Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

JISAJILI USHINDE GARI LA BUREEEEE KABISA

0
0
Umeshawahi Kufikiria Kupata Gari la Bure bila Kulipa Chochote... Basi hii Kampuni ya Cars From Japan Wanakupa Nafasi Hiyo ...

CHAKUFANYA NI Fuata Maelekezo hapa chini Jinsi ya Kuweza Kuwa Mshindi wa Gari hilo..

Bonyeza Hapa >>> SHINDA GARI YA BURE <<< Kujisajili ni Bure tu...

Kisha Jisajili kwa Kuweka Jina na Email Yako

Fahamu Njia Nne za Kulinogesha Penzi Lako Kwake Daima..!!!

0
0

KUPITIA safu hii uipendayo, leo ninakupa njia nne zitakazolifanya penzi lako liendelee kunoga, hata kama litakuwa limeanza kufubaa utaliamsha upya.

Wengi wamekuwa hawaelewi mambo mengi kuhusu uhusiano ndiyo maana huishia kulalamika kwamba wanapenda sana lakini mwisho wa siku huishia kutendwa.

Hakuna mtu ambaye hahitaji faraja, kila aliyekuwa na mpenzi wake anahitaji kuwa na furaha. Hakuna mtu ambaye anaingia kwenye mapenzi ili apate msongo wa mawazo, kila mtu anayediriki kuutoa moyo wake, kitu cha kwanza anachokitarajia ni faraja kisha furaha.

Ipo hivyo! Watu wengi wanakuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi huku wakiwa na matumaini kwamba hao waliokuwanao inawezekana watakuwa wapenzi wa maisha yao yote. Pasipo kujua, wakati mwingine kuna makosa hufanyika, mtu hajui afanye nini ili penzi alilonalo kwa mpenzi wake linoge, hajui ni njia zipi zitamfanya kupendwa kila siku.

Leo nitakutajia njia chache ambazo kama utazifanya, nakuhakikishia penzi lenu litashamiri zaidi ya lilivyo hivi sasa.

MPE UHURU KWANZA

Kila mtu anapenda kuwa huru, kuachwa afanye mambo yake anayoyapenda. Hakuna mtu anayependa kuingiliwa, hasa kwenye masuala ya kutumia simu yake. Kama kweli unahitaji penzi linoge, usitake kuingilia mambo yake hasa katika matumizi ya simu, unachotakiwa ni kumwambia muda ambao hupendi kuona akizungumza na simu na si kwamba kila unapoona simu yake inaita, unaichukua kwa nguvu.

Mapenzi hayapo hivyo, mpe uhuru mwenza wako. Haimaanishi mtu kama hajatulia basi kuchukua simu muda wote inapoita ndiyo kutamfanya kutulia, hapana, bali kwa kufanya hivyo utampa mbinu nyingine ya kuweza kupambana nawe. Unachotakiwa ni kumfanya kuwa huru, usimuingilie.

CHUKUA MUDA WAKO KUMTOA ‘OUT’

Wengi hukosea hapa, huwa hawapendi kwenda matembezi na wapenzi wao. Wengine hujifanya wapo bize, hata ukimwambia Jumamosi nataka tutoke out atakwambia anataka kufanya hili na lile.

Rafiki yangu, kila mtu anahitaji kuwa karibu na mpenzi wake, hakuna anayependa kuwa na mpenzi ambaye muda wote yupo bize tu. Mchukue, nenda naye sehemu. Kutoka mitoko ya mara kwa mara itawafanya muwe karibu zaidi, itawafanya muda wote mzidi kupendana, ila kama utajifanya upo bize, jua kuna mtu ataitumia nafasi hiyo kutoka na umpendaye.

PENDELEA KUFANYA UTANI

Hakuna mtu anayempenda mpenzi ambaye yupo siriazi saa ishirini na nne. Pata muda wa kukaa na kutaniana naye. Mchombeze kwa vineno vya utani, mpetipeti, mlaze kitandani na uanze kupiganapigana naye vibao vya kimahaba hata kwa kutumia mito ya kulalia.

Unapokuwa siriazi kila wakati inakuwa ni vigumu mwenzako kulifaidi penzi, pendelea kutabasamu inapobidi kila unapokuwa na mpenzi wako, siyo kila atakachokwambia wewe uso wako umekunja ndita kiasi kwamba ataonekana kukuogopa na kumtafuta mtu mwingine ambaye atahitaji kuliona tabasamu lake, atahitaji kuona akifanyiwa utani wa mahaba nk.

HEBU MSIFIESIFIE BASI

Wengi wanaogopa kuwasifia wapenzi wao, hawajui kama kila mtu duniani anapenda kusifiwa. Mpenzi wako anapovaa nguo nzuri zilizomtoa, usikae kimya, mwambie amependeza kwani hilo litamfanya kufurahi sana. Kama utakuwa na mpenzi halafu kila siku humsifii hata akifanya kitu gani, jua kwamba atajisikia vibaya, wakati mwingine atahisi hayupo sawa kwa kuwa tu hujawahi kumsifia.
Unapomsifia mpenzi wako kunamfanya kuongeza umakini katika kuvaa kwake, kununua manukato na hata jinsi atakavyosuka au kunyoa atafanya kwa ubora wa hali ya juu kwa kuwa anajua utamsifia

Dalili 5 Za Mwanaume Anayekupenda Kwa Dhati

0
0
MAPENZI
Undapo utaona dalili hizi kwa mwezi wako wa kiume basi tambua fika basi, ya kwamba anMapenzi ya kweli.

1. Anakusaidia fedha pale unapokua umekwama kabisa, yuko na jukumu la kukusaidia kiuchumi.
Anapenda kukupa kile ambacho amejaaliwa nacho. Hana mkono wa birika, Huyu anakupenda!

2.  Anazungumzia future yake na wewe, mipango ya baadae pamoja na wewe, huyu anayo dhamira ya dhati ku Anakupigia simu mara kwa mara na kukuuliza siku yako imeendaje. Anafanya hivi kirafiki na kwa upendo, haigizi. Anakupenda kweli.

3. Anakutembelea mara kwa mara, anakuwa karibu na wewe kipindi unaumwa, hii inamaanisha kwamba yupo tayari kukuvumilia katika shida na raha. Mpende mwanaume huyu.

4. Anawapenda ndugu zako kama ndugu zake. Anaongea nao vizuri na kusaidiana mambo ya hapa na pale. Mtizame kwa jicho la tatu huyu mwanaume!


5. Anaongea na wewe kwa adabu na kwa upole, anakukosoa bila wasiwasi kama kuna mambo unaenenda visivyo. Anakuelekeza njia zilizonyoka..sio wa kumuacha huyu!

Jinsi Ya Kumfanya Mwanamke Apagawe Kwako

0
0
mAPENZI
Kuna vitu vingi ambavyo unaweza kutumia kwa manufaa yako ili kufanya wanawake wakuone unavutia. Amini usiamini, hivi vitu si lazima uwe tajiri wala uwe na urembo wowote. Mwanzo kati ya vitu hivyo vingi ni rahisi kuvitumia kwa urahisi. Hii hapa ni orodha ya mambo ambayo ukiyazingatia yatakufanya wewe uwe na mnato kwa mwanamke yeyote yule.

