Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104781 articles
Browse latest View live

Kauli ya Mwisho ya Mzee Ndesamburo Yazua Utata,,Alimtaja Bashite Kimafumbo..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo Jumamosi ya 3/6/2017..!!!


Mkwasa..Ushiriki wa Simba Kimataifa Umetuongezea Gharama za Usajili kwa Yanga..!!!

$
0
0

Baada ya Simba kufanikiwa kupata tiketi ya kushiriki michuano ya kimataifa mwakani, imeelezwa kuwa gharama za kusajili wachezaji nyota zimeongezeka.

Simba ambao ni mabingwa wa Kombe la shirtikisho, wataiwakilisha Tanzania Bara katika michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika, wakati mabingwa wa Ligi Kuu Young Africans watapeperusha bendera ya nchi kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Katibu Mkuu wa Young Africans, Boniface Mkwasa, alisema msimu huu watalazimika kuongeza bajeti kwa sababu wachezaji wamekuwa na nafasi zaidi ya moja katika kufanya uamuzi wa timu za kujiunga nazo.

Mkwasa alisema wakati Simba ilipokua haiwakilishi nchi kimataifa, gharama za usajili wa wachezaji zilikuwa za kawaida, lakini msimu huu mambo yamebadilika.

“Kiukweli uhitaji sasa umeongezeka, uhitaji umekuwa mkubwa, kila upande unahitaji kujiimarisha, kiasi cha fedha wanachotaka kimeongezeka na hii inatokana na kuwa na uhakika wa kucheza mashindano ya kimataifa,” Alisema Mkwasa.

Alisema misimu miwili iliyopita klabu yake ilikuwa na uwezo wa kusajili kabla ya ligi haijamalizika, lakini msimu huu hilo halijawezekana.

Baadhi ya wachezaji wa Young Africans ambao wamegoma kusaini mikataba mipya na sasa wako huru ni pamoja na Ngoma, Haruna Niyonzima, Thabani Kamusoko, Ally Mustapha ‘Barthezn na Simon Msuva.

Familia ya Ivan Matatani kwa Kufukia Pesa ya Uganda Kaburini..!!!

$
0
0

Wanasheria nchini Uganda wameamua kuifikisha familia ya Ivan Mahakamani kwa makosa ya kuzika pesa halali za Jamhuri ya Uganda katika kaburi la ndugu yao Ivan. Kwa nchi yoyote kitendo hicho hakikubaliki kwani pesa hizo zingeweza kutumika katika shughuli zingine na kukuza uchumi wa nchi.

Kitendo hicho kinakuja baada ya marafiki wa Ivan kumwaga mamilioni ya pesa ndani ya kaburi la Ivan kama njia ya kumuaga rafiki yao aliyekuwa maarufu kwa matumizi makubwa ya pesa.

Wanasheria wakiongozwa na Tugume Gideon wa Human Rights Defenders Association Uganda wamesema hawakufurahishwa na kitendo cha RICH GANG cha kuzika mamilioni ya pesa ndani ya kaburi, na kwa vile ni kinyume cha sheria,

wameamua kwenda mahakamani kuomba kaburi la Ivan lifukuliwe, pesa zitolewe zikafanye shughuli nyingine na waliohusika washitakiwe kwa kuharibu kwa makusudi alama ya taifa.

Gwajima Aaanika Utajiri Wake wa Kutisha..Adai Utajiri Wake Unamfanya Kuwa Miongoni mwa Mamilionea 10 Nchini Wenye Uwezo Mkubwa Kuliko Wengine..!!!

$
0
0

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church (GCTC) ‘Ufufuo na Uzima’, Askofu Josephat Gwajima, amejitapa hadharani kuwemo kwenye kumi bora ya orodha ya matajiri wakubwa wenye viwango vya umilionea nchini, kauli iliyopokelewa kwa hisia tofauti miongoni mwa waumini na watu mbalimbali, Amani linawasilisha.

Jumapili ya wiki iliyopita, mwandishi wetu alihudhuria ibada ya askofu huyo ambaye alianza kwa mbwembwe na majigambo makubwa ya ‘kumvua‘ mtu taulo, jambo ambalo hakulifanya kwa madai ya kuelekeza nguvu kwenye ishu ya mchanga wa dhahabu, ambapo pamoja na mambo mengine, Gwajima alimshukuru Mungu kwa ukwasi wa kutisha alionao na kuwataka Watanzania kuamka na kuzitumia fursa za kimaendeleo zilizopo nchini.

Akitembea kwa madaha na kuhubiri kwa mikogo na staili mbalimbali za madoido kama ilivyo ada yake, mchunga kondoo huyo wa Bwana mwenye ‘madini’ ya kutosha kichwani, alisema tatizo kubwa la Watanzania ni kutegemea miujiza ya mafanikio kuliko kujitolea kufanya kazi ndiyo maana wengi hubaki maskini licha ya kuwa na kila sifa ya mafanikio ikiwemo usomi wa kiwango cha juu.

