho la Soka duniani (Fifa) na kilichobakia ni wao kusubiri uamuzi utakaotolewa na shirikisho hilo.

Simba imepeleka malalamiko yake Fifa ikitaka kupewa pointi katika mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Kagera Sugar ambao walimchezesha Mohammed Fakhi anayedaiwa kuwa na kadi tatu za njano.

Credit - Nipashe

Eti Amber Lulu Hapigi Tena Picha za Utupu!

$
0
0
MWANAMUZIKI na video queen anayesumbua Bongo, Amber Lulu amefunguka kuwa, kuelekea mwezi mtukufu wa Ramadhani hawezi kuthubutu kupiga picha za nusu utupu kama alivyokuwa anafanya na kwamba huo ndiyo utakuwa mwisho wake wa kupiga picha hizo.

Akichonga na Showbiz, Amber amesema ameamua kufikia maamuzi hayo baada ya watu kumsema sana mitandaoni lakini pia ingawa siyo muumini wa Dini ya Kiislamu ila ameamua kutumia mwezi Mtukufu kusahihisha makosa yake.

 “Ni kweli mapicha ya nusu utupu yananiweka mjini, lakini niyaache kwanza kupisha mwezi mtukufu wa Ramadhani, nafikiri mbali na kuupisha mwezi nitaangalia namna ya kupiga picha zangu na kuniingizia kipato kuwakacha watu wasichonge sana,” alisema Ambar Lulu.

KALA Jeremiah Atangaza Nia ya Kugombea Urais..!!!

$
0
0

Msanii wa muziki wa hip hop, Kala Jeremiah amefunguka kwa kusema kuwa hawezi kugombea ubunge kwani tayari ameshafanya kazi hiyo kwa miaka mingi na sasa anasubiri muda ufike aweze kugombea nafasi ya Urais.

Akiongea na umati wa watu uliojitokeza katika show ya ‘Wapo Tour’ya rapa Nay wa Mitego iliyofanyika Dar Live weekend hii, Kala atiwata mashabiki wake wajiamini katika mambo yao kama yeye anavyoamini siku moja anawekuwa Rais.

“Urais ndiyo ishu kwa sasa, kusema ukweli tayari nimeshakuwa mbunge kwa miaka mingi hata mashabiki wangu wanajua. Lakini kusema tena niende kugombea ubunge hapana siwezikufanya hivyo kwa hadhi yangu. Nafasi ya Urais ndiyo nayoitaka lakini siwezi kusema ni lini ila jua ipo siku mimi nitagombea nafasi hiyo,” Kala aliiambia alisema muda mchache baada ya kushuka kwenye steji.

Rapa huyo amedai hakuna kitu kinachoshindikana kwenye dunia kama mtu akiamua kufanya jambo lake.

SHAMBULIO la Kigaidi Laua 19 Katika Tamasha la Muziki Uingereza..!!!

$
0
0

Watu 19 wameuawa na wengine 50 kujeruhiwa baada ya bomu kulipua ukumbi wa tamasha la muziki, katika mji wa Manchester, Uingereza.

Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May ametaja tukio hili kama kitendo cha ugaidi.

Iwapo shambulio hilo litathibitishwa kuwa ni la kigaidi, linatajwa kuwa ni baya zaidi kuwahi kuikumba Uinereza.

 Shambulio kubwa zaidi lilitokea Julai 2005 ambapo watu zaidi ya 50 walipoteza maisha baada ya kutokea mlipuko, jijini London.

Katika tukio la jana, mashuhuda wanasema shambulio hilo lilitokea mara tu baada ya mwanamuziki wa Marekani Ariana Grande kumaliza kuwatumbuiza mashabiki wake.

Mashudhuda  wa tukio hilo wamesema waliona misumari iliyotapakaa sakafuni na harufu ya  mabomu.

Eneo kulikotokea mulipuko huo limezingirwa na polisi waliojihami wanaendelea kushika doria.

