Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Breaking: Mzee Philemon Ndesamburo wa CHADEMA Afariki Dunia

$
0
0
#TANZIA Aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini na Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoani Kilimanjaro, Philemon Ndesamburo 'Ndesa Pesa' amefariki dunia.
#RIP Mzee Ndesamburo


Godbless Lema Afunguka 'Yeriko Nyerere Amekamatwa au Ametekwa?'

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema) Godbless Lema ameuliza swali je, Yeriko Nyerere amekamatwa au ametekwa?

Lema ameuliza swali hilo katika ukurasa  wake wa Twitter leo na kuongeza: “Msiogope. Lakini kwa kadiri ya walivyowatesa ndivyo walivyoongezeka na kuzidi kuenea. "

Yeriko anayefahamika kuwa ni kada wa Chadema, amekamatwa leo saa tisa alfajiri na watu wanaodhaniwa kuwa ni polisi akiwa nyumbani kwake, Kigamboni, Mbutu.

Meya wa Ubungo, Boniphace Jacob amethibitisha kukamatwa kwa Yeriko.
Yerico amekamatwa au ametekwa ? MSIOGOPE. Kwani imeandikwa "Lakini kwa kadiri ya walivyowatesa ndivyo walivyoongezeka na kuzidi kuenea "
— Godbless E.J. Lema (@godbless_lema) May 31, 2017

Steve Nyerere Afyata Mkia...Ajisogeza Kwa Mama Wema Sepetu Baada ya Kutofautiana

$
0
0
Muigizaji mkongwe wa Filamu Tanzania Steve Nyerere kati ya mambo aliyozungumza ni kuhusu kuyaweka pembeni mambo yote yaliyotokea baina yake na Mama yake Wema Sepetu.

Steve Nyerere amesema katika kipindi hiki cha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ameamua kusamehe na kusahau kila kilichotokea baina yao na lazima waanze upya kwa sababu hata Vitabu vya Dini vinaeleza.

"Lazima tusamehe ili kuanza mwanzo. Kwa hiyo, mimi nasema kwanza vile vitu vilipita – yaliyopita si ndwele tugange yajayo. Yule ni Mama – ni Mama yangu, ni rafiki yangu, ni ndugu yangu, ni mwanafamilia. Yaliyopita si ndwele tugange yajayo.
 “Mzazi haombi samahani; mzazi hakosei. Mzazi anapatia lakini mwenyewe ndani ya nafsi yake anasema pale nilimkwaza mwanangu au pale nilimkosea mwanangu. Naamini ndani ya nafsi yake anasema hapa nilimkwaza mwanangu au hapa nilimkosea mwanangu.” – Steve Nyerere.
.
.
TOA MAONI YAKO HAPA

Mzee Yusuph Agonga Mwamba Kuifuta Bendi ya Jahazi Modern Taarab....Aambiwa Ajifute Yeye ila si Bendi

$
0
0
Baada ya kuacha kufanya muziki, Mzee Yusuf alitaka kuifuta kabisa Jahazi Modern Taarab, lakini Baraza la Sanaa la Taifa, BASATA lilimzuia.

Amesema kwa mujibu wa sheria za serikali, haiwezekani tu kuifuta bendi kwakuwa inaweza kuendelezwa na watu waliosalia.
“Nilikusudia niivunje Jahazi kama ninavyovunja nyumba,” Mzee Yusuf alikiambia kipindi cha Hatua Tatu cha Times FM. “Lakini sheria za nchi hakuna utaratibu huo, wewe ondoka na ujiachishe kila kitu.”

Aliongeza kuwa kwa sasa hajui chochote kinachooendelea kwenye bendi hiyo na wala hataki kujua. Hata hivyo alikiri kuwa tangu ameacha muziki ameyumba kiuchumi japo hajutii na moyo wake una amani.

VIDEO: IGP Sirro Akitangaza Dau la Milioni 120 Ukiwakamatisha Hawa

$
0
0
MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro kwa mara ya kwanza amefanya mazungumzo maalum na wanahabari jijini Dar es Salaam na kutangaza dau nono la Sh10 milioni kwa atakayetoa taarifa kuhusu mauaji ya Kibiti, Rufiji na Mkuranga.

“Niwaambie ukweli kuwa katika hili, maneno yatakuwa machache lakini vitendo vitakuwa vingi zaidi,” amesema katika mkutano huo.

Pia IGP Sirro amewatangazia kiama madereva wa bodaboda na kuwataka kuacha kuvunja sheria za barabarani kwa makusudi.

“Huu ni wakati wa kutii utawala wa sheria bila shuruti na nimeshaongea na makamanda wa polisi nchi nzima,” amesema

Msikilize hapo chini akiongea

Ukweli Mchungu...Tanzania ya Viwanda Hamuiwezi - Lema

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini (CHADEMA) Mhe. Godbless Lema amefunguka na kusema serikali ya awamu ya tano haiwezi kuibadili Tanzania na kuwa nchi ya viwanda kwa sababu fedha zilizopelekwa katika sekta hiyo ni ndogo.


Godbless Lema akizungumza bungeni alisema viwanda ndiyo imekuwa ajenda kubwa ya serikali ya awamu ya tano lakini kiwango cha fedha zilizopelekwa ni kidogo sana hivyo anaona hakiwezi kufanya mabadiliko na kuleta viwanda nchini.

