Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

VIDEO: Gwajima Amjibu Makonda, Amuita 'Zero Brain'

$
0
0
Unaweza kusema ni vita ya mdomo kati ya Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda na mchungaji wa kanisa la ufufuo na uzima Akofu Josephat Gwajima, kama utakuwa na kumbukumbu wiki mbili zilizopita Makonda akiwa kwenye mahojiano na televisheni ya Star Tv alisikika akisema " Gwajima sio Askofu", Sasa Gwajima kupitia ibada yake ya leo Jumapili ya Juni 4, Amemjibu kila kitu na kumuita "Zero Brain"

TAZAMA FULL VIDEO HAPO CHINI:

Taarifa 'feki' inayosambaa mtandaoni kumuhusu Anna Mghwira

$
0
0
Mimi Anna mgwira nimejivua uwanachama wangu ACT-Wazalendo ili nikaweze kuwatumikia wana Kilimanjaro

Kwakua nimejivua uwanachama mwenyewe moja Kwa moja nyadhifa zangu zote zitakuwa hazipo

Namshukuru sana mh zitto Zuheri kabwe na wanachama wote ACT-Wazalendo kwakuniamini na kunipa nafasi ya kuwaongoza

Hivyo kuanzia Leo tarehe 4/6/2017 Mimi sio mwanachama tena wa ACT-Wazalendo

Kazi yangu sasa ni kuwatumikia wananchi kupitia nafasi yangu ya sasa ya Ukuu wa Mkoa Kilimanjaro

Hii ni heshma kubwa kwangu na Kwa familia yangu Kwa ujumla

Mungu awabariki

Anna mgwira

Leo 4/6/2017: saa7:30 mchana

Hata muda mchache baada ya kusambaa kwa taarifa hiyo, Ofisa habari wa chama cha ACT-Wazalendo Abdallah Hamisi amekanusha taarifa hiyo.

Je, Halima Mdee na Esther Bulaya wanastahili tena Msamaha wa Bunge?

$
0
0
Huyu ni Mheshimiwa Halima James Mdee, Mbunge wa Jimbo la Kawe Jijini Dar es Salaam. Kwenye hii picha anaonekana akimvuta shati Askari wa Bunge mpaka kuichana sare ya Askari huyo. Mdee alikuwa anawazuia Askari hao wasimtoe ukumbini Mbunge wa Kibamba, Mheshimiwa John Mnyika aliyefanya kosa la kudharau kiti cha Spika na hivyo Spika Job Ndugai kuamuru atolewe nje.

Kwa kuwakumbusha tu ni kwamba, Bunge kwa umoja wao walimsamehe Halima Mdee kutokana na kosa la kumtukana Spika Ndugai kwa masharti kuwa hatafanya tena kosa. Na endapo atafanya tena kosa, ataadhibiwa bila hata ya kuitishwa Kikao cha Kamati ya Maadili na Madaraka ya Bunge.

Kwa ushahidi huu ni wazi kuwa Halima Mdee anakabiliwa na adhabu kali sambamba na mwenzake Esther Bulaya ambaye naye alisamehewa kwa masharti.

Kwa mtazamo wako, je unadhani Halima Mdee anastahili tena msamaha wa Bunge? Au safari hii apewe adhabu kali ili ajutie makosa yake?

Mfanyakazi wa Ndani ( House Girl) ni Mtu Muhimu Sana na Wakuthamini...Haya Hapa Ndo Huwafanya Wawe Watu Wabaya

$
0
0
Kumekuwa na matukio mbalimbali yanatokea yakihusu wafanyakazi au wasaidizi wa kazi za ndani. Matatizo mengi yanatokea katika familia nyingi hayaji tu kama radi lazima kuna sababu zinazopelekea kutokea kwa matatizo hayo. Huwezi kupanda mahindi shambani halafu ukategemea kuvuna mbaazi.

Hivyo siku zote utavuna kile ulichopanda. Kama ukipanda mbegu bora ya upendo katika familia yako tegemea kuvuna mbegu bora ya upendo. Vivyo hivyo, kama ukipanda chuki katika familia yako tegemea kuvuna mauti. Hii ni sheria ya asili unapokea kile unachotoa.

Kwa tafiti zisizo rasmi, ukitembelea nyumba kumi kati ya nyumba hizo kumi moja tu ndio wanaishi vema na wasaidizi wao wa kazi za ndani. Nyumba nyingi ni matatizo sana je matatizo haya yote yanasababishwa na nani? Lazima tuchunguze nini kiini cha kosa au tatizo kwanza. Huwezi kutatua tatizo bila kuchunguza kiini cha kosa.

Visa vimekuwa vikitawala ndani ya nyumba nyingi kwa wale wanaoishi na wasaidizi wao wa kazi za ndani. Wasaidizi wa kazi za ndani wanafanyiwa ukatili na waliowaajiri ndio maana nao wanalipa visasi kwa watoto wao. Wasaidizi wa kazi za ndani wanarusha visasi wanavyofanyiwa na waajiri wao kwa watoto.

Watoto wanakua wahanga wa matatizo mengi wanaumizwa na kuteswa na kuona dunia ni chungu na siyo sehemu salama ya kuishi kutokana tu na kuishi maisha yaliyokosa upendo ndani yake. Waajiri wa kazi za ndani wanapandikiza chuki kwa wafanyakazi wao wa ndani na wasaidizi wao wanaona sehemu sahihi ya kulipiza kisasi ni kwa watoto.

