Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104701 articles
Browse latest View live

Mghwira Aenda Kuhani Familia ya Marehemu Ndesamburo...!!!

$
0
0

Baada ya kutia saini kitabu cha wageni katika ofisi yake mpya jana Alhamisi, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mgwhira, ameenda kuhani msiba wa aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema, mkoa huo, marehemu Philemon Ndesamburo.

Mghwira ametoa rambirambi kwa familia ya Ndesamburo, aliyewahi kuwa mbunge wa Moshi Mjini kwa awamu tatu mfululizo.

Mghwira aliyeteuliwa hivi karibuni na Rais John Magufuli amewasili katika eneo lake jipya la kazi ikiwa ni siku mbili tu baada ya kuapishwa na Rais,  Ikulu jijini Dar es Salaam.

Mghwira anaanza kazi wakati Chama cha ACT-Wazalendo kikimuondoa katika nafasi yake ya Mwenyekiti wa chama hicho kutokana na matakwa ya katiba ya chama hicho.

Hata hivyo, Mgwhira ataendelea kuwa mwanachama wa ACT-Wazalendo.

Bajeti Kuu ya Serikali 2017/18..Pato la Mtanzania Laongezeka kwa Asilimia 11...!!!

$
0
0

Pato la kila mtanzania kwa mwaka 2016 limeongezeka kwa asilimia 11 kutoka shillingi 1,918,897 kwa mwaka 2015 mpaka kufikia shilling 2,131,299 kwa mwaka 2016.

Takwimu hizi zimebainishwa na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt Philip Mpango wakati akiwasilisha Bungeni Mjini Dodoma Taarifa ya Hali ya Uchumi ya mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa mwaka 2017/2018.

Akifafanua kuhusu ongezeko hilo Mhe. Dkt Philip Mpango amesema kuwa Pato la Taifa kwa mwaka 2016 lilifikia Shillingi million 103,744,606 kwa bei za mwaka husika na kiasi hiki kiligawanywa kwa idadi ya watu 48,676,698 walipo Tanzania Bara na kufanya wastani wa Pato la kila mtanzania kufikia kiasi cha Shillingi 2,131,299.

Ameeleza kuwa kwa thamani ya Dola za Marekani, wastani wa pato la Kila mtu liliongezeka kutoka Dola 967.5 mwaka 2015 hadi Dola 979.1 kwa mwaka 2016 ikionesha kuwa Tanzania inaelekea kwenye kundi la Uchumi wa kati.

“Serikali inaendelea kutatua changamoto mbalimbali ili tuweze kufikia Uchumi wa Kati kwa kuongeza fursa mbalimbali za uzalishaji nchini,” alisistiza Mhe. Dkt Mpango.

Mhe. Dkt. Phili Mpango ameongeza kuwa Serikali imejipanga kuboresha shughuli za uzalishaji wa tija katika Sekta zinazoajiri hususan katika Sekta ya Kilimo cha mazao,Ufugaji na Uvuvi.

Mwambusi Ataja Mchawi wa Yanga Baada ya Kutolewa Mapema Kwenye SportPesa Cup..!!!

$
0
0

Kocha msaidizi wa Klabu ya Yanga SC, Juma Mwambusi amefunguka na kuitetea klabu yake baada ya kichapo cha goli 4-2 dhidi ya AFC Leopards kutoka Kenya na kutupwa nje ya michuano ya SportPesa Super Cup kwa kusema timu yake imekosa muda wa maandalizi.

Juma Mwambusi ambaye kwenye michuano ya Supersport Super Cup amechukua nafasi ya Kocha mkuu Lwandamina aliyelikizo amesema Klabu ya Yanga imetolewa kwa kukosa muda wa maandalizi kwani michuano hiyo haikuwa na muda mrefu wa kuruhusu vilabu kujiandaa.

“Tumetolewa kweli michuano ilikuwa ni migumu kwetu hatukuwa na muda wa kutosha wa maandalizi ya michuano hii muda ulikuwa mfupi sana, hii imetuathiri sana kwenye michezo yetu yote miwili”Amesema Mwambusi mapema baada ya mchezo kumalizika.

Klabu ya Yanga inakuwa timu ya nne kutolewa kwenye michuano hiyo yenye msisimko wa aina yake inayodhaminiwa na kampuni ya Kubashiri ya SportPesa, baada ya Simba,Singinda United na Jang’ombe Boys ya Zanzibar.

