Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Mke Wangu Kalipenda Hili Jitu Nini?

$
0
0
Waheshimiwa nina mgeni ambae sasa anaelekea kumaliza wiki akiwa hapa kwangu, ni binamu yangu huwa anaishi mkoani amekuja kwa shughuli zake binafsi, ataondoka atapokamilisha yaliyomleta.

Nimewaandikia kwa sababu, huyu jamaa amenishangaza sana, imagine weekend hii iliyokwisha anashinda na boxer kutwa nzima tena kifua wazi, au kwasababu amevimba kifua anataka tumwone au?

Mke wangu na house girl wanafua nguo Jumamosi asubuhi eti anaenda pale awasaidie kufua, natoka ndani namuuliza wife mbona mgeni anafua nguo, najibiwa kuwa eti ameomba mwenyewe, hii ni sawa kweli?

Yote tisa, kumi ni Jana, inafikia hatua linamkuta wife jikoni anasonga ugali linaomba limsaidie kusonga ugali, mgeni gani wa namna hii?

Wadau nitumie njia gani kulitimua hili jitu hapo nyumbani? Kabla halijaleta madhara maana mdogo wa mke wangu naona kama yuko nalo karibu sana, pia wife kaniuliza kama mimi pia naweza kufanya mazoezi nikawa kama hilo jitu badala ya kitambi, ingawa alinieleza kwa utani huku tukifurahi na kutaniana ila najiuliza kwanini aseme sasa wakati hili jitu lipo?

Linakaa hapo sebuleni kwenye video hadi usiku mwingi likiwa na mdogo wa mke wangu bila kujali maadili.

Jumapili nilienda kwenye Bonanza la timu yetu ya veterans narudi nimekuta nyumba nzima hawapo wameenda beach wote pamoja na huyu jamaa.

Hivi unaendaje ugenini halafu unaanza kuleta ujuaji wa namna hii?

Wadau msaada wa mawazo unatakiwa haraka.

Tetesi za Ujauzito wa Mchumba Ronaldo Gumzo

$
0
0


Madrid, Hispania. Tetesi za ujauzito wa mchumba wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez zimezidi kushika kasi baada ya mrembo huyo kuweka picha Instagram akiwa na daktari.

Georgina Rodriguez alituma picha hiyo katika mtandao wake wa Instagram akiwa na daktari siku chache baada ya kusambaa kwa tetesi kuwa Ronaldo anategemea kupata mtoto mwingine.

Tetesi hizo zilianza baada ya nyota huyo wa Real Madrid kutuma picha yake katika Instagram akiwa ameweka mkono wake tumboni mwa mchumba wake huyo mwenye miaka 22.

Hata hivyo tetesi hizo zilipigwa na mama yake Ronaldo akisema mwanaye hategemei kupata mtoto wa pili kwa sasa.

Prof. Muhongo Awaondoa Hofu Wapiga Kura Wake Baada ya Kufutwa Kazi

$
0
0
MARA: Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini na Mbunge wa Musoma Vijiji Prof. Sospeter Muhongo amewasihi wakazi wa jimbo hilo kutokuingiwa na hofu kufuatia uamuzi wa Rais Dkt Magufuli kumfuta kazi.

Prof. Muhongo amewataka wapigakura wake na rafiki zake kutokuwa na hofu kwani kwa pamoja watafanikiwa.

Kwa mujibu wa taarifa za ofisi yake, amewaahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha kuwa wanafikia malengo yao ya kimaendeleo kwa kutimiza ahadi zake.

Taarifa hiyo ilitolewa na Katibu wa Mbunge huyo, Juma Ramadhan ambaye alisema kuwa kilichotokea ni cha kawaida kwenye siasa na inawapasa kusahau hayo ili waweze kusonga mbele katika kutekeleza miradi ya maendeleo.

Kwa sasa tunajielekeza kujenga vyumba vya madarasa na miradi mingine ya maendeleo, hivyo ni vyema tukaungana pamoja ili kuweza kutekeleza majukumu haya, alisema msaidizi huo.

