Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104694 articles
Browse latest View live

Yasemwayo Mitandaoni Baada ya Rais Magufuli Kumteua Anna Mghwira wa ACT Kuwa Mkuu wa Mkoa

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo amemteua Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo, Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Rais Magufuli amefanya uteuzi huo ambapo Mghwira anachukua nafasi ya Said Meck Sadick aliyeandika barua kwa Rais akiomba kujiuzulu mwezi Mei mwaka huu.

Uteuzi huo umemkuta mwenyekiti wa ACT Wazalendo akiwa katika kongamano la chama hicho lililokuwa likijadili sakata la kuzuiwa kwa mchanga wa madini kusafirishwa kwenda nje. Hadi sasa chama hicho na mteule hawajatoa taarifa yoyote kuhusu uteuzi huo.

Watu mbalimbali kupitia mitandao wametoa maoni yako kuhusu uteuzi huo, jambo kubwa likiwa ni kwa namna gani kiongozi huyo atakwenda kutekekeleza ilani ya Chama cha Mapainduzi. Wengi waliotoa maoni walisema kuwa, Mkuu wa Mkoa ni mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM na mjumbe wa vikao vya CCM Mkoa, hivyo swali linakuwa, je! Anna Mghwira ambaye ni mwanachama wa ACT Wazalendo, ataingia kwenye vikao vya CCM?

Hapa chini ni maoni ya baadhi ya watumiaji wa mitandao kuhusu uteuzi huo. Na wewe unaweza kuandika maoni yako chini mwishoni mwa habari hii.

KATIBA INASEMA MKUU WA MKOA AMBAYE NI MWANACHAMA KUMBE KUNA AMBAYE SIYE MWANACHAMA ….HAIHITAJI DEGREE YA SHERIA
KUONA HILI 

— HENRYAMANI (@HENRYMSUYA1) JUNE 3, 2017
HONGERA SANA MAMA 👏👏KWA KUTEULIWA NA RAIS KUWA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO, NAKUAMINI SANA 

— DAVID GUNDA (@DAVIDGUNDA1) JUNE 3, 2017
MKUU WA MKOA NI MJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CCM NA MJUMBE WA VIKAO VYA CCM MKOA! JE, ANNA MWIGIRA ATAKUWA ANAHUDHURIA VIKAO VYA CCM?

— OLE’SEIF (@MBOBEZI) JUNE 3, 2017
SASA WABUNGE WA CCM WAJIFUNZE KUTOKA KWA MHESHIMIWA RAIS. WAKATI YEYE ANAONA KARAMA YA UONGOZI KWA UPINZANI, WABUNGE CCM WAFUATE NYAYO HIZO

— DOTCODOTTZ (@BMATUNGWA) JUNE 3, 2017
KWA MAANA HIYO CHAMA CHA MAPINDUZI HAKINA MWANACHAMA AMBAYE ATAWEZA KUWA MKUU WA MKOA?

— NTOBI (@IMMANTOBI) JUNE 3, 2017
KITILA KATIBU WA WIZAR YA MAJI ANNA MWINGIRA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO KWA MAANA @ACTWAZALENDO KUNA VIONGOZI MAKINI SOON @ZITTOKABWE

— DR SOKO JR (@NATHANIELIMANI) JUNE 3, 2017
SIO TU KAWA MKUU WA MKOA KILIMANJARO; BALI PIA MJUMBE WA KAMATI YA SIASA YA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA KILIMANJARO! @ZITTOKABWE @CHAHALI

— LIBERATUS MWANG’OMBE (@LIBEBAGASA80) JUNE 3, 2017
KITILA ACT :KATIBU MKUU WIZARA YA MAJI
ANNA MGWIRA ACT :MKUU WA MKOA KILIMANJARO
ZITTO KABWE ACT :WAZIRI NISHATI NA MADINI. END OF STORY.

— HANDSOME LA KIJIJI (@MANENOIZAAK) JUNE 3, 2017
MKUU MPYA WA MKOA WA KILIMANJARO KWENYE MAJUKUMU YAKE ATATUMIA ILANI IPI SASA?YA CHAMA CHAKE AU TAWALA?BADO NAWAZA🤔



KWA MUJIBU WA KATIBA YA CHAMA CHETU, MKUU WA MKOA NI MJUMBE WA KAMATI YA SIASA YA MKOA, HONGERA ANNA MGWIRA NA KARIBU CCM !!

— MCHOKOZI!! (@OLEMTETEZI) JUNE 3, 2017
ITAKUWAJE MAMA MGHWIRA ATAKAPOPEWA “MAELEKEZO KUTOKA JUU” KUZUWIA MKUTANO WA ZALENDO MKOANI MWAKE? #THINKINGALOUD  

— EVARIST CHAHALI (@CHAHALI) JUNE 3, 2017
ACT ND’O IMEISHA HIVO…KITILA KACHUKULIWA, MSANDO KACHUKULIWA NA GIGY…ANNA MGHWIRA NAYE KACHUKULIWA…KABAKI ZITTO PEKE YAKE😂😂😂

— MR BEN (@ERICBERNARD692) JUNE 3, 2017
NAENDELEA KUMTIA MOYO @ZITTOKABWE ASIVUNJIKE MOYO HATA KAMA UTALAZIMISHWA KUPITA KWENYE MTEREMKO WENYE UTELEZI MKALI. KEEP DOING WHAT YOU DO