“Namshukuru sana Mungu kwamba miongoni mwa mamilionea 10 nchini Tanzania na mimi nimo, hilo halina shaka kabisa yaani nasema kwa msisitizo nimo kwenye orodha ya matajiri 10 wa nchi hii. Unajua ngoja niweke wazi jambo moja muhimu, nchi yetu imejaaliwa kuwa na rasilimali nyingi sana, tatizo letu ni mafundi wa kuongea na si kufanya kazi, tunategemea miujiza kutoka kwa Mungu.

“Mungu mwenyewe alisema nitabariki kazi za mikono yenu, hakusema nitawabariki kwa kukaa bila kufanya kazi, mimi namshukuru kwa alichonijaalia maana nafurahia maisha na wewe unayenisikiliza nakuomba uamke upambane na maisha, maana Tanzania ina kila kitu, mito na maziwa kwa kilimo, ukichimba shimo hadi kiunoni, kwa wale wakazi wa Shinyanga unapata madini, tuamke na tufanye kazi ndipo tuwe na pesa, mimi ninao utajiri wa kutosha,” alisema Askofu Gwajima. Miongoni mwa matajiri wakubwa wanaotajwa kuongoza nchini Tanzania, ni pamoja na Mohamed Dewji, ambaye ni Mkurugenzi wa Mohamed Enterprises Tanzania Limited (MeTL), Rostam Aziz, mfanyabiashara wa masuala ya madini na Dk. Reginald Mengi, mwenyekiti wa Makampuni ya Industrial Products Promotions (IPP). Wengine ni Said Salim Bakhressa, Mwenyekiti wa Azam Group of Companies, Yusuf Manji ambaye ni Mwenyekiti mstaafu wa Quality Group na wengine wengi.

Ndugu wa Ivan Wamlipua Zari, Wamtaka Asizisogelee Mali za Ndugu Yao

$
0
0

IVAN Ssemwanga amekwenda lakini huku nyuma ameacha kimbembe kufuatia baadhi ya ndugu zake kumlipua aliyekuwa mkewe, Zarinah Hassan ‘Zari’ na kudai kuwa, anatakiwa akae mbali na mali za ndugu yao kwa kuwa alimtenda vibaya enzi za uhai wake.

Ndugu hao mara tu baada ya mazishi walionekana kumzodoa Zari na kuviambia vyombo vya habari vya nchini Uganda kuwa, wameshangazwa na ukaribu wake kwa ndugu yao kipindi alipokuwa anaumwa wakati huko nyuma alikuwa kamtosa.

Mtandao mmoja wa nchini Uganda uliandika kuwa, Zari amekuwa hana amani kufuatia maneno ya baadhi ya ndugu wa Ivan wanaodhani ukaribu wake ni ili apate sehemu ya mali za marehemu.

“Wanamsema sana na yote hii ni kwa sababu ya mali ila busara inatakiwa itumike katika kipindi hiki kwa kuwa Zari ana watoto wa marehemu.

“Mawifi wamekuwa mstari wa mbele kumsakama lakini kibaya zaidi ni lile tamko la msemaji wa familia kusema kifo cha mtoto wao kimesababishwa na Zari,” uliandika mtandao huo.

Kiongozi wa familia aliyetambulishwa kama baba mlezi wa Ivan, Herbert Luyinda alikaririwa na gazeti la Uganda liitwalo Bukedde akisema: “Kama familia, hatuna shaka kwamba Zari ndiyo chanzo cha kuumwa kwa Ivan na hatimaye kufariki dunia.

Tangu wametengana, Ivan hakawahi kuwa vizuri. Mtoto wetu alimpenda sana na akamjali kwa hali zote lakini akamtosa. Hili lilimchanganya sana na kusumbua afya yake. “Aidha, Zari siyo mjane wa marehemu, tunayemjua sisi ni mwanamke wa Afrika Kusini aitwaye Ddudu ambaye ni mjamzito.”

Maneno hayo ndiyo yalizidisha kasi ya Zari kushambuliwa, lakini kwa ujasiri wake amekuwa imara na mara nyingi ameonekana akiwa na watoto wake aliozaa na Ivan wakifarijiana. Kufuatia yote yanayosemwa, juzikati Zari aliposti mtandaoni maneno haya: “Katika maisha kuna wakati utajua nani ni muhimu kwako na nani siyo.

Kuna watakaokuwa wanajifanya wako upande wako kumbe ni uongo. Lakini katika ulimwengu huu kilichopo katika mlango wangu ipo siku kitakuja kukugongea kwenye mlango wako.”

Ukweli Mchungu..Askari wa Bunge, Wabunge wa CCM Mjipiime Upya. Hawa Wabunge wa Upinzani Tumewaagiza Sisi Walipa Kodi ..!!!

$
0
0

Nina maswali yananitatiza sana kichwani kwangu juu ya nani mwenye mamlaka ya kulitumikia taifa bila bughuza na kuheshimiwa mawazo yake.

Jana nilikuwa natizama bunge, nikastaajabisha kuona wabunge wa CCM kuanza kumshambulia kwa maneno mbunge wa CHADEMA Mh. John Mnyika huku wakikataa kufuta kauli zao huku wakiwa comfortable bila wasiwasi wowote.

