Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Dewji Akubali Kuisaidia Simba Milioni 200 za Kuwabakisha Ajib,Mkude na Kotei..

$
0
0
Dewji

Wachezaji muhimu wanataka kusepa Simba baada ya mikataba yao Kuisha Simba walimshirikisha tajiri Mohamed Dewji Kwa Ajili ya kuwasaidia kuwabakiza wachezaji hao mhimu.

Kutokana na ripoti ya kocha wa Simba ameshauri waongezwe wachezaji sita wa kazi golikipa mmoja, beki watatu, Winga mmoja, na Mshambuliaji mmoja, Katika ripoti hiyo inatabainisha kuwa wachezaji ambao hawajaisaidia timu hata kwa asilimia 20 waachwe hata kwa kupelekwa Kwa mkopo. Pia ripoti ikasisitizia wachezaji mhimu wasiondoke kwenye timu kama mikataba imeisha waongezewe.

Baada ya ripoti hiyo kukabidhiwa kamati ya utendaji ya kupelekwa Kwa kamati ya usajili chini ya Zacharia Hanspope ikajadiliwa na ikaonekana Mapendekezo ya Omog yatafuatwa Kwa asilimia zote tatizo likaja Kwa wachezaji mhimu ambao wanamaliza mikataba ikawa changamoto kubwa. Ndio kamati ikapeleka barua ya ombi Kwa tajiri kijana MO aweze kuwasaidia.

Baada ya Mo kupokea barua hiyo aliwakubalia Simba Kwa Sharti moja tu fedha ambayo ataitoa iwekwe kwenye mchakato wa mabadiliko ya Simba. Mjumbe mmoja kutoka kamati ya usajili ambaye ni rafiki wa Mo ameagizwa kuzungumza na wachezaji wanne (Mkude, Ajibu, Kotei na Banda) ili kuona namna ambavyo wanaweza kubaki katika tetesi za usajili Mkude anataka milion 70 na kuendelea, Ajibu anataka Milioni 50, Banda na Kotei wote wanataka milioni 40 kila mmoja mambo yakienda Sawa MO atatoa milioni 200 kuwabakiza Nyota hao.

Mpaka sasa Simba imetumia zaidi ya Milioni 200 kuwasajili Nyota watano watatu kutoka azam (Manula, Kapombe, Bocco) Jamali Mwambeleko kutoka Mbao na Yusuph Mlipili kutoka Toto . Ikiwa Manula Milioni 70, Kapombe milioni 50, Bocco milioni 47, Mwambeleko milioni 30, na Mlipili milioni 10 .

Hatimaye JWTZ Yaingia Kibiti,Ikwiriri na Mkuranga Kudhibiti na Kutafuta Wauaji wa Polisi na Raia..

$
0
0
kikosi cha JWTZ

Hatimaye Serikali imepeleka kikosi cha JWTZ huko Pwani kudhibiti mauaji na kutafuta wauaji.

Kikosi hicho cha JWTZ kina wana jeshi wenye uzoefu mkubwa wa kivita na makomandoo kiasi.

Lengo kuu ni kuleta amani mkoa wa Pwani ktk maeneo hayo ambayo usalama wake umekuwa wa mashaka.

Asemavyo Bashir Yakub Kuhusu ACACIA Kutosajiliwa Tanzania Kisheria..

$
0
0
Acacia Mining

UFAFANUZI MUHIMU KUHUSU USAJILI WA ACCACIA.

Waraka wa BASHIR YAKUB
+255784482959.

Kwa kutumia kigezo cha usajili, Tanzania tunazo aina kuu mbili za kampuni. Kampuni za ndani(Local companies) na kampuni za kigeni ( foreign companies). 
  

Kampuni za ndani ni zile zote zilizoanzishwa hapa nchini na kusajiliwa hapa nchini. Hata kama wanahisa wake wote ni raia wa kigeni kwasababu tu ya kuanzishwa hapa na kusajiliwa hapa zinakuwa ni kampuni za ndani.

Kampuni ya kigeni ni ile iliyoanzishwa na kusajiliwa nje ya Tanzania lakini ikaanzisha ofisi/biashara/tawi hapa Tanzania. Sheria Na. 12 Sheria ya Makampuni kifungu cha 433 kinasema hivyo. Kampuni kama imeanzishwa nje hata kama wanahisa wake wote ni Watanzania, hapa kwetu hiyo bado ni kampuni ya kigeni.

Kampuni ya ndani inaposajiliwa hupatiwa cheti cha usajili kiitwacho "Certificate of Incorporation" kwa mujibu wa kifungu cha 15(2) Sheria ya Makampuni. Kampuni ya ndani inapopata cheti hiki basi usajili wake huwa umekamilika na inatambulika rasmi kama kampuni ya ndani.

Kampuni ya kigeni inaposajiliwa hapa Tanzania hupatiwa cheti kiitwacho "Certificate of Compliance" kwa mujibu wa kifungu cha 435(1) Sheria ya Makampuni. Kampuni ya kigeni inapopata cheti hiki basi usajili wake huwa umekamilika na hutambulika rasmi kama kampuni ya kigeni.

Acacia ni kampuni ya kigeni. Kwa maana kuwa ilianzishwa nje ya Tanzania na kufungua shughuli zake hapa nchini. Kwa hiyo ili ihesabike imesajiliwa Tanzania ilitakiwa kuwa na cheti kiitwacho"Certificate of Compliance". Kutokuwa na cheti hiki maana yake ni kuwa haijasajiliwa Tanzania na haitambuliki.

Nimesikia mjadala BBC SWAHILI leo wanaojadili wakijiuliza inawezekanaje kampuni kubwa kama hii ikafanya biashara bila usajili. Watanzania wengi pia wanajiuliza swali hili.

Jibu lake ni hili. Acacia ni kampuni tanzu(Subsidiary Company) ya Barrick. Kampuni inakuwa tanzu pale ambapo zaidi ya nusu ya hisa zake zinamilikiwa na kampuni nyingine. Ile inayomiliki huitwa "holding company" na inayomilikiwa huitwa "subsidiary company". Kwahiyo Barick ni " holding" wakati Acacia ni "subsidiary".

