Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Chadema Watangaza Kushusha Bendera Nusu Mlingoti Nchi Nzima..!!!

0
0

Kufuatia kifo cha mmoja wa Waasisi wa CHADEMA, Mzee Philemon Ndesamburo Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, (CHADEMA), Dkt. Vincent Mashinji, ametoa maelekezo kwa watendaji nchi nzima kupeperusha bendera nusu mlingoti

Mashinji ametoa maelekezo hayo leo wakati akiongea na Waandishi wa Habari Makao Makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam na kusema bendera zinapaswa kupeperushwa nusu mlingoti hadi mwili wa kiongozi huyo utakapopumzishwa katika nyumba yake ya milele. 

"Chama kitashiriki katika msiba huu kwa heshima zote kumuenzi mmoja wa waasisi wa siasa za mabadiliko ya kweli na Uhuru wa kweli nchini, msiba huu ni msiba wa CHADEMA, ni msiba wa Watanzania, ni msiba wa Taifa letu kutokana na mchango mkubwa wa Mzee wetu kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa nchi yetu, Mhe. Ndesamburo ndiye aliyekifadhili Chama kwa mara ya kwanza kwa kukipatia ofisi eneo la Kisutu jijini Dar es salaam" amesema Dkt. Mashin

‘Mjane wa JPM’ Aangukia Pua Tena Kortini..!!

0
0

Kwa mara nyingine mama aliyeangua kilio mbele ya Rais John Pombe Magufuli (JPM) akidai kudhulumiwa mirathi ya marehemu mumewe, ameangushwa tena mahakamani, baada ya Mahakama ya Wilaya ya Tanga kutupilia mbali kesi dhidi ya wakili aliyekuwa akimtuhumu kushiriki kumdhulumu.

Mama huyo, Swabaha Mohamed (Shosi), aliangua kilio mbele ya JPM, kwenye maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini, Februari 2, akimtuhumu wakili Alfred Akaro wa Tanga kwa kula njama na kughushi wosia wa marehemu Mohamed Yusufu Shosi.

 Mbali na wakili huyo pia mama huyo aliwatuhumu watendaji wa vyombo vya utoaji haki kuwa wanamnyima haki. Mama huyo alidai pia kutishiwa maisha. 

Kutokana na madai hayo, Rais Magufuli alimwagiza aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP  Ernest Mangu  kumpa ulinzi mama huyo.

 Pia, alimwagiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP),  kushughulikia matatizo yake na ikiwezekana waihamishe kesi yake ya mirathi kutoka Tanga.

Kutokana na tuhuma hizo dhidi ya Wakili Akaro, wakili huyo na mwenzake Abubakari Shaaban, ambaye ni mfanyakazi wa  familia ya marehemu Shosi walifunguliwa kesi ya jinai katika Mahakama ya Wilaya ya Tanga.

Katika kesi hiyo walikuwa wakikabiliwa na mashtaka ya kughushi wosia wa marehemu Shosi na kuuwasilisha kwa familia ya marehemu Shosi.

 Hata hivyo, katika hukumu iliyosomwa jana na hakimu Lutala aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo, alitupilia mbali tuhuma zilizokuwa zimetolewa na mama huyo dhidi ya wakili huyo na mwenzake

Dunia Imeishaaa..Wanaume Mashoga Watangaza Kutarajia Kupata Mtoto..Mmoja Abebeshwa Mimba kwa Njia ya Kupandikizwa..!!!

0
0

Two gay dads have spoken of their delight as they prepare to welcome their first biological child.

Biff Chaplow and Trystan Reese are already adoptive parents to two young children Riley and Hailey, but the couple had always longed for a baby of their own.

Trystan, who is transgender, first managed to conceive in 2016 but they suffered the heartbreak of a miscarriage at six weeks. They had considered waiting up to a year before trying again.

But because of the medical complications of Trystan having to go off testosterone they decided to continue. And the married couple, who live in Portland, Oregon, have confirmed Trystan is due to give birth in the summer.

Tahadhari..Epukana na Zaidi ya Magonjwa 100 ya Saratani ya Mwili kwa Kuacha au Kupunguza Matumizi ya Bidhaa za Plastiki..!!

0
0

MAISHA ya mwanadamu kwa  sasa yanategemea mno  bidhaa za plastiki katika kuhifadhia  mizigo mbalimbali ikiwamo vyakula, maji na mafuta ya kula.

Licha ya kutumika katika matumizi mbalimbali katika kuhifadhia vitu, imebainika kuwa plastiki ina madhara makubwa katika matumizi ya binadamu.


Utafiti uliofanywa na Jumuiya ya Madaktari wa Marekani ulitoa tahadhari kuhusu matumizi ya vyombo vya plastiki vinavyotumika kufungashia na kubebea vyakula.

Wanasayansi hao wanasema plastiki ina madhara makubwa endapo ikikutana na joto kali na kutoa kemikali iitwayo BPA(bisphenol A).

Mwaka jana, Serikali kupitia Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na  Mazingira, January Makamba alipiga marufuku moja kwa moja, utengenezaji, usambazaji, uingizaji na matumizi ya mifuko ya plastiki nchini kuanzia mwaka huu.

Makamba alisema mifuko ya plastiki imekuwa na changamoto kubwa ya mazingira kwa kuwa sehemu kubwa ya mifuko hiyo hutolewa bure na kusambaa ambapo husababisha  mafuriko na athari nyingine kubwa za kimazingira.

Anasema ofisi yake inakamilisha majadiliano ndani ya serikali na baadae kuwahusisha wadau kuhusu dhamira ya kupiga marufuku moja kwa moja matumizi ya mifuko ya plastiki nchini.

Anasema serikali itatoa muda kwa waliojiajiri na kuajiriwa kwenye biashara ya mifuko ya plastiki kujiandaa kuacha shughuli hizo na itawezesha mazingira ya utengenezaji na upatikanaji wa vifungashio mbadala.

