Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Chadema Watoa Tamko Hili Kufuatia Kifo cha Utata cha Mzee Ndesamburo..!!!

$
0
0


Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe ametangaza msiba wa mmoja wa Waasisi wa CHADEMA, Mzee Philemon Ndesamburo na kusema kuwa nchi imempoteza mmoja wa watu mahiri waliopigania demokrasia na maendeleo, kwa maneno na vitendo, kwa ajili ya maendeleo ya nchi kwa vizazi vya sasa na baadae.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma kuhusu msiba huo uliotokea leo ghafla asubuhi, Mhe. Mbowe amesema chama kimempoteza mmoja wa 'makamanda' waliokiasisi na kusimamia agenda za mabadiliko kwa miaka zaidi ya 25 bila kuchoka pamoja na kuwepo vikwazo mbalimbali katika mapambano hayo.

"Nimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za kifo cha Mhe. Philemon Ndesamburo aliyefariki mapema leo Jumatano Mei 31, 2017, majira ya asubuhi. Ni hudhuni kubwa na maumivu makali yasiyoelezeka kwa kumpoteza Kiongozi na Mzee watu.

"Mzee Ndesamburo ni mmoja wa waasisi wa Chama Chetu cha CHADEMA na siasa za mabadiliko kwa ujumla nchini. Amekuwa Mbunge wa Moshi Mjini kwa miaka 15, ni Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Kilimanjaro na Mjumbe Baraza Kuu la CHADEMA na juzi tu siku ya Jumamosi 27 Mei 2017 alishiriki kikao cha Baraza Kuu mjini Dodoma.

"Leo alikuwa na miadi ya kukutana na Meya wa Jiji la Arusha Mhe. Lazaro Kalist kwa ajili ya kumpatia rambirambi yake kwa watoto wa Shule ya msingi ya Lucky Vincent ya Arusha waliofariki katika ajali mbaya gari hivi karibuni. 

"Mstahiki Meya alifika ofisini kwa Mhe. Ndesamburo, ili aandikiwe hundi hiyo, wakati amechukua kalamu aandike hundi hiyo aghafla Mzee wetu akajisikia vibaya akaangua hivyo akalazimika kukimbizwa hospitalini ambapo mauti yalimkuta," amesema Mhe. Mbowe na kuongeza;

"Chama kimempoteza mpambanaji na mpigania ukombozi na mabadiliko ya kweli ndani ya Taifa, alifahamu kupigania na kutafuta haki, uongozi bora na demokrasia katika Taifa letu.

"Kwa niaba ya chama na viongozi wenzangu, natoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wote bila kusahau wanachama, wapenzi wote wa CHADEMA nchi nzima na Watanzania wote walioguswa na msiba huu mkubwa kwa kumpoteza Kiongozi wetu."

Mhe. Mbowe amesema kuwa katika maisha ya mwanadamu huu ndio wakati mgumu kuliko wote, ambapo ameomba Mwenyezi Mungu awatie nguvu familia ya Mhe. Ndesamburo katika wakati huu mzito wa majonzi ya msiba huo.

Mhe. Mbowe amemuelezea Mzee Ndesamburo kama kiongozi shupavu, jasiri, aliyejiamini.

Ameongeza kuwa ingawa kimwili hatuko nae lakini, hekima, busara na matendo yake yataishi milele yakifanya akumbukwe daima.

Bwana alitoa, Bwana ametwaa. Jina lake lihimidiwe. 

Imetolewa na: 

Tumaini Makene

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA

Utata Waibuka Kuhusu Maziko ya Mzee Ngosha Aliyebuni Nembo ya Taifa..!!!

$
0
0

“HATUNA jibu mzee huyu atazikwa lini na wapi, lakini mwili wake bado tumeuhifadhi hapa na Serikali inaendelea kuwatafuta ndugu zake halisi ili kujua taratibu za mazishi,” amesema Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).

Mkurugenzi huyo wa Hospitali ya Muhimbili, Profesa Lawrence Mseru alisema hayo jana alipozungumza na HabariLeo na kusisitiza kuwa, mwili wa Mzee Francis Kanyasu maarufu kama Ngosha (86) aliyefahamika hivi karibuni kuwa ndiye aliyebuni Nembo ya Taifa, kwa sasa umehifadhiwa katika Hospitali hiyo hadi watakapopatikana ndugu zake halisi tayari kwa mazishi.

Katika mazungumzo hayo, Profesa Mseru alisema ndugu wa marehemu Ngosha wanatafutwa na serikali kwa kushirikiana na jamaa waliokuwa wakiishi na mzee huyo Buguruni Dar es Salaam. Alisema kwa mujibu wa taarifa alizozitoa Ngosha katika uhai wake, baadhi ya ndugu zake wanaishi Sengerema, hivyo watatafutwa ili watoe kauli kuhusu mazishi ya ndugu yao.

“Wale walioishi na Mzee Ngosha ni jamaa tu waliishi naye, lakini sio ndugu zake halisi… Ni sahihi wana nafasi yao kwa mzee huyo, lakini lazima tuwatafute ndugu zake halisi,” alisema Profesa Mseru.

Kuhusu afya yake, Profesa Mseru alisema kuwa hajakabidhiwa taarifa ya uchunguzi ya mzee huyo kujua alikuwa akikabiliwa na tatizo gani ingawa kwa mujibu wa taarifa ya mwisho iliyotolewa na daktari katika hospitali hiyo, mzee huyo alikuwa na matatizo ya kifua.

Mmoja wa wanafamilia katika familia iliyokuwa ikiishi na Mzee Ngosha, Said Chume, alisema mzee huyo walipozungumza naye Mei 27, mwaka huu aliwataja ndugu zake wawili wanaoishi Sengerema.

“Alitutajia ana ndugu ambao ni Nyanzala Budodi ambaye ni dada yake na John Siang’a ambaye ni mpwa wake. Alisema hao ndugu zake wanaishi Sengerema katika nyumba za Shirika la Nyumba,” alisema Chume.

Familia hiyo ilisema kuwa Mzee Ngosha alikuwa hapendi kwenda hospitali, akiumwa huchuma majani na mizizi ambayo huomba wamtwangie ili anywe na kwamba alikuwa akisumbuliwa na kifua kutokana na uvutaji sigara kwa muda mrefu.

Kabla ya kufariki, mzee huyo aliwaambia waandishi wa habari kuwa yeye ndiye aliyebuni Nembo ya Taifa baada ya kuombwa na Mwalimu Julius Nyerere miaka ya 60 kabla ya uhuru akifanya kazi katika mashamba ya mkonge Tanga...

Tetesi..CCM Kuwafukuza Nape Nnauye na Bashe kwa Kuwa Wanatumika na Chadema..!!!

$
0
0

Taarifa kutoka chanzo cha ndani kabisa ndani ya CCM zinasema kwamba kuna uwezekano mkubwa katika Kikao kijacho cha CCM takribani Wanachama 11 wakafutiwa Uanachama ambapo ndani yao wapo Vigogo Watatu ambao ni Nape Nauye, Hussein Bashe na Msukuma.

Nape na Bashe wanafukuzwa baada ya kugundulika kuwa wanatumika na Chama cha Upinzani CHADEMA huku Msukuma anafukuzwa kwa kosa la kuwa mropokaji, mweneza chuki na mtu asiye mkweli kwa Wanachama wenzie.