Naona jinsi gani mbunge yule kijana mdogo kabisa anavyovunjwa moyo na wabunge wenye uwezo mdogo ambao hawakuweza kulinyasua kivyovyote taifa hili maskini kwa miaka kibao japo wapo katika chama tawala, mfano yule mbunge wa mtela ambako hali yake siyo nzuri kabisa unaweza sema ni kati ya majimbo duni kabisa hapa Tz.

Swala la pili:- Najiuliza kwanini viongozi wa bunge na wabunge wanataka bunge liwe lilelile la kukubali kila kitu na hawataki akili mpya na mawazo mapya yatolewe ili kujitathmini na kuliendeleza taifa na siyo kila siku hali kuwa ileile ya kukubali kila kitu? Nani amewaambia kwamba sisi watanzania tunavutiwa zaidi na wanachotaka wao na sio mawazo yenye kuhoji kama akina Mnyika?

Kwann viongozi wa bunge wanataka wabunge wa upinzani wawe kama watoto wakiwa ambao hawana uhalali na nchi hii na wabunge wa CCM wawe comfortable kama kwamba nchi ni yao peke yao?

Mwisho, hivi hawa walinzi wa bunge kwanini hawana staha kwa viongozi wa upinzani kusema kwamba wao wameajiliwa na CCM na hao wanaowasukuma sukuma kwa dharau siyo viongozi wao na hawatakuja kuwa viongozi wa juu kabisa wa nchi hii, askari wa bunge wajia asses upya, hawako fair hata kidogo, wanalipwa na kodi za hao wanaowasukuma kama Mbwa na siyo vingine.

Chanzo JF

Kutana na Mtaalamu wa Tiba Asili Ostadh Khamis Kutoka Mombasa..Yupo Tanzania....Anatibu Magonjwa Yafuatayo

$
0
0

Kutana na OSTADH khamis kutoka Mombasa Kenya kwa sasa yupo Tanzania nibingwa watiba za asili:

Miguu kuuma miguu kufagazi nakuwaka moto
Unashida na mchumba au pesa haikai muone haraka 
Kurudisha mpenziwako alie kukimbia ndani ya siku (3)
Dawa ya ( LIMBWATA) kumtawala mpenzi wako kwasababu maalumu   
Pete ya bahati inayo endana nanyota yako itakayo kuletea pesa bila mashart yeyote
Kuongeza uume saizi uipendayo 
Dawa ya ulijali 
Dawa yakuongeza hips
Kumuliki Mali isiokuwa namasharti yeyote 
Kurudisha Mali iliopotea au kudhurumiwa ndani yasiku(3) 
Napia OSTADH KHAMIS anafunga kesi nakupata hakiyako kwa haraka 
Dawa ya mvuto pia inapatikana mvuto Wa biashara kuuza Mali yako kwa haraka 
Kuzuiya chuma ulete na kupandishwa cheo kazini PAMOJA na kusafisha nyota njoo ufunguliwe vifungo ulivyo fungwa

Call+255718746825 au +255754765246 WhatsApp IMO +255783708487

EXCLUSIVE: Wakili Aeleza Sheria Kuhusu Kufukuliwa Kaburi la Ivan (+Video)

$
0
0
June 2, 2017 Mahakama Kuu Uganda iliomba kufukuliwa Kaburi la aliyekuwa Mfanyabiashara maarufu Uganda Ivan Ssemwanga na kutolewa fedha zilizotupwa hatua iliyokuja baada ya Bank Kuu kutoa tamko kuvitaka Vyombo vya Dola kuwachukulia hatua waliotupa fedha hizo…sheria inasemaje?

Kufuatia ombi hilo la Mahakama ya Uganda leo June 3, 2017 Ayo TV na millardayo.com zimetaka kujua jambo hilo kisheria likoje na zinaye kwenye EXCLUSIVE Wakili wa kujitegemea na Mwanaharakati wa Haki za Binadamu Tanzania Jebra Kambole ambaye anafafanua zaidi…

“Nilichokiona kwenye shauri ambalo limefunguliwa Uganda ni maombi ambayo yamefikishwa Mahakamani na Mahakama ndiyo ina jukumu la kuyatafsiri yale maombi. Kwa hiyo siyo amri ya Mahakama moja kwa moja.

“Ni maombi ambayo yamepelekwa chini ya kifungu namba 42, kifungu pia cha 17, kifungu kidogo cha kwanza (a) na (i) ya Katiba ya Uganda ya mwaka 1965, lakini pia kifungu cha 50 cha Katiba ya Uganda.

“Kimsingi, vifungu hivyo ambavyo nimevitaja hapo awali vya Katiba ya Uganda ni vifungu ambavyo moja kwa moja vinatoa wajibu kwa kila raia kuheshimu alama za Taifa ikiwemo pamoja na pesa ya nchi.” – Jebra Kambole.

Kujua mengi zaidi kuhusu nini kifanyike kutokana na ombi la Mahakama kuhusu kufukuliwa Kaburi la Ivan Don pamoja na matakwa ya Sheria, nimekuwekea VIDEO hapa ambayo unaweza kuplay na kutazama ukajiua zaidi.