"Serikali imekuwa ikipigia sana kelele kuhusu suala la viwanda lakini katika bajeti inayoishia kati ya bilioni 42.1 serikali ilipeleka bilioni 7.6 asilimia 18 tu ndiyo maana Mh Mwijage anavyosema cherehani nne ni viwanda halafu watu wakimshangaa mimi nawashangaa hao wanaomshangaa, ni ukweli viwanda vya serikali ya awamu ya tano ni cherehani nne. Mh. Mwenyekiti hii ndiyo ajenga kubwa ya serikali ya wamu ya tano viwanda kati ya bilioni 42 mnapeleka bilioni 7 hamtaweza kuibadili hii nchi kwenda kuwa taifa la viwanda" alisema Lema 

Mbali na hilo Mbunge huyo aligusia pia suala la maji na kusema maji ni hitaji muhimu kwa kila binadamu hivyo serikali ingeweza kuona hiyo fursa na kutengeneza miundombinu mizuri ili ijipatie pesa kupitia maji.

"Maji ni biashara Mh. Mwenyekiti najiuliza kwanini nchii hii haijawahi kuona maji ni biashara, tena maji ni biashara ambayo haihitaji matangazo sababu kila mtu anahitaji maji mahitaji namba moja ya binadamu anayeishi ni maji, mmeshindwa kutengeneza mipira, mmeshindwa kutengeneza miundombinu mizuri na kuweka mita ili serikali iweze kukusanya fedha kutoka kwenye maji, kama hatujaweza kuona kuwa maji ni biashara cherehani nne lazima zitakuwa ni viwanda" alisisitiza Lema 

Zitto Kabwe Amefunguka Haya Mazito Kufuatia Kifo cha Mzee Ndesamburo..!!!

$
0
0

Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Kabwe ametoa ya moyoni kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa zamani wa Moshi mjini kupitia tiketi ya Chadema, mzee Philemon Ndesamburo ambapo pia ametuma salamu za rambirambi kwa mtoto wa mzee huyo.

Mhe. Zitto ametoa salamu hizo leo kwenye ukurasa wake wa faceebook ambapo ameeleza alivyomtambua mzee Ndesamburo.

Salaam zangu za rambirambi Kwa dada yangu mpenzi Lucy Owenya Kwa kupotelewa na baba mzazi Mzee Philemon Kiwelu Ndesamburo. Ni msiba mkubwa Kwa watu wa Kilimanjaro na hasa Moshi Mjini ambapo Mzee Ndesa Pesa alikuwa mwakilishi wake Bungeni kuanzia Mwaka 2000 mpaka Mwaka 2015. Kilimanjaro imepoteza mtu ambaye aliweka maslahi ya mkoa wake mbele kuliko kitu kingine chochote.
Ni msiba mkubwa Kwa wanachama wa CHADEMA ambacho alikuwa Mwenyekiti wake Wa Mkoa tangu Chama kimeanzishwa mpaka mauti yalipomkuta. Huwezi kutaja maendeleo ya CHADEMA kwa nchi yetu bila ya kutaja jina la Mzee Ndesamburo. Nimepata bahati ya kufanya naye kazi Kwa karibu, naweza kutamka bila wasiwasi kwamba ni mmoja wa watu waliokipenda Chama chake Kwa dhati Kabisa.
Ni msiba mkubwa Kwa Watanzania. Mzee Ndesamburo alitumia uwezo wake Wa kifedha na kiakili kuimarisha mfumo wa Vyama vingi nchini kwetu. Mchango wake katika kupigania Demokrasia nchini ni wa kupigiwa mfano na Kwa Kweli wengi wetu Leo tunafaidi matunda ya Vyama vingi Kwa sababu ya kazi kubwa ambayo Mzee Ndesamburo na wenzake walio hai na waliotangulia mbele ya haki walifanya.
Mzee Ndesamburo amechangia Sana ukuaji wa sekta ya utalii nchini. Kupitia kampuni zake za Keys Hotels ameweza kuchangia Sana ukuaji wa sekta ya Utalii nchini kwetu. Bungeni alikuwa mstari wa mbele kutaka uhifadhi wa mlima Kilimanjaro kutokana na tishio la theluji kuondoka katika uhai wetu ( in our life time). Kwa hakika Vyuo Vikuu vyetu vya Umma vingekuwa vinatenda haki Mzee Huyu angepewa Shahada ya Uzamivu ya Heshima Kwa mchango wake katika Maendeleo ya sekta ya Utalii nchini kwetu.
Nawapa pole Sana watoto, wajukuu na vitukuu vya Mzee Ndesamburo. Mzee wetu aliishi maisha yake na ameacha ‘ legacy ‘ yake. Najua maumivu yenu lakini tupo wengi tunaoumia nanyi. Mungu awavushe kwenye mtihani huu mkubwa. Muwe wamoja na mshikamane.
Poleni Sana ndugu zangu wa CHADEMA Kwa kupotelewa na Kiongozi wenu na Kiongozi wetu pia.
Poleni Sana wana Moshi Mjini na wana Kilimanjaro wote. Poleni Sana Watanzania.
Pumzika Kwa Amani Philemon Kiwelu Ndesamburo. Hiyo ni njia yetu sote. Amina

JE Una Tatizo la Maumbile Madogo, Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo?

