Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104771 articles
Browse latest View live

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Siku ya Leo......


Wizi wa Vipuli vya Magari Dar-es-Salaam na Ukimya wa Polisi na Serikali

$
0
0
Wizi wa Vifaa vya gari
Nimerudi kutoka kazini mida ya saa 12 jioni, nikapaki gari langu ndani ya fence, nikaamua niangalie TV na nakufanya shughuli zangu za ofisini.

Baada ya kula mida ya saa mbili, nikaenda kulala mapema tu.

Naamka hasubuhi, nakuta gari limesogweza karibia na geti na limeibiwa vipuli vya gari, (kuanzia taa za mbele na nyuma, site mirror, bumper la mbele na nyuma, na vitu vya ndani).

Nikaamua kwenda Police kuripoti, nikaambiwa awa watu wako sana na hizi kesi tunazipata kila siku ya mungu, na Police wawili wakakiri ata wao wameshaibiwaga.

Baada ya kuongea na rafiki zangu kuhusu tukio langu, nikaambiwa kitu hichohicho kwamba ata maeneo yeo wamepiga magari kama manne siku za karibuni, na wengine wakinisimulia matukio hayo ya uwizi yalivyowatoke kwao au kwa familia/rafiki zao miezi michache iliyopita.

Kitu kimoja walichokuwa wanaongea sawa na kukubaliana (Police and Raia) ni kwamba wote wanajuwa hivyo vitu vinapopelweka “GEREZANI MNADANI”. Na ata vya kwangu nikaambiwa viko na mpaka wanajuwa vimeibiwa wapi na lini.

Swali langu na natumaini watu wengi wanajiuliza!

Kwa hiyo hii taabia itaendelea mpaka lini? Tunazungumzia vifaa vyenye thamani mpaka zaidi ya million 7 saa nyinginee watu wanaibiwa na visivyopunguwa laki 6.

Hii ni biashara kubwa yenye mtandao mkubwa na inaaribu uchumi wa wananchi wema na kama sio wa Nchi.

Tunashindwa nini kwenda kupafunga Gerezani Mnadani na kuwakamata wausika watoe ushirikiano kuhusu watu wanaofanya uwizi huwo. Kwa ujumla ni eneo linalo ifadhi vitu vya ujambazi, Mpaka wanajigamba kwamba “Si Serikali ya Magufuli wala ya Mtu yeyote itakayoweza kuwafanya kitu”.

Hii ni kauli ya Dharau kwa vyombo vya Dola na Serikali ya Rais wetu Mchapa kazi Magufuli asiyependa watu kama hao wanaotaka kuishi kwa majasho ya watu wengine.

Ombi langu kwa wananchi wenzangu:

Mie nimeanza kupaza sauti , lakini sauti yangu ni ndogo sana, tukishirikiana mimi na wewe hii sauti itakuwa kubwa na itasikika, na Amin’ na waambia RAIS WETU MAGUFULI Hashindwi kuwashughulikia awa watu na hii tabia ikapungua ama kuisha kabisa.

Note: HAKUNA KINACHOSHINDIKANA KATIKA DUNIA.

By Ruukada

Mapenzi ya Video za Ngono Yameniharia Penzi Langu

$
0
0
Mapenzi
Juzi kati nilikutana na shogangu hapo Mcity, akawa yupo bothered!
Akanilalamikia

Money Penny me nina mpenzi wangu tunapendana sana sana sana
Lakini huyu bwana me simwelewi kabisa sikuhizi ni kama mapenz yangu kwake yamekufaaa, huu ni mwaka wa 2 na wa mahusiano lakini yupo addicted na por.nography

Na tukifanya mapenzi nikawa naona simridhishi, nikaamua kum join kwenye sekta ya por.n, akawa ananifanyia kama wa kwenye por.n ndio anaskia raha namwona kabisa yupo satisfied
Lakini money penny me haya mambo ya por.n hata siyapendi kabisa ila nikaamua kujitoa sadaka

Tukaangalia por.n for 6 months bdae nikabamba sms zake ana chat na side chic wanaonyeshana maungo ya miili yao anafurahi mwenyewe na washakutana wakapigana dudu na kufi..rana

Hii ni relationship ya 2yrs na bwana nampenda sana ila sasa sijui nafanyaje tena?

