Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104690 articles
Browse latest View live

STARS Kuianza Safari ya Cameroon Leo kwa Kishindo...Mbwana Samatta Afunguka

$
0
0
Mbwana Samatta
Mbwana Samatta

KOCHA Mkuu wa timu soka yaTaifa, Taifa Stars, Salum Mayanga amejigamba kuifunga Lesotho leo katika mechi ya kutafuta kufuzu fainali za michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) 2019.

Mechi hiyo ya kukata na shoka inatarajiwa kuchezwa saa 2 usiku katika uwanja wa Azam, Chamazi, Jijini Dar es Salaam. Mayanga alisema jana, wamefanya maandalizi ya kutosha kwa ajili ya mchezo huo hivyo wana matumaini makubwa ya kushinda.

Alisema miezi miwili iliyopita walicheza michezo miwili ya kirafiki na walipiga kambi ya ndani na nje nchini Misri. “Tunacheza na timu nzuri ambayo msimu uliopita ilionesha kiwango kizuri katika mashindano haya. Pia nimeangalia mechi ambazo wamecheza nyuma na kugundua udhaifu wao upo wapi,” alisema Mayanga.

Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta alisema timu ipo vizuri na wachezaji wamejiandaa vizuri kushinda. Kocha wa Lesotho, Moses Malieho alisema nao wamejiandaa vizuri kwa sababu wanafahamu Tanzania siyo timu rahisi.

Alisema amefuatilia michezo ya Taifa Stars ya nyuma waliyocheza na Nigeria na Botswana na kubaini maeneo yenye upungufu atakaoutumia ili kuwashinda. “Tulijiandaa kwa kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Msumbiji na kushinda 1-0 lakini tumekuja kupambana kwani Tanzania si timu ya kubeza,” alisema.

Viingilio vya mchezo huo vimepangwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuwa Sh 5,000 viti vya kawaida na Sh10,000 VIP. Katika michuano hii ya AFCON, Tanzania iko kundi L na Lesotho, Uganda na Cape Verde. Timu itakayoongoza kundi ndiyo itafuzu kwa fainali za 2019 Cameroon.

Ongeza Hips, Makalio, Mapaja, Miguu, Uume na Nguvu za Kiume, Kuwa Mweupe na Kuondoa Madoa Bila Madhara

$
0
0
Tiba Mbadala
OKOA NDOA YAKO SASA. ONGEZA MAUMBILE, NGUVU NA HAMU YA TENDO LA NDOA HATA KWA WENYE KISUKARI. 

Tatizo la maumbile madogo, nguvu za kiume na ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limekuwa likiwasumbua wengi na kusababisha kushindwa kujiamini ktk tendo hivyo kusababisha ndoa nyingi kuvunjika pamoja na mahusiano. Upungufu wa nguvu na hamu ya tendo husababisha mambo kama:-
(a)Uume kulegea wakati wa tendo 
(b)Kukosa hamu ya tendo la ndoa 
(C)Kuwahi kufika kileleni 
(D)Uume kuchelewa kusimama baada ya round ya kwanza. 
(E)Kuchoka sana baada ya round moja n.k 
@Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo kwa kutumia bidhaa zilizotengenezwa kwa mimea na matunda zisizo na kemikali wala madhara na kuthibitishwa kiafya. Pata hizi👇👇👇👇
🍉 🌿🍅🍒🍍🍓🍉🍎🍀

1.HANDSOME UP ni kifaa chenye uwezo wa 99 % kuongeza uume (size unayohitaji) na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo hata mara 3 @130,000/=
Kwa Bidhaa hizi na nyingine kama:-
5.Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi @130,000/=
7.Kutengeneza shepu (hips, makalio na mapaja) @200,000/= 
8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni @120,000/=
9.Kuwa mweupe na soft mwili mzima bila kuacha sugu 120,000/=
10.Kurudisha usichana (bikra) @120,000/=
11.Kupunguza au kuongeza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120,000/=
Wasiliana nasi kwa (+255)
0767447444 au 0714335378.
NB: Matokeo ni uhakika na garantii na upate risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii.

