Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

IGP Sirro: Ni Kosa Polisi Kudai Hela ya Mafuta kwa Raia..!!!!

$
0
0

Mkuu wa Jeshi la polisi nchini (IGP), Simon Sirro amewataka makamanda wa polisi mikoa kuhakikisha wanatumia vizuri mafuta ya magari wanayowekewa ili kuepuka malalamiko ya wananchi kwa magari ya polisi kukosa mafuta.

Pia amesema hataki kusikia polisi hawajafika katika tukio kutokana na kisingizio cha kutokuwa na mafuta.

IGP Sirro alisema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari jana mkoani Morogoro na kuongeza kuwa ni kosa kwa mwananchi kudaiwa fedha za mafuta ya gari la polisi.

IGP Sirro yupo katika ziara ya kuangalia hali ya uhalifu katika mikoa akitokea mkoani Dodoma.

Alisema mafuta ya gari yapo katika bajeti ya Jeshi la Polisi kwa kila mkoa hivyo kinachotakiwa ni makamanda wa mikoa kuhakikisha kuwa wanayatumia vizuri.

“Ni jambo la kusikitisha mwananchi kutakiwa kuchangia mafuta ya gari la polisi,hili hatuliruhusu kabisa,” alisema Sirro

Hivi karibuni, wakazi wa Malinyi walimlalamikia Mkuu wa Wilaya hiyo Jacob Kassema kwa kuwachangisha Sh800,000 za mafuta ya gari lake. Hata hivyo, Kassema alikanusha suala hilo.

Mbali ya suala la mafuta, IGP Sirro aliwatoa hofu wananchi na kusema Serikali inaendelea na uchunguzi wa kina kuhusu mauaji yanayoendelea mkoani Pwani.

“Ni kweli kuna tatizo la mauaji Pwani lakini askari wetu wapo kazini mchana na usiku kutafuta suluhisho la tatizo,” alisema Sirro.

Kampuni ya Japan Yaajiri Paka na Mbwa ili Kuwaliwaza Wafanyakazi Wenye Mawazo Pindi Wanapokuwa Ofisini..!!

$
0
0

Makampuni ya Japan yanafahamika kwa kuwa na muda mrefu zaidi wa kazi pamoja na misongo ya mawazo inayowakabili wafanyakazi wake, na sasa baadhi yamedai kuwa waajiriwa wapya ambao ni wanyama ‘paka’ na ‘mbwa’ wanaweza kuwa dawa ya matatizo hayo.

Kampuni ya Workaholic inayotajwa kwa kuwa na muda mrefu zaidi wa kazi, imedai kuwa tangu iwaajiri wanyama hao ufanisi wa kazi umeongezeka.

Wanyama hao huongeza furaha na ‘kampani’ kwa wafanyakazi.

Hidenobu Fukuda, kiongozi mkuu wa kampuni hiyo amesema kuwa amekuwa akiwalipa mishahara paka na mbwa hao wanaoingia ofisini, na kwamba anaridhishwa na kazi wanayoifanaya kwani hata baadhi ya wafanyakazi wamekiri kupunguza msongo wa mawazo.

“Mbali na mishahara, pia huwa ninalipa ¥5,000 ($45) kila mwezi kwa wote wanaoangalia usalama wa paka hao,” alisema Fukuda.

Alisema kuwa watumishi hao wapya ambao kazi yao kubwa ni kuwafariji na kuwapa kampani wafanyakazi ofisini, wamefunguliwa akaunti kwenye mitandao ya kijamii.

Baada ya Leseni ya Magari Kufutwa..Polisi Waagizwa Kuyaachilia Magari Yote Yaliyokamatwa kwa Kutokuwa na Leseni..!!!

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba ametoa agizo kwa Jeshi la Polisi nchini kuyaachia magari yote ambayo yanashikiliwa na Jeshi hilo kwa kosa la kutolipia ada ya mwaka ya leseni ya magari.

Waziri Mwigulu ametoa agizo hilo baada ya Serikali kufuta ada hiyo ambayo italipwa mara moja tu gari litakaposajiliwa.

Serikali imetangaza kufuta ada hiyo pamoja na kutoa msamaha wa kodi, riba na adhabu zinazoambatana na madeni yote (Tax Amnesty) ya ada hiyo yaliyolimbikizwa kwa miaka ya nyuma.

Majaliwa Apokea Taarifa Uchunguzi wa Salfa, Ni ya Makontena 211 Yaliyokuwa Bandarini Dar..!!!!

$
0
0

Waziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema salfa iliyoingizwa nchini kwenye makontena 211 haina kasoro na inafaa kwa matumizi ya kupulizia kwenye mikorosho.

Majaliwa amesema hayo wakati akizungumza na wajumbe wa kamati maalum, waagizaji wa salfa na baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Korosho nchini (CBT) kwenye kikao alichokiitisha kwenye makazi yake, Oysterbay, jijini Dar es Salaam.