Chanz JF

Kama Hujui Hii Ndio Nguvu ya Pesa Kwenye Mahusiano..!!!

$
0
0

Pesa kwenye Biblia takatifu imezungumzwa katika vifungu 2,350 .Pesa ndio humpa mwanadamu heshima,umaarufu na jina zuri.Pesa ni ulinzi na ngao ya kujikinga na mambo mengi ukiwa ungali hai ijapokuwa tunaziacha duniani.

Baadhi ya wanaume wenye pesa huwa hawajui wanawake wazuri na bora ,Najiuliza ni mwanaume gani jasiri anayemtafutia ,Iggy Azalea mwanamke mwenzie kwa uzuri na urembo alio nao Iggy Azalea?

Pesa huficha tabia mbaya, na Ukiona mwanamke amekuacha kwa ajili ya pesa ,basi jua akienda kwa mwanaume mwenye pesa atamuacha kwa ajili ya mapenzi ya dhati.

Na ukiona mwanaume amekuacha wewe mwanamke kwa ajili huna shape nzuri jua akienda kwa mwanamke mwenye shape nzuri atakosa mapenzi ya dhati .Nguvu ya kiume ni pesa na sio viroba wala supu ya Pweza.When money speaks, the truth remains silent.#Money 

Magufuli Afanya Uteuzi Mpya Benki Kuu,,Ateua Manibu Gavana Wawili kwa Mpigo..!!!

$
0
0

Rais John Magufuli jana, Jumatano ameteua manaibu Gavana wawili wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Taarifa ya Ikulu imesema, Rais amemteua, Dk Yamungu Kayandabila kuwa Naibu Gavana anayeshughulikia Uchumi na Fedha na Dk Bernard Yohana Kibese (Uthibiti na Usimamizi wa Sekta ya Fedha).

Kabla ya uteuzi huo, Dk Kayandabila ambaye anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk Natu Mwamba aliyememaliza muda wake, alikuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi,  Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

 Dk Kibese aliyekuwa mtaalamu wa uchumi na fedha wa BoT, anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Lila Mkila ambaye amemaliza muda wake.

Taarifa za Awali: Moyo wa Hayati Ndesamburo Ulikuwa na Matatizo Makubwa..!!!

$
0
0

Wakati uchunguzi wa kifo cha Hayati Philemon Ndesamburo ukiendelea,taarifa za awali zinadokeza kuwa moyo wake ulikuwa na matatizo makubwa.

Kiongozi wa wachunguzi wa kitabibu,Prof. Elisante Masenga amesema kuwa taarifa hiyo ni ya awali na taarifa kamili itatolewa hapo baadaye baada ya uchunguzi kukamilika.

R. I. P. Hayati Ndesamburo!

Chanzo: ITV Habari

Akaunti 88 za Rais Jammeh Zafungwa, Waziri wa Serikali Mpya Adai Alikwapua Dola Milioni 50..!!!

$
0
0

WAZIRI wa Sheria wa Gambia, Abubacarr Tambadou, amesema kiongozi wa zamani wa nchi hiyo, Yahya Jammeh, ameiba kiasi cha dola za Marekani milioni 50 kutoka katika kampuni ya mawasiliano ya taifa hilo na tayari mahakama imetoa amri ya kutaifisha mali zake.

“Rais Yahya Jammeh yeye binafsi au kwa kutoa maelekezo mahsusi amekwapua dola za Marekani zisizopungua milioni 50,” anasema waziri huyo na kuongeza; “..Jumatatu (Novemba 22, 2017) tumepata amri ya mahakama kuhusu kutaifisha mali zake au kuzizuia.”

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la AFP, hii ni mara ya kwanza kwa serikali mpya ya taifa hilo kutoa maelezo rasmi kuhusu wizi alioufanya rais huyo wa zamani aliyeongoza taifa hilo kwa miaka takriban 22 mfululizo.

Waziri Tambadou aliwaeleza waandishi wa habari kwamba mahakama ya nchi hiyo imeamuru kufungwa kwa akaunti takriban 88 zenye jina la Jammeh katika benki mbalimbali, sambamba na ‘kuzishikilia’ kampuni 14 zinazohusishwa na mkuu huyo wa nchi wa zamani.

Yahya Abdul-Aziz Jemus Junkung Jammeh alizaliwa Mei 25 mwaka 1965, ni mwanasiasa aliyetokea katika jeshi na alianza kuiongoza Gambia kuanzia mwaka 1994 hadi 2017, akiwa mwenyekiti wa Baraza la Utawala la Kijeshi (AFPRC)  na baadaye kuwa rais wa nchi hiyo kuanzia 1996 hadi 2017.

Zitto Kabwe Aumbuka Kuhusu Ndege Mpya Itakayonunuliwa na JPM..Kumbe Hata Haijaanza Kutengenezwa Tofauti na Anavyosema..!!!

$
0
0

Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT), Zitto Kabwe ameangukia pua baada ya kubainika kuwa hoja anayojenga bungeni ni ya “kubumba”, Uchunguzi wa JAMHURI umebaini.

Kwa muda sasa Zitto amekuwa akitoa matamko bungeni na kuandika katika mitandao ya kijamii kuwa ndege ya Boeing 787 – 800 iliyonunuliwa na Serikali ni mbovu, wakati uhalisia ndege hiyo ndiyo kwanza matengenezo yake yameanza.

Ukweli kuhusu ndege mpya aina ya Boeing 787-800 Dreamliner iliyonunuliwa na Serikali, umejulikana.

Kwenye mitandao ya kijamii na hata katika Bunge, Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT), amekuwa akitoa taarifa zenye mwelekeo wa kuaminisha umma kuwa Serikali imenunua Terrible Teen ambazo zina matatizo ya kiufundi na kwa gharama kubwa.

Hata hivyo, uchunguzi wa kina uliofanywa na JAMHURI umebaini kuwa sakata hili limegubikwa zaidi na vita ya kibiashara. Nyaraka za mawasiliano ambazo JAMHURI limezipata zinathibitisha hilo.

Uchunguzi umebaini kuwa si kweli kuwa ndege inayosemwa imenunuliwa kwa dola milioni 224.6 za Marekani (zaidi ya Sh bilioni 450).

JAMHURI limefanikiwa kuona mkataba wa Boeing na Serikali kwenye ununuzi wa ndege hiyo ya Boeing 787-800 Dreamliner na kubaini kuwa imenunuliwa kwa dola milioni 150 za Marekani (zaidi ya Sh bilioni 330).

Hadi makubaliano hayo yanafikiwa kati ya Boeing na Serikali, kulikuwa na majadiliano ya kimkataba yaliyoongozwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali; Wakala wa Ndege za Serikali; Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) na Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA).

Uchuguzi uliofanywa na JAMHURI umethibitisha kwamba kulikuwa na muda wa kutosha wa majadiliano kabla ya kusaini mkataba wa matengenezo ya Dreamliner.

JAMHURI limebaini kuwa Dreamliner iliyonunuliwa na Serikali ya Tanzania na inaweza kuruka kutoka Dar es Salaam hadi Guangzhou China ikiwa imejaza abiria na na mzigo wa tani 13.3 ukilinganisha na Terrible Teens, ambayo ina uwezo wa kubeba tani 5.8 tu.

Hii ina maana ndege iliyonunuliwa na Serikali inabeba mzigo tani 7.5 zaidi ikilinganishwa na hiyo yenye matatizo anayoisema Zitto.