1. Uwezo wako wa nishati
Nishati inaweza kuwa na mkusanyiko wa vitu kadhaa, kama vile kuhisi kwa vipepeo ndani ya tumbo, kusuka, wasiwasi ama vitu tofauti kabisa. Kwa mtizamo wa moja kwa moja, nishati inahusiana na yote yale ambayo yanamfanya mwanamke kujiskia raha wakati anapokuona ama kutaka kuutumia muda wake mwingi akiwa na wewe. Nishati inacheza nafasi kubwa katika mapenzi kama wataka kumtongoza mwanamke na ufaulu kwa urahisi. Ili kupeana nishati zaidi kila wakati unapokuwa na mwanamke, hakikisha kile kikuu unachohitaji kufanya ni kumchekesha, kumsapraiz, umguse kwa bahati mbaya mara kwa mara, kuwa mwenye michezo nk. Zote hizo zitamfanya kukufikiria wewe mara 24/7.

2. Mbinu utakayoitumia kumsifu
Kulingana na utafiti kutoka NBC unadai ya kwamba wanawake wengi hawajiskii huru kupewa ama kupokea sifa kutoka kwa wanaume. Lakini usikatwe na tamaa! Vile ambavyo utampongeza mwanamke inaweza kucheza pakubwa kufaulu kumpata mwanamke unayempendae baada ya muda. Afterall ukimsifu kitofauti tofauti anaweza kukubali ama kukuona kama wewe ni mzaha kwake. So kuhepa aibu kama hizi ndogo ndogo, unafaa umsifu mwanamke kwa jambo ambalo ni la kwake pekee, yaani kitu ambacho utamsifu nacho hakipatikani kwa mwingine. Mfano waweza kumakinika kwa kitu ambacho anafanya wakati flani na utumie ujuzi wako wa kiume kumsifia na jambo hilo. Mfano unaweza kumsifu kwa uwezo wake wa kuimba, kuchora, mtindo wake wa kutembea nk. [Soma: Mbinu ya kutongoza kwa wale wanaojifunza]

3. Upambo wako
Si lazima uwe mwanamume wa kuvutia ili umvutie mwanamke. Utafiti umebainisha kuwa wanawake hawavutiwi na urembo wa mwanamume, nywele zake wala ngozi yake. Mwanzo kuwa mrembo kama mwanamume kuna ubaya wake mwingi ikizingatiwa kuwa unaweza kuonekana kama pleya ambaye unapendwa na wanawake wengi.

Kile ambacho unachohitajika hapa ni uhakikishe kuwa uwe nadhifu kimwili na mavazi yako. Kufanya hivi kutakusaidia wewe kuonekana mtu timamu halikadhalika inakufanya wewe kuwa na confidence ya kapproach demu yeyote yule.

4. Ujuzi wako wa kutangamana 
Lazima atleast uwe na ujuzi ambao utakusaidia wewe kuweza kutangamana na wengine. Kama mwanamume lazima uwe na ujuzi ambao utakusaidia wewe kutangamana na wengine kwa urahisi. Hii inamaanisha kuwa lazima uwe na ujuzi flani wa kuongea na wanawake ndipo utakapojua jinsi ya kumfanya apagawe na wewe.

5. Kiwango chako cha kujiamini
Kitu cha mwisho ambacho ni muhimu kwako kuwa nacho ni kujiamini. Kujiamini ni njia moja wapo ya lazima uwe nayo ili uweze kuiteka hisia ya mwanamke yeyote yule.[Soma: Njia za kuwa na confidence kama mwanaume]

KUMBUKA: Vitu vyote tulivyoeleza hapo juu havitakuwa na manufaa yeyote yale iwapo kama hutaweza kujiamini kama mwanamume. Hivyo ni lazima kwako kuhakikisha kuwa mwanzo unajijenga kwa kuwa na confidence. Hii ni kuanzia kujitambua wewe mwenyewe bila kujishuku, kuongea bila woga wowote wala kutoingiwa na wasiwasi wakati wowote ukiwa karibu na mwanamke.

He Rapéd Me & Now He’s My Boyfriend

0
0
Am a young girl of 20, and a 300-Level student. In Nov 2011, things fell apart between my boyfriend and I. I was madly in love with him at the time and he had denied me in presence of my friends.
I was finding it very hard to move on; I started drinking heavily, I made friends with a neighbor of mine whom we both stayed in the same hostel off campus. I started sharing my problems with him and we soon became really close.

One day, one of my friends who came to spend some time with me invited her boyfriend over so I decided to give them little space so I left to my neighbour’s room, after spending some time on returning to my room I realised my friend’s boyfriend had slept off, it was about past 11 pm and a face-off was going on between two rival cults in school making it very risky to move at night.
My friend pleaded with me to pass the night at my neighbour’s room because it was early in the semester and other students were not yet in school. So I went back to his room and asked if I could spend the night and he said yes.

Later on that night he started acting up trying 2 touch me, I pleaded and begged him that I could not do it and was still a virgin, but he didn’t listen. I had little or no strength that night because I was drunk as usual, then he forced himself on me.

After the incident he begged me that he was sorry and he never believed that I was saying the truth when I told him I was a virgin, then he started asking me out. I was reluctant at first but I couldn’t speak out, I couldn’t stand how my parents would treat me when they realised I had lost my virginity, especially to rapé. I was going to be considered as damaged goods, so I kept it all to myself and concluded that I had nothing else to lose if I dated him, so I did.

In the beginning of the relationship he treated me badly, forcing himself on me whenever he was in the mood; whether I wanted it or not when he had to get down, he had to get down.
This continued for some months till he forced himself again on me one afternoon when I was ill, the pain was too much for me that in the struggle I tore his clothes and injured his hands. After he had finished, he changed his clothes and travelled leaving me crying on the balcony, he didn’t call for months.

I heard so many stories from his room mate telling my friends that he had a girlfriend and I was just a side chick and in fact that I was the one who was throwing advances to him and I willingly agreed to be his bedmate.

I was shattered and I tried pulling myself back together only for him to return 3 months later calling and telling me he was sorry and he wanted to be serious with me this time and he was for real.
After so many condemnations from my friends, I returned to him. Since then he has been caring at least so I thought but one thing still continued; the continuous séxual abuse. It didn’t matter if I was on my period, or I was sick, or even if I was in tears, he’d tie my hands and even use the pillow to cover my mouth to prevent people from hearing my voice.

After he’s done he becomes sane and he says he’s sorry and expects everything to just be fine. Last month I discovered I was pregnant, my boyfriend took it like a joke, asking me to stop being dramatic that it’s a normal thing that girls do all the time.

Four days after the abortion even though I was still bleeding, he started demanding for séx, and when I refused he started ranting about how he does things for me and that he gains nothing from me in return and then he had his way as usual even after I had told him that it was advisable to desist from séx at this times because my womb was still open and fragile and it could lead to infection.
On Wednesday, he read a chat between I and a friend of mine whom I usually share my private issues with and he accosted me angrily, I tried explaining things to him but he hit me and my lips started bleeding.

