Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Kimenukaa..Mtoto wa Nyerere Aibuka na Kuinyooshea Kidole Serikali ya Magufuli..!!!

$
0
0

KAIMU Mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali  la Global Resource Alliance, Madaraka Nyerere, ameiomba serikali kupunguza kodi  katika bidhaa zinazotengeneza  nishati  ya jua.

Alisema hatua hiyo itawawezesha wananchi    vijijini kupata nishati hiyo na hivyo kupungu za matumizi ya kuni na mkaa inayochangia kuharibu misitu.


Alikuw akizungumza hivi karibuni   katika wiki ya maadhimisho  ya mazingira iliyofanyika kitaifa  wilayani hapa.

Madaraka  alisema shirika lake kwa kushirikiana na Kampuni ya GoSol Ltd kutoka    Finland  limebuni jiko la kutumia mionzi ya jua.

Alisema  jiko  hilo   litakuwa   ukombozi kwa wajasiriamali wadogo vijijini ambao  hawana uwezo  wa kumudu gharama za umeme, mafuta na gesi.

Akifafanua  faida ya jiko  hilo  linalotumia  vioo  vya  kawaida kukusanya  mionzi  ya jua, Meneja  Mradi  wa GoSol  kutoka Finland, Heikki  Lindfors, alisema  jiko hilo  ni ukombozi  kwa wakazi wa vijijini  zaidi ya bilioni tatu duniani.

Alisema jiko hilo  linaweza  kuokoa zaidi ya tani tisa ya miti  inayokatwa kwa mwaka duniani.

“Teknolojia  hii  tumekwisha kuieneza  katika  nchi mbalimbali duniani kama vile Nigeria, India na Kenya.

“Tanzania tumeanzia  hapa  Musoma mkoani Mara…  teknolojia  hii  itawasaidia vikundi vya  kina mama  ambao wana kazi kubwa  za uhitaji  wa nishati ya jua,” alisema Lindfors.

Alisema  jiko  hilo  lina  uwezo wa  kupika  vyakula  mbalimbali     na kukausha   karanga, kubani   kanyama,  kukausha ndizi  na kupata unga, kukausha    mihogo  na mitama na   lina   uwezo wa  kuoka   unga  wa mikate  wenye uzito  wa kilo 10.

Monica Macha, mjasiriamali  kutoka kikundi cha Alpha Alliance cha Musoma kilichoanza kutumia  teknolojia hiyo, alisema   kabla  ya kutumia jiko hilo walikuwa  wanatumia debe moja la mkaa kwa siku katika kuoka mkate au chapati jambo  ambalo kwa sasa ni ndoto kwao.

LISSU: Magufuli Akiniteua Sitokubali, Siwezi Kutumikia Utawala wa Katiba ya Kidikteta...!!!

$
0
0

Leo akiongea kutokea mahakamani na waandishi wa habari, Mwanasheria mkongwe na kada wa Chadema, Tundu lissu amesema kamwe hawezi kukubali kuteuliwa katika utawala wa kidikteta.

Amesema pia kwamba hawezi kuwa katika sehemu ambayo katiba ya nchi inakandamizwa na akiniteua ni mpaka abadilishe katiba ya nchi kwanza,

Ameongeza kwa kusema kwamba mghirwa ni CCM na sasa wanarudi walipotokea baada ya kuona mambo magumu kwao.

ACT wanateuliwa kwa sababu wao pia walikuwa ni CCM na sasa wanarejea walipokuwepo mwanzoni.

Tundu Lissu: ACT Waliazishwa Kuuwa Upinzani, Sasa Wanazawadiwa..!!!

$
0
0

Akijibu swali na mwandishi wa habari juu ya maoni yake kwa uteuzi wa Magufuli kwa wapinzani 

Lissu amesema ACT sio wapinzani, bali walianzishwa kkwa ajili ya kuuwa upinzani na sasa 
wanazawadiwa, Kitila Mkumbo na Anna Mghwira ni zawadi

Amedai serikali hawajawi kuwa na shida na ACT bali shida yake kubwa ni Chadema na CUF na hao wengine ni CCM wakiwa wamevaa magwanda tofauti

Kimenukaa..Zile Sauti za Kimahaba Mtandaoni za Wema na Mbowe..Kumbe Mchezo Mzima Hivi Ndivyo Ilivyokuwa A- Z..!!!

$
0
0

Siku chache baada ya kusambaa kwa sauti katika mitandao ya kijamii, ikiwemo WhatApp na Facebook, inayodaiwa kutengenezwa kwa lengo la kumchafua Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe na mrembo wa Tanzania mwaka 2006, Wema Sepetu, hatimaye ‘dude’ limeamka na sasa kimenuka.

HAPA NDIPO ILIPOANZIA

Mwishoni mwa wiki iliyopita, sauti iliyorekodiwa kama ya watu wanaoongea kwenye simu, zilianza kusambaa kwa kasi mitandaoni, ambazo kwa kuzisikia harakaharaka, zilionekana kufanana na watu hao wawili, zikisikika kama za watu waliokuwa katika uhusiano.

Wakati sauti hizo zinasambaa, muda mchache baadaye, majibizano ya meseji kwenye simu yakaanza kusambaa pia, ambayo nayo yanahisiwa kuwa yalitengenezwa, yakiwahusisha viongozi wawili wa ngazi za juu katika Mikoa ya Arusha na Dar es Salaam, wakipongezana kwa kukamilika vizuri kwa kazi hiyo (ya kutenegeneza na kusambaza sauti). Katika majibizano hayo ya meseji za simu, ‘viongozi’ hao wawili walimsifu mtu waliyemwita Steve (anadhaniwa kuwa Steve Nyerere) kwa kuifanya kazi hiyo vizuri (ya kuigiza sauti ya kiongozi huyo).

