Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Lowassa Ampa Tano Rais Magufuli, Ataka Watanzania Wamuache Apitishe Fagio..!!!

$
0
0

Waziri Mkuu aliyejiuzuru kwa kashfa ya kampuni ya Richmond na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa amewataka watanzania kumuacha Rais Dkt. Magufuli kuendelea kupitisha fagio sehemu mbalimbali kwani nchi ilipokuwa imefikia ni pabaya.

Lowassa amesema kuwa ni kweli kuna baadhi ya mambo anakosea lakini si wakati wake kumkosoa kwa sasa hivyo watanzania wanatakiwa wamuunge mkono kwa kile anachokifanya kwakuwa anafanya kwa maslahi ya Taifa.

“Rais Magufuli ameanza vizuri kwa kubana baadhi ya mambo ambayo hayakuwa ya msingi, kuna mambo mazuri sana mengi ameyafanya mapaka dakika hii, lakini mwalimu Nyerere alishawahi kusema kuwa wakati unafagia ni lazima uwe makini kwani unaweza kufagia hata shilingi, na sasa Rais Magufuli anafagia shilingi nyingi, kwasasa tumuache afanye kazi yake lakini tutamhukumu muda ukifika,”amesema Lowassa.

Wenger Apewa Paun Milioni 165 za Usajili..Aambiwa Msimu Ujao Ubinga Utue Emirates Stadium..!!!

$
0
0

Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger ambaye anafahamika kwa ubahili, amepewa kitita kikubwa cha fedha akiambiwa azitumie kufanya usajili wa wachezaji wapya.

Mabosi wa klabu hiyo wamemtengea kocha huyo Mfaransa Pauni 165 milioni na kumweleza azitumie kuimarisha kikosi chake.

Bodi ya klabu hiyo imempa kitita hicho kikubwa cha fedha ili kumwezesha kushindana na wababe wengine England kwenye soko la usajili.

Tayari, Wenger anayo majina ya Riyad Mahrez wa Leicester City na Mturuki Arda Turan ambaye ameachwa na Barcelona.

Wenger ameambiwa awe makini na kikosi chake Arsenal msimu ujao kwani mwisho wa msimu atatakiwa kutwaa taji ambalo amelikosa tangu msimu wa 2004.

Picha ya Beckham Akimbusu Binti Yake Akiwa Tanzania Yazua Gumzo Kubwa ..Wazazi Wamjia Juu..!!!

$
0
0

Nguli wa soka, David Beckham ambaye hivi karibuni alikuwa nchini Tanzania, amezua mjadala wa kimalezi baada ya kuweka mtandaoni picha inayomuonesha akimpa busu zito la mdomo mwanae wa kike.

Baadhi ya wazazi walielezea picha hiyo kuwa haikuwa na maadili na inashangaza kwa kuzingatia kuwa mwanae Harper ana umri wa miaka mitano tu.

“Kwa kuwa mkweli, kumbusu mwanao wa kike mdomoni kama hivi kidogo inashangaza… ndio inashangaza,” aliandika mtu mmoja.

“Ninajaribu kutohukumu lakini nashindwa, lakini nadhani kidogo inashangaza na sio sawa kuona anambusu mwanae kwenye midomo kwa kuzingatia umri wake,” aliandika mwingine.

Hata hivyo, wazazi wenye mtazamo tofauti walijitokeza kumtetea mwanasoka huyo ambaye ni baba wa watoto wanne.

“Ni picha nzuri ya upendo inayoonesha uhusiano mzuri kati yako (Beckham) na binti yako,” 
aliandika shabiki mmoja. “Achana na wenye chuki. Ni wapumbavu. Harper sio binti mdogo, ni mtoto mdogo tu na hakuna ubaya kwa hilo,” aliandika mwingine.

Hivi karibuni, Beckham alionekana akiingia Tanzania kwa ajili ya kutembelea mbuga za wanyama, akiwa na familia yake. Ujio huo ulionekana kuwa binafsi na wa kimyakimya.

Makada CCM Wamnunia Magufuli kwa Kumteua Mpinzani Kuwa Mkuu wa Mkoa..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 5/6/2017..!!!

Majeruhi wa Ajali ya Wanafunzi 32 Arusha ,Doreen Mshana Aruhusiwa Kutoka Hospitalini Marekani..!!

