Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104427 articles
Browse latest View live

A to Z ya Video Chafu ya Gigy Money na Wakili Msando...Msando Adai Gigy Amelipiza Kisasi

0
0

Aibu! Siri nzito imevuja baada ya video chafu iliyomhusisha wakili maarufu hapa nchini ambaye pia aliwahi kusimamia kesi ya Wema Sepetu, Albert Msando na muuza sura katika video za wasanii wa Bongo Fleva, Gift Stanford ‘Gigy Money’.

Video hiyo inamuonyesha Msando akimshikashika sehemu nyeti msichana huyo ambaye naye anajibu kwa kumkatikia mauno mwanasheria huyo msomi. Wakati wadau mbalimbali wakimlaumu Msando kwa kile walichosema amejishushia heshima, Risasi Mchanganyiko limebaini kuwa ishu hiyo haikutokea kwa bahati mbaya, bali ni kisasi kilichopangiliwa kwa ustadi.

MWANZO WA MCHEZO

Gigy Money alikuwa katika ziara ya kimuziki katika Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro akiwa na rafiki yake mmoja ambaye jina lake halikufahamika, aliyekuwa akifanya mawasiliano na mwanasheria huyo maarufu nchini, ambaye wakati huo alikuwa Arusha.

HUYU HAPA GIGY AKIMWAGA MBOGA…

Akizungumza baada ya video hiyo kuvuja, Gigy alisema wiki iliyopita alikuwa na shoo maeneo ya Boma, Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro ambako akiwa huko alipata mwaliko kutoka kwa Msando wa kwenda kumtembelea katika klabu yake iitwayo The Don, iliyopo Arusha.

“Kweli Msando nilikuwa sijawahi kuonana naye live, ila aliposikia nipo Hai akanipa mwaliko, nikamwambia siwezi kwenda kwa kuwa nilikuwa bize na shoo, pia sikuona umuhimu sana wa kumuona maana sicho kilichonipeleka. “Baada ya kusema atanitumia usafiri, nikakubali, nilipomaliza kazi alikuja na gari akiwa na watu wanne, wanaume wawili na wanawake wawili, tulifika Arusha tukaenda club, nikalewa sana na baada ya hapo wakanipa tena lifti kwenye gari yao kwenda hotelini.

“Tukiwa kwenye gari huku nimelewa, nilisikia Msando akimwambia mmoja wa wale watu aturekodi nami sikuelewa ana maana gani, wakanishusha nikaenda kulala peke yangu, sijalala na mtu yeyote, kesho yake nikaiona kwenye mitandao, kiukweli kitendo hicho hakijanifurahisha hata kidogo, kimeniudhi mno maana kimenidhalilisha,” alisema Gigy.

MSIKIE MSANDO SASA

Risasi Mchanganyiko lilijaribu mara kadhaa kumpigia simu yake ya mkononi bila kupokelewa, lakini baada ya kutumiwa ujumbe mfupi wa simu, likijitambulisha na kuomba kupata ufafanuzi kuhusu video iliyopo mtandaoni, Msando alipiga simu na kuzungumza.

Risasi: Mambo vipi kaka!

Msando: Safi aisee.

Risasi: Pole kwa kilichotokea mzee.

Msando: Aaah ndiyo imeshatokea tena haina jinsi.

Risasi: Kwani ilikuwaje kaka?

Msando: Aaah, unajua kilichotokea ni kama huyu dada amenilipizia hivi!

Risasi: Kivipi? Msando: Si unajua huyu dada aliwahi kusema kuwa hakumbuki ame-date na watu wangapi? Sasa mimi kuna siku nilipost (kuandika katika mitandao ya kijamii) nikishangaa kama kwa miaka miwili tu ameshawasahau, basi kuna tabu.

Sasa najua kuanzia pale akawa na hasira na mimi.

Risasi: Kwani mnafahamiana kabla ya leo?

Msando: Sijawahi kuwa na mawasiliano naye hata mara moja.

Risasi: Khaa, sasa kama hamjawahi kuwasiliana ilikuwaje ikawa kama vile ilivyokuwa?

Msando: Mimi nilikuwa nawasiliana na dada mmoja ambaye alikuwa anatumia simu ya Gigy, aliniambia wanataka sana kuja kupaona klabu kwangu, nikaona isiwe tabu, nikawakaribisha.

Risasi: Kwani wewe una klabu?

Msando: Ndiyo, inaitwa The Don, ipo Njiro.

Risasi: Aisee, safi kaka, uko vizuri. Enhee, ikawaje sasa?

Msando: Basi wakaja ile usiku sana, tukawa pamoja tunapata mambo, hadi kunakaribia kucha tukaondoka.
Risasi: Sasa ile video ilirekodiwa wapi?

Msando: Ndani ya gari wakati tunarudi, aliyekuwa anatupiga picha ni rafiki yake. Risasi: Hukuelewa kama unarekodiwa au uliruhusu jambo hilo lifanyike?

Msando: Aaah, si unajua tena mambo yale, sikufikiria chochote aisee.

Risasi: Lakini Gigy analaumu kuwa ni wewe ndiye uliyeingiza mtandaoni ile video. Msando: No, ni namba ya Gigy ndiyo iliyoingiza mtandaoni.

Risasi: Kwa hiyo unafikiria kumchukulia hatua za kisheria Gigy? Msando: Hapana, nina vitu vingi sana vikubwa vya kushughulika navyo kuliko kushughulika na mtu kama Gigy, ninamuacha tu! Risasi: Dah, na vipi mke wako ameshaiona?

Msando: Yes ameiona. Risasi: Vipi mapokeo yake?