He ripped off all my clothes, dragged me on the floor to his bathroom in tears,(although this was not the first time it would happen other times he’d threaten me with a knife, even though at the end of it all he always says he was joking and didn’t mean it).
He washed my body and had séx with me again.

After he was done he told me he didn’t see anything wrong in what he had done but that he was sorry though, he has being apologizing since then but at this point I really don’t know what to do. He didn’t even send me a val card, message or even a handkerchief, although he could really be caring at times.
I am quite attractive and I get offers from many other guys outside but I’m scared that they’ll turn out to be worse than he is and maybe they are also just hiding their true intentions.

He’s still apologizing and claiming he was under the influence of alcohol and he claims he loves me very much, but I must really say I do not know what to do.

Should I move on? Or should I stay and hope that he’ll change for real this time?

Profesa wa Kenya Amwagia Sifa Kedekede Rais Magufuli..Adai Akikaa Miaka 10 Madarkani Tz Itakuwa Juu Kiuchumi..!!!

0
0

MWANATAALUMA kutoka nchini Kenya, Profesa Patrick Lumumba amesema kuwa endapo Rais John Magufuli ataendelea na jitihada za kupambana na ufisadi kwa miaka 10, uchumi wa Tanzania utakuwa juu.

Profesa Lumumba alisema jana kwenye Tamasha la Tisa la Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), alipokuwa akizungumzia mwanasiasa kuinuka na kuanguka barani Afrika.

Katika maelezo yake, Profesa Lumumba alisema rushwa imeondoa afya barani Afrika, wanasiasa wanapoiacha ikawatawala inawaletea shida. Alisema kwa kipindi kifupi Rais Magufuli alipoingia madarakani, ameonesha njia kwa wanasiasa wengine barani Afrika, ambao wamekumbatia rushwa na kuwaacha wananchi.

“Magufuli ana pumzi ya hewa safi, kama ataendelea hivi baada ya miaka 10 uchumi wa Tanzania utakua juu. Mungu msaidie Rais John Magufuli,” alisema Profesa huyo. Kwa upande mwingine, alisema kuwa Afrika ni bara zuri na lenye uwezo, ila kilichofanyika kwa miaka 30 iliyopita kumekuwa na viongozi wabinafsi, lakini katika miaka ya sasa wameibuka viongozi wazalendo kama Magufuli, Rais Paul Kagame wa Rwanda, Rais Yoweri Museveni na wengineo.

“Viongozi kama hawa wakiungwa mkono na wananchi wazalendo, Afrika itapiga hatua,” alisema. Aliwataka waafrika wajue watambue kuwa umoja ni nguvu utengano ni udhaifu, hivyo ni jambo linalochukua muda mrefu. “Ni jambo lililonifurahisha kuwa Magufuli ametoa mafichoni watu waliohodhi mali zetu kwa muda mrefu na kukubali kulipa. Ni hatua nzuri inastahili kupongezwa,” alisema.

Bad News..Watu Watatu Wachinjwa Kama Kuku Rukwa..Kisa Kizima Hiki Hapa..!!

0
0

WATU watatu wameuawa kikatili kwa kuchinjwa katika matukio tofauti yalitokea mkoani Rukwa, mmoja kati yao akiwa ni mfanyabiashara kutoka jijini Mbeya, Elizabeth Kalenga (36).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando alithibitisha mauaji hayo akisema yalitokea Juni 6, mwaka huu saa 3:45 usiku katika Kijiji cha Sakalilo kilichopo katika Bonde la Ziwa Rukwa, Kata ya Ilemba wilayani Sumbawanga.

Alisema kabla ya kuuawa, wauaji walimvunja Elizabeth taya la kushoto walipomvamia. “Chanzo cha mauaji hayo ya kikatili bado kinachunguzwa,” alisisitiza Kamanda Kyando . “Watuhumiwa walimkuta marehemu akiwa nje ya nyumba yake na kumuuliza kama mtoto wake wa kiume ambaye ni Justine Kalenga yupo na alipowauliza wa nini, ndipo walipofyatua risasi moja juu na kumpiga na kumvamia,” alisema.

Kwa mujibu wa Kamanda Kyando watuhumiwa wawili ambao hakuwa tayari kuwataja majina yao wamekamatwa kwa mahojiano zaidi na watafikishwa mahakamani pindi upelelezi wa awali wa kipolisi utakapokamilika.

Katika tukio lingine; watu wawili mmoja akijulikana kwa jina moja la Rasi wameuawa kwa kushambuliwa na kuchinjwa kisha miili yao kuchomwa na kuteketezwa kwa moto katika Kijiji cha Mpui kilichopo katika Wilaya ya Sumbawanga wakituhumiwa kwa wizi wa mifugo.

Kamanda Kyando alisema kuwa tukio hilo lilitokea Juni 14 mwaka huu mchana katika kijiji cha Mpui, Kata na tarafa ya Mpui wilayani Sumbawanga. “Chanzo cha mauaji hayo ni wizi wa mifugo ambapo wawili hao walihisiwa kuwa ni wezi, ambapo walibambwa na wananchi wenye hasira wakiwa wanaswaga ng’ombe wawili wa wizi,” alisema.

Katika tukio lingine Mkazi wa Mtaa wa Kashai katika Manispaa ya Sumbawanga, John Chinga (29) alikutwa akimiliki risasi mbili za bunduki aina ya shotgun bila kuwa na vibali halali. Kamanda Kyando alisema mtuhumiwa huyo ambaye amekamatwa kwa mahojiano alikutwa akiwa na risasi hizo chumbani kwake katika Mtaa wa Kashai katika Manispaa ya Sumbawanga. Alisema mkasa huo ulitokea Juni 13 mwaka huu saa 3:5o usiku

Neema Yatua Jangwani..Manji Arudi na Kusajili Kimya Kimya ..Sasa Waapa Kuwashangaza Simba Kwenye Usajili..!!!

0
0

NEEMA imeanza kunukia Yanga baada ya Mwenyekiti wao, Yusuf Manji kudaiwa kurejea kimya kimya ili kuinusuru timu hiyo katika kipindi hiki cha usajili. Taarifa za ndani kutoka Yanga zinadai kuna uwezekano mkubwa wa kurejea kwa Manji baada ya wanachama kumuomba.

Manji alitangaza kujiuzulu karibuni na mara kadhaa wanachama wa Yanga wamemwomba arudi ili kuinusuru na ukata. Tangu ajiuzulu, Yanga imekuwa katika wakati mgumu kifedha kutokana na kumtegemea kwa asilimia kubwa katika masuala mbalimbali hasa katika usajili.

Taarifa za ndani ya Yanga zinadai Manji amerejea kimya kimya na kufanya usajili wa mshambuliaji wa Simba, Ibrahim Ajibu na wachezaji wengine maarufu waliopo. Mbali na Ajibu, inadaiwa kawashawishi pia mshambuliaji Donald Ngoma na kiungo Thaban Kamusoko waendelee kuchezea Yanga baada ya mikataba yao kumalizika.

Mwenyekiti huyo anadaiwa kurejea huku kukiwa na habari kuwa, kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima amesajiliwa Simba ingawa awali alikiri kuwa atabaki Yanga. Mchezaji ambaye pia hana uhakika wa kurudi Yanga ni mshambuliaji Amis Tambwe aliyemaliza mkataba wake.

