Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Kaburi la Ivan Kufukuliwa? Police wa Interpol Waingilia Kati Kuhakikisha Alikufa Kweli

$
0
0
Kimenukaaa Kifo cha Ivan kina utata! Police wa InterPol wanataka kufukua kaburi la Ivan kuhakikisha kama Ivan yumo ndani..Gazeti moja la South Africa wameandika kuwa kutoka na kifo cha Ivan kuwa na utata Kitengo cha Polisi wa Kimataifa Interpol watahakikisha kwa kufukua kaburi...



Emmanuel Mbasha Adaiwa Kuwa na Msongo wa Mawazo..Kisa Flora Mbasha....Afanya Hilo Kumkumbuka

$
0
0

Kwenye ukurasa wake wa Fb,Emma Mbasha amemtakia heri mkewe wa zamani Frola,kwa kuandika "Happy Birthday Mrs Daud Kusekwa"

Watu wa karibu wa Emmanuel Mbasha wanasema amekuwa na msongo wa mawazo kwa muda mrefu mara baada ya kutalikiana na mkewe.Hali hii imemfanya kuwa anajitahidi kupost hapa na pale matukio anayofanya yenye unasaba na starehe(kula bata) ili kuonyesha kuwa yupo "Ok"

Ila ukweli ni kuwa anateseka,na hasa ukizingatia alijijengea mazingira ya "umariooo",hali inayomfanya kuhangaika huku na kule

Familia ya Ivan Matatani Kwa Kufukia Pesa ya Uganda Katika Kaburi la Ivan Don

$
0
0
Wanasheria nchini Uganda wameamua kuifikisha familia ya Ivan Mahakamani kwa makosa ya kuzika pesa halali za Jamhuri ya Uganda katika kaburi la ndugu yao Ivan. Kwa nchi yoyote kitendo hicho hakikubaliki kwani pesa hizo zingeweza kutumika katika shughuli zingine na kukuza uchumi wa nchi.

Kitendo hicho kinakuja baada ya marafiki wa Ivan kumwaga mamilioni ya pesa ndani ya kaburi la Ivan kama njia ya kumuaga rafiki yao aliyekuwa maarufu kwa matumizi makubwa ya pesa.

Wanasheria wakiongozwa na Tugume Gideon wa Human Rights Defenders Association Uganda wamesema hawakufurahishwa na kitendo cha RICH GANG cha kuzika mamilioni ya pesa ndani ya kaburi, na kwa vile ni kinyume cha sheria,

wameamua kwenda mahakamani kuomba kaburi la Ivan lifukuliwe, pesa zitolewe zikafanye shughuli nyingine na waliohusika washitakiwe kwa kuharibu kwa makusudi alama ya taifa.

JE Una Tatizo la Maumbile Madogo, Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo?

$
0
0

JE, UNA TATIZO LA MAUMBILE MADOGO, NGUVU ZA KIUME NA KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA?
Maumbile madogo ya uume, kupungukiwa nguvu za kiume pamoja na kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa wanaume limekuwa likiwaathiri wanaume wengi kutokana na sababu mbali mbali na kusababisha kushindwa kujiamini ktk mapenzi. Tatizo hili limesababisha kuvurugika kwa ndoa nyingi na mahusiano.
@Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo yakiwemo:-
1.Uume kulegea wakati wa tendo
2.Kukosa hamu ya tendo la ndoa
3.Kuwahi kufika kileleni
4.Uume kuchelewa kusimama baada ya round ya kwanza.
5.Kuchoka sana baada ya round moja n.k.
🍉🌿🍎🍍🍒🍓🍀🍅🍅
PATA BIDHAA HIZI ZILIZOTENGENEZWA KWA MIMEA NA MATUNDA ZISIZO NA KEMIKALI WALA MADHARA. ZIMETHIBITISHWA KIAFYA.
👇👇👇👇👇👇👇
1.HANDSOME UP ni kifaa chenye uwezo wa 99 % kuongeza uume (size unayohitaji) na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo hata mara 3 @130,000/=
Kwa Bidhaa hizi na nyingine kama:-
5.Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi @130,000/=
7.Kutengeneza shepu (hips, makalio na mapaja) @200,000/=
8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni @120,000/=
9.Kuwa mweupe na soft mwili mzima bila kuacha sugu 120,000/=
10.Kurudisha usichana (bikra) @120,000/=
Wasiliana nasi kwa (+255)
0767447444 au 0714335378.
NB: Matokeo ni uhakika na garantii na upate risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii.
Follow us
@Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr

Bangi Yazua Mtafaruku Bungeni...Yachafua Hali ya Hewa Leo

$
0
0
Leo wakati mkutano wa saba , kikao cha 40 kikiendela bungeni Dodoma umeibuka mjadala wa dawa za kulevya aina bangi baada ya baadhi ya wabunge kusema kuna vitendo vinavyofanywa na baadhi ya polisi nchini vinatokana na polisi hao kuwa wamelewa bangi.

Katika mjadala huo Mh Spika Job Ndugai naye alichomekea kuwa huwa anasikia watu wanasema bangi zinaongeza nguvu, hivyo naye alitaka kujua hizo bangi zinaongeza nguvu za aina gani, huki akiwauliza wabunge ambao wanatokea maeneo ambayo bangi imekuwa ikiripotiwa sana.
Kufuatia mjadala huo kuendelea alisimama Mbunge Esther Matiko Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mara na kusema yeye mwenyewe huwa anaona polisi wakichoma bangi katika maeneo hayo na kudai huenda baadhi ya vitendo vinavyofanywa na polisi wetu ni kutokana na kuathirika na moshi wa bangi wakiwa wanachoma bangi hizo. Lakini katika ufafanuzi wa Naibu Waziri wa Afya alisema polisi hao wao huwa hawaathiriki na moshi huo.

