Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

Ajabu: Wezi Wapika Kuku, Kula na Kuosha Vyombo Kabla ya Kuiba na Kutokomea

0
0
KENYA: Majambazi wamevamia nyumba ya Mchungaji eneo la Mweiga katika Kaunti ya Nyeri wakachinja kuku wake, wakampika na kumla na kisha wakaosha na vyombo walivyotumia.

Mchungaji Joseph Muraya alisema kuwa wezi hao waliingia katika eneo lake majira ya saa mbili usiku  na kuwatisha kuwaua kwa kuwapiga risasi endapo wangewataarifa majirani zao.

Nilirudi nyumbani saa majira ya saa mbili na nilishangaa kukuta geti langu limefunguliwa nusu, nilisikia mbwa wana bweka na nilipokwenda kuwaangalia nilikuta mtu mmoja yupo nje, na baadae niligundua kuwa kuna wengine watano wamo ndani, alisema mchungaji huyo.

Majambazi hao baada ya kupika na kuosha vyombo, waliondoka na mali za ambazo thamani yake haijulikani.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Kaunti ya Nyeri, Peter Okiring alisema kuwa Jeshi la Polisi tayari limeanza uchunguzi kuwabaini wahalifu hao.

Comments

Kisa cha Polisi kuwapiga Mabomu ya Machozi Walemavu Dar

0
0

POLISI jana walitumia mabovu ya machozi kutawanya watu wenye ulemavu waliokuwa wamekusanyika na kufunga barabara ya Sokoine jijini Dar es Salaam.

Mabomu hayo yalizua taharuki kwa watumiaji wa njia hiyo na kusababisha usumbufu kwao uliodumu takriban dakika kumi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni, aliliambia Nipashe jana kuwa polisi walilazimika kutumia mabomu kama njia ya kuwakamata watu hao.

Kamanda Hamduni alisema kutokana na kitendo hicho, polisi wanawashikilia watu 40 akiwamo mwanamke mmoja.

Alisema lengo la mkusanyiko huo ulikuwa kwenda kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala kuwasilisha malalamiko yao dhidi ya kukamatwa na askari polisi wa usalama barabarani.

“Ni kweli tunawashikilia watu 40 akiwamo mwanamke mmoja kwa kosa la kufanya mkusanyiko kinyume cha sheria.

“Watu hawa walikuwa wanakwenda kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala kupeleka malalamiko yao kuhusu kitendo cha kukamatwa na askari wa usalama barabarani,” alisema.

Kamanda Hamduni alisema baada ya polisi kufika eneo hilo na kutoa amri mara tatu ya kuwataka kutawanyika, walemavu walikaidi ndiyo maana waliamua kutumia mabomu ya machozi.

Alisema nguvu hiyo ya kutumia mabomu ilikuwa na lengo la kurahisisha ukamataji wa watu hao waliokaidi amri ya polisi kutawanyika.
 Facebook  Twitter  Goog

CHADEMA:Rais Magufuli Aliandika Ripoti za Mchanga Mwenyewe

0
0
Katika masuala ya saikolojia (medical psychology) mtu hawezi kupewa mapendekezo zaidi ya 20 halafu akayakubali yote kwa asilimia 100 bila kuwa na chembe ya wasiwasi. Rais aliyakubali mapendekezo yote ya kamati kwa sababu ripoti ile ya uchunguzi wa mchanga wa madini aliiandika yeye mwenyewe, alieleza kiongozi wa CHADEMA.

“Kisaikolojia haiwezekani kitu ambacho hukijui ukakikubali chote bila kuwa na mashaka,” alisema Katibu Mkuu wa Chama cha Demikrasi na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Vicent Mashinji.

Kiongozi huyo ametoa kauli hiyo leo alipokuwa  akizungumza na waandishi wa habari kuelezea msimamo wao juu ya sakata la madini ambapo wamesema wao hawawezi kushangilia maneno matupu bali wanasubiria matokeo.

“Tunataka kuona hatua kwanza na sio pongezi ambazo sasa hivi zinaambatana na ushabiki wa kisiasa na kauli tupu nyingi nyingi, mara mwizi, mara mwanaume.”

Aidha, Dkt Mashinji alimtaka Rais Magufuli kuueleza umma wa Watanzania kama kampuni ya Barrick ambao ni wamiliki wakubwa wa Acacia ni wezi au ni wanaume. Akitolea ufafanuzi, neno mwanaume, Dkt Mashinji alisema kwa mazingira ya kitanzania neno mwanaume linamaanisha mtu mchapakazi, mtenda haki, anayejituma. Hivyo Rais aseme kama Barrick ni wezi au wachapakazi.

“Ukiongea katika lugha ya kitanzania ukisema huyu jamaa ni mwanaume kwelikweli, tafsiri yake ni rahisi tu, kwamba huyu jamaa ni mchapakazi, ni muungwana ni mtu wa watu, ndivyo tunavyotumia. Hatuongelei mwanaume kwa sababu ya maumbile yake.“

Wakati huo huo, Dkt Mashinji alisema, kama Rais Dkt Magufuli anawapenda Watanzania kama ambavyo anadai, awape katiba ya Warioba kwani ndiyo chaguo lao na ndio itakayomaliza matatizo yote.

Alisema kuwa, wao waamini kama Rais ataruhusu mchakato wa katiba ya Warioba kupitishwa, basi wabunge wa CCM wanaopitisha sheria kiushabiki na kutotimiza majukumu yao hawatarudi bungeni sababu watawajibishwa na wananchi.