Alipoulizwa kuhusu Manji kudaiwa kurejea na kusajili, Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa alisema hana taarifa hizo wala za usajili wa Ajibu. “Sina hizo taarifa lakini watu waendelee kusubiri huwezi jua nini kitatokea mbele. Kuhusu usajili tunaendelea na kama kuna taarifa tutawaeleza,” alisema Mkwasa.

Mkwasa aliwataka mashabiki wasiwe na wasiwasi kuhusu usajili wanaofanya kimyakimya na muda si mrefu kuna mambo makubwa ya kushangaza yanakuja Yanga. Kauli ya Mkwasa imetafsiriwa kuwa inaashiria kurejea kwa Manji ingawa hapendi kuweka wazi juu ya kauli hiyo.

Juzi Yanga ilifanikiwa kumnasa beki wa Jang’ombe Boys ya Zanzibar, Abdallah Shaibu Ninja na kuwabakisha beki Nadir Haroub Cannavaro na Niyonzima. Hata hivyo, haikusema nani kalipia usajili wao.

Mkwasa amesema ukimya wao kwenye usajili hautokani na ukata bali ni utaratibu mpya waliojiwekea kutowapa nafasi wapinzani kujua wachezaji wanaowasajili. Mkwasa alisema kikosi chao hakihitaji marekebisho makubwa kama ambavyo wengine wanadhani ndiyo maana wako kimya wakiangalia wachezaji sahihi ambao wataweza kutimiza kile wanachokihitaji.

“Ukimya wetu una maana na siyo kwamba tuna tatizo la pesa. Tuna fungu la kutosha kufanya usajili ila tunafuata kile ambacho kimeelekezwa kwenye ripoti ya kocha hasa ukizingatia kikosi chetu kinahitaji marekebisho madogo,” alisema Mkwasa.

Alisema kilichowachelewesha kuanza zoezi la usajili ni kuwaongeza mikataba baadhi ya wachezaji wao nyota ambao mikataba yao ya awali ilifikia mwisho msimu huu. Alisema tayari wamekamilisha kazi hiyo kwa baadhi ya wachezaji na wengine watafanya hivyo wakirudi nchini kutoka michuano ya kimataifa wanayoshiriki.

Alisema wamekusudia kutompoteza mchezaji wao hata mmoja ambaye wanamhitaji na hilo limefanikiwa baada ya wachezaji wote kukamilisha mazungumzo na kilichobaki ni kusaini mikataba mipya.

Baada ya Jina Lake Kutajwa Kwenye Ripoti ya Ufisadi wa Madini..Karamagi Afunguka Haya Mazito

0
0

MMOJA wa vigogo waliotajwa na Rais John Magufuli kuwa anatakiwa kuhojiwa na vyombo vya dola kuhusu mikataba ya madini, Naziri Karamagi, ameibuka na kudai kwamba hadi sasa hajui anatafutwa asaidie kitu gani kwenye sakata hilo.

Katika mazungumzo yake na Raia Mwema, Jumanne wiki hii, Karamagi alisema taarifa za kutakiwa kuhojiwa na vyombo vya dola kuhusu ushiriki wake katika inayodaiwa kuwa hasara ambayo Tanzania imepata katika sekta ya madini, amezipata kupitia magazeti na mitandao ya kijamii na hajui zaidi ya hapo.

“Nashukuru sana kwa kunitafuta. Habari na mimi nimezipata kwenye magazeti na mitandaoni na sijajua hasa ni kitu gani nahitajika kumsaidia Rais kufikia azma yake ya kurekebisha sekta ya madini. Nikishakujua hilo, mimi mwenyewe nitakutafuta,” alisema Karamagi.

Karamagi alikuwa waziri wa Nishati na Madini wakati wa utawala wa Rais Jakaya Kikwete na ndiye aliyekuwa waziri wakati serikali ikiingia mkataba mpya wa mgodi wa Buzwagi ulioleta matatizo bungeni katika wakati wake.

Katika hotuba yake ya Jumatatu wiki hii, baada ya kupokea Ripoti ya Kamati ya Makinikia II iliyoongozwa na Profesa Nehemia Osoro, Rais John Magufuli, alimtaja hadharani Karamagi akidaiwa kuwa mmoja wa watu wanaotakiwa kuhojiwa na vyombo vya dola kutokana na uhusika wake huo.

Ripoti hiyo ya Makinikia, pamoja na mambo mengine, ilieleza matatizo chungu nzima ya sekta hiyo, ikiwamo kwamba Taifa limepoteza mapato ya takribani shilingi trilioni 108 katika kipindi cha kati ya mwaka 1998 hadi mwaka huu, kutokana na uzembe wa usimamizi wa sekta hiyo.

Karamagi alikuwa mmoja wa vigogo 10 waliotajwa na ripoti; wakiwamo mawaziri wengine waliopita wa wizara hiyo, waliowahi kuwa wanasheria na washauri wa kisheria wa serikali pamoja na watu waliowahi kuwa makamishina wa madini katika kipindi chote cha upotevu huo.

Hayo yakiendelea, juzi usiku, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba, alitoa taarifa kwamba watu wote waliotajwa kwenye ripoti hiyo ya Profesa Osoro hawatatakiwa kusafiri kwenda nje ya nchi katika kipindi hiki ambacho vyombo vya dola vitaanza kazi zake.

Orodha hiyo ya vigogo inahusisha watu maarufu kama vile Andrew Chenge, William Ngeleja, Dk. Peter Kafumu, Julius Malaba, Sazi Salula, Paul Masanja, Maria Kejo na  Johnson Mwanyika.

Kulinganisha na Ripoti ya Makinikia I, katika ripoti ya Osoro jambo moja kubwa limeibuka ambalo linahusu uhalali wa Acacia kufanya biashara yake nchini ilhali ikidaiwa haijasajiliwa na Wakala wa Usajili wa Biashara nchini (BRELA).

Mmoja wa wanasheria wabobezi katika eneo la madini nchini, Dk. Rugemeleza Nshalla, aliliambia gazeti hili juzi Jumatatu kwamba Acacia wanafanya shughuli zao kupitia kampuni zilizosajiliwa hapa nchini.

Kwa mfano, alisema mgodi wa Bulyanhulu unaendeshwa na kampuni ya Bulyanhulu, ule wa Buzwagi unaendeshwa na kampuni ya Pangea wakati ule wa North Mara unaendeshwa na kampuni ya North Mara.

“Ni jambo la kawaida kwa kampuni hizo kuanzisha kampuni nyingi kwa ajili ya kurahisisha mambo yao. Unaweza kukuta Acacia haijasajiliwa lakini zile za ndani zimesajiliwa.

“Nisichokipenda mimi ni kwamba linapokuja suala kama la sasa, unakuta Acacia ndiyo inakuwa msemaji wa kampuni hizi za hapa. Sasa kama wanataka, si wasajili hapa na hiyo Acacia yao?” alihoji.

Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS), Godwin Ngwilimi, alisema ameisoma ripoti yote ya Osoro na akasema mambo ya msingi yanafahamika lakini suala la Acacia linaweza kupata maelezo ya kisheria.