$
0
0

Mtoto Doreen Mshana, manusura wa ajali ya Lucky Vincent, ameruhusiwa kutoka Hospitali na sasa ameungana na wenzake wawili katika nyumba maalum wanamoishi, Marekani, jimbo la Iowa.

 Awali, wanafunzi wengine waliokuwa wakitibiwa katika Hospitali ya Mercy Hospital, Sioux City, Saidia Awadh na Wilson Tarimo,   waliruhusiwa kutoka hospitali walimokuwa wakitibiwa.

Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu, ameandika katika ukurasa wake wa facebook na kueleza kuwa sasa Doreen, ameungana na wenzake baada ya hali yake kuimarika.

 Doreen, alibaki hospitali hapo kutokana na majereha makubwa aliyopata na hivyo kulazimika kufanyiwa upasuaji mkubwa wa uti wa mgongo.

 Wanafunzi hao walinusurika katika ajali ya basi la shule ya msingi ya Lucky Vincent, iliyoua wanafunzi 32, walimu wawili na dereva, Mei 6 mwaka huu, Karatu, Arusha.

Chadema Wambebesha IGP Sirro Sakata la Kupotea kwa Ben Saanane..!!!

$
0
0

MKUU mpya wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro, ametakiwa kutoa kauli kuhusu wapi alipo Mkuu wa Idara ya Sera na Utafiti wa Chadema, Ben Saanane, ambaye alipotea katika mazingira ya kutatanisha tangu Novemba 18, mwaka jana.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha), Patrobas Katambi katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika Makao Makuu ya chama hicho, Kinondoni, Dar es Salaam.


Katambi ambaye alizungumzia kuhusu vitendo vya utekaji, ubambikaji kesi na uvunjaji wa haki za binadamu, alisema Jeshi la Polisi liko kimya juu ya taarifa za wapi alipo Saanane.

“Mnakumbuka majibu ya Waziri Mkuu (Kassim Majaliwa) alipoulizwa kuhusu alipo Ben alitafuna maneno, hali iliyoonyesha anajua nini kinaendelea kuhusu Ben. Bavicha tunamtaka IGP mpya Sirro kutoa kauli ya Jeshi la Polisi kuhusu wapi aliko Ben, hasa kwa kuwa aliahidi kuwa vitendo vya kihalifu vitakoma na tunamtaka aanze na hili la Ben,” alisema.

Katambi pia alisema IGP Sirro anapaswa kubadili mfumo wa utendaji wa jeshi hilo, ili kuondoa uonevu dhidi ya raia, kuminya uhuru wa maoni, kukamata na kubambikia kesi raia wasio na hatia.

Alisema vijana wengi wanadhalilika kwa kukamatwa, hasa wa Chadema na kwamba katika mwendelezo huo, hata Yeriko Nyerere alikamatwa na watu wasiojulikana.

Katambi alisema yeye mwenyewe aliwahi kutekwa na watu wasiojulikana mara mbili, ikiwapo mwaka wa Uchaguzi Mkuu 2015, hivyo anashindwa kuelewa hadi imtokee nani ndipo hatua zichukuliwe.

“Tunazungumza ili hatua stahiki zichukuliwe, ikishindikana tutachukua hatua na sheria mikononi kumtafuta Ben Saanane,” alisema Katambi.

Akizungumzi suala la kutolewa silaha hadharani, alisema limeshawatokea baadhi ya viongozi waliokuwa serikalini, hivyo IGP Sirro ana wajibu mkubwa wa kusimamia utawala wa sheria.

Tahadhari..Kuwa Makini na Kofia za Helment za Bodaboda..Wanazipaka Dawa Zitakazokupoteza Fahamu Ili Wakuibie..Sambaza Ujumbe Huu kwa Mwezako..!!!

$
0
0

Hii imenitokea tarehe 28/05/2017 maeneo ya ubungo 

Iko hivi hawa jamaa waendesha bodaboda wamebuni mbinu mpya za kuwaibia wateja wao.

Niipanda Boda Boda pale ubungo river side baada ya kumweleza naelekea wapi nikapewa kofia (helmet) nikavaa ,baada ya kuivaa mara moja dereva alianza safari na akawa anaendesha mbio ilikuwa jioni ya saa 1:30 kwenda saa mbili usiku.