 “Tumetuma wataalamu wa serikali katika nchi zilizofanikiwa kwenye jambo hili ili kujifunza namna bora ya kulitekeleza jambo hili,” anasema Makamba.

Nchi ya Rwanda na  Zanzibar zimefanikiwa katika upigaji marufuku wa mifuko ya rambo baada ya kuonekana ni chanzo cha uchafuzi wa mazingira na mafuriko kutokana na mifuko hiyo kuziba katika mitaro.

Licha ya serikali kupiga marufuku matumizi ya mifuko plastiki, vyombo vya plastiki aina ya sahani, bakuli, vikombe vimeendelea kutumika huku viwanda vikizidi kuvizalisha kwa wingi hivyo kufanya afya ya mwanadamu kuwa hatarini kukumbwa na magonjwa ya saratani.

Walter Miya ni Makamu Mwenyekiti wa Asasi ya Marafiki wa Watoto wenye Saratani Tanzania, anasema plastiki imetengenezwa kwa kemikali zaidi ya 200 ambazo  zinaweza kusababisha aina 100 za saratani.

Anasema toka matumizi ya plastiki yazidi kuongezeka nchini, ugonjwa wa saratani nao umeongezeka  hasa kwa upande wa akina mama  ambapo ugonjwa huu huharibu ukuaji wa mfumo wa uzazi hususani kwa watoto ambao bado hawajazaliwa, mabadiliko ya kijenetiki, matatizo ya kushindwa kuona, uyeyushaji wa chakula tumboni kuwa wa tabu au kutokamilika na ini kushindwa kufanyakazi vizuri.

Anasema kutokana na utafiti mdogo walioufanya inaonesha kuwa asilimia 60 ya saratani zimesababishwa na matumizi ya vifaa vya plastiki.

“Watu wengi wanatumia vifaa vya plastiki bila kujua madhara yake, ukienda majumbani utakuta wanawake wengi wanachemsha maji na kuyahifadhi katika ndoo za plastiki yakiwa bado ya moto.

“Baada ya muda ukija kuchunguza ile ndoo utakuta ina mabaka mabaka maana yake imeshatoa kemikali nyingi na athari hutoiona kwa muda huu, mpaka ifike miaka 10 au 15 na ndio maana huwezi kugundua saratani yako imesababishwa na nini,” anasema Miya.

Anasema pia kuna kinamama ambao hutumia mifuko ya rambo kufunikia wali wakati wa kupika ili uweze kuiva haraka bila kujua kuwa mifuko  hiyo ina athari kubwa kutokana na kemikali zilizopo kuingia katika chakula hicho.

Miya anasema jamii inapaswa kupunguza matumizi ya plastiki au kutumia zilizo na viwango ambavyo hazitoleta madhara na kwa upande wa wachemshao maji wanapaswa kusubiri hadi yapoe ndipo wamimine katika ndoo.

“Licha ya jitihada zinazoendelea kufanywa na watu mbalimbali, bado jamii haina uelewa kuhusiana na vifaa hivyo vya plastiki.

“Hivi karibuni kuna taarifa ilisambazwa katika mitandao ya kijamii kuwa watu wasitumie vikombe vya plastiki, sahani, bakuli na hata mifuko ya rambo katika matumizi ya vyakula, lakini ukipita mitaani utakuta bado wanaendelea navyo,” anasema Miya.

Anasema kuna vitu vingi ukiviangalia unaweza ukaogopa ila huwezi kuvikimbia ni kuangalia ni namna gani tunaweza kuvipunguza ili athari ya saratani isizidi kuongezeka.

“Binafsi natembea na kontena langu la aina ya glass ili kuweza kuhifadhia chakula pindi ninapoenda kununua , nimeamua kutembea nalo kutokana na mama lishe wengi kutumia vyombo vya plastiki katika kuwekea chakula,” anasema.

 “Kutokana na kukithiri kwa matumizi ya  plastiki wakati serikali ilipiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki, tunahitaji sera na sheria dhidi ya matumizi ya vifaa hivi.

“Inatakiwa iwepo sera ya kutoruhusu kusafirisha maji bila kuwa na vifaa vinavyodhibiti joto kama wafanyavyo wanaposafirisha maziwa,” anasema Miya.

Anashauri iwepo sheria ya kuwadhibiti wauzaji wa  maji juani kuanzia asubuhi hadi jioni kutokana na kupata kemikali nyingi inayotoka kwenye chupa za plastiki kwa sababu ya kuwapo juani kwa muda mrefu. 

Somo la Kujifunza Kutoka kwa Muammar Gaddafi..!!!

0
0

Mwaka 1955 Libya iliingia mkataba wa kuchimba mafuta na kampuni ya Kimarekani iliyokuwa inaitwa 'Libyan American Oil Company' wakati huo Libya ikiwa chini ya Mfalme Idris. Baadaye Marehemu Muhammar Gaddafi akafanya mapinduzi na kuitawala Libya.

Muammar Gaddafi alikuta Libya ipo kwenye mikataba ya ajabu ya Mafuta na kampuni hiyo ya USA ambayo ilikuwa inanufaisha wazungu kuliko Libya na siku moja kwa hasira sana na uchungu wa kuona nchi yake inanyonywa kwa neno MKATABA alisema... "WANANCHI WA LIBYA WALIISHI MIAKA 5,000 BILA OIL HAKUKUWA NA TATIZO KWA HIYO WANAWEZA KUACHANA NA OIL MPAKA NITAKAPOREKEBISHA MIKATABA UPYA ILI WANUFAIKE NA MAFUTA YAO" 

Muammar Gaddafi kwa ujeuri mkubwa akafanikiwa kubadilisha mikataba na kwa mara ya kwanza Libya ikaanza kuchukua 51% ya mapato ya mafuta yake kutoka 25% ya mikataba uchwara na akafanikiwa kutaifisha uchimbaji na utafutaji mafuta Libya kwa 100% ikawa chini ya Taifa lake.Libya ikawa Taifa la kwanza Duniani kufanikiwa kuwa na Majority Share ya Mafuta yake ingawa pia Mabadiliko hayo ya sheria yaliingiza Libya katika migogoro mkubwa sana na Kampuni ya Libyan American Oil Company kiasi cha kufungua kesi dhidi ya Libya kama nchi na baadaye Libya kulazimishwa kuilipa kampuni hiyo pesa nyingi na mahakama ya Dunia.