Msando: Mke wangu ni sapota wangu namba moja, anajua baada ya pale hakuna kilichoendelea, kwa hiyo iko vizuri. Mimi nina mke, watoto na ndugu zangu na wa mke wangu pia, kwa hiyo hili jambo liko vizuri tu kwa upande wangu.

Risasi: Sawa, lakini una wateja wako na watu wengine wanaokuheshimu, unawaambia nini kwa hili?

Msando: Nimeandika kwenye ukurasa wangu wa Instagram, unaweza kupitia.

Risasi: Asante, nitakutafuta kukiwa na ishu nyingine broo.

Msando: Asante karibu. Katika akaunti yake ya Instagram, Msando aliandika maneno haya kwa wateja wake, marafiki na watu wake
wa karibu. Nikikaa kimya nitakuwa mnafiki. Nimekosea. Kilichotokea hakikupaswa kutokea. I will be a man enough and say sorry kwa wote ambao nimewakwaza na kuwaangusha. Am so sorry. But the beauty of all this is we are all human. Kuna watu ambao wamekuwa wepesi kuhukumu. Siwalaumu. Ni sawa, ni haki yao. I made a stupid mistake. I take full responsibility. Mwisho wa siku maisha lazima yaendelee. It could have been worse. And to all those who took time to text I appreciate. Thats friendship. Kulikuwa na maneno katika baadhi ya mitandao, wakitaka Chama Cha Wanasheria Tanzania (TLS) kumchukulia hatua Msando, kwani amekidhalilisha. Lakini Risasi Mchanganyiko lilipofanya mawasiliano na rais wa taasisi hiyo, Tundu Lisu alisema;

TUNDU LISU APIGILIA MSUMARI

“Msando ni mwanachama wetu, lakini sisi kama chama hatuwezi kumchukulia hatua yoyote, angekuwa amefanya kosa hilo akiwa katika kazi zake za kisheria, hapo sawa, lakini hili ni jambo binafsi. Wakili hazuiwi kunywa pombe, hazuiwi kuchukua malaya, kwa sababu hayo ni mambo yake, ni juu ya kanisa lake au mke wake kushughulika naye, siyo sisi.”

AJIUZULU

Wakati tukienda mitamboni, Wakili Msando alitoa taarifa ya kujiuzulu nafasi yake kama Mshauri Mkuu wa Chama Cha ACT-Wazalendo, ambayo aliielekeza kwa kiongozi wake mkuu, Mbunge wa
Kigoma Mjini, Zitto Kabwe. “Napenda kuchukua nafasi hii kukujulisha uamuzi wangu wa kujiuzulu nafasi yangu kama Mshauri Mkuu wa Chama.

Uamuzi huu ni kutimiza hitaji langu la kuishi kama mfano kwa jamii inayonizunguka. Kama kiongozi nastahili kuwajibika kutokana na video clip iliyorekodiwa na kusambazwa. Ni wajibu wangu kwa chama changu na nchi yangu kuwajibika kama kiongozi. “Nitaendelea kuwa mwanachama mtiifu nikishirikiana nawe kujenga chama na kuhakikisha nchi yetu inaendelea mbele.

Nakushukuru kwa kuniamini kwa kipindi chote tulichofanya kazi pamoja,” alisema Msando katika taarifa yake. Zitto hakuchelewa kumjibu mshauri huyo, akisema amepokea barua yake ya kuomba kujiuzulu nafasi yake na yeye amekubali. “Ndugu Albert Msando amekuwa kiongozi mwenye mchango mkubwa katika chama katika nafasi mbalimbali alizoshika.

Chama kinamshukuru kwa moyo wake wa kizalendo na mchango alioutoa. Ni matumaini yetu ataendelea kushirikiana nasi katika ujenzi wa chama kwa kadiri atakavyoweza na atakapohitajika kama mwanachama. “Nikiwa kiongozi wa Chama nimekubali kuwajibika kwake na kumtakia kheri katika kujisahihisha kwake. Ndugu Msando Albert ameomba msamaha kwa jamii kwa uwazi na ni wajibu wetu kumsaidia kupita katika mitihani iliyomkumba,” ilimalizia taarifa hiyo ya Zitto jana.

Video: Chadema Hawana Shukrani Kabisa..Sikuwahi Kuwa Mwanachama Wao - Wolper

0
0

Malkia wa filamu bongo, Jacqueline Wolper amefunguka sababu za kuacha kuendelea kuisapoti CHADEMA ni viongozi wa chama hicho kushindwa kuutambua mchango wake alioutoa wakati wa uchaguzi mkuu hali iliyomfanya ajihihisi mpweke na kama ametelekezwa .

Ikiwa ni mara ya kwanza Wolper kufunguka ishu hiyo katika kipindi cha KIKAANGONI kinachorushwa kwenye ukurasa wa facebook EATV, amesema hajawai kuwa msaliti kwani hakuwa mwanachama wa chama hicho lakini alisikitishwa na uongozi wa chama kushindwa hata kumshukuru kwa kazi aliyoifanya wakati wa uchaguzi mkuu kwa kujitoa pasipo kulipwa hata shilingi elfu 10 za kitanzania.

Pamoja na kuwa alifanya kampeni za kumsapoti Mgombea uraisi kupitia mwamvuli wa UKAWA Mhe. Edward Lowassa, Wolper amedai kuwa hakuwa anasapoti chama kizima bali mgombea kwa kuwa yeye ni shabiki wa kiongozi huyo na familia yake kwa ujumla ndiyo maana hakukubali kulipwa katika kampeni hizo.