Tundu Lissu Kumpeleka Spika wa Bunge Job Ndugai Mahakamani

$
0
0
Tundu Lissu
Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu amesema kuwa watakwenda mahakamani kupinga maamuzi ya kusimamishwa kwa wabunge wa CHADEMA, Esther Bulaya (Bunda) na Halima Mdee (Kawe) baada ya kupewa adhabu hiyo mwanzoni mwa wiki walipopatikana na hatia ya kudharau Mamlaka ya Spika wa Bunge.

Lissu amesema kuwa atakutana na wabunge hao waliosimamishwa na kuandaa hoja watakazopeleka Mahakama Kuu na kwamba uamuzi aliochukua Spika wa kuwafungia wabunge hao wa kutohudhuria vikao vya Bunge kwa miezi kumi ni makosa makubwa.


Tunataka Mahakama ituambie kwenye ‘Judicial review’ je, Bunge linaweza kufuta ubunge wa Mbunge wake, kama wanavyotafsiri hawa akina Ndugai? Je, Bunge linaweza likatoa adhabu hata nje ya adhabu iliyopo kwenye kanuni? Je, Bunge lina uwezo wa kumuadhibu Mbunge bila kumpa fursa ya kujitetea kwenye Kamati na Bunge lenyewe?

Tutaomba Mahakama Kuu itupe tafsiri. Kwa vyovyote vile utaratibu huu hatutakubaliana nao. Tukienda hivi, hawa CCM wa Bungeni kuna siku wataamua Mbunge asiingie Bungeni kwa miaka mitano halafu wanasema Bunge lina mamlaka lisiingiliwe. Bunge haina mamlaka hayo.

Kuna kanuni za kutoa adhabu kwa Mbunge yeyote anayefanya kosa. Adhabu ya kumfungia Mbunge kwa miezi 10 haipo kwenye Kanuni za Bunge la Tanzania. Lakini kumekuwa na tabia na utamaduni, sasa inapofika wabunge wa upinzani wanapewa adhabu kubwa kubwa ambazo zipo nje kabisa ya utaratibu wa kanuni zilizopo,” alisema Lissu.

Amesema kuwa Sheria na kanuni za Bunge zinasema adhabu ya Mbunge ni kumfungia vikao 20 kwa maana ya siku na kwamba adhabu nyinginezo haiwezi ikawa kifungo cha siku 100 au miezi kumi. Pia alisema kuwa tafsiri nyengine ya kanuni hizo si kumzuia Mbunge kuhudhuria vikao 20, bali inaweza ikawa kumnyima Mbunge huyo mshahara wake, kuzuia bima yake ya afya na kumfutia posho ya jimbo.

Sikiliza Wimbo Mpya wa Saida Karoli Aliyochanganya Wimbo wa Diamond na Darassa

$
0
0
saida karoli na Diamonda Platnumz
Baada ya kurudi kwenye tasnia ya muziki kupitia wasanii waliotumia vionjo vya nyimbo zake na hivyo kupelekea watu kumkumbuka tena nguli huyu, na yeye ameamua kuingia studio kukumbushia makali yake ya kipindi cha nyuma.

Saida Karoli ambaye amekuwa akiimba nyimbo za asili alitamba sana miaka ya mwanzoni mwa 2000 ambapo waimbo wake ambao ni maarufu zaidi ni Chambua ambao siku za hivi karibuni wasanii kama Darassa, Belle 9, Diamond Platnumz walitumia vionjo vya wimbo huo na kutengeneza nyimbo zao zilizofanya vizuri sana.

Said Karoli ametoa wimbo wake mpya ambao na yeye ametia vionjo vya wasanii hao waliotumia wimbo wake. Wimbo huo una jina asili ambalo kwa kiswahili linamaanisha Maneno Maneno. Usikilize wimbo huo hapa chini;

Sioni Aibu Kuolewa na Mwanaume Niliyemzidi Miaka 7 – Riyama

$
0
0
Riyama Ally na Mchumba wake
Muigiza wa Filamu nchini, Riyana Ally na mumewe ambaye ni msanii wa Bongo Fleva, Leo Mysterio wamesema hawaoni aibu kuishi pamoja kisa umri.