RISASI LAWASAKA WAHUSIKA

Ili kupata mkanda kamili wa ishu hiyo, Risasi Mchanganyiko liliingia mtaani na kuifanyia kazi ili liweze kuwapa wasomaji wake kitu cha kueleweka. Freeman Alkael Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema Taifa, hakupokea simu aliyopigiwa, lakini wakati Risasi Mchanganyiko likienda mitamboni, alisikika kupitia kituo kimoja cha redio jijini Arusha, akiikana sauti hiyo na kusisitiza kuwa hajawahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na muigizaji huyo na kwamba kinachofanyika ni siasa chafu, kitu ambacho kitashughulikiwa na chama.

Wema Sepetu naye simu yake iliita bila kupokelewa na hata baada ya kutumiwa ujumbe mfupi, hakujibu licha ya kuonekana kuwa umepokelewa na kusomwa.

HUYU HAPA MLEZI WA WEMA CHADEMA

Hata hivyo, Risasi Mchanganyiko lilifanikiwa kumpata mtu aliyepewa jukumu la kumlea Wema ndani ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniphace Jacob ambaye pia ni Meya wa Ubungo jijini Dar es Salaam na hapa anafunguka kuhusu ishu hiyo; “Tumeshaongea na wanasheria juu ya hatua kali za kisheria, kuwachukulia hatua

wote wanaoigiza sauti za viongozi wetu na kuzitumia vibaya kwa nia ya kuwadhalilisha na kuwashushia heshima, pamoja na kutoa taarifa kwenye vyombo vya dola juu ya uchunguzi ufanyike kubaini sehemu na watu wanaofanya “voice studio” kwa lengo ovu.

“Pili tumemtia moyo kamanda wetu Wema kuwa asihofu na siasa za majitaka na kwamba yote yanafanyika na wapinzani wetu, kwa sababu wanamuhofia na kumuogopa

juu ya namna anavyofanya mikakati ya kufuta

“UTUMWA WA WASANII KWA CCM”

kazi ambayo ameifanya na mpaka sasa ameandaa ujio wa wasanii wakubwa 20 ndiyo maana wanataka kumuondoa nje ya agenda yake.”

STEVE NYERERE NAYE AFUNGUKA

Steve Nyerere ambaye kwa mujibu wa meseji zilizoenezwa mtandaoni alionekana kama ndiye aliyeshughulika kutengeneza sauti hiyo ya kiume, aliruka kimanga kuhusika na suala hilo, aliloliita la kijinga na kipumbavu. “Mimi sihusiki, sikutengeneza ile sauti kwa vile sina sababu ya kufanya hivyo,

hicho ndicho ninachoweza kukuambia ila kwa nyongeza tu, niwatake Watanzania waachane na kufuatilia mambo ya kijinga na kipumbavu, tuna vitu vingi sana vya kufanya badala ya kukuza vitu kama hivi.”

SASHA NAYE AZUNGUMZIA ‘SAUTI YAKE’

Sasha, msanii ambaye hutumika kama video queen kwenye nyimbo mbalimbali za Bongo Fleva, ambaye

amefanana sauti kwa kiasi kikubwa na Wema Sepetu, anahusishwa kutumika kutengeneza sauti ya kumuigiza malkia huyo wa filamu Bongo. “Nimetumika kuiga sauti ya Wema? Hapana, sijawahi kupigiwa simu na mtu yeyote na wala sijafanya kitu kama hicho, nikuambie ukweli kuwa hili jambo ndiyo kwanza wewe unaniambia, sijui kabisa,” alisema msanii huyo.

TUNDU LISU ABEZA

Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lisu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, alipotakiwa kulizungumzia suala hilo, alisema ni propaganda dhaifu, zilizolenga kumchafua mwenyekiti wao, ambayo imeshindwa. “Lengo lao lilikuwa ni kumchafua mwenyekiti wetu, lakini hawajaweza kwa sababu hawezi kuchafuka kwa staili hii. Tunajua hili jambo hata tukilipeleka polisi ni kama kujisumbua tu, hawana historia ya kushughulikia shida za wapinzani.”

HAWA HAPA POLISI MAKOSA YA MTANDAO.

Risasi Mchanganyiko lilimpata mmoja wa maofisa wa kitengo cha makosa ya mtandao, ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Fadhil, akisema yeye siyo msemaji wa suala hilo. “Ila ninachoweza kukusaidia kwa hili ni kwamba Cyber Crime haifanyi kazi pasipo kupokea malalamiko. Hao ambao sauti zao unasema zimeigwa, wanatakiwa waje kulalamika hapa na hapo ndipo polisi watakapoanza kufuatilia suala hilo. “Lakini kama wenyewe watakaa kimya bila kulalamika, basi suala hilo litaishia kama lilivyo, endapo watakuja suala hilo litafanyiwa kazi mara moja,” alisema.

Breakning News ..ACT Wazalendo Wamvua Uenyekiti Mama Anna Mgwhira..Wadai Hawajashirikishwa Uteuzi Wake wa Ukuu wa Mkoa..!!!

$
0
0

Kamati kuu ya uongozi imekaa Imezingatia haya

=>Hatuna kipangamizi Rais kumteua yeyote

=> ACT Wazalendo ni chama cha siasa cha kutumikia wananchi

=> Rais kavunja mwiko kwa kuanza kuteua wapinzani

=>Huu ni uthibitisho kwamba ACT ina viongozi bora hivyo inaweza kuongoza nchi.

=>Bado tunao wazalendo wa kutosha, hivyo raia asisite kuchagua wengine 
=>CCM wajifunze kupitia kwetu kuchagua viongozi bora

=>Kamati ya uongozi inamshauri Rais kuweka mfumo bora wa kuazima watu kutoka vyama vingine kwa kuweka mashauliano ili kuepuka migongano ndani ya vyama.Japo anao uwezo, hii ni kuimarisha umoja wa kitaifa

=> Kuteua bila mashauriano kunaleta wasiwasi miongoni mwao

=>ACT inampongeza Anna Mghwira kwa kuteuliwa

=> ACT imeona kutakuwa na mgongano kati ya nafasi yake na chama

=> Katiba ya ACT Wazalendo, Mama Anna Mgwhira amekoma kuwa mwenyekiti.

