Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

‎'Help, I Want To Cheat On My Husband'

$
0
0
I am so confused and didn't know where else to go with such a tough decision! I will just give you the main details and maybe you could help me out.

I have been married for almost 2 years to a perfect husband. I trust him with all my heart. He does almost everything a wife wants. We do have some difference in some areas in our marriage but other than that all is perfect. My husband and I also share 3 children together.

My husband has a good friend I will call 'Jim'. I have known Jim ever since I met my husband. About 2 years ago I started feeling an attraction towards him but never revealed it to anybody. Some time ago, we were all out together and Jim and I both had too much to drink and began to discuss this mutual attraction. After that night nothing more was ever really said.

Last weekend, we were all hanging out again and Jim and I started talking about our feelings again. Saying that maybe we should just sleep together and then maybe the whole thing would go away since we will know what it would be like, (to make matters worse, he is also married with children). We continued to joke about this throughout the night.

Yesterday he stopped by to see my husband but he wasn't here so we started talking. We discussed how if nobody knows, then nobody can get hurt. We also discussed consequences and many other things. I know it would be immoral for me to cheat on my husband, but what do I do with these feelings?

I am not a bad person, I have never been a cheater! We made plans for a 'date' today while my husband is with his family. The more I have been running this through my head the more I realize how much is at stake.

Should I do it once and then maybe that will kill the curiosity? Or just tell Jim that we just can't do it?

I guess I know what I SHOULD do, but honestly tell me what you would do in this situation.

Je Wewe ni Mwanaume? Je Unatamani Mwanamke Akupende na Kukusifia

$
0
0
Je wewe ni Mwanaume???
Je unatamani Mwanamke akupende na kukusifia kwamba Ur the Man na wewe ni Husband Material??
Its easy...Kuwa tu mjinga!Huwezi kumsatisfy Mwanamke kama wewe sio mjinga!
Akisema usiangalie Mpira wa Man U na Arsenal anataka muende muvi ya Die Hard we kubali tu...
Akisema amekumiss uende home hata kama una party na washkaji mnahave Fun we jifanye mbwiga nenda,shes lonely na anakutaka wewe...
Akiomba hela ya Shopping Laki1 we mpe tu hata kama viatu vyako ulinunua buku 20 tena kwa kugombana na Machinga hadi ukamwaga mate kama Mvua..
Wanawake wana endless needs..Zingine zinaboa na kukera jazz band,ila huna jinsi,if you really want to satisfy her,You must be a fool...Akikuamsha amekumiss sa9 usiku amka umbusu,ukijifanya kukoroma kimenuka...Hao ndo Wanawake...Hii ndio Yangaaaaaaa!!
Message from:
Seth De Jesus Giovanni

Umaskini Wote Unaanzia Hapa

$
0
0
Kuna wakati umekuwa ukujiuliza sana kwa nini wewe ni maskini na kwa nini wengine ni matajiri, labda nikwambie tu hivi, usiendelee kujiuliza swali kama hili ngoja tu ni kupe jibu la moja kwamba, umaskini au utajiri unaanzia kwenye akili yako.

Kile unachokifikiria sana kwa muda mrefu bila kujali unafikiria umaskini au utajiri hicho ndicho utakachokipata. Hauzuiliwi kufikiria na kutenda kitajiri hata kama pato lako ni dogo au hata kama unajiona ni maskini, lakini tambua chanzo cha umaskini au utajiri ni akili yako.

Kwa hiyo kwa mfano unajiona umepigika, huna pesa mfukoni na umejikuta umekuwa ni mtu wa kukopa huku mara kule, hiyo ni dalili tosha kwamba pia  ni matokeo ya akili yako iliyopigika ama akili ya kimaskini ambayo umewekeza kwa muda mrefu.

Kama upo katika hali hii, haina haja ya kujichukia au kujiona hovyo hovyo kubali kujirekebisha na kuchukua hatua zitakazokuwezesha kusonga mbele kimafanikio. Ukiwa mbishi, nikupe uhakika huu utaendelea kuteseka na umaskini.

Kwa hiyo unatakiwa uangalie na kujua kwamba kinachokufanya uendelee kuwa maskini sio kwa sababu huna pesa au huna mtaji, bali ni kwa sababu ya matokeo ya mfumo wa mawazo yako ulionao na umeujenga kwa muda mrefu.

Dawa pekee ya kuweza kukata mizizi ya umaskini ni kwa wewe kuamua kubadili mfumo wa mawazo ambayo unayo ya kimaskni na kujenga mfumo mzuri chanya utakao kuwezesha kukusaidia kufanikiwa.

Chanzo cha utajiri na umaskini wowote ule ni matokeo ya mawazo yako. Matokeo ya mawazo yako yanakuja na kile unachojifunza na kukiweka mara kwa mara akilini mwako,

hicho ndicho kinachoonekana kwa nje.

Ni wapi unatakiwa kuanzia ile ufutilie mbali historia ya umaskini?
1. Jifunze kila siku kuhusu mafanikio kwa kutafuta kanuni na mbinu mbalimbali zitakazokuwezesha kufanikiwa kupitia vitabu au semina.

2. Kaa na watu wenye mafanikio kwa pamoja. Jifunze kwao. Acha kung’ang’ania kuwa na watu ambao hata wewe hawana uwezo wa kukusaidia chochote.

Njia sahihi ya kukufanya wewe ukafanikiwa na kuwa na mawazo sahihi. Yatafute mawazo hayo sahihi kila siku ya maisha yako na uwe miongoni mwa watu wenye mafaniko makubwa.