Wamiliki wa Makentena ya Magogo yaliyonaswa Bandarini Kukiona cha Moto

0
0
SERIKALI inaendelea kuchunguza wamiliki wa Makontena matano ya magogo yaliyokamatwa bandarini   mwaka juzi, kuwafikisha  mahakamani.

Shehena hiyo ya magogo ya mti aina ya Mkulungu ilikamatwa Novemba 5, 2015 yakionyesha yanatokea Zambia kwa ajili ya kusafirishwa nchi za Mashariki ya Mbali.

Akizungumza na Nipashe jana kwa njia ya simu, Mkurugenzi wa Mipango na Matumizi ya Rasilimali za Misitu, Mohamed Kilango, alisema makontena hayo yalikamatwa baada ya kukosekana kwa nyaraka za mzigo huo.

“Wale wahusika tuliwaambia watuletee ‘documents’ (nyaraka) wakashindwa. Sasa tulichokifanya ni kuendelea na taratibu za kiserikali ili watu hao wapelekwe kwenye mkondo wa sheria. Uchunguzi bado unaendelea siwezi kusema ulipofikia,” alisema.

“Nyaraka zimeshaletwa lakini zinahitajika kuthibitishwa. Lazima tukubaliane na serikali ya nchi ambazo zimetoka kwani utaratibu wa kimataifa upo ili kujiridhisha. Kwa sasa tuko kwenye hatua nyingine,” aliongeza.

Kilango alisema suala hilo limechukua muda mrefu kwa kuwa linahusisha nchi mbili, hivyo uchunguzi unafanyika kwa nchi zote ili kujiridhisha.

Kilongo alisema kama mtu anasafirisha magogo kwenda nje ya nchi, kuna vitu vitatu ambavyo mhusika anatakiwa kuwa navyo. Alivitaja vitu hivyo kuwa ni cheti cha ubora wa mazao ya nchi, cheti cha  kuruhusiwa kusafirisha mazao katika nchi anayotoka na kibali halisi cha nyaraka.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi, alisema nchi hairuhusiwi kusafirisha magogo kwenda nje na kilichoruhusiwa ni mbao kwa kibali maalumu

Sababu za Wanawake Kuvutiwa na Wanaume Wenye Uwezo Mkubwa Kiakili

0
0

  • Mwanamke akiwa na uwezo mkubwa kiakili, lazima atahitaji mwanaume anayeufikia au kuzidi uwezo huo ili waweze kujadiliana mambo mbalimbali.
  • Wanaume wenye akili sana hawazungumzii ngono wakati wote, wana mambo mengi sana ya kuzungumzia. Mwanamke mara zote huvutiwa sana na uwezo wa mwanaume kumudu mazungumzo ya kina kwa mada mbalimbali.
  • Wanawake wanapenda kuwa na mwanaume atakayevutiwa naye mara zote. Mwanaume mwenye uwezo mkubwa kiakili anavutia wanawake kirahisi sana.
  • Mvuto wa kingono unaazia akilini mwa mtu, mwanaume mwenye akili nyingi ana uwezo wa kuingia akilini mwa mwanamke mwenye uwezo mkubwa kiakili.
  • Uwezo mkubwa wa akili kwa mwanaume unaothibitisha kuwa unatafiti kutaka kujua na kujifunza mambo mbalimbali, njaa hiyo hiyo ya kutaka kujua mambo ndio atakayoionesha au atakayokuwa nayo kutaka kumjua mwanamke wake, vitu anavyothamini na pia katika kuujua mwili wa mwanamke wake. Mwanamke mwenye akili anapenda sana achunguzwe na mwanaume wake.
  • Mwanamke ni zaidi ya chombo cha kumstarehesha kingono mwanaume wake; bali ni kiumbe mwenye akili zake, mwenye imani, mwana jamii, mbunifu na kiumbe ambaye haeleweki kirahisi. Mwanaume mwenye uwezo mkubwa kiakili ana uwezo wa kuchunguza na kujua vitu vyote kuhusu mwanamke wake.
  • Mwanaume mwenye uwezo mkubwa kiakili ni chachu kubwa ya kufanikisha maendeleo ya kimaisha kwa mwanamke. Mwanamke anapenda kuwa na mwanaume ambaye anaweza kujifunza mengi kutoka kwake au watakaofanya maendeleo ya pamoja. Mwanamke akiwa na mwanaume wa aina hii atajikuta anapenda mara zote kuwa karibu na mwanaume wake. Atakubali starehe na shida zote watazozipata pamoja akiichukulia kama ni kutengeneza hadithi ya maisha yao.
  • Mwanaume mwenye uwezo mkubwa kiakili ambaye pia hana majivuno au kiburi ni rahisi kuishi naye, ni rahisi kufanya naye kazi na ni rahisi kuzungumza naye. Wanawake huwa wanasisimka wakiwa katika maongezi ya kimapenzi na mwanaume wa aina hii. Mhusishe mwanamke wako kwenye mazungumzo mazuri na yeye atakupatia mapenzi kwa kiwango kitakachokushangaza kabisa.
  • Mwanaume mwenye uwezo mkubwa kiakili anakuwa amepevuka kiasi kwamba uso wake, macho na muonekano wake wa nje tu unaweza kumuelezea alivyo. Mara nyingine jambo pekee unalotakiwa kufanya ni kumuangalia tu na yeye atapata hisia na ujumbe wa kutakwa kimapenzi na mwanaume wake.
  • Mwanaume mwenye uwezo mkubwa kiakili ana “kidunia chake” kila anapokuwepo. Anaingia sehemu akiwa anajiamini sana na uwepo wake lazima uonekane. Ni mtu imara mwenye akili thabiti inayojua mambo mengi. Akiwa karibu na mpenzi wake, mwanamke huyo mara moja atataka aendelee kuwepo sehemu hiyo.