SHAMSA Ford :Ninaweza Kufa Kwa Presha Nikiongezewa Mke wa Pili

$
0
0
Shamsa Ford na Mumewe Chid Mapenzi
Muigizaji wa filamu bongo Shamsa Ford amefunguka na kusema kwamba hataweza kukubali Mume wake kuongeza mke wa pili kama hataweza kumpa sababu maalumu kwa kuwa anaamini anamtosheleza mume wake kwa kila kitu.

Shamsa amefunguka hayo kwenye FNL na kusema kuwa wivu alionao juu ya mume wake hafikirii kama atakubali kirahisi kuongezewa mke mwenza huku akiwa hana matatizo yoyote,

"Wivu nilionao siwezi kukubali kuongezewa mke wa pili hata mume wangu (Rashid) anajua kwa sababu yeye mwenyewe ana wivu sana na mimi. Ukweli kabisa nahisi ninaweza hata kufa kwa presha nikiongezewa mke wa pili. Inabidi kwanza kabisa kabla ya kuniomba aoe, anatakiwa anipe sababu za msingi kwannii anaamua kufanya hivyo na ikiwa sababu zinamashiko na mimi nikazielewa basi nitamruhusu kwa kuwa dini inasema hivyo kwa sababu pia ni ibada. Lakini kama hazina msingi siwezi kukubali kwa sababu naamini namtosheleza kwa kila mtu na sina kasoro yoyote", Shamsa aliongeza

Pamoja na hayo Shamsa ameweka wazi malengo ya kuongeza mtoto mwingine kwani amekuwa akipata usumbufu kutoka kwa mwanae ambaye kila siku amekuwa akisisitiza kuomba mdogo kae.

SERIKALI Itoe Tamko Rasmi: Daudi Albert Bashite ni Nani?

$
0
0
Bashite
Huu mjadala si wa kisiasa. Mkuu (Mh. Rais) alisema wenye vyeti feki waachie ofisi ifikapo May 15, 2017. Huu ulikuwa msamaha na wote watakao kaidi wafungwe miaka 7. Sasa Gwajima askofu kafafanua kila kitu ila serikali haikanushi wala kutoa tamko kuhusu ukweli wa Daud Abert Bashite.

Naomba kama kweli kutoka Kolomije s/msingi ni Daudi bashite, Pamba secondary ni Daudi Bashite (zero kama anavyosema Gwajima na mjue Gwajima yuko youtube live na dunia yote mwenye internet anamwona na kumsikia). Ni aibu kwa nchi kutangazwa vibaya kwa mteule wa rais.

Toeni tamko kama gwajima, kolomije na Pamba Sec ni waongo au wakweli ila rais aamue kulingana na madaraka yake kuhusu DAB.
Ramadhani Kareem.

MWANAUME Afariki Dunia Akiwa Gesti

$
0
0
Mwanaume Afariki Gesti
MKAZI wa Uvinza mkoani Kigoma, Idris Sadala (65), amekutwa amefariki dunia kwenye nyumba ya wageni ya wageni ya New Legeza Mwendo iliyoko mtaa wa Kisangani, Manispaa ya Kigoma/Ujiji.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Ferdinand Mtui, alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 11:40 jioni  kwenye nyumba hiyo na kwamba Sadala alikutwa amefariki dunia katika chumba alichokuwa amepanga.

Alisema Sadala alifika kwenye nyumba hiyo Juni 6, mwaka huu na kupanga chumba namba 101 na siku iliyofuata saa 12 jioni, aliingia chumbani kulala na hakuamka tena.

Kamanda Mtui alisema juzi baada ya baada ya kuona ukimya umetawala katika chumba chake, wahudumu wa nyumba hiyo walienda kutoa taarika katika kituo kikuu cha polisi kwa kutoonekana kwa mteja wao kwa muda wa siku mbili tangu alipoingia kulala.

Kutokana na taarifa hizo, mtui alisema polisi walifika  eneo la tukio na kufungua mlango wa chumba na kukuta mgeni huyo akiwa amefariki dunia.

Alisema ndani ya chumba hicho, polisi walikuta chupa moja ya soda aina ya Coca Cola ikiwa imebaki kidogo na chupa ya maji pamoja na vibahasha vinne vya dawa mbalimbali za hospitali ambazo bado hazijatambuliwa na watalaamu wa afya.