Yaliyomkuta Davido Kutoka Sony, Sasa ni Zamu ya Alikiba

$
0
0
Label ya sony imekuwa ikilalamikiwa jinsi inavyotreat wasanii mbalimbali wanaotokea Africa, pia imekuwa ikihusishwa na uuaji wa vipaji vingi barani hapa

Baada ya mwaka jana, Msanii Davido kusoteshwa na kuzuiliwa kutoa nyimbo mpya na label yake hii ya sony baana ya kusain nao mkataba mpaka hali hii ikazua maswali na mtafaruku mkubwa juu ukimya wake wa muda mrefu isivyo kawaida, sasa hali hiyo imemkuta msanii wetu kipenzi cha watu ALIKIBA

Ni zaidi ya mwaka sasa tangu alikiba alipoachia smash hit yake iliyotamba sana "Aje"
baada ya hapo ukimya umetawala pasi na washabiki wake wasijue nini cha kufanya

inasemekana sasa Sony ndio wanamuhenyesha nguli huyu na kusubilisha kutoa ngoma mpya mpaka hapo watakapoamua!

Hili jambo litakuwa na impact mbaya kwa Kiba, hasa ukiangalia jinsi ushindani ulivyo kwa sasa katika game yetu hapa nchini na afrika kwa ujumla

Sony, tuachieni msanii wetu atupe Raha "tumechoka" sasa

Kutana na Mtaalamu wa Tiba Asili Ostadh Khamis Kutoka Mombasa..Yupo Tanzania....Anatibu Magonjwa Yafuatayo

$
0
0

Kutana na OSTADH khamis kutoka Mombasa Kenya kwa sasa yupo Tanzania nibingwa watiba za asili:

Miguu kuuma miguu kufagazi nakuwaka moto
Unashida na mchumba au pesa haikai muone haraka 
Kurudisha mpenziwako alie kukimbia ndani ya siku (3)
Dawa ya ( LIMBWATA) kumtawala mpenzi wako kwasababu maalumu   
Pete ya bahati inayo endana nanyota yako itakayo kuletea pesa bila mashart yeyote
Kuongeza uume saizi uipendayo 
Dawa ya ulijali 
Dawa yakuongeza hips
Kumuliki Mali isiokuwa namasharti yeyote 
Kurudisha Mali iliopotea au kudhurumiwa ndani yasiku(3) 
Napia OSTADH KHAMIS anafunga kesi nakupata hakiyako kwa haraka 
Dawa ya mvuto pia inapatikana mvuto Wa biashara kuuza Mali yako kwa haraka 
Kuzuiya chuma ulete na kupandishwa cheo kazini PAMOJA na kusafisha nyota njoo ufunguliwe vifungo ulivyo fungwa

Call+255718746825 au +255754765246 WhatsApp IMO +255783708487

Ben Pol na Mchekeshaji Abitoke Sio Siri Tena..Abitoke Afunguka

$
0
0

From @ebitoke - Nimeona niweke comedy pembeni leo naongea kitu siriazi.

Najua wengi hamjawahi kuona nikipost mpenzi wangu ila nimeona leo niweke wazi. Kwa muda mrefu nimeficha hisia zangu kwa mwanaume huyu sababu nilikua naogopa kumueleza ukweli leo nimeona niseme ukweli.

Nampenda sana @iambenpol Natamani awe mpenzi wangu wa maisha, sijui kama anayempenzi wake au laa ila natanguliza samahani kama nimemkosea kumueleza hisia zangu mtandaoni nahisi siwezi kumueleza live naomba mliokaribu nae mumueleze hisia zangu.

Niko tayari kuolewa nae wakati wowote. Najua wengine mtanitukana au kunikejeli kua sina hadhi ya kuwa mpenzi wake.

Naombeni mumfikishie ujumbe huu @iambenpol
Mwambieni NAMPENDA
💟💟💟💟 😍😍😍😍
#TrueLove -

Huzuni Sana ..Zari Asimulia Alivyokiona Kifo cha Ivan Siku Chache Kabla ya Kufa..Afunguka Mengine ya Siri Kuhusu Ivan na Yaliyokuwa Maisha Yao kwa Ujumla..!!!

$
0
0

SIKU chache baada ya mfanyabiashara maarufu nchini Uganda, Ivan Ssemwanga ‘Ivan Don’ kuzikwa, aliyekuwa mkewe Zarina Hassan ‘Zari the Boss Lady’ ameeleza namna alivyokiona kifo cha Ivan Don.

Akizungumza na mtandao mmoja wa burudani, Zari alisema alipewa taarifa na madaktari mapema baada ya hali ya Ivan kubadilika.


Zari alikuwa akijibu swali aliloulizwa na mtandao huo iwapo tetesi kuwa aliyekuwa mumewe Ivan alikufa kwa sumu au lah.

 “Ivan alikuwa na presha ya kupanda na hakuwahi kupima… na kama alipima hakuwahi kuichukulia serious na kuanza kutumia dawa.

“Kilichotokea ni kwamba alipata kiharusi, hapo presha nayo ikapanda… presha ikiwa juu, akapooza upande mmoja wa mwili wake ambao ulikuwa wa kushoto.

“Kiharusi kilimpiga vibaya, akapasuka mshipa kichwani ambao ulimwanga damu kwenye ubongo. Madaktari wakaniambia asilimia kubwa ya wagonjwa wa aina yake, asilimia 80 hufariki dunia mara moja.