Wakazi wa jimbo hilo waliahidi kutoa ushirikiano kwa mbunge wao katika kutekeleza miradi hiyo kwani yeye si kiongozi wa kwanza kuondolewa kwenye wadhifa wake. Aidha, wakazi hao walisema kuwa kuondolewa kwa Prof. Muhongo kuwe funzo kwa wateule wengine kuwa nafasi hizo si za kudumu.

Mei 24 mwaka huu Rais Dkt Magufuli alimfuta kazi Waziri Muhongo kufuatia kile alichosema ni kushindwa kusimamia kwa umakini sekta ya madini na hivyo kupelekea serikali kupata hasara.

Jambazi Mwingine wa Kike Kenya Atunguliwa Risasi na Kuuwawa...Alikuwa Rafiki wa Yule Alieuwawa Mwanzo

$
0
0
Police on Sunday gunned down two suspected gangsters believed to be members of the same gang as slain gangster, Claire Njoki Mwaniki, famously known as “Clea Adi Vybz.”

One of the suspects, known by her alias- “Marsha Minaj”, is said to have been the best friend of the late Claire Njoki.



Marsha Minaj (left) with her friend Clea Adi Vybz
“Minaj” was shot dead together with a male suspect believed to be her boyfriend on Sunday afternoon at a house in Migingo, in Patanisho area.

The suspects were gunned down following a tip-off from members of the public on the whereabouts of the wanted criminals.

Confirming the shooting, Nairobi County Police Commander Japheth Koome said when the police went to the house they were in, they found the two and attempted to arrest them but they engaged them in a shoot out.

“The officers were forced to return fire and they managed to fatally injure the two and recovered a pistol, five rounds of ammunition and three spent cartridges from the suspects,” Mr Koome said.

After the shooting, a mysterious police officer who identifies himself as “Hessy wa Kayole” on Facebook,  posted gory pictures of the killed suspects on the Facebook group called Kayole Crime Free.

Hessy had previously warned the female suspect through the same platform, that she would be killed if she did not reform from a life of crime.

Below are the photos. Viewer discretion is advised


Atumia Sare za JWTZ Kuwatapeli Raia..!!!

$
0
0

Mkazi wa Kitangili, Shinyanga Francis Kilalo  (31)anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora kukutwa na sare na vifaa vingine vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) ambavyo anatuhumiwa kuvitumia kupateli na kuwadanganya wananchi kwa kuchukua fedha kutoka kwa vijana wanaotafuta nafasi ya kujiunga na Jeshi hilo.

Taarifa hiyo imetolewa jana na Kamanda wa Mkoa wa Tabora Wilbroad Mtafungwa alipozungumza na waandishi wa habari Ofisi kwake juu ya hatua mbalimbali walizochukua katika kupambana na uhalifu mkoani humo.

Amesema kuwa polisi walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo katika Hoteli ya JM iliyopo Wilayani Igunga akiwa  na sare mbalimbali za  JWTZ zikiwa na cheo cha Koplo ambavyo ni pamoja na kofia tatu, begi, sweta, buti  jozi moja, magwanda na  mikanda mitatu.

Mali nyingine zilizokamatwa kwa mtuhumiwa huyo ni pamoja na fomu za likizo cha likizo , fomu za kujaza vijana wanaotaka kujiunga  na Jeshi hilo na Jeshi la Kujenga Taifa(JKT) kwa mujibu wa Sheria na hiari na mihuli zenye nembo inayofanana na Jeshi hilo.

Kamanda Mtafungwa alisema kuwa mtuhumiwa alikuwa akitumia nyaraka  na sare za Jeshi hilo kuchukua fedha kwa kuwadanganya na kuwatapeli wananchi mbalimbali kwa kudai atawatafutia ajira katika majeshi ya Kujenga Taifa na la Wananchi.

Kamanda huyo wa Mkoa wa Tabora aliongeza kuwa mtuhimiwa huyo pia alikutwa barua kutoka Serikali za mitaa za Dar es Salaam na gari aina ya Toyota Starlet yenye namba za Usajili T633 ARF ambalo wanaendelea kuchunguza uhalali wa umiliki wake.