$
0
0

JE, UNA TATIZO LA MAUMBILE MADOGO, NGUVU ZA KIUME NA KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA?
Maumbile madogo ya uume, kupungukiwa nguvu za kiume pamoja na kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa wanaume limekuwa likiwaathiri wanaume wengi kutokana na sababu mbali mbali na kusababisha kushindwa kujiamini ktk mapenzi. Tatizo hili limesababisha kuvurugika kwa ndoa nyingi na mahusiano.
@Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo yakiwemo:-
1.Uume kulegea wakati wa tendo
2.Kukosa hamu ya tendo la ndoa
3.Kuwahi kufika kileleni
4.Uume kuchelewa kusimama baada ya round ya kwanza.
5.Kuchoka sana baada ya round moja n.k.
🍉🌿🍎🍍🍒🍓🍀🍅🍅
PATA BIDHAA HIZI ZILIZOTENGENEZWA KWA MIMEA NA MATUNDA ZISIZO NA KEMIKALI WALA MADHARA. ZIMETHIBITISHWA KIAFYA.
👇👇👇👇👇👇👇
1.HANDSOME UP ni kifaa chenye uwezo wa 99 % kuongeza uume (size unayohitaji) na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo hata mara 3 @130,000/=
Kwa Bidhaa hizi na nyingine kama:-
5.Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi @130,000/=
7.Kutengeneza shepu (hips, makalio na mapaja) @200,000/=
8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni @120,000/=
9.Kuwa mweupe na soft mwili mzima bila kuacha sugu 120,000/=
10.Kurudisha usichana (bikra) @120,000/=
Wasiliana nasi kwa (+255)
0767447444 au 0714335378.
NB: Matokeo ni uhakika na garantii na upate risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii.
Follow us
@Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr

Mwijage ‘amzima’ Kubenea bungeni

$
0
0

Dar es Salaam. Waziri Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage amezima hoja mbunge Ubungo, Said Kubene ambaye alitaka Serikali kutatua matatizo yanayovikabili baadhi ya viwanda.

Kabla ya Mwijage kumjibu, Kubenea alisema kuwa kuna baadhi ya viwanda nchini kikiwemo cha Urafiki na EPZ ambavyo vimekuwa na matatizo, hivyo alitaka kujua ni lini Serikali itatatua matatuzo yaliyopo kwenye viwanda hivyo.

“…Mwenye shiba hamjui mwenye njaa,”amesema Mwijage na kuongeza;

“Urafiki na EPZ vinatoa ajira kwa vijana wengi licha ya changamoto kadhaa zinazowakabili. Lakini kama kuna aliye mbaya mlete kwangu.”

Hawa ndio Nyota 10 waliotemwa Simba SC

$
0
0

KLABU ya Simba imepanga kuwabakiza wachezaji 15 pekee kati ya 25 iliowasajili msimu uliopita wa Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho (FA). Timu hiyo, inataka kukiimarisha kikosi chake kwa ajili ya kujiandaa na michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika watakayoshiriki mwakani.

Wakati wakipanga kuwaacha wachezaji hao, tayari nyota wao muhimu wameshaanza kuaga akiwemo Abdi Banda ambaye mkataba wake umemalizika, wengine ni Jonas Mkude na Ibrahim Ajibu ambao nao wamemaliza mikataba.

Akizungumza na Championi Jumatano, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, alisema bado hawajapokea rasmi ripoti ya Kocha Mkuu wa timu hiyo, Mcameroon, Joseph Omog lakini tayari Kamati ya Utendaji ilikutana kufanya tathmini ya kikosi chao kwa ajili ya usajili.


Hans Poppe alisema wameona wachezaji 10 ambao hawana mchango na kupanga kuwaondoa katika kikosi hicho ambao wapo watakaotolewa kwa mkopo kwa ajili ya kukuza viwango vyao. “Msimu huu tulikuwa na kikosi kipana kilicholeta ushindani na kufanikisha malengo yetu lakini licha ya kuukosa ubingwa, kuna kitu tumeonyesha na kufanikiwa kupata Kombe la FA.

“Katika kuhakikisha msimu ujao wa ligi na mashindano ya kimataifa tunakuwa bora zaidi, tumepanga kuwaacha wachezaji 10 kati ya hawa 25 tuliokuwa nao msimu huu.

“Wakati tukiwaacha hao, tumepanga kuongeza idadi ya wachezaji 10 kati yao tunataka wenye uwezo wa kucheza mashindano ya kimataifa, kama unavyojua mwakani tutaiwakilisha nchi kwenye Kombe la Shirikisho Afrika, hivyo ni lazima tuwe na kikosi imara,” alisema.

Nimeambukiza Ukimwi Maelfu ya Wanaume Jijini Dar.....

$
0
0


Mimi ni Jane naishi mwenge Dar es salaam naomba utalifuta jina la baba yangu maana sitaki liwe kwenye blog watu watanijua na kuniangamiza maana nimeshawaangamiza wengi sana kwa UKIMWI ila mengine yote usifute hata moja ili dunia ijue tu japokua mimi nitakufa kwa huu ukimwi nilionao.