"Mimi nilifanya siasa kwa sababu namkubali Lowassa, na mimi ni shabiki wake na familia yake kwa ujumla. Nilianza kumsapoti Lowassa tangu yupo CCM. Mimi ni mfanyabiashara na muigizaji, sijawahi kuwa mwanasiasa ndio maana nilikuwa namsapoti mtu mmoja mmoja na siyo chama. Hata hivyo mimi siyo Yuda kwa CHADEMA kwa sababu sijawahi kuwa mwanachama wao na sina chama  chochote lakini wao baada ya uchaguzi walinitelekeza kiasi cha kunifanya nijisikie mpweke. Hata kama hawakushinda uchaguzi walipaswa hata viongozi wawili wanishukuru tu kwa maneno ili na mimi nipate faraja lakini hawakuweza kufanya hivyo - Wolper

Hata hivyo Wolper amekiri wazi hata tatizo na Mhe Lowassa na hawezi kumlaumu kwa yaliyotokea bali atakuwa naye bega kwa bega tena kumsapoti endapo atapata tena nafasi ya kugombea urais 2020.

Mtazame hapa chini Wolper akifunguka kwa undani zaidi.

Mbunge wa Geita Joseph Musukuma Afunguka Jinsi Atakavyowavimbisha Matumbo Wakazi wa Dar es Salaam

0
0
Mbunge wa Geita (CCM), Joseph Kasheku Musukuma amesema hawezi kumsifia hata kidogo Prof. Jumanne Maghembe, Waziri wa Maliasili na Utalii kwani yeye na watu wake wa Wizara wanafanya mambo ya ajabu hasa kwa watu wa Kanda ya Ziwa.

Musukuma anasema watu wa Wizara ya Maliasili wamekuwa wakiuza ng'ombe za watu jamii ya wasukuma na kuzipiga mnada kwa dili kwa lengo la kujinufaisha wenyewe, hivyo mbunge huyo amesema wasukuma wameamua kuwa wataziroga ng'ombe zote ili wanaokula ngo'mbe hizo Dar es Salaam wavimbe matumbo.

"Napata shida sana kujiuliza labda sisi watu wa kanda ya ziwa labda tulikuja kwa bahati mbaya Tanzania hii, mbona yanayofanyika Kanda ya Ziwa hayafanyiki Kanda ya Kaskazini wakati nao wana mapori, Waziri ametoa siku tatu tukamatiwe ng'ombe kwa kisingizio kwamba ni ng'ombe za Wanyarwanda wakati huo huo watumishi wake wanaowaingiza Wanyarwanda wanawaambia toeni ng'ombe, mnaenda kukamata ng'ombe za Wasukuma halafu unazipiga mnada na mnada wenyewe unavyopigwa ni wa dili" Alisisitiza Musukuma 

Mbunge huyo aliendelea kuelezea namna watu wa Wizara ya Maliasili wanavyofanya minada hiyo huku wakiwaumiza wafugaji

"Yaani ng'ombe 600 unaambiwa ulete milioni tatu halafu wanatoa watu wao wa Ubungo sasa hapo nikupongeze kwa sababu gani? Tunajua mipango inayoendelea kwenye wizara yako na niliwapigia kabisa watumishi wako, wananiambia mliipenda wenyewe kwa kauli yake kama Mwenyekiti wa Chama kesho yake akapiga ng'ombe za watu mnada yaani ng'ombe 500 zinauzwa milioni tatu" Alisema Musukuma 

Joseph Msukuma aliendelea na msimamo wake :
"Nataka nikwambie sisi Wasukuma sasa tumeamua na ninazungumza uelewe tutaziroga hizo ng'ombe mtavimba matumbo mnaozila huko Dar es Salaam, haiwezekani kwanini wanunuzi watoke Dar es Salaam peke yake yaani leo siku ya mnada watu wametoka na malori Pugu wamejuaje kama wanakuja kushinda kwenye minada. Mnatukamatia ng'ombe hivi hii serikali imekosa sehemu ya kukusanya hela mpaka mkanyang'anye ng'ombe za wafugaji haiwezekani Mh. Maghembe"

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo

0
0

Barua Nzito Kwa Bongo Fleva Wote baada ya kuondokewa na Dogo Mfaume..!!!

0
0

Mungu wangu ninakushukuru kwa siku ya leo, asante pia kwa ajili ya wasomaji wangu ambao wamekuwa wakinipa maoni na ushauri wao mwingi kuhusu safu hii. Wote tunajua kuwa wiki iliyopita, wadau wa burudani walipatwa na msiba mzito, baada ya kuondokewa na msanii Mfaume Seleman ‘Dogo Mfaume’ aliyewahi kutamba na nyimbo za Hereni, Kazi Yangu ya Dukani na nyinginezo.

Dogo Mfaume alifariki dunia kwa tati zo la uvimbe kichwani, akiacha kumbukumbu ya kuwa mmoja kati ya vijana waliofanya vizuri sana kati ka Muziki wa Kizazi Kipya, akichagua Mchiriku na Mnanda, ambako pia kulikuwa na wasanii wengine wakali kama Omari Omari na Juma Mpogo. Maneno ya mashabiki na wadau wa muziki huo wanasema ni kama wakali wa Mchiriku wameisha, baada ya wote hapo juu kuwa wameaga dunia.

Hili lilikuwa ni pigo kubwa kwa tasnia ya burudani. Kwa utamaduni wetu kama jamii, tunayo jadi ya kulia na kuzikana pamoja. Ni matarajio ya watu kuwaona waandishi wa habari wengi kati ka msiba wa mwanahabari mwenzao, kuwaona manesi na madaktari wengi kati ka mazishi ya mwanataaluma mwenzao.

Hivi ndivyo ilivyotarajiwa kati ka msiba wa Dogo Mfaume, kijana aliyefariki akiacha doa la kuwahi kuwa mtumiaji mzuri wa madawa ya kulevya kati kaharakati zake za maisha.