Wakizungumza katika kipindi cha Twenzetu cha Times FM, Riyama amesema yeye binafsi haoni aibu wala hana hofu kuolewa na mwanaume ambaye yeye amemzidi umri zaidi ya miaka saba. Kwa upande wake Leo Mysterio ameeleza wakati anataka kumuoa Riyama alisemwa sana na kukosolewa vikali.

Eti kwa sababu umri ni mkubwa lakini kwa sababu sisi ni watu wa dini haikua kazi kumaliza swala la ndoa. Niliwahi kutoa wimbo maalum kwa ajili ya Riyama na ilinitoka moyoni kabisa kitu ambacho kiliwashangaza wengi,” amesema Leo Mysterio.

Bajeti Kuu ya Serikali..Haijapata Kutokea ...Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo Ijumaa 9/6/2017..!!!!

Shilole Awalaani Waliomwibia Account yake ya Instagram

$
0
0
Shilole Katika Pozi
STAA wa Muziki wa Bongo Fleva, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ amemlilia Mungu na kulaani vikali watu walioingilia akaunti yake katika Mtandao wa Instagram ambako huwa anaposti mambo yake mbalimbali ya kikazi.


Akizungumza na Za Motomoto News, Shilole alisema mpaka sasa wanaendelea kuishughulikia akaunti hiyo irudi na hana mpango wa kufungua nyingine ila waliofanya hivyo anawakabidhi kwa Mungu awafanyie kazi mwenyewe.

Sifungui akaunti nyingine, bado tunaishughulikia hii maana watu wengi wanaijua na napata wateja wengine hasa kwenye biashara yangu ya chakula na shoo mbalimbali, hao walioiba nawakabidhi kwa Mungu,” alisema Shilole.

Nisha Adai Kuwa Na Uhusiano Na Mbwa

$
0
0
Salma Jabu aka Nisha

WAKATI waumini wa Dini ya Kiislam wakiendelea na Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, msanii wa filamu, Salma Jabu ‘Nisha’ ametoa kali ya mwaka kufuatia kukiri kuwa na uhusiano na mbwa.

Nisha alifanya hivyo juzikati baada ya kuweka picha kwenye ukurasa wake wa Facebook akiwa amevaa gauni jeupe la harusi huku mkononi akiwa ameshika mkanda wa mbwa na kuandika kuwa, mnyama huyo ndiye mpenzi wake, jambo ambalo liliwachefua baadhi ya marafiki zake.



Dada acha kukufuru halafu huu ni Mwezi Mtukufu, Kiislam mbwa ni najisi halafu wewe ni Muislam unashika mbwa na kusema ndiyo mpenzi wako, tangu lini mbwa akawa na uhusiano na binadamu?” aliandika mmoja wa mashabiki aliyeonekana kukerwa na kitendo hicho. Jitihada za kumtafuta Nisha kuzungumzia kitendo alichokifanya hazikuzaa matunda baada ya simu yake kutopokelewa na hata alipotumiwa SMS hakujibu.

Je Unajua Marehemu Ivan Don Alipotajirikia...Hii Hapa Historia Yake Fupi Itakayo Inspire Wengi

$
0
0
Ivan Don
RIP Ivan Don

Moja kati ya watu waliopata kuniinspire ni huyu Ivan - huyu jamaa nilimfahamu tangu hata Zari hajaachana nae... Jamaa alizamia kuingia SA kwa shida sana, alitoka UG akiwa masikini wa kutupa, hata alivyofika mpakani Zambia ama Zimbabwe (sikumbuki vzr) alikamatwa kwa kukosa vibali, lkn mwisho wa siku akatusua.

Baada ya kuingia SA akapambana sana sana sana ktk kile ambacho alikijua zaidi, huyu jamaa alikua daktari wa jadi "Mganga" - but very focused. Aliweza kuwatibu watu wazito sana akiwemo Mke wa Thabo Mbeki, alipooanza kupiga pesa za kibabe akawa anawaleta wauganda kutoka kijijini kwao anawatrain anachokijua kisha anawaachia clients wake.

Baadae akaanza kumiliki vitu vyenye akili, akaanzisha Brooklyn College ambayo inahusu sana mambo ya nursing, madini, uongozi na utawala, pamoja na technology. Jamaa baadae akarudi kuwekeza Uganda akajenga 4 star hotel njia ya kuelekea kijijini kwao, akajenga nyumba 2 huko kijijini kwao Manyonyo. Kisha akarudi SA akajenga Pretoria na Sandton (haya ni maeneo ya ushuani hasa).