Kitendo cha kusogea mbele kidogo nilianza kuishiwa nguvu huku Dereva naye akianza kupotelea machochoroni baada ya muda mfupi nilipoteza fahamu sikuwa najitambua tena .

Ilinichukua masaa kama matatu hivi kuja kuzinduka kutoka usingizini,wakati huo nilijikuta vitu vyangu vyote nilivyobeba sikuwa navyo ikiwa ni pamoja na pesa kiasi cha shs 180,000 pamoja na laptop yangu na vitu vingine .

Hivyo nawaonya mnaopanda bodaboda muwe makini hasa nyakati za usiku helmet Inapakwa madawa yanayosababisha kuishiwa nguvu kabisa na hii haijalishi mwanamke ,mwanaume kuweni makini na madereva msiowajua.

Mume Ainyonga kwa Mtandio Baada ya Kugombana na Mkewe..!!

$
0
0

Mwanamume aliyefahamika kwa jina la Luhende Lusangija (34) mkazi wa Mwinamila Kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga amekutwa amejinyonga nyumbani kwake kutokana na kile kilichotajwa kuwa mke wake alikuwa anauza mali za familia kutokana na mikopo aliyokuwa anadaiwa. 

Tukio hilo limetokea Jumamosi Juni 3,2017 majira ya saa 11 alfajiri ambapo marehemu akiwa na watoto wake watatu nyumbani, aliamka na kisha kuchukua mtandio huku watoto wake wakiwa wamelala, na kuamua kujitundika kitanzi sebuleni, na kusababisha kifo chake papo hapo. 

Mashuhuda wa tukio hilo walisema Mwanamume huyo amejiua kutokana na kile kinachodaiwa kuwa ni ugomvi wa siku nyingi na mke wake ambaye siku kabla ya tukio alikuwa ameshaukimbia mji wake. 

Wakisimulia tukio hilo majirani zake Safina Javali, alisema marehemu alikuwa na ugomvi na mkewe muda mrefu ambapo kila siku walikuwa wakipigana, kwa madai kuwa mwanamke alikuwa akikopa mikopo, na baada ya kushindwa kuirejesha alikuwa akiuza vitu vya ndani wakati mumewe akiwa safarini kwenye majukumu yake ya kikazi. 

"Juzi alipokuja mwanamume kutoka safarini akakuta kitanda kimefungwa kwenda kuuzwa, ili mwanamke alipe deni la mikopo aliyokuwa akiichukua, ndipo ugomvi mkubwa ulipozuka hadi kusababisha mwanamke kuukimbia mji wake na kwenda kusiko julikana", alisema Javali.

Akiongea kuwa baada ya tukio hilo kutokea walimsikia mtoto wake wa miaka 7 majira ya saa moja asubuhi akilia kwa uchungu na kupiga kelele, kuwa baba yake amekufa kwa kujinyonga na walipofika kwenye nyumba na kuchungulia mlangoni ndipo wakamuona amening'inia kwenye paa la sebuleni akiwa ameshafariki.

Naye mwenye nyumba Halima Issa ambapo marehemu alikuwa mpangaji wake, alisema mji huo ulikuwa na ugomvi mara kwa mara na walikuwa wakiwasuluhisha lakini ugomvi wao ulikuwa pale pale, na walipopata taarifa ya kifo chake walifika eneo la tukio kisha kuwasiliana na uongozi wa mtaa ili kufuata taratibu za kisheria.

Aidha Mwenyekiti wa mtaa huo wa Mwinamila Ngokolo mjini Shinyanga Yohana Munisa, alikiri kupokea taarifa za marehemu huyo majira ya saa moja asubuhi, na alipofika eneo la tukio alimkuta Lusangija akiwa tayari amejinyonga, ndipo akatoa taarifa polisi ambapo nao wakafika ili kuuchukua mwili wa marehemu.

Kwa upande wake Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Elias Mwita alithibitisha kutokea kwa tukio hilo, na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga, huku ndugu wa marehemu wakitafutwa ili kuuchukua mwili huo kwa taratibu za mazishi.

Ajib Ataka Milioni 60 Asaini Singida United..!!!