Kutokana na hali hiyo, alisema polisi walichukua mwili wa marehemu na kuupeleka katika Hospitali ya Rufani ya Mkoa Maweni kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi pamoja na kutambuliwa na ndugu.

Pia alisema chanzo cha kifo hicho bado hakijafahamika na uchunguzi wa kifo hicho unaendelea.

Kamanda Mtui aliwataka wamiliki wote wa nyumba za wageni kuchukua taarifa muhimu za wateja wao pindi wanapowasili zikiwomo jina, kazi, mahali anakoishi, anakotoka na anakokwenda.

Kwa kufanya hivyo, Mtui alisema itakuwa rahisi pindi wateja hao wana[pokumbwa na matatizo ikiwamo vifo.

BILL Nas Aupiga Chini Mziki..Sababu Hizi Hapa

$
0
0

MSANII wa Bongo Fleva, Bill Nas amefunguka kuwa kwa sasa ameamua kuupiga chini muziki ili kuhakikisha anashiriki vyema na kutumia muda wake wote kwenye masomo aliyobakiza katika Chuo cha Biashara (CBE).

Akichonga na Mikito Nusunusu, Bill Nas alisema kuwa, chuoni hapo anaposomea masomo ya ‘Procurement and Supply’ amebakiza muda wa mwezi mmoja ambapo katika kipindi hicho akiwa bize na masomo ameamua kuweka kando masuala yote yanayohusiana na muziki.

“Shule ni muhimu pia, nimeamua katika kipindi hiki cha kumalizia masomo niweke kwanza muziki pembeni mpaka pale nitakapomaliza ili niweze kufanya vyema katika masomo maana kuchanganya mambo mawili kwa wakati mmoja ni ngumu,” alisema Bill Nas.

ANNA Mghwira Amng'oa Kiongozi ACT Wazalendo Baada ya Kuteuliwa

$
0
0

Ikiwa ni Siku chache baada ya Mwenyekiti wa Chama cha Act-Wazalendo Anna Mghwira kuteuliwa kuwa Mkuu wa Mkao wa Kilimanjaro leo ameibuka Katibu wa chama hicho Mkoa wa Mbeya  Bahati Longopa na kutangaza kujiuzuluzu nafasi hiyo kwa alichodai kutoridhia uteuzi huo

Longopa amesema  kuendelea kuwa kiongozi wa chama kutampa wakati mgumu kuhamasisha wanachama wapya katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2020.
Amesema kuwa kwa hiari yake ameacha nafasi hiyo ndani ya chama kutokana na kitendo cha viongozi wa juu wa Chama hicho kuingia ndani ya Seriklai iliyopo madarakani ambayo ni ya chama pinzania kwao wao viongozi wa chini hawataweza kuwashawishi wanachama wapya kujiunga na chama hicho
Kuhusu kujiunga na chama  kingine cha siasa amesema kwa sasa ni mapema mno kuzungumzia hilo kwani ataendelea kukaa pembeni na kutojihususisha kwenye mambo ya siasa  huku akitafakari nini cha kufanya.
Mwenyekiti wa ACT- Wazalendo, Wilaya ya Mbeya, Ally Mbika alisema wamepata taarifa  za chini chini, lakini kama chama bado hawajakabidhiwa barua yoyote kutoka kwa kada huyo kutamka kujiuzulu rasmi. 
Amesema  wanasubiri  kukabidhiwa  rasmi ili kuweza kulizungumzia kwa vyombo vya habari barua na  viongozi wa chama  watapitia katiba yao na kupata mwongozo na kuangalia namna ya  kuziba nafasi hiyo mpaka Uchaguzi  Mkuu  wa  mwaka 2020. 
Mbika amesema kuwa kujiengua kwa kada huyo ni pigo kwa chama kwani alikuwa ana mchango mkubwa wa ushawishi na kujenga umoja na mshikamano wa kweli wa ndani na nje ya mkoa.

