Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Alichokisema Julius Mtatiro Baada ya Mhe Anna Mghwira wa ACT Wazalendo Kukubali Uteuzi wa Kuwa Mkuu wa Mkoa..!!!

$
0
0

Na. Mtatiro J

#UTEUZI_WA_KITILA
Niliunga mkono uteuzi wa Prof. Kitila kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji. Kitila tangia hapo amekuwa mtendaji ndani ya Serikali kwa hiyo kilichofanyika ni kumhamisha tu kutoka kutumikia Chuo Kikuu hadi Wizara mojawapo serikalini.

#UTEUZI_WA_BI_MGHWIRA
Siungi mkono Uteuzi wa Anna Mghwira kuwa RC, japo naendelea kumheshimu na kuheshimu uamuzi wake wa kupokea uteuzi. Kama JPM angelimteua kuwa Mbunge, ningeunga mkono na kumpigia makofi makubwa sana.

#UTEUZU_WANGU
Na hapa ieleweke kuwa, kama leo JPM ananiteua mimi kuwa Mbunge, ntakwenda Bungeni na ntabakia na hadhi ya kutumikia mawazo ya wananchi na ntaipa changamoto serikali na kuisaidia huku nikijenga chama changu. Lakini leo JPM akiniteua kuwa Waziri au Mkuu wa Mkoa ntamshukuru kwa kiingereza. "NO, THANK YOU!"

#MANDELA
Unajua, hizi siasa tulizomo zina misingi yake na lazima uijue, uisimamie na uipiganie. Nelson Mandela alifuatwa Gerezani mara kadhaa na Makaburu, wakamuomba akubali kutolewa gerezani ili apewe Umakamu wa Rais wa Afrika ya Kusini na hadhi kubwa sana. Mandela alisema "NO, UNTIL MY PEOPLE ARE FREE FROM APARTHEID" (Sitaki, hadi watu wangu wawe huru na kuondoka kwenye Utawala wa Kibaguzi).

Maneno ya Mandela yanatukumbusha kuwa, tunapokuwa na majukumu makubwa na tumeaminiwa na kupewa nyadhifa kubwa za kisiasa kwenye taasisi zetu, kipaumbele chetu kinapaswa kuwa AGENDA ya Taasisi yetu na chombo tunachokitumia kuisimamia ajenda hiyo (Forum).

#MASHARTI
Mathalani, ukitaka mimi nifanye kazi katika Serikali ya Magufuli (katika cheo kisicho Ubunge) ntakupa masharti magumu na ya msingi. Sharti la kwanza, Je Serikali ya Magufuli iko tayari kusimamia Demokrasia hapa Tanzania? Je, iko tayari kuruhusu Uhuru wa Mawazo na Tofauti ya Mawazo? Je iko tayari kuruhusu Uhuru wa Bunge na Ukuu wa Katiba? Je iko tayari kufuata na kulinda Sheria za nchi? Je iko tayari kuwa sikivu na isiyofanya maamuzi kwa ubabe na ukuu wa mtu mmoja?

Ikiwa Serikali ya Rais Magufuli ingelikuwa imeamua kufuata utaratibu wa kuleta mabadiliko nchini kwa njia ya kulinda demokrasia, kuheshimu katiba na sheria za nchi, kuimarisha nguvu na umuhimu wa Bunge na Mahakama na Kukuza Misingi ya Umuhimu wa Vyama Mbadala na Uhuru wa Kutoa mawazo; ningeliunga mkono uteuzi wa Mama Mghwira!

#UTAMADUNI_NA_UTARATIBU
Lakini niwakumbushe jambo lingine, kwamba masuala ya VIONGOZI wa chama kimoja kuteuliwa kujiunga na Serikali ya Chama kingine, hufanywa kwa heshima kubwa. Yaani, uteuzi wa KIONGOZI wa chama cha ACT kujiunga Serikalini duniani kote, ulipaswa kufanywa kwa heshima. Kwa kawaida, Rais alipaswa kuwasiliana na Kiongozi Mkuu wa chama na kumjulisha nia hiyo, hata kama Kiongozi Mkuu wa ACT na chama chake wangelikataa, Rais angelikuwa ametimiza wajibu wake wa Ustaarabu wa Kidemokrasia.

Ndiyo maana, Katibu Mkuu wa UN alipotaka kumteua Dk. Rose Migiro kuwa Naibu Katibu Mkuu wa UN kwanza aliomba ruhusa kwa Rais Kikwete (Rais aw Tanzania), huo ndiyo utaratibu IKIWA UTEUZI UNAFANYWA KWA NIA NJEMA!

#GNU_ZNZ
Ama, unapotaka kuteua Kiongozi kutoka Chama kingine kunapaswa kuwa na mazungumzo ya kivyama. Mathalani, uundaji wa GNU Zanzibar (2010 - 2015) ambapo wakati wa kuandaa Baraza la Mawaziri, CUF ilipendekeza majina ya watu wanaopaswa kuteuliwa na Rais Shein, na Shein akawateua, hakujiamulia tu! Mambo haya huhitaji utaratibu, na unapovunjwa yanachukuliwa kama michezo michafu, kudhoofishana, kushughulikiana, kupeana rushwa za madaraka, vyeo, ukubwa, mali, fedha n.k.