Wakati huo huo Waziri Mkuu Theresa May anatarajiwa kuongoza kikao cha dharura cha kamati ya usalama baadaye leo.

HII Hapa Taarifa ya Yanga Kuhusu Manji Kujiuzulu Uenyekiti wa Klabu..!!!

$
0
0

Klabu ya Yanga imekanusha taarifa zilizogaa mitandaoni kuhusu kujiuzuru kwa Mwenyekiti wao, Yusuph Manji na kusema kuwa taarifa hizo si za kweli na wanachama wote wanatakiwa kuzipuuza.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Klabu hiyo, Charles Mkwasa ambapo amesema kuwa hajapata taarifa rasmi juu ya ukweli wa suala hilo lakini amethibitisha kuwa bado hajawasiliana na Manji kama kweli amechukua uamuzi huo.

“Sijapata taarifa hizo rasmi, mimi ndiyo mtendaji mkuu wa klabu, bado sijakabidhiwa barua kwa kuwa sifanyi kazi kwa kutumia mitandao, tunajua kuwa mitandaoni kuna taarifa nyingi ambazo siyo za kweli na zipo nyingine ambazo zimesababisha baadhi ya wahusika kufikishwa kwenye vyombo vya sheria, hivyo nasubiri kuona kama ni kweli, basi nitapatiwa barua rasmi na nitatoa taarifa za ukweli kuhusu suala hilo.”amesema Mkwasa.

Hata hivyo, mapema hii leo kumekuwa na taarifa inayosambaa mitandaoni ya kujiuzuru kwa Manji huku ikiwa imesainiwa na Mwenyekiti huyo akieleza uamuzi wake wa kutangaza kujiuzuru.

AMUUA Mama Yake ‘Siku ya Mama Duniani’, Azurura Mtaani na Kichwa Chake..!!!

$
0
0

Katika hali isiyo ya kawaida, wakati dunia nzima ikizizima kumshukuru mama na kumuombea kwa kuleta uhai wa kila mmoja wetu, raia wa Marekani aliyetajwa kwa jina la Joshua Lee Webb aliitumia siku ya mama duniani kumuua kikatili mama yake mzazi aliyekuwa akiishi naye, Tina Marie Webb.

Kwa mujibu wa taarifa iliyoripotiwa na USA Today, baada ya mauaji hayo Webb mwenye umri wa miaka 36 alibeba kichwa cha mama yake na kuzunguka nacho kwenye mgahawa mmoja na kisha kumchoma kisu mtu mwingine aliyetajwa kwa jina la Michael Wagner.

Hata hivyo, wananchi walifanikiwa kumkamata Webb na kutoa taarifa Polisi katika eneo la Oregon ambao walifika na kumtia nguvuni. Jeshi la polisi la eneo hilo limeviambia vyombo vya habari kuwa tayari wamemfungulia mashtaka ya mauaji ya mama yake pamoja na jaribio la kumuua Wagner. Walisema Wagner alikimbizwa hospitalini ambako anaendelea na matibabu.

Webb anashikiliwa katika mahabusu ya eneo la Clackamas, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Jumatatu wiki hii na wa kitengo cha polisi.

Wakati huohuo, polisi walieleza kuwa walipokea simu kutoka kwenye nyumba ya Webb iliyoko Colton, umbali wa maili 12 kutoka eneo waliloukuta mwili wa mama yake Webb.

Polisi hawakutoa maelezo ya kina ya sababu zilizopelekea mauaji ya kikatili ya mama Webb, lakini uchunguzi juu ya tukio hilo unaendelea.

Hili ni tukio baya kutokea hususan katika siku hiyo ambayo kila mmoja aliitumia kumshukuru zaidi mama yake na kumpa ujumbe mzuri. “Hakuna kama mama, mama ndiye chanzo na mhimili wa uhai wetu. Heshima zote kwa mama.”

KIMENUKAA...Basata Waibuka na Kutoa Kauli Hii Baada ya Ben Pol Kusambaza Picha Zake za Uchi Mitandaoni..!!!

