Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Tangaza Biashara yako Kwenye Blog yetu kwa Bei Rahisi

$
0
0
Tangaza nasi
Tangaza Biashara yako Hapa kwa bei rahisi...

Tunapokea matangazo madogo madogo kama vile uuzaji wa viwanja, nyumba, magari, Maduka na Biashara nyingine

Piga simu namba 0714604974 kwa maelezo zaidi

EWURA Wasitisha Mchakato wa Kuiongezea Leseni Kampuni ya IPTL....Ni Baada ya Waziri Mkuu kumsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu

$
0
0
EWURA
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imesitisha mchakato wa kushughulikia maombi ya IPTL ya kuongezewa muda wa leseni yake ya biashara kwa miezi 55 ili iendelee kuzalisha umeme na kuiuzia TANESCO.

Mbali na kusitisha mchakato huo, EWURA imesitisha pia upokeaji wa maoni kutoka kwa umma na wadau mbalimbali kuhusu kusudio lake la kuiongezea muda wa kufanyakazi nchini Kampuni ya IPT

Kimenuka Acacia Mining Wagundulika Kuwa Hawana Kibali cha Kufanya Kazi Nchini

$
0
0
Acacia Mining
Wakati Ripoti ya pili ikiendelea kusomwa mbele ya Rais , Imesema kuwa Kampuni ya Madini ya Acacia Mining Haikuwa na kibali cha kufanya Kazi Nchini wala hawakuwahi kusajiliwa

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Siku ya Leo

Sumaye Nchi Inaendeshwa Kishabiki

$
0
0
WAZIRI Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Fredrick Sumaye, amesema nchi inashindwa kuendelea kwa sababu inaendeshwa kishabiki  na kwamba mambo yanayofanyika hayana masirahi kwa taifa.

FREDRICK SUMAYE.
Akizungumza kwenye  Kongamano la Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha) na Umoja wa Vijana wa Vyuo Vikuu ambao ni wanachama wa Chadema (Chaso) jijini Mbeya alipokuwa mgeni rasmi, Sumaye alisema mambo mengi yenye masirahi ya taifa yakifanywa kimzaha yatasababisha madhara kwa taifa.

Sumaye ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, alisema miongoni mwa mambo ambayo ni ya maslahi ya taifa lakini  yanendeshwa kishabiki ni mikataba ya madini na bajeti isiyokuwa na uhalisia.

Mengine aliyoyataja ni uendeshaji wa Bunge ambalo kikatiba ni chombo huru ambacho hakipaswi kuiingiliwa na wabunge kufanya maamuzi kwa maslahi ya vyama vyao vya siasa huku wengine wakishangilia na kuzomeana.

Nchi kwa sasa inayumba na inashindwa kuendelea kutokana na kuendeshwa kishabiki, Bajeti yetu ya mwaka uliopita fedha za miradi ya maendeleo zilitolewa kwa asilimia 34 pekee na serikali ilikiri, lakini sasa hivi wanakuja na bajeti kubwa zaidi ya hiyo ambayo haijatekelezwa na wabunge wa CCM wanashangilia,” alisema Semaye na kuongeza:

Mambo haya yanaliingiza taifa kwenye matatizo makubwa, deni la Taifa linazidi kuongezeka, mikataba ya madini na mingine iliyokuwa ni yenye maslahi ya taifa sasa inakuwa ni ya hasara kwetu, lakini ukiangalia wabunge wanapiga meza wakishangilia.”

Sumaye alisema wasomi wa vyuo vikuu hawatumiki ipasavyo kwa maslahi ya taifa ikiwamo kujadili mikataba na bajeti ya taifa na mawazo yao kutumika katika kufanya marekebisho.

Alisema kipindi hiki ambacho bajeti ya 2017/18 inaanza kujadiliwa leo bungeni, ilitakiwa midahalo mbalimbali ifanyike vyuoni kuichambua, lakini kwa sasa ukifanya hivyo unaonekana umetumwa na vyama vya upinzani, kitu ambacho siyo sahihi.

Alisema miaka ya nyuma viongozi wa serikali walikuwa wanahudhuria katika Ukumbi wa Nkrumah katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kusikiliza mawazo ya wasomi, lakini kwa sasa vyuo vikuu vinatumika kama sehemu ya vijana kupata taaluma pekee.

Alisema Chadema imeamua kujitoa ili kupambana na taabu wanazopata wananchi kwa kuondoa ushabiki wa kisiasa.

Chadema tumeamua kuhakikisha tunawaeleza wananchi ukweli hata kama siasa zimezuiliwa, lakini tutafanya siasa mpya za kutumia akili kubwa,” alisema Sumaye.