=> Kuteuliwa kwake kuwa Mkuu wa Mkoa hawezi fanya kazi kwa ufanisi kwa ACT- wazalendo.

=>ACT inamshukuru kwa kufanya kazi kwa uzalendo na ACT Wazalendo imemteua ndugu Yeremia Maganja kuwa Makamu Mwenyekiti mpya

Maswali

1. Je, hamjashauriana katika uteuzi huu?

=> Kama tulivyoeleza mwanzo, Rais alimteua mama wakati yupo nje ya nchi na sisi tulipata taarifa na tukamtafuta kwa mashauriano. Tumetoa tamko baada ya kushauriana na Mama Mghwira

2. Mama bado ni Mwanachama halali wa ACT Wazalendo, Kupewa ilani ya CCM mnaichukuliaje?

=> Rais na vitengo vyake vyote vimejilidhisha kwamba ACT ina viongozi waadilifu, huu ni ujumbe kwa watanzania kwamba ACT-Wazalendo ipo tayari kupewa nchi. Na watanzania wenyewe wameona 

=>Ni mujimu haya mambo yakaeleweka, tunapofanya uchaguzi, wananchi wanasoma na kuchagua ilani ambayo wanaona inafaa. Kwa hivi sasa chama kinachoongoza ni CCM na ilani inayotekelezwa ni ya CCM. Mwaka 2015 Mama Anna pia alimpa ilani ya ACT Wazalendo na tunaamini kuna mambo mazuri ya Ilani ya ACT

=>ACT tungeshinda tungeunda serikali ya umoja wa kitaifa, hivyo hiki kinachofanywa ni moja ya Malengo tuliyokuwa nayo.ACT tungechagua watu kutoka vyama vyote

Baada ya Kufungiwa Kuhudhuria Vikao vya Bunge..Ester Bulaya Atoa Salamu Hizi kwa CCM na Spika Ndugai..!!!

$
0
0

Mbunge wa Bunda Mjini Mh. Ester Bulaya ametoa salamu kwa Wabunge wa CCM pamoja na Spika Job Ndugai kutambua kwamba hata baada ya kumuadhibu kutohudhuria vikao bya bunge siyo silaha ya kuwafunga midomo.

Bulaya amefunguka hayo akiwa Mkoani Kilimanjaro na kusema kwamba uamuzi uliofanya na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Wabunge CCM pamoja na Spika wa bunge haujawatendea haki wananchi wao kwa sababu ni kwa muda mrefu watakosa wawakilishi bungeni ingawa siyo mwisho kwa wao kupigania haki na kuwatumikia wananchi kwa njia zingine.

"Wamekosea sana kwa sababu wananyima wananchi wetu haki ya kupata wawakilishi wa matatizo yao bungeni. Ingawa tayari tumekwishaweza kujipanga namna ya kwenda kuwatumikia na kupeleka maendeleo kwa katika kipindi hichi ambacho tutakuwa nje ya bunge. Lakini niweke wazi adhabu hii kutolewa siyo silaha ya kutuifanya kuacha kupigania demokrasia na haki. Bulaya alifunguka. 

Aidha Bulaya ametupa lawama kwa Mh. Ndugai na kudai kuwa ni kiongozi asiyeweza kuzuia hasira ndio maana amekuwa na maamuzi ya kuhukumu haraka wakati yeye ni baba anayepaswa kuwa na subira na uvumilivu wa kuongoza.

Mbunge  Bunda Mjini, Mh. Esther Bulaya pamoja na Halima Mdeewa Kawe wamesimamishwa kuhudhuria vikao vyote vya Bunge vinavyoendelea mpaka mkutano ujao wa Bunge la Bajeti la mwaka  2018/19 kwa kile kinachodaiwa kuonyesha utomvu wa nidhamu ndani ya bunge.

Mwanasheria Mkuu wa TBS Kizimbani...!!!

$
0
0

Mwanasheria Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Baptister Marco (54) amepandishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka matatu ya kuishi na kufanya kazi nchini bila kuwa na  kibali.

Mwendesha Mashtaka wa Uhamiaji, Novatus Mlay alimemsomea mashtaka hayo leo Jumatano kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa.

Akisoma hati ya mashtaka,  Mlay alidai kuwa  Mei 19, 2017  huko Kinondoni katika ofisi ya uhamiaji,  Marco akiwa raia wa Burundi alikutwa nchini bila kuwa na kibali cha kumuwezesha kuishi.

Marco katika shtaka la pili amedaiwa kuwa siku hiyo alikutwa akifanya kazi kama Mwanasheria Mkuu wa TBS bila ya kuwa na kibali kinachomruhusu kufanya kazi hapa nchini.

Katika shtaka la tatu, Mlay alidai kuwa, Julai 6 mwaka 2011 katika ofisi ya Uhamiaji ya Dar es Salaam iliyopo Wilaya ya Ilala, mshtakiwa huyo akiwa raia wa Burundi alitoa taarifa za uongo kuhusu maelezo yake binafsi wakati akijaza fomu ya kuomba hati ya kusafiria namba CT (5)(Ai).

Wakili Mlay alisema kitendo hicho cha kutoa taarifa za uongo kilimuwezesha Marco kupata hati ya kusafiria ya Tanzania yenye namba AB 474856 huku akijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria za nchi.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, alikana na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Mshtakiwa alitakiwa kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika ambao kila mmoja atasaini bondi ya Sh 20 milioni na alikamilisha. Kesi imeahirishwa hadi Juni 21, 2017 kwa ajili ya kutajwa.