Barrick inamiliki hisa za Acacia 63.9%. Kwa kusema hivi maana yake Barrick ndiye mwenye Acacia. Hata hivyo kwa mujibu wa sheria hizi zinahesabika kampuni mbili tofauti na kila moja inabeba wajibu na hatia zake yenyewe(its own responsibility& liability).

Basi kumbe kilichotokea ni kuwa Acacia walikuwa wakifanya biashara kwa jina la Acacia lakini wakibebwa na mgongo wa Barrick. Walijificha hapa na wakaweza kuishi bila usajili wa kwao kama wao. Walijibeba kwenye usajili wa Barrick.

Barrick wao wanao usajili na wanayo " Certificate of Compliance" ya kwao ambayo tayari wameitoa hadharani. Kwakuwa haya ni makampuni mawili tofauti kila moja inatakiwa kuwa na cheti chake kwa mujibu wa kifungu cha 487 Sheria ya Makampuni na kutokufanya hivyo ni kosa kabisa. Kwa hiyo hivi ndivyo ilivyowezekana kampuni hii kufanya biashara bila usajili miaka hii yote.

Adhabu ya kosa kama hilo ni kifungo jela. Sheria Na. 12 Sheria ya Makampuni iliyofanyiwa Marekebisho mwaka 2002, kifungu cha 472 kinasema hivyo.

Dotto: Kama Kweli Watanzania Wanaumia na Wizi Huu wa Mali za Umma Tuanze Shinikizo la Haya Yafuatayo..!!!

$
0
0

Anaaandika Mtangazaji wa Startv Dotto Bulendu . 
Kama kweli watanzania wanaumia na wizi huu wa mali za umma tuanze shinikizo la haya yafuatayo!.

1.Tuilazimishe serikali itake isitake Rasimu ya Warioba irejeshwe na kupitishwa ili kuondoa kinga kwa maraisi wastaafu na wafike mbele ya vyombo vya sheria na wawaambie watanzania kwa nini haya yalifanyika chini yao na sheria ichukue mkondo wake!.

2.Wale wote waliohusika kuichakachua Rasimu Warioba waombe radhi na wachukuliwe hatua za kinidhamu!.

3.Waliokuwemo kwenye "cabinet"kuanzia cabinet(baraza la mawaziri) la 1990-1995,ambapo walipitisha mkataba mmoja.1995-2005,waliopitisha mikataba ya hovyo mitano na hawa wa 2005-2015,waliopotisha mkataba mmoja wote washtakiwe kwa kuiingizia nchi hasara,masuala ya nchi hufanyika kwa uwajibikaji wa pamoja(collective responsibility)na siyo individual responsibility!.

4.Wabunge wote waliopiga kura ya ndiyo kupitisha sheria ya kodi na ile ya uwekezaji ya mwaka 1997,pamoja na sheria ya madini ya mwaka 2010,wafikishwe mahakamani kwa kuliingizia taifa hasara!.

5.Wabunge wote waliopitisha hoja ya kumfukuza Zitto Kabwe bungeni mwaka 2007 baada ya kumtuhumu waziri Karamagi kuwa alikula rushwa kwenye mkataba kati ya serikali na Barrick Gold wote wafikishwe mahakamani kwa kutetea mkataba wa hovyo na kuipa ruhusa kampuni ambayo haijasajiriwa nchini kuchimba madini na hivyo kulisababishia taifa hasara!.

6.Wale wote waliounda timu ya wataalam wa kulishauri baraza la mawaziri kuhusu mikataba ya madini kuanzia mwaka 1995 mpaka sasa,wakamatwe na kufikishwa mbele ya sheria ili wajibu kama huu ndiyo ulikuwa ushauri wao!.

7.Wale wote waliokuwa wanaopinga sheria hizi na mikataba kuwekwa wazi,watajwe hadharani na kuwaomba radhi watanzania!.

8.Maspika wote walioongoza utungwaji wa sheria hizi nao wafikishwe mbele ya vyombo ya sheria kwa tuhuma za kuhujumu uchumi!.

9.Waandishi wote waliokuwa wanaandika habari ama kutengeneza vipindi vya kutetea wawekezaji nao waombe radhi kwa kutetea wizi huu!.

10.Yote katika yote kama watanzania hatutaanzisha vuguvugu la kuitaka Rasimu ya Warioba tutakuwa hatuvitendei haki vizazi vijavyo na tutakuwa tunapoteza muda!.

11.Usalama wa taifa watuambie je walikuwa wanatoa taarifa kwenye mamlaka juu ya wizi huu?kama hapana nao washughulikiwe!.

11.CCM ya Mkapa na Kikwete iseme wazi kwa nini iliacha kuisimamia serikali na kuacha wizi huu uliolipotezea taifa Trilioni karibu 180?kwa ni waliacha kuisimamia serikali kama alivyowahi himiza Katibu mkuu Kinana?.

Prof. Muhongo, Andrew Chenge na Wahusika Wengine Wazuiwa kutoka nje ya Mipaka ya Tanzania

$
0
0
Andrew Chenge
Andrew Chenge
Serikali imeagiza, Mawaziri, Wanasheria Wakuu wa Serikali na Manaibu wao, Wakurugenzi wa idara za mikataba, na Makamishna wa madini, wanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini na watumishi wengine wa Serikali na watu wote waliohusika katika kuingia mikataba ya uchimbaji madini, utoaji wa leseni za uchimbaji wa madini na kuongeza muda wa leseni, watumishi na wamiliki wa makampuni ya madini kuto toka nje ya mipaka ya Tanzania.

Agizo hilo lilitolewa jana  na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ambaye alisema kuwa, wote waliotajwa kuhusika katika kulisababishia taifa hasara kupitia sekta ya madini, hawaruhusiwi kutoka nje ya mipaka ya Tanzania isipokuwa kwa kibali maalum kutoka serikalini.

“Naelekeza wote waliotajwa kuhusika hakuna kutoka nje ya mipaka ya nchi yetu isipokuwa kwa kibali maalum kutoka serikalini. Vyombo vitekeleze maagizo ya Rais kwa utimamu,” aliandika Waziri Nchemba kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.

Agizo hili limekuja ikiwa ni saa chache tangu Rais Magufuli alipoagiza kuwa, viongozi wote na watumishi mbalimbali waliohusika katika kusaini mikataba mibovu na kushiriki kwa namna yoyote ile, wahojiwe.