$
0
0

Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania, BASATA, Godfrey Mngereza amelaani picha za nusu za utupu za msanii wa muziki, Ben Pol ambazo imezua tafrani kubwa kwenye mitandao ya kijamii.

Akiongea  Jumatatu hii, Mngereza amewataka wasanii kufanya kazi nzuri ambazo zinaweza kuwaweka sehemu nzuri na siyo kutengeneza mazingira ambayo yanautia dosari muziki wao.

“Sisi kama BASATA tumeona hizo picha mtandaoni, siyo kitu kizuri, kwanza hakiendani na tamaduni zetu. Kwahiyo sisi tunamtafuta Ben Pol halafu tumsikilize, atueleze zile picha ilikuwaje mpaka zikasambaa mitandaoni. Tukiongea naye tunaweza kutoa kauli yoyote na kulaani matukio ya namna hiyo,”

Aliongeza,” Pia naungana na wasanii waliolaani kitendo hiko ambacho ni cha ajabu sana na baraza kwa mamlaka yake kama mzazi haiwezi kukaa kimya lazima tujue kama ana tatizo la akili au maadili limemkumba Ben Pol.”

Pia Mngereza amewaomba wasanii wa Tanzania kwa upande wa muziki wafanye muziki mzuri wasitegemee kiki.

JE Dada Unapenda Kuwa Mrembo? Na Kaka Unapenda Kuwa Mtanashati na Kurudisha Heshima ya Ndoa?

$
0
0

JE, DADA UNAPENDA KUWA MREMBO? NA KAKA UNAPENDA KUWA MTANASHATI NA KURUDISHA HESHIMA YA NDOA? Tumia Bidhaa halisi za MARKSON kwa mafanikio ya uhakika na bila madhara.
Zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kuthibitishwa kiafya.
🍉🌿🍓🍒🎄🍍🍀🍓🍉
Pata hizi 👇👇👇👇👇👇

1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @120,000/=
2. Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa (a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200,000/=
(b)Vidonge @180,000/=
3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @120,000/=
(11)Vidonge @150,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa :-
(a) Gely ya kupaka @130,000/=
(b) Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu hata kwa wenye kisukari @130,000/= (c)Handsome up (mashine) original @200,000/=
6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @120,000/=
7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula @120,000/=
8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a) Dawa ya kunywa au kupaka @120,000/=
(b)Mkanda wa kawaida @100,000/=
(c)Mkanda wa umeme @200,000/=
9 .Kupunguza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120,000/=
10.Kushepu miguu na kuwa minene na kuondoa migimbi @120,000/=
11.Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @100,000/=
12.Kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @120,000/=

NB: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
Wasiliana nasi :-
(+255) 0767447444 na
0714335378
👉🏻Ili kuona bidhaa zetu na baadhi ya shuhuda za waliotumia bidhaa zetu
Follow us on instagram
👇👇👇👇👇👇👇👇👇
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr

BREAKING NEWS: Alberto Msando ajiuzulu Ushauri wa chama cha Act-Wazalendo

$
0
0

Mkuu wa Chama Cha Act-Wazalendo Zitto Kabwe amethibitisha kupokea barua ya kujiuzulu kwa mshauri mteule wa Chama hicho Albarto Msando.

"Nimepokea barua ya Wakili Albert G. Msando kuomba kujiuzulu nafasi yake ya Ushauri wa Chama chetu cha ACT Wazalendo".

Zitto amesema kuwa  Msando anawajibika Kwani anapaswa, nanukuu  "kuishi Kama mfano Kwa jamii inayonizunguka".

Ndugu Albert Msando amekuwa kiongozi mwenye mchango mkubwa katika chama katika nafasi mbalimbali alizoshika ndani ya chama. Chama kinamshukuru kwa moyo wake wa kuzalendo na mchango alioutoa katika Chama. Ni matumaini yetu ataendelea kushirikiana nasi katika ujenzi wa chama kwa kadri atakavyoweza na atakapohitajika kama mwanachama.