“Pia tumebaini kuwa gari hilo hilo, mtuhumiwa alikuwa akilitumia na kuwafanya baadhi ya wananchi wamuamini kuwa atawasaidia kupata nafasi katika majeshi,” amesema Kamanda

Ameongeza kuwa mtuhimiwa huyo pia alikuwa  na barua za maombi ya watu ya kuomba kujiunga na Jeshi, Fomu za Matibabu za Hospitali ya Jeshi ya Lugalo na nakala ya Vyeti vya kumaliza elimu ya Sekondari vya baadhi ya watu.

Kufuatia tukio hilo alitoa wito kwa waananchi waliowahi kutapeli ndani na nje ya Mkoa wa Tabora kujitokeza katika vituo vya Polisi ili waweze kutoa ushahidi utakasaidia kuonyesha ni jinsi gani walivyumizwa na mtuhumiwa huyo.

Kamanda Mutafungwa alisema kuwa Polisi inaendelea kushirikiana na JWTZ ili iweze kubaini sare  na vifaa hivyo alivipata wapi , kwa lengo lipi na ni nani aliyompatia ili wahusika wote waweze kufikishwa katika vyombo vya Sheria kwa hatua zaidi.

Ivan Don Azikwa na Mamilion ya Pesa Kaburini Kwake....Picha

$
0
0

KUTOKA KWENYE MAZISHI UGANDA...... pesa zaidi ya 30 mil zamwagwa ndani ya kaburi la Ivan Don... Kabla ya maiti kuwekwa....!! Ni balaaaaa..... RIP IVAN DON ila ingekuwa hapa bongo ingebidi hlo kaburi lilindwe hata miez mitatu mpaka hzo pesa ziharibike kwa joto maana la sivyo watu wangemfukuaje!..yaan asubh mwil ungekutwa pembeni..pesa ilivyongumu jamani

Mzee Yusuph: Maisha Yangu Yamekuwa Magumu Baada ya Kuacha Muziki...!!!

$
0
0

Aliyekuwa Msanii nguli wa Taarab nchini Mzee Yusuph amesema kwa sasa maishayake yamekuwa magumu baada ya kuacha muziki

Baada ya kuacha muziki anadai alijaribu shughuli nyingine ikiwemo kufungua duka Kariakoo lakini duka likafeli, lakini anasema maisha yamekuwa ya amani kuliko zamani na hata mtu akimuomba hela haogopi kumwambia hana kwa sababu hana kazi

Pia alipoacha muziki alikuwa ameshachukua milioni 25 za show na alipoulizwa itakuje na show alizochukua hela alisema Allah ndio atajua

Waziri Mahiga: Tukisafiri Nje ya Nchi Tunaitwa Watalii,..!!!

$
0
0

Waziri mahiga ambaye ni waziri wa wizara ya mambo ya nje na Afrika mashariki amesema kwamba kipindi viongozi wakisafiri kwenda nje ya nchi, watanzania wengi hulaumu sana na kuwaita watalii, lakini sasa viongozi wamepunguza safari wanaitwa wasaliti na pia wengine wachache huchukizwa na viongozi kukaa ndani bila kwenda kutafuta fursa nje ya nchi.

Picha za Uchi Zampa Dili Ben Pol,Kampuni Yajitokeza Kumdhamini Ili Apige Nyingi Zaidi..!!!!

$
0
0

Msanii wa Bongo Fleva, Ben Pol amefunguka kwa kusema kuwa baada ya kusambaza mtandaoni picha zinazomuonyesha akiwa nusu mtupu na mng’ao wa mafuta, sasa amepata dili ya kuwa balozi wa mafuta ya kujipaka na kwa sasa wapo kwenye hatua za mwisho za mazungumzo.

Ben Pol amekimbia kipindi cha Kwetu Flavor ya Magic Fm kuwa baada ya picha kusambaa, kuna makampuni yamemfuata  na kutaka kufanya naye biashara ya matangazo.