Chadema Wamtwika Zigo Mke wa Edward Lowassa

$
0
0
Mke wa Lowassa Regina Lowassa
Wanawake wa Chadema wamemtwishwa Regina Lowassa mzigo wa kuongoza mapambano ya ushindi katika Uchaguzi Mkuu wa 2020.

Akizungumza na wajumbe wa Baraza Kuu la Wanawake wa Chadema (Bawacha) mjini Dodoma jana, Regina ambaye ni mke wa waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa, alisema maandalizi ya uchaguzi huo yanapaswa kuanza sasa.

Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Lowassa aligombea urais kupitia Chadema kwa kushirikiana na vyama vilivyounda umoja wa katiba ya Wananchi (Ukawa) na hivyo kuweka ushindani mkubwa dhidi ya chama tawala, ingawa hakushinda.

Jana, Regina alisema ushindi wa chama hicho uko mikononi mwa wanawake wa Tanzania. “Kwanza niwashukuru sana kwa mapambamo mliyoyafanya mwaka 2015. Nataka mfahamu kuwa bado Chadema inapendwa na ina nguvu kubwa kuliko wakati mwingine. Msikatishwe tamaa bali tusonge mbele,” alisema Regina.

Mama huyo aliwataka wajumbe kujiamini zaidi na kupeleka ujumbe kwa wenzao ambao wamedhamiria kufanya mageuzi makubwa, lakini akawataka wasilale.

Mwenyekiti wa Bawacha, Halima Mdee aliwataka wanawake kujitoa zaidi katika kukisaidia chama hicho, hasa katika maandalizi ya uchaguzi ujao.

Mdee aliwashauri wanawake wenye nafasi, kama wabunge, kutumia nafasi zao kukisaidia chama.

Alisema wakati walionao kwa sasa si wa kujivunia nafasi walizonazo, bali wanapaswa kuongeza nguvu zaidi na kugombea nafasi za uongozi wa juu wa Chadema ili waendeleze mapambano ya ukombozi.

Katika kipindi hiki ambacho tunaona demokrasia inaminywa kwa vyama vyote vya siasa, ni vema wanawake ambao ni jeshi kubwa tukawa mstari wa mbele katika mapambano si kurudi nyuma. Lazima kuwa na nidhamu ndani na nje ya chama ili tufanikiwe katika vita hii,” alisema Mdee.

Katika kuonyesha msisitizo huo, alimuagiza katibu mkuu wa Bawacha, Grace Tendega kuwaandikia barua wabunge ambao hawakuhudhuria kikao cha jana ili wajieleze kabla ya kuchukuliwa hatua.

Alisema ni jambo la aibu na fedheha kwa viongozi kutoka mbali wakasafiri hadi Dodoma kwa ajili ya kikao, lakini wabunge ambao wako mjini hapa wakashindwa kuhudhuria.

Mbunge wa Viti Maalumu, Devotha Minja alisema chachu ya ushindi na mapambano ndani ya chama hicho kwa sasa ni kubwa kwa kuwa wameamua kufanya kazi usiku na mchana kwa ajili ya kuisaidia Chadema.

Rais Magufuli Kushusha Panga Jipya Mchanga wa Dhahabu

$
0
0
Rais Magufuli
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli, leo anapokea ripoti ya kamati ya pili aliyoiunda kufuatilia athari za kiuchumi na za kisheria kuhusiana na usafirishwaji wa mchanga wa dhahabu kwenda ughaibuni.

Aidha, wakati Rais akitarajia kukabidhiwa ripoti hiyo Ikulu jijini Dar es Salaam na tukio hilo kurushwa moja kwa moja kupitia matangazo ya luninga, kuna taarifa kuwa baadhi ya viongozi katika mamlaka mbalimbali zinazohusika na suala hilo wameingiwa na hofu kwa kujua kuwa wanaweza kuchukuliwa hatua ya kutumbuliwa endapo itabainika kuwa kuna kasoro katika usimamiaji wa suala hilo, kama ilivyotokea kwa aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo.

Ripoti atakayokabidhiwa Rais Magufuli kesho kuhusiana na suala la mchanga wa dhahabu (makinikia) ni ya pili, ikiwa ni baada ya kupokea ripoti ya awali ya kamati iliyohusisha wataalamu nane wa masuala ya madini, wakiongozwa na mwenyekiti wake, Prof. Abdulkarim Mruma.

Magufuli alitangaza kumuondoa Muhongo katika uwaziri na pia kuwaondoa viongozi kadhaa wa Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA) baada ya ripoti kubaini kuwapo kwa tofauti kubwa kati ya kiwango kinachoripotiwa na uhalisia wa kile kilichomo katika makontena 277 ya mchanga wa madini yanayoshikiliwa katika Bandari ya Dar es Salaam na maeneo mengine nchini ambako yalikuwa tayari kusafirishwa kwenda nje ya nchi.

Taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, ilieleza kuwa Rais Magufuli atapokea taarifa ya kamati ya pili ya wachumi na wanasheria iliyofanya uchunguzi wa madini yaliyomo kwenye makontena hayo ya mchanga wa madini.

“Tukio hili litarushwa hewani moja kwa moja (mubashara) kupitia vyombo mbalimbali vya habari vya redio, televisheni, mitandao ya kijamii na tovuti rasmi ya Ikulu ambayo ni www.ikulu.go.tz, kuanzia saa 3:30 asubuhi,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa.

Wakati wa kuundwa kwa kamati hiyo ya pili ya wanasheria na wachumi Aprili 10, mwaka huu, Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu, Balozi John Kijazi, aliwataja wajumbe wake kuwa ni ni Prof. Nehemiah Osoro, Prof. Longinus Rutasitara, Dk Oswald Mashindano, Gabriel Malata, Casmir Kyuki, Butamo Philip, Andrew Massawe na Usaje Usubisye.

RIPOTI KAMATI YA WATAALAMU Katika ripoti ya kamati ya wataalamu wa madini iliyokabidhiwa kwa Rais Magufuli, Jumatano ya Mei 23, mwaka huu, ilibainika kuwa taifa limekuwa likipoteza mapato makubwa kupitia usafirishaji wa mchanga wa madini.

Akiwasilisha ripoti hiyo kwa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam, Prof. Mruma, alisema kuwa kwa ujumla, thamani ya madini yote katika makinikia kwenye makontena 277 yaliyozuiliwa ni Sh. bilioni 829.4 kwa kutumia viwango vya wastani na Sh. trilioni 1.44 kwa kutumia viwango vya juu.

Kwa mujibu wa kamati, kiasi hicho cha fedha ni jumla ya thamani ya madini ya dhahabu, shaba na madini mengine ya metali mkakati (strategic metals) yakiwamo ya Sulfur, chuma, Iridium, Rhodium, Ytterbium, Beryllium, Tantalum na Lithium.

Mbali na Mruma, wajumbe wengine wa kamati ya kwanza ya wataalamu walikuwa ni Prof. Justianian Ikingula, Prof. Joseph Bushweshaiga, Dk. Yusuf Ngenya, Dk. Joseph Philip, Dk. Ambrose Itika, Mohamed Makongoro na Hery Gombela.

HOFU YA PANGA JINGINE Baada ya kupokea ripoti ya kamati teule ya wataalamu, ndipo Rais Magufuli alipotengua uteuzi wa Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Muhongo na kuviagiza vyombo vya ulinzi na usalama viwachunguze na ikiwezekana wachukulie hatua watumishi waliokuwa wakihusika kubariki usafirishaji wa mchanga huo wa dhahabu, kuanzia Kamishna wa Madini aliyepita, watumishi wa Wakala wa Ukaguzi wa  Madini (TMAA) na kila mmoja.

Uamuzi huo wa Rais Magufuli utokanao na ripoti ya kamati ya wataalamu unatajwa kuwa ndiyo chanzo cha kuwapo hofu, baadhi wakijua kuwa ripoti ya wachumi na wanasheria inaweza pia kuwaondoa kwenye nafasi zao ikiwa itabainika kuwa kuna mahala walihusika kufanya uzembe.

“Wapo wakubwa hivi sasa hawana raha. Hofu imewajaa kwa kujua kuwa Rais hana simile katika suala hili lenye maslahi makubwa kwa taifa,” chanzo kimoja kiliiambia Nipashe kwa sharti la kutotajwa jina.

Hata hivyo, Nipashe haikuweza kuthibitisha kupitia vyanzo vingine huru juu ya kuwapo kwa vigogo wenye hofu ya kuondolewa kwenye nafasi zao kesho.

Live Updates:Haya Hapa Ndio Mambo Yaliyogunduliwa na Kamati ya Wanasheria na Wachumi ya Kuchunguza mchanga wa Madini

$
0
0

1.Kamati ya wanasheria na wachumi ya kuchunguza mchanga wa madini iliteuliwa Aprili 10 ikiongozwa na Prof. Nehemiah Osoro.

2.Miongoni mwa hadidu za rejea ambazo kamati ilipewa ni kujua idadi ya makotena yaliyosafirishwa nje ya nchi tangu 1998.

3.Kamati pia ilitakiwa kuchunguza kama Tanzania inauwezo wa kutengeneza 'smelter' nchini, gharama zake na muda utakaotumika.

4.Kamati ilitakiwa kuchunguza tofauti ya mapato ambayo Tanzania ilipata na ambayo ilitakiwa kuyapata tangu mwaka 1998.