Tulifanya S*x For Fun Sasa Anataka Kujenga Kibanda.

$
0
0
Hi Wadau
Kunua msichana tulikutana nikampiga sound kikaeleweka, km miezi 8 hivi iliyopita.
Tumegegedana kwa mda mie nikijua tunapunguziana stress.

Sasa hiv nataka nitulie nioe ( mchumba nimeshampata)
mie nataka nikate kamba ili nianze maisha mapya na huyu mpenzi wangu.

Imekuwa shida mi nilikuwa najitoa kisailensa, km kuacha kumtumia sms, kupunguza kupiga sim, kupunguza kutoa huduma (financial) tangia mwaka huu uanze sijamgegeda ila naona kama haelewi, bado anangangania.

Nimekuwa natumia ubinadamu kwa kutomwambia kavukavu kuwa nataka kuoa so tuachane, nikimwonea huruma kuwa ataumia sana, coz yy anaona km vile amefika wakati hatukuwa na huo mkakati wakati tunaanza.

Kwa wale wataalam wa hizi issue huwa mna-solve namna gani bila kuacha uadui kati yenu?


By Godbless

TANZIA:Mke Mdogo wa Mzee YUSUPH Afariki Dunia Akijifungua...

$
0
0
Innalillah wainaillah rajuun mke mdogo wa Mzee Yusufu Chiku amefariki dunia usiku huu alipokuwa akijifungua na mtoto amefariki taarifa zaidi tutaendelea kupeana!!

Chiku amekutwa na mauti jana Jumamosi June 17,2017 jioni katika hospitali ya Amana, Ilala ya jijini Dar es Salaam alipopelekwa kujifungua.

Mzee Yussuf amesema alimpeleka mkewe Hospitalini hapo June 17,2017 saa 10 alasiri kwa ajili ya kujifungua na kwa bahati mbaya alikutwa na mauti hayo baada ya upasuaji uliofanywa kutokwenda salama hivyo kusababisha kumpoteza mkewe na mtoto aliyezaliwa.

MADHARA ya Kiafya ya Kuvaa NGUO za Kupana Mwili.....

$
0
0
Na Carolyne B Atangaza.

Kwa msaada wa viguo vya kubana na vivazi vyote vinavyochonga shepu ya mwili, wengi mchana huonekana na maumbile mazuri yanayovutia kuangalia na usiku wanarudi kwenye miili yao iliyotepweta baada ya kuzivua nguo zao.

Hatuoni tabu yoyote hata kujipaka mafuta ikibidi mradi tuweke kuingia kwenye jinzi za kubana au hata kuvaa ‘skini taiti’ mbili, vyovyote iwavyo ili mradi tuonekane wembamba kuliko tulivyo, tuonekane wazuri na wenye mvuto kuliko tulivyo na nyakati nyingine kwakuwa tunataka tuonekane vijana kuliko tulivyo.

Kama unaihusudu sana jinzi yako ya kubana, bila shaka ushawahi kupata tatizo la mwili kupatwa na ganzi kuanzia mapajani na kupoteza hisia kabisa kwenye mguu mzima mpaka chini. Madaktari wanaiita hali hii kwa jina la kitaalamu la meralgia paresthetica ambayo hutokea kwa sababu ya kukandamiza kwa muda mrefu mishipa ya neva za fahamu inayotoka kwenye kiunoni ambayo kazi yake ni kuleta hisia kwenye mapaja.

Mwili wa binadamu unatoa ishara fulani kama nguo au mapambo fulani tuliyovaa yanabana sana hata kama tukijidai kudharau tunayoyaona kwa macho yetu kupitia kioo ukiwa unajikagua kama umependeza ama la. Yafuatayo ni baadhi tu ya madhara ya kiafya unayoweza kuyapata kutokana na kuvaa nguo zinazobana mwili:

Ugumba

Dkt. George Bwesigye, daktari katika hospitali ya Najeera anatoa maelezo ambayo yanaweza kuwatisha wanaume wengi. “Kokwa zinazotengeneza mbegu za kiume zinatakiwa ziwe kwenye joto la chini tofauti na joto la mwili, ndio sababu zikawa nje ya mwili. Kwa hali hii, zinakuwa na uwezo wa kuzalisha mbegu za kiume kwa wingi. Kwahiyo, kuzibana na nguo kunazuia au kupunguza kwa kiasi kikubwa kazi yake hii ya msingi na huweza kusababisha ugumba.”

Maambukizi

Anasema kuwa chupi zinazobana husababisha joto linaloleta unyevu kwenye eneo hilo nyeti. Unyevu katika sehemu hiyo husababisha vjidudu vya fangasi kwa wanaume au utandu wa vijidudu unaosababisha muwasho na maambukizi kwa wanawake.

Mzunguko mdogo wa damu

Nguo za kubana zinazuia mzunguko unaotakiwa wa damu, ikizuia mzunguko wake wa kawaida wa kupeleka damu na kuirudisha kwenye moyo kwa ajili ya kutumika tena mwilini.

Hili linaleta maumivu, uvimbe au kuvimba/kupinda kwa mishipa ya damu ya miguu kutokana na presha kubwa inayopelekwa sehemu ya chini ya mwili. Kama una tatizo la kuwa na mafuta mengi mwilini, kuvaa nguo za kubana kunaliongeza tatizo hilo kwakuwa mzunguko wako wa damu utaathirika zaidi.

Matatizo ya mmeng’enyo wa chakula

Bwesigye anaendelea kueleza kuwa suruali na mikanda ambavyo vinabana sana tumbo vinakuwa vinalizuia tumbo kutanuka jambo ambalo ni la muhimu sana kwa ajili ya usagaji wa chakula ulichokula.

