Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Huyu Ndiye Bilionea Dangote ..Apanga Kununua Kiwanda Hiki Kikubwa cha Kutengeneza Magari Afrika..!!!

$
0
0

Mfanyabiashara tajiri Afrika, Aliko Dangote anasubiri idhini ya Benki Kuu ya Nigeria ili anunue kiwanda cha kuunda magari aina ya Peugeot akishirikiana na majimbo mawili.

Kampuni ya Usimamizi wa Mali ya Nigeria (AMCON), iliyoundwa wakati wa kuyumba kwa benki, inakaribia kuuza Kiwanda cha Magari cha Peugeot cha Nigeria (PAN).

“Tumeshakamilisha mchakato wote wa zabuni miezi miwili iliyopita na sasa tunasubiri idhini ya Benki Kuu,” alisema ofisa mtendaji mkuu wa AMCON, Ahmed Kuru alipoongea na Reuters.

PAN, kiwanda cha kuunda magari kilichopo jimbo la Kaduna, kina ubia wa kiufundi na PSA Peugeot Citroen na kikiwa na uwezo wa kuunganisha magari 90,000 kwa mwaka.

Dangote, kwa kushirikiana na majimbo ya Kaduna na Kebbi na Benki ya Viwanda (BOI) waliomba zabuni ya kuwa wamiliki wakubwa wa hisa za PAN mwaka jana kutokana na AMCON kutaka kuuza baadhi ya mali zake ilizozichukua wakati wa matatizo ya taasisi za kifedha.



Wakati Joto la Mchanga wa Madini Likiendelea Kuvuma..Zitto Kabwe Akoleza Moto kwa Kusema Haya..!!!

$
0
0

MBUNGE wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, amesema Tanzania inapaswa kuhakikisha sheria na sera za madini zinalazimisha rasilimali madini kuwa mali ya Watanzania ndipo nchini itanufaika.

Aidha, amesema ni wakati muafaka kwa Taifa kujitoa katika mfumo wa kodi za Kimataifa akiuelezea kuwa umeonesha kunyonya nchi maskini zaidi na kunufaisha zile  tajiri.

Zitto alisema hayo jana wakati akizungumza kwenye kipindi cha Mizani ya Wiki kinachorushwa na televisheni ya Azam Dar es Salaam.

Alisema kwa kuwa Rais John Magufuli ameamua kupigania vita hiyo ni jukumu la kila Mtanzania kupigana hadi kuhakikisha kuwa madini yanakuwa ni mali ya wananchi wa Kitanzania.

Zitto alisema kwa mujibu wa sheria iliyopo inaanisha kuwa baada ya mwekezaji kuingia mkataba na Serikali madini ni mali yake jambo ambalo halikubaliki.

“Hii vita ni vita ngumu ila kwa sababu Rais ameamua kuipigana pamoja na ukweli kuwa anajua jitihada za Serikali iliyopita tunapaswa kumuunga mkono ili tuweze kunufaika.

“Mimi nataka mambo haya mawili yaangaliwe ili kuhakikisha kuwa rasilimali madini inatambulika kama mali yetu kwani kwa sasa ni mali ya mwekezaji,” alisema.

Alisema iwapo sheria inapaswa kumtambua mwekezaji kama mkandarasi kwani kwa sasa inamfanya aonekane ndiye mwenye mali.

Mbunge huyo alisema kwa mujibu ya sheria ya gesi na mafuta mwekezaji ni mkandarasi ambapo akipata bidhaa husika anarejesha gharama yane na katika faida nchi inagawana na mwekezaji kwa sawa au nchi kupata zaidi.

Alisema jambo la pili ni mfumo wa kodi wa kidunia umeweka mazingira ambayo kampuni za Kimataifa zinauwezo wa kuhamisha mapato yake kwenda kwenye visiwa ambavyo kodi zipo chini hali ambayo inachangia wasilipe kodi.

Mbunge huyo alisema mfano mwaka 2011 Kampuni ya Barick wakati huo ambayo kwa sasa ni Acacia ilitoa taarifa ya kupata hasara nchini ila ilionesha kupata faida nchini Uingereza hivyo kulipa kodi kwa Malkia.

Zitto alisema katika kukabiliana na hali hiyo dunia ilianza mjadala wa kuhakikisha kuwa kodi hizo zinapatikana na Tanzania ilikuwa ni mwenyekiti wa mjadala huo ila tangu Serikali ya awamu ya tano iingie madarakani imeonekana kuachwa.

“Ni masikitiko makubwa kwa Serikali ya Tanzania kuacha mjadala ambao tulikuwa tunaongoza wa mfumo wa kodi za Kimataifa ambao ungeweza kutuletea mabadiliko chanya ya rasilimali madini ambayo inaonekana haina faida kwa nchi na wananchi,” alisema.