“Asilimia 20 inayobaki, asilimia kumi huweza kufariki ndani ya mwezi mmoja na asilimia kumi nyingine; kama wakibahatika kupona huwa hawawezi kufanya chochote tena. Ni wa kuwavalisha pempasi, kuogeshwa, kulishwa na nk,” anasema Zari.

Zari anaongeza: “Baadaye wakaamua kumfanyia upasuaji lakini haikufanikiwa kwa sababu presha yake ilikuwa inapanda na kushuka kila wakati, wakamrudisha wodini kujaribu kumsaidia kwa njia nyingine.

Anasema siku mbili baadaye alipigiwa simu na daktari akamwambia aende kumuaga Ivan kwa sababu hali yake haikuwa nzuri.

Presha yake ilikuwa ikipanda hadi kufikia 220, badala ya kiwango cha kawaida cha 120 – 125, hali ambayo Zari anaielezea kuwa madaktari walimwambia haikuwa nzuri.

“Siku anafariki, nilipigiwa simu mida ya saa mbili usiku, nikaambiwa kwamba Ivan amefariki. Lakini siku moja kabla tulielezwa hilo na tulizuiwa kumtembelea wodini maana alikuwa kwenye process ya kufariki. Tukashauriwa tumwache apumzike akiwa kwenye hali ya utulivu.

“Tuliambiwa tumuage, tukafanya hivyo. Siku hiyo iliisha bila taarifa yoyote hadi siku iliyofuata saa mbili usiku. Kwahiyo siyo sumu, Ivan amekufa baada ya mshipa wa kichwani kupasuka na kusambaza damu kwenye ubongo, pamoja na kiharusi,” anasema Zari.





MAMBO YALIYOZUA GUMZO MSIBANI

Ivan Don alizikwa Jumanne wiki hii, katika makaburi ya ukoo, kijijini kwao Kayunga, nje ya jiji la Kampala, Uganda ambapo walihudhuria maelfu ya watu wakiwemo mastaa  wa Uganda na nchi jirani.

Kwa hakika maziko ya Ivan Don ambaye alikuwa kiongozi wa Kundi la Uganda Rich Gang Family, yamedhihirisha namna alivyokuwa  na utajiri wa mali na watu wenye mapenzi mema naye.

Yametokea mengi kwenye msiba huo, lakini hapa utaona  yale yaliyozua gumzo zaidi siku na wakati wa msiba wake.



DIAMOND KUTOHUDHURIA

Mpenzi wake na Zari, mwanamuziki Diamond Platnumz aliahidi kuhudhuria maziko hayo, lakini hakuweza kufanya hivyo.

Jambo hilo lilizua gumzo kubwa mitandaoni kwani wengi waliamini angefika kutokana na ahadi yake lakini hata namna alivyoonyesha utu na kujali kiasi cha kumruhusu Zari kusafiri hadi Sauzi alipokuwa akipatiwa matibabu kabla ya kifo chake.

Hata hivyo Meneja wa Diamond, Sallam SK alisema walipanga Diamond ahudhurie maziko hayo, lakini ratiba ziliingiliana.

Anasema walipanga Diamond aingie huko Alfajiri ya Jumanne, lakini ndugu wa marehemu wakaamua kusafirisha mwili usiku wa Jumatatu hivyo mipango ikavurugika.



AZIKWA NA FEDHA

Katika kile kilichoonekana kufuru, wakati mwili wa Ivan ukiwa tayari kaburini, marafiki wa marehemu Ivan, matajiri wa Uganda walianza kutupia fedha kaburini.

Ni kama vile walikuwa wakimtuza mtu, lakini ukweli ni kwamba walikuwa wakimwaga fedha kaburini, jambo ambalo lilizua maswali mengi kuliko majibu.



BIASHARA MSIBANI

Kwenye eneo la msiba kulikuwa tofauti kabisa na misiba mingine; msiba wa Ivan ulikuwa maalum na wa kistaa.

Wafanyabiashara wadogo walitumia nafasi hiyo kutengeneza fedha kwa kuuza vyakula, tisheti, kofia na vipeperushi vyenye picha na maelezo kidogo juu ya marehemu.



ZARI ATUKANWA

Wakati shughuli za msiba huo zikiendelea, Zari alikuwa akiposti picha na maelezo kwenye ukurasa wake wa Instagram ili kuwaonyesha wadau kinachoendelea, lakini wapo ambao hawakumuunga mkono na kumtolea lugha sizizo na staha.

Hata hivyo,  mwigizaji wa Bongo, Wastara Juma alijitosa kumtetea ambapo alisema wanaomsema vibaya Zari wamekosa utu.

“… mimi ni mama sijawahi kusahau uchungu wa mwana na wala sijamsahau aliyenifanya niitwe mama lakini usiniulize kwanini sipo na niliyezaa naye ni mambo binafsi sana sio lazima kila mtu ajue lakini akifa nitaenda na ikibidi kulia nitalia sababu alikuwa na bado atakuwa baba wa watoto wangu…

“Lakini why why why mtu atukanweee weee asemwee kipindi kibaya cha uchungu na mawazo kama hiki? Hivi jamani mnajua kufiwa kweli wenzangu, mbona hili la Zari kutukanwa limenishinda kabisa kuvumulia. Mungu amlaze mahali pema Ivan – Amen.”