Kuna Beef Baraka The Prince na Ali Kiba? Baraka Afunguka Yote Kwanini Hawako Karibu Tena Kama Zamani

$
0
0
Moja ya story ambayo iliwahi kuchukua headlines nyingi katika mitandao siku za nyuma ni kuhusu staa wa Bongofleva Baraka the Price kutokuwa karibu na staa mwingine Alikiba baada ya kuwa pamoja wakifanya shuguli za muziki.

New story leo June 2, 2017 ni kuwa Baraka the Price amefunguka na kueleza sababu za watu hao kutokuwa karibu tangu alipotoa wimbo aliomshirikisha Alikiba akisema sababu ni kuwa buys akiandaa album yake mpya.

Akiongea kwenye XXL ya Clouds FM Baraka the Prince amedai kuandaa albamu yake mpya kumemfanya awe busy huku Alikiba akiwa kwenye tour nje ya nchi:

“Ujue mimi natoa Albam mwaka huu kwa hiyo tangu mwaka umeanza nimekuwa busy natengeneza album yangu ndio maana sionekani niko karibu na Ali. Kwanza Ali amekuwa haonekani Dar es Salaam sana. Amekuwa yupo safarini na tunakuwa tunawasiliana sana kwenye simu na massage lakini ile kuonekana kama zamani ni kwa kuwa yupo kwenye kazi zake na mimi nipo kwenye kazi zangu.

“Zamani kilichokuwa kinatufanya tuwe karibu ni kwa sababu tulikuwa tufanya kazi ya kutukutanisha. Tulikuwa chini ya Rock Star kampuni moja na ikitokea suala la wasanii wa Rock Star lazima utaniona niko na Ali lakini sasa hivi nilikuwa na maandalizi ya album yangu na inakaribia kwisha.”– Baraka the Prince

Baraka The Prince haukubali wimbo wa Ben Pol, aeleza sababu

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

$
0
0

Bodaboda Achinjwa Kinyama na Kuporwa Pikipiki

$
0
0
Mwanaume mmoja (30) mkazi wa Nyankumbu wilayani Nyamagana mkoani Geita anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la mauaji ya dereva bodaboda yaliyotokea majira ya 3:00 Usiku tarehe 06.05.2017.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza ACP Zarau Mpangule amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Andrea anayedaiwa kupora pikipiki na kumuua dereva wa pikipiki Bw. Alphonce Sekagi (32) mkazi wa wilayani Sengerema wakilishirikiana na wenzake wawili kisha kutoroka na pikipiki kusikojulikana.

Taarifa zinaeleza kuwa marehemu alikuwa dereva bodaboda wa mji wa Sengerema na siku ya tukio alipakia abiria watatu kwenye pikipiki yake wakitokea Sengerema mjini kwenda kijiji cha Tabaruka na kwamba wakati wakiwa njiani abiria hao walimkata dereva huyo na kitu chenye ncha kali shingoni kisha wakamchinja kwa kutumia panga shingoni na kupelekea kupoteza maisha papo hapo.

Kamanda Mpangule amesema wananchi walitoa taarifa polisi kuhusiana na tukio hilo ambapo askari walifanya ufuatiliaji wa haraka hadi eneo la tukio na kufanya msako mkali wa kuwatafuta watuhumiwa wa mauaji hayo katika maeneo mbalimbali kwa kushirikiana na wananchi ndipo  tarehe 01.06.2017 majira ya saa 8:30 mchana wakafanikiwa kumtamata mtuhumiwa mmoja akiwa na pikipiki waliyoipora katika mauaji hayo.

Kamanda Mpangule ameendelea kwa kusema upelelezi na msako wa kuwatafuta watuhumiwa wengine wawili ambapo wanadaiwa kushiriki katika mauji hayo pamoja na uporaji unaendelea huku mtuhumiwa aliyekamatwa anafanyiwa mahojiano na uchunguzi ukikamilika atapandishwa mahakamani.

Chuchu Afungukia Kubuma 40 Ya Mwanaye

$
0
0
BAADA ya 40 ya mtoto wa mastaa wa filamu za Kibongo, Chuchu Hans na Vincent Kigosi ‘Ray’, anayejulikana kwa jina la Jaden kudaiwa kubuma, mwanamama huyo amefunguka kuwa licha ya kuchelewa bado ipo na inakuja ‘soon’. Chuchu aliongea hayo baada ya habari kuenea kuwa mastaa hao wameshindwa kumfanyia mtoto wao sherehe ya kumtoa nje ‘40’ kutokana na hali ya kifedha kuwa mbaya kwao.


“Ni kweli tumechelewa kumfanyia 40 mtoto wetu lakini ‘soon’ itafanyika tu na haya yote yanatokana na maamuzi ya baba yake ndiye aliyepanga hivyo siyo kukosa pesa kama wanavyodai, siku ya shughuli ikikaribia utasikia fununu tu,” alisema Chuchu.

Gigy Aumbuka Na Tattoo Ya Bwanaa’ke

$
0
0
IKIWA imepita miezi michache tangu ajiapize kuwa hatakuja kujichora tattoo ya mwanaume yeyote atakayekuwa naye katika uhusiano, muuza sura kwenye video mbalimbali za wasanii wa Bongo Fleva, Gift Stanford ‘Gigy Money’ ameumbuka baada kunaswa akiwa amejichora jina la mwandani wake, Mourad Alpha ‘Moj’.