#SISI_NA_WAO
Sisi ambao tunathubutu kujadili teuzi hizi za JPM tunaambiwa tuna wivu, tuna gere n.k. huo ni upuuzi tu. Sisi binadamu tulivyoumbwa, wapo watu akiona VX kubwa la Serikali na Walinzi wa kumlinda, anaona AMEUKATA! Tupo watu tunaoona vitu hivyo kama MATERIAL THINGS (vitu vya kupita tu). 

Wapo watu huamini kuwa siku wakiteuliwa na kuwa na MAMLAKA juu ya Maelfu na Makumi Elfu, huko ni KUUKATA...Tupo sisi wengine ambao tunaamini vyeo ni vitu vya kupita tu. Leo mama Anna Mghwira ameteuliwa, amekubali uteuzi huo, amekiacha chama chake "bila kukubaliana nacho," ameacha misingi yake alokuwa anaisimamia, na ameungana na wale wasiotaka kabisa chama chake kifanye hata mkutano wa hadhara, amepokea uteuzi bila hata kumwambia mteuzi "heshimu katiba na sheria za nchi." 

#TUSIMHUKUMU
Tusimhukumu, tumjadili tu ili itupe mafunzo mbeleni. Lakini nataka kuwaambia kuwa ANAYESALITI imani yake kwa sababu ya cheo hujidanganya yeye mwenyeww, vyeo, ukubwa, mamlaka na ukuu vinapita haraka mno, kama upepo na historia inaandikwa juu ya kila mmoja wetu.

#BOB_MARLEY
Hayati Bob Marley alipata kusema "Wapo wanamuziki wana Pesa na Utajiri mkubwa sana kwa sababu ya muziki lakini fedha zao hazitadumu. Mimi (Marley) nina utajiri wa Mashairi, siyo fedha, mashairi yangu yatadumu milele, ujumbe wake utadumu milele, maana sikuwa naimba ili kupata pesa, bali kusimamia misingi nayoiamini."

Mtatiro J,
juliusmtatiro@yahoo.com
Whatsup; 0787536759.

Kibiti: Askari Mgambo Auawa kwa Kupigwa Risasi..!!!

$
0
0

Mkazi wa Kitongoji cha Kazamoyo, wilayani hapa, Erick Mwarabu (37) ameuawa kwa kupigwa risasi usiku akiwa nyumbani kwake. Watu wa karibu katika eneo hilo wamesema marehemu huyo aliyekuwa askari mgambo alipigwa risasi tatu akiwa uvunguni mwa kitanda alikokuwa amejificha. 

Mkazi mmoja wa eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina moja la Simon amesema watu hao wanaosadikiwa kuwa ni majambazi walivunja mlango wa nyumba yake saa 9.00 usiku kisha kuingia ndani na kutekeleza mauaji hayo. 

Simon amesema baada ya watu hao na kuingia ndani walipitiliza moja kwa moja hadi kwenye chumba chake ambapo walimkuta mkewe marehemu na kumhoji alipo mumewe. Amesema baada ya kuona mkewe hataji mahali alipo mumewe walianza kumtafuta ndani ya nyumba yake na kufanikiwa kumuona marehemu akiwa amejificha uvunguni mwa kitanda ndipo wakamfyetulia risasi na kuondoka. 

Simon amesema baada ya kutekeleza mauaji hayo hawakuchukua kitu chochote. Mganga mkuu wa kituo cha afya Ikwiriri, Dk Iddy Malinda amesema katika uchunguzi walioufanya walibaini marehemu alikuwa na majeraha matatu ya risasi katika maeneo tofauti ya mwili wake. 

“Majeraha mawili yalikuwa kwenye ubavu wa kulia na moja kichwani,” amesema. Dk Malinda amesema mwili huo tayari umekabidhiwa kwa ndugu zake kwa ajili ya mazishi. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga amesema polisi wanaendelea kufuatilia tukio hilo.

Miss Tanzania Diana Edward kumfuata Wema Sepetu alipo

$
0
0

Miss Tanzania 2016/7 Diana Edward ameweka wazi yupo mbioni kuingia katika tasnia ya uigizaji wa filamu nchini [Bongo Movie] kama alivyofanya aliyekuwa Miss Tanzania mwaka 2006 Wema Sepetu.

Mrembo huyo amesema lengo la kuingia katika uigizaji, nikutaka kubadilisha mtazamo wa Watanzania kuwa nchini hakupatikani filamu zenye ubora au hazipo habisa, na yeye atajikita katika uigiaji wa filamu za action.

“Kila kitu kipo tayari, nimeshafanya mazoezi sasa hivi nasubiria mambo yangu yakikaa sawa nianze kutengeneza. Napenda action movie kwa sababu am so addicted in action movie, staki kusema mengi sana kwa sababu nasubiria maamuzi kutoka kwa meneja wangu itakuwaje, kwa hiyo msubiri,” amekiambia kipindi cha Twenzentu cha Times FM.

“Mimi nilikuwa naigiza kuanzia muda mrefu ingawa sikutoa movie yoyote,” ameongeza.