“Ngoja nikwambie, kwenye biashara kuna jina la biashara na alama ya biashara. Acacia imesajiliwa huko ilikosajiliwa lakini inaweza kutumia hilo jina ambalo ni alama yake hapa bila kuathiri kampuni zinazofanya kazi zake hapa.

“Kwa mfano, watu wengi wanajua kwamba Vodacom ndiyo inamiliki M-Pesa lakini ukweli ni kwamba huduma za M-Pesa zinaendeshwa chini ya kampuni tofauti kabisa inayojulikana kama M-Pesa Limited. Nadhani hata Azam inaweza kuwa mfano mzuri,” alisema.

Kwa upande wake, waziri mkuu wa zamani, Jaji Joseph Warioba, ametia mkono katika suala hilo akisema kinachotakiwa sasa ni kuyaweka mambo ya rasilimali chini ya ulinzi wa Katiba.

“Ni wajibu wa kila mtu kulinda mali za umma. Baada ya kamati hizi mbili, matatizo yote yanaonekana wazi wazi na hasa katika suala la mikataba na si mikataba tu ya dhahabu bali maliasili yetu yote.

“Kuna udhaifu katika mikataba na usimamizi wa mikataba. Kwenye hili suala tunapambana na watu wazito lakini ni pia hili ni suala la kitaifa. Pamoja na matatizo ya miaka ya nyuma tukubali kwamba ni suala la ulinzi wa rasilimali za nchi ni letu sote. Tuungane.”

Warioba pia alizungumzia tatizo la maadili ambalo vile vile lilijitokeza katika maoni ya wananchi wa Tanzania wakati wa ukusanyaji maoni yao kwa ajili ya mchakato wa kuandika Katiba Mpya chini ya usimamizi wa Tume ya Katiba aliyoiongoza akiwa mwenyekiti.

Kuhusu maadili alisema; “Tatizo la maadili ni kubwa sana. Hili suala lilizungumzwa na wananchi, kubadili sheria pekee hakutoshi kinachotakiwa kufanywa sasa ni kuhakikisha suala la misingi ya kulinda rasimali na maadili iwekwe kwenye katiba ya nchi, liwe suala la kikatiba.

Hisa za Acacia

Wakati sakata la makinikia likiendelea, hisa za kampuni hiyo zimekuwa zikiporomoka katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), kutoka kiwango cha juu cha shilingi 13,000 miezi michache iliyopita hadi wastani wa shilingi 8,000 kufikia jana.

Hata hivyo, wakati ripoti ya kwanza ya makinikia iliyoongozwa na Profesa Abdulkarim Mruma ilipokabidhiwa kwa Rais Magufuli mwezi uliopita, thamani ya hisa za Acacia zilishuka kwa asilimia 40 lakini baada ya ripoti ya Profesa Osoro, hisa zimeporomoka kwa asilimia 13 tu.

Wakati wa shughuli za ununuaji na uuzaji wa hisa zilizofanyika DSE jana asubuhi hadi mchana, bei ya kufungua soko ilikuwa pauni 264 kwa hisa lakini mpaka soko linafungwa bei ilikuwa pauni 261.

Mwisho wa yote ni nini?

Raia Mwema limezungumza na mmoja wa wabobezi wakubwa katika sekta ya madini ambaye aliwahi kushiriki katika mojawapo ya tume zilizoundwa katika miaka ya nyuma ambaye alisema jambo hili linapaswa kuchukuliwa kwa umakini.

Alisema njia pekee ya jambo hili kumalizika kwa usalama ni kwa serikali na Acacia kushirikiana katika kujenga mtambo wa uchenjuaji wa madini hapa nchini na kuziba upungufu uliokuwepo huko nyuma.

“Mwisho wa hili ni nini? Ipo hatari ya marais wastaafu kuletwa mahakamani kutoa ushahidi. Sasa marais wastaafu wakiitwa na kuzungumza mwisho wake ni nini? Mimi naunga mkono juhudi za Rais lakini lazima tuangalie mwisho wa haya.

“ Ni lazima itafutwe kitu kinaitwa win-win situation. Wawekezaji waone wametendewa haki na serikali pamoja na Rais Magufuli ni lazima nao waone juhudi zao zimezaa matunda. Ikipatikana win-win mapema, itaepusha mengi,” alisema.

Mapendekezo ya Kamati ya Makinikia II

Jambo jingine katika hitimisho la sakata hili ni mapendekezo ya kamati ya makinikia II. Mapendekezo hayo ni pamoja na serikali, kupitia BRELA ichukue hatua za kisheria dhidi ya kampuni ya Acacia Mining Plc ambayo imekuwa inaendesha shughuli zake nchini kinyume na matakwa ya sheria. 

Serikali idai kodi na mrahaba kutoka kwa makampuni yote ya madini ambayo yamekwepa kulipa kodi na mrahaba stahiki kwa mujibu wa sheria. 

Serikali iendelee kuzuia usafirishaji wa makinikia nje ya nchi mpaka hapo kampuni za madini yanayodaiwa zitakapolipa kodi, mrahaba na tozo stahiki kwa mujibu wa sheria. 

Serikali ianzishe utaratibu utakowezesha ujenzi wa kiwanda cha uchenjuaji wa makinikia (smelter) ili kuondoa upotevu wa mapato na kutengeneza ajira kwa watanzania. 

Serikali ifanye uchunguzi  na kuchukua hatua za kisheria  dhidi ya waliokuwa mawaziri, wanasheria wakuu wa serikali na manaibu wao, wakurugenzi wa idara za mikataba, na makamishna wa madini, wanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini na watumishi wengine wa serikali na watu wote waliohusika katika kuingia mikataba ya uchimbaji madini, utoaji wa leseni za uchimbaji wa madini na kuongeza muda wa leseni, watumishi na wamiliki wa kampuni za madini, kampuni zilizohusika kuandaa nyaraka za usafirishaji wa makinikia (Freight Forwarders (T) Ltd na kampuni za upimaji wa madini kwa kuvunja sheria za nchi na upotoshaji.  

Serikali ifute utaratibu wa kupokea malipo ya mrahaba ya asilimia na kusubiri malipo ya asilimia 10 kulipwa baadaye wakati kampuni hizo za madini huuza madini hayo na kupewa  fedha taslimu kwa mkupuo. 

Serikali ifanye uchunguzi kuhusu mwenendo wa watumishi wa idara ya walipakodi wakubwa katika Mamlaka ya Mapato Tanzania katika kushughulikia madai ya kodi ambayo Mabaraza ya Rufani ya Kodi na Mahakama zimekwisha yatolea uamuzi na vilevile ichunguze mienendo ya watumishi wa mabaraza ya kodi kwa kutotolea uamuzi kesi za kodi kwa muda mrefu kuhusu mashauri yaliyochukua muda mrefu kukamilika katika vyombo hivyo. 

Benki Kuu ya Tanzania ifuatilie malipo ya fedha za kigeni yanayotokana na mrahaba kwa mauzo ya madini.   

Serikali ianzishe utaratibu wa kulinda maeneo ya migodi na viwanja vya ndege vilivyop migodini ili kudhibiti vitendo vya hujuma vinavyoweza kuwa vinafanywa na kampuni za migodi ikiwemo utoroshaji wa madini. 