"Jamani tunapojadili juu ya suala la madawa ya kulevya si jambo la mdhaa, ni kwamba polisi wanapokwenda kuchoma bangi mashambani huwa wanajifunika vifaa maalum lakini hata kama hawajifuniki vifaa hivyo bado ile bangi ikiingia kwenye miili yao itaondoka ndani ya siku 30 kwani inageuka na kuwa chumvi na kutoka kwa njia ya mkojo na jasho. Lakini kwa watu ambao wanatumia kila siku yaani leo, kesho, kesho kutwa na kuendelea wao wanakuwa ni clonic wa dawa hizo" alisema Kigwangalla

Licha ya Naibu Waziri wa Afya kutoa ufafanuzi juu ya uchomaji wa bangi lakini Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Joakim Mhagama alisimama na kutoa ufafanuzi wake pia akisema kuwa polisi hawajaathirika na bangi kutokana na namna ambavyo huwa wanachoma bangi hizo kwa kufuata utaratibu mzuri.

"Mh. Spika vikosi vya polisi vinavyofanya utekeketezaji wa bangi, zipo njia nyingi wanatumia kuteketeza bangi hizo, kwanza wakiwa wanafanya zoezi hilo huwa wanaangalia uelekeo wa upepo lakini pia maandalizi mengine ya vifaa vyao vya uteketezaji wa bangi, aina ya mafuta yanayotumia kwenye kuchomea bangi hizo vinawafanya kuwa salama kabisa, kwa hiyo siyo kweli kwamba likitokea tatizo kwenye jeshi la polisi kwamba polisi wetu wameathirika na matumizi ya bangi, kwani polisi wetu ni weledi na wanafanya kazi kwa kufuata utaratibu na sheria" alisisitiza Mhagama 

Kwa kumalizia mjadala huo Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema kuwa nchi nzima na viongozi wamesikia juu ya jambo hilo hivyo wanapaswa kuwa makini katika utekelezaji wa mambo hayo.

Mabasi ya Mwendo Kasi ni Kichefuchefu...Nikki Mbishi Awashtaki Kwa Magufuli

$
0
0
Rappa, Niki Mbishi amemtaka Rais John Pombe Magufuli kutupia jicho katika mradi wa mabasi yaendayo kasi (DART) kwamba kama asipofanya hivyo kuna uwezekano mkubwa mradi huo ukafa bila kutimiza malengo yaliyokusudiwa.


Nikki anayetamba na 'hit' ya 'Dada pumzisha mwili wako' amefunguka hayo kupitia ukurasa wake wa twitter baada ya kuona mapungufu kutoka kwenye mradi huo ambapo ma -bus yamekuwa yakijaza idadi kubwa ya watu na kudai ni kupitiliza kiwango kilichokusudiwa.

"Hadhi ya mwendokasi ni 'level seat' siyo kushonana kama embe toka kibada Mzee Magufuli tazama hilo, mradi unakufa 'soon'. Mwendokasi watu wanajazana kama '3rd class train' ya India yatadumu kweli
?"aliandika Nikki Mbishi

Je Wajua Kifo cha Mwalimu Nyerere Ni cha Utata..Daktari Wake na Mtoto Wake Mkubwa Watoa Siri Hii Nzito..!!!

$
0
0

Tangu mwaka jana juhudi za chini chini zilianza kufanywa na baadhi ya Watanzania ambao hawajaridhika kuwa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alifariki kifo cha kawaida.
Wito sasa umeanza kutolewa wa kuhakikisha kuwa kifo hicho kinachunguzwa kama inavyofanywa sasa kwa aliyekuwa Kiongozi wa Palestina, Yasser Arafat, ambaye taarifa za karibuni zinasemekana kuwa aliuawa kwa kulishwa sumu.

Baadhi ya wafuasi wa Mwalimu Nyerere, wamekuwa wagumu kuamini kama kweli Mwalimu alikufa kifo cha kawaida, kutokana na ukweli kwamba maradhi yaliyomuua - saratani ya damu (leukemia) - hayana desturi ya kuua kwa kasi kama ilivyotokea kwake.

Samuel Kasori, aliyekuwa Katibu Myeka wa Mwalimu, amezungumza na JAMHURI na kusema; “Mwalimu anakuwa kwenye rekodi ya kufa haraka sana kwa ugonjwa wa saratani ya damu. Ugonjwa huo huua taratibu, lakini kwa Mwalimu ilikuwa tofauti kabisa. Kuna nini kilichotokea? Sitaki kuhoji sana, lakini naamini kuna siku Watanzania na walimwengu wataujua ukweli.”

Maneno ya Kasori yanaendana na ya Mwalimu James Irenge (Mwalimu wa Baba wa Taifa), aliyoyatoa mwanzoni mwa mwaka jana baada ya mvutano wa kisiasa kati ya Rais mstaafu Benjamin Mkapa, na Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (Chadema).

Baada ya kauli ya Mbunge Nyerere kumtaka Mzee Mkapa aeleze chanzo cha kifo cha Mwalimu, Mwalimu Irenge alijitokeza na kusema amefurahishwa mno kusikia kuwa amepatikana kiongozi jasiri wa kuhoji namna Mwalimu alivyougua hadi kufariki dunia.

“Mfikishieni pongezi nyingi Mbunge Nyerere... huyo mtoto amefanya jambo la maana sana kuuliza jambo hili, miaka yote nalia kwa sababu naamini Mwalimu aliuawa.

“Kwa kuwa suala hili limeulizwa hadharani, sasa nipo radhi kufa. Nikifa nitakwenda moyo wangu ukiwa na furaha kwa sababu nimekuwa nikijiuliza ni nani anayeweza kuhoji namna Mwalimu… mwanafunzi wangu alivyokufa,” alisema Mwalimu Irenge.

Kauli hiyo ya Mwalimu Irenge ya Machi, mwaka jana haikupita bure, kwani Julai, mwaka huo, aliaga dunia mjini Musoma na kuzikwa kijijini kwake Busegwe Nyanza wilayani Butiama.

Mwalimu Irenge alianza kumfundisha Mwalimu Nyerere katika Shule ya Mwisenge kuanzia mwaka 1934 hadi 1936. Mwalimu Irenge aliwahi kuhojiwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) na kusema, binafsi hakuafiki Mwalimu kupelekwa kutibiwa nchini Uingereza.