Bado Muammar Gaddafi hakujali alisema.... "HATA TUKIWALIPA MAPATO YOTE TUNAYOYAPATA LAKINI CHA MSINGI NI PESA YA MAFUTA YETU SIO YAO KAMA ILIVYOKUWA"

Baadaye Libya ilifanikiwa kumaliza deni na kuwa Taifa la kwanza Afrika kufanikiwa kuwa na Social Security ya kuwatunza wazee wote nchini humo.

Leo Tanzania miaka 55 ya uhuru bado tunahangaika na wachimba madini yetu, leo Rais Magufuli anataka tuanze kufikiria kama Muammar Gaddafi kuna wanaopinga na kutaka tuendelee kuwalamba miguu Wazungu. Hapana tunaweza kufanya aliyoyafanya Muammar Gaddafi. Yaani Tunaweza kuchimba madini yetu kama tutaachana na Dollar na kununua 'TECHNOLOGY' ya kuchimba madini yetu wenyewe.

Rais Magufuli kanyaga twende, asiyetaka akae pembeni! ..

Fahamu Machache ya Kushangaza Usiyoyajua Kuhusu Mnyama Mamba..!!!

0
0

MAMBA ni mnyama anayekula nyama, huweza kuishi nchi kavu lakini maisha yake kwa kiasi kikubwa hupendelea kukaa majini, tofauti na fikra za watu wengi ambao hufikiri mamba anazaa ukweli ni kwamba huwa anataga, ambapo kwa wastani hutaga mayai 35 mpaka 50, najua utajiuliza sasa huyu kiumbe anaatamia vipi wakati maisha yake ni ya heka heka? Mamba hutengeneza kiota kwa kuchimba pembezoni mwa mto au ziwa na kisha kufukia mayai yake mpaka hapo ambapo mayai yatakapokuwa tayari.

Mayai yake yanapokuwa tayari kwa kutoa watoto, mamba husikia sauti na akiyatoa mayai hayo katika kiota watoto wake hujitoa wenyewe, yaani watoto hutumia nguvu binafsi na kuvunja gamba la yai, kisha hutoka katika ulimwengu mpya, kazi ya mama kwa wakati huo inakuwa ni kuhakikisha anawachukua wanawe na kuwapeleka majini na huwabeba kwa kutumia mdomo wake.

Wakati huu baadhi ya wanyama ambao huliwa na mamba nao hulipiza kisasi, mfano kenge, mijusi wakubwa pamoja na ndege, humtegea anapopeleka watoto wa awamu ya kwanza wale wanaosalia hujeruhiwa vibaya, au kubebwa kama chakula na wanyonge wa mamba. Hujisikia tabu kiasi kwamba anapoibuka katika maji huwatazama kwa jicho la shari.

Watoto wa mamba ukiwaona katika udogo wao wanashangaza, hutokaa ufikirie kwamba ndio hao wafikapo ukubwani hufikia urefu wa futi 10 na zaidi, uzito wa kilo zaidi ya 600, ni viumbe ambao huonekana wadogo unaweza kuhisi labda ni kenge.

Katika hatua za mwanzo watoto wa mamba hutumia samaki kama chakula chao, kwa kadri muda unavyokwenda watoto hao nao huanza kuwinda wanyama na zoezi hilo huwa jepesi kwa kuwa idadi kubwa ya wanyama hufuata maji katika makazi yao, mnyama mkubwa ambaye maisha yake huathiriwa na mamba ni nyumbu na hii ni kwa sababu pindi wanyama hawa wafikapo mtoni hukamatwa kwa urahisi kwa kukosa tahadhari ya kutosha.

Kwa taarifa yako, mamba ni miongoni mwa wanyama wakubwa duniani, meno yake yamejipanga kwa mfano wa msumeno, ana macho makubwa, ngozi ngumu na mkia mrefu ambao humsaidia katika kuwinda, hupendelea kukaa kwenye maji lakini jua linapochomoza na linapo karibia kuzama, ndio wakati hutoka majini na kukaa nchi kavu.

Ajabu ya mnyama huyu ni moja, pamoja kwamba wanyama wanaokula nyama tu ndio huishi muda mfupi, lakini yeye maisha yake ni marefu anaweza kufika miaka 50 na zaidi. Namna unayoweza kuwatofautisha kwa jinsia zao ni muonekano wao, dume huwa mrefu zaidi ya jike pia huwa mzito zaidi jike.


SIFA ZAKE ZA KIPEKEE 


1. Ni mnyama ambaye ana uwezo mzuri na mkubwa katika kuyamudu maji hasa kuogelea.

2. Huishi katika maji baridi na makazi yake huweka sehemu zisizo na kina kirefu.

3. Mashambulizi yake ni ya kushtukiza, anaweza akawa anakuvizia na usijue kwamba yupo jirani kukukamata.

4. Ana akili na mjanja mno anapomuona mnyama ambaye hana uwezo wa kumkimbiza, hujifanya amelala usingizi ili uingie katika maji.

5. Pia anaweza kukukamata hata akiwa amelala usingizi, jicho lake moja huacha wazi anapolala na lina uwezo wa kufikisha taarifa ya kila kinachoendelea.

6. Huwa na nguvu maradufu awapo kwenye maji, ni vigumu kumshinda katika mapambano naye ndani ya maji.

7. Hapatani na simba kabisa kwa kuwa ndiye mnyama ambaye hupenda kumbughuzi awapo mapumzikoni, hivyo wawili hawa wanapokutana nchi kavu huwa kama watani.