$
0
0

KIUNGO Mshambuliaji wa Simba, Ibrahim Ajib, amewataka Singida United kumpa Sh milioni 60 ili wapate saini yake kwa ajili ya kuwatumikia msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Ajib ambaye kaonyesha nia ya kuondoka Simba baada ya mkataba wake kuisha na kwenda kutafuta changamoto nyingine ya soka, jina lake limetajwa na kocha Hans Pluijm kwenye kikosi chake.

Tayari mchezaji huyo amekwishaweka bayana kuwa anahitaji fedha hizo na endapo itashindikana, hawezi kujiunga na timu hiyo mpya kwenye Ligi Kuu msimu ujao.

Mbali na Ajib pia timu hiyo imeonyesha nia ya kumtaka mchezaji wa Yanga, Deus Kaseke ambaye naye anahitaji Sh milioni 40.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Singida United, Festo Sanga, alithibitisha kufanya mazungumzo na wachezaji hao, lakini bado hawajafikia hatua ya kuwafanya wasaini katika klabu hiyo.

“Ni kweli tunawahitaji na tumefanya nao mazungumzo na tumeweka wazi kiasi ambacho tunacho mkononi, ila inaonekana wao bado hawapo tayari, hivyo tunawasubiri  wao wakiwa tayari sisi hatuna shida muda wowote wakitufuata tutasaini,” alisema Sanga.

Alisema kuwa malengo yao msimu huu ni kusajili wachezaji 25, wapya wakiwa 14, saba kutoka nje na saba wengine kutoka ndani, huku mpaka sasa wachezaji wa ndani bado watatu kwa kuwa wamesajili wawili tu.

Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid, Je? Unapata Pesa Haikai? Umeachwa na Mpenzi, Mke au Mme Anakusumbua?

$
0
0


MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI. (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 72 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI: SHEKH SHARIFU RASHID ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran dawa za asili dawa za kiarabu, na njiwa, Anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango kwa kina mama, ngiri maji na n.k, anakuvutia mali zilizo potea au kudhulumiwa, pia anatoa Pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali, Wenye matatizo ya uzazi, jini mahaba, mapepo ya kichawi, vifungo vya kimaisha, ndoto mbaya za usiku, uelewa mdogo wa ufahamu shuleni kwa watoto wote, pia anauwezo mkubwa wa kumaliza kazi zilizoachwa na wataalamu wengine ndani ya masaa 48 tu, Pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo. WASILIANA NAE KWA WhatsApp na SIMU NO: +255 718-668347 na +255 767-204308 +255 685-224047 Email shekhsharifurashidi@gmail.com.

USHAURI: ni vyema kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate huduma kwa haraka.

Uwoya astushwa na habari za Ujauzito

$
0
0

DAR ES SALAAM: Sexy lady wa sinema za Kibongo, Irene Pancras Uwoya ‘Mama Krish’ amefungukia madai kuwa, kwa sasa ametengeneza urafiki wa muda na ndimu, samaki wabichi na ukwaju kwa kinachosemekana ni mjamzito.

Huku akionesha kushtushwa na habari hizo zinazoenezwa bila kutaja mhusika wa kibendi hicho, Uwoya alikuwa na haya ya kusema:

“He! Mimi? Mjamzito? Jamani imekuwa too much (imezidi), watu wanaongea kama hawana mambo ya kufanya maishani, kinachowashtua wengi ni mabadiliko ya mwili wangu. Unajua nimenenepa kwa kweli, inafika mahali mtu anaridhika na maisha.

Mwili nao unabadilika kutokana na sababu za kibaiolojia, sina njaa kama zamani. Napata madili mengi, hivyo lazima niridhike na kunenepa, wengi wanadhani ni mimba na hata familia yangu, walidhani ni hivyo, lakini sina mimba na hata sifikirii kufanya hivyo kwa sasa,” alisema Uwoya.

Mbasha Ahofia Kupata Shambulio la Moyo Kama la Ivan Don

$
0
0

MWIM-BAJI wa Mu-ziki wa Injili, Emmanuel Mbasha ameibuka na kusema kuwa amekubaliana na yote kwa aliyekuwa mkewe, Flora Mbasha ili kuepuka yaliyompata mzazi mwenzake na Zari, Ivan Ssemwanga wa Uganda ya kufariki dunia kwa shambulio la moyo.

Akipiga stori na Over Ze Weekend baada ya habari kuzagaa kwamba ana msongo wa mawazo unaosababishwa na aliyekuwa mkewe, Flora ambaye kwa sasa ni mke wa mtu, alikanusha vikali akisema yupo sawa na hawezi kuwa hivyo kwa kuwa amekubaliana na kila kilichotokea.

