Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Gwajima Atangaza Kuwaumbua Wanaomchokoza..Adai Atawavua Taulo Hadharani..!!!

$
0
0

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amewatahadharisha wanaomchokoza akisema ni sawa na mtu anayeanzisha ugomvi huku akiwa amevaa taulo.

Akihubiri jana, Gwajima amesema wakiendelea atawavua mataulo ili jamii iwaone.

Bila kufafanua kuhusu kauli hiyo, Gwajima amesema hawezi kunyamaza wakati watu wanaendelea kumfuata fuata.

"Leo nitakwapua mataulo ya   watu,"amesema huku akishangiliwa na waumini wake.

Ikulu ya JPM Yafafunguka Haya Kuhusu Malalamiko ya Kampuni ya Acacia Juu ya Ripoti ya Mchanga wa Madini..!!!

$
0
0

Uamuzi wa Serikali kuhusu suala la usafirishaji wa mchanga wa madini, utategemea ripoti ya kamati ya pili iliyoundwa na Rais John Magufuli kuchunguza suala hilo.

Hayo yamebainishwa jana na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais (Ikulu), Gerson Msigwa ikiwa ni siku moja baada ya kampuni ya Acacia kuitaka Serikali kuunda kamati huru kuchunguza kiasi cha madini kwenye makontena yake 277 yaliyozuiwa bandarini.

Wiki iliyopita, Rais Magufuli alikabidhiwa ripoti na kamati ya kwanza iliyoongozwa na Profesa Abdulkarim Mruma ambayo ilibaini kuwa makontena hayo yana tani 7.8 za dhahabu.

Pia, Acacia wanadai hawakupewa ripoti ya kamati hiyo licha ya kutoa ushirikiano wakati wa uchunguzi.

“Sijui chochote kuhusu hao Acacia kuomba iundwe kamati huru, lakini tunasubiri ripoti ya kamati ya pili iliyoundwa kuchunguza sakata hili wampelekee ripoti Rais,” alisema Msigwa.

Wakati Ikulu ikisema hayo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alizungumzia ripoti ya kamati ya Profesa Mruma na kusema chanzo cha hayo ni sheria mbovu za madini pamoja na mikataba iliyotungwa katika kipindi cha utawala wa Serikali ya Awamu ya Tatu chini ya Rais Benjamin Mkapa. “Tanzania inaruhusu kupitishwa kwa sheria mbovu na wizi halafu baadaye wanapiga kelele, wapinzani tunasema sheria zote lazima zifumuliwe na kupangwa upya,” alisema.

Mbowe ambaye pia ni mbunge wa Hai alionyesha shaka kuwa ni lazima Taifa litaingia kwenye migogoro mikubwa ya kidiplomasia kutokana na ukiukwaji wa sheria unaofanywa ikiwamo sakata la mchanga huo.

Alisema itachukua muda mrefu kwa wawekezaji kuiamini tena Tanzania na kuja kuwekeza kwa kuwa hata waliopo wameanza kuondoka.

Pia, Mbowe alisema kuna tetesi kuwa uchunguzi huo ambao ulimng’oa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo una upungufu mwingi.

Suala la fedha nalo limeibuka katika sakata hilo.

Akizungumzia suala hilo, aliyekuwa mjumbe wa Mpango wa Uhamasishaji wa Uwazi katika Mapato ya Madini, Gesi na Mafuta (Teiti), Bubelwa Kaiza alisema ipo haja ya kupitiwa upya kwa taarifa za fedha za kampuni za madini ambazo zilikuwa zikiwasilishwa.

Kaiza alisema kwa mujibu wa ripoti ya kamati ya kuchunguza mchanga wa madini iliyowasilishwa siku chache zilizopita ni wazi kampuni hizo hazikuwa zikitoa taarifa sahihi.

Alisema Teiti ilikuwa inapitia taarifa za fedha ambazo zilikuwa zinawasilishwa kwa hiari na kampuni husika na si kuchunguzwa, hivyo upo uwezekano walikuwa wanatumia mwanya huo kutoa taarifa za uongo.

Bont wa Mugabe Azidi Kulindikiwa Vyeo Zimbambwe..Ateuliwa Kuwa Mkurugenzi wa Benk..!!!

$
0
0

BINTI wa Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, ameteuliwa kuwa mjumbe wa bodi ya wakurugenzi ya benki mpya nchini humo, ikiwa ni mara ya pili kupata uteuzi ndani ya wiki moja.

Bona (27) mapema wiki hii aliteuliwa kuwa mjumbe wa bodi ya Sensa, jambo ambalo lilisababisha ‘mashambulizi’ dhidi ya Rais kuwa amempendelea na anataka kuiweka familia yake katika nafasi nyeti.

Wakati habari hizo zikiwa bado za motomoto, gazeti la Independent la nchi hiyo limesema binti huyo ameteuliwa kuwa mjumbe wa bodi ya Benki ya Empower, ambayo inamilikiwa na serikali kwa aisilimia 100.

Kuibuliwa kwa taarifa hizo kumesababisha mitandao ya kijamii kushadadia na kusema Bona anaandaliwa mazingira ya kupewa nafasi za juu serikalini wakati ‘umri wa baba yake ukienda saa za magharibi’. Mugabe kwa sasa ana umri wa miaka 93.

Gazeti hilo lilimkariri Waziri anayeshughulikia masuala ya uzawa, Patrick Zhuwao, ambaye ni mpwa wa Mugabe kuwa Bona na maofisa wengine wawili vijana wameteuliwa kuwa  wajumbe wa bodi hiyo si kwa sababu ya taaluma zao bali kutokana na sera ya  wizara kuwapa nafasi vijana.

Pamoja na kulalamikiwa kuwa anapendelewa kutokana na kuwa mtoto wa Rais, Bona ana sifa ya kuwa mjumbe wa bodi hiyo kwa kuwa ana shahada ya uzamili katika masuala ya benki na fedha kutoka Singapore.Hata hivyo, hakuna rekodi zinazoonyesha kuwa alishawahi kufanya kazi benki baada ya kuhitimu elimu yake ya chuo kikuu.

Licha ya kwamba Mugabe hajamtaja mrithi wake pamoja na umri wake kuwa mkubwa, kumekuwa na minong’ono kwamba kiongozi huyo, baba wa watoto watatu, anataka kuweka mazingira kuhakikisha familia yake inaendelea kubaki katika maeneo ya fedha na siasa baada ya kufariki dunia.

Kimenukaa..Zari na King Lawrence Wagombania Mali za Ivan,,King Lawrence Amchana Bila Chenga Zari Kuhusu Kuachana na Ivan,Amwambia Hana Chake..!!!

$
0
0

Kufuati kifo cha mfanyabiashara maarufu nchini Uganda na Afrika Kusini, Ivan Ssemwaga, familia na marafiki wa marehemu wamepinga vikali kuhusu aliyekuwa mkewe, Zarina Hassan kutaka kurithi mali za marehemu.

Hali hiyo imebainishwa na Mtandao wa Big Eye wa Uganda ambao ulimhoji mmoja wa marafiki wa Ivan aliyeeleza hali halisi ilivyo. Chanzo cha habari hii kilisema kuwa Zari amevutana sana na Lawrence Kiyingi ‘King Lawrence’ ambaye alitaka kupora mali za Ivan likiwemo gari la bei mbaya aina ya Lamborghini.

King Lawrence alikuwa rafiki wa karibu wa Ivan na pia ni mwanachama wa kundi la Rich Gang ambalo ni maarufu nchini Uganda kwa kuandaa na ku-host shoo za nguvu.

Chanzo hicho kilieleza kuwa ilifikia wakati madaktari wakawatimua Zari na King Lawrence hospitalini alipokuwa amelazwa Ivan kwa sababu walizua mtiti wakigombana kuhusu mali za Ivan.

“At one point, these fights reached hospital and the two together with other family members had to be thrown out of hospital for the peace and sanity of the sick person. Ivan saw these fights, read some on Facebook but he just could not reply to anything. Someone had to hold the phone for him. And he had no reply just the hissing sounds. Deep down, he must have felt betrayed, used and abandoned by those he considered his closest,” chanzo hicho kilisema.

Zari alionekana kwenye video Instagram akigombana huku akisema kuwa mali za mumewe wa kitambo ni za watoto wake watatu aliowazaa akiwa bado ni mke wa Ivan. Hii ilikuwa siku moja kabla ya Ivan kuaga dunia.

Chanzo hicho pia kilisema kuwa Zari aliwaomba madaktari kuahirisha kutangaza kifo cha Ivan ili aweze kujipanga kabla ili kuwadhibiti wanaopanga kuiba mali za mume wake huyo wa zamani.

Mwanasheria wake aliyetakiwa kuwasiliana naye ili kuweka mipango sawa, alikuwa amesafiri kuelekea Ufaransa ndipo akaomba madaktari wampe siku moja ili kujipanga kabla ya kutangaza msiba huo.

Mrembo huyo alitangaza mwenyewe kifo cha mumewe usiku wa kuamkia juzi Alhamisi baada ya kumaliza kuondoa vitu vyote ndani ya nyumba na kuvihamishia kwingine.

Inasemekana Ivan aliaga dunia Jumanne asubuhi baada ya madaktari kudhibitisha kuwa viungo vyake vya mwili vilishindwa kufanya kazi.

Inasemekana ugomvi wa Zari na familia ya Ivan siyo mpya, ulianza kitambo na chanzo chake ilikuwa ni hizo mali na alichokuwa akiwaeleza ni kwamba mali hizo ni za watoto watatu ambao Zari amezaa na Ivan wakiwa mke na mume.

Kutokana na ugomvi huo, mmoja ya mashabiki kupitia Facebook, alimjibu King Lawrence;

“King Lawrence tafuta maisha yako. Ivan Ssemwanga siyo baba yako. Ivan ana watoto na bado ni wadogo kurithi na kuendeleza mali za baba yao, Zari anaweza kuwasaidia. Ndugu wa Ivan wanaweza kufanya kazi zao wenyewe, acheni kuwa wavivu kugombania mali zisizo za kwenu. Mnataka Zari aachane na mpenzi wake (Diamond) kwa sababu ya mali. Anaweza kuwa na dunia yote……”

Hivi Ndivyo Madini Aliyoshtukia JPM Yanavyosakwa Duniani...!!!

$
0
0

WAKATI Rais John Magufuli akikazia msimamo wa kuzuia usafirishaji nje ya nchi makontena ya mchanga wa dhahabu (makinikia), imebainika kuwa baadhi ya madini yaliyotajwa kuwamo katika mchanga huo, yanasakwa kwa udi na uvumba kutokana na umuhimu wake kiuchumi.

Aidha, imebainika kuwa mataifa yaliyopiga hatua kubwa kiuchumi kwa kuzalisha bidhaa za kielektroniki kama China na Japan, hutegemea madini hayo katika uzalishaji wa bidhaa kama simu za mkononi, kompyuta, DVD, vifaa vya ndege, betri za magari, satelaiti na hadi utengenezaji wa vinu vya nyuklia.

Jumatano iliyopita, Rais Magufuli alipokea ripoti kutoka kwa kamati teule aliyoiunda kuchunguza kila kilichomo katika makontena 277 yaliyoshikiliwa katika Bandari ya Dar es Salaam ili mwishowe kulinda mapato ya nchi. Matokeo ya ripoti hiyo, iliyowasilishwa na mwenyekiti wake, Prof. Abdulkarim Mruma, yalionyesha kuwa kwa ujumla, thamani ya madini yote yaliyokutwa ni Sh. bilioni 829.4 kwa kutumia viwango vya wastani na Sh. trilioni 1.44 kwa kutumia viwango vya juu.

Kwa mujibu wa kamati, kiasi hicho cha fedha ni jumla ya thamani ya madini ya dhahabu, shaba na mengine ya metali mkakati (strategic metals) yaliyokuwa hayarekodiwi kabisa na kudaiwa kuinyima serikali mapato. Madini hayo ya mkakati yalitajwa kuwa pamoja na Sulfur, Iridium, Rhodium, Ytterbium, Beryllium, Tantalum na Lithium,Katika uchunguzi wa Nipashe uliohusisha rejea za taarifa mbalimbali kuhusu metali mkakati, imebainika kuwa madini ya jamii hiyo yana umuhimu mkubwa kwa sasa duniani na ndiyo yanayochangia kwa kiasi kikubwa kuiinua China kiuchumi.

Katika taarifa mojawapo iliyowahi kuchapishwa na jarida la Asia Times, toleo la Novemba 24 mwaka jana, ilionyesha kuwa ni madini ya jamii hiyo ndiyo yanayotumiwa na  China kama silaha kubwa ya vita ya kiuchumi dhidi ya mahasimu wao Marekani walio chini ya Rais Donald Trump na pia Japan, wakitumia kete ya kutishia kutowauzia madini hayo au kuyauza kwa bei ya juu.

Aidha, kwa mujibu wa gazeti la The Telegraph, toleo la Jumapili ya Machi 21 mwaka huu, China ndiyo kinara wa kuzalisha metaliki mkakati, wakishikilia asilimia 97 ya soko lote duniani.

Marekani, Japan na mataifa mengine yaliyoendelea hutumia madini hayo kwa matumizi mbalimbali yakiwamo pia ya kutengeneza vifaa vya udhibiti wa makombora na rada.

Akizungumza na Nipashe jana, Mhandisi wa Madini ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Karim Baruti, alisema metali mkakati zilizotajwa na kamati ya Prof. Mruma zina faida nyingi, ikiwamo kwenye utengenezaji wa vifaa vya elektroniki, mbolea na hata dawa.

MATUMIZI YA METALI MKAKATIWakati akielezea matumizi ya kila metaliki mkakati iliyotajwa na kamati ya kina Mruma, Dk. Baruti alisema Sulfur ndio chanzo kikuu cha ‘sulphuric acid’, inayotumika kutengeneza aina zote za mbolea ya sulfate (ammonium na potash) na pia hutumika kupunguza nyongo ya udongo aridhini kwa ustawi wa mazao. Pia hutumika kutengeneza madawa mbalimbali yakiwamo ya kuangamiza fangasi.

Kuhusu Rhodium, Dk. Baruti alisema kazi yake mojawapo ni kutengenezea vifaa mbalimbali vyenye uwezo wa kustahimili joto kubwa kama kwenye injini za ndege.

Dk. Baruti alisema madini ya Iridium huchanganywa na madini ya Platnum ili kuyaongezea nguvu yaweze kutumika kwenye mazingira ya joto kali na pia yakichanganywa na Osmium, hutengeza ncha ya kalamu na kompasi (compass bearings).

Akielezea baadhi ya matumizi ya madini ya Tantalum, Dk. Baruti alisema ni pamoja na kutengeneza vifaa vya kielektroniki kama vile kompyuta, simu za mkononi, seti za televisheni na vifaa vingine vya aina hiyo.

Aidha, Dk. Baruti alisema madini ya Lithium hutumika kutengeneza betri za simu za mkononi, vilainishi vya magari na pia hutumika kwenye viwanda vya kutengeneza vioo na katika uzalishaji wa madini mengine ya aluminum.

Kuhusu madini ya Ytterbiaum,  alisema baadhi ya matumizi yake ni pamoja na kutengenezea mashine za X-ray.

Madini ya Beryllium yana matumizi mengi muhimu kwa dunia ya sasa pia ikiwamo kutumika katika vipimo vya X-rays, utengenezaji wa ndege, satelaiti, vifaa vya kuzuia milipuko na pia katika vinu vya mionzi ya nyuklia.

Uwezo wa Kujibu Maswali ya Interview Unaombeba Diamond Platnumz

$
0
0

HE IS THE MASTER OF ANSWERS NA KAMA KUNA KITU AMBACHO KINAFANYA INTERVIEW NYINGI ZA Diam ZIWE NA MVUTO NI UWEZO MKUBWA ALIONAO WA KUJIBU MASWALI HASA LINAPOKUJA SWALA LA KUULIZWA KUHUSU UTOFAUTI BAINA YAKE NA MTU FLANI.

Naweza kiri kabisa kuwa Diamond amekuwa anajitahidi sana ku hannd dle maswali yanayohusu yeye na Ali Kiba na anapojibu amekuwa anaweka kwanza u Tanzania mbele na kuhakikisha anazuia watu kutumia matatizo yao kama njia ya wao kufanikisha mambo yao.

Nakumbuka kwenye XXL kipindi kile ndio ametoka kutupiwa makopo kwenye fiesta alifanyiwa interview na akaulizwa juu ya kile kilichotokea watu wakiwa wanafikiri diamond atasema wale waliorusha makopo ni watu wametumwa na hasimu wake alijibu tofauti kabisa kitu kilichofanya kila mtu ashangae jinsi alivyokuwa mtulivu wakati wa kujibu mpaka nakumbuka Adam Mchomvu alikiri kuwa majibu ya Diamond ni majibu ambayo huwezi yategemea kuwa yanajibiwa na mtu ambaye ametoka kuzomewa.

Diamond naamini kungekuwa na tuzo ya kujibu maswali angekuwa ashapewa nyingi.Ila kitu cha msingi kwake anaendeshwa na busara na hekima sio hisia mana ukiwa ubafanya interview halafu unajibu kwa hisia zako eidha za chuki ndio mwisho wa siku mtu anapaniki.

KATIKA REKODI YANGU SIJAWAHI KUONA DIAMOND AMEPANIKI KWENYE INTERVIEW HATA SWALI LIWE LAKUKERA KIASI GANI.

MASWALI ANAYOKUTANA NAYO DIAMOND KUHUSU MUZIKI,MAISHA YAKE YA MAHUSIANO,FAMILIA KWA UJUMLA NA KASHFA ANAZOZUSHIWA ANGEKUWA HAJAPEWA UTULIVU NA HEKIMA KUNA KILA SIKU ANGEKUWA ANAGOMBANA NA WATANGAZAJI NA KUSUSIA MAHOJIANO.

By Abby

Mambo 10 Ambayo ni Sumu Katika Mapenzi

$
0
0
KATIKA harakati zako za kutafuta mpenzi, unaweza kukutana na mwanamke ambaye kwa sababu moja au nyingine anakwondolea uwezo wako wa kufikiri, kutumia mantiki na pia kutumia akili yako ya kuzaliwa. Si lazima awe amekufanyia kitu, lakini inaweza kuwa ni ulevi wako tu unaosababisha ufanye mambo yasiyo ya kawaida. Pengine ndiyo maana baadhi ya wasanii huzungumzia suala la “kudata” kutokana na mapenzi.

Ni jambo jema kudhani kuwa wewe na mpenzi wako mnapendana kwa dhati na kwamba kila mmoja amefika kwa mwenzake, lakini kama mojawapo ya mambo haya kumi yaliyoelezwa hapa chini litajitokeza, basi fahamu kuwa yamkini umependa kuliko kawaida, yaani ni kama umenyweshwa sumu ya penzi. Kumbuka kupenda ni kuzuri, lakini kupenda kupindukia kunaweza kukutumbukia nyongo, kwani katika kila jambo kinahitajika kiasi.

1. WIVU WA KUPINDUKIA
Ni jambo jema kwa mwanamume kumtakia heri mpenzi wake na kufanya kila awezalo kuhakikisha kuwa hapati madhara, lakini iwapo utakuwa mtu wa wasiwasi na mashaka pale unapomwona mpenzi wako akizungumza na mwanamume mwingine, au anapotoka na marafiki zake wa kike, au anapovaa nguo inayomfanya atamanishe, basi fahamu kuwa tayari umekunywa sumu ya mapenzi.
Katika uhusiano wa kimapenzi, kuaminiana ni jambo muhimu sana. Kama kweli unataka mpenzi wako akupende kwa dhati, mwoneshe kuwa unamwamini na unaheshimu maamuzi yake, ikiwa ni pamoja na maamuzi ya kutoka na marafiki zake wa kike na kuwa na marafiki wa kawaida wa kiume. Ondoa hofu na acha kabisa kumpeleleza, maana wapo wanaume ambao hutumia muda wao mwingi kuwapeleleza wapenzi wao ikiwa ni pamoja na kuwategeshea kamera na rekoda za simu.

2. KUTOMWACHIA NAFASI MPENZI
Kama huishi na mpenzi wako ni jambo la kawaida kuwa na hamu ya kumwona mara kwa mara, lakini kumbuka kuwa mpenzi wako naye ana maisha yake na anahitaji nafasi ya kuwa peke yake kwa ajili ya mambo yake binafsi.
Hisia za kutaka kuwa na mpenzi wako muda wote zinaweza kudhaniwa kuwa ni za mapenzi ya dhati, lakini kwa hakika hiyo si ishara njema ya mapenzi ya kudumu. Hebu jiulize kama unaweza kuendeleza hali hiyo maisha yako yote. Ni wazi kuwa utachoka. Kwa hiyo, mpe mpenzi wako fursa ya kupumua. Namna hii mpenzi wako atajenga hamu ya kutaka kukutana nawe lakini ukiwa naye muda wote hamu hiyo itaisha.

3. KUMWAMULIA MPENZI MAMBO YAKE
Unaweza kujikuta ukisukumwa kumwambia mpenzi wako awe anavaa nini wakati gani, akutane na nani na kwa wakati gani au ale nini. Ukiona hivyo, fahamu kuwa hayo si mapenzi, bali umepitiliza na pengine mwisho wa uhusiano wenu unanukia.
Hata ukiachilia mbali suala zima la usawa wa jinsia, hakuna mwanamke ambaye angependa apangiwe kila kitu kuhusiana na maisha yake. Kama ilivyodokezwa hapo juu, kila mtu ana maisha yake na kilichowaunganisha ni mapenzi tu. Kama utataka kumpangia kila kitu ni wazi kuwa utaishia kuishi peke yako.

4. KUMUULIZA MPENZI MASWALI
Iwapo utajikuta ukimuuliza mpenzi wako maswali mengi yanayoonesha wasiwasi wako kuhusiana na mwenendo wake, fahamu kuwa kuna tatizo na tatizo hilo lisipopatiwa ufumbuzi utakuwa mwanzo wa mwisho wa uhusiano wenu.
Mwanamke angependa umuulize maswali ya kawaida kuhusiana na jinsi siku yake ilivyokuwa na kama marafiki zake hawajambo au la, lakini kila jambo lina mpaka wake. Mwanamke hatarajii kuwa kila mnapokutana atakuwa kama ameingia kwenye chumba cha mtihani au usaili wa kazi.

5. KUTOAMINI ANACHOKWELEZA MPENZI
Wakati mwingine watu hushindwa kuwaamini wenzao, lakini kwa sababu ambazo ni za msingi, lakini kuna wakati ambapo mtu hushindwa kumwamini mwenzake bila sababu yoyote ya msingi, au kwa sababu zisizo sahihi, kisingizio kikiwa ni mapenzi.
Kuna tatizo la kisaikolojia la kujishuku au kuwashuku wenzako. Hili ni jambo ambalo linaweza kukuharibia mustakabali wako katika mapenzi, maana husababisha kujengeka kwa mazingira ya kutokuaminiana. Ili uweze kwenda sanjari na mpenzi wako, amini kila anachokweleza hadi pale utakapokuwa na sababu za msingi za kutokumwamini. Na hata unapokuwa umelithibitisha jambo, endelea kuwa katika uhalisia wako.

6. KUACHA HOBI, MARAFIKI
Mahusiano ya kimapenzi mara nyingi huhusisha kila mmoja kuacha baadhi ya mambo yake kwa ajili ya mwenzake. Hata hivyo, lengo ni kuweka tu uwiano wa mahitaji, si kuacha kila kitu ulichokuwa nacho kwa ajili ya mwenzako, ama kwa shinikizo, au kwa kulewa penzi.
Iwapo utabaini kuwa marafiki zako sasa wamekuwa ni marafiki zako wa zamani na hobi zako zimebaki tu katika kumbukumbu japo kwa hakika bado unahisi mapenzi katika hobi hizo, basi tambua kuwa huyo mrembo wako amekunywesha sumu ya penzi na sasa huwezi hata kuitumia vema mantiki yako.

Mbaya zaidi, iwapo utabaini kuwa marafiki zako wapya ni marafiki wa siku zote wa mpenzi wako na hobi zako ni zile za mpenzi wako, basi tambua kuwa huna tena nafsi yako, bali umejisalimisha mzima mzima kwa mpenzi wako. Lakini msemo mmoja wa hekima unatwambia usiweke mayai yako yote kwenye kikapu kimoja. Yamkini unaelewa.

7. KUKUBALI KUPELEKESHWA
Pengine unakumbuka kuwa kuna nyakati ambapo ulikuwa na uwezo wa kujikita katika jambo moja na kulifanya kwa umakini, huku ukiwa pia mwerevu, mjanja na unayejisimamia, lakini leo unayeyuka kirahisi tu kama barafu iliyowekwa juani! Hii ni hatari kwa mustakabali wa maisha yako.
Mbaya zaidi ni pale utakapoiacha kazi yako inayokulipa vizuri na kufanya kazi nyingine kwa ajili ya kumfurahisha mpenzi wako. Ukifika hali hii ujue wewe mwenyewe kuwa hapo hakuna mwanamume.

8. UTAYARI WA KUFA KWA AJILI YAKE
Umewahi kujisikia kuwa na utayari wa kufa kwa ajili ya mpenzi wako? Kama jibu ni “ndiyo”, basi fahamu kwa hakika kuwa hayo uliyo nayo si mapenzi bali ni upumbavu. Pengine huku ndiko kunywesha sumu ya mapenzi. Kwa hakika, hakuna mwanamke ambaye anastahili kumfanya mwanamume yeyote kufa kwa ajili yake.
Yamkini wanaume wanaolengwa katika makala haya si wavulana wanaosoma sekondari, waliobalehe majuzi, ambao wakipenda au kupendwa hujiona kama wako katika sayari yao. Mwanamume aliyepevuka hujiamini na hayaweki maisha yake yote mikononi mwa mwanamke, hata kama mwanamke huyo angekuwa ndiye mrembo wa dunia.

Iwapo, ama kwa ujinga au kwa kufahamu umewahi kumwambia mpenzi wako: “Ukiniacha nitajiua,” na ukawa unaamini hivyo kabisa, basi yamkini unahitaji kutafuta msaada wa ushauri nasaha, maana kwa hakika umepotoka.

9. MUDA WOTE UNAWASILIANA NAYE
Vijana wa siku hizi ni watumiaji wazuri sana wa simu, lakini iwapo utabaini kuwa asilimia kubwa ya muda wako unautumia ama kwa kuongea au kuwasiliana kwa ujumbe mfupi na mpenzi wako, basi fahamu kuwa kuna tatizo ambalo linahitaji ufumbuzi wa haraka.
Kumbuka kuwa mapenzi hayachukui nafasi ya kila kitu. Yamkini huyo mpenzi wako amekukuta unaishi na kuna mambo ya muhimu ya kufanya. Hebu achana na simu kwanza ufanye mambo ya muhimu kuhusiana na maisha yako. Kama mpenzi wako hakwelewi katika hili basi hakufai.

10. NDUGU ZAKE WANAKUFUATILIA
Iwapo utabaini kuwa marafiki, ndugu na jamaa za mpenzi wako wanamtonya mpenzi wako kuhusiana na kile wanachokiita mwenendo wako mbaya, usipuuze hali hii. Kuna uwezekano mkubwa kuwa watu hawa wanayo sababu ya kuwa na wasiwasi na mwenendo wako, kwa hiyo jichunguze na kuangalia jinsi unavyoenenda.
Hata hivyo, jambo hili si ishara njema ya mustakabali mwema wa uhusiano wenu. Iwapo mpenzi wako ataweka watu wake wakufuatilie, maana yake halisi ni kwamba hakuamini. Katika hali kama hii, haitarajiwi kuwa mustakabali wa uhusiano wenu utakuwa mzuri, kwani kutakuwa na uingilizi mwingi wa ndugu, jamaa na marafiki zake. Unaweza kukubali kuendelea kuishi katika hali hii kwa kisingizio cha mapenzi, lakini ukweli ni kwamba hayatakuwa mapenzi bali karaha.

KUWA MAKINI
Kama unavyoona, hizi ni baadhi tu ya dalili kuwa mapenzi yako kwa mwanamke sasa yanaelekea katika ulevi, mithili ya ule wa dawa za kulevya. Jambo moja la kukumbuka ni kwamba kweli mapenzi ni kitu kizuri, lakini pia mapenzi yanahitaji kuwa jambo linaloashiria mustakabali mwema kwa wahusika wawili. Yakiwapo mambo haya kumi hauwezi kuwapo mustakabali mwema katika mapenzi

KUTANA na Mtabibu Ostadhi Khamisi Kutoka Mombasa Kenya Kwa Sasa Yupo Tanzania Kwa Ajili ya Kukupa Matibabu

$
0
0
Kutana na ostadhi khamisi kutoka mombasa Kenya kwa sasa yupo Tanzania ni mtabibu na mtafiti Wadawa za asili anatibia kama vile:
Miguu kuuma
Miguu kufagazi
Miguu kuwakamoto
Chango lauzazi kwakina mama
Dawa ya uzazi wakina mama inapatikana
Kusafisha nyota ili uwe namuonekano kwa kila mtu
Kumrudisha mpenzi wako na liekukimbia ndani yasiku 3 bila yapingamizi yoyote
Kumshika mume au mke asitoke nnje ya ndoa
Pata pete ya Bahati inayo endana na nyota yako
Kurudisha mali ilipotea au kudhurumiwa ndani yasiku 3
Pata utajili usiokuwa namashaliti yoyote
Dawa za nguvu za kiume
Dawa ya biashara inapatikana
Dawa ya kuzuia chuma ulete kwenye biashara inapatikana
 Zindiko la nyumba au shamba
 Anatuliza familia zinazogombana DUWA pamoja navisomo vya ufunguzi wa mwili wako njoo ufunguliwe vifungo ulivyo fungwa kutana na ostadhi khamisi utimiziwe ahadi ulizo hadiwa acha kuteseka acha kuhangaika ostadh khamisi yupupo tanzania kwajili yako...

Call +255718746825 +255754765246 kwa what'sapp +255783708487

Diamond Platnumz: Wasanii wa Kike Wanaliwa Sana, Sitaki Tiffa Awe Msanii

$
0
0
Mwanamuziki Diamond amesema angependa mwanae Nillan awe msanii ila hatapenda mwanae Tiffa awe msanii kwa kuwa wasanii wa kike wamekuwa wakiliwa sana
Amesema pia yeye amepita na wanawake wengi sana kutokana na status aliyonayo ila kwa sasa ametulia na Zari na anampenda kwa kuwa anajua maisha:

Mwili wa Ivan TheDon wawasili Uganda, Zari wa Diamond Alia Kwa Uchungu

$
0
0
Ikiwa ni takribani siku 3-4 tangu Ivan The don (Ex wa zari) kufariki akiwa amelazwa nje ya nchi ya Uganda (southafrica) jana mwili wake umepokelewa kwa machozi na huzuni na watu wa rika tofauti huku mpenzi wake Zari akiwepo katika kuaga mwili wa mpenzi wake wa zamani

Zari amesema atakuwepo pamoja na diamond mpenzi wake wa sasa katika mazishi ya kuuwaga mwili wa Ivan TheDon

Tazama Video:

Pedeshee Jack Pemba Aongea Mazito Kuhusu Marehemu Ivan Don

$
0
0
Pedeshee Jack Pemba aongea mazito kuhusu marehemu Ivan Ssemwenga Adai Marehemu Ivan Don alikuwa ni mshiriki wake wa Kibiashara huko South Afrika

Video:

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Siku ya Leo

$
0
0

Kamanda Sirro Aapishwa Rasmi Kuwa IGP Mpya

$
0
0
Rais John Magufuli amemuapisha mkuu mpya wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro aliyeteuliwa jana kuchukua nafasi ya Ernest Mangu.

Hafla hiyo imehudhuliwa na viongozi mbalimbali akiwemo Makamu wa Rais, Samia Suluhu, Waziri wa Mambo ya Ndani , Mwigulu Nchemba na makamishna mbalimbali wa jeshi hilo.

Sirro baada ya kuapishwa amekula kiapo cha maadili mbele ya Rais Magufuli kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake mapya.

OFFER:Jipatie Water Dispenser Yenye Warrant Ya Mwaka (1) kwa Bei nafuu Mnoo!

$
0
0

*OFA YA MWEZI*

Jipatie Water Dispenser Yenye Warrant Ya Mwaka (1) kwa Bei nafuu Mnoo!

Dispenser mashine ya Friji chini Tsh *300000*

Dispenser Ya Maji baridi&Moto,Haina Friji Tsh 195000/= Kuweka Oda 🔴0743 757575

Tufollow instagram

@beinafuu_Shop
@beinafuu_Shop

Baada ya Kutumbuliwa Kwa Mara ya Pili..Profesa Muhongo Ashauriwa Kurudi Shule

$
0
0

MCHAMBUZI wa masuala ya siasa amemshauri aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini mpaka katikati ya wiki iliyopita, Profesa Sospeter Muhongo kuacha siasa na kurudi chuoni kufundisha elimu ya giologia baada ya kupata 'ajali' mbili za kisiasa ndani ya miaka miwili.

Profesa Muhongo alifukuzwa kazi na Rais John Magufuli Jumatano, ikiwa ni miezi 28 kamili tangu ajiuzulu nafasi hiyo Januari 24, 2015 chini ya Rais wa nne, Jakaya Kikwete.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, Mhadhiri mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Benson Bana alisema baada ya miaka mitano ya ubunge wake ni vyema Prof. Muhongo akarudi kufundisha ambako atatoa uzoefu wa kuwa kiongozi serikalini na mwanasiasa.

"Hatima ya kisiasa amejijengea vizuri kwa kuwa wapiga kura wake wamemuelewa na wana imani naye ndiyo maana walimchagua," alisema mchambuzi Prof. Bana. "Ataendelea kuwa mbunge mzuri wa jimbolake."

"Lakini kwa misukosuko hii asipokuwa na roho ngumu anaweza kukata tamaa."

Prof. Bana ambaye ni mtaalamu wa sayansi ya siasa, alisema kiongozi huyo bado ana nafasi ya kurudi kufundisha vyuoni kwa kuwa ni msomi mzuri wa miamba na madini na kwamba ameshajizolea umaarufu kwenye medali za siasa na kufahamika, ikiwamo uwezo wake kitaaluma.

"Kama mwaka 2020 Rais John Magufuli atapewa ridhaa ya kuendelea kuongoza, Profesa Muhongo hawezi kurudi tena kwenye uwaziri," alisema Prof. Bana hivyo, akitafakari ni vizuri akarudi chuoni kutoa uzoefu wake wa serikalini na kuendelea na umahiri wake wa miamba na madini na kuachana na siasa.

"Siasa na madaraka ya uwaziri ameshaonja, machungu yake ameyaonja, abaki kuwa mshauri... aachane na siasa za leo ambazo ni ngumu sana.
"Kwa wasomi tumezoea kusema baibui ni baibui, lakini kwenye siasa ni tofauti."

Prof. Bana alisema ni wazi hata hivyo kuwa wakati anaingia kwenye siasa, Prof. Muhongo alitegemea mambo hayo kwa kuwa siasa hazina adui wala rafiki wa kudumu.

"Aliingia kwenye siasa na kuaminiwa kwa kiasi kikubwa, akapewa nafasi kubwa serikalini kama ilivyokuwa kwa Profesa Anna Tibaijuka.

"Usomi ndiyo uzoefu wake wa muda mrefu, lakini kama tujuavyo siasa za nchi changa kama yetu unakuwa na madaraka ambayo wengi wanayapigania. Nirahisi kukuangusha kwa namna yoyote."

Kwa upande wake Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alisema hatima ya Prof. Muhongo kisiasa itajukana baada ya kutolewa kwa ripoti ya uchunguzi wa kamati huru kwenye mchanga wa madini.

Alisema kwa sasa ni vigumu kuthibitisha kumhukumu mbunge huyo kwa kuwa changamoto ya kutonufaika kwa Tanzania katika madini yake ilisababishwa na mawaziri waliomtangulia wizarani hapo na kitendo cha serikali kuwasilisha bungeni miswada ya sheria za madini na nishati kwa hati za dharura na kupitishwa haraka bila wabunge kupata muda mwingi wa kuijadili.

"Kifo cha Prof. Muhongo kisiasa ni pale tu ikiundwa kamati huru ya kuchungumza mchanga wa madini na kubaini alihusika katika uzembe uliolisababishia taifa hasa ya matrilioni ya shilingi," alisema.

"Kwa sasa ni vigumu kumhukumu kwa sababu makosa yalifanywa na mawaziri waliomtangulia na serikali ya CCM iliyotengeneza sheria za madini zinazonufaisha wawekezaji."

WAPIGA KURA
Mhadhiri mwingine wa siasa UDSM, Dk. Bashiru Ally alisema bado Prof. Muhongo ana nafasi ya kwenye ulimwengu wa siasa kwa kuwa wenye kuamua hatima yake kisiasa ni wapiga kura wa jimbo la Musoma Vijijini.

Alisema kiongozi huyo amewajibishwa kwa uwaziri na siyo ubunge hivyo ataendelea kuwatumikia wananchi wake ambao wana imani naye.

Alisema mkataba wake na wananchi unaisha baada ya miaka mitano na hatima yake kisiasa iko mikononi mwa wapigakura wake kwa muda wa sasa na miaka ijayo kama atapenda kuendelea kuwatumikia.

Alipotafutwa na Nipashe jana kuzungumzia hatima ya Prof. Muhongo kisiasa, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, alisema mwanasiasa mwenzake huyo bado ana nafasi ya kurejea kwenye Baraza la Mawaziri na hata kuwa kiongozi mkubwa nchini.

"Prof. Muhongo bado ana nafasi ya kusaidia nchi kama mbunge na anaweza kurudi kwenye Baraza la Mawaziri au hata nafasi kubwa zaidi ya hiyo. Mungu tu ndiye anajua mbeleni pakoje," alisema Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Mjini.

Nipashe pia ilimtafuta Katibu wa Wabunge wa CCM, Jasson Rweikiza, ambaye alisema Prof. Muhongo bado anayo nafasi ya kuitumikia nchi akiwa mbunge.
Alisema kuwa katika uchaguzi mkuu uliopita, mwanachama mwenzake huyo aliomba ubunge na si uwaziri.

"Lakini baada ya kupata uwaziri, Rais aliona anafaa kumpangia kazi nyingine zaidi, akaamua kumpa ili amsaidie lakini sasa Rais ameona kazi hiyo aliyompa, ameshindwa kuifanya na ameamua kumuondoa," alisema.

Alisema kuondolewa kwenye uwaziri siyo mwisho wa safari yake kisiasa na haimuondolei ubunge wake kwa kuwa wapo wengi waliokuwa kwenye uwaziri na sasa wapo kama wabunge wa kawaida.

"Wapo wengi walikuwa kwenye uwaziri wakaondolewa kama Ezekiel Maige, Prof. Anna Tibaijuka na Andrew Chenge, na wengine wengi tu lakini wakagombea ubunge bila shida yoyote na wamepata," alisema.

Rweikiza ambaye pia ni Mbunge wa Bukoba (CCM), alisema wananchi wa Jimbo la Musomo Vijijini walimpa ubunge Prof. Muhongo ili awatumikie na siyo uwaziri, hivyo anaweza kugombea na akarejea tena bungeni katika uchaguzi ujao wa mwaka 2020.

Naye Mbunge wa Kigamboni, Dk. Faustine Ndugulile (CCM), alisema Prof. Muhongo bado anayo nafasi ya kurejea tena kwenye Baraza la Mawaziri kwa kuwa mchango wa utaalamu wake ni muhimu kwa taifa.

Alisema ubobezi wa Prof. Muhongo katika jiolojia ni muhimu si tu kwa Tanzania, bali duniani, hivyo mchango wake bado unahitajika katika maendeleo ya nchi.

"Sidhani kama huu ndiyo mwisho wa Prof. Muhongo kisiasa. Kumbuka katika uchaguzi uliopita, aliomba ubunge na si uwaziri," alisema na kufafanua zaidi:

"Nafikiri sasa atakuwa na wakati mzuri zaidi wa kuwatumikia wananchi wa jimbo lake. Anaweza kugombea tena uchaguzi ujao na kurejea bungeni kisha kupewa nafasi nyingine ya kuitumikia serikali akiwa waziri.

"Ally Hassan Mwinyi alijuzulu uwaziri wa kutokana na vifo vya wafungwa na hivi karibuni tumeshuhudia mmoja wa mawaziri wa Ubelgiji akijiuzulu kutokana na shambulizo la kigaidi, Huko ni kuwajibika kutokana na changamoto iliyotikea.

"Prof. Muhongo bado anayo nafasi ya kuwania ubunge, kurejeshwa kwenye Baraza la Mawaziri na hata nafasi nyingine kubwa serikalini."

TEGETA ESCROW
Kutumbuliwa kwa Muhongo kunakuja miaka miwili na miezi minne kamili tangu ajiuzulu nafasi hiyo kufuatia kashfa ya uchotwaji wa mabilioni katika Akaunti ya Tegeta Escrow, Januari 24, 2015.

Prof. Muhongo alimuandikia barua ya kujiuzulu Rais wa nne, Jakaya Kikwete akieleza nia yake ya kujiuzulu baada ya kujadiliwa na kuazimiwa bungeni, kwa sababu “nataka nchi isonge mbele”.

Dalili kwamba Prof. Muhongo angeondoka na matokeo ya uchunguzi wa kamati iliyoongozwa na Profesa Mruma zilikuja mapema Ikulu siku hiyo baada ya Rais Magufuli kumtaka ajipime.

“Ninampenda sana Profesa Muhongo, lakini pia ni rafiki yangu, lakini kwenye hili ajifikirie! Aji-asses (ajitathimini) na bila kuchelewa nilitaka aachie madaraka,” alisema Rais Magufuli akionekana mwenye huzuni.

Muhongo ni Mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini kwa tiketi ya CCM, ambaye alichaguliwa mwaka 2015.

Hali ya Mchezaji wa Simba Jonas Mkude Baada ya Kupata Ajali iliyoua Shabiki wa Simba

$
0
0
Nahodha wa Simba, Jonas Mkude anaendelea vizuri katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam ambako amefanyiwa vipimo na kupata matibabu kwa ujumla.

Mkude alikuwa kati ya watu sita waliopata ajali iliyotokea jana na shabiki mmoja wa Simba, Shose Fidelis amepoteza maisha.

Ajali hiyo ilitokea siku moja tu baada ya Mkude kuingoza Simba kubeba ubingwa wa Kombe la Shirikisho kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Kiungo huyo alifikishwa Muhimbili kwa matibabu zaidi ili kupata uhakika.

Lakini hali yake inaonekana kuimarika na imeelezwa jana alikuwa akilalama sana maumivu lakini sasa ana nafuu.

“Anaendelea vizuri, labda tuangalie kidogo kujua zaidi,” alisema mmoja wa viongozi wa Simba.

Hawa Hapa Kumrithi Profesa Muhongo.....

$
0
0
Rais John Magufuli, anatarajiwa kufanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri wakati wowote kuanzia sasa ili kujaza nafasi ya waziri wa Nishati na Madini.

Nafasi hiyo iliachwa wazi baada ya Profesa Sospeter Muhongo kung’olewa katika wadhifa huo Mei 24, kutokana na ripoti ya kamati maalumu iliyoundwa na Rais, kuchunguza mchanga wa dhahabu katika makontena 277.

Kamati hiyo iliyoongozwa na Profesa Abdulkarim Mruma ilisema kampuni ya Acacia, haikutangaza kiasi cha madini yote yaliyokuwa katika makontena 277 ambayo yalizuiwa kusafirishwa nje kwa amri ya Rais.

Matokeo ya kamati hiyo yanaonyesha kuwa thamani ya madini yote yaliyopo kwenye makontena 277 ni kati ya Sh829.4 bilioni na Sh1.439 trilioni, tofauti na thamani iliyotolewa na Acacia ya Sh97.5 bilioni.

Hii ni mara ya pili kwa Profesa Muhongo kung’olewa katika wizara hiyo. Januari 24, 2015 alijiuzulu wadhifa huo baada ya kuhusishwa na kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow ikiwa ni shinikizo la Bunge, baada ya kutolewa kwa maazimio ambayo pamoja na mambo mengine, yalitaka mamlaka ya uteuzi wake imwajibishe.

Vyanzo mbalimbali vimedokeza kuwa Rais Magufuli hana jinsi zaidi ya kufanya mabadiliko madogo ya baraza lake la mawaziri ili kujaza nafasi hiyo huku wanaofaa kumrithi wakitajwa.

“Unajua bajeti ya wizara hii inakuja Alhamisi na Ijumaa ijayo, kwa hiyo hapa katikati tunatarajia kuwapo na mabadiliko madogo ya baraza la mawaziri,” kilidokeza chanzo chetu.

Chanzo hicho kilisema Rais anaweza kufanya moja kati ya mambo mawili, ama kuteua waziri wa Nishati na Madini bila kupangua wengine au kufanya pia mabadiliko ya baraza lake.

“Anaweza akateua waziri wa Nishati na Madini akaishia hapo. Lakini anaweza pia kutumia fursa hiyo kuboresha baraza lake la mawaziri kwa kufanya mabadiliko madogo,” alisema.

Majina yanayotajwa kumrithi Profesa Muhongo, ni pamoja na Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi na Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene.

Kundi la Weusi Bado Wana Ganga Njaa na Bado Wanaishi Nyumba za Kupanga

$
0
0
Msanii wa muziki wa hip hop, Nyandu Tozi, kutoka B.O.B Micharazo amefunguka kwa kuwaponda kundi la Weusi kuwa hawana mafanikio yoyote waliyoyapata katika maisha sababu bado wanaishi katika nyumba za kupanga.

Rapa huyo amesema hayo baada ya kuulizwa swali juu ya ukimya wao katika muziki pamoja na mafanikio waliyoweza kuyapata kama kundi ukilinganisha na Weusi kutoka jiji la Arusha.

“Ukiniambia Weusi wana maendeleo kuliko B.O.B unanishangaza wakati wao wamepanga, B.O.B kila mtu anaishi katika ‘empire’ zao,” Nyandu alikiambia kipindi cha Enewz cha EATV “B.O.B Micharazo ni ukoo kwa hivyo unavyoona B.O.B wapo kimya katika muziki utakuta labda sasa hivi wapo ‘busy’ mambo mengine kwa sababu watu wana majukumu yao binafsi siyo kwamba tutegemee muziki tu ‘a hundred percent no’ lazima ujishughulishe na uwe na biashara au uwe na maduka ni vitu ambavyo ‘movement’ vijana wengi wasasa wameamka hakuna kijana ambaye amekaa tu ategemee atoe nyimbo i-hit afanye ‘show” Nyandu alifunguka.

Pamoja na hayo, Nyandu amesema kundi lao la B.O.B Micharazo haliwezi kufa kutokana na ukimya wao wa muda mrefu katika ‘game’.

Godbless Lema Amuomba Rais Magufuli Alivunje Jiji la Arusha

$
0
0
Sakata  la madalali kuendelea kukusanya kodi za Halmashauri ya Jiji la Arusha kutoka kwa wapangaji wa vibanda vinavyomilikiwa na jiji hilo, limezidi kuchukua sura mpya huku, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), akimwomba Rais Dk. John Magufuli kuunda tume ya uchunguzi au avunje halmashauri.

Kauli ya mbunge huyo imekuja baada ya hivi karibuni kikao cha Baraza la Madiwani katika Jiji la Arusha kupitisha azimio la kodi za vibanda vilivyojengwa stendi ndogo mjini Arusha kutakiwa kulipia halmashauri moja kwa moja na si kupitia madalali.

Jana  Lema alisema kwa muda mrefu kumekuwa na hali ya kutoheshimiwa kwa maazimio yanayotolewa na Baraza la Madiwani jambo ambalo halileti picha nzuri kwa jamii.

Alisema jiji liliingia mkataba wa miaka 10 na waliojenga vibanda hivyo tangu mwaka 1994 na baada ya hapo vitarudi chini ya umiliki wa halmashauri ya jiji lakini tangu wakati huo hadi sasa kumekuwa na kutoelewana na Serikali imekuwa ikikosa mapato yake.

“Tunajua huenda ni mkakati maalumu unaofanywa na Mkurugenzi wa Jiji (Athuman Kihamia) kupitia Mkuu wa Mkoa wa Arusha (Mrisho Gambo).

“Ni wazi huu ni  mkakati wa kudhoofisha halmashauri ambazo zipo chini ya upinzani hasa Chadema ili zionekane zimeshindwa kusimamia rasilimali ikiwemo ukusanyaji wa mapato.

“Kutokana na hali hii ninamwomba sana Rais Dk. John Magufuli, kama aliweza kuunda tume na ikachunguza suala la mchanga wa dhahabu na akawafukuza kina Acacia basi afanye hivyo na kwa jiji la Arusha na kama itaonekana vinginevyo avunje Baraza la Madiwani nasi tutarudi mtaani na kuwa madiwania wa wananchi kuliko kutoheshimiwa maamuzi ya vikao.

“Mtu amejenga kibanda miguu mitatu kwa mitano tangu mwaka 1994 anakusanya kodi je hadi leo hajarudisha fedha zake? Kuna nini kinachoendelea na kwanini madiwani wanadharauliwa? Nakuombas Rais Magufuli tupia jicho lako Arusha,” alisema Lema

Mbunge huyo alikwenda mbali na kudai kwamba wapo baadhi ya viongozi wa Serikali wamekuwa wakiandaa mikakati kwa kushirikiana na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)  yenye lengo la kudhofisha maeneo yanaongozwa na wapinzani.

“Tunaona wazi huu huenda ni mkakati wa kudhofisha upinzani kwani hata kauli ya CCM kupitia kwa Katibu Mwenezi wake, Humphrey Polepole kwamba viongozi wa Serikali kupelekwa kwenye maeneo ya upinzani. Kauli hii aliitoa akiwa Arusha na kilio chetu hiki tumekifikisha hadi kwa Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene naye anajua kila kitu,” alisema

Alisema suala la malipo hayo awali wafanyabiashara walikubaliana na uamuzi wa jiji lakini baada ya kuteuliwa kwa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya Arusha ambaye kwa sasa ni mkuu wa mkoa, Mrisho Gambo aliingia suala hilo na kumpa maagizo kwa kuwakingia kifua watu waliojenga vibanda hivyo.

VIDEO:Diamond Platnumz Alivyo Perfom Kwenye Tamasha Nairobi

$
0
0
Mwimbaji Staa wa Bongofleva Diamond Platnumz alialikwa kwenye tamasha la Koroga Festival Nairobi Kenya May 28, 2017 ambapo alitumbuiza akiwa na Band yake.

Baada ya kukonga nyoyo za mashabiki katika Tamasha hilo Diamond Platnumz anatarajiwa kwenda Uganda kushiriki mazishi ya Ivan Don ambaye alikuwa mume na mzazi-mwenza wa Zari the Boss Lady aliyefariki hivi karibuni akiwa Hospitali Afrika Kusini akipatiwa matibabu.

Bonyeza Play hapa chini kutazama full Video..

Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images