Lakini kwa namna ya kusikitisha sana, kulikuwa na idadi ndogo ya wasanii wa Bongo Fleva, tena hata wale wanaopiga muziki wa aina aliyokuwa akiimba ambao hivi sasa unaitwa Singeli. Nilisikiti ka sana kuona kati ka mastaa wote waliopo, ni Juma Nature, Inspekta Haroun, Suma G, Mzee Yusuf na Dullayo pekee ndiyo walionekana. 

Ingawa kuhudhuria mazishi ni hiyari ya mtu, lakini utu unatutuma tujione wakosefu tunaposhindwa kushiriki matukio kama hayo, hasa yanapowahusu watu ambao kwa namna moja au nyingine tulishiriki nao wakati wa uhai wao.

Najaribu kujiuliza, kisa ni nini? Au kwa kuwa alikuwa hatambi tena kimuziki? Matarajio ya watu wengi ilikuwa kuona wasanii wa Muziki wa Kizazi Kipya wakifi ka kwa wingi, lakini nilichokishuhudia mimi mwenyewe ni cha
kusikiti sha.

Ni kweli enzi zake zimekwisha, lakini wasanii wa Bongo Fleva mlipaswa mmpe heshima yake bila kujali alikufa akitoka kati ka kuishi maisha ya namna gani! Tunawaona wasanii wa Bongo Fleva kati ka mazishi ya wacheza mpira, waigizaji wa fi lamu na hata wanamuziki wa Dansi.

Kwa nini mmeamua kumsusa mwenzenu? Wale jamaa waliokuwa mateja na wakaacha ambao wameishi naye sober house Dogo Mfaume kwa muda gani kama siyo mwaka na mwezi mmoja tu.

Nyinyi je? Si mmekaa naye zaidi ya miaka mitano kwenye tasnia ya muziki! Mmeshindwa nini kuisamehe siku moja kwa ajili ya kumsindikiza mwenzenu? Yawezekana sikuwaona wengine lakini kwa umati uliokuwepo si rahisi kwa msanii kuwepo na usionekane hata kama nisingekuona basi tungesikia salamu za rambirambi kutoka Bongo Fleva, lakini na zenyewe hazikuwepo.

Bongo Fleva mmeti a aibu, mmehuzunisha, mmesikiti sha, kama mmeshindwa kuhudhuria kwenye msiba, mnategemea mtashirikiana kwenye nini? Au labda kwa kuwa hakuwa na pesa kama ilivyo kwa baadhi ya wasanii? Kati ka vitu ambavyo yatupasa kushikamana, basi ni wakati wa shida, hasa tukiwa wagonjwa na hata mauti yanapotufi ka.

Kulikuwa na ugumu gani kwa wasanii hao kwenda Chanika kumzika mwenzao na kurudi? Hatuwezi kukubali kisingizio cha umbali, kwa sababu tuliwaona kwa mamia walivyosafi ri hadi Morogoro kumsindikiza Ngwair, itakuwa Chanika, sehemu ambayo wangeweza kukodi basi aina ya Coaster? Anyway, maisha ni vile mtu unavyotaka kuyaishi, lakini hakuna faraja mtu unapata kama pale unapofi kwa na matati zo, halafu watu ulioshirikiana nao wanapokuwa wa kwanza kuonyesha masikiti ko yao. Dogo Mfaume, tangulia mshkaji, lakini hawa Bongo Fleva wenzio siyo kabisa!

Tundu Lissu 'Kwa Hili La Mchanga wa Madini Tutanyolewa Bila Maji'

0
0

Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu ameibuka na kuishauri serikali jambo la kufanya kutokana na matokeo ya uchunguzi wa mchanga wa madini uliofanywa na kamati ilyoundwa na Rais John Magufuli.

Tundu Lissu anasema Tanzania ni mwanachama wa 'The MIGA Convention' hivyo ukiwa mwanachama ukachukua mali za wawekezaji wao utapelekwa kwenye mahakama za kimataifa na kwenda kushughulikiwa huko, hivyo Tundu Lissu ametoa ushauri wa namna nzuri ya kushughulika na watu

"Sisi Tanzania ni wanachama wa kitu kinaitwa 'The MIGA Convention' Multilateral Investment Guarantee Agency ya benki ya dunia, ukiwa mwanachama wawekezaji wakileta mali zao kwako, ukichukua mali zao kama walivyochukuliwa mali zao namna hii utapelekwa kwenye mahakama zao za kimataifa unaenda kushughulikiwa huko, tumesaini mkataba wa ulinzi wa wawekezaji na mataifa wanayotoka wawekezaji hao Marekani, Canada, Uingereza wote ni mabosi wakubwa makampuni ambayo Rais ameyakamatia mali zao yanatoka kwenye hizi nchi tuna 'bilateral investment treaties ambazo zinalinda mikataba hii" alisema Tundu Lissu 


Tundu Lissu anasema hili suala tusipokuwa makini nalo linaweza kuleta matatizo makubwa huku akimtaja muhusika wa mikataba iliyolifikisha taifa katika hasara iliyobainika katika uchunguzi huo.
"Rais anajiingiza kwenye mgogoro mkubwa, akimkamata Dalali Kafumu peke yake, tutamwambia kwanini siyo Gray Mwakalukwa mikataba yote hii imeingia wakati wa Mr. Gray Mwakalukwa, kwanini siyo Daniel Yona, kwanini siyo Jakaya Kikwete sababu alikuwa Waziri na mimi nina mkataba wa Bulyankulu na kwanini siyo mawaziri wote, kwa sababu mikataba iliingiwa wakiwa mawaziri" alisema Tundu Lissu 

Lakini mbali na kusema yote hayo Tundu Lissu alitoa ushauri wake katika suala hilo...