“Sitaki kupata tatizo la moyo na tangu mwanzo hata kabla hatujaachana kwa talaka mahakamani mawazo mabaya yalikuwa yakinijia nikayakataa kwa sababu ningeyasikiliza ningejikuta nikiziharibu ndoto zote za maisha yangu, nilishayakubali yote, nimeshazoea hiyo hali” alisema Mbasha.

Aliendelea kueleza kuwa sababu za kumweka Flora kwenye ukurasa wake wa Instagram siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake aliyokuwa akiadhimisha Juni Mosi, mwaka huu na kumtakia mema ni kutokana na upendo tu kwani siku hiyo huwa inamkumbusha mengi waliyokuwa wakiyafanya.

“Nakumbuka kila tarehe moja ya mwezi wa sita kila mwaka tulivyokuwa tunaifurahia, namnunulia zawadi tunafanya pati kidogo nyumbani au sehemu yoyote,.

“Kuposti kwangu huko nimeshangaa watu maneno yamewatoka sana kwa kweli, niliposti kiroho safi tu na kwa upendo maana nilishayakubali matokeo, sina msongo wa mawazo maana najua ni hatari naweza nikapoteza uhai kama ilivyotokea kwa mume wa Zari, Ivan nikashindwa kutimiza ndoto zangu za kuwa mfanyabiashara mkubwa na mtumishi wa Mungu mku-bwa sana duniani,” alisema.

Harmonize amuonesha mpenzi wake mpya

$
0
0

Baada ya kuachana na mrembo wa filamu Tanzania Jacqueline Wolper, muimbaji wa  wimbo  Happy BirthDay kutoka WCB, Harmonize, ameonesha picha ya mpenzi wake mpya mzungu pamoja na kuthibitisha ni mjamzito.

Muimbaji huyo ambaye alikuwa kimya kuzungumzia mahusiano yake mapya na mzungu huyo licha ya kuzungumzwa na watu kwenye mitandao ya kijamii, Jumapili hii ameonyesha vipimo vya Ultrasound vikionesha mpenzi wake huyo mzungu ni mjamzito.

“Mnh! nawaza huu mchanganyiko wa damu ya kimakonde na ya kizungu sijui itatuletea mwana gani… asa nikiona kakomwe hapo, kananistua😁…Chonde mtoto chukua vyote kwangu ila kwenye rangi jitahidi uibe ya mama yako…..!!! nikavimbe Mtwara 😊,” aliandika Harmonize Instagram.

Hata hivyo muimbaji huyo hakuweka wazi ujauzito huo ni wa miezi mingapi.

Halim Mdee na Ester Bulaya Wazuia Kuingia Bungeni Hadi Mwakani Kwenye Bunge la Bajeti..!!!

$
0
0

Halima Mdee na Esther Bulaya wamehukumiwa kutohudhuria vikao vyote vya bunge linaloendelea mpaka mkutano ujao wa Bunge la Bajeti ya 2018/19.

Hukumu hiyo imeungwa mkono na wabunge wengi waliopitisha azimio hilo.

Mapema leo, Jumatatu Kamati ya Maadili  ilisema Bulaya na Mdee wamemaliza adhabu za kawaida zilizopo kwenye kanuni za bunge.

Hata hivyo, Bunge liliendelea  kujadili makosa ya wabunge hao wa Bunda na Kawe.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, George Mkuchika aliliomba Bunge kujadili adhabu inayostahili kulingana na makosa yao.

Kanuni inasema, mbunge anayefanya kosa la kwanza anaweza akazuiwa kuhudhuria vikao visivyozidi 10 na atayakosea kwa mara ya pili anaweza kuzuiwa kuhudhuria vikao visivyozidi 20.

Bunge Lawasulubisha Halima Mdee na Ester Bulaya leo

$
0
0

Mbunge wa Kibamba (Chadema), John Mnyika amesema atachukua hatua kwa kitendo cha kusukumwa kilichofanywa na askari wa Bunge mwishoni mwa wiki.


Alisema atafanya hivyo mara baada ya kumaliza msiba wa mmoja wa waasisi wa chama hicho, Philemon Ndesamburo.