Hivyo wasaidizi wa kazi za ndani nao wanatoa kile walichopokea na siku zote chuki huzaa mauti. Ndio maana kuna faida kubwa sana kwa waajiri kupanda mbegu ya upendo ambayo itakwenda kuota kwa kila mwanafamilia na hatimaye watakuja kuvuna upendo.

Mpendwa msomaji, jaribu kuvuta picha ni matukio mangapi umeyasikia au kuyaona kwa macho yako yanayosababishwa na wafanyakazi wa ndani. Na je wahanga wakubwa wa matatizo hayo katika familia ni kina nani? Kama sio watoto? Wafanyakazi wa ndani ndio wanaonekana wana makosa au wakosa kama hujachunguza kiini cha tatizo au kosa kwanza.

Wanawake wengi walio na waume zao wanawaachia wadada wa ndani kila kitu wafanye hata zile kazi ambazo hawapaswi kufanya, kazi ambazo angetakiwa kufanya na mama au mwanamke aliyeolewa ambaye yeye ndio mlinzi wa familia. Wanawake wengi wanawatengenezea mazingira mabaya wao wenyewe na unakuta nafasi ya mke sasa anachukua dada wa kazi. Kwa kisingizio kua yuko bize na kazi mpaka anasahau wajibu wake kama mke au mama wa familia.

Lazima muwe na mipaka ya kazi na wasaidizi wenu wa kazi siyo kumuachia akufanyie kila kitu katika nyumba yako unayoishi. Wasaidizi wa kazi za ndani unakuta wanajua vitu vingi kuliko mama wa familia ndani ya nyumba sasa hii ni hatari sana.

Kutokana na mwanamke katika familia yake kushindwa kuwa mlinzi wa familia yake matokeo yake hata wale wanaume wasiokua waaminifu katika ndoa zao wanatembea na wasaidizi wao wa kazi kwa sababu mazingira hayo wanayasababisha wao wenyewe. Unampatia msaidizi wako wa kazi kufua nguo za muwe wako hata za ndani na kumwandalia kila kitu mume wako unafikiri unategemea nini?

Hujaolewa kwenda kuwa mtalii wa nyumba bali mwanamke aliyeolewa anakwenda kuwa mlinzi wa nyumba yake na baba kuwa kichwa cha familia yake. Na kazi hizo wamepewa na Mungu. Ndio jukumu la mke na mume wakishindwa kutimiza wajibu wao kila mmoja kinachofuata ni machozi tu.

Ukiwa ni mama wa kutoa agizo dada naomba nenda kamtandikie baba anataka kulala, au kamuandalie maji ya kuoga, chakula, mwangalie mtoto kama amekula, kama anaumwa, waangalie watoto kama wameenda shule nk na wewe umekaa sebuleni unaangalia tv na kubadilisha chaneli utakuja kupata hasara tu.

Kama wewe ni mwanamke ndani ya nyumba usikwepe majukumu yako na kumwachia dada wa kazi na wewe kama ni baba wa familia simama kama kiongozi kweli na mwanamke linda nyumba yako.

Mpendwa msomaji, unajua ni kwa nini matatizo yanatokea kwa wasaidizi wa kazi za ndani?

Sasa karibu ujionee viini vya matatizo hayo. 

1. Kukosa upendo;
wasaidizi wa ndani wanakosa upendo badala yake wanapewa chuki ambayo ndio inakuja kuzaa matatizo mengi katika nyumba nyingi. Hakuna kitu kama upendo wewe lisikie tu neno hili upendo lina maana kubwa sana kwa binadamu.

Kama vile wewe unahitaji kupewa upendo na watu wengine mpatie na msaidizi wako wa kazi naye anakurudishia upendo. Mpende kama unavyojipenda wewe, kama unavyoipenda familia yako na mfanye awe sehemu ya familia yako. Vaa viatu vyake halafu utaona kama utavuna ubaya kutoka kwake.

2. Kukosa kuthaminiwa;
mwanasaikolojia mmoja aliwahi kusema, hitaji la kwanza la binadamu ni kuthaminiwa. Anza leo kumthamini mfanyakazi wako uone naye atakavyokuwa anakuthamini. Unatoa kile unachopokea katika maisha yako.

Binadamu akihisi anakosa kuthaminiwa anakua amekufa kisaikolojia kabisa. Ni nani ambaye hahitaji kuthaminiwa? Kila mtu anataka kuthaminiwa katika hii dunia. Hakuna mtu aliyezaliwa kuja kupata mateso duniani mwache kila mtu afurahie na kuonja thamani yake hapa duniani.

3. Kukosa uhuru;
kukosa uhuru ni utumwa katika maisha. Ndio maana watu wanapelekwa gerezani kufungwa ili wakose ule uhuru wao. Kila mtu anahitaji uhuru. Sasa hawa wasaidizi wa ndani hawapewi fursa ya uhuru. Ukimbana sana mtu na kukosa uhuru na ni mtu mzima lazima atatafuta uhuru. Naye ni binadamu anahitaji uhuru kama wewe, uhuru wa kufanya mambo yake na usimtawale kama vile mtoto mdogo.

