Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

CHADEMA Watangaza Kumuunga Mkono Uhuru Kenyatta..Wadai Raila Odinga Aliwasaliti Mwaka 2015..!!!

0
0

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimetangaza rasmi kumuunga mkono Uhuru Kenyatta katika uchaguzi wa Kenya utakaofanyika mwezi Agosti mwaka huu.

Msimamo huo umetolewa jana katika mkutano wa Baraza Kuu la Chama hicho unaofanyaki mjini Dodoma, ikiwa ni maamuzi ya Baraza hilo, na kutangazwa rasmi na mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe.

Akizungumzia uamuzi huo, Mbowe amesema sababu kuu ya uamuzi huo ni kugeukwa na mgombea wa muungano wa ODM Raila Odinga, ambaye chama hicho kilikuwa kikimuunga mkono mara zote.

Mbowe amesema "Kwa muda mrefu chama chetu kimekuwa kikimuunga mkono Raila Odinga achukue nafasi ya kuliongoza Taifa la Kenya. Mwaka 2015 ilipofika zamu yetu rafiki yetu Raila Odinga alitugeuka na kumuunga mkono adui yetu. Sisi kama Chama, safari hii tunamuunga mkono Rais Uhuru Kenyatta na Umoja wa vyama vinavyounda JUBILEE".

Chama hicho kinaendelea na Baraza Kuu mjini Dodoma, baada ya hapo jana kumaliza kikao cha Kamati Kuu yake, na kimedhamiria kutoka na maamuzi mazito kuhusu mustakabali wa taifa.

Mechi la Juve na Madrid Kuchezwa Huku Paa la Uwanja Likiwa Limefungwa Kuhofia Mabomu ya Kujitoa Muhanga ya Islamic State..!!!

0
0

 Paa la Uwanja wa Taifa wa Wales litafungwa kwa sababu za kiusalama wakati wa fainali ya Ligi ya Mabingwa itakayofanyika mjini Cardiff.

Mashabiki wanaokadiliwa kufikia 170,000 wanategemewa kusafiri na kushudia mechi hiyo dhidi ya Real Madrid hapo Juni 3.

Itakuwa ni mechi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa kuchezwa kwenye uwanja huku paa lake likiwa limefungwa.

Shirikisho la Soka la Wales (FAW) limesema usalama ndiyo kipaombele chao cha kwanza.

Paa litafungwa kwa sababu ya kuhofia mashambulia ya drone kwa kile kinachotokea kunapofanyika mechi kubwa duniani.

Diamond - Nitaenda Kumzika Ivan ..!!!

0
0

Diamond athibitisha kuwa atahudhuria katika mazishi ya Ivan Ssemwanga ambaye alikuwa mzazi mwenzake na Zari The Bosslady.

Muimbaji huyo amesema hayo mbele ya wanafunzi wa Chuo kikuu cha Nairobi, katika kipindi cha The Trend kilichokuwa kinaruka moja kwa moja kupitia runinga ya NTV.

“Kiukweli umekuwa wakati mgumu na mpaka sasa umekuwa wakati mgumu, nilikuwa nipo booked muda kidogo kuhusiana na msiba umetokea, sasa kucancel to ghafla show ya watu unajua inawezekana ukapata twasira tofauti, wengine wakachukulia tofauti sikuwa na jinsi.Lakini niliongea na mzazi mwenzangu akanielewa lakini nikimaliza hapa show nitaenda Uganda kwa sababu ya mazishi na baada ya hapo ndio nitarudi nyumbani,” amesema Diamond

Lowassa Ageuka Mwimbisha Nyimbo Chadema..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo Jumapili 28/5/2017..!!!

Kundi la Kigaidi la Islamic State (IS) Lavamia Malawi na Kuua Askari 40 Chapchap..!!!

0
0

Kundi la wapiganaji wa Islamic State (IS) limevamia mji wa Malawi ambao upo kusini mwa kisiwa cha Mindanao nchini Ufilipino.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Serikali ya Ufilipino imeeleza kuwa zaidi ya siku mbili wanajeshi wa nchi hiyo wamekuwa wakifanya mashambulizi ya anga katika mji wa Marawi, ambao umevamiwa na wanamgambo wa IS.

Chanzo cha mapambano hayo ni baada ya wanajeshi wa Ufilipino kuvamia nyumba moja ikimtafuta Kiongozi wa IS nchini Ufilipino, Isnilon Hapilon na kiongozi wa kundi la Abu Sayyaf.

Wanajeshi Takriban na Polisi 40 wameripotiwa kuuawa kwenye mapambano ya kurushiana risasi, huku maelfu ya raia kukimbia makazi yao.