TAARIFA ya Ikulu kuhusu kamati ya Pili Mchanga wa Dhahabu

$
0
0

Taarifa ya Ikulu kuhu

Kamati ya Pili iliyoundwa na rais kuchunguza Mchanga wa Dhahabu imekamilisha kazi yake na kwambwa itakabidhi ripoti ya such unguis wao Tarehe 12 Juni Mwaka

IGP Sirro: Hatulali Tunafanya uchunguzi wa Kina mauaji ya Kibiti

$
0
0

Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro amewataka Watanzania wawe wavumilivu kwa kuwa Polisi wanafanya uchunguzi wa kina kuhusu mauaji yanayoendelea mkoani Pwani.

Sirro ameyasema hayo leo (Jumamosi) katika ziara yake ya kwanza mkoani Morogoro tangu ateuliwe kuwa IGP na kusisitiza kuwa polisi wanafanya kazi usiku kucha kudumisha hali ya usalama.

“Hatulali, tunafanya kazi kwa juhudi kubwa, lakini ni lazima wananchi watupe ushirikiano na nyinyi waandishi wa habari pia mnatakiwa mwandike kwa hekima bila uchochezi,” amesema.

Sirro amesema amefanya ziara hiyo Morogoro na katika maeneo mengine nchini ili kuzungumza na polisi namna ya  kusimamia ulinzi na usalama katika maeneo yao.

Irene Uwoya: Bongo Movie Hatuna Hela, Magari na Nguo Huwa Tunaazima na Hatuna Raha Kuwa Wasanii..!!!

$
0
0

Msanii wa bongomovie Irene Uwoya amedai wasanii wa Bongo movie hawana hela na vitu na maisha wanayoonekana wanayo ni vya kuazima na sio vya kwao

Amedai inabidi waazima kwa kuwa ni maarufu na wanaona soo kuonekana hawana hela wakati wana majina makubwa na hii inawafanya wakose raha kuwa wasanii

Ripoti ya Kamati ya Pili Uchunguzi wa Mchanga wa Madini Kutua kwa Magufuli Jumatatu..!!!

$
0
0


Rais John Magufuli, Jumatatu atapokea taarifa ya kamati ya pili ya wachumi na wanasheria iliyofanya uchunguzi wa madini yaliyo kwenye makontena yenye mchanga wa madini (makinikia) yaliyopo katika maeneo mbalimbali nchini.

Taarifa iliyotolewa leo (Jumamosi) na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema tukio hilo litarushwa hewani moja kwa moja kupitia redio, televisheni, mitandao ya kijamii na tovuti rasmi ya Ikulu ambayo ni www.ikulu.go.tz kuanzia saa 3:30 asubuhi.

Ikulu imewakaribisha wananchi kufuatilia matangazo hayo kupitia vyombo hivyo au simu za mkononi kwa kutembelea tovuti hiyo.

Mei 24, Rais Magufuli alipokea ripoti ya kamati ya kwanza yenye wajumbe wanane iliyochunguza aina na viwango vya madini yaliyomo kwenye mchanga wa madini uliomo ndani ya makontena yaliyozuiliwa na Serikali kusafirishwa nje ya nchi.

Kamati hiyo aliiteua Machi 29, mwaka huu ikiwa na wajumbe ambao ni wana taaluma katika fani za jiolojia, kemia, uhandisi kemikali na uhandisi uchenjuaji madini.

Baada ya kuipokea ripoti hiyo, Rais Magufuli alitengua uteuzi wa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.

Rais Magufuli pia aliivunja Bodi ya Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA) na kumsimamisha kazi mkurugenzi mtendaji wake.

Mwigulu: Nilitegemea Mawakili Wakubwa na Wasomi Kama Lissu Wajitokeze na Kuanza Kuwashitaki ACACIA..!!!

$
0
0

Akiwa Singida Mwigulu Nchemba amesema watu wa Singida wana matatizo kidogo kutokana na Kaka yao, Mwanasheria Tundu Lissu kutetea watu wanaoibia rasilimali za Tanzania na kutishia tutashitakiwa.

Amesema pia alitegemea mawakili wakubwa na wasomi wajitokeze na kuanza kuwashitaki ACACIA.

