Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104764 articles
Browse latest View live

Aliyekuwa Mkurugenzi Tanesco Kabla ya Kutumbuliwa na Rais Magufuli Ageukia Uchungaji..Aaandaa Semina ya Maombezi..!!!

$
0
0

Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umeme Nchini(Tanesco) Mhandisi Felchesm Mramba sasa aibukia Kanisani ambapo ameandaa semina itakayoambatana na maombezi katika kanisa la TAG Changanyikeni.

Yanga Yampigia Magoti Manji

$
0
0

VIONGOZI wa Kamati ya Utendaji ya Yanga wameigomea barua ya kujizulu waliyoandikiwa na mwenyekiti wao, Yusuf Manji na kumuomba abatilishe uamuzi wake huo ili aendelee kuongoza.

Manji, Jumanne iliyopita aliandika barua ya kujiondoa nafasi hiyo huku akitaja sababu kubwa ni kuwapisha watu wengine wapya waiongoze timu hiyo kwa mafanikio.

Wakati anaaga kuondoka, siku hiyohiyo Wenyeviti wa Matawi ya Yanga, haraka walikutana kwenye makao makuu ya klabu hiyo kwa ajili ya kupinga uamuzi huo wa Manji.

Mmoja wa Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga aliliambia Championi Jumamoi kuwa, juzi Alhamisi jioni walikutana na kufanya kikao cha dharura kujadili uamuzi huo wa mwenyekiti wao.

Mtoa taarifa huyo alisema, katika kikao hicho wajumbe hao kwa pamoja walikubaliana kukutana na Manji kumuomba aendelee kuiongoza timu hiyo kwa kipindi chote alichokibakiza.

“Ni ngumu kukubali kirahisi kumuachia Manji aondoke Yanga, kama uongozi tumeipata barua ya Manji ya kuomba kujiuzulu katika nafasi yake, lakini niseme tu huu siyo wakati wake kuondoka.

“Wajumbe tumekataa na tumeikataa barua yake aliyoikabidhi kwa viongozi na jana (juzi) tulikutana na kujadiliana juu ya hilo na tumefikia muafaka wa Manji kuendelea na nafasi yake,” alisema mjumbe huyo.

Alipotafutwa Katibu Mkuu wa Yanga, Boniface Mkwasa kuzungumzia hilo alisema: “Hilo la kikao cha dharura kufanyika kwa wajumbe ni kweli walikutana na kwa upande wangu siwezi kulizungumzia hilo.”

Zitto Kabwe:Tulipofikishwa ni kwasababu hatujua Utajiiri wa Nchi ni Mali ya Nani?

$
0
0

Kiongozi wa Chama Cha Act-Wazalendo Zitto Kabwe kupitia kumbukumbu ya Makala yake kwenye Gazeti la  RAIA MWEMA, JAN 10, 2013



NANI ana miliki ya dhahabu yote iliyogunduliwa Tanzania hivi sasa? Nani ana miliki yote ya misitu iliyopo nchini? Nani ana miliki ya gesi asilia iliyogunduliwa hivi karibuni mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara? Watanzania wachache sana wanayo majawabu ya maswali haya.


Inasikitisha hata Watanzania tuliopewa fursa ya kuwaongoza wenzetu milioni 45 hatuna majawabu na wala hatutafuti majawabu ya swali hili. Viongozi tunawaambia wananchi kwamba “maliasili ya nchi ni mali ya umma.” Ni kweli mali ya umma? Umma ni nani? Hebu tuangalie mfumo wetu wa miliki ya rasilimali za madini, mafuta na gesi asilia.


Katiba ya sasa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haisemi lolote kuhusu ‘miliki’ ya utajiri wa taifa. Isipokuwa katika ya kifungu cha tisa (c) na (i) na ibara ya 27 (1) suala la maliasili ya nchi limewekewa masharti ya Katiba.


Ibara ya 9 (c) inasema shughuli za serikali zitatekelezwa kwa njia ambazo zitahakikisha utajiri wa taifa unaendelezwa, unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya wananchi wote kwa ujumla na pia kuzuia mtu kumnyonya mtu mwingine. Ibara ya 9(i) inasema matumizi ya utajiri wa taifa yatatilia mkazo maendeleo ya wananchi na hasa zaidi yanaelekezwa kwenye jitihada ya kuondosha umasikini, ujinga na maradhi.


Ibara ya 27 inahusu wajibu wa raia kulinda maliasili ya Jamhuri ya Muungano. Ibara ya 9 kuna masharti ya Katiba ya kujenga Ujamaa. Hakuna ibara ya Katiba inayozungumzia ‘miliki’ ya utajiri wa taifa. Suala hili liliachiwa sheria zilizotungwa na Bunge. Kwa suala utajiri tuliochagua kufanyia kazi katika makala haya sheria hizo ni Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 na Sheria ya Utafutaji wa Mafuta ya Mwaka 1980.


Nani anamiliki madini nchini?


 Sheria ya madini ya mwaka 2010 imesema madini ni mali ya umma, hata hivyo, imeweka masharti ya kuhamisha umiliki huu kwa watu na kampuni binafsi kwa mtindo wa leseni.


Dhahabu ni mali ya umma pale tu utafutaji wake na hatimaye uchimbaji haujatolewa kwa mtu binafsi. Leseni ikishatolewa miliki (mineral right) inahamia kwa mwenye leseni na hapo taifa linabakia kupata mrabaha tu kama tozo ya uvunaji wa rasilimali hii.


Kiuhalisia, mfumo huu unaruhusu maliasili ya nchi kumilikiwa na watu binafsi wawe raia wa Tanzania au la. Angalia mfano huu.


Kampuni iitwayo ZiMinerals LTD kutoka Canada inakuja Dar es Salaam katika Wizara ya Nishati na Madini na kuomba leseni ya kutafuta dhahabu huko Kahama. Wizara inampa leseni ya utafutaji ya mamia ya kilometa za mraba. ZiMinerals inakwenda kujiandikisha katika soko la mitaji la huko Australia na kuanza kukusanya fedha kwa kutumia leseni ya utafutaji dhahabu Tanzania.


Ikishapata fedha inaanza kazi ya kutafuta na baada ya kupata kiwango cha dhahabu wanatangaza na bei ya hisa za kampuni hii zinapanda maradufu. Serikali inaipa kampuni hii leseni ya kuanza kuchimba na kampuni sasa inaanza kuuza dhahabu duniani au inauza miliki hii kwa kampuni nyingine kubwa na yenye uzoefu zaidi au mtaji zaidi.


Kitendo cha ZiMinerals kuuza hisa zake huko Australia tayari miliki ya rasilimali iliyopo Tanzania inakuwa inamilikiwa na wananchi wa nchi hiyo au raia wa nchi nyingine yoyote duniani mwenye kuweza kununua hisa katika soko ambalo hisa za ZiMinerals zinauzwa.


