Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104667 articles
Browse latest View live

Kocha wa Lesotho afurahia sare na Tanzania

$
0
0

Kocha wa timu ya taifa ya Lesotho Moses Maliehe amesema kupata sare ugenini ni matokeo bora kwao ukizingatia walikuwa wanapambana na timu yenye uwezo mkubwa.

Matokeo ya sare kwa upande wetu ni mazuri kwa sababu unapocheza mechi ugenini hutakiwi kushambulia mwanzo mwisho kwa timu kama Tanzania kwa sababu wana kasi na kama nilivyotangulia kusema mwanzo Tanzania ni timu nzuri.

“Tunafurahi kupata sare ugenini na tumecheza kama tulivyopanga awali dhidi ya Tanzania, sare ni matokeo bora sana kwetu.”

Maliehe amesema walikuja wakiwa na lengo la kushinda lakini kutokana na ubora uliooneshwa na Stars hawakufanikiwa kupata ushindi badala yake wakaambulia sare ya kufungana bao 1-1.

“Tulijipanga kushinda lakini haikuwezekana kwa sababu tumecheza na timu nzuri (Tanzania) wanakimbia sana uwanjani .”

“Mchezo ulikuwa mgumu sana na tulitarajia hivyo kwa sababu tulikuwa tunacheza ugenini, ukiangalia wachezaji wangu walicheza kwa kujituma kwa dakika zote.”

Tanzania itajipanga tena kwa ajili ya mechi ya mwezi ujao dhidi ya Rwanda kuwania kufuzu michuano ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani maarufu kama CHAN.

China Wazindua Basi la Ajabu Linaloruhusu Magari Kupita Chini Yake..Linaweza Kupakia Abiria Zaidi ya 300 kwa Mkupuo..!!

$
0
0



CHINA inaendelea kufanya makubwa kwenye ulimwengu wa teknalojia na sasa inazindua basi kubwa la aina yake ambalo kwa chini litaruhusu magari mengine kupita kama ilivyo kwenye daraja.

Mfumo huu mpya wa usafiri ni sawa na mwendo kasi zinazohudumia wakazi wa Jiji la Dar es Salaam lakini huu ni wa kisasa zaidi.


Basi hilo lenye mita mbili kwenda juu linaitwa TEB na litaanza kuhudumia umma wa Wachina kuanzia Agosti mwaka huu.

Likitumia nguvu ya umeme, basi hilo linauwezo wa kubeba hadi abiria 300 kwa mara moja huku likiwa na urefu wa futi 72 na upana wa futi 25. Basi hili litaweza kupita hata sehemu yenye foleni kwa sababu ya upana wake na nafasi ya wazi iliyo kwa chini ikiyaacha magari mengine kwenye foleni

Video ya basi hilo la kwanza kutengenezwa, ilizua mjadala huku likiwashangaza wengi baada ya kuwekwa hadhari mwishoni mwa Mei.

Majaribio ya basi hilo tayari yameshafanyika katika mji wa Qinhuangdao ulioko kaskazini mashariki mwa China.

Basi hilo ambalo lina uwazi mkubwa chini yake kiasi cha kuruhusu magari mengine kupita, linaweza kukimbia hadi kufikia kilomita 60 kwa saa huku likivuka reli pamoja na kupita katika njia za barabara za kawaida.

“Faida moja kubwa ni kuwa basi hili litatumia nafasi ndogo wakati linapokuwa ya barabarani,” Injinia wa mradi huo Song Youzhou aliliambia shirika la habari la China Xinhua.

Basi la TEB linafanya kazi kama ambavyo Subway linafanya lakini gharama za utengenezaji ni nafuu zaidi ukulinganisha na Subway,” anaeleza injinia mwingine Bai Zhimini.

Basi hilo la TEB litaweza kufanya kazi inayofanywa na mabasi ya kawaida 40 kulingana na maelezo ya watengenezaji wake. Hata hivyo, bado haijafahamika ni lini litatumika kwa wingi katika miji mbalimbali nchini China.

Kwa mara ya kwanza, wazo la kuwa na basi la aina hii lilionekana kama mzaha hasa baada ya kampuni inayolitengeneza kuonyesha mchongo mdogo kwenye maonyesho ya kimataifa ya teknolojia za hali ya juu ya Beijing.

Baada ya maonyesho hayo, kampuni mzalishaji ilitengeneza basi la kwanza ambalo lilifanyiwa majaribio na kuonyesha ufanisi mkubwa barabarani. Mamilioni ya watu walivutiwa na kushangazwa na basi hilo baada ya video yake kuwekwa mtandaoni.

Niliona picha za basi hili muda si mrefu uliopita lakini sasa naona zimegeuka kuwa basi kweli. Basi hili limejengwa kwa mwendo wa Kichina,” anasema mmoja wa watu waliolishuhudia basi hilo.

Likitazamwa kama mwarubaini wa foleni, TEB limeweza kuwa la aina yake kwa kuwa litaweza kutumia njia moja na magari mengine, pia halitalazimika kusimama wakati magari mengine yakisimama wakati wa foleni kali.

Barabara zetu bado zinakabiliwa na changamoto ya foleni,” anasema Wang Yimin mkazi wa mji ambao basi hilo lilifanyiwa majaribio ya kwanza.

Wazo la kutengeneza basi la aina hii lilikuwapo tangu mwaka 2010 wakati Jarida la Times lilipoandika makala ya kushawishi kampuni zenye uwezo kuwekeza kwenye usafiri ambao utasaidia kupunguza foleni barabarani.

Kampuni ya TEB Technology Development ilionekana kuvutiwa na wazo hilo na kuamua kulifanyia kazi. Mradi huo ambao kama utaweza kwenda kama unavyotarajia utasaidia tatizo la foleni na unaelezewa kuwa ni wa gharama nafuu ukilinganisha na aina nyingime za usafiri wa umma.

Vyombo vya habari vya Serikali ya China vilielezea kuwa uzinduzi wa huduma hiyo ulikuiwa wenye mafanikio makubwa huku tukio lake likivutia vyombo vya habari vya kimataifa kama shirika la habari la kimataifa la Reuters ambalo pia lilipewa nafasi ya kutembelea mradi huo pamoja na kufanya mahojiano ya kina.

Bila haka kama aina hii ya mabasi ingeletwa Tanzania na hususani Jiji la Dar es Salaam, pengine ingekuwa ni suluhisho la tatizo la kujazana kwenye mwendo kasi zetu ambazo zinaonekana kushindwa  kuhudumia umma.

Logo ya Iphone na Apple Inavyoleta Utata na Dhana Kwamba ni Mkataba Kati ya Shetani na Binadamu..!!!

$
0
0


Kuna mambo ambayo yanatokea humu duniani ambayo yanamfanya mtu yoyote yule ajiulize maswali mengi bila kupata majibu,kuna zile habari za vyama vya siri ambazo leo zinaonekana kama ngano kwa baadhi ya watu na kwa wengine zikiwa kama ni mambo ambayo yana uhalisia wake

Nimekuwa nikijiuliza sana kuhusu hii logo ya bidhaa zinazokwenda kwa jina la Apple,ni kwanini hiyo logo au icon inaonekana imeng'atwa?

Yaani linaonekana tunda hilo la Apple limeng'atwa kipande,kwanini iko hivyo?

Kuna nadharia nyingi sana kuhusiana na hili lakini ile ambayo inaonekana kupata nguvu ni ile ya tunda hilo kuwakilisha tunda lililoliwa pale Eden na Adam na Hawa kuashiria dhambi kuingia duniani,hili linaonekana kupata nguvu kwasababu ya mazingira yenyewe ya logo hiyo

Wenye kukubaliana na hii ya Eden wanaendelea kusema kuwa hili linawakilisha wenye bidhaa hizi kukubaliana na dhana ya shetani kutaka kumuokoa mwanadamu na 'udikteta" wa Mungu na kumpa uhuru hivyo wanaendeleza mapambano ya kumuondoa binadamu kutoka kwenye huo udikteta na ndio maana wanakubaliana na shetani

Hebu tazama hizi picha hapa chini ......


Hizo ndio logo za hawa jamaa,kama kuna mtu ambae ana maelezo ya kwanini ziko hivyo basi sio vibaya akatueleza hapa nasi tukaelewa maana kuna watu kama hawa hawa wanaendelea na dhana kama hizi;

Apples represent knowledge and man's first sin. Given the Illuminati's satanic rituals and devil worship, the apple has great significance. To those that follow Beelzebub, Adam and Eve's first bite of the forbidden fruit became the dawn of a new era, the era where the devil could rule the world. The selection of the apple symbolizes the Illuminati's push toward technological knowledge with the endorsement of satan.

Hebu tujaribu kuangalia na hili ili tuweze kupata majibu angalau kidogo ambayo yataweza kuturidhisha .....!!