TPA Yasaini Mkataba na Wachina wa Kupanua Bandari ya Dar,Itakuwa na Uwezo Mkubwa Kuliko Zote Katika Bahari ya Hindi..!!!

$
0
0

Mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imesaini mkataba wa upanuzi na uongezaji wa kina cha bandari utakaowezesha bandari ya Dar es Salaam kupokea meli kubwa za mizigo na kushindana na bandari nyingine katika pwani ya bahari ya hindi.

Upanuzi huo utakaofanywa na kampuni ya China Harbor Construction ya China utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 336 na utadumu kwa miezi 36, ambapo utahusisha uongezaji wa kina cha lango la bandari na uongezaji wa kina cha maji kati ya gati namba 0, 1 hadi 7.

Akizungumza katika hafla ya utiaji saini mkataba huo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amesema hatua hiyo inalenga kuifufua upya bandari ya Dar es Salaam ili ifanye kazi kwa ushindani na kuhudumia wateja wengi kuliko ilivyo sasa.

“ Kukamilika kwa upanuzi na uongezaji wa kina cha maji katika gati namba 1 hadi 7 kutoka mita 8 hadi 15 kutawezesha meli kubwa na za kisasa zenye uwezo wa kubeba hadi makontena elfu kumi na tisa kutia nanga katika bandari ya Dar es Salaam na kuongeza ufanisi na kukuza uchumi wa Tanzania”, amesema Prof. Mbarawa.

Aidha Prof. Mbarawa amesisitiza kuwa pamoja na upanuzi wa bandari ya Dar es Salaam Serikali inaendelea na ujenzi wa miundombinu wezeshi ya reli na barabara ili kuhakikisha mizigo haikai muda mrefu bandarini.

“Ujenzi wa reli ya kisasa ya Standard Gauge toka Dare s Salaam hadi Kanda ya Ziwa na Kigoma na ufufuaji wa reli ya Tazara kutawezesha bandari ya Dar e s Salaam kufanya kazi kwa ufanisi na kuvutia wafanyabiashara wengi hivyo nawataka wafanyakazi wote wa bandari kufanyakazi kwa bidii na uadilifu”, amesisitiza Prof. Mbarawa.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TPA Eng. Deusdedit Kakoko amesema kiasi cha dola za Marekani milioni 421, kitapatikana kwaajili ya ujenzi huo ambapo kati ya fedha hizo Benki ya Dunia itatoa mkopo wa masharti nafuu wa dola milioni 345.

Kukamilika kwa ujenzi huo kutaondoa adha ya baadhi ya meli kusubiri kwa muda mrefu kupata nafasi ya kutia nanga na kutaongeza hadhi ya bandari ya Dar es salaam na kuvutia wasafirishaji wengi kutoka ndani na nje ya nchi.

IRENE Uwoya Atumbua Jibu..Adai Maisha ya Wasanii ni Duni Kiasi Huwa Wanaazima Nguo

$
0
0

Msanii wa bongomovie Irene Uwoya amedai wasanii wa Bongo movie hawana hela na vitu na maisha wanayoonekana wanayo ni vya kuazima na sio vya kwao

Amedai inabidi waazima kwa kuwa ni maarufu na wanaona soo kuonekana hawana hela wakati wana majina makubwa na hii inawafanya wakose raha kuwa wasanii.

Hivi Ndivyo Tsh 40 za Mafuta Katika Bajeti ya Serikali Zinavyowafanya Watu Wapige Kelele Mjini..!!!

$
0
0

Kwa bajeti ya Sh31.7 trilioni, ongezeko la Sh40 katika mafuta lisingetegemewa kuibua mjadala mzito, lakini hali imekuwa tofauti; wako waliolipokea kwa mikono miwili na wako wanaolipinga kwa nguvu zote.

Ongezeko hilo lilitajwa wakati Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alipokuwa akieleza mapendekezo kadhaa ya sheria ya kodi na ushuru, na hasa kuondolewa kwa kodi ya leseni ya magari.

Ushuru huo sasa utalipiwa mara moja tu wakati wa kusajili gari.