Nikiwa Kiongozi wa Chama nimekubali kuwajibika kwake na kumtakia kheri katika kujisahihisha kwake.

Ndugu Msando Alberto ameomba msamaha Kwa jamii kwa uwazi na ni wajibu wetu kumsaidia kupita katika mitihani iliyomkumba.

Kabwe Z. Ruyagwa Zitto
Kiongozi wa Chama - ACT Wazalendo
Dar es salaam
Mei 23, 2017

Uchunguzi wa kuhusu Makontena ya Dhahabu mikononi mwa JPM

$
0
0


Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania anatarajia kupokea taarifa ya uchunguzi kuhusu usafirishwaji wa Makontena ya Dhahabu.

Taarifa Mawasiliano ya Ikulu imethibitisha.

JE Wajua Suala Vyeti vya Bashite, Linaweza Kabisa Kumng'oa Rais Magufuli Pale Ikulu?...Tazama Hapa Uone Jinsi Inavyokuwa Kisheria!!!?.

$
0
0

Baada ya mahojiano ya jana ya mtu kukwepa kuzungumzia suala la kufoji vyeti vya elimu, kuna watu wanaliona hili ni jambo dogo, hivyo kujitokeza kule, kumelimaliza rasmi, no its not over until it is over!.

Japo kwa mujibu wa katiba yetu, rais wa JMT ndio mamlaka kuu kupita zote, lakini sii wengi wanaotambua kuwa mamlaka ya juu kabisa ni katiba ya JMT, na rais wa JMT, japo amejiweka juu ya katiba, lakini kiukweli yuko chini ya katiba, hivyo hili suala la mteuliwa Daudi Bashite, watu wanalichukulia kimzaha mzaha au kiutani utani, lakini tungekuwa ni nchi nyingine yenye watu wanaojielewa, jee unajua suala kama hili lingeweza kabisa kumng'oa rais Magufuli pale Ikulu kwa mujibu wa sheria akaondoka na Bashite wake?.

Tanzania ni nchi inayoongozwa na Katiba kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni. Ikithibika beyond reasonable doubt kuwa Daudi Albert Bashite ni kweli alifeli kisha akafoji vyeti na kufoji jina, kujiendeleza kielimu hadi kuteuliwa, then huyu ni muhalifu kama wahalifu wengine wote, then hata rais wa JMT ampende vipi, anaweza kulazimishwa kutengua uteuzi wake kwa kuamrishwa, na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria, na rais asipofanya hivyo, then rais anaweza kushitakiwa na Bunge na kuondolewa madarakani!.

Watanzania tumekuwa ni watu wa kupiga sana kelele, kulaumu, kulalamika, kushutumu bila kuchukua hatua zozote ili hali sharia zipo lakini hatuzitumii.

Sakata la Bashite ni jambo dogo sana kulishughulikia kisheria.

Hatua za kufuata.
1. Any interested party mwenye ushahidi usio shaka kuwa Daudi Albert Bashite ni muhalifu wa kufoji vyeti na kuiba jina, kupitia kwa mwanasheria binafsi anaweza kufungwa mashitaka ya kijinai dhidi ya Daudi Albert Bashite as a private investigations. Atapewa vibali vyote toka ofisi ya DPP. Kuanzisha uchunguzi.

2. Uchunguzi utaanzia kwa Daudi Bashite mwenyewe kuitwa kwa samansi ya kuhojiwa kijinai chini ya kiapo. Na akikiri tuhuma, suala la uchunguzi wa kijinai unaishia hapa, mtuhumiwa anaandika barua ya kujiuzulu na issue hii inamalizika rasmi.