Kuchanganya mapenzi na por.n kumeniulia mahusiano hata sielewi wanaume huwa wanataka nini jamaa!

Eti wadau, huyu shogangu afanyaje?! Bwanake naona kaota mapembe sa sijui tumwongezeeje mkiaa?!

Zitto Kabwe na Profesa Kitila Mkumbo watofautiana kwa mara ya kwanza hadharani

$
0
0
Kitila Mkumbo na Zitto Kabwe
Kwa mara ya kwanza, Kiongozi Mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe ametofautiana hadharani kimtazamo na aliyekuwa mshauri wa chama hicho, Profesa Kitila Mkumbo ambaye aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji.

Profesa Mkumbo na Zitto walitofautiana jana kuhusu Bajeti ya Serikali ya Mwaka wa Fedha 2017/2018 iliyosomwa jana bungeni na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango.

Msomi huyo alikuwa wa kwanza kuandika kwenye akaunti yake ya Twitter akiimwagia sifa bajeti hiyo pamoja na namna ilivyowasilishwa na Dk. Mpango, akieleza kuwa ni bajeti safi na kwamba anajivunia kuwa sehemu ya timu iliyoiwasilisha.

Hata hivyo, Zitto aliibuka na mawazo kinzani akieleza kuwa bajeti hiyo haitekelezeki, huku akikumbusha kuwa katika bajeti iliyopita ni asilimia 30 pekee ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo zilitolewa na kwamba asilimia 20 ya fedha hizo zilipotea.
Jana, idadi kubwa ya wabunge walionesha kuipokea kwa furaha kuu bajeti iliyosomwa na Dk. Mpango ambayo pamoja na mambo mengine ilitaja kuondoa ada ya mwaka ya leseni ya magari, kupunguza kodi ya bidhaa za mazao huku ikipandisha kodi ya mafuta na bia.

Matokeo Yamweka njiapanda Waziri Mkuu Uingereza

$
0
0

Theresa May

Uingereza. Matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika jana Alhamisi, nchini Uingereza yanaonyesha wazi kuwa hakuna chama kitakachopata ushindi mkubwa wa wabunge wa kukiwezesha kuunda serikali peke yake.

Hili ni pigo kwa Waziri Mkuu, Theresa May aliyeitisha uchaguzi wa mapema akiamini kuwa atapata uungwaji mkono na kuaminiwa, ili aweze kuongoza serikali peke na kuepuka serikali ya muungano.

Hakufanikiwa. May na chama chake cha Conservative anatarajiwa kupata ushindi wa viti 318, huku kile cha Labour kikitarajiwa kupata 262. Hadi asubuhi leo Ijumaa, Conservative ilikuwa na viti 314 na Labour 261 huku Bunge zima likiwa na wabunge 650.

Waziri Mkuu May amesema baada ya matokeo ya mwisho kutangazwa, kutakuwa na muda wa uthabiti huku kiongozi wa Chama cha Labour, Jeremy Corbyn akimtaka May ajiuzulu.

Conservative ilikuwa inahitaji viti 326 ili kuongoza serikali peke yake, lakini kwa namna mambo yalivyo, itabidi kupata uungwaji mkono kutoka chama kingine ili kuunda Serikali.

Haijafahamika iwapo May ataendelea kuongoza chama hicho kutokana na matokeo haya mabaya, kinyume na matarajio yake au atajiuzulu. Kazi kubwa iliyo mbele ya serikali mpya itakayoundwa ni kuendeleza na kufanikisha mchakato wa kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya.

Mkurugenzi wa Zamani FBI Amlipua Trump

$
0
0

Donald Trump
Washington, Marekani. Aliyekuwa Mkuu wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI), James Comey ameishtumu Ikulu ya Marekani kwa kumharibia jina na kusema uongo kuhusu shirika hilo.