Hivi ndivyo inafanyika. Wanakuja watu hawana hata nguo ya kubadili, wanapata leseni wanakwenda kwao kukopata fedha kwenye masoko ya mitaji na wanakuwa matajiri wakubwa kwa kutumia miliki ya rasilimali za Tanzania na Watanzania wanabaki fukara.


Hivyo ndivyo ilivyofanyika Bulyanhulu, Kampuni ya Sutton Resources ilipewa leseni, ikaenda sokoni kufanyia biashara leseni hiyo, wakawekeza dola za Marekani 20,000 kwenye utafutaji kisha wakauza leseni yao kwa Kampuni ya Barrick Gold, kwa Dola milioni 348. Kwa hiyo tunaposema maliasili hii ni ya taifa tunajidanganya tu. Ukishatoa leseni kinachobaki cha taifa ni ule mrabaha wa asilimia nne tu kwa mujibu wa sheria mpya ya madini ya mwaka 2010 iliyoshinikizwa na sakata la Buzwagi.


Kwa upande wa rasilimali ya gesi asilia na mafuta hali ni tofauti. Miliki ya umma inakuwa ni milki ya serikali na inasimamiwa na Shirika la Umma la Mafuta, hivi sasa TPDC. Kwa hiyo, kwa mfano, kampuni ya ZiGas Limited kutoka Australia inapokuja hapa nchini na kuruhusiwa kutafuta mafuta au gesi na kisha kuchimba, inakua imeajiriwa na TPDC.


Ikienda kule Australia kutafuta fedha itauza kwenye soko ile asilimia yake tu, mara nyingi ni asilimia kati ya 80 na 85. Lakini pia hata ikiuza mafuta au gesi, kulingana na kiwango cha mauzo hayo, asilimia sio chini ya 60 ya mauzo baada ya kuondoa gharama za uzalishaji inachukuliwa na TPDC (serikali).


Hata hivyo tofauti na madini, mrabaha sasa unalipwa na TPDC kwa serikali na sio hii kampuni ambayo ni kama mkandarasi (contractor) wetu. Kwenye gesi tunaweza kusema mali yetu, ingawa si kwa asilimia 100.


Kwa nini mifumo tofauti?


Hakuna maana yoyote ile zaidi ya umazwazwa (ujuha) tu. Kwa nini kampuni za ndani ama za serikali au za watu binafsi haziendi kutafuta fedha kwenye masoko ya mitaji na kufanya utafutaji na kisha kuvuna utajiri huu? Ni ujuha tu maana yote yanawezekana.


Walipokuja Ophir Energy hapa Tanzania na kupata mkataba wa kutafuta mafuta kwenye kitalu namba moja kule Bahari ya kina kirefu mkoani Mtwara, walikwenda kuuza hisa kwenye soko la mitaji na hisa moja ilikuwa inauzwa senti nne ya Pauni ya Uingereza (4 pences). Huu ulikuwa ni mwaka 2006.


Mwaka 2011 baada ya kupata gesi asilia kwenye visima kadhaa, hisa moja ya kampuni hii ilifika senti 654 ya Pauni (654 pences). Licha ya bei kupanda namna hii lakini pia waliuza sehemu ya kampuni yao kwa Kampuni ya BritishGas na kupata mabilioni ya pauni za Uingereza bila Tanzania kupata lolote licha ya biashara hii kuwa ni mali iliyopo Tanzania.


Hivi kweli baadhi yetu tunasimama na kusema gesi asilia mali ya umma? Dhahabu mali ya umma? Almasi mali ya umma? Tunawadanganya wananchi. Lazima kufanya mapinduzi ya kifikra na kivitendo. Maandamano ya watu wa Mtwara yasukume Watanzania kufukua zaidi kuhusu unyonyaji wa utajiri wa nchi. Mapinduzi ni lazima.


Katiba ya nchi sasa iseme kinagaubaga kuwa rasilimali ni mali ya wananchi (sio mali ya umma). Miliki (mineral right) ya utajiri  wa nchi iwekwe kwenye mikono ya wananchi wenyewe kwenye maeneo ambayo rasilimali imepatikana au inatafutwa. Serikali itakuwa ni msimamizi wa uvunaji wa rasilimali hii kwa manufaa ya wananchi wote.


Wananchi wa eneo ambalo rasilimali inatafutwa au imepatikana wawe na haki ya kuridhia kuvunwa kwa rasilimali hiyo kabla Serikali Kuu haijatoa ruhusa ya kuvunwa kwa rasilimali hiyo (The right of prior informed consent).


Mapinduzi haya ya umiliki wa rasilimali za nchi kutoka kwa serikali kwenda kwa wananchi wa maeneo yenye rasilimali kutawezesha mrabaha wote unaolipwa na kampuni za uvunaji wa rasilimali kulipwa kwa wananchi hawa kupitia serikali zao za mitaa na majimbo (provinces).


Mapato haya ndio yatafidia kuondolewa kwa wananchi kwenye mashamba yao kupisha uvunaji huu au kufidia samaki wanaopotea kutokana na uchimbaji mafuta na gesi kwenye bahari. Ieleweke kwamba mrabaha si kodi bali ni tozo la fidia kwa kunyonya (kuvuna) mali katika eneo husika.


Viongozi tunaposema maliasili ni mali ya taifa tuna maana fedha zitokanazo na maliasili ni mali za taifa. Hivi tumewahi kujiuliza madhara ya uharibifu wa mazingira nayo ni madhara kwa taifa zima?


Kwa mfano madhara ya kuchimba mafuta kule Mtwara, madhara ya kimazingira ikiwamo sumu yanamilikiwa kwa pamoja kati ya Kigoma na Mtwara au Kigoma itafaidi tu dola zitakazotokana na gesi ya Mtwara lakini Mtwara itaumia peke yake na uharibu mkubwa wa mazingira unaotokana na uchimbaji wa gesi.


Tusiwe na midomo mikubwa kuona fedha za kugawana nchi nzima na kufumbia macho uharibifu mkubwa wa mazingira na upoteaji wa maisha unaowaathiri Watanzania wanaoishi kwenye maeneo fedha hizo zinatoka.


Sumu katika Mto Tigite kule Tarime haigawanywi kwa Watanzania wote isipokuwa mapato ya dhahabu, japo nayo ni kidogo tu maana miliki ni ya kampuni binafsi, inayovunwa na kuchafua maji ya mto huu inagawanywa kwa Watanzania wote.


Hatuwezi kuendelea kuwa na taifa ambalo Wilaya ya Geita yenye mgodi mkubwa zaidi wa dhahabu barani Afrika, ukiondoa Ghana na Afrika Kusini lakini ni masikini zaidi Tanzania. Halafu tunasema maliasili ni mali ya taifa. Turudishe rasilimali kwa wananchi.

Waraka wa Tundu Lissu kwa Wanachama wa CCM na Watanzania Wanaounga Mkono Sakata la Mchanga wa Madini..!!!

$
0
0

Na mimi ni Mtanzania pia.