4. Kudharauliwa, kutengwa na kuchukuliwa kama siyo sehemu ya familia;
wasaidizi wa ndani wanachukuliwa kama watu wenye shida sana, siyo wa umuhimu na hafai kuwa sehemu ya familia. Wanalala sehemu isiyostahili kulala, wanavaa mavazi yasiyo nadhifu yaani ukienda nyumba nyingine unatamani hata kutokwa na machozi watoto wa familia wamevaa nguo nadhifu ukimuona yeye kachoka kabisa anachukuliwa siyo mtu muhimu.

Mtu anayekupikia, kukuangalizia watoto na nyumba yako halafu unamdharau ndio maana hata wengine wanawekewa sumu kwa sababu ya mateso wanayofanyiwa na wanafamilia. Wakati wa kula chakula dada wa kazi anakula jikoni peke yake wanafamilia wamekaa mezani wanakula hivi wewe ungekuwa unafanyiwa hivi ungejisikiaje? Wakati mwingine hata chakula wanapewa masalia wanafamilia kwanza. Ishi na msaidizi wako kwa upendo.

5. Kutukanwa, kupigwa na kudharauliwa;
baadhi ya wasaidizi wengine wanateswa na wanatukanwa matusi ya kila aina yaani wamegeuzwa kama jalala la matusi. Mwisho wa siku dada wa kazi anakua anapata majeraha ya moyo. Wengine wanapigwa na kuteswa na kunyimwa hata chakula. Halafu ukifanyiwa jambo baya utasikia wafanyakazi wa ndani sio watu siku hizi.

Kabla ya kulalamika chunguza kiini cha kosa ni nani msababishi wa yote haya? Wanafamilia wanatendea vibaya wadada wa kazi ndio maana nao wanawatendea mabaya. Ndio maana dawa ya chuki huzaa mauti, unamfanyia mwenzako mabaya halafu unategemea mazuri? Sahau kuhusu hilo.

6. Kusemwa maneno makali;
wanasemwa maneno makali yenye chuki ambayo yanakwenda kutengeneza majeraha katika moyo. Maneno ni mabaya kwani yanakwenda kutengeneza chuki ndani ya moyo. Acha kuwasema sana maneno mabaya bali mtie moyo na hamasa ya kufanya kazi na kushirikiana naye hata kama unamlipa. Kuwa kiongozi mzuri katika familia yako.

7. Kutopewa nafasi ya kujieleza na kushindwa kumpata mtu wa kumuelezea matatizo yake; nguvu ya pesa wakati mwingine huwa inatumika kwa kuwakandamiza wadada wa ndani. Ananyimwa mahitaji ya msingi anaingiwa na tamaa ya kuiba halafu akiiba nguvu ya pesa inatumika anakamatwa na kupelekwa polisi bila hata kupewa nafasi ya kujieleza.

Na kukichunguza kiini cha kosa utagundua mwajiri wake ndiye msababishi. Unakuta wakati ana shida anakosa mtu wa kumwambia watu wote ndani ya familia wamegeuka kuwa miiba hivyo anaendelea kubaki na uchungu ulioumbika na matokeo yake wanafanya matukio ya ajabu.

8. Kupewa ujira mdogo na kucheleweshewa ujira wao; dhahiri kwamba wafanyakazi wengi wa ndani wanalipa ujira mdogo na wanafanya kazi nyingi zaidi ya masaa 12 bila mapumziko. Kama anakufanyia kazi zako mpe stahiki yake hata kama ni kidogo.

Kama humpatii mahitaji yake binafsi lazima umpatie hela ili aweze kujitegemea. Kuna wengine hawapewi kabisa wanaambulia maneno kama haya unakula bure tu, kulala hapa na kujaza choo hapa. Mambo kama haya unakuwa unamuumiza msaidizi wako.

Mwisho, ndugu msomaji, panda mbegu bora ya upendo kwa manufaa yako na kwa jamii nzima. Mpe malazi mazuri na chakula bora. Mtendee mwenzako kama vile unavyotaka wewe kutendewa na vaa viatu vya mwenzako. Kuwa mfano sahihi kama unamwambia msaidizi wa kazi kuamka saa 11 au 12 na wewe onesha mfano. Siyo wewe unatoa agizo halafu unaamka saa 2 jihukumu kwanza wewe mwenyewe kabla ya kumhukumu mwenzako.

Zitto Kabwe Atoa Msimamo wa ACT Wazalendo Baada ya Mwenyekiti Wao Anna Mghwira Kuteuliwa Kuwa Mkuu wa Mkoa..!!!

$
0
0

Nimekuwa naulizwa Sana kuhusu uteuzi wa Mwenyekiti wa Chama chetu kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Nimekuwa kimya Kwa sababu tumepokea Taarifa za uteuzi kutoka katika vyombo vya Habari. Mwenyekiti yuko nje ya nchi na kutokana na tofauti za masaa bado hatujawasiliana nae. Tutatoa tamko kamili atakapokuwa amerejea nchini. 

Ninawataka wanachama wote wa Act Wazalendo wawe watulivu na Kama kuna masuala yanayohusu maamuzi ya vikao vya Chama tutawajulisha.

Aliyeteuliwa ni Mwenyekiti wa Chama Taifa, sio mshauri au mwanachama tu. Ni mmoja wa viongozi wa juu wa Chama chetu. Uteuzi wake unahitaji kikao cha Kamati Kuu ya Chama kukaa na kujadili. Nitaweza kutoa Taarifa baada ya vikao vya Kamati Kuu ya Chama. Kwa sasa umma usubiri vikao Kwa mujibu wa Katiba ya Chama chetu.