Tukio Hili Linaweza Kuwa Ushahidi Kwamba Tukifa Tunarudi Duniani kwa Miili Mingine...!!!?

$
0
0

Mtoto mmoja wa kiume huko India aliwahi kuwaacha hoi wazazi wake baada ya kuanza kudai aliwahi kuishi kabla ya kizaliwa

Mtoto huyo wa kiume, Taranjijt Singh anasema aliwahi kuishi miaka michache nyuma, ambapo alifariki kwa ajali ya pikipiki akiwa bado mdogo.

Mtoto huyo akiwa na umri wa miaka miwili alianza kusema kuhusu maisha yake ya nyuma na alikuwa akitoroka sana nyumbani . Alikuwa akiwaambia wazazi wake kwamba anakumbuka kijiji alichokuwa akiishi na hata jina la shule aliyokuwa akisoma.

Alikumbuka pia jina la baba yake wa zamani {kabla hajafa}. Awali ilionekana kama aina fulani ya kisirani cha mtoto, lakini ilibidi wazazi wake waanze kuwa na wasiwasi kwa kadiri alivyokuwa akiongezeka kiumri.

Mtoto huyo alikumbuka pia siku aliyokufa . Aliwaambia wazazi wake kwamba, alikufa September 10,1992. Alikufa baada ya kugongwa na pikipiki wakati akiwa kwenye baiskeli akiwa anakwenda shuleni asubuhi. Baada ya ajali hiyo alipata majeraha kichwani na alifariki siku ya pili baada ya ajali.

Baba yake wa sasa hivi, Ranjit Singh, anasema, mtoto wake alipozidi kusisitiza kuhusu maisha yake ya zamani, waliamua na mkewe kumpeleka huko kijijini anakodai kwamba, ndiko alikoishi kabla hajafa. Awali hawakuweza kumpata mtu ambaye alikuwa anafanana na maelezo ya mtoto huyu. Mkazi mmoja wa kijiji hicho aliwaomba waende kijiji cha jirani kinachofuata.

Kwenye kijiji hicho walikwenda kwenye shule ya kijiji ambapo mwalimu mkuu wa shule hiyo alithibitisha kamba, September 10, 1992 alikufa mwanafunzi wa shule hiyo kwa ajali ya pikipiki. Kupitia shuleni hapo, walibaini mahali wazazi wa mtoto yule aliyekufa kwa ajali ya pikipiki, walipokuwa wakiishi.

Ni kweli waliwakuta wazazi ambao walithibitisha kufiwa na mtoto katika tarehe na njia iliyoelezwa. Baba wa sasa wa mtoto huyu, Tanjit Singh alieleza kwamba, mtoto wao aliwaambia kwamba madaftari aliyokuwa nayo wakati wa ajali yalilowa damu baada ya ajali ile na alitaja kiwango cha fedha ambazo zilikuwa kwenye mkoba wake wa shule.

Mama wa zamani wa mtoto huyu ambaye kwa maana hiyo ni mama wa mtoto aliyefariki mwaka 1992 aliposikia hivyo aliangua kilio kikubwa , kwani maelezo hayo yalikuwa sahihi bila doa la kosa. Alisema vitabu na fedha hizo bado vipo, kwani aliviweka kwa kumbukumbu ya kifo cha mwanaye .

Baadae mtoto huyu alirudi na wazazi wake wa sasa nyumbani kukiwa na maswali yasiyo na majibu. Wazazi wake wa zamani pamoja na ndugu zake, walikwenda kumtembelea kwao baadae. Mtoto huyu aliibaini picha ya siku ya ndoa ya wazazi wake, ambayo walikuja nayo wakati walipokwenda kumtembelea kwa wazazi wake wapya.

Awali mwanasayansi, Vikram Chauhan, alikataa kukubaliana na maelezo kuhusu mtoto huyu , lakini baadae alijipa moyo wa kuanza uchunguzi. Alitembelea vijiji vyote viwili , cha zamani alikozaliwa na kufa na hiki cha sasa alipozaliwa.

Alizungumza na wazazi wote na kupata maelezo ambayo yalimfanya kuona kuna jambo la maana kuhusiana na kifo na ‘kufufuka’ kwa mtoto huyu. Kwenye kijiji alichozaliwa na kufa mtoto huyu, muuza duka mmoja alikiri kwamba ni kweli , mtoto kama huyo alikuwepo na yeye alimkopesha madaftari jana yake na alipogongwa alikuwa akielekea dukani kwake kumlipa madaftari hayo.

Chauhan alichukua sampuli ya mwandiko wa mtoto huyu na ule wa kwenye madaftari ya marehemu. Ilipokwenda kupimwa na wataalamu wa mwandiko, ilibainika kwamba, ilikuwa ni ya mtu mmoja.
Kumbuka kwamba mwandiko wangu hauwezi kuwa sawa na wa mtu yeyote, kama ilivyo alama za vidole. Kila mwandiko una sifa zake maalum ambazo haziwezi kupatikana kwenye mwandiko wa mtu mwingine.

Wataalamu wana uwezo wa kubaini mwandiko wa kughushi hata kama umefanywa na mtaalamu wa kiasi gani wa kughushi miandiko.

Kubwa zaidi ni kwamba mtoto huyu ambaye alishaanza kusoma kwenye maisha yake ya kabla ya kifo, hivi sasa hajapelekwa shule, kwa sababu familia yake ya sasa ni maskini. Hata hivyo katika jambo la kushangaza zaidi alipotakiwa kuandika alifabeti za kiingereza na ki-punjabi aliweza kufanya hivyo bila tatizo. Kama hajasoma ingewezekana vipi kufanya hivyo? Anatumia akili ya zamani ya kabla hajafa.

Familia yake ya zamani imeomba kukabidhiwa mtoto wao, lakini familia yake ya sasa imesema hapana, huyo ni mtoto wao. Kisheria, bila shaka, familia yake ya sasa ambayo ni maskini sana, wakati ile ya zamani ilikuwa na uwezo, ndiyo yenye uhalali wa kuishi na mtoto huyu.

Huenda baada ya sayansi kuthibitisha kwamba watu hufa na baadae kurudi wakiwa wanamiliki miilia tofauti, familia kama hii ya zamani ya mtoto huyu, ndipo itakapoweza kupata haki.

Hata hivyo, bila shaka kila familia kati ya hizo mbili, itakayoishi naye, itakuwa na mashaka ya aina fulani.

Ni vigumu kupingana na maelezo ya mtoto huyu, ambaye tangu akiwa na umri wa miaka miwili, alikuwa akizungumzia kuhusu kumbukumbu alizonazo juu ya maisha yake ya nyuma. Ugumu wa kupinga unatokana na ukweli kwamba, hatimaye maelezo yake yalithibika

Jambo hili linathibitisha maisha baada ya kifo

Lakini sio maisha baada ya kifo peke yake bali pia kukubali kwamba huenda binadamu ataendelea kuwepo, kwa sababu uwepo {being} haujapotea na hauwezi kupotea. Mwili wako utaharibika, lakini uwepo wa binadamu hauwezi kupotea.

Karibuni kwa maoni ndugu zangu woote!

Watoto wa Shule za Msingi Korea Kaskazini Wafundishwa Kutumia Silaha Ili Kumlinda Rais Wao Dhidi ya Marekani..!!!

$
0
0

WATOTO wa shule nchini Korea Kaskazini hulazimishwa kushiriki katika aina tofauti tofauti ya michezo ikiwamo matumizi ya silaha kali.

Wakati wakifunzwa kumlinda Kiongozi wa Taifa hilo dogo la kikomunisti, Kim Jong-un jeshi la watoto hao wachanga lilionekana likikimbia huko na kule likiwa limejihami na silaha bandia aina ya AK-47s na magrenada ya kurusha kwa mikono.

Watoto hao wadogo walilazimishwa kukabiliana na vikwazo mbalimbali wakibeba Kalashnikovs feki huku umati mkubwa ukishuhudia katika sherehe zilizofanyika kwenye jengo jipya mjini  Pyongyang hivi karibuni

Mmoja wapo Myong Hyon-Jong (10) anaeleza kuwa anataka kujiunga na jeshi wakati atakapokuwa mkubwa ili kumlinda ‘kiongozi mpendwa wa taifa hilo mheshimiwa’ Kim Jong-un kwa nguvu ya kijeshi.”

Aliendelea kueleza kwamba wanapaswa kujiandaa wenyewe kulinda nchi yao.

Mwalimu wake Ri Su-Ryon kisha akasema mafunzo yamelenga kuwapatia watoto moyo wa kizalendo wa kuilinda nchi yao wakati watakapokuwa wakubwa na kujiandaa kimwili na kiakili kuwashinda maadui wowote wale.