Baada ya yote hayo akaona yupo vzr akaamua kuanzisha philanthropy (kutoa misaada) - hapa ndio mwanzo wa Rich Gang, akajenga orphanages 2, 1 SA na ingine UG... akawalea watoto yatima na wale waishio mazingira magumu. Akawa anatoa misaada sana kwa wamama ambao ni single parents nk, hata kabla hajafa alitoka UG akatoa misaada sana...

Na pia yeye alijulikana kama mwenyekiti wa waUG nchini SA, mUG yeyote akifika SA afu akawa hana dira basi akifika kwa Ivan anapata msaada, anapewa michongo na guidance ya kupiga pesa.

Jamaa kafariki na moyo wake... kafariki watu wanampenda... hana ugomvi na mtu, sijawahi kusikia akiwa na kashfa yoyote ya kulaghai, kutapeli, kunyanyasa nk. Yani alikua ni mtu safi sana... kafariki mapema sana... alikua humble sana, kwa familia yake alijitoa sana awe baba bora... Wanawake tunawajua akili zao - siwezi zungumza sana lakini Zari dada'ngu sijui kilitokea nini akashindwa kuelewana na Marehemu na Kumuacha.

Rest in peace rich gang president.

By ONTARIO

Baada ya Kutemana na Harmonize..Wolper Apata Ugonjwa wa Wanaume..!!!

$
0
0

STAA wa filamu Bongo Jacqueline Wolper amesema kuwa, japo wanaume wengi wenye nazo wamekuwa wakimsumbua kumtaka kimapenzi, haoni haja ya kuwa nao kwa kuwa anaamini ni wasumbufu tu hawana mapenzi ya kweli.

Akizungumza mawili-matatu na Star Mix, Wolper alisema, kutokana na upendo wa kweli anaojitahidi kumuonyesha mwanaume anapokuwanaye kwenye uhusiano na kujikuta akiambulia maumivu, ameona bora aweke kando masuala ya mapenzi na kuwa`bize’ na kazi zake. “Sina mpenzi kwa sasa nimeona bora niweke pembeni haya mambo nidili na kazi zangu tu ndo muhimu, nikipenda hawa wanaonisumbua `now’ nitapenda na nitakuwa kimapenzi, lakini bado wote wanaonisumbua hakuna aliyefaulu kunishawishi niwe naye,” alisema Wolper

Rasmi..Baada ya Kupona Roma Mkatoliki Aaanika Haya Mengine Mapya Kuhusu Yeye na Tukio la Kutekwa Kwake..!!!

$
0
0

RAPA kipenzi cha Watanzania, Ibrahim Mussa ‘Roma Mkatoliki’ amefunguka kuwa afya yake imeimarika na sasa yupo tayari kupanda jukwaani kukamua shoo kama kawaia yake.

ROMA ameyasema hayo jana wakati akitoa neno la shukrani kwa uongozi na wafanyakazi wa Kampuni ya Glopbal Publishers kwa kuendelea kumsapoti, kufanya naye kazi, kuboresha mahusiano yaliyo mema na kumfariji hasa katika kipindi kigumu alipopatwa matatizo ya kutekwa akiwa na wenzake watatu.

“Nimfika hapa kwa ajili ya kutoa neno la shukrani kwa jinsi ambavyo tmekuwa tukifanya kazi pamoja, pamoja na matatizo yaliyotukuta mimi na wenzangu lakini nyinyi Global Publishers mmeendelea kuwa na mimi katika kipindi chote hicho.

“Mtu akiona nimeweza kutembea kutoka nyumbani mpaka kufika hapa ofisini (Global PUblishers), basi ajue nipo fiti, na ninaendelea vizuri. kama nimeweza kushika maiki, nikazungumza basi hata Dar Live naweza kushika maiki (akimaanisha kufanya shoo).

“Niliona kipindi cha matatizo mlitupigania, magazeti ya Global Publishers yalifanya coverage nzuri na mlikuwa upande wetu. Kiukweli tulifarijika kuona watu wengi wakitutia moyo na kutupatia neno la faraja,” alisema Roma.

Msechu Atangaza Dau la Milioni Moja kwa Atakayemuandikia Wimbo Mzuri..!!!