“Nitatoa tamko na kuchukua hatua nikimaliza msiba, leo (jana) na kesho (leo) nipo msibani huku Moshi, lakini nitafafanua na kuzungumzia hilo nikimaliza,” alisema.


Mnyika alitolewa bungeni kwa nguvu na askari wa Bunge baada ya Spika wa Bunge, Job Ndugai kuwaamuru kumtoa ndani akidaiwa kukiuka kanuni za Bunge wakati akichangia mjadala wa Wizara ya Nishati na Madini.


Pia, mbunge huyo alipewa adhabu ya kutohudhuria vikao saba vya Bunge, huku askari hao wakimtoa ndani kwa nguvu na kumsukuma.


Ndesamburo, ambaye amewahi kuwa Mbunge wa Moshi Mjini kwa miaka 15 mfululizo ataagwa leo katika Uwanja wa Majengo mjini Moshi na baadaye mwili wake utapelekwa nyumbani kwake ambako taratibu za mazishi zitafanyika kesho.


Wakati Mnyika akisubiri kumzika Ndesamburo, Chadema Wilaya ya Ubungo imelaani kitendo alichofanyiwa mbunge huyo ikisema hakikuwa cha kiungwana na kilikiuka hadhi yake.


Katibu Mwenezi wa Chadema wilayani humo, Perfect Mwasiwelwa alisema kitendo alichofanyiwa Mnyika kingeweza kumletea majeraha kama angeanguka kutokana na mazingira ya eneo aliposukumiwa.


Mwasiwelwa alisema mwanasiasa huyo anawawakilisha wananchi zaidi ya 78,000 hivyo Chadema inalaani kitendo hicho kwa sababu si cha utu.


“Alitolewa nje katika mazingira ambayo sio ya utu, sio ya Kitanzania, sisi kama chama ngazi ya wilaya tunasema hakikuwa kitendo cha kawaida kabisa,” alisema.


Wakati huo huo, wabunge wawili wa Chadema; Halima Mdee (Kawe) na Esther Bulaya (Bunda Mjini) leo watasomewa hukumu yao baada ya Kamati ya Kudumu ya Maadili ya Bunge kuwajadili na kumshauri Ndugai hatua sahihi za kuwachukulia.


Bulaya na Mdee watasomewa hukumu kutokana na kulivalia njuga suala la Mnyika kutolewa ndani ya ukumbi wa Bunge wakati spika alipoamuru atolewe na askari wa chombo hicho.

Mavugo Amsainisha Ndikumana Simba Sc,,Hivi Ndivyo Mchezo Ulivyokuwa..!!

$
0
0

SIMBA inahitaji huduma ya beki Mrundi wa Mbao FC, Yusuf Ndikumana, katika msimu ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na sasa imeamua kumpa dili hilo Mrundi mwenzake, Laudit Mavugo ili alikamilishe.

Ndikumana ameonyesha kiwango kizuri akiwa katika kikosi cha Mbao FC ambayo ilipandishwa daraja kucheza msimu huu Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya kutokea upangaji wa matokeo kwa timu za Geita Gold na Polisi ya Tabora.

Beki huyo ambaye yuko katika rada za timu tatu hapa nchini Simba, Yanga na Kagera Sugar ambapo nao wanahitaji huduma ya mchezaji huyo, amedaiwa kuwa ameamua kuzipiga chini timu mbili na kukubali kutua Msimbazi.

Uongozi wa Simba umemtumia straika wao, Mavugo baada ya kubaini ukaribu uliopo kati yake na Mrundi huyo mwenzake na mambo yanaenda vizuri.

Ndikumana kwa sasa ni mchezaji huru mara baada ya kumaliza mkataba wake wa kukitumikia kikosi cha Wauza Mbao  mkoani Mwanza.

Taarifa za uhakika kutoka ndani ya klabu ya Simba, zinaeleza kwamba mchakato wa kumpata beki huyo mwenye uwezo wa kucheza kama kiungo ulianzia baada ya kumalizika kwa fainali ya michuano ya Kombe la FA, mjini Dodoma.

Alisema Simba wameridhika na kiwango kilichoonyeshwa na mchezaji huyo, hali iliyopelekea kupendekeza jina lake katika usajili.