Mara atakapomaliza kozi anasema: “Narusha grenada la mkono nikiwa na imani siku moja nitamrushia rasmi na kumshinda adui yeyote atakayejaribu kupenya ndani ya mipaka ya nchi yetu”.

Shughuli hiyo ilikuwa kusherehekea Siku ya Muungano wa Watoto Korea –inayosimamiwa na taasisi ambayo watoto wote nchini Korea Kaskazini wanakuwa moja kwa moja wanachama.

Lengo lake ni kuwapumbaza akili watoto wawe na heshima na watiifu na waaminifu kwa mamlaka na kuwa tayari kupigania kwa ajili ya Korea Kaskazini.

Watoto huaminishwa mamlaka zao zikiongozwa na kiongozi wao mkuu Kim Jung-un zina upendo mkubwa kwao, hazilali zikifanya kila ziwezalo kuwalinda na kuilinda nchi yao.

Na kwamba Marekani na washirika wao wengine ni adui yao mkubwa, mnyonyaji, mwenye kiu ya damu, ambaye anaweza kuwashambulia wakati wowote. Propaganda hii inawafanya waichukie vilivyo Marekani na kuwa tayari kujitoa kwa ajili ya kiongozi na taifa lao.

Mara nyingi watoto au hata watu wazima wanapokutana na Kim huonekana wakilia katika kile kinachoonekana kuwa wanaigiza au wamepumbazwa akili kuonesha kilio chao ni mapenzi makubwa walio nayo kwake huku wakimchukulia kama mungu mtu.

Korea Kaskazini iko katika tahadhari kubwa ya uwezekano wa kuvamiwa na Marekani wakati wowote. Ni hali inayowafanya wakazanie na program za nyuklia na makombora ya masafa marefu licha ya kuwekewa vikwazo na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.


Tangu kuanza kwa mwaka jana, taifa hilo limefanya majaribio kadhaa ya nyuklia na masafa marefu yanayoilenga Marekani, licha ya kwamba Rais Donald Trump kusisitiza hilo halitotokea.

Uhusiano wa Namba Hizi na Majini,Shetani ....!!!

$
0
0

Sina kawaida ya kudharau jambo hata kama linaonekana ni la kijinga na nimeshapata faida kubwa kutokana na mtazamo wangu huu,nimeshafanikiwa kwenye mambo mengi ambayo watu waliyaona ni ya kijinga na wengine walijifunza kupitia hili

Leo naomba niwashirikishe jambo hili ambalo ni mewauliza watu kadhaa na wameonekana kunishangaa mtu kama mimi ni kwanini hasa nimeamua kulifuatilia hili,lakini najua kupitia hili naweza kujifunza kitu ambac ho sikua nakijua au nikajikuta napoteza muda wangu,yote haya ni matokeo na nimejiandaa kwa yote

Kuna namba watu wamekuwa wakidai kuwa kama unataka kuzungumza na Shetani au majini basi unaweza kuzipiga,kuna jamaa yangu aliwahi kuzipiga nikiwa nae na simu iliita na ikapokelewa halafu aliulizwa shida yake na alisema lakini aliepokea simu alimuambia kuwa "huwezi wewe na usitusumbue"

Kuna jamaa yangu mwingine alipiga nae simu ilipokelewa na aliambiwa kuwa wapo busy hivyo hawahitaji usumbufu

Ukiangalia namba hizi hazina namba kiunganishi ili ujue hata location ya namba hizi,kitu hiki kimenifanya nijiulize sana kama hii inakubalila kwa mamlaka husika za mawasiliano

Sina ufahamu hasa wa mambo ya mawasiliano na nadhani hapa kuna watu wengi wanaweza kunipa maelezo ya kutosha na nikaridhika kuhusiana na dhana hii kuwa namba hizi ukipiga unazungumza na shetani au majini,sidhani kama jambo hili halina maelezo kwa wale ambao wanajua kuhusu mawasiliano na ndio maana nikaamua kuja kuuliza hapa ili jambo hili niachane nalo

Namba zenyewe ni 11111111111 na 999999999 nadhani zipo na zingine,hebu wakuu nisaidieni hapo ili niweze kujua

Nikwanini hakuna namba kiunganishi lakini simu inaita?
Je ni akina nani wanaopokea simu hizi?

Karibuni ....

KUTANA NA SHEKH SHARIFU SIMBA mtabibu wa nyota Tanzania na duniani kote

$
0
0

KUTANA NA SHEKH SHARIFU SIMBA mtabibu wa nyota Tanzania na duniani kote,

✨SHEKH SHARIFU SIMBA anatoa shukrani kwa wote mnaopiga simu mlioko ndani na nje ya Tanzania, wanatoa shukrani na wale wenye matatizo, pia anawashukuru wote wanaomshirikisha na kutoa shuhuda jinsi tiba zake zinavyo wasaidia.
✨Bado ujachelewa piga simu na uweze kusaidiwa, SHEKH SHARIFU SIMBA yupo kwaajili ya kutatua matatizo yote yanayo wakabiki wanadamu,

🦅SHEKH SHARIFU SIMBA ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili anatumia kitabu cha QUR'AN, dawa za asili, dawa za kiarabu na majini,

✨je umeachwa na Mme/ mke, mchumba au umpenzi wako? SHEKH SHARIFU SIMBA anauwezo wa kurejesha mahusiano yako ndani ya masaa (72)
✨je umahangaika kupata mtoto bila mafanikio?
✨je mikosi inakuandama na umekuwa mtu wa kilia kila siku bila kupata msaada wowote?
✨je madeni yanakuandama?
✨je umesimamishwa kazi au kushushwa cheo bila sababu? SHEKH SHARIFU SIMBA anatoa kisomo na kusafisha NYOTA na kung'arisha, ili ung'ae upya kwa kila mtu na mahali popote,
💍SHEKH SHARIFU SIMBA anatoa Pete za bahati zilizoambatana na jini Mali,
✨Anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume chango kwa kina mama, ngizi na n.k, pia anatibu miguu kuuma na kufa ganzi, tumbo kujaa gesi na kuunguruma na magongwa mengine ya siri,
🇺🇸pia anatibu kwa njia ya simu kwa wale walioko mbali au nje ya nchi,
📞SHEKH SHARIFU SIMBA anapatikana BAGAMOYO, kwa wale walio nje ya nchi tumia WhatsApp no +255 719361792, kwa wale wa ndani ya nchi piga simu no: 0719-361792 au 0689-476132 na 0745-281712.
[6/4, 17:10] maleojr jm: MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI. (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 72 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI: SHEKH SHARIFU RASHID ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran dawa za asili dawa za kiarabu, na njiwa, Anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango kwa kina mama, ngiri maji na n.k, anakuvutia mali zilizo potea au kudhulumiwa, pia anatoa Pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali, Wenye matatizo ya uzazi, jini mahaba, mapepo ya kichawi, vifungo vya kimaisha, ndoto mbaya za usiku, uelewa mdogo wa ufahamu shuleni kwa watoto wote, pia anauwezo mkubwa wa kumaliza kazi zilizoachwa na wataalamu wengine ndani ya masaa 48 tu, Pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo. WASILIANA NAE KWA WhatsApp na SIMU NO: +255 718-668347 na +255 767-204308 +255 685-224047 Email shekhsharifurashidi@gmail.com.

USHAURI: ni vyema kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate huduma kwa haraka.

Maalim Seif Alaani Adhabu ya Mdee, Bulaya..!!!

$
0
0

Siku chache baada ya Bunge kuwazuia wabunge Halima Mdee na Ester Bulaya kuingia vikao vyote vya Bunge hadi Bunge la Bajeti mwakani, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amesema vitendo hivyo ni mwendelezo wa kupigwa mateke kwa demokrasia Tanzania.

Pia amesema hiyo ni ishara kuwa watawala waliopewa madaraka hawataki kufuata misingi ya demokrasia iliyopo.

Mdee na Bulaya wote kutoka Chadema walikumbana na adhabu hiyo kutokana na vitendo vyao wakati Spika Job Ndugai alipoagiza Mbunge wa Kibamba, John Mnyika ambaye alipewa adhabu ya kutohudhuria vikao vitano vya Bunge hili linaloendelea, aondolewe ukumbini wakati wa mjadala wa Wizara ya Nishati na Madini.

Mdee ambaye ni Mbunge wa Kawe, alionekana akimvuta shati mmoja wa askari waliokuwa wakimtoa Mnyika, wakati Bulaya wa Bunda Mjini alionekana akiwashawishi wabunge wa upinzani kutoka nje kuonyesha mshikamano kupinga uamuzi wa Spika.

Maalim Seif alitoa kauli hiyo juzi wakati akizungumza na mwandishi wetu muda mfupi baada ya kushiriki hafla ya futari iliyoandaliwa na Baraza la Mtendeni Namba Mbili, lililopo Buguruni Mtaa wa Madenge, Dar es Salaam.