“Hapa sasa hivi tunaongea kuhusu majukumu yangu kama balozi, nione nina show ngapi katika hiyo event na mambo ya maslai inakuaje, nione matangazo ya runinga na mabango na nijue amount ya kazi yote ilivyo ni kiasi gani ninaweza kunufaika.Tukifikia muhafaka watu wataniona kwenye mabango, nimekoleza mafuta nimeweka na logo za hiyo kampuni,” amesema Ben Pol.

Wastara afunguka kwa Uchungu Kuhusu Zari Kutukanwa

$
0
0

Wastara afunguka kwa Uchungu Kuhusu Zari Kutukanwa:

From @wastara84 - Ukimuona nyani kazeeka na bado anaishi ujue kakwepa mishale mingi saana mtanisamehe kwa masamiati huu
Lakini mim ni mama sijawahi kusahau uchungu wa mwana na wala sijamsahau aliyenifanya niitwe mama lakini usiniulize kwanin sipo na niliyezaa nae ni mambo binafsi sana sio lazima kila mtu ajue
Lakini akifa nitaenda na ikibidi kulia nitalia sababu alikuwa na bado atakuwa baba wa watoto wangu.....
Lakini why why why mtu atukanweee weee asemwee kipindi kibaya cha uchngu na mawazo kama hiki hivi jamani mnajua kufiwa kweli wenzangu mbona hili la zari kutukanwa limenishinda kabsa kuvumulia...
Mtazameni huyo mtoto mdogo kwenye pic anamtazama babaake kwenye pic aliyoishika huku akitabasam utafikiri anasema baba upo umeenda kutembea siku moja utaludi tuu
Pangine
Ajui hta maana kufa ailewi aelewi maskini
Acheni basi fikirieni machungu yenu mpate hata robo ya maumivu wanayopata viumbe hawa #kufaanapesaavifanani
Pole wafiwa @zarithebosslady
Mungu amlaze mahali pema ivan ameen

Wizara ya Fedha Yaliomba Bunge Sh 11.7 Tilioni..!!!!

$
0
0

Wizara ya Fedha na Mipango imeliomba Bunge iliidhinishie Sh11.757trilioni ili iweze kutekeleza majukumu yake kwa mwaka wa fedha 2017/2018, kwa mafungu yote tisa yaliyo chini ya Wizara hiyo.

Maombi hayo yametolewa leo na Waziri wa Fedha na Mipango Philip Mpango, wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizaya hiyo, Bungeni Mjini Dodoma.

 Dk Mpango amesema kuwa kati ya fedha hizo, Sh10.328trilioni  ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Sh1.429trilioni  ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.

 Amefafanua kuwa matumizi ya kawaida yanajumuisha Sh87.996bilioni kwa ajili ya mishahara, Sh778.6bilini kwa ajili ya matumizi mengineyo (OC) na Sh9.4trilioni ni kwa ajili ya kulipa Deni la Taifa na Huduma nyingine.

 Pia katika fedha za matumizi ya maendeleo, Sh1.382trilioni  ni fedha za ndani na Sh46.1bilioni ni fedha za nje.

Mambo Muhimu 11 Unayopaswa Kumwambia Mpenzi Wako Kila Siku

$
0
0

Kutengeneza uhusiano wenye nguvu ni moja ya mambo yenye changamoto kubwa. Japo hakuna maelekezo maalum, kuna mambo machache na rahisi ambayo unaweza kumwambia mpenzi wako yakaujenga zaidi. Weka desturi ya kusema mambo haya kwa mpenzi wako na muda mfupi tu mtakuwa couple itakayowapa wivu marafiki zetu.

1. Nakupenda

Nakupenda ni kitu rahisi na cha wazi cha kumwambia mpenzi wako. Hakikisha tu kuwa unamaanisha. Jaribu kulisema neno hilo pindi mpenzi wako anapokuchekesha au pale anapofanya kitu kinachokukumbusha kwanini mko pamoja.

2.Nilikuwa nakuwaza

Ni muhimu kumjulisha mpenzi wako kuwa unamuwaza hata kama hamko sehemu moja. Ukiona kitu kizuri au cha kuchekesha katika siku yako ambacho kinakufanya umkumbuke, mjulishe.