“Mchakato unaendelea vizuri, kwa upande wa mchezaji huyo haina shida kwani tayari maelekezo amepewa Mavugo ili msimu ujao awepo katika kikosi cha timu yetu,” alisema.

Alisema mara baada ya jina hilo kufika mezani, viongozi walifuatilia rekodi za mchezaji huyo kwa kujiridhisha  ambapo mchakato wake sasa umefika katika hatua nzuri ya makubaliano ya kusaini miaka miwili.

DIMBA lilikuwa shuhuda wakati Ndikumana na Mavugo walipokaa pembeni na kuzungumza mara baada ya kumalizika kwa fainali, lakini pia mmoja wa wachezaji hao aliomba mawasiliano ya simu.

Ndikumana alipoulizwa juu ya hilo, hakutaka kuweka wazi na kusisitiza kwamba kwa sasa hajafanya mazungumzo na timu yoyote na kuhusu Mavugo alidai ni mtu  wanayefahamiana kwa muda mrefu.

“Mavugo ni rafiki yangu tulikuwa wote timu ya Taifa ya Burundi, suala la Simba kama wapo tayari  kutoa kiwango cha fedha anachotaka, nitajiunga nao,” alisema.

Maalim Seif Afunguka ya Myoni Juu ya Kitendo cha Rais Magufuli Kumteua Mpinzani Kuwa Mkuu wa Mkoa..!!!

$
0
0

KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad amemkingia kifua Rais Dk. John Magufuli kwa uamuzi wake wa kumteua Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Maalim Seif alisema Rais Magufuli hajakosea kwa uteuzi huo kwa kuwa hapangiwi nani amweke wapi na nani asimweke.

“Uteuzi ni haki yake, wala hatuingilii maamuzi yake kwa sababu kuteua au kutoteua ni yeye na kuteua ACT na kuacha vyama vingine huenda yeye mwenyewe ana yake moyoni na kwamba hajaamua kufanya hivyo.

“Mimi sikuingia katika moyo wake na kwa kufanya hivyo si jambo geni kwa kuwa wapo waliopita waliwapa wapinzani ubunge, lakini pia ni Rais wa kwanza kuingiza mtu wa chama kingine kwenye serikali katika utendaji…si jambo baya kwa maana linaweza jenga upya Serikali,’’ alisema.

Alisema Rais Magufuli ametumia mfumo ambao pia hutumiwa na nchi za Bara la Ulaya na Marekani, ambapo Rais Mstaafu wa Marekani, Barack Obama naye aliutumia.

“Siwezi kushangaa kwani inaweza ikatokea siku akamteua Naibu Katibu Mkuu wangu, Joran Bashange kuwa Waziri wa Nishati na Madini,” alisema Maalim Seif huku waandishi na maofisa wa chama hicho wakiangua kicheko.

UVCCM

Nao Umoja wa  Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM),  umesema hatua ya Rais Dk. Magufuli kumteua Anna Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ni kitendo cha kijasiri na cha kizalendo kwa sababu  hakuna alipokosea.

Pamoja na hali hiyo, umoja huo umesema uteuzi wa nafasi ya RC Mghwira, ni wazi ataisimamia na kuongoza kwa hekima, busara na uzalendo kwa masilahi ya Taifa.

Kauli hiyo, imetolewa  Dar es Salaam jana na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka.

Alisema uteuzi huo, usiibue nongwa na kuonekana kuna jambo limekosewa.

Pamoja na hali hiyo Shaka, alisema Katiba ya nchi hairuhusu mgombea binafsi na kwamba kila mgombea urais, udiwani au ubunge hutokana na chama cha siasa ila anaposhinda urais huwa na mamlaka ya kuteua mtu yeyote ili mradi awe Mtanzania bila ubia.

Alisema Rais Dk. Magufuli, ana haki na wajibu wa kumteua mtu yeyote atakayeona anafaa kushika nafasi atakayomteua ilimradi aliyeteuliwa awe ana hisia za uchapakazi, mpenda umoja na mzalendo.

Shaka alisema katiba ya CCM imetamka ikiwa kutakuwa na mkuu wa mkoa anayetokana na CCM atashiriki vikao vya Kamati ya Siasa ya Mkoa wakati wa vikao lakini kwa suala la Mghwira lipo tofauti kwani anatokana na chama kingine na ikiwa ataona kuna haja ya kujiunga na CCM basi naye atapata fursa ya kushiriki vikao hivyo.