Comey ambaye aliyefutwa kazi ghafla na Rais Donald Trump alisema hayo jana Alhamisi, baada ya kuanza kutoa ushahidi mbele ya maseneta nchini Marekani kuhusu tuhuma kwamba Urusi iliingilia Uchaguzi Mkuu wa Marekani mwaka uliopita.

Mkuu huyo wa zamani wa FBI amewaambia maseneta waliomhoji kuwa alikuwa na mazungmzo ya siri na Rais Trump. Aidha, ameshtumu matamshi ya Ikulu ya Marekani kuwa FBI ilikosa imani naye.

Trump alimfuta kazi Comey Mei 9, mwaka huu baada ya FBI kutangaza kuchunguza madai ya Urusi kuingilia Uchaguzi wa Marekani, madai ambayo Urusi imekanusha.

Comey amesema, Trump alimwambia asitishe mchakato wa FBI kumchunguza Michael Flynn, aliyekuwa mshauri wake wa masuala ya usalama wa Taifa kwa madai kuwa alikuwa na mawasiliano ya karibu na maofisa wa Urusi kipindi cha uchaguzi.

Rose Muhando, Hii Ni Fedheha Kubwa Kwako!

$
0
0
Rose Mhando
NI jambo lisilohitaji mjadala, kukubaliana kwamba Rose Muhando, ni mmoja wa watu ambao Muziki wa Injili Tanzania, una damu yake, hasa unapozungumzia kile kitendo cha kuutoa ndani ya nyumba za ibada na kuuleta nje, tena kwenye majukwaa.

Ndiyo, Gospo ni muziki wa ndani ya nyumba za ibada, ukipigwa na wanakwaya kwa miaka mingi hapa kwetu na ilipolazimika kutoka nje, basi ni kwenye matamasha ya shughuli za kidini na hakukuwahi kuwa na mtu mmoja aliyeweza kusimama peke yake kuimba.

Lakini Rose Muhando ni miongoni mwa waimbaji wa kwaya walioamini wanaweza kufanya vitu viwili kwa wakati mmoja, kuimba kwa kumsifu Mungu, lakini wakati huo huo wakajiingizia kipato.
Alifanya hivyo na akakubalika sana, kwani mashabiki wa nyimbo zake hawakuwa watu wa kanisani tu, hata watu wa imani nyingine walivutiwa na nyimbo zake.


Ndiye aliyekuwa kioo cha waimbaji wengine kujitokeza na kuonyesha uwezo wao, kiasi kwamba wengi wakaanza kumtumia kama chanzo cha mapato, akiitwa huku na kule kutumbuiza katika matamasha na zinduzi mbalimbali za albamu na nyimbo za wanakwaya wenzake.
Ukubwa wa jina na kazi yake ukawavutia hadi watu wa Sony Music ambao waliweza kuingia naye mkataba wa kumsimamia katika shughuli zake za muziki.

Kuwavutia watu kama Sony siyo jambo dogo, maana hawa jamaa wanafanya kazi kimataifa na wako na wasanii wengi dunia nzima. Achana na tuhuma za utumiaji wa madawa ya kulevya, acha ile ya maneno kuwa anazaa nje ya ndoa, maana hivi vitu ni kwa faida yake, afanye, asifanye shauri yake na maisha yake.

Lakini kuna hili jambo ambalo mwanzo lilianza kama tetesi, baadaye ikaja kujulikana kuwa ni kweli. Binafsi nimeshawahi kuzungumza naye juu ya hili jambo, akakataa kabisa, akitoa madai kuwa kuna watu wamejipanga kumchafua na anawajua. Ni hili la utapeli katika shoo zake.

Tuhuma zinasema Rose anachukua hela kwa ajili ya kushiriki matamasha ya nyimbo, lakini hatokei. Nimekutana na watu wengi wanaomlalamikia kuhusu tabia yake hii, ambayo tofauti na yale mawili ya mwanzo, hili ni jinai, linaweza kumfunga jela.