“Kwakuwa mfumo wa usagaji chakula haufanyi kazi sawa sawa, mtu atajikuta anapata viungulia na kujaa kwa kemikali tumboni, na matatizo mengine mengi,” amesema.

Maambukizo ya njia ya mkojo (UTI)

Mbunifu wa mavazi kwa watu mashuhuri, Solomon Tazibone amesema kuwa wanawake wanaovaa nguo za kubana mara nyingi sana hukwepa kutumia vyoo vya kadamnasi, ambavyo vinahatarisha wanawake wengi sana kupata maambukizi ya njia ya mkojo.

“Si rahisi kutua nguo zilizokubana sana hasa kwenye vyoo vinavyotumiwa na watu wengi. Kwahiyo wanawake wengi hujikuta wakizuia haja ndogo kwa saa kadhaa wakisubiri kwenda sehemu walizozizoea na salama kwao kama majumbani mwao,” anasema.

“Tatizo kubwa zaidi ni pale nguo hizi zinapovaliwa na mabinti wadogo. Tunaweza tukabisha lakini hali halisi ni kwamba wanaume wanapenda kuona vitu vinavyowavutia na hawatasita kumuita mtoto wa miaka 11 aliyevaa kaptura au hata kumuangalia kwa matamanio.

Kama wazazi ni jukumu lenu kuwalinda watoto wenu hata kama utaitwa mshamba au mkoloni.

KUMEKUCHA TFF: Haya Hapa Majina ya Waliopitishwa Kugombea Urais wa TFF

$
0
0
Ifuatayo ni orodha kamili ya Wagombea wanaowania nafasi mbalimbali za uongozi TFF katika Uchaguzi Mkuu ujao utakaofanyika Agosti 12, mwaka huu mkoani Dodoma.

Wanafamilia hao ni wale waliojitokeza jana Ijumaa na leo Jumamosi katika ofisi za TTF, Karume jijini Dar es Salaam.

URAIS
Jamal Malinzi
Imani Madega
Wallace Karia
Fredrick Masolwa

MAKAMU RAIS
Mulamu Nghambi
Michael Wambura
Geofrey Nyange

WAJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI
Soloum Chama
Ephraim Majinge
Elias Mwanjala
Saleh Alawi
Kaliro Samson
Vedastus Lufano
Kenneth Pesambili
Mbasha Matutu
Samwel Daniel
Dunstan Mkundi
Athuman Kambi
Shaffi Dauda
Golden Sanga
Charles Mwakambaya
Benista Rugola.
Thabit Kandoro
Goodluck moshi
James Mhagama
Husen Mwamba
Sarah Chao
Isaa bukuku
Stewat Masima
Emmanuel Ashery
Abdul Sauko
Musa Sima
Stanslaus Nyongo
Ayoub Nyenzi
John Kadutu
Baraka Mazengo
Khalid Mohamed
Mohamed Aden
Cyprian Kuyava
Saleh Abdul

 IMETOLEWA NA:
Alfred Lucas
Ofisa Habari TFF

KIMENUKA:Video ya Polisi Wakiwapiga Walemavu DAR Yawakera Wengi...Itazame Hapa

$
0
0

Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam jana lililazimika kutumia mabomu ya machozi kukabiliana na kundi la walemavu wa viungo waliokuwa wamefunga barabara ya Sokoine wakishinikiza kuonana na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala.

Mabomu hayo hayakusababisha wakati mgumu kwa walemavu hao waliokuwa wamefunga njia tu bali hata kwa watumiaji wengine wa barabara hiyo.

Walemavu hao walitaka kuonana na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala kumueleza kero wanayokumbana nayo ya kukamatwa na Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni alisema kuwa walilazimika kutumia mabomu hayo kama njia ya kuwatawanya na kuwa hadi sasa wanawashikilia watu 40  kwa kosa la kufanya mkusanyiko kinyume na sheria.

Alisema kuwa walilazimika kutumia njia hiyo ya mabomu baada ya watu hao kupewa amri mara tatu ya kutawanyika na kukaidi. Hivyo akasema utumiaji wa mabomu hayo ulifanyika ili kurahisisha ukamataji wa wananchi hao waliokaidi amri ya Polisi.

Aidha, licha ya kiongozi huyo kusema hivyo, watu mbalimbali kikiwemo na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimelaani nguvu iliyotumiwa na polisi katika zoezi hilo na kusema ni nguvu kubwa ambayo haikuhitajika kukabiliana na walemavu ambao hawawezi kupambana na Polisi.

Wengi waliotoa maoni yao kuhusu video hii kwenye  mitandao ya kijamii wamemtaka Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba kuwachukulia hatua Polisi hao wanaoonekana wakiwapiga walemavu hao na kuwaingiza kwenye magari ya Polisi kwa kutumia nguvu kubwa.

ITAZAME HAPA CHINI:



Zimebaki Siku 2 Tu Jisajili Ushinde Gari La Bure, Shindano Hili Ni La Kweli Usipuuzie

$
0
0
Umeshawahi Kufikiria Kupata Gari la Bure bila Kulipa Chochote... Basi hii Kampuni ya Cars From Japan Wanakupa Nafasi Hiyo ...

CHAKUFANYA NI Fuata Maelekezo hapa chini Jinsi ya Kuweza Kuwa Mshindi wa Gari hilo..

Bonyeza Hapa >>> SHINDA GARI YA BURE <<< Kujisajili ni Bure tu...