Kumekucha: Washereheshaji(MCs) na Wapiga Picha Kuanza Kutozwa Kodi..!!!

$
0
0

Wabunge wataka Washehereshaji(MCs) na Wapiga picha waanze kutozwa kodi ili Serikali iweze kukusanya mapato ya kutosha.

Wakati huo huo, Mbunge wa Iramba Mashariki (CCM), Allan Kiula amesema maeneo mapya ambayo yanaweza kuanzishiwa kodi kuwa ni pamoja na Ushauri Elekezi (Consultancy Agencies) sambamba na kuimarishwa kwa ukusanyaji wa kodi ya zuio ya asilimia 10 kutoka kwa wamiliki na wapangaji wa nyumba na makazi.

Msajili wa Vyama Azungumzia Sakata la Maalim Seif Kufungua Ofisi Mpya za CUF..!!!!

$
0
0
Kutokana na Chama cha Wananchi (CUF) kufungua ofisi mpya za chama hicho katika eneo la Mtaa wa Idrisa Kata ya Mzimuni, Magomeni wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Msajili wa Vyama vya Siasa amesema anaamini chama hicho kinafanya mambo yake kwa kuzingatia sheria.

Jana  Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, alisema hajapata taarifa yoyote ya chama hicho, kufungua ofisi mpya zaidi ya kuona katika vyombo vya habari.


“Ukiondoa taarifa za kwenye media sijapata taarifa yoyote kutoka CUF labda wawe wameleta leo (jana), lakini naamini chochote wanachofanya wanaelewa taratibu wataleta taarifa, “ alisema Jaji Mutungi.

Jaji Mutungi alisema sheria inawataka wanapofungua ofisi watoe taarifa ndani ya siku 14, ambazo hazijaisha hivyo anaamini wanajua hilo. 

Upande wa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad wamefungua ofisi hizo, baada ya tukio la kuvamiwa katika Ofisi Kuu za Buguruni na kundi la Profesa Ibrahim Lipumba.

Jaji Mutungi alisema atakapopokea taarifa rasmi ataangalia kama taratibu zilifuatwa kwani ufunguaji wa ofisi mpya una taratibu zake. 

“Nikiletewa taarifa ndio nitajua kama walifata taratibu au la, ufunguaji wa ofisi una taratibu zake najua wanazijua pia, “ alisema Jaji Mutungi.

Alisema taarifa hiyo ataipata kutoka kwa mwenyekiti au msemaji wa chama, ambaye ni katibu mkuu ambao wanatambuliwa na ofisi ya msajili wa vyama vya siasa. 

Akizindua ofisi hiyo Juni 4 mwaka huu, Maalim Seif alisema ofisi hiyo imetolewa na wabunge 40 wa CUF.

Alisema uamuzi wa wabunge hao kumpatia ofisi ya kufanyia kazi hapo ni kitendo cha kiungwana na kiungwe mkono na wanachama wote. 

Alisema kwa miezi 10 sasa, wamekuwa wakishindwa kufanya kazi kwa upande wa Tanzania Bara, jambo ambalo limewaathiri hivyo kupatiwa ofisi kutamsaidia kutimiza majukumu bila hofu yoyote.

Katibu huyo alisema ana imani na mahakama kuwa itawapatia haki stahiki hivyo kuwataka wanachama kuendelea kuwa na subira.

Msajili wa Vyama Azungumzia Sakata la Maalim Seif Kufungua Ofisi Mpya za CUF..!!!!

$
0
0

June 6, 2017 Katibu wa Itifaki na Uenezi na Mawasiliano ya Ummma wa ACT Wazaledo Ado Shaibu ametoa taarifa iliyosema kuwa Kamati ya uongozi ya chama hicho itakutana June 7, 2016 kutafakari namna ambavyo Anna Mghwira atatekeleza wajibu wake wa Uenyekiti wa chama na majukumu mapya. Basi ilipofika leo Majira ya Saa tisa alasir chama hicho kupitia Kaimu Kiongozi mkuu SamsoN Mwigamba wametamka kuwa Anna Mghwira hataweza tena kuendelea Mwenyekiti wa chama hicho

Serikali: Tutaendelea Kununua VX V8 kwa Viongozi wa Serikali Magari Mengine Hayafai na Hayana Ubora..!!!!

$
0
0

Serikali imesema matumizi ya magari aina ya Toyota Land Cruiser VX kwa viongozi wake wa ngazi mbalimbali kwa Tanzania Bara yataendelea na haina mpango wa kutumia Toyota Prado kwa sasa kama ilivyo kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Msimamo huo umewekwa wazi leo bungeni mjini Dodoma na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, wakati akijibu swali la mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa aliyehoji ni kwanini serikali isitumie Prado badala ya VX ili kuokoa fedha kutokana na gharama za ununuzi na matengenezo kwa VX kuwa juu kuliko Prado.

Kwa mujibu wa Mwambalaswa, gari moja aina ya VX inanunuliwa kwa zaidi ya shilingi milioni 220, wakati Prado inanunuliwa kwa shilingi milioni 120 na endapo serikali itanunua magari 200 ya Prado badala ya VX itaweza kuokoa shilingi bilioni 2 ambazo zinaweza kutatua kero ya maji katika jimbo lake la Lupa.

Kigoma: Uteuzi wa Mgwhira Wafanya Baadhi ya Viongozi wa ACT Wajiunge na CHADEMA..!!!

$
0
0

Pichani ni Viongozi wa Chadema Mkoa wa Kigoma wakiwapokea Viongozi na wanachama wa ACT wazalendo walioamua kujitoa katika chama chao baada ya kuchukizwa na kitendo cha Mwenyekiti wao wa Taifa na viongozi wao wa Kitaifa kukubali uteuzi wa Mkiti wao kuwa Mkuu wa Mkoa na kutekeleza ilani ya CCM. 