8. Ni mwepesi wa kuzira kitu, hapendi kujitesa anapokutana na changamoto huamua kukaa pembeni.

Kutana na Dave Murphy ..Jamaa Anayekunywa Mkojo Badala ya Maji..Adai Umemsaidia Kupunguza Uzito..!!!

0
0

BABA wa watoto wawili amefichua kwamba hunywa glasi ya mkojo wake mwenyewe kila siku na anausifu kwa kumwezesha kupunguza uzito kwa kilo 50.

Kwa kipindi cha miaka sita iliyopita, Dave Murphy (54) mkazi wa Basildon, Essex nchini Uingereza amekuwa akinywa mkojo wake, anaosema kuwa unahusika si tu kupungua kwa unene wake bali pia kumletea mwonekano wa ujana na siha njema.

Dave, ambaye aliweza kupunguza uzito kutoka kilo 127 hadi kilo 76 kwa tiba hiyo, pia anaamini mkojo unaweza kuwa suluhu ya uhaba wa chakula duniani na kuweza kubana matumizi kwa wanaofuja fedha baa.


Sehemu kubwa ya siku, Dave hutumia pesa kidogo kwa mlo, ambao pia unahusisha chungwa moja na glasi mbili za mkojo wake mwenyewe.

Kile anachopenda zaidi ni sehemu ndogo ya chips kutoka duka lililo jirani, ambazo huagiza mara tatu kwa wiki.

Wakati fulani mwaka 2012 kwa kipindi cha siku 30, Dave hakula kitu kingine chochote zaidi ya mkojo wake.

Dave pia hutumia mkojo wake kunawa uso na kuogea na anasisitiza kuwa mkojo ni bidhaa muhimu ya kuzuia hali ya kuzeeka.

Dave anaeleza: “Baada ya kunywa mkojo wangu, nilijihisi kuwa na afya na mkakamavu kuliko nilivyokuwa kabla na nilipunguza uzito wa kilo 50.

“Zaidi ya hayo, sihitaji fedha zaidi ili kuishi kwa sababu ninachotumia ni mkojo niunywao, ambao unanifanya nisiwe na haja ya kula chakula kingi.

“Kama wanadamu, hatupaswi kutumia kiasi kikubwa kama hicho cha chakula. Mkojo unaweza kutusaidia kupunguza kile tunachohitaji kuingiza tumboni – maana ndani yake kuna kila kitu binadamu anachohitaji.

“Watu wengi wanadhani mkojo wakiunywa ni uchafu lakini si hivyo. Kiuhalisia ni msafi kuliko maji.

“Mkojo ni taswira ya kile ambacho mwili wako unahitaji lakini umezidi zaidi kimanufaa.

“Kwa mfano, iwapo una maambukizo kisha mkojo wako utakuwa na silaha za kupambana nazo. Huboresha mfumo wa kinga na hata kuponya pumu iliyonisumbua kwa muda mrefu wa maisha yangu.

“Tiba ya mkojo si kuhusu kuunywa tu, unaweza kuogea na kujipaka. Ni bidhaa inayozuia ngozi kuzeeka – mikunjo na makunyazi yaliyokuwamo ngozini mwangu usoni na kwingineko mwilini imetoweka tangu nilipoanza kutumia mkojo wangu kuogea na kunawia.

“Unawea kuutumia hata kuondoa maumivu au muwasho na kama vile ya macho.

“Mkojo ni tiba kwa kila kitu. Iwapo watu watabadili mtazamo wao kuhusu tiba hii, hakika kisha kila mtu atashuhudia maajabu na manufaa makubwa ya maji haya kutoka mwilini mwetu.”

Dave alianza matumizi ya mkojo Mei 2011 baada ya awali kusita sita kabla ya kuhudhuria mkutano kuhusu tiba ya mkojo.

Je, kweli mkojo hufanya kazi?

Tiba ya mkojo inaelezwa kurudi nyuma nyakati za Biblia na nyaraka za kihistoria zinaeleza namna ulivyokuwa ukiponya majeraha yaliyoambukizwa na manufaa yake pia yameandikwa katika riwaya za Kihindi na Kichina.

Mkojo kwa kiasi kikubwa ni msafi, ukiwa na asilimia 95 ya maji na asilimia tano ya virutubisho kama vile protein, vitamini na madini.

Madini hayo ni pamoja na urea, chloride, sodiamu, potassiamu na chuma.

Baada ya kula na mmeng’enyo wa chakula kufanyika, maji pamoja na mabaki yaliyomeng’enywa husafirishwa katika kibofu cha mkojo.

Maji hayo ndiyo husaidia kufanya usafirishaji wa mabaki hayo hadi katika kibofu cha mkojo.

Aidha, wakati wa mchakato wa usagishaji,  maini hushughulika na sumu na kuziondoa.

Kisha damu inaenda katika figo, ambako huchujwa tena na vitu visivyohitajika mwilini hukusanywa katika mchanganyiko wa maji ambao hutoka kama mkojo.

Lakini Dk. Rob Hicks alisema: “kwa miaka mingi watu wengi walidai uwapo wa faida za kiafya kwa kunywa mkojo wao, lakini kwa kadiri nijuavyo hakuna ushahidi wa kisayansi kuunga mkono madai hayo.

“Figo ni mfumo fanisi wa uchujaji wa kuondoa taka mwilini na hiyo ni kazi yake ya asili. Binafsi naamini kuna njia nzuri zaidi na isiyoleta kinyaa za kuufanya mwili kuwa na afya ikiwamo kutovuta sigara, kula mlo bora na kutoruhusu msongo wa mawazo.”

Lakini Dave anakumbushia jinsi alivyokuwa na uzito mkubwa huku akiwa na afya mbovu ikiwamo kusumbuliwa na pumu tangu utotoni, kitu ambacho tangu atumie mkojo kimetoweka.