"Kama unataka kufanya haya unayoyafanya elewa hali halisi ilivyo, tatizo liko wapi kama tatizo ni kwamba tunapata mapato kidogo na kweli wanatupiga kweli kweli ila kama utaka kufanya mambo kweli kweli kajiondoe kwanza MIGA ili hao wawekezaji wasikushtaki kwenye hizo mahakama za huko, maana wakikushtaki kule unanyolewa bila maji, hakuna ndege ya Tanzania itakanyaga hizo nchi wataikamata, hakuna hela tutaweka kwenye nanii za kimataifa watazikamata, kwa sababu tunavunja mikataba ya kimataifa inayolindwa na sheria za kiwekezaji za kimataifa, kwa hiyo anzia huko juu ukimaliza mikataba ya kimataifa, njoo kwenye mikataba kati ya nchi na nchi ondoa hiyo mikataba ukishaondoa hiyo hushtakiki nje, baada ya hapo njoo ndani sababu bado unaweza kushtakiwa ndani" alisisitiza Tundu Lissu 

Kisa Mahojiano ya RC Makonda..Mtangazaji Cyprian Musiba wa Radio Free Africa Aamua Kuacha Kazi

0
0

Mtangazi na kiongozi wa Radio Free Africa bwana Cyprian Musiba ameamua kuacha kazi kutokana na issue ya maadili mara baada ya mahojiano ya Rc Makonda.

Kupitia ukurasa wake wa insta amebainisha hayo.


Ujumbe wa Diamond Platnumz Baada ya Ivan Kufariki Dunia leo

0
0
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Diamond Platnumz ameandika ujumbe huu "Mbele yako, Nyuma yetu" Ujumbe huo ni baada ya Aliyekuwa mume wa Zarina Hassan ‘Zari The Bosslady’, Ivan Semwanga kufariki dunia akiwa hospitali nchini Uganda alipokuwa amelazwa kutokana na matatizo ya moyo usiku wa kuamkia leo Mei 25, 2017.


Ivan aliyekuwa baba wa watoto watatu wa kiume wa Zari, aliachana na mwanamama huyo miaka michache iliyopita ambapo Zari alihamishia mapenzi kwa mwanamuziki Diamond Platinumz ambaye mpaka sasa wamezaa  watoto wawili, wa kike mmoja na wa kiume mmoja.

Ivan alikuwa maarufu Afrika Mashariki kutokana na biashara zake kubwa alizokuwa akifanya zikiwemo umiliki wa vyuo mbali mbali nchini Afrika Kusini, pamoja na Tycoon Ivan.

Zitto Kabwe 'Kwa Hili Sisi ni Matajiri Kuliko Afrika Kusini na Ghana'

0
0
"Mwaka 2016, Afrika Kusini ilizalisha tani 140 za dhahabu na Ghana tani 90 hivyo kuongoza Afrika. Kwa Taarifa ya Prof. Mruma, Tanzania huzalisha tani 112  za dhahabu kutoka kwenye makanikia yaliyokutwa kwenye makontena ya migodi 2 tu ya Buzwagi na Bulyanhulu. Ukiongeza uzalishaji wa migodi ya North Mara na Geita, Tanzania inakuwa mzalishaji mkuu wa dhahabu Afrika nzima.


Sisi ni matajiri Sana. Tunapaswa kuwa Donor Country LoL"- Ameeleza Zitto Kabwe kupitia ukurasa wake wa Facebook leo Mei 25.

Lowassa na Lipumba Wakutana Uso kwa Uso Msibani..Lipumba Akimbilia Kumsalimia Harakaharaka..!!!!

0
0

Baada ya kimya kirefu , hatimaye Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa amekutana na uso kwa uso na Mwenyekiti wa  Chama cha Wananchi (CUF) anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba.

Wawili hao wamekutana leo, Alhamisi katika msiba wa aliyewahi kuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Kitwana Kondo (92) nyumbani kwake Upanga wilayani Ilala.

Wa kwanza kuwasili alikuwa na Profesa Lipumba kisha Lowassa, ambaye alisalimiana na watu waliokuwa karibu yake.

Lakini baada ya swala ya mchana Profesa Lipumba alisalimiana na Lowassa.

Haya Hapa Maneno ya Hekima ya Mzee Lowassa kwa Waislamu Wote Nchini Kuelekea Msimu huu wa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani..!!

0
0

Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa amewatakia mfungo mwema wa Ramadhani Waislamu wote akiwaomba kutumia ibada zao kuwaombea viongozi wa nchi hekima na busara na kuombea nchi amani na utulivu.

Waumini hao wanatarajiwa kuanza mfungo mtukufu wa Ramadhani Jumamosi baada ya mwezi kuandama.

Lowassa amesema kuanza kwa mfungo huo ni kutekeleza moja ya ibada zao muhimu kwa waumini hao.

“Ni kipindi ambacho Waislamu wanatakiwa kutenda mema zaidi na kuwa karibu zaidi na mwenyezi Mungu kwani malipo katika mwezi huu ni mara dufu zaidi ya miezi mingine.”

“Nachukua nafasi hii kuwatakia ndugu zangu Waislamu mfungo mwema katika mwezi huo mtukufu wa Ramadhani, na kuwaomba wafanyabiashara kutopandisha bei za vyakula katika mwezi. Pia nawaomba  ndugu zetu akristo na wa dini nyingine kuwa na ushirikiano na wenzao kama ilivyo desturi yetu, ili watimize ibada hii muhimu kwao.”

“Kwa wale wenye uwezo tuwasaidie wenzetu wasiyokuwa nao na pia katika ibada zetu tuiombee nchi yetu amani na utulivu  na pia kuomba hekima na busara zitawale ndani ya vichwa vya viongozi wetu,”amesema Lowassa.