Mmoja wa maafisa wa Boeing, Morris Keelan, ameliambia JAMHURI kuwa ndege inayotengenezwa kwa ajili ya Tanzania, si miongoni mwa Terrible Teen, huku akithibitisha kwamba ndege iko kwenye matengenezo kuanzia ngazi ya awali kabisa (tazama picha ukurasa wa kwanza).

“Kwa ufafanuzi, kulikuwa na ndege chache za Boeing 787-800 zilizokuwa zinatengenezwa kiwandani kwetu, vyombo vya habari viliziita ‘terrible teens’ kwa sababu namba za kutengenezwa kwake zilikuwa kati ya 12-20.

“Ndege hizo zimekwishauzwa na kukabidhiwa kwa wateja wetu, na zimekuwa zikiendelea kufanya vizuri na kuthibitisha ubunifu wetu katika teknolojia na uchumi imara kama zilivyo Boeing 787 Dreamliners,” amesema Keelan.

Akizungumza kuhusu Dreamliner, ndege yenye uwezo wa kubeba abiria 264, Keelan anasema ndege hiyo kwa ajili ya Tanzania bado haijaanza kuunganishwa (assembling), huku akithibitisha kuwa shughuli ya kutengeneza vifaa vya kuunganisha ndege hiyo inaendelea vizuri.

“Bado hatujaanza kuunganisha ndege ya Tanzania, hatuwezi kuanza leo, ni mpaka mwaka 2018 kama tulivyokubaliana kwa mujibu wa mkataba…sasa tunaendelea kuandaa mahitaji muhimu katika ndege hiyo kama mahitaji tuliyopewa na mteja wetu,” amesema Keelan.

Anasema, hadi Oktoba 31, mwaka jana kampuni ya Boeing ilikuwa imepokea oda 1,208 za ndege aina ya Boeing 787-800 Dreamliner zinazofanana na ile iliyonunuliwa na Tanzania (line number 719).

Keelan ameliambia JAMHURI kuwa kazi ya uchaguzi wa namna ndege ya Tanzania itakavyokuwa (configuration) ilimalizika katikati ya Machi, wakati uchaguzi wa injini bado unaendelea.

“Hivyo, ndege ya Tanzania ndio iko katika hatua za mwanzo kabisa za ununuzi wa vifaa vya kuitengeneza,” amesema.

Taarifa ambazo JAMHURI limezipata zinaonesha kwamba mpaka sasa Serikali inaendelea na uchambuzi wa aina ya injini zitakazotumika katika Boeing 787-800 Dreamliner. Wauzaji wakubwa wa injini hizo duniani ni General Electric (GE), Rolls-Royce na United Technologies (Pratt & Whitney).

Mchakato wa kutengeneza ndege unahusisha utengenezaji wa sehemu mbalimbali (parts) na mifumo ya ndege ambayo hutengenezwa nchi tofauti duniani na baadaye kupelekwa katika kiwanda kimoja kwa ajili ya kuunganishwa.

Mfano, mkia na mabawa ya ndege zilizo nyingi hutengenezwa nchini Malaysia na kuuzwa kwa nchi za Magharibi ikiwa sehemu mfu wa biashara ya ndege wenye kunufaisha nchi nyingi kwa wakati mmoja inapotengenezwa na kuuzwa ndege angalau moja.

Hatua hiyo hufuatiwa na uunganishaji (assembling) wa sehemu hizo ili kupata umbo kamili la ndege, uwekaji mifumo na mitambo mbalimbali inayotumiwa na ndege, kuweka muundo wa ndani wa ndege (interior installation) uliochaguliwa na mnunuzi, na mwisho upakaji rangi.

Baadaye uunganishaji hufanyika katika kiwanda cha Boeing nchini Marekani. Mnunuzi wa ndege anaweza kushiriki ukaguzi wa awamu mbalimbali za uunganishwaji wa ndege ili kujiridhisha kama ubora umefuatwa katika utengenezaji wa ndege yake.

Ndege iliyonunuliwa na Serikali ni Boeing Line number ni 719 na serial number yake ni 64249, tofauti na maelezo yaliyoko katika tovuti inayodai kuwa Tanzania imenunua ndege mojawapo ya ndege za Boeing zijulikanazo kama Terrible Teens Dreamliners zilizokataliwa na mashirika mengine ya ndege duniani.

Maelezo ya ndege inayodaiwa kununuliwa na Tanzania ni tofauti kabisa na maelezo rasmi yaliyotolewa na kampuni ya Boeing, serial number na line number (ambayo huonesha ni ndege ya ngapi kutengenezwa) ilizopewa ndege ya Tanzania ni tofauti na zilizoko katika tovuti isiyomilikiwa na Boeing.

Ndege moja haiwezi kuwa na line number na serial number mbili tofauti, hata kama ikiwa imefanyiwa ukarabati mkubwa line number na serial number hubaki zile zile.

Akizungumza na JAMHURI, Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL, Mhandisi Ladislaus Matindi amesema kuna maneno mengi yanasemwa kuhusu ndege hiyo mpya ambayo ni upotoshaji mtupu.

“Kuna taarifa kuwa ndege ni ya zamani na bei yake ni kubwa, lakini sitaki kuzungumzia mambo ya mkataba hapa, zaidi ya ukweli kwamba ndege yetu bado haijaanza kutengenezwa kwani ni lazima tuhusishwe katika awamu zote za utengenezaji.

“Kwa mujibu wa vigezo tulivyovichagua kama wanunuzi ili kuhakikisha kuwa ndege tuliyonunua na kukubaliana katika mkataba ndio inaletwa Tanzania, ratiba ya utengenezaji wa ndege yetu tunayo. Kwa ufupi hiyo ndege inayosemwa mitandaoni na bei yake haviko katika makubaliano kati yetu na Boeing,” amesema Matindi.

Mei, mwaka huu, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, aliliambia Bunge; “Serikali imeingia Mkataba na Boeing wa kutengeneza ndege mpya yenye line number 719, ndege inayozungumzwa hapa [inayosemwa na Zitto] Kama tumechukua ilikuwa iende Rwanda ina line number 19. Yetu sisi ni line number 719; ni tofauti.”

Akizungumza na JAMHURI, Kabwe ambaye amekuwa mstari wa mbele katika ‘kuhoji’ gharama za ndege hizo na ubora wake kwa mujibu wa fedha zilizotolewa, amesema hoja yake kubwa ni kwamba kama Serikali imenunua Terrible Teens, basi bei yake ilipaswa kupungua kama ilivyokuwa kwa Shirika la Ndege la Ethiopia.

“Boeing wanasema bei (list price ni USD 224.6 milioni). Serikali muda wote imekuwa ikiliambia Taifa kwamba wamenunua ndege hiyo kwa bei inayotajwa na Boeing.

“Hata hivyo Waziri amesema ndani ya Bunge kuwa pamoja na kuwekewa bei hiyo kwenye tovuti mazungumzo marefu yalifanyika na ndio tulipewa punguzo kubwa.

“Swali linaloibuliwa sasa ni, kama tunanunua ndege mpya kabisa na siyo Terrible Teen, kwanini tumepewa punguzo kubwa sana? Sasa tumelipa kiasi gani baada ya hilo punguzo? Mazungumzo marefu yalihusu nini kama tunanunua ndege mpya kabisa?” Amehoji Zitto

Anasema amepitia taarifa ya Serikali bungeni, hususan randama za Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ili kuona taarifa ya miamala ya malipo kwa ndege hii. Serikali imelijulisha Bunge kuwa imeshalipa takribani asilimia 44.6 ya bei ya ndege iliyoagizwa.

