Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104431 articles
Browse latest View live

Ukweli Mchungu..Wabunge Waliotumia Muda Wao Kuishangilia Bajeti Wajipime Sana, ni Kitendo cha Aibu Walichofanya..!!!

0
0

Hawa watu sijui tuwaelimisheje. Wanakutana eti na kipengele cha kuondoa road license kwenye bajeti wanapiga makofi na kushangilia kijinga kabisa. 

Wakikutana na kipengele kigumu kwao wanakaa kimya kwa muda ila kikija kizuri tu kwa sura tena hata ambacho hawakielewi wanaanza kushangiliashangilia hovyo hovyo tu. 

Pale badala wangetumia muda wao kusikiliza kwa makini tena umakini mkubwa, wachambue na kuandika mambo muhimu wanabaki kupiga mayowe tu! 

Baada ya kutoka weupe jana kwa kushangiliashangilia kitakachofuata ni kuchangia vitu visivyo na maana na bajeti inapita na mapungufu yake mengi tunarudi tena mwakani na ujinga ule ule wa kila siku. 

Spika naye anaingia kwenye mkumbo wa ushangiliaji huku akiwa na lengo la "kuwaondoa wabunge wake wa CCM kwenye umakini kama ambavyo wanafanya siku zote" Huu ni utapeli wa kisiasa. 

Inakera sana kuwaona hawa watu wakifanya mambo ya kitoto kabisa.

Chanzo JF

Simba Sc Yasajili Wawili Kutoka Mwanza..Kaburu Adai Anamajina Mengine Sita Makubwa Yatasaini Simba Hivi Karibuni..!!

0
0

Klabu ya Simba SC imeanza kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao wa Kombe la Shirikisho la Afrika, baada ya jana kukamilisha usajili wa walinzi wawili kutoka jijini Mwanza.

Simba imevuta beki wa kushoto, Jamal Mwambeleko kutoka Mbao FC na beki wa kati Yussuf Mlipili kutoka Toto Africans ambao wote wametokea jijini Mwanza

Kwa mujibu wa Makamu wa Rais wa Simba SC, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ amesema kwamba, Mlipili amesaini miaka mitatu na Mwambeleko amesaini miaka miwili adai mchezaji Mlipili anatua kwa mara ya kwanza kabisa Simba SC, wakati Mwambeleko yeye ni kama anarudi nyumbani sababu amewahi kuchezea timu ya vijana ya Wekundu hao wa Msimbazi.

Mbali na hilo Kaburu baada ya kukamilisha usajili huo amesema mashabiki na wapenzi wa Simba wakae mkao wa kula kwa taarifa za kuvutia zaidi kuhusu usajili wa timu yao hiyo ambao unaendelea sasa.

“Kwa ujumla nina wachezaji sita ambao wamekwishakamilisha usajili wao hapa Simba, lakini nitakuwa nachomoa mmoja mmoja namtambulisha” Alijinasibu Kaburu 

Mlipili na Mwambeleko wote waliichezea Simba SC kwa mara ya kwanza kwenye mashindano ya SportsPesa Super Cup 2017 huku Simba ikitolewa kwa penalti 5-4 na Nakuru All Stars ya Kenya.

Okoa Ndoa Yako Sasa, Ongeza Maumbile, Nguvu na Hamu ya Tendo la Ndoa na Products za Markson

0
0


OKOA NDOA YAKO SASA. ONGEZA MAUMBILE, NGUVU NA HAMU YA TENDO LA NDOA HATA KWA WENYE KISUKARI.
Tatizo la maumbile madogo, nguvu za kiume na ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limekuwa likiwasumbua wengi na kusababisha kushindwa kujiamini ktk tendo hivyo kusababisha ndoa nyingi kuvunjika pamoja na mahusiano. Upungufu wa nguvu na hamu ya tendo husababisha mambo kama:-
(a)Uume kulegea wakati wa tendo
(b)Kukosa hamu ya tendo la ndoa
(C)Kuwahi kufika kileleni
(D)Uume kuchelewa kusimama baada ya round ya kwanza.
(E)Kuchoka sana baada ya round moja n.k
@Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo kwa kutumia bidhaa zilizotengenezwa kwa mimea na matunda zisizo na kemikali wala madhara na kuthibitishwa kiafya. Pata hizi👇👇👇👇
🍉 🌿🍅🍒🍍🍓🍉🍎🍀
1.HANDSOME UP ni kifaa chenye uwezo wa 99 % kuongeza uume (size unayohitaji) na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo hata mara 3 @130,000/=
Kwa Bidhaa hizi na nyingine kama:-
5.Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi @130,000/=
7.Kutengeneza shepu (hips, makalio na mapaja) @200,000/=
8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni @120,000/=
9.Kuwa mweupe na soft mwili mzima bila kuacha sugu 120,000/=
10.Kurudisha usichana (bikra) @120,000/=
11.Kupunguza au kuongeza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120,000/=
Wasiliana nasi kwa (+255)
0767447444 au 0714335378.
NB: Matokeo ni uhakika na garantii na upate risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii.
Follow us
@Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr

Hawa Hapa Waliochaguliwa Kidato cha Tano, Wanafunzi 3,000 Waliofaulu Waachwa..!!!

0
0

Serikali imetangaza orodha ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na vyuo vya ufundi kwa mwaka 2017 huku wanafunzi 2,999 wakiachwa.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), George Simbachawene ametoa idadi hiyo leo Juni 9, mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa ufaulu kwa mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 3.75 ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2015.