Huwezi Kuamini Haya Ndio Mambo 12 Yaliyowafanya Wabunge Washangilie Bajeti kuu ya Serikali

$
0
0
Bajeti ya Serikali
Mlipuko wa furaha kutoka kwa wabunge uliojitokeza jana wakati Serikali ilipotangaza kufutwa kwa ada ya mwaka ya leseni ya magari (motor vehicle licence), ulitosha kuonyesha ukubwa wa kero hiyo uliokuwapo kwa jamii.

Si kero hiyo tu, kelele za furaha kutoka kwa watunga sheria hao pia zilisikika kwa wingi ilipotangazwa kufutwa kwa ushuru wa usafirishaji wa mazao chini ya tani moja, ushuru wa huduma kwenye nyumba za kulala wageni na kutoza ushuru wa forodha wa asilimia sifuri badala ya 25 kwenye malighafi na vifaa vinavyoagizwa mahsusi kwa matumizi ya walemavu.

Zaidi ya mara mbili, Spika wa Bunge, Job Ndugai alilazimika kumtaka Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango kurudia alichokisema au kumwambia inatosha na anaweza akaishia hapo kwani wabunge wamemuelewa na hana haja ya kuendelea kuisoma bajeti hiyo.

Ijumaa ya Juni 2, mjadala mkubwa wa kuondolewa kwa ada ya road license uliibuka bungeni, kilio cha wabunge kikiwa ni kuwapo kwa magari ambayo yameegeshwa siku nyingi kutokana na ama ajali au uchakavu wa kutotumika tena hivyo kuitaka Serikali kuifuta ili kuwapa wananchi nafuu na kutoendelea kudaiwa.

Hoja hiyo iliyotolewa na Mbunge wa Busega (CCM), Dk Raphael Chegeni kwenye kipindi cha maswali na majibu ilichangiwa na wabunge wengi akiwamo Spika bila kujali itikadi zao za vyama vyao.

Hapakuwa na majibu ya uhakika siku hiyo kutoka kwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji ambaye aliishia kusema amelipokea pendekezo hilo na kwamba baada ya kukamilisha taratibu, Serikali itaona hatua sahihi za kuchukua.

Wiki hiyo ikielekea ukingoni, Dk Mpango ametangaza kuifuta sambamba na malimbikizo yake kwa wote waliokuwa wanadaiwa hivyo kuibua nderemo miongoni mwa wabunge hao walioonyesha kufurahishwa baada ya kusikilizwa na kufanyiwa kazi kwa maoni yao. “Serikali inatoa msamaha wa kodi, riba na adhabu zinazoambatana na madeni yote ya ada hiyo yaliyolimbikizwa kwa miaka ya nyuma,” alisema Waziri Mpango.

Bunge lilitawaliwa na kelele za CCM… CCM… CCM mara baada ya waziri huyo pia kutangaza kufuta ushuru kwenye usafirishaji wa mazao yasiyozidi tani moja pamoja na kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye vifaa vya walemavu vinavyotengenezwa nchini.

Ilikuwa hivyo pia alipotangaza mpango wa kuimarisha ukusanyaji wa mapato kwa kutoza asilimia sifuri ya ushuru wa forodha kwenye Mashine za Kielektroni (EFD) kutoka asilimia 10 zilizokuwapo.

Hali ilikuwa hivyo pia ilipotangazwa kuondolewa kwa tozo kwa nyumba za kulala wageni.

Kufutwa kwa ada ya ukaguzi wa viwango ukaguzi wa mionzi na ada ya Wakala wa Vipimo kwenye mbolea ni hatua nyingine iliyowafurahisha wawakilishi hao wa wananchi.

Korea Kaskazini Wazidi Kuwa Kichwa Ngumu....Warusha Makombora Yakutungua Meli za Kivita

$
0
0
Korea Kaskazini
 Pyongyang, Korea Kaskazini. Korea Kaskazini imesema makombora iliyoyafanyia majaribio jana Alhamisi ni mahsusi kwa ajili ya kushambulia ‘kundi la meli za kivita’ ambazo zimekuwa zikiitishia nchi hiyo.