Miongoni mwa watakaoathiriwa na zuio hilo, ni pamoja na Maafisa wa TRA, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Andrew Chenge, Mwanyika, na Werema, Mkurugenzi Idara ya Mikataba, Mary Ndosi, Kamishna Dalali Peter Kafumu, Waziri Prof. Muhongo, Waziri Daniel Yona, Waziri Nazir Karamagi, Jaji Julius Malaba, Waziri William Ngeleja.

Awali Waziri Nchemba alimpongeza Rais Magufuli kwa jitihada alizozichukua katika kuhakikisha analinda rasilimali za wanyonge na kusema kuwa hakuna uzalendo kama huo.

“Hakuna uzalendo zaidi ya kulinda rasilimali za Taifa, Hakuna utetezi wa wanyonge zaidi ya kulinda rasilimali zao.Hongera sana Mh.Rais kwa uzalendo wa vitendo kwa Taifa letu.”

MSAADA...Nimepoteza Vyeti vya Shule na Documents Zingine Kwenye Usafiri Wakati Nahama

$
0
0
vyeti
Naitwa Julieth Benjamin Nkya, Usiku wa Tarehe 11/2/2017 Nilipoteza Vitu vifuatavyo Wakati Nahama Kutokea Buguruni Kuja Bunju Kwenye Gari lililonibebea Mizigo

1. Birth Certificates za Julieth Benjamin na Ezekiel Noel
2.Cheti cha Form Four cha Julieth Benjamin Nkya
3.Cheti cha Form Six cha Julieth Benjamin Nkya
4. Results Slip ya Chuo cha University College of Cooperative (Muccobs) ya Julieth Benjamin Nkya
5. Certificate ya Chuo cha University College of Cooperative (Muccobs) yenye jina la Julieth Benjamin Nkya
6.TIN namba yenye Jina la Julieth Benjamin Nkya
7.Vyeti viwili vya Ndoa vyenye Majina ya Julieth Benjamin Nkya na Fredy Mongi


Naomba kama kuna mtu ameviokota au kuwa na taarifa kwa vyeti vilivyopotea vyenye jina hilo piga simu namba ifuatayo: 0718230571

Zawadi Itatolewa Kwa atakaye fanikisha kupata Docoments hizi

Kampuni ya Madini ya Acacia Yatangaza Kupunguza Wafanyakazi 400

$
0
0
Acacia
Kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia imethibitisha kuwa ipo katika mpango wa kupunguza wafanyakazi wake hasa walinzi wa mgodi huo.

Meneja habari na mahusiano ya jamii wa Acacia, Bi. Nectar Foya amesema kuwa kampuni hiyo itaingia mkataba na kampuni binafsi itakayoendesha shughuli za ulinzi wa migodi yake yote mitatu ya North Mara, Bulyanhulu na Buzwagi.

Kampuni hiyo imejikuta kwenye msukosuko mkubwa baada Rais John Magufuli kupiga marufuku kusafirisha makontena ya mchanga wa madini kwenda nje ya nchi kwa ajili ya kuchenjua na kuunda kamati ya kuchunguza kiasi cha madini kilichokuwa ndani ya mchanga huo na kujua tathmini ya athari yake kiuchumi.

Kampuni hiyo imetangaza mara kadhaa kuwa zuio hili limewasababishia hasara kubwa. Walisema kuwa wanapata hasara ya dola za Marekani milioni moja (Tsh. bilioni 2.238) kila siku kutokana na katazo hilo la ghafla kutoka kwa serikali.

“Tumeamua kuingia mkataba na kampuni ya ulinzi kwa sababu tunaamini hiyo ndio njia pekee ya kulinda rasilimali zetu na kuzuia tusiendelee kupata hasara,” alisema Bi. foya.

Kauli hii ameitoa baada ya tamko alilotoa Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Migodini Tanzania, Bw. Nicodemus Kajungu mwisho wa wiki iliyopita kwamba kampuni hiyo ipo kwenye mpango wa kupunguza wafanyakazi 400.

Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa Apongeza Ukarimu wa Vodacom Tanzania Foundation

$
0
0
Kassim Majaliwa akiwa vocacom
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa ameipongeza Vodacom Tanzania Foundation kwa kuendelea kuwafuturisha watoto na wazee waishio katika mazingira magumu nchini.

Mh. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Kassim Majaliwa Kassim(katikati) akishuhudia Shekh mkuu wa Ruangwa mkoa wa Lindi akipokea boksi lenye tende kwa niaba ya watoto wanaoshi katika mazingira magumu mkoani hapo toka kwa Meneja mauzo wa mkoa huo,Omary Kilumanga na Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo,Jacquiline Materu baada ya kufuturu futari mwishoni mwa wiki iliyoandaliwa na Vodacom Tanzania Foundation  mkoani humo ikiwa ni sehemu ya kujitolea katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.

Mh. Waziri Mkuu ameyasema hayo mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Ruangwa Lindi katika futari iliyoandaliwa na Vodacom Tanzania Foundation mkoani humo ikiwa ni sehemu ya kujitolea katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.

Huu ni mwendelezo wa kampeni ya “Ukarimu wa Vodacom” ambayo ina lengo la ukarimu, ushirika na utoaji katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhan na katika maisha ya kila siku.

Huduma hii yenye lengo la kuendeleza mshikamano inakwenda sambamba na kuwawezesha Waislamu na Watanzania kwa ujumla wao kujiunga na kifurushi kinachowapatia muda wa maongezi, SMS na kuwawezesha kupiga simu BURE wakati wakisubiri muda wa kula daku, kugawa tende pamoja na maji. Pia huduma hiyo inawakumbusha muda wa kuswali na kuwapatia Mawaidha na Hadith. Ili kujiunga na huduma hii mteja anapiga *149*01# kisha anachagua aina ya bando kulingana na uwezo wake wa kifedha, kuna bando linalodumu kwa saa 24 na lingine linadumu kwa siku 7.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Kassim Majaliwa Kassim akiongea na wakazi wa Ruangwa mkoa wa Lindi mara baada ya kufuturu futari mwishoni mwa wiki iliyoandaliwa na Vodacom Tanzania Foundation  mkoani humo ikiwa ni sehemu ya kujitolea katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.
Mtazame Mkuu wa Kitengo cha Maendeleo ya Pwani wa Vodacom Tanzania Plc, Aileen Meena akifafanua kampeni mpya "Ukarimu wa Vodacom" katika msimu huu wa Ramadhan.



Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Maalim HUSSEIN Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa...Anatibu Magonjwa Yafuatayo

$
0
0

Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Maalim HUSSEIN Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika

Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa  PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.
Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,

HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp: +255 674 835107 
Calls: +255746757102

Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote..

Diamond Afunguka Mchango wa Wema Sepentu Kwenye ‘Chibu Perfume’

$
0
0
Diamond Platnumz na Wema Sepetu
Msanii wa muziki, Diamond platnumz amefunguka kuuzungumzia mchango wa malkia wa filamu, Wema Sepetu kwenye perfume yake ya ‘Chibu Perfume’.

Diamond amekiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM kuwa, yeye na Wema wanakutana na kuongea sana na wakati mwingine hushauriwa mambo mengi ya kibiashara na mwanadada huyo ambae alikuwa mpenzi wake .

“Mimi na Wema labda watu hawajui sisi tunaongea sana wakati mwingine tunakutana tu sana lakini sio kwenye media. Tushakuwa kila mtu ana mahusiano yake tofauti yeye ana familia yake hata ukiangalia katika Perfume yangu lile neno THE SCENT YOU DESERVE alilitoa Wema” alisema Diamond.

Muimbaji huyo kwasasa yupo kwenye mahusiano ya Zari na tayari wamefanikiwa kupata watoto wawili.

Yanayotokea Sasa Zitto Aliwahi Yasema Akapigwa....Mwenyewe Adai 'Hata Mungu Akinichukua Sasa Nakwenda Huku Nimetabasamu'

$
0
0
Zitto Kabwe

"Mwisho wa siku historia inaandikwa tu. Uzalendo ni kufanya jambo ambalo wengi hawakuelewi lakini wewe unajua Ni jambo sahihi na unakubali kutukanwa, kususubikwa, kusimangwa, kuzushiwa, nk. Unapambana tu. Mwisho wa siku waliokuita msaliti watakuita shujaa. Waliokuzomea wanashangilia. Wewe unafanya nini? Unakaa kimya kwani kwenye kukaa kimya pia kuna kusema kukubwa zaidi. Muhimu Nchi ifaidike.

Huko nyuma nilipata kusema, hata mungu akinichukua sasa unakwenda ukiwa umetabasamu kwani unakuwa umetimiza wajibu wako duniani. Kina Josina Umm Kulthum wataishi Kwa heshima inshallah"

Ameandika Zitto Kabwe kupitia ukurasa wake wa Facebook mara baada ya ripoti ya pili ya mchanga wa madini kuwasilishwa

Madee Awafungukia Wasanii Wanaotoa Misaada ili Kutafuta Kiki

$
0
0
Mwanamuziki Madee
MKALI wa Ngoma ya Hela, Hamad Ally ‘Madee’ amewashangaa baadhi ya mastaa ambao katika Mwezi wa Mfungo wa Ramadhani wamekuwa na utamaduni wa kutoa vitu kwa jamii na kupiga picha kisha kujionesha kwenye mitandao ya kijamii kitu ambacho siyo sawa na matakwa ya Dini ya Kiislamu.

Akipiga stori na Show Biz, Madee alisema, kwa upande wake suala la kujitoa kwa jamii inayomzunguka ndiyo limemfi kisha katika mafanikio hayo aliyonayo na kuwa hufanya hivyo mara kwa mara na hata pale anapofanya hawezi kujinadi kwenye mitandao ya kijamii kama baadhi ya wasanii wanavyofanya.

“Unajua katika Dini ya Kiislamu hatujaelezwa kutoa na kujinadi kwenye mitandao ya kijamii.

Tumetakiwa kutoa kwa moyo. Sasa kwa upande wangu huwa ninawashangaa sana baadhi ya mastaa ambao wakitoa misaada basi kwao hiyo ndiyo inakuwa kiki.

“Kiukweli si sawa na wanatakiwa kubadilika maana huko mitaani kuna watu wengi mno wanatoa lakini hawajitangazi kama wao,” alimaliza Madee.

Wanaume Akili Zenu Huwa Mnaziacha Wapi Wakati wa Majambozi Kitandani?

$
0
0
Mapenzi

*UFUNUO KTK TENDO LA NDOA..!!*
Kuna tofauti kubwa baina ya mwanamke na mwanaume wanapokuwa katika tendo la ndoa.

MWANAMKE:

1) Aibu huongezeka
2) Nguvu za mwili humuishia na mwili hulegea
3) Uwezo wa kufikiria huongezeka na kufika (to themaximum)

MWANAUME:

1) Aibu hutoweka kabisa
2) Nguvu za mwili huongezeka
3) Uwezo wa kufikiria(IQ) hushuka na kufikia zero! (hasa anapokuwa kileleni).
Katika hayo kuna mambo
tunajifunza:

a) Kumbe ndio maana vitabu vya mungu vinasema (mwanamume) aziniye na mwanamke hana akili kabisa; kwa
sababu kimaumbile na kisaikolojia uwezo wa kufikiri hutoweka!

b) Kama mwanamke anakuwa na uwezo mkubwa wa kufikiria (to the maximum) na mwanamume akili
na uwezo wa kufikiria vinashuka (to zero), bila shaka unaweza ukatambua kwa nini Samson “asingesalimika”

Kwa namna yeyote ile mbele ya Delila!
Nadhani wanaume tunapata somo letu
hapa;

“Mwanamke unaempa mwili wako kupitia tendo la ndoa, ikiwa ana nia mbaya ni rahisi mno kukumaliza kiulaiiiiiiiiiiiniiiiiiii”. Katikati ya tendo hili (akili yako inapokuwa sifuri) unaweza kujikuta unakabidhi mshahara wote!
Unaweza kujikuta unaahidi kumnunulia gari wakati hata pikipiki imekushinda!
Unaweza kuikana familia yako mchana kweupe!

Na asikwambie mtu; “Ahadi unazozitoa katikati ya tendo hili zina nguvu kubwa kuanzia ulimwengu wa roho hadi katika fikra. Ndio maana ukidakwa na ukajikuta umeropoka ahadi, ujue huo ni msala na hilo litakuganda mpaka ujute!”.