3.Kwenye mahojiano hayo kama atakanusha kuwa yeye si Daudi Bashite kama alivyodanganya jana pale Star TV, then kazi ya kukusanya ushahidi inaanza kwa kutolewa samansi ya kuwahoji wahusika wote wakuu isipokuwa mke, mzazi, walimu, hospitali kufuatia kitu kinachoitwa "fiduciary relationship" ambapo sheria inampa kinga ya kuhojiwa kijinai mtu wa karibu kama mke dhidi ya mume, mzazi na mtoto, mwalimu na mwanafunzi, daktari na mgonjwa, mwanasheria na mteja, padri na muumini etc. Hivyo kuanzia hospitali aliyozaliwa utakusanywa ushahidi wa documentary evidence aliandikishwa kwa majina gani?. Kisha Vizazi na Vifo kupata cheti cha kuzaliwa. Shule alipoandikishwa darasa la kwanza. Shule ya sekondari, Necta, vyuo, ajira alipitia, hadi idara ya uhamiaji.

4. Baada ya kukamulisha kukusanya documentary evidence, usio tia shaka kuwa Daudi Bashite amefoji vyeti. Then linafunguliwa shauri lunaloitwa "quo warranto" kuwa rais amemteua muhalifu, hivyo mahakama inajiridhisha na ushahidi uliiowasilishwa mbele yake.

5. Ndipo mahakama inatoa hati ya Quo Warranto kumlazimisha rais wa JMT, atake asitake, kutengua uteuzi wa Daudi Bashite kwa makosa ya uhalifu wa kijinai. Kwa mujibu wa katiba yetu, rais wa JMT, hana mamlaka ya kumteua muhalifu kwenye utumishi wa umma.

6. Kama rais atetengua uteuzi huu, then DPP atakuwa huru kumpandisha kizimbani Daudi Bashite kujibu tuhuma za jinai zinazomkabili na kuhukumiwa kwa mujibu wa sheria.

6. Iwapo Rais wa JMT asipotekeleza amri halali ya mahakama, anakuwa amepoteza sifa za urais zilizoainishwa na katiba ya JMT ya mwaka 1977. Hivyo rais anashitakiwa bungeni na kuondolewa kwenye urais kupitia process ya impeachment.

NB.
7. Process nilizoziweka hapo ni kwa mujibu wa katiba, sasa suala kama mahakama zetu zina weza kutoa amri ya Quo Warranto au laa linabaki kwenye utelelezaji, kitu cha muhimu ni kuelimishana kuwa rais wa JMT sio kila kitu, katiba ndio kila kitu. Maadam sheria zipo, suala la sheria kufuatwa au kutofuatwa hili sio langu.

8. The same applies to impeachment process, kuna watu wanadhani mtu akiishachaguliwa kuwa rais wa JMT, anaweza kujifanyia lolote analotaka, no! . Urais wa JMT ni kwa mujibu wa katiba, rais wetu atatekeleza majukumu yake ya urais kwa mujibu wa katiba, na ili kumkinga asibuguthiwe, ndio maana katiba yetu imempa kinga ya kutokushitakiwa mahakamani, lakini hakuna kinga ya kutokushitakiwa na Bunge pale anaposhindwa majukumu yake ya urais ikiwemo kututeulia wahalifu wa makosa ya jinai if proved beyond reasonable doubt, rais anashitakiwa na Bunge na anang'olewa na kuondoka na Bashite wake. Sasa suala la Bunge letu kama linauwezo wa kufanya hivi au laa, hili sio langu ni la wabunge wenyewe. Kitu cha muhimu hapa ni kujua kuwa hata rais anaweza kung'olewa madarakani na Bunge.

9. Hili sio lazima lifanywe na sheria, hata sisi media tunaweza, tukiwa na strong media yenye uzalendo usiatia shaka yenye kujua wajibu wake kwa umma, unaweza kuchunguza ukweli wa tuhuma hizi na kuziripoti, hivyo ama kumlazimisha rais wa JMT atimize wajibu wake, au kile kiti akione kichungu na kuachia kwa aibu kama ilivyowahi kutokea nchini Marekani kwa rais Richard Nikson kuachia ngazi kwenye kashfa ya Watergate.