Amesema kati ya wanafunzi 96,018 waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu ni wanafunzi 93,019 pekee waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi.

Amesema kutokana na mwongozo wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wa Mei 15, 2017 jumla ya wanafunzi 93,019 ndiyo wenye Sifa za kuchaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi kwa kuwa wamefaulu kwa vigezo vyote vya msingi ambapo kati ya hao 92,998 ni wa shule na wanafunzi 21 ni wale waliosoma taasisi ya elimu ya watu wazima.

Aidha amewataka wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano kuwasili kwa wakati katika shule walizopangiwa Julai 17 mwaka huu na kwamba hakutakuwa na mabadiliko ya shule walizopangiwa.

"Na kama kuna mwanafunzi ambaye hataripoti kwenye shule aliyopangiwa kwa muda wa siku 14 nafasi yake itachukuliwa na mtu mwingine," amesema Simbachawene



Swali Pagawishi: Lowassa Angemuunga Mkono 2015 Tungekuwa Tunazungumzia Serikali ya CHADEMA/UKAWA..!!!?

0
0

CHADEMA walitapelewa sana 2015 - unaweza kuita ni utapeli wa juu kabisa wa kisiasa kuwahi kutokea nchini (the biggest political con in our history); hesabu zao ilikuwa ni kwamba Lowassa angekuja na watu wengi sana na hivyo itawapa uwezo wa kushinda hata mbinu chafu. Jinsi ya watetezi wa ujio wa Lowassa walivyoona wakati ule ni kuwa "Dr. Slaa hachaguliki" lakini Lowassa "anakubalika sana". Hawakuwahi kujiliza Lowassa anakubalika na nani na kwanini.

Na ushahidi unaonesha ni kweli Lowassa alikuja na "kura" nyingi zake kuliko kuja na watu wengi kumfuata hadharani. Walichosahau ni kuwa hawakutegemea kuwa baadhi ya watu wao wenyewe wangewakimbia hasa baada ya move ya Slaa kuondoka.

Ni rahisi kuona kuwa kuna uwezekano mkubwa sana watu waliokuwa wamfuata Lowassa "aliko waweko" wengi hawakutegemea kuwa angeenda CHADEMA. Wakati makundi ya vijana yalikuwa tayari kumfuata huko kuna ushahidi mkubwa makundi ya watu wazima na wazee wenye hekima hawakuwa tayari kufanya hivyo hata kama walikuwa tayari "kumpigia kura". Kitendo cha kukosekana watu wengi mashuhuri walioimba "tuna imani na Lowassa" kwenda kumfuata CHADEMA lilikuwa ni pigo kubwa sana kwa matumaini ya Lowassa ndani ya CHADEMA.

Ndugu zangu, nawahakikishia kama Lowassa angekuja alivyokuja lakini angesema amekuja kumuunga mkono Dr. Slaa katika kugombea Urais leo tungekuwa tunazungumzia mambo mengine kabisa... combination ya Lowassa, Slaa, Mbowe na inawezekana hata Zitto angemuunga mkono Slaa.. CCM wangetegemea zaidi kura zao wenyewe kuliko za wasio wana CCM.

Badala yake, kura za CCM zilimeguka kwenda na Lowassa CHADEMA na wakati huo huo kura za CHADEMA zikamegekuka kwa watu waliomkimbia Lowassa. Hili unaweza kuona kwenye baadhi ya matokeo ya Ubunge ambapo watu walikuwa tayari kumpa kura Mbunge wa CHADEMA lakini kwenye Urais wakampa Magufuli!

Alichofanya Magufuli kiukweli kabisa ni kujiuza yeye mwenyewe na siyo chama chake. Matokeo yake alivuta kura nyingi kwake yeye binafsi na hakuvuta kura nyingi kwa chama chake. Takwimu za uchaguzi zinaonesha wazi trend hii.

Kuelekea 2020 Zitto atakuwa eligible to run. CUF maskini ndio sijui tena maana sioni kupitia CUF nani mwingine baada ya Lipumba na Maalim kuvurugana. Lowassa hata akiamua kugombea tena sidhani kama itakuwa rahisi kivile tena na hasa katika mahali ambapo lile dubwasha a.k.a UKAWA limegeuka UKIWA wa IKAWA halipo tena.

Kwenye uchaguzi ambapo ndani atakuwepo Lowassa, Magufuli, Zitto (je Zitto anaweza kuungana na Lowassa kama Lowassa na Juma Duni Haji?) au mgombea wa chama chake kuna uwezekano kweli wa kuwa na matokeo tofauti?

Ni katika mazingira ya kumsimamisha nani katika upinzani kusimama dhidi ya Magufuli kutokea upinzani?

Lowassa
Lissu
Zitto
Nape (wakitoka/tolewa CCM)
Muhongo (akitoka/tolewa CCM)
Januari (akitoka CCM)

Au tuanze kuzungumzia siasa za 2025? na hii 2020 watu wasalimu amri bila hata kunyanyua mikono kujaribu?

Credit  - Mzee Mwanakijiji From jf

Wabunge wa CCM na Upinzani Watofautiana Kuhusu Bajeti ya Serikali...!!!

0
0

Wabunge wa CCM wameipongeza bajeti ya mwaka wa fedha 2017/18 wakisema inalenga kuondoa kero za wananchi wa hali ya chini huku wenzao wa upinzani wakisema ni bajeti ya maumivu kwa watu wa hali ya chini baada ya mafuta kuongezeka.