Pengine la muhimu (kwa wote) ni kujitahidi kuheshimu miili yetu na inapotolewa kutumika basi iwe ni “sadaka ya amani na haki” kwa wale wa halali na wanaostahili.

Mungu awabariki sana .

By Nazjaz

Nafasi za Ajira zilizotangazwa Siku ya Leo

ACACIA Wapinga Vikali Matokeo ya Kamati ya Pili ya Rais..!!!

$
0
0

Acacia imeona matokeo ya kushtua ya kamati ya pili ya Rais iliyowasilishwa kwa Rais wa Tanzania Mh. Dk John P. Magufuli leo asubuhi ambayo imeangalia nyanja za historia za kiuchumi na kisheria ya mauzo ya nje ya makanikia ya madini.

Kamati ya Pili imetoa matokeo yake kwa kutumia matokeo ya Kamati ya Rais ya Kwanza, iliyotangazwa tarehe 24 Mei 2017, ambayo Acacia imeikanusha vikali. Kamati hiyo ilipata matokeo yake kwa kutumia sampuli ya kontena 44. Kwa mujibu wa data za zaidi ya miaka 20 tulizonazo ni vigumu kuoanisha matokeo yetu na yaliyokutwa na kamati, na kamati imetoa thamani ya juu kwa zaidi ya mara 10 kuliko thamani halisi ya makanikia 

Kamati ya Pili inadai kuwa Acacia imetangaza kiasi cha chini cha mapato kuliko inavyopata na kulipa kodi kidogo kuliko inavyostahili kwa miaka mingi na kuficha mabilioni ya dola ya Marekani. Na hivyo imefanya mapendekezo kadhaa ikiwa ni pamoja na Acacia kulipa kodi inayodaiwa na mirahaba, kufanya majadiliano upya ya mikataba mikubwa ya uchimbaji madini, umiliki wa Serikali katika migodi, na muendelezo wa marufuku ya kuuza nje.

Acacia inakanusha vikali tuhuma hizi mpya zisizo na ushahidi. Sisi tumefanya biashara zetu kwa utaratibu bora kabisa na kwa kufuata sheria zote za Tanzania. Tunarudia kusema tena tumeweka wazi kila kitu chenye faida tulichokuwa tunazalisha tangia tuanze uchimbaji Tanzania na tumelipa kodi na mirabaha yote inayotakiwa kulipwa, na kwa kuongezea mahesabu yetu tunayotoa yanakaguliwa kila mwaka kwa viwango vya kimataifa vinavyoendana na IFRS.

Acacia kwa muda mrefu tulitaka kushirikiana na Serikali ya Tanzania kwa kuwa tunaamini wote tuna malengo sawa katika kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini. Hata hivyo, ushirikiano huu lazima uwe na misingi ya haki kwa wadau wote, ikiwa ni pamoja na 96% ya wafanyakazi katika migodi yetu ambao ni Watanzania, na wanahisa wetu ambao wamechangia dola bilioni 4 za uwekezaji ambazo Acacia imefanya ndani ya nchi hadi sasa.

Acacia bado inakaribisha mazungumzo na Serikali kuhusu suala hili na inaendelea kutathmini nini inaweza kufanya . Tutatoa taarifa zaidi kwa soko kadri tutakavyoweza kufanya .

Kwa taarifa zaidi tembelea tovuti yetu
www.acaciamining.com

Acacia Yaliibia Taifa Zaidi ya Trilioni 108...!!!

$
0
0

TANZANIA imepoteza kati ya Sh trilioni 68.6 na Sh trilioni 108.5 tangu kampuni ya Accacia inayochimba dhahabu hapa nchini ilipoanza kusafirisha ‘mchanga wa dhahabu’ nje ya nchi mwaka 1998.

Fedha hizo ni kodi ambayo Serikali ingepata kutoka kwa mwekezaji huyo ambaye ndiye mmiliki wa migodi ya Pangea, Bulyanhulu na Buzwagi ambayo ndiko makinikia yanachukuliwa na kusafirishwa nje ya nchi kupitia bandari za Dar es Salaam na Tanga. Kati ya fedha hizo kwa makadirio ya wastani, Kodi ya mapato ya makampuni ni Sh trilioni 55.67, Kodi ya zuio la kodi bilioni 94.4, Mrabaha Sh trilioni 11.1 na gharama za meli kutia nanga Sh trilioni 1.67.

Makadirio ya juu, Kodi ya mapato ya makampuni Sh trilioni 95.5, Kodi ya zuio la kodi Sh bilioni 94.4, mrabaha Sh trilioni 11.1 na gharama za meli kutia nanga na upakuaji Sh trilioni 1.7. Mwenyekiti wa Kamati Maalumu ya Uchumi na Sheria ambayo iliundwa na Rais John Magufuli Profesa Nehemia Osoro, alisema thamani ya madini yote katika makontena 61,320 yaliyosafirishwa nje ya nchi katika kipindi hicho ni kati ya Sh trilioni 183.6 na Sh trilioni 380.5.

“Jumla ya mapato ya Serikali ambayo Serikali ilipoteza ni Sh trillion 68.59 ambazo ni sawa na bajeti ya miaka miwili ya Serikali kwa kigezo cha makadirio ya mwaka 2017/2018. Aidha, robo ya fedha hizo zingetosha kujenga reli ya Standard Gauge kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza,” alisema Profesa Osoro. Alisema kwa makadirio ya juu Serikali ilipoteza Sh trilion 108.46, ambazo ni sawa na bajeti inayokaribia Miaka Mitatu ya Serikali kwa kigezo cha Makadirio ya Matumizi ya mwaka 2017/2018 na gharama ya kujenga reli ya Standard Gauge kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza.

Alisema dhahabu peke yake iliyokuwa kwenye kontena moja uzito wake ni kilo 28 na katika makontena 44,277 yatakuwa ni tani 1,240 za dhahabu, kiasi hicho thamani yake ni kati ya Sh trilioni 108.06 na Sh trilioni 183.32. Madini mengine na thamani yake kwenye mabano ni Silver Sh bilioni 329.66 na Sh bilioni 378.3, shaba Sh trilioni 2.86 na Sh trilioni 3.72, Sulphur Sh bilini 227.94 na Sh bilioni 296.9, chuma kati ya Sh bilioni 09 na Sh bilioni 576. Zinc kati ya Sh bilioni 11.6 na Sh bilioni 23.1, Nickel kati ya Sh bilioni 18.3 na Sh bilioni 52.