Wamesema kitendo hicho ni kukisaliti chama, miongoni mwa wanachama hao kuna wengine wemeamua kuachana kabisa na siasa.

Mgambo wa Pili Apigwa Risasi Kisogoni Akivuna Ufuta Rufiji..!!!

$
0
0

Askari Mgambo, Nurdin Kisinga (33) Mkazi wa Kijiji cha Umwe Kaskazini Ikwiriri, wilayani Rufiji mkoani Pwani amelazwa katika Hospital ya Mchukwi baada ya kupigwa risasi ya kisongoni.

Huyu ni mgambo pili kipigwa risasi ndani ya siku mbili baada ya Erick Mwarabu kuuawa juzi saa tisa usiku akiwa uvunguni mwa kitanda chake.

Tukio la leo Jumatano limetokea katika eneo la Ngomboloni lililopo katika Kijiji cha Umwe Kaskazini ikiwa ni takribani saa 19 tangu Mkuu wa Jeshi la Polisi(IGP), Simon Sirro kufanya mkutano wa mazungumzo na wazee wa wilaya za Kibiti na Rufiji ili kukomesha mauaji katika wilaya hizo.

Akielezea jinsi tukio hilo lilivyotokea, kaka wa majeruhi aliyejitambulisha kwa jina la Kisinga Athumani Kisinga akiwa katika Hospitali ya Mchukwi alisema ndugu yake alipigwa risasi akiwa shambani kwake.

Alisema Nurdin alikuwa akivuna ufuta wake shambani kwake ndipo watu ambao hawajajulikana idadi yao walimpiga risasi moja ya kisogoni na kutokomea kusikojulikana.

Kisinga alisema Nurdin alikuwa ameambatana na vijana wawili ambao ni watoto wake kuvuna ufuta huo.

Alisema mara baada ya kuanguka chini wadogo zake waliomba msaada kwa kupiga yowe na ndipo mtu mmoja alifika eneo la tukio na kumchukua kwa baiskeli hadi barabarani.

Alisema mara baada ya kufika barabarani alifanikiwa kubebwa kwa pikipiki hadi kituo cha Polisi Ikwiriri.

Alifafanua kuwa baada ya hapo alikimbizwa katika kitio cha Afya Ikwiriri ambapo alipatia huduma ya kwanza kituoni hapo na baadaye alipelekwa Mchukwi kwa matibabu zaidi.

Mganga wa zamu katika hospitali hiyo Emmanuel Humbi alisema wanampeleka kwenye chumba cha X Ray kwa ajili ya uchunguzi.

Ongeza Hips, Makalio, Mapaja, Miguu, Uume na Nguvu za Kiume na Products za Markson Beauty

$
0
0

ONGEZA HIPS, MAKALIO, MAPAJA, MIGUU, UUME NA NGUVU ZA KIUME. PIA KUPUNGUZA UNENE, KUWA MWEUPE BILA SUGU NA KUONDOA MADOA.
@Markson_beauty_pr Tunakuletea bidhaa bora zenye matokeo ya uhakika na haraka zisizo na kemikali wala madhara. Zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kudhibitishwa kiafya.
🍉🌿🍅🍍🍒🍉🍓🍅🍒
NB÷ Matokeo ni uhakika na garantii. Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
BIDHAA ZETU:-

1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @120,000/=
2. Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa:-
(a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200,000/=
(b)Vidonge @180,000/=
(c)BOTCHO 10× ya kupaka @ 150,000/=
3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:-
(1)Mafuta @120,000/=
(11)Vidonge @150,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-
(a) Gely ya kupaka @130,000/=
(b) Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu hata kwa wenye kisukari @130,000/=
(C)Handsome up original @200,000/=
6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @120,000/=
7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula @120,000/=
8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a) Dawa ya kunywa au kupaka @120,000/=
(b) Mkanda wa kawaida @100,000/=
(c) micro-computer belt wa umeme @170,000/=
9 .Kupunguza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120,000/=
10.Kushepu miguu (CHUPA YA BIA) na kuondoa vigimbi @120,000/=
11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @120,000/=
12.Kurudisha usichana (bikra) @120,000/=
Wasiliana nasi :- (+255)
0767447444au 0714335378
👉🏻Ili kuona bidhaa zaidi na shuhuda za waliotumia bidhaa zetu. ...............
Follow us on instagram @Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr

Fahamu Faida ya Kutoa Kile Kilicho Kizuri Zaidi kwa Wengine ..!!!

$
0
0

Siku zote katika maisha yako kabla hujatenda kitu chochote, kabla hujasema kitu chochote, jiulize kitu unachotaka kutenda au kitu unachotaka kusema je, kitaleta matokeo chanya kwako au hata kwa wengine?

Sio kwa sababu unayo nafasi nzuri ya kutenda au kusema hiyo ikawa na maana kwako ufanye au useme tu hata mambo yanayoumiza wengine. Unatakiwa kuwa makini na kuzingatia ni nini matokea ya kile ambacho unakwenda kutenda au kukizungumza. Kwani kila wakati tunakumbushwa ya kwamba ni heri kufikiri kabla ya kutenda.

Nisisitiza suala la kufikiri kabla ya kutenda kwa sababu wengi wetu hukurupuka katika kutenda mambo fulani, na kufanya hivyo kumekuwa chanzo cha kutotimiza jambo hilo. Hivyo kwa jambo lolote kabla ya kulitenda au kulisema ni heri kulitakari mara dufu zaidi.

Pia kufikiri kabla ya kutenda ni muhimu kwa sababu ni dhahiri wapo watu ambao moja kwa moja utawaumiza, kama utatenda au kusema maneno  hasi, hata kama hujui jinsi unavyowaumiza. Pia uelewe wapo watu utakaowaponya kama utaamua kusema au kutenda matendo chanya ambayo yana msaada mkubwa katika maisha yao kwa ujumla.