Kisha Jisajili kwa Kuweka Jina na Email Yako

GOOD NEWS Kutoka Marekani Walipolazwa Watoto Waliopata Ajali Arusha

$
0
0
Watoto watatu walionusurika katika ajali iliyoua wanafunzi 32, walimu wawili na dereva wa Shule ya Lucky Vincent ya mjini Arusha, huenda wakaruhusiwa kurejea nchini baada ya miezi miwili.

Taarifa hiyo imetolewa na Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu katika mtandao wake wa kijamii wa Facebook.

Pia, Nyalandu ameandika katika mtandao huo kuwa watoto hao; Doreen Mshanga, Saidia Ismael na Wilson Tarimo wanategemewa kutembea tena.

Hata hivyo, kwa sasa Doreen, atahamishiwa katika kituo maalumu kwa ajili ya matibabu ya uti wa mgongo cha Madonna katika mji wa Lincoln, Nebraska.

“Katika watoto wote hao watatu, Doreen ni muujiza mkubwa zaidi,” amesema Nyalandu.

PENDEZA na Markson Beauty, Ongeza Hips, Makalio, Kuwa Mweupe na Softi Kwa Kutumia Bidhaa Zetu

$
0
0
PENDEZA NA MARKSON BEAUTY. ONGEZA HIPS NA MAKALIO, KUWA MWEUPE NA SOFTI, ONGEZA MAUMBILE YA KIUME, NGUVU NA HAMU YA TENDO N.K @Markson_beauty_pr Tunakuletea bidhaa bora zenye matokeo ya uhakika na haraka zisizo na kemikali wala madhara. Zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kudhibitishwa kiafya. NB. Matokeo ni uhakika na garantii.

🍉🌿🍅🍍🍒🍉🍓🍅🍒 BIDHAA ZETU:- 1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @120000@120,000/=
2. Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa:-
(a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200000@200,000/=
(b)Vidonge @180000@180,000/=
(c)BOTCHO 10× ya kupaka @ 150,000/=
3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @120000@120,000/=
(11)Vidonge @150000@150,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150000@150,000/=
5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-
(a) Gely ya kupaka @130000@130,000/= (b) Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu hata kwa wenye kisukari @130000@130,000/= (C)Handsome up original @200000@200,000/=
6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @130000@130,000/=
7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula @120000@120,000/=
8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a) Dawa ya kunywa au kupaka @120000@120,000/= (b) Mkanda wa kawaida @100000@100,000/= (c) micro-computer belt wa umeme @170000@170,000/=
9 .Kupunguza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120000@120,000/=
10.Kushepu miguu (CHUPA YA BIA) na kuondoa vigimbi @130000@130,000/=
11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @120000@120,000/=
12.Kurudisha usichana (bikra) @120000@120,000/=

Wasiliana nasi :- (+255) 0767447444 au. 0714335378

TAHADHARI: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako. 👉🏻Ili kuona bidhaa zaidi na shuhuda za waliotumia bidhaa zetu. ...............

BANK ya Dunia Imetaja Nchi Zilizokua Haraka Kiuchumi 2017, Tanzania Je?

$
0
0
Bank ya Dunia (WB) wametoa list ya nchi ambazo zinakuwa haraka kiuchumi mwaka 2017 huku nchi za Afrika na Asia zikionekana kushika kasi katika kukuza uchumi wake kutokana na kukua kwa biashara na miundombinu.

Katika list hii Ethiopia inakamata nafasi ya kwanza ambapo uchumi wake umekua kwa 8.3% huku Tanzania ikitajwa miongoni mwa nchi 10 ikikamata nafasi ya 5 uchumi wake ukikua kwa 7.2% huku uchumi wa Djibouti ukikua kwa 7% licha ya kukabiliwa na ukame mkubwa.


HATIMAYE Beyonce Ajifungua Watoto Mapacha

$
0
0
Ni nyakati za furaha kwa wapenzi/wanandoa Beyonce na J-Z baada ya kuwakaribisha mapacha wao wachanga kabisa mwishoni mwa wiki hii. Gazeti la US Weekly liliripoti.

Kulikuwa na siku za mijadala katika mitandao ya kijamii kuhusu kujfungua kwa mwanamuziki nguli mwenye miaka 35 katika kituo kimoja cha afya huko Los Angeles nchini marekani. Mdogo wa mwanamziki huyo, Solange Knowles alionekana akirandaranda kwenye kituo hicho cha afya, ndipo mapaparazi walipojisogeza ili kufahamu undani wa jambo hili.

Mwanzoni mwa mwaka huu mwanadada huyu alipiga picha mbele ya ua kubwa huku kashikilia tumbo lake na kupost kwenye ukurasa wake wa instagram kwamba wamebarikiwa kwa kutarajia kuleta zawadi nyingine.

Supastar wa miondoko ya Hip Hop Jay Z, mwenye miaka 47 Jumanne iliyopita alionekana akiondoka kwenye kasri lao lililopo Beverly Hills na kuelekea kwenye kituo hicho cha afya na mara ulinzi katika kituo hicho uliimarishwa.

 
Mapacha hawa wanaungana na Blue Ivy, binti wa wapenzi hawa mwenye umri wa miaka mitano.