MTOTO MWINGINE WA IVAN

Baada ya kifo cha Ivan, imeelezwa kuwa mbali na watoto watatu aliozaa na Zari (Pinto, Didy na Quincy), ana mtoto mwingine mmoja wa kike.

Akifafanua hilo, Zari alisema ni kweli Ivan anaye mtoto huyo lakini siyo wa kumzaa bali alimuasili kutoka kwa kaka yake ambaye alifariki kwa kupigwa risasi na majambazi waliokuwa wakijaribu kumwibia Zari, ndipo Ivan kwa heshima akaamua kumuasili mtoto huyo kwa vile baba yake alifariki akipigania familia yake.

Mchanga wa Madini Waendeleza Mvurugano Bungeni..Wabunge Waungana Kutaka Mikataba Yote Ipelekwe Bungeni !!!

$
0
0

Zuio la kusafirisha mchanga wa madini kwenda nje ya nchi liliwagawa wabunge katika mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini uliofanyika wiki hii.

Licha ya wabunge wengi kukubali kwamba Taifa halinufaiki ipasavyo kutokana na uchimbaji wa madini pamoja na rasilimali nyingine zinazoendelea kuvunwa nchini, baadhi ya wabunge, hasa wa upinzani, hawakubaliani na namna mchakato mzima unavyoendeshwa.

Hoja inayotolewa na wapinzani ni ubovu wa sera, sheria na mikataba yote ya madini ambayo mingi haijawekwa wazi hivyo kutolinufaisha Taifa kwa kiasi kilichotarajiwa.

Wapinzani wanataka mchakato wa kufanya marekebisho yoyote uanzie katika mikataba badala ya mchanga ambao ni sehemu ndogo ya kinachopotea.

Akichangia hoja, mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa alisema agizo la Serikali linaweza likawa na athari kwa wawekezaji wa sekta ya madini ambao mitaji yao imeelekezwa huko.

Alikumbusha kwamba wizi wa madini ulielezwa siku nyingi hata ripoti ya baadhi ya tume zilizoundwa zilibainisha mapungufu yaliyomo na kushauri yaliyoelezwa ndiyo yanapaswa kupewa kipaumbele katika mapambano haya.

Mwita Waitara, mbunge wa Ukonga (Chadema), alisema tatizo lililopo ni mikataba ya madini ambayo haijawahi kupelekwa bungeni ili wawakilishi hao wa wananchi waione na kutafuta namna sahihi ya kurekebisha kasoro zilizopo.

Alisema licha ya Rais kuunda kamati ya kuchunguza na wabunge wengi kuguswa na wizi wa madini, bado mjadala unaoendelea unakosa uhalisia kwa sababu kila mmoja anatoa hoja bila kujua mkataba una vifungu vipi vinavyotekelezwa. Alisema kwa kuwa mikataba ilipitishwa na chama tawala ambacho leo kimegundua kuibiwa, “wabunge wanahitaji kuiona mikataba hiyo na kujua mambo mliyokubaliana.”

Wakati wabunge hao wakipendekeza hayo, Waziri Kivuli wa Nishati na Madini, John Mnyika alisema mwisho wa siku atakayepoteza kwenye vita hivi ni Serikali ambayo italazimika kuilipa Kampuni ya Acacia inayosafirisha mchanga huo fidia kutokana na hasara itakayopata kwa muda wote wa zuio.

Wabunge wengi wa chama tawala wanamuunga mkono Rais kwa hatua hiyo, wakisema ni namna sahihi ya kwenda kwenye mabadiliko ya mikataba iliyosainiwa siku nyingi na wawekezaji waliopo.

Mbunge wa Mbinga Mjini (CCM), Sixtus Mapunda alisema hata kama watakaoathirika na agizo hilo wataenda mahakamani na Serikali ikawa na uhakika wa wizi huo, itashinda kwa kuwa suala hilo halikuwa sehemu ya mkataba.

“Hawatafanya chochote tukiwa na ushahidi. Tume ya kwanza imeonyesha udanganyifu ambao ni kinyume na masharti ya mkataba. Hata wakienda popote tutawashinda. Nampongeza Rais kwa anachokifanya,” alisema.

Msimamo wa Mapunda unafanana na wa Mbunge wa Muheza, Balozi Adadi Rajab ambaye alisema mchakato huo unapaswa kuendelea kwani hakuna kitakachoitisha Serikali.

“Tukiwa na ushahidi, hata tukishtakiwa tutaenda kutoa argument. Tunaibiwa, huo ni ukweli, tunaweza kubishana kwenye kiwango tu,” alisema ambaye kitaaluma ni mwanasheria.

Wabunge kutoka maeneo yenye migodi walitoa ushahidi wa wizi unaofanywa. Mbunge wa Msalala (CCM), Ezekiel Maige alisema suala hilo lilikuwapo anakotoka kiasi cha kuwashawishi wananchi kuyavamia malori yaliyokuwa yanasafirisha mchanga huo na kuuiba.

“Walipochenjua kwa njia za kienyeji, kiroba cha kilo 50 cha mchanga kilitoa mpaka Sh50 milioni. Sasa hivi ulinzi umeimarishwa, malori hayo yanasindikizwa na askari wenye silaha,” alisema Maige ambaye ni mtaalamu wa biashara.