Shirika la Habari la Serikali la KCNA limesema majaribio hayo ya jana ya makombora ya ardhini kwenda baharini ni ya hivi karibuni katika msururu wa vitendo vya ukiukaji wa vikwazo vya Umoja wa Mataifa na yalishuhudiwa na kiongozi wa nchi hiyo Kim Jong-Un.

Majaribio hayo yamefanyika siku moja baada ya Umoja wa Mataifa kuongeza makali ya vikwazo dhidi ya taifa hilo.

"Makombora hayo yaliyorushwa yaliweza kutambua kwa ufasaha vifaa vilivyolengwa vilivyokuwa vinaelea kwenye bahari ya mashariki mwa Korea," KCNA wamesema, wakizungumzia Bahari ya Japan, ambako kuna meli mbili kubwa za Marekani za kubeba ndege za kivita.

Korea Kaskazini inawezekana inazilenga meli za USS Carl Vinson na USS Ronald Reagan zilizoongoza mazoezi ya siku tatu ambayo yalimalizika Juni 3 yakihusisha meli zaidi ya 10 za kivita za Marekani pamoja na mbili za Japan. Mazoezi hayo yalionekana kulenga kuitisha Korea Kaskazini.

Marekani imezidisha shughuli zake za kuonyesha ubabe wa kijeshi eneo hilo, ambapo ina nyambizi inayotumia nguvu za nyuklia, USS Cheyenne yenye uzani wa tani 6,900.

Imegundulika Kumbe Baraka The Prince Ana Chuki Kwa Ben Pol na Jux...Chanzo Hichi Hapa

$
0
0
Baraka the Prince na Ben Pol
Hivi karibuni msanii kutokea Bongo flevani Baraka the prince aliingia kwenye headlines baada ya kuukosoa wimbo wa mwanamuziki Ben Pol “Tatu”na kusema wimbo ni mbaya na haukustahili mtu kupiga picha bila ya nguo kwa kiki ya nyimbo kama ile.

Sasa leo June 9, 2017 Ben Pol ametoa ya moyoni akiwa kwenye Ayo TV na millardayo.com akielezea kinachoendelea baina yake na Baraka The Prince hasa baada ya maoni kuhusu wimbo huo na namna alivyoyapokea…

Tazama Video Hapa Chini:

Wema Sepetu Amzimikia Rayvanny Amtabiria Makubwa Tuzo za BET

$
0
0
Wema Sepetu na Raymond

RayVanny ni msanii pekee kutoka Tanzania na Afrika Mashariki ambaye anatuwakilisha kwenye tuzo za BET zitakazofanyika Marekani baadaye mwezi huu akiwania Viewers Choice Awards ama (Pendekezo la Mashabiki ama watazamaji) huku BET wakitangaza namna ya kuwapigia kura wasanii ili washinde tuzo hizo.

Pamoja na baadhi ya mastaa kama Elizabeth Michael kumpigia na kumuombea  kura RayVanny kwenye kurasa zao za Social media, Wema Sepetu naye ametumia ukurasa wake wa Instagram kumpigia kura RayVanny akiandika:

Umechaguliwa tu kuwania lakini kwangu wewe ni mshindi tayari …Unastahili kabisa! V-Vanny Boy. Na haiishii hapa Tuendelee kupiga kura. 
Wasanii wanaowania tuzo ya Viewers Choice Awards pamoja na RayVnanny ni pamoja na  Dave (UK ) Jorja Smith (UK) Amanda Black (South Africa) Changmo (South Korea) Daniel Caesar (Canada) Remi (Australia) Skip Marley (Jamaica).

Vita Ya Malipo Kiduchu Haijawahi Kumuacha Modo Salama!