Polepole Avishukia Vyama vya Upinzani Juu ya Mauaji ya Makada wa CCM na Polisi Yanayoendelea Kibiti..!!!

0
0

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amekemea vikali mauaji yanayotokea mkoani Pwani.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa leo, Alhamisi   Polepole amesema kuwa kama CCM wanataka kuona mauaji hayo yanaendelea kukemewa zaidi.

Polepole ameonyesha  masikitiko yake kwa vyama vya upinzani kukaa kimya badala ya kuungana kama Taifa kukemea mauaji ya watendaji wa CCM yanayoendelea mkoani Pwani.

"Kuungana kwenye ruzuku, hapana vyama vinapaswa kuwa na umoja katika masuala mbalimbali ikiwamo mauaji hayo," amesema Polepole.

Baada ya Rais Magufuli Kufichua Ufisadi Mkubwa wa Serikali ya Awamu ya Nne na Tatu Jana..Afande Awataka Mkapa na Kikwete Kutubu..!!!!

0
0

Msanii wa muziki wa bongo fleva, Afande Sele amefunguka na kusema kama angekuwa ni mmoja kati ya Rais wa awamu ya tatu au awamu ya nne basi angekaa kimya na kujifungia ndani huku akitubu na kuwaomba radhi wananchi kwa mambo waliofanya.

Afande Sele ambaye pia ni mwanasiasa aliyegombea ubunge jimbo la Morogoro Mjini kupitia ACT Wazalendo, amesema hayo siku moja baada ya Rais John Pombe Magufuli kupokea ripoti ya uchunguzi wa madini ambayo imeonyesha kulikuwa na wizi mkubwa jambo lililopelekea Rais kumtengua Prof. Muhongo katika nafasi yake ya Waziri wa Nishati na Madini.

"Baada ya kupata matokeo ya taarifa ya tume iliyoundwa na Rais Magufuli kuhusu usitishwaji wa kusafirisha mchanga wa madini kwenda nje ya nchi. Nimechoka mwili na akili kwa jinsi kama taifa lenye mamilioni ya watu masikini sana tulivyokuwa tunapoteza mabilioni ya dolla kikatili kabisa kwa makusudi ya watanzania wenzetu wachache tena wale tuliokua tumewapa dhamana kuu za kutuongoza." alisema Afande Sele

Afande Sele alizidi kusisitiza kuwa viongozi hao wanapaswa kuomba radhi kwa wananchi kwa madudu ambayo wamefanya kipindi cha utawala wao 

"Kwa sababu uso umeumbwa na haya na kwa sababu mimi siyo mwanahizaya. Laiti kama mimi ningekua ni mmoja kati ya watu hawa daima ningefunga mdomo wangu, ningejifungia ndani kwangu, ningetubu kwa Mungu wangu, ningewaomba msamaha wananchi wenzangu kwani wametia aibu wanapaswa kutubu" alisema Afande Sele 

Kesi ya Scoripon Mtoboa Macho Yafikia Hatua Hii..!!!

0
0

Kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha na kujeruhi inayomkabili Salum Njetwe maarufu ‘Scorpion’ imeshindwa kuendelea kusikilizwa kwa mara ya nne mfululizo baada ya wakili wa utetezi kushindwa kufika mahakamani.

Wakili huyo, Juma Nassoro ameshindwa kufika leo, Alhamisi katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala kwa ajili ya kumtetea mteja wake, baada ya kuwa na kesi nyingine Mahakama Kuu.

Wakili  Mwandamizi wa Serikali, Nassoro Katuga ameiambia Mahakama kuwa alipewa taarifa na wakili huyo kuwa alikuwa na kesi nyingine Mahakama kuu kwa Jaji Wambura.

“Mheshimiwa hakimu,  mshtakiwa yupo mbele ya mahakama yako lakini nimepata taarifa kutoka kwa wakili wake kuwa yupo Mahakama Kuu kwa Jaji Wambura mbapo anasikiliza kesi , hivyo tunaiomba Mahakama yako itoe ahirisho la mwisho na kupanga tarehe nyingine kwa ajili ya  kuendelea na ushahidi”Alidai Katuga.

Hakimu  Mkazi  Flora Haule , anayesikiliza shauri hilo amekubalia ombi la upande wa mashtaka na kuahirisha kesi hiyo hadi Juni 8, mwaka huu na mshtakiwa amerudishwa rumande kutokana na shtaka linalomkabili kutokuwa na dhamana kwa mujibu wa sheria.

Ben Pol Amefunguka Haya Ikiwa ni Wiki Moja Sasa Toka Asambaze Picha Zake za Utupu Mitandaoni..!!!

0
0

Baada ya Ben Pol kuchafua hali ya hewa kwenye mitandao ya kijamii kuanzia Alhamisi ya wiki iliyopita kutokana na picha zake zinazomuonyesha akiwa nusu mtupu kuenea mitandaoni na kumsababishia kukutana na mvua kubwa ya matusi, msanii huyo amefunguka sababu ya kufanya hivyo.

Muimbaji huyo ambaye ameachia wimbo wake mpya ‘Tatu’, ameisema Junanne hii kuwa alifanya hivyo ili kuendana na kasi ya biashara ya muziki ambayo amedai kwa sasa inahitaji matangazo.

“Ile picha unajua muziki umebadilika na unataka kufanya promotion ya kitu chako unatakiwa kutoa material zote ya project yako. Sasa mimi nilikuwa anatoa wimbo ambao unazungumzia ufungwa, mtu ambaye hana uhuru, hawezi kusema,” alisema BenPol. “Kwahiyo mimi nimefanya hivyo ili kuwakilisha kile kitu ambacho nimekifanya ndani ya wimbo, sikuona kama nina sababu na kufanya kitu tofauti wakati kuna njia moja ya kupita ili kufanikishha jambo langu,”

Hata hivyo muimbaji huyo amedai hakufanya vile ili kutafuta kiki kama baadhi ya watu wanavyodai kwenye mitandao ya kijamii.