Anasema kwa mujibu wa randama hizo, Serikali imeshalipa dola milioni 67 za Marekani, (zaidi ya Sh bilioni 134) kwa kampuni ya Boeing ambako dola milioni 10 za Marekani (zaidi ya Sh Bilioni 22) zililipwa Desemba, mwaka jana.

“Kwa niaba ya wananchi wote wa Tanzania nimechukua hatua ya kumwandikia Spika kumwomba kupatiwa mkataba kati ya Serikali na Boeing na ushahidi wa miamala yote ya malipo ya fedha kutoka Hazina ya Tanzania kwenda Boeing au kwingine kokote kunakohusiana na ununuzi wa ndege hii Dreamliner Boeing 787-800,” amesema Zitto.

Uhuru huo wa kuomba kupatiwa nyaraka hizo, unatajwa katika kifungu cha 10 cha Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge, Sheria Na. 3 ya mwaka 1988.

Akizungumza na JAMHURI, Katibu Mkuu anayeshughulika na Sekta ya Uchukuzi, Dk. Leonard Chamriho, amesema kumekuwapo mchakato wa wazi katika kuwapata wazabuni wawili ambao kimsingi ndio watengenezaji wa ndege hizo kubwa.

“Kutokana na ukweli kwamba watengenezaji wa ndege aina hiyo ni wawili tu, tuliamua kutumia ‘restricted tender’ ambayo kimsingi Sheria ya Unuuzi na Ugavi inaturuhusu kufanya. Tulifanya hivyo kutokana na mazingira yenyewe tuliyonayo,” amesema Dk. Chamriho.

Amesema, katika zabuni hiyo zilijitokeza kampuni mbili za utengenezaji wa ndege, ambazo ni Boeing na Air Bus.

Ameliambia JAMHURI kuwa kampuni zote ziliruhusiwa kuwasilisha taarifa za bidhaa zao mbele ya jopo la wataalamu. Dk. Chamriho anasema wote walionesha ugumu wa kupatikana ndege kwa haraka, lakini pamoja na vingine vilivyozingatiwa, ilikuwa gharama pamoja na mahitaji ya ndege hiyo kwa wakati ambao inahitajika.

“Ninakumbuka Air Bus walituambia wataweza kutupatia ndege hiyo kuanzia mwaka 2023, huku wakitupatia chaguo la kukodi ndege kama hiyo. Hatukuhitaji kukodi maana tunayo historia mbaya katika mikataba ya kukodi ndege.

“Boeing wao walisema wanaweza kutupatia slot ndani ya Juni 2018; kutokana na mazingira tukalazimika kuendelea na mazungumzo na Boeing, walitutaka kuweka fedha za dhamana ya kutengeneza ndege hiyo. Tuliwalipa dola milioni 10 za Marekani (zaidi ya Sh bilioni 22).

“Baada ya kulipa malipo hayo, tulipewa muda wa mwezi mmoja kujadiliana kuhusu masharti ya mkataba wetu wa kununua ndege hiyo pamoja na vipimo (specification) kwa mujibu wa mahitaji yetu,” Katibu Mkuu, Dk. Chamriho ameliambia JAMHURI.

Amesema Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Wilson Masilingi ameshiriki katika kuhakikisha mambo yanakwenda vizuri.

“Balozi Masilingi alifanya ziara makao makuu ya Boeing na kukutana na rais wa kampuni hiyo, mazungumzo yao yameleta ahuane kubwa sana katika majadiliano mpaka kufikiwa kwa makubaliano ya mkataba,” amesema.

Kuhusu muda wa majadiliano hadi kufikia makubaliano ya kusaini mkataba, Katibu Mkuu huyo anasema iliwachukua “muda wa kutosha” kujadiliana na hatimaye kusaini mkataba wa ununuzi wa ndege.

Dk. Chamuriho amesema baada ya kutiliana saini, ulifanyika utaratibu kwa ujumbe wa Boeing kwenda kumwona Rais John Magufuli. “Walikwenda kufanya ‘courtesy call’, hiyo ilikuwa baada ya makubaliano yetu kukamilika”.

Hata hivyo Dk. Chamriho, hakuwa tayari kuliambia JAMHURI, serikali imelipa kiasi gani, huku akisisitiza kwamba, serikali haikulipa kiasi cha fedha kilichowekwa kwenye mtandao wa Boeing.

“Pale kwenye mtandao wao wameweka list price, baada ya majadiliano bei ilipungua, lakini kwa mujibu wa mkataba tulioingia na kampuni hiyo, sitakiwi kusema tumekubaliana kiasi gani, lakini kwa hakika maana sisi tulikuwa na fedha mkononi, gharama ilipungua,” amesema Dk. Chamriho.

Taarifa ambazo JAMHURI limezipata na kuthibitishwa na vyanzo vyetu, zinasema Air Bus, baada ya kukosa zabuni walianza kutoa vitisho vikiwamo vya kuishitaki Tanzania kwa Benki ya Dunia na Umoja wa Ulaya (EU), wakidai kuwa kulikuwa na utapanyaji fedha katika ununuzi wa ndege hiyo.

Aidha, Air Bus na wapambe wake walikwenda mbali zaidi hata kumchongea Dk. Chamuriho kwa Rais Magufuli.

Katibu Mkuu alishitakiwa kwa Rais Magufuli, kupitia barua iliyoandikwa na Air Bus kwenda Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Katika barua hiyo, walimtuhumu Dk. Chamuriho kutowapatia kandarasi na badala yake kuwapatia Boeing zabuni hiyo ya mabilioni ya shilingi.

Alipoulizwa na JAMHURI kuhusu tuhuma hizo, Dk. Chamriho alisema ni kweli alishtakiwa kwa Rais Magufuli, kutoa upendeleo kwa kampuni ya Boeing.

“Uchunguzi umeshafanyika, nadhani waliochunguza walipata ukweli wa tuhuma hizo dhidi yangu, lakini pamoja na hayo nililazimika kuandika maelezo na naamini ukweli umebainika,” amesema Dk. Chamriho.

Katibu Mkuu huyo anawataja Hadi Akoum, Makamu wa Rais wa Air Bus, anayeshughulikia mauzo katika bara la Afrika na ukanda wa Bahari ya Hindi, pamoja na Jerome Charieras, Mkurugenzi wa Mauzo pamoja na uhusiano wa wateja, ambao walikwenda kulalamika wakihoji Boeing kupewa zabuni hiyo badala ya wao.

Anasema katika mazungumzo yao walionesha kwamba hata Boeing hawataweza kukamilisha kwa wakati, na kwamba nafasi waliyonayo ni sawa na Air Bus yaani mwaka 2023.

Dk. Chamriho amesema wakazidi kumshawishi kwamba Boeing wataiuzia Tanzania ndege zilizokataliwa za ‘Terrible Teens’.

“Waliniambia kutorishwa kwao na mchakato, lakini wakasema lolote linaweza kutokea kwa nchi za Kiafrika…nikawauliza mnamaanisha nini? Kwamba nimepokea rushwa? Wakasema inawezekana, nikawataka waondoke ofisini kwangu, maana kwangu hiyo ilikuwa ni dharau kubwa,” amesema Dk. Chamriho.