Tofauti kati yangu mimi na wewe na Magufuli ni hii: Mimi nimepigania nchi yangu katika masuala haya tangu mwaka '99.

Wakati huo tulikuwa na mgodi mmoja tu wa dhahabu, Resolute Golden Pride Nzega. Bulyanhulu ilikuwa haijajengwa. Geita ndio kwanza walikuwa wanafukuza wanakijiji wa Mtakuja.

Nadhani nilikuwa wa kwanza katika nchi hii kupiga yowe kwamba tutaibiwa sana kwenye sekta ya madini.

Wewe sijui ulikuwa wapi wakati huo. Najua Magufuli alikuwa wapi: upande wa MaCCM na wawekezaji hawa.

Nimepigana na wawekezaji hawa mahakamani, kwenye medani ya kisiasa ndani na nje ya nchi hii kwa zaidi ya miaka 15. Nimetetea wananchi completely free of charge Bulyanhulu, Tarime, Nzega, Geita, n.k.

Sijui wewe ulikuwa wapi lakini najua Magufuli alikuwa upande wa nani: wa MaCCM na wanyonyaji hawa.

Soma Rai ya tarehe 17 Julai, 2001, uone tulimwambia nini Mkapa siku anaenda kuzindua Mgodi wa Bulyanhulu.

Sijui ulikuwa wapi lakini najua Magufuli alikuwa wapi: alikuwa anatetea tumbo lake na matumbo ya wanyonyaji hawa.

Nilikamatwa na kushtakiwa kwa uchochezi kwa sababu ya Bulyanhulu. Hiyo ilikuwa December 2002. Nilikaa na kesi hiyo mahakamani Kisutu kwa miaka sita.

Sijui ulikuwa wapi ila najua Magufuli alikuwa wapi: upande wa watesi wa wananchi na wanyonyaji wa rasilmali zetu.

Leo Magufuli anajifanya mzalendo na anahoji uzalendo we yeyote anayepingana nae.

Ni muongo. Anatafuta umaarufu wa kisiasa kwa wasiojua na wasiokumbuka. Ataupata. Kwa siku chache tu. Mark my words: ataumbuka na mtaumbuka.

Mimi ninampinga hadharani. Sio mnafiki, na sijahongwa. Ninampinga kwa sababu atatusababishia matatizo makubwa zaidi kuliko tuliyonayo sasa.

Huo mchanga atauachia upelekwe ambako umepelekwa kwa miaka 16 iliyopita. Kama sheria ndiyo hiyo na mikataba ndiyo hiyo hana pakwenda.

Tatizo ninaloliona ni kwamba by the time anawarudishia mchanga wao, Tanzania itakuwa imekuwa a basket case kama Zimbabwe.

Na tutakuwa tumelipishwa mapesa mengi kama fidia na arbitral tribunals za kimataifa kwa kuvunja mikataba na wawekezaji hawa.

Kama kuna anayefikiri uzalendo ni kufumbia macho masuala haya basi huyo na amuunge mkono Magufuli kwenye upofu wake wa kujitakia.

Ripoti ya Prof. Mruma haitamaliza hata nusu saa under serious scrutiny. Zaidi ya majina ya maprofesa walioiandaa, ripoti hii haina credibility yoyote. Ni kazi ya kisiasa iliyopakwa rangi ya usomi.

Kama umefuatilia taarifa za kitaalamu za Bulyanhulu hata kabla ya Barrick Gold kuingia mwaka '99 utajua ninasema nini.

Sutton Resources, Outukumpu Oy na hata STAMICO walishafanya utafiti mkubwa juu ya utajiri wa Bulyanhulu. Taarifa zipo na zimekuwepo kwa hata mbumbumbu wa jiolojia ya madini kama mimi.

Hiki alichoambiwa Magufuli ni rubbish, hata kama ni ya kiprofesa. Rubbish. Hatuibiwi kwenye mchanga, that's the rubbish fed on the unlettered.

Tunaibiwa kwenye sheria. Kama hamuoni hilo then God have mercy on us.

Ukweli Mchungu..Kwa Hili la Mchanga wa Madini..Rais Magufuli Umetuonyesha Sura Yako ya Pili Kuhusu Nafasi Yako ya Urais..!!!

$
0
0

Rais John Magufuli angalau amefanya jambo la ujasiri,haya yalimshinda Rais wa awamu ya nne Mh Jakaya Kikwete ambaye pamoja na kuunda kamati mbili,ile ya Jaji Mark Bomani na ile ya Laurence Masha, baada ya kumaliza kazi ziliwekwa kabatini!.

Kuiweka wazi Ripoti ya Prof Mruma ili watanzania wajue angalau kinachoendelea kwenye mgodi wa Kahama,kumeibua angalau hasira kidogo kwa watanzania,moja ya madhaifu ya watanzania wengi huwa hawakasiriki hata pale wanaponyonywa,wanapoibiwa tena waziwazi!.

Madhaifu makubwa ya watanzania ni upole na unyonge hata pale wanapotendewa mambo ya hovyo,wanaoonyanyaswa,miaka yote wakazi wa Geita,Kahama,Nzega,Tarime,Biharamulo wameishia kitazama tu mali zao zikipanda ndege na kwenda Ulaya,Asia na Marekani!.

Angalau Mrehemu Chacha Wangwe aliyekuwa mbunge wa Tarime alivishinda kwa kiasi chake vita hivi,Wangwe alihakikisha wana wa Tarime wanapata angalau kiasi kidogo,alisimama kidete kuhakikisha kila mkazi wa vijiji vinavyozunguka mgodi wa North Mara wanapata karo ya shule/Chuo kama sehemu ya kufaidi utajiri wao!.

Angalau Tundu Lissu wakati hata akiwa hajawa mbunge alizunguka kuanzia Kahama mpaka Nyamongo akitoa msaada wa kisheria kwa walioitwa wavamizi wa mgodini,nakumbuka akiwa na shirika la wanasheria watetezi wa masuala ya mazingira walitoa masaada wa bure kwa waliokamatwa kwa kudaiwa kuvamia mgodi!.

Nakumbuka jinsi Lissu alivyokumbana na kesi ya uchochezi pale alipopaza sauti baada ya kuwepo kwa taarifa za watu kufukiwa huko kwenye mgozi wa dhahabu wa Bulyanhulu!.

Angalau wewe Lissu uliuweka uwoga pembeni ukaandika kitabu kwa kushirikiana na Mark Curtus mlichokipa jina la "The golden opportunity"kitabu mlichokiandika kwa lugha ya kiswahili na kingereza,kitabu hiki kimeleza kinagaubaga jinsi tunavyoibiwa!.Kama serikali ingeamua kukifanyia kazi kitabu hiki,tusingefika hapa leo!.

Angalau Comrade/wakunyumba Hamis Kigwangala wakati fulani alisimama kidete kupinga wana wa Nzega kuishi maisha ya ufukara wakati Mungu kawajalia dhahabu,ndugu yangu huyu nakumbuka alivyojikuta mikononi mwa polisi!.