Wakitoa maoni yao kwa nyakati tofauti mara baada ya bajeti hiyo kusomwa bungeni jana, wabunge wa CCM walisema bajeti hiyo imemaliza kila kitu.

Mbunge wa Sumbawanga Mjini (CCM), Aeshi Hilaly alisema bajeti hiyo imekidhi matakwa ya wabunge ingawa bado hawajafahamu wananchi wataipokea vipi.

“Kimsingi yale tuliyokuwa tunayapinga mwaka jana, mwaka huu wameyaondoa. Nataka nimpongeze waziri ameleta bajeti nzuri sana tumeipokea kwa mikono miwili. Kazi iliyobaki ni kwenda kuipitia ili maeneo ya kurekebisha tufanye hivyo.

Mbunge wa Lupa (CCM), Victor Mwambalaswa alisema katika kipindi cha miaka 15 aliyokuwa ndani ya Bunge haijawahi kutokea bajeti nzuri iliyowalenga wananchi wa chini kama ya mwaka huu.

“Kwa mfano maeneo ya kodi katika mazao ya wakulima, pembejeo, mbolea na kodi za magari za kila mwaka. Ingekuwa ni uwezo wangu mimi hatuhitaji hata kuijadili, sema Katiba inasema tujadili,” alisema.

Mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea alisema kuwa ni jambo zuri kwa Serikali kuondoa kodi za magari za kila mwaka lakini kwa kuifidia katika mafuta kunalenga kumuongezea mzigo mwananchi wa hali ya chini.

“Eneo jingine ni kutegemea misaada kutoka nje na bahati mbaya wafadhili huwa hawatimizi masharti. Kuondoa kodi ya mabango kwenye halmashauri na kuipa TRA (Mamlaka ya Kodi Tanzania) jukumu la kukusanya, inaonyesha kuwa kuna njama katika halmashauri zinazoongozwa na wapinzani,” alisema na kufafanua:

“Halmashauri zenye mabango nyingi zipo mjini na zinaongozwa na upinzani. Hizi ndizo kodi kubwa ambazo halmashauri ilikuwa inategemea.”

Mbunge wa Vunjo (NCCR-Mageuzi), James Mbatia alisema bajeti hiyo ni changa la macho kwa sababu asilimia 37 ya fedha inategemea mikopo yenye masharti nafuu na misaada kutoka nje ya nchi.

“Pia Deni la Taifa limekua kutoka Sh39 trilioni hadi Sh50 trilioni, kwa maana hiyo kila Mtanzania anadaiwa zaidi ya Sh1 milioni,” alisema Mbatia.

“Ni maumivu kwa Watanzania, ni wangapi ambao wana magari lakini kwa kupeleka kodi ya magari katika mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa inamaanisha gharama za kusaga, usafiri na usafirishaji zitaongezeka,” alisema

Mbunge wa Mtwara Mjini (CUF), Maftaha Nachuma alisema ni bajeti ambayo imeakisi matakwa ya wananchi kwa kuondoa ushuru ambao ni kero kwenye maeneo mbalimbali.

“Kuondoa ushuru katika bidhaa zinazosafirishwa nje ya nchi ndiyo kilio chetu, sasa kitafanya watu ambao walikimbia kutumia bandari zetu kurejea na hivyo kukuza uchumi wa nchi,” alisema.

Mbunge wa Tarime Mjini (Chadema), Esther Matiku alisema kuondoa kodi ya mabango katika halmashauri kutashusha makusanyo ya halmashauri.

“Hizi halmashauri zilikuwa tayari zimepanga bajeti zao. Je, kulikuwa na mawasiliano kati ya halmashauri na Serikali Kuu kuhusu maeneo haya waliyoyaondoa kodi?” alihoji.     

Matokeo ya Uchaguzi Yamweka Njiapanda Waziri Mkuu Uingereza..!!!

0
0

Matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika jana Alhamisi, nchini Uingereza yanaonyesha wazi kuwa hakuna chama kitakachopata ushindi mkubwa wa wabunge wa kukiwezesha kuunda serikali peke yake.

Hili ni pigo kwa Waziri Mkuu, Theresa May aliyeitisha uchaguzi wa mapema akiamini kuwa atapata uungwaji mkono na kuaminiwa, ili aweze kuongoza serikali peke na kuepuka serikali ya muungano.

Hakufanikiwa. May na chama chake cha Conservative anatarajiwa kupata ushindi wa viti 318, huku kile cha Labour kikitarajiwa kupata 262. Hadi asubuhi leo Ijumaa, Conservative ilikuwa na viti 314 na Labour 261 huku Bunge zima likiwa na wabunge 650.

Waziri Mkuu May amesema baada ya matokeo ya mwisho kutangazwa, kutakuwa na muda wa uthabiti huku kiongozi wa Chama cha Labour, Jeremy Corbyn akimtaka May ajiuzulu.

Conservative ilikuwa inahitaji viti 326 ili kuongoza serikali peke yake, lakini kwa namna mambo yalivyo, itabidi kupata uungwaji mkono kutoka chama kingine ili kuunda Serikali.

Haijafahamika iwapo May ataendelea kuongoza chama hicho kutokana na matokeo haya mabaya, kinyume na matarajio yake au atajiuzulu. Kazi kubwa iliyo mbele ya serikali mpya itakayoundwa ni kuendeleza na kufanikisha mchakato wa kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya.