Mwanadada huyo ambaye mara kwa mara amekuwa akiingia kwenye mgogoro na Moj kwa madai kuwa amekuwa akimpiga bila sababu za msingi hivyo anatumia nguvu kubwa kuachana naye lakini anashindwa, amejikuta akiumbuka kwa kujichora tattoo ya jina lake. Alipobanwa baada ya kunaswa na tattoo hizo, Gigy alisema;

“Haa unaniuliza, sijui hata nikujibu nini? Nguvu ya mapenzi ndiyo imenisababisha kufanya hivi, migogoro ni kawaida katika mapenzi na kupigwa kila wakati nimeshazoea.

Mfahamu Zaidi Mkuu Mpya Wa Jeshi La Polisi(IGP) Simon Nyakoro Sirro..!!!

$
0
0

Simon Nyakoro Sirro alizaliwa eneo la Kiabakari wilaya ya Butiama mkoani Mara mwaka 1963.
Kuhusu elimu yake, Simon Sirro alisoma Shule ya Sekondari ya Ilboru jijini Arusha na Tosamaganga kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu kusoma Shahada ya awali katika Sheria.

Sirro amesoma pia seminari (masomo ya upadri) na kufikia ngazi ya juu kabla ya kuacha na kujiunga na Jeshi la Polisi.

Kamanda Sirro alisema kuwa kama isingekuwa baba yake basi leo yeye angekuwa ni Padri wa Kanisa Katoliki kwani ndiyo ndoto yake kubwa, lakini baada ya wazazi wake kumkatisha ndipo alipojiunga na jeshi hilo.

Unajua wazazi kule kwetu Musoma walikuwa hawakuelewi usipooa. Mzazi aliona mimi ni kijana mkubwa akasema haiwezekani,” alisema Sirro alipofanya mahojiano na Mwananchi kipindi cha nyuma.

Sirro amewahi kuwa Mkuu wa Upelelezi Kituo cha Polisi Buguruni mwaka 1998, Mkuu wa Upelelezi Tarafa ya Magomeni kwa miaka 5 na Mkuu wa Upelelezi Msaidizi Mkoa wa Tabora.
Mwaka 2002 alikuwa Mkuu wa Upelelezi Msaidizi Mkoa wa Dar es Salaam akiwa ni msaidizi wa Abdallah Zombe.

Sirro ni Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam wa tatu ambapo aliteuliwa na Rais Dkt Magufuli Februari 15 mwaka 2006 akichukua nafasi ya Suleiman Kova aliyeshika wadhifa huo tangu mwaka 2008. Kabla ya Kova aliyekuwa akiongoza Kanda Maalum ya Dar es Salaam ni Alfred Tibaigana.

Wakati Suleiman Kova akiongoza Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Sirro alikuwa msadizi wake ambapo baadae alirithi mikoba yake.

Kabla ya kuongoza Kanda Maalum Dar es Salaam, Sirro amewahi kuwa Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Tanzania. Moja ya opersheni kubwa alizowahi kuongozi ni Operesheni Kimbunga dhidi ya wahamiaji haramu mwaka 2012.

Lakini pia, Simon Nyakoro Sirro amewahi kuwa Kamanda wa Polisi wa Mikoa mbalimbali ambayo ni Tanga, Mwanza na Shinyanga.

Wakuu wengine wa Jeshi la Polisi ni;
1.Elangwa Shahidi (1964-1970), alistaafu.

2.Hamza Azizi (1972-1973), aling’olewa na Mwl. 3.Nyerere kwa matumizi mabaya ya madaraka.
4.Samwel Pundugu (1973-1975).

5.Philemon Mgaya (1975-1980), aliachishwa kazi kwa manufaa ya umma.
6.Solomoni Liani (1980-1984), alihitimisha kipindi cha mwisho cha Mwl. Nyerere.

7.Harun Mahundi (1984-1996), alistaafu.
8.Omari Mahita (1996-2006), alistaafu.
9.Said Mwema (2006-2013), alistaafu.

10.Ernest mangu (2013-2017), atapangiwa kazi nyingine, na
11.Simon Sirro (2017-) yupo madarakani.

Mkuu wa Jeshi la Polisi, Simon Nyakoro Sirro ameoa mke mmoja na ana watoto wanne

Sakata la Manula Kusaini Simba..Azam Watoa Tamko Hili..!!!

$
0
0

Afisa Habari wa klabu ya Azam, Jaffar Iddi amefunguka na kukanusha taarifa zinazoendelea mitaani kuwa kipa namna moja wa Azam FC, Aishi Manula amesaini mkataba na klabu ya Simba na kudai kuwa mchezaji huyo bado atabaki Azam FC.

Jaffar Iddi amesema hayo leo wakati akiongea na waandishi wa Habari ambapo alikuwa akitoa picha jinsi klabu ya Azam itakavyoendeshwa sasa kwa kusema saizi wao watatoa kipaumbele zaidi kwa wachezaji wanaochipukia na kusema klabu hiyo saizi haiwezi haiwezi kutumia gharama kubwa sana kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma katika usajili, huku akisisitiza kuwa mazungumzo ya kuwabakisha Manula na Shomari Kapombe yapo katika hutua nzuri. 