Niliwahi msikia Augustino Mrema akizunguka nchi nzima akiwatuhumu Ashanti Gold mine kuwa walimhonga kiongozi wa juu wa serikali ya awamu ya tatu,angalau ulipaza sauti kulikemea hili!.

Angalau Zitto Kabwe ulisimama kidete kuusaka ukweli ndani ya bunge mwaka 2007,juu ya waziri wa kipindi hicho Nazir Karamagi kwenda Uingereza na kusaini mkataba kati ya Tanzania na Barrick ili wachimbe madini Buzwagi!

Angalau Marehemu Dr Sengondo Mvungi ulipinga bila woga kwenye maandiko na hata ulipoalikwa kwenye vyombo vya habari kiongozi mkuu wa nchi kujiuzia mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwila tena kwa bei ya kaptula!

Angalau aliyepata kuwa mbunge Mh Kimaro yeye alipambana bungenu na Mzee Sitta kupaza sauti kupinga kiongozi wa juu kabisa kujiuzia mgodi,kelele hizi zilioazwa sana na Dr Wilbroad Slaa kila akisimama bungeni alikuwa mwiba kuhusu mgodi wa Kiwila,nakumbuka sauti zenu zilizaa matunda mpaka serikali ikatangaza kuurejesha mgodi ule serikalini!.

Angalau kamati ya viongozi wa dini ya haki na amani,mlitimiza wajibu wenu,amlizunguka nchi nzima mkiongozwa na akina Askofu Mkuu Paul Ruzoka,Shehe Fereji na maaskofu wengine na mashehe,nakumbuka jinsi mlivyozuiliwa kuingia kwenye mgodi wa Geita bila kujali nafasi zenu kwenye jamii,jinsi mlivyotafuta ukweli wa kilichoitwa sumu za mto Tigithe huko Mkoani Mara.

Ripoti yenu ambayo hata mimi mlinioatia imethibitisha kuwa majinya mto tigite yalikuwa na sumu kutoka mgodini,watu waliyatumia wakafa,wakababuka,lakini mgodi ukaishia kuwaita wavamizi,watumishi wa Mungu mmeacha alama kwenye utetezi wenu dhidi ya wizi huu!.

Mh Rais Magufuli akiongea kwa uchungu mara baada ya kukabidhiwa ripoti na Prof Mruma,na alichukua hatua pale pale!.

Mh Rais geukia sasa upande wa sheria zako,hawa wakezaji muda wote huo wamekuwa wanafanya biashara halali ya kinyonyaji,serikali ya awamu ya tatu iliasisi huu ukwapuaji wa madini yetu!.

Tarehe 26.3.1997,serikali ilipeleka mapendekezo ya miswada miwili ya sheria,ile ya kodi na ile ya uwekezaji,ikiwa ni kipindi kifupi toka sera ya madini itungwe mwaka 1997.

Serikali ya Mkapa ilikuja na sera za kuwakaribisha wawekezaji na kuvutia mitaji kutoka nje(FDI),ikatunga sheria laini kwa wawekezaji,ikiwapa kipindi kirefu cha kuchota bila kulipa kodi,na hata walipoanza kulipa kodi walilipa kiduchu!.

Haya unayoyalilia Mhe Rais Magufuli ni matokeo ya watanzania kuwa na tabia za kutokasirika hata wanaponyonywa,haya ni matokeo ya wataalamu wa serikali ya awamu ya tatu ya mzee mkala,wabunge wa bunge ya Mzee Msekwa,baraza ka mawaziri la Mzee Mkapa kutuletea na kupitisha kwa hati ya dharua sheria mbili za kodi na ile ya uwekezaji!.

Mh Rais sasa badili sheria,waandae wataalamu wako wa sheria,zungumza nao ujue katika hili taifa litanasuka vipi na unyonyaji huu uliotengenezwa na sheria zetu wenyewe!.

Mh Rais bunge ambalo na wewe ulikuwa sehemu yake,miaka kumi iliyopita liliitaka serikali iipeleke bungeni ripoti ya ukaguzi kwenye sekta ya madini kutoka kutoka kampuni kutoka Marekani ya Alex Stewart Assayers(ASA report).

Nakumbuka ASA baada ya kukamilisha ukaguzi wao,walizungukza na waandishi wa habari,mbaya zaidi hawakusema jambo,walipoambiwa waseme wamebaini nini?jibu likawa,"Kazi tukiyotumwa na serikali imekamilika,hatuwezi sema chochote kwa sababu tunafungwa na sheria za ukaguzi za kimataifa",alisema Alex mbele ya waandishi wa habari jijiji Dsm!

Mh Rais mwaka 2007,Kuliibuka sakata la mkataba wa serikali na kampuni ya madini ya Barrick kutoka Canada juu ya uchimbaji wa madini huko Buzwagi,nakumbuka wewe ulikuwa naibu waziri,waziri wa nishati na madini Ndugu Nazir Karamagi alituhumiwa kusaini mkataba mbovu tena hotelini,bunge lilipoudai mkataba huo,liliambiwa mkataba ni siri,si media wala wabunge wamewahi uona mkataba huo,ni mkataba wa Buzwagi pekee ndiyo baadhi nasikia waliwahi uona baada ya kuvuja!.

Mh Rais badili sheria,ondoa kipengere cha usiri kwenye mikataba hii ya madini na maeneo mengine,ruhusi wananchi kupitia bunge wajadili mikataba hii inayowahusu!.

Na ndiyo maana ya utawala bora wenye dhana kama,uwajibikaji,utawala wa sheria,uwazi,haki za binadamu,n.k.

Ripoti ya Prof Mruma imetupa picha kiduchu cha tatizo kwenye sekta ya madini,hatujajua tunachopoteza Geita,kwenye mgodi mkubwa barabj Afrika,ripoti ya Prof Mruma haijagusa Geita,ripoti hii imepapasa tu kuhusu uhalisia kwenye sekta ya madini!.

Rais badili sheria ili unasuke katika mapambano haya,tunapambana na wizi ,kilio cha muda mrefu,ni sisi hawa hawa tuliojigunga kupitia sheria ya kodi na na ile ya uwekezaji zilizopitishwa kwa mbwembwe kwa hati ya dharura na kutusababishia umasikini,badili sheria Mh Rais tuwabane wawekezaji,ruhusu uwazi,hii ni biashara halali ya kinyama,iliyoruhusiwa na serikali na bunge letu huko nyuma!.

Katika vita hii dhidi ya mali zetu wenyewe,tujilaumu wenyewe,tulitunga sheria mbovu wenyewe,tukazipigia debe wenyewe,zimetifanya masikini,ni wakati wa wanasheria wetu kutuonesha tunapita wapi ili tutoke salama!.

Kumbuka hii ni vita na mabeberu,ukitaka kujua nguvu ya hawa mabwana,fanya utafiti juunya akina nani wanaunda Geopolitics department ya kampuni la GGM!.

