Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

BAADA ya Rugemalira Kufikishwa Mahakamani Baadhi ya Viongozi Watoa Neno

$
0
0
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) baada ya kuwafikisha mahakamani, Habirnder Seth Singh na James Rugemalira kwa makosa ya uhujumu uchumi baadhi ya viongozi wameweza kuandika jambo kuhusiana na watu hao kufikishwa Mahakamani.

Naibu Waziri wa Afya Mandeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto ametwee hivi:
Mshahara wa dhambi ni mauti. Hakika hakuna marefu yasiyo na ncha. Leo Ndg. Harbinder Singh Sethi na Rugemalira wako mbele ya jicho la sheriaLeo vita dhidi ya ufisadi, uhujumu uchumi na matumizi mabaya ya ofisi imepata sura mpya.

Kwa upande wake Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe nae katweet kuhusu tukio hilo huku akiweka picha za wahusika hao.

Leo ninaona vita dhidi ya ufisadi Ina maana kubwa. Kumkamata Harbinder Singh Seth na kumfikisha mahakamani ni hatua kubwa ya kupongezwa Rais Magufuli nimekuwa nakupinga kwenye mambo mengi, na nitaendelea kukupinga, lakini kwenye hili la IPTL umetendea nchi haki. Hongera Sana Leo Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Kamishna Valentino Mlowola akizungumza na waandishi wa habari alisema leo wamewafikisha mahakamani watuhumiwa wawili, kwa makosa ya kuhujumu uchumi ambao ni Habirnder Seth Singh na mfanyabiashara James Rugemalira.

UKIYAFANYA Haya Mafanikio Makubwa Yapo Upande Wako

$
0
0
Kwa muda mrefu umekuwa ukijiuliza ni vipi utapata mafanikio unayoyahitaji?  Lakini jibu ni kwamba mafanikio unayo wewe mwenyewe ila tatizo ni kwamba unakuwa ni mtu wa kusuasua kuanza mambo hayo ya kusaka mafanikio. Ngoja nikukumbushe ya kwamba hakuna muda maalumu wa kuyasaka mafanikio. Utawasikia watu wengine wanasema eti nikiwa ukifika miaka 35 au 40 eti ndo utaanza kuyasaka mafanikio kwa kuwa na nyumba, magari na mengineyo. Hii sio kweli  kumbuka ya kwamba muda wa mafanikio ni sasa na wewe ndio mwamuzi wa kuamua  kuanza kuchangamkia fursa zilizopo ili uweze kuwa miongoni  mwa matajiri ambao utakuwa unatajwa midomoni  mwa watu,  naamini  ya kuwa unaweza.

Wapo baadhi ya matajiri wakubwa tunaowajua.  Leo ukijaribu kusoma historia zao wengi wameanza kuwa na mitaji midogo kabisa  lakini leo hii ndio ambao wapo midomoni mwetu. Kwa sisi ambao bado hatujapata mafanikio kwa muda mwingi tunakaa vijiweni tunawajadili , kuwasifia na kuwapa sifa nyingi nzuri bila wao kutusikia hata kutujua majina yetu,  huku wao wakiingiza  fedha na kuzidi kutajirika zaidi. Yapo baadhi ya mambo ambayo leo hii tukiyafanya , sisi  wengine ambao hatuna siri hii ya utajiri  tujijua tutakuwa kama wao.

Yauatayo ndiyo Baadhi ya mambo ambayo leo hii ukiyafanya mafanikio makubwa yatakuwa upande upande wako;

Tenga muda wa kufikiri mambo yako.
Muda ni jambo la msingi sana katika safari ya mafanikio. Kisaikolojia binadamu wote ni sawa ila tunatofautina sana  katika matumizi ya muda. Ngoja nikupe mfano huu ili uweze kunielewa zaidi.  Kwa siku kuna masaa 24. Masaa haya jinsi anavyotumia masikini na tajiri ni tofauti kabisa. Tajiri masaa haya huyaona hayotoshi kwa sababu ana mambo mengi ya kufanya. Ndo maana hata baadhi ya matajiri ukiwa hufanyi vizuri katika kazi zao utawasikia wanasema usinipotezee muda  maana kwao muda ni mali.