Pichazzz Hivi Ndivyo David Beckham Alivyotua Bongo Kimya Kimya..!!!

Fahamu Maana ya Ndoto Zinazohusu Nyoka..!!!

0
0

NDOTO NA NYOKA

Maana yake:-

Ndoto za Nyoka zinaashiria mtoto wa kiume, mtu asiyekuwa na heshima, Adui, mali iliyofichwa, ushirikina, mabadiliko, uwezo, kiongozi mbaya, na mwanamke.

Nyoka katika ndoto anawakilisha mtu anayeishi Bondeni, vilevile

Nyoka katika ndoto ni ishara ya uadui kutoka kwa wakwe zako au watoto au ni ishara ya uovu na wivu kutoka kwa majirani zako.

Ukiota unamuona nyoka maana yake ni kwamba utadanganywa na mkeo au mumeo.

Ukiota unapigana na nyoka ni ishara ya kuwashinda au kuwapindua adui zako.

Ukiota unakimbizwa na nyoka ni ishara ya uadui unaokujia kutoka kwa adui yako.

Ukiota umemuona nyoka mwenye vichwa saba ni ishara ya wewe kutenda dhambi au makosa makubwa.

Ukiota unamuona chatu anakushambulia ni ishara ya kwamba mwanamme au mwanamke mwenye uwezo ambaye ni adui yako atakusumbua sana. Kama ukiota ameshindwa kukuumiza maana yake utapewa sifa za uongo. Ukiota umemuuwa ni ishara ya kuwashinda maadui zako.

Ukiota nyoka amejikunja ni ishara ya kupatwa na hatari au kifungo. Pia ni ishara ya kupata maradhi na kuchukiwa na watu.
Ukiota nyoka amelala maana yake ni adui aliyelala hasa kwa mtu ambaye ni muovu.

Ukiota nyoka wa kwenye maji maana yake ni kwamba utapokea msaada au utapata uamuzi kuhusu jambo lako.
Ukiota unafuga nyoka au unamiliki nyoka hiyo ni ishara ya kupata uwezo au madaraka.

Ukiota nyama ya nyoka maana yake ni fedha za adui au ni ishara ya wewe kupata furaha.

Ukiota umevaa ngozi ya nyoka maana yake ni kwamba utamgundua adui yako.

Ukiota umemuua nyoka na damu yake ikakurukia kwenye mikono yako maana yake ni kwamba utamshinda vibaya adui yako.
Ukiota umemwona nyoka anauliwa barabarani hiyo ni ishara ya kutokea vita au magomvi.

Ukiota nyoka mdogo ni ishara ya matatizo kwa mtoto wako au mtoto yeyote unayemhudumia au kumsaidia.

Ukiota unawinda nyoka maana yake ni kwamba utamdanganya adui yako.

Nyoka mweusi katika ndoto ni ishara ya adui yako mwenye nguvu.

Nyoka mweupe katika ndoto ni ishara ya adui mnyonge.

Ukiota nyoka anakusemesha na anakuambia maneno mazuri maana yake ni kwamba utapata bahati ya kukaa vizuri na adui zako na utanufaika nao.

Ukiota nyoka anakusemesha na anakukaripia kwa maneno makali hiyo ni ishara ya kwamba adui yako atakutesa na kukunyanyasa.
Ukiota umegeuka nyoka ni ishara ya kwamba utatoka dini yako na kwenda dini nyingine.

Ukiota umegeuka nusu nyoka na nusu mtu huyo ni ishara ya kwamba utafanikiwa kupunguza nusu ya nguvu za adui yako.

Ukiota umegundua ngozi ya nyoka ambaye imetengenezwa kwa dhahabu maana yake ni kwamba utagundua mali iliyofichwa.

Ukiota nyoka anakumeza hiyo ni ishara ya kupata madaraka makubwa ya uongozi.

Ukiota nyoka amekukalia kichwnai hiyo ni ishara ya kupata heshima kubwa kutoka kwa watu wenye madaraka au viongozi.

Ukiota uwanja mkubwa uliojaa nyoka hiyo ni ishara ya kwamba itanyesha mvua kubwa ambayo italeta madhara.

Ukiota nyoka mwenye pembe ni ishara ya kupata mafanikio ya kibiashara.
Nyoka mweusi na chatu katika ndoto wanaashiria viongozi wa kijeshi.

Nyoka wa majini ni ishara ya pesa au utapata pesa.
Ukiota shamba lako limejaa nyoka ni ishara ya kwamba utapata mazao mengi msimu huo.

Ukiota nyoka anaondoka nyumbani kwako maana yake ni kwamba nyumba yako itavunjwa.