3. Siku yako ilikuaje?

Muulize masuala ambayo mpenzi wako anakutana nayo katika shughuli za kila siku. Muulize kuhusu huyo mfanyakazi mwenzie anayemkera au kazi kubwa waliyokuwa wakifanya. Kumpa nafasi mpenzi wako kushare sehemu zingine za maisha yake kutasaidia kuunganisha dots kati ya muda mnaokuwa pamoja.

4. Nakuunga mkono

Mpe moyo mpenzi wako kwa kumjulisha kuwa unaunga mkono maamuzi yake. Unaweza ukaenda mbali zaidi kwa kujaribu kumsaidia afanikishe malengo aliyojiwekea. Maisha yamejaa vikwazo vingi, na ile hisia kuwa una mtu mwingine upande wako zinaweza kukusaidia kuvivuka. Msiwe couple tu, kuweni timu. Kumkumbusha mpenzi wako kuwa upo nyuma yake kutaimarisha uhusiano wenu.

5.Umependeza

Picha na OGS Studio

Kama umekuwa kwenye uhusiano kwa muda mrefu, ni rahisi kujisahau katika mengi. Ni muhimu kumkumbusha mpenzi wako kuwa anakuvutia. Kumjulisha kuwa ‘gauni hilo limekupendeza sana’ kutamfanya ajisikie vizuri na kukumbusha kwanini ulimchagua yeye.

6. Samahani

Kila mtu hukosea wakati fulani. Wakati mwingine hujikuta tukiongea maneno kwa hasira na baadaye kugundua kuwa hatukuwa sahihi. Ubishi hauna nafasi kwenye uhusiano wenye furaha, hivyo omba msamaha unapofanya kosa. Omba msamaha kwa kukasirika. Omba msamaha kwa kuumiza hisia za mpenzi wako. Omba msamaha hata kwa vitu ambavyo sio kosa lako.

7. Hakuna kama wewe

Mpenzi wako anatakiwa kuwa rafiki yako. Kama hautaki kutembea naye, basi hamkupaswa kuwa kwenye uhusiano. Mfanye mpenzi wako ajue kuwa yeye ni bora na hakuna kama yeye.

8. Napenda mawazo yako

Mwambie mpenzi wako kuwa unapenda mawazo yake. Mjulishe kuwa unaona ana akili, mcheshi, anajua kupenda na ana kipaji.

9.Nakuheshimu

Kama ulivyo uhusiano wa marafiki, heshima ni kitu muhimu kwako na mpenzi wako. Mpe nafasi ya kukushauri au kukupa mawazo kwenye mambo yanayokutatiza. Mtu anapohisi anaheshimiwa, hujisikia pia furaha na salama, vitu ambavyo ni muhimu kwenye uhusiano wowote mzuri.

10. Napingana na hilo

Sehemu moja wapo ya kumheshimu mpenzi wako ni kumjulisha pale usipokubaliana naye. Hakuna mtu anapenda kuoa mtu anayekubaliana na kila kitu na hakuna mwanamke anayetaka kuzaa watoto na mwanaume asiye na msimamo. Mnaweza kuwa timu, lakini nguvu ya timu yoyote ipo kwenye mawazo na matendo ya kila mmoja. Kuwa na maoni yako na yaseme kwa mtindo wa heshima. Kumpa mpenzi wako mtazamo tofauti kunaweza kumsaidia kupata suluhisho kwa tatizo ambalo hakuwa ameliwaza.

11. Usiku mwema

Tunaishi kwenye wakati ambapo mawasiliano ni rahisi mno. Kwa kubonyeza tu kitufe tunaweza kutuma ujumbe kuvuka bahari, hivyo hakuna kisingizio cha kushindwa kusema ‘usiku’ mwema.

Haimjulishi mpenzi wako tu kuwa unataka kulala, bali pia inamjulisha kuwa unamfikiria. Hata kama hamjaongea siku nzima na hasa kama mmejibizana, maliza siku na kishindo chanya.

Wakenya wataka kuipiku Tanzania ili wacheze na Everton

$
0
0

Michuano ya SportPesa Super Cup, imeanza kuwa gumzo huku Wakenya wakitamba zaidi kuwa wanataka timu yao ichukue ubingwa na kupata nafasi ya kucheza na Everton ya England.