Jifunze Namna ya Kutumia Tsh 300000 Kama Mtaji wa Kufugia Kuku..!!!

0
0

Hapa tuta hitaji kuku 11 tu wakubwa wanaotaga yani majike 10 na Jogoo 1 tu. Kwa kutumia kuku hao 11 baada ya miezi mitatu unaweza ukawa na kuku mia Tatu (300) au na zaidi kama unataka.

Nunua kuku wako katika chanzo cha kuaminika kuepuka magonjwa usinunue kuku sehemu za masokoni au kwenye mabanda ya njiani au kuku wanao safirishwa kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine.Tafuta sehemu ya uhakika na nunua kuku wenye matunzo na kinga ili wasipatwe na magonjwa na wenye afya nzuri.

Unapo nunua kuku wakubwa kwanza unapo wafikisha wape chanjo ya mdondo (Newcastle vaccine) ili kuweka rekodi yako ya chanjo maana chanjo hii hurudiwa kila baada ya miezi 3. Ukumbuke tarehe uliyo wachanja na tarehe utakayo wachanja tena baadae.

Usinunue kuku kabla hujaandaa banda la kutosha kulingana na idadi ya kuku na kwa ajili ya badae kwa kuwa mradi utaongezeka kadri siku zinavyoenda na Chakula.

Katika sh. 300000 toa sh.69500 ambayo utanunua Chakula cha kuku, kuku hawa hawana formula ya Chakula hivyo unaweza kununua material ukachanganya Chakula mwenyewe ampapo utaokoa pesa nyingi pia.

Mchanganuo Wa 69500 ni:-
- Pumba gunia 1. Shs.20000 gunia la pumba lina kilo 70.

- Paraza kilo 25 = 700x25 =17500. Paraza ni mahindi yaliyo vunjwa vunjwa kwaajili ya Chakula cha kuku.

- Mashudu ya alizeti kilo 15. 700x15=10500

- Layer's consetraite kilo 25 kifuko. = 21500

Ukijumlisha utakuwa umepata kilo 135 kwa shs 69500. Ambapo kila kilo moja ya Chakula utakuwa umenunua kwa shiling 514.8.

Chakula hicho kichanganye kwa kutumia chepe kichanganye vizuri kichanganyike pumba lazima iwe kavu kabisa ikaushe usiwape kuku pumba mbichi.

Kumbuka kuku anayetaga anakula Gram 130 kwa siku hivyo kuku 10 watakula kilo 1.3 kwa siku ambayo ni gram 1300. Hivyo tutaweza kuona Chakula chetu kitatupeleka zaidi ya siku 100 ya zaidi ya miezi mitatu.

TOA SHS 170000 AMBAYO UTANUNULIA KUKU.


Mchanganuo wake

Kwa kila kuku mzuri ambaye ajazeeka anayetaga utampata kwa shilingi 15000 na Jogoo nzuri utampata kwa shilingi 20000.
Jogoo 1 = 20000
Majike 10 x15000= 150000 jumla 170000.
Itakuwa imebaki shs. 60500

Hii pesa iliyobaki ni kwa ajili ya kununu material ya bei nafuu na kutengeneza banda la kuku 10 hadi 20. Kuku hawa hawaitaji banda Kubwa kwasababu hawashindi ndani wataingia ndani wakati Wa kulala jiaoni na mchana wakati wa kutaga.

Kuku wachiwe eneo la kutosha na lenye mchanga watakao itumia kuoga kuondoa wadudu km papasi na utitiri sehemu wanayopenda kuoga nyunyizia Dawa ya utitiri.

Banda tengeneza la kuhamisha la futi 4x8x4 yani urefu kwenda juu futi 4 upana futi 8 kipenyo futi 4. Tumia materio yaliyo karibu nawe kama mirunda, mabanzi, Mabati reject au yaliyochakaa chicken wire au wire mesh, fito mbao 2x2 au 4x2 n.k. Kama ni sehemu za mjini litakugharimu kama Tsh 50,000-60,000.Vijijini au nje ya mji ambapo miti ni mingi litakugharimu Tsh 25,000 hadi 35,000.

Haya jinsi ya kuwaendeleza hao kuku ili kupata kuku wengi hadi utakao wataka. Hapa itabidi ukubali kupeleka Mayai sehemu ambapo wanatotolesha ambapo trey 1 ni shilingi 10000.

Hapa kuku hawa 10 watakupa wastani Wa Mayai 8 kwa siku ambapo kwa mwezi ni Mayai 240. Kila baada ya siku 7 peleka Mayai kwenye Mashine yakutotolea (incubator). Hivyo kwa mwezi utapeleka Mayai 240 utapata wastani Wa Vifaranga 200. Hivyo baada ya mwezi nakushauri usitotoleshe tena hao Vifaranga 200 ni wengi sana kwa kuanzia kwa kuwa tayari tunenunua Chakula cha kuku cha kutupeleka miezi mitatu basi Mayai utakayo endelea kuokota utayauza kwaajili ya kupata hela ya Chakula cha Vifaranga watakao toka hao zaidi ya 200.

Hivyo mradi huu utakuwa unajiendesha wenyewe. Nikiwa na maana kama kuku 10 watakupa wastani Wa Mayai 8 kwa siku na Mayai 240 kwa mwezi ni wazi kwamba kuku hao wanakuingizia 120000 kwa mwezi ambaya sasa hela Hii itatumika kununua Chakula cha kulea hao Vifaranga ambapo Mayai ya mwezi tu yataweza kununua Chakula ambacho Vifaranga 200 watakula mwezi pamoja na chanjo na Dawa zote.