"Nisema tu kwamba Aishi Manula, Shomari Kapombe mikataba yao inakaribia kuisha lakini mazungumzo ya Aishi Manula na Shomari Kapombe yapo katika hatua za mwisho kabisa na nisema tu yanakwenda vizuri. Aishi Manula ataendelea kubaki Azam FC kilichobaki saizi tunategemea wakitoka Misri basi tukamilishe taratibu zao na ninawatoa shaka kuwa Aishi ataendelea kubaki Azam FC hata yeye wakati anakwenda Misri na timu ya taifa aliongea na waandishi wa habari akisema 

"Sitatoka Azam FC labda niende nje ya nchi nikacheze lakini kwa timu za hapa nyumbani sitaweza kufanya hivyo" kwa hiyo kauli yake inaenda na kauli ya klabu ni kweli alikuwa anazungumzwa kuwa anakwenda kwenye klabu za hapa nyumbani lakini yeye mwenyewe ameweka wazi hilo" alisema Jaffar Iddi 

Mbali na hilo Jaffar Iddi amesema kikosi cha Azam FC hakitakwenda nchi yoyote ili kupiga kambi kwa ajili ya maandalizi ya msimu mwingine wa Ligi Kuu Tanzania Bara bali wao wataweka kambi hapa hapa nchini na kudai watakuwa Chamanzi, huku akibainisha kuwa wao wataanza maandalizi ya msimu mpya mwezi wa saba. 

Fahamu Mambo 10 Usiyojua Kabisa Kuhusu Diamond..Afunguka Siku Akiwa Rais Nini Atafanya..!!!

$
0
0

Msanii Diamond Platnumz ameeleza baadhi ya mambo pengine ni vigumu kuyajua kwa kuwa si rahisi kuulizwa katika interview za kawaida. Kupitia kipindi cha The Grill cha Capital Tv Kenya, Diamond amefunguka mambo haya 10 ambayo hupaswi kuyakosa.

1. Mchezo upi wa utotoni unaukumbuka zaidi?.
Jibu: Kibaba baba.

2. Kitu gani unachojivunia?.
Jibu: Kupendwa.

3. Chakula gani unapendelea?.
Jibu: Ubwabwa.

4. Ni mstari upi au wimbo upi usioweza kuhusau?.
Jibu: My Number One.

5. Show yako ya kipekee ni ipi?
Jibu: Niliyofanya Zambia.
6. Ni jambo gani au hali iliyokutia aibu?
Jibu: Nilishawahi kumfumania mpenzi wangu wa zamani.

7. Kama ukipewa nafasi ya kusafiri sehemu yeyote ulimwengu ungependelea kwenda wapi?.
Jibu: Uk (United Kingdom, Uingereza).

8. Ni Mwanamuziki yupi anayekuvutia?
Jibu: Usher Raymond.

9. Hofu yako kubwa ni ipi?
Jibu: Kufa na kuwaacha watoto wangu.

10. Kama ukiwa Rais ni kitu gani cha kwanza kufanya?
Jibu: (anacheka) Kama nitakuwa Rais nitatengeneza mfumo ambao utatoa ajira kwa wengi.

Mwakyembe Awapeleka Serengeti Boys Kucheza Everton ya Uingereza..!!!

$
0
0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk Harrison Mwakyembe amesema ataviomba vilabu vingine vya nje viwachukue wachezaji wa timu ya taifa ya wenye umri chini ya miaka 17 wakapate uzoefu na kukuza vipaji.

“Nimeomba (Everton FC) wachukue vijana wawili kwenye vituo vyao vya kukuza soka la vijana, wamelipokea. Nataka kuona miaka michache ijayo tunakuwa na wachezaji wengi katika anga ya kimataifa,” amesema.

Pia Waziri Mwakyembe amesema ataendelea kuikumbusha klabu hiyo mara kwa mara ili kutimiza lengo hilo na kusisitiza kuwa kuna haja ya kuwatafutia wachezaji hao vituo vya soka vya kimataifa wakapate uzoefu wakuze vipaji baada ya kung’ara kwenye michuano ya Afrika nchini Gabon.

Wasambazaji wa dawa za kulevya wabadili gia

$
0
0

HUENDA wauzaji na wasambazaji wa dawa za kulevya sasa wamebuni mbinu mpya ya kuingiza dawa hizo nchini, kutokana na udhibiti mkali uliowekwa na Serikali.

Badala ya kuingiza kete ambazo zimetengenezwa tayari kwa ajili ya matumizi, wanaingiza kemikali ambazo zina uwezo wa kutengeneza dawa hizo hapa hapa nchini.

Hayo yalielezwa jana na Kamishna Msaidizi Ukaguzi wa Sayansi ya Jinai, Betha Mamuya, alipozungumza na waandishi wa habari katika Bandari kavu ya AMI, iliyopo Tabata Relini.

Katika bandari hiyo jana, maofisa wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Wakala wa Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) walifanya ukaguzi na kubaini makontena mawili yenye zaidi ya lita 5,000 za kemikali bashirifu zinazodaiwa kuingizwa nchini kinyume cha sheria.

Mamuya alisema kemikali hizo zina uwezo wa kutengeneza dawa aina ya heroin na cocaine.