Serikali Kuingiza Magari 200 ya Doria..!!!!

0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba amesema serikali inatarajia kupokea magari zaidi ya 200 nchini ambayo yatagawiwa katika maeneo mbalimbali yenye uhitaji mkubwa wa katika shughuli za doria na kuimalisha ulinzi na usalama

Mwigulu amebainisha hayo wakati akijibu Bungeni Mjini Dodoma kuhusu mpango wa serikali wa kutatua changamoto wanazopata askari wa jeshi la polisi kuhusiana na uhaba wa mafuta na magari hasa katika kipindi hiki kigumu cha askari kupambana na uhalifu.

"Bajeti hii tuliyopitisha fedha zilizotengwa kwa ajili ya mafuta, doria pamoja na shughuli zingine imeongezeka tofauti ilivyokuwa inatoka awamu ya kwanza mwaka wa fedha uliopita, kwa maana hiyo tutakuwa tumepunguza changamoto kubwa ya ukosefu wa mafuta katika shughuli zetu za doria". Alisema Mwigulu

Vile vile, Waziri aliendelea kufafanua baadhi ya mambo kwa kusema "Mwaka jana tulipokea magari 77 kwa ajili ya askari wetu na kati ya mwezi huu (Mei) mpaka wa saba (Julai) tunategemea kupokea magari mengine zaidi ya 200 na tutayagawa katika maeneo yenye uhitaji mkubwa kwa ajili ya shughuli za doria ikiwemo mikoa ya Kagera, Kigoma, Katavi pamoja na maeneo mengine ambayo wanahitaji magari hayo kwa ajili ya doria katika sehemu zao".

Kwa Wanaume Mlliopanga Kwenye Nyumba za Choo Cha Nnje..Hivi Ndivyo Mnavyogongewa Wake/Madem Zenu Wakati wa Kwenda Kuoga..!!!

0
0

Ewe Mwanaume mwenzangu uliyepanga katika Nyumba ambayo Choo chenu na Bafu lenu lipo kwa nje usije kujidanganya kuwa Demu wako/Mkeo huyo hakusaliti abadan bali leo napenda nikufichulie tu Siri kubwa ambayo karibia akina Dada au Wanawake wengi mliopo nao humo wanavyowasalitini na kukuta kuwa kumbe Mbunye zao hizo huwa mnashea 24/7 na Masela / Wapigaji ( Wezi wa Mapenzi )


Ifuatayo ndiyo mbinu kubwa wanayoitumia na kama wewe msomaji wa kiume hapo ulipo umeshawahi kukutana nayo hii au pengine kila siku inakukuta basi nakuomba kuanzia leo hii andika maumivu na kwamba umeshabanduliwa/kukanyagiwa mno tu.



Ni kwamba Demu/Mkeo akishakuwa na Mahusiano ama na Mwanaume mpangaji mwenzio humo ndani au hata wa Nyumba tu za jirani atakachokifanya ili kila mara aweze Kukusaliti pasipo Wewe kujua ni kwamba Yeye huwa tayari ameshapanga na huyo Hawara yake hivyo kinachofanyika hapo ni kwamba wakati ule Wewe unarudi tu kutoka Kazini na kutaka kwenda Kuoga basi ndipo hapo hapo unapoumizwa.



Kinachofanyika ni kwamba ukisharejea tu Demu / Mkeo ataanza kukuhadaa na kukulazimisha Kwanza ukaoge kisha Yeye anaenda kukuweke maji bafuni na pamoja na Mtaulo wako kisha atarudi kukuambia ukaoge na wakati ule Wewe unaenda Kuoga huku nyuma Yeye anawasiliana na ile Njemba / Msela (Mbanduaji) kuwa akae tayari tayari ili kuliamsha Dude na mara nyingi huyo Mwanaume (Mwizi wa Mapenzi) huwa hachezi mbali na ama Nyumba yenu au Bafu lenu.



Kitendo cha Wewe kutoka tu Bafuni na kuingia ndani huku nyuma yule Mwanaume ( Mwizi wa Mapenzi ) huzama haraka sana mule Chooni / Bafuni kisha Wewe unapoingia tu ndani mwako ukiwa mwenyewe umeshikilia Mndoo na Mboksa wako huku umejifunga Mtaulo wako uliochakaa utamkuta Demu / Mkeo naye tayari keshajiandaa kwenda Kuoga na ukiingia tu ndani na Yeye atakuambia anaenda kuoga mara moja.



Ule muda ambao anakuaga anaenda Kuoga basi jua kuwa tayari yule Mwanaume ( Mwizi wa Mapenzi ) anakuwepo mule Bafuni / Chooni hivyo Kitendo tu cha Demu / Mkeo kuelekea na kuingia mule ndiyo hapo unapoumizwa kwani Kitendo bila kuchelewa na haraka haraka Jamaa huchojoa na kuuchomoa Mkuyenge huku Demu / Mkeo akiwa tayari ameshainama na Mbunye yote imejikusanya tayari sehemu moja kama Magugu Maji ( Water Hyacinth )



kisha Jamaa anauchomeka tu fasta fasta anapiga tako zake saba hadi tisa na anamkojolea / anamnyunyizia madhiwa ya asili kwa bao moja tu na akimaliza yule Demu / Mkeo atajifanya anaoga na kutoka mule Bafuni / Chooni haraka na kurudi ndani mwenu na huku nyuma Jamaa nae anachomoka na kuondoka zake ama nae kurudi humo humo ndani mnakopanga nae au anaenda anapoishi na mchezo unakuwa umeisha.