Anaeleza: “Miaka sita iliyopita nilikuwa na uzito mkubwa na mgonjwa sana, nilitumia steroids kuikabili pumu.

Nikiwa nafanya kazi kama mtaalamu wa program za kompyuta katika Jiji la New York, mlo wangu ulitisha. Ungeniona nikila chocolate siku nzima achilia mbali chakula cha mchana na usiku.

“Wakati nilipotania kwa kuzungumzia tiba ya mkojo na wafanyakazi wenzangu wakati wa tamasha moja, kiukweli sikuwa na lengo hilo. Lakini mwishowe  tukaamua tujaribu!”

Tangu hao nikaanza kunywa glasi ya mkojo mara mbili kwa siku. Pamoja na kuwa muwazi kuhusu hilo, anakiri awali alisita na kuona kinyaa kunywa mkojo wake mwenyewe kabla ya kuzoea.

Dave anasema tangu hapo akazoea na kuona ni jambo zuri na matokeo ya unywaji mkojo wake ni kupungua uzito, kuwa na siha ya ujana pamoja na maradhi ya pumu kumtoka.

Ukiachana na hilo mkojo mbali ya kuelezwa kuwa na manufaa kiafya, wanayansi na watafiti Uingereza wameshavumbua nguvu za mkojo katika kuzalisha nishati ambayo inaweza kuchaji simu kwa muda wa dakika 25 na pia kumwezesha mteja kutuma ujumbe na kuperuzi intaneti.

Mbali ya hilo hivi karibuni watafiti nchini Ujerumani wamedai kutengeneza pombe kutokana na mkojo.

Hizi Hapa Sababu Kuu Sita (6) Ni Kwanini Unatakiwa Kuacha Kutumia Sukari Kwa Wingi...!!

0
0

Kwa sasa vipo vyakula vingi sana ambavyo vimekuwa na sukari na tunavitumia karibu kila siku. Kwa bahati mbaya au nzuri vyakula hivi vya sukari vimekuwa vikipendwa na wengi bila ya kujali madhara yake kiafya yakoje.

Wengi wetu hatujui sana kiundani hasa pale tunapotumia vyakula vingi vya sukari, ni madhara gani ambao yanaweza kukutokea zaidi, tumekuwa tukijua juu juu tu kwamba ukila vyakula vya sukari vinaweza kukuletea shida hii au ile bila kuwa na uhakika sana.

Kwa sababu hiyo ndani ya makala haya ya afya, tutakueleza kinagaubaga sababu ya msingi ni kwa nini unatakiwa uache kutumia sukari kwa wingi mwilini mwako na ikiwezekana kuacha kabisa baadhi ya matumizi ya vitu vyenye sukari nyingi sana.

1. Sukari nyingi mwilini ni kisababishi cha magonjwa.

Matumizi ya sukari kwa wingi ni chanzo kimojawapo cha kuongezeka kwa uzito, lakini si hivyo tu sukari inapokuwa nyingi mwilini inaweza kukupelekea kupata magonjwa kama vile magonyjwa ya moyo na kuongezeka kwa shinikizo la damu jambo ambalo ni hatari kwa afya yako kwa kiasi kikubwa.

2. Sukari nyingi mwilini inapunguza uwezo wa kuona.

Mara nyingi wanaoutumia sukari kwa wingi sana au wale amabao viwango vya sukari vimeongezeka mwilini mwao,  moja ya madhara yake kwa baadae ni kutokuona vizuri. Hilo hutokea kwa sababu,  sukari inapokuwa nyingi hupelekea lensi ya jicho kuongezeka na matokeo yake matatizo ya macho huanza kujitokeza kwa mhusika.

3. Sukari nyingi huozesha meno.

Bila shaka hili umeshawahi kulisikia au kuliona. Na mara nyingi hutokea sana kwa watoto, meno huweza kuoza baada ya matumizi ya sukari kwa wingi. Kinachotokea sukari huzalisha bakteria wenye sumu ambapo hao huweza kuharibu meno na kupelekea kuweza kuoza kabisa.

4. Sukari nyingi inapoteza uwezo wa mwili kukabiliana na magonjwa.

Wale wote ambao sukari inakuwa imeongezeka miili yao inakuwa haina uwezo wa kukabiliana na magonjwa. Unajua ni kwa nini? iko hivi,.. unapokuwa na sukari nyingi mwilini inatabia ya kuua seli nyeupe ambazo husaidia kupambana na magonjwa. Kwa hali hiyo ndio maana watu wenye visukari hawaponi vidonda kwa sababu kama hii.

 5. Sukari nyingi mwilini zinasababisha mwili kuonekana umeezeka.

Kila sukari inapokuwa nyingi mwilini, inazalisha kemikali ambazo baadae kemikali hizo hupelekea mwili wako kuanza kuoneana kama vile umezeeka. Hapa njia pekee ya kuondokana na hali hiyo ni kupunguza matumizi ya sukari. Vinginevyo utaanza kuonekana kikongwe.

6. Sukari nyingi husababisha viungo vya mwili kulegea.

Zipo ‘joints’ kama vile za miguu hasa pale unapokuwa unatembea zinakuwa zinachoka upesi na kulegea kama mwili wako una sukari nyingi. Hali hii hutokea sana hasa kwa wagonjwa wenye kisukari. Hii ninhali ambayo huwakuta wengi wagonjwa wa kisukari na inakuwa ni hali inayosumbua.

Mwisho kabisa hapa sina shaka mpaka unafika mwisho wa makala haya utakuwa umeelewa hatua za kuchukua na hiyo haitoshi ni vyema ukamshirikisha na mwingine makala haya ili aweze kujifunza na kundokana na matatizo ambayo pengine yangemkuta.

Ni wako rafiki katika mafanikio,

IMANI NGWANGWALU,
0628 92 98 16,

Magufuli - Nina Laini za Mitandao Yote ya Simu,,na Ninazitumia Zote ..!!!