  • Uwezo mkubwa wa kiakili unatokana na ukomavu wako tu, haijalishi kama una elimu za juu sana kama digrii ya chuo kikuu au PhD. Ni hali ya mtu kuwa na busara, kuwa na fikra kubwa, kuwathamini wanawake wote na kumuwezesha na kumuinua mwanamke pekee unayempenda maishani mwako.

Wazazi Wengi Huwakataza Watoto Wao Wasioe Wanyakyusa, Wachaga na Wahaya...Nini Sababu?

0
0
Habari wadau.... Topic hapo juu inajieleza huwa najiuliza hili swali bila majibu..coz wazazi wengi huishia kusema tuu nimesema usioe mnyakyusa,mhaya au mchaga..bila kutoa ufafanuzi..kwanini..hebu tujadiliane..kama unafahamu chochote kuhusu makatazo Haya Funguka Hapa Tafadhali. .
By kibona

Nisha Adaiwa Kula Makombo ya Shilole...Adai Kuishi na Bwana Aliyetemwa na Shilole

0
0
STAA wa filamu za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’ anadaiwa kuwa kwenye mahaba motomoto na aliyekuwa mpenzi wa msanii mwenzake, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ anayejulikana kwa jina la Boy Caro. Chanzo makini kililieleza Risasi Jumamosi kuwa, Nisha anapika na kupakua na mwanaume huyo bila hata aibu ambapo amehama Mbezi Makonde jijini Dar alikokuwa akiishi mwanzo na kuhamia Mikocheni kwa mwanaume huyo.


“Mapenzi ya Nisha na Boy Caro siyo siri tena kwani wanaishi pamoja, wanapika na kupakua hata hivi karibuni aliweka mtandaoni picha ya mkono wa mwanaume uliochorwa tatuu ambapo watu waligundua kuwa ni wa Boy Caro kwani aliichora wakati yupo na Shilole.


“Kiukweli wasanii tumekuwa tukijidhalilisha sana na tunamshangaa Nisha kula makombo ya mwenzake Shilole, je likija suala la ugonjwa si ndiyo tutakufa wote jamani? Maana wasanii wa kike tumezidi sana kushea mabwana,” kilimwagika chanzo ambacho ni msanii wa filamu ambaye hakutaka kuchorwa jina lake gazetini.

Baada ya kupata ubuyu huo wa moto, mwandishi wetu alimtafuta Nisha ili kujua ukweli wa madai hayo, alipopatikana alisema;“Jamani kwani kuwa karibu na Boy Caro ni tatizo? Kama ni Shilole walishaachana, ukaribu unaweza usiwe wa mapenzi, unaweza kuwa wa kikazi na mambo mengine, kuhamia Mikocheni siyo kwa ajili yake bali niliamua kubadilisha mazingira tu.”

SHILOLE ANASEMAJE?“Huyo mtu nilishaachana naye na sikuwahi kumpenda labda yeye ndiye alinipenda sana ndiyo maana hata nilipomuacha alichanganyikiwa, sijawahi kujuta kumuacha hivyo kama yupo na huyo hayanihusu mimi, bidii yangu ni kwenye kazi tu kwa sasa.”

STORI: GLADNESS MALLYA

Je, Kujamiiana Huondoa Msongo wa Mawazo kwa Wanawake?

0
0
UTAFITI uliofanywa na Chuo Kikuu cha State cha jijini New York nchini Marekani unaeleza kuwa manii ni nzuri kwa wanawake kwani huwaondolea msongo wa mawazo.

Pia, watafiti hao wamesema wanawake wanaofanya tendo la ndoa mara kwa mara bila kutumia kinga (mapenzi salama) wanakuwa na kiwango kidogo cha msongo wa mawazo na hufanya vizuri katika vipimo vya akili.

Hali hii wamesema wataalam hao kuwa inatokana na manii kuwa na kemikali ambazo humfanya mtu kuwa vizuri kihisia, huongeza upendo/unyenyekevu, huchochea mtu kupata usingizi na huwa na angalau aina tatu za kemikali za kuondoa msongo wa mawazo (anti-depressants).



Utafiti huo uliofanywa kwa kuwahoji wanawake 293 kwa kufuatilia maisha yao ya kujamiana dhidi ya afya za akili zao. Manii huwa na mchanganyiko wa kemikali aina ya cortisol ambayo huongeza upendo, kemikali aina ya esterone na oxytocin ambazo zote humfanya mtu kuwa vizuri  kihisia.



Pia, huwa na homoni aina za ‘thyrotropin releasing hormone’, ambayo huondoa msongo wa mawazo, melatonin ambayo huchochea usingizi na serotonin ambayo ni homoni inayoondoa msongo wa mawazo.