“Bodi kaandaeni taratibu za kawaida kusambaza salfa kwa wakulima ili waanze kupuliza dawa hiyo. Wasichelewe kupuliza kwa sababu msimu umeshaanza,” amesema.

Juni 4, mwaka huu Waziri Mkuu alimuagiza Mkemia Mkuu wa Serikali, Prof. Samuel Manyele aende kuchunguza mzigo wa salfa ulioko bandari ya Dar es Salaam baada ya kutokea mkanganyiko uliosababishwa na ripoti ya TPRI kuwa ya salfa iliyoingizwa nchini na kampuni ya ETG Inputs Ltd kwa niaba ya Bodi ya Korosho haijakidhi viwango.

Waziri Mkuu alichukua hatua hiyo baada ya kubaini kuwa kuna mkanganyiko miongoni mwa wakulima juu ya matumizi ya kiuatilifu hicho licha ya kuwa Serikali ilikwishapokea taarifa ya bodi, na taarifa ya kampuni iliyotengeneza salfa hiyo na taarifa iliyoletwa na mwagizaji ambayo 
imethibitishwa na makampuni matatu ya kimataifa. Aliyataja makampuni hayo matatu kuwa ni InterTech, Bureau Veritas na SGS.

Akitoa taarifa ya uchunguzi wao mbele ya Waziri Mkuu, Prof. Manyele alisema walifanya uchunguzi kwenye makontena 21 ambayo ni sawa na asilimia 10 ya makontena yote 211 ili kubaini ubora wake.

“Uchunguzi ulifanyika kwenye maeneo ya purity, acidity na moisture contents kama ulivyokuwa umeelekeza. Sampuli zilichukuliwa kutoka GALCO Inland Container Depot iliyoko Chang’ombe ambako ndiko mzigo wa salfa ulioletwa na kampuni ya ya ETG Inputs Ltd unahifadhiwa,” alisema.

“Kwa kuzingatia matokeo ya kiuchunguzi wa kimaabara uliofanyika, viwango (specifications) vilivyowekwa ndani ya mkataba na viwango vya Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) kuhusiana na kiuatilifu cha salfa ni maoni yetu kuwa mzigo wa salfa ulioko ndani ya makasha (containers) 211 unakidhi viwango,” alisema kwenye taarifa yake.

Naye, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho nchini, Bw. Maokola Majogo alisema yeye pamoja na Bodi yake watatekeleza maelekezo ya Waziri Mkuu na akawataka wakulima wasisite kutumia salfa hiyo kwani imekwishathibitishwa na Mkemia Mkuu kwamba haina matatizo.

Mali za Rafiki wa Ivan Bongo Zakamatwa, Aingizwa Kwenye Sakata la Madawa ya Kulevya..!!!

$
0
0

Majanga! Lile sakata la tuhuma za kujihusisha na biashara na matumizi ya madawa ya kulevya ‘unga’ lililowagusa watu wa kada mbalimbali, wakiwemo baadhi ya mastaa wa Bongo kwa majina yao kutajwa kwenye orodha ya mkuu wa mkoa, miezi kadhaa iliyopita, limemkumba rafiki wa aliyekuwa mume wa Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, marehemu Ivan Ssemwanga ‘Don Ivan’ ambaye pia ni msanii wa Bongo Fleva, Patrick Christopher ‘PCK’ (29).
BREAKING NEWS

‘Breaking news’ zilizolifikia Risasi Jumamosi zilieleza kuwa, kufuatia tuhuma hizo, mali za msanii huyo ambazo ni nyingi kiasi cha kushangaza kutokana na umri wake mdogo, zinadaiwa kukamatwa jijini Dar. Chanzo makini kilicho karibu na msanii huyo kilidai kuwa, katika orodha ya mkuu wa mkoa wa Dar, jina lake liliingizwa kwenye listi ya kwanza iliyotolewa na mkuu huyo, lakini hakuwepo nchini hivyo aliporejea ndipo akajaa kwenye mikono ya polisi na sasa kesi yake hiyo, tayari ipo mahakamani

“Mali za PCK zinashikiliwa yakiwemo magari matatu, Toyota Prado (shilingi milioni 60), Nissan Murano (shilingi milioni 45) na Toyota V-Mark (shilingi milioni 32) na nyumba ya ghorofa ya kifahari iliyopo maeneo ya Kigamboni (Dar) jirani kabisa na Ufukwe wa Bahari ya Hindi huku akaunti zake zote za benki zikifungwa kutokana na kuwa kiasi kikubwa cha fedha hadi kesi yake itakapomalizika kwa sababu inasemekana mali hizo siyo za halali.

“Unaambiwa sasa hivi jamaa ana hali ngumu mno maana kesi iko Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu (Dar) huku hati ya kusafiria na vitambulisho vyake vyote vikiwa vimeshikiliwa na haruhusiwi kutoka nje ya Jiji la Dar.