Mbunge wa Geita (CCM), Joseph Msukuma aliwataka wabunge wenzake, bila kujali itikadi kuungana kwenye vita hii kwani jamii zinazozunguka migodi zinafahamu athari za kudumu za wawekezaji wa sekta hii.

“Wametuachia mashimo makubwa. Njooni muyaone. Wameondoka na kila kitu wakati wananchi wanaozungua bado ni masikini na hawana huduma za uhakika za jamii,” alisema Musukuma.

Aliwananga wanaopinga hasa Chadema kwamba wanawatetea wezi hao wa madini ambao kamati imeanika wanachokifanya kwakuwa wamepokea fedha ili wafanye hivyo na wanachokisema kinawaondolea uzalendo mbele ya jamii.

“Nawafahamu waliopewa fedha. Niwataje…niwataje! Semeni basi. Tunajua kuwa mna-retire imprest mlizolipwa,” alisisitiza Musukuma.

Ni suala lililomgusa hata Spika wa Bunge, Job Ndugai aliyesema Bunge lake linaunga mkono hatua alizochukua Rais kukabiliana na jambo hilo kubwa ambalo halifai kufumbiwa macho na akataka kupuuzwa kwa wanaowatetea wezi wa madini. “Hatuwezi kuwa tunaibiwa halafu tunacheka cheka. Hii ni vita kubwa ingawa wapo wat wanaotetea. Unakuta ni mbunge anayetoka sehemu yenye upungufu wa madawati, dawa hospitalini na barabara mbovu. Hii ndiyo namna ya kuwatambua. Mngejuaje sasa? alisema Ndugai akiahirisha kikao cha Bunge Ijumaa.

Chadema Watoa Tamko Juu ya Mnyika Kusukumwa na Askari wa Bunge...!!!

$
0
0

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Ubungo kimesema kitendo cha Mbunge wa Jimbo la Kibamba, John Mnyika kutolewa kwa nguvu Bungeni Juni 2, si cha kiungwana.

Akizungumza leo (Jumapili), Juni 4,  Katibu Mwenezi wa Chadema, Ubungo, Perfect Mwasiwelwa amesema Wapinzani akiwamo na Mnyika wamekuwa watetezi wa masuala ya madini kwa miaka takribani 20 ila sasa wanaonekana sio wazalendo wa Taifa lao.

"Kitendo cha Mnyika kubebwa mzobemzobe na kutupwa nje ya mlango wa bunge na ukiangalia mazingira alitaka kudondoka, kwa kweli ni kitendo cha kinyama, sio cha kiungwana, sio cha kibinadamu na Kitanzania kabisa," amesema Mwasiwelwa.

Amesema kuwa Chadema inapinga matumizi ya nguvu  kwa ajili ya kuzima upinzani kupigania suala la madini kama ilivyofanyika kwa Mnyika ambaye ni Waziri kivuli wa Wizara ya Nishati na Madini.

Taarifa mpya za mtoto Doreen wa ajali ya Lucky Vincent

$
0
0

Mtoto Doreen Mshana, manusura wa ajali ya Lucky Vincent, ameruhusiwa kutoka Hospitali na sasa ameungana na wenzake wawili katika nyumba maalum wanamoishi, Marekani, jimbo la Iowa.


 Awali, wanafunzi wengine waliokuwa wakitibiwa katika Hospitali ya Mercy Hospital, Sioux City, Saidia Awadh na Wilson Tarimo,   waliruhusiwa kutoka hospitali walimokuwa wakitibiwa.


Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu, ameandika katika ukurasa wake wa facebook na kueleza kuwa sasa Doreen, ameungana na wenzake baada ya hali yake kuimarika.


 Doreen, alibaki hospitali hapo kutokana na majereha makubwa aliyopata na hivyo kulazimika kufanyiwa upasuaji mkubwa wa uti wa mgongo.


 Wanafunzi hao walinusurika katika ajali ya basi la shule ya msingi ya Lucky Vincent, iliyoua wanafunzi 32, walimu wawili na dereva, Mei 6 mwaka huu, Karatu, Arusha.

Q Boy Msafi akana kuupinga mtandao wa wasafi.com

$
0
0

Msanii wa Bongo Fleva, Q Boy Msafi ambaye alikuwa mbunifu wa mavazi ya Diamond Platnumz amesema si kweli alikuwa anapinga ujio wa mtandao wa wasafi.com kitu kilichopelekea kutimuliwa WCB.

Q Boy ameiambia kipindi cha cha The Play List cha Times FM,  wakati mtandao huo unaanzishwa yeye tayari alikuwa nje ya WCB.

“Suala la wasafi.com hata walipozindua mimi sikuwepo. Hata maandalizi for real nilikuwa mbali na vikao ambavyo walikuwa wanafanya kwa sababu nilikuwa out of wasafi na nilikuwa nimeshanza kufuatilia ishu zangu lakini nilikuwa na fununu kuwa wasafi wanafungua mtandao,” amesema Q Boy.

Katika hatua nyingine Q Boy amesema sababu ya wimbo wake mpya ‘Karorero’ kutokuwepo katika mtandao huo ni kwamba tayari alikuwa ameshauuza kwa watu wengine.

“Wimbo wangu wa pili sikuupeleka ila bosi Tale aliniandikia kwenye Whats App fanya ulete wimbo wako kwenye wasafi .com lakini mimi nilikuwa nimeshakaa chini na watu ambao nilitaka kuwapa caller tunes, so sikuweza kuchanganya,” ameongeza

Ukweli Mchungu..Freeman Mbowe Chukua Mfano Kutoka kwa Msando, Jiuzulu Uwenyekiti wa CHADEMA..!!!