0
0

Rais John Magufuli amesema anajivunia kuwa na mitandao mingi ya simu ambayo inamsaidia kuwasiliana bila kero wakati wowote.

 Amesema hayo jana Juni Mosi, wakati wa uzinduzi wa mfumo wa ulipaji kodi kwa njia ya kielektroniki.

“Mimi nina mitandao yote ya simu, nina Tigo, Airtel, Vodacom na hata TTCL, mtu akinitafuta huku Airtel,akanikosa ninaweza kuweka Tigo, ili mradi ninatambalika kila mahali,” amesema

 Pia amesema, mitandao hiyo ya simu inamsaidia kupata taarifa mbalimbali zinazoendelea nchini na duniani.

Hata hivyo, Rais amezitaka kampuni za simu kuhakikisha zinalipa kodi ili serikali isikose mapato yake.

Pia Rais amesema hataki kuona taasisi nyingine zinajenga vituo vya ukusanyaji taarifa (Data centre)na badala yake  fedha hizo zitumike kwa ajili ya shughuli nyingine za maendeleo.

 “Data Centre kama hii ni mkombozi mwingine wa kupunguza kero mbalimbali, kwa sababu ukijaza vocha yako uko Zanzibar, ukinunulia vocha yako Kigoma au Moshi, hiyo pesa inakuja TRA, hakuna mabishano” amesema

 Rais amesema hayo leo Juni Mosi, wakati wa uzinduzi wa mfumowa wa serikali wa ulipaji kodi kwa njia ya kielektroniki ambako pia alitembelea kituo hicho cha ukusanyaji taarifa.

 Amesema chombo hicho kina faida yake na hivyo akawaomba watanzania, wawekezaji na wafanyabiashara kukitumia chombo hicho kwa manufaa ya taifa zima.

Malkia wa Nguvu: Wampa Pole Zari..!!!

0
0

Washindi wa Tunzo ya Kimataifa ya "Malkia wa Nguvu" kwa umoja wao wamemtumia salamu za rambirambi The Boss Lady Mrs. Diamond Chibu kuwa kufiwa na mumewe was zamani DR. Ivan. Kiasi cha rambirambi walichotoa kitatangazwa baadae.

Ratiba ya Awali, Mazishi ya Mzee Philemon Ndesamburo...!!!

0
0

Kwa wale ambao wangependa kujua kuhusiana na ratiba ya mazishi ya kumpumzisha mzee wetu Mh Philemon Ndesamburo ambaye alikuwa mbunge wa Jimbo la Moshi mjini kwa tiketi ya CHADEMA kabla ya kustaafu ni kwamba ipo hivi : 


Tarehe 5/06 siku ya Jumatatu katika uwanja wa Mashujaa Moshi ndipo ndugu jamaa na marafiki na wageni watapata fursa ya kutoa heshima za mwisho.


Tarehe 6/06 siku ya Jumanne ndiyo siku rasmi ya kumpumzisha mzee, ibada ya mazishi inategemewa kufanyika nyumbani kwake kdc-kiboroloni na ndipo atakapozikwa.


Tutaendelea kujuzana kila litakalojiri.

Inna Lillahi Wa Inna Ilayhi Rajiun.

Ukweli Mchungu ..Daimond Mtazame Zari kwa Jicho la 3..!!!!

0
0

Kabla ya kuanza kueleza ni kwa nini nimeamua kuandika uzi huu,natoa angalizo(Sina team so tusitukanane)Hoja hujibiwa kwa hoja.

Niende direct kwenye mada,Binafsi nieona watu wakimsifia Zari na kumuita mwanamke Shujaa ama shupavu,lakini nimekuja kugundua kuwa mwanamke wa kweli hapaswi kuwa na haiba kama ya Zari.Nasema hivi kwa sababu zifuatazo...

1) Amefiwa na mtu aliyeishi naye pika pakua kwa zaidi ya miaka 10 lakini alikuwa na nguvu ya kupost picha mtandaoni(Siyo moja)na captions juu wakati bado mazishi hayajafanyika

2) Jana kwenye kipindi cha Amplifier alihojiwa na Millard na alikuwa anaonge kwa kujiamini na sauti yake haikusikika kuwa na majonzi hata kidogo(Note:Angekuwa mwanamke mwingine angekuwa bado yuko down sana na pengine angeshindwa hata kuongea kwenye Interview)

3) Ni opportunist Mzuri sana,Kama aliweza kuzaa na Ivan watoto watatu na akapata ujasiri wa kumuacha na kwenda kwa wanaume wengine,,basi hata Dai anaweza kukuacha vile vile(Anachojua yeye ni kuwa once yo dating a rich guy,future yako na watotot wako ni ya uhakika)Mfano halisi ni sasa,aliitwa Zari the boss lady sababu ya jeuri ya fedha za Ivan,now ataitwa Zari the Don sababu ya jeuri ya fedha za Ivan pia

4) Siamini ndani ya moyo wangu kama Zari alimpenda Diamond kama Diamond,naamini ile fame ya Dai ndo iliyomvuta yeye kuwa na Dai(Na kwa hili amefariki,kwa sasa Zari ni moja ya wanawake maarufu sana Africa)So Dai watch out you never know siku fame ikiisha,je atastick up na wewe au atamove on huku akiendelea kupata child support?Ukitaka kuprove hili,jiulize ni kwa nini kipindi kile mna mgogoro mpaka mama Dai akampost Wema(Japo Maza alifanya uswahili kwa hili) Hujiulizi ni kwa nini Zari alikimbilia kushika mimba nyingine wakati Tifa alikuwa bado mdogo sana?