Kutokana kuwapo kwa mchanganyiko wa kemikali na homoni hizo kwenye manii

Matokeo ya utafiti

Matokeo muhimu ya utafiti huu ambao umechapishwa katika jarida la ‘Archives of Sexual Behaviour’ ni kwamba hata baada ya baadhi ya watafitiwa kuongeza kiwango chao cha kujamiana, wale ambao walikuwa hawatumii kinga yoyote walikuwa na kiwango kidogo cha msongo wa mawazo tofauti na wale ambao walikuwa wakitumia kinga kama kondomu wakati wa kujamiana.

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Siku ya Leo

0
0

Rolls Royce Wazindua Gari Lenye Thamani Kubwa Duniani..Linauzwa Bilioni 29 ..Tayari Mteja wa Kwanza Ameweka Oda..!!

0
0

KUENDESHA gari zuri la kifahari ni moja kati ya ndoto za binadamu wengi. Tatizo huja kwenye uwezo wa kununua gari hilo.  Lakini kwa wenye nazo si tatizo, wanapata kilicho bora kwa kutumia fedha zao.

Katika hali isiyo ya kawaida, kampuni maarufu ya kutengeneza magari ya kifahari zaidi duniani ya Rolls Royce, imezindua gari lake dogo aina ya Rolls Rorce Sweptail  linalouzwa Dola za Marekani milioni 13 sawa na Sh bilioni 29 za Kitanzania.  Wataalamu wa magari ya kifahari wanasema gari hilo ndio la gharama kubwa zaidi kuwahi kutengenezwa duniani.


Rolls Royce ni moja kati ya kampuni za kwanza kutengeneza magari ya kifahari na ambayo kipindi cha nyuma na hata mpaka sasa hutumiwa na viongozi wakubwa duniani. Mara baada ya Uhuru, Mwalimu Julius Nyerere alipewa gari aina ya Rolls Royce na Serikali ya Uingereza kwa ajili ya matumizi ya kiserikali. Kwa ambao wamepata nafasi ya kutembelea makumbusho ya taifa yaliyopo jijini Dar es Salaam, bila shaka watakuwa wamepata nafasi ya kuona baadhi ya magari aina ya Rolls Royce yaliyotumiwa na Serikali ya Mwalimu Nyerere

Gari hili jipya ambalo limewaacha midomo wazi watu wengi duniani ikiwamo matajiri wenye ‘pepo la magari ya kifahari’ limetengenezwa baada ya mteja binafsi ambaye hakutaka kutajwa jina lake kusema yupo tayari kulinunua kwa ofa hiyo.

Rolls Royce walikataa kumtaja mteja huyo lakini walisema ni mtu mwenye ukwasi usio na shaka na alikuwa ametoa kazi kwa kampuni nyingine zimtengenezee ndege binafsi na boti ya kifahari kwa muundo ambao utakuwa na mfanano na gari hilo jipya.

“Sweptail ni aina ya gari la kifahari zaidi na gharama kubwa kuwahi kutengenezwa na kampuni yetu. Gari hili limetengenezwa kwa maombi ya mteja binafsi,” anasema Giles Taylor mkurugenzi wa ubunifu wa kampuni ya Rolls Royce Motor Cars.

Timu ya Rolls Royce ilifanya kazi kwa karibu na mteja huyo na kutengeneza gari hilo ambalo linamuonekano kama Rolls Royce ya mwaka 1920 na 1930 ikiwa na sehemu za kuhifadhi vitu vya gharama vya mteja huyo.

Gari hilo lina uwezo wa kubeba watu wawili na sehemu yake ya juu imetengenezwa kwa kioo cha aina yake ambacho kinalifanya kuwa na muonekano wa kipekee.

Kwa kiasi kikubwa Sweptail limetengenezwa kwa matairi ya aluminium na kampuni hiyo imesema hakuna gari jingine walilowahi kutengeneza kwa mfumo huo.

Kwa mujibu wa Rolls Royce Motor Cars, mteja alitaka gari hilo kuwa dogo lakini la kisasa na lenye uwezo wa kubeba abiria wawili tu. Mbao aina ya Macassar Ebony na Paldao ziliunganishwa na ngozi nyeusi na vionjo vingine vya siri kunakshi muundo wa ndani wa gari hilo.

Kuna batani moja kubwa ya kubonyeza ambayo akibonyeza sehemu maalum hufunguka ambapo huweza kuhifadhi briefcase yake. Batani nyingine iliyopo kati kati kufugua sehemu ambayo anaweza kuhifadhi mvinyo wake na ukaendelea kupata ubaridi.

Akiitambulisha gari hiyo nchini Italia, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Rolls Royce Torsten Müller-Ötvös aliielezea Sweptail kama gari la aina yake ambalo linaonyesha ni kwa kiasi gari kampuni yake inavyomjali mteja.

“Sweptail inaeleza kila kitu kuhusu kumjali mteja. Siku zote huwa tunamsililiza mteja na kufanya kadiri ya matakwa yake ili kumfanya awe sehemu ya bidhaa aliyokuwa akiitamani,” anasema

Moja kati ya jambo la kushangaza ni kuwa, magari yote ya Rolls Royce, hutumia ngozi ya ng’ombe dume peke yake kutengenezea siti zake. Sababu ni kuwa  watengenezaji wake huepuka ngozi za ng’ombe jike kwa kuwa zinaweza kuwa na mikwaruzo ambayo mara nyingi hupatikana wakati ng’ombe jike akiwa ana mimba.