Jack Wolper Atoa Onyo Hili Kali

$
0
0

MUIGIZAJI mwenye jina Bongo, Jacqueline Wolper ‘Wolper’ amefunguka kuwa kuna watu wamekuwa wakipiga pesa kwenye mitandao ya kijamiii kwa njia mbalimbali kupitia jina lake jambo ambalo hapendezwi nalo.

Akichonga na Uwazi Showbiz, Wolper aliongeza kuwa taarifa juu ya watu hao anazo na anazifanyia kazi, upelelezi wake ukikamilika atawafikisha kwenye vyombo husika ili wakacheze na mkono wa sheria.

“Kuna watu mitandaoni wanapiga pesa kupitia jina langu kwa njia mbalimbali ambazo nimeshazifahamu. Sasa mimi nawaonya tu na kuwataka waache mara moja maana dawa yao inachemka jikoni,” alisema Wolper.

Ongeza Hips, Makalio, Mapaja, Miguu, Uume na Nguvu za Kiume

$
0
0

ONGEZA HIPS, MAKALIO, MAPAJA, MIGUU, UUME NA NGUVU ZA KIUME. PIA KUPUNGUZA UNENE, KUWA MWEUPE BILA SUGU NA KUONDOA MADOA.
@Markson_beauty_pr Tunakuletea bidhaa bora zenye matokeo ya uhakika na haraka zisizo na kemikali wala madhara. Zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kudhibitishwa kiafya.
🍉🌿🍅🍍🍒🍉🍓🍅🍒
NB÷ Matokeo ni uhakika na garantii. Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
BIDHAA ZETU:-

1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @120,000/=
2. Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa:-
(a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200,000/=
(b)Vidonge @180,000/=
(c)BOTCHO 10× ya kupaka @ 150,000/=
3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:-
(1)Mafuta @120,000/=
(11)Vidonge @150,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-
(a) Gely ya kupaka @130,000/=
(b) Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu hata kwa wenye kisukari @130,000/=
(C)Handsome up original @200,000/=
6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @120,000/=
7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula @120,000/=
8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a) Dawa ya kunywa au kupaka @120,000/=
(b) Mkanda wa kawaida @100,000/=
(c) micro-computer belt wa umeme @170,000/=
9 .Kupunguza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120,000/=
10.Kushepu miguu (CHUPA YA BIA) na kuondoa vigimbi @120,000/=
11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @120,000/=
12.Kurudisha usichana (bikra) @120,000/=
Wasiliana nasi :- (+255)
0767447444au 0714335378
👉🏻Ili kuona bidhaa zaidi na shuhuda za waliotumia bidhaa zetu. ...............

Kuoa Mwanamke Kutoka Uswahilini au Alieishi Maisha Duni ni Kujichimbia Kaburi na Kujipa Umaskini

$
0
0

Kuna jamaa yangu amezua hoja nzito kwamba kamwe hawezi kuoa mwanamke anaetoka familia ya kimaskini maana wengi wao hawana shukrani maishani.. anakwambia angalau watoto wa kishua japokuwa wavivu kazi za ndani ndogo ndogo but wanajua kupenda na hata cheating ni ngumu sana.

But mwanamke anaetoka familia yenye dhiki wengi wao vigeu geu mwepesi sana kubadilika badilika.. na ametoa mifano hai mingi tu ya ndoa za tunaowafahamu..
Pia wengi wanaamini sana mambo ya Ushirikina kwenye mapenzi

Wadau hii mnaonaje?

Je kuna ukweli wowote hapo?

Aslay Afunguka Mambo Haya Matatu Ambayo Kamwe Hatayasahu Kuhusu Ya Moto Band..!!!

$
0
0

Msanii wa muziki Aslay anaye tamba na kibao cha  ‘Angekuona’  azungumzia mafanikio aliyoyapata akiwa na Bendi ya Yamoto ikiwa chini ya mkubwa Fella amesema ni mengi ila haya ni machache na yenye kipaumbele katika mafanikio yake kimuziki

Kutembea Nchi mbalimbali
“Yamoto bandi tumeweza kutembea sehemu mbalimbali hapa duniani jambo ambalo ni  neema kwa mwanamuziki kwakutengeneza Connection, tumezunguka marekani,Asia na Hata baadhi ya nchi za afrika kama vile Rwanda na kwingineko”

2.Kujengewa Nyumba

“Tumejengewa nyumba tukiwa yamoto bandi kila msanii anayumba yake ,hilo ni jambo kubwa sana kwani kuna baadhi ya watu wanafanyiwa management lakini hawapati  nafasi hiyo binafsi namshukuru sana Mkubwa Fella kwa kutufanya tuwe na makazi ”

3.Kuwa mimi kama mimi  na kujijenga zaidi

“Kwasasa ninamaisha yangu ambayo naweza kupata riziki za hapa napale  na ninaweza kuendesha familia yangu vizuri pasipo na shida na nimefanikiwa kufungua biashara ndogo ndogo ambazo zinaniingizia kipato cha kila siku”

Je, Wanawake Mnaijua Hii Kazi Nyingine ya Limao? Jifunze Hapa..!!!

$
0
0

Moja ya mambo ambayo huchanga kuharibu afya ya nywele ni pamoja na tatizo la mba ambalo huchangia pia mhusika kupata muwasho wa kichwa wa hapa na pale.