$
0
0
Amber Lulu
AMANDA Swartbooi moja kati ya wauza nyago katika video Afrika akitokea Afrika Kusini. Amanda ametokea kujizolea umaarufu kwa kipindi kifupi cha mwaka jana ambapo ametokea katika video kadhaa Afrika ikiwemo Coolest Kid ya Davido akimshirikisha Nasty C wa Afrika Kusini, Four4 ya JR pamoja na Show Me ya Rich Mavoko akiwa na Harmonize.

Licha ya kufanya poa huko, ameshawahi kukiri kuwa kuuza nyago katika video hizo kunamlipa kwani kumempa mafanikio ya kujisomesha katika Chuo Kikuu cha Afrika Kusini (UNISA) akiwa mwaka wa pili katika masomo ya biashara. Ukija Bongo wapo wauza nyago katika Video za Kibongo ambao ni ‘visu’ lakini wanaangushwa na malipo kiduchu kutoka kwa wasanii husika kiasi cha kufikia kuangalia kazi nyingine za kufanya huku baadhi wakijiingiza katika muziki.
Agness Masogange


Katika makala haya nimekuchambulia baadhi tu ya wauza nyago (modo)ambao vita hii ya malipo kiduchu haijawahi kuwaacha salama kwani wengine wameamua kuachana na kuuza sura na wengine kujiingiza katika kuimba.

Alikuja kwa kasi, akavuma katika Video ya Kwetu ya Rayvanny na baada ya hapo akatokomea. Kutokana na kuitendea haki video hiyo, wengi walimtabiri kama miongoni mwa wauza nyago watakaokuja kuliteka soko. Hajashiriki tena katika kuuza sura kwenye video nyingine hadi sasa huku ikisemekana kukwepa malipo kiduchu kwa kila anayemfuata kufanyanaye kazi.


Alianza kuuza sura katika Video ya Naogopa ya Mirror kisha katika Remix ya Burger Movie Selfie ya Belle9 na baada ya hapo aliamua kuachana na suala la kuuza nyago na kujiingiza rasmi kwenye Muziki wa Bongo Fleva. Lulu anasema malipo kiduchu na mastaa wengine wakitaka kumtumia bure katika video zao ndivyo vilivyomkimbiza kwenye kuuza sura na kuamua kuimba ambapo kwa sasa anabamba na Ngoma ya Usimuache.

lulu Diva
Ni modo ambaye pia muuza nyago katika video za Kibongo. Kutokana na malipo kiduchu katika video hizo kumemfanya kupotea kimyakimya katika orodha wauza sura Bongo. Ameshawahi kukiri kulipwa kiasi kikubwa katika video moja tu (Salome ya Diamond) tangu aingie katika kuuza nyago huku akiwa na kumbukumbu ya kulipwa kiduchu katika Video ya Magubegube ya Barnaba.
Gigy Money



Naye ni miongoni mwa wauza nyago walioanza kupotea kwenye ramani ya muziki Bongo kisa hazilipi. Alianza kutokea katika Video ya Masogange ya Belle9 na baada ya hapo akaonekana kwenye Video ya Magubegube ya Barnaba iliyotoka 2012. Mara ya mwisho kuonekana katika ulimwengu wa wauza nyago ilikuwa katika Video ya Msambinungwa ya Tunda Man akishirikiana na Ali Kiba iliyotoka mwanzoni mwa mwaka 2014.

Mkurugenzi wa Zamani FBI Amlipua Trump..!!!

$
0
0

Aliyekuwa Mkuu wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI), James Comey ameishtumu Ikulu ya Marekani kwa kumharibia jina na kusema uongo kuhusu shirika hilo.

Comey ambaye aliyefutwa kazi ghafla na Rais Donald Trump alisema hayo jana Alhamisi, baada ya kuanza kutoa ushahidi mbele ya maseneta nchini Marekani kuhusu tuhuma kwamba Urusi iliingilia Uchaguzi Mkuu wa Marekani mwaka uliopita.

Mkuu huyo wa zamani wa FBI amewaambia maseneta waliomhoji kuwa alikuwa na mazungmzo ya siri na Rais Trump. Aidha, ameshtumu matamshi ya Ikulu ya Marekani kuwa FBI ilikosa imani naye.