Mbali na ajenda hiyo, wakamwambia hapakuwa na ushindani wa wazi, na kwamba Tanzania imekuwa ikipokea misaada kutoka EU na hivyo watakwenda kuishtaki huko na katika Benki ya Dunia.

JAMHURI limewasiliana na Hadi Akoum kwa barua pepe ili kuthibitisha baadhi ya tuhuma zao, mpaka tunakwenda mtamboni hakuwa amejibu.

Masuala muhimu katika mkataba

a) Dhamana: Kuna dhamana ya uwezo wa ndege (aircraft performance), kuna dhamana ya aina ya ndege iliyochaguliwa (aircraft model applicability), kuna dhamana ya mwonekano na vifaa/nakshi vilivyochaguliwa kuwekwa ndani ya ndege.

b) Bei ya ndege: Bei ya mwisho ya ununuzi wa ndege inatokana na bei iliyotolewa kampuni (listed price), na ukitoa punguzo (concessions).

C) Bei ya kampuni kwa jumla inahusisha bei ya umbo la ndege (airframe), bei ya injini, bei ya vitu vya nyongeza vinavyochaguliwa na mnunuzi (optional features), bei ya mifumo ya burudani ndani ya ndege (inflight entertainment system), na punguzo.

Mengine ni punguzo litokanalo na majadiliano (Basic credit memorandum), punguzo la kimkakati (Strategic relationship memorandum), na punguzo la kumwezesha mteja kukidhi mahitaji ya utumiaji wa ndege (Goods and services memorandum).

Katika mazungumzo yao walikuja na hoja kwamba walikuwa na mkataba na Air Tanzania (ATCL) pamoja na Senangol ya China, ambayo iliingia mkataba na ATCL mwaka 2012, huku wakisisitiza kwamba walishachukua fedha ya kiasi cha Dola za Marekani Milioni 2.5, (Zaidi ya Sh Bilioni 5) kama sehemu ya mkataba wao na washirika hao wawili.

Dk. Chamuriho amesema, aliwajibu kwamba sehemu ya mkataba huo hauna uhusiano na ununuzi wa ndege mpya aina ya Boeing 787-800 Dreamliner, isipokuwa hiyo ilikuwa inanunuliwa na Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA).

Terrible Teens ni nini?

Terrible Teen ni ndege za mwanzo Aina ya dreamliner 787 zilizotengenezwa kati ya miaka 6-7 iliyopita. Ndege iliyonunuliwa ina uzito kidogo ukilinganisha na dreamliner za zamani, za sasa 787 zina uzito wa tani 4-6 ukilinganisha na dreamliner za mwanzo

Kutokana na kufanyiwa marekebisho ya mara kwa mara, ndege hizo zilizidi uzito kwa tani 3.2 ikilinganisha na uzito uliotakiwa. Kutokana na kuongezeka uzito ndege hizo zikapunguza hata uwezo wake. Ina uwezo wa kwenda umbali wa Nautical Mile 5,900, hiyo ina maana inaweza kufika Guangzhou China ikiwa imejaza abiria na na mzigo wa tani 5 tu.

Kutokana na hili makampuni yaliotaka order za mwanzo kama All Nippon, Maroc na mengineyo yaligoma kuchukua ndege hizo kutokana na kutengeneza hasara katika safari kama wangeamua kuzitumia.

Terrible Teen zilizokosa soko, ni pamoja na L10, L12, L13, L14, L15, L16, L17, L18, L19, L22. Terrible Teens line namba 11 inatumiwa na Boeing business jet, namba 12 Ethiopia airways wameonyesha nia kuichukua, terrible teens line namba 4 na namba 5 zinatumiwa na boeing kama ndege za majaribio.

Mwezi April, mwaka huu, Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL, Ladislaus Matindi, alinukuliwa akisema shirika lake limefanikiwa kukusanya Sh Bilioni 9 kwa Miezi minne tu kwa kutumia ndege mbili za Bombardier.

Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL) ilianzishwa mwezi Novemba 2002 baada ya Serikali kubinafsisha lililokuwa Shirika la Ndege la Tanzania (Air Tanzania Corporation, ATC).

Ujio wa ndege hizo mbili za ATCL, umeweza kupunguza ukiritimba katika usafiri wa anga kwa safari za ndani. Mwanzo kulikuwa na mashirika mawili tu yaliyokuwa yakitoa huduma hiyo ya usafiri wa anga.

Chanzo: Jamhuri

Spika Ndugai Amlilia Mzee Ndesamburo..Adai Mchango Wake Ulikuwa Mkubwa..!!!

$
0
0

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Job Ndugai amemtumia salamu za rambirambi Mwenyekiti wa CHADEMA, Mh. Freeman Mbowe, kufuatia kifo cha Mzee Ndessamburo kwa kuweka wazi kwamba ni kiongozi ambaye alikua mchapakazi kwa wananchi wake.

“Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mh. Ndesamburo ambaye pia ni baba wa Mbunge wa Viti Maalumu Lucy Owenya kilichotokea mkoani Kilimanjaro hakika ni pigo kubwa” Alisema

Aidha Mh. Ndugai amesema kuwa marehemu Ndesamburo, aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Moshi mjini mwaka 2000 - 2015 atakumbukwa kwa uchapakazi wake wakati akiwa mbunge hasa katika kuwaletea wananchi wa jimbo lake maendeleo.

Mhe. Ndesamburo aliyezaliwa 19 Februari 1935, amefariki leo tar 31 Mei 1935 akiwa hospitali ya KCMC mjini Moshi.

Lissu; Nia Njema ya Magufuli Inatupeleka Pabaya..!!!!

$
0
0

Suala sio nia njema ya Rais. Suala ni consequences za hiyo nia njema. The road to hell is paved with good intentions.

Mugabe most likely alikuwa na nia njema. The consequences za nia njema hiyo ni kwamba Zimbabwe ya leo haina hata sarafu yake na imegeuka kuwa ya kuomba chakula wakati ilikuwa a major food exporter. 

Kama kweli Rais Magufuli ana nia njema angeanza na mfumo mzima wa kisheria, sio kuhangaika na magwangala. 

100% ya uzalishaji wa dhahabu ya Geita unafanyikia mgodini na Geita Gold Mine ni mgodi mkubwa kuliko yote nchini. 

Kwa logic ya Magufuli ni kwamba GGM hawatuiibii kwa sababu tu smelting yote inafanyikia Geita. 

Acacia wanayeyushia dhahabu yote ya Nyamongo mgodini Nyamongo. 

Kwa logic hiyo hiyo, hawa wezi wa mchanga wa Bulyanhulu na Buzwagi hawaibi Nyamongo kwa sababu tu wanafanya kila kitu Nyamongo. 

Resolute walisafisha 100% ya dhahabu yao Nzega mpaka walipokomba kila kitu na kuacha mashimo na maji ya sumu tu.

Kwa logic ya wazalendo wetu, hatukuibiwa Nzega kwa sababu wawekezaji hao hawakusafirisha mchanga wa dhahabu. 

Acacia walishakomba kila kitu Tulawaka na kuacha mashimo na maji ya sumu. Kwa sababu tu hawakusafirisha mchanga, basi hawakuwa wezi.

Hii ni logic ya mtu asiyeelewa biashara ya uchimbaji dhahabu katika nchi hii kabisa. 

Tangu tumeanza kuwakaribisha wawekezaji hawa, hatujawahi kufikisha 10% ya mapato ya kikodi kutokana na mauzo ya dhahabu yote iliyochimbwa na kuuzwa nje. 