Nilizaliwa mkoa wa Dodoma na nilishi vizuri tu tangu utotoni na hata sikujihusisha na ngono hadi nilipomaliza form 4 mwaka 2006 baada ya kumaliza nilikuja hapa Dar kuishi kwa mama mdogo aliyeolewa hapa Mwenge.

Nilipata marafiki wengi tu na kuna kijana mmoja alinitongoza kwa muda mrefu sana na siunajua vijana wengi hutumia muda mrefu kutongoza ili msichana unadhani kwamba labda huyo anakupenda kumbe anataka tu ngono na wadada wengi sana hudhani kufuatiliwa kwa muda mrefu na mvulana basi huyo yuko serious kumbe hakuna lolote.

Nilimkubalia tukawa wapenzi ila nilikataa kuhusu kufanya mapenzi maana anayekupenda kiukweli sio uongo lazima asitake ngono kabla ya ndoa.

Kwa miezi kama 5 hadi 6 aliniambia kuhusu kufanya mapenzi nilikataa alitumia mbinu nyingi sana kwa kunibembeleza na hata kulia mbele yangu ili tufanye tu mara moja ila nilikataa, alisema atavumilia hadi siku ya ndoa yetu ambapo tulipanga kuoana mwaka sept 2009.

Siku moja aliniambia twende kwenye kumbi za starehe na mimi kwa sababu ya upagani na kumwamini pia kwa sababu nampenda nilikubali tulienda huko na kulikua na bendi fulani maarufu ya mziki wa dansi ilikua inatumbuiza.

Tulitafuta sehemu na kukaa na mpenzi wangu akaagiza pombe alianza kunywa huku akinionjesha, nilikataa kwa sababu nilikua sijawahi kunywa pombe katika maisha yangu yote, hata sijui alinishawishi vipi nilijikuta nakunywa kidogo kidogo na kwa kuwa tulikaa pale kwa muda zaidi ya masaa 5 nadhani nikunywa kama bia 3 au 4 japokua nilikua nakunywa kidogo kidogo tu tena kwa kunywesha na mpenzi wangu maana nikama nikua nanyweshwa kila baada kama ya dakika 25 ndipo nakunywa mara moja na sikujuia kama nakunywa pombe ila niliihisi tu naonja ili kumlizisha mpenzi wangu.

Ilipofika saa 10 alfajiri nilihisi usingizi na pia nilijiona wa tofauti najua nililewa hata kama sikujua kama nimelewa maana nakumbuka tulitoka pale huku amenishika mkono huyo mpenzi wangu. Tulikodo tax na kuondoka na siku hiyo aliniambia twende kwake alikokua amepanga chumba maana tulikua na usingizi sana nilikubali huku nikidhani hatuwezi kufanya mapenzi.

Tulifika salama na kuingia ndani ukweli pombe ni kichocheo cha ngono na ningekua mimi ndio Raisi wa Tanzania ningefunga bar zote. Nilijikuta natamani kufanya mapenzi na huyu mpenzi wangu hata alikua hana nia maana alijua atanichukiza sana na uhusiano ungekufa siku hiyo lakini kwa sababu ya pombe nilimwambia siku hiyo tufanye kidogo maana mwili wangu unataka.

Ni kweli siku hiyo kwa sababu ya pombe nilifanya mapenzi na huyo mpenzi wangu na baadae akanipeleka nyumbani baada ya wiki mbili maana tulikaa wiki mbili bila kuonana alikuja na kunieleza habari ambayo sikuihitaji katika maisha yangu maana nilikua nasikia tu kwa watu wengine lakini sio kwangu alisema ”JANE ISHI KWA MATUMAINI KUANZIA SASA”

Nilidhani utani lakini aliniambia kuwa yeye ana UKIMWI tangu miaka mitano iliyopita na anapenda tu ngono maana hawezi kuacha.

Nililia sana na baada ya wiki moja baadae nikaenda kupima na kukutwa nina ugojwa ambao niliusikia tu kwa watu na chanzo cha yote ni pombe, kupenda starehe,disko na upagani unaotusumbua wanadamu wengi.

Nilikua na UKIMWI na kwa hasira maana mpenzi wangu alihamia Arusha huku akisema neno moja la mwisho kwamba ”shetani amemtuma kuwaambukiza wanadamu UKIMWI”

Sikujua, sikujua, sikujua, sikujuaaaaaaaaa, basi tu ooh YESU nihurumie mimi leo.Nilibebeshwa mzigo ambao haukunistahili mimi. Hata leo hua najiuliza kwamba nilijitunza kwa miaka 23 yote lakini pombe na huyu wakala wa shetani wamenifanyia hivi. Baada ya kujua nina UKIMWI na hali hiyo nikaikubali na kulikua na kundi kubwa sana la wanaume ambao walikua wamewahi kunitongoja na niliwakataa sana kwa sababu hii niliwakubali ili nami nife na wengi.

Nilianza kumkubali kila mmoja na kuna baba mmoja ambaye ana wake 3 niliwahi kumtukana sana kipindi cha nyuma kila aliponitongoza lakini wakati huu nilimkubali na hakuamini na tukafanya ngono tena bila kinga na akaniaachia pesa laki 6 kama zawadi ya kumkubali kumbe naye hakujua kuwa namwambukiza na hata leo hua nawahurumia tu wale wake zake ambao wana UKIMWI uliotoka kwangu.