Bingwa wa michuano hiyo atapata nafasi ya kucheza na Everton kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Tayari makundi mawili ya SportPesa Super Cup yametangazwa na yatajumuisha timu za Tanzania Bara, Visiwani na Kenya.

Timu kutoka Tanzania ambao ni wenyeji ni Simba, Yanga, Singida United na Jang'ombe.

Wakati kutoka Kenya ni Gor Mahia, Express na Nakuru All Stars.

Makundi ya michuano hiyo yako hivi; Kundi la kwanza linakwenda kwa mfumo huu, LEopards wanatcheza na Singida na Yanga itawavaa Tusker. Mshindi wa kila upande watakutana kucheza nusu fainali na mshindi atakwenda fainali.

Kundi la pili, Gor Mahia atawavaa Jang'ombe na Simba itakuwa dhidi ya Nakuru. Washindi watakutana kucheza nusu fainali na mshindi atakwenda fainali.

Mashabiki wengi wa soka kutoka Kenya wamekuwa wakiandika mitandaoni kutoa maoni wakizisisitiza hasa Gor Mahia na Leopards kulinda heshima ya Kenya na kupata nafasi hiyo ya kucheza na Everton.

Faida 4 za Kufunga Mwezi Huu Mtukufu wa Ramadhan..!!!

$
0
0

Kwa mujibu wa dini ya kiislam tunakumbushwa kuwa kila muislam mzima na mwenye afya njema anatakiwa kushiriki katika swaumu ambayo ni ibada ya kufunga chakula na kinywaji mcahana na kutwa sambamba na kujizuia kushiriki toka alfajiri hadi magharibi.

Pamoja na hayo, matendo hayo yatoba hupaswa kuendana na kuswali sana pamoja na kusoma quran kwa wingi.

Katika mwezi huu wa Ramadhani kadhalika inatakiwa kwa muislam kuwa mengi ya maneno yake yawe katika kumtaja Allah (Subhaanahu wa Ta’ala), kwani ni jambo ambalo linasaidia katika kuusafisha moyo  wake na kuiboresha funga yake.

Mbali na hayo zipo pia faida nyingine za kufunga kama zifuatazo

1. Ni kutekeleza mojawapo ya amri za Mwenyezi Mungu alizotuteremshia na faida ya utekelezaji huu ni kuingia peponi siku ya mwisho.

2. Faida ya pili ya mfungaji wa swaumu ni kujizoesha kuwa na subira, yaani katika mwezi Mtukufu wa Ramadhan, mtu anajifunza jinsi ya kuwa mvumilivu na kustahamili njaa, kiu na matamanio ya kimwili.

3. Faida nyingine ni kuwa muadilifu na kujifundisha usawa baina ya masikini na  tajiri.

4. Pia funga hutusaidia kiafya kwani huifanya mifumo kadhaa ya mwili nayo kupata wasaa wa kupumzika kwa mda fulani.

Spika Ndugai: Natamani kupanda mabasi ya mwendo kasi

$
0
0

Dodoma.  Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema anatamani kupanda mabasi ya mwendo wa haraka yaliyoko jijini Dar es Salaam.

Pia, ameishauri kampuni ya usafiri ya Udart kuangalia uwezekano wa kuwekeza mjini
Dodoma.

Akizungumza leo (Jumanne) baada ya kukutana na maofisa wa Udart waliomkabidhi majarida ya kutimiza mwaka mmoja tangu kuanza shughuli za usafirishaji, Ndugai amesema siku akifika Dar es Salaam atahakikisha anapanda mabasi hayo, akiwataka wasaidizi wake kumkumbusha ili kujionea jinsi linavyoendeshwa.

Amesema kitendo cha mradi huo mkubwa kuendeshwa na Serikali kwa kushirikiana na mbia ambaye ni Mtanzania ni kielelezo kwamba Watanzania wanaweza.

Ndugai amewataka Udart kuboresha usafiri huo kwa kuongeza mabasi na kampuni hiyo kuangalia namna ya kuwa na mabasi mjini
Dodoma kwa kuwa ndiko yaliko makao makuu ya nchi na watu wameongezeka.