Sio kwa sababu wawekezaji walikuwa wana-underdeclare mchanga wa dhahabu, bali ni kwa sababu sheria zetu zinawaruhusu kutokulipa kodi kama hawajatangaza faida. 

Ni sheria, sheria, sheria. Sio mchanga wa dhahabu. Hilo ni changa la macho tu la kufumbia wasioelewa. 

Kama Magufuli ana nia njema angeanza na sheria. Hajaanza na sheria, hana nia njema. 

Mnaambiwa tusiogope kushtakiwa. ******* ujinga na hao hao waliowaruhusu wageni kuchota mali zetu: akina Magufuli na CCM yao. 

Tumeshalipishwa na tunaendelea kulipishwa mabilioni mengi kutokana na kesi za Richmond/Dowans, IPTL/Tegeta Escrow, City Water, Samaki wa Magufuli, n.k. kwa sababu tumekuwa tunakiuka mikataba 'kwa nia njema.' 

Tumekuwa tunaingia hasara kubwa kama taifa kwa sababu za kijinga. Badala ya kukataa ujinga huu tunaushabikia kwa sababu tu umefanywa 'kwa nia njema.' 

Magufuli atauachia huo mchanga wa dhahabu kwa wenyewe. Mark my words. 

Hana jinsi. 

Sheria yetu ya madini inasema huo mchanga ni mali yao. Na imesema hivyo tangu mwaka '98.

Mkataba wao unasema ni mali yao. Na umesema hivyo tangu mwaka 2000.

Mikataba ya kimataifa tuliyosainishwa na wenye nia njema hawa inasema mchanga ni mali ya Acacia. 

Mchanga huo umehakikiwa na TRA, TMAA, GST na SGS. Zote hizi ni taasisi za Serikali hii hii na zimepewa mamlaka kisheria na kimkataba na Serikali hii hii kuhakiki mchanga huo. 

Kamati ya Prof. Mruma haina mamlaka hayo. Ripoti yake haina maana yoyote kiushahidi. 

Sio kupiga ramli au kuagua kusema kwamba tutapigwa asubuhi kwenye arbitral tribunals za kimataifa. 

Tutawarudishia mchanga na tutawalipa hasara yote waliyopata kwa sababu ya matendo yenye nia njema lakini yasiyozingatia sheria wala busara katika mambo haya. 

Tunarushiwa changa la macho lingine. Tunaambiwa kuna Kamati ya wachumi na wanasheria inaleta ripoti nyingine. Hii itakuwa Kamati ya nne tangu mwaka 2004. Tulikuwa na Kamati ya Dr. Jonas Kipokola (2004); Lau Masha (2006) na Jaji Mark Bomani (2008). Tumekuwa na taarifa lukuki za watafiti binafsi na kwa muda mrefu. Ni kitu gani hasa cha kiuchumi au kisheria ambacho hatukijui hadi sasa na ambacho kinahitaji kuundiwa Kamati nyingine??? Wajinga ndio waliwao. Mimi sio mjinga. Na sijahongwa kama hawa wanajiita wazalendo. Ninapinga na nitaendelea kupinga ujinga huu unaotupeleka kuzimu.....

Tundu Lisu

Kilichomuua Ndesamburo Ghafla Hiki Hapa..Alikua Akisaini Hundi ya Mchango wa Msiba ..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 1/6/2017..!!!

Marekani Waanza Kujipanga Dhidi ya Makombora ya Korea Kaskazini..!!!

$
0
0

Marekani imesema kuwa imefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika jaribio lake la kwanza la mtambo wa kutungua makombora ya nyuklia ya masafa marefu.

Mtambo huo wa ardhini umefungwa katika kambi ya kijeshi iliyopo Califonia kwaajili ya kujihami na vitisho ambavyo vimekuwa vikitolewa na maadui zake ikiwemo Korea Kaskazini.

Aidha, Pentagon imesema kuwa jaribio hilo limefanyika baada ya Korea Kaskazini kufanya majaribio yake ya makombora tisa ya masafa marefu mwaka huu hivyo kutishia usalama wa nchi hiyo.

“Mfumo huu ni mhimu sana kwa ulinzi wa taifa letu na jaribio hili ni uthibitisho mkubwa kwamba tuna uwezo wa hali ya juu wa kujilinda na kutetea usalama wa raia wetu,” amesema Mkurugenzi wa kitengo cha ulinzi wa makombora, Admirali Jim Syring.

Je, Wajua Mchezaji Gofu Maarufu Duniani Tiger Woods Huwa Hajitambulishi Kama Mtu Mweusi..!!!?

$
0
0

Tiger Woods anaamini yeye ni mtu wa asili nyingi na hata alijiundia jina mseto kueleza asili yake, na kusema asili yake ni Cablinasian. Cablinasian ni neno linalotokana na Caucasian(Mzungu), Black American (Mwafrika Mmarekani), American Indian (Mmarekani Asilia), na Asian (Asia). Babake, Earl, alikuwa wa asili ya Mwafrika Mmarekani, Mchina na Mmarekani Asili. Mamake Kultida, ni wa asili ya Thailand, Uchina na Uholanzi.

SOLUTIONS: Mh. Magufuli Mpe Waziri Wako Ndg. Mwijage Afanye Haya Within 7 Days Kuokoa Nchi..!!!

$
0
0

Sitaki kuandia mastori marefu kupoteza muda kwa sababu wananchi wamechoka kusoma magazeti marefu.

Upo ushaidi uliosheheni kuwa ipo colleration kati ya mazingira ya kufanya biashara, Foreign Direct Investment (FDI) inflows na mambo ya International Trade performance.

Wito wangu kwa Mheshimiwa Rais, mpe waziri wako wa Biashara ndugu Mwijage siku 5 kama si siku 7 afanye yafuatayo 

1. Wizara hii ifanye overhaul ya ICT system kuanzia kwenye ngazi ya kata mpaka taifa ili iwe rahisi kufungua biashara na isichukue dakika 10 kwa sabau vitambulisho vyote vipo kwenye sistem. Mtu hahitaji ku saini makaratasi luluki kufungua kampuni. Kinachohitajika ni ID na malipo hivyo kila mwenye sim ya mkononi aweze kufungua kampuni ONLINE na kuregister na TRA pia kusichukue dakika 10 mtu kupata TIN number.


2. Bandari na airport bado ni tatizo, clearence ya mizigo isichukue zaidi ya dakika 30. hii ni mizigo ya ndani na nje. Yote haya hayahitaki luluki ya makaratasi kama kweli ICT systems zinafanya kazi...


3. Ondoeni urasimu wa visa za wawekezaji kuungia na kutoka bila longolongo. As a matter of fact ondoeni visa ya watalii kabisaa....pesa za visa zitabaki kwenye matumizi wa hawa watalii wakiiingia ndani. Lakini muhimu zaidi kuna umuhimu wa kuondokana na urasim kwa wageni na wataliii....


4. Mwambieni waziri wa Ardhi Lukuvi aache blah blah....property registration ifanywe online kwa kila mwenye kitambulisho na data zote wekeni ONLINE ili iwe rahisi mtu ku search na kujua kama nyumba au kiwanja au shamba ni la nani, limelipiwa kodi au la na limelipiwa kiasi gani na pia kama mu akitaka kulipa afanye malipo ONLINE kwa kutumia sim yake bila mlolongo wa foleni na mianya ya rushwa kwenda wizara au ofisi ya ardhi.