Tuwaruhusu wanasheria waoneshe njia,wataalam wa miamba wameshaonesha udhaifu,wasikilizeni sasa magwiji wa sheria,tupo katika kipindi kigumu!.

Wasalaaam!.

TCU Yaachana na Utaratibu wa Kuwapangia Vyuo Wanafunzi..Sasa Kila Mwanafunzi Kujiunga na Chuo Akipendacho..!!!

$
0
0

HATIMAYE Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), imeanza rasmi utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli la kutowapangia vyuo vya kujiunga wanafunzi na badala yake kuwaacha waombe moja kwa moja kwa utashi wao.

Kwa mujibu wa tangazo lililopo kwenye tovuti ya TCU, sasa wanafunzi wanatakiwa kuomba nafasi za masomo kwa mwaka 2017/18 katika vyuo husika na siyo kwa kutumia mfumo uliokuwa ukitumika awali kupitia kwao (TCU).

Aprili 15, mwaka huu, Rais Magufuli alipokuwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa mabweni mapya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), katika utekelezaji wa ahadi yake Juni mwaka jana, alisema utaratibu wa sasa unawachanganya wanafunzi.

 “Ninaamini kama wanafunzi wangepewe nafasi ya kuchagua vyuo wanavyovipenda wenyewe, vyuo vya serikali kama vile UDSM, Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na Chuo Kikuu cha Mzumbe vingekuwa na wanafunzi wengi sana,” alisema.

 Rais Magufuli alisema TCU imekuwa ikiwachagulia wanafunzi vyuo visivyo na sifa na ambavyo havina makazi ya wanafunzi hivyo kusababisha wanafunzi hao kusoma katika mazingira magumu na wanapomaliza masomo yao kukosa ajira kutokana na vyuo hivyo kutokuwa na sifa.

 Aidha, Rais aliitaka TCU kubaki na udhibiti, ikiwamo kuhimiza ubadilishaji wa maarifa/elimu kwa njia ya kuunganisha kimtandao vyuo Vikuu na Vyuo Vikuu, uthibitishaji wa program za kitaaluma, uthibitishaji na uratibu wa udahili wa wanafunzi.

 Mengine ni ufuatiliaji na udhibiti wa elimu bora Vyuo Vikuu na Vyuo Vya Vyuo Vikuu, ukusanyaji na usambazaji wa taarifa/data kuhusu elimu ya juu.

Katika tovuti hiyo, TCU imeainisha sifa za wanafunzi wanaopaswa kuomba kujiunga na masomo ya vyuo vikuu, na kwamba maombi yataanza rasmi Julai 22 hadi Agosti 13, mwaka huu, na masomo yataanza rasmi Oktoba 30, mwaka huu.

Kabla ya mfumo wa sasa, TCU ilioyoanzishwa Julai Mosi mwaka 2005, pamoja na majukumu mengine, ilikuwa na kazi ya kudahili wanafunzi kupitia mfumo uitwao Central Admission System (CAS).

Rais Magufuli Atweet Asubuhi Hii Kuhusu Mradi Mkubwa..!!!!

Jamani Hii Kitu ni Kweli Kwamba Eti Paka Ana Nanii........?!!!

$
0
0

Inasemekana kwamba Paka ndiyo Mnyama pekee ambaye anaweza kwa haraka sana kutambua ama roho mbaya ya Mtu au roho nzuri yake na kwamba huweza kukutambua kwa muda wa kati ya sekunde tatu hadi tano tu kukujua.

Ni kwamba kama ukiwa mmekaa Watu wawili na kuendelea kisha mara ghafla akatokea Paka na kwamba ukimwona tu huyo Paka anawatembelea ( kuwapapasa ) sana Wenzio pale tena bila wasiwasi huku Wewe akikuchunia jua ya kwamba tayari anakuwa ameshajua Kipaji cha Upendo cha wale wenzako na pia kukijua Kipaji chako cha Roho mbaya iliyokutukuka.

Hii kitu imekwenda mbali zaidi na kusemekana kwamba hata kwa Mzazi ambaye una Mtoto wako mdogo ( Toddler ) kama ukitaka tu kujua haraka jinsi tabia yake itakavyokuja kuwa kama akikuwa basi mchukue Paka kisha msogeze nae na ukiona yule Paka anaonyesha ushirikiano nae vizuri kila mara jua umezaa Mtoto mwema na kama ukiona kila ukijitahidi tu kumbeba Paka na kumweka na Mwanao huyo ama Paka analia au anataka kukimbia au pengine hata Kukung'ata jua ya kwamba umetuletea Tanzania Njemba yenye roho mbaya sana.

Je hili lina ukweli gani Wadau?

Karibuni mtiririke na mserereke.

Shikamoo Paka!

Kocha Agoma Kung'atuka Mbao FC

$
0
0

Kocha wa Mbao FC, Ettiene Ndayiragije raia wa Burundi, amesema mkataba wake unamzuia kuanza kufikiria kujiunga na timu nyingine ambazo zinatajwa kumuwania.

Ndayiragije ambaye aliwahi kuinoa Vital’O ya nchini kwao, ameyasema hayo huku kukiwa na tetesi kwamba anatakiwa kwenda kuchukua mikoba ya Mmalawi, Kinnah Phiri ya kukinoa kikosi cha Mbeya City.

Mrundi huyo amesema kuwa, kutokana na mkataba wake alioingia na Mbao, unamnyima nafasi ya kuanza kupigia hesabu timu nyingine.

“Si kweli kama nataka kwenda Mbeya City, mimi ni kocha wa Mbao na watu wanatakiwa kulitambua hilo kwamba sina mpango wa kuondoka sasa hivi na mkataba wangu na Mbao unanizuia kuanza kufikiria kujiunga na timu nyingine, inawezekana ipo timu inayonihitaji lakini binafsi sina taarifa hizo na sijafanya mazungumzo na timu nyingine,” amesema Ndayiragije.

Kocha huyo alisaini mkataba wa mwaka mmoja ambao unaisha hivi karibuni, lakini mwenyewe amesisitiza kuna makubaliano ambayo aliingia na mabosi wake. Makubaliano hayo alidai ni siri yao.

Rais Magufuli Awaapisha Hawa Leo

$
0
0

Dar es Salaam. Rais John Magufuli amewaapisha viongozi mbalimbali walioteuliwa hivi karibuni akiwamo Rajab Luhwavi anayekuwa Balozi wa Tanzania, Msumbiji.

Taarifa iliyotumwa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu imesema wengine walioapishwa ni Tixon Nzunda aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) - anayeshughulikia Elimu.

Wengine ni Bernard Makali ambaye ameapishwa kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa na Clifford Tandari, kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro.

Pia Rais Magufuli amemuapisha Geoffrey Mwambe kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).

“Viongozi wote walioapishwa wameahidi kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi wa hali ya juu katika kuwaletea wananchi maendeleo,” inasema taarifa hiyo

Hafla ya kuapishwa viongozi hao imehudhuriwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan,Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki   Augustine Mahiga na viongozi mbalimbali wa Serikali.