Gari moja hutumia ngozi za ng’ombe dume wanane ili kuweza kukamilika. Ng’ombe dume ambao hutumika kutengenezea muundo wa ndani wa Rolls Royce hufugwa sehemu maalumu barani Ulaya ambako hali ya hewa ni baridi kiasi kwamba mbu hawezi kuishi na hivyo kuwafanya kutoa ngozi isyo na mkwaruzo wa aina yoyote.

Mchanga wa Makinikia Haujawaacha Watuhumiwa Waliotajwa Salama...Takururu Wala Sahani Moja Nao

0
0
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Takukuru imesema kuwa inaendelea kuwahoji watuhumiwa wote walitajwa kwenye sakata la kusafirisha Makinikia ya madini nje ya nchi

Ofisa Habari wa  (Takukuru), Mussa Misalaba, amesema kuwa taasisi yao inaendelea na uchunguzi kufuatilia endapo kuna vitendo vya rushwa kwa wote waliohusika na masuala ya usafirishaji wa makinikia.

“Sisi tunaangalia rushwa iliyopo kwenye hiyo biashara kwa kuwa pale kuna wadau wengi… kuna wengine hawahusiki kwenye mikataba na wengine wapo kwenye utekelezaji. Siwezi kusema ni wangapi tumewahoji ama ambao wanatarajiwa kuhojiwa. Kazi yetu inaendelea,” alisema Misalaba.

Hizi Ndizo Adhabu za Watuhumiwa wa Makinikia Wakikutwa na Hatia

0
0
BAADHI ya wanasheria, wabunge waliomo katika kamati inayoshughulikia sheria na katiba na pia wachambuzi wa masuala ya kisheria, walisema kuwa yeyote miongoni mwa wanaochunguzwa sasa na vyombo vya dola anaweza kukumbana na adhabu ya kifungo cha miaka mingi jela au kufilisiwa mali zote alizozipata kwa njia haramu ikiwa mahakama itamkuta na hatia, hasa kutokana na kosa la uhujumu uchumi.

Ilielezwa kuwa miongoni mwa mali ambazo zinaweza kufilisiwa kwa wale watakaothibitika mahakamani kuwa wana hatia ya uhujumu uchumi ni pamoja na nyumba, mashamba, magari, fedha kwenye akaunti zao benki na mali nyinginezo kulingana na vile itakavyoamuliwa na mahakama.

“Kati ya makosa mazito mahakamani ni pamoja na la uhujumu uchumi…anayekutwa na hatia katika kosa hilo hukumbwa na adhabu kali ikiwamo hiyo ya kufilisiwa na pia kuna kufungwa miaka mingi gerezani,” alisema mmoja wa wachambuzi wa masuala ya sheria.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba (Jukata), Deus Kibamba, alisema upo uwezekano kwa watakaokutwa na hatia kukumbana na adhabu nzito mahakamani pindi wakikutwa na hatia.

Hata hivyo, alitahadharisha kuwa wale wote wanaotajwa sasa ni watuhumiwa tu na kwamba, iwapo watabainika wana jinai na rushwa, ndipo majalada yao yatapelekwa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) na kisha kufikishwa mahakamani.

“Uchunguzi utakaowabaini na DPP kuridhika na mashtaka kwamba kuna rushwa ndani yake ndipo jalada hupelekwa mahakamani,” alisema Kibamba.
Alisema kama mhusika anakutwa na kosa la uhujumu uchumi, mwenye kuamua adhabu yake huwa ni mahakama.

“Mwamuzi ni mahakama pekee ambayo inaweza kuamua kwamba mtuhumiwa wa uhujumu uchumi ahukumiwaje… lakini ikibainika kuna hatia, mtu anaweza kufungwa kifungo cha miaka 30, kwa nchi kama Brazili au Venezuela hapo uhujumu uchumi tunasema ni miaka hadi 50 au 60,” alisema Kibamba.

Mkurugenzi wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadam (THRDC), Onesmo Olengurumwa, alisema iwapo watuhumiwa wakibainika walifanya makosa ya kiofisi na ikiwamo waziri kushindwa kusimamia au kuwajibika katika majukumu yake, itakuwa ni makosa ya kiutawala ambayo kwa hivi sasa hayatawahusu waliokuwa nje ya ofisi.

Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anna Henga alisema kutokana na kosa hilo linalowakabili watuhumiwa kuwa kubwa, wakibainika kisheria walihusika kwa namna moja au nyingine wanaweza kuhukumiwa kifungo, ama faini pamoja na mali zao kufilisiwa kulingana na sheria ya jinai ya kiuchumi.

Alisema kosa la jinai lina adhabu tofauti, ikiwamo kifungo au faini na kila kosa lina adhabu zake, ikiwa ni pamoja na kuhudumia jamii kwa kufanya usafi maeneo mbalimbali ya umma au kuripoti mahakamani kila siku.

“Mali inaweza ikarudi kwa umma kwa kuwa si za kwao. Iwapo wakibainika wana hatia, kisheria adhabu inaweza kuwa pamoja na kufilisiwa,” alisema.

Mbunge wa Rufiji (CCM), Mohamed Mchengerwa, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba na Sheria, alisema adhabu ya watu waliotajwa kwenye sakata la mchanga wa madini na kuthibitika kuwa wana hatia itategemeana na vifungu watakavyoshitakiwa navyo, lakini mojawapo ya maamuzi inaweza kuwa ni kufilisiwa mali zao.