Alisema mzigo huo ni mali ya Kampuni ya Tecno Net Scientific, inayomilikiwa na Benedict Assey na kwamba umeingizwa nchini ukitokea Ufaransa na India.

“Hili ni tatizo la dunia, serikali imedhibiti uingizwaji wa dawa hizi nchini, lakini kwa ‘trend’ hii tunayoiona, tunadhani wamebadili mbinu na kuanza kuzitengeneza nchini na pengine zinasafirishwa kwenda nje,” alisema.

Aliongeza: “Ndiyo maana tunafanya ukaguzi huu, tumeanzia Dar es Salaam, lakini tutakwenda nchi nzima, tutafanya uchunguzi wa kina kujua mzigo huu uliwasili lini nchini.

“Na kwa kuwa mmiliki wa mzigo huu hivi karibuni tulimkuta akiwa na mzigo mwingine, huku taarifa za Wakala wa Mkemia Mkuu wa Serikali zikionesha kibali chake kimekwisha muda, tutachunguza kujua huu wa leo (jana) aliingiza lini, baada ya ukaguzi wa kwanza au kabla.

“Na tutachunguza pia katika maeneo yote ambayo alikuwa akisambaza kemikali hizi, mahitaji halisi yalikuwa kiasi gani na kama zilikuwa nyingi, wapi ambapo walikuwa wakipeleka kiasi kinachobaki,” alisema.

Aliwataka wafanyabiashara ambao wanazileta kihalali kwa mujibu wa sheria wasizichepushe matumizi yake, kwani sheria itachukua mkondo wake.

“Lazima tudhibiti, maana vijana wanaharibiwa kutokana na matumizi ya dawa hizi,” alisisitiza.

Kamishina wa Operesheni wa Mamlaka hiyo, Msekela Mihayo, alisema ukaguzi huo umefanyika baada ya kupata taarifa juu ya uwapo wa mzigo huo katika bandari hiyo.

“Hivyo tunawasihi wananchi waendelee kushirikiana na sisi ili kwa pamoja tuweze kukabiliana na uingizwaji huu tunusuru jamii yetu,” alisema.

Hivi karibuni, Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele, alisema ofisi yake kwa kushirikiana na DCEA na TFDA wamewasilisha taarifa ya pamoja ya ukaguzi kwa vyombo vya dola ili kufanya uchunguzi wa shughuli zinazofanywa na kampuni hiyo.

“Taratibu za uchunguzi zitakapokamilika tunakusudia kuifikisha kampuni hii mahakamani kujibu tuhuma za kuendesha shughuli za kemikali huku ikitambua kuwa kibali chake kimekwisha tangu Aprili 30, mwaka jana,” alisema.

Alisema zipo taarifa kuwa, kampuni hiyo imekuwa ikighushi vibali na njia nyingine za udanganyifu kuingiza kemikali nchini.

“Kwa mujibu wa sheria, baada ya muda wa usajili kwisha kampuni husika hutakiwa kusitisha shughuli zake hadi hapo itakapopata kibali.

“Baada ya muda wa kibali kwisha kampuni hii iliwasilisha maombi ya kuhuisha usajili wake, lakini ilitakiwa kusubiri kibali, lakini iliendelea na shughuli zake, jambo ambalo ni kinyume cha sheria,” alisema.

Profesa Manyele aliwataka wafanyabiashara wa kemikali kuzingatia sheria za uingizaji, usafirishaji, uhifadhi na utumiaji wa kemikali, ikiwamo bashirifu.

Hivi karibuni, Assey alikamatwa kwa kuingiza kemikali bashirifu zenye ujazo wa lita 6,494 kwa kukiuka sheria na taratibu.

Mbunge ammwagia sifa Wema Sepetu, Adai ameumbika

$
0
0

ACHANA na umahiri wake awapo bungeni. Weka pembeni sauti yake ya mamlaka na wala usijishughulishe hata kidogo na ujasiri wake wa kumnaga yeyote. Joseph Kasheku ‘King Msukuma’ ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini ametoa ya moyoni na kukiri urembo na ‘figa’ ya msanii Wema Sepetu haupishani na uzuri wa samaki aina ya Nguva, Ijumaa bwana teh…teh… teh…teheeeeee.

Jumatatu ya wiki hii, saa saba na dakika zake mchana, mwandishi wetu akiamini King Msukuma atakuwa nje ya viunga vya bunge akiifaidi posho yake, aliamua kumtafuta kupitia simu yake ya mkononi kwa lengo la kubadilishana naye mawazo juu ya mambo mbalimbali ya kimaendeleo ndipo suala la uhusiano wake na Wema Sepetu likaibukia katikati ya mazungumzo na mbunge huyo kulitolea ufafanuzi.