5) Katika malezi nimeona ana mazuri yake kama vile kuwafundisha watotot wake kujitegemea wakiwa bado wadogo lakini nimegundua pia siyo mama mzuri pia,Mama anayejisheshimu hasa wa KIAFRIKA hawezi kupiga picha anakulana denda au kashikwa ta*k*o kisha akapost mtandaoni wakati watoto wake n wakubwa,na kibay zaidi anayemshika hivyosiyo baba yao na ni mtu ambayee hawezi kuwa baba yao hata katika maisha halisi zaidi kuwa kaka yao. 

Namalizia kwa kusema hivi,Japo Zari ana roho ngumu lakini ana mazuri yake pia,Huyu mwanamke ni msafi,unaweza ukathibitisha hili kuptia picha zake,Sebule yake ni safii,Wardrobe yake poa kabisaa lakini hata yeye anajipenda sana jao she's acting like an 18 girl wakati ni mama mtu mzima anayepaswa kukaa akibehave ili wanae wajifunze kutoka kwake.

Chanzo FB

Ushauri kwa Diamond Kuhusu Kurasa Zake za Social Media..!!!

0
0

Aiseee Kwanza Daimond mimi ni Fan wako sanaa Hapa Duniani....kinachofanya ni kupende Ni vile unavojituma na kuto kukata tamaa kwako!!

Kabla sijakushauri nilicho taka nikushauri kwanza Kabisaaa nikupongezeee Kwa moyo mweupee....'KUTO KWENDA KWENYE MSIBA WA IVAN!' Hapo ulicheza kama Pele Mond...Huo ni uanaume na mwanaume msimamo...Japo mpango wako ulikuwa ni kwenda ila ratiba zilipishana lakini mimi nilifurahi ambavyo hukwendaa...

Kifupi ni kuwa insta na social media zingine zote zingechafukaaaa kwa Maneno ya shombo na ya kejeri! Msiba wa IVAN wewe ulikuwa haukuhusu kwa namna yoyote ile Labda KIBINADAMU lakini kivingine vyovyote vile Ule msiba wewe ulikuwa haukuhusu buanaa...Kwanini umshobokee mtu asiekuhusu? Hamjawahi hata kuongea nae wala kuonana WHY? Wewe ilikuwa ni kumliwaza zari tuu......

Sasa nije kwenye Kilichonileta...Diamond wewe sasa hivi ni msanii mkubwa sanaaa una followers wengi duniani kote! Unachoshindwa ni kimoja tuuuu....Kumanage Account zako za Social media....Mzee unapost sanaaaaaaaa.....unapost hadi vitu visivyokuwa na maana.....

Unatoa support hata kwa vitu ambavyo msanii kama wewe hukutakiwa kutoa....Wewe ni Bonge la msanii inabidi ukipost kitu watu waseme kweli leo nimepitia insta Ya Diamond kapost....Ulinikera sana ulivyompost gwajima Who is Gwajima? Kwako wewe.....mbali na huyoo yapo mengi tuu Diamond unapost ambayo hukutakiwa kufanya hivyoo

Chukulia akina Christian Ronaldo, akina Chris Brown, Akina Niki Minaji na mastaa wengi wanavyomanage account zao kwa siku post moja Tuuu......Sasa Mzee baba wewe kwa siku unaweza hata weka post 15 what For? Eti Diamond?.....

Tusiende mbali angalia akina Davido na Wizkid wakipost unasema kweli wamepost Sasa na wewe badirika sio kila kitu lazima upost vingine unaweza ukaacha Sisi Team zako tukapost....

Unatutumia kwenye group sisi tutapost. Wewe Account yako inabidi ziwe na Uzitooo.....Now unaenda kufikia Followers Million 4 insta lakini ukiendelea na mtindo wako wa kupost post hovyo hvyooo utakuwa sawa na Mwenye followers laki Moja!

Pia wewe ni staaa inabidi usionekane onekane hovyohovyo sio kidogo tuu watu wamekuona kidogo wamekuona...wewe ni wa kwenda South unakaa hata Mwezi...Yaani Tusikuzoee... Wewe Sasa hivi yaani usitake mazoea

Najua kibongo bongo watasema umefulia sijui nini lakini achana nao Jifunze kuishi kistar. Bora waseme hata unawaringia sawa... Wewe kuhangaika na kuishi kwa tabu huko nyuma hizo kawaida sasa tunaangalia ulipo..Wewe ni wa kuringa sasa sio kila kitu kwako Ndio....

Sio kila mtu anakuhoji hovyohovyo hapana, achana nao wanaokuhoji wawe wana hadhi ya kukuhoji yaani ukiwa Interview kweli upo kwenye interview na unajieleza kidogo kwa muda mfupii sio ujielezeee kama unatafuta mchumba Redioni wewe ni Star Ishi kistar Diamond

Ni hayo tuuu Diamond....

DIAMOND ISHI KISTAR

Chanzo JF

Kimenukaa..Rais Mstaafu Mkapa Atajwa Kwenye Sakata la Mchanga wa Madini..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo Ijumaa 2/6/2017..!!!

Ndesamburo Kuzikwa Jumanne ..Ataagwa Viwanja vya Mashujaa..!!!

0
0

Mbunge wa zamani wa Moshi Mjini (Chadema), Philemon Ndesamburo aliyefariki dunia jana atazikwa Jumanne ijayo.

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Aman Golugwa ameliambia gazeti hili kuwa Ndesamburo atazikwa katika makaburi ya familia nyumbani kwake eneo la Mbokomu.

Golugwa amesema Jumatatu, Juni 5 kwenye viwanja vya mashujaa mjini Moshi wananchi watapata fursa ya kuaga mwili wa Ndesamburo.

Katibu huyo amesema wakati wa kuaga mwili wake kutakuwa na salamu kutoka kwa viongozi wa Serikali, vyama vya siasa, viongozi wa dini na wawakilishi wa makundi mbalimbali.

Golugwa amesema msiba wa Ndesamburo umewagusa wengi nchini kutokana na mchango wake katika kukuza misingi ya demokrasia ya vyama vingi na kuchangia ustawi wa sekta ya utalii.