Alisema alipinga kwa sababu alijua Waingereza si marafiki wa kweli wa Mwalimu, kwa kuwa aliongoza harakati za kuwang’oa katika Tanganyika na katika mataifa mengine, hasa Afrika Kusini na Zimbabwe, ambako Serikali ya nchi hiyo ilikuwa ikiunga mkono utawala wa kidhalimu wa Wazungu wachache.

Mwakyusa na kifo cha Mwalimu

Profesa David Mwakyusa alikuwa daktari wa Baba wa Taifa tangu mwaka 1987 hadi Oktoba 14, 1999, siku Mwalimu alipofikwa na mauti jijini London, Uingereza, kutokana na ugonjwa wa saratani ya damu (leukemia).

Katika mahojiano aliyopata kufanya muda mfupi baada ya kifo cha Mwalimu, Profesa Mwakyusa alisema walimjulisha Mwalimu kila kitu kuhusu ugomjwa wa leukemia. Hata hivyo, kwenye maelezo yake anathibitisha namna ugonjwa huo ulivyobadilika ghafla na kumsababishia mauti, ilhali kila alipopimwa ilionekana hakuwa na sababu za kuanza matibabu mapema.

Swali: Mwalimu alikuwa anajulikana kwa Watanzania kama mtu mwenye afya nzuri. Wewe kama daktari wake unasemaje kuhusu afya ya Mwalimu kwa ujumla.

ibu: Mwalimu alikuwa mtu mwenye afya nzuri kwa ujumla, ukiacha matatizo madogo madogo ninayoweza kuyaita ya kawaida. Alikuwa na desturi ya kufanya mazoezi na alikuwa mtu anayefuata masharti na ushauri aliokuwa akipewa na madaktari.

Daktari wa kwanza aliyekuwa anamhudumia Mwalimu baada ya Uhuru alikuwa Profesa Mhonoli. Kuanzia mwaka 1979 alihudumiwa na Profesa Makene akisaidiwa na Profesa Mtulia na mimi. Mwalimu alipostaafu mwaka 1985 alibakia daktari mmoja tu, Profesa Makene. Makene alistaafu mwishoni mwa mwaka 1987 na tangu wakatu huo mimi ndiye niliyekuwa daktari wake hadi alipoaga dunia tarehe 14 Oktoba 1999.

Swali: Baada ya kulazwa katika Hospitali ya Mtakatifu Thomas jijini London, ndipo Watanzania tulipotangaziwa kwamba Mwalimu aligundulika kuwa na ugonjwa wa kansa ya damu mwishoni mwa mwaka 1998. Je, ugonjwa huu unafikiri aliupataje?

Jibu: Ugonjwa wa kansa ya chembe chembe nyeupe za damu, huwapata watu wenye umri mkubwa na utafiti wa kisayansi haujafanikiwa kutambua ni kitu gani hasa kinacholeta kansa hii. Kwa kawaida, kansa hii haioneshi dalili wakati inapoanza na wengi wanagundulika kuwa nayo bila kuihisi.

Wagonjwa wengi wanaishi zaidi ya miaka miwili bila kuhitaji matibabu, ni pale tu ambako kansa hii inapoathiri kazi ya chembe chembe nyingine nyeupe au nyekundu ndipo matibabu yanapoweza kufikiriwa.

Kinachohitajika ni mgonjwa kuonwa na daktari mara kwa mara, ili athari hizi zikionekana matibabu yaanze mara moja.

Swali: Baada ya kugundulika kwa ugonjwa wa Mwalimu, ulimshughulikia namna gani?

Jibu: Baada ya Mwalimu kugundulika kuwa na kansa mwezi Agosti 1998, alielezwa kuhusu ugunduzi huo na kuambiwa kuwa wakati ule ugonjwa ulikuwa haujafikia hatua ya kuhitaji matibabu. Alielezwa haja ya kwenda kupimwa mara nyingi zaidi kuliko ilivyokuwa kawaida yake na kwamba hapakuwa na sababu ya kubadilisha mwenendo wa shughuli zake.

Ratiba tuliyopewa ilimfanya Mwalimu arejee London, Novemba 1998, na majibu yaliyoonesha kuwa hakukuwa na sababu ya kuanza matibabu. Aidha, mwezi Januari 1999 alipimwa tena kwa mara nyingine ikaonekana hakuna haja ya kuanza matibabu.

Mwezi Mei 1999 alikwenda tena London akapimwa. Aliambiwa hakukuwa na sababu ya kuanza matibabu na akapewa tarehe nyingine mwezi Agosti, 1999.

Safari hii hitilafu zikaonekana katika damu. Hitilafu hizo zilionesha ulazima wa matibabu ya kansa kuanzishwa. Mwalimu alishauriwa kurudi London, Desemba 1999. Lakini hali yake ikabadilika kabla ya kurejea nyumbani hadi ikabidi alazwe katika hospitali ya Mtakatifu Thomas ambako alipoteza maisha yake.

Swali: Mmoja wa watoto wa Mwalimu amedai kuwa familia haikujulishwa kuhusu ugonjwa wa Mwalimu. Kuna ukweli wowote katika madai hayo?

Jibu: Mwalimu mwenyewe aliwaeleza baadhi ya wanafamilia yake waliokuwa karibu naye, kuhusu maradhi yake na mimi nilijua hivyo kwa vile hao aliowaeleza waliniambia na wakawa wakiniuliza maswali kuhusu ugonjwa wake.

Swali: Ukiwa daktari wa Mwalimu kwa muda mrefu, uliyekuwa ukisafiri naye mara nyingi na kuwa naye karibu, je, unaweza kuzungumzia lolote kuhusu maisha yake?

Jibu: Mara nyingi tukiwa pamoja aliuliza maswali mengi kuhusu ugonjwa wake na alisoma vijitabu kuhusiana na ugonjwa huo. Nadiriki kusema kwamba aliufahamu ugonjwa huo kwa kina.
Madaraka Nyerere azungumza

Madaraka Nyerere, mmoja wa watoto wanane wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, amezungumza na kusema ingawa haafiki kuanza uchunguzi wa kifo cha babake, lakini kuna viashiria fulani fulani vinavyotia shaka.