5. Ondoeni kodi zisiko na kichwa wala miguu kwenye Renewable energy sources kama solar, wind na zinginezo. Point hapa ni ku unleash private sector waweze kuinvest kwenye power generation kwa kutumia hizi nguvu mbadala. issue ilipo ni kuweka wazi PPA na rates na kama vipi binafsisheni part ya TANESCO lakini uweli ni kuwa bila reliable electricy ni ngumu kufika hapo tunakotaka kwenda. As it is TANESCO hawana pesa za kuinvest in power generation lakini si vibaya tukapata workable solution ambayo itakuwa na manufaa kwa wawekezani na serikali na wananchi...


6. Rahisisheni upatikanaji wa documentation za contruction permits.


7. Ombi maalum kwa rais: Iachie wizara ya TAMISEMI ifanyekazi na wapeni wananchi kwenye ngazi za kata, wilaya na mkoa nguvu za kujiamulia matumizi mambo yao na hasa pesa zitokanazo na vyanzo kwenye maeneo husika. Dar/Dodoma iache kuingilia mipango maendeleo na investment huko mikoani

8. Mheshimiwa Rais PIGA MARUFUKU huu ushirikina wa kukimbia na moto wa mbio za mwenge na pesa za ziende kwenye maendeleo na wananchi wafanye kazi

Chanzo JF

Msanii Aliyeshika Kichwa Bandia cha Rais Trump Kikiwa Kimekatwa Kufunguliwa Mashtaka..!!!

$
0
0

Msanii mchekeshaji raia wa Marekani mwanamama Cathy Griffin alieonekana live kupitia kipindi cha TV kinachorushwa na CNN akiwa ameshika kinyago kinachofanana kabisa na kichwa cha rais Trump huenda akashtakiwa kutokana na kile kilichotajwa kama kuvuka mipaka ya Uhuru wa habari.

Msanii huyo mwenye umri wa miaka 57 alionekana akiwa amebeba kinyago cha Rais Trump akiwa amekatwa kichwa, Jambo ambalo limezua hasira miongoni mwa watu wengi wakiwemo wapinzani wa Trump nchini marekani.

Baada ya Tukio hilo Kituo cha TV cha CNN kilitangaza kumfukuza kazi msanii huyo na kukifuta kipindi chake mara moja 

Baadhi ya watu maarufu nchini Marekani akiwemo rais Trump mwenyewe wamekilaani kitendo hicho na kusema ni dhihaka na udhalilishaji kwa familia za Wanajeshi na baadhi ya waandishi wa habari wa Marekani waliochinjwa na Kikundi cha kigaidi cha ISIS

Taarifa iliyotolewa na Idara ya Ulinzi wa Rais nchini marekani (Secret Service) imesema uchunguzi umekamilika na wanajiandaa kumfikisha mahakamani Cathy Griffin.

Msikiti Wagoma Kuuzika Mwili wa Kijana Aliyefanya Shambulio la Manchester na Kuuwa 22..!!!!

$
0
0

Msikiti Mkubwa katika Jiji la Manchester wagoma kuuzika na kujihusisha na mazishi ya kijana aliyefanya shambulio lililouwa watu 22 na kujeruhi wengine wengi. Mpaka sasa taarifa zinasema mwili wa kijana huyo bado upo katika chumba cha kuhifadhia maiti.

Maafisa wanaohusika mazishi pia wamekataa kuuzika mwili wa kijana Salman Abedi ikiwa ni kuepusha mwili wa kijana huyo kuzikwa katika ardhi ya jiji la Manchester.


=====
One of Manchester's biggest mosques has refused to bury the body of the Manchester terrorist who killed 22 last week. It is thought his body remains unburied councils, funeral directors and now the city's mosques, refuse to deal with it. According to the Daily Mail, the bomber's body remains in a morgue outside Manchester.

The Manchester Evening News has reported that the city’s authorities are reportedly doing "everything in their power" to stop him being cremated, buried, or laid to rest in any way in the Greater Manchester area.

A source told the Manchester Evening News: "Just like Ian Brady, every effort is going in to making sure that there is not a chance Abedi can be buried or cremated in Greater Manchester."

Inquest proceedings will soon be heard, and the disposal of his body will be decided by the coroner. A source told the MEN that his body has never been kept in the same place as his victims. Now, at least one mosque is taking the same course of action as the council.

Manchester Central Mosque, one of Manchester's largest Muslim funeral providers, has said it will have nothing to do with the body. A spokesman from the place of worship told the Evening Standard that its executive committee had met and agreed not to inter the remains of Abedi if his family made a request.

Afisa Wa Ngazi Za Juu Wa Marekani Aionya Tanzania..!!!!

$
0
0

Kaimu Balozi wa Marekani Nchini, Virginia Blaser ameonya juu ya dalili za kudumaa kwa Uwazi, Haki za Binadamu na Utawala wa Sheria.

Pia Kaimu Balozi huyo amesema kuwa Serikali wakati ikiwa inajisifu kwa kupambana na rushwa inapaswa kuhakikisha pia Uwazi, Haki za Binadamu na Utawala wa Sheria unaimarika.


In Summary
Ms Virginia Blaser, the Chargé d’Affaires at the US Embassy in Tanzania and the East African Community (EAC), spoke on Thursday in an exclusive interview with The Citizen, ostensibly her last before the end of her four-year tour of duty in the country.
Dar es Salaam. A top US diplomat has expressed concern about “discouraging signs” of backtracking on transparency, human rights and the rule of law in Tanzania, which if unchecked could undermine business and the country’s place as a key player in regional security.

Ms Virginia Blaser, the Chargé d’Affaires at the US Embassy in Tanzania and the East African Community (EAC), spoke on Thursday in an exclusive interview with The Citizen, ostensibly her last before the end of her four-year tour of duty in the country.

She said while the government should be applauded for the positive path it had taken in fighting corruption, it should also sincerely take stock of its record on transparency and the rule of law, and pay attention to some worrying retrogressive signs, especially on the private sector.

“Tanzanians need a future, and that won’t come from development partners; that is not going to come from government jobs; it needs to come from a broad-based, healthy, strong, confident private sector,” she said.

“And instead, I see some discouraging signs on the private sector side; and I worry about what path that will take Tanzania.” She added that she would like to see more US companies in the country, but that would depend on a “more open, and transparent, and supportive private sector environment”.

Ms Blaser, currently the most senior diplomat at the US embassy in Tanzania, spoke barely two months after the US-based Symbion Power took the Tanzania Electric Supply Company (Tanesco) to the International Court of Arbitration in Paris, seeking $561 million settlement for breach of contract.

In March, the firm filed an application for arbitration at the court after efforts lasting over a year to amicably resolve the dispute about the validity of the 15-year Power Purchase Agreement (PPA) failed.

The disputed PPA was signed in December 2015, handing the US firm a long-term contract to supply Tanesco with 112 MW through the firm’s Ubungo gas-powered generators until December 2030. However, on January 26, 2016 Tanesco wrote to Symbion, saying the PPA was put on hold.

“I think it’s really important when a US company signs an agreement, that both parties receive the goods and services and payments that have been agreed upon… that is an issue of rule of law; that’s an issue of transparency,” said Ms Blaser. “I think there can be some improvements there.”