Sheria iongeze kiwango cha adhabu zilizoainishwa kwa makosa ya ukiukwaji wa Sheria ya Madini na Sheria za Kodi. 

Serikali kupitia wataalamu wabobezi katika majadiliano na mikataba (expert in negotiation and contract) wapitie mikataba yote mikubwa ya uchimbaji madini (review) na kufanya majadiliano na kampuni za madini ili kuondoa misamaha yote ya kodi isiyokuwa na tija kwa taifa na badala yake kuweka masharti yenye tija kwa pande zote mbili kwa kuzingatia maslahi ya nchi; 

Sheria iweke kiwango maalumu cha asilimia ya hisa ambazo zitamilikiwa na serikali katika kampuni zote za madini nchini. Aidha, sheria ielekeze serikali kufanya majadilaino ili kuwezesha kununua hisa katika kampuni za uchimbaji madini ili kuiwezesha kupata mapato zaidi na ushiriki katika uamuzi mbalimbali muhimu kwenye biashara ya madini. 

Serikali iunde chombo cha kusimamia biashara ya usafirishaji bidhaa nje ya nchi kupitia bandari kama ilivyokuwa shirika la NASACO ili kudhibiti biashara haramu na kuondoa mianya ya ukwepaji kodi.  

Sheria itamke bayana kuwa madini ni mali asili ya Watanzania na iwekwe chini ya udhamini na uangalizi wa Rais kwa manufaa ya Watanzania.        

Sheria itamke bayana kuwa mikataba yoyote ya uchimbaji mkubwa wa madini (Mining Development Agreement) isiwe ya siri na lazima iridhiwe na Bunge kabla ya kuanza kutekelezwa. 

Sheria itoe masharti ya wazi ya kuzingatiwa na iondoe uhuru wa mamlaka ya (discretionary powers) Waziri wa Nishati na Madini, kamishna wa madini na maafisa madini wa kanda katika utoaji wa leseni za uchimbaji madini.  

Sheria ya madini iweke masharti kwamba mwombaji wa leseni ya uchimbaji mkubwa wa madini lazima aoneshe mchanganuo wa kina kuhusu namna mafunzo kwa wazawa yatakavyotolewa kwa lengo la ajira kama wataalamu na kuchukua nafasi za uendeshaji wa migodi husika na kupunguza au kuondoa kabisa wataalamu kutoka nje ya nchi.  

Sheria ielekeze kampuni za madini kuweka fedha zinazotokana na mauzo ya madini katika benki zilizopo nchini ili kuimarisha uchumi wa nchi na kuondoa mianya ya ukwepaji wa kodi na tozo mbalimbali. 

Serikali ipitie na kufanya marekebisho au kufuta na kubadili kabisa Sheria ya Madini na Sheria za Kodi ili kuondoa pamoja mambo mengine, masharti yote yasiyokuwa na manufaa kwa taifa ikiwa ni pamoja na masharti yaliyomo kwenye kifungu thabiti (stability provision). 

Serikali igharimie na kutoa mafunzo kwa watumishi wa serikali ili kuwapatia uelewa na weledi katika nyanja ya majadiliano na uendeshaji wa mashauri yatokanayo na mikataba ikiwemo ya mikataba ya madini (skills in negotiation and arbitration). 

Serikali kupitia kamishna wa madini iwe inafanya ukaguzi wa mara kwa mara  kwa kampuni za madini ili kujihakikishia uzingatiaji au ukiukwaji wa sheria na taratibu za uendeshaji na kuchukua  hatua ipasavyo.

Credit - Raia Mwema

Baada ya Kimya Kirefu..Makonda Aibuka na Haya Makubwa Kuhusu Jeshi la Polisi...!!!

0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amesema jeshi la Polisi katika Mkoa huo linatakiwa kuwa la mfano wa kuigwa katika kukabiliana na kila wimbi la uhalifu, ili wananchi waishi kwa amani kutokana na umuhimu wa biashara.

Makonda ameyasema hayo  wakati wa kupeleka magari 26 ya polisi kwenye ukarabati katika gereji iliyoko maeneo ya Utalii mkoani Kilimanjaro, kwa ajili ya matengenzo pamoja na ufungaji wa Kamera katika magari hayo alipokuwa anazungumza na jeshi la polisi leo Osterbay jijini Dar es Salaam.

Amesema katika kukabiliana na rushwa na jeshi hilo, watafunga kamera katika kila kituo ndani ya jiji la Dar es Salaam, ambapo OCD , kanda maalumu, pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi wataweza kuona kile ambacho kinafanyika.

Makonda amesema jeshi la Polisi Mkoa wa Dar es Salaam linatakiwa kuwa la kisasa zaidi katika kukabiliana na uhalifu wa kila namna ikiwa ni pamoja na kuwa na vifaa vya kisasa.

Amesema katika maboresho hayo wataweka Kompyuta kila kituo ili kuachana na kuandika maelezo katika karatasi na mtu yeyote, baada ya kuwekwa kompyuta hizo asikubali kuandikiwa maelezo katika karatasi.

Aidha amesema kuna baiskeli ziko njiani ambazo zitagawiwa kwa polisi ikiwa ni sehemu ya kukabiliana na uhalifu katika mazingira ambayo kifaa hicho kinaweza kupita.

Nae Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya amesema Jeshi la Polisi kanda maalumu inakabiliwa na changamoto ya magari pamoja na mafuta na kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi katika kukabiliana na wahalifu wa kila namna .

Amesema kuwa kutokana maboresho hayo yataweza kubadilisha hata takwimu zilizo katika kipindi hiki zisirudie kutokana na maboresho hayo.

MAGAZETI YA LEO 16/6/2017

JPM Aporomoka ..Ni kwa Mujibu wa Twaweza..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo Ijumaa 16/6/2017..!!

Hawa Ndio Magaidi Hasa wa Mkuranga na Kibiti (Tanzania) Waliotajwa Rasmi...

0
0
Mkuranga

Ni wazi kabisa kuwa Ugaidi ni Uadui mkubwa sana katika dunia hii, Pia ni Upumbavu na Dhambi.

Nimefurahi sana kusikia hatua iliyoamua kuchukuliwa na Serikali kuwa watapeleka "Wanajeshi" katika Wilaya za Mkuranga na Kibiti ili kuwadhibiti hao Magaidi walioua viongozi wa vijiji, mapolisi na wananchi.

Mwaka 1998, serikali ilichukua hatua kama hiyo ya kuwapeleka wanajeshi wilayani Ngorongoro wakisaidiana na Wamasai ili kupambana na majangili ya kisomali (baada ya mapolisi kushindwa kuwathibiti na OCD wao kuuawa na majangili hayo)

Mpaka leo hii Ngorongoro kumetulia tuli.

Magaidi waliotajwa rasmi wapo 11 na waliotiwa mikononi ni wanne.

Imethibitika kuwa Magaidi hao wote ni waumini wa dini ya kiislam hivyo wengi kuhusisha ugaidi wao na imani ya dini yao. 