Katibu mkuu huyo ambaye alikuwa Makamu wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar katika Serikali iliyopita, alisema kitendo hicho si cha kiungwana na kinasikitisha kwa sababu wabunge hao ni wa majimbo ambao wanachaguliwa na wananchi.

“Wananchi wa Kawe na Bunda wamewachagua hawa ili wakawasilishe kero zao. Sasa unawasimamisha muda mrefu wananchi wa maeneo haya si watakosa uwakilishi? Waingereza wanasema bila uwakilishi hatuwezi kutozwa kodi.Sasa leo wabunge wanazuiliwa, hivi wananchi wa Kawe na Bunda wakisema hawalipi kodi kwa sababu hawana mwakilishi mtawalaumu?” alihoji Maalim Seif.

Alisema pamoja na maelezo mazuri ya kufuata kanuni, lakini watambue kuwa wanapo waadhibu wabunge, athairi ina kwenda kwa watu wengi ambao wanakosa mwakilishi katika chombo hicho kikuu cha kutunga sheria.

Alisema CUF haikubaliani na jambo hilo na kudai kwamba hivi sasa kinachotumika ni wingi wa wabunge wa CCM ambao wanakanyaga misingi ya demokrasia.

Msiba wa Ndesamburo

Akizungumzia yaliyotokea katika mazishi ya mbunge wa zamani wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo, Maalim Seif alisema kitendo cha viongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro kuwanyima Chadema Uwanja wa Mashujaa ni mwendelezo wa kuwanyima haki wapinzani.

Alisema baadhi ya viongozi wa Serikali na wabunge wa CCM walisikika wakitoa kauli za kumsifia Ndesamburo, kwamba alikuwa mzee mwenye hekima na mwenye kutoa michango mizuri alipokuwa bungeni.

“Sasa ilipofika wakati wa kumsindikiza mwenzetu (Ndesamburo), wanaanza kuleta fujo. Tunaambiwa shughuli zote huwa zinafanyika Uwanja wa Mashujaa na Mahakama zinakuwapo lakini iweje kwa Ndesamburo haiwezekani,” alihoji Maalim Seif.

“Kwa hili la Ndesamburo, hii inatoa picha kuwa hakutakuwa na shughuli za kijamii zitakazofanyika kwa sababu kuna Mahakama na vitu vingine,” alisema.

Aliwataka viongozi wa Serikali kuacha tabia ya kuchagua mambo badala yake wawe na msimamo mmoja unaoeleweka,

Maalim Seif alisema ni jambo la kawaida kwa wapinzani kuzuiwa kufanya baadhi ya mambo lakini ikitokea viongozi wa CCM wamefariki dunia watapitishwa mtaani.

“Watu wa Moshi wamekosa fursa ya kumuaga mzee wao aliyekuwa mbunge kwa miaka 15. Yaani mnaweka vipingamizi hadi katika barabara ili watu wasitoe heshima ya mwisho? Narudia kusema tena hii ni alama kuwa demokrasia haina nafasi Tanzania,” alisema.

Maalim Seif alitumia nafasi hiyo kumuomba Rais John Magufuli kutenda haki kwa watu wote bila kujali itikadi za vyama vya siasa kwani yeye ni kiongozi wa Watanzania.

“Wapinzani hawana tatizo na kuweka amani mbele ya Taifa hili. Mbona walivyoenda kumuaga Uwanja wa Majengo hakukuwa na vurugu zozote? Tusiogope watu, na viongozi lazima tuwaheshimu watu,” alisema.

Katibu wa Baraza la Mtendeni Namba Mbili, Mohamed Ally Mwinyi alisema lengo la kuunda baraza hilo ni kuwakutanisha pamoja wanachama wa CUF na kujadali masuala ya maendeleo ya chama hicho.

“Baada ya ofisi ya makao makuu kuchukuliwa na upande mwingine, tuliamua kuunda baraza kama hili ili kuimarisha chama. Tunakushukuru Maalim Seif kwa kujumuika na sisi kwenye futari,” alisema Mwinyi.

Mabasi ya Jiji la London Yaitangaza Zanzibar Kama Kituo Bora cha Utalii Duniani..!!!

$
0
0

Kwa siku mbili mfululizo sasa mabasi ya jiji la London yamekuwa yakibeba tangazo ya shirika la ndege la Uturuki ambalo linapigia debe kituo chake kipya cha safari ya ndege zake “Zanzibar*.

Hatua hiyo ya shirika la ndege la Uturuki kuitangaza Zanzibar limeiweka Zanzibar katika maeneo muhimu ya utalii “Tourist Destination”

Kampuni ya ACACIA Ipo Katika Mkakati wa Kupunguza Wafanyakazi 400..!!!

$
0
0

Kampuni ya Acacia iliyoenda kinyume na Makubaliano kuhusu mchanga wa Madini ipo kwenye mkakati wa kupunguza wafanyakazi hasa kwenye sekta ya ulinzi. Inadaiwa watu 400 wataondolewa.

Chanzo: The Citizens Tanzania

Mange Kimambi Afichua Madudu Mapya Kuhusu Ndege za Bombardia..Adai Moj Imeharibika Zaidi ya Miezi Imepaki Tu kwa Kukosa Mafundi..!!!

$
0
0

Bombadier moja imeharibika miezi sasa haifanyi kazi. Tunaomba wabunge muhoji issue ya hii Bombadier. Hizi ndege tuliambiwa ni brand new iweje leo ipaki.?

Mainjinia karibu hamsini wameshajalibu kutengeneza iyo ndege imeshindikana wameamua kuiacha tu ni kitambo sana imepaki tu.

Nimeamua Nithubutu Ingawa Nina Mtaji Pungufu ya Laki Saba. Nawe Waweza Jaribu Mahali Unapoishi..!!!

$
0
0

Tatizo kubwa kwa sisi wanavyuo hatuwazi nje ya box,kila mtu akipata vilaki kadhaa(mwanachuo) anakimbilia kufungua banda la chipsi.OK fine malengo yako baada ya hilo banda?.

Ok Mimi ni mwanachuo wa mwaka wa pili,nimeamua kuja na ubunifu tofauti wa biashara yangu.Nimendunduliza nikafikisha laki sita na nusu na ninadream zakuja kuwa bakharesa hapo baadae.Unajua nimefanya nini?.

Nimetafuta vijana waaminifu wawili niliosoma nao wakafeli school.Mmoja yupo huko hom(mkoani) mwingine nimemtumia nauli elfu 50 aje dsm nikae nae geto(kashafika).

Nimechofanya yule wa mkoani(ninamuamini sana) nilimtumia laki nne na nusu,akanunua mchele kg 400.kilo kwa sasa mchele mpya ni 1000Tzsh.Kwahiyo apo ilienda sh laki nne.akabakiwa na sh elfu arobain,nmejumlisha na hela yakutoa mchele mashineni na magunia yakuuwekea.

Baada ya hapo akaenda tafuta usafiri ambao kila kg 100,wamemtoza sh elfu 10000.kwahiyo kg 400 akawa kamaliza ela mpaka mzigo kufika dar.

Sasa unajua nmeamua kuifanya vipi hii biashara.Mimi nauza kuanzia Kg 5. Kwa shilling 1800 kila kilo.Nmechukua oda ya mama ntilie wanao uza chakula chuo nacho somea,pia na baadhi ya mama ntilie wamtaani.

Pia nawauzia wanafunzi wanaojipikia kwenye magheto.Jambo la msingi nimelofanya nikuwa mtu akihitaji mchele ananipigia simu nampelekea mchele mpaka mahali anapokaa.
Kama itakuwa mbali sana ambapo nitahitaji usafiri basi itabidi kg1 mteja ainunue kwa sh 1900.

Mchele ninaouza quality yake kwenye maduka ya mitaani ni sh 2200.
Sasa nimeanza na hizi kg 400,ambazo nikiziuza kwa kg1, sh 1800. Nitatoa sh 720000.Na hii nategemea ndani ya siku 10, mpaka 12 nitakuwa nimeshaipata, kwahiyo awamu ijayo nitatuma kg zaidi ya 580 kama bei haitopanda 

Tumekubaliana nahawa jamaa zangu wawili tutaanza kulipana japo hela ya sabuni baada ya miezi minne.Na huku nikiwa nimesubiri hela ya bum nitoe kama laki tatu niongezee ili mtaji ukue baada ya mauzo.

Pia nimekopa mizani nitakuwa nalipa kidogo kidogo kadiri mauzo yangu yatakavyokuwa.

Chakula ambacho nakula mie na huyu jamaa yangu kipo nje ya bajeti ya mtaji.