Hivi Ndivyo Ilivyokuwa Baada ya RC Gambo Kuhudhuria Msiba wa Mzee Ndesamburo Leo..!!!

$
0
0

Kutokana na geographical nearness ya Arusha na Moshi kuwa ni Mwendo wa Lisaa Limoja hadi Moshi. Mrisho Gambo ameamua aache shughuli zake zote za Leo na kwenda Kuhuduria na kutoa Pole Kwa Familia ya aliyekua Mbunge na Mmoja wa wasisi wa Chadema Ndugu Philemon Ndesamburo.

Mrisho Gambo akisalimiana Na Mbunge wa Rombo ndugu Joseph Selasini nyumbani kwa Marehemu Ndesamburo. Mungu Alilaze Roho ya Marehemu Mahala Pema.

Habari Picha ..Hivi Ndivyo Edward Lowassa Alivyofika Nyumbani kwa Marehemu Ndesamburo Kutoa Pole..!!!

$
0
0


Waziri mkuu mstaafu na mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA Mh. Edward Lowassa mchana huu amefika nyumbani kwa marehemu Dr. Philemon Ndesamburo mjini Moshi kutoa pole na kutia sahihi kitabu cha maombolezo nyumbani hapo.

Rasmi..Mrisho Ngasa Ajiunga na Yanga,,Kuanza Kuichezea Kwenye Michuano ya Sport Pesa..!!!

$
0
0

Mshambuliaji Mrisho Ngassa ataanza kuichezea Yanga katika michuano ya SportsPesa Super Cup kesho.

Yanga itaivaa Tusker FC ya Kenya katika mechi ya pili baada ya Singida United kuwa imeanza mechi ya kwanza dhidi ya AFC Leopards.

Ngassa amefanya mazoezi na Yanga jana na leo asubuhi tayari kwa mechi hiyo ya SportsPesa Super Cup.

Taarifa zimeeleza kwa kuwa michuano hiyo wachezaji huru wanaweza kushiriki, Yanga imeamua kumtumia Ngassa baada ya yeye kuomba kwa kuwa ni mchezaji huru.

Takwimu za Mchanga wa Madini Zatiliwa Shaka

$
0
0
Wadau wa masuala ya madini nchini wameshauri kubadilishwa kwa mfumo wa uchimbaji madini ili kuondokana na mfumo wa sasa ambao una mbinu nyingi za kukwepa kodi.

Ushauri huo umetokana na maazimio yaliyotolewa jana katika kongamano la rasilimali za madini lililoitishwa na chama cha ACT-Wazalendo na kuwashirikisha wadau wa masuala ya madini akiwamo Dk Rugemeleza Nshala, Dennis Mwendwa na Nico Kajungu.

Maazimio hayo yameshauri serikali kubadilisha mfumo wa uchimbaji madini kwa kuhamia kwenye mfumo wa kugawana mapato.

Pia wadau hao wamekosoa takwimu zilizotolewa na kamati ya Profesa Abdulkarim Mruma, kuhusu kiwango cha madini kwenye makinikia.

“Takwimu zilizotolewa na Kamati ya Profesa Mruma, licha ya mchango wake katika kuibua mjadala, zina walakini. Takwimu hizi, zikukubaliwa kama zilivyo, zinaifanya Tanzania kuwa mzalishaji namba moja wa dhahabu Afrika,” yamesema maazimio hayo

Wadau hao walitoa azimio la kuwepo kwa  timu huru ya kupitia takwimu zilizotolewa na Kamati ya Profesa  Mruma ili kuthibitisha uhalali wake.

Maazimio mengine ni kufanya mabadiliko ya sheria ya madini na katiba ili kuyafanya madini na maliasili nyinginezo kuwa mali ya wananchi milele.

Mengine ni watu wote walioshiriki katika kuingia mikataba ya madini na kufanya maamuzi yanayolitia hasara taifa wawajibishwe na kuchukuliwa hatua bila kujali vyeo vyao au lini makosa hayo yalifanyika.

Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe aliongoza kongamano hilo.

Askofu Gwajima Amshambulia Bashite Kwa Kishindo. Aonyesha SMS ya Anthony Diallo

$
0
0
Leo katika kanisa la Ufufuo na Uzima Yule askofu machachari Askofu Gwajima amejibu mashambulizi ya hotuba ya RC wa Dar Es Salaam yaliyofanyika television ya Star TV majuma kadhaa yaliyopita. Amechambua hotuba yote aliyofanya RC pale Star TV, ameeleza elimu ya Nape Nnauye, amechambua tukio la uvamizi pale Clouds FM na akaeleze uhalali wa jina la Bashite Kwa RC. Askofu Gwajima ameshusha nondo zake za kutosha kudhihirisha kuwa muhusika wa hotuba jina lake halali ni Bashite. Ameenda mbali na kudai kuwa hata namba za simu za baba yake kwenye miamala ya fedha zimesajiliwa kwa jina la Bashite. Na akaitaja namba husika. Anasema kabla sakata halijapamba moto bila wao kushtukia aliruka had mwanza na ana picha alizopiga kwenye rejesta za shule ya msingi na sekondari na majina ya muhusika yalikuwa ni Bashite. Pia askofu Gwajima anasema wiki iliyopita aliwasiliana na Anthony Diallo kumuuliza kwa nin aliruhusu kipindi cha kumdhalilisha. Askofu anasema Mh Diallo alimjibu kuwa aliweza kumruhusu kumpa kipindi kwa kuwa Bashite alimuambia kuwa nataka kuonyesha vyeti kwa watanzania na hivyo Diallo akaona ni jambo jema. Askofu anasema hata baada ya kipindi Mh Diallo alishangaa kwa sababu Bashite hakufanya kama alivyoomba. Askofu akaonyesha ujumbe mfupi wa simu uliotoka kwa Diallo. Video:

Sababu za Watu Kufumba Macho Wakati wa Kubusu

$
0
0
Ulishawahi kujiuliza kwanini watu wengi waliopo kwenye mahusiano ya kimapenzi hufumba macho yao wakati wa kubusu? Hakuna sheria iliyopitishwa kuwataka wafumbe macho lakini hufumba, na kwanini unatakiwa ufumbe macho? Twende pamoja katika makala hii kuelewa sababu chache.

1. Acha midomo yako iongee

Kabla ya wapenzi hawajaanza ku kiss, huwa na muda wa kuzungumza na kujadiliana mambo kadha wa kadha yanayohusu maisha yao. Sasa inapofika wakati wa kubusu, ni muda wa kuacha midomo (lips) zako zielezee ile habari ambayo usingeweza kuisema. Hivyo watu hufumba macho ili kuacha midomo yake pekee ndiyo iwe inafanyakazi wakato huo.

2. Ni ishara ya raha

Kwa kawaida, binadamu hufumba macho yake pale anapofanya au kusikiliza kitu kinachouburusisha moyo wake na kufanya awe na furaha. Fikiri wakati unasikiliza mziki mzuri, ukila kitu kitamu, ukiimba kwa hisia, ukifika kilele. Hivyo kufumba macho wakati wa kubusu, ni njia ya kuonyesha kuwa unaburudika.

3. Ni ishara ya uaminifu

Mtu akiwa amesimama sehemu ya hatari au kujiegemeza, huwezi ukamwambia afumbe macho akakuelewa kwa sababu si sehemu salama lolote linaweza kutokea. Lakini wakati ukiwa unabusu na mpenzi wako, upo sehemu salama isiyo na hatari, huhitaji kufumbua macho uangali nini kinakuja kwa sababu unauhakika upo sehemu salama.

4. Huongeza kufurahia

Unapofumba macho na kuyaelekeza mawazo yako kwenye kile unachokifanya, inakufanya uwe na hisia zaidi, mawazo yako yawe kwenye kile unachokifanya, na hivyo kukufanya usikie raha zaidi.

5. Huonyesha hali ya kujisalimisha

Hii ni ishara kuwa umejisalimisha kwa huyo uliyenaye, haufanya mambo kwa haraka na kukurupuka. Ni sawa na kumkabidhi mtu mwili wako na hisia zako.

6. Kuepuka vitu vya ajabu

Kwanza baadhi ya watu huogopa kuangaliana kwenye macho, hivyo ili kuondoa ile aibu wakati anakubusu,inamlazimu kufumba macho awe kama amejitoa ufahamu. Pili, kuepuka vitu vinavyoweza kukutoa uweponi nwa unachokifanya. ‘Attention’ ni jambo la muhimu kufurahia unachofanya.

7. Kujiweka sawa (turn on)

Watu hufumba macho ili kujitenga na yaliyokaribu nao au kwenye akili zao. Katika lugha ya kimapenzi unaweza kusema anajipeleka ulimwengu mwingine wa mahaba. Anajiweka mwili wake kuwa tayari kwa ajili ya mambo yanayofuata.

VIDEO: “Spika Ndugai alimdhalilisha Mbunge John Mnyika”-BAVICHA

$
0
0
June 2 2017, Mbunge wa Kibamba, John Mnyika aliingia kwenye headline baada ya Spika wa bunge kuamuru atolewe ndani ya ukumbi wa bunge kwa mada ya kuonyesha utovu wa nidhamu.

Sasa leo June 3 2017 Baraza la vijana la CHADEMA ‘BAVICHA’ limelaani kitendo cha kumsukuma Mbunge John Mnyika wakidai kuwa  Mnyika hakukaidi amri ya Spika kutoka nje na walitumia nguvu iliyopita kiasi.

Aidha wamelaani kitendo cha Spika wa Bunge Job Ndugai kuwaagiza askari kumtoa nje kwa nguvu Mbunge Mnyika hata pale ambapo alikuwa anajiandaa kutoka ndani ya ukumbi wa bunge kiistaarabu, Bonyeza play hapa chini kutazama:

Fahamu – Vyakula Sita Asivyotakiwa Kula Mwanaume Riajali

$
0
0
Chakula ni kitu muhimu kwenye maisha yetu, ila kunavyakula sita ambavyo mwanaume hastahiki ama haruhusiwi kula.

1. Punguza kula vyakula feki kuzuia kupoteza nywele


Vyakula feki (junk foods) ni hivyo vinapatikana kwenye fast foods na takeaway centers nyingi hasa mijini kadharika vyakula vile vyote vya kwenye maboksi.Vyakula hivi feki vina kiasi kingi mno cha lehemu (cholesterol) na lehemu hii hupelekea kile huitwa kwa kitaalamu kama ‘pregnenolone’ na kupelekea kiasi kikubwa cha ‘dihydrotestosterone’ (DHT) na hatimaye kupotea kwa nywele kichwani a.k.a upara.