$
0
0

Msanii wa Bongo Fleva, Peter Msechu amesema kutokana na muziki wake kwa sasa kuhitaji mchango wa watu wengi ili kuwa bora zaidi amelazimika kutoa fursa kwa mashabiki wake kumuandikia nyimbo na kununua.

Mwimbaji huyo ameeleza kuwa mtu yeyote mwenye wimbo mkali amtafute na wakae chini kuongea kwa ajili ya kupatana bei, lakini kiasi cha fedha unachoweza kupata kinaweza kufika hadi sh. milioni moja.

“Kuna mtu amenicharge juzi wimbo moja sh. milioni moja na ni wimbo mkubwa sana, ninafikiri ndio wimbo utakaofuata baada ya Ramadhan,” Msechu amekiambia kipindi cha Ladha 3600 cha E Fm.

“Kuna mdada mmoja anakaa Arusha ameniandikia nyimbo mbili aiseee!!, nilitengemea hata atanidai milioni tano au sita lakini alikataa kabisa akaniambia kwa heshima yako wewe ziimbe tu, unaona kabisa wapo watu wenye vipaji hivyo lakini wamejificha,” ameongeza.

Msechu ameongeza kuwa toka awali alishaweka wazi kuwa yeye hajui kuandika nyimbo hivyo watu wasishangae kwani anafanya hivyo ili kuepuka kukurupuka kutoa nyimbo kama ilivyokuwa awali ila sasa hivi anajaribu kujipa muda.

Bajeti ya Waziri Mpango Yaibua Shangwe Nchi Nzima..!!!

$
0
0

Serikali  ya Jamuri ya Muungano wa Tanzania imewasilisha bajeti yake kwa mwaka wa fedha 2017/18, huku ikiwa imetangaza kufuta na kupunguza tozo, ushuru na kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwenye sekta mbalimbali hapa nchini.

Bajeti hiyo imewasilishwa leo Juni 08, na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango ambapo amependekeza kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye bidhaa za mtaji ili kupunguza gharama za mashine na mitambo kwa ajili uanzishwaji wa viwanda vidogo na vya kati, 
kwenye bidhaa zinazosafirishwa nje ya nchi kuifanya Tanzania iwe njia bora ya kupitisha bidhaa na kuongeza mapato kupitia bandari pamoja na kwenye vyakula vya mifugo vinavyotengenezwa nchini.

 Waziri Mpango pamoja na kupunguza kodi za kampuni kutoka asilimia 30 hadi 10 kwa miaka mitatu ya uzalishaji, pia amefuta rasmi  ada ya mwaka ya leseni ya magari huku akisema kwamba uamuzi huo umechukuliwa ili ada hii ilipwe mara moja pale gari linaposajiliwa na baada ya hapo iendelee kulipwa katika ushuru wa bidhaa kama  mafuta ya petroli na dizeli. 

Katika bajeti iliyowasilishwa, Waziri huyo amependekeza kuondolewa kwa ushuru wa huduma unaotozwa na halmashauri kwenye mabango na vibao vya matangazo vinavyoelekeza mahali zilipo huduma muhimu za kijamii kama vile shule na hospitali huku akitangaza rasmi kuwa kuanzia mwezi Julai mwaka huu, na kwamba Mamlaka ya Mapato (TRA) ndiyo watakaokuwa wakihusika na ukusanyaji wa ushuru wa mabango katika halmashauri zote nchini.

Vilevile bajeti hiyo ya Waziri Mpango imegusa kupunguza ushuru wa mazao kutoka 5% hadi 3% kwa mazao ya biashara na 2% kwa mazao ya chakula na kufuta kabisa ushuru kwa mazao yasiyozidi tani moja yanayosafirishwa kutoka halmashauri moja kwenda nyingine, ikiwa ni pamoja na kupendekeza kutoza ushuru wa forodha kwa 0% badala ya 25% kwenye malighafi kwa ajili ya vifaa vya watu wenye ulemavu, na kufuta ushuru wa huduma kwenye nyumba za kulala wageni 'Guest House'

Dkt. Mpango ametangaza rasmi ukusanyaji wa kodi ya majengo katika miji na vijiji vyote nchini ambapo amesema majengo/nyumba ambazo hazijafanyiwa uthamini kodi yake itakuwa Shilingi 10,000 kwa nyumba ya kawaida na 50,000 kwa nyumba za ghorofa.

Bajeti Mpya: Wafanyakazi Tumeikosea Nini Awamu ya Tano ?