Kila wakati, unayo nafasi nzuri sana ya kutoa mazuri katika dunia, ingawa uamuzi ni wako. Acha kutenda au kusema mara moja kile kinachokujia kichwani mwako, Jipe muda wa kukifikiri kitu hicho na kujua ni nini matokeo yake katika maisha yako na ya wengine.

Kuanzia leo jifunze kutoa yale mazuri katika hii dunia jenga utamaduni wa kutoa yale matendo au maneno mazuri iwe sehemu ya utamaduni wako. Ukifanya hivyo dunia itakupa mazuri pia na utafurahia  maisha yako kutokana na mazuri unayoyatoa.

Simama imara katika kuhakikisha  unalitenda hili vyema kila wakati. Simamia katika ukweli, ili kutengeneza amani ya moyo wako na mioyo ya watu wengine. Usiwe kichocheo katika kusababisha watu wengine wakose furaha, bali jitahidi kuwa katika kusimamia ukweli na haki daima. 

Kumbuka sana TOA YALE MAZURI KATIKA MAISHA YAKO,  GIVE GOODNESS TO LIFE, ukifanikisha hili furaha na mafanikio vitakuwa upande wako.

Mwisho tuweke nukta kwa kusema ya kwamba wewe ni matokeo ya mafanikio ya watu wengine kama utaamua kuwa mkweli kwa kutakari kabla ya kusema na kutenda utafanya vichocheo vya mafanikio kwa watu wengine.

Imeandaliwa na mtandao wa dira ya mafanikio,
Imani Ngwangwalu & Benson Chonya,

Utafiti ..Bodaboda na Baiskeli Zinaathiri Nguvu za Kiume..!!!!

$
0
0

Kazi ya kuendesha baiskeli za kubeba abiria pamoja na baiskeli zinazopatikana kwenye vituo vya mazoezi (gym) vimebainika kuwa chanzo cha kupunguza uwezo wa wanaume wanaposhiriki tendo la ndoa.

Hayo yamebainika kupitia utafiti uliofanywa hivi karibuni na jopo la wataalam wa afya ya uzazi likiongozwa na mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Jomo Kenyatta, Wamalwa nchini Kenya.

Matokeo ya utafiti huo uliowahusisha waendesha baiskeli (bodaboda) 115 wenye umri kati ya miaka 18 na 40, katika eneo la Bungoma, Mashariki mwa Kenya, ulibaini kuwa asilimia 35.9 walikuwa na matatizo ya uwezo mdogo wa kushiriki tendo la ndoa ipasavyo, kwakuwa wameathiriwa misuli ya uume.

Vijana hao walipimwa na wataalam wa Afya kutoka Hospitali ya Taifa ya Kenyatta wakishirikiana na wataalam kutoka Chuo Kikuu cha Jomo Kenyatta, ambapo majibu yalionesha kuwa asilimia 39.5 walikuwa na tatizo la kusisimua misuli ya uume.

Utafiti huo ulionesha kuwa vijana hao waliathirika kutokana na kutumia nguvu nyingi katika kuendesha baiskeli na kwamba walioendesha baiskeli kwa muda wa saa 60 au zaidi kwa wiki ndio waliathirika zaidi.

Wamalwa alitahadharisha pia kuwa vijana wengi walio kwenye vituo vya kufanyia mazoezi (gym) wakiendesha baiskeli zisizokuwa na vizuizi maalum dhidi ya sehemu za uume, wako kwenye hatari ya kukutwa na tatizo la kutokuwa na uwezo wa kushiriki ipasavyo tendo la ndoa.

Aidha, matokeo ya utafiti huo pia yanaendana na matoekeo ya tafiti zilizofanywa na watafiti wengine sita wa Chuo Kikuu cha Moi zilizowahusisha vijana 131 wa mjini Eldoret, wenye umri kati ya miaka 18 na 56. Kati ya waliopimwa, asilimia 76 walibainika kuwa na matatizo ya kutosisimua ipasavyo misuli ya uume.

“Ujumbe wetu ni muhimu kwao pia, kwamba wanafaa kuwa wanapumzika kwa muda kutoka kwa kazi yao. Wanapojikakamua kutafuta posho, wanafaa pia kujali uwezo wao kitandani,” Mhadhiri Wamalwa ameviambia vyombo vya habari.

Makamu wa Rais Akazia Juu ya Serikali Kutotoa Chakula Bure kwa Wenye Njaa..!!

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amesema kamwe Serikali haitagawa chakula kwa wananchi wavivu ambao hawataki kufanya kazi na kusubiri chakula kutoka Serikalini.

Mhe Suluhu ametoa kauli hiyo wakati akihutubia mamia ya wananchi wa Manispaa ya Musoma katika mkutano wa hadhara ambapo amesisitiza kuwa Serikali itapeleka chakula kwa wananchi ambao mazao yao yaliharibiwa kwa mvua au yalikauka kwa ukame au kwa  maafa mengine na sio kwa wananchi wanaokaa vijiweni mchana kutwa bila kufanya kazi wakisubiri neema ya chakula kutoka kwa Serikali.

Amewahimiza wananchi kote nchini kuendelea kufanya kazi kwa bidii ikiwemo shughuli za kilimo na pindi wanapovuna wajiwekee akiba na waache tabia ya kuuza mazao yote wanayoyavuna ili kukabiliana na tatizo la uhaba wa chakula kwenye familia zao.

Aidha Mh. Makamu pia amewataka viongozi wa mkoa wa Mara washirikiane na wananchi katika kuwaelemisha mbinu bora za kilimo ili waweze kupata mazao mengi ikilinganishwa na hali ilivyo kwa sasa.