Ukiota umemuua nyoka ni ishara ya ndoa na vile vile utawashinda adui zako na wote wanaokuchukia.

Ukiota unakula na nyoka meza moja maana yake ni kwamba utatengana na rafiki yako.

Ukiota umemwona nyoka wa Jangwani maana yake ni kwamba mtavamiwa na majambazi.

TAFSIRI YA NDOTO 10 ZA KUMUONA NYOKA USINGIZINI

1.unapomuota nyoka amekufa,ni ishara Umeepushwa na uadui na shari yake

2-unapomuota nyoka mdogo ni biashara ya kupata mtoto

3-unapoota umemuuwa nyoka juu ya kitanda chako,utafiliwa na mkeo

4-ukiota umemuuwa nyoka kwa fimbo ni ishara ya kuwa utaowa

5-ukiota umemuuwa nyoka kwa jiwe ni dalili ya kupona sihri uliyonayo na kutoka kwa jini mwilini mwako

6-ukiota umemuuwa nyoka kwa upanga na kumgawa vipande v3 utamtaliki mkeo talaka 3

7-ukiota joka kubwa linajizongazonga mwilini mwako ni dalili ya jini aloingia mwilini anatafuta sehem ya kujificha ndani ako

8-ukiota nyoka anaungua kwa moto ni dalili ya kufanya kazi kwa kile kisomo cha Ruqya alicho fanyiwa mgonjwa

9-ukiota unafukuzwa na nyoka ni dalili ya kuwa jini aliekuingia hajakaa vizuri mwilini mwako,au ni jini afriti jini mbaya anakuandama

10-ukiota una nyoka shingoni mwako ukamkata kata utatoa talaka kwa mkeo

11. Kuota nyoka mara kwa mara ni dalili ya wewe una Jini mahaba ana kuandama mwilini mwako ukiwa ni Mwanamme utakuwa una jini Mwanamke anaye kuharibia nguvu zako za kiume na kukuharibia kazi na maisha yako yanakuwa ni magumu kila unacho kifanya hakiwi. Ukiwa ni Mwanamke unaota kila mara nyoka ni dalili ya wewe kuwa una jini Mwanamme Jini Mahaba anaye kutia mikosi na kukuharibia Wanaume na kizazi chako na maisha yako fanya umtoe haraka.

Credit - Mzizi Mkavu

Polepole: Rais Magufuli Alitaka Kuhongwa Bilioni 300 Ili Asifanyie Kazi Taarifa ya Mchanga wa Madini..!!!

0
0

Humphrey Polepole kasema kuwa Magufuli alitaka kuhongwa Billioni 300 ili asifanyie kazi taarifa ya mchanga wa madini .

Polepole ambaye ni Katibu wa Uenezi wa CCM,amesema hayo kwa uchungu akitoa msimamo wa chama juu ya uchunguzi uliofanyika

Wakati Nchi Ikijiandaa Katika Vita ya Kiuchumi na Acacia, Mfahamu Vizuri Peter Munk,...!!!

0
0

Peter Munk (83), Mkurugenzi Mtendaji na Mwanzilishi wa Barrick Gold Corporation, kampuni inayomiliki zaidi ya asilimia 60 ya Hisa za Acacia.

Alizaliwa November 8, 1927, Ni raia wa Canada, mfanyabiashara na mtoa misaada mashuhuri zaidi duniani . Munk ndie Mwanzilishi na Mwenyekiti wa kampuni kubwa zaidi ya madini duniani ya Barrick Gold Corporation .

Munk alizaliwa katika mji wa Budapest, Hungary, katika familia ya kitajiri ya Wayahudi, kijana wa Katherine (Adler) and Louis L. Munk. Baada ya Hungary kuvamiwa na utawala wa Nazi wa Ujerumani chini ya Adolp Hittler mnamo Machi ,1944 Peter Munk alikuwa kijana mdogo wa umri usiozidi Miaka ishirini. Familia yake ilitoroka kupitia treni ya Kastner , Treni ambyo ilibeba wayahudi takribani 1,684 na kuwapeleka nchini Switzerland, mpango ulioratibiwa na Rudolf Kastner, Mhafidhina wa taasisi iliyojulikana kama Zionist Aid and Rescue Committee .

Taasisi hii ilitumika kuwatorosha Wayahudi kutoka Hungary kufuatia majadiliano na Afisa wa ngazi za Juu ya Ulinzi wa Hungary Adolf Eichmann kwa kubadilishana fedha, dhahabu, almasi kwa kile kilichojulikana kama Mapatano ya damu na vito vya thamani ( "blood for goods" deals )
Munk alihitimu katika Chuo Kikuu cha Toronto, Canada na kutunukiwa shahada ya electrical engineering mnamo Mwaka1952.