$
0
0
Bunge

Nimesoma hotuba ya bajeti kurasa zote kuanzia ukurasa wa kwanza mpaka wa mwisho hakuna chochote kilichozungumzwa kuhusu maslahi ya mfanyakazi wa umma hususani mshahara wa mtendaji huyu wa serikali.

Licha ya matambo na mbwembwe nyingi katika uwasilishaji lakini serikali imeshindwa hata kutaja kima cha chini tu cha mshahara!Imeshindwa hata kusema tu maneno machache ''tumezingatia maslahi ya mtumishi katika bajeti hii''

Hii serikali toka iingie madarakani imekuwa na mazoezi kandamizi tu kwa mfanyakazi, watumishi hewa, vyeti feki, lawama za kila aina lakini imekuwa jeuri kuhusu kuzingatia maslahi ya wafanyakazi hawa.

Wabunge tunawaomba msimamie na kupigia kelele suala hili katika mjadala wa bajeti.

Chanzo JF

Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid, Je? Unapata Pesa Haikai? Umeachwa na Mpenzi, Mke au Mme Anakusumbua?

$
0
0

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI. (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 72 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI: 

SHEKH SHARIFU RASHID ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran dawa za asili dawa za kiarabu, na njiwa, Anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango kwa kina mama, ngiri maji na n.k, anakuvutia mali zilizo potea au kudhulumiwa, pia anatoa Pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali, Wenye matatizo ya uzazi, jini mahaba, mapepo ya kichawi, vifungo vya kimaisha, ndoto mbaya za usiku, uelewa mdogo wa ufahamu shuleni kwa watoto wote, pia anauwezo mkubwa wa kumaliza kazi zilizoachwa na wataalamu wengine ndani ya masaa 48 tu, Pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo. WASILIANA NAE KWA WhatsApp na SIMU NO: +255 718-668347 na +255 767-204308 , +255 685-224047 Email shekhsharifurashidi@gmail.com. 

USHAURI: ni vyema kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate huduma kwa haraka.

Ulaji wa Nyama ya Kiti Moto Wapigwa Marufuku Dodoma

$
0
0
kitimoto
MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Christina Mndeme, amepiga marufuku uingizaji na uchinjaji wa nguruwe, kufuatia mlipuko wa homa ya nguruwe.

Alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akizungumza na madiwani na watendaji wa Manispaa ya Dodoma.

Alisema hadi sasa zaidi ya nguruwe 200 tayari wameshakufa kutokana na mlipuko huo.

Aliwataka wakazi wa manispaa hiyo kutokula mizoga ya nguruwe ili kuepuka maambukizi ya homa ya nguruwe ambayo kwa asilimia 100 inaua.

Aliwataka kula nyama ya nguruwe iliyopimwa na wataalamu wa afya.

Alisisitiza madiwani kutoa elimu kwa usahihi kwa wananchi wao kuhusu madhara ya mlipuko huo.

Alitaja kata zilizokumbwa na mlipuko huo kuwa ni kata ya Ipagala na Miyuji ambayo zaidi ya nguruwe 200 wameshakufa.

Aliagiza kufanyika doria na kuwakamata watu wote watakaobainika kukaidi amri hiyo.

Ninawaagiza nyinyi madiwani pamoja na watendaji hakikisheni mnatoa elimu iliyo sahihi kwa uwazi bila kificho, ukizingatia kuwa ugonjwa huu unaua tena kwa asilimia mia moja, hivyo ni marufuku kuingiza ndani ya wilaya hii na wala kuchinja pasiporuhusiwa na wataalamu wa afya,” alisema.

Alisema ingawa ufugaji wa nguruwe ni sehemu ya kujiingizia kipato, kipindi hiki cha mlipuko hakuna sababu ya kupuuza bali wanatakiwa kujiepusha ulaji holela wa nyama hiyo.

Aliwataka wafugaji kujiepusha na uchukuaji wa vyakula vinavyobaki hotelini na sokoni kwa kuwa vinasadikiwa kuwa na vimelea vinavyochangia uwepo kwa homa hiyo.

Producer wa Ali Kiba Abydad Afunguka WCB ilivyovunja Mahusiano yake na Kiba

$
0
0
producer abydady
Mtayarishaji wa wimbo Aje wa Alikiba, Abydad, amefunguka kwa kudai kuwa mahusiano yake na muimbaji huyo yalivunjika baada ya studio yake kufanya kazi na wasanii wa WCB, Diamond na Rich Mavoko.


