Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104431 articles
Browse latest View live

Lemutuz Afunguka ' Ni Haki ya Zari Kupigania Mali za Marehemu Ivan Don Mwanzo Mwisho'

0
0
By @lemutuz_nation
With my Friend @zarithebosslady 2013 at that point and time tuliokuwa tunamfahamu kwa karibu hapa Bongo hatukuwa tunazidi hata 5 as opposed na sasa hivi ambapo almost kila mmoja anadai kumjua mpaka kutaka kumpangia maisha yake ....again MUNGU AMPE NGUVU KIPINDI HIKI KIGUMU CHA KUONDOKEWA NA BABA WA WATOTO WAKE ....NOW Kinachoendelea sasa hivi in her life ni NONE OF OUR BUSINESS ila kwa vile ni Super Star na very much active member wa Instagram inatupa haki ya kusema something on kinachoendelea ...MY OPINION ni Zari ana haki zote za kupigania haki ya Watoto wake 3 wala haihitaji mjadala au Compromise she should fight all the way to the end kuhakikisha Urithi wa Watoto wake unapatikana hatakama ni kwenda Mahakamani ...naona wabongo wengi wanashindwa kutenganisha Chuki kwa Zari na haki za watoto ni vitu Viwili tofauti na it has nothing to do na Diamond ....infact at this point and time Diamond anatakiwa ampe Space Zari ya ku navigate future ya Watoto wake ...it does not matter Zari aliikuwa anaishi au haishi na marehemu ni Watoto wake ni haki yao kupewa jasho la Baba yao kwa hiari au kwa sheria...again it is none of our business but it is ok kutia neno Zari ni mama wa watoto 3 aliozaa na Marehemu ni haki yake kuwapigania watoto wake haki yao ....ZARI SHOULD FIGHT FOR THAT ALL THE WAY TO END ....NO COMPROMISE OR NEGOTIATIONS ..
.
.
JE KATIKA HILI.. LEMUTUZ KAONGEA POINT AU PUMBA??? .

Mangu Afunguka Haya Kuhusu IGP Sirro..!!!

0
0

Aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Ernest Mangu amewataka wananchi kumpa ushirikiano IGP mpya, Simon Sirro katika kukabiliana na matukio ya uhalifu nchini hasa katika Mkoa wa Pwani.

Mangu ameyasema hayo leo Ikulu jijini Dar es salaam baada ya Rais John Magufuli kumwapisha Sirro kuongoza jeshi la polisi nchini.

Mangu ambaye anasubiri kupangiwa kazi nyingine amesema anamfahamu Sirro kama mchapakazi mzuri na ataweza kutekeleza majukumu yake ya kuhakikisha kwamba Tanzania inakuwa na amani.

Alipoulizwa wito wake kwa Sirro kuhusiana na hali tete katika wilaya za Rufiji na Kibiti mkoani Pwani, Mangu amesema "Sirro anafahamu anachotakiwa kufanya katika hilo, nimefanya naye kazi kwa karibu, ninachoomba ni askari na wananchi wote wampe ushirikiano."

Sirro ameapishwa leo kuwa IGP, kabla ya uteuzi huo alikuwa kamanda wa polisi (RPC) katika mikoa ya Tanga, Mwanza na Shinyanga. Baadaye alikwenda kitengo cha operesheni na mafunzo polisi makao makuu, kisha akahamishiwa kitengo hicho kanda maalumu ya Dar es Salaam kabla ya kuwa kamishna wa kanda hiyo.

Siri ya IGP Mangu Kutenguliwa Yafichuka..Sirro Anena Haya Baada ya Uteuzi..!!!

0
0

Wakati mauaji ya watu zaidi ya 30 katika wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji mkoani Pwani yakiendelea kuumiza vichwa vya Watanzania, Rais John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Ernest Mangu.

Kutenguliwa kwa uteuzi wa Mangu kutoka katika wadhifa huo kumetajwa kuwa huenda kumesababishwa na mfululizo wa matukio ya mauaji yaliyotokea katika wilaya hizo na miongoni mwa waliouawa wamo askari wanane waliokuwa katika doria.

Askari hao waliuawa katika Kijiji cha Jaribu mpakani mwa wilaya za Kibiti na Rufiji walipokuwa doria ya kukabiliana na matukio ya mauaji ya viongozi wa CCM, askari na raia baada ya gari lao kushambuliwa na wahalifu. Taarifa iliyotolewa jana jioni na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi ilieleza kuwa Rais John Magufuli amemteua aliyekuwa Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Mangu ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Ingawa taarifa hiyo haikutaja sababu za kuondolewa kwa Mangu, wachambuzi wa masuala ya kijamii wanahusisha uamuzi huo na mauaji yaliyotokea katika wilaya hizo ambazo Serikali imeamua kuziundia kanda maalumu ya kipolisi ili kukabiliana na uhalifu.

Hadi sasa takriban watu 31 wameauawa katika wilaya hizo kwa mujibu wa taarifa ambazo Mwananchi imezifuatilia kuanzia Mei, 2016.

Mauaji ya watu hao ambayo yameendelea kulaaniwa na watu mbalimbali, yamelifanya Jeshi la Polisi kupeleka kikosi maalumu kuimarisha usalama.

Pia, wakati wa uongozi wa Mangu yamewahi kuwapo matukio kadhaa ya uvamizi wa vituo vya polisi, askari kuuawa na kuporwa silaha.

Wiki iliyopita, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba alitembelea Kata ya Bungu wilayani Kibiti na kuzungumza na askari hao, sambamba na kuwataka wananchi kuwafichua wanaojihusisha na mauaji hayo. Mwigulu alisema Serikali haitaendelea kuvumilia kuona watu wakiuawa ilhali watuhumiwa wa mauaji wanafanya hivyo wakishirikiana na baadhi ya watu.

“Hakuna chama cha siasa ambacho kina thamani sawa na uhai wa binadamu, mtu kuwa chama anachotaka hajafanya kosa hata kustahili kuuawa, kwa maana hiyo mimi kila nikitafakari naona kuna kamchezo kanakochezwa, hatutawaacha wanaoua na wala hatutawaacha wanaoshirikiana na wanaoua,” alisema Mwigulu.

Sirro azungumzia uteuzi

Sirro ambaye aliteuliwa kushika wadhifa wa kamishna wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam akitokea katika nafasi ya mkuu wa operesheni wa kanda hiyo, alisema kuwa anamshukuru Rais John Magufuli kwa kumwamini na kumkabidhi wadhifa huo ili awatumikie Watanzania. Alisema anamshukuru Rais kwa kumuona na kumuamini kwa utendaji wake wa kazi, hivyo hawezi kumuangusha.

“Tuombeane tu ndugu yangu hii nafasi si ndogo ni kubwa kwa Jeshi la Polisi, hivyo naomba ushirikiano kutoka kwenu na mengi nitaongea kesho (leo)” alisema Sirro.

Akizungumzia uteuzi huo, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Richard Mbunda alisema uwajibikaji wa Sirro ndiyo chanzo cha kuteuliwa na Rais kwa nafasi hiyo. Alisema Sirro alikuwa mstari wa mbele kiutendaji.

Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete Desemba 30, 2013 alimteua Mangu akiwa Kamishna wa Polisi kuwa IGP akichukua nafasi hiyo iliyokuwa ikishikiliwa na Saidi Mwema aliyestaafu.

Kabla ya uteuzi wake huo ulioanza Januari Mosi, 2014 Mangu alikuwa Mkurugenzi wa Intelijensia ya Jinai katika Jeshi la Polisi.

Uvamizi wa vituo vya polisi

Baadhi ya matukio ya vituo vya polisi vilivyovamiwa na askari kuporwa silaha ni kama ifuatavyo; Julai 12, 2015 majambazi wenye silaha walivamia kituo cha Polisi Stakishari, Ukonga na kuua askari wanne na raia watatu na kupora silaha.

Juni 12, 2014 katika kituo cha Polisi Mkamba Kimazichana majambazi wenye silaha walivamia kituo hicho na kuua askari polisi mmoja na mgambo na kupora silaha.

Juni 21, 2015 katika kituo cha Polisi Ikwiriri majambazi wenye silaha walivamia kituo hicho na kuua askari wawili na kupora silaha.

Januari 27, 2015 mjini Tanga, majambazi wenye silaha waliwajeruhi askari polisi wawili waliokuwa doria na pikipiki na kuwapora silaha.

Februari 3, 2015 wilayani Kilombero kundi la watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi walivamia stoo ya kituo kidogo cha polisi Mgeta na kuiba silaha.

Machi 30, mwaka 2015 eneo la Kongowe Pwani, majambazi wenye silaha waliwaua askari wawili na kumjeruhi mmoja na kupora silaha.

Mei 29, 2015 jijini Dar es Salaam majambazi wenye silaha walivamia askari waliokuwa lindo eneo la Tazara na kupora silaha.

Aprili 13, 2017 askari polisi waliokuwa wakirejea katika kambi yao iliyopo Bungu wilayani Kibiti walishambuliwa kwa risasi na majambazi. Katika tukio hilo askari wanane waliuawa na silaha ziliporwa.

Februari 21, 2017 ofisa upelelezi wa polisi wilaya ya Kibiti, Peter Kubezya, mlinzi wa kituo cha ukaguzi wa mazao ya misitu Shabani Ngamba na Peter Katundu aliyekuwa akikusanya ushuru wa Serikali wa Halmashauri ya wilaya ya Kibiti, waliuawa kwa kupigwa risasi na majambazi waliovamia kituo cha ukaguzi wa mazao ya misitu katika kijiji cha Jaribu kata ya Mjawa wilayani Kibiti. 

Credit - Mwananchi

Serikali ya Magufuli Yaaanza Kusaidia Nchi Masikini..Waanza nkwa Kutoa Msaada Huu kwa Nchi ya Puntland..!!!

0
0

Serikali kupitia Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC) itaisaidia serikali ya jimbo la Puntland la Somalia kuboresha sekta yake ya utumishi wa umma kwa kuendesha mafunzo mbalimbali kwa watumishi wa umma wa jimbo hilo.

Puntland ni Jimbo la Kusini mwa Somalia ambalo limejitangazia mamlaka yake ya ndani, ingawa halitaki kujitenga moja kwa moja na Somalia yenye machafuko.

Mkataba wa makubaliano hayo ulisainiwa jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora), Angela Kairuki na Waziri wa Kazi, Vijana na Michezo wa Puntland, Abdurahman Ahmed Abdulle.

Kwa mujibu wa makubaliano hayo TPSC itashirikiana na Chuo Kikuu Cha Puntland kuendesha kozi mbalimbali kwa watumishi wa umma wa Puntland hususani za muda mfupi na watumishi wengi wa umma wa jimbo hilo watanufaika na programu kadhaa za mafunzo.

Mpango huo wa Puntland umefadhiliwa na Benki ya Dunia ambao pia umeuwezesha ujumbe wa Puntland kuzuru Tanzania mara kadhaa kwa lengo la kufanikisha makubaliano hayo.

Waziri Kairuki alisema makubaliano hayo yanalenga kuboresha uhusiano wa watu wa Tanzania na Puntland na yatasaidia kuimarisha utendaji kazi wa watumishi wa Umma wa Jimbo la Puntland.

Kwa mujibu wa Kairuki, Tanzania kupitia chuo cha Utumishi wa Umma kimekuwa kikishirikiana na taasisi za ndani na nje kuboresha sekta ya umma.

Kwa upande wake Waziri Abdulle alisema jimbo lake limechagua kuja kujifunza Tanzania kutokana na umadhubuti wake katika sekta ya utumishi wa Umma.

Alisema anaamini mkataba huo utanufaika jimbo lake.

Sakata la Mchanga wa Madini… Gwajima: Watanzania Tumerogwa..Nampongeza Rais Magufuli

0
0
Ulozi! Siku chache tangu liibuke sakata la mchanga wa madini (makanikia), kufuatia ripoti ya kamati maalum iliyoundwa na Rais Dk John Pombe Magufuli kusomwa na kuibua mazito, Askofu wa Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church (GCTC) ‘Ufufuo na Uzima’, Dk Josephat Gwajima ameibuka na kutema cheche kuwa Watanzania wamerogwa.

Katika mahubiri yake Jumapili ya jana, Askofu Gwajima alimpongeza Rais Magufuli kwa hatua alizochukua na kumtaka azidi ‘kukaza uzi’ kwani Watanzania tunashangaza kuishi kwenye umaskini licha ya nchi yetu kujaliwa rasilimali nyingi ambazo kama zingetumika kwa usahihi tungekuwa tunaogelea kwenye utajiri.

Askofu Gwajima alisema haiwezekani nchi yenye madini mengi zaidi ya 320 anayoyajua, wingi wa mito, maziwa na mbuga za wanyama, lakini bado inaomba msaada ikiwemo wa chakula kutoka kwa mataifa ambayo kwa uhalisia yalitakiwa kuomba msaada kutoka kwetu.

“Nataka niseme ukweli pasipo kupindisha mambo kuwa, sisi Watanzania tumerogwa na mchawi wetu ni special (maalum), kwa sababu haiwezekani kwa nchi yenye utajiri mkubwa kama huu, madini, maziwa, mito, mabonde na mambo mengine yenye kuvutia ikiwemo mbuga za wanyama, lakini bado wananchi wake wanauza karanga na ubuyu, huko ni kurogwa.

“Nampongeza sana Rais Magufuli kwa kuamua kukata utepe ambao ulikuwa umedumu kwa muda mrefu, eti wachimbaji wachukue asilimia zote za madini na kutuachia asilimia nne tu, inaingia akilini kweli? Kuna aina 320 za madini ninayoyajua, mengine hata ukitajiwa majina unabaki unashangaa, sasa watu wanakuja na kuchukua yote, huku sisi tunabaki maskini, sasa kama siyo kurogwa huko ni nini? Watanzania tumerogwa, wewe zaidi ya makontena 277 yalitakiwa yapelekwe nje, hakika tumerogwa na tunatakiwa tuamke sasa,” alisema Askofu Gwajima.

Gigy Money, Lulu Diva Waingia Kwenye Bifu Zito

0
0
WAREMBO wawili ambao ni Video Queen, Gift Stanford ‘Gigy Money’ na Lulu Abbas ‘Lulu Diva’ wameingia kwenye bifu zito baada ya Gigy kumtolea maneno machafu mwenzake na kusema kuwa anatakiwa kurudia kazi yake ya zamani ya u-baamedi.


Gigy alifikia hatua ya kumtolea maneno hayo Lulu kutokana na kauli yake aliyowahi kusema kwamba hataki kufananishwa naye kwa kuwa siyo levo yake kwa sababu hivi sasa ni mwanamuziki siyo video queen tena. Maneono ya Lulu yalimkera Gigy ambaye ameamua kumjibu kwa kumwambia kuwa anamtambua kama baamedi kwani hiyo ndiyo ilikuwa kazi yake hivyo anajiona yupo juu kwa kuwa alizoea kufunua visoda.

Baada ya Gigy kutoa maneno hayo, Risasi Jumamosi lilimtafuta Lulu ambaye baada ya kuelezwa alijibu kwa ufupi; “Acha aongee maana huwezi kumkataza binadamu kuongea kwa sasa siwezi kujibizana na mtu wa aina hiyo anayetafuta kiki.

Nimeshikwa Live Nikiwa na Chupi ya House Girl Mkononi

0
0
Jumapili familia yangu walienda kanisani kwenye ibada, mimi sikwenda nikawa nipo nyumbani tu pekee yangu naangalia TV, hata hivyo jumapili huwa hakuna vipindi vizuri kwenye chanel mbali mbali

Nikawa nimepata wazo nifungue porn videos kwenye simu yangu, basi nikawa naangalia video moja baada ya nyingine, hadi Hali yangu ya mwili ikawa mbaya kuliko maelezo, nikawa Nimeshawishika kujisaidia mwenyewe, nikaenda bafuni nikachukua vitendea kazi nikarudi kwenye kochi nikaanza kazi bila kujua kumbe mdogo wake na mke wangu hakwenda kanisani yupo chumbani kalala hakua anajisikia vizuri

Aliamshwa na kelele nilizokua napiga, akafungua mlango na kujua nn kinachoendelea hapo, kwa kweli sikumsikia, nilistuka kumuona huyu hapa sebuleni, nikiwa nalia kwa nguvu huku nikiwa na kufuli la house girl mkononi kuvutia hisia, maana hg ni mzuri mno, huku nikiliita jina Lake kwa sauti kubwa

Shemeji hakunisemesha akarudi chumbani hadi sasa toka hiyo Jana hatujaongea hilo jambo lakini nimeshikwa na fedheha na aibu kubwa, maana nina wasi wasi atamueleza wife halaf naweza kutimuliwa nyumbani maana naishi kwa huyu mwanamke kwa Muda sasa Ingawa hatuja funga ndoa, ila tunatambuliwa na jamii inayotuzunguka kama wanandoa

Wadau mnaweza kunisaidia mawazo nifanye nn juu ya hili au nikae tu kimya, au nimbeleza yule binti asiseme?

By baptiste

Kimenuka..Nape Nnauye Awaponda Wabunge wa CCM Wanaosifia Kila Kitu

0
0
Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amefunguka na kusema wabunge wa Chama Cha Mapinduzi ambao wanaishauri na kuikosoa serikali ni watu ambao wana mapenzi mema na Rais na serikali yake kuliko wanao sifia kila kitu.

Nape Nnauye amedai wabunge ambao kazi yao ni kusifia kila kitu hata kama kuna mapungufu hao hawana mapenzi ya kweli kwa Rais Magufuli na serikali kiujumla na kudai yeye anaitumia nafasi yake vizuri kutoa ushauri kwa serikali kupitia bunge sababu ndiyo njia sahihi aliyonayo kwa sasa.
"Kimsingi kazi kubwa ya Mbunge hasa wabunge wa CCM ni kuishauri serikali yake sisi tunaoshauri tunampenda zaidi Rais na tunaipenda zaidi serikali ifanye vizuri kuliko wale ambao watakuja na kusifu na kupongeza kwa kila kitu, hata pale wanaona kabisa hapa tungeweza kushauri na mambo yakarekebishika"alisema Nape Nnauye 

Mbali na hilo Nape Nnauye amedai kuwa watu ambao wanashangaa yeye kuishauri serikali sasa kupitia bunge anasema hawafahamu pia alipokuwa kwenye Baraza la Mawaziri, alikuwa akifanya hivyo.

Amber Lulu Astaafu Kuuza Sura..Sasa Kuwauza Wenzake

0
0
Msanii wa bongo fleva mwenye 'hit song' ya 'Watakoma' Amber Lulu amefunguka kwa kusema sasa hivi hatajishughulisha tena na masuala ya 'video queen' na badala yake atafungua kufungua kampuni yake ya 'video vixen' hivi karibuni.


Amber Lulu amebainisha hayo baada ya kusumbuliwa na wasanii wengi katika simu wakimuhitaji aende kuwafanya kazi yake aliyokuwa anaifanya hapo awali ya unenguaji katika muziki kabla ya kuamua kuingia rasmi katika kuimba huku wengine wakimtaka awatafutie warembo kwa ajili ya kazi hiyo.

"Mimi sifanyi hivyo vitu tena, mimi sasa hivi ni msanii kwa hiyo siwezi kurudi nyuma, sasa hivi natakiwa niwaite ma-video vixen ambao watakuwa kwenye ngoma zangu. Mimi ni boss wa ma- video queen na soon nafungua kampuni yangu ambayo itakuwa inajishughulisha na warembo na wapo tayari wakali 10 ambao ntakuwa nawatoa kwa malipo ukiwataka wafanye video yako" alisema Amber Lulu.

Kimenuka..Mbowe Aitaka Serikali Iwachukulie Hatua Lowassa na Sumaye

0
0
Freeman Mbowe

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameitaka serikali kuwachukulia hatua viongozi mbalimbali waliohusika katika kuliingizia serikali hasara ya mabilioni kutoka kwenye sekta ya madini.

Freeman Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Hai Mkoani Kilimanjaro alitoa kauli hiyo katika Mkutano Mkuu wa CHADEMA mjini Dodoma alipokuwa akizungumzia sakata la mchanga wa madini ambalo limepamba moto kwa sasa nchini.

“Tunafukuza watu kwa makosa yaliyofanywa miaka 15 iliyopita, lakini wale waliofanya makosa wapo uraiani, wapo huru” alinukuliwa Mbowe akizungumza.

Kwa kauli hii ya Kiongozi Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni ni kuwa, baadhi ya waliokuwa viongozi wakuu wa shughuli za serikali wakati mikataba hii ikisainiwa na kazi hizi za usafirishaji wa mchanga ambao ni wananchama wa chama hicho, nao watachukuliwa hatua endapo serikali itaamua kuwashughulia wote waliohusika kwa namna yoyote.

Kama serikali ingekuwa inamchukulia kila mtu hatua tangu mikataba hii iliposainiwa, basi ni dhahiri Mawaziri Wakuu wasataafu Frederick Sumaye na Edward Lowassa ambao nao ni wanachama wa CHADEMA, kwa namna moja au nyingine wangehusika kwani wao pia walikuwa wasimamizi wa shughuli za serikali.

Mbali na  jambo hilo lakini Mbowe alikikosoa pia Chama cha Mapinduzi kuwa kiliingia mikataba mibovu iliyopelekea nchi kupata hasara ya mabilioni. Mbowe alisema kuwa tatizo kubwa katika sekta ya madini ni sheria, ambazo wapinzani wamekuwa wakipiga kelele kila mara kuwa zirekebishwe.

Aidha, Mbowe aliwataka wanachama wa chama hicho kusimama kisawasawa na asiwepo mtu mwenye uwoga wa aina yoyote kwani wamedhamiria kushika dola mwaka 2020.

Haya ndio madai ya Shamsa Ford Kumpokonya Mumewe Duka

0
0

DAR ES SALAAM: Raha ya ubuyu ukae kitako usikilizie utamu! Baada ya kudaiwa kumfilisi mumewe, Rashid Said ‘Chid Mapenzi’, staa wa sinema za Kibongo, Shamsa Ford amefungua duka Mitaa ya Mwananyamala, Dar, lakini nyuma yake kuna ubuyu mzito.

Ubuyu wa motomoto unadai kuwa, Shamsa amempokonya mumewe duka hilo kwani badala ya kuuza vitu vya wanaume kama lilivyokuwa awali, sasa anachanganya na vitu vingine huku muda wote akishinda mwenyewe.

Sosi wa ubuyu huo alisema ndugu wa Chid wanalalamika kuwa, Shamsa amekuwa juu ya mumewe kiasi cha kufikia hatua ya kumpokonya duka ambalo awali alisingizia mumewe kukosa kodi hivyo likafungwa.

“Unajua Shamsa ni mjanjamjanja sana. Ndugu wa mume wanalalamika kuwa ndiye aliyemshawishi mumewe wafunge duka la awali kwa kisingizio kuwa kodi ni kubwa, lakini kwa sasa amefungua duka lingine na zamu hii anauza mwenyewe.

“Cha kushangaza ameweka mpaka nguo za kike, tofauti na duka la Chid lilivyokuwa spesho kwa ajili ya nguo za kiume,” alitonya sosi wetu.


Shamsa Ford na mumewe Chid Mapenzi
Sosi huyo aliendelea kumwaga mchele kwenye kuku wengi kuwa, Shamsa amemfanya mumewe hafurukuti kwani hata akiwa naye kwenye matembezi anambana kiasi kwamba hawezi kujiachia kama alivyokuwa akijiachia zamani.

“Unaambiwa Shamsa anakaba hadi kivuli. Hata wakitoka kwenye matembezi yao, mwanaume hawezi kuthubutu kujichanganya na watu hasa wanawake kwani mwanamama anakaba kila kona. Zamani mshkaji alikuwa anajichanganya, hata ungemkuta na washkaji alikuwa haoni shida, lakini kwa sasa hafurukuti,” alidai sosi huyo ambaye ni shabiki kindakindaki wa mwigizaji huyo.

Baada ya kunyetishiwa ubuyu huo, Wikienda, kupitia safu hii ya Ubuyu Ulionyooka lilimsaka Shamsa aliyekiri kuwa na duka lingine na kudai kuwa hajampokonya mumewe bali mume wake ameamua kumpa duka hilo kama zawadi tu ili ajiendeleze, asikae bila kazi kwani huu ni wakati mgumu kiuchumi.

BOFYA HAPA KUMSIKIA SHAMSA

“Mh! watu bwana! Hawajui naongea nini na mume wangu tuwapo chumbani, wanachonga tu. Mume wangu ameamua kunizawadia, nikatae kwa sababu ya maneno? Mbona wameshasema mengi? Mimi nadunda tu,” alisema Shamsa.

SHAMSA AFUNGUKA MENGINE Baada ya kuchoshwa na maneno, Shamsa alifunguka mazito zaidi ambapo alidai kwa sasa amekuwa sugu wa maneno kwani watu walisema atakaa kwenye ndoa miezi miwili tu atatoka, lakini sasa anamaliza mwaka.

“Watu hawajui mimi na mume wangu tulikutana vipi, amewapitia wangapi? Tena wengine wazuri kuliko mimi lakini mbona akanichagua mimi? Alilopanga Mungu, mwanadamu hawezi kupangua, ndoa yangu itadumu miaka mia nane,” alifunguka Shamsa.

AWANANGA MASTAA WENZAKE

Shamsa alienda mbali zaidi na kuwananga mastaa wenzake ambao wamekuwa wakidai kuwa, hawataki kuolewa kwa sasa lakini ukweli ni kwamba ni waongo na hawajapata wa kuwaoa kwani kuolewa si mchezo.

“Kuolewa si mchezo jamani, wapo mastaa wengi unasikia wanasema hawataki kuolewa kwa sasa, ni wanafiki wakubwa na waongo, hakuna asiyetaka ndoa bali hawajatamkiwa, asikwaambie mtu kuolewa si mchezo mimi namshukuru sana Mungu,” alisema Shamsa.

AJIPANGA KUACHA POMBE

“Kutokana na mambo ya ustaa, unakutana na mambo mengi, ndoa yangu itadumu kwa sababu mume wangu si mtu wa mambo mengi, hapendi starehe, hapendi pombe, mimi mwenyewe nimejipanga nimeweza kupunguza pombe na sasa naacha kabisa ili kuinusuru ndoa yangu. Mungu hakika atanisaidia na mfungo umeanza naamini sitarudi tena huko. Wabaya wangu wajipange sana.

“Kila kukicha ni zaidi ya jana kwangu mimi na mume wangu, mahaba tunayopeana kamwe shetani hataingia kwa uwezo wake allah,” alimalizia Shamsa.

NENO LA MHARIRI

Shamsa, kama kweli amejipanga kwa sababu ya maneno ya watu, ajipange kwelikweli na abadili mienendo yote kwani unapofunga ndoa tu, shetani hunyemelea wakati wote ili kukuvuruga.

Huu Ndio Ukweli Juu ya Mahusiano ya Diamond,Zari na Marehemu Ivan..!!!

0
0

Diamond Platnumz, Zari Hassan and her late ex-husband Ivan Ssemwanga who will be buried next week on Tuesday as his body is set to arrive in his native Uganda on Sunday from South Africa.

In Summary
It’s alleged that the curvaceous, London-educated lass from Jinja, decided to walk out of a 12-year-old marriage she termed as toxic and abusive. Ivan was rumoured to have made a habit of physically abusing Zari.
He denied the claims, saying his baby mama’s injuries were as a result of a car crash. In her interview with NTV Uganda in December 2015, Zari opened up to presenter Faridah Nakazibwe, saying that she did put in a lot of effort in trying to salvage the union to no avail.

Zari Hassan’s flamboyant baby daddy Ivan Ssemwanga will be buried next week on Tuesday as his body is set to arrive in his native Uganda on Sunday from South Africa, where he had been residing.

The death of Ivan, the business tycoon who was married to Zari for over 10 years and with whom he had three children, left many distraught. With his demise, the shaky relationship between him, Zari and her current husband Diamond Platnumz comes under the spotlight again.

Zari visited Ivan when he was in hospital, sharing the evidence on social media. 

SPOT IN HIS HEART

In one of her interviews with NTV Uganda in 2015, Zari was quoted as saying:

“Having been my husband for 10 years and the father of my children, he (Ivan) will always have a spot in my heart and I am sure that I also have a spot in his.”

A number of Ugandan blogs have reported that Ivan, a flamboyant businessman and well-known party animal, died a lonely man. Some even suggest that he still pined for his ex-wife Zari. We trace the complex relationship from the time the two parted ways to date.

ZARI DUMPS IVAN

It’s alleged that the curvaceous, London-educated lass from Jinja, decided to walk out of a 12-year-old marriage she termed as toxic and abusive. Ivan was rumoured to have made a habit of physically abusing Zari. He denied the claims, saying his baby mama’s injuries were as a result of a car crash. In her interview with NTV Uganda in December 2015, Zari opened up to presenter Faridah Nakazibwe, saying that she did put in a lot of effort in trying to salvage the union to no avail.

“I tried so much to mend the relationship but it failed. I was abused by Ivan even in front of my kids. Sometimes it happened in public places. I think everyone knows that now. It’s a common thing in relationships so it shouldn’t be a secret,” said the mother of five now. Ivan’s attempts to reconcile with Zari were futile as she had already made up her mind to leave him.

ZARI MEETS DIAMOND

After dumping Ivan, Zari moved on and would then fall in love with another basket-baller, Farouk Sempala, with whom they had a short-lived relationship. Farouk then went on the rampage claiming that Zari aborted his kids and that was the reason for their breakup, according to Uganda Exposed.

In December 2014, a picture of Diamond, who had just broken up with his bongo movie actress Wema Sepetu, emerged showing him canoodling with Zari in South Africa. The two denied being in a relationship, with Zari saying that they were working on some music project which never materialised.

She said: “Diamond is just a friend of mine. It’s never been written that females and males can’t be friends. It is backward people that use that kind of perspective to blow things out of proportion, ” she insisted.

However, their union was confirmed a few weeks later when Zari graced the red carpet hand-in-hand with Diamond Platnumz during the Channel O Video Music Awards ceremony in South Africa.

IVAN FIGHTS DIAMOND

When news broke that Zari was pregnant with Diamond’s first-born (baby Latifah Dangote) all hell broke loose, forcing Ivan, who had been quiet about his ex-wife’s new love affair with a successful musician, decided to make his voice heard. .It was widely reported that Ivan was shocked and disgusted to find out his baby mama was pregnant again at her “old” age.

According to Uganda showbiz blog Big Eye, he said, “Zari is an old woman who may not manage the stress that comes with bringing a new life into the world”. It added that Ivan was surprised because they had agreed that even with their separation she should never bring someone else to the world but rather concentrate on co-parenting the three sons. With the aid of his close friend King Lawrence, Ivan started attacking Diamond via social media posts asking him to leave Zari alone.

In one of his Facebook posts in December 2015, King Lawrence offered Diamond $40,000 (Sh4 million) to leave Zari alone and allow her to return to South Africa from Tanzania to take care of her children, who he claimed were missing her mother. Diamond did not respond. A few weeks later Zari flew to Uganda and hosted the Zari All White party, which Ivan attended. Diamond, too, was supposed to attend the event but despite being in Uganda, he did not show up. This led to rumours that he didn't turn up to support Zari because he was afraid of a confrontation with Ivan.

Later, after returning home to Tanzania, Diamond was forced to address the claims, saying he wasn’t afraid of Ivan:

“Watu wanasema namuogopa (Ivan), mimi siwezi kumwogopa, hii code chafu kabisa kutoka Tandale mimi nimwogope mtu! Sijawahi kuwa na matatizo naye,nishakutana naye wakati naenda kwenye MTV alikuwepo, mara nyingi tulikuwa tunapishana hivi na hivi kabisa. Hatujawahi kusalimiana sababu sijawahi kuwa na mahusiano naye niseme nimsalimie ni uongo. Halafu nilikuwa nikipita, nipo na crew,security, yeye anakua anapita tu maskini ya mungu,” Cloud FM radio, quoted Diamond as saying.

Explaining his absence, he said that he missed Zari’s All White Party because he had an agreement with his promoter that required him to keep away from the public eye before his scheduled show with Patoranking in Kampala, which was to take place on the following day.

NEVER-ENDING BEEF

Diamond’s beef with Ivan would never end, with both men flaunting their wealth on social platforms in a show of might. Sometime in September 2016, Diamond posted a photo of his new mansion in South Africa and when he unveiled it, he took a jab at Ivan, captioning the photo: “They are busy bragging that they are rich yet their kids are still living in a rented house… and now a person whom they abuse daily saying that he’s broke and poor bought a house, so that their kids can have a better life.” Later on, Ivan shot back terming it a rental home. In April 2017, Diamond posted a picture of him with his new ride, a Hummer, that he said cost him five million shillings. A few hours later, Ivan also posted a picture of himself with a Hummer.

Diamond seemed to have buried the hatchet, however, after Ivan’s death. He passed his condolences via an Instagram post accompanied by a picture of a lit red candle and wrote, “Mbele yako, nyuma yetu...” (You have gone ahead, we are right behind you).

Uwezekano wa Kuyashitaki Makampuni ya Madini Kurejesha Hasara Tuliyoipata Huu Hapa..!!!

0
0

Na Bashir Yakub. +255784482959

Mikataba yoote ya kimataifa huongozwa na wajibu wa aina mbili. Wajibu ulioandikwa(express obligation) na wajibu ambao haukuandikwa(implied obligation). 

Wajibu ulioandikwa ni masharti yote ya mkataba yaliyo katika maandishi ambayo wahusika husoma na kuridhia, wakati wajibu usioandikwa ni masharti ya mkataba ambayo hayakuandikwa katika mkataba lakini yapo kwa asili au yapo kwakuwa tayari yalishasemwa na sheria na hivyo si lazima kuyaandika ktk mkataba.

Mathalan, mfanyakazi wako wa duka hawezi kukuibia halafu akasema kwenye mkataba wangu wa ajira hakuna sharti la uaminifu. Laa hasha uaminifu ni sharti la asili "implied obligation" kwa hiyo liandikwe au lisiandikwe bado lipo tu.

Kwenye mikataba ya kimataifa kama ile ya kwetu na makampuni ya madini masharti yafuatayo ni ya asili na hayahitaji kuwa yameandikwa ili kuyatekeleza :
1. Wajibu wa kuanika taarifa zote muhimu kuhusu shughuli inayotekelezwa katika mkataba( Implied covenant to disclose all necessary information over the subject matter).

2. Wajibu wa kutekeleza na kutenda kwa nia njema(Implied covenant to act in good faith and fair dealing).

3. Wajibu wa kila mhusika katika mkataba kuwa mkweli . Hili huwa ni katazo la udanganyifu(Fraud).

Haya yawe yameandikwa kwenye mkataba au hayakuandikwa yakikiukwa tafsiri yake ni kukiuka masharti ya mkataba.

Matendo kama kulaghai kuhusu uzito wa madini yanayochukuliwa, kulaghai kuwa unachukua dhahabu huku ukijua unachukua zaidi ya dhahabu, kulaghai kuhusu bei , kutotoa taarifa sahihi za kipi unapata na kipi hupati,nk ni kukiuka wajibu na masharti ya mkataba jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

Na ikiwa wamekiuka mkataba kwa misingi hiyo basi Tanzania inaweza kufanya yafuatayo;

1. Kuendelea na mkataba lakini kwa sharti la kurudisha kile chote kilichopotea kwa mda wote( specific performance).

2. Kutoendelea na mkataba na kudai fidia, hasara tuliyopata,pamoja na riba zake kwa kipindi chote( 
breach of contract).

Ndugu zangu, wajibu wa kutekeleza na kutenda kwa nia njema (implied covenant to act in good faith and fair dealing), kuwa mwaminifu na kutoa taarifa sahihi katika utekelezaji mikataba ni matakwa ya lazima duniani kote.

Sheria ya biashara ya Amerika Uniform Commercial Code vifungu vya 1 - 12 habari hii imeelezwa kwa upana.

Sheria ya biashara ya Ufaransa na Ujerumani The German Civil Code(BGB) na Civil Code of France zimeeleza vitu hivi.

Pia mahakama kuu ya Uingereza katika kesi ya Yam Seng PTE vs International Trade Co. Ltd (2013) EWHC 111 ( QB) iliamua kuwa masuala ya uaminifu na kutoa taarifa sahihi katika kutekeleza mikataba ni wajibu ambao upo hata Kama haukuandikwa kwenye mkataba.

Halikadhalika sheria yetu ya Mikataba, Sura ya 345 vifungu vya 18 na 13 vimeyafanya masuala ya udanganyifu na kutoa taarifa zisizo sahihi kama mambo ambayo ni makosa na yanayobatilisha mkataba.

Kamati ya Profesa Mruma imebaini upotevu wa Bilioni 829.4 x Miezi 12 kwa miaka 18 = Trilioni 829.4. Hizi ni pesa nyingi mno. Tunayo kesi nzuri ya madai na uhakika wa kurejesha fedha tulizopoteza. Ni vema mda huu pamoja na mambo mengine, nguvu nyingi ikatumika kuona ni namna gani tunapata hii fedha. Makosa yapo na yametendwa na hilo halina Shaka. Iko wapi haja kukhofu, hakika haipo.

Yumkini haitakuwa rahisi kutokana na aina ya mabepari ambao tunashughulika nao. Ni mabepari hatari wenye mtandao mkubwa wa kisiasa na nchi wafadhili pamoja na taasisi kubwa kama IMF, WB, UN nk.

Hata hivyo tumeshasema hii ni vita na vita sharti ipiganwe ili waliosiginwa wawe huru. Tunaweza kuumia kwa mda ila mwisho wa maumivu hayo itakuwa ni neema kubwa na ya milele.

Mungu ibariki Tanzania na mbariki rais kwa pamoja tushinde vita hii.

Kudadadeki..IGP Sirro Aanza Kazi kwa Kutoa Amri Hii kwa Polisi Wote Nchini..!!!

0
0

Leo baada ya kamanda Simon sirro kuapishwa kuwa IGP ametoa onyo kwa wahalifu wote wanaendelea kufanya mambo ya ajabu.

"Watanzania sasa tushirikiane kukomesha Uhalifu kwa pamoja, atoa salamu kwa wahalifu wote" asema kamanda Sirro.

Sasa wale wauaji wa Kibiti na sehemu nyingine mjiandae Kamanda amekuja tena.

Harmorapa Atangaza Kujiunga na Freemason,Asambaza Picha Akiwa na ..!!!


Mwigulu Nchemba Awachongea Andrew Chenge na Warema kwa Kuhusika na Kusaini Mikataba Mibovu ya Madini..!!!

0
0

Waziri   wa Mambo ya Ndani, Mwingulu Nchemba amewachana  wanasheria wakuu wa Serikali wastaafu kwa kuwataka waeleze hadharani maslahi walionayo kwenye kampuni za madini zinazosafirisha mchanga nje ya nchi.

Wanasheria hao wakuu wa serikali wastaafu, ni Andrew Chenge na Jaji Frederick Werema na amewataka wamwache  Rais John Magufuli aendelee kulinda rasilimali za umma, zisiliwe na watu wachache.

Mwingulu amesema hayo juzi wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliohudhuriwa  na mamia ya wananchi wa Tarafa ya Ndago, jimbo la Iramba.

 Alisema Chenge na Werema kwa nyakati tofauti wakiwa wanasheria wakuu wa Serikali, pamoja na majukumu yao mengine, wameshiriki kusaini  mikataba mikubwa mikubwa, ikiwemo ya makampuni ya kuchimba madini.

 “Kwa akili ya kawaida tu, baadhi ya mikataba mikubwa ikiwemo ya makampuni ya madini, haikuwa sawa… Ndio maana imelalamikiwa kwa muda mrefu,” alifafanua Mwigulu.

Jeshi la Polisi Lawamani Tena..Lamuua Mwanafunzi Mwingine wa Chuo Kikuu kwa Kumpiga Risasi Nyumbani Kwao..!!!

0
0

Utata umeibuka kuhusu kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Uvuvi Mbegani, Boniventure Kimali (25) baada ya ndugu kudai ameuawa kwa kupigwa risasi na polisi akituhumiwa kuwa jambazi.

Kimali aliyekuwa akihudhuria mafunzo kwa vitendo katika Soko la Samaki Feri akitarajiwa kuhitimu stashahada Juni mwaka huu katika fani ya uchakataji samaki, ubora na masoko inadaiwa aliuawa nyumbani kwao, CCM Shule eneo la Vijibweni.

Mwandishi wa habari hii aliyefika nyumbani hapo na kuonyeshwa eneo ambalo inadaiwa aliuawa kulikuwa na damu ukutani.

Pia, mwandishi alionyeshwa maganda ya risasi ambayo ndugu zake wameyahifadhi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Gilles Muroto alipotafutwa kuzungumzia tukio hilo, alielekeza atafutwe kaimu wake. “Mimi nipo nje ya ofisi mtafute kaimu wangu.”

Kaimu kamanda huyo, Nyigesa Wankyo hakupatikana kwa siku ya mkononi iliyoita bila kupokewa vivyo hivyo kwa Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro.

Naftani Balampame, ambaye ni kaka wa Kimali alisema tukio hilo lilitokea Ijumaa saa 3:30 usiku walipokuwa mbele ya nyumba yao, huku mdogo wake akiwa anafua.

“Tulikuwa tunazungumza hapa nje, yeye (marehemu) akawa amechukua simu yangu anazungumza, ghafla tukasikia milio ya risasi, sisi tulikimbilia ndani yeye alikimbia akielekea nyuma ya nyumba,” alisema Balampame.

Alifafanua kuwa walisikia milio ya risasi nyuma ya nyumba na baadaye walisikia sauti anazodai ni za askari wakisema “si yeye huyu” na mmoja wao alizungumza na simu kuita gari.

“Mdogo wangu aliniita akitaka nimpeleke hospitali, nilipojaribu kusogea walinifukuza, walimwingiza kwenye gari na kuondoka naye. Tulikwenda kituo cha polisi ambako walituambia amepelekwa Hospitali Kigamboni,” alisema.

Alisema walipokwenda hospitali walielezwa hawakumpokea kutokana na kukosa maelezo kumhusu na kwamba polisi Kigamboni waliwaeleza aliuawa kimakosa, kauli iliyobadilishwa baadaye.

Kaka mwingine wa marehemu, Daudi Gwelenza alisema katika Hospitali ya Taifa Muhimbili walipewa taarifa kwamba umepokewa mwili wa kijana asiyejulikana.

“Niliomba kuuona mwili nikamkuta ndiye yeye ana tundu la risasi tumboni na ana mchanga wa bahari. Maelezo yanaonyesha alifikishwa saa 10:00 alfajiri na askari Fatuma Abdallah ikielezwa amekufa kwa kipigo,” alisema Gwelenza.

Mkurugenzi wa Mafunzo na Utafiti kutoka Chuo cha Uvuvi Mbegani kilichopo Bagamoyo mkoani Pwani, Ambakisye Simtoe alisema kifo hicho kimeushtua uongozi wa chuo kwa kuwa mwanafunzi huyo aliruhusiwa kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo wiki mbili zilizopita.

Msemaji wa familia hiyo, Goodluck Kimali alisema hawajui watazika lini wakisubiri polisi watoe tamko. “Kwetu ni Kigoma, tunatarajia wafanye uchunguzi ijulikane wazi nini msimamo wao na wetu, ili tuuchukue mwili tukazike nyumbani,” alisema.     

Sakata la Mchanga Lahamia Zanzibar..Wawakilishi Waikaba Koo SMZ..!!!

0
0

Msimamo wa baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi juu ya kuizuia Bajeti ya Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifungo na Uvuvi ya mwaka 2017-2018 hadi pale watakapopata majibu yenye kueleweka juu ya hatua ya rasilimali ya mchanga kuhodhiwa na Serikali badala ya wananchi wenyewe kama ilivyokuwa awali utapata majibu leo wakati waziri wake, Hamad Rashid atakapojibu hoja zao.

Hatua ya wajumbe hao imetokana na malalamiko ya wananchi waliokuwa wakimiliki mashamba ambayo sasa yanachimbwa mchanga chini ya uangalizi wa Serikali huku wao wakiambulia patupu.

Awali, mashamba hayo yalikuwa yapo chini ya wananachi ambao walikuwa wakiyatumia kuvuna na kuuza mchanga huo kwa wamiliki wa magari na kampuni mbalimbali za ujenzi.

Mwakilishi wa Mfenesini, Machano Othman Said alisema  pamoja na rasilimali hiyo kuonekana kupungua kwa kiwango kikubwa, haikusatahili wananchi kupokonywa mashamba yao bila makubaliano maalumu.

Mwakilishi wa Kijitoupele, Ali Suleima Ali ‘Shihata’ alisema utaratibu uliowekwa na Serikali juu ya mchanga ni hatari na unahitaji kufanyiwa marejeo ili kuepusha athari zinazoweza kuepukika.

Ukweli Mchungu: Magufuli Hakuahidi Maisha Bora kwa Kila Mtanzania! Alisema, 'Hapa kazi tu'...!!!

0
0

Sioni kama kuna sababu legitimate ya mwananchi yeyote kulalamika kuwa maisha yamekuwa magumu zaidi tangu Magu ashike nchi...

Tofauti na Kikwete ambaye aliahidi maisha bora kwa kila Mtanzania na hayakupatikana mpaka anaondoka madarakani, Magufuli hakuahidi kitu kama hicho. Alichosisitza ni kuwa katika kipindi chake, watu watalazimika kufanya kazi zaidi ili wapate the same level of income compared to kipindi cha JK.

So ukweli mchungu ni kuwa, Msi mdrive Magu, kudeliver kitu ambacho hakuahidi kwenye kampeni zake. Aliahidi kuwa mtachapa kazi na kweli sasa hivi kila mtu anachapa kazi kwa bidiii haswa.
Ubora wa maisha au kutajirika haikuwa ahadi yake na hivyo, hawajibiki kwa hilo...

Chanzo Jf

Jokate Afunguka Haya Baada ya Jarida la Forbes Kumtaja Kama Kijana Mwenye Mafanikio kwa Mwaka 2017..!!!

0
0

Jokate Mwegelo ameonyeshwa kufurahishwa baada ya kuchaguliwa na jarida la Forbes Africa la kuwa miongoni mwa vijana walio na umri chini ya miaka 30 wenye mafanikio katika sekta mbalimbali kwa mwaka 2017.

Mrembo huyo ameonyesha furaha hiyo katika mtandao wa Instagram, wakati alipoweka picha ya cover la jarida hilo na kuandika, “Looks whose on the cover of Forbes Africa with some other amazing young Africans doing amazing things to create wealth and transform our economies? God is so amazing. 🙏🏽😩❤️🤧.”

“Never underestimate your own strength. You were born for a purpose and are blessed with an ability to achieve it. Mpaka kieleweke 🙏🏽🙈😘,” ameongeza katika picha nyingine aliyoiweka katika mtandao huo.

Naye Lavie Makeup ni mrembo mwingine kutoka Tanzania aliyetajwa na jarida hilo pamoja na Jokate.
Viewing all 104431 articles
Browse latest View live




Latest Images