$
0
0

Wiki kadhaa nyuma mjumbe wa kamati ya juu wa chama cha ACT na wakili aliyebobea alikutwa na kashfa baada ya video yake na msanii Gigi kuvuja jambo lililopelekea jamii ku-react na kuanza kumshambulia Msando sababu kaidhalilisha familia yake.Bila ya hiari Albert Msando alichukua hatua ya kuandika barua na kujiuzulu wadhifa wake kama uwajibikaji.

Leo kuna jumbe ya sauti ya mwenyekiti wa enzi wa chadema Mh.Freeman Aikael Mbowe ikionekana ikichepuka na kada mpya Wema Sepetu.Hii scandal haina tofauti na ya Albert Msando.Kama Albert Msando tulimshambulia kwa kutoka na Gigi na tuliongea mengi kama vile kaidhalilisha ndoa yake na hakumfanyia fair mke wake na pia taswira yake kwenye jamii ameiharibu basi hivyo hivyo kwa mwenyekiti wa chadema.

Kwako Mbowe jambo ulilolifanya halikubaliki "sex scandal" viongozi wengi USA na Eu waliwajibika sababu ya sex scandal na hapa nyumbani wakili msomi Msando aliwajibika baada ya video yake kuvuja.Tunakutaka uwajibike chukua mfano kutoka kwa Msando jiuzulu uwenyekiti wa chadema na uongozi wa kambi rasmi ya upinzani ili ulinde reputation yako.

Chanzo JF

Kimenukaa..Gwajima Aaanzisha Upya Vita na Makonda,Magufuli na Mmiliki wa Star Tv..Leo Amefunguka Haya Mazito Kanisani Kwake..!!!

$
0
0

Leo akiongea katika kanisa la UFUFUO NA UZIMA maeneo ya Ubungo Tanesco amesema kwamba Makonda au bashite ni ziro brain na kwamba bado hana uwezo wa kuongoza watu na pia kumuomba Mh Rais Magufuli ampangie kazi nyingine.

" Professa Muhongo alipendwa na Rais Magufuli sana lakini siku ya mwisho ameondolewa, itakuwa huyu mwenye ziro brain yaani sifuri kabisa..." alisema MchungajiJosephat Gwajima.

Pia amesema hawezi kila siku kuongelea kuhusu huyu Bashite na kwamba ana shughuli nyingi za maendeleo za kuzifanya na huu mjadala wa Daudi Albert Bashite ameshaufunga sema kuna vijana wanamchokono chokonoa sana.

"..alikuwepo Kamanda Kova, Sheikh Yahaya lakini Leo wako wapi? Atakuwa huyu ziro brain kabisa yaan hamna kitu kichwani (Bashite)..." Alisema Dr Bishop Josephat Gwajima.

Pia ameenda zaidi na kutoa no ya baba yake Paul makonda ambaye ni Albert Nyange Bashite ambaye ana no ya simu iliyosajiliwa kwa jina hilo 0755543803 MPESA.

Amesema Makonda anamtukana Ruge wa Clouds na kwamba RUGE ana Degree of Marketing toka Califonia Marekani (USA) pia kitendo cha makonda kuvamia Clouds sio Uvamizi but ni igizo lakini kwa nini alienda na Askari wenye silaha katika studio za Cloids Media.

Nape ana elimu kubwa sana amesoma India diploma, degree pia na Masters amechukua Mzumbe lakini Bashite/ Makonda hana hata Cheti cha Nursery wala Certificate..

Gwajima amesema pia kwamba yeye ana PhD na kwamba Makonda sio size yake kabsa kwa sababu yeye ni ziro brain.

Amwambia Antony Diallo kwamba kwa nini alimruhusu huyu Ziro Brain ambaye alikataliwa na Media zote.

Antony Dialo amemwambia Gwajima kwamba " nilimpa nafasi Mh Paul Makonda katika kituo changu ili atoe vyeti vyake kwa maana ndo tulivyokubaliana..." in Gwajima voice

"wakati Makonda akiwa Mkuu wa wilaya ya kinondoni, majimbo yote ya Kinondoni kama Kawe, kinondoni etc yalichukuliwa na upinzani hii inamaanisha kwamba jamaa bado ni ziro brain kabsa.." in gwajima Voice

Kimenukaa..Wema Sepetu Akiri Ujumbe Unaosambaa Mitandaoni ni Wake..Adai Umesambazwa na Mke wa Mbowe Makusudi..!!!

$
0
0

Asema ujumbe huo utakuwa umesambazwa kutokea kwa Mbowe mwenyewe(mke wake au girl friend wake) Msikilize Wema:


Fahamu Wanawake Wenye Hips naShida Wanazokabiliana Nazo Kila Siku!L

$
0
0

Wanawake wengi wenye hips , ni wanawake ambao si kwa mwanaume tu hata kwa wanawake wenzie husifia kuwa fulani kajaliwa, ki maumbile, ni kweli wana mvuto wapekee, humwagiwa sifa nyingi za urembo, lakini pia kwa upande mwingine wa shillingi nimatatizo tupu.

Sifa:

1. Huwatesa sana wakina baba wanapokuwa katika vyombo vya usafiri kama daladala, treni, meli na ngalawa, mababa wengi hujawa na hisia kali za mahaba kiasi kwamba hupata mfadhaiko.