Mbunge huyo alisema tipoti ya Profesa Abdulkarim Mruma haina jipya katika ripoti ya Jaji mstafufu Mark Boman ambayo ilianisha yote yaliyoanishwa kwa sasa.

Zitto alisema kamati hiyo ilipendekeza miaka tisa iliyopita kuwepon kwa mashine ya uchenjuaji inakuwepo ikiwa ni pamoja na kuwepo sera na sheria sahihi kwa sekta hiyo.

“Nakumbuka nilikuwa masomoni nchini Ujerumani nilirudi kupitisha sheria hiyo ambayo ilipangiwa kutumia wiki moja ila muda haukutosha ikawa wiki mbili na tulishirikisha watu asasi za kiraia ili kutusaidia kupata mkuafaka,” alisema.

Mbunge huyo alisema kwa ushirikiano huo ilikuwa rahisi wajumbe wa kamati ya Bunge ya Nishati na Madini kufanya kazi na kuja na mapendekezo sahihi kuhusu rasilimali hiyo.

Alisema wao kama chama wamejipanga kufanya mjadala mwisho wa wiki hii kuhakikisha jamii inatambua rasilimali madini kwa undani ili kila mtu aweze kufahamu kila kitu.

Kwa upande wake Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Benson Bana alisema ni wakati muafaka wa Watanzania kujitathmini kuwa wana matatizo gani.

Alisema ni vema kuangalia uwezekano wa kutumia wataalam mbalimbali duniani kuhusu rasilimali zake ili ziweze kunufaisha jamii kwa ujumla.

Bana alisema ukifuatilia mfumo wa kutunga sera na sheria za nchi unaonekana kufuata misingi nataratibu zinazohitajika ila kumekuwepo na changamoto ya usimamizi na utekelezaji.

“Wakati mwingine najiuliza tunakwama wapi ila nabakia na tafsiri mbili kwamba kuna mashinikizo ya wazi na yasiyo ya wazi hivyo tunapaswa kujipanga kukabiliana na hali hiyo,” alisema.

Duh..Hivi Ndivyo Magari ya Kifahari Yalivyotawala Msiba wa Ivan..Matajiri Waliokuja Nayo Wamwaga Pesa za 'Sadaka Lawe' kwa Masikini..!!!

$
0
0

 Magari ya kifahari yameonekana jana katika mazishi ya bilionea Ivan Ssemwanga yaliyofanyika nyumbani kwao Kayunga jijini Kampala.


Ivan aliyekuwa mume wa Zari Hassan maarufu ‘Zarithebosslady’ ambaye kwa sasa ni mpenzi wa Diamond Platnumz, alifariki dunia wiki iliyopita baada ya kupata kiharusi na kuwa katika hali ya koma kwa wiki mbili mfululizo katika hospitali ya Steven Biko huko Pretoria nchini Afrika Kusini.

Gazeti la Uganda, Daily monitor linaripoti kuwa miongoni mwa magari hayo ni pamoja na yale ya marehemu likiwemo Hammer lenye jina la Ivan 9, yale ya vizito mbalimbali wa jiji la Kampala waliohudhuria mazishi hayo pamoja na gari la tajiri wa Tanzania Jack Pemba aina ya Audi lenye jina la A Pemba ambalo lilionekana kuwa la kifahari zaidi.

Katika hali ambayo haikuonekana kuwa ya kushangaza, baadhi ya waombolezaji walionekana wakiomba na kupewa fedha kutoka kwa matajiri mbalimbali waliohudhuria.

Hata hivyo kaburi la Ivan liliwekwa mafungu ya fedha chini ikiwa ni maandalizi ya kuuweka mwili wa bilionea huyo.

Mwili wa Ivan ambao uliwasili Uganda siku mbili zilizopita katika ndege kubwa iliyobeba watu 50, umezikwa katika makaburi ya familia pembeni ya kaburi la baba yake.

Credit - Mwananchi

Lema Ataka Kambi Rasmi ya Upinzani ya Upinzani Ivunjwe..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo Jumatano 31/5/2017..!!!

Wenger Alamba Mkataba Mpya Arsenal..Apewa Miaka Miwili ya Matumaini..!!!!

$
0
0

Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amekubalia kusaini mkataba wa miaka mwili wa kuendelea kuifundisha klabu hiyo kuendeleza utawala wake wa miaka 21 ndani ya Emirates.

Wenger na mmiliki wa klabu hiyo Stan Kroenke walikutana Jumatatu kuzungumzia hatma yake na uamuzi huo ukacheleweshwa kutolewa na bodi leo Jumanne.

Arsenal imepanga kesho kumtangaza rasmini Mfaransa huyo kuendelea na jukumu lake.