Abydad ameiambia Bongo5 kuwa hakuna chochote ambacho anadhani kumewatenganisha yeye na Alikiba zaidi ya project ya Rich Mavoko na Diamond, Kokoro.

“Najua kuna baadhi ya watu watanishambulia, watazunguza maneno mabaya lakini mwisho wa siku ukweli humweka huru mtu,” alisema Abydad. “Mimi sio producer wa msanii mmoja, naweza kufanya kazi na kila msanii,”

Aliongeza, “Sijazungumza kwa ubaya, hata haya mambo ya team kwa wahusika wenyewe nilikua najua tu ni mashabiki wenyewe ndio wanagombana au wanawagombanisha sikudhani kama mhusika mkuu wa pande hii na pande ile watakuwa wana ugomvi lakini baada ya hili tukio ndipo nilipoamini kuwa kweli ndani yake kuna kitu”

Hata hivyo bado Alikiba hajazungumza chochote kuhusu suala hilo, B5 bado inafanya jitihada za kumtafuta.

Man U kumuacha Ibrahimovic?

$
0
0
Ibrahimovic
Klabu ya Manchester United huenda isimuongeze mkataba mpya mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic ambaye mkataba wake wa sasa unamalizika Juni 30.


Ijumaa hii kwa mujibu wa mtandao wa Goal, Klabu hiyo inatarajiwa kutangaza wachezaji kadhaa ambao wanaachwa na klabu hiyo huku jina la mshambuliaji huyo likidaiwa kuwepo.

Zlatan mwenye miaka 35 alisaini mkataba wa mwaka mmoja na kukiwa na kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi.

Lakini mpaka sasa hakuna mjadala wa mkataba mpya na jeraha la goti alilopata mwezi April katika mchezo wa kombe la Europa ligi huenda likaongeza chachu ya kutopewa mkabata mpya.

Mshambuliaji huyu amecheza michezo 46 msimu huu na kufunga magoli jumla ya magoli 28

Wamachinga Sasa Kupewa Vitambulisho vya Kazi Yao....

$
0
0
Wamachinga
KATIKA mwaka wa fedha 2017/18, serikali imesema itawatambua rasmi wafanyabiashara wadogo wadogo wasio rasmi kwa kuwapatia vitambulisho maalumu vya kazi wanazozifanya.

Akiwasilisha Bungeni mapendekezo ya serikali kuhusu makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2017/18, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango, alisema jana mbali na kupatiwa vitambulisho maalum pia watatengewa maeneo.

Alisema wafanyabiashara hao ni pamoja na mama lishe, wauzaji mitumba wadogo, wauza mazao ya kilimo wadogo kama mboga mboga, ndizi, matunda na kadhalika.

Biashara zafungwa

Akizungumzia kuhusu kufungwa kwa biashara, Dk. Mpango alisema jumla ya biashara 7,277 zilifungwa katika mikoa mbalimbali nchini kwa mwaka wa fedha unaomalizika Juni 30.

Alisema suala hilo lilizungumzwa sana na wananchi na wabunge kutokana na kasi ya kufungwa kwa biashara hususan eneo la Kariakoo katika Jiji la Dar es salaam na katika miji mingine.

“Kwa mujibu wa taarifa zilizofikishwa TRA, katika kipindi cha kuanzia julai 2016 hadi machi 2017, jumla ya biashara 7,277 zilifungwa katika mikoa mbalimbali nchini,” alisema.

Alibainisha kuwa mwenendo huo kwa ujumla siyo mzuri kwasababu wananchi wanapoteza ajira na kipato, serikali inakosa mapato ya kodi na uchumi unadorora.

Alisema ni muhimu pale wimbi la kufungwa kwa biashara linapotokea jitihada zifanyike kuelewa aina gani za biashara zinafungwa, kwanini zinafungwa na hatua gani zichukuliwe kudhibiti hali hiyo.

Aidha alisema zipo sababu nyingi zinazoweza kuwa zimepelekea hali hiyo, ikiwa ni pamoja na ushindani mkali wa kibiashara, usimamizi dhaifu wa biashara, kuongezeka kwa gharama za kufanya biashara kama vile usafirishaji, kodi na tozo mbalimbali
Viewing all 104701 articles
Browse latest View live


Latest Images