Viashiria hivyo, kwa mujibu wa Madaraka, ni namna alivyoanza kuikosoa Serikali kwa mambo mengi, jambo analosema inawezekana halikuwafurahisha wengi.

“Binadamu wengi wanapenda sana kuamini kuwa kila jambo likitokea, basi kuna mkono wa mtu. Na hivi karibuni kifo cha Mwalimu Nyerere kimehusishwa na njama mahususi za kumuua.

“Kwa desturi za Kizanaki, hakuna mtu anayekufa kwa sababu ya ugonjwa au uzee, lazima yuko mtu miongoni mwa wale waliobaki hai ambao wamesababisha kifo chake kwa njia za uchawi. Kwa mfano, Bibi Christina Mugaya wa Nyang’ombe, mama mzazi wa Mwalimu Nyerere, mara baada ya kifo cha mume wake, Mtemi Nyerere Burito, tarehe 30 Machi 1942, alitimuliwa Butiama na kuhamia kwa ndugu zake katika kijiji jirani cha Muryaza, baada ya kutuhumiwa kuwa alisababisha kifo cha mume wake.

“Kwa hiyo hakurithiwa kama ilivyo desturi za wakati ule za mila za Kizanaki na akaishi kwa jamaa zake hadi Mwalimu Nyerere alipotoka masomoni Uingereza na kudai arudi nyumbani na akarudi, ingawa baadhi ya ndugu zake hawakufurahia kurudi kwake Butiama.

“Kwa hiyo basi, ni kawaida kabisa kwa hisia kama hizi kuwapo ndani ya jamii. Lakini, kusema hivi haina maana kuwa haiwezekani kuwa tuhuma hizo ni za kweli. Lakini mtu yeyote muungwana hawezi kuanza kutoa shutuma nzito kama hizi bila kuwa na ushahidi usiotiliwa shaka na ambao hauna dosari.

“Lakini naweza kuelewa kwanini baadhi ya watu ambao wanashikilia hizi tuhuma kuwa zinaweza kuwa ni kweli. Tunamfahamu Mwalimu Nyerere kuwa, hata baada ya kustaafu, hakukalia kimya uamuzi au matukio ambayo aliamini yanaathiri baadhi ya misingi ambayo yeye aliiona kuwa ni nguzo inayoshikilia nchi yetu. Baadhi ya haya ni uadilifu ndani ya uongozi, umoja, uzalendo, na sera zenye kujali masilahi ya wengi badala ya sera zinazokuza na kulinda nafasi kwa wachache kujinufaisha.

“Na kwa kweli ukichunguza baadhi ya matukio kwenye nyanja ya siasa katika kipindi hiki ambacho amefariki, yametokea mengi ambayo tunaamini kuwa kama angekuwa hai asingenyamaza na angeyazungumzia kuyapinga na kuyakemea au kuyatungia kitabu pale ambako ujumbe wake aliona unapuuzwa.
Kwa hiyo, mtu yeyote anayefuatilia hali ya uongozi nchini, na watu wengi wanasema hivi, ni kuwa Mwalimu Nyerere angekuwapo labda baadhi ya uamuzi na mienendo ya baadhi ya viongozi wetu ungekuwa tofauti kwa kuogopa kauli yake au kuandikiwa kitabu , kitakachojenga hoja inayopingana na uamuzi wa viongozi. Na pengine baadhi ya uamuzi ambao umefanyika, usingefanyika.

“Kwa hiyo kwa mantiki hii unaweza kuanza kujenga hoja kuwa baadhi ya wale waliofanya uamuzi unaoonekana unaenda kinyume au na maadili ya uongozi, au unapingana na masilahi ya umma, walitafakari kuwa njia rahisi ya kurahisisha mipango yao ni kumuondoa huyu mzee mapema. Hiyo unaweza kusema, lakini haitakuwa sahihi kufanya hivyo bila kuwa na ushahidi.

“Nimewahi kusikia tuhuma kuwa Rais Kikwete anatuhumiwa kuwa ndiye mtu aliyetumwa na nchi za Magharibi kukimaliza Chama Cha Mapinduzi (CCM). Nilivyosikia tuhuma hizi niliona kichekesho, lakini ukiangalia baadhi ya matukio katika uongozi wake ambayo yanaweza kuashiria hoja hiyo, unaweza kuyapata.

“Enzi za Mwalimu Nyerere waliotuhumiwa kwa makosa mbalimbali ya uongozi waliitwa pembeni na kuambiwa wajiuzulu. Miaka ya hivi karibuni wale ambao walikabiliwa na tuhuma za aina hiyo waliombwa kutafakari wao wenyewe uamuzi sahihi wa kuchukua. Uamuzi mgumu haufanyiki, upinzani wanapata mada ya kuzungumzia kwenye mkutano wao ujao, na CCM inazidi kudhoofu. Kama nilivyosema hakuna ushahidi wa wazi, lakini kuna viashiria tu.

“Nafikiri njia nzuri ya kufunga mjadala huu ni kuzungumza kama wanasheria wanavyosema: hakuna ushahidi mpaka sasa unaothibitisha hizo tuhuma juu ya njama za kumuua Mwalimu Nyerere.

“Hoja kuwa uchunguzi ufanyike kubaini kama aliuawa, sioni kama zitaleta faida yoyote kwa sababu ameshafariki tayari na hakuna uchunguzi utakaorudisha uhai wake. Tunamkumbuka Mwalimu Nyerere kwa maandishi na matamshi yake. Na naamini kuwa katika uhai wake aliandika na kutamka masuala yote aliyoamini ni ya msingi kwake na kwa jamii.

“Kuna kiongozi mmoja aliyewahi kusema iwapo kuna wazo la msingi ambalo binadamu amelisema katika uhai wake, basi hilo wazo litadumu hata kama aliyelisema hayuko tena duniani. Badala ya kutafuta wachawi sasa hivi, mimi nafikiri wale wote ambao wanaamini kuwa Mwalimu Nyerere alitoa mchango mkubwa kwa nchi hii, watumie muda wao kutafakari kazi aliyofanya na kujumuisha fikra zake na matendo yake kupima yale ambayo bado yanaweza kuwa suluhisho dhidi ya baadhi ya changamoto zinazoikabili Tanzania sasa hivi.