Arsenal 'The Gunners' imemaliza katika nafasi ya tano msimu huu wa Ligi Kuu ikiwa ni mara ya kwanza tangu Wenger alipochukua jukumu la kuifundisha timu hiyo mwaka 1996.

Imemaliza ikiwa nyuma kwa pointi 18, kwa mabingwa Chelsea,  lakini ilifanikiwa kuifunga Blues mabao 2-1 katika fainali ya Kombe la FA iliyofanyika Wembley Jumamosi iliyopita.

Mkataba wa Wenger uliokuwa unamalizika mwisho wa msimu huu.

Wenger ameiongoza Gunners kutwaa mataji matatu ya Ligi Kuu England na makombe manne ya FA katika misimu yake tisa ya kwanza.

Msimu wa 2003-04, alikuwa kocha wa kwanza tangu 1888-89, kuiongoza timu kucheza msimu mzima bila ya kufungwa mchezo wowote.

Dola ya Marekani Yatikisika Katika Soko la Dunia..Trump Adaiwa Kuwa ni Chanzo..!!

$
0
0

WATUNGA sera kutoka Benki Kuu ya Marekani, wamesema wanafuatilia kilichoko katika uchumi wa taifa, kutokana na kuongezeka kiwango cha riba za benki nchini humo na imefanya thamani ya fedha za dola kushuka.

Mchumi wa nchi hiyo, Gus Faucher, anasema ni hali ya kushangaa kuonekana Dola za Marekani, inashuka thamani hivi sasa.

"Nadhani takwimu tulizopata kutoka mkutanoni inaonyesha vigezo," anasema Faucher, huku wachumi wakieleza shaka yao dhidi ya hali halisi ya sera za Rais mpya, Donald Trump.

Inaelezwa kwamba katika kipindi kifupi kilichopita, tangu Machi mwaka huu, serikali iliongeza kiwango cha riba zake mara tatu.

Pia, katika sura nyingine, inaelezwa kuwa benki zimeendelea kuwa imara katika majukumu yake ya kila siku.

Kwa miaka mingi na katika sehemu nyingi, Dola ya Marekani imekuwa marejeo cha kiwango cha mabadilishano katika fedha za dunia.

Pia, kuna fedha kama za Euro ambazo ni za Jumuiya ya Ulaya (EU) na Pauni za Uingereza, nazo zimeshika nafasi hiyo .

Nane Waidhinishwa Kuwania Urais Kenya...!!!!

$
0
0

Tume ya Uchaguzi na Mipaka nchini Kenya, IEBC, imeidhinisha majina ya wagombea nane kuwania Urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Agosti mwaka huu

Kati ya wagombea hao, ushindani mkubwa unatarajiwa kuwa kati ya Rais Uhuru Kenyatta anayewania muhula wa pili na mgombea wa muungano wa vyama vya upinzani NASA Raila Odinga.

Hata hivyo, zoezi la mchujo liliwaacha wengine zaidi ya 10 nje ya kinya'nga'nyiro hicho akiwemo Peter Solomon Gichira aliyefikishwa Mahakamani kwa madai ya kutaka kujiua baada ya kuondolewa katika orodha hiyo kwa kutokidhi vigezo.

Ushindani unaotarajiwa kati ya Rais Kenyatta na Bw. Odinga, unarejesha nchi hiyo katika historia ya siasa kati ya baba zao, Jomo Kenyatta aliyekuwa Rais wa kwanza na Jaramogi Oginga Odinga aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais baada ya Uhuru mwaka 1963.

Wagombea wengine sita ambao wanawania Urais ni pamoja na Cyrus Jirongo (UDP), Ekuru Aukot kutoka chama cha Thirdway Alliance, Abduba Dida (ARC).

Wagombea binafsi ni pamoja na Joseph Nyagah, Michael Wainaina na Japheth Kavinga, ambao wamejinadi kama chaguo sahihi la kuleta mabadiliko.

Msaada: Bahati Mbaya Nimetuma Video za Ngona Katika Group la What's app la Familia

$
0
0

Jamani nipo kwenye group la familia pamoja na;
1: Baba na Mama,
2. Dada zangu na mashemeji zangu,
3: Wadogo zangu na wajomba,
5: Ndugu wengine,

Sasa bahati mbaya nimetuma video za ngono Tatu bila kujua yani dah nime left na kuzima data..Hapa kichwa kinawaka Moto balaa... Kwani niaibu kubwaa hii... Naombeni ushauri nifanyeje kujisafisha nisionekane punguani...!!! Msinitukane lakini !