Lakini masaa hayohayo kwa maskini huwa ni masaa mengi sana kwa sababu hana mambo mengi ya kufanya hata kufikiria pia. Maskini huyohuyo akitaka kuamka asubuhi utamsikia anauliza hivi jua limechomoza. Kwa maana ya kwamba yeye huongozwa kwa kulitazama jua. Halikadhalika akiamka asubuhi utamskia usiku wa leo ulikuwa mrefu sana. Ewe  msomaji wa makala haya ukifanya hivo mafanikio utayasikia kwa kina billgate tu.

Jambo la muhimu kumbuka ya kwamba kama kweli umeuchoka na hali ya umaskini hakikisha unatenga muda wa kufikiri mambo ya mafanikio kila siku.  Wakati upo katika muda wa kufikiri mambo yako ya kimafanikio hakikisha ya kwamba unakaa sehemu tulivu ambazo hazina kelele za aina yeyote ile kama vile watoto,  simu, radio, tv na sauti zingine mabazo zitakufanya ufikilie vizuri mambo yako ya muhimu. Pia kumbuka wazo zuri ambalo utalipata lifikirie mwanzo hadi mwisho wa jambo hilo. Pia liwe ni japo moja. Liandike kwenye karatisi au mahali popote ambapo unahisi hatapasau kwa urahisi.

Andika mikakati mizima ya utekezaji wa jambo hilo. Kwa kuangalia zana ambazo zitatumika kuangalia jambo hilo, pia jaribu kutazama changamoto ambazo unahisi zitajitokeza juu ya jambo hilo pamoja na jinsi ya kukabiliana changamoto hizo na jaribu kuona matoteo ya jambo hilo. Kwa ufupi lazima uone maono (VISION) ya wazo lako.

Badili ratiba ya kufanya mambo yako.
Kuna baadhi ya watu tunafanya vitu kimazoe sana hii inapelekea  siku zote tunabaki  vilevile huku tukilalamika ya kuwa maisha ni magumu.

Tukumbuke ya kwamba Kufanya vitu kimazoea kunamfanya mtu asiweze kusongo mbele.
Watu wengi ambao wanalamika juu ya maisha asilimia kubwa utagundua ya kwamba wanafanya vitu kimazoea.  Kama kweli unapenda jambo Fulani la kimafanikio kuwa basi usilifanye  kwa mazoea.
Fanya vitu tofauti na ulivyozoea utaona matokeo makubwa ya kimafanikio yapo upande wako.
Kama umezoe kuamuka saa mbili kamili asubuhi basi amka saa kumi na mbili asubuhi ili uwone mpaka saa mbili utakuwa umefanya nini, kama umezoea kufunga biashara yako saa tatu usiku basi ongeza muda wa kufunga biashara yako hadi saa tano ili uwone kama kuna mabadiliko. Kama wewe ni mvivu basi anza kuwa miongoni mwa watu wanaofanya kazi kwa bidii.

Endapo utafanya hayo yote kwa kuzingatia wewe ni msaka tonge mafanikio makubwa yapo upande wako. Usikate tamaa katika kila jambo unalolifanya. Kuwa shupavu kama simba,  maana simba akikosa nyama hawezi kula nyasi atapambana huku na huko ili apate nyama.

Kama una maswali , ushauri au mapensekezo usisite kuwasiliana na afisa maendeleo na mipango mwandishi wa makala haya  Benson Chonya.  Usisite pia kumshirikisha mwenzako ili aweze kujifunza pia.

NIMEMZIMIKIA Kimapenzi Binti Aliyekuwa Anatangaza Kipindi cha Mkasi TV....

$
0
0
Wadau
Nilikuwa mfuatiliaji mzuri sana wa Kipindi cha Mkasi TV Kabla hakijafutwa

Kuna huyu binti Mtangazaji anaitwa Salama Jabir alikuwa ananikosesha amani kwa uzuri wake. Yaani nilikuwa nikimuona kwa TV tu basi mapigo ya moyo yanaenda kasi sana.

Ananifanya hata nashindwa kwenda kulala ili nibaki namuangalia yeye tu.

Yaani kuanzia shape yake mimi hoi, ukija kimo ndo kabisa natetemeka mwili. Upande wa sauti ndio siongei hata kidogo.

Midomo yake ni ile iliyobinuka Kwa style flani hivi ya Anjelie Jolie halafu kwenye macho yani akuongezea kula kungu basi nahonga kila nlichonacho. