Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104428 articles
Browse latest View live

Haji Manara Aendelea Kuweweseka na Ndoto za Ubingwa wa Ligi Kuu..Leo Amesema Tena Haya..!!!

0
0

Aliyekuwa msemaji wa klabu ya Simba SC, Haji Manara ameendelea kusisitiza kuwa klabu hiyo ndio mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara kwa msimu huu kinachosubiriwa sasa ni maamuzi kutoka FIFA kwani ubingwa wao ni wa jasho na damu.

Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii Manara ameandika, ‘Simba ni bingwa wa kombe la Shirikisho, ni Bingwa wa ligi kuu ya Vodacom msimu huu, ndio ni bingwa wa nchi msimu huu, ni kusubiri tu wenye mpira wao FIFA waturudishie points zetu tatu zilizo wazi kwa kanuni zote ili tutawazwe rasmi kuwa machampioni wa nchi hii.

Yes no way, mchezaji awe na kadi tatu za njano zilizothibitishwa pasina shaka yoyote na ripoti za waamuzi na makamisaa wa michezo husika na bodi ya ligi yenye jukumu halali la kikatiba la uendeshaji na usimamizi wa ligi, kisha eti kwa matakwa ya ajabu ya Shirikisho na kamati yake isiyo na nguvu ya kisheria na kikanuni iipoke points Simba kwa sababu zozote zile, ni kuibaka kanuni ambayo ipo wazi na ni dhulma isiyohitaji touchi kuiona.

INSHAALAH bingwa halali atatangazwa hivi karibuni.Yes ni ubingwa wa Jasho na damu, ni ubingwa uliotafutwa kwa nguvu zote halali na uliomwaga damu za wanasimba walioumia na kupoteza maisha yao katika kuusaka.

“Alikuwa na pesa nyingi, lakini ameshindwa kununua uhai” Waigizaji wa Bongo Movie waongea matope kuhusu kifo cha Ivan

0
0

Tofauti na wasanii wengine ambao walitoa salamu za rambirambi kufwatia kifo cha Ivan Ssemwanga, Steve Nyerere and Faiza Ally wameeleza hisia kali kuhusu kifo cha aliyekuwa mume wa Zari.

Waigizaji hao wa Bongo Movies wameongea matope kuhusu kifo cha Ivan, hisia zao kuhusu kifo cha mwenda zake zinaonyesha uadui tu.

“Alikuwa na pesa nyingi, alikuwa na uwezo wa kufanya chochote, alikuwa na uwezo wa kununua chochote lakini ameshindwa kununua uhai. Nimejifunza kitu kupitia wewe, tuishi vizuri na watu maana hakuna ajuaye kesho,” Steve Nyerere aliandika.


“Binaadamu akikuchukia hata zuri kwake ni baya na ndio maana huwa na maisha yangu tu kama mimi bila kutaka kuwa yoyote, hakuna zuri mbele ya mtu mbaya. Unajua nini wala sijali naona upuuzi tu kama ya kipuuzi mengine yote yalio pita.

“Maisha yangu na wanangu yako kwenye mikono salama hata kushinda mikono yangu, yako kwenye mikono ya Mungu mwingi wa rehma. Leo Ivan na matajiri wengine wako wapi? Mali sio kila kitu kwenye maisha yetu tunahitaji amani, mapenzi, maelewano makubaliano.


“Nimetoka kwenye kutokua na mlo mpaka sasa namiliki milo, huo ni utajiri mkubwa maana kwanza ni kushiba akili ikae sawa ndio upange habari zingine, so at the end my heart is pure and that what give me amani ya moyo, hayo mengineyo tena yako nje ya uwezo wangu ni mipango ya Mungu, Faiza Ally aliandika.

Kijana Unapoamua Kuoa Mwanamke Mrembo, Msomi au Binti wa Kidigital Basi Kubaliana na Haya...!!!

0
0

Vijana wenzangu unapoamua kuoa mrembo, msomi na binti wa digital, lazima ukubaliane na haya;

1. Wasichana wengi sasa hawajui kupika. Wanajifanya wamechoka nitanunua msosi sana tu, tena usipokaza hata chai ataenda kununua.

2. Usishangae nguo zako kutofuliwa wiki mbili, anaweza kumuita mdogo ake anamlipa afue. Yeye anachart sio na wewe ujue ni shotizo.

3. Kupiga deki sahau kijana mwenzangu. Aanze tu kupinda mgongo. Kama unataka usafi wa nyumba yako tafuta housegirl.

4. Jua kuwa utawahi wewe kuamka, yeye bado kalala. Amechoka kazi za ofisini za jana yake.

5. Bajet ya saloon iwepo ya kila wiki nywele na kucha.

Usilalamike ndo gharama za kufanya maamuzi hayo.

Amekuoa Lakini.... Lazima Asote Kuipata..!!!!

0
0

Japo amekuoa, kuipata papuchi yako lazima akubembeleze sana na umfikirie sana, ndipo aipate. Siyo kwamba kwa kuwa amekuoa basi anakuwa anakugeuza na kukutumia kadri apendavyo. No ! No thank ü.

Atakuchakaza. Unatakiwa uendelee kutizamwa ukipita barabarani. Si unajua tena mwanamke kupendeza ? Wengine wanasema mwanamke mazingira.

Wanaume wamekuwa na tabia ya kumgegeda mke frequently na ukikubaliana naye atakuchakaza halafu aanze kutamani vibinti vidogo. Lazima mwanamke uendelee kutunza urembo wako kwa kutoa papuchi yako aste aste (namaaanisha kwa nadra). Kuna visingizio vingi unaweza kutumia mfano : sijisikii, nimechoka, niko mp, n.k.

Na ikatokea numéo kachepuka, ukainyaka na kuthibitisha na wewe muonyeshee kuwa unaweza kuchepuka. Chepuka na ww makusudi mazima. Maana si unavyo vigezo vya kuchepuka ?? Ndiyo. Bado unalipa.

Wanawake hunyanyasika sana, unakuta yy kakongoroka aliyemkongorosha anaanza kutia jeuri. Sasa dawa yenu ndiyo hiyo.

Mapenzi siyo kuchomeka tu !!

Bamia Hii Hii Unayoijua..Pambana na Magonjwa Yafuatayo kwa Kutumia Bamia..!!!

0
0

watu wengi tumekua hatutumii bamia either kwa radha yake au tu kasumba ya kuona Bamia ni MBOGA ya walala hoi !!!. 

Leo Naomba ufahama Bamia kama moja ya Mboga za majani ndio MBOGA yenye uwezo wakusaidia afya zetu ,,,Bamia ina unatajiri wa nutrients mbali mbali ,, nutrients izo ni 

1)- Calories - 30 calories
2)-Vitamin C- 21 Milligrams
3)-Carbohydrates - 7.6 Grams 
4)-Fatty - 0.1 grams 
5)-Magnesium - 16 milligrams
6)-Diatery Fibers - 3 grams .

Kutokana na kua nautajiri huo mkubwa,, Tafiti zimethibitisha kua BAMIA ni kiboko ya Magonjwa yafuayo 

- Diabetes ( kisukari)
-Asthima ( inayoanza na iliyokwisha kuathiri)
-Cholesterol
-Kidney Disease (Magonjwa ya figo)
Ulcers (Vidonda vya tumbo ).
-Mimba ,,husaidia mtoto kukua akiwa na Afya njema na aliyekamilika .
-Anemia 
-Matatizo ya kutoona Vizuri .
-Pia Bamia huongeza nguvu ktk mfumo wa mwili wa kinga ktk kupambana na magonjwa .

- Kuondoa Maumivu wakati wakutoa haja kubwa 
-Kuimarisha Mifupa lege lege .

NAMENGINEYO MENGI AMBAYO SIJAYAANDIKA ,, .

Watu wazaman walifanikiwa kuishi miaka mingi kwa kutumia vitu km ivi...

Mtoto Akatwa Makalio na Baba ake

0
0

Mwanamume mmoja mkazi wa Ndofe wilayani Nyamagana mkoani Mwanza amemfanyia kitendo cha ukatili mtoto wake kwa kumkata na kisu sehemu za makalio kwa madai ya utoro shuleni.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Ahmed Msangi amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Nuhu James (50) anayedaiwa kumfanyia ukatili mtoto Ndalo Nuhu (14) ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha pili Shule ya Sekondari Igoma kwa kumfunga kamba miguuni na mikononi kisha kumchapa fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake na baadaye kumkata na kisu sehemu za makalio, tukio analodaiwa kulifanya majira ya saa 11:00 alfajiri ya tarehe 25 Mei, 2017.

Inadaiwa kuwa mtuhumiwa aliaamua kumfanyia ukatili wa aina hiyo mtoto wake baada ya kugundua kwamba mwanaye ni mtoro shuleni.

Kamanda Msangi amesema baada ya mama wa mtoto alipoona ukatili anaofanyiwa mwanaye na hali yake kiafya kuzidi kubadilika alishindwa kuvumilia na jana (Tarehe 28 Mei.2017) aliamua kutoa taarifa kituo cha polisi

Kamanda Msangi ameendelea kusema kuwa polisi wapo katika upelelezi na mahojiano na mtuhumiwa pindi uchunguzi utakapokamilika, mtuhumiwa atafikishwa mahakamani huku majeruhi akipelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu na hali yake inaendelea vizuri.

Chuo cha Sokoine Kinanuka Ngono..Walimu Wajichukulia Vijana w Kiume na Kike Kiulaini Kabisa.!!!

0
0

Ni wiki ya tatu sasa tangu taasisi ya Harakati Bora ilipowasilisha malalamiko kwa Uongozi wa Chuo kwa niaba ya wanafunzi wake 'wanaotumiwa vibaya' na waadhiri wao ikiwemo wanafunzi wa kike kutakwa kingono na waalimu kwa kutishiwa kufelishwa NA wanafunzi wa kiume kutumiwa kama 'makasuku' na walinzi wa waalimu kwa ahadi ya kusaidiwa kupata ajira baada ya masomo hayo. 

Chuo cha Sokoine-Kilimo kimekuwa hakikui kuendena na kasi ya mabadiliko katika sekta ya kilimo, teknolojia na kinazalisha wahitimu wasio na impact katika jamii kutokana na Elimu ya vitisho, ulaghai wa wahadhiri kwa wanafunzi. Chuo hiki kimegeuka genge la waalimu kupata 'mademu'.
Chuo cha Sokoine kina historia kubwa ya waalimu wake kuzaa na hata kuoana na wanafunzi wake. Hii ni aibu na tishio katika mustakabadh wa elimu Tanzania ikizingatiwa Chuo cha Sokoine ni chuo cha kilimo kikubwa Tanzania!

Ni lini mara ya mwisho taifa limevuna utaalamu, uvumbuzi au ubunifu kutoka kwa wanafunzi na wa chuo cha Sokoine? HAKUNA! na ni kwa sababu CHUO KINANUKA NGONO. 
Hata Ajira ktk chuo cha Sokoine zinatolewa kwa watoto wa Maproffesor waliodumu chuoni hapo. Na nitaleta mifano na ushahidi hapa jukwaani hivi karibuni.

8.May.2017 Uongozi wa Chuo uliwasilishiwa mashitaka juu ya mhadhiri George S.S Fasha anayetuhumiwa na wanafunzi wa Chuo cha Sokoine kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi watatu kwa mpigo lakini hadi leo hii bado chuo kinafanya uchunguzi usio na dalili ya mwisho. 
Nimeambatanisha ushahidi wa mawasiliano kati ya Mkuu wa Idara Proff Damian Gabagambi na Idara ya HarakatiBora. Ikiwa taasisi hiyo imewasilisha malalamiko kwa niaba ya wanafunzi wake kwa Vice Chancellor wa chuo na utatuzi haujapatikana hadi leo hii. 

Sambamba na hayo, Mhadhiri George S. Fasha akishirikiana na mhadhiri mwenzake Marwa Raphael Masanda, wamekuwa wakiwatishia wanafunzi kutokusema ukweli na wakiwatafuta wanafunzi waliohusika katika kushitaki matendo yao. Hii inazidi kuwapa hofu wanafunzi wa Chuo cha Sokoine haswa katika hatma ya masomo yao na ufaulu katika mitihani.

Chanzo Jf

Mapya Yaibuka: Maafisa wa TMAA Walihongwa Mabilioni ya Pesa Ili Smelter ya Kuchanjua Mchanga wa Madini Isijengewe Tanzania..!!!

0
0

Kuna mambo mapya yanayozidi kujitokeza tangu rais Magufuli awasimamishe maafisa wakuu wa Taasisi ya TMAA inayosimamia MADINI ambayo pia ilimfanya rais Magufuli kumvua Uwaziri Mh.Muhongo kama Waziri wa Madini kwa sababu zilizo wazi. 

Inavyosemekana ni kuwa mwaka wa 2009 TUME maalumu iliyojulikana kama PRESIDENTIAL MINING REVIEW COMMISSION,iliyoongozwa na JAJI Mark Bomani. Tume hii ilitoa MAPENDEKEZO kuwa SMELTER ijengwe hapa nchini. 

Lakini cha kushangaza ni kuwa maafisa hao wa TMAA wakawa tayari wamekuwa COMPROMISED na Makampuni husika yaani WAKAHONGWA ili WANAYAMAZISHE matakwa ya Tanzania Kuwa na UWEZO wake na TEKNLOJIA HIYO.

Katika mbinu zao za kuzima ripoti na mapendekezo ya tume TMAA, miaka sita iliyopita hivi wakaanza mipango ya KUYAMWAGIA MAJI mapendekezo YOTE ya Tume ya Jaji Mark Bomani ili KUIDHOOFISHA kabisa
Na mwishowe KUZIZIMA kabisa NDOTO za Watanzania kuwa na mitambo yao ya SMELTER. 
Na hivyo KUTUSALITI sawasawa ili tuendelee KUIBIWA VIZURI na hayo Makampuni.

Mwaka wa 2011 MAAFISA wa TMAA walitembelea miji ya TOKYO na SAGANOSEKI Copper concentrate Smelter nchini JAPAN ili WAJIONEE wenyewe TEKNOLOJIA hiyo na jinsi nchi yetu inavyoweza KUJIJENGEA Smelter yake yenyewe. 

Katika safari yao ilikuwa pia wajue GHARAMA za UWEKEZAJI/UJENZI na uwezo na gharama za uendeshaji nchini.

Ikikikumbuka kuwa tume ya Jaji Mark Bomani ilikuwa pia imeenda huko kabla wakati ikiandika na kuchukuwa DATA, ili kutayarisha ripoti mpya ya sheria ya MINIMG LAW/Sheria mpya za MADINI. 

Mwaka 2011 TMAA nao wakatoa ripoti yao iliyojulikana kama:
"A STUDY on VIABILITY to CONSTRUCTING a COPPER Concentrate SMELTER in Tanzania"

Ripoti yao ILIPINGA VIKALI mapendekezo ya Tume ya Jaji Bomani.
Na hivyo Kuwaachia wezi field day ya kuiba mchanga wetu WATAKAVYO na WAPENDAVYO. Maana tayari TMAA walikuwa wamekuwa compromised/WAMEHONGWA.

Kwa wale wanaolaumu uamuzi wa Rais Magufuli na kupendelea Makampuni wanaposikia haya si WAONE HUZUNI kuwa hakika TULIIBIWA Vya KUTOSHA na IMETOSHA?
Na Tanzania INAWEZA kabisa KUJIJENGEA yenyewe hiyo MITAMBO.

Maana NIA TUNAYO na UWEZO TUNAO tukishikana pamoja na kushirikiana kama Watanzania
HAKUNA lolote ambalo Tanzania HAITALIWEZA KULIFANYA.

Kwa Maafisa kama hawa wa TMAA WALIOTUSALITI wanastahili kuwa JELA bila HURUMA.

Hatuwezi kuwa taifa la OMBAOMBA wakati kila RASLIMALI tunayo. 
Na hali watu wachache wenye tamaa wanataka tubaki Maskini huku wao wakijenga magorofa
TUNAKATAA kama Watanzania. 
Mungu IBARIKI Tanzania na Rais Magufuli.
Chanzo: The EastAfrican.

Lazima Huwa Unafanya Moja ya Vitu Hivi vya Aibu Unapohisi Hakuna Anayekuona....!!!!

0
0

1.Kunusa baadhi ya maeneo ya mwili wako kuona kama yanatoa harufu!, mara nyingine unajikuna kisha unapeleka mkono puani kuona ni harufu gani utaskia.

2. Kuigiza kama unafanyiwa interview. Unajiuliza maswali kadhaa na kujijibu kwa kujiamin huku unatabasamu kana kwamba kuna mtu anakuona.

3. Kutoa uchafu puani kwa kutumia kidole kwa dakika kadhaa, na mtu akitokea ghafla, unajidai unakuna shavu!

4.Kula haraka haraka kwa kificho (tunda, kitafunwa nk) ofisini, nyuma ya mlango nk na kujifuta mdomo ili asigundue mtu!

5. Kutengeneza Sura mbalimbali mbele ya kioo na kuangalia unaonekanaje!



6 Kutoa Hewa chafu kwa sauti (Farting Loud). Hii hairuhusiwi kwenye jamii yetu!

7.Kutoa Haja ndogo wakati wa kuoga

8 Kufanya baadhi ya vitu kwa kutumia miguu badala ya mikono! Kufunga mlango au Kuokota vitu kwa kutumia vidole vya mguuni

9. Kula paketi nzima ya chakula Fulani ambayo pengine ungekula kwa siku kadhaa taratibu

Tuambie ni nini huwa unafanya ukiwa mwenyewe hapo chini

January Makamba Akana Kuutaka Uwaziri Mkuu...!!!

0
0

Waziri wa Mazingira, January Makamba amekana katu katu kuwa alichukia na kususa baada ya Rais Magufuli kumtosa katika nafasi ya Waziri Mkuu wa awamu ya tano.

Akitiririka mubashara, Makamba ametabainisha kuwa baada ya uchaguzi siku zote amekuwa akiomba asichaguliwe katika wadhifa huo mkubwa bongolala maana ungeweza kumharibia keria yake kwenye siasa.

Bado nina umri mdogo na nina safari ndefu sana kwenye siasa na kuwatumikia wananchi. Ukichaguliwa nafasi hizo kubwa ina maana unaua karia na huwezi kuendelea na siasa.

Watalii Wanne Wachomwa Kisu Zanzibar Wakiwa Kwenye Mgahawa..!!!

0
0

Watu sita wakiwemo raia wanne wa kigeni wamejeruhiwa vibaya kwa kuchomwa na  kisu usiku wa kuamkia leo katika mgahawa wa Lukman Mkunazi Mjini Zanzibar.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Hassan Nassir Ali amewaambia waandishi wa habari ofisini kwake leo Jumatatu kuwa tukio hilo lilitokea saa 1:20 usiku Jumapili.

Kamanda huyo amesema kuwa mtuhumiwa aliyetenda tukio hilo  ambaye jina lake halijatambulika ila  kwa sura anafahamika, anakisiwa kuwa na umri wa miaka (25), lakini bado hajapatikana.

Amesema kuwa kwa mujibu wa uchunguzi wao wa awali wamebaini kuwa mtuhumiwa huyo alifika katika mgahawa huo na kuwachoma watu watatu ambao walikuwa  mgahawani hapo kwa ajili ya kujipatia chakula.

Aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni Mauget Gerarol (66) raia wa Ufaransa ambaye amejeruhiwa pembeni ya jicho la kulia, Jennifer Wolf (24) raia wa Ujerumani aliyejeruhiwa kichwani na Anna Catharina(20) raia wa Ujerumani aliyejeruhiwa kichwani pia.

Kamanda huyo alisema baada ya mtuhumiwa huyo kuwachoma visu watu hao alikimbia na akiwa njiani umbali wa mita 60 kutoka eneo la tukio la awali alikutana na vijana wengine waitwao Hassan  Abdallah mkazi wa Kiponda (24), Liying Liang ambaye ni raia wa Canada na kuwajeruhi kwa kuwachoma kisu mdomoni na shavuni.

Alisema alimchoma kisu pia Sajad Hussein  (55) na kwamba majeruhi hao wote walikimbizwa hospitali ya Tasakhtaa Global iliyopo Majestic kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Alisema kuwa  majeruhi hao wote walipatiwa matibabu na kuruhusiwa lakini Mauget Gerarol raia wa Ufaransa bado amelazwa hospitalini hapo na anaendelea kupatiwa matibabu.




Lissu Atoa Kauli Nzito Juu ya Sakata la Mchanga wa Dhahabu..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 30/5/2017..!!!

Marafiki wa Zari na WCB Wadaiwa Kumkacha Zari Msibani.....

0
0

Pamoja bado yupo kwenye majonzi ila Team Wema bado wanaendelea kurusha vibomu kwa Zari, Huyu hapa chini anawashutuma marafiki wa Zari Kumkacha rafiki yao kipindi hichi kigumu kwake:

From @wemakingdaily - Hakuna hata rafiki either from SouthAfrica Or Tanzania😞Hata rafiki yake VeraSidika yuko jirani hapo kenya kashindwa kuja😠 Kwenye 40 ya Nillan watu kibao walifika kumsupport ila leo yuko peke yake,Madam Rita ndo kabisaa anaomboleza msiba insta halafu hata mtu mmoja kutoka WCB hata wa kuwakilisha hakuna😢😢 Diamond mwenyewe katudanganya atakuja kwenye kuaga kumbe hola mpaka maiti inaelekea kuzikwa😭😭 Hata hao wanaojiita TeamZari kutukana watu na kuchamba watu wameshindwa kujichangisha kwenda kumuunga mkono Star wao😭😭😭@zarithebosslady atakuwa amejifunza kitu hapa! aache kunyali wenzie

Upepo Mkali Kuvuma Dar, Wananchi Watakiwa Kuchukua Tahadhari..!!!

0
0

Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) imetoa tahadhari ya upepo mkali na mawimbi makubwa katika maeneo ya ukanda wa pwani.

Taarifa ya TMA iliyotolewa jana imesema upepo huo unatarajiwa kuendelea hadi kesho.

Maeneo yanayotarajiwa kuathirika ni mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Dar es Salaam, Tanga, pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

Mamlaka imesema hali hiyo inatokana na msukumo wa upepo wa kusi unaotokana na kuimarika kwa mgandamizo mkubwa wa hewa katika ukanda wa pwani ya Tanzania. TMA imetoa angalizo kwa watumiaji wa bahari na wakazi wa maeneo hayo kuchukua tahadhari na hatua stahiki

CUF ya Maalim Seif Wakataa Maamuzi ya Mahakama Kuhusu CUF ya Lipumba..!!!

0
0

Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Wananchi (CUF) kupitia wakili wake, Hashimu Mziray imewasilisha kusudio la kukata rufaa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Kupinga uamuzi uliotolewa Mei 21, 2017 na Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri wa kuyatupilia mbali maombi yao waliyoyafungua mahakamani hapo dhidi ya wabunge wawili, Magdalena Sakaya(Kaliua),  Maftah Nachuma(Mtwara Mjini) na wenzao sita.

Walikuwa wakiomba mahakama hiyo iwazuie kwa muda kujihusisha katika masuala ya uongozi na kufanya mikutano ya chama.

Akiwasilisha kusudia la kukata rufaa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Mziray alisema hawakuridhika na uamuzi huo kwa sababu si kweli kuwa  CUF haina bodi ya wadhamini.

Wakili Mziray alisema CUF ni chama ambacho kipo hai, kina wabunge, madiwani, majengo, wanachama na hata Msajili wa Vyama vya Siasa hajakifuta.

Alibainisha kuwa Hakimu Mashauri akulielewa tangazo la Wakala wa Vizazi na Vifo(RITA) hivyo wanaiomba Mahakama Kuu kutengua uamuzi wake kwa madai kuwa ni batili.

Awali katika uamuzi uliotolewa na Hakimu Mashauri ambao uliyatupilia mbali maombi ya Bodi hiyo alizisikiliza pande zote mbili na kuzitolewa uamuzi huo.

Serikali Yatenga Bilioni 1.5 Kupambana na Ugonjwa wa Ebola Nchini..!!!

0
0

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Ally Mwalimu amesema mpaka sasa hakuna mgonjwa wa Ebola wala anayehisiwa kuwa na virusi vya ugonjwa huo nchini Tanzania huku Tsh. bilion 1.5 zikiwa zimetumika kuukabili ugonjwa huo.

Ummy amebainisha hayo wakati alipokuwa anazungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam na kusema wananchi wasiwe na hofu ila wanapaswa kuchukua tahadhari huku akisisitiza kuwa wameweka kifaa maalum 'register' ambacho kitawalazimu wasafiri wote kujaza wakiwa wanakwenda  katika nchi ya DRC na pindi wakiwa wanatoka huko kuingia nchini.

"Hadi sasa hakuna mgonjwa hata mmoja wa Ebola wala mwenye virusi Tanzania, tumechukua tahadhari katika mikoa yote inayopakana na nchi ya Congo DRC.

Wasafiri wote wanaotoka DRC wakifika Tanzania lazima waandikishwe kimaalum ili kufuatiliwe kama huko alikotoka hali ikoje na kama hana virusi nyemelezi.

Tunawaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza katika kuwapima wasafiri wote kwenye mipaka yetu na Congo DRC" alisema Ummy.

Aidha, Ummy amesema serikali imeagiza mashine nne za nyongeza kutoka nje ya nchi ili kuongeza nguvu ya upimaji wa virusi vya ugonjwa huo.

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Wakutwa na Misokoto 59 ya Bangi..!!

0
0

Watu wawili wamefariki dunia katika matukio mawili  tofauti huku jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro linawashikilia wanafunzi wa Shule ya Msingi Msamadi iliyopo wilayani Hai kwa kukatatwa na bangi misokoto 59.

Kamanda wa polisi mkoani hapa, Hamisi Issah alisema Mei 28, mwaka huu, majira ya saa 10:30 Kijiji cha Kyengia wilayani Siha mwananmke mmoja Ephrata Masaki(53), alipigwa na shoti ya umeme wakati akianua nguo.

Alisema nguo hizo zilikuwa zimeanikwa kwenye waya uliokuwa umegusana na waya wa umeme nyumbani kwake na kwamba waya huo ulikuwa umechubuka na kusababisha kifo chake.

Alisema Mei 28, mwaka huu, majira ya saa 12:00 jioni, Kata ya Soweto mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Sadia Kamote(39), mkazi wa Sanya juu, aligundua kufariki kwa mtoto wake wa darasa la kwanza.

Alisema mwanafunzi huyo aliyejulikana kwa jina la Selemani Said(8) ni wa Shule ya Msingi Kilingi alifariki baada ya kuteleza kutoka kwenye jiwe na kusombwa na maji katika mto Karanga katika daraja la Mangia Shirimatunda.

“Mwanafunzi huyo alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu huku wenzake aliokuwa akiogelea nao katika mto huo wenzake watatu kunusulika kifo,”alisema Kamanda Issah.

Alisema mwili wa marehemu Masaki umehifadhiwa katika hospitali ya Kibong’oto kwa taratibu za mazishi huku mwili wa mtoto huyo umehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mawenzi.

Katika tukio lingine  Mei 28, mwaka huu, majira ya saa 10:30 katika kijiji cha kwa Sadala jeshi hilo liliwakamata wanafunzi wanne wakiwa na begi dogo jeusi na baada ya kuwapekuwa walikutwa na bangi.

“Tulipowahoji watoto hao walisema walipewa mzigo huo na mama aliyejulikana kwa jina la Francisca Limo(43) kwa lengo la kwenda kuuza na tayari tumeshawakamata watuhumiwa kwa mahojiano zaidi,”Kamanda Issah.

Sirro Akubali Kujifunga Katika Mambo Haya Mbele ya JPM..Akikiuka Hata Jambo Moja Atatumbuliwa..!!!

0
0

Rais John Magufuli jana amemvisha cheo kipya na kumuapisha Mkuu wa Jeshi la Polisi mpya (IGP) Simon Sirro Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Baada ya tukio la kuapishwa kwa IGP Sirro alikula kiapo cha uadilifu kwa uongozi wa umma na kuahidi kuwa atakuwa mzalendo kwa nchi yake ya Tanzania na mtii wa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"Nitakuwa muadilifu na mfano wa watumishi wa umma na watu wengine katika kukuza na kusimamia maadili, sitatumia cheo changu na wadhifa wangu kwa maslahi binafsi ya familia yangu, ndugu zangu au marafiki zangu, isipokuwa kwa maslahi ya umma.

Nitalinda na kuitumikia rasilimali ya umma kwa maslahi ya umma, nitatekeleza majukumu yangu kwa kuzingatia sera, sheria, kanuni na taratibu na miongozo kwa maslahi ya umma. Sitaomba wala kushawishi kutoa au kupokea rushwa" alisema Sirro

Wadada Acheni Kubania Namba Mtakosa Waume wa Kuwaoa

0
0
Hivi nyie wadada mnaoombwa namba na sie wanaume halafu mnagoma kutoa mna maana gani?
Masuala ya kubania kutoa namba za simu yamepitwa na wakati ,halafu unakuta demu kazeeka unajua kabisa huyu kakosa wa kumwoa sasa unamwomba namba ili muyajenge yeye anakua mbishi kutoa
Mdada unaweza kukosa mume kizembe zembe hivi hivi Kwa tabia yako ya kubania kutoa namba
Acheni hizo wahenga wanasema usikatae wito kataa maneno sasa kinachotakiwa utoe namba then uamsikilize jamaa anataka nini Ila kukataa jumla kutoa namba unapoteza bahati

Jirekebisheni
By Sigara Kali

Tundu Lissu : Tusishabikie Maamuzi ya Kijinga Kwasababu tu Yamefanywa na Raisi

0
0
Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki kupitia Chadema ambaye pia Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Lissu amesema wabunge wanatakiwa kutoshabikia maamuzi ya kijinga hata kama yamefanya na raisi.

"Tusishabikie maamuzi ya kijinga kwasababu tu yamefanywa na raisi"- Mchanga wa Makanikia

Viewing all 104428 articles
Browse latest View live




Latest Images