Mkuu wa Kitengo cha Habari Msaidizi wa Udart, Joe Beda amesema watafanya kila linalowezekana kuhakikisha mradi huo unakuwa endelevu kwa kuwa ni
moja ya miradi ya aina yake barani Afrika.

Huyu Omond Huyu Jamani..Ona Hpa Picha Zake Mpya Akiwa Kama Mwanamkee..!!!

Zifahamu Faida 6 za Juisi ya Tangawizi, Halafu Nenda Kajaribu Uone Ajabu Yake..!!!

$
0
0

Tangawizi ni kati ya viungo mahili vinavyochochea ladha nzuri katika vyakula vya aina mbalimbali na hivyo kuwavutia walaji kula chakula husika.

Tangawizi pia inapowekwa kwenye vyakula vigumu kama nyama huifanya ilainike na hivyo kuweza kuiva kwa haraka zaidi.

Leo nataka kukueleza msomaji wangu kuhusu hizi faida nyingine za kutumia juisi ya tangawizi kama ifuatavyo:-

1. Hutumika kama kituliza maumivu.

2. Husaidia kuboresha mmeng'enyo wa chakula tumboni

3. Huthibiti shinikizo la damu

4. Huboresha afya ya kinywa

5. Hukinga matatizo ya ngozi hasa chunusi

6. Husaidia kukuza nywele (kulinda afya ya nywele)

Sentensi 3 Zinazotajwa Kawaida, Ambazo Mwanamke Hapaswi Kabisa Kumwambia Mmewe/Mchumba..!!!

$
0
0

Ulimi ni kiungo muhimu sana kwenye maisha ya binadamu. Neno moja linaweza kujenga au kubomoa ukuta mkubwa wa ndoa uliojengwa kwa gharama kubwa ya uvumilivu, uaminifu na upendo.

Hivyo, ni jambo muhimu sana kukumbushana japo kwa machache baadhi ya sentensi zinazotumika mara kwa mara na kuonekana kuwa za kawaida, lakini zinaweza kuwa chanzo cha kuvunja ndoa au kuvuruga uhusiano uliostawishwa kwa gharama kubwa.

Leo nitagusia sentensi tatu za kawaida kabisa ambazo hutumiwa na baadhi ya wanawake bila kufahamu kuwa zinaweza kuwa chanzo kikuu cha kuutafuna uhusiano wao.

“Mama Yangu Alinionya Kuwa Utanifanyia Hivi.”…

Sentensi hii inaweza kumfanya mmeo kuwaza mengi sana kuliko ulivyomaanisha wewe pale unapotaka kumkosoa kwa alichokifanya. Kwanza atagundua kuwa una watu wengi nyuma yako ambao wanakusaidia kumfikiria ‘hasi’.

Kibaya zaidi unapomuweka kwenye kundi hilo mama yako ambaye yeye anamheshimu sana. Hii linaaweza kupelekea mchumba au mme wako kutokumuamini mama yako na kuanza kumuona kama adui wa uhusiano wenu. Unadhani mama yako akiwashauri jambo atalichukuliaje? Hata kama ni zuri.

“Unafikra Kama Za Baba Yako” (Unapomkosoa)

Bila shaka unafahamu ni kiasi gani wanaume huwaheshimu sana na kuwaamini sana baba zao ambao wamewashauri mengi hadi walipofika hapo. Hata kama huwa anakueleza baadhi ya fikra au mawazo ya baba yake asiyokubaliana nayo, usidhubutu kabisa kumtolea mfano kumuonesha kuwa na wewe unamchukulia hivyo mzazi wake.

Kukosoana ni suala zuri katika maisha ili kurekebishana lakini angalia njia nzuri ya kupinga hoja ya mwenzi wako, kwa ustaarabu kuepuka kumkera.

“Hivi Lini Utapata Kazi Mpya..?”