“Iwapo hoja zake zina nguvu katika mazingira ya sasa, basi hazihitaji yeye mwenyewe kuzisemea. Wanaoziamini wazichambue na wazitumie kama silaha ya kupambana na upungufu ambao tunauona leo katika nyanja mbalimbali.

“Lakini pia ni muhimu kwa vijana kujitafutia elimu kuhusu hayo yaliyopita, ili kupata mifano mizuri ya uongozi ambayo iliweka masilahi ya Taifa mbele na kuzuia kabisa hizi hoja za siku hizi za kumpa kila mtu fursa ya kufanya anavyotaka. Zinazungumzwa fursa za mwananchi, lakini ukweli ni kuwa baadhi ya viongozi wanapigana vikumbo na wananchi hao hao kutafuta fursa zao binafsi,” amesema Madaraka.
CHANZO GAZETI LA JAMHURI.

Hii Ndio Sababu Kubwa ya Paka Kutumika Kichawi Zaidi ya Mbwa..!!!

$
0
0

KWANINI PAKA HUTUMIKA

katika viumbe vya kufugwa na mwanadam,Paka hawezi muona mchawi, ni kipofu kabisa, ndo maana anatumwa, Paka ameonekana kuwa kiumbe kinachotumiwa sana na wachawi na washirikina hii ni kwasababu Paka ana kichwa chepesi, anaelewa haraka na kukariri, paka anaweza tumwa chochote nyumbani kwako, paka anaweza kuja kukuchunguza maisha yako kichawi, mtakubaliana na mimi inaweza ukawa umejifungia ndani au umeleta kitu kwa siri ndani kwako ila utashangaa kibibi kichawi kinakwambia naona umenunua kitu fulani mjukuu wangu. sasa ndo ujiulize kimejuaje wakati kinakaa mtaa wa pili na wewe umeleta kwa siri? paka anao uwezo wa kukamata vitu kwa haraka,wengine watumwao ni ndege njiwa na bundi maana hawaoni uchawi.

MBWA JE YUKOJE?

kwa mbwa ni kinyume kidogo, mbwa anaona wachawi, anauwezo mkubwa sana wakuona uchawi, anakichwa kizito, hawezi tumwa na wachawi maana ataharibu kabisa kwakuwa anaona wachawi wengine, mbwa hafai, wengine hadi humwita mbwa ni najisi, hili ni kwasababu mbwa havumilii kuona majini au wachawi wanakatiza lazima atabweka! mbwa ameonekana kufaa katika ulinzi kwasababu anaona usiku wezi na wachawi. ukiona mbwa anabweka sana usiku nyumbani kwako usipuuzie chunguza lazima utakuta kuna tatizo.wengine wenye uwezo wa kuona ni KUKU na BATA ...hao wanaouwezo wa kumwona mchawi...hakikisha unawatumia wanyama wako kukurinda kwa kusikiliza milio yao.

Lowassa Awajibu Wanaomtuhumu Kutovaa Sare za CHADEMA, Asema Ahukumiwe kwa Matendo Yake..!!!

$
0
0

Aliyekuwa mgombea wa Urais 2015 kwa tiketi ya CHADEMA na waziri mkuu mstaafu Mzee Edward Lowassa amesema si kweli kuwa havai sare za CHADEMA, na pia asihukumiwe kwa kuvaa au kutokuvaa sare hizo bali kwa matendo yake.

Waziri Mkuu huyu mstaafu tokea ajiunge na chama cha kikuu cha upinzani Tanzania amekuwa akituhumiwa na wanachama na wengine nje ya chama kwa kutokuvaa kabisa sare za chama maarufu kama gwanda.

Baada ya Lowassa Kutangaza Kumuunga Mkono Uhuru Kenyatta..Raila Odinga Aibuka na Kumpigia Magoti Amuunge Mkono..!!

$
0
0

Mgombea urais wa Kenya kwa tiketi ya umoja wa vyama vya upinzani wa NASA, Raila Odinga ameweka wazi ombi lake kwa Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania, Edward Lowassa kuhusu mchakato wa uchaguzi huo.

Amesema kuwa Lowassa pamoja na Rais John Magufuli waliochuana kwenye uchaguzi mkuu uliopita ni marafiki zake, na kuwaomba wote wamuunge mkono kwenye uchaguzi huo.

Ombi la mwanasiasa huyo mkongwe wa Kenya na Waziri wa zamani wa nchi hiyo limekuja siku chache baada ya Lowassa kuweka wazi kuwa atamuunga mkono Rais Uhuru Kenyatta ili aendelee kuitawala nchi hiyo.

“Mimi na familia yangu tunamtumikia Mungu lakini vilevile kwa dhati kabisa sisi wana Monduli tunamuunga mkono Uhuru Kenyatta kwenye mbio za Urais nchini Kenya. Naomba nitamke wazi na dunia yote ijue kuwa sisi tunampenda Uhuru Kenyatta naye anatupenda, kwa hiyo tunamuunga mkono kwa kuwa tunaamini ana uwezo wa kuwaunganisha Wakenya na Watanzania,” alisema Lowassa alipotembelewa na wabunge wanawake kutoka Kenya, nyumbani kwake Monduli takribani mwezi mmoja uliopita.

Lowassa ana ushawishi kwa kiasi fulani kwenye uchaguzi huo kwa kuwa ni kiongozi mkuu wa Wamasai (Leigwanan) katika ukanda wote wa Afrika Mashariki.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo pia kimeweka wazi kuwa kitamuunga mkono Kenyatta kwa kuwa kinaridhika na namna alivyofanya kazi hususan kuruhusu demokrasia nchini kwake.

Hata hivyo, msemaji wa vyama vya upinzani nchini Kenya, Philip Etale alisema kuwa Odinga ni rafiki wa Lowassa na Magufuli na kwamba asingependa urafiki huo upotee kwa sababu za kisiasa.