Madini mengine ni Rhodium, Iridium, Ytterbium, Beryllium, Tantalum na Lithium. Yona, Karamagi walivyohusika Profesa Osoro alimtaja marehemu Dk Abdallah Kigoda kuwa ndiye aliyesaini kwa niaba ya Serikali mkataba na mgodi wa Bulyanhulu ambako Serikali ilipata asilimia 15. Lakini baadaye kwa nyakati tofauti Dk Kigoda alisaini tena mkataba ulioondoa asilimia 10 na baadaye akasaini tena mkataba ulioondoa asilimia 5 ya Serikali.

“Katika marekebisho hayo Serikali ilikubali kulipwa dola za marekani milioni 5 ikiwa ni malipo ya mauzo ya hisa za Serikali,” alisema nakuongeza kuwa Serikali ilikubali kulipwa dola za Marekani 100,000 kwa kila mwaka: “hata hivyo kamati haikuweza kupata uthibitisho wa kufanyika kwa malipo ya jumla ya dola za marekani 6,800, 000 tangu mkataba huo usainiwe.

Kwa upande wa mgodi wa Pangea, aliyesaini ni mkataba huo ni Daniel Yona na Nazir Karamagi Desemba 2003. Alisema katika mikataba hiyo Serikali haina hisa na inatoa nafuu kubwa za kodi kwa mwekezaji jambo ambalo alisema linaikosesha Serikali kodi nyingi na mapato. Mkataba wa mgodi wa North Mara ulisainiwa na Daniel Yona mwaka 1999 na Nazir Karamagi. Alisema katika mkataba wa awali uliosainiwa na Yona ulitoa nafuu ya asilimia 15 ya nyongeza ya mtaji wa kampuni na kuifanya Accacia yakwapua kodi ya trilioni 108/- kampuni hiyo iwe inajilipa kwanza ili kurudisha mtaji wake na asilimia 15 iliyopewa na Serikali.

“Jambo hili lilisababisha kampuni kutangaza hasara katika biashara kila mwaka, jambo hilo limekuwa linaikosesha Serikali kodi ya mapato,” alisema. Mkataba wa mgodi wa Geita ulisainiwa na Dk Abdallah Kigoda na serikali haikupata hisa yoyote. Ngeleja, Chenge watajwa Mwenyekiti huyo alifafanua kuwa mikataba ya uchimbaji madini inaeleza kuwa inaongeza na kurekebisha masharti yaliyomo katika leseni ya uchimbaji madini. Alisema kamati yake inaona kuwa masharti ya aina hiyo ni batili kisheria kwani waziri hawezi kurekebisha masharti ya leseni yaliyotolewa kwa mujibu wa sheria na kanuni kwa kupitia vifungu vya mkataba wa uchimbaji wa madini.

Alisema kamati yake imebaini kuwa kumekuwa na uongezaji wa muda wa leseni wa maeneo ya uchimbaji madini kinyume cha sheria na bila kuzingatia maslahi ya taifa. Alimtaja waziri wa zamani wa madini William Ngeleja na Proresa Sospeter Muhongo ambao waliongeza muda wa leseni kwa kampuni za North Mara na Pangea. Alimtaja aliyekuwa kamishna wa madini Paul Masanja, Peter Kafumu na kaimu kamishna Ally Samaje kuwa walitoa leseni ambazo hazikuwa na maslahi kwa taifa.

Pia aliwataja wakuu wa Serikali kwa masuala ya kisheria kuwa ni Andrew Chenge, John Mwanyika na manaibu wanasheria wakuu ambao ni Felix Mrema na Sazi Salula na wakuu wa idara ya mikataba Maria Ndossi Kejo na Julius Malaba. Kitanzi cha mikataba Profesa Osoro alisema mikataba ya uchimbaji madini ina vifungu thabiti ambavyo vinazuia marekebisho ya sera na sheria kuathiri masharti yaliyomo katika mikataba ya uchimbaji madini. Alisema pamoja na kuwepo vifungu hivyo, Serikali haizuiliwi kurekebisha au kubadili sera na sheria zinazoweza kuathiri mikataba ya uchimbaji madini.

“Mkataba wowote ule hauwezi kisheria kuwa juu ya mamlaka asili ya nchi na maslahi ya umma kuhusu rasilimali zake za asili,” alisema mwenyekiti na kuongeza kuwa mikataba hiyo ina vifungu vinavyoruhusu serikali na makampuni ya uchimbaji kujadili na kurekebisha sharti lolote la kimkataba, hivyo mikataba hiyo inaweza kurekebishika. Misamaha ya kodi Mwenyekiti alisema mikataba ya uchimbaji madini ina vifungu vingi vinavyotoa misamaha mingi ya kodi ambayo haina maslahi kwa taifa. Alisema kwa kutumia mikataba hiyo, makampuni yamekuwa hayalipi kodi kwa kutumia kinga hiyo.

“Inatosha kusema kuwa mikataba hii haina manufaa kwa taifa.” Alisema kitendo cha mikataba kuruhusu fedha zinazotokana na mauzo ya madini kuhamishiwa nje ya nchi, kamati yake iliona kuwa hali hiyo inainyima nchi nafasi ya kukuza uchumi, kuongeza thamani ya fedha yake kutokana na mauzo ya madini kwa sababu fedha haziwekwi katika benki za ndani ya nchi.

“Kamati inaona kuwa utarataibu wa kuweka fedha katika mabenki ya ndani ungewezesha kupunguza mianya ya ukwepaji kodi unaofanywa na makampuni ya madini, ni wakati sasa nchi yetu ikaachana na uhuru ambao kampuni za migodi zimepewa ya kuhifadhi fedha zitokanazo na madini nje ya nchi,” alisema Profesa Osoro.