Diamond Ali Uwe na Sifa ya Ziada ya Kujiunga na WCB,Ni lazima Utoke Katika Familia ya Kimasikini Kabisa..!!!

$
0
0

Rais wa lebo ya WCB, Diamond Platnumz ametaja sifa za kujiunga na lebo hiyo. Msanii huyo amesema ni lazima uwe umetoka katika maisha ya chini kabisa, yaani familia isiyojimudu kiuchumi.

Diamond amesema hawawezi kuchukua watu wanaotokea familia zinazojimudu kiuchumi [tajiri] kwa sababu ni vigumu kwa wao kupambana kwa kuwa kila kitu wanacho.

“Sifa ya kwanza WCB ni mtu aliyetoka katika hali ngumu, maisha magumu kwa sababu sisi tunajitahidi kujiajiri mwenyewe kwa wenyewe. Japo kuwa muziki wetu haujawa na riziki lakini angalau kidogo hichi  tule wote,” amekiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM.

“Tunaamini watu kutoka mtaani wanakuwa na talent ya kweli, wanakuwa na njaa ya kujituma na nidhamu kwa sababu wanaogopa wasije wakarudi tena katika mtaa. Lakini mtoto wa kitajiri mimi sikudanganyi wanakuwa hawana nidhamu kwa sababu wanajua sisi tuna hela, kwa hiyo yeye haogopi au kufanya kazi kwa bidii,” ameongeza.

Diamond amesisitiza ni mara kumi wakatumia nafasi walionayo kuwasadia wale walio mtaani kwa sababu wapo wengi na wanahitaji kushikwa mkono ili kesho na kesho kutwa wakazisaidie familia zao.

Hector Bellerin Afikiria Kukiahasi Kikosi cha Wenger..Atangaza Kurudi Zake Barcelona..!!!

$
0
0

Beki wa pembeni wa Arsenal Hector Bellerin huenda akaihama klabu hiyo na kurejea mjini Barcelona Hispania kujiunga na FC Barcelona katika kipindi hiki cha usajili wa majira ya kiangazi.

Bellerin ameonyesha kuwa tayari kuondoka kaskazini mwa jijini London, kufuatia kauli yake aliyoitoa wakati akihojiwa na gazeti la Mundo Deportivo jana jumanne.

Beki huyo alisema suala la kuondoka ama kutoondoka Arsenal linategemea na wakati, kwa sababu hajui nini kitatokea kesho, kutokana na ufahamu alionao katika medani ya soka.

Alisema suala la usajili lipo wazi siku zote na inapotokea pande mbili zinakubaliana hakuna budi kwa muhusiaka kuondoka kwa sababu kitakachofanyika ni biashara.

“Nipo hapa kwa ajili ya kuitumikia Arsenal, ninaipenda na kuithamini, lakini likitokea la kutokea nitaondoka na kwenda popote pale ninapohitajika.” Alisema beki huyo mwenye umri wa miaka 22.

Leo Ndiyo Leo..Macho na Masikio Yote Dodoma Bungeni Ambapo Bajeti ya Trilioni 32 Itakavyotabiri Hali ya Maisha kwa Watanzania..!!

$
0
0

NCHI za Afrika Mashariki ikiwamo Tanzania zinawasilisha bajeti zao kwa mwaka wa fedha 2017/2018. Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango anatarajiwa kuwasilisha bajeti hiyo bungeni leo mjini hapa kuanzia saa 10 kamili jioni.

Kabla ya kufanya hivyo, asubuhi Dk Mpango atawasilisha Taarifa ya Hali ya Uchumi ya nchi, ambayo itajikita katika kueleza mipango ya maendeleo kwa mwaka ujao. Kwa mujibu wa ratiba ya Bunge la Tanzania katika Mkutano wake wa Saba wa Bunge la Bajeti, wabunge watatumia kesho kusoma na kutafakari hotuba hiyo.

Kuanzia Jumatatu ijayo Juni 12 hadi Juni 20, mwaka huu, wabunge watajadili Taarifa ya Hali ya Uchumi na Bajeti ya Serikali kwa siku saba kabla ya jioni ya Juni 20, mjadala kuhitimishwa kwa upigaji kura ya wazi.

Machi 29, mwaka huu, Dk Mpango alisoma bungeni mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa na kiwango cha ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa 2017/18, na kueleza kuwa serikali katika bajeti hiyo inatarajia kuwa na ukomo wa Sh trilioni 31.6.

Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/2017 inayomalizika Juni 30, mwaka huu ilikuwa ya Sh trilioni 29.5. Katika Sh trilioni 31.6, za maendeleo zimeongezeka kutoka Sh trilioni 11.8 katika mwaka 2016/17 hadi Sh trilioni 11.9 katika mwaka wa bajeti 2017/18.

Ongezeko hilo ni kiasi sawa na asilimia 38 ya bajeti hiyo tarajiwa. Dk Mpango alisema maeneo kipaumbele ya bajeti ni miradi ya maendeleo inayolenga kufanikisha utekelezaji wa Malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025.

Aliitaja miradi ya maendeleo ni ule wa makaa ya mawe wa Mchuchuma na Liganga, ujenzi wa reli ya kati kutoka Dar es Salaam, Tabora hadi Kigoma yenye urefu wa kilometa 1,251 kwa kiwango cha standard gauge.

Pia ujenzi huo ni pamoja na matawi ya Tabora kupitia Isaka hadi Mwanza (kilometa 379), Isaka hadi Rusumo (kilometa 371), Kaliua kupitia Mpanda hadi Karema (Kilometa 321), Uvinza kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga, Tanzania na kusomesha vijana wengi zaidi katika stadi za mafuta na gesi, uhandisi na uboreshaji huduma za afya.