Na wewe mwanafunzi mahali ulipo/mtu mwenye mtaji mdogo waweza jaribu hii nahakika itakulipa.

Au kama mtu yeyote mwenye ushauri zaidi namna nitakavyoboresha zaidi anaweza kunisaidia(tusaidia).

Sitaki kazi.

Vifo vya Watu Watatu wa Familia Moja Vyaacha Taharuki Mara..Yadaiwa Chanzo ni Asali ..!!!

$
0
0

Watu watatu wa familia moja wakazi wa Kijiji cha Nyantira wilayani hapa mkoani Mara wanadaiwa kufariki katika mazingira ya kutatanisha huku wanannchi wakihusisha vifo hivyo na ulaji wa asali.

Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Polisi Tarime, Rorya, Sweetbert Njewike akizungumza kwa simu akiwa Shirati wilayani Rorya, amesema hana taarifa hiyo ofisini kwake.

Mwenyekiti wa kijiji cha Nyantira, James Chacha amesema tukio hilo lilitokea kati ya Juni 7, 8 na 9 na kuzua taharuki kijijini hapo kutokana na aina ya vifo vya wanafamilia hao watatu kufariki kwa kufuatana.

Amewataja waliofariki kuwa ni Kerato Nyangerela (70), Regina Kerato (50) na Samwel Kerato (12) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tatu Shule ya Msingi Nyantira.

Chacha amesema, "Juni 7 tulizika mzee baada ya kumkimbiza Kituo cha Afya, Muriba, baada ya saa 12 akafariki, tukamleta nyumbani kuzika, tulipomaliza maziko mtoto naye akawa kwenye hali mbaya, tukamkimbiza kituoni, akafa siku tunazika akaanza mama naye akafa pia," alisema.

Ameongeza kuwa kufariki kwa watu hao kwa mfuatano kijiji kumeibua hali ya wasiwasi na huzuni hasa kwa kuwa wameacha watoto wadogo.

Akizungumzia vifo hivyo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Tarime, Mkumbo  Odari alisema,"asali kama asali haina madhara kwenye mwili wa binadamu isipokuwa pale inapokuwa imechanganyika na sumu ndipo inapoweza kuleta madhara, na ndiyo maana asali inatumiwa kama dawa, kwenye chakula na kupaka kwenye mikate," alibainisha Odari.

Naye Diwani wa Kata ya Nyansicha, Sunday Magacha alisema hadi sasa chanzo cha vifo vya wanafamilia hao hakijajulikana na uchunguzi bado unaendelea ili kufahamu chanzo licha ya kuwa uchunguzi wa awali uliofanywa na kituo cha afya Muriba ulionyesha kuwa walikuwa wamekula sumu.

Alisema tukio hilo lilikuwa la kwanza na la aina yake ambalo limewaacha wananchi wakiwa wameathirika kisaikolojia.

Gor Mahia Yatwaa Ubingwa SportPesa ..!!!

$
0
0

Gor Mahia ya Kenya imefanikiwa kuwa timu ya kwanza kutwaa ubingwa wa SportPesa Super Cup baada ya kuifunga AFC Leopards kwa mabao 3-0 kwenye mchezo wa fainali uliofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam leo Jumapili.

Mchezo huo ulizikutanisha Gor na Leopards ambao ni watani wa jadi nchini Kenya maarufu kama Mashemeji. Ushindi huo uliwafanya Gor kupachikwa jina la ‘mashemeji wa kweli’.

Mabingwa hao waliondoka na kiasi cha Sh60 milioni kama zawadi pia kupata fursa ya kucheza na Everton ya England kwenye mchezo wa kirafiki utakaofanyika kwenye Uwanja wa Taifa Julai 13.

Kipigo kwa Leopards kiliongeza uchungu kwani kimewafanya kufungwa idadi kama hiyo ya mabao mara mbili mfululizo katika kipindi cha wiki tano, jambo ambalo limewaweka katika wakati mgumu.

Katika michuano hiyo, timu za Simba na Yanga ziliaga mapema baada ya kufungwa na timu za Nakuru All Stars na AFC Leopards hivyo kutoa fursa kwa Mashemeji hao kukutana.

Pamoja na Kuwa Katika Muungano wa Kivyama ..Odinga, Musyoka Watofautiana Upigaji Kampeni..Kila Mmoja Awataka Wakenya Wachague Chama Chake!!!

$
0
0

Mgombea urais kupitia muungano wa Nasa, Raila Odinga ametofautiana hadharani na mgombea mwenza wake Kalonzo Musyoka kuhusu upigaji kura kwa vyama sita katika uchaguzi mkuu ujao.

Wakizungumza wakati wa Futari iliyoandaliwa na Gavana wa Mombasa, Hassan Joho juzi, Musyoka aliwataka wafuasi wa chama cha ODM waache kuwapigia kampeni wagombea wao tu kwani hiyo itasababisha kukosekana usawa.

“Msishangilie ODM, ODM ODM na badala yake chukueni kila kitu kwa sababu vinginevyo tutabaki bila kitu,” alisema Musyoka.

Aliongeza, “Katika ushirikiano wetu kuna chama cha Amani National Congress na vingine ndani ya Nasa. Hebu tuache kuwaambia wapigakura wachague wagombea wa ODM pekee.”

Lakini ilipofika zamu ya Odinga kuzungumza, aliwataka wapigakura kuchagua wagombea wa ODM akisema hata kama wote wako kwenye muungano, kila chama kinapiga ngoma ili wagombea wake wachaguliwe.

“Nafahamu kwamba Musyoka atapiga kampeni kwa ajili ya chama chake cha Wiper, Musalia Mudavadi atapigia debe ANC, Moses Wetangula Ford-Kenya na Isaac Ruto ataomba mbinu zifunguke ili mvua inyeshe mazao ya Chama Cha Mashinani yakue. Lakini ninasema wachagueni wagombea wa ODM hapa Mombasa,” alisema Odinga.

Wagombea hao waliwahimiza wapigakura kuchagua wagombea kutoka muungano wa Nasa ili waweze kuiondoa madarakani serikali ya Jubilee Agosti 8.

“Serikali hii, kuliko nyingine yoyote imewatesa Waislamu. Mpaka leo hawajulikani walipo baadhi ya vijana wa Kiislamu na mashehe na sisi Waislamu tunatendewa kama raia wa daraja la chini,” alisema Joho.

Odinga, Musyoka, Mudavadi, James Orengo, Joho na wabunge Junet Mohamed (Suna Mashariki), Abdulkadir Mohamed (Mbalambala), naibu spika wa zamani wa Bunge Farah Maalim na Abdulswamad Nassir (Mvita) wote waliilaani serikali ya Jubilee kwa mauaji ya siri ya Waislamu.

Zitto Kabwe Aibua Mazito Kutimuliwa Kazi kwa Mkurugenzi Mkuu wa Ewura..!!!

$
0
0

Zitto Kabwe, Mb

Ni muhimu sana Rais afahamu kwamba kuna kazi kubwa ya chinichini inafanywa na wasaidizi wake ( sina hakika kama yeye Rais anajua na au ameruhusu kazi hiyo ) kuendeleza wizi huu wa watu wa PAP ya Harbinder Singh Seth na IPTL. Kwenye kesi ya Standard Chartered Bank dhidi ya TANESCO huko mahakama ya ICSID ambapo TANESCO wanatakiwa kulipa shilingi 352 bilioni kwa Benki hiyo, Wanasheria wa TANESCO na wale wa PAP/IPTL wanashirikiana kwa karibu mno. Kwenye rufaa, TANESCO wametakiwa waweke fedha hizo kwanza kwenye akaunti ya Benki ya nje kabla ya rufaa kusikilizwa.
PAP/IPTL wanalinda ufisadi wao kwa kujifanya wanashirikiana na TANESCO kwenye kesi. Kwenye Taarifa ya PAC kuhusu Tegeta Escrow Account, tuliweka wazi kuwa PAP/IPTL waliweka dhamana kuwa ikitokea madai yeyote yale dhidi ya TANESCO basi PAP/IPTL italipa. 

Madai yametokea, matapeli hawa wanajifanya kushirikiana na Shirika letu na Wanasheria wa Serikali wanawasaidia matapeli hawa na sasa wanataka kuwaongezea leseni ya Biashara. Kwanini Serikali isitumie ile Indemnity kuwataka PAP kulipa hizi fedha? Kwanini Serikali inayosema inapambana na ufisadi inawakumbatia mafisadi wa PAP/IPTL? Kwanini Serikali iliyoonyesha ujasiri wa kupambana na Kampuni kubwa kama Acacia/Barrick inayumbishwa na matapeli hawa? Tena tapeli mmoja tu Harbinder Singh Seth?