Hivyo baada ya miezi mitatu utakuwa na Vifaranga wakubwa Wa miezi miwili na Chakula cha kuku wakubwa ndo kitakuwa kinaishia hapa utachanganya Chakula cha aina moja tu wale Vifaranga watakuwa wameshakuwa kiasi cha kula Chakula chochote.Kumbuka kujibana ili kuongeza banda.


Lulu Michael Amzimikia Mwanamuziki Aslay...Adai Ndio Mfalme Wake

0
0

Kupitia mtandao wa Twitter wa Mwandada huyo ameonesha mapenzi ya wazi wazi ya ushabiki wake kwa Mwanamuzili Aslay kwa kuandika "Aslay ni Mfalme wangu wa Bongo Fleva🙌🏿🙌🏿 Ni Moto🔥Anaunguza🔥🔥🔥🔥🔥🔥" Lulu amezitaja nyimbo 3 za Aslay alizoachia hivi karibuni na kusema zote ni kali.

Hatari ya Matumizi ya Chumvi, Fahamu Njia ya Kuepuka Matumizi ya Chumvi Nyingi Kwenye Chakula..!!!

0
0

Miili yetu inahitaji chumvi kwa kiasi kidogo sana kwasababu chumvi huupatia mwili madini ya Sodium ambayo huhitajika kusafirisha taarifa za mfumo wa fahamu n.k.

Matumizi ya chumvi nyingi huongeza uwezekano wa kupata shinikizo kubwa la damu ambalo pia huweza kuchangia uwezekano wa kupata magonjwa mengine sugu kama yale ya figo, moyo na pia mifupa kama "Osteoporosis".

Jinsi ya Kupunguza Matumizi ya Chumvi
1. Mpishi wa familia anahitajika kupunguza chumvi inayowekwa kwenye chakula wakati wa kuandaa au kupika chakula na ni vyema akaambiwa wazi kuhusu madhara yatokanayo na ulaji wa chumvi nyingi.

2. Epuka kuweka chumvi mezani, kwa kuwa huchangia walaji kuongeza chumvi bila hata kuonja.

3. Epuka ulaji wa vyakula vilivyosindikwa kwa kutumia au kuongezwa chumvi, kama nguru aliyekaushwa kwa chumvi pamoja na baadhi ya vyakula vya makopo au paketi.

4. Soma lebo kwa makini wakati wa manunuzi ya bidhaa zako na uchague vyakula vilivyosindikwa bila ya chumvi iliyoongezwa.

5. Jenga utamaduni wa kula vyakula fresh unavyopika mwenyewe kwani itakuwa kwako ni rahisi kutambua kiasi cha chumvi unachotumia.

China Waisifia Bajeti ya Tanzania Iliyosomwa Bungeni Hivi Karibuni..!!!

0
0

Balozi wa China nchini, Lu Youging amempongeza Rais John Magufuli na Serikali kwa bajeti nzuri iliyowasilishwa jana, Juni 8 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Phillip Mpango.

Balozi Youging ametoa pongezi hizo jana (Ijumaa) Ikulu jijini hapa alikokwenda kufanya mazungumzo na Rais.

Amesema bajeti hiyo imeakisi dhamira za kuongeza kasi ya maendeleo katika sekta mbalimbali za ikiwamo ya ujenzi na miundombinu.

“Lakini pamoja na bajeti nzuri kuwasilishwa uchumi wa Tanzania umeendelea kuimarika na kuwavutia wadau wengi wa maendeleo kuwekeza nchini,” amesema.

Ameongeza kuwa Tanzania inapewa kipaumbele na nchi ya China na kwamba Serikali ya nchi hiyo itaendelea kuwashawishi wawekezaji wengi zaidi kuwekeza hapa nchini.


Simba Yafanya Kufuru Kumsajili Emmanuel Okwi Kwa Dau la Dola 50,000..!!!

0
0

AKITUA tu nchini na kumalizana na Simba, mshambuliaji mwenye kasi na mwendo wa kuyumba uwanjani, Emmanuel Anorld Okwi ndiye atakuwa mchezaji ghali zaidi wa Simba.

Simba imejipanga kumalizana na Okwi kwa dau la dola 50,000 (Sh milioni 110), pia atakabidhiwa nyumba ya kuishi katika maeneo ya Sinza, Mbezi Beach au Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Simba, tayari kupitia kamati ya ufundi na ile ya usajili, wamekubaliana kuwa Okwi ndiye chaguo namba moja kwa wachezaji wa kigeni.

Juzi, Okwi aliliambia Championi kutoka Senegal kwamba bado hawajafanya mazungumzo “siriaz” na Simba, lakini wakikubaliana yuko tayari kuja.

Imeelezwa kwa kuwa Okwi yuko huru, yaani hana mkataba na Sports Club Villa anayoichezea, kamati hiyo imekuwa ikipambana kuhakikisha dau hilo linashuka angalau kufikia dola 25,000 (Sh milioni 55).

Kiongozi mwingine anayehusika na usajili alisema: “Fedha hizo ni nyingi sana, Okwi hana mkataba na Villa, hivyo najua itapungua ili kuhakikisha mambo yanakwenda vizuri. Simba tungependa kununua wachezaji kwa kupunguza gharama.”