Trump alimfuta kazi Comey Mei 9, mwaka huu baada ya FBI kutangaza kuchunguza madai ya Urusi kuingilia Uchaguzi wa Marekani, madai ambayo Urusi imekanusha.

Comey amesema, Trump alimwambia asitishe mchakato wa FBI kumchunguza Michael Flynn, aliyekuwa mshauri wake wa masuala ya usalama wa Taifa kwa madai kuwa alikuwa na mawasiliano ya karibu na maofisa wa Urusi kipindi cha uchaguzi.

Exclusive. Hatimaye Nabii Frank Afichua Kiini cha Mauaji ya Kibiti na Rufiji..!!!

$
0
0

Akizungumza mapema asubuhi ya leo na Kituo cha Luninga cha Channel Ten na Magic fm Radio Nabii anayekuja kwa Kasi nchini Nabii Frank leo amefunguka na kueleza mambo makuu mawili ambayo ndiyo chanzo cha mauaji yanayoendelea Kibiti na Rufiji na amezitaka Mamlaka husika kuyafanyia Kazi ili kumaliza mauaji.

Amesema kwamba mauaji hayo yanatokana na sababu za Harakati za Kidini ( yaani kuna dini moja inataka kuwa ndiyo inayoaminika na kukubalika katika huo Ukanda hivyo wanaua Watu hasa wa dini fulani ili kuwatisha na wakimbie au wahame hayo maeneo na wabaki wao tu ) na sababu ya pili kasema kwamba Mfumo wa Kiuchumi wa Watu wa hayo maeneo umeharibiwa hivyo Wauwaji wameamua sasa kuwauwa wale wote ambao wanahisi ndiyo chanzo cha Mfumo wao huu kuharibiwa. Na inasemekana kwamba Mfumo mkubwa wa Kiuchumi au uingizaji Kipato kwa asiimia kubwa ya Watu wa hayo maeneo ni Mkaa na kama tunavyojua Serikali imepiga marufuku huku ikiweka Sheria kali dhidi ya wale watakaokamatwa.

Zitto: Tumemtoa Mghwira Ili Kuondoa Dhana Kwamba ACT ni "CCM B"..!!!!!

$
0
0

Mbunge wa Kigoma Mh Zitto Zuberi Kabwe ambaye pia ni kiongozi wa ACT wazalendo amesema kwamba wameamua kumuweka pembeni mwenyekiti wao wa zamani Mama Anna Mghirwa ili kutoa dhana kwamba ACT ni CCM B.

"Sasa tunaweka kanuni ambazo mtu akichaguliwa na uongozi wa juu unaoongozwa na Chama kingine tofauti na ACT basi tufanye kwanza mazungumzo kabla ya mtu kukubali tu bila kutoa taarifa" alisema Mh Zitto Kabwe.

Pia akaongeza kwa kusema kwamba kwa sasa wameshachagua kaimu mwenyekiti wao wa Chama na anaendelea na majukumu kama kawaida.

Kimenuka Act Wazalendoo..Baada ya Mgwhira Kuondolewa Uenyekiti Wake Juzi..Aibuka na Kutoa Povu Hili Zito kwa Kina Ziti na Wenzake Waliomtosa..!!!

$
0
0

Mkuu Mpya wa Mkoa wa Kilimanjaro Mh.Anna Mgwira amepinga kuondolewa uenyekiti wa ACT Wazalendo na kusema kuwa utaratibu haujazingatiwa. Mama Anna amesema bado anao uwezo wa kutumikia wana Kilimanjaro na chama chake pia.

Kiongozi Mkuu wa ACT alitangaza kuvuliwa uenyekiti kwa Anna Mgwira na nafasi hiyo kukaimishwa kwa mtu mwingine.

Ikumbukwe kwamba jana Mh.Mkuu wa Mkoa alifanya kikao na kamati kuu ya CCM mkoa wa Kilimanjaro jambo linalompa wakati mkuu katika kutumikia mabwana wawili

Chanzo: Nipashe

Meya Arusha Amjia Juu RC Gambo, Amtaka Amuombe Radhi..!!!