Vyombo vya Serikali pia vinahusika na kuwalinda hawa matapeli. Kwa mfano, huko ICSID Shirika letu la TANESCO kupitia wanasheria wake wamepeleka hoja kwamba Maazimio ya Bunge kuhusu Tegeta Escrow hayana msingi wowote wa kisheria na kwamba Bunge linapiga porojo tu. Wanasheria hawa wameomba Ofisi ya Bunge iwape barua kuthibitisha kuwa Maamuzi ya bunge hayana msingi wowote na ni maoni tu yanaweza kudharauliwa na kutupiliwa mbali. Shirika la Umma linalosimamiwa na Bunge linapeleka barua kwenye vyombo vya kibeberu kuwa Bunge porojo tupu.

Pia kwa kudanganywa na PAP/IPTL, TANESCO wamepeleka madai kuwa PAC ilihongwa kufikia maamuzi yaliyofikiwa na Bunge. Wametengeneza barua pepe za kujaribu kushawishi madai yao hayo na hata Taasisi muhimu kama PCCB waliingia kwenye mkenge huo na kuniita kunihoji. Niliwapa ushirikiano wote na kuwapa simu na computer zangu wachunguze barua pepe zile za kuchonga wakakuta hakuna lolote. Sikuwaacha, niliwaambia kuwa wao ni mawakala wa mashetani. Wanashirikiana na matapeli kuwaibia Watanzania. Idara ya Usalama wa Taifa, inahusika moja kwa moja na kazi hii inayofanywa na PAP/IPTL ili kufanikisha mradi huu wa kitapeli. Sina hakika kama Rais aliidhinisha haya maana TISS na PCCB wanawajibika kwa Rais moja kwa moja.

Hivyo, inawezekana kabisa mpango wa kuongeza leseni ya IPTL akawajibishwa mtu wa EWURA kwa sababu ndiye alitoa tangazo la leseni, lakini huyo mtu wa EWURA anaweza kuwa ameshinikizwa na watu wa Usalama wa Taifa kufanya hivyo. Mimi naamini Rais, kwa jinsi alivyo, hawezi kuwa anahusika na haya matapeli, lakini Rais mtumbuaji anakaaje miezi 20 kwenye Kiti za Enzi bila kumaliza suala la IPTL ilhali kuna Maazimio ya Bunge yanayopaswa kutekelezwa?

Nawapa kazi ndogo Watanzania, tazameni lile Tangazo la EWURA kuhusu IPTL nililowawekea hapa siku limetoka. Tazameni umiliki na wamiliki wa IPTL hivi sasa. Kuna hisa 16% kwa kampuni mbili zenye majina ya ujanja ujanja. Kina nani hao wamegawiwa hizo hisa tena wakati wa Uongozi wa Rais John Pombe Magufuli.

Wakati Kesho Rais Magufuli Akipokea Ripoti ya Pili ya Mchanga wa Madini..Hatimaye General Manager Wa Acacia Akimbia Nchi..!!!

$
0
0

Hatimaye General Manager wa MGODI wa ACACIA BULYANHULU Bw Graham ameacha kazi katika mgodi huo na kukimbia nchi. Hili limetokea masaa machache baada ya kutangazwa kuwa kamati ya Rais ya wachumi na wanasheria inatarajia kukabidhi ripoti yao kuhusu uchunguzi wa mchanga wa dhahabu (Makinikia) mapema Jumatatu ijayo jizi limeona libwage manyanga.

My Take: Kumbe ndiyo maana mtetezi wa wezi wa madini TUNDU alikuwa akiwapigia wezi hao na kuwaomba taarifa ili aweze kuwatetea. Ninatamani Sokoine angekuwa hai leo TUNDU ungeelewa maana ya uzalendo kwa vitendo.

Wakati huohuo Waziri mkuu Kassim Majaliwa amemsimamisha Kazi mkurugenzi wa uthibiti wa huduma za nishati na maji (EWURA) Bw Felix Ngamlagos.

"Kazi hii nilipewa na Mungu sikupewa na mtu yeyote, nipo tayari kutoa sadaka mwili wangu kwa ajili ya watanzania wanyonge"-----Rais John Pombe Magufuli.

Mungu mlinde Rais John Pombe Magufuli huyu ni mzalendo halisi.

Sanaa ya Kufikishwa Kileleni na Kutoa Maji Mengi Ukeni..!!!

$
0
0

Sexing ni sanaa ambayo lazima uwe updated ili mwenzio asikuchoke. Kama wewe umezoea kila siku ni kifo cha mende ama doggy style elewa unamboa mwenzako. Creativity inahitajika sana kwenye kufanya sex yenye viwango. Basi, hebu tupeane dondoo ili tufurahie sex zetu

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, hebu tusaidiane kuelewa zaidi na kutofautisha kati ya mwanamke kufikishwa kileleni na kutoa maji mengi ukeni. Lets have a walk

Kufika kileleni kwa mwanamke
Huu ni wakati ambapo mwanamke anakuwa ameridhika kihisia wakati wa tendo la ndoa ambapo hufikia point huwa anakojoa. Kukujoa huku kuna weza kuambatana na maji kidogo ama maji kiasi kwenye uke wake. Wengine hutokwa na maji mengi na ni sababu za kibaiolojia zaidi lakini hii ni tofauti na maji mengi ninayozungumzia leo

Kutoa Maji mengi Ukeni (Squirting)
This is more advanced. Hapa hatuongelei yale maji maji yanayoambatana na kufika kileleni kwa awamu ya kwanza. Maji yanatoka ukeni kama yanavyotoka kwenye mpira wa bomba na huchukua sekunde kadhaa yakiwa yanatoka kwa muendelezo. Nazungumzia maji mengi sana ambayo kama ukiamua kuyakinga yanaweza kufika hata robo lita (250 Mil). Inasemekana kuwa kila mwanamke ana maji mengi sana ukeni na kama akifanyiwa techniques fulani atayatoa tu, na wengi zaidi ya asilimia 90 hawajapata kushuhudia kitu namna hii. Hii ni zaidi ya kufika kileleni.

Najua kuna wengi ambao tunawaacha nyuma kwenye hili, wanawake kwa wanaume. Wanaume wengine wanaona hii ni siri ambayo lazima ifichwe ili kutofautisha sexing zao na wengine.

Wataalamu Wazitaja Dalili Tano za Wanandoa Wanaotoka Nje ya Ndoa..!!

$
0
0

Ndoa inatajwa kuwa ni elimu pekee ambayo mtu anapata cheti kabla ya kuingia darasani.

Licha ya misukosuko mingi iliyomo ndani yake ndoa imeendelea kuwa tukio muhimu katika jamii zote duniani na kurithishwa kwa vizazi na vizazi.

Moja ya misukosuko ya ndoa ni uaminifu, ambao baadhi yao wametokea kuukosa na kusababisha nyingine kuyumba au kufa kabisa.

Wataalamu kutoka maeneo mbalimbali duniani walijadili suala hili la hilo na kuja na dalili tano za wanandoa wasio waaminifu.

Kuchukia majukumu ya msingi ya ndoa

Watalaamu wanaeleza kuwa dalili mojawapo ni mwanandoa kutopenda kufanya mambo na kazi za familia.

Mtaalamu wa masuala ya ndoa kutoka Marekani Jeannie Ingram anayefanya shughuli za kutoa ushauri wa kindoa eneo la Nashville, Tennessee anasema zipo sababu nyingi za mmoja wa wanadoa kutoka nje ya ndoa, ikiwamo kutoshirikiana kwenye masuala mengi yakiwamo ya kifamilia.

Anasema mara nyingi mwanandoa anayetoka nje ya ndoa hana muda wa kusikiliza familia ina tatizo au furaha gani. Anafafanua kuwa hiyo inatokana na muda wote kufikiria mambo ya familia nyingine hata kama ni ya mtu huko alikoanzisha uhusiano.

“Akiwa anatoka nje ya ndoa hana muda wa kupoteza kufikiri vitu vingine zaidi ya mambo yake na jinsi atakavyokutana na mtu au watu wake anaoshirikiana nao kwenye usaliti, ” anasema Ingram.

Kuchukia kushiriki tendo la ndoa

Anasema wengi wao hufanya mapenzi na wenza wao kwa kujilazimisha na wakati mwingine kulazimishwa kwa uwazi kabisa.

“Wakiwa siyo waaminifu , hawavunjia pia uhusiano na wenza wao, aliliambia Jarida la HuffPost, ukweli ni kwamba uhusiano wa kindoa unahitaji kuimarishwamara kwa mara.

“Kukutana kimwili ni mojawapo ya mambo yanayopandisha mapenzi na kuamsha hisia ya kila mmoja wao kutamani kushiriki tendo hilo, jambo ambalo huwafanya kuwa pamoja muda wote ”anasema Ingram.