Habari kutoka ndani ya Simba tayari wanahangaika kupata fedha hizo na tayari kiasi fulani kimepatikana tayari kumshusha Okwi Dar es Salaam.

“Kamati imepitisha na tumekubaliana, tunataka mtu wa kuamua matokeo timu inapokuwa imezidiwa. Tunataka mtu wa kushirikiana na wenzake kumaliza kazi na Okwi hatuna shida naye,” alisema.

Kama hiyo haitoshi, imeelezwa mmoja wa wanachama wenye nazo ndani ya Simba, yeye ameamua kutoa gari lake ili Okwi awe analitumia wakati akiwa Tanzania.

Mganda huyo yupo Senegal ambako timu ya taifa ya Uganda, The Cranes imeweka kambi na wikiendi hii inacheza dhidi ya Ivory Coast.

Baada ya hapo, Okwi atarejea Kampala na matumaini makubwa kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa, dili litakuwa limefungwa na Okwi kutangazwa rasmi huku akirudishiwa jezi yake namba 25.

Credit - Champion

Ubuyu wa MotoMoto...Zari Ataka Kuzichapa Kikao Cha Familia ya Ivan, Kisa Maamuzi ya Kushangaza Kuhusu Mirathi Yake..!!!

0
0

Watatoana roho Yarabi kwa mali alizoacha marehemu! Wengi walitabiri kuwa, kufuatia mtifuano mkali juu ya mali alizoziacha mumewe aliyefariki dunia Mei 25, mwaka huu, Ivan Ssemwanga ‘Don Ivan’, aliyekuwa mkewe, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, ipo siku atazichapa kavukavu na hasimu wake aliyekuwa msiri mkubwa wa baba watoto wake huyo, Lawrence Muyanja ‘King Lawrence’.

WATAKA KUVUNJANA SHINGO

Hicho ndicho kilichodaiwa kujiri hivi karibuni ambapo Zari na King Lawrence, ilibidi waamuliwe baada ya kutaka kuvunjana shingo kwenye kikao cha familia ya Ivan kilichofanyika nyumbani kwa marehemu, Muyenga jijini Kampala, Uganda. Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika kilichoutonya mtandao maarufu wa habari za udaku nchini humo, Zari na King Lawrence walitaka kutoana roho mbele ya ndugu wa karibu waliokuwa wamekutana kujadili jinsi mali zilizoachwa na marehemu Ivan zitakavyosimamiwa.

UAMUZI WA KUSHANGAZA

Ilidaiwa kuwa, kilichosababisha tafrani hiyo ni kufuatia familia ya Ivan kupitisha uamuzi wa kushangaza kwamba, mali hizo zisimamiwe na King Lawrence, jambo ambalo lilimfanya Zari acharuke kisha kuvaana na jamaa huyo kabla ya kuamuliwa na kikao kuvunjika kwa muda. Hata hivyo, ilielezwa kuwa, katikati ya kikao hicho, familia ilidai kutoa tamko hilo kama mapendekezo tu ili kufungua mjadala wa ishu hiyo kwa sababu King Lawrence alisemekana kujua orodha ya mali zote za Ivan, lakini Zari aligeuka mbogo na macho yake kubadilika rangi na kuwa mekundu.

 ZARI KAMA COBRA

“Sijawahi kumuona Zari akiwa na uchungu au hasira kama ilivyokuwa kwenye kikao kile. Alionekana kama cobra (aina ya nyoka mwenye sumu kali) aliyekuwa kwenye mawindo yake huku akitema sumu,” kilikaririwa chanzo hicho kikieleza ‘mudi’ aliyokuwa nayo Zari aliyekuwa na wanawe watatu aliozaa na Ivan baada ya kusikia kauli hiyo ya familia. Sosi mwingine aliyehudhuria kikao hicho alikaririwa akisema kuwa, katika kikao hicho, ulifika muda Zari akashindwa kuendelea kuwepo hivyo aliondoka huku akifoka kwa hasira. “Wewe (King Lawrence) ni maskini uliyekuwa unamganda Ivan kama kupe anavyomnyonya ng’ombe damu na sasa unajifanya kujua sana mali zake.

ZARI: NAMCHUKIA KING LAWRENCE

“Wewe (King Lawrence) bila Ivan ulikuwa hujui utakula nini. Sasa kwa kuwa amekufa, unawaza utapata wapi chakula? Nakuchukia,” alisikika Zari huku akiondoka kwenye kikao hicho kwa hasira na watoto wake.

KING LAWRENCE: NAMCHUKIA ZARI

Ilidaiwa kuwa, awali, King Lawrence hakuwepo Uganda na hata mazishi ya Ivan hakuhudhuria kutokana na kuchelewa ndege kutoka nchini Afrika Kusini lakini alipotua tu nchini humo aliingia kwenye vita nzito na Zari juu ya umiliki wa mali alizoziacha Ivan zikitaka kuwatoa roho. “Namchukia Zari kwa sababu anafanya mambo ya kitoto na siyo kama mama,” alisema King

Lawrence katika mahojiano ya simu na chombo kimoja cha habari nchini humo baada ya kikao hicho.