Kiukweli tangu may 2009 hadi 2012 nimeshatembea na wanaume zaidi 1500 maana ilifika kipindi nala na wanaume 3 kwa siku na lengo langu niwakomeshe kama mimi nilivyokomeshwa na nina uhakika kutokana na mimi wameambukizwa UKIMWI wanadamu zaidi ya 10,000 na hili tangazo la ”TUKO WANGAPI” huwa linaniliza kila siku maana hata mimi najua kabisa nilianzisha mtandao kama huo wa ngono kwa idadi kubwa sana ya watu.

Nimeokoka miezi 7 iliyopita na siku naombewa nilikutwa na mapepo mengi sana na hata waombeaji wakashangaa. Ningejua ningeokoka tangu nikiwa na miaka 5 lakini ndio hivyo sina jinsi wala uwezo wa kubadirisha hali hiyo.

Na naomba kila atakayesoma ujumbe huu ajue kuanzia leo kuwa pombe ni dhambi pia kwenda disko ni dhambi,kuuza pombe ni dhambi na kila kichochoe chochote cha dhambi ni dhambi. Hadi sasa mtu yeyote hawezi kujua kama nina UKIMWI na sijui MUNGU ana mpango gani na mimi maana kwake yote yanawezekana. Nauamini uponyaji wake na sijawahi kutumia ARV hata siku moja na afya yangu iko sawa tu na huwezi hata wewe kujua kama uovu huu nimefanya mimi.

Ndugu zangu kama una UKIMWI nenda kanisani ukaombewe na kama una akili mpe YESU maisha yako maana pia baada ya kifo ni hukumu. Yasalimishe maisha yako kwa YESU na usiambukize wengine tena.

Mimi tangu niokoke sijawahi kufanya mapenzi tena na sitafanya hivyo wala sitaolewa na mtu yeyote maana yatosha kwa uovu niliofanya na hadi sasa wapo ninaowajua zaidi ya 15 wameshafariki na nilihudhulia misibani huku nikijua kabisa chanzo ni mimi.

Mwisho nawashauli wababa kulidhika na wake zao na wamama pia lidhikeni na waume zenu, vijana ambao hamjaoa wala kuolewa subiri hadi utakapooa au kuolewa na kabla ya kuolewa au kuoa kapimeni kwanza kwani wenye UKIMWI ni wengi kuliko unavyozani.

Fuata unachofundishwa kanisani na pia soma BIBLIA na uwe mtakatifu.

Alichokisema Lowassa Baada ya Kifo cha Mzee Ndesamburo..!!!

$
0
0

Mjumbe wa Kamati ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa ameeleza kusikitishwa na kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo (Chadema) na kueleza kuwa alikua shujaa wa mabadiliko.

Ndesamburo aliyekuwa Mbunge kuanzia mwaka 2000 hadi 2015 amefariki dunia ghafla leo hii wakati akipata matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC, Moshi mkoani Kilimanjaro.

Lowassa kupitia ukurasa wake wa mtandao wa twitter ametweet, “Nimesikitishwa sana na kifo cha ghafla cha Mzee Ndesamburo, Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi natoa pole kwa familia na wote. Mzee Ndesamburo alikua shujaa wa kweli wa mabadiliko wa miaka mingi na mwenye mchango mkubwa kwenye siasa za demokrasia katika Taifa letu.

Rais Magufuli Naye Ametoa ya Moyoni Kuhusu Kifo cha Ndesamburo...!!!

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameeleza kusikitishwa na taarifa za kifo cha Mbunge mstaafu wa Jimbo la Moshi mjini Mzee Philemon Ndesamburo kilichotokea asubuhi ya leo.

Katika salamu za rambirambi alizozitoa Rais Magufuli kwenda kwa wafiwa pamoja na viongozi na wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) amesema amepokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa.

“Kwa masikitiko nimepokea taarifa za kifo cha Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Moshi Mjini, Mzee wangu Philemon Ndesamburo kilichotokea leo tarehe 31 Mei, 2017 katika hospitali ya rufaa ya KCMC iliyoko Moshi Mkoani Kilimanjaro. Namkumbuka Mzee Ndesamburo kwa hekima zake na uongozi wake uliozingatia siasa za kistaarabu” alisema Rais Magufuli

Aidha, Rais Magufuli amesema alifanya kazi na marehemu Philemon Ndesamburo wakati wote wakiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wakati wote walishirikiana, kutaniana huku akimkumbuka kwa namna ambavyo alitumia muda wake bungeni kupigania mambo yenye maslahi kwa wananchi wa jimbo lake la Moshi Mjini.

Pamoja na hayo, Dkt. Magufuli ameitaka familia ya marehemu Philemon Ndesamburo na wote waliguswa na msiba huo kuwa na moyo wa subira, uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu walichonacho.

Kwa upande mwingine Rais Mgufuli amemuombea dua marehemu apumzishwe mahali pepa peponi

PICHA: Kwa mara ya kwanza Rayvanny amempost mtoto wake na Ujumbe mzito

$
0
0

Mwimbaji staa wa Bongofleva kutoka WCB Rayvanny leo May 31, 2017 kupitia account yake ya Instagram kwa mara ya kwanza amepost picha ya mtoto wake Jaydan ikiwa ni kumtambulisha kwa mashabiki wake.