Wanatumia muda mwingi pamoja, lakini kila mmoja anafanya lake

Mtaalamu wa saikolojia kutoka Marekani Jimbo la Cororado Aaron Anderson anaitaja sababu ya kwanza kuwa ni pamoja na kutumia muda mwingi wakiwa pamoja, lakini kila mmoja ana shughuli zake ikiwamo kuchezea simu, kufungua kompyuta mpakato na kufanya kazi.

“Kama wewe na mke wako mnatumia muda mwingi katika chumba kimoja lakini kila mmoja ana shughuli zake na hakuna jambo lolote mnalojadili kuhusu uhusiano wenu mmoja au wote wawili mnatoka nje ya ndoa,” anasema Anderson.

Anasema siyo jambo la kawaida kwa wanandoa wanaopendana kutumia saa mbili kila mmoja akiperuzi kwenye mitandao ya kijamii.

Anasema kwa kawaida wapendanao wanapokaa wawili kila mmoja huzima simu, kompyuta na kuzungumza na mwenzake kwa namna yoyote ile.

“Hili halihitaji darubini huja lenyewe bila kufahamu, kuna ambao wakiwaona wenza wao husahau kila kitu , ”anasema.

Hawashirikiani katika mipango ya “mitoko” ya mwisho wa juma

Licha ya kuishi nyumba moja lakini kila mmoja hupanga mipango yake ya namna atakavyomaliza mapumziko ya wiki.

Mmoja wa wanandoa Said Miraji anasema kuwa alipomuoa mkewe ilikuwa kawaida mkewe kumlazimisha amsindikize hadi anapokwenda kutengeneza nywele.

Anasema baada ya kupata mtoto mmoja mambo hayo yalipungua na hatimaye kwisha kabisa.

“Nilipochunguza baada ya mambo ya kutaka kujitenga kuzidi, nilichobaini sitaki kusema, ninachoweza kukuambia ni kuwa ameolewa na mwanamume mwingine na ana watoto wawili na mimi kaniachia wawili ”anasema Miraji.

Kauli ya Miraji inaungwa mkono na mwanandoa mwingine Kuruthumu Rajabu anayesema kuwa mabadiliko yakitokea ndani ya ndoa mwisho wake ni kuachana.

Anasema baada ya kukaa kwenye ndoa na mumewe kwa miaka minne mwenza wake huyo alianza tabia ya kuchelewa kurudi isivyo kawaida.

Anasema mbali ya hilo, pia alikuwa hali chakula cha nyumbani, hajulikani anapumzika lini, kwa sababu kila siku anakwenda kazini, kibaya zaidi alikuwa hataki hata kuongozana naye.

“Ilifikia mahali hata nikimsubiri hatuwezi kwenda kulala pamoja lazima atatafuta kisingizio abaki sebuleni na kuja kulala kwa muda wake”anasema Kuruthumu.

Anasema licha ya kuwa mama bora, mcha Mungu, anayejali familia ya pande zote na kujaribu kuvumilia mapungufu ya mumewe, “Tuliishia kuachana, haikuwa kazi rahisi kumbadili alichoka manung’uniko yangu akaniacha”.

Hawaulizani hali, safari zinaongezeka

Anderson katika andiko lake alilochapisha kwenye jarida la Le wedding magazine la Ufaransa anasema kuwa ni nadra kwa mwanandoa anayetoka nje ya ndoa kumuuliza mwenzake habari za atokako hata kama amesafiri mwezi mzima.

“Anaweza asiulize hali za watoto pia bila kujali ni mwanamume au mwanamke, kwa sababu anawaza vitu vingine na kuchukia kwa nini aliolewa, ” anasema.

Anasema mwenza anayetoka nje ya ndoa muda mwingi anakuwa mtu wa safari za ndani au za nje ya eneo analoishi.

Huwasimanga au kuwasema vibaya marafiki, ndugu wa mwenza wake.

Kungwi maarufu Chausiku Salumu Maele maarufu Bi Chau anasema kuwa mbali na mabadiliko ya aina zote, kikubwa mwanandoa anayetoka nje ya ndoa huwachukia marafiki na ndugu wa mwenza wake.

Anasema anaweza kuwasema vibaya wakiwepo au pembeni.

“Huona kama wanaingilia uhuru wake wa kumbeza mume au mke, hivyo huwachukia na hutamani wasiwepo maisha.

“Ikitokea kwa bahati mbaya akapishana maneno ya mmoja wa watu hao kamwe hatomsamehe na huliweka hilo kama kosa kubwa maishani, ”anasema Bi Chau.

Anasema kuwa mwanandoa asiyemwaminifu pia huwa mgumu kujadili migongano ya ndani ya ndoa na akiulizwa hujibu “Sina muda wa kujadili suala hilo”.

Anasema kumsoma mwenza wako na kutambua mabadiliko ya tabia yake ni jambo muhimu ili kukwepa kuvunjika kwa ndoa.

Anafafanua hajawahi mwanaume au mwanamke kutoka nje ya ndoa na mpenzi mmoja kwa miaka miwili mfululizo na ndoa yake ikawa salama.

“Njia pekee ya kunusuru ndoa ni wanandoa kujuana tabia, kujibizana maswali panapotokea sintofahamu. Kukaa kimya na kupuuzia hisia kumekuwa chanzo kikubwa cha kuvunjika kwa ndoa nyingi, ”anasema Bi Chau.

Anachosema Bi Chau kinashadidiwa na Anderson anayesema mwanandoa anayetoka nje ya ndoa pia hana mapenzi na familia ya mmoja wao. Pia ndoa iliyoingia usaliti wanandoa huwasema vibaya marafiki wa wenza wao, kuwakashifu na kuwadhihaki.

“Ujue hapo hakuna ukweli kuna usaliti unaendelea kuwa makini, ”anasema Whetstone.

Mtaalamu wa saikolojia kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Lusajo Kayula anasema kila ndoa au uhusiano una tabia yake ambayo wahusika wameizoea.

Anasema kwa sababu hiyo mabadiliko ya mwanandoa asiye mwaminifu hutegemea na mazoea yao.

Anafafanua kuwa dalili, tabia za mmoja kati yao anayetoka nje ya ndoa hulingana na walivyozoea ndiyo maana siyo rahisi kufanana kutoka ndoa moja na nyingine.

“Zipo tabia tofauti ambazo zinatia shaka ikiwamo kuwa makini na simu zaidi ya kawaida, kutotaka ukaribu na mwenza wake na kupoteza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanandoa mwenza, ”anasema Kayula.

Kayula anafafanua kuwa zipo dalili nyingine ambazo mwanandoa anaweza kuwa nazo na bado asiwe anatoka nje ya ndoa.

Anafafanua kuwa wengi wanaamini mwanandoa anayechelewa kurudi nyumbani anakuwa na uhusiano, “Wapo wanaorudi saa 11 jioni na bado wanatoka nje ya ndoa, hicho siyo kigezo.

Anaeleza hata kupoteza hamu ya tendo la ndoa siyo kigezo kwa sababu wapo wanaopoteza kwa sababu ya msongo wa mawazo.

“Ndiyo maana nilisema hapo mwanzo hutegemea wahusika walizoea nini, kimetokea nini kwenye maisha yao, ”anasema.

Baadhi ya sababu za kutoka nje ya ndoa

Bi Chau anazitaja baadhi ya sababu za kutoka nje ya ndoa kuwa ni pamoja na wanandoa hususani wanawake kuaminishwa kuwa moja ya jukumu lao ni kuficha siri za ndani ya ndoa.

Anasema iwapo watatoka na kutafuta tiba ya matatizo mbalimbali yanayowakuta ndani ya ndoa hali hii haitakuwepo, “Sitaki kukudanganya tatizo la kutokuwa na nguvu za kiume limekuwa kubwa.

“Wanawake hawawezi kulalama kuhusu hilo matokeo yake wanakuwa watumwa wa ngono, wanaume nao halikadhalika, kutokana na kutoka nje ya ndoa wanapunguza mapenzi kwa wake zao na hatimaye kutotamani kukutana nao na kuwa watumwa wa mapenzi wa nje ya ndoa, ”anasema.

Anafafanua kuwa hizo ni baadhi ya sababu, zipo nyingi na zinahitaji kutafutiwa majibu na wanandoa wote.

“Kiukweli hili ni jinamizi, hakuna ambaye yupo salama, wanandoa wengi wanatoka nje ya ndoa zao, ili usiwe mmoja wao kuwa makini.

“Dawa ni kusema, kujadili kukubaliana , kueleweshana kwa pamoja badala ya kila mmoja kumuona mwenzake mkosaji, ”anasema.

Fahamu Faida na Madhara ya Kutumia Dawa za Kupata Six Packs na Kusisimua Misuli ya Mwili..!!!