Poleni sana Wanaume wenzangu mliopanga katika Nyumba zenye Vyoo vya nje / Bafu za nje kwani kiukweli nawaonea mno / sana huruma kwakuwa Mademu / Wake zenu wanawasaliti kwa kiasi kikubwa hasa kwa hii hii mbinu ambayo leo nimeona niwapeni na kwa yoyote atakayeweza na kuwa na roho ya Kishujaa namwomba aijaribu kisha najua atapata mrejesho huu huu niliouweka hapa na pengine hata kunishukuru kwa kuwafichulieni siri hii kubwa ya Usaliti wa Wapenzi / Wenza wenu.


Zijue Silaha Tano Muhimu za Kulinda Maahusiano Yako..!!!

0
0

Maisha ya mapenzi ya kweli ni yale yaliyo na furaha pande zote mbili na kwamba kila mmoja anaridhika na mwenzi wake kwa hali na mali.

Mapenzi kama yanavyosemwa na watu ni sanaa kama sanaa zingine zilivyo. Kama ni mchezo, basi una sheria zake. Leo nakuonyesha mbinu ambazo ukizingatia ndoa yako haitokuwa na matatani.

Ni maoni tofauti tofauti kutoka kwa wadau pamoja na wazoefu wa masuala haya ya mahusiano.
Upendo

Kila mwanaume anataka kujisikia anapendwa. Anataka kuona kuwa mwenza wake anampenda kiuhalisia na anamjali wakati wowote.

Heshima

Hata pale anapokuwa hayupo, anataka mwenzake wake awe nyuma yake, kumuongelea na kumheshimu.

Kukubalika

Kila mwanaume anataka kujisikia mwenza wake anamkubali na kumthamini kwa mambo mbalimbali kama vile penzi lake, muda, jitihada, anavyojituma na kila anachokifanya kwa mwenza wake.

Yeye ni bora zaidi

Anataka mwenza wake kujisikia kuwa yeye ni bora zaidi. Kila mwanaume anataka ajisikie kuwa yeye ni mwanaume bora zaidi kuliko wote aliowahi kuwa nao, na wengine wanataka kujisikia kuwa ni mwanaume pekee ambaye umewahi kuwa naye hata kama anajua si kweli.

Uaminifu

Mwanaume anahitaji mwenza wake awe mwaminifu. Uaminifu husaidia kujenga mapenzi zaidi, kila kitu kwa mwanaume na kadiri mwenzake anavyokuwa mwaminifu, ndivyo hawezi kuwa na wivu kwani anakuwa ameshajiaminisha.

Ukweli

Kila mwanaume anahitaji kujua kuwa anaweza kumwamini mwenza wake na kwamba naye anamwamini, ukiwa mkweli ni rahisi mume kukujengea imani, kuwa mkweli kwa kila jambo.

Mose Iyobo afungukia mipaka ya kuigiza aliyomuwekea Aunt Ezekiel

0
0

Dancer wa WCB ambaye pia ni mzazi mwenza wa staa wa Bongo movie Aunt Ezekiel, Mose Iyobo amefunguka kukubaliana na mpenzi wake huyo kuwa hakuna haja ya kulala kambini wakati wanatengeneza movie bali anatakiwa kurudi nyumbani kila wakimaliza kupiga picha.

Iyobo amezungumza kupitia 255 ya XXL May 25, 2017 na kusema hakuna haja ya Aunt Ezekiel kulala kambini kwa sababu hata hizo scene ana-shoot mchana hivyo ni vizuri arudi nyumbani na hakuna haja ya kulala huko.

“Mwanzoni hiyo hali ilikuwa inaniumiza lakini tulipokubalina kuwa mimi ni baba na yeye ni mama basi vitu vya kambini vikaisha. Kama anaenda ku-shoot siku nzima, aka-shoot na ahakikishe anarudi nyumbani lakini sio kulala huko huko.

“Utalalaje huko wakati una nyumba? Halafu kama ku-shoot hafanyi hivyo asubuhi, sasa kwa nini akalale kambini. Ni kweli haamki mapema, anaamka karibu saa 6 mchana kwa hiyo ni bora alale nyumbani asubuhi aende kazini. Ni wivu tu wa mapenzi na wasiwasi ndio akili sasa kwa nini akalale huko?” – Mose Iyobo

RC Shinyanga azuiwa kuingia mgodi wa Bulyanhulu

0
0

Kahama. Msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Tellack umezuiwa kuingia katika mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu alikokwenda kukagua iwapo uzalishaji unaendelea bila kuwepo kwa Maofisa wa Wakala wa Ukaguzi wa Madini(TMAA).

Maofisa hao waliondoka mara baada ya ripoti ya uchunguzi wa mchanga wa dhahabu kupokelewa na Rais John Magufuli.

Akizungumza kwa njia ya simu jioni hii, Tellack anayefanya ziara ya kikazi wilayani Kahama amesema ameagiza jeshi la polisi kuimarisha ulinzi katika eneo lote la mgodi huo kuhakikisha hakuna mtu anyetoka wala kuingia.

Mapema leo, mkuu huyo wa mkoa alitembelea mgodi mwingine wa Buzwagi ambao pia unamilikiwa na kampuni ya Acacia kama ulivyo ule wa Bulyanhulu.

Katika mgodi wa Buzwagi, Tellack na msafara wake waliruhusiwa kuingia na kishuhudia shughuli za uchimbaji ukiwa umeshitishwa kwa kukosekana maofisa wa TMAA walioondoka mara baada ya Rais Magufuli kutangaza kuvunja bodi na kutengua uteuzi wa watendaji wakuu wa wakala hiyo.
Viewing all 104427 articles
Browse latest View live




Latest Images