Kimenukaa..JPM Aaagiza Kampuni Hizi za Simu Kufutiwa Usajili Nchini Mara Moja..Tigo Ikiwemo..!!!!

0
0

Rais John Magufuli ameiagiza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuyafuta makampuni ya simu yatakayoshindwa kujiunga na Soko la hisa la Dar es Salaam.

Rais Magufuli amesema hayo jana Juni Mosi, wakati akizindua mfumo mpya wa ulipaji kodi kwa njia ya kielektroniki, Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Pia ameziagiza taasisi za Serikali na kampuni binafsi kujiunga na mfumo wa ukusanyaji mapato ili kuiwezesha Serikali kupata kodi bila uonevu kwa upande wowote.

Rais Magufuli amesema dhamira ya Serikali ni kukusanya kodi bila kuwepo kwa malalamiko kutoka upande wowote.

Pia amepiga marufuku wizara na taasisi nyingine za Serikali kuanzisha vituo vya taarifa kwa kuwa vilivyopo ni vingi na wakati huo vinatumia gharama kubwa katika kuanzisha.

“Data Centre kama hii ni mkombozi mwingine wa kupunguza kero mbalimbali, kwa sababu ukijaza vocha yako uko Zanzibar, ukinunulia vocha yako Kigoma au Moshi, hiyo pesa inakuja TRA, hakuna mabishano” amesema

NB.Hadi hivi sasa ni Vodacom Pekee Ndio Wanajulikana kuwa wamejisajili na soko la hisa ,makampuni mengine aidha yapo kwenye mchakato au hayajajisajili kabisa

Aliyewakatakata Watalii Mapanga Zanzibar Akamatawa na Polisi..!!!

0
0

Polisi imemkamata mtuhumiwa anayedaiwa kuwajeruhi watu sita kwa kisu mjini Zanzibar Mei 29.

Mtuhumiwa huyo alikamatwa jana saa 8:30 mchana akituhumiwa kuwajeruhi watu hao katika mgahawa wa Lukmaan uliopo Mkunazini mjini Zanzibar.

Katika tukio hilo, raia wa kigeni wanne na Watanzania wawili walijeruhiwa maeneo mbalimbali ya miili yao kwa kuchomwa kwa kisu.

Mtuhumiwa anashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Madema.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Hassan Nassir Ali amethibitisha kushikiliwa kwa mtuhumiwa huyo.

Amesema wanaendelea kumhoji ikiwa ni hatua za awali za upelelezi.

Serikali Yajitwisha Zigo la Madeni ya ATCL..!!!

0
0

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt Philip Mpango amesema serikali itaendelea kuliboresha shirika lake la ndege nchini ATCL ikiwa ni pamoja na kuchukua madeni yake mbalimbali ili kuhakikisha shirika hilo linafanya kazi kama ilivyokusudiwa .

Dkt Mpango ametoa kauli hiyo wakati akijibu hoja za wabunge waliochangia bajeti ya Wizara hiyo ya fedha kwa mwaka wa Fedha 2017/2018.

“Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali amekamilisha ukaguzi wa shirika letu la ndege, ilikukamilimisha mizania ya kampuni, lakini tumeamua kuyachukua madeni yote ya ATCL ili kuweza kusafisha hiyo mizania,” alisema Dkt Mpango.

“Muheshimiwa Rais ameteua bodi mpya ya wakurugenzi ambayo inaweledi katika mambo ya usafirishaji wa anga, menejimenti mpya lakini kuhakikisha shirika linakuwa na mpango wa biashara wa muda wa kipindi cha kuanzia mwezi Julai mpaka mwezi Juni mwaka huu.”

Kesi ya Wema ya Matumizi ya Madawa ya Kulevya Yafikia Hatua Hii Mahakamani..!!!

0
0

Malkia wa filamu nchini Wema Sepetu Alhamisi hii amepanda tena katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, Dar es Salaam kwa mara ya tatu kusikiliza kesi yake inayomkabili ya tuhuma za kutumia na kukutwa na madawa ya kulevya.

Mrembo huyo alisindikizwa na baadhi ya waigizaji wenzake akiwemo Neema Ndepanya. Hata hivyo madam Sepenga amekana shtaka hilo na kesi hiyo imeahirishwa mpaka Julai 14 ndio itasikilizwa tena.

Wema alitiwa mbaroni na jeshi la polisi mapema mwezi February mwaka huu na kusota rumande kwa siku saba huku akituhumiwa kukutwa na msokoto wa bangi nyumbani kwake baada ya kufanyiwa msako mkali.

Kutana na Mtaalamu wa Tiba Asili Ostadh Khamis Kutoka Mombasa..Yupo Tanzania....Anatibu Magonjwa Yafuatayo

0
0

Kutana na OSTADH khamis kutoka Mombasa Kenya kwa sasa yupo Tanzania nibingwa watiba za asili:

Miguu kuuma miguu kufagazi nakuwaka moto
Unashida na mchumba au pesa haikai muone haraka 
Kurudisha mpenziwako alie kukimbia ndani ya siku (3)
Dawa ya ( LIMBWATA) kumtawala mpenzi wako kwasababu maalumu   
Pete ya bahati inayo endana nanyota yako itakayo kuletea pesa bila mashart yeyote
Kuongeza uume saizi uipendayo 
Dawa ya ulijali 
Dawa yakuongeza hips
Kumuliki Mali isiokuwa namasharti yeyote 
Kurudisha Mali iliopotea au kudhurumiwa ndani yasiku(3) 
Napia OSTADH KHAMIS anafunga kesi nakupata hakiyako kwa haraka 
Dawa ya mvuto pia inapatikana mvuto Wa biashara kuuza Mali yako kwa haraka 
Kuzuiya chuma ulete na kupandishwa cheo kazini PAMOJA na kusafisha nyota njoo ufunguliwe vifungo ulivyo fungwa

Call+255718746825 au +255754765246 WhatsApp IMO +255783708487
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images