“Kiukweli jamaa anatia huruma maana unajua mtu ukishazoea maisha ya kitajiri na uhuru ni vigumu sana kuwa sawa pale unapokosa hivyo vitu. “Mali zake zimekamatwa kwa kuwa inasemekana siyo za halali kwani haijulikani anafanya biashara gani ambazo zinaweza kumwingizia kipato kikubwa kiasi hicho hivyo anachunguzwa ndiyo maana zinashikiliwa,” kilisema chanzo hicho.

RISASI JUMAMOSI LAMSAKA

Baada ya kunyaka ishu hiyo, Risasi Jumamosi lilimsaka PCK kwa siku tatu hadi alipopatikana ambapo alibanwa hadi akakubali kufunguka. Msanii huyo anayetamba na Nyimbo za Nitazame Usoni na Sweet Baby aliyomshikisha Mwanamuziki Barnaba Elias alikiri mali zake kushikiliwa na akaunti zake kufungwa huku akieleza kuwa, hawezi kuzungumza zaidi kwani atakuwa anaingilia uhuru wa mahakama.

“Ni kweli mali zangu zimeshikiliwa yakiwemo magari na nyumba iliyopo Kigamboni. Pia vitambulisho na hati za kusafiria zimeshiliwa. Siwezi kusema ni shilingi ngapi zilizopo benki wala siwezi kuzungumzia sana ishu hii maana tayari iko mahakamani Kisutu,” alisema PCK.

NI RAFIKI WA IVAN

Risasi Jumamosi lilimweleza kuwa, lilitonywa kwamba ni rafiki wa marehemu Ivan hivyo kumtaka kufafanua juu ya hilo ambapo alifunguka: “Ni kweli Ivan alikuwa ni rafiki yangu sana. Ndiye aliyenitoa kwenye maisha ya ziro mpaka hivi nilivyo sasa na ukaribu wetu ulikuwa mkubwa sana. “Niliishi naye jijini Kampala Mtaa wa Munyonyo (Uganda) kati ya mwaka 2000 na 2001.

“Mwaka 2002, Ivan alihamia Afrika Kusini, nikabaki Kampala, ilipofika mwaka 2004, aliniita huko (Afrika Kusini) nikawa nimehamia. Mwaka 2007 niliamua kurudi Bongo kwa sababu ndiyo nyumbani na kuanza kujitegemea mwenyewe, lakini bado urafiki na biashara zetu ziliendelea na muda mwingi tulikuwa wote Afrika Kusini kwenye biashara zetu wiki kadhaa zilizopita kabla ya kuumwa na kufariki dunia.

“Nimeanza kuhaso na maisha haya muda mrefu sana. Huwa sichagui kazi ya kufanya hivyo nafanya biashara mbalimbali kwa kusafiri nje ya nchi kama Uingereza, China, Afrika Kusini na kwingineko. Pia nafanya Muziki wa Bongo Fleva.”

MSIKIE MWANASHERIA WAKE

Risasi Jumamosi lilizungumza na mwanasheria wake anayesimamia kesi hiyo ambaye alijitambulisha kwa jina la Musa Ngonyani ambaye alisema mteja wake huyo anashitakiwa kwa kumiliki mali haramu. “Kesi inaendelea Mahakama ya Kisutu na namba yake ni CC 247/2017 na inaendeshwa na Hakimu Kihawa na itatajwa tena Juni 13, mwaka huu.”

MAMLAKA YA MADAWA YA KULEVYA

Akizungumzia kinachoendelea juu ya vita dhidi ya madawa ya kulevya, Afisa Habari wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Florence Bahati Khambi alisema kuwa, vita hiyo inaendelea na hakuna ambaye atabaki salama, awe muuzaji, mtumiaji au yeyote yule.

Hizi Hapa Sababu za Bosi wa Ewura Kutumbuliwa Jipu Usiku wa Manane ..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo Jumatatu ya 12/6/2017..!!!

Wanaharakati Walia Baada ya Serikali Kusahau Bajeti ya Pedi za Wanawake Kwenye Bajeti Kuu ya Serikali..!!!

$
0
0

Wakati idadi kubwa ya watu wakiisifia bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2017/2018 kwa kuwakumbuka wanyonge, baadhi ya wanaharakati wameikosoa bajeti hiyo kwa kutokumbuka kupunguza gharama ya pedi za wanawake.

Mkurugenzi wa Baraza la Usambazaji maji, Wilhelmina Malima amesema kuwa ingawa serikali imeondoa kodi kwenye bidhaa mbalimbali, imesahau eneo muhimu zaidi la afya ya akina mama na wasichana.

Alisema kuwa wapo wanafunzi wengi wa kike ambao wamekuwa wakiacha shule kutokana na kushidwa kujihifadhi kwa usafi na usalama wanapokuwa katika siku zao za mwezi, na kwamba baadhi yao kutokana na kushindwa kumudu gharama za pedi wamekuwa wakitumia vipande vya nguo ambavyo sio salama.

“Tunawezaje kulinda haki za wanawake na wasichana bila kukumbuka afya yao kama kipaumbele cha kwanza?” alihoji.