Dk Mpango alisema badala ya kodi hiyo iliyoondolewa, ambayo ilikuwa kati ya Sh150,000 na Sh250,000, Serikali sasa itatoza Sh40 kwa kila lita ya mafuta ya taa, petroli na dizeli.

Awali ilionekana kama tozo hiyo itakuwa ya kuwasaidia wamiliki wa magari tu, lakini mjadala ulioibuka umetoa picha tofauti.

“Ushuru huo wa mafuta utapandisha bei za bidhaa na huduma na hivyo watakaoathirika ni wananchi wote,” alisema Profesa Honest Ngowi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe.

“Ushuru ulioongezwa katika mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa, utabebwa na kila mwananchi anayetumia bidhaa na huduma mbalimbali.”

Alisema ushuru huo utasababisha bei ya mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa kupanda na kwamba gharama hiyo itafidiwa na mlaji wa mwisho ambaye ni mwananchi.

Alisema mmiliki wa gari ndogo ya abiria akipandishiwa gharama ya petroli kutokana na kuongezwa kwa ushuru huo, naye atapandisha bei ya huduma yake.

Alisema mwenye lori pia atapandisha gharama za kusafirisha bidhaa na mazao, hivyo gharama hizo zitafidiwa na mnunuzi wa mazao na bidhaa.

Alisema matokeo yake gharama za vyakula na bidhaa zinaweza kupanda ili kufidia ongezeko hilo la bei ya mafuta.

“Mafuta ni kila kitu, ukipanda daladala ukienda sokoni kununua vyakula, ukiwa mkulima au mfugaji utachangia gharama za ushuru wa mafuta,” alisema.

Dhana kama hiyo alikuwa nayo mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Haji Semboja, ambaye hata hivyo alisema mabadiliko hayo yatamuhusisha kila mtu katika kuchangia barabara badala ya wamiliki wa magari pekee.

“Kabla ya bajeti hii, kodi ya barabara ililipiwa na wenye magari, lakini sasa wapandaji wote wa magari watasaidiana na wamiliki kulipia gharama ya ushuru wa mafuta,” alisema.

Alisema utaratibu huo wa kushirikisha jamii yote kulipia kodi ni ubunifu mzuri wa kuipatia Serikali fedha nyingi zaidi kuliko ilivyokuwa ikifanyika awali kwa kuwabana wenye magari pekee yao.

Kwa upande wake, Godfey Mramba ambaye ni mtaalam wa kodi alisema ingawa ongezeko hilo si kubwa, kila mtumiaji wa barabara atachangia ushuru huo wa mafuta.

“Hii ina mwenye basi, mwenye bajaji na abiria watalipia gharama, mwenye trekta, mkulima na mlaji wa vyakula watalipia kupitia ushuru huu wa mafuta,” alisema.

Msomi mwingine aliyekubaliana na mabadiliko hayo ya kuondolewa kwa kodi ya magari ni Ali Mufuruki, ofisa mtendaji mkuu wa kampuni ya Infotech ya jijini Dar es Salaam.

“Sasa utalipia kodi kwa kadri utakavyotumia gari,” alisema Mufuruki katika mahojiano na gazeti la Mwananchi.

Alisema mtu asiyetumia gari maana yake hatanunua mafuta na hivyo hatalipia ushuru huo wa Sh40 kwa lita kwa kuwa hatatumia mafuta.

Mwenye mawazo tofauti alikuwa mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Kasheku, maarufu kwa jina la Msukuma, ambaye alishangazwa na kitendo cha Serikali kuitikia mapema kilio cha kuondoa kodi ya leseni za magari.

Akizungumza na kituo cha redio cha Clouds FM, Msukuma alisema suala hilo liliibuka katika kipindi cha maswali na majibu bungeni, lakini likakuzwa na mjadala.

Alisema anashangaa jinsi lilivyokuwa kubwa hadi Serikali ikakubali kuliondoa wakati wakulima wana malalamiko ya muda mrefu ambayo hayafanyiwi kazi.

Alisema kuondoa kwa kodi hiyo hakuwezi kuwanufaisha wakulima na wafugaji ambao sasa wanalazimika kupunguza ng’ombe kutokana na hali ngumu wakati kimila wanatakiwa watoe mahari hadi ya ng’ombe 100.