Rayvanny aliandika kwenye picha hiyo:

“Mungu Akukukuze Mwanangu, Katika Mema na Mafanikio Katika Maisha Yako.Wewe Nifuraha Yangu Na pia Wewe Ndio sababu Ya Mimi kumwaga Jasho Nakufanya Kazi kwa Bidii Kila Siku. Ni bora Nikose Vyote Lakini Sio Wewe Mwanangu. I LOVE YOU SON” – Rayvanny

IGP Sirro Atangaza Vita Pwani..Adai Ubaya Wataulipa kwa Ubaya..!!!

$
0
0

IGP Simon Sirro amewaonya wahalifu wanaojishughulisha na mauaji mkoani Pwani kuacha mara moja kwani ndani ya muda mfupi ataenda kuwafichua kwa kutumia vyombo vyake vya dola ili kulinda amani ambayo imepotezwa na kikundi cha watu wachache.

IGP Siro ametoa onyo hilo wakati akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es salaam na kusema kuwa haki lazima iende kutoa majibu ya watu wanaofanya mauaji maeneo ya  kibiti, mkuranga, Ikwiriri kwa ndani ya muda mfupi huku akiongeza hakuna sababu ya watu wema kufanyiwa ubaya na kama jeshi ni wajibu kuilinda amani.

"Hakuna haja ya watu kufanya ukatili na ubaya kwa watu wasiostahili. Sisi tutawajibu ubaya wanaofanya ubaya. Watanzania pamoja na vuiongozi wangu wanataka maji ya nani anayefanya haya mauaji, lakini tayari tumeshapata kujua ni kikundi cha watu wachache niwahakikishie mimi pamoja na vyombo vya dola tutawapatia majibu ndani ya muda mfupi"- IGP Sirro aliwaambia wanahabari.

Pamoja na hayo katika mkutano huo na wanahabari IGP Sirro amewataka wafanyabiashara wa dawa za kulevya kuachana na biashara hiyo haramu kwani hailipi kama jinsi wanavyofikiria na badala yake itawahamisha uraiani na kuwatenga na familia zao kutokana na jinsi watakavyo shughulikiwa na sheria za nchi.

Sambamba na hayo Sirro ametumia nafasi hiyo kuwaasa wananchi kuacha kujichukulia sheria mikononi kwa makosa madogo madogo yanayojitokeza mitaani na kwamba ni kinyume cha sheria za nchi nawote wanaofanya hivyo ameahidi kuwashughulikia kwa sheria.

"Kila mtu atahukumiwa kwa mujibu wa sheria za nchi. Kuna wale watu wanajidai kwamba wanahasira kali hadi kufikia kumuua mtu aliyeiba kuku, niwaambie tu kuku hana thamani ya mwanadamu na hao wenye hasira kali nitaenda nao sambamba kwa sababu imefika hatua eti vifo vya silaha ni vichache kuliko vya hasira kali" - aliongeza IGP Sirro

Hivi Ndivyo JPM Alivyotumia Siku 572 Kutea na Kutengua Watu Mbalimbali Kwenye Serikali Yake..!!!

$
0
0

Wakati akitimiza takriban siku 572 akiwa Ikulu, Rais John Magufuli anaonekana bado hajapata timu sahihi inayoendana na falsafa yake ya utendaji kazi, akiendelea kupanga na kupangua viongozi na watendaji wa Serikali.

Kitendo cha kutengua uteuzi wa Profesa Sospeter Muhongo, mtu ambaye alitumia maneno mazuri mbele ya wananchi kuwaonyesha kuwa waziri huyo wa zamani wa Nishati na Madini ni mchapakazi na kumtaka ajitahmini, ni kati ya viashiria kuwa bado JPM anasaka timu sahihi.

Pia Rais alivunja bodi ya Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA), kumsimamisha mkurugenzi mkuu na kutaka wafanyakazi wa TMAA na wizara wachunguzwe, kinaonyesha bado Magufuli anaendelea kujenda timu ya “kuchapa kazi tu”.

Mbali na hilo, mkuu huyo wa nchi amekuwa na mtindo wa kuwapa watendaji nafasi za kukaimu, kama alivyofanya kwa Profesa Ibrahim Hamisi Juma, ambaye anakaimu nafasi ya Jaji Mkuu, jambo lililoibua mijadala.

Tayari Rais Magufuli ameshaacha mawaziri watatu tangu alipounda baraza lake mapema mwaka jana, wawili akiwa ametengua uteuzi wao na mmoja kumuacha katika mabadiliko madogo.

Uteuzi wa Charles Kitwanga, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Muhongo ulitenguliwa kwa makosa tofauti, wakati Nape Nnauye aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo aliachwa katika mabadiliko hayo madogo.

Pia, ameshabadilisha mawaziri kutoka wizara moja hadi nyingine katika kipindi kisichozidi miaka miwili tangu aapishwe Novemba 5 mwaka juzi.

Kwenye panga pangua hiyo ya watendaji, Rais Magufuli ameonekana ni mwiba mkali hadi kufikia hatua ya kuwaengua marafiki zake wa karibu aliowateua kushika nyadhifa mbalimbali ikiwamo uwaziri.

Tukio ambalo halikutegemewa ni la kutengua uteuzi wa Ernest Mangu, aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) na kumteua Simon Sirro kushika nafasi hiyo, akiahidi kumpangia kazi nyingine Mangu.