Sasa leo naomba nikupatie hii mbinu asili ambayo huweza kusaidia kumaliza haraka tatizo la mba

Tumia juisi ya limao

Namna ya kufanya utatakiwa kutafuta malimao mawili makubwa kisha kamua kwenye kikombe cha chai chenye maji. Kisha tumia maji hayo yenye mchanganyiko wa limao kwa kuweka kichwani na uchanganye vizuri kisha acha kwa dakika 5 hadi 10 kabla ya kuosha nywele zako.

Fanya zoezi hilo kutwa mara mwili ndani ya wiki mbili mfululuzo na utaona mabadiliko

Maajabu..Kanisa Nchini Ghana Wafanya Ibada ya Kujipongeza Baada ya Chelsea Kutwaa Ubingwa wa Uingereza..!!

$
0
0

Kanisa la Living Stream International la nchini Ghana limefanya ibada maalum ya shukrani baada ya Chelsea kufanya vizuri kwenye Ligi Kuu ya Uingereza na kufaniliwa kuchukua kombe.

Unafahamu Umuhimu wa Tende Mwilini..? Jibu Liko Hapa..!!!

$
0
0

Tende ni tunda ambalo linayeyuka kirahisi tumboni na lenye faida nyingi sana ambazo hulifanya liwe tunda la kipee.

Zifuatazo ni faida ya tunda la tende katika mwili wa binadamu.

Kwa watu wenye matatizo ya tumbo, nicotinic inayopatikana kwenye tende husaidia kurekebisha matatizo ya tumbo na huleta ahueni kwa watu wenye matatizo ya kupata choo.

Tende husaidia kuuimarisha moyo. Iloweke tende kwenye maji kwa usiku mmoja na asubuhi kunywa maji hayo pamoja na tende zilizolewekwa baada ya kuondoa mbegu, ukifanya hivyo mara mbili kwa wiki, moyo wako utakuwa imara.

Tende husaidia pia kwenye mambo ya malavi davi. Iloweke tende kwenye maziwa ya mbuzi usiku, asubuhi changanya maziwa hayo na asali kisha kunywa, njia hii husaidia kuongeza nguvu na stamina.

Utafiti umeonyesha kuwa tende husaidia kutanua misuli ya mji wa mimba wakati mwanamke anapokaribia kujifungua, hii husaidia kumfanya mwanamke asipoteze damu nyingi wakati wa kujifungua.

Wataalamu wa vyakula, wanazichukulia tende kama chakula bora kwa wanawake wanaonyonyesha kwani husaidia kuyapa maziwa virutubisho muhimu vinavyomfanya mtoto awe na afya njema.

Tende husaidia kupunguza kiwango cha kilevi (alcohol) kwenye damu. Maji ya kunywa ambayo tende imelowekwa ndani yake husaidia kuondoa haraka alcohol mwilini.

Tende husaidia kuchelewesha dalili za uzee na pia husaidia kurekebisha ngozi na huondoa mabaka ya kuungua na jua.

Rihanna Awajia Juu Waliomuita Kibonge

$
0
0

Msanii wa muziki Rihanna amewajibu watu wanao mkejeli kwa kumuita kibonge nyanya.

Wiki iliyopita watu walisambaza picha mitandaoni zikimuonyesha mrembo huyo jinsi alivyonenepa na huku wengine wakihisi ni mjamzito na wengine wakimuandikia maneno ya kashfa..

Hata hivyo Rihanna ameamua kukata mzizi wa fitina na kuamua kuwajibu kupitia mtandao wa Instagram, kwa kupost picha ya Gucci Mane enzi zake alivyokuwa mnene na ile ya sasa hivi inayomuonyesha amepungua zaidi na kuweka picha ya mdoli akiwa analia.

AT: “Ugomvi wa Alikiba na Diamond ulianzia Oman 2010, mimi Shahidi”

$
0
0

Mwimbaji staa wa miondoko ya Mduara AT amefunguka kwenye XXL ya Clouds FM na kudai kuwa aliwahi kushuhudia ugonvi wa Alikiba na Diamond ambao kwa mujibu wake ulianzia Uarabuni naye alikuwa shahidi.

AT amesema watu wengi wanakurupuka kuhusu ugomvi wa Alikiba na Diamond kwa kuwa alikuwepo Oman mwaka 2010 ambapo Alikiba na Diamond walikuwa wanacheza Game chumbani kwake kwenye Hotel waliyofikia.

“Tulikuwa Oman kwenye Hotel moja. Tulikuwa na Show, sasa walikuwa wanacheza Game Alikiba na Diamond huku Alikiba akiwa amechagua Real Madrid na Diamond amechagua Barcelona. Alikiba akilikuwa amefungwa mbili, Diamond tatu.

“Kwa hiyo Alikiba alikuwa nataka kupiga free-kick kwenye game Diamond akamsukuma Alikiba na Alikiba akastopisha game akamwambia kuwa mwanangu nilikuwa nakutafuta muda mrefu sana ikabidi mimi ninyanyuke sasa niwaamue.” – AT

Mhe Mghwira - Mimi Sio Mpinzani wa Maendeleo..!!!