Wamiliki wa magari wanena

Kwa mujibu wa mapendekezo hayo, mtu anayenunua gari lenye injini ya ukubwa wa cc 3,000, atalipia hadi Sh300,000 wakati akisajili badala ya Sh 250,000 ambazo angekuwa akilipia kila mwaka kwa mujibu wa sheria ya sasa.

Hali kadhalika kwa mtu atakayenunua gari lenye injini ya ukubwa wa cc 1501-2500 atakayelipia Sh250,000 badala wakati wa kulisajili na anayenunua gari la cc 501-1500 atalipia Sh200,000 badala ya Sh150,000 alizotakiwa kulipia kila mwaka.

Akizungumzia mapendekezo hayo, mmiliki wa gari aina ya Toyota Brevis yenye cc 3000, Nelson Mashambu alipongeza hatua hiyo kwa vile itawabana wajanja wachache waliokuwa wakitoa taarifa za uongo kwa Mamlaka ya Mapato nchini(TRA).

Mkazi huyo wa eneo la Kimara anayetumia kati ya lita 10-15 za mafuta kwa siku, alisema baadhi ya wamiliki wa magari wamekuwa wakitoa taarifa za uongo kwa TRA kwa kutoa idadi ndogo ya magari ili wakwepe kulipa kodi ya barabara.

“Mimi naona uamuzi huu ni mzuri kwa vile unaweza kumkuta mtu anamiliki magari matano lakini baadaye anaandika barua TRA akisema gari yake moja mbovu haitumii lakini sasa hata kama utadanganya utakamatwa kwenye mafuta,” alisema.

Hoja inayofanana na hiyo ilitolewa pia na mfanyabiashara anayejishughulisha na usafirishaji abiria , Richard Matiku.

Matiku, anayemiliki gari aina ya Toyota Hiace, alisema uamuzi huo umewaondolea usumbufu wananchi ambao wakati mwingine walilazimika kulipia kodi hata magari ambayo yalikuwa hayatembei.

Lakini alionyesha wasiwasi wake namna Serikali itakavyoweza kukusanya kodi hiyo inayokusudiwa kuongezwa kwenye mafuta akisema baadhi ya vituo vya kuuzia mafuta hayo havina mashine za kielektroniki.

Mwananchi mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Robin Fungameza ambaye ni mkazi wa Kibaha alilalamikia mfumo huo mpya akisema unawabana wamiliki wengi wa magari.

“Hili jambo siliafiki hata kidogo. Fikiria mimi dereva natoka Dar narudi nyumbani Kibaha halafu njiani nakutana na bonge la foleni, itanilazimu kusimama ili nipate angalau bia chache kusubiria foleni,” alisema.

“Sasa unafika kwenye bia nako kodi imeongeza ...jamani sasa tutapumulia wapi?”     

Ukweli Mchungu..Sakata la Kibiti Mwigulu Nchemba ni Wakati wa Kujitafakari na Kujiuzulu Ateuliwe Adadi Rajab..!!!

$
0
0

Watanzania wengi tu tumechoshwa na Mauaji kibiti.

Hii wizara inahitaji wataalam wa mambo ya ulinzi na wabobezi kama Adadi Rajabu. Ushauri wangu Mwigulu sio strategic katika hili yeye ni mchumi , haitaji eleimu ya Chuo kikuu kuona kuwa kakwama 100%; Tunaweza sema tatizo lilikuwa IGP , katolewa IGP bado wembe ni ule ule. niwakati wa Mwigulu kuchukua maamuzi magumu ya kuachia ngazi ; Kama Ally Hassani Mwinyi , kule Shinyanga.

Si wa kwanza . Kaenda mpaka Kibiti kafanya Mikutano , Karusha picha za watuhumiwa na Donge nono . Bado Fail

Chanzo JF

Picha ya Utupu ya Amber Rose Yafutwa..!!!

$
0
0

Mtandao wa kijamii wa Instagram wenye watumiaji zaidi ya milioni 500 duniani umefuta picha ya utupu ya mwanamitindo Amber Rose.