10. Nawahakikishia hata mimi mwenyewe tuu kupitia kampuni yangu ya PPR, hili naliweza kabisa, ila kwa bahati mbaya sana, siwezi kulifanya kwa sababu kampuni yangu ya PPR, imejikita kwenye habari za kimaendeleo tuu zenye maslahi kwa taifa, yaani developmental news za Tanzania hapa tulipo, tufanyeje ili tufike kule tulikopaswa na sio habari kama hizi za vyeti vya Bashite.

Jumanne Njema.

Paskali

Chanzo - Jf

KIMENUKAA..Baada ya Makonda Kudai Nape Hakuna na Mamlaka ya Kumchunguza Katika Sakata la Clouds..Nape Amefungyka Haya Mazito..!!!

$
0
0

Mbunge wa Mtama, Nape Moses Nnauye amemjia juu kwa mara nyingine Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa kusema kwamba hakuunda kamati ya kumchunguza yeye, bali aliunda kamati ya kuchunguza tukio la kuvamiwa kwa kituo cha utangazaji cha Clouds Media Group.

Nape ameyasema hayo mapema leo asubuhi kupitia ukurasa wake wa Twitter, ambapo alieleza kwamba, kama kiongozi huyo alikuwa ni mmoja wa wavamizi wa kituo hicho, basi hayupo juu ya sheria.

“Niliunda kamati kuchunguza tukio la kuvamiwa kituo cha utangazaji sio kumchunguza RC. Kama RC alikuwa mmoja wa wavamizi, hayuko juu ya sheria,” aliandika Nape

Alipoulizwa kwanini Waziri wa Habari aunde kamati ya uchunguzi wa tukio la uvamizi badala ya kamati hiyo kuundwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Nape alijibu kwa kuuliza swali kama kila kamati inaundwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Majibu haya ya Nape yamekuja ikiwa ni saa chache baada ya kuulizwa ni yapi maoni yake kuhusu kauli ya Makonda kwamba hakuwa akifahamu mipaka yake ya kazi ndio sababu alikwenda kuunda tume ya kumchunguza.

Kauli ya Nape kuhusu kuunda kamati imekuja ikiwa ni takribani saa 24 tangu Makonda aliposema kuwa aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo aliunda kamati ya kumchunguza.

Makonda alisema hayo jana, ambapo alidai kuwa kamati iliyoundwa na Waziri isingeweza kumhoji kwa sababu haikuwa na uwezo huo kutokana na wajumbe wa kamati hiyo kutofahamu mambo yanayohusiana na masuala ya uvamizi.

JINSI Utawala wa Magufuli Ulivyowaumbua Wanahabari Makanjanja, Wengi 'Wamepotea'...!!!

$
0
0

Sasa ni dhahiri shahiri wanahabari wengi makanjanja wamekuwa na maisha magumu sana kwani wengi walitegemea kuishi kwa kuwasifia 'wanasiasa' na 'wapiga dili'. Mathalani, Ma-don wakubwa wa unga,makontena nk walikuwa wanamiliki kundi la waandishi wa habari wenye lengo moja kuu tu 'kuwasafisha'.

Hali imegeuka, magenge mengi yameyeyuka huku wakiwaacha vijana wao (waandishi makanjanja) wasijue cha kufanya. Kundi kubwa la makanjanja kwa sasa limegeukia mitandao ya kijamii kutengeneza akaunti feki zenye mrengo wa kupotosha. katika pitapita zangu nimekutana na baadhi ya wahariri ambao kabla ya Manji kubanwa walikuwa wenye 'fujo' nyingi mjini lakini ghafla hali yao imedhohofu. Udhibiti wa posho kwa wanasiasa pia umesababisha waandishi wengi kukosa ujira kwani hakuna mwanasiasa anayemudu kubeba waandishi kwa kukosa pesa za kuwalipa.