Madaraka ya waziri Kamati hiyo ilisema kuwa sheria ya madini ya sasa inatoa uhuru wa madaraka ya waziri katika kuingia katika mikataba ya madini, hivyo imeshauri mikataba yote mikubwa ya madini inapaswa kupata idhini ya Bunge kama nchi nyingine zinavyofanya. Pia kamati hiyo imeona hakuna sababu ya kupeleka migogoro nje ya nchi kwa ajili ya usikilizwaji na uamuzi ikiwa wahusika katika mikataba hiyo wote ni Watanzania na migodi hiyo ipo Tanzania. mwenyekiti alisema kuna mahakama kuu kitengo cha biashara ambayo ipo kwa ajili ya migogoro kama hiyo

Waziri Mwigulu Nchemba Apiga Marufuku Safari za Nje kwa Wote Waliotajwa Kwenye Sakata la Mchanga..!!!

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba apiga marufuku safari za nje ya mipaka ya nchi kwa wote waliotajwa kwenye sakata la mchanga isipokuwa kwa kibali maalum kutoka Serikalini.

======

Hakuna uzalendo zaidi ya kulinda rasilimali za Taifa, Hakuna utetezi wa wanyonge zaidi ya kulinda rasilimali zao. Hongera sana Mh.Rais kwa uzalendo wa vitendo kwa Taifa letu.

Naelekeza wote waliotajwa kuhusika hakuna kutoka nje ya mipaka ya nchi yetu isipokuwa kwa kibali maalum kutoka serikalini. Vyombo vitekeleze maagizo ya Rais kwa utimamu.

Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi.
12/06/2017

Baba Mzazi wa Mhe Anna Mghwira Afunguka Haya Kuhusu Mwanae Kuteuliwa..Adai Umri Wake wa Kuishi Utaongezeka..!!

$
0
0

Baba mzazi wa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira, Elisha Mghwira (87) amesema taarifa za kuteuliwa kwa binti yake na Rais John Magufuli kushika wadhifa huo amezipokea kwa furaha na kwamba zitamwongezea muda wa kuishi.

Anna ambaye alikuwa mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, aliteuliwa hivi karibuni na Rais Magufuli kujaza nafasi ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Saidi Meck Sadiki aliyejiuzulu.

Akizungumza na gazeti hili nyumbani kwake katika Kata ya Kibaoni mjini hapa jana, mzee Mghwira alimtaka mwanaye kuendeleza uadilifu alionao ili asimwangushe kiongozi aliyemteua.

“Ingawa kumbukumbu nyingi nimeanza kuzisahau kutokana na uzee wangu, lakini niujuavyo Mkoa wa Kilimanjaro ni mkoa wenye wasomi wengi kuliko mkoa wetu wa Singida na mikoa mingine mingi,” alisema.

Aliongeza: “Kwa hiyo, mtoto wangu Anna ana mtihani mkubwa katika kuwatumikia wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro, lakini Mungu atamtangulia aweze kuwatumikia vyema.”

Alisema Anna ni mtoto wake wa tatu kati ya watoto tisa na kwamba, amekuwa na bidii ya kujisomea kuanzia shule ya msingi, ni mchapakazi asiye na rekodi ya udanganyifu.

Akizungumzia uteuzi huo kanisani jana, Askofu wa Kanisa la Pentekoste (FPCT) Singida Mjini, Dk Paulo Samwel aliwataka wazazi mkoani humo kuwasomesha watoto wao wa kike ili mkoa huo uweze kutoa viongozi wengi zaidi.

“Tukiwa na wasomi wazuri wa kike ipo siku mkoa wetu wa Singida utatoa kiongozi wa ngazi ya juu zaidi ya ukuu wa mkoa. Namshukuru Dk Magufuli kwa kumteua Anna Mghwira nina uhakika hatajutia uamuzi wake,” alisema.

Ametoa wito kwa wanaume wanaosababisha watoto wa kike kutotimiza ndoto zao kielimu kwa kuwabebesha mimba wafichuliwe ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.

Baada ya Kutajwa Jana..Ngeleja,Chenge na Kafumu Wavunja Ukimya Juu ya Uhusika Wao Katika Sakata la Madini ya Acacia..!!

$
0
0

VIGOGO waliotajwa katika ripoti ya pili ya kuchunguza makontena yenye mchanga wa madini (makinikia)  kuisababishia Serikali hasara ya matrilioni ya fedha kupitia sekta ya madini, walipokuwa wakihudumu katika nyadhifa zao serikalini wamevunja ukimya.

Vigogo hao wamezungumzia ripoti hiyo ya pili iliyowasilishwa kwa Rais Dk. John Magufuli Ikulu Dar es Salaam jana, ambapo kamati husika ilichunguza hasara ambayo nchi imepata tangu 1998 usafirishaji wa mchanga wa dhahabu nje ya nchi ulipoanza.


Mbunge wa Bariadi, Andrew Chenge (CCM), alipoulizwa maoni yake juu ya kutajwa na kamati hiyo, alisema hataki kuzungumza chochote juu ya ripoti hiyo, huku Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (CCM), akisema sheria ya madini ya 2010 ingefuatwa, nchi isingekuwa hapa ilipo.

Kwa upande wake Kamishna wa Madini wa zamani, Dk. Dalaly Kafumu, alisema kwa sasa  hawezi kuzungumza jambo lolote kwa kuwa ni yeye ni mmoja wa watuhumiwa waliotajwa kwenye ripoti hiyo.

Chenge

Baada ya kutoka kwenye kipindi cha asubuhi cha Bunge ambacho alikuwa akikiendesha, Chenge alipotakiwa kuzungumzia ripoti hiyo, alijibu kwa ufupi.

“Sizungumzi na mtu,” na alipoulizwa kama hata salamu hataki, alisema. “Sizungumzi na mtu mimi,” alisema Change ambaye aliwahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Chenge alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali kati ya 1972 na 1990, ambapo mwaka 1993 aliteuliwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali nafasi ambayo alidumu nayo hadi mwaka 2005.

Dk. Kafumu

MTANZANIA ilimpomtafua Mbunge wa Igunga, Dk. Dalaly Kafumu (CCM), ambaye ametajwa kutaka kuingilia ripoti ya kamati ya kwanza iliyochunguza mchanga huo, alisema hataki kuzungumza chochote kwa sasa ingawa anaamini kila kitu kiko sawa.