HAKUNA Kama Rais Magufuli Afrika Nzima....Soma Magazeti ya Leo Jumapili

ALINISALITI, Nilichomfanyia Hatokaa Anisahau Daima

$
0
0
 Jumamosi iliyopita nikiwa katika matembezi ya hapa na pale katika fukwe moja hapa jijini,nimekaa na co worker napata juice ya baridi huku yeye akiisindikiza siku na castle light.wanaingia wanawake wawili mmoja mnene sana kimaumbile.wanaketi meza jirani kidogo na tulipo sisi,Ghafla nakosa amani,mapigo ya moyo yanaongezeka.. Nakua nawatazama sana hawa wanawake,ila wao naona hawa ja pay attention kwetu hivyo hawajatuona..baada ya muda huyu co worker ananiuliza kama kuna tatizo,najishtukia kidogo najikaza namwambia hamna tatizo lolote.ila kiukweli macho na akili yote imehamia kwa huyu mwanamke mnene,kila nikimtizama nahisi kumfahamu licha ya kutoonana nae kwa muda mrefu sana, ni jioni tulivu,anakuja muhudumu wanatoa oda,baada ya muda mhudumu anarudi na Smirnoff (vodka) club soda,glass mbili na vipande vya limao. Wanafungua wanaanza kunywa taratibu, muda unaenda nakosa uvumilivu namfuata huyu mwanamke, nafika walipokaa namshika begani,


"Habari yako???"
Ghafla anashtuka sana,Ananiangalia kwa muda kisha anainuka na kunikumbatia humu akitaja jina langu. Ananiachia na kunitizama tena kwa Mara nyingine,kisha anaanza kuniuliza
"Za masiku? Upo kweli? Mbona unazidi kua kijana?unafanya sana mazoezi eh?nimekutafuta sana mbona, blah blah blah + maswali mengi yasiyo na mwisho.
Mara ya mwisho namuona alikua binti mwenye umbo lililojengeka ipasavyo,nashindwa kuvumilia namuuliza " ndugu huu unene ni wa uzazi nini???anacheka anajibu hapana ni maisha tu.anaangalia mezani kwetu na kuhoji kulikoni mbona unakunywa juice unatumia dawa nini??natabasamu namwambia nipo kwenye dozi kweli(japokua si kweli)Tunaongea mawili matatu narudi mezani kwangu huku tukiwa tumeahidiana tutaongea zaidi maana bado tupo sana.


Huyu mwanamke ni nani????

August 2008, nafamiana na huyu msichana mrembo,baada ya urafiki wa muda tunaanza mahusiano ya kimapenzi. Mimi nafanya kazi katika shirika la kiserikali yeye akiwa mwaka wa pili chuo, baada ya muda mapenzi yananawiri sana ikafika hatua nikawa nimemtambulisha kwa baadhi ya ndugu jamaa na marafiki,katika kipindi cha mwaka na nusu hivi mpaka ilipofikia hatua anahitimu chuo kwa kweli kwangu alikua 'perfect woman'. Akaniteka haswa nikasahau habari za wanawake wengine kabisa, anahitimu chuo natumia influence yangu namtafutia kazi kwenye kampuni flani hapa hapa jijini, anaanza kazi na tunaanza kuishi wote.(japo kwao aliwaambia kua anaishi kwa rafiki wake wa kike)...muda unaenda huku mapenzi yakishamiri, asubuhi nampeleka kazini na mimi naenda ofisini,akitoka anakuja kunisubiri(ye anawahi kutoka) tunarudi wote nyumbani.


Baada ya mwaka tunaanza process za ndoa,hakutaka kuzaa kabla hatujaoana. Utaratibu wa kutambulishana unafanyika,ndoa inapangwa baada ya miezi nane kutokana na majukumu ya kikazi,kila mmoja ana furaha moyoni mwake. Nampa full power kwenye baadhi ya miradi yangu asimamie yeye..simfatilii huko kwenye hio miradi wala kuhoji financial status zaidi ya kumwambia awe makini maana nataraji kuanza ujenzi mwingine inaweza kufika mahali nikahitaji msaada wake..namuonea huruma anavyotoka kazini mapema na kuja kunisubiri mimi kila siku ya kazi, namfundisha kuendesha gari,anapata kauzoefu hatimaye siku yake ya kuzaliwa namfanyia surprise namnunulia gari.. Mipango ya harusi inaendelea pande zote mbili


Usaliti unaanza
Nikiwa sijui hili wa lile akaanzisha tabia mpya ya kuchelewa kurudi nyumbani, nikawa natoka kazini nampigia hapokei(hili halikunipa shida sana maana alikua si mzoefu sana barabarani hivyo akiwa anaendesha hapokei simu) nafika nyumbani simkuti,akirudi kila siku sababu mpya, muda si muda akaanza tabia anaondoka na gari asubuhi akirudi jioni anakuja kachelewa na gari haji nalo,analiacha kazini,sababu anazotoa yani nilikua hata sijielewi,Mara naona uvivu kuendesha,jioni sioni vizuri blah blah blah, alikua na mdogo wake kaanza 1st year udsm pale akamfanya kama cover story yake, kila akichelewa anadai alikua nae anampa company.simu zangu akawa mgumu sana kupokea,akabadilika ghafla. Kuna siku kachelewa kurudi,nimekaa sebleni nakunywa whisky na kujisomea kitabu Fulani,alivyofika akaniambia Ana akshi sana twende chumbani, baada ya mambo mambo ile nataka kuingia ikulu nikahisi kabisa hii ikulu imedukuliwa na wajanja,the thing is am old enough na huyu mwanamke namjua sana so nika notice something haipo sawa hapa.nikakaza moyo konde nikaingia mchezoni japokua akili haikuwa sawa kabisa. Bado kama miezi minne ndoa inakuja,maisha yamebadilika, ye anawahi kutoka kazini ila kufika nyumbani kila siku ananikuta mimi, nyumbani hapiki kuna mahali akawa anapitia chakula karibu kila siku(napajua)