Magazeti mengi yaliyotamba miaka mitano iliyopita yamekufa au yanatoka mara moja moja sana, huku gazeti la Jamvi la habari likitokomea kusikojulikana.

Ushauri wangu ni kwamba kundi hili la 'wapambe' na 'makanjanja' wa habari sasa waelekeze nguvu zao katika mambo yenye tija kwa ajili yao binafsi na kwa taifa kwani kwa sasa hata zile kurasa zao maarufu zenye kukejeli serikali katika mitandao ya kijamii zimedorora.

Heshima imerudi mjini.

Credit - Jf

KAMANDA Sirro ni Mtu Pekee Anayefahamu Vyema Mauaji Yanayotokea Kibiti na Ikwiriri na Huenda Akawa na Majibu Yake..!!!

$
0
0

Mwaka 2012, Huko Ikwiriri wakati wa mapigano ya wakulima na wafugaji, aliyekuwa kamanda wa operesheni maalumu wa jeshi la polisi SACP Simon Sirro alitumwa kwenda kuweka mambo sawa.

Sirro akazungumza na wakulima, wafugaji, viongozi na polisi wa ikwiriri, lakini cha ajabu kidogo(kwa viongozi wa Tanzania), Simon Sirro alifanya jambo nadra kulifanya kwa viongozi wa kiafrika.

Akitoa majumuisho ktk mkutano wa hadhara akawatuhumu jeshi la polisi wa Ikwiriri Kuwa ndo chanzo cha mgogoro huo, kwani wamekuwa wakichukua "maziwa" kwa wafugaji na kusababisha kutotenda haki.

Akaendelea kuwalaumu polisi kuwa wanapaswa kutenda haki na "hali hiyo ikiendelea italeta shida na shaka siku za mbele".

Leo ni miaka mitano tumeona utabiri wa Simon Sirro, Mauaji ya polisi, viongozi wa chama dola na serikali wakiwa ni walengwa zaidi.

Hata ukweli upingwe vipi ila kwa sura ya nje Kibiti na Ikwiriri Kuna tatizo kubwa, huenda kuna kundi linalipa kisasi kwa uonevu walioupata mahala.

Kwa sasa ni mtu mmoja tu anaweza kutumia akili, uwezo na busara zake kuweka mambo sawa Kibiti, ni kamanda wa polisi wa mkoa wa DAR ES SALAAM wa sasa ndugu yangu Simon Sirro.

Nina hakika hata jeshi la polisi likiamua kufanya reform na likafanya mapinduzi ya kimuundo na kiutawala ili kujiweka ktk hali ya kukwepa lawama na chuki dhidhi yake kama raia kubambikiwa kesi, kujiingiza ktk siasa, matumizi makubwa ya nguvu, changamoto za ndani ya jeshi nk. huenda huyu bwana akaweza kuwa ni kiongozi wa mabadiliko hayo.

By Shukuru Ngonyani wa JF

UKWELI Mchungu..Kwa Vyerehani Vinne na 70mil ya Kufufulia General Tyre Sera ya Viwanda Ilikuwa ni Ulaghai..!!!

$
0
0

Kama mlivyosikia kwamba ukiwa na vyerehani vinne tayari ni kiwanda, yaani ukiwa na vyerehani 40 una viwanda 10. 

Hii issue imenikumbusha mwaka 2013, kuna rafiki yangu flani alikua anafanya kazi kwenye kampuni flani ya wahindi ina deal na security, firefighting na mambo ya cartrucking, sasa wao walikua kitengo cha Marketing na mhindi flani, wanachofanya wanaenda site kuongea na wateja ambao sometimes wanawapata kupitia majarida mbalimbali na kuwapigia simu.

Sasa bwana wakaongea na Mangi mmoja kwenye simu kwamba wao wanatoa huduma mbalimbali kwenye makampuni, maduka, na office mbali mbali, basi wakapanga appointment, kumbuka kazi wanazofanya wao ni kwenye office kubwa kubwa, kwenye makampuni makubwa.