Lema Amtabiria Mwigulu Kusimamishwa Uwaziri Muda Wowote Kuanzia Sasa

$
0
0

Mbunge Godbless Lema kupitia account yake ya Twitter Amtabiria Mwigulu Kusimamishwa Uwaziri Muda Wowote Kuanzia Sasa ikiwa ni siku chache zimepita baada ya Prof Muhongo Kutumbuliwa....
.
Mdau Una maoni gani?

Edo Kumwembe ' Simba inahitaji wanaume watatu wa nguvu'

$
0
0


Edo Kumwembe afunguka haya:

Makala ambayo msemaji wa Simba kasema ni mbovu...shabiki wa Simba uisome hapa na utafakari akili za msemaji wako

.

JICHO LA MWEWE: Simba inahitaji wanaume watatu wa nguvu
By EDO KUMWEMBE

TUKUTANE uwanja wa ndege. Simba itakuwa inasafiri labda kwenda Rwanda, Yanga itakuwa inasafiri kwenda Misri. Kule kwa Yanga kiasi wametimia, huku kwa Simba kunahitajika wanaume watatu wengine kabla ya kupanda ndege kwenda hiyo safari yao.

Simba inahitaji kuingia sokoni kwa umakini na kununua wachezaji watatu wa kigeni wa maana ambao, kwa hapa nchini sijawaona mpaka sasa. Mgongo wa timu ni mlinzi wa kati kiongozi mwenye uzoefu.

Kisha kiungo mahiri mwenye nguvu na uzoefu, halafu mshambuliaji wa nguvu anayeweza kufunga mabao 20 ya msimu.

Kwa kuanzia katika ushambuliaji Simba wamekwenda kwa John Bocco. Siyo mbaya. Kwa kulinganisha washambuliaji ambao wanao sasa hivi, Bocco ni bora zaidi. Bocco aliye fiti bila ya majeraha ni bora kuliko Laudit Mavugo au shujaa wa juzi, Fredric Blagnon.

Anahitajika mtu kama Donald Ngoma wa Yanga. Mtu msumbufu, mwenye nguvu, asiyeogopa, lakini cha msingi zaidi awe na jicho la kuona lango. Niliandika mitandaoni, Ngoma hajaichezea Yanga katika Ligi tangu Januari, lakini Mavugo hakuweza kufikia mabao yake katika ligi.

Kwa muda mrefu Simba imekosa mshambuliaji tishio huku ikishindwa kufanya vyema katika soko la uhamisho la wachezaji wa kimataifa. Tangu alipoachwa huru Amiss Tambwe na kununua Dan Sserunkuma, Simba haijapata mtu wa uhakika pale mbele.

Katika nafasi ya ulinzi Simba wanahitaji mtu kiongozi, mbabe, mwenye akili ya mpira kama Serge Paschal Wawa. Huyu Method Mwanjali inaonekana umri umesogea na ndiyo maana hata majeraha yake yamechukua muda mrefu.

Hata kama angekuwa fiti, katika mechi za kimataifa Simba tayari ilikuwa inahitaji beki wa nguvu wa kucheza naye sambamba. Juzi James Kotei amecheza vizuri katika nafasi hiyo, lakini nadhani bado anahitajika mlinzi wa nguvu zaidi.

Simba pia wanahitaji kiungo mwingine mwenye mamlaka uwanjani. Kiungo ambaye pia atakuwa kama kiongozi wa eneo hilo. Kuna utoto mwingi katika eneo la kiungo la Simba hasa

Mbunge - Dunia Nzima Itamwiga Rais Magufuli..Hadi Trump Ipo Siku Atamwiga Tu..!!!

$
0
0


Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CCM), Peter Serukamba amefunguka na kusema jambo alilofanya Rais Magufuli kuzuia mchanga litakwenda kuigwa duniani kote na kuleta mapinduzi katika "Extractive Industries" (sekta za uchimbaji madini)

Serukamba alisema hayo jana bungeni na kusema ukiona mpinzani wako anakupinga katika jambo lolote lile basi ujue umefanya jambo ambalo ni sahihi ila ukiona mpinzani wako anakusifu ujue umefanya jambo baya, hivyo kwa kuwa wapinzani wanalalamika basi Rais amepatia katika maamuzi yake, na anatakiwa kupewa ushirikiano wa wananchi na wabunge.

"Mimi kama mwanasiasa ukiona mtu ambaye ni adui yako umefanya jambo akakusifia ujue lipo tatizo, ila ukiona umefanya jambo adui yako akasema umekosea maana yake umepatia sana. Mimi naomba nimpongeze Rais Magufuli kwa kazi kubwa aliyofanya na niwaambie waheshimiwa wabunge, duniani kote 'Extractive Industries' inaenda kubadilika atakaye kuwa kwenye historia ya kubadilisha Extractive Industries ni Rais Magufuli, leo duniani kote kila kwenye migodi mambo yatabadilika kwa sababu ya Magufuli amefungua milango, niwaambieni watanzania tusiogope kwenye hili lazima tuwe nyuma ya Rais tumuunge mkono aendelee na nina hakika wawekezaji watakuja mezani" alisisitiza Serukamba 

Lissu Afyatuka Tena Bungeni Kuhusu Sakata la Mchanga wa Madinii..!!!