5.ACACIA inayojinasibu kama mmiliki wa migodi ya Bulyanhulu na Buzwagi haijawahi kuwasilisha nyaraka za umiliki huo.

6. Kamati imebani kwa mujibu wa nyaraka kuwa kampuni ya ACACIA PLC haikusajiliwa nchini

7.Kamati imebaini kuwa wamiliki wa makampuni ya madini nchini wametenda makosa mbalimbali ya jinai.

8.Kamati imeridhia baadhi ya watumishi wa serikali, makampuni ya usafirishaji na TMAA wameliingiza Taifa hasara kwa makusud.

9.Makampuni ya Pangea na Bulyahulu yamepatikana na hatia ya kuliingizia Taifa hasara kwa kutokutoa taarifa sahihi juu ya uzito wa makinikia:.

9.Idadi na uzito wa makontena ya mchanga ulionekana kuwa mkubwa kwenye meli tofauti na kwenye nyaraka za bandarini.

10.Baadhi ya makampuni ya wakala wa meli ziliwasilisha nyaraka za uongo za usafirishaji wa madini kati ya 1998 na 2017.

11.Makontena 30 ya futi 20 yenye makinikia yalionekana kwenye nyaraka yamesafirishwa, lakini ukweli yalisafirishwa 33.

12.Kupitia hati ya usafirishaji wa makontena melini, idadi kubwa ya makontena yalikuwa yakisafirishwa bila kuorodheshwa.

13.Migodi ya Bulyanhulu na Pangea imekuwa ikipata faida lakini faida halisi haikuwa ikionyeshwa.

14.Kamati imebaini makontena 44,277 kwa kiwango cha chini yalisafirishwa nje ya nchi kati ya 1998 na 2017.

15.Viwango vya dhahabu kwa kila kontena ni 28kg, kwa miaka yote ni tani 1,240 kwa kiwango cha chini, thamani yake Tsh 108tril

16.Jumla ya thamani ya madini yaliyosafirishwa nje ya nchi kati ya 1998 hadi 2017 ni trilioni 132.56 kwa kiwango cha chini.

17.Jumla ya thamani ya madini yaliyosafirishwa nje ya nchi kati ya 1998 hadi 2017 ni trilioni 229.9 kwa kiwango cha juu.

18.Jumla ya thamani ya madini yaliyosafirishwa nje ya nchi kati ya 1998 hadi 2017 kwa Kiwango cha wastani ni trilioni 188.58

19.Kodi ya Mapato ambayo Tanzania imepoteza tangu 1998 hadi Machi 2017 ni trilioni 55 katika usafirishaji wa makinikia.

20.Kodi ya Zuio ambayo Tanzania imepoteza tangu 1998 hadi Machi 2017 ni bilioni 94 katika usafirishaji wa makinikia.

21.Mh Rais jumla ya Kodi tulizopoteza ni Sawa na makadirio ya bajeti ya serikali kwa kiwango cha Mwaka 2017/18 kwa miaka 2.

22.Taarifa ambazo zimekuwa sikiwasilishwa TMAA kuhusu uchenjuaji wa makinikia hazina ukweli wowote.

Ripoti ya Pili ya Mchanga wa Madini Yabaini Makubwa...Watanzania Tuamke

$
0
0

Baada ya kufanya uchunguzi Kamati imebaini kuwa ACACIA haikusajiliwa nchini Tanzania, ACACIA haina sifa ya kupata leseni ya kuchimba wala kufanya biashara ya madini nchini:- Mwenyekiti Prof. Nehemiah Eliachim Osoro

ACACIA MINING inafanya biashara ya madini kinyume na sheria za nchi, hili jambo ni la ajabu linaweza kufanyika Tanzania tu lakini nchi nyingine haliwezekani - Mwenyekiti Prof. Nehemiah Eliachim Osoro

Kuna Taasisi za serikali kama TRA wamekuwa wakishirikiana na ACACIA wakati watu hao hawatambuliki kisheria, hili jambo linaweza kutokea Tanzania tu si nchi nyingine - Mwenyekiti Prof. Nehemiah Eliachim Osoro

Baadhi ya watumishi wa serikali wamelitia aibu Taifa, kwa kutoa taarifa za uongo, kujipatia mali kwa njia ya udanganyifu - Prof. Nehemiah Osoro. #RipotiYaMchanga

#RipotiYaMchanga

Chenge na Ngeleja Watajwa Kwenye Ripoti ya Pili ya Mchanga wa Madini..!!!

$
0
0

Ripoti ya kamati ya pili kuhusu mchanga wa madini imewaibua Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge na Mbunge wa Sengerema, Wiliam Ngeleja kuhusu mikataba ya madini iliyoingiwa miaka iliyopita.