Hata hivyo, alisema siyo sahihi kuamini moja kwa moja kuwa kila mmoja atashtakiwa kwa sababu hilo linategemea namna atakavyojieleza.

“Kwa hiyo si lazima mtu afunguliwe mashtaka. Inategemea yeye atakavyojieleza na wakaangalia wakaona kuna kosa,” alisema Mchengerwa.

Alisema kama kuna jambo lilifanywa nje ya sheria kwa ajili ya mtu kujinufaisha yeye mwenyewe, sheria itaangalia ukubwa wa mchango wake katika hasara iliyopatikana halafu ndipo itaangaliwa kama kuna kosa.

“Huwezi mfungulia mashtaka mtu kama huna ‘element’ ya kosa. Kwa mfano, unaweza kusema mtu ameingia mkataba ameisababishia hasara nchi… lakini ameingia mkataba kwa mujibu wa sheria,” alisema na kuongeza kuwa ni lazima kuwapo na viashiria vya kosa ndipo mtu atashtakiwa kwa kosa la jinai.

Aidha, Mchengerwa ambaye kitaaluma ni mwanasheria, alisema katika sakata la makinikia kuna uwezekano mtu akashtakiwa kuwa kwa kosa la kuhujumu uchumi kama alifanya makosa nje ya sheria inavyomtaka na kusababisha hasara.

Alisema kuhujumu uchumi kuna makosa mengi na miongoni mwa adhabu zake ni mhusika kutakiwa alipe mara mbili au mara tatu ya fedha inayotakiwa au kifungo cha miaka 5 au 10.

“Masuala ya uhujumu uchumi mara nyingi huangalia hasara uliyosababisha na kama hiyo fedha hakuna mwisho wa siku mahakama inaweza kuamua,” alisema.

Ripoti iliyowasilishwa na Prof. Osoro ilionyesha baadhi ya viongozi waliokuwa katika awamu mbalimbali za uongozi, walishiriki kulikosesha taifa mapato kutokana na maamuzi yao mbalimbali. Ilielezwa zaidi kuwa nchi inaweza kuwa imepoteza Sh. trilioni 489 katika kodi na mali (madini) tangu mwaka 1998 na kati ya fedha hizo, kiwango cha kodi kilitajwa kuwa Sh. trilioni 108.

Mtanzania Atupwa Jela Uingereza Kwa Kutupia Picha za Marehemu Facebook

0
0

Mwanaume mmoja anayedaiwa kuwa ni Mtanzania amehukumiwa kifungo cha miezi mitatu jela nchini Uingereza kwa kosa la kurusha katika ukurasa wake wa Facebook, picha za mtu aliyefariki dunia kutokana na moto uliounguza jengo la ghorofa la Mnara wa Grenfell lililopo nchini humo.

Pia, mtu huyo ametakiwa kulipa faini ya Sh579,880 kwa mwathirika wa tukio hilo.

 Mtanzania huyo, Omega Mwaikambo (43) alituma video na picha za mwili wa marehemu uliokuwa kwenye begi  na baadaye picha nyingine tano zikionyesha uso wa  marehemu huyo.

Gazeti la mtandaoni la The Telegraph limeandika kuwa Mwaikambo amekiri makosa ya kutuma mara mbili picha zisizopendeza kwa umma katika mitandao ya kijamii mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Westminster jana.

Mwaikambo ambaye anaishi hatua chache kutoka lilipo jengo la Grenfell akifanya shughuli za upishi, alishuhudia jinsi jengo hilo lilivyoungua moto usiku na alikuwa ni miongoni mwa wapishi waliowapikia chai wafanyakazi wa zimamoto walipokuwa wakizima moto huo.

“Lakini juzi Jumatano asubuhi alipoangalia miili hiyo nje ya nyumba yake alichukua picha kwa kutumia simu yake aina ya iPad na kuzipakia kwenye mtandao wake wa Facebook,” liliandika gazeti hilo.

Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Tom Little amesema; “Anaishi karibu zaidi na mnara wa Grenfell, kama ambavyo mahakama inajua janga hilo lilitokea Juni 14.”

Akitoa hukumu, Jaji wa mahakama hiyo, Tanweer Ikram amesema; “Dunia nzima imeshtushwa na yaliyotokea hapa kutokana na janga la moto, ni hali ya kutisha isiyostahimilika, wafu ni lazima waheshimiwe.”

Ameongeza; “Ulichokifanya kupakia hizo picha kwenye Facebook ni dhahiri kuwa hujaonyesha heshima kwa waathirika wa tukio hilo, kuonyesha uso wake  hadharani ni kosa kubwa na halielezeki.”

Mpaka sasa watu zaidi ya 17 wanadaiwa kufariki dunia kutokana na moto uliounguza jengo hilo refu na maarufu Magharibi mwa Uingereza.

I Made My Boyfriend Eat My Menstrual Blood

0
0
I’m Linda 21 years, at the University and I stay with my Boyfriend…… I caught my bf with another girl, when I confronted him he denied it and said they are just friends. I got so angry that night and as I was preparing his supper, something bad came to mind and I felt I should put my blood (Menses blood) into his meal.

So I removed my pad, soaked it with some little water, then squeezed the blood into his food, put some other ingredient and gave him to eat. Now am worried coz he might get some complications or diseases….if he gets any diseases, should I tell him what I did so that he can go for medical checkup or I shud just remain quiet?? Am afraid coz he might beat me up to coma!