Aliongeza kuwa bidhaa hiyo ni muhimu kwa kina mama wakati wa kujifungua, lakini ameshangaa kuona hali hiyo haipewi nafasi kwenye bajeti husika.

Naye Mkugugezi wa program ya mtandao wa jinsia (TGNP), Lilian Liundi ameliambia gazeti la The Citizen kuwa Serikali imekuwa ikiahidi kutoa kipaumbele kwa afya ya wanawake na wasichana lakini haijaonesha jinsi ambavyo itasaidia upatikanaji wa pedi kwa gharama nafuu.

Gharama za bidhaa hiyo imekuwa changamoto zaidi hasa maeneo ya vijijini na kwa familia masikini ambazo watoto wengi wametajwa kutohudhuria shule pale wanapokuwa katika siku zao.

Mlela Achekelea Dili la Kuigiza Tamthilia Kenya..!!!

$
0
0

BAADA ya mwaka jana kula shavu la ku­cheza tamthiliya nchini Kenya kwa mwaka mmoja ambalo limeisha mwezi huu, staa wa fil­amu Bongo, Yusuf Mlela amejikuta akichekelea baada ya kupata kazi ny­ingine tena.

Akipiga stori na Risasi Jumamosi, Mlela alisema ana furaha kubwa kupata kazi nyingine inayokwenda kwa jina la Nyota ambayo ni ya miezi saba watai­fanya na wasanii wa Kenya pamoja na wa Tanzania ambao ni Daud Michael ‘Duma’, Salama Salmini ‘Sandra’ na Hasheem Kambi.

“Nimefurahi sana kwa kweli maana kazi ya kwanza ndiyo nimemaliza mwezi huu sasa nimepata nyingine ambayo tut­aifanya kwa miezi saba, najiona mwenye bahati sana kwa kweli maana Kenya ninajifunza mam­bo mengi yanayohusiana na filamu, lakini pia nitatengeneza pesa zaidi kupitia kazi yangu hii,” alisema Mlela.

Credit - Risasi

Huzuni Sana..Soma Maneno Haya ya Kanumba Aliyoyaweka Kwenye Blog Yake Siku Chache Kabla ya Kufa...!!!

$
0
0

Look at this pic careful,,,moja ya vitu tulivyotofautishwa na wanyama na ndege ni Akili ya kujua mema na mabaya,tizama hao ndege na huyo mbuzi hawana akili kabisa lakini wanapendana ndio maana unaona wako pamoja ILA binadamu aliyepewa akili ana roho mbaya sana,katika mafundisho ya YESU KRISTO alisema neno kuu nawapeni PENDANENI.hata uwe na uwezo wa kuhamisha milima kama huna upendo ni bure,mpende jirani yako kama unavojipenda,upendo 

haujivuni,hauhesabu mabaya,hautakabari,hauhusudu.....nk,1WAKORINTHO 13.Mungu ana akili sana kutuumba kwa mwili huu wa nyama laiti kama angetuumba kwa vioo au sightmirror ili uweze kuona mwenzako anakuwazia nini?anakufanyia nini?anapanga nini juu yako ungekuta ni heri ukaishi msituni na wanyama wakari kuliko kukaa na binadamu,katika tafiti zangu nimegundua kuna dawa mbalimbali mfano ya kichwa,homa,nk Lakini dawa ya Chuki na roho mbaya hakuna,,kama hiki kingekuwa kipindi kama kile cha zamani za Sodoma na Gomora au cha Nuhu ambacho Mungu alikuwa akiadhibu hapo hapo watu wengi sana wangeumbuka hasa wale wanaojifanya wasafi usoni lakini rohoni ni tofauti,Mungu atusaidie sana hasa sisi vijana tujue kusimama katika ukweli na uwazi,tuubebe upendo wa dhati toka rohoni huku mdomoni tukitamka amani ya kweli impendezayo Mungu ili watoto wetu waje watuenzi kwa mazuri na dunia ijivunie uwepo wetu.

Chambuso Amtetea Aslay kwa WCB..Adai Hayupo Karibu na Ali Kiba

$
0
0
Vita ya Diamond na Alikiba haijawahi kumuacha mtu salama.

Meneja wa Aslay, Chambuso amemtetea msanii wake huyo kuwa hajawahi kuwa na ukaribu na Alikiba. Hilo limekuja baada ya kusambaa maneno kuwa hitmaker huyo wa ‘Muhudumu’ ameingia kwenye mgogoro na WCB kutokana na ukaribu wake na Alikiba.

Akiongea Ijumaa hii katika kipindi cha FNL, Chambuso amesema, Aslay hajawahi kuwa karibu na Kiba na wala hakuwa na wimbo wowote ambao tayari wameurekodi kama inavyosemwa na baadhi ya watu. Ameongeza kuwa wala hakuna tatizo lolote kati ya Aslay na WCB.

Chambuso amepigilia msumari kwa kusema, nyimbo alizoachia Aslay ni kama zawadi hajaanza kufanya kazi rasmi ila baada ya kupita mwezi mtukufu wa Ramadhan wataanza kuachia nyimbo za msanii huyo rasmi.