2. Punguza kunywa pombe au acha kabisa kuzuia kuota matiti

Wanaume wengi wanaokunywa bia kupita kiasi huwa na uwezekano mkubwa wa kupatwa na tatizo la kuota matiti kama wamama tatizo lijulikanalo kwa kitaalamu kama ‘gynecomastia’.



Kwenye bia au pombe kuna kitu kama homoni ya oestrogen.Mara nyingi hakuna lishe ya moja kwa moja na hivyo hukufanya ujisikie njaa au hata kuongzeka kwa njaa zaidi na ndiyo sababu unaambiwa kama huna uhakika utakula wapi ni bora usinywe pombe ili kulinda afya yako.

3. Acha kutumia mafuta ya mboga mboga kuepuka saratani ya tezi dume

Mafuta yatokanayo na mboga mboga au mimea yamekuwa yakipigiwa debe kwa miaka mingi na watu wanaojihusisha na lishe na wale wenye hasira sana na mafuta yatokanayo na wanyama. Hata hivyo leo nakujulisha mafuta hayo si salama sana kutumika na mwanaume kila siku. Hili limekuja hasa kutokana na kuongezeka kwa magonjwa ya moyo na lehemu na watu wakahimizwa kutumia mafuta ya namna hiyo.

Lakini mafuta haya ya mboga mboga ndiyo kitu kibovu kabisa unatakiwa kukiepuka ili usipatwe na saratani ya tezi dume. Linapokuja suala la kujilinda saratani ya tezi dume basi mafuta yenye omega 3 ndiyo suluhisho la kudumu na siyo omega 6 kama ilivyo kwenye vyakula vingi vya kwenye makopo, mafuta ya alizeti, maharage ya soya, mafuta ya canola na mafuta ya corn na mengine yote yenye omega 6.

4. Popcorn/Bisi


Popcorn au bisi ni chakula kingine mwanaume hatakiwi kula, hupikwa kwa kutumia mafuta yasiyo na afya, sodiamu nyingi na ni chanzo cha baadhi ya kansa. Kuna kitu kinaitwa ‘Diacetyl’ kinachopatikana kwenye popcorn ambacho kinahusika na kusababisha kansa na kuna kingine kiitwacho ‘Perfluorochemicals’ ambacho huathiri tezi ya thyroid na ugonjwa wakati huo huo husababisha ugonjwa wa kupungukiwa umakini ujulikanao kwa kiingereza kama ‘Attention-deficit/hyperactivity disorder (ADHD)‘.

5. Mkate mweupe

Mkate mweupe una wanga mwingi zaidi usio na faida. Kwenye hatua za kutengeneza mkate mweupe vitamini zote za kundi B hupotea, hupotea pia nyuzinyuzi (fiber). Siyo hivyo tu mkate mweupe umesemekana kuwa ni sababu ya ugonjwa wa kisukari na kuongeza uzito zaidi mwilini wakati huo huo ukisababisha tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu sana.


Kula mkate ambao ngano yake haikukobolewa (brown bread), kula ugali wa dona na chai unaweza kutumia tangawizi au mdalasini badala ya majani ya chai.

6. Chumvi ya mezani



Chumvi ya mezani ile ya unga nyeupe haifai kwa mwanaume. Kila mmoja amesikia chumvi hii husababisha shinikizo la juu la damu na pamoja na hayo bado sehemu kubwa ya watu wanatumia chumvi hii.
Chumvi ya mawe ya baharini ile ambayo haijapita kiwandani (unrefined sea salt) ndiyo nzuri zaidi kwa afya ya mwanaume.

Chanzo Dk Fadhili Paulo

Utafiti wangu: 'Massage Parlour' ni Z'aidi ya Maduka ya Ngono

$
0
0
Wakuu niliamua kwa mara nyingine kujipa kazi ya kufanya "Utafiti" katika maeneo ya "Massage Parlour" katika jiji la Dsm na vitongoji vyake.Raha ya utafiti wa aina hii ni kujivika "uhusika" haswaa ili upate mambo ya ndani ya kujifunza hasa undani wa jambo lenyewe,ama hakika nimejifunza mengi na kwa kweli hii ndio Dsm,mambo ni motomoto ndani ya kuta nne za vyumba.

Nilianza kwa kutembelea "Massage Parlour" za mitaa ya Sinza(Sitataja majina kwa sababu maalumu).Humu nimejionea mambo mengi sana na mazito,ama hakika mji huu una mambo.Hizi si Massage Parlour tena bali ni maduka ya ngono yasiyo rasmi yenye leseni ya "Massage Centres"

Nilianza mitaa fulani ya Sinza ambapo pale nilikuta Massage yenye bei mbili tofauti,moja ya Tsh 25,000/= na nyingine ni 35,000/=,yaani hiyo ya elfu 25 haina choo na bafu la ndani kwa ndani wakati hiyo ya elfu35 maanake unapata chumba chenye choo ndani,huna haja ya kutoka kwenye korido kwenda kuoga au msalani.Ndani ya chumba unakutana na huduma kadha wa kadha,kwanza unaambiwa unataka huduma ya aina gani?Maana kuna

1)Soft Massage
2)Hard Massage
3)Medium Massage
4)Body to body Massage
5)Honey Massage nk

Huduma hizi zote zinapatikana humo ndani,yaani kama hiyo ya body to body maanake mtoa huduma anatoa kila kitu halafu anakupaka mafuta na kuanza kuusugua mwili wako akiwa mtupu,hiyo hard ni kwa wale wenye kutaka kunyoosha misuli,medium inakuwa kati ya soft na hard na wakati soft hiyo ni hatari sana maana inaamsha mambo yote ya dunia ya mwili.