Nikaanza upelelezi, sina tabia ya kugusa simu yake na sikuona sababu ya kuanza kufanya hivyo,kuna siku nampigia,after kama missed call 5 anapokea,ni SAA 3 usiku hajarudi nyumbani,namuuliza alipo ananiambia bado bado kuna foleni,basi namwambia ptia chakula anasema haya,nawasha gari naenda hii sehemu anapochukulia chakula napaki kwa mbali kidogo najibana mahali nakunywa bia yangu taratibu,muda si muda anaingia my wife to be na kijana mmoja,wanafungiwa chakula wanaenda parking,jamaa anamtolea mkoba kwenye gari kisha wana French kiss jamaa anaondoka wife anachukua bajaji anaondoka pia. Hapa ndo nikaelewa kwanini gari analiacha kazini,after work kuna MTU anakuja kumchukua.

Naamini humu tu watu wazima na kila mmoja wetu anafahamu hisia za usaliti zilivyo hivyo sihitaji kuelezea.. Narudi baanyumbani SAA 9 usiku nikiwa nimelewa sana,nafika nalala sebleni huku wife to be akijifanya analalamika sana,najitahidi kumpuuza,kesho yake nashindwa kwenda kazini.simuulizi chochote,, baada ya siku mbili anarudi kachelewa,baada ya kumkiss nagundua amekunywa, ndugu nlikua sijawahi kumpiga mwanamke maishani mwangu ila hio siku nilimpa kichapo vijana wa sasa hivi wana msemo wao kua 'sio cha nchi hii' yani pombe ikakatika akanieleza anavyogawa uroda a-z!!! Nikasaidiana na mlinzi tukampeleka hospitali maana alipasuka ikabidi wamshone bila ganzi maana alikua amekunywa pia.kesho yake baada ya kujadiliana tukawasiliana na pande zote mbili harusi isogezwe miezi minne mbele kutokana na sababu mbalimbali.p


Time for revenge
Nlijitahidi sana kumsamehe lakini sikuweza,akawa mnyenyekevu kupita kiasi lakini moyo wangu ukakataa kabisa,sikumwambia MTU yoyote na mipango ya harusi inaendelea, nikawa chapombe,si kazini si nyumbani pombe akawa ndo rafiki yangu.. Sina hisia na huyu mwanamke tena,kilichobaki na kumfanyia kisasi kisha nimuache(sina moyo wa kusamehe,I tried but it didn't work).kila aina ya kisasi naona kama hakitoshi,I went crazy kuna muda nlitamani ata kumuua yanii... Nakaa naye namwambia achukue likizo ya bila malipo twende vacation ya kimya kimya kabla ya harusi tuone ni jinsi gani tunaweza rejesha penzi..naongea na bosi wangu(long time friend) namwambia a-z bila kumficha, kuna nafasi zilitoka kwenda kuongeza ujuzi nje pale kazini sikufatlia maana ziliingiliana na ratiba ya harusi,tuka force na bosi pale akanichomeka. Nikatumia ka ushawishi kidogo kwenye hii kampuni ya bidada wakampa ka likizo japokua kishingo upande sana


Vacation inaanzia unguja na huyu mwanamke,mi napanga kisasi tu,ye anajua tunaenda tafuta muafaka,nshakua pombe MTU hapo... Kwa kifupi Mwezi mzima tulitembea mikoa kadhaa hapa nchini,katika kipindi hiko chote sikuwahi kupata hisia nae tena,nlimpa tabasamu la kinafiki muda wote. Tulipokua znz mwanzo wa vacation nikamshawishi sana nianze 'kuruka ukuta'(samahani kama ntamkwaza MTU hapa) anakua mgumu ila baada ya ushawishi na influence ya pombe anakubali. Yani nlikua simjali hata kidogo,akawa Analia kila siku kua namuumiza lakini nikawa nampoza kinafiki,mwezi mzima nikamfanyia uchafu bila huruma.

Tunarudi jijini,naenda kwa mama namwambia kua Hamna mke pale wala ndoa,naanza maandalizi kimya kimya ya kwenda nje,narudisha usamamizi wa miradi yangu yote,siku si siku bidada yupo kazini nabadilisha lock za milango,natoa kila chake nampa mlinzi na kinote ampe kikiwa na maneno machache tu. Nakaa kwa boss kwangu siku mbili naenda nje

Nakutana na binti wa kitanzania(RIP) nje,nae kachoshwa na mahusiano,tunasaidiana 'kupambana na baridi la ulaya' katangulia mbele ya haki Ila kaniachia zawadi ya mapacha(boy and a girl). Ni mwaka wa pili tangu tumzike na ilikua ndio siku yangu ya mwisho kunywa pombe!!!!!

Maisha yanasonga,sitaki kusikia habari za kuoa maana najua sina moyo wa kusamehe na maisha ya sasa ndo mwendokasi kwelikweli. Sasa hivi watoto wangu ndo dunia yangu, +work and gym.
Eway huyu mwanamke jumamosi alinipa namba ila nikazifuta,maisha safari ndefu wakuu. Poleni kwa Uzi mrefu

The best revenge is forgiveness, don't follow my path

By 2017/JF

JE ni Kweli Pesa za Kale Zina Nguvu za Kichawi?