“Odinga aliweka bayana wakati wa kampenzi za uchaguzi wa Tanzania kuwa anawaunga mkono wote na kutaka mgombea bora ashinde. Kama ODM tunaamini katika demokrasia na tusingependa wakati wowote ule, tupoteze marafiki zetu kwa sababu ya siasa,” huo ulikuwa ni ujumbe wa Etale

Kenya inatarajia kufanya uchaguzi mkuu Agosti 8 mwaka huu, uchaguzi ambao unatajwa kuwa na ushindani mkubwa zaidi kwani katika uchaguzi uliopita, Kenyatta na Odinga walizidiana kwa kiasi kidogo cha kura.

Fundisho kwa Serikali ya CCM. Upinzani sio Uadui

$
0
0
Katika kuazimisha Siku ya Uhuru wa Kenya, Rais Kenyatta amewaalika viongozi wa upinzani kwa mazungumzo Ikulu. Hii inaonyesha katika mambo ya kitaifa wao ni wamoja na siasa haziwatenganishi undugu wao.

Hapa kwetu hata kwenda kwenye harusi ya mpinzani taarifa zako zinachunguzwa maana unahisiwa kuwa ni msaliti. Tujifunze kutoka Kenya ambako tumekuwa tunawatolea mifano mibaya kumbe wao ndio wako vizuri kuliko sisi.

Leo mtu kuwa Chadema kesho ccm au ccm kesho Chadema au CUF lionekane ni jambo la kawaida muhimu utetezi kwa nchi tuu. Maana ndani ya nchi wapo ndugu na jamaa zako watakuwa katika vyama tofauti na chako.

Vita ya mali za Urithi yaanza rasmi kati Zali na Ndugu wa Marehemu Ivan

$
0
0
IVAN Ssemwanga amekwenda lakini huku nyuma ameacha kimbembe kufuatia baadhi ya ndugu zake kumlipua aliyekuwa mkewe, Zarinah Hassan ‘Zari’ na kudai kuwa, anatakiwa akae mbali na mali za ndugu yao kwa kuwa alimtenda vibaya enzi za uhai wake.

Ndugu hao mara tu baada ya mazishi walionekana kumzodoa Zari na kuviambia vyombo vya habari vya nchini Uganda kuwa, wameshangazwa na ukaribu wake kwa ndugu yao kipindi alipokuwa anaumwa wakati huko nyuma alikuwa kamtosa.

Mtandao mmoja wa nchini Uganda uliandika kuwa, Zari amekuwa hana amani kufuatia maneno ya baadhi ya ndugu wa Ivan wanaodhani ukaribu wake ni ili apate sehemu ya mali za marehemu.

“Wanamsema sana na yote hii ni kwa sababu ya mali ila busara inatakiwa itumike katika kipindi hiki kwa kuwa Zari ana watoto wa marehemu.

“Mawifi wamekuwa mstari wa mbele kumsakama lakini kibaya zaidi ni lile tamko la msemaji wa familia kusema kifo cha mtoto wao kimesababishwa na Zari,” uliandika mtandao huo.

Kiongozi wa familia aliyetambulishwa kama baba mlezi wa Ivan, Herbert Luyinda alikaririwa na gazeti la Uganda liitwalo Bukedde akisema: “Kama familia, hatuna shaka kwamba Zari ndiyo chanzo cha kuumwa kwa Ivan na hatimaye kufariki dunia.

Tangu wametengana, Ivan hakawahi kuwa vizuri. Mtoto wetu alimpenda sana na akamjali kwa hali zote lakini akamtosa. Hili lilimchanganya sana na kusumbua afya yake. “Aidha, Zari siyo mjane wa marehemu, tunayemjua sisi ni mwanamke wa Afrika Kusini aitwaye Ddudu ambaye ni mjamzito.”

Maneno hayo ndiyo yalizidisha kasi ya Zari kushambuliwa, lakini kwa ujasiri wake amekuwa imara na mara nyingi ameonekana akiwa na watoto wake aliozaa na Ivan wakifarijiana. Kufuatia yote yanayosemwa, juzikati Zari aliposti mtandaoni maneno haya: “Katika maisha kuna wakati utajua nani ni muhimu kwako na nani siyo.

Kuna watakaokuwa wanajifanya wako upande wako kumbe ni uongo. Lakini katika ulimwengu huu kilichopo katika mlango wangu ipo siku kitakuja kukugongea kwenye mlango wako.”

Breaking News: Wabunge wa Upinzani Wasusia Bunge na Kutoka Nje...Kisa John Mnyika

$
0
0
Mbunge John Mnyika atolewa nje ya Bunge kwa amri ya Spika Job Ndugai na kuamriwa kutohudhuria vikao kwa siku 7 baada ya kutokea malumbano leo.

Kufuatilia tukio hilo Wabunge wa Upinzani wametoka nje baada ya Mbunge huyo kutolewa nje na Askari wa Bunge kwa amri ya Spika.

Vilevile, Mamlaka ya Bunge kupitia Kamati ya Maadili kumjadili Mbunge Esther Bulaya kwa kuhamasisha wabunge kutoka nje ukumbi wa Bunge

Kufuru..Je Wajua Kiasi Cha Pesa Walichopewa Chelsea Baada ya Kutwaa Ubingwa wa Ligi ya Uingereza?

$
0
0
Chelsea ni mabingwa wa ligi ya England 2016-17

Klabu ya soka ya Chelsea imelipwa paundi milioni 150.8 na chama cha soka cha England FA baada ya kushinda ubingwa wa ligi kuu msimu wa 2016-17.

Msimu wa 2015-16 ulishuhudia ongezeko kubwa kwa mkataba wa matangazo ya Televisheni ukitoa takriban Paundi bilioni 2.4 kwa timu 20 zaidi ya msimu uliopita zilipolipwa Paundi bilioni 1.6.

Timu iliyoshika mkia kabisa Sunderland imepata Paundi milioni 93.471.

Fedha hizo zinatokana na matangazo ya Televisheni, mikataba ya kibiashara sambamba na zawadi.

Yanga Wamemfanya nini Hamis Tambwe...Mwenye Afunguka Haya Kwa Uchungu Akiwa Kwao Burundi

$
0
0
STRAIKA wa Yanga, Amissi Tambwe, huenda msimu ujao asionekane katika kiko­si cha timu hiyo kutokana na kutojua hatima yake ndani ya klabu hiyo mpaka sasa.