Kifupi wakati wa kuingia unakuta wadada wamekaa kama sebuleni,na ukiingia pale wanaitana wooote na wanapanga foleni,hairuhusiwi kukubaliana na mmoja wakati wenzake hawapo pale sebuleni/mapokezi.Wakikusanyika wote unaambiwa uchaguwe wa kwenda kukuhudumia.Sasa ukiwa kauzu unapitia mmoja baada ya mwingine then unachaguwa.Yaani wakati wa kuchaguwa kila mtu analegeza macho na madoido ili achaguliwe yeye,inakuwa kama "ng'ombe mnadani".

Baada ya hapo ni kwenda kupata huduma,huko ndani kwenye huduma ni balaa tupu,yaani ukitoka salama ni bahati,yaani ni kama bahati ya UKAWA kuanzisha maandamano mbele ya Central Polisi bila kibali cha maandamano halafu wakaachwa.Kiukweli hii ni aina ya biashara ambayo wale wadada wasioweza kujipanga foleni pale Sinza Ambiance basi wanakuwa huku,na pia kwa wale wasioweza kuopoa pale wanahamia huku.Nimejifunza kuwa biashara hii ni ngumu sana kupambana nayo moja kwa moja sbb binadamu wana mbinu nyingi sana.

Katika utafiti wangu nikagundua wateja wengi ni waume za watu ambao pengine wake zao hwafanyi au hawajui namna ya kufanya hizi massage.Wahudumu wengi wanakiri kuhudumia waume za watu hasa siku za weekend na mida ya jioni baada ya kazi,kwani watu wengi hawapendi kuingia mchana huku wakionekana.Na huduma hizi zinazotafutiana kutokana na mazingira na mazingira.Huko Mikocheni,Mbezi na Masaki bei zake ni kubwa sana.Wachina na Wafilipino wengi wanafanya baishara hii na ile "extra" kwa mgongo wa Massage Parlour.

Kuna centres nyingine wapo kikazi haswaa,hii ni kwa sababu kuna watu wenye matatizo ya neuros(?),migongo na wameshauriwa na madaktari wanatumia sehemu hizi kwa ajili ya matibabu ya migongo na viuno.Hiivyo si wote wapo kwa ajili ya ile "biashara".

Mashoga wengi hushinda na hawa wadada,na hukaa humu na kufanya kazi hiyo,pia wavutaji wa shisha na madawa pia humu ndio centres zao.Mtu anaingia anajidunga anasinzia mpaka anaamka ndio anatoka.Kifupi kila unapozuia hili binadamu anavumbua hili,kila kitu kina majibu yake.Humu ndani ya Masage Parlour ni hatari wakuu...Kuingia bure kutoka lazima uwe umakauka.

Hii ni sehemu ya kwanza ya muendelezo wa utafiti wangu ndani ya hizi Massage Centres...Nipatapo wasaa nitakuja tena hapa kumalizia.

Muwe na siku Njema Wakuu

Madam Flora: Tujifunze kuwa na maamuzi binafsi

$
0
0

Ikiwa leo ni mwezi mmoja na siku kadhaa toka msanii wa Injili Madam Flora kufunga ndoa kwa mara ya pili na mume wake Daudi Kusekwa baada ya kuachana na aliyekuwa mume wake Emmanuel Mbasha, Fora amefunguka na kuwataka watu kuwa na maamuzi binafsi.

Msanii huyo amewataka watu kuwa na maamuzi binafsi kama wanataka kufikia ndoto zao na kudai kuwa unaweza ukawa unamshirikisha mtu lakini mtu huyo asiwe na nia njema na wewe hivyo anaweza kukushauri ndivyo sivyo.

"Jifunze kuwa na maamuzi yako binafsi, sio kila jambo lazima ushirikishe watu ndipo ulifanyie maamwuzi kwani si kila unayemshirikisha anakuwazia mema. Pokea ushauri vizuri kabisa lakini jifunze kuwa na maamuzi binafsi ili kutimiza ndoto yako" alisema Madam Flora

Breaking: Anna Mgwira Ajivua Uanachama wa ACT Wazalendo....

$
0
0

Taarifa Kwa vyombo vya habari
Mimi Anna mgwira nimejivua uwanachama wangu ACT-Wazalendo ili nikaweze kuwatumikia wana Kilimanjaro
Kwakua nimejivua uwanachama mwenyewe moja Kwa moja nyadhifa zangu zote zitakuwa hazipo
Namshukuru sana mh zitto Zuheri kabwe na wanachama wote ACT-Wazalendo kwakuniamini na kunipa nafasi ya kuwaongoza
Hivyo kuanzia Leo tarehe 4/6/2017 Mimi sio mwanachama tena wa ACT-Wazalendo
Kazi yangu sasa ni kuwatumikia wananchi kupitia nafasi yangu ya sasa ya Ukuu wa Mkoa Kilimanjaro
Hii ni heshma kubwa kwangu na Kwa familia yangu Kwa ujumla
Mungu awabariki
Anna mgwira

Leo 4/6/2017: saa7:30 mchana

Nikinywa Pombe na Kuvuta Bangi ndio Napata Raha Sana Wakati wa Kufanya Mapenzi

$
0
0

Nadhani wapenzi wa hayo mambo hapo juu watakubaliana nami kuwa ukinywa pombe au kuvuta bangi na ukamkamata mwanamke hakika kunastarehe ya ajabu isiyo na mfano, konyagi ndio kiboko ya yote, kunywa konyagi halafu ugegede ndio mwanamke atalijua jiji.