$
0
0

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu amesema kuwa msimamo wake wa kupinga kitendo cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli cha kuzuia mchanga wa dhahabu kusafirishwa nje uko pale pale.

Ameyasema hayo  bungeni mjini Dodoma, ambapo amesema kuwa kuzuia mchanga huo wa dhahabu kusafirishwa kwenda nchi za nje kutaathiri uchumi kwani atakuwa ameenda kinyume na mikataba ya kimataifa.

“Rais Dkt. Magufuli amefanya kitendo ambacho ni kinyume na mikataba ya kimataifa, kwa hiyo hapa tutegemee hasara kubwa na kutengwa na jumuiya ya kimataifa,”amesema Lissu

Mrembo Maunda Zorro Akubwa na Skendo ya Kutumia Madawa ya Kulevya....

$
0
0
MREMBO mkali wa Bongo Fleva, Maunda Zorro amebwatukia tuhuma za utumiaji wa madawa ya kulevya na kuweka wazi kuwa hajawahi kubwia unga na kuwataka watu waache kupandikiza maneno akidai yupo tayari kwenda kupima.

Akizungumza na Risasi Vibes mwishoni mwa wiki iliyopita, kwa sauti yenye kukwaruza na ya juu zaidi, Maunda alisema amekuwa akitajwa na baadhi ya watu kwamba ni teja, jambo linalompa usumbufu na kuwashangaa watu wanaoshindwa kufanya mambo yao muhimu, badala yake wanajikita kusingizia watu kwa mambo yasiyofaa.



“Jamani, unajua nashangazwa sana na maneno ya watu kuwa natumia madawa ya kulevya, nani alishawahi kunikuta maskani navuta au nani huwa ananinunulia? Mbona tunazushiana mambo ya kijinga? Niko tayari kwenda kwa mkemia mkuu kupimwa kama natumia madawa hayo, au nikuulize, kwenye ile orodha ya waliotajwa ulisikia jina langu? Niacheni jamani, niko bize na maisha mengine na kwa sasa nimeamua kuwa mama wa nyumbani,” alisema Maunda.

Kutana na Mtaalamu wa Tiba Asili Ostadh Khamis Kutoka Mombasa..Yupo Tanzania....Anatibu Magonjwa Yafuatayo

$
0
0

Kutana na OSTADH khamis kutoka Mombasa Kenya kwa sasa yupo Tanzania nibingwa watiba za asili:

Miguu kuuma miguu kufagazi nakuwaka moto
Unashida na mchumba au pesa haikai muone haraka 
Kurudisha mpenziwako alie kukimbia ndani ya siku (3)
Dawa ya ( LIMBWATA) kumtawala mpenzi wako kwasababu maalumu   
Pete ya bahati inayo endana nanyota yako itakayo kuletea pesa bila mashart yeyote
Kuongeza uume saizi uipendayo 
Dawa ya ulijali 
Dawa yakuongeza hips
Kumuliki Mali isiokuwa namasharti yeyote 
Kurudisha Mali iliopotea au kudhurumiwa ndani yasiku(3) 
Napia OSTADH KHAMIS anafunga kesi nakupata hakiyako kwa haraka 
Dawa ya mvuto pia inapatikana mvuto Wa biashara kuuza Mali yako kwa haraka 
Kuzuiya chuma ulete na kupandishwa cheo kazini PAMOJA na kusafisha nyota njoo ufunguliwe vifungo ulivyo fungwa

Call+255718746825 au +255754765246 WhatsApp IMO +255783708487

Mtabiri: Majini ya Madini Yanawamaliza Mawaziri wa Tanzania

$
0
0
DAR ES SALAAM: Siku chache baada ya Rais Dk. John Magufuli kutengua uteuzi wa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, mtabiri maarufu nchini, Hassan Yahya Hussein, amesema sababu za mawaziri kutodumu katika wizara hiyo kunatokana na nguvu za majini zilizopo.

Akizungumza na Risasi Mchanganyiko ofi sini kwake, Magomeni Mwembechai Dar, mtabiri huyo alisema kinyota, madini asili yake ni majini, hivyo waziri yeyote anayepewa kitengo hicho lazima awe na nguvu ya maombi kwa Mwenyezi Mungu na awe amejitengeneza vilivyo.