KING LAWRENCE AIBUA JIPYA

Ilielezwa kuwa, King Lawrence amekuwa akisema kuwa anajua vitu vingi kuhusiana na Ivan hivyo kuibua jipya juu ya nyumba ya mojawapo ya nyumba za marehemu Ivan. King Lawrence amekuwa akidai kwamba, hata nyumba ya Ivan ya Muyenga, Kampala ambayo ndipo msiba uliopowekwa kabla ya kwenda kupumzishwa kijijini Nakalilo, siyo ya marehemu kama ambavyo watu wengi wanajua hivyo. “Ni nyumba yangu. Kama kuna watu wanabisha, wanaweza na wanahitaji kuona nyaraka, waje nitawaonesha,” alikaririwa King Lawrence aliyedaiwa kuwa ni binamu wa Ivan. Hata hivyo, kikao hicho ambacho pia kilidaiwa kuhudhuriwa na baba wa Zari, Hassan Tiale kilimalizika kwa kuundwa kamati ya watu wanne kwa ajili ya kusimamia mali za marehemu Ivan.

HATIMAYE ZARI UHAKIKA

Ilielezwa kuwa, kamati hiyo ilimpa jukumu la kwanza Zari kusimamia mali hizo hadi watoto aliozaa na Ivan watakapofikisha umri wa miaka 18. Wengine waliochaguliwa kwenye kamati hiyo ni Ritah Ssemwanga (dada wa Ivan),

King Lawrence na George Ssemwanga ambaye ni kaka mkubwa wa Ivan. Katika makubaliano hayo, Zari alitakiwa kusimamia shule za Ivan zilizoko Afrika Kusini kikiwemo chuo chake cha Brooklyn na nyumba mbili zilizopo Sandton na Pretoria, Afrika Kusini. Pia Zari alitakiwa kuishi na watoto wake wote kwenye nyumba moja na nyingine ipangishwe ili kujipatia kipato kwa ajili ya malezi ya watoto hao.

ZARI VS KING LAWRENCE

Zari na King Lawrence wamekuwa kwenye mtifuano kwa muda mrefu hata enzi za uhai wa Ivan ambapo King Lawrence alikuwa akimtuhumu Zari kumwacha Ivan na kumsababishia ‘stresi’. Wakati Ivan akiwa amelazwa kwenye Hospitali ya Steve Biko huko Pretoria, Afrika Kusini, wawili hao walidaiwa kutibuana kiasi cha kutimuliwa na madaktari kwenye chumba cha wagonjwa.

Gigy Money - Nakonda Ili Kumridhisha Mo J..!!!

0
0

BAADA ya kuonekana amepungua katika picha mbalimbali za mitandaoni na kuzua minong’ono kwa baadhi ya mashabiki wake, Gift Stanford (Gig Money) amefunguka na kusema kuwa mpenzi wake, Mo J, ndiye anayetaka apungue.

Gigy ameongeza kwamba, mwonekano huo ndio unaoendana na umri wake, kwa kuwa bado msichana mdogo kiumri, hivyo mwili mkubwa kwake haumuonyeshi uhalisia wake.

“Mimi ni msichana mdogo, hivyo kuwa na mwili mkubwa siyo poa, lakini pia namridhisha mpenzi wangu Mo J, anapenda nikiwa hivi, anasema ndiyo navutia zaidi,” alisema Gigy, msichana asiyeishiwa vituko.

Hata hivyo, Gigy alisema wanaomfikiria vibaya kwamba anaumwa watakuwa wanakosea, amejipunguza unene kutokana na matakwa ya mpenzi wake anayempenda na hataki kupingana naye katika hilo.

Familia ya Ivan Yamtenganisha Zari na Diamond Kiaina..Yamtaka aishi Aishi Afrika Kusini na Watoto wa Ivan..!!!

0
0

KAMATI ya watu wanne walioteuliwa kushughulikia namna ambavyo mali za marehemu Ivan Ssemwanga zitasimamiwa, imempa mpenzi wa mkali wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, Zari Hassan, moja ya nyumba za marehemu huyo iliyopo nchini Afrika Kusini ili aishi na watoto wake.

Kwa mjibu wa mtandao wa Kenya moja, kamati hiyo iliwajumuisha Ritah Ssemwanga (dada wa Ivan), George Ssemwanga Pinto (kaka wa Ivan), Lawrence Kiyingi Muyanja maarufu King Lawrence (rafiki mkubwa wa Ivan) ambaye pia ni kiongozi wa kundi la matajiri wanaojiita (Rich Gang) na Zari Hassan (mke wa Ivan).

Kwa pamoja kamati hiyo imekubaliana kwamba licha ya kumpa Zari nyumba hiyo, pia imempa madaraka ya kusimamia chuo cha Ivan cha Brooklyn, kilichopo Afrika Kusini.

Pia Zari ameamliwa kuishi na watoto wake katika moja ya nyumba za Ivan zilizopo Afrika Kusini na nyingine itapangishwa ili kusaidia familia hiyo kiuchumi, huku kamati hiyo ikiendelea na usimamizi wa jumla hadi watoto hao watakapofikia umri wa kujitambua wa miaka 18.

Kutokana na hilo, Zari ameondoka Uganda na kuelekea Afrika Kusini, ingawa bado haijajulikana kama ataishi katika moja ya nyumba za Ivan huko Pretoria, Afrika Kusini au ataishi na watoto wake kwenye nyumba ya mpenzi wake, Diamond Platnumz, aliyonunua jijini Johannesburg.

Wema Sepetu Alia Kuwa Staa..Adai ni Mateso..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo Jumamosi ya 10/6/2017..!!!