Tambwe ambaye ameon­goza Yanga kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara mara tatu mfululizo tangu alipojiunga nayo msimu wa 2014/15 akitokea Simba, ame­liambia Championi Ijumaa kuwa kwa jinsi mambo yanavyoenda inawezekana asiitumike timu hiyo msimu ujao.

Alidai kuwa mpaka sasa hakuna chochote kina­choendelea kati yake na uongozi, hivyo kama hali hiyo itaendelea mpaka mwezi Julai, basi ata­chukua uamuzi wa kwen­da kutafuta maisha sehe­mu nyingine katika timu ambazo zimeonyesha nia ya kutaka kusajili za hapa nchini na nje ya nchi.

Kwa sasa Tambwe amei­fungia Yanga mabao 46 katika michuano ya ligi kuu tangu alipojiunga nayo, yupo kwao nchini Burundi kwa ajili ya mapumziko na hajui lini atarejea nchini.

“Kwa hiyo, kutokana na hali hiyo sijui nitarejea lini nchini, lakini ninachoweza kusema ni kwamba bado ninaipenda Yanga na ndiyo maana nimeamua kusitisha mipango yangu mingine mpaka niwasikilize wao kwanza.

“Lakini wakiendelea kuwa kimya mpaka Julai basi ni­tachukua uamuzi mwingine kwa sababu soka ndiyo kazi yangu, naweza kujiunga na timu yoyote hapo nchini au nje ya nchi ambazo tangu zamani zimekuwa zikinihi­taji,” alisema Tambwe am­baye mkataba wake na Yan­ga tayari umeshamalizika.

Hii Ndio App Pekee Iliyopo Kwenye Simu Anayotumia Rais wa Marekini Donald Trump

$
0
0
Watu wengi wanaotaka kununua simu janja/Sikanu (Smartphone), mojawapo ya jambo wanaloangalia pindi wafanyapo uchaguzi wa simu ni ukubwa wa uhifadhi wa ndani (storage).

Sababu kubwa ya kufanya hivyo ni kupata wasaa wa kusanidi (Install) App nyingi zaidi kadri iwezekanavyo, lakini hilo ni tofauti sana kwa Rais wa Marekani Donald Trump.

Kwa mujibu wa ripoti mpya imeelezwa Simu binafsi ya Rais wa Donald Trump imesanidiwa (Installed) App moja tu.

Mwandishi wa habari za kisiasa na mhariri wa AXIOS Media, Mike Allen, anasema Rais Trump anatumia simu ya iPhone na kwamba simu yake imewekwa App ya Twitter tu.

Sababu ya kufanya hivyo na kumuwekea App hiyo ni kupunguza hatari ya uwezekano wa simu yake kudukuliwa. Aidha pia kumpunguzia muda wa matumizi ya simu na ili ajielekeze zaidi katika mambo ya kio�si zaidi.

Muda mwingi hutumia kuangalia TV ili kujua matukio yanayoendelea duniani.

Simu ya awali ambayo alizuiwa kuitumia baada ya kuwa Rais ilikuwa ni Samsung. Alibadili kutoka Android kwenda iOS mwezi Machi mwaka huu.

Mpaka anaapishwa kuwa Rais wa Marekani inaelezwa simu aliyokuwa anatumia ni Samsung Galaxy S3 ambayo ilitolewa mwaka 2012.

Rais aliyepita Baraka Obama alisema wakati wa kuingia madarakani kwamba anatumia BlackBerry na matumizi yake yalikuwa ni kutuma ujumbe, kupiga picha na kusikiliza Muziki.

Chanzo: Teknokona

Mwanasheria Aomba Mahakama Uganda Iruhusu Kaburi la Ivan Don Kufukuliwa

$
0
0

Mwanasheria Tugume Gideon ameiomba Mahakama Kuu ya Uganda iruhusu kaburi la Ivan Semwanga lifukuliwe ili watoe fedha zilizomwagwa ndani akidai kuwa ni kunyume cha Sheria

Hii Hapa Sababu ya Kada wa Chadema Yeriko Nyerere Kukamatwa ..Bado Andelea Kusota Jela...!!!

$
0
0

Mke wa Yeriko Nyerere, (kada wa Chadema) Neema Alex amesema mumewe ameshindwa kufikishwa mahakamani jana kutokana na kutokamilika kwa baadhi ya mambo.

Hata hivyo, Neema hakuwa tayari kutaja kilichokwamisha Yeriko kufikishwa mahakamani na kusema kila kitu kiliandaliwa na nyaraka zote zilikuwa tayari kwa ajili ya Yeriko kufikishwa mahakamani.

“Wakati tukimsubiri atoke na kuelekea mahamakani ghafla simu ikapigwa na mmoja wa wakubwa wa polisi akitoa amri ya kwamba asipelekwe mahakamani hadi atakapopiga simu tena.

“Nahisi bado hawajaridhika na maelezo aliyoyatoa mume wangu (Yeriko) ingawa sina uhakika,” alisema Neema wakati akizungumza kwa simu na gazeti hili jana.

Yeriko alikamatwa saa tisa alfajiri juzi akiwa nyumbani kwake Mbutu, Kigamboni na watu wanaodaiwa kuwa maofisa usalama wa mitandao kisha kumpeleka katika Kituo Kikuu cha Polisi cha Kanda Maalumu.

Katika tukio hilo, maofisa hao waliambatana na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mbaragande, Jamal Hassan anakoishi Yeriko. Neema alisema kuwa jana wakiwa na baadhi ya viongozi wa Chadema walikwenda Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa ajili ya kumsubiri mumewe ambaye hakupelekwa kama walivyotarajia.

Hata hivyo, Neema alisema alifanikiwa kuonana na kuzungumza na Yeriko ambaye alisema yupo katika hali nzuri na hana wasiwasi wala tatizo lolote.

Wakili wa Yeriko, Peter Kibatala alisema hadi jana mchana hakupata taarifa zozote kutoka polisi kwa kuwa alikuwa na majukumu ya kushughulikia kesi nyingine.