Mbali na hao pia imewaibua marehemu Dk Abdallah Kigoda aliyekuwa Mbunge wa Handeni na Daniel Yona aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini.

Majina ya viongozi hao yameibuka leo wakati  mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Nehemiah Osoro alipokuwa akiwasilisha matokeo ya ripoti yake.

Wabunge Wajazana Mgahawani Bungeni Kushuhudia Ripoti ya Pili ya Mchanga wa Madini Kwenye Luninga..!!!

$
0
0

Wakati kipindi cha maswali na majibu kikiendelea bungeni leo Jumatatu, baadhi ya wawakilishi wametoka ukumbini na kwenda kantini ya Bunge kufuatilia ripoti ya pili ya usafirishaji wa mchanga wa dhahabu inayorushwa mubashara kupitia vituo vya televisheni kutoka Ikulu jijini Dar es Salaam.

Baadhi wa wabunge wakinywa chai huku wengine wakijiburudisha kwa vinywaji baridi wamekuwa kwenye makundi matatu kulingana na idadi ya runinga zilizopo katika kantini hiyo.

Ilipotajwa hoja ya udanganyifu katika taarifa inayotolewa kisha Rais John Magufuli na Waziri Mkuu wake, Kassim Majaliwa kuonekana kwenye kioo cha televisheni wakitazamana, wengi wameguna ishara kwamba hoja hiyo ni nzito.

 Hata yaliposomwa makosa ya jinai yanayoambatana na usafirishaji huo, miguno mingine imesikika.

 Ukwepaji kodi, udanganyifu na makosa mengine yaliyobainishwa na mwenyekiti wa kamati hiyo ya pili, yamewagusa wabunge wengi wanaofuatilia.

 Bila kujua kama wanaambizana au ni shauku ya kila mmoja kusikia kinachowasilishwa na kamati hiyo, idadi yao imekuwa ikiendelea kuongezeka kantini.

Yanga Hawana Hela za Usajili?Mkemi Anaishia Kupiga selfie tu na Wachezaji.

$
0
0
Yanga

"Kutembea tutembee na Azam,mimba aipate Yanga"....Wakati Simba ikichanua katika usajili Yanga wamekuwa wakosoaji wakubwa wa usajili wa Mnyama unaondelea.

Ajabu ni kwamba wao Mkemi ambaye ni kiongozi wa Yanga anaishia kupiga nao picha tu wachezaji wanaotamani kuwasajiri lakini wino unamwagwa timu nyingine isiyotegemewa!

Watani wamesemwa kusubiri kuokoteza baada ya wenye visu kuchukua chao mapema.

Kwa upande wa Simba mambo yanayoendelea kule ni hatari.Wanasoka wanaonya Simba ipunguze kasi tusije kujikita Taifa Stars yote inatokea Simba SC.

Chanzo JF

Ukweli Mchungu...Mikataba Inasainiwa "Gizani", Ripoti Inakabidhiwa Hadharani! Tuendelee Kushangilia..!!!?

$
0
0

Kuna mambo yanatafakarisha sana. Na hili ni miongoni mwa mambo hayo! Leo ripoti ya pili ya "wataalamu" (wanasheria na wachumi) inakabidhiwa kwa Rais. Tangu juzi kumekuwa na hamasa kubwa mitandaoni ya kututaka wananchi leo tukae mbele ya tv kutazama tukuo hilo. 

Kuna tuswali twa kujiuliza:
1. Kama mikataba ya madini tuliyoingia ilisainiwa "gizani" kwanini ripoti iliyochunguza mikataba hiyo hiyo inakabidhiwa hadharani huku vyombo vyote vya habari vikitakiwa kusitisha shughuli zingine na kuhamia kwenye tukio hilo?

2. Kama kuna vipengele vya kisheria vinavyotaka kuwepo kwa "usiri" kwenye mikataba hiyo (kama ambavyo huwa tunaambiwa [wanasheria wanaweza kunisaidia hapa]) hiki kinachofanywa sasa hakina athari yeyote kisheria?

3. Hao wanaotaka ripoti hizo zikabidhiwe hadharani lengo lao ni nini hasa?

4. Je, ni sawa na ina tija kwetu wanyonge kiasi cha kushangilia mno, ripoti ya uchunguzi kuhusiana na mikataba ya ACACIA kukabidhiwa hadharani, lakini mikataba ya ununuzi wa bombadier; na mengine kufanyika gizani?

Na mimi pia ni mzalendo!

Chanzo JF

Ukweli Kuhusu Issue ya Shilingi 40 kwa Tozo ya Motor Vehicle Iliyopangwa na Serikali Ambayo Inapotoshwa Mitandaoni na Watu..!!!