2. Hawana haraka sana kwani mwendo wao, hutembea kwa maringo, hata daladala likisimamia mbali hawawezi kukimbia kuwahi.

3. Hutongozwa wanaume watano kwa siku, hata wanaume wasiposema kitu angalau ukonyeza.

4. Ni wasikivu sana wakati wa kudatemaana wengi ni warefu hupenda sana kukuinamia kusikia zaidi uliongealo.

Matatizo.

5. Kwa kuwa huwa wanavutia sana nirahisi kurubuniwa kwani mwanamke yeye duniani hawezi kutongozwa watu elfu 2000 asimpendemmojawapo.

6. Hawana raha kwani ukodolewa sana machona watu, si wanawake wala wanaume.

7. Upata magonjwa sana asa fungus kwani sehemu zao za siri hazipati hewa ya kutosha kufatana na kubanana kwa nyama na msuguano kila watembeapo.

8. Wana gharama sana kuwatunza kwa sababu hawatakiwi kutembea kwa muda mrefu kuogopa msuguanahivyo umuoapo ni lazima ughalimike usafiri au unatakiwa kumunulia skin taiti kila mara kwa kuwa zinahariibikamuda mfupi sehemu ya mapaja.

Mh Kikwete Ampa Tahadhari Rais Magufuli..Adai Hivi sasa Yeye Analala Usingizi Murua Nyumbani Kwake Msoga..!!!

$
0
0

Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amefunguka na kusema suala la kuongoza nchi ni kazi kubwa mno na kusema yeye toka amestaafu kazi hiyo saizi anaweza kulala na usingizi ukaisha vizuri lakini kipindi cha nyuma haikuwa hivyo.

Kikwete amesema hayo jana kwenye Futari maalumu iliyoandaliwa na Kampuni ya simu za mkononi nyumbani kwake Msoga, Pwani na kusema saizi mzigo huo ameubeba Rais Magufuli na kudai huwa anamtia moyo kuwa anapaswa kupambana kwani hata wao wamepitia mambo ambayo yeye anapitia. 

"Sasa nimestaafu muda wa kuwasaidieni ninao tofauti na zamani, zamani mambo mengi kubeba mzigo wa kuongoza nchi kazi kubwa sana saizi anahangaika nao Rais Magufuli wakati mwingine nampa moyo tu bwana wewe pambana, wenzako wote ndiyo hivyo hivyo tulipitia humo humo pale unapodhani unatenda jema asubuhi wanakuponda, ndiyo muziki wenyewe lakini mara kuna hili kuna lile saizi mimi nalala usingizi unaisha kabisa kama kuna watu wananisumbua watakuwa ni wajukuu tu" alisema Kikwete 

Lowassa: Rais Magufuli anafagia fedha za Watanzania

$
0
0

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA na aliyekuwa Waziri Mkuu, Mh. Edward Lowassa amefunguka na kusema kuwa Rais Magufuli alianza vizuri kwani yapo mambo aliyoyafanya ni mazuri lakini pia yapo mambo mengine amefanya yana matatizo.


Lowassa amesema haya alipokuwa akifanya mahojiano na kusema kwa sasa tumuache Rais Magufuli aendelee na kazi yake lakini baadaye ndiyo watu waweze kumuhukumu kutokana na mambo ambayo ameyafanya.


"Rais Magufuli ameanza vizuri kubana mambo mazuri amefanya lakini kuna mambo mengine yana matatizo, lakini Mwalimu Nyerere aliwahi kusema wakati unafagia, unaweza kufagia hata shilingi sasa Rais Magufuli anafagia shilingi nyingi. Lakini tumuachie aendelee na kazi tumuhukumu baada ya kipindi fulani" alisisitiza Lowassa 

Lowassa - Tumuache Rais Magufuli Afanye Kazi Yake Ipasavyo..Kama Kukosolewa Akosolewe Baadae Lakini Sio Sasa Hivi..!!

$
0
0

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA na aliyekuwa Waziri Mkuu, Mh. Edward Lowassa amefunguka na kusema kuwa Rais Magufuli alianza vizuri kwani yapo mambo aliyoyafanya ni mazuri lakini pia yapo mambo mengine amefanya yana matatizo.

Lowassa amesema haya alipokuwa akifanya mahojiano na kusema kwa sasa tumuache Rais Magufuli aendelee na kazi yake lakini baadaye ndiyo watu waweze kumuhukumu kutokana na mambo ambayo ameyafanya.

"Rais Magufuli ameanza vizuri kubna mambo mazuri amefanya lakini kuna mambo mengine yana matatizo, lakini Mwalimu Nyerere aliwahi kusema wakati unafagia, unaweza kufagia hata shilingi sasa Rais Magufuli anafagia shilingi nyingi. Lakini tumuachie aendelee na kazi tumuhukumu baada ya kipindi fulani" alisisitiza Lowassa 

Mashabiki 400 wa Juventus Waanguka kwa Presha Turin Baada ya Timu Yao kuchakazwa Goli 4-1 na Madrid Jana..!!!

$
0
0

Zaidi ya Mashabiki 400 wa Juventus wameripotiwa kuzirai baada ya timu yao kupokea kipigo cha aibu cha mabao 4-1 kutoka kwa Real Madrid jana Jumamosi.