She also called for the creation of a private sector environment that will help Tanzanians create more companies and jobs for the country’s robust youth population, so they can have a future after graduating.

“The United States has invested a lot to help see that future… we believe that the health, the safety, the security of Tanzanians, the growth, positive growth of Tanzania is in our interest as friends, trade partners and a longtime ally.”

She referred to the current statistics the government has released showing that exports of manufactured goods went down in the last quarter, saying there is a need to pay attention to those signs.

“It’s just a quarter, but we need to pay attention to these signs and look to see how we can create a private sector environment, how do we encourage entrepreneurism so that Tanzanians can create companies, and create jobs that as youth get out of schools they have a future.”

According to the latest Bank of Tanzania (BoT)’s Monthly Economic Review (MER), exports of manufactured goods dropped significantly by 37.5 per cent to $879.7 million during the year ending March 2017 from $1.408 billion during the year ending March 2016 as manufacturers grappled with a lack of funds to boost their operations.

The BoT report and Ms Blaser’s comments on the negative signs also come in the wake of a widespread outcry from across the business spectrum over the tight liquidity situation and lack of support credit to the private sector.

A significant number of companies have closed, scaled down operations and laid off workers in recent months. They cited poor business, mainly arising from the slow implementation of public investment. The International Monetary Fund has also recently warned that the cloud of uncertainty about the government’s economic strategies could adversely affect growth.

However, Ms Blaser said the US would continue supporting Tanzania to stay on course because it “has invested a lot” to help create a future for the country’s robust young population and university graduates.

But she quickly pointed out that the onus is on government to create a more enabling environment for business through transparency and respect for the rule of law.

“I see a scenario, which we, as friends, as partners, as trade partners, people who count on Tanzania for its engagement in the region, you know, its help with security in the region, and peace building in the region… there needs to be a Tanzania that has a democratic, forward-meaning, positive path. And there are a lot of signs that that’s the way Tanzania will go as we are still on these crossroads.”

Kutana na Mtaalamu wa Tiba Asili Ostadh Khamis Kutoka Mombasa..Yupo Tanzania....Anatibu Magonjwa Yafuatayo

$
0
0

Kutana na OSTADH khamis kutoka Mombasa Kenya kwa sasa yupo Tanzania nibingwa watiba za asili:

Miguu kuuma miguu kufagazi nakuwaka moto
Unashida na mchumba au pesa haikai muone haraka 
Kurudisha mpenziwako alie kukimbia ndani ya siku (3)
Dawa ya ( LIMBWATA) kumtawala mpenzi wako kwasababu maalumu   
Pete ya bahati inayo endana nanyota yako itakayo kuletea pesa bila mashart yeyote
Kuongeza uume saizi uipendayo 
Dawa ya ulijali 
Dawa yakuongeza hips
Kumuliki Mali isiokuwa namasharti yeyote 
Kurudisha Mali iliopotea au kudhurumiwa ndani yasiku(3) 
Napia OSTADH KHAMIS anafunga kesi nakupata hakiyako kwa haraka 
Dawa ya mvuto pia inapatikana mvuto Wa biashara kuuza Mali yako kwa haraka 
Kuzuiya chuma ulete na kupandishwa cheo kazini PAMOJA na kusafisha nyota njoo ufunguliwe vifungo ulivyo fungwa

Call+255718746825 au +255754765246 WhatsApp IMO +255783708487

Rais Kenyatta Atangaza Adhabu ya Kifo kwa Atakaye Haribu Treni yake

$
0
0
Muda mchache jana baada ya kuzindua Miundombinu ya Reli ya Kisasa Jijini Nairobi, Rais Uhuru Kenyatta alindika kwenye ukurusa wake wa Twitter kuwa "Sitosita kusaini adhabu ya kifo kwa yeyote atakaye patikana na hatia ya kuharibu miundombinu ya reli, kwakuwa atakuwa amehujumu uchumi"



Itatumia muda wa saa nne na nusu kutoka Mombasa hadi Jiji la Nairobi,, Awali wasafiri walikuwa wakitumia takriban saa 8 kwa njia ya basi,


Reli hiyo ina urefu wa kilomita 472 ambapo treni zitakuwa zikisafiri kwa kasi ya wastani ya kilomita 120 kwa saa na kutumia muda wa saa nne na nusu kutoka Mombasa hadi kufika Jiji la Nairobi, ikiwa ni safari ambayo ilikuwa ikitumia takriban saa 8 kwa njia ya basi.


Baadhi ya wananchi walioshuhudia uzinduzi huo wamesema treni hiyo itakuwa mkombozi kwao kwa madai kuwa hapo awali walikuwa wanapata shida kubwa katika kusafiri kutoka Mombasa hadi Nairobi.

"Hakika ni develepment ya maana sana kwa maana upande wa transport kitambo ilikuwa inachukua muda mwingi sana kwa gari kutoka Mombasa hadi Nairobi lakini hii nasikia inachukua masaa manne so itakuwa ni imetupeleka 'far with other developed courients" alisema Samuel Umma kutoka kaunti ya siaya

Jack Wolper Afunguka Ndoa yake na Ali Kiba

$
0
0
Staa wa filamu za Kibongo asiyepungukiwa mbwembwe kwenye mapenzi, Jacqueline Wolper.
 Stori: Ally Katalambula, Amani, Habari

UTAMU wa ubuyu ukae chini na umung’unye taratiiibu! Staa wa filamu za Kibongo asiyepungukiwa mbwembwe kwenye mapenzi, Jacqueline Wolper, amefunguka kuwa ilibaki kidogo tu aolewe na msanii wa Bongo Fleva, Ali Kiba kama wasingekuwa mastaa maishani mwao.

Gazeti la Amani  lilizungumza na Wolper ambaye alidai kuwa penzi alilolikuta na kulipata kwa Kiba ni penzi ambalo hawezi kulisahau maishani mwake.

ASIMULIA PENZI LA KIBA LILIVYO

“Ni mtu mwenye upendo wa kweli, anajua kujali, anathamini na ninaamini moyo wangu ulimpenda kwa dhati.

WALIVYOKUTANA

“Sikumbuki ilikuwa mwaka gani, ninachokumbuka ilikuwa ni Mtaa wa Lindi uliopo Kariakoo wala sikumbuki nilienda kufanya nini siku hiyo.

MUDA WALIO-DATE

“Ni muda mrefu, maana imekuwa siku nyingi. Kipindi hicho wote hatukuwa na majina makubwa (mastaa) kama tuliyonayo sasa. Tulipendana na tulikuwa na matarajio makubwa mbeleni.

KUTENGANA KWAO

“Baada ya kuwa mastaa, kila mmoja akajiona mkubwa zaidi ya mwenzake, ndoto na matarajio yote yakatoweka, polepole penzi likaanza kuyeyuka na hatimaye kufa kabisa, ingawa hatujakoseana kihivyo kiasi cha kushindwa kusalimiana kama wengineo. Naamini tulipendana lakini usupastaa ukazidi nguvu ya penzi letu.

ANACHOKIKUMBUKA KWA KIBA

“Mengi nakumbuka, kubwa ni upole wake pamoja na unyenyekevu, hii ni tofauti na wanaume wengine ambao nimewahi kukutana nao.

KUHUSU KURUDIANA NAYE

“Swali hilo naomba nisilijibu na ibaki kuwa siri yangu, ingawa ni muda mrefu na kila mtu ana mambo yake mengi zaidi,” anasema Wolper
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images