Mwaka 1958, Munk pamoja na wenzake walianzisha kampuni ya Clairtone kwa usaidizi David GilmourFrank Sobey. Baada ya hapo, amekuwa na mafanikio na changamoto nyingi katika biashara zake.

Amewahi kuwa Mhadhiri katika Chuo kikuu James Gillies Alumni Lecture, York University, Toronto. Amekuwa mjumbe katika bodi mbalimbali zikiwamo;


  • Trustee of the Toronto General Hospital.
  • Chairman of the University of Toronto Crown Foundation.
  • Member of the World Gold Council.


Pia Munk ni mjumbe wa heshima wa bodi ya taasisi ya Jewish National Fund (JNF) of Toronto, taasisi ambayo imekuwa na jukumu la kupora ardhi ya palestina na kuendeleza makazi ya Wayahudi kinyume na Azimio la Umoja wa Mataifa.

Taasisi hii ndio imekuwa kitovu cha ushirikino wa familia za Wahahudi wote ulimwenguni , ambapo moja ya jukumu lake kubwa ni kurudisha ardhi ya Israel iliyopotea kwa kuchangisha fedha na kununua ardhi kutoka kwa Palestine, kupanda miti, kujenga makazi na miundombinu mbalimbali.

Kutokana na uwezo, ushawishi na mafanikio yake, Munk amepata PHD za heshima katika Vyuo vikuu mbalimbali;


  • Doctorate from Upsala College, New Jersey.
  • Doctorate from Bishop's University, Quebec.
  • Doctorate from Concordia University, Montreal.
  • Doctorate from Technion – Israel Institute of Technology, Haifa, Israel
  • Doctor of Laws from Trinity College, University of Toronto,1995
  • Doctor of Sacred Letters from Trinity College, University of Toronto ,2004


Kutokana na tuzo hizo, Munk anatajwa kuwa afisa ambaye anaheshimika zaidi nchini Canada
Pia ni mwanzilishi wa Munk School of Global Affairs, kupitia mchano wa fedha kutoka taasisi yake ya Peter and Melanie Munk Foundation.


Simba Watoka Matopeni...Warejea Rasmi Kimataifa

0
0

Klabu ya soka ya wekundu wa msimbazi ya simba imetwaa ubingwa wa kombe la shirikisho la TFF baada ya jioni ya leo kuinyuka Mbao FC bao 2-1 kwenye mechi ya fainali iliyopigwa kunako dimba la Jamhuri mkoani Dodoma.

Kwa ushindi huo Simba imejinyakulia milioni 50 na kujikatia tiketi ya kucheza kunako michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika kwa mara ya kwanza tangu msimu wa mwaka 2012/13, huku mshindi wa pili akiambulia patupu zaidi ya medali kwa kuwa hakuna zawadi ya fedha kwa mshindi wa pili wa michuano hiyo.

Wahujumu Uchumi Walitaka Kumhonga Rais Magufuli Bilioni 300, uchunguzi Makinikia

0
0
Ikiwa imepita siku mbili tangu Rais John Magufuli kueleza kuwa kwa sasa nchi iko katika vita ya uchumi na kwamba ana majina ya watu waliotaka kuingilia na kuharibu uchunguzi wa Kamati Maalumu aliyoiunda ili kuchunguza thamani na viwango vya madini vilivyomo kwenye mchanga wenye madini (Makinikia) katika makontena 277 yaliyozuiliwa kusafirishwa nje ya nchi, ili kupoteza ushahidi.

Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Humphrey Polepole Mei 25, 2017 aliibuka na kudai kuwa kuna wahujumu uchumi walitaka kumhonga kiasi cha Bilioni 300 Rais Magufuli, ili kusitisha zoezi la uchunguzi huo, huku akihoji masilahi wanayopata watu wanaofanya biashara ya kusafirisha makinikia hayo nje ya nchi.

“Vita ziko za aina nyingi, ziko zile tunazopigana kwa silaha mtu na mtu, na nchi na nchi, lakini sasa ziko vita za kiuchumi, ni mbaya zaidi zinalenga kuturudisha nyuma.Wahujumu uchumi hawapigani na rais, bali wanapigana na maisha ya wananchi wa Tanzania, tukiwa wamoja tutashinda vita hii, wako watu wanaipinga vita hii yenye dhamira njema, huu si wakati wa kutofautiana ni wakati wa kusimama kumshinda adui,” alisema.

Polepole aliyasema hayo, wakati akitoa wito kwa wananchi, kumuunga mkono Rais Magufuli katika kipindi hiki kigumu kwani nchi iko katika vita mbaya ya uchumi ambayo wahujumu uchumi wamelenga kupigana na maisha ya watanzania na kurudisha nyuma maendeleo ya Taifa.

“Kuna watu walitaka kumhonga rais bilioni 300 ili kusitisha uchunguzi. Walitaka kuhonga bilioni 300 kwa ajili ya kusitisha uchunguzi huo, hivi wao wanapata fedha kiasi gani? Lakini rais akawatolea nje, akasema subirini uchunguzi ukamilike. Tusiamame naye na hakika tutashinda na historia itaandikwa kwamba tulisimama katika kulinda urithi wetu,” amesema.

Katika hatua nyingine, Polepole aliwajibu baadhi ya wanansiasa wanaoikosoa CCM kutokana na viongozi wake waliopita kutunga na kupitisha sheria za madini ambazo zinatetea masilahi ya wawekezaji kuliko nchi, kwa kusema kuwa viongozi walioko sasa ni tofauti na waliopita, na kwamba serikali iliyoko madaraka itarekebisha sheria hizo.

“Tumehujumiwa sana, tumedhurumiwa sana mali za watanzania ambazo tumezirithi kutoka kwa mababu zetu na tuna dhamana ya kuhakikisha zinawafikia watoto wa watoto wetu,” alisema.

Weusi ni Ubunifu Wangu - Nisher

0
0
Muongozaji wa video za muziki wa bongo, Nisher amefunguka kufafanua kwa nini amekuwa akitumia rangi nyeusi katika kazi zake na kudai ni ubunifu wa kujitofautisha na watu wengine wengi wanaofanya kazi hiyo.


Nisher amefunguka hayo baada ya maswali mengi mtaani kuzagaa kwa kipindi kirefu  kwa nini anatumia rangi nyeusi, kwa kudai kwamba video ni kama nguo ikivaliwa leo kesho itapumzishwa hivyo yeye kuweka rangi nyeusi ni kubadilisha mionekano ya rangi za video kama ilivyokuwa imezoeleka hapo awali.

Picha ya  wimbo wa weusi 'Gere' aliouongoza Nisher.

Aidha Nisher amefafanua na kusema kwamba  elimu ya uongozaji wa videoi aliyoipata nchini Marekani inamsaidia sana katika kufanya kazi zake kitaalamu jambo ambalo lilimfanya wasanii wengi kumkimbilia tangu alipojiingiza kwenye tansnia ya muziki.

"Kutumia elimu kwenye tasnia ya video ni nzur kwa sababu inakufanya uwe smart kuanzia kwenye makubaliano ya kazi mpaka ufanyaji wake. Siyo mbaya mtu kutumia kipaji chako cha mtaani lakini ukichanganya na suala la emu lazima mtu atakuwa anakeheshimu jinsi ambavyo unaifanya kazi yako" - Nisher aliongeza.

Akizungumzia kuhusu wimbi la waongozaji video kuongezeka kila Siku Nisher amesema "Ma- directors wanavyoongezeka kila siku ni tafsiri ya kuwa industry yetu imekua, suala la kusema huyu hajui siyo tatizo kwa kuwa hata mtoto anapokuwa anakua kuna mambo anakuwa anakosea mpaka anakuwa mtu mzima. Hivyo ma director wachanga nao wakikosea siyo dhambi kwani na wao wanahitaji muda wa  kujifunza zaidi".

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Maalim HUSSEIN Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa

0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Maalim HUSSEIN Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika

Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote

..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa  PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.

Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14.

Na mengi zaidiWhatsapp +255 674 835107 
Calls +255746757102

Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote.

Mbowe Aeleza Sababu za Chadema Kuamua Kumuunga Mkono Rais Kenyatta Uchaguzi Kenya....

0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe ametangaza rasmi leo kuwa chama hicho kinamuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Kenya, Uhuru Kenyatta katika uchaguzi mkuu wa Agosti mwaka huu nchini Kenya.

Mbowe amesema kuwa uamuzi wa chama hicho kumuunga mkono umekuja baada ya kujiridhisha pasi na shaka kuwa katika kipindi cha uongozi wa Rais Kenyatta, demokrasia imezidi kukua kwa kasi nchini Kenya.

Hayo yamesemwa na kiongozi wa chama kikuu cha upinzani leo katika Mkutano Mkuu wa CHADEMA uliofanyika mkoani Dodoma na kuhudhuriwa na mamia ya viongozi wa chama kutoka maeneo mbalimbali ya nchi.

Akieleza baadhi ya matukio yanayoashiria kukua kwa demokrasia nchini Kenya, Mbowe alisema kwa kipindi chote cha uongozi wa Kenyatta hakuna kiongozi yeyote wa kisiasa aliyewekwa kizuizini, mabadiliko ya katiba, bunge kuachwa kufanya kazi zake kwa mujibu wa sheria na pia viongozi kuheshimu utawala wa sheria.

Baada ya tamko hili la CHADEMA kutolewa leo, baadhi ya watu wamelikosoa na kusema kuwa si sahihi kwa CHADEMA kumuunga mkono Kenyatta kwani akishinda na kuingia madarakani hatoweza kuwaunga CHADEMA mkono kwenye uchaguzi wa mwaka 2020 kwa sababu za kidiplomasia.

Ikulu Yajibu Acacia Kuhusu Mchanga wa Madini

0
0
Uamuzi wa serikali kuhusu suala la kusafirisha mchanga wa madini kwenda nje ya nchi utategemea ripoti ya kamati ya pili iliyoundwa na Rais Magufuli kuchunguza sakata hilo.

Hayo yamesemwa jana na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa ikiwa ni siku moja tangu Kampuni ya Acacia ilipotaka kuundwa kwa kamati huru ya kuchunguza kiasi cha madini kilichomo kwenye makinikia hayo.

“Sijui chochote kuhusu hao Acacia kuomba iundwe kamati huru , lakini tunasubiri ripoti ya kamati ya pili iliyoundwa kuchunguza sakata hili wampelekee ripoti Rais,” alisema Msigwa.

Kamati ya awali iliyokuwa ikiongozwa na Prof. Mruma ambayo ilikabidhi ripoti yake Mei 24 mwaka huu ilionyesha kuwa kiwango cha madini yaliyomo kwenye makinikia hayo ni zaidi ya yale ambayo hujazwa kwenye makabrasha.

Mbali na kuonekana kiasi kuzidi, lakini kamati hiyo ilibaini pia kuna madini makakati (strategic metals) ambayo yamo kwenye makinikia hayo lakini hayakuwa yakitajwa na kampuni zinazosafirisha mchanga nje jambo lililosababisha serikali kupata hasara ya mabilioni.

Kwa upande wao Acacia, walipinga ripoti hiyo na kusema wao hutangaza kila kitu kwa mujibu wa sheria na kulipa tozo zote stahiki hivyo kuomba iundwe kamati huru kuchunguza upya kiasi cha madini kwenye mchanga huo.

JE Dada Unapenda Kuwa Mrembo? Na Kaka Unapenda Kuwa Mtanashati na Kurudisha Heshima ya Ndoa?

0
0
JE, UNAPENDA KUWA NA SHEPU NZURI NA WEUPE USIO NA DOA? MWANAUME UNA TATIZO LA MAUMBILE MADOGO, NGUVU ZA KIUME NA KUKOSA HAMU YA TENDO? @Markson_beauty_pr Inakuletea bidhaa bora na zenye matokeo ya haraka na bila madhara. Pata punguzo kwenye bidhaa hizi 👇👇👇👇

1.HANDSOME UP ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa uhakika na kuimarisha misuli iliyolegea @200000@200,000/=
2.MEN GELY huongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130000@130,000/=
3.MAX MAN 2 huongeza nguvu za kiume na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130000@130,000/=
4.BOTCHO MULT-PLUS 10× huongeza shepu (hips , makalio na mapaja) @200000@200,000/=
5.Kupunguza unene na manyama uzembe @150000@150,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi tena @130000@130,000/=
7.Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito @120000@120,000/=
8.Kupunguza au kuongeza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120000@120,000/=
9.Kushepu miguu (CHUPA YA BIA) na kuondoa vigimbi @120000@120,000/=
10.Kurudisha usichana (bikra) @120000@120,000/= NB : Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako. Ili kuona bidhaa zetu na baadhi ya shuhuda za waliotumia bidhaa zetu 

👇👇 Follow us
@Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr au Wasiliana nasi kwa no
0767447444 au 0714335378.

Samatta Apiga Bao, KRC Genk ikishinda 3 - 0

0
0
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta usiku wa jana amefunga bao la tatu timu yake, KRC Genk ikishinda 3-0 ugenini dhidi ya Sint-Truiden Uwanja wa Luminus Arena mjini Genk, Ubelgiji kwenye mchezo wa Kundi B kuwania tiketi ya kucheza michuano ya UEFA Europa League mwakani.

Hilo linakuwa bao lake la 20 Samatta katika mechi 59 tangu ajiunge na Genk Januari mwaka jana akitokea TP Mazembe ya DRC. Na kwa ushindi huo, Genk inaendelea kuongoza Kundi B katika kuwania tiketi ya Europa League 2018 ikifikisha pointi 26 baada ya kucheza mechi 10.