Gor Mahia Mabigwa SportPesa Super Cup 2017: Yaigaragaza AFC Leopards goli 3-0

$
0
0
Gor Mahia
Baada ya mbio ndefu za michuano ya SportPesa Super Cup hatimaye Jumapili hii Klabu ya Gor Mahia kutoka nchini Kenya wamechukua kombe hilo kwa ushindi wa goli 3-0 dhidi ya mahasimu wao, AFC Leopards ambao pia wanatoka nchini Kenya.



Gor Mahia wamepata goli lao kwanza kupitia kwa mshambuliaji wao Otieno Philemoni kunako dakika ya 18 kipindi cha pili. Timu hiyo iliongeza kasi zaidi na kujipatia magoli mengine wawili na kuufanya mchezo huo kumalizika kwa kuwafunga AFC Leopards goli 3 kwa nunge.


Gor Mahia kwenye safari yake mpaka kufika fainali ya SportPesa Super Cup imezitoa klabu za Jang’ombe Boys kutoka Zanzibar na Nakuru All Stars .

Kwa ushindi huo klabu ya Gor Mahia imeibuka na kitita cha Dola elfu 30,000 za kimarekani na imepata nafasi ya  kuchuana na Klabu ya Everton kutoka England Tarehe 13 July mwaka huu.

Michuano ya SportPesa Super Cup imeandaliwa na Kampuni ya kubashiri ya SportPesa ambao ni wadhamini wa Klabu za Simba SC, Yanga SC pamoja na Singida United zote kutoka Tanzania na jumla ya timu 8 zilishiriki michuano hiyo ambapo timu zote nne kutoka Tanzania zilitolewa.

Leo Ndio Leo..Rais Magufuli Kukabidhiwa Ripoti ya Pili ya Mchanga wa Madini

$
0
0
John Pombe MAgufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Magufuli leo Juni 12, anatarajiwa kupokea taarifa ya Pili ya wachumi na wanasheria iliyofanya uchunguzi wa madini yaliyo kwenye makontena yenye mchanga wa madini yaliyopo katika maeneo mbalimbali nchini.
Tokeo la picha la magufuli
Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais imesema, tukio hilo linatarajiwa kurushwa mubashara kupitia vyombo vyote vya habari zikiwemo Runinga, Redio, mitandao ya kijamii na tovuti rasmi ya Ikulu.
Rais Magufuli alipokea  ripoti ya kwanza ya uchunguzi kuhusu mchanga wa madini ambao husafirishwa nje ya nchi kwa kutumia makontena, mnamo Mei 24, mwaka huu na baada ya Kamati kuwasilisha taarifa hiyo.

Wachumi na wasomi sanjari na wabunge walitoa maoni tofauti kuhusiana na sakata hilo lililobaini Tanzania hupoteza mabilioni ya fedha kupitia rasilimali zake kutokana na baadhi ya wawekezaji na watumishi wa Umma kutokuwa waaminifu.

Hata hivyo ripoti hiyo ya kwanza ilisababisha Waziri wa nishati na Madini, Pro. Sospeter Muhongo na baadhi ya watendaji wa sekta hiyo kufukuzwa kazi.

Zitto Kabwe Afunguka Mazito kutimuliwa kazi kwa Mkurugenzi Mkuu wa EWURA

$
0
0
Zitto Kabwe
Hili la Mkurugenzi Mkuu wa EWURA linahusu tangazo la leseni ya Kampuni ya kifisadi ya IPTL?

Ni muhimu sana Rais afahamu kwamba kuna kazi kubwa ya chinichini inafanywa na wasaidizi wake ( sina hakika kama yeye Rais anajua na au ameruhusu kazi hiyo ) kuendeleza wizi huu wa watu wa PAP ya Harbinder Singh Seth na IPTL.

Kwenye kesi ya Standard Chartered Bank dhidi ya TANESCO huko mahakama ya ICSID ambapo TANESCO wanatakiwa kulipa shilingi 352 bilioni kwa Benki hiyo, Wanasheria wa TANESCO na wale wa PAP/IPTL wanashirikiana kwa karibu mno. Kwenye rufaa, TANESCO wametakiwa waweke fedha hizo kwanza kwenye akaunti ya Benki ya nje kabla ya rufaa kusikilizwa.

PAP/IPTL wanalinda ufisadi wao kwa kujifanya wanashirikiana na TANESCO kwenye kesi. Kwenye Taarifa ya PAC kuhusu Tegeta Escrow Account, tuliweka wazi kuwa PAP/IPTL waliweka dhamana kuwa ikitokea madai yeyote yale dhidi ya TANESCO basi PAP/IPTL italipa.

Madai yametokea, matapeli hawa wanajifanya kushirikiana na Shirika letu na Wanasheria wa Serikali wanawasaidia matapeli hawa na sasa wanataka kuwaongezea leseni ya Biashara. Kwanini Serikali isitumie ile Indemnity kuwataka PAP kulipa hizi fedha? Kwanini Serikali inayosema inapambana na ufisadi inawakumbatia mafisadi wa PAP/IPTL?