Advice me on what to do please!

Upo Tayari Kulipwa Sh10 Milioni Kuambukizwa Kikohozi?

0
0

Upo Tayari Kulipwa Sh10 Milioni Kuambukizwa Kikohozi?
Je ni fedha kiasi gani zinaweza kukushawishi kukubali kuambukizwa kikohozi ili kusaidia uvumbuzi wa kisayansi?

Watafiti wa Chuo Kikuu cha Southampton wamesema watampa pauni 3,526 (sawa na Sh10.3 milioni)  mtu yeyote atakayejitokeza ili kukubali changamoto hiyo.

Lengo lao kubwa ni ili kutengeza chanjo bora ili kuwalinda watoto na watu wazima ambao wapo hatarini kuambukizwa ugonjwa huo.

Ili kusaidia ni sharti mtu awe na umri wa kati ya miaka 18-45, awe na afya bora, awe tayari kutengwa kwa siku 17 na kuimba.

Kikohozi ni ugonjwa unaoweza kuambukizwa kwa haraka na huenezwa kupitia hewa ya kikohozi kutoka kwa mtu ambaye ameambukizwa.

Kundi hilo la watafiti wa Chuo Kikuu cha Southampton linataka kuwaambukiza watu walio na afya nzuri kwa kuwawekea puani viini vinavyosababisha maambukizi hayo na kuwachunguza.

 Baadhi ya watu waliojitolea watakuwa wagonjwa, lakini wanasayansi wanawataka wale ambao hawatakuwa na dalili zozote licha ya kuwekewa viini hivyo katika pua zao.

Hatu hii inalenga kujua wale wenye kinga ya asili ya ugonjwa huo.

 Vilevile, wapo wanaobeba ugonjwa huo kwa siri na huwaambukiza watu wengine, lakini huwa hawaambukizwi.

Mwananchi

Rapper Rosa Ree Aanza Tambo....Adai Msimfananisha na Kina.......

0
0
Rapper Rosa Ree Aanza Tambo....Adai Msimfananisha na Kina.......
BAADA ya kutoka kimuziki, msanii wa Hip Hop anayekimbiza na Ngoma ya Up In The Air, Rosary Robert ‘Rosa Ree’ ameanza tambo kwa kusema kuwa hakuna rapa yeyote wa kike anayeweza kufanana au kufananishwa naye hapa Bongo.


Akichonga na Mikito Nusunusu, Rosa Ree ambaye yupo chini ya Lebo ya The Industry inayosimamiwa na Navy Kenzo alisema, kila mwanamuziki ana tofauti yake na hata wanaokuwa wanamfananisha na baadhi ya wasanii wanakuwa wanakosea sana.

“Kuna watu huwa wananifananisha na baadhi ya wasanii wa kike hapa Bongo wanaofanya muziki wa kurap, lakini ukweli ni kwamba nipo tofauti na hao wanaonifananisha nao ambao naona hata kuwataja hapa ni kuwapa kiki kirahisi, kitu ambacho siwezi kufanya kwani hawawezi kufanana nami,” alisema Rosa Ree.


GPL

Nimerekodiwa Video ya Ngono Bila Kujijua. Nifanyeje?

0
0
Wadau natumaini mu wazima Mi ni mjasiriamali toka Arusha but huwa nakuja Dar kwa ajili ya kuchukua bidhaa, nikiwa Dar napenda kujibururdisha ama MEEDA au KONA BAA/AMBIANCE AFRIKA SANA huwa nikipata demu wa kupiga nampelekaga Guest/hotel niliyofikia tunafurahia "game" asb namlipa chake anatambaa.

Sasa katika kuingia guest kadhaa za hapa Dar nimegundua hawa jamaa wa guest wanaweka SECURITY CAMERAS kuanzia kwenye parking, kwenye korido, karibu na milango, vyumbani hadi bafuni. Je, ni haki kuweka security camera hadi vyumbani/bafuni?

    Jana nikiwa kwenye foleni Magomeni Mapipa dogo mmoja akaja na DVD kibao za dini, chini yake ameweka DVD ya X ina picha ya WEMA nikainunua ile kufika hotelini nikaweka kwenye laptop najiona mimi na demu niliyemchukua wk 2 zilizopita.

    Hakika nilichoka, sijui cha kufanya nishaurini wadau.

By lex

Zari Mambo Ya Mitandao Waachie Mabinti

0
0
NIANZE kwa kumpa pole sana mama wa watoto watano, Zarinah Hassan ‘The Bossy Lady’ ambaye wiki chache zilizopita, alipata msiba mkubwa baada ya kufiwa na baba wa watoto wake watatu wakubwa, Ivan ‘Don’ Ssemwanga. Kwa namna yoyote, ule ni msiba mkubwa mno, hasa unapomkuta mwanamke, kwani inaonyesha wanaume, licha ya nao kuwa na moyo wenye damu unaoonja maumivu, angalau ni wavumilivu kidogo, wanaweza kujikaza na kusahau ndani ya muda mfupi.