Zaidi baadhi ya wananchi wa wilaya hizo walihojiwa na kusema kuwa watu hao wamekuwa wakisema kuwa wanawachukua vijana wao na kuwapeleka Somalia kwa ajili ya mafunzo mbalimbali ya kujikwamua kiuchumi.

Hata hivyo, haijathibitishwa kwa asilimia zote kuwa walipata support za kiimani ya dini yao.

Wafuatao ndio wahusika wa ugaidi waliotajwa:-

1) Faraj Ismail Nangalava

2) Anaf Rashid Kapera

3) Said Ngunde

4) Omari Abdallah Matimbwa

5) Shaban Kinyangulia

6) Haji Ulatule

7) Ally Ulatule

8) Hassan Uponda

9) Rashid Salim Mtulula

10) Sheikh Hassan Nasri Mzuzuri

11) Hassan Njame


Source: Gazeti la Jamhuri trh 13-19.

Ukweli Mchungu..Kama JK na Mkapa Hawaguswi..Kisheri Chenge na Genge Lake Pia Hawastahili Kuguswa,na Wkienda Mahakamani Wanaweza Kujitetea kwa Njia Hizi..

0
0
Andrew Chenge

Mahakama huendeshwa na doctrine au itikadi ya haki bila upendeleo.

Kauli tata za Magufuli na Ndugai za kuwakingia watuhumiwa nambari moja ufisadi wa Madini akina Mkapa na JK ni utetezi tosha kwa Muhongo, Karamagi, Yona na Ngeleja.

Watakapowapeleka mahakamani mawaziri wa zamani wa Madini watakuwa na utetezi wa aina tano:-

1) Moja, "collective responsibility" yaani uwajibikaji wa pamoja katika baraza la mawaziri kwa hiyo hawawezi kutolewa kafara kwa kutekeleza maamuzi ya baraza la mawaziri.

Mahakama itawaachia huru kwa sababu tu wamebaguliwa na haki zao za kikatiba za kutendewa sawa na wajumbe wote wa baraza la mawaziri hususani wenyeviti wa vikao hivyo ambao ni Mkapa na JK. Utetezi huu unaitwa "misjoinder of the accused".


2) Kutomshtaki JK wakati alipokuwa waziri wa Mambo ya Nje miaka ya 1997-2000 wakati mikataba ya Bulyanhulu na mingineo ilisainiwa baada ya kupitishwa na baraza la mawaziri na hakuwa na kinga ya Urais kwenye vipindi tajwa na kutomshtaki ni kuwabagua mawaziri walioshtakiwa na utetezi wa " misjoinder of the accused" ni haki yao na lazima wapewe kwa kuachiwa huru.

3) Sheria ya wawekezaji ya mwaka 1997, sheria ya madini ya 1998 na hata ya 2010, sheria za kodi kuanzia 1998-2004 zilirandana na sera ya CCM ya kuvutia wawekezaji. Wao kwa kusaini mikataba husika walikuwa wakitekeleza sheria na misamaha walioitoa ni kuharakisha kasi ya kuwavutia wawekezaji.

Utetezi hapo ni kuwa hakuna jinai katika kutekeleza sera na sheria za nchi. Hakuna mahakama itawatia hatiani kwa hili.

4) Kauli zembe za Magufuli na Ndugai zinaingilia uhuru wa DCI, DPP, TAKUKURU na Mahakama kwa kuwasafisha watuhumiwa wakuu wa ufisadi ambao ni Mkapa na JK huku watuhumiwa Muhongo na wenzie wakitajwa na taarifa za kamati zilizoundwa na Rais kukidhi kiu za kisiasa na kuwatoa watuhumiwa tajwa kama makafara ya kisiasa haiwezekani vyombo vya utoaji haki kama mahakama viwatendee haki.

Kwa kuhukumiwa kwenye majukwaa ya kisiasa ni dhahiri tayari wamedhulumiwa haki zao za kujitetea kwa sababu Rais Magufuli na Spika Ndugai wameingilia uhuru wa mahakama.

Utetezi huu ni mzito wa watuhumiwa haki zao za kikatiba zimekiukwa pale mihimili miwili ya dola ambayo ni serikali na Bunge imeingilia uhuru wa muhimili mwingine wa mahakama katika kutoa haki.

Huu ni utetezi tosha wa kuwafutia mashitaka feki yenye msukumo wa kumjenga Magufuli na CCM yake kwa kupitia migongo dhaifu ya watuhumiwa.

Mahakama haitachelea kulinda uhuru wake kwa kufuta mashitaka ya kubambikiziwa.

5) Hakuna makosa yoyote ya kupokea rushwa ambayo wametuhumiwa kwa hiyo Mahakama haina jinsi bali kuwaachia tu. Makosa tajwa yangelidhoofisha utetezi wao kwenye namba 1-4 hapo juu kwa kubainika wajumbe wa baraza la mawaziri ambao hawajashtakiwa hawana makosa binafsi ya jinai. Hivyo, hawajabaguliwa.

USHAURI

Kama Mkapa na JK ni "untouchables" then their sidekicks are also the "untouchables"

Chanzo JF

Jiwe la Gizani..Babu wa Loliondo,ACACIA na Media Zetu..

0
0
Mkuu wa Barack na Rais Magufuli

Toka juzi baada ya Magufuli kukutana na CEO wa Barick vyombo karibu vyote vya habari vimejaa 'habari za pongezi' kwa Rais kwa 'kuweza kufanikisha kulipwa' tulichokuwa tunaidai hiyo kampuni.

Taarifa za habari za TV karibu zote na magazeti habari ni hizo hizo.

Licha ya ukweli kuwa jana hiyo hiyo Barrick na ACACIA wote wametoa taarifa za kukataa kulipa chochote sisi vyombo vyetu ni kama hiyo taarifa 'haituhusu' kabisa tuko bize na pongezi.

Inanikumbusha wakati wa Babu wa Loliondo jinsi ambavyo media zoote zilivyokuwa zinaripoti 'miujiza' ya babu huyo huku zikiwa hazitaki kabisa kuripoti taarifa za wagonjwa waliokuwa wanakufa baada ya kutoka huko Loliondo.

Hata taarifa za wataalam wa nje waliofika na kusema 'hakuna tiba' huko Loliondo wagonjwa wasiache dozi za hospitali zilipuuzwa.

Tulikuwa nchi nzima tuko excited na babu wa Loliondo na kikombe chake.

Yeyote aliongea vingine alionekana 'msaliti' na sio 'mzalendo'

Wapo waliotaka Babu wa Loliondo apewe tuzo maalum na kadhalika na kadhalika.

Vyombo vyetu vya habari ndo viligeuza habari ya 'kuuza' na kuwajaza watu ujinga uliopelekea hata watu wengine kupoteza maisha la kusikitisha hii tabia haijawahi kukemewa.

Sasa tuko na kupongezana na kuambiana uwongo mtupu licha ya wahusika kutoa ukweli wao kuwa hakuna walichokubaliana kulipa sisi ndo kwanza na wengine wanataka tuzo kwa tume na Rais aongezewe muda kwa 'haya mafanikio ambayo siyo ya kawaida'.