Hakuna sababu zilizotolewa za mabadiliko hayo, hivyo kuacha fursa ya ubashiri kuwa huenda kulitokana na kutosimamia vyema vitendo vya mauaji ya viongozi na askari wa Jeshi la Polisi katika wilaya tatu za mkoani Pwani.

“Ili kuongoza unatakiwa kuwa na watu au wasaidizi wenye maono sawa na wewe,” alisema mhadhiri wa Idara ya Sayansi Asilia ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Frank Tily.

“Baada ya kuingia madarakani Rais alichagua baadhi ya watendaji akiamini kuwa watamsaidia, lakini mwisho wa siku wanaonekana wapo tofauti na maono ya mkuu.”

Alisema kwa mamlaka aliyokuwa nayo, Rais ana haki ya kutengua na kuteua mtendaji anayeona anafaa na kuhakikisha malengo yao yanafanana ili kuwatumikia vyema Watanzania.

“Anaisuka Serikali iwe safi, ili afikie malengo yake. Mwanzo wakati wa kuingia madarakani hakuwajua vizuri baadhi ya watendaji,” alisema Dk Tily.

Maoni kama hayo yalitolewa na mhadhiri mstaafu wa UDSM, Dk Ahmed Kiwanuka aliyesema Rais Magufuli ana nia njema na Taifa hili, pia ana wajibu wa kisheria na madaraka ya kuwapima watendaji kwa kutumia vigezo vyake.

“Ni wajibu wake kutekeleza majukumu haya. Ukiwa nje huwezi kujua ugumu anaoupata wakati wa kutekeleza majukumu yake,” alisema Dk Kiwanuka.

Alisema kufanikiwa kwa Rais Magufuli ni mafanikio ya Taifa na Watanzania kwa ujumla hivyo aungwe mkono katika jitihada zake za kuleta maendeleo.

Naye mhadhiri wa Idara ya Siasa, Sayansi na Utawala ya Chuo Kikuu Huria (OUT), Hamad Salim alisema kiongozi hawezi kufanya peke yake, bali huwa na timu na pale anapoona kuna kinachomkwamisha, anaweza kufanya mabadiliko.

“Serikali siyo klabu ya karata au watu kucheza bao kwa hiyo hata rafiki kama hafanyi kazi vizuri, unaweza kumuondoa,” alisema.

Alisema mwaka 2020 ni wa uchaguzi na wananchi watamuuliza kama alitimiza malengo yake alipokuwa madarakani.

Mhadhiri huyo alisema, hata hivyo, kuwa panga pangua hiyo ina athari zake kwa kuwa kiongozi hakai muda mrefu sehemu moja na hivyo anashindwa kujifunza au kupanga mipango yake ya maendeleo.

Tangu aingie madarakani, Rais Magufuli ameonyesha kutostahimili viongozi wanaokwenda kinyume na sera zake, akiwatimua baadhi kwa kutofuata maagizo yake, kutowajibika ipasavyo katika masuala muhimu kama ukwepaji kodi bandarini, kukiuka maadili na kutuhumiwa kwa ufisadi.

Panga pangua hiyo iliondoa hadi watu aliowatangaza hadharani kuwa marafiki zake, kama Kitwanga, mbunge wa Misungwi (CCM) aliyetenguliwa kwa kuingia bungeni akiwa amelewa.

Kabla ya kutenguliwa, Kitwanga alikuwa akizongwa na wabunge kumtaka ajiuzulu akituhumiwa kuwa na hisa katika kampuni iliyohusika katika mkataba wa Lugumi Enterprises na Jeshi la Polisi ambao haukutekelezwa ipasavyo.

Nafasi ya Kitwanga ilichukuliwa na Mwigulu Nchemba aliyekuwa Waziri wa Kilimo na Uvuvi, kisha Rais Magufuli alimteua Dk Charles Tizeba kuziba nafasi ya Nchemba.

Mbali na hao, Rais Magufuli alimuacha Nape katika mabadiliko madogo yaliyofanyika siku moja baada ya mbunge huyo wa Mtama (CCM) kupokea ripoti ya kamati aliyoiunda ya kuchunguza uvamizi wa studio za televisheni za Clouds Media, huku mteule wa Rais akituhumiwa kuongoza tukio hilo.

Rais hakutaja sababu za kumuacha Nape badala yake katika mabadiliko hayo alimteua Dk Harrison Mwakyembe kushika nafasi yake huku Profesa Palamagamba Kabudi akiteuliwa kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.

Diwani Athuman atenguliwa

Mbali na uteuzi wa Kamanda Sirro kuwa IGP, Rais Magufuli pia alimuondoa aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Diwani Athuman na baadaye kumteua kuwa katibu tawala wa Mkoa wa Kagera.

Taarifa ya Ikulu haikueleza sababu za kutenguliwa kwa Diwani, lakini ilikuwa ni siku moja baada ya Rais kutembelea ofisi za Idara ya Maliasili kuthibitisha shehena ya pembe za ndovu zilizokamatwa na kuhoji sababu za mtu anayeitwa Mpemba kuwasumbua polisi.

Nafasi yake ilichukuliwa na Robert Boaz, aliyekuwa kamishna wa polisi.