MEYA wa Rusha Calist na Mkuu wa Mkoa Gambo Mtafutano Waendelea

0
0
Meya Calist Kushoto, RC Gambo kulia
 
Meya wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro, amempa siku saba Mkuu wa Mkoa Arusha, Mrisho Gambo kumwomba radhi yeye na viongozi wa dini aliowaweka ndani wakati wakijiandaa kupokea rambirambi ya wafiwa wa wanafunzi wa shule ya Lucky Vincent.

Akizungumza leo na waandishi wa habari Arusha, Meya Calist amesema kitendo cha kuwakamata wakiwa wamekusanyika shuleni hapo Mei 18, mwaka huu, kilikuwa ni ukiukwaji wa sheria na kwamba kabla ya kuwakamata alitakiwa awe na amri ya mahakama inayofafanua ukamataji wao, lakini haikuwa hivyo jambo ambalo anadai kuwa ni matumizi mabaya ya madaraka

Hata hivyo Mh. Calist amesema kuwa Mh. Gambo asipofanya hivyo baada ya siku hizo atampeleka mahakamani kwa kuwadhalilisha na kuwaweka ndani bila kosa lolote kwa kuwa hadi sasa hawajaambiwa kosa lao lilikuwa lipi.

AFANDE Sele Aibuka na Kuwapa Tano Wavuta Sigara...Adai Taifa Liendelee Kuwaombea

0
0
Afande Sele
Msanii Afande Sele amefunguka na kusema kama Taifa tunakila sababu ya kuendelea kuwaombea watu wanaovuta sigara na walevi wa pombe kwa kuwa kila mwaka ndiyo watu ambao wanaibuka vinara kwenye kuchangia kulijenga taifa kwa mapato.

Afande Sele amesema hayo baada ya jana Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango kuwasilisha bungeni mapendekezo ya makadirio ya bajeti ya serikali kwa mwaka 2017/18 ambapo Afande Sele anakiri kuwa ni kweli bajeti hiyo ni nzuri na kusema kama Taifa halijawahi kuwa na bajeti mbaya sana bali huwa na tatizo kubwa katika utekelezaji wa mipango hiyo.

"Kweli bajeti ya mwaka huu ni nzuri sana kabisa. Ingawa kama Taifa hatujawahi kuwa na bajeti mbaya sana. Lakini tumewahi kuwa na utekelezaji mbaya sana wa malengo ya bajeti miaka yote. Mipango siyo matumizi haya basi tuendelee kuwaheshimu na kuwaombea walevi na wavutaji wasigome, wasiugue na ikibidi wasife mapema ili waendelee kuwa vinara wa kulichangia na kulijenga Taifa kupitia ongezeko la kodi kwa bidhaa zao kila mwaka" alisema Afande Sele
Afande Sele alisema haya baada ya serikali kuendelea kupandisha kiwango cha ushuru kwenye vinywaji baridi, bia pamoja na sigara.

SASA Madereva Kucharazwa Viboko - Massauni

0
0
Viboko
Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Naibu Waziri Wa Mambo ya Ndani Massauni amefunguka na kusema hivi sasa madereva ambao watakuwa wakikiuka makosa ya barabarani wanapaswa kuchukuliwa hatua kali ikiwezekana hata kuchalazwa viboko.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamadi Massauni
Massauni amesema hayo leo wakati akitoa taarifa ya tathimini ya utekelezaji wa mpango wa mkakati wa kupunguza ajali barabarani nchini kwa asilimia 10 katika kipindi cha miezi sita kuanzia Agosti 2016 hadi Januari 2017.

"Suala la kwanza tunataka kulipa kipaumbele ambalo hatukufanikiwa katika mkakati wetu wa kwanza ni kuhusu NUKTA katika leseni za udereva tulisema tuanze lakini hatukufanikiwa lakini suala la pili ni kuchukua hatua kali dhidi ya madereva wanaokiuka sheria za usalama barabarani, ikibidi hata kuwachapa viboko maana lazima muda mwingine twende hivyo hatua zitakuwa kali sana safari hii" alisema Massauni 

Mbali na hilo Massauni alisema pia watu wengine ambao wanapaswa kuchukulia hatua kali ni pamoja na wauzaji wa pikipiki ambao wanauza pikipiki bila kubadilisha usajili na umiliki wa pikipiki zao na kuziuza, pia na watu ambao wanamiliki leseni za udereva ambazo ni feki wanatakiwa kutafutwa na kukamatwa.

Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid, Je? Unapata Pesa Haikai? Umeachwa na Mpenzi, Mke au Mme Anakusumbua?

0
0
Tiba Asili

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI. (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 72 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI: 

SHEKH SHARIFU RASHID ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran dawa za asili dawa za kiarabu, na njiwa, Anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango kwa kina mama, ngiri maji na n.k, anakuvutia mali zilizo potea au kudhulumiwa, pia anatoa Pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali, Wenye matatizo ya uzazi, jini mahaba, mapepo ya kichawi, vifungo vya kimaisha, ndoto mbaya za usiku, uelewa mdogo wa ufahamu shuleni kwa watoto wote, pia anauwezo mkubwa wa kumaliza kazi zilizoachwa na wataalamu wengine ndani ya masaa 48 tu, Pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo. WASILIANA NAE KWA WhatsApp na SIMU NO: +255 718-668347 na +255 767-204308 , +255 685-224047 Email shekhsharifurashidi@gmail.com. 

USHAURI: ni vyema kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate huduma kwa haraka.
Viewing all 104431 articles
Browse latest View live




Latest Images