TULIANZIA HAPA

Siku nne mfululizo za wiki iliyopita, mwandishi wa habari hii alimtafuta mbunge huyo kwa lengo la kufanya naye mahojiano juu ya mambo mbalimbali, ambapo alipokea simu na kusikiliza huku akimuomba mwandishi ampigie baada ya dakika tano kwa kile alichodai… “kuna kitu naweka sawa hapa…”

ATAFUTWA TENA

Baada ya muda huo, mwandishi wetu akiwa na shauku kubwa ya kufanya mahojiano na mbunge huyo machachari ikiwa ni mara yake ya kwanza kuingia bungeni akiwakilisha jimbo jipya, alimpigia simu tena lakini hakupokea, lakini alipotafutwa saa moja usiku siku hiyohiyo, alipokea na kumsikiliza mwandishi wetu kwa kirefu.

AKUBALI KUFANYIWA MAHOJIANO

Muda huo wa saa moja, King Msukuma alikubali ombi la mwandishi ambapo alimuomba ampigie siku iliyofuata (Ijumaa) saa nne asubuhi.

ATAFUTWA, ATOA UDHURU TENA!

Gazeti la Ijumaa huwa halikati tamaa. Siku iliyofuata alitafutwa lakini alimtaka mwandishi wetu amuache kwani alikuwa hospitali akidai kusumbuliwa na tumbo, jambo lililomfanya mwandishi kumpa muda wa kupumzika.

JUMAMOSI NA JUMAPILI ZIII…!

Jitihada za kumtafuta mbunge huyu ziliendelea kwa siku za Jumamosi na Jumapili lakini hakuwa akipokea simu jambo lililoacha maswali mengi kwa mwandishi wetu.

HATIMAYE JUMATATU TIII…!

Sisi nao! Jumatatu ya wiki hii, kama ilivyoelezwa kwenye aya ya pili ndipo mheshimiwa huyo aliweza kuzungumza kwa kirefu na mwandishi wetu ambapo bila kuremba alimtaka aeleze alichofanya jimboni kwake ikiwa ni pamoja na kufungukia madai ya muda mrefu ya kuwahi kuwa ‘close’ sana na msanii Wema Sepetu. Kuhusu mambo ya maendeleo jimboni kwake alimtaka mwandishi wetu avute subira hadi Bunge la Bajeti lipite ndipo atapata muda mzuri wa kukusanya data kamili za utendaji na utimizaji wa ahadi zake jimboni, lakini suala la Wema akalifafanua.

MSIKILIZE MWENYEWE

“Hayo mambo hayawezi kuwa na maana yoyote ya kimaendeleo, muhimu ni kuzingatia utendaji kazi wa mtu na si kutazama mambo ya namna hiyo. Wewe mwenyewe unamuona jinsi huyo mwanamke (Wema) alivyo, mtoto kaumbika kama nguva (aina ya samaki, yaani mtoto ni mashallah na, tena kaumbika namna hiyo, kawaida sana katika maisha,” alisema mheshimiwa huyo.

WEMA ATAFUTWA

Mwandishi wetu pia alifanya jitihada za kumtafuta Wema ili kuzungumzia sifa alizopewa na mheshimiwa huyo lakini kila simu yake ilipopigwa ilikuwa ikiita bila kupokelewa. Hata hivyo, kwa wanawake wengi wamekuwa wakijisikia poa sana wanaposifiwa na wanaume na pia si jambo baya kwa mwanaume kumsifia mwanamke. Kwa maana hiyo alichokifanya Mheshimiwa Msukuma ni kueleza hisia zake, jambo ambalo siyo dhambi hata kidogo.

Usirogwe Ukampa Mtu Lift Njiani Usiyemjua, Kumbe Niliyembeba Alikuwa Mgonjwa Sana Akafariki..!!!

$
0
0

Duniani kuna mambo mengi sana,na mengine ni mikosi!

Kuna siku nilikuwa nasafiri na gari kutoka kijiji kimoja kwenda kingine. Njiani porini nikamkuta jamaa mmoja anatembea kwa miguu kuelekea uelekeo niliokuwa na kwenda na alikuwa kabeba mfuko we rambo mweusi. Alionekana kachoka sana, nikajua ni sababu ya jua na umbali mrefu.

Nilipotembea kama 10 km, nikafika kijiji alichosema anakwenda, basi nikasimamisha gari. Nikaita "mzee..mzee...tumefika shuka". Akawa kimya. Nikarudia tena, kimya. Kugeuka nyuma ya seat naona mtu kalala. Nikamshika mkono, tingisha kimya. Mungu wangu, nikasema nini tena hii.

Akili ikanijia nimshushe pale barabarani nisepe. Kucheck pembeni nikaona wanakijiji wamekaa. Nikajua hapa noma sasa. Nikamuacha kwenye gari, nikawasha gari na kukimbia kituo cha Polisi. Kufika Polisi na kutoa maelezo, kucheck mtu amefariki. Sitasahau.

Nikawekwa rokapu kwanza kwa siku moja. Kesho yake baada ya uchunguzi, Polisi wakaniambia yule alikuwa mgonjwa na alitoka hospitali kwa daktari kuchekiwa. Na mfuko wake wa rambo ulikuwa na kadi ya hospitali na dawa alizopewa huko hospitali.

Hiyo ikawa pona yangu.

Lakini nilipoteza muda, hela, kuharibu ratiba zangu sana kwa sababu ya kumoa lift mtu nisiyemjua halafu kumbe ni mgonjwa.

Tuwe makini sana.
Viewing all 104781 articles
Browse latest View live




Latest Images