Hata kama ni mgumu kiasi gani kufika kileleni lazima siku hiyo ataomba poo.

Kuna mwanamke wa kijaluo trembling alikuwa kila akienda na mwanaume haridhiki, Siku hiyo akaingia kwenye anga zangu nikiwa nimekunywa nusu mzinga wa konyagi na safari mbili, wee wee, alishinda anaongea kijaluo, hadi leo hataki kuniacha najiliavijisent vyake.

Kwa kweli konyagi na mapenzi ni sawa na pikipiki na petrol.

Wasiokunywa pombe wana hasara kubwa sana hapa duniani na hawajui mautamu tunayopata

Je wewe Kwako ikoje ?

By Mdau

Kagame atangazwa kuwa mgombea Urais Rwanda

$
0
0

Katika hatua iliyowashangaza wengi nchini Rwanda vyama viwili vya siasa vikongwe nchini humo vimemtangaza Rais Paul Kagame kuwa mgombea wao katika uchaguzi wa urais utakaofanyika mwezi wa 8 mwaka huu, kabla hata chama chake cha RPF kumtangaza kuwa mgombea wake.

Hadi sasa ni wagombea binafsi 3 waliokwishatangaza nia ya kusimama katika uchaguzi huo.

Katika mikutano mikuu ya vyama hivyo, chama cha Social Democratic na Liberal Party licha ya kwamba ilifanyika mnamo nyakati tofauti, kauli yao ilikuwa moja, kuunga mkono Rais Paul Kagame wa chama tawala cha RPF katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi wa 8 mwaka huu.

Hoja iliyotolewa na vyama hivyo pia haitofautiani.

Ni kwamba chaguo lao limetokana na pendekezo lililoungwa mkono na wananchi wengi wa Rwanda la kubadili katiba na kumpa rais Paul Kagame uhuru wa kugombea muhula wa tatu kupitia kura ya maoni iliyopitisha katiba mpya mwaka jana.

Haya yametokea wakati ambapo hata chama tawala RPF hakijamtangaza Rais Paul Kagame kama mgombea wake, wakati mchakato wa uteuzi bado umekuwa ukiendelea katika ngazi ya mashinani.

Wengi walitarajia kuwa vyama hivi vingeteua na kutangaza wagombea wake katika uchaguzi huo kama ilivyotokea katika uchaguzi wa urais mwaka 2010.

Chama cha Social Democratic kilisimamiwa na Dr Jean Damascene Ntawukuriryayo aliyepata asilimia 4,9 ya kura ilhali Liberal Party kilisimamiwa na Higiro Prosper aliyeambulia asilimia 1 nukta 3 ya kura.

Chama cha ANC Waanza Kumpinga Rais Zuma..Wataka Achunguzwe kwa Rushwa..!!!

$
0
0

Chama tawala cha Afrika Kusini, African National Congress (ANC) kimetaka vyombo vya dola kuchunguza barua pepe zilizoibua kashfa ya rushwa kati ya familia ya Rais Jacob Zuma na familia ya wafanyabiashara wakubwa nchini humo ya Gupta.

Kwa mujibu wa ANC wameeleza kuwa tuhuma hizo nzito zinapunguza imani na heshima ya serikali yake, hivyo  kashfa hizo hazipaswi kuvumilika au kupuuzwa.

Baadhi ya vigogo wa ANC waliungana na upande wa upinzani hivi karibuni wakitaka Rais Zuma ajiuzulu kutokanana na kuandamwa na kashfa za rushwa. Kura za kumtetea zilitosha kumpa nafasi kiongozi huyo kuendelea kuliongoza taifa hilo, huku akiomba radhi kwa kutumia fedha za serikali kukarabati jumba lake kinyume cha sheria.

Hata hivyo, wanasheria wa Zuma wameendelea kupinga vikali kashfa hizo kwa madai kuwa barua pepe zilizovujishwa zilikuwa na mkakati wa kisiasa nyuma yake dhidi ya mteja wao.

Tuhuma za rushwa kati ya familia ya Rais Zuma na familia ya mabilionea ya Gupta zilidai kuwa familia hiyo ya kitajiri imekuwa na nguvu kubwa katika upangaji wa nafasi za uteuzi za Serikali hiyo kwa kutumia uwezo wake wa kifedha.

Serikali Yatangaza Kuuchukua Msitu wa Mwal Nyerere Butiama..!!!

$
0
0

Ofisi ya Waziri Mkuu, imesema itaanza kuusimamia na kuutunza msitu wa baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, uliopo Butiama, Mara kama sehemu ya kumuenzi na kuendelea kutunza mazingira.

 Hayo yamesemwa jana na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan katika kongamano la mazingira lililofanywa wilayani humo kama sehemu ya maadhimisho ya Siku ya mazingira duniani, yaliyofanyika kitaifa, wilayani Butiama.

“Sisi tutauangalia msitu huu, lakini tunaomba ushirikiano wa wakazi wa Butiama, tukiwaomba wiki hii mfanye kitu hiki, mtusaidie na tushirikiane,” amesema Makamu wa Rais


Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images