$
0
0

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, amemshukuru Rais Magufuli kwa kumteua kuwa mkuu wa mkoa huo, huku akisema kuwa yeye sio mpinzani wa maendeleo.

Bi Anna Mghwira amesema hayo wakati wa hafla ya kuapishwa iliyofanyika leo, Jumanne jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

“Ninasema hii ni heshima kwa Taifa letu, ni heshima kwa umoja wa nchi yetu, ni heshima kwa siasa za umoja wa nchi yetu, kumekuwa na minong’ono mingi sana kuwa Rais analeta nini, kuteua watu wanaitwa wapinzani, mimi sio mpinzani wa maendeleo,” amesema Mghwira.

Kakakuona Waweka Rekodi ya Mauzo Duniani..Wawazidi Tembo na Simba..!!!

$
0
0

Inakadiriwa kuwa zaidi ya kakakuona laki moja wanawindwa, kuuzwa na kuweka rekodi ya kuwa wanyama wa porini wanauzwa zaidi duniani kwa mwaka. Kwa mujibu wa Mtandao wa AFRICANIISM.

Nyama ya kakakuona inasadikika kuwa na soko zaidi  katika nchini  ya China, Vietnam na maeneo mengine ya Bara la Asia, huku ikiwa na matumizi mengine.

Hata hivyo  inasemekana kuwa nyama yake ikipikwa na kuungwa inasaidia kutibu ugonjwa wa kansa na kuongeza uwezo wa kunyonyesha kwa wakina mama.

Watafiti walionya mwaka jana kuwa ulaji wa nyama za kakakuona unatishia uhai wa wanyama hao, kwani imekua ikihitajika sana na kufanya uwindaji uongezeka.

IGP Sirro Afanya Ziara Kibiti Mkoani Pwani..Atangaza Donge la Milioni 10 kwa Atakayewafichua Waalifu..!!!

$
0
0

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro amefanya ziara katika maeneo ya Kibiti na Mkuranga kutimiza ahadi baada ya kuombwa na wazee wa maeneo hayo kufuatia mauaji ambayo yamekuwa yakiripotiwa kutokea mara kwa mara.

Mara baada ya kuzungumza na wazee hao, IGP Sirro amesema kuwa wazee hao wametoa ushirikiano mkubwa ikiwa ni pamoja na namna ya kuwapata waharifu ambao wamekuwa wakifanya mauaji katika maeneo hayo.

Sirro amewaahidi wananchi wa maeneo hayo kuwa atatoa kiasi cha shilingi milioni 10 kwa raia mwema atakayetoa taarifa sahihi kwa watu wanaofanya mauaji mkoani. Tazama hapa

Msiba wa Ivan Wamuibua Baba Yake Zari..Afunguka Haya Mazito..!!!

$
0
0

Kwa muda mrefu staa wa muziki na mjasiriamali wa Afrika Mashariki, raia wa nchini Uganda, mwenye maskani yake mengine huko Pretoria, Afrika Kusini, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, amekuwa akionekana Bongo na mama yake mzazi, Halima Hassan hivyo kuibua sintofahamu juu ya alipo baba yake, Hassan Tiale.

Hata hivyo, kifo cha mkwe wake yaani aliyekuwa mume wa mwanaye, Zari, Ivan Ssemwanga ‘Don Ivan’ aliyefariki dunia Mei 25, mwaka huu, kimemaliza utata huo baada ya kumuibua mzee huyo aliyekuwa amejaa tele kwenye msiba huo nchini Uganda. Mzee Hassan alikuwa mmoja wa watu lukuki waliohuzunishwa na kifo cha Ivan ambapo alisema kuwa, alilazimika kuacha shughuli zake ili kuhudhuria msiba huo kwa namna alivyokuwa akiivana na Ivan. “Msiba huu umenigusa sana. Nilipigiwa simu nikiwa Nairobi (Kenya) ambako nilikwenda kumuozesha kijana wangu bibi (mke).

“Nilisikia Ivan aliteleza kwa ajili ya presha, akaanguka chini, akachukuliwa, akapelekwa hospitalini Afrika Kusini, akawekwa ICU (chumba cha wagonjwa mahututi). “Niliendelea kupigiwa simu nyingi, nikaambiwa hali inazidi kuwa mbaya. Niliambiwa mshipa wa kupeleka damu kwenye ubongo ulipasuka. Hadi zilipopita saa ishirini na nne na kuendelea ndiyo niliambiwa amefariki dunia.

“ B a s i , n d i y o nikaacha shughuli z a n g u nikaja hapa (nyumbani kwa Ivan, Kampala) k w e n y e m s i b a maana alikuwa mtu mzuri sana. Hayo mengine ni manenomaneno ambayo ya nasemwa.

“Kwa kweli Ivan alikuwa mtu mzuri sana na ndiyo maana kila mtu anamzungumzia vizuri,” alikaririwa mzee huyo.

Naye dada wa Zari aliyejitambulisha kwa jina la Madina Hassan alisema kuwa, alifahamiana na Ivan alipofika nyumbani kwao kujitambulisha wakati Zari alipopata mtoto wao wa kwanza wa kiume, Pinto.