Rais pia amekuwa akifanya mabadiliko katika taasisi nyingine nyeti ya Mamlaka ya Mapato, akiwa ameshafanya mabadiliko mara tatu katika nafasi ya kamishna mkuu.

Mara alipoingia alimteua Dk Philip Mpango kuongoza taasisi hiyo, lakini baadaye akamteua kuwa mbunge na kumfanya awe Waziri wa Fedha na Mipango. Nafasi yake ikachukuliwa na Alphayo Kidata, aliyekuwa akikaimu nafasi ya kamishna msaidizi.

Ndani ya kipindi hicho kifupi, Rais Magufuli alimbadilisha tena Kidata na kumpeleka Ikulu, huku akimteua Charles Kichele kuongoza mamlaka hiyo muhimu.

Taasisi nyingine muhimu ni Takukuru, ambako alimuondoa mkurugenzi wa zamani, Dk Edward Hoseah kwa kutowajibika ipasavyo katika masuala ya ukwepaji kodi na ushuru wa makontena bandarini.

Badala yake, alimteua Valentino Mlowola kukaimu nafasi hiyo na baadaye kumthibitisha kuwa mkurugenzi mpya.

Hatua kama hiyo aliichukua kwa mkurugenzi wa Tanesco, Felschemi Mramba baada ya taasisi yake kuwasilisha maombi ya kutaka bei ya umeme iongezwe.

Rais pia alifanya mabadiliko katika shirika kubwa la Hifadhi ya jamii (NSSF) kwa kumuondoa Dk Ramadhan Dau kwa kumteua kuwa balozi, katika kipindi ambacho shirika hilo lilikuwa linamulikwa na taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Fedha za Serikali (CAG).

Mwiba huo wa Rais Magufuli haukuacha kuwagusa pia, wakuu wa mikoa, wilaya, makatibu tawala na wakurugenzi.

Anne Kilango Malecela, aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga, alitenguliwa kwa kosa la kusema uongo kuhusu idadi ya watumishi hewa katika mkoa wake.     

Credit - Mwananchi

Baada ya Kimya Kirefu..Bashe Aibuka na Hili Jipya Bungeni..!!!

$
0
0

Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe ameitaka Serikali kukaa na walipakodi wakubwa kupata maoni yao namna ya kuongeza mapato ya kodi ili kuokoa kudorora kwa uchumi.

"Takwimu za Wizara ya Fedha zinaonyesha biashara 7,500 zimefungwa. Athari yake inaonekana kwani mapato ya kodi nyingi yameshuka. Kwa mwaka mzima Wizara inasema biashara 200 zimeanzishwa lakini mchango wake hauonekani," amesema Bashe.

Ametolea mfano Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) ambayo kodi yake imepungua kwa Sh50 bilioni huku ikipunguza wafanyakazi wake.

"Wizara ikikaa na watu hawa ikajua maitaji yao, mapato ya kodi yataongezeka na mwananchi mnyonge atapata nafuu. Kodi inalipwa na wafanyabiashara sio wanyonge," amesema.

Msichana wa Miaka 21 Achoma Nyumba na Kuhatarisha Maisha ya Watu 7 kwa Wivu wa Mapenzi...!!!

$
0
0

Jeshi la Polisi Mkoani Singida linamshikilia msichana mmoja amabye anaumri wa miaka ishirini na moja(21) kwa kosa la kuchoma moto nyumba waliyokuwemo watu 7 na kuhatarisha maisha yao. 

Yadaiwa sababu kubwa iliyomsukuma binti huyo mpaka akajikuta anaitia kiberiti nyumba hiyo ni wivu wa mapenzi.

Mbunge wa CCM Ashangiliwa na Upinzani Bungeni Baada ya Kuhoji Zilipo Milioni 50 Kila Kijiji...!!!

$
0
0

Katika hali ya kushangaza mbunge wa CCM ameshangiliwa na upinzani bungeni mara baada ya kuhoji zilipo Milioni 50 ambazo katika Ilani ya Chana cha mapinduzi zilitajwa kugaiwa kwa kila kijiji nchi Tanzania...

Alipongezwa na wabunge ambao wengi wao ni kutoka upinzani

Nini maoni yako katika hili?

Kuna Ufisadi Kwenye T. Shirt Zilizotumika Wakati wa Baraza Kuu la CHADEMA Lililofanyika Dodoma..!!!!

$
0
0

Nimepata habari kuwa kuna ufisadi mkubwa umefanyika ndani ya CHADEMA kwa kutumia fedha za ruzuku. Kwamba, T. Shirt moja iliyovaliwa wakati wa Kamati Kuu na Baraza Kuu la CHADEMA lililofanyika Doeoma hivi karibuni imetengenezwa kwa shilingi 120,000 na kwamba kila aliyevaa ametakiwa kulipa nusu ya bei na nusu nyingine kimegharamia chama.

Taarifa hizo zinasema kuwa baadhi ya wajumbe wamegoma kulipa gharama hizo kwa madai kuwa bei ni kubwa mnooooo! Inadaiwa pia kuwa wajumbe wengine waligoma kuzivaa ili wasiwe sehemu ya ufisadi huo.

Kama habari hizi ni za kweli basi kale kaugonjwa kalikokimbia CCM kametaga mayai CHADEMA

Chanzo JF
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images