Sasa siku ya siku ikafika asubuhi na mapema wakaingia kwenye "NAVARA" safari ya kwenda kwa Mangi kibaha maili moja ikaanza, kichwani wanaimagine huko tutakuta supermarket, au kiwanda flan, au jamaa atakua ni Transporter, basi bwana, gia mosi, gia pili mara kibaha mizani ya zamani hii hapa, wakampigia simu, ndio tunaingia maili moja hapa tupe ramani vizuri.. Mangi akawaelekeza.

Mara Vuuu, break zinakanyangwa mbele ya Mangi, walichokiona ilibidi muhindi awashe sigara yake ya Malboro kwanza, ilikua ni kituko!! Yaani walikuta ni kioski, yaani ni kiduka cha mbao kidogo dogo flan hivi kimechoka sana, yaani kwa haraka haraka mali iliyokuwemo mule kioskini ilikua kama ya laki mbili hivi au pungufu ya hapo, Jamaa hata hawakutaka kuongea nae, wakatia reverse gear, wakarudi kinondoni wakiwa hoiii..

Sasa ukikumbuka jinsi CCM kupitia JPM ilivyokua inajitapa kuhusu viwanda utacheka sana jinsi saivi wanavyoongelea hivi viwanda. Nakumbuka katika mkutano wa kampeni uliofanyika kibaha JPM akiongozwa na Bulembo waliongea maneno matamu sana kuhusu viwanda, ila kumbe walikua wanamaanisha viwanda kama vyerehani na kijiwe cha "shoe shine" cha kushonea viatu.

Na ili kulielewa hili wazia juzi wametangaza kua eti kiwanda cha "General Tyre" kimetengewa milion 70 kukifufua, REALY??? Yaani kiwanda cha matairi ukifufue kwa only 70,000,000? Pesa ambayo ambayo ukililia sana ndo utapata horse ya scania mtumba flan hivi umechokachoka wa R420!!

Yaani hiyo 70mil hakuna kitu itafanya, ikumbukwe hapo inainclude material and operational cost... Ifike mahala serikali iache utani na Nchi yetu. Wao wanatembelea chuma zenye thamani ya 200mil+ ila hata kusema basi hiki kiwanda tukipe japo pesa yenye thamani ya VX V8 japo 5 tu hawawezi.

Ukweli ni kwamba mpaka miaka Mitano itakapoisha hakuna kiwanda chochote kitakachosimama na kuwaajili Watanzania, hata hiyo General Tyre haiwezi kusimama kwa 70mil.. 

Nchi ya viwanda na uchumi wa kati ilikua ni AHADI HEWA NA HADAA KWA UMMA WA WATANZANIA. Sisi tumejizoelea maisha yetu ya kawaida tu, hamkua na haja ya kututamanisha vitu msivyoweza kutimiza, leo unasema vyerehani vinne ni kiwanda, basi sawa, kwahiyo basi hata kwa wakaanga chips ni "Food Processing Industries"

Nimalize na mfano Huu; kuna siku rafiki yangu mwengine mbali na yule wa hapo juu alijikoki na wenzie( kutoka Madrasa flani hivi Mabibo pale), walikua wanaenda kufanya Dua/ kisomo kwenye nyumba flani hivi ya Muarabu, kwenye akili yao wakajua leo huko kutakua na msosi wa nguvu kuanzia Biriani na mazagazaga ya kutosha(si unajua tena hawa ndugu zetu kwa msosi-samahani lakini, ni utani), maskini wakabeba ndizi wakazitia ndani ya kanzu kila mtu kwaajili ya makamuzi, kufika pale hamna harufu yeyote kusema labda msosi unasababishwa, wakajipa moyo anyway labda muarabu kaamua kuagiza "catering" so after duaa mzigo utaletwa hapa, weeeeeee, watu wamemaliza dua zimeletwa chupa za chai na biscuts..

Chanzo - Jf

Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images