“Nilishtushwa sana na kifo chake kwa sababu alikuwa mtu aliyependa kufurahi wakati wote, hivyo ni pigo kubwa kwangu,” alisema Madina. Ivan aliyezaa watoto watatu wa kiume na Zari kabla ya kutengana alizikwa Mei 30, mwaka huu kijijini kwao, Nakalilo nchini Uganda.

Credit GlopalPublisher

Mourinho - Madrid Nipeni Morata Niwape De Gea Wenu..!!!

$
0
0

Mvutano kati ya Manchester United na Real Madrid kuhusu David De Gea umeanza upya, ambapo Madrid wanamtaka De Gea kwa nguvu zote huku United hawako tayari kumruhusu De Gea aondoke United.

Taarifa zinaeleza kuwa wiki iliyopita klabu ya Manchester United iliitolea nje ofa ya Real Madrid ya thamani ya zaidi ya £50m na kuwataka Madrid waende wakajipange zaidi.

Kufuatia kasi kubwa ya Madrid ya kumtaka mlinda mlango huyo, Meneja wa Man United, Jose Mourinho kwa kuwa wana kipa mwingine mzuri, Sergio Romero, ameamua kuwapa Real Madrid ofa ili wampate David De Gea huku akiwapa masharti.

Mourinho amewataka Real Madrid kutoa kiasi cha £22m pamoja na mchezaji Alvaro Morata ili kumruhusu De Gea ajiunge Real Madrid.

Mourinho amesema kama Real Madrid watatoa kiasi hicho cha pesa pamoja na Morata ambaye hapewi sana namba katika kikosi cha Madrid, atakuwa tayari kumuacha De Gea aondoke.

JPM Kuna Wabunge wa CHADEMA Wananiomba Vyeo Serikalini..Siwateui Ng'oo..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 7/6/2017..!!!

RC Anna Mghwira Afungukia Mazingira Yote ya Uteuzi Wake..!!

$
0
0

Kwa mara ya kwanza, mkuu mpya wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Elisha Mghwira amezungumzia na kuweka wazi mazingira yote ya utezi wake ambapo pamoja na mambo mengine, amesema kuwa, wakati akiteuliwa, hakuwa nchini hivyo hakuwa na taarifa za uteuzi wake na kwamba hakuwa hewani kimawasiliano, jambo ambalo lilimpa mshangao mkubwa.

Katika mazungumzo na Uwazi kwa njia ya simu jana jioni, Mama Mghwira ambaye alikuwa Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha ACT-Wazalendo alisema alikuwa nje ya nchi kwa kazi zake binafsi ambapo alirejea juzi (Jumapili) usiku na kukutana na habari za uteuzi huo.

Mghwira: Kwanza sikuwepo nchini wakati wa uteuzi, nimerejea jana (juzi) usiku na kukutana na habari hizo nje ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia).

Uwazi: Kwani hakukuwa na mawasiliano kwa njia ya simu kutoka mamlaka ya uteuzi?

Mghwira: Sikuwa hewani kwa muda mrefu, simu yangu iliibwa na mtu akawa anatumia namba yangu, hivyo watu wa mtandao wakaifunga, nimeirejesha leo tu na wewe ni miongoni mwa watu wa mwanzo kabisa kunipigia.

Uwazi: Kwa hiyo hujapokea taarifa rasmi kutoka mamlaka ya uteuzi?

Mghwira: Taarifa rasmi niliziona kwenye barua kupitia mitandaoni na kama nilivyokueleza, nimewasili jana usiku, sijafanya chochote na hata wao hawajui kama nipo na nawatafuta muda si mrefu kuanzia sasa.

Uwazi: Sasa utajigawaje kikazi? Mkuu wa mkoa ni serikali na wewe uko chama cha upinzani?

Mghwira: Kwani upinzani ni nini? Nadhani muhimu ni kuleta maendeleo katika jamii, lakini tutakaa na kutoa tamko rasmi la chama.

Siku Chache Toka Atumbuliwe Uwaziri..Prof Muhongo Adai Ukweli Utabaki Kuwa Ukweli Daima..!!!

$
0
0

ALIYEKUWA Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amesema kwa sasa hatazungumzia kuondolewa kwake kutoka kwenye nafasi hiyo lakini amesisitiza kuwa “ukweli utabaki kuwa ukweli”.

Katika mazungumzo yake mafupi na Raia Mwema yaliyofanyika juzi Jumatatu, Muhongo aliwataka Watanzania watulie hadi pale ukweli utakapokuja kujidhihiri na kwamba yeye hana la kusema kwa sasa.

“Ahsante sana ndugu yangu kwa kunitafuta. Huwezi kupata lolote kutoka kwangu kwa sababu sitaki malumbano ila ukweli utabaki kuwa ukweli. Mimi sitaki malumbano ya aina yoyote,” alisema Muhongo.

Katika mazungumzo hayo, msomi huyo hakutaka kufafanua kuhusu ukweli huo ambao anaamini utabaki kuwa ukweli.

Profesa Muhongo, mmoja wa wasomi wabobezi katika masuala ya miamba duniani, alijiuzulu wadhifa wake huo wiki iliyopita, baada ya Rais John Magufuli kumtaka ajitathmini baada ya kutolewa kwa ripoti ya Kamati ya Profesa Abdulkarim Mruma.