$
0
0
Moja kwa moja utawaza kuhusu rupia(rupee ya mjerumani) na pesa nyingine za kale na yale yanayosemwa kuzihusu hasa kwenye habari nzima za kichawi
Watu wamezinguka na kuzinguliwa hasa watu wametapeliwa na wengine kufa wakitafuta hivi vitu vinavyotajwa kuwa na thamani kubwa


Ukweli huu hapa na si pesa tu bali na vitu vingine vya kale

1. Aina ya malighafi iliyotumika
Wakati huo vilitengenezwa vitu imara sana kutokana na upatikanaji wa malighafi ya kutosha ...vitu kama vyombo vya bati na chuma urembo kama bangili mikufu pete nk leo hii ukivipata na kuviyeyusha kila kimoja unaweza kutengeneza kumi kupitia hicho kimoja

2. Uhifadhi
Wajerumani kwa hapa kwetu walikuta malighafi vito na madini ya kutosha sana! Kutokana na uhifadhi hafifu wakati huo vingi ya hivi vitu viliwekwa tu majumbani mwao wakiviandaa kuvidafirisha kwao
Vita ya pili ya 1939-45 iliwachanganya mno na walipoelekea kushindwa waliamua kuficha mali yote kwenye mashimo makubwa mashambani misituni kwenye mahandaki na milimani kusikofikika kwa urahisi kisha wakawaua watu karibia wote walioshiriki na wanaojua yale maficho wakasepa
Huku kote mali hizo zilihifadhiwa kwenye vyumba imara vilivyojengwa kwa zege gumu hasa ili iwe ngumu kuchimbua ama kuvunja na kama ni mapangoni yalikuwa mapango ya mbali hasa milimani na misituni

3. Dhana ya majoka na viumbe wa ajabu
Huko kwenye hayo maficho kuna baadhi ya watu walisalimika hivyo wakasimulia vizazi vilivyofuata
Kizazi cha kusaka utajiri wa haraka kikaona fursa na kuamua kuchangamkia dili. ..Wajerumani hawakuweka ulinzi wowote wa majoka! Hao ni viumbe tu walijitwalia makazi huko ambako ndio maisha yao yaliko
Watu walioenda bila tahadhari waliumwa na hayo madubwana na kupoteza maisha! Waliosalimika walitimua mbio na kuunda stories za kufikirika

4. Dhana ya uchawi na majini
Kwa wale waliosaka kwenye mahandaki na mashimo marefu yenye vyumba vilivyojengwa kwa zege , baada ya kufanikiwa kuvunja hayo mazege na kutaka kuingia ndani nao walikutana na mauzauza ya kila aina
Unajua ni kwa nini? Sehemu yoyote yenye mfumo wa nyumba ama chumba isiyokaliwa na binadamu roho zinazotangatanga na mapepo hufanya makazi yao kumbuka ile mada ya kutakasa makazi! Hivyo ukiingia huko lazima ukutane na vitu vya ajabu...Mjerumani hahusiki kabisa!

5. Uamuzi wa kufanya kafara ama tambiko kabla ya kuchimba ama kuingia pangoni
Wengi walitafuta waganga wa kienyeji kwenye hili na hawakufanikiwa. ..waliofanikiwa walifanikiwa kwa ujanja tuu....ukienda kwenye pango misituni ukachinja mnyama ukapiga manyanga automatically mkiondoka ile nyama italiwa na kuna wakati manyanga huleta kelele na kufukuza mnyama yoyote aliyeko pangoni...ndio maana baada ya kafara hamuingii siku hiyo hiyo bali kesho yake nk
Wale wa kwenye mashimo NA mahandaki ni ibada tu ya kuziomba roho ziondoke ama kuzifukuza kwa kutumia mitishamba na harufu wasizozipenda....mkikutana na roho korofi mtachezea kichapo mpaka muache kila kitu na kutimua mbio kali sana

6. Ukweli hasa ni UPI?
Baada ya vita ya pili kukoma na baadae Uhuru wajerumani walishindwa kurudi kwa ubabe hivyo wakatumia njia za kijanja kurudi
Unajua waliondoka na ramani zote kule mali zilikofichwa hivyo walirudi kuzichukua kwa njia ya kununua yale maeneo na kuyaendeleza kwa kujenga shule vyuo hospital nk ama miradi ya barabara ufugaji na kilimo
Kwa njia hii walichukua vyao kiulaini mno

7. Thamani na umaarufu wake ni UPI?
Vitu vya kale kwa wenzetu vina thamani kubwa sana....wenzetu wana utaratibu wa kuweka vituo vya antiques na kuchaji watalii pesa ndefu kuviangalia . kila kimoja kinakuwa kimeandikiwa historia yake. Kwa hiyo wakija huku kuvitafuta wengi huenda kuviuza kwenye hayo maduka kwa bei kali mno

8. Nguvu ya utajiri
Biashara imevamiwa , vitu vya kale haviwezi kukupa utajiri wa miujiza ..havina huo uwezo bali kuna baadhi kutokana na malighafi iliyotumika kuvitengeneza vina mvuto kwenye ulimwengu wa giza kama mabangili ya shaba

9. Usumbufu
Kuna watu wanawachezea wenzao shere na kuwasumbua bila sababu.. Miaka hiyo pesa ilitengenezwa kwa mpango maalum(nadhani hata sasa) na zilitengenezwa kwa miaka... Kuna miaka pesa hazikutengenezwa. Sasa mtu anakupa dili na kukuahidi kukupa pesa ndefu ukimletea rupee ya mwaka fulani Rupie_robo_DOA_1913.JPG

10. Hitimisho
Kuna baadhi ya sehemu kulikofichwa hizo mali wafichaji walinuizia ama kufanya mambo ya giza ili atakayejaribu kuchukua ama apate madhara au asizione kabisa...lakini kwa sehemu kubwa ni habari zilizotiwa chumvi nyingi


JUMAPILI NJEMA

DINI ya Kiislam Yenye Mfumo wa Kilokole Yaja

$
0
0

Gazeti la Jibu Limeandika:

Watakuwa wanaswali jumapili

Watakuwa wanaswali kwa sauti za juu

Lengo ni kuwaslimisha wakristo

VIDEO:Sitti Mtemvu Azungumzia Rushwa ya Ngono Kamati ya Miss Tanzania

$
0
0

Aliyekuwa Miss Tanzania 2014, Sitti Mtemvu amefunguka kuzungumzia tuhuma za rushwa ya ngono ambazo zimekuwa zikielekezwa mara kwa mara kwenye kamati inayoandaa mashindano ya urembo nchini, Miss Tanzania.