 Kwanini Serikali iliyoonyesha ujasiri wa kupambana na Kampuni kubwa kama Acacia/Barrick inayumbishwa na matapeli hawa? Tena tapeli mmoja tu Harbinder Singh Seth?

Vyombo vya Serikali pia vinahusika na kuwalinda hawa matapeli. Kwa mfano, huko ICSID Shirika letu la TANESCO kupitia wanasheria wake wamepeleka hoja kwamba Maazimio ya Bunge kuhusu Tegeta Escrow hayana msingi wowote wa kisheria na kwamba Bunge linapiga porojo tu.

Wanasheria hawa wameomba Ofisi ya Bunge iwape barua kuthibitisha kuwa Maamuzi ya bunge hayana msingi wowote na ni maoni tu yanaweza kudharauliwa na kutupiliwa mbali. Shirika la Umma linalosimamiwa na Bunge linapeleka barua kwenye vyombo vya kibeberu kuwa Bunge porojo tupu.

Pia kwa kudanganywa na PAP/IPTL, TANESCO wamepeleka madai kuwa PAC ilihongwa kufikia maamuzi yaliyofikiwa na Bunge. Wametengeneza barua pepe za kujaribu kushawishi madai yao hayo na hata Taasisi muhimu kama PCCB waliingia kwenye mkenge huo na kuniita kunihoji.

Niliwapa ushirikiano wote na kuwapa simu na computer zangu wachunguze barua pepe zile za kuchonga wakakuta hakuna lolote. Sikuwaacha, niliwaambia kuwa wao ni mawakala wa mashetani.

Wanashirikiana na matapeli kuwaibia Watanzania. Idara ya Usalama wa Taifa, inahusika moja kwa moja na kazi hii inayofanywa na PAP/IPTL ili kufanikisha mradi huu wa kitapeli. Sina hakika kama Rais aliidhinisha haya maana TISS na PCCB wanawajibika kwa Rais moja kwa moja.

Hivyo, inawezekana kabisa mpango wa kuongeza leseni ya IPTL akawajibishwa mtu wa EWURA kwa sababu ndiye alitoa tangazo la leseni, lakini huyo mtu wa EWURA anaweza kuwa ameshinikizwa na watu wa Usalama wa Taifa kufanya hivyo. Mimi naamini Rais, kwa jinsi alivyo, hawezi kuwa anahusika na haya matapeli, lakini Rais mtumbuaji anakaaje miezi 20 kwenye Kiti za Enzi bila kumaliza suala la IPTL ilhali kuna Maazimio ya Bunge yanayopaswa kutekelezwa?

Nawapa kazi ndogo Watanzania, tazameni lile Tangazo la EWURA kuhusu IPTL nililowawekea hapa siku limetoka. Tazameni umiliki na wamiliki wa IPTL hivi sasa. Kuna hisa 16% kwa kampuni mbili zenye majina ya ujanja ujanja. Kina nani hao wamegawiwa hizo hisa tena wakati wa Uongozi wa Rais John Pombe Magufuli.

RC Makonda Amwaga Mamilioni Fainali ya Mashindano ya Qur-an Dsm

$
0
0
Paul Makonda
Ikiwa ni nje ya Zawadi zilizokuwa zimeandaliwa kwajili ya Washindi wa mashindano makubwa afrika ya kuhifadhi na kusoma Qur-an juzuu 30 Kati ya washiriki 17 kutoka nchi 15 Barani Afrika yaliyofanyika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam, Tanzania, Katika hotuba yake Mkuu wa mkoa wa jiji hilo Paul Makonda naye kwa upande wake alitamka kuongeza shilingi Milioni 5 kwenye zawadi za washindi watano waliopatikana.

Mohamed Abdullah Aden kutoka Somalia ndiye ameibuka mshindi wa mashindano makubwa Afrika ya kusoma na kuhifadhi Qur-an juzuu 30 amekabidhiwa hundi ya Shilingi Milioni 15 kutoka Amana Bank, halikadhalika amepewa cheti cha ushindi, Ipod na kuchagua kwenda nchi yeyote duniani, kijana huyo wa miaka 12 ametoa wito kwa vijana kujibidisha Katika kusoma Qur-an.

Mashindano hayo ya 18 yaliyo andaliwa na Taasisi ya Al-hikma Foundation yamehudhuriwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kasim Majaliwa, Mufti Mkuu wa Tanzania Abubakar Zubeiry, Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda, Skeikh Mkuu Dar es salaam Alhad Mussa Salum, Rais mstaafu Ali Hassani Mwinyi Sambamba na ujumbe Maalumu kutoka nchini Saudiarabia.

Mwanariadha Usain Bolt Awaaga Mashabiki Wake Kibabe

$
0
0
Usain Bolt
Mwanariadha maarufu duniani kutoka Jamaica, Usain Bolt amewaaga rasmi mashabiki wake kushiriki mashindano ya riadha nchini humo kwa kushinda mbio za mita 100.


Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 30 ambaye ni mshindi wa medali 8 za dhahabu katika michuano ya Olimpiki, ameshinda kirahisi katika mashindano ya mita 100 yaliyofanyika juzi huko Kingstone, Jamaica kwa kutumia sekunde 10.03.

Mbali na ushindi huo aliyoupata juzi, Bolt alikiri kuwa haikuwa kazi rahisi kwa kuwaalijawa na uoga kwa kuogopa kuaga mashabiki wake kwa aibu.

“Nimezoea kuona mashindano yote kama kawaida tuu kwani huwa najiamini ila ya leo nimeona migumu sana na nilishikwa na hofu kama ningeshindwa ningeumia sana kuwaaga mashabiki wangu“Alisema Usain Bolt kwenye mahojiano yake na mtandao wa MSN.

Hata hivyo Usain Bolt anatarajia kustaafu mchezo huo mwezi Agosti mwaka huu baada ya mashindano ya dunia ya riadha yatakayofanyika London, Uingereza.

Mtoto wa Marehemu Gaddafi Aaachiliwa Huru Baada ya Kuzuiliwa kwa Miaka 6..!!!

$
0
0

Mtoto wa pili wa Kiongozi wa zamani wa Libya Muammar Gaddafi, Saif al-Islam Gaddafi ameachiwa huru baada ya kuzuiliwa kwa kipindi cha miaka sita.

Saif al-Islam aliyependekezwa na babake kuwa mrithi wake amekuwa akizuiliwa na kundi la wanamgambo wenye itikadi kali Abu Bakr al-Siddiq Battalion katika mji wa Zintan kwa miaka sita.       ambaye alitekwa anadaiwa kuachiliwa huru baada ya kupewa msamaha.

Taarifa kutoka mtandao wa Al Jaazera zinasema Wanamgambo hao walimuachilia huru jana Jumamosi ingawaje mpaka sasa bado hajaoneshwa hadharani.

Saif al-Islam Gaddafi  alihukumiwa kifo na mahakama mjini Tripoli, magharibi mwa nchi hiyo bila yeye kuwepo mahakamani kwa makosa ya umwagaji damu kwa raia waliokuwa wakiandamana dhidi ya utawala wa baba yake.

Maeneo ya magharibi yanatawaliwa na serikali inayopingana na serikali ya mashariki mwa Libya, lakini serikali hiyo ya magharibi yenye makao yake makuu Tripoli ndiyo inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa.

Awali ziliwahi kuvuja taarifa za uongo kuachiliwa kwake, na wataalam wa masuala ya kidiplomasia na kisiasa wanasema kuachiwa kwake huenda hatua hiyo ikatikisa zaidi hali ya kisiasa na kiusalama nchini Libya.

Saif al-Islam anatafutwa pia na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) yenye makao yake mjini The Hague, Uholanzi kwa tuhuma za uhalifu dhidi ya binadamu, makosa anayodaiwa kuyatekeleza wakati wa juhudi zilizofeli za kujaribu kuzima maasi kabla ya babake kuondolewa madarakani na kuuawa.

Pwani: Kiongozi Mwingine wa CCM Auawa Kinyama Ikwiriri..!!!

$
0
0

Wingu la mauaji limezidi kutanda katika Wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani. Taarifa zinasaema kiongozi mwingine wa CCM ambaye ni mjumbe wa shina, ameuawa katika kijiji cha Ikwiriri na watu wasiojulikana na mwili wake kutelekezwa eneo la Daraja tatu Wilayani humo.

Akizungumza na Mtanzania jana Ndugu wa Marehemu, Isaka Hamis alimtaja ndugu yake aliyeua kuwa ni Masunga Mayuka.

Nlipokea taarifa za tukio hilo leo(jana) asubuhi wakati huo nikiwa nyumbani kwangu. Mdogo wangu ambaye anaishi Ikwiririndiye wa kwanza kunijulisha juu ya tukio hilo, alinipigia simu, alisema Isaka.

Alisema kwa mjibu wa Maelezo ya mdogo wake huyo, ndugu yao aliuawa akiwa njiani kwenda Msikitini kufanya ibada.

" Mdogo wangu alinieleza, inadaiwa Mayuka alikutana na wauaji njiani ambao walimpiga Risasi na baada ya kitendo hicho walitokomea kusikojulikana" alisema.

Alisema saa chache baada ya kupokea simu ya mdogo wake huyo, alipokea tena simu ya ndugu yake mwingine ambaye naye alimjulisha jambo hilo hilo la kusikitisha.

"Nlielezwa kwamba ndugu yangu aliuawa huku akiwa anajitetea mbele ya watu hao Wasimdhuru, Sasa tupo msibani tunajiandaa kwa maziko" alisema Isaka.

Akizungumza na Mtanzania Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga, alise,a hajapokea taarifa hizo na kuahidi kuzifanyia kazi. "Sina hizo taarifa, sijazipokea labda na mimi nizifuatilie hivi sasa". alisema.