$
0
0
mafuta

Jana niliona mjadala wa kitoto ulioanzishwa na Mdude Chadema Nyagali Mwanachama wa CHADEMA. Mjadala huo ulianza kwenye Ukurasa wa Facebook wa Mdude Chadema Nyagali na kusambaa kwenye mitandao mingine. Katika mjadala huo ambao aliuita mazungumzo baina yake na dereva wa Bus linalotoka Dar es Salaam hadi Sumbawanga, alijenga hoja kuwa Tozo ya Motor Vehicle iliyopendekezwa kufutwa na Waziri wa Fedha, Philip Mpango ni nafuu zaidi kuliko inayopendekezwa.

Katika mjadala huo, Mdude alifahamishwa na dereva wake kuwa kwa siku anatumia lita 400 kutoka Dar es Salaam hadi Sumbawanga kwa Bus aina ya Yutong. Tena aliupa uzito mjadala huo kwa kuweka picha ya Bus la Shabiby ambalo sina hakika kama linafanya safari hiyo. Kwa maelezo yake, kwa kuwa gari linatumia lita 400, kwa hali hiyo hadi Sumbawanga Busi hilo litalipa motor vehicle ya shilingi 16,000 kwa maana 400 x 40. Kwa Mwezi atalipa Motor Vehicle ya shilingi 16,000 x 30 = 480,000 na kwa mwaka shilingi 480,000 x 12 = 5,760,000. 

Mjadala huo ulivuta hisia za wafuasi wa CHADEMA ambao nao bila kutumia akili ipasavyo, wakaanza kushangilia na kujiona wameshinda. Ni kwa bahati mbaya sana Mdude CHADEMA hajawahi kumiliki hata pilipiki kwa hiyo hajui lolote kuhusu consumption ya mafuta kwenye magari. Binafsi nilijiuliza, je umbali wa kutoka Dar es Salaam hadi Sumbawanga unaweza kutumia lita 400? Kama ni hivyo, je abiria wa huko wanalipa nauli kiasi gani? Twende taratibu.

Mabasi mengi yanatumia wastani wa lita moja Diesel kwa kila kilomita 7 hadi . Na kwenye barabara za Highway, consumption ya mafuta ni tofauti na kwenye maeneo ya mijini. Kwa maana hiyo lita 400 anazotuma huyo dereva ukizidisha mara 7 gari hilo litalazimika kutembea kilomita 2800 ili kumaliza mafuta hayo yaani 7 x 400 = 2,800. Je Umbali wa kutoka Sumbawanga hadi Dar es Salaam unafika kilomita hizo?

Haya tufanye gari hilo ni mkweche kiasi cha kutumia kilomita 5 tu kwa lita moja. Maana yake ni kwamba gari hilo litalazimika kutumia kilomita 2000, hadi kumaliza mafuta yote yaani 5 x 400 = 2000. Je umbali wa kutoka Dar es Salaam hadi Sumbawanga unafikia kilomita 2000?

Basi tuseme Tank la Mafuta la Gari hilo linavuja na kwa hali hiyo hutumia lita moja kwa kila kilomita 3 tu. maana yake ni kwamba 3 x400 ni sawa na kilomita 1,200. Je umbali wa kutoka Sumbawanga hadi Dar unafikia kilomita 1,200?

Baada ya kushirikisha ubongo wangu, nilijiuliza maswali haya? Je Mdude Chadema ana uelewa wa matumizi ya mafuta kwenye magari? Au huyo Dereva anampiga cha juu bosi wake na ndo maana akataja kiasi kikubwa cha mafuta? 

Ukweli ni kwamba, Motor Vehicle iliyopendekezwa inapunguza sana gharama na hasa kwa sisi tunaoishi huku mikoani. Mathalan, mimi nikijaza full Tank huku Songea natumia wastani wa siku 18 hafi 25 hadi kwenda tena kituo cha mafuta. Kwa maana gari langu aina ya Toyota Harrier ina CC 2160 na ujazo wa Tank ni lita 65. Na inatumia wastani wa kilomita 8 kwa lita moja. Kwa maana hiyo, kwa lita 65 ili ziishe zote ingawa haijawahi kutokea, nitalazimika kutembea kilomita 520 ambayo kwa mzunguko wa mji wetu wa Songea nitatumia wastani wa siku 18 hadi 25 kumaliza na kama ninazurura sana nitatumia siku zisizopungua 10. 