“Kwa kuwa nimetajwa kama mtuhumiwa, sitaki kusema kitu kwa sasa kwa sababu hili ni sawa na jambo lililo mahakamani tu kwa kuwa wamesema tutahojiwa, lakini kila kitu kiko sawa,” alisema Dk. Kafumu.

Alipoulizwa kama ni kweli alikutana na Profesa Abdulkarim Mruma, aliyekuwa mwenyekiti wa kamati hiyo ya kwanza na ni nini walichozungumza, Dk. Kafumu alisema. “Nimeshasema no comment (sina la kusema ),” alisema Dk. Kafumu.

Dk. Kafumu ni moja ya watumishi waliohudumu ndani ya Wizara ya Nishati na Madini ambapo alifanyakazi kazi ndani ya wizara hiyo kuanzia mwaka 1983 hadi 2011, alipoacha na kwenda kugombea ubunge katika uchaguzi mdogo wa marudio wa Igunga, baada ya kujiuzulu kwa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Rostam Aziz.

Taarifa zilizopo kwenye tovuti ya Bunge zinaonesha, mwaka 1983 mpaka 1987, Dk. Kafumu alikuwa mtaalamu wa miamba na madini wa wizara hiyo, mwaka 1987 mpaka 1992, mkufunzi na mtafiti wa madini, mwaka 1992 mpaka 2002 akawa mtaalamu mwandamizi wa madini, mwaka 2002-2004, mtaalamu wa miamba mkuu na mbobezi  wa madini, mwaka 2004-2006, alikuwa ofisa mawasiliano na mwaka 2006 mpaka 2011, alikuwa kamishna wa madini.

Ngeleja

Kwa upande wake Ngeleja aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, kuanzia mwaka 2008 hadi 2012, alisema hataki kuzungumzia juu ya kilichoelezwa na kamati hiyo ikiwamo kutajwa kwake, bali anachoweza kusema ni kuwa, Rais Magufuli ameonesha uzalendo. 

“Sitaki kuzungumza yaliyo kwenye ripoti ya uchunguzi, ila tu nisema kwa wale tuliosikiliza wakati ripoti inawasilishwa na wakati Rais mwenyewe anazungumza, unaona hisia za uzalendo ambazo Rais anazo, na ameeleza kwa uchungu mkubwa namna ambavyo tunastahili kupata zaidi kuliko tunachopata sasa.

“Lakini jambo kubwa alilolifanya, amesema atamkabidhi taarifa (Spika wa Bunge), kwa sababu msingi wa mambo yote haya ni sera na sheria za nchi.

“Kwamba sisi kama Bunge tutimize wajibu wetu tuhakikishe mapungufun yote yaliyo pale tunayafanyia kazi, lakini kikubwa  amesema chenji (fedha zilizokwepwa na migoni) yetu irudi na amewakaribisha wawekezaji wakae mezani, lakini baada ya kuzingatia masilahi ya upande wetu, ni jambo jema.

 “…wakati nachangia bajeti ya Wizara ya Nishati nilisema, sheria hata tuliyo nayo sasa tungekuwa tumeitekeleza vizuri tusingekuwa hapa tulipo na moja ni kuhusu mikataba iliyofungwa kabla ya mwaka 2010,” alisema

Alisema kifungu cha 116 cha Sheria ya Madini, kinasema mikataba yote iliyofungwa kabla ya kutungwa kwa sheria ya madini ya mwaka 2010, inatakiwa iheshimu na  itambulike kwa utaratibu wa sheria hiyo.

“Kwenye kifungu cha 11 cha hii sheria ya madini, inasema kila baada ya miaka mitano baada ya kuanza kutumika hii sheria, mikataba yote ya madini ipitiwe upya.

“Mimi nilijiuzulu uwaziri Mei 4, 2012, sasa ni miaka mitano imepita, na wakati najiuzulu mimi tulikuwa tumemaliza kutunga kanuni, ninachotaka kusema ni kwamba kupitia hicho kifungu cha 11 hilo ndilo dirisha la kujadiliana yale ambayo kipindi kile kilishindikana,” alisema

Waziri huyo wa Nishati na Madini wa zamani, alisema kuwa kifungu cha 10 cha sheria hiyo kimeweka wazi namna Serikali inavyoweza kumiliki hisa kimkakati kwa kutumia dirisha hilo.

“Utaratibu huo ndiyo tumeutumia kwa Mchuchuma na Liganga, ambapo serikali ina asilimia 20 za bure, Ngaka ina asilimia 30 za bure, hayo ndiyo niliyosema,” alisema Ngeleja.

Credit - Mtanzania

Ukarimu wa Vodacom Tanzania Wawafikia Wakazi wa Kiwangwa Bagamoyo

$
0
0

Vodacom
Kampuni ya mawasiliano inayoongoza nchini Vodacom Tanzania kupitia kampeni yake ya “Ukarimu wa Vodacom” yenye lengo la ukarimu, ushirika na utoaji katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhan na katika maisha ya kila siku imewafuturisha wakazi wa Kiwanga wilayani Bagamoyo katika mkoa wa Pwani.

Huduma hii yenye lengo la kuendeleza mshikamano inakwenda sambamba na kuwawezesha Waislamu na Watanzania kwa ujumla wao kujiunga na kifurushi kinachowapatia muda wa maongezi, SMS na kuwawezesha kupiga simu BURE wakati wakisubiri muda wa kula daku, kugawa tende pamoja na maji. Pia huduma hiyo inawakumbusha muda wa kuswali na kuwapatia Mawaidha na Hadith. Ili kujiunga na huduma hii mteja anapiga *149*01# kisha anachagua aina ya bando kulingana na uwezo wake wa kifedha, kuna bando linalodumu kwa saa 24 na lingine linadumu kwa siku 7.

Akizungumza mara baada ya kupata futari, kiongozi wa msafara wa Ukarimu wa Vodacom kanda ya Pwani, Neema Mjuba alisema “Tunashukuru sana tumeshatembelea maeneo tofauti tofauti kanda ya Pwani na Misikiti mbalimbali, tunawashukuru sana wenyeji wetu wa kuweza kutupokea vizuri na kufurahia ofa hii ya ukarimu wa Vodacom”. Zaidi tazama video hapa chini.

Viewing all 104689 articles
Browse latest View live


Latest Images