$
0
0

Meya wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro ametoa siku saba kwa  Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amuombe radhi kwa kosa la kumuweka ndani wakati alipokuwa anakabidhi rambirambi kwa wazazi waliofiwa kwenye ajali ya gari la Shule ya Msingi Lucky Vincent.

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo Ijumaa, Lazaro amesema mpaka sasa ameshindwa kuelewa ni kwanini mkuu huyo aliagiza meya pamoja na wenzake wakiwemo viongozi wa dini, madiwani, wawakilishi waliotoa rambirambi na mwenye shule kukamatwa na Jeshi la Polisi na kuwekwa ndani.

"Mimi sikuwa na shida na RC na kitendo cha kumuweka ndani kiongozi wa dini, paroko, kiongozi wa dini ya Kiislamu ni kitendo ambacho si cha kibinadamu na anapaswa aombe radhi umma,"amesema.

Pia, amemtaka kutafakari nafasi yake na kuona kuwa anafaa kuendelea kuwa mkuu wa Mkoa wa Arusha kwasababu ameonyesha kuwatumikia wananchi ambao hawaheshimu.

"Hana heshima na mbunge, madiwani, watu wenye degree zao, haheshimu viongozi wa dini halafu bado anataka uongozi,"amesema.

Manispaa ya Ubungo Yasaini Mikataba 30 Yenye Neema..!!!

$
0
0

Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo  imesaini mikataba 30 na wakandarasi mbalimbali kwa ajili ya kutekeleza shughuli za miradi ya maendeleo za halmashauri hiyo yenye miezi nane tangu kuanzishwa kwake.

Miongoni mwa miradi hiyo ni uboreshaji miundombinu ya maji na  huduma za afya katika Hospitali ya Sinza Palestina na usafi wa barabara za manispaa hiyo.

Mikataba hiyo imesainiwa leo Ijumaa kati ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo, John Kayombo, Meya  wa manispaa hiyo, Boniface Jacob na baadhi ya wakandarasi.

Halfa ya kusaini mkataba huo imefanyika katika ofisi za makao makuu ya manispaa hiyo zilizopo Kibamba.

Kayombo amewaeleza wanahabari kuwa mikataba hiyo ina thamani ya Sh4 bilioni na utekelezaji wake unatarajiwa kuanza wakati wowote.

Kwa upande wake, Jacob amesema wakarandasi waliopatikana wamefuata sheria na kanuni na hakuna aliyepata tenda kwa njia ya udanganyifu.

"Nikueleze tu mkurugenzi, mtu atakayeshindwa kutekeleza majukumu kwa ufanisi usisite kumchukulia hatua ikiwamo kusistisha mkataba wake,"amesema Jacob.

Duh..Kijana wa Kiume Akamatwa Akimfanyia Mtihani wa Chuo Mpenzi Wake wa Kike..!!!

$
0
0

Imetokea huko Zimbabwe,wote wamekamatwa wapo polisi kijana wa kiume alidai aliamua kumsaidia mpenzi wake maana amerudia mara nne anafeli tu.


Kamanda wa Pwani Afafanua Mauaji ya Watu Watatu..!!!

$
0
0

Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga amesema kwa taarifa alizonazo, watu wawili wamepigwa risasi katika kijiji cha Nyamisati, Kibiti, kisha waliofanya uhalifu huo kuwachukua majeruhi na kuondoka nao.

Awali taarifa zilizotolewa na mashuhuda wakazi wa kijiji hicho zilisema watu watatu wameuawa kwa kupigwa risasi usiku wa kuamkia leo.

Lakini akizungumza na Mwananchi leo asubuhi, Kamanda Lyanga amesema watu wawili wamejeruhiwa kwa risasi na wahalifu kutokomea nao kusikojulikana.

“Tunaendelea na uchunguzi.” Amesema Kamanda Lyanga
Viewing all 104771 articles
Browse latest View live




Latest Images