Sasa twende taratibu, lita 65 x 40 = shilingi 2,400. Kwa maana hiyo kila siku 15 nitalipa Motor Vehicle ya shilingi 2,400 tu. kwa Mwezi nitalipa shilingi 4,800 tu na kwa mwaka nitalipa shilingi 4800 x 12 = 57,600 tu. hii ni pungufu ukilinganisha na shilingi 200,000 ninayolipa sasa. Yaani nitaokoa shilingi 142,400. Na hapa chukulia kama gari inatembea siku zote. Kama kwa nyakati kadhaa gari halitumiki maana yake ni kwamba kiasi cha Motor Vehicle nitakacholipa kitapungua.

Kwa wale wa Dar es Salaam ambao foleni husababisha matumizi makubwa ya mafuta, twende na mfano huu. Kwa wanaoishi Mbagala, ama Vikindu, ama Kibamba, ama Bunju na wanafanya kazi katikati ya Jiji, hutumia wastani wa lita 70 kwa wiki. Maana yake ni kwamba Motor Vehicle atakayolipa mtu huyo ni kama ifuatavyo; Kwa wiki itakuwa 70 x 40 = 2,800. Kwa mwezi itakuwa 2,800 x 4 = 11,200 na kwa mwaka itakuwa shilingi 11,200 x 12 = 134,400 tu. kwa hali hiyo, mtu mwenye gari kama langu ataokoa shilingi 65,600 kila mwaka iwapo tozo mpya ya Motor Vehicle itapitishwa. Hizi ni hesabu za kitaalam na wewe kama unamiliki gari unaweza kufanya hesabu zako ili kujua utalipa kiasi gani kwa wiki, mwezi na mwaka. Uzuri wa tozo pendekezwa ni kwamba inalipwa kulingana na jinsi unavyolitumia gari lako. Kama weekend una kawaida ya kupumzika basi utaokoa kiasi kikubwa sana cha fedha. Na kama una kawaida ya kupanda daladala siku moja moja ili kuchangamana na jamii kama nifanyavyo mimi basi utaokoa fedha nyingi sana.

Niwasihi Watanzania, tusimezeshwe tu kila kitu. Wengine wanaotumezesha hawajui lolote. Tutumie akili alizotupa Mungu ili kuchanganua mambo. 

Nawasilisha

Chanzo JF

Fumbo la Mke wa Lutu na Sodoma na Gomora

$
0
0
Sodoma na Gomora

Sodoma na Gomorrah ni miji iliyokuja kuangamizwa kwa sababu wakazi wake walifanya kufuru ya starehe mpaka kumsahau Mungu kabisa....na kibaya zaidi ni ile dhambi ya kutenda kinyume na maumbile

Ndani ya miji ile akawepo mchamungu mmoja naye alikuwa Lutu...mweledi mnyenyekevu na msikivu sana.. Baba wa mke mmoja na mabinti wawili

Mungu alikasirika na kuamua kuiteketeza ile miji miwili.,lakini akaamua kumuokoa mtumishi wake Lutu na familia yake ila kwa sharti moja! Kwamba Lutu aondoke na familia yake kabla miji ile haijateketezwa lakini 'ATAKAYEGEUKA NYUMA' atageuka jiwe la chumvi

Kwanini kugeuka nyuma? Fumbo la Sodoma hilo! Mke wa Lutu aligeuka nyuma na akageuzwa kuwa jiwe la chumvi!je

naye alikuwa mteja

Lutu na mabinti zake hawakugeuka nyuma na wakaenda kuishi mlimani mpaka Lutu alipokuwa mzee kabisa!

Mabinti zake wakajiongeza wakaona baba anazeeka mama hayupo na sisi ni mabinti! Tusipofanya namna kizazi kitapotea

Makatengeneza mvinyo mkali wakampa mzee akanywa akalewa.....wakampa unyumba baba yao....wakashika ujauzito na kizazi kikaendelea(hakuna ubaya hapa!)

Kinachonitatiza kwanini Mungu alisema atakayegeuka nyuma atageuka kuwa jiwe la chumvi?
Leo ni jumatatu twendeni kazini..mambo mengine hayana majibu

Ilitokea Lakini Haijawahi Kuandikwa..Fahamu Tukio la Padri Kumzaba Kibao Mwalimu Nyerere Kanisani..!!!

$
0
0

Mwalimu nyerere alikua na tabia ya kila mahala anapoenda kama kuna kanisa karibu basi huwa anaingia kusali haswa misa za wiki asubuhi.Alipotembelea mkoa Wa Kilimanjaro kuna kanisa la parokia ya karanga magereza aliingia kusali.sasa akaketi kwenye viti vya mbele ambavyo vimetengwa kwa ajili ya watawa tu.Akaingia padri mmoja anaitwa Jerome .alipita mlango Wa nyuma kwa hiyo hakujua kama ni mwalimu nyerere.akamzaba kibao cha nguvu akimwambia "nani kakuambia ukae kwenye viti vya watawa".mwalimu kugeuka padri bado kidogo azimie.akamuomba msamaha.misa ikafanyika wakatoka wakicheka na kwenda kupata breakfast ya nguvu.