Mashabiki mbalimbali walikusanyika maeneo mbalimbali kufuatilia mechi hiyo ikiwamo katika mgahawa wa Piazza San Carlo, nchini Italia.

Video mbalimbali zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii zilionyesha mashabiki wakiwa wamefura kwa hasira, huku wengine wakionekana kuinamisha vichwa chini.

Hali hiyo ya mashabiki kuanguka, ilielezwa ilitokana na hazira za kipigo ilichopokea timu  yao.

Kocha wa Juventus, Massimiliano Allegri baada ya mchezo aliwatuliza wachezaji na mashabiki wa klabu hiyo akisema, “Nimesikitishwa kwa kile kilichotokea kwa mashabiki wetu kule Turin. Watambue kwamba hii kilichotokea, haikuwa bahati yetu.”

Kocha huyo, alinukuliwa na Shirika la AFP akiwataka mashabiki na wachezaji wapunguze hasira kutokana na kukosa ubingwa wa Ulaya.

Daktari atuhumiwa kuwapa mimba wanawake 60 bila wenyewe kujua

$
0
0

Mahakama moja nchini Uholanzi imeidhinisha ombi la familia zinazotaka vipimo vya vinasaba DNA vichukuliwe juu ya mmiliki wa kliniki ya uzazi ya daktari anayeshutumiwa kutumia mbegu zake za kiume katika makumi kadhaa ya kesi.



Jan Karbaat anatuhumiwa kuwa baba wa watoto wapatao 60 katika kituo cha afya alichomiliki katika eneo la Bijdorp, karibu na Rotterdam.

Vipimo sasa vitafanyika juu ya vifaa vilivyochukuliwa kutoka kwenye nyumba yake baada ya kifo chake mwezi Aprili, akiwa na umri wa miaka 89.

Wakili wa familia yake anasema hakuna ushahidi wa kuthibitisha madai hayo.

Jan Karbaat alijiita “Muasisi wa fani ya uzazi wa kusaidiwa”.

Kliniki yake ilifungwa mwaka 2009 wakati kulikuwa na taarifa kwamba alidaiwa kugushi data, uchunguzi na maelezo ya watoaji wa mbegu za kiumena kuzidisha idadi inayoruhusiwa ya idadi ya watoto sita kwa kila anayejitolea kutoa mbegu za uzazi.

Katika kesi ya mahakamani mwezi uliopita, wakili wa wazazi 22 na watoto walisema kwamba visa vinavyoshukiwa vinajumuisha mtoto wa mteja wao mwenye macho ya hudhurungi wakati alikuwa na macho ya blu na mvulana wa mteja wakeambaye anasura inayofanana na daktari.

Taarifa za vinasaba DNA zitasalia kuwa siri hadi pale watoto watakapoonyesha kuwa kuna sababu za kuamini daktari alikuwa baba yao, kulingana na mwandishi wa BBC Anna Holligan, ambaye alikuwa katika mahakama ya wilaya ya Rotterdam.

Hatimae, kama taarifa za vinasaba-DNA zitawiana na watoto hao ambao wengi wao walizaliwa miaka ya 1980s, kutakuwa na tumaini la kumshitaki daktari, labda kwa misingi ya kwamba hawangepaswa kuwepo, ameongeza Anna Holligan.

Joey, ambaye anaamini Jan Karbaat huenda ni baba yake ameiambia BBC: ” Ina maana kubwa kwangu … Tunatumai kupata majibu .”

Wakili wa familia ya Karbaat anapinga kufanyika kwa vipimo vyovyote vya vinasaba DNA.

Wakati wa uhai wake, daktari mwenyewe alikataa kufanya vipimo hivyo.

Hata hivyo, mwezi uliopita,kijana yake Jan Karbaat alitoa vinasaba vyake DNA vipimwe ambavyo vilionyesha kuwa daktari anaweza kuwa baba wa watoto 19, waliozaliwa kwa njia ya uzazi wa kutungishwa mbegu kwa lugha ya kitaaamu IVF, kulingana na ripoti ya shirika la habari la AFP.

Hii sauti ukiisikiliza ni kama ya WEMA Sepetu na MBOWE, lakini nina mashaka na huyu mtu mmoja

$
0
0
Hii audio note inayosambaa inawezekana ikawa ya Wema sepetu na Mwenyekiti Freeman Mbowe lakini bado hakuna proof yoyote, wengi wana mashaka inawezekana ni Steven ndo ameigiza sauti ya Mbowe kumchafua kwa njia moja au nyingine lakini wengine wana mashaka kwamba sauti ya wema ni ya Mtangazaji fulani hivi wa Redio ambae ameigiza sauti hiyo.

Hapa nani Mchawi ni Siasa au Kuliamsha dude kwa KIKI?
Steven inabidi akane kama sio yeye au kama vipi akili mwenyewe kama ni uzushi tu..

VIDEO: Wema Sepetu Amshutumu Mbowe Kuvujisha Sauti Yao

$
0
0
Baada ya Audio Ambayo imewekwa kwenye mtandao wa Jamii Forums Ikisikika sauti zinazosemekana kuwa ni Wema Sepetu na Freeman Mbowe Wakiongea Kimahaba Wakipanga kukutana Kwa ajili ya Dating..., Basi imesikika sauti yake tena akizungumza na Steve Nyerere kuhusu Sauti hiyo....
Viewing all 104694 articles
Browse latest View live


Latest Images