Picha hiyo ambayo Amber aliiweka kwenye mtandao huo, ilifutwa kutokana na kukosa maadili. Mara nyingi mtandao huo huziondoa picha ambazo zinaripotiwa kutokuwa na maadili.

Baada ya kufutwa picha hiyo ya utupu ambayo imewatoa udenda vidume wengi mitandaoni, Amber ameandika ujumbe mwingine kwenye mtandao huo unaoonyesha masikitiko yake baada ya kufutiwa picha hiyo huku mashabiki wakimuunga mkono kwa kitendo hicho.

Ripoti hii Itamuumbua Tundu Lissu Kama Ile ya Kwanza Ilivyomuumbua Zitto Kabwe..!!!

$
0
0

Kama Kawaida Rais Magufuli huwa hafanyi vitu kwa Kubahatisha Mmeshambiwa Mkangeze Airtime za Ving'amuzi vyenu siku ya Jumatatu ni Disaster the report Must drag out some People nadhani Mnakumbuka Kile Kijembe chake cha ukiwa Mwanasheria Unaogopa Kesi?

Mpaka Sasa Katika Budget iliyosomwa Bungeni Sijaona Makosa Makubwa na Wachumi wengi wa  wako Kimyaa 

Ngoja tusikilize Na Wale Vijana wa Acacia kaeni Mkao wa Kula Ripoti hii itamfuta Tundu Lissu kwenye Siasa za Tanzania.

Chanzo JF

Jay Moe - Nilisoma na Rais wa Congo Joseph Kabila..Kipindi Hiko Nilikua Sijui Kama Tz Kuna Nyumba za Udongo..!!!

$
0
0

Msanii wa Bongo Fleva, Jay Moe ameeleza changamoto alizokumbana nazo shule hadi kupelekea kutoa albamu ya Ulimwengu Ndio Mama, licha ya hiyo kuna vitu ambavyo anajivunia ikiwemo kusoma shule moja na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Joseph Kabila.

Rapper huyo amesema kutokana na kukulia maisha ya kishua hadi unafika wakati ambao anaenda boarding school alikuwa hajui kama kuna nyumba za udongo nchini zaidi ya kuziona kwenye movie za Vietnam.

Ameeleza kuwa wakati anaenda Mbeya kuanza form one mwaka 1993 ndipo alianza kuona nyumba za udongo kitu kilichomfanya kuanza kulia lakini baba yake na ndugu zake walipomueleza kuwa amekua hivyo hana budi kuachana na mambo ya kitoto na kupambana.

“Siku ya kwanza nilipofika Irambo (secondary) jamaa wameniibia begi la mamisosi, kwa hiyo kule ndipo nilipojifunza maisha kiasi kwamba nilipofika form three mzee wangu alitaka anihamishie Dar es Salaam lakini ikamwambi hapana mimi nabaki, nimeshazoea ingawa maisha ni magumu,” Jay Moe amekiambia kipindi cha The Play List cha Times FM.

“Kingine kinacho-inspire  image mimi nimesoma na Joseph Kabila  ambaye ni Rais wa kongo, nimesoma na Cesi, nimesoma na Clara ambao wote ni watoto wa mzee Kabila.  Mimi nikiwa form two Jose ndio anamaliza form six na alikuwa kaka mkuu wa shule, kwa hiyo nilijifunza kama huna mama basi, kuna ulimwengu ambao utakufunza kama mama,” amesema Jay Moe

Uteuzi wa Mghwira Kuwa Mkuu wa Mkoa Wamtoa Povu Hashim Rungwe..Adai Rais Adipewe Madaraka ya Kuteua Teua Ovyo..!!!

$
0
0

Mgombea wa urais mwaka 2015, kupitia chama cha CHAUMA, wakili msomi Hashimu Rungwe amesema Rais Magufuli achague wote na kwamba achague na wabunge toka upinzani na sio kama njia inayofanywa sasa ya kuteua tu wapinzani walioandaliwa na vyama vyao.

Rais asipewe madaraka ya kuchagua kila mtu apendavyo yeye. Na katiba ya nchi inatakiwa kubadilishwa na kuwekwa sawa.
Viewing all 104690 articles
Browse latest View live




Latest Images