Chnzo JF

Ongeza Hips, Makalio, Mapaja, Miguu, Uume na Nguvu za Kiume, Kuwa Mweupe na Kuondoa Madoa Bila Madhara

$
0
0
Tiba Mbadala
OKOA NDOA YAKO SASA. ONGEZA MAUMBILE, NGUVU NA HAMU YA TENDO LA NDOA HATA KWA WENYE KISUKARI. 

Tatizo la maumbile madogo, nguvu za kiume na ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limekuwa likiwasumbua wengi na kusababisha kushindwa kujiamini ktk tendo hivyo kusababisha ndoa nyingi kuvunjika pamoja na mahusiano. Upungufu wa nguvu na hamu ya tendo husababisha mambo kama:-
(a)Uume kulegea wakati wa tendo 
(b)Kukosa hamu ya tendo la ndoa 
(C)Kuwahi kufika kileleni 
(D)Uume kuchelewa kusimama baada ya round ya kwanza. 
(E)Kuchoka sana baada ya round moja n.k 
@Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo kwa kutumia bidhaa zilizotengenezwa kwa mimea na matunda zisizo na kemikali wala madhara na kuthibitishwa kiafya. Pata hizi👇👇👇👇
🍉 🌿🍅🍒🍍🍓🍉🍎🍀

1.HANDSOME UP ni kifaa chenye uwezo wa 99 % kuongeza uume (size unayohitaji) na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo hata mara 3 @130,000/=
Kwa Bidhaa hizi na nyingine kama:-
5.Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi @130,000/=
7.Kutengeneza shepu (hips, makalio na mapaja) @200,000/= 
8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni @120,000/=
9.Kuwa mweupe na soft mwili mzima bila kuacha sugu 120,000/=
10.Kurudisha usichana (bikra) @120,000/=
11.Kupunguza au kuongeza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120,000/=
Wasiliana nasi kwa (+255)
0767447444 au 0714335378.
NB: Matokeo ni uhakika na garantii na upate risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii.

Upinzani Walipuka Bungeni, Waimba Wana Imani na Mkapa, Kikwete..Ni Baada ya Ripoti ya Mchanga wa Madini Kutaka Mikataba Yote Iwekwe Wazi..!!

$
0
0

Bunge limezizima kwa makofi baada ya hotuba ya mpango wa bajeti ya kambi rasmi ya upinzani.

Wabunge wa upinzani ambao ndiyo wengi waliobaki ukumbini baada ya wengi kwenda kufuatilia ripoti ya kamati ya pili ya Rais John Magufuli kuhusu usafirishaji wa makinikia.

Wabunge wamesimama na kuanza kuimba huku wakipiga makofi, marais wa awamu zilizopita; Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete wametajwa.

"Tuna imani na Mkaaapa...oya oya oya

Mkapa kweeeli...kweli

Kweli, kweli, kweli Mkapa.

Tuna imani na Kikweeetee...oya oya oya

Kikwete kweeli

Kweli, kweli, kweli Kikwete."

Wimbo huo umeimbwa baada ya Waziri Kivuli wa Fedha na Mipango, David Silinde kulitaka Serikali kuileta bungeni mikataba yote ya madini ili ijadiliwe.

Nina Uhakika Baba wa Taifa huku alipo Machozi yanamtoka- JPM

$
0
0
Rais Magufuli
 
"Tumechezewa vya kutosha sasa tunasema hapana

"Ni lazima tuchukue maamuzi magumu, bila kujali yanamuhusu nani" JPM

"Hata tulipokuwa tukiwapeleka mahakamani tukishinda, Wana Appeal"- JPM

" Baba wa taifa Mwl Nyerere alisubiri kwanza akasema mpaka tutakapokuwa tayari, Nina uhakika hata huko aliko Machozi yatakuwa yanamtoka"

"Kwa wele watakaokuwa wanaropoka Bungeni tutadili nao Vizuri, Sasa spika nenda ka deal nao vizuri, Na wakisema nje ninatawashughulikia"
"Saa nyingine unakaa unajiuliza kwanini Mungu ulinipa nafasi hii? Why me?"

Rais JPM Ataka Vyombo vya Dola Viwahoji Viongozi Waliohusika Kwenye Mikataba ya Mchanga

$
0
0
Magufuli
Rais John Magufuli avitaka vyombo vya Dola viwahoji watendaji wa serikali walioshiriki kwenye mikataba ya madini tuliyoinga tangu mwaka 1994.

Rais Magufuli amesema kuwa watendaji hao walikosa uzalendo kwa kuweka mbele maslahi yao binafsi.
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images