Waziri wa Nishati na Madini ambaye Rais Dkt.John Magufuli alitenguliwa uteuzi wake, Profesa Sospeter Muhongo.
“Madini asili yake ni majini, hivyo anayesimamia hapo lazima awe na nguvu, kama hajajizatiti lazima uondoke tu, hata kama kosa siyo lako, unajikuta ukitumbuliwa kutokana na ushawishi wa majini,” alisema mtabiri huyo, mtoto wa gwiji wa utabiri Afrika Mashariki na Kati, hayati Yahya Hussein.

Akisisitiza kuhusu suala hilo, alisema inawezekana Waziri Muhongo hakuwa na makosa, lakini makosa yakawa ni ya watu wengine kutokana na kushawishiwa na majini, ndipo balaa likamwangukia yeye.

“Katika wizara ambazo ni ngumu kuziongoza kutokana na kuwa na nguvu za majini na mashetani ni Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Mali Asili na Utalii na Wizara ya Ardhi. Wanaoteuliwa kuongoza wizara hizo wanatakiwa kuwa makini sana kwa kumuomba Mungu au kujitengeneza kwa njia yoyote ili wawe na nguvu,” alisema.

Waziri Muhongo alitumbuliwa siku ambayo Rais Magufuli alipokea taarifa ya kamati ya kuchunguza mchanga wa dhahabu wa makontena 277 yaliyokuwa yamezuiliwa katika Bandari ya Dar es Salaam kwa amri ya mkuu huyo wa nchi.


Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini wa Awamu ya Nne, William Ngereja.
Katika ripoti hiyo iliyotolewa na mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Mruma, ilibainika kuwa kulikuwa na madini mengi ya dhahabu, shaba na sulphur, katika michanga hiyo, tofauti na maelezo yaliyotolewa awali na Wakala wa Ukaguzi wa Madini, TMAA ambayo ni taasisi iliyo chini ya wizara, kitu kilichomfanya Rais Magufuli kuhoji usimamizi wa waziri katika kitengo hicho.

Baadhi ya mawaziri waliowahi kukalia wizara hiyo ni pamoja na Nazir Karamagi, Dk. Ibrahim Msabaha, William Ngeleja na Prof. Muhongo mwenyewe, ambao wote waliondolewa kwa kashfa tofauti na George Simbachawene aliyehudumu kwa muda mfupi baada ya Muhongo kuondolewa mwishoni mwa uongozi wa serikali ya awamu ya pili kwa kashfa ya Escrow.

Nawashangaa Wanaonihusisha Mimi Binafsi na Sheria ya Makosa ya Mtandao - January Makamba

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira na Muungano, Mh. January Makamba katika mahojiano maalum na Kwanza TV ameeleza kuhusu uamuzi wake wa 'kupotea' kwenye mitandao ya kijamii mara tu baada ya Uchaguzi Mkuu, 2015.

Pia asema katika vitu vinavyomshangaza ni kuendelea kuhusishwa yeye binafsi na utungwaji Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015 (CyberCrime Act).

 Tazama Video:

DAR: Yericko Nyerere Akamatwa Akiwa Nyumbani Kwake. Wachukua Simu na Laptop

$
0
0
Watu waliojitambulisha kuwa ni Polisi kitengo cha cyber crime! Wamefika mda huu majira ya saa 7:04 usiku, Kwa Yericko Nyerere wakiambatana na mwenyekiti Wa mtaa (Mbutu), walipofika wamemchukua yeye pamoja na vifaa vyake ikiwemo simu na laptop yake na kuondoka naye kuelekea kituo cha police kigamboni wakimtuhumu kuhusika na kosa la kimtandao.(ingawa hawakueleza kosa halisi kafanya lini na wapi).

Taarifa zaidi mtaendelea kuzipata baadae.
Ikumbukwe hii ni Mara ya pili kukamatwa kwake, baada ya kesi yake iliyodumu Kwa miaka miwili tangu kipindi cha uchaguzi ambapo alishinda na kuachiwa huru mapema April 2017.



UPDATES:

Taarifa zilizonifikia hivi punde nikwamba; kituo cha kigamboni hakija mshikilia Yericko, na wala hawajui alikamatwa Kwa kosa gani; kutokana na taratibu za kazi wao kama polisi.

Wenyeji walitoa ushirikiano kutokana na jiografia ya eneo analoishi Yericko kuwa ni porini pembezoni mwa mji, kiasi kwamba Kwa gari yao (oppa) waliokuja nayo, isingekuwa rahisi kufika, Kigamboni waliombwa msaada wa gari (Defender) ili kuweza kufika eneo husika, na walipomkamata walimpekua, na baadaye kuondoka naye Kwa gari yao kuelekea makao makuu!

Kigamboni Polisi hayupo na wala hakufikishwa, walimchukua juu Kwa juu kwenye gari yao nakuondoka naye.