“Ila kwa sasa hasa baada ya kuripoti katika eneo lake la kazi hatoweza kuhudhuria vikao vya Kamati ya Siasa ya Mkoa kwa kuwa si mwana CCM ila kama ataona kuna haja ya kujiunga na CCM hazuiwi na atakuwa na haki ya kuhudhuria vikao vyote.

“Kwa hili Rais Dk. Magufuli anabaki kuwa nembo ya demokrasia ya kweli nchini kwetu kwa kushirikisha wapinzani kwenye nafasi nyeti za utendaji.

“Viongozi wa Serikali wakiteuliwa hula viapo vya utii ambavyo vimeandikwa kisheria katika medani za uendeshaji Serikali, mteule wa Rais hali kiapo cha kisiasa bali huapa kiapo cha kutumikia nchi na watu wake kwa mujibu wa sheria za nchi na Katiba,” alisema Shaka.

Beki wa Klabu ya Liverpool Mamadou Sakho Atua Tanzania Kimyakimya na Kujichimbia Arusha..!!!

$
0
0

Beki wa Liverpool anayetakiwa na Crystal Palace, Mamadou Sakho ametua Arusha akiwa njia kutembelea mbuga za wanyama.

Sakho anafuata nyayo za David Beckham aliyekuwa nchini wiki iliyopita na kutembelea mbuga ya wanyama ya Serengeti.

Sakho alipoteza mvuto katika kikosi cha Liverpool chini ya kocha Jurgen Klopp aliyeamua kumtoa kwa mkopo Crystal Palace mapema Februari.

Hata hivyo, dau la pauni 30 milioni wanalotaka Liverpool linaonekana kumshinda mwenyekiti wa Palace,  Steve Parish akisema fedha hizo nyingi kwao.

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Kiliamnjaro Meck Sadick Ampa Tahadhari Anna Mghwira Kuhusu Mkoa wa Kilimanjaro..!!!

$
0
0

Aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Said Meck Sadiki amesema uteuzi aliyoufanya Rais John Magufuli kwa kiongozi wa Chama cha ACT- Wazalendo, Anna Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, ni sahihi.

Sadiki aliliambia gazeti la Habarileo, kuwa Rais hajakosea kumteua Mghwira kuwa kiongozi wa mkoa wa Kilimanjaro kwani mwana mama huyo ni mchapakazi, mzalendo na asiye na ubaguzi, na uongozi unahitaji mtu wa aina hiyo.

Meck alisema kuna maeneo matano ambayo angependa mteuliwa huyo ayape kipaumbele ikiwa ni pamoja na uharibifu wa mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji. Alisema kama mazingira yataharibiwa zaidi ndani ya miaka 10 mkoa utakuwa jangwa na kukumbwa na baa la njaa. Katika eneo hilo, alitaka Mghwira ashirikiane na taasisi na viongozi wengine kutunza mazingira na vyanzo vya maji.

Hata hivyo eneo jingine alisema ni uvushwaji wa bidhaa za magendo kutoka Tanzania kwenda Kenya. Alisema mkoa unakosa mapato mengi kutokana na mbinu za ujanja za wafanyabiashara wasio waaminifu. Alimtaka kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa kujipanga vyema kudhibiti hilo. Dawa za kulevya Alisema kuwa zimekuwa zikiathiri maendeleo ya mkoa.

Bi Anna anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Saidi Meck Sadiki.

Lowassa na Mbowe Waupokea Mwili wa Ndesamburo..!!!

$
0
0

Viongozi wa juu wa Chadema, Freeman Mbowe na Edward Lowassa wameupokea mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema, Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo baada ya kuwasili katika viwanja vya Majengo.

Ndesamburo alifariki ghafla wiki iliyopita wakati akipata matibabu katika hospitali ya KCMC.

Mwili wa Ndesamburo ambaye pia aliwahi kuwa mbunge wa Moshi Mjinim,utaagwa katika viwanja hivyo na leo saa kumi jioni utapelekwa nyumbani kwake kwa ajili ya taratibu za mazishi.

 Wabunge na Viongozi mbalimbali wa Chadema, akiwamo muasisi wa chama hicho, Edwin Mtei, Frederick Sumaye wapo uwanjani hapo kwa ajili ya kumuaga Ndesamburo.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images