Tangu mauaji hayo yatokee, inadaiwa watu takriban 38 wamekwisha kuuawa.

Chanzo: Mtanzania

Ukweli Kuhusu Ndege ya Air Tanzania "Kuegeshwa" Bila Kuruka

$
0
0
Ndege ya Air Tanzania
Kifupi na kwa taarifa rasmi za kiufundi japo nipo mbali na nyumbani ni kuwa,ndege hiyo ya ATCL haijaharibika na sio kweli kuwa eti mainjinia 50 wameshindwa kuitengeneza.Daah!!Jamani huu uongo na masimango kwa shirika letu la ndege inatoka wapi?

Ni kweli hata mimi kuna mambo sikubaliani na JPM,hasa katika masuala ya bunge kuonekana mubashara na uminywaji wa upinzani,lakini simtakii mabaya wala kuizushia serikali yake uwongo.Yoyote unaemuuliza,wewe umepata wapi taarifa hizo?Atakwambia "Mange kasema"....Huyu anayetajwa ni Mhandisi?

Kwa wale waliofuatilia ujio wa ndege hizi wakati zinaletwa Tanzania,watakumbuka kuwa ndege moja ilitangulia kabla ya nyingine,iliyotangulia ni ile iliyokuja na namba za usajili za Canada za C-FHNF ambapo ilipofika Tanzania ikapewa namba ya 5H-TCB.

Hii 5H-TCB ndio ilianza kufanya kazi mbele ya ile ya pili yenye usajili wa 5H-TCD.Kwa hiyo hata kwa masaa ya kukaa hewani,hii iliyotangulia ya 5H-TCB ndiyo yenye masaa mengi hewani kuliko 5H-TCD iliyokuja baadae na kuanza kufanya kazi.

Ndege iliyoegeshwa kwa muda kwa ajili ya matengenezo madogo ni 5H-TCB,na hii si Tanzania tu,bali dunia nzima.Ndege inapofikisha masaa kadhaa kuwa hewani,let say masaa 12000 hewani,inatakiwa kuwa grounded ili kuweza kubadilishiwa vifaa kadhaa ambavyo masaa yake yanakuwa yamekwisha kwa vyenyewe kutimika.

Hii ni hata kwenye magari,tunashauriwa kutumia matairi ya magari kwa masaa kadhaa,yakipita hayo masaa basi tunapaswa kubadilisha,lakini kiswahili-swahili watu huendesha tu magari mpaka yanawapasukia na kupata ajali.Usafiri wa anga ni tofauti,mambo ya "safety" ni jambo la kwanza na la muhimu.

Kilichotokea kwa ndege moja ya ATCL ni kuwa grounded kwa sababu za kiufundi na kiusalama (safety),ili kufanyiwa "cheki" ya baadhi ya vifaa na kuweza kubadilishwa ili irudi hewani kwa uhakika zaidi.Hii ni kote duniani.

Sisi tunaweza kuona kwa wepesi sababu shirika letu la ATCL lina ndege mbili tu,moja ikienda "hunger" (maintanance area) inakuwa rahisi kujulikana sababu moja tu ndio inabaki ku-operate,lakini jambo hili ni kawaida,leo ukienda Kenya utakuta ndege zilizoegeshwa sbb ya masaa kupita,ukienda KLM,Swiss International,South Africa Airways,Qatar nk.Si jambo la ajabu,kwanini libebwe kama mada?

ATCL ni moja ya kampuni yenye wahandisi wazuri walio wazawa.Na kwa aina ya mkataba wa kampuni ya bombardier,mpaka sasa ATCL imekuwa "attached" na mtaalamu mmoja (Consultant) toka Canada,atakayekuwa kwa muda fulani kama mshauri wa kiufundi moja kwa moja toka kiwandani.

Habari hizo tuzipuuze,si njema kwa mafanikio ya heri ya shirika letu.Tuwatie moyo ATCL,inawasaidia sana watu katika usafiri wa ndani ya nchi.Kwa sasa safari zake za Dodoma,K'njaro,Tabora,Kigoma,Mtwara na Songea zimeokoa muda na kusaidia watu wengi.Safari ya Hahaya-Commoro imekuwa na mafanikio makubwa na yenye faida....Sio kila kitu yule "Binti" akisema kinakuwa na ukweli....

ATCL-The Wings of The Kilimanjaro.......

By Barafu

Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Maalim HUSSEIN Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa

$
0
0

Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Maalim HUSSEIN Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa  PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidiWhatsapp +255 674 835107 -calls +255746757102
Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote..

LIVE: Kamati ya Pili ya Mchanga wa Madini Ikiwasilisha Ripoti Yake kwa Rais Magufuli

$
0
0
Rais John Pombe Magufuli
Leo Kamati ya Pili ya Mchanga wa Madini Inawasilisha Ripoti Yake kwa Rais Magufuli. Fuatilia Matangazo ya Moja Kwa Moja Hapo Chini

 
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live




Latest Images