"Askari Wa Doria kigamboni alijaribu kuwahoji wale jamaa kutaka kujua mtuhumiwa ana kosa gani, jamaa walimjibu Kwa mkato " AMEPIGA PALEFU"

Taarifa zaidi mtajuzwa baadae! Kama kuna mtu yeyote anaweza kujitokeza Kwa mambo ya dhamana na taratibu za kisheria mnakaribishwa tukutane pale makao!
-----

New Updates..

Kwa mujibu wa Malisa G; Yericko Nyerere alipokamatwa usiku wa saa 5, alilazwa ktk kituo cha Polisi Kigamboni na asubuhi hii amehamishiwa Central(Dar) ambapo viongozi wa CHADEMA watawasili kudai maelezo ya sababu za kukamatwa kwake.


Source:Jamii Forums

A- Z ya Jinsi Harmoapa Alivyotoa Nduki Jeshini..Baba Yake Amefunguka Haya Kwa Uchungu..!!!

$
0
0

Baba mazi wa msanii Athuman Omary 'Harmorapa amefunguka na kudai kwamba mwanae huyo aligoma kujiunga na jeshi alipomaliza kidato cha nne kwa madai ya kutaka kufanya muziki licha ya kuwa tayari alikwisha tafutiwa nafasi.

Bw. Omary (baba Harmorapa) amesema hayo kupitia kipindi cha Planet bongo ya EATV na kusema alipoona mtoto wake amekataa nafasi hiyo ya jeshi hakutaka kumlazimisha bali ilibidi akubaliane naye kwani hakutaka kumkatisha kwenye kutimiza ndoto zake.

"Athuman alisoma shule kuanzia la kwanza mpaka la saba, baada ya hapo alikwenda form one mpaka four ila alipomaliza nilimtafutia nafasi ya kujiunga jeshini lakini alinikatalia, mimi kama mzazi sikutaka kumlazimisha nikasema ngoja nimuache labda ana ndoto zake. Ila nilimwambia kwenye muziki huko kunahitaji pesa na mimi pesa sina akaniambia baba usijali nitapambana na kweli nikamuacha" - baba yake Harmorapa alifunguka.

Mbali na hilo mzazi huyo amesema suala la mwanaye kuonekana na kiki yeye anaona si kibaya sababu hakuna jambo baya ambalo amelifanya, na kusema anaamini muziki ndiyo unahitaji mambo hayo ila siku akiona kuna kitu kibaya amefanya atamwita na kumweleza.

Kwa upande wake Harmorapa amesema kuwa ipo siku atakuja kumfanyia jambo kubwa baba yake huyo mzazi ambaye anaishi jijini Dar es Salaam.

Lema Ataka Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Ivunjwe..Adai Haina Kazi ya Msingi Amabyo Inakubalika na Serikali ya CCM..!!

$
0
0

MBUNGE wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbles Lema (Chadema), amelitaka Bunge kuvunja Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kutokana na maoni ya kambi hiyo kutosikilizwa.

Aidha, Lema amedai kuna kuchujwa kwa maneno yanayochangiwa na wabunge wa kambi hiyo katika mijadala katika taarifa za kumbukumbu za Bunge(hansard), alikodai kunafanywa na wafanyakazi wa Studio ya Bunge.

Aliyasema hayo bungeni mjini hapa jana asubuhi aliposimama na kuomba mwongozo wa Kiti cha Spika akidai kuwa michango ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imekuwa ikihaririwa na baadhi ya maneno yamekuwa yakiondolewa na hivyo kutorushwa kwenye studio hiyo na hata kwenye taarifa wanazopewa waandishi wa habari wa redio na televisheni.

Hata hivyo, katika mwongozo wake kuhusu suala hilo muda mfupi kabla ya kuahirisha shughuli za Bunge jana mchana, Mwenyekiti wa Bunge, Najma Murtaza Giga, aliyekuwa akiongoza kikao cha jana, alisema Studio ya Bunge haina utaratibu wa kuchuja michango ya wapinzani isipokuwa kwa maelekezo ya Kiti cha Spika.

Katika hoja yake, Lema alisema ni bora Bunge lingetoa mwongozo wa kuivunja Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na lisipokee tena maoni yoyote kutoka kwao kutokana na maoni yao kutosikilizwa.

"Mwongozo wangu Mheshimiwa Mwenyekiti kupitia Kanuni ya 68(7) cha jambo lilotokea jana (juzi) jioni, michango ya wabunge tunayochangia humu ndani ni rekodi ya wabunge kama ambayo inavyoingia katika ‘Hansard’ na ni rekodi kwa matumizi yetu binafsi," alisema.

Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani ya Nchi huyo alisema zaidi: "Lakini baadhi ya michango yetu ukifuatilia kule ambako inahifadhiwa kama kumbukumbu zetu binafsi kwa matumizi yetu, Mheshimiwa 'wana-edit' (wanahariri) kwa zaidi ya asilimia 70 na wanaweka mambo ambayo wanayataka wao.

"Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimechangia Wizara ya Mambo ya Nje na (Ushirikiano wa) Afrika Mashariki, nikaenda nikaambiwa nijaze fomu, nimejaza kutaka kumbukumbu ya mchango wangu, mchango ambao haukuwa hata na mwongozo, haukuwa na taarifa wala utaratibu (bungeni).

"Nimekwenda mambo yote yanayohusu mambo ya Acacia na Diplomasia ya Uchumi yametolewa, wamenibakizia pale panaposema tu kupinga na mtu yoyote anayepinga rasilimali ni mwendawazimu na kipande hicho ndiyo kinazungushwa.

"Sasa Mheshimiwa Mwenyekiti, michango yetu hapa bungeni ni kumbukumbu zetu na hili Bunge Mheshimiwa Mwenyekiti, limeondolewa kuwa 'live' (matangazo ya moja kwa moja) na uhuru wake umeminywa halafu michango yetu ambayo ni halali tukiifuatilia kwa kumbukumbu zetu 'mna-edit'.

"Sasa Mheshimiwa Mwenyekiti, ni bora Bunge hili likatoa mwongozo wa kuvunja Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na msipokee maono yoyote kutoka kwetu."

Awali akijibu mwongozo huo asubuhi, Giga alisema angefuatilia kama madai ya Lema yana ukweli au la na baadaye kutoa majibu bungeni.

"Ni kwamba michango ambayo tunachangia kwa maandishi tunaletewa kwanza hapa kwa ajili ya kuweza kurekebisha lakini kama ni ‘clip’, basi hili suala itabidi nilifuatilie kwa sababu sina uhakika nalo kama ni kweli au siyo kweli, baadaye tutaweza kuleta majibu yangu. Huo ndiyo mwongozo wangu," alisema Giga.

Ndipo kabla ya kuahirisha shughuli za Bunge mchana, Mwenyekiti wa Bunge huyo alisema amefuatilia na kupata maelekezo kwamba studio ya chombo hicho cha kutunga sheria na Ofisi ya Bunge kwa ujumla hawana utaratibu wa kuchuja michango ya wabunge isipokuwa tu kwa maelekezo ya Kiti cha Spika yanayotolewa bungeni.

Alisema taarifa zinazokuwa kwenye 'hansard' zinapaswa kuwiana na 'clip' za mchango wa mbunge husika.

"Kilichotokea kwa mchango wa Mheshimiwa Lema ni kosa la kiufundi na linafanyiwa kazi na likitatuliwa, anaweza kuomba na kupewa mchango wake wote," alisema.

Giga aliongeza kuwa mbunge yeyote atayekumbana na changamoto kama iliyompata Lema, awasilishe malalamiko yake kwenye Ofisi ya Katibu wa Bunge.

Imefichukaaa..Hii Hapa Sababu Kubwa Nyuma ya Pazia ka Nini Diamond Hakuhudhuria Mazishi ya Ivan Jana..!!!!

$
0
0

Baada ya Diamond Platnumz kutangaza kwamba angehudhuria mazishi ya aliyekuwa mume wa Zari, Ivan Ssemwanga, ameshindwa kuhudhuria mazishi hayo yanayofanyika jioni hii katika makaburi ya ukoo wa marehemu yaliyoko Kayunga, nchini Uganda.

Muimbaji huyo  weekend hii alishambuliwa na mashabiki wake katika mitandao ya kijamii kutokana na kitendo chake cha kufanya show nchini Kenya licha ya mama watoto wake, Zari kufiwa na mume wake huyo wa zamani.

Meneja wa msanii huyo, Sallam amedai Diamond ameshindwa kuhudhuria mazishi hayo kutokana na ratiba kuingiliana.

“Kwenye mazishi hatujahudhuria, ilikuwa twende leo alfajiri lakini sasa kumbe wao wametoka usiku kwenda kijijini. Kwa hiyo nadhani ratiba yetu imeingiliana maana na sisi tulitoka Nairobi jana jioni.” Sallam alikiambia kipindi cha U-heard cha Clouds FM.

Pia Sallam amekanusha taarifa za kwenye mitandao ya kijamii kwamba wameshindwa kuhudhuria mazishi hayo baada ya kuzuiwa airport kuingia nchini Uganga kutoka na ishu za usalama.

Alisema wao walitaka kuhudhuria mazishi hayo kwaajili ya mkupatia pole Zari  kwa kuwa huyo ndiye  mtu wao.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images