“Sijui chochote kwa sasa? Kwa sababu asubuhi niliamkia mahakamani kwa ajili ya kesi ya Lissu (Tundu-Mwanasheria wa Chadema),” alisema Kibatala.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Mbaragande, Hassan alilieleza juzi kuwa maofisa hao walimwambia wanamkamata Yeriko kwa sababu ya makosa ya mtandao.    

Credit - Mwananchi 

Hii ndio idadi ya watu wanaosafiri kwenye mabasi ya mwendokasi kwa siku

$
0
0

Dar es Salaam. Mradi wa mabasi yaendayo haraka (BRT) sasa unasafirisha watu 200,000 kwa siku kutoka watu 50,000 iliyokuwa ikisafirisha mwaka jana baada ya mradi huo kuanza kazi.

Kuongezeka kwa idadi hiyo inaelezwa kuwa ni ishara ya wananchi kuukubali mradi huo na kuutumia kila siku waendapo sehemu zao za kazi au majumbani.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika waliotembelea mradi wa BRT, Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usafiri wa Haraka Dar es Salaam (DART), Hazina Mfinanga amesema mafanikio ya mradi huo yametokana na ushirikiano mkubwa uliopo baina ya wadau mbalimbali.

Mfinanga amewataja wadau hao kuwa ni kampuni ya UdaRT ambayo ndiyo inaendesha mabasi, Maxcom Africa ambao wanaendesha mifumo ya kukusanya nauli na benki ya NMB ambayo inasimamia upatikanaji wa fedha za mradi huo.

"Bado tuko kwenye kipindi cha majaribio wakati tukiendelea na mchakato wa kupanua njia za BRT katika jiji hili ili watu wengi zaidi waweze kunufaika na mradi huu," amesema Mfinanga.

Mfinanga ambaye pia ni Meneja Rasilimali watu wa DART, amesema wazo la kuanzisha mradi huo lilikuwa ni kutatua changamoto zinazowakabili wakazi wa Dar es Salaam ambazo ni pamoja na kupoteza muda kwenye foleni na uchafuzi wa mazingira.

Lowassa amponza Yericko Nyerere

$
0
0

Mfuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendele (Chadema) Yericko Nyerere amepandishwa Kizimbani na kusomewa mashtaka Matano yanayohusu kusambaza Taarifa za Uoungo kupita mtrandoa wa Facebook.

Mbele ya Hakimu Mkazi Wilbard Mashuari wakili wa Serikali Athaas Elia amemsomea Nyerere mashtaka hayo pamoja na  Kuandika kwenye ukuirasa wake wa Facebook Taarifa za kupotosha.
Wakili Elia alidai kuwa Nyerere siku ya Tarehe 25 Oktoba Mwaka 2015, sehemu isiyojulikana ndani ya jiji la Dar es Salaam aliandika maneno haya" Mateso ya Ulimboka na Kibanda, Mateso ya kijana wetu wa JKT. Ukikumbuka haya fanya uamuzi sahihi bila ushabiki."

Shtka la Pili ni kuchapisha Taarifa ya uongo ambapo  Tarehe 24 Oktoba Mwaka 2015 sehemu isiyojilikana Dar es Salaam,  Nyerere aliindika kupitia ukurasa wake wa Facebook kuwa "Taifa la Tanzania kuanzia leo halihitaji AMANI, linahitaji Haki tu" 

Shitaka la Tatu ni kuchapisha taarifa za uongo ambapo mshitakiwa katika ukurasa wake wa Facebook siku ya Tarehr 24 Oktoba mwaka 2015 aliandika kuwa "Siku ya leo mpaka siku ya kuapishwa Lowassa Taifa hili halihitaji AMANI bali Taifa hili linahitaji HAKI tu. Amani ilishatoweka siku nyingi, kilichosalia ni uvumilivu tu. Njia sahihi ya kulitibu Taifa hili ni kwa dola dharimu kutenda HAKI hata kama itawauma. Uchaguzi huu ni vita, anaedhani ni demokrasia apimwe akili. Hii ni vita kati ya UMMA na DOLA, ni vita kati ya wema na ubaya, ni vita kati ya shibe na njaa, ni vita kati ya masikini na matajiri"

Shitaka la la nne lilomkabili Nyerere ni kuchapisha taarifa za  uongo ambapo tarehe 24 Agosti mwaka 2015 sehemu isiyojulikana ndani ya jiji la Dar es Salaam, kyupitia mtandao wa Facebook aliandika kuwa "Mipango ya hujuma ya JK toka Ngordoto Arusha muda huu. Kikwete yuko Ngordoto arusha na wakuu wote wa mikoa na Wilaya Tanzania nzima, Pia wakuu wa vyombo vya dola na wanadimu mbalimbali Wakuu wa Mikoa wanaelezwa kwamba kuwa NEC kwa kushirikiana na CCM tayari wameshatengeneza kura bandia kwa kutumia mfumo wa kalamu za kichina, pia wanaamuliwa kuhakikisha wanahujumu kampeni za UKAWA kwa kutumia vyombo vya dola"

Pia wanaagizwa kuhakikisha kamatakamata ya vijana bodaboda wiki moja kabla ya uchaguzi, na zaidi ni wakuu hao wa mikoa wanaagizwa wakawaagize ma DC kote nchini kuhakikisha wanalinda maslahi ya CCM popote walipo siku ya uchaguzi.
Shitaka la Mwisho ni la kuchapisha Taarifa za uongo pia ambapo mtuhumiwa aliiandika kwenye mitandao ya kijamii siku ya Terehe 3 Septemba mwaka 2015 aliandika kuwa HSBC BANK, NORTH LONDON BRANCH. Ccm has deposited 1.5 Pound Million fraudulently in favour of Dr Wilbroad Slaa Through his fuience Josephine Mushumbusi being Curruption from ccm to win Tanzania General Election 2015.
mshtakiwa amekana mashtaka yote na kudhaminiwa kwa shilingi 10 Milioni.
kesi hiyo itatajwa tena tarehe 5 mwezi juni mwaka huu.



.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live


Latest Images