Zari, licha ya kuwa ni shemeji yetu, lakini pia ni mtu ambaye anaonyesha jinsi gani mwanamke anapaswa kuwa mtafutaji badala ya kumtegemea mwanaume kama dada zetu wengi walivyo. Ni mbunifu katika mipango ya kupata mkwanja, tena ule wa maana. Ameonyesha hivyo mara nyingi, kwani kwa muda mchache ambao amekuwa ‘mtu wetu’, amejidhihirisha kuwa ni wa tofauti na mastaa wetu ambao ujanja wao mwingi unategemea pochi za wanaume.
Kuna ile Zari White Party, ni moja ya matukio machache kubuniwa na mdada huyo na kufanikiwa, likifanyika pale Mlimani City, miaka michache iliyopita. Anajiamini, anajua anachofanya na kizuri zaidi, anajua kutumia fursa. Unapozungumzia juu ya wanawake jasiri ambao ungependa binti yako aige, huyu ni miongoni mwa mifano hai, maana ni watoto wachache wa kike ambao wanaweza kuingia ‘front’ kusaka mkwanja sawa na wanaume! Lakini kuna jambo ambalo dada yangu huyu amelifanya, ambalo kidogo naona haliko sawa.

Pamoja na msiba mzito ambao ameupata kwa mumewe wa zamani, Zari amefanya vitendo ambavyo haviendani na utamaduni wa kiasili wa wabantu, bila kujali ni wa nchi gani. Kwa kawaida, mtu anapopatwa na msiba mzito, kama wa kufiwa na mume, tena mzazi mwenzio wa watoto watatu, unapaswa, angalau kwa muda, kuonyesha majonzi, siyo tu kwa sura, bali hata matendo.
Lakini Zari, baada ya mzazi mwenzake kuzikwa, siku mbili baadaye, akaja kwenye mitandao ya kijamii, akatupia video iliyomuonyesha anacheza kwa furaha kana kwamba alikuwa ametoka shughulini. Ni kweli kwamba kwa muda wote wa kuhani msiba huwezi kuwa na sura ya majonzi, kuna wakati mfiwa anaweza kujikuta akicheka, kutegemea na kinachotokea, lakini siyo kukata mauno halafu bila hata kufikiri, unatupia mtandaoni!

Acha hiyo, lakini kitu kingine ambacho hakiko sawa, ni kitendo chake cha kuondoka eneo la msiba, jijini Kampala kwa haraka mara tu baada ya mazishi hayo, kitu ambacho kibantu pia siyo sawa. Mama wa Kiafrika umefiwa na baba wa watoto wako, tena watatu, uko msibani unaondokaje mapema? Labda tungeweza kusema kukaa hapo kutakufanya ugharamie zaidi, lakini si kwa mtu mwenye fedha zake kama alivyokuwa Ivan.

Ni wazi kuwa hakuwa sawa na watu wa ukoo wa mumewe, kitu ambacho pia ni tatizo. Angalau angebakia Kampala hadi ile sisi tunasema 40 ifike, ndipo aondoke. Lakini kama hiyo haitoshi, ndani ya siku 15 tu, tangu amzike mwenzake, tayari ameshaanza kujirusha kwa kuonyesha picha akiwa swimming pool na mwanaume, khaa! Hii haikai sawa, hasa kwa binti ambaye wengi tulimchukulia kama mfano.

Inapotokea hivi, ni rahisi kujenga hisia kuwa mtu huyu hana majonzi, kwa sababu mtu uliyefiwa na mwenza wako, unawezaje kupata faraja kiasi hiki ndani ya muda mfupi? Kuna taabu gani kusubiri siku 40 zipite halafu maisha mengine yaendelee kama kawaida? Zari ni kama mfano tu, lakini wako wadada wengi pia hata hapa Bongo ambao hukosa utu baada ya waume zao kutangulia mbele ya haki. Kama mtu hana hofu kwa mzazi mwenziwe, vipi rafiki, ndugu na jamaa? Kuna haja ya Zari kujitazama upya kwa sababu vitendo ndivyo vinavyotafsiri tabia ya mtu!


GPL

Jisajili Uweze Kushinda Gari la Bure Mwisho Terehe 20 Mwezi Huu

0
0
Umeshawahi Kufikiria Kupata Gari la Bure bila Kulipa Chochote... Basi hii Kampuni ya Cars From Japan Wanakupa Nafasi Hiyo ...

CHAKUFANYA NI Fuata Maelekezo hapa chini Jinsi ya Kuweza Kuwa Mshindi wa Gari hilo..

Bonyeza Hapa >>> SHINDA GARI YA BURE <<< Kujisajili ni Bure tu...

Kisha Jisajili kwa Kuweka Jina na Email Yako

Siri ya Rayvanny na Jason Derulo yafichuka

0
0
Rayvanny ameonekana kuanza kutumia fursa vizuri baada ya kukutana na Jason Derulo nchini Kenya kwenye Coke Studio.

 Msanii huyo wa WCB alionekana akiwa karibu zaidi na Jason kwenye ukumbi wa hoteli ya Stanley iliyopo mjini Nairobi huku wakibadilishana namba na kufanya maongezi kwa muda mrefu.


Akiongea na Mzazi Willy Tuva kutoka Mseto FM ya Kenya, Ray amethibitisha kwamba alichangamkia fursa hiyo adimu iliyotokea mbele yake na kujadili na msanii huyo wa Marekani masuala muhimu yanayohusu muziki wake.

Hitmaker huyo wa ‘Mbeleko’ ameongeza kwa kusema, amepewa mualiko maalum na Derulo wa kurekodi nyimbo katika studio za nyumbani kwake na huenda wakafanya kazi ya pamoja na staa huyo wa RnB ambaye alionesha kumkubali Rayvanny.

Imeandikwa na: Teddy Agwa
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images