$
0
0

Pengine  ni katika harakati za kuutafuta utanashati  au  ukosefu wa ajira,  na huenda ikawa ni mtindo wa kimaisha kwa vijana wengi hapa nchini na duniani kote wanaotunisha misuli. Hata hivyo wanaume walio katika harakati za kutunisha misuli au kupata maumbo yenye miraba minne, wamekuwa wakitumia dawa ili kuyapata maumbo hayo badala ya kufanya mazoezi  ya viungo.

Vijana wengi hivi sasa  wananunua kwa wingi dawa za kutunisha misuli maarufu kama ‘doping’ kwa sababu zinazotajwa kuwa ni kutafuta ajira kama vile ulinzi kwenye kumbi za starehe, ulinzi wa watu maarufu(bodyguard) na wengine mashindano ya kunyanyua vitu vizito huku wengine wakiutafuta utanashati.

Steroids

Wataalamu wa afya wanataja baadhi ya dawa zinazonunuliwa na wajenga misuli kuwa ni Anabolic Steroids, ambazo husaidia kujaza misuli na kutochoka haraka.

Ripoti  ya Wizara ya Afya na Huduma za Jamii ya Marekani inaeleza hivi: “Dawa za steroids za kuongeza ukubwa wa misuli ni kemikali zinazohusiana na homoni za kiume (tetosterones). Dawa hizo huchochea ukuzi wa misuli na kustawi kwa maumbile ya kiume. Wavulana wanapobalehe homoni hizo huongezeka na kubadilika na hivyo kuchochea mabadiliko ambayo humfanya mvulana awe mwanamume. Nyingine ni Creatine ambazo huuzwa katika hali ya unga unga na kama ilivyo Steroids, dawa hii nayo hujenga misuli na kuondoa maumivu ya mwili na Human Growth Hormone, vichocheo ambavyo hukuza misuli ya mtu kwa wiki chache tu.

 Dawa nyingine zenye nguvu na zinazotumiwa zaidi na wanaume wanaotaka kujenga misuli ni Optimal Stack, Precision Power, Estoforce Edge, Muscle Ex Edge na Muscle Rip Edge.

Miaka ya 70, watunisha misuli wengi akiwemo Arnold Schwazenerger, walikiri kutumia Steroids kama dawa zinazowasaidia kukuza misuli yao   hata hivyo mwaka 1990,  Marekani, ilianzisha sheria ya kuzuia dawa za Steroids na kuiweka katika kundi la dawa zilizopigwa marufuku.

 Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa baadhi ya vijana hutumia dawa za vichocheo vya wanaume  kama testosterone kukuza misuli hiyo. Wengi hutumia dawa hizo kwa kiwango kikubwa kiasi cha mara 10 hadi 100 zaidi ya kile ambacho daktari anaweza kukuandikia.

Wengi huzipata dawa hizi nchini Afrika Kusini ambako huletwa na watu binafsi na kuzisambaza katika nyumba za mazoezi (gym) ambako vijana wengi hufanya mazoezi ya kujenga vifua.

Gosbert Msuya, mlinda mlango wa klabu ya muziki ya Maisha, anakataa kutumia dawa za kutunisha misuli, lakini anakubali kuwa wapo vijana wanaotumia dawa hizo kwa sababu mbalimbali kubwa ikiwa ni ajira na mwonekano. “Sasa ukiwa na mwili mkubwa unapata kazi za kuwalinda watu maarufu, kulinda ‘stage’ pindi wanamuziki wanapoburudisha. Ajira nyingine ni wakati wa maadhimisho makubwa ya kitaifa, kucheza filamu, na mwonekano mzuri,” anasema Msuya.

Kijana anayekunywa dawa hizi huweza kuongezeka kilo tano hadi 15 ndani ya miezi miwili. Mzunguko na msukumo  wa damu yake huongezeka kiasi cha asilimia 20, jambo linalosababisha misuli yake kujaa.

Misuli hii huonekana wazi zaidi kwani dawa hizi husaidia kuchoma kalori kwa kiasi kikubwa  n husababisha mwili  kupoteza mafuta mengi.

Madhara

Madhara yanayoweza kuwakuta vijana wanaotunisha misuli kwa kutumia  vidonge vya vichocheo au steroids ni pamoja na maradhi ya moyo, lehemu mbaya mwilini, chunusi, upara, mabadiliko ya utendaji kazi wa moyo, ini na figo huweza kuharibika. Wengine huweza kupata matiti kama ya mwanamke. Kwa upande mwingine, wanawake wanaotumia dawa hizi hupata sauti za kiume na ndevu.   Mengine ni kukosa uwezo wa tendo la ndoa, kusinyaa au kupotea kwa korodani, tezi dume kukua, kuwa na hasira, shinikizo la damu.

Madhara mengine ni ogani muhimu kushindwa kufanya kazi ghafla, kama vile ini. Kifo cha ghafla, saratani na figo kushindwa kufanya kazi.   Lakini pia, wataalamu wanasema wengi wanaotumia dawa hizi hugeuka kuwa wajeuri na wenye hasira za haraka.

Namna ya kumfahamu anayetunisha misuli kwa dawa

Ingawa ni vigumu kumfahamu mtu anayetumia dawa za kutunisha misuli kwa asilimia 100 hasa kwa wale ambao hawajatumia dawa kwa muda mrefu, lakini unaweza kumfahamu mtu aliyetumia dawa hizo.

Kwanza wengi hupata misuli mingi kwa wiki chache, na misuli yao hujitokeza nje ya ngozi kama imepigwa ‘pampu’.

 Hata hivyo wataalamu wa afya wanasema, misuli ya mtu anayetumia dawa si imara kama ya mtu anayefanya mazoezi.

Watunisha misuli waliopatwa na vifo vya ghafla

Inasadikiwa kuwa asilimia kubwa ya watunisha misuli hawa, walifariki dunia ghafla kutokana na dawa za kutunisha misuli na wakati mwingine wakizichanganya na dawa za kulevya. Wa kwanza ni Carlos Rodrigues, Mohammed Benaziza, Chuck Sipes, Ray McNeil, Andreas Munzerm, Sonny Schimidt, Don Youngblood na Paul Demayo.

Mfamasia katika Hospitali ya Mirrs ya Mwenge, David Cyprian anasema, kikubwa kinachofanywa na watunisha misuli ni matumizi mabaya(abuse), ambapo dawa zinazotumika kufanya kitu kingine hutumiwa  kujenga misuli. Anatoa mfano kuwa, dawa za vichocheo vya kiume(testosterone) na Steroids, zina kazi ya kuwasaidia watu wanaochelewa kupata balehe, wenye matatizo ya ugumba na waliopoteza uzito mkubwa kwa sababu ya maradhi ya HIV.

 “Hata wanariadha nao hutumia dawa za aina hii kwa sababu ya kuongeza nguvu na kujenga misuli. Lakini ili kupata uhakika iwapo mtu ametumia dawa za aina hiyo, mkojo wake hupimwa” anasema.

Mlinzi Mkuu wa Ukumbi wa Swispub, Tabata na mwalimu wa mazoezi, Selemani Bwagege anashauri vijana kufanya mazoezi na kufuata nidhamu ya mazoezi badala ya kutumia dawa.

“Mambo mengine tunayaiga ingawa hayana umuhimu kwetu kiafya. Ukifanya mazoezi unapata umbile kubwa na langu,” anasema.

Anakiri kuwa, vijana wengi wanaotaka miili mikubwa wanafanya hivyo kwa ajili ya ajira.

 Zifahamu dawa za  Steroidi

Mfamasia wa Msuya anaeleza kuwa Steroidi zilitengenezwa viwandani kwa mara ya kwanza katika miaka ya 30 ili kuwatibu wanaume ambao walishindwa kutokeza homoni za kutosha. Leo, steroidi hutumiwa kurekebisha kudhoofika kwa mwili kunakosababishwa na virusi vya Ukimwi na magonjwa mengine.

“Hata hivyo, Steroidi hutumiwa sana na watu wasio na uhitaji wa kitiba. Katika miaka ya 50, steroidi zilianza kupatikana kimagendo, na wana-michezo waliojitakia sifa walianza kuzitumia kuongeza nguvu mwilini,” anasema.

TFDA wazungumzia dawa hizo

Msemaji wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Gaudensia Simwanza anasema dawa za kutunisha misuli zinaingia nchini kwa utaratibu wa uingizaji wa dawa na kabla ya kusajiliwa hupitia maabara na kupimwa.

Hata hivyo, anasema dawa hizo zinapotumika bila kuandikiwa na daktari na kutumiwa kiholela, huweza kusababisha madhara ingawa zikitumika kwa sababu husika madhara ni madogo, lakini zikitumiwa kwa sababu nyingine husababisha madhara.
Viewing all 104667 articles
Browse latest View live




Latest Images