Samatta alifunga lake dakika ya 55 jana akimalizia pasi ya beki wa Jamhuri ya Czech, Jakub Brabec, baada ya kiungo mkongwe Mbelgiji mwenye umri wa miaka 36 Thomas Buffel kufunga la kwanza dakika ya 32 na kiungo Mholanzi, Jean-Paul Boetius kufunga la pili dakika ya 43.

Kati ya mechi hizo 59, michezo 18 Samatta alicheza msimu uliopita na 41 msimu huu na kati ya hiyo, ni michezo 37 tu ndiyo alianza, 10 msimu uliopita na 27 msimu huu.

Mechi 21 kati ya hizo alitokea benchi, nane msimu uliopita na 13 msimu huu, wakati 11 hakumaliza baada ya kutolewa, tano msimu uliopita na sita msimu huu na katika mabao hayo 19, 14 amefunga msimu huu na tano msimu uliopita.

Kikosi cha KRC Genk jana kilikuwa: Ryan, Uronen, Colley/Janssens dk84, Brabec, Castagne, Berge, Malinovskyi/Heynen dk70, Writers, Boetius/Naranjo dk76, Buffalo na Samatta.

STVV: Pirard, Mechele, The Petter, Peeters/Sart dk62, Gerkens, Ceballos/Abrahams dk77, Dussaut/Bagayoko dk71, Kotysch, Fernandes, Vetokele na Bolingoli.

Lukuvi Afunguka Alivyokuna Wabunge CCM na CHADEMA..!!!!

0
0

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, ameanika sababu za bajeti yake kupitishwa kwa kishindo na wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wa upinzani wakiwamo Halima Mdee na Ester Bulaya wa Chama cha Demnokrasia na Maendeleo (Chadema).

Kuanzia juzi, karibu wabunge wote waliochangia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka ujao wa fedha walimpongeza waziri huyo kwa kuchapa kazi na kuunga mkono bajeti ya wizara yake.

Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe na Waziri Kivuli wa Fedha na Mipango, Mdee ni miongoni mwa wabunge waliompongeza Lukuvi kwa utendaji mzuri wa kazi.

Katika mahojiano na Nipashe nje ya Ukumbi wa Bunge mara tu baada ya bajeti ya wizara yake kupitishwa na chombo hicho cha kutunga sheria, Lukuvi aliwapongeza wabunge kwa kutambua juhudi zake.

"Nafikiri wabunge ndiyo wanajua sababu hasa ya kunipongeza na kuunga mkono bajeti ya wizara yangu, kina Mbowe nafikiri wanajua zaidi kuhusu," alisema.

"Kikubwa nawashukuru wabunge wote kwa 'ku-appreciate' (kuthamini) kazi ambayo ninafanya. Kama unavyojua, baada ya kuapishwa, ilibidi tuingie moja kwa moja kutekeleza kauli mbiu ya 'Hapa Kazi Tu' kwa vitendo.

"Kama ambavyo Mheshimiwa Rais amekuwa akisisitiza tuwatumikie Watanzania wote kwa haki bila kujali hali zao za kiuchumi, vyama vyao vya siasa.

"Wizara yangu inafanya kazi kwa kuzingatia hilo. Tunawahudumia Watanzania wote kwa haki."
Akichangia mjadala huo jana, Mbowe alimpongeza Lukuvi kwa uchapakazi wake na kuwataka mawaziri wengine kufuata nyayo zake.

Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), ndiye aliyekuwa mbunge wa kwanza wa upinzani kumpongeza Lukuvi juzi akilieleza Bunge kuwa mbunge huyo wa
Ismani (CCM) amefanya kazi nzuri anazozifanya katika wizara hiyo na baadaye wabunge wengine wengi wakiwamo wa upinzani wakaendelea kumwaga pongezi kwa uongozi wa wizara hiyo.

Kutokana na hali hiyo, Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya (Chadema), ambaye juzi alikuwa anakalia kiti cha Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, alikiomba Kiti Cha Spika kitengue kanuni ili mjadala huo uhitimishwe jana saa 8:00 mchana badala ya saa 2:00 usiku.

Katika kujemga hoja yake, Bulaya alisema mjadala huo ulipaswa kuhitimishwa mapema kwa kuwa bajeti imeungwa mkono na pande zote mbili.

Mbunge huyo pia alisema haoni sababu ya kurefusha mjadala huo hadi saa 2:00 ilhali wabunge wa chama tawala, Chama Cha Mapinduzi (CCM) na upinzani walichangia kwa kuiunga mkono.