Swali hili sio baya lakini kwa jinsi lilivyoulizwa lina kila dalili za kuleta shida sana kwenye fikra za mumeo/mchumba wako. Kwanza atajua ni kiasi gani unafikiria vibaya kuhusu maisha yenu hasa kiuchumi.. Ni bora kumwambia, “Mume wangu ninakuombea sana upate kazi mpya.” Ni ujumbe uleule lakini jinsi ulivyofikishwa unatofautiana sana.

Kwa Mara ya Kwanza Nchi Imekuwa na ma-IGP Wawili..!!!

$
0
0

Kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi yetu tumekuwa na maIGP wawili. Mmoja amepewa madaraka ya kuwa mkuu wa jeshi la polisi na mwingine amevuliwa madaraka hayo lakini amebaki na cheo chake.

Wengi hawajui kuwa IGP ni cheo na sawa na vyeo vingine kama Inspekta wa polisi au Mrakibu wa polisi au Koplo. Tofauti ni kwamba vyeo vya chini vinaweza kushikwa na watu wengi lakini cheo cha juu kabisa ambacho ni IGP hushikwa na mtu mmoja tu. Yani makoplo wanaweza kuwa wengi, makamishna wengi, mainspekta wengi lakini IGP mmoja.

Huyo IGP mmoja ndo hupewa madaraka ya kuongoza jeshi la polisi. Kumbuka kuna tofauti kati ya CHEO na MADARAKA. Mtu mwenye cheo cha IGP ndio hupewa madaraka ya kuongoza jeshi la polisi. Sasa kwa mara ya kwanza tumekua na watu wawili wenye cheo kimoja cha IGP.

Tofauti ni kwamba mmoja ameondolewa madaraka ya kuongoza jeshi la polisi, na mwingine kapewa madaraka hayo. Huyu aliyeondolewa madaraka, ameambiwa atapangiwa kazi nyingine. Lakini bado amebaki na cheo chake cha IGP. This means Mangu akiteuliwa balozi atatambulika kama Balozi IGP Ernest Mangu maana cheo chake hajavuliwa. Ni sawa na wale wanajeshi wanaoteuliwa kuwa wakuu wa mikoa, wanabaki na vyeo vyao.

Na kwa kuwa Mangu hajastaafu utumishi, siku akistaafu basi atastaafishwa kwa cheo chake cha IGP. Japo wakati huo anaweza kuwa na madaraka mengine kama ukuu wa mkoa, ubalozi etc.

SWALI: Je ni sahihi kuwa na maIGP wawili kwenye nchi? Yani watu wenye vyeo vinavyolingana japo wana madaraka tofauti. Hii iko sawa au mkuu amechemsha? Maana haijawahi kutokea tangu uhuru. Hebu wale ndugu zetu ambao ni askari watusaidie uelewa kdg.!

Malisa G

Shilingi Imeaimarika? Kwanini Srikali inapenda kusema uongo hata kwa mambo yaliyo wazi?

$
0
0

Kwanini serikali inapenda kusema uongo hata kwa mambo yaliyo wazi? Waziri wa fedha amesema kuwa sarafu yetu (shilingi) imezidi kuimarika dhidi ya dola kwa mwaka huu wa fedha unaoishia. Huu ni uongo wa wazi kabisa. Ukweli ni kwamba shilingi imezidi kuporomoka maradufu dhidi ya dola kwa kipindi cha mwaka huu wa fedha.

Kwa mujibu wa records za BOT, tarehe 1 July mwaka jana thamani ya dola moja ya Marekani ilikua sawa na TZS 2,126.07/= (bei ya kuuzia), leo tarehe 29 mwezi May 2017, dola moja ya Marekani ni sawa na TZS 2,280.80/= (bei ya kuuzia). This means sarafu yetu imeporomoka kwa 7.2% dhidi ya dola ya kimarekani.

Sasa Waziri Mpango anaposema sarafu imeimarika anamaanisha nini? Uongo huu ni kwa faida ya nani? Kama serikali inaweza kusema UONGO kwenye mambo yaliyo wazi kama haya, vp kwa yale yasiyo wazi?? Kwanini mnatafuta credit kwa kusema uongo? Mkisema ukweli mtapoteza nini? Shame on u.!!
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images