“Maeneo mengine ni viwanda vya kukuza uchumi wa viwanda, kuwianisha maendeleo ya uchumi na ya watu na mazingira ya wezeshi kwa uendeshaji biashara na uwekezaji,” alieleza Dk Mpango.

Aidha, alilitaja eneo jingine muhimu ni uendelezaji sekta za ubia kati ya sekta ya umma na binafsi pamoja na maeneo mengine muhimu kwa ukuaji wa uchumi na ustawi wa taifa.

Alisema lengo la uandaaji wa mpango wa bajeti, unaongoza serikali katika kusimamia mambo ya uchumi ikiwamo kuongeza kasi ya ukuaji wa Pato la Taifa kufikia asilimia 7.5 katika mwaka huu, asilimia 7.9 mwakani na asilimia 8.2 mwaka 2019.

Aliongeza kuwa mpango huo unalenga kudhibiti kasi ya mfumuko wa bei na kubaki na tarakimu moja hadi kufikia asilimia 5.0 katika kipindi cha muda wa kati, kuwa na pato ghafi la taifa la Sh trilioni 123.9 kwa mwaka 2017/18, Sh trilioni 139.7 kwa mwaka 2018/19 na Sh trilioni 165.4 mwaka 2019/2017 na mapato ya kodi kufikia asilimia 14.6 ya pato la taifa mwaka 2017/18, asilimia 15.5 mwaka 2018/19 na asilimia 15.8 mwaka 2019/20.

Alifafanua kuwa Sh trilioni 31.6 zitakazokusanywa na kutumika 2017/18, mapato ya ndani yanatarajiwa kuwa Sh trilioni 20.872 sawa na asilimia 63 ya mahitaji yote. Kati ya mapato hayo, serikali inalenga kukusanya mapato ya kodi ya Sh trilioni 18.097 (sawa na 87% ya mapato ya ndani), na mapato yasiyo ya kodi Sh trilioni 2.022 na kutoka vyanzo vya halmashauri yanatarajiwa kuwa Sh bilioni 753.3.

Alieleza kuwa serikali inategemea kukopa kiasi cha dola za Marekani milioni 900 (Sh trilioni 2.080) kutoka vyanzo vya nje vyenye masharti ya kibiashara na Sh trilioni 4.434 zinazotarajiwa kupatikana kutokana na mikopo ya ndani ili kulipia hatifungani na dhamana za serikali zinazoiva.

Kwa mujibu wake, Sh trilioni 1.859, sawa na asilimia 1.5 ya Pato la Taifa ni mikopo mipya ya ndani kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Pia washirika wa maendeleo wanatarajiwa kuchangia Sh trilioni 3.7.

Kati yake, Sh bilioni 496.3 ni misaada na mikopo nafuu ya kibajeti (GBS), Sh trilioni 2.821 ni misaada na mikopo kwa ajili ya miradi ya maendeleo na Sh bilioni 382.4 ni misaada na mikopo nafuu ya mifuko ya pamoja ya kisekta.

Aidha, matumizi ya maendeleo yatakuwa Sh trilioni 13.164, sawa na asilimia 40 ya bajeti yote, ambapo fedha za ndani ni Sh. trilioni 9.960, sawa na asilimia 76. Wakitoa maoni yao yao juzi, wabunge wengi waliishauri serikali kuongeza fedha zaidi kwenye sekta ya maji na sekta ndogo ya umeme ili kuharakisha maendeleo pamoja na kuondoa kero za wananchi wengi wa vijijini.

Pia walipendekeza katika bajeti hiyo ya leo serikali ipunguze Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) hadi kufikia asilimia 16 kutoka 18 ya sasa na iondoe kodi hiyo katika bidhaa zinazoagizwa kutoka nje.

Aidha, walitaka VAT iondolewe katika malighafi za mazao yanayozalishwa nchini, na kusiwapo na ushuru wa bidhaa katika pembejeo za kilimo, pamoja na kutopandisha ushuru wa bia na vinyaji baridi.

Akizindua kituo maalumu cha ukusanyaji kodi jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Rais John Magufuli pia aligusia suala la bajeti kila mwaka kupandisha kodi katika vinywaji baridi na bia, akitaka mamlaka husika zitafune namna ya kupata kodi katika vyanzo vingine vya mapato.

Aidha, katika bajeti inayofikia ukomo Juni 30, mwaka huu, wabunge walilalamikia baadhi ya kodi zilizopitishwa. Baadhi yake ni VAT kwenye miamala ya benki na kampuni za simu za mikononi, pamoja na kukatwa kodi katika kuweka vocha za matumizi ya simu hizo.

Mbali na kodi hizo, ongezeko la VAT kwenye mizigo inayosafirishwa nje ya nchi pamoja na kwenye utalii zimeelezwa kuyumbisha kwa kiasi kikubwa sekta hizo. Katika mijadala yao, pia wabunge wametaka kuongezwa kwa tozo ya mafuta kutoka Sh 50 hadi kufikia Sh 100 ili fedha zinazopatikana ziende kusaidia sekta ya maji vijijini hasa kwa kuwa na Mfuko wa Maji Vijijini.

Aidha, akijibu swali bungeni juzi, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji alieleza kuwa serikali itawasilisha katika bajeti yake mapendekezo ya kufuta misamaha ya kodi isiyo na tija.

Dk Kijaji alisema mpango wa serikali ni kuhakikisha misamaha ya kodi inashuka mwaka hadi mwaka na katika mwaka ujao wa fedha, serikali italeta mapendekezo ya marekebisho ndani ya bajeti itakayosomwa kesho.

Majibu ya hoja hizo na nyinginezo, yatakuwa yamepata ufumbuzi au kujulikana jinsi serikali ilivyoyazingatia wakati itakapofika saa 12 jioni leo, wakati Dk Mpango atakapokuwa amekamilisha hotuba yake ya bajeti ya pili ya utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano.

Credit - Habari Leo
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images