TAZAMA VIDEO:

NIKKI wa Pili Awapa za Uso Bongo Movies Kwa Kutafuta Kiki Zisizo na Maana

$
0
0

Nikki wa Pili anasema "Wasanii wa Bongo Movie ni wakubwa na wenye ushawishi mkubwa sana! Ila wanashindwa kuutumia ushawishi wao katika ku-promote kazi zao! Ndio maana Bongo Movie inayumba!"●

Akiwa na maana kuwa mtu kama @wolperstylish, @auntyezekiel na hata @elizabethmichaelofficial ni watu ambao tunawasikia kwenye Kiki mbali mbali kila kukicha ila kibaya ni pale kiki zao zinapokuwa haziambatani na kazi zao! ●

Nikki ametoa pongezi kwa Wana Bongo fleva kwa utaratibu wao wa kufanya Kiki kabla ya kutoa ngoma akidai kwamba Kiki zinasaidia kutangaza kazi zao na kufanya sanaa yao inakua tofauti na Bongo Movie ambao mara nyingi Kiki zao haziambatani na Kazi zao. ●

Mfano mzuri @nikkwapili ameutoa kwa @iambenpol ambaye aliamua kuchukua attention za watu kabla ya kuachia ngoma yake ya #Tatu ikiwa ni Nadra sana kuona mambo kama hayo kwenye Tasnia ya Bongo Movie

Tfda yatafuta ukweli kuhusu mchele wa plastiki Dar

$
0
0

MAMLAKA ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) imeunda kikosi maalum ili kupata ukweli juu ya mchele unaodaiwa kutengenezwa kwa kutumia plastiki baada ya picha kusambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa umeanza kutumiwa na baadhi ya mamalishe jijini Dar es Salaaam.

Baada ya picha hiyo kusambaa kwenye mitandao ya kijamii, ikielezea mchele huo kutumiwa na mamalishe kariakoo jijini Dar es Salaam, baadhi ya wananchi hususan wanaopata huduma ya chakula kwa mama lishe hao, walianza kuingiwa na hofu.

Mkurugenzi Mkuu wa (TFDA), Hiiti Sillo,jana alisema mamlaka imeanza kufuatilia suala hilo na kwamba imeunda timu maalum ili kubaini ukweli wa suala hilo.

Aidha, alisema taarifa za awali walizipata kupitia mtandano wa kijamii na Juni 8, mwaka huu, walitoa taarifa ya ufafanuzi kuwa hapakuwa na mchele wa aina hiyo ingawa wanaendelea kufuatilia.

“Mchele ambao upo na ambao TFDA tunautambua ni wa Basmati ambao huitwa Sunrice. Huu wa kutengenezwa kwa plastiki tunaendelea kufuatilia kama taarifa hizo ni za kweli au la,” alisema.

Alisema timu hiyo imeanza kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini kama ni kweli mchele huo uko sokoni. Aliwataka wenye taarifa za ziada kuhusu mchele huo wawapelekee ili kurahisisha uchunguzi.

“Tunaomba wenye taarifa za wapi mchele huu unauzwa, waliotumia watuletee au wapeleke taarifa serikali za mitaa wanakotoka, polisi au kwenye ofisi zozote za serikali ili tuweze kufuatilia jambo hili kwa urahisi,” alisema.

Mkurugenzi huyo alikiri kwamba mamlaka yake imepata taarifa juu ya mchele huo ingawa hadi sasa haijadhibitisha kama kweli umeshaingia nchini.

“Tayari nimeshatoa maelekezo kwenye kanda zetu za TFDA zikiwamo Mwanza, Arusha, Mbeya kuanza kufuatilia na ninavyozungumza ni kwamba ukaguzi unaendelea. Kama taarifa hizi ni za kweli tunamwomba huyu aliyetuma ‘clip’ (picha) hii kwenye mitandao ya kijamii ajitokeze ili atusaidie ni wapi alikula mchele huu maana clip inaonyesha mkono tu,” alisema.

Katika ‘clip’ hiyo, kijana huyo anaeleza kuhusu chakula hicho (wali) walioletewa na mama lishe huko Kariakoo huku akifinyanga tonge na kuonyesha tofauti yake na ule wa kawaida.

Sillo alisema taarifa mbaya zinazohusu chakula zinagusa watu na maisha yao kwa ujumla ndiyo maana wanamwomba mtu huyo awape ushirikiano ili wawajue wauzaji na wasambazaji.

“Wito wangu kwa watu wanaponunua kitu chochote wadai risiti hii itasaidia matatizo kama haya yanapojitokeza inakuwa rahisi kumkamata mhusika,” alisema.

Kuibuka kwa taarifa juu ya kuwapo mchele wa plastiki, kumezua taharuki na gumzo kwa wakazi wa Dar es Salaam ambao asilimia kubwa ndicho chakula chao na wengi hula kwa mama lishe.
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images