Kamati ya Mruma ilipewa kazi ya kuchunguza makinikia yaliyokuwepo  katika makontena yaliyozuiwa kusafirishwa kutoka nchini na kwenda nchi za nje kwa ajili ya kufanyiwa uchenjuaji.

Baada ya uchunguzi huo wa takribani miezi miwili, kamati hiyo ilibaini kwamba makinikia hayo yalikuwa na madini ya dhahabu ya takribani tani 15 ambazo serikali ingeweza kupata mrabaha wenye thamani ya hadi shilingi trilioni 1.4.

Matokeo ya uchunguzi huo uliohusisha makontena 277 ya makinikia ndiyo yaliosababisha Rais Magufuli kutamka hadharani kwamba Muhongo anapaswa kujitathmini kama bado anafaa kuwa waziri na ikiwezekana ajiuzulu.

Barua ya kujiuzulu

Hata hivyo, jioni ya siku hiyo, Ikulu ilitoa taarifa ya Ikulu kutengua uteuzi wa Muhongo kuwa Waziri wa Nishati na Madini; lakini baada ya taarifa hiyo – takribani saa moja baadaye, mitandao ya kijamii ilisambaziwa barua ya kujiuzulu kwa Muhongo.

Katika barua hiyo, Muhongo hakukiri makosa yoyote katika jambo hilo lakini alieleza kwamba alitekeleza wajibu wake wote kama ambavyo alielekezwa na Rais Magufuli.

“Mheshimiwa Rais, napenda kukufahamisha kwamba nimejitahidi kufanya kazi kwa uwezo wangu wote kuitumikia Wizara ya Nishati na Madini tangu uliponiteua kuwa Waziri mnamo Desemba 12, 2015. Nakushukuru sana kwa miongozo yako ya kazi ambayo imenisaidia sana katika utekelezaji wa majukumu yangu ya kazi,” ilieleza barua hiyo iliyoandikwa Mei 24, 2017.

Baadhi ya wanasheria walioiona barua hiyo kupitia mitandao ya kijamii, walitafsiri maelezo hayo ya Muhongo kama ya kutokubali kukosea lolote isipokuwa kukubaliana na mamlaka ya uteuzi iliyomtaka aachie ngazi.

Wakati huo huo, wanasheria mashuhuri nchini wamesema huu ni wakati wa kumsaidia Rais Magufuli na serikali yake katika kuhakikisha kwamba utajiri wa maliasili uliopo Tanzania unanufaisha nchi na si mataifa yaliyowekeza hapa nchini.

Wanasheria hao wameonya kwamba Tanzania imesaini mikataba ya kimataifa ambayo kama haitaangaliwa vema, huenda taifa likapata hasara kubwa badala ya faida inayotarajiwa.

Makamu Rais wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS), Godwin Ngwilimi, alisema suala alilolianzisha Magufuli la kupigania rasilimali za taifa halina vyama wala itikadi isipokuwa ni la kitaifa.

“Kwa maoni yangu, ningependekeza iundwe sasa tume ya wataalamu itakayojumuisha watu kutoka serikali ya Tanzania na kampuni za madini zilizopo nchini ili kwanza ukweli huu uwekwe wazi, baada ya hapo itakuwa rahisi kwetu kushitaki kwenye vyombo husika,” alisema Ngwilimi.

Kauli hiyo ya Ngwilimi iliungwa mkono na mmoja wa wanasheria maarufu nchini, Dk. Adelatus Kilangi, aliyesema kwamba kwa hali ilivyo sasa kwa kuzingatia mikataba ambayo Tanzania imeingia kimataifa, hatuwezi kuvunja mikataba ya madini iliyopo sasa kwa sababu ya ripoti ya Mruma.

“Hatuwezi kuivunja. Tumesaini mkataba wa MIGA na wa ICSID. Tutashtakiwa kwa kuvunja Customary Law Principle ya 'Fair and Equitable Treatment', na 'State Responsibility' na ya 'Respect for Acquired Rights'. Tutapelekwa mbele ya ICSID na kuhukumiwa, kisha tutaminywa na MIGA itakayokamata mali zetu popote zilipo.

“Kuwashtaki makampuni kwa kutudanganya? Tunaweza, na tutatumia hoja kuwa wamevunja Customary Law Principle ya 'Good Faith and Prohibition of Abuse of Rights'. Lakini wakisema uchunguzi wa mchanga tumeufanya kwa upande mmoja wanaweza kushinda. Ndiyo maana ni muhimu tufanye uchunguzi wa pamoja,” alisema Kilangi.

Katika andishi lake aliloliandika kwa jumuiya ya wanafunzi waliowahi kusoma katika Shule ya Sekondari ya Sengerema na ambalo baadaye lilisambazwa katika makundi mbalimbali ya WhatsApp hapa nchini, Kilagi alieleza kwa kina kuhusu changamoto za kisheria, kodi na utawala zilivyochangia nchi kufika ilipo sasa.

Kwa mfano, alisema ni wazi kuwa wakati nchi ikiingia kusaini baadhi ya mikataba ya rasilimali, taifa lilikuwa limetekwa na vikundi maslahi ambavyo vilikuwa vikifikiri kwa niaba ya serikali.