Chadema Yamgeuka Raila Odinga wa Kenya

$
0
0

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimetangaza rasmi kumuunga mkono Uhuru Kenyatta katika uchaguzi wa Kenya utakaofanyika mwezi Agosti mwaka huu.

Msimamo huo umetolewa leo katika mkutano wa Baraza Kuu la Chama hicho unaofanyaki mjini Dodoma, ikiwa ni maamuzi ya Baraza hilo, na kutangazwa rasmi na mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe.

Akizungumzia uamuzi huo, Mbowe amesema sababu kuu ya uamuzi huo ni kugeukwa na mgombea wa muungano wa ODM Raila Odinga, ambaye chama hicho kilikuwa kikimuunga mkono mara zote.

Mbowe amesema "Kwa muda mrefu chama chetu kimekuwa kikimuunga mkono Raila Odinga achukue nafasi ya kuliongoza Taifa la Kenya. Mwaka 2015 ilipofika zamu yetu rafiki yetu Raila Odinga alitugeuka na kumuunga mkono adui yetu. Sisi kama Chama, safari hii tunamuunga mkono Rais Uhuru Kenyatta na Umoja wa vyama vinavyounda JUBILEE".

Chama hicho kinaendelea na Baraza Kuu mjini Dodoma, baada ya hapo jana kumaliza kikao cha Kamati Kuu yake, na kimedhamiria kutoka na maamuzi mazito kuhusu mustakabali wa taifa.

Tumuunge Mkono Mhe.Rais kwa Kupigania Rasilimali za Nchi Zisipotee Lakini Tuzuie Wajinga Wachache ...!!!

$
0
0

Anaandika Malisa Godlisten 
Tumuunge mkono Mhe.Rais kwa kupigania rasilimali za nchi zisipotee lakini tuzuie wajinga wachache wanaotaka kubeba jambo hili kisiasa. Nimemsikia Polepole akiwalaumu watanzania na viongozi wa dini eti wamekaa kimya wakati rasilimali za nchi zikiibiwa.

Ndugu Polepole hajawatendea haki watanzania wala viongozi wa dini, anapaswa awaombe radhi. Hivi waliotuingiza kwenye mikataba mibovu ni viongozi wa dini? Polepole anasahau kuwa mikataba yote ya hovyo inayoliangamiza taifa hili imepitishwa na serikali ya CCM na kuungwa mkono kwa kura nyingi za NDIYO kutoka kwa wabunge wa CCM?

Kimsingi Polepole hana "moral authority" ya kujadili suala hili maana CCM yake na wabunge wake ndio waliotuingiza kwenye matatizo yote haya. Kikubwa anachoweza kufanya Polepole ni kuomba radhi kwa niaba ya chama chake, kwa serikali yake kuliingiza taifa kwenye hasara kubwa. Na sio kuwalaumu viongozi wa dini.

Viongozi wa dini hawatungi sera, hawapitishi sheria, hawana nguvu ya dola. Sasa wanalaumiwa kwa lipi? Yani uache kulaumu wabunge wa CCM waliopitisha sheria mbovu za madini, uje kulaumu wachungaji, mapadri na masheikh? Upuuzi gani huu?

Serikali ya Rais Mkapa ndiyo iliyopitisha sheria inayoruhusu mchanga kusafirishwa nje ya nchi. Kwahiyo kama ni kuibiwa tumeibiwa tangu wakati wa Mkapa. Lakini Mkapa hakuwa TLP wala TADEA. Alikua CCM. Na wabunge wa CCM ndio waliopitosha sheria hiyo kwa wingi wao.

Leo watu walewale waliopitisha utaratibu huo kwa makofi ya shangwe, ndio haohao wanaompigia makofi aliyetengua utaratibu huo. Unafiki.!!

Wabunge wa upinzani walipokataa kupitisha sheria ya madini kwa dharura walifukuzwa bungeni. Walipohoji kwanini sheria nyeti inayolinda rasilimali zetu ipitishwe kwa dharura wabunge wa CCM walizomea.

Waziri Muhongo akasimama na kuwadhihaki wanasheria wa madini kuwa hawajui kiingereza. Spika akawafukuza wabunge wa upinzani, wale wa CCM wakabaki ndani na kupitisha sheria hiyo kwa kura ya NDIYO. Leo watu walewale, wa chama kilekile kilichotuingiza kwenye matatizo badala ya kuomba radhi, wanaibuka na kuwalaumu viongozi wa dini. Huu ni wendawazimu.!

Serikali ya CCM na wabunge wake wametuingiza kwenye matatizo makubwa sana kama taifa. Rais anapochukua hatua tunapaswa tumuunge mkono kwa umoja wetu kama taifa. Rais anafanya kazi ya nchi, sio kazi ya CCM. Kama mnataka afanye kazi ya CCM jengeeni matawi aje kuzindua.

Viongozi wengi wa upinzani walipohoji mambo haya waliitwa wachochezi. Leo Rais anafanya yaleyale ambayo wapinzani walihoji then viongozi wachache wa CCM wanataka kujivika ushujaa. Ujinga wa kiwango cha lami.

Na hili la madini ni moja tu kati ya mengi ambayo serikali ya CCM imetuingiza kwenye matatizo. Huko kwenye utalii, maliasili, uvuvi, uwekezaji etc kuna mengi mazito kuliko haya. Kwa mfano Loliondo kuna mwekezaji amepewa kibali cha uwindaji lakini amegeuza eneo hilo kuwa sehemu ya nchi yake. Ukiingia ktk himaya yake network ya simu ya mitandao ya ndani inapotea na inasoma United Arabs Emirates.

Mwarabu huyo anadaiwa kuwafukuza wakazi wa eneo hilo ambao ni wamasai na kuwachomea nyumba zao na kuchoma mifugo yao. Pia amejenga uwanja mkubwa ambapo ndege hutua moja kwa moja huko mbugani na kubeba wanyama kwenda uarabuni bila kukaguliwa na mamlaka yoyote ya ndani.

Jambo hili limepigiwa kelele na wapinzani kwa muda mrefu lakini wakaitwa wachochezi. Lakini siku Rais Magufuli akiamua kumfukuza huyu mwekezaji, viongozi wa CCM watakua mstari wa mbele kumpongeza Rais, wakati CCM hiyohiyo na wabunge wake wamemlinda Mwekezaji huyo kwa muda wote huu.

Tuache unafiki kwenye masuala ya kitaifa. Polepole aache kuwalaumu viongozi wa dini, instaed akilaumu chama chake na wabunge wake wa CCM kwa kupitisha mikataba ya hovyo inayoligharimu taifa. Rasilimali za nchi hii sio za CCM, sio za CHADEMA sio za ACT. Ni za watanzania wote. Yoyote anayezitetea tutamuunga mkono bila kujali tofauti zetu za itikadi za vyama.!

Malisa GJ

Busara za Steven Job (Mmiliki wa kampuni ya Apple Inc)..!!!

$
0
0

Y.O.L.O-Steven Paul Jobs alikuwa mwanzilishi wa kampuni ya Apple Inc. ,alizaliwa mnamo February 24, 1955 na amefariki akiwa na utajiri wa $19 billion ,na alitangulia mbele ya haki October 5, 2011 akiwa na umri wa miaka 56.

Siku moja akiwa ofisini kwake ,Steven Paul Jobs alimuulizia director of quality wa kampuni ya Apple, aliyekuwa anaitwa Ron Givens ambaye walikuwa wanakaribiana ofisi kuwa, ''Secretary wangu yupo wapi mbona simuoni mpaka sasa ofisini''.?

Baadaye secretary kuja ofisni ,Ron Givens alimueleza secretary kuwa ,bosi ambaye ni , Steven Paul Jobs anakuulizia kwa nini umechelewa kuja kazini ? Secretary alimfuata na kumuelezea Steven Paul Jobs ,kuwa gari yake ilipata matatizo na ndio maana alichelewa kuja ofisini.

Ilipofika mida ya mchana ,Steven Paul Jobs alirudi ofisini na funguo ya gari aina ya Jaguar mpya na kumpa secretary wake na kumuambia ''"Here, don't be late anymore." 

Darasa:Unyoofu wako utawapa watu fursa ya kuiga na usipokuwepo watu watasikitika kukukosa,maana matunda ya kazi njema ni utukufu.Duniani tunapita ila utu na upendo hudumu milele.

Steven Paul Jobs, ametangulia mbele ya haki na kuziacha pesa kiasi cha $19 billion ,ila mimi na secretary wake tunamkumbuka kwa wema wake na moyo wake wa kutoa bila kutangazia watu .We make a living by what we get, we make a life by what we give.#Giving

Ramadan Kareem !! Ramadan Kareem

Diamond Platnumz:Naogopa Kuanguka na Naiogopa Kesho,,!!!

Ukweli Mchungu...Hili la Mchanga ni Pigo Kubwa Sana kwa Upinzani...!!!!

$
0
0

Hatua aliyoichukua Rais juu ya swala hili la Mchanga wa dhahabu ni kitendo kilichoonesha umakini na nia ya dhati ya serikali kusimamia rasilimali zetu hivyo kuongeza imani waliyokuwa nayo wananchi juu ya awamu hii ya uongozi.

Wakati hilo likitokea kitendo hicho cha rais ni moja ya misumari muhimu itakayosiliba kabisa matumaini ya wapinzani.

Kauli za baadhi ya wapinzani katika kukosoa kitendo hiki cha kizalendo ni matokeo na hasira za kupunguziwa hoja za kuinenea mabaya serikali.

Ni jambo lililowazi kuwa mambo hayakuwa sawa huko migodini wengi walilalamika hilo limedhihirishwa na matokeo ya kamati ya wataalam aliyoiunda Rais.

Ila baada ya juhudi hizo za wazi kuonesha mwanga wa utatuzi wa malalamiko yetu ya muda mrefu; wale wale waliokuwa kati ya walalamishi wameanza kugeuka kauli zao na kuanza kutuambia kwamba kilichofanyika ni makosa eti tutapata hasara kama Taifa.

Kauli hizo na nyingine nyingi toka upinzani zinatufanya baadhi yetu tuanze kujiuliza lengo halisi la upinzani hapa nchini ni nini?

Je malengo ya upinzani ni kuibua mabaya tu ili kupata umaarufu?

Je; serikali inatakiwa kukosea tu kila mara ili ikosolewe na upinzani?

Je; serikali haina haki ya kufanya mambo sahihi kwa watu wake?

Je; ni upinzani pekee ndio wenye haki ya kufanya mambo sahihi kwa wananchi.

Je; ni lazima upinzani ukosoe hata yale mazuri ya serikali?

Mwisho wa yote fikra zinamuongoza mtu kuona kama jambo hili jema limepunguza kete za upinzani na upinzani hawajalifurahia kwakua wanakosa agenda za kwenda nazo kwa wananchi.

Na fikra hizo hizo zinakutuma kuona kwamba upinzani wamekosa uzalendo na zaidi sana wanawaza umaarufu wao.

Katika Hili..Rais Magufuli Endelea Kuwa Dikteta Tu...!!!

$
0
0

kulingana na ripoti iliyotolewa  na tume ya rais kuhusu MCHANGA ambao kwa miaka 17 tumekuwa tukiibiwa kama nchi ukiwa na MADINI mbali mbali na kuwa undervalued ili tuibiwe, IMEKASIRISHA sana kila mtu.
Katika hili sitakuwa nimekosea kumwomba Magufuli awe DIKITETA MZURI/BENEVOLENT dictator.

Aina hii ya UDIKTETA huwa INAKUBALIKA maana huwa ni ya mtu anayetaka kuwafanyia WANANCHI wake MAZURI kwa MANUFAA ya taifa lake.

Tunaweza kuiga mfano wa aliyekuwa mwanzilishi wa taifa la Singapore. "Lee Kuan Yew"
Yeye aliwafukuza kazi na hata KUWAFUNGA JELA RAFIKI zake na jamaa zake waliojihusisha na UFISADI.

Na kuiweka nchi yake katika ulimwengu wa KWANZA/ First world na kipato kikubwa zaidi ya baadhi ya nchi za ULAYA.

Ni nini kilichomsaidia? Ni udikteta mzuri. Hakuwa na huruma.
Jambo la kwanza KABLA ya yote FREEZE/ZIFUNGE ACCOUNT zao zote za WATUHUMIWA zilizo na FEDHA NYINGI ambazo source yake ni ya MASHAKA.


Magufuli ukicheka na mtu Tanzania HAITABADILIKA.
Kuagiza vyombo vya ulinzi na usalama vifanye kazi ni vizuri. Lakini KUFUATILIA na KUTENDEA kazi MAAGIZO yako hilo nalo ni lingine.Things should start rolling ASAP& NOW!

Mfano mwingine ni ule wa juzi Juzi wa Rais mpya wa Gambia ame FREEZE Dola millioni 50 zilizokuwa ZIMEIBIWA na rais aliyetoka madarakani Jammeh.

Ukitaka nchi INYOOKE. Ni VIZURI Watanzania waanze kuona MALI ZAO na FEDHA zao zilizoibiwa ZIKIRUDISHWA serikalini. BILA kuwa na HURUMA huyu ni mtoto wa nani ama alikuwa nani.
Usipokuwa DIKTETA mzuri sasa basi Tanzania HATUTAPATA MWINGINE tena.

WACHACHE watalia lakini MAMILIONI ya Watanzania WATAKUPENDA na kusema UMETUOKOA.
Mungu IBARIKI Tanzania na Rais Magufuli

Nimekuwa Mtumwa wa Wanawake

$
0
0

Nimeficha ficha haya mambo ila najiona kabisa naangamia hivyo ni bora leo niombe ushauri maana hapa pana watu wazima, wanasaikolojia na viongozi wa dini.

Mkasa wangu ni wa hakika na bado nipo katika mateso hata sasa.

Wakati nipo balehe nilikutana na wasichana mbali mbali waliouteka moyo wangu na nikawaeleza hisia zangu, kwa bahati mbaya nilijibiwa karaha na kutoswa sababu ya maisha yangu ya dhiki.

Hali ilikwenda hivyo kwa muda mrefu mpaka moyo wangu ukajenga chuki na wanawake, niliwaona hawana usawa na sio wa kuwa nao karibu.

Katika utafutaji wangu wa maisha ghafla mambo yakabadilika na nikawa nina pesa na kuishi vizuri na nikaanza kujenga nyumba na pia nikawa na miradi pamoja na gari ya kutembelea.

Ni hapo ndipo wasichana wakaanza kuwa karibu na mimi na kunihitaji kimapenzi, na mimi nilishajenga chuki moyoni na nikapanga kuwakomoa, nikajikuta natembea na wanawake wengi tofauti kuanzia wanafunzi, walimu, wasichana tu wa mtaani, machangudoa na wapenzi wa watu.

Nikajikuta dhaifu mbele ya wanawake yaani siwezi kulala hata siku moja peke yangu bila mwanamke na pia mda mwingine nilifanya mapenzi na wasichana wawili tofauti kwa siku moja, haswa kama huyo wa pili aliyenitafuta ni mzuri sana.

Haya mambo sipangi bali najikuta tu inatokea na kila nikimaliza najuta na kusema ndio mara ya mwisho ila punde tu naingia katika vishawishi tena, nilioa mke safi kabisa ili niepuke hali hii ila tuliachana baada ya kunifumania mara kadhaa.

Sasa nina mke mwengine na safari hii nimeoa mke wa ndoto yangu mtoto mzuri sana shombe shombe kiasi kwamba marafiki wanasema kweli mwamba umepata kifaa.

Ila bado ninajikuta natembea na rafiki zake pia wasichana wa mtandaoni kama vile Jf, Badoo, Fb nk na pia nimekuwa maarufu madanguro mengi sana mpaka naona noma.

Mara kadhaa nasafirisha mademu wakali toka mikoa tofauti na kunifuata mimi, sihongi sana na wala sijatetereka ki uchumi na wala sijaathirika ila tu najiuliza nini kipo nyuma ya nguvu hii inayonishinda kujizuia?

Kilichonifanya nijione naingia katika hatari ni kwamba, juzi kushinda jana nilikwenda guest na msichana fulani nilikutana nae juu juu tu, tukafanya mapenzi na tulipomaliza wakati tunatoka kuna jitu la miraba minne lilikuwa likituangalia sana na yule msichana akashtuka sana.

Baadae nilipomuuliza akasema yule jamaa anafanya kazi na mume wake ni FFU kitengo cha doria.

Hakika nikaona hiki ni kifo cha wazi sasa na nimefikia pabaya, haya mambo sipangi ila imekuwa kama ulevi na siwezi kuacha.

Naombeni ushauri wa kunijenga wadau

Fifa Yatoa Majibu Kuhusu Malalamiko ya Simba

$
0
0

Shirikisho la Soka la Kimataifa limerudisha majibu ya rufaa ya Simba na kusema, matokeo yanaendelea kubaki kama yalivyo.

Hivyo, kwa majibu hayo ya Fifa, Yanga wanaendelea kubaki mabingwa wa Ligi Kuu Bara na Simba wakiwa katika nafasi ya pili.

Shirikisho la Soka la Kimataifa limerudisha majibu ya rufaa ya Simba na kusema, matokeo yanaendelea kubaki kama yalivyo.

Chenge Afunguka Mazito Sakata la Mchanga wa Madini Kupelekwa Nnje..Awa Mbogo Kuhusu Yeye Kuhusika na Mikataba Mibovu..!!!

$
0
0

Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), kati ya mwaka 1993 hadi 2005, Andrew Chenge, jana alifunguka kuhusu sakata la usafirishaji wa mchanga wa dhahabu kwenda nje ya nchi.

Hata hivyo, akizungumza nje ya ukumbi wa Bunge, Chenge alisema ripoti ya Jaji Mark Bomani ilikuwa ndio mwarobaini wa usafirishaji mchanga huo nje kama mapendekezo yake yangefanyiwa kazi.

“Yawezekana nyinyi hamkumbuki historia. Ripoti ya Jaji Bomani ilitoa mapendekezo ya Serikali ione uwezekano wa kufanya smelting (kuchakata) hapa nchini,” alisema.

“Mtu akikumbumsha kwa jambo jema (kama Rais John Magufuli alivyofanya), atakuambia kwanini hamjafanya toka wakati huo, labda kuna sababu. Lipo kwenye ripoti ya Jaji Bomani.”

“Ukisema kwamba requirement (mahitaji) ya smelter (mtambo) kwa maana ya gharama na production (uzalishaji) iliyopo itakuwa gharama sana basi waambie Watanzania.”

“Unatakiwa ujibu hiyo kwamba production iliyopo pale Buzwagi na Bulyanhulu haitoshelezi na useme je ni suala la umeme au nini au ni hayo makenikia uwaeleze Watanzania watakuelewa.”

Alipoombwa maoni yake kwamba akiwa AG ndipo mikataba mingi iliingiwa, Chenge alikuwa mkali, akihoji “AG kwa kitu gani. AG kwa kitu gani? Rais ameshatoa maoni yake, kuna marais wawili?”

Alisema akiwa Serikalini na Rais wa awamu wa kwanza, Jullius Nyerere walianza na kufafanua kuwa yeye ni mtanzania aliyesomeshwa na kubobea katika mikataba ya madini na petroli.

“Nasema Rais (Magufuli) ameamua kuwakumbusha mapendekezo ya Bomani ambayo kama tungeyatekeleza tusingefika hapo. Baaada ya hapo sasa ndio muulizane inawezekana au haiwezekani?”

Marekani Waonyeshana Ubabe na Korea Kaskazini..Wapanga Nao Kuanza Kufyatua Makombora ya Masafa Marefu..!!!

$
0
0

Idara ya jeshi nchini Marekani imesema  kwa mara ya kwanza itajaribu kudungua kombora la masafa marefu lililo na uwezo wa kufyatuliwa kutoka bara moja hadi bara lingine.

Maafisa wa Pentagon wanasema jaribio hilo litafanyika Jumatano, wiki ijayo licha ya kuwepo na wasiwasi mjini Washington kuhusu uboreshaji wa miradi ya kinyuklia na makombora ya masafa marefu ya Korea Kaskazini.

Wasiwasi huo umeonekana kwa taifa la Marekani kuhusu mpango wa Korea ya Kusini wa kutengeza makombora mbali na mpango wake wa Kinyuklia, ambao una uwezo wa kutengeneza kombora lenye uwezo wa kufikia Marekani.

Viewing all 104764 articles
Browse latest View live




Latest Images