Chanzo JF

Roma Adai Kutekwa ni Aibu Kwa Serikali, Atia Neno Kugombea Ubunge

0
0
Roma Mkatoliki
Msanii wa muziki wa hip hop, Roma Mkatoliki wamewata baadhi ya watu kuacha kufikiria kwamba kutekwa ndio kumemfanya arudi kwa jamii na kutoa misaada huku akidai kutekwa sio njia ya kumfunza mtu na ni aibu kwa jamii na serikali kwa ujumla.

Tazama Video:

Simba Wamsotea Niyonzima Uwanja wa Ndege..Bin Kleb Amwambia Akitua Bongo Tu Afikie Jangwani..!!!

0
0

WAKATI Yanga wakimsubiria kiungo wao mchezeshaji, Haruna Niyonzima atue nchini kwa ajili ya kumuongezea mkataba watani wao wa Simba wenyewe hawakauki Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere ili wamsainishe. 

Hiyo, ikiwa ni siku chache tangu tetesi zienee kuwa kiungo huyo anayemudu kucheza namba nane tayari amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Simba. Kiungo huyo, hivi sasa ni mchezaji huru anayeruhusiwa kufanya mazungumzo na klabu nyingine kutokana na mkataba wake kumalizika mwezi ujao kwa mujibu wa kanuni za Fifa.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo gazeti la  Championi Ijumaa linazo, kutoka kwa ndugu wa karibu wa Niyonzima viongozi wa Simba walikuwa tayari wapande ndege kumfuata kiungo huyo Rwanda, lakini ilishindikana kutokana na kukatishwa tamaa na meneja wake.

Mtoa taarifa huyo, mfanyabiashara maarufu nchini, Mohammed Dewji ‘Mo’ ndiye alikuwa anawasiliana na Niyonzima kwa ajili ya kwenda kumsainisha nchini Rwanda kwa dau la shilingi milioni 70. “Nikwambie ukweli tu, ni ngumu Niyonzima kwenda kusaini mkataba wa kuichezea Simba, kwani mpango wao wa kwanza walioupanga umeshindikana kwani walipanga wamfuate Rwanda alipokuwa kwenye majukumu yake ya timu ya taifa.

“Mipango hiyo ilishindikana ni baada ya meneja wake kuuzuia
uongozi wa Simba usiende huko na badala yake wamsubirie hadi ataporejea nchini na baada ya kuona wamekwama, viongozi hao wa Simba wakaanza kwenda kumwinda uwanja wa ndege kwa kukagua muda wa ndege wa Rwanda Air na mratibu wa hilo ni Mo.

“Lakini wakati wakipanga hayo, Bin Kleb (Abdallah), yeye aliwasiliana na Niyonzima na kumwambia mara baada ya kutua nchini asionane na yeyote zaidi yake yeye,” alisema mtoa taarifa huyo. Championi Ijumaa,lilimtafuta Niyonzima na kuzungumza naye moja kwa moja kutoka Rwanda kuhusiana na taarifa za yeye kusaini Simba alisema kuwa: “Hayo maneno tu wanaongea, 
nikuhakikishie mimi sijasaini Simba na kama unakumbuka mimi nilikwambia nimeichezea kwa amani Yanga miaka sita hivi sasa.”

Saida Karoli Awasema Wasanii wa Kike Kupitia ‘Bongo Bahati Mbaya’

0
0
Saida Karoli
Msanii wa nyimbo za asili, Saida Karoli amesema kipindi amekaa nje muziki alikuwa akishangaa kuona hakuna msanii wa kike akiimba muziki wa asili zaidi ya kuiga muziki kutoka Ulaya.



Akizungumza na kipindi cha Twenzetu cha Times FM, Saida amesema wasanii hao ni sawa na wimbo wa Rapper Young Dee ‘Bongo Bahati Mbaya’ kwa kufanya kila kitu ni Ulaya na si hapa nchini.

“Tatizo nilikuwa sioni wasanii wakiimba nyimbo za asili hasa wanawake, siwaoni. Nawaona wanaimba nyimbo zinazofanana na za Ulaya, mavazi ya Ulaya, sauti ya Ulaya, sioni sauti za Tanzania kwa wanawake,” amesema Saida Karoli.

“Huwezi kutoa maoni kule nilipokuwa, nikasema labda watu wameamua kuwa Ulaya, ndio maana juzi niliongelea wimbo wa tupo Bongo Bahati Mbaya, kila kitu Ulaya, sauti na mavazi yao ni Ulaya,” ameongeza.

By Peter Akaro

Picha: Lady Jaydee Aonyesha Mjengo Wake Mpya

0
0
Lady Jay Dee
Mambo yanazidi kumnyookea mkongwe wa muziki wa Bongo Flava, Lady Jaydee.


Msani huyo ameonyesha picha za mjengo wake mpya wa kisasa alioujenga ambao upo maeneo ya Kimara Temboni jijini Dar es Salaam.

Kupitia mtandao wa Instagram, mrembo huyo ameweka baadhi ya picha za jumba hilo na kuandika,
“Jide Ville.” Mashabiki wameanza kujiuliza, je huo ndio mjengo ambao yatakuwa makazi mapya ya Jide na mpenzi wake Spicy kutoka Nigeria?

lady jay Dee

Lady Jay dee

Kauli ya CCM Baada ya Viongozi Wao Kutajwa Sakata la Mchanga wa Madini

0
0
Hamphrey Pole pole
Chama Cha Mapinduzi (CM) kimewataka viongozi na wote waliotajwa katika sakata la mchanga wa madini kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola baada ya kutuhumiwa kulisababishia Taifa hasara kubwa ya matrilioni ya fedha kutokana na usafirishaji wa mchanga wa madini kwenda nje ya nchi.

Hayo yameelezwa leo na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ndogo za chama hicho Lumumba jijini Dar es Salaam.

Aidha, Polepole alisema kuwa, chama hicho hakitasita kuwachukulia hatua kwa wanachama wake iwapo watabainika kuliingizia taifa hasara kupitia njia mbalimbali ikiwamo hii ya sasa ya kupitia mchanga wa madini. Polepole amesema kwa sasa chama kinaviachia kwanza vyombo vya dola vifanye kazi yake ya kuwahoji waliotajwa kwenye ripoti hizo mbili.

CCM imepongeza Rais Dkt John Pombe Magufuli ambaye ni mwenyekiti wa chama hicho kwa jitihada kubwa anazofanya katika kuhakikisha kuwa rasilimali za nchi zinawanufaisha watanzania wote.

Polepole alisema nashangaa kuona baadhi ya wanasisasa na watu wengine wakikejeli hatua mbalimbali zilizochukuliwa na Rais Magufuli katika kupigania rasilimali za taifa na kusema hatua hizo ni za kihistoria kwani hazijawahi kuonekana popote.

Pamoja na mambo mengine, Polepole amesema kilichofanywa na Rais Magufuli ni utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ambayo imeelekeza kukomesha wizi unaofanywa na baadhi ya wawekezaji katika migodi ya madini hapa nchini.

Hata hivyo, CCM kimepongeza hatua za awali zilizooneshwa na Mmliki wa Kampuni ya Acacia kwa kukiri kukosea na kuahaidi kufanya mazungumzo na serikali ili kulipa kiasi cha pesa kinachodaiwa na Tanzania.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images