“Kuna tatizo kubwa sana linalozikumba hasa nchi za Afrika na baadhi ya zinazoendelea zilizo nje ya Afrika. Hili ni tatizo la 'state capture' (nchi kutekwa na vikundi maslahi). Kama ilivyo concept ya 'river capture' kwenye somo la jiografia, basi state capture linamaanisha ushawishi unaofanywa na watu wa kada ya juu, wafanyabiashara au wawekezaji kiasi kwamba serikali inashindwa kufikiri na kuachia kundi hilo kufikiri kwa niaba yake.

 “Wakati wa kufuata falsafa ya soko huria katika rasilimali, Tanzania iliingia kwenye utekwaji huu. Ndio kusema tuliondoa kichwa chetu tukaweka kichwa kingine. Tukawa tunafikiri kwa mfumo wa hicho kichwa kingine. Sasa tumeanza kurudisha kichwa chetu,” alisema.

Tanzania ilivyobanwa

Katika andishi lake hilo refu, Dk. Kilangi alieleza namna Tanzania ilivyozidiwa akili katika hatua za mwanzo za kuingia katika mikataba ya nishati na madini.

Kwa mfano, alitoa mfano wa madini ambapo wawekezaji walikataa kuweka sheria inayoruhusu nchi inayoibiwa utajiri wake kuomba kupitiwa upya kwa mikataba endapo kutakuwa na udanganyifu.

“Ili uweze kufanya mapitio ya mikataba, ni lazima kwenye mikataba tuliyoingia tuwe na kipengele kinachohusiana na doctrine ya 'clausula rebus sic stantibus. Hiki ni kipengele  kinachoruhusu kupitia upya mikataba kama mambo fulani yakibadilika.

“Lazima kifungu hiki kiwe kwenye mikataba. Hawa jamaa (wenye kampuni za madini) walihakikisha hakimo kwenye mikataba yetu. Kwa hiyo, ukianza mchakato wa kupitia mikataba mwenyewe bila ya kuwashirikisha wao watasema umevunja kanuni ya 'fair and equitable treatment'. Hivi ndivyo ilivyo,” aliandika mwanasheria huyo.

Kwa mujibu wa msomi huyo, tatizo hilo la kwenye madini lipo pia kwenye sekta ya nishati, ambapo wenye kampuni huwa tayari kuidanganya nchi kwa misaada wanayojua inahitajika sana; ikiwamo misaada ya wataalamu, lakini kumbe wanatengenezea sheria itakayowezesha kutuibia.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo (LEAT), Dk. Rugemeleza Nshala, alisema Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 na mabadiliko yaliyofanyika mwaka 2015 ilitengenezwa kwa kufuata matakwa ya Benki ya Dunia (WB) na kampuni za madini zilizopo nchini.

Alisema kuna haja ya kufanya mapitio ya mikataba yote ambayo serikali iliingia na wawekezaji katika eneo la rasilimali kwa vile ilipitishwa na watendaji waliokuwa hawajui thamani ya madini hayo.

Nshala alishauri upitiaji wa sheria hii ujumuishe taasisi na wadau wote wa ndani ya nchi na iandikwe na Watanzania wenyewe na serikali ikatae msaada wa uandikaji wa muswada wa sheria hiyo kutoka Benki ya Dunia au mataifa yaliyoendelea kwa kuwa ajenda yao ni kuwa kampuni za nje ndizo zenye haki ya kuchimba na kunufaika na madini ya nchi husika.

“Uchimbaji na uchenjuaji wa Tanzanite pamoja na utengenezaji wa bidhaa za mwisho za madini hayo lazima ufanyike Tanzania. Kampuni kama Tiffany ziambiwe kuwa ni lazima waanzishe viwanda vya utengenezaji vito na mapambo yatokanayo na Tanzanite nchini. Hivyo nchi yetu ndiyo iwe duka la bidhaa za Tanzanite na si Marekani kama ilivyo sasa,” aliongeza.

LEAT ni mojawapo ya asasi za kiraia za kwanza kabisa nchini kupinga ubinafsishaji wa migodi ya madini uliofanywa na Serikali ya Awamu ya Tatu na Nshala pamoja na aliyekuwa mwenzake katika taasisi hiyo, Tundu Lissu (sasa mbunge), waliwahi kufunguliwa mashitaka na serikali kwa sababu ya upinzani wao kwa sera hizo.

Kuhusu MIGA na ICSID

MIGA ni taasisi iliyo chini ya WB ambayo wawekezaji kutoka nchi zilizoendelea huweka bima kwa miradi yao ya uwekezaji wanayoifanya katika nchi masikini. Taasisi hii ilianzishwa mwaka 1965.

Endapo nchi inayoendelea kama Tanzania itavunja mkataba wake na kampuni hiyo, kampuni hiyo hupeleka kesi yake katika Mahakama ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kiwekezaji (ICSID) na kama itashinda MIGA italipa fedha ambazo kampuni hiyo itadai kupoteza kutokana na uvunjwaji huo wa mkataba.

MIGA ikishalipa, kazi yake itakuwa ni kufuatilia kuona nchi husika inalipa fedha hizo na taasisi hiyo ina uwezo wa kukamata hata mali za nchi husika ilimradi nayo ilisaini mkataba wa kukubali MIGA.
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images