"Kwa kuwa bajeti hii imeungwa mkono na karibu wabunge wa vyama vyote, Mheshimiwa Mwenyekiti, nakiomba Kiti kiruhusu kutengua kanuni ili kikao cha Bunge kesho (jana) kihitimishwe saa 8:00 mchana badala ya saa 2:00 usiku ili kutoa fursa kwa wenzetu Waislamu kuwahi kwenda kuungana na familia zao kuanza mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani," alisema.

Kutokana na ombi hilo, Mwenyekiti wa Bunge, Najma Murtaza Giga, alikubali kutengua kanuni na jana asubuhi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, alitoa hoja ya kutengua kanuni na wabunge wengi wakaridhia mjadala wa bajeti hiyo uhitimishwe saa 8:00 mchana.

Hata hivyo, upitishaji wa bajeti hiyo haukufika hata saa 8:00 mchana, kwani Bunge lilimaliza kazi hiyo saa 7:15 mchana.

Mbali na Mdee, wabunge wengine walimwagia pongezi Lukuvi kwa kazi nzuri, ni pamoja na Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Tarime Mjini (Chadema), Esther Matiko.

Wengine ni Joseph Hasunga (Vwawa-CCM), Anna Lupembe (Viti Maalum-CCM), Balozi Adadi Rajabu (Muheza-CCM), Rashid Shangazi (Mlalo-CCM), Shabani Shekilindi (Lushoto-CCM) na Abdallah Chikota (Nanyamba-CCM).  

Mbali na kumpongeza Lukuvi, Shangazi na Shekilindi walimuomba waziri huyo kuwasaidia kumwondoa mwekezaji wa mradi wa shamba la katani katika Wilaya ya Lushoto ambaye anaendelea na uzalishaji licha ya kunyang'anywa ardhi kwa agizo la Rais.

"Kupimiwa ardhi Lushoto ni shida. Mwekezaji wa shamba la katani anadai ameishika serikali kama alivyosema Shangazi. Mtu huyu anatusumbua sana. Hatujui anajiamini kwa lipi. Nawaaminia sana watendaji wa wizara hii, naamini ninyi hamjashikwa," alisema Shekilindi.

Naye Chikota aliiomba serikali kuajiri watumishi wanaohitajika kutatua changamoto za ardhi nchini hasa jimboni kwake Nanyamba huku akimpongeza Rais John Magufuli kwa kuivunja iliyokuwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Mkuu Dodoma.A

Nikki wa Pili Aaanza Kuingia Wasiwasi na Mtandao wa Diamond wa Wasafi.com..Adai Hautawasaidia Wasanii..!!!

0
0

Msanii wa muziki wa Hip Hop kutoka Weusi, Nikki Wa Pili amefunguka kuzungumzia changamoto zilizopo katika platform mbalimbli za kuuza muziki nchini.

Rapa huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Yakulevya’, amedai Watanzania hawapendi kununua muziki huku akidai bado mambo ni magumu licha ya kunzishwa kwa platform mbalimbali za kuuza nyimbo za wasanii.

“Watanzania hawapendi kununuwa muziki, platform kama Wasafi.Com haita leta tija, kama bado unataka kupata wimbo bure kwenye ma groups ya whatsaap,” alitweet Nikki wa Pili.

Kabla ya Diamond kuanzisha kampuni ya Wasafi.Com, Mkito ndiyo kampuni pekee ya Tanzania ambayo ilikuwa ikiuza nyimbo za wasanii.

Ushauri:Namna ya Kudeal na ACACIA na Makampuni ya Madini na Nishati Kama Nchi..!!!

0
0

1. Tanzania inapaswa kusitisha au kujitoa kwenye Makubaliano ya Kimataifa kuhusu usuluhishi au uamuzi wa migogoro ya kimataifa. Hii itawazuia watakaoguswa kwenda nje kutushtaki na kutubabaisha.

2. Sheria zote za zinazohusu madini na nishati zipitiwe upya na kurekebishwa ili kulinda maslahi ya nchi. Itakuwa ni nafasi ya kurekebisha mrabaha na maslahi mengineyo

3. Mikataba yote ya madini na nishati ifumuliwe na kusukwa upya kwa lengo kama la kwenye nambari 2. Mikataba itamke wazi usuluhishi au uamuzi juu ya migogoro ufanyike katika Mahakama za Tanzania au kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki.

4. Serikali ya Tanzania inapaswa kuwa na hisa katika kila kampuni ya madini au nishati. Hili lielezwe vyema kwenye Sheria na Mikataba. 

5. Kuwepo na timu imara za majadiliano za Serikali kuhusu madini na nishati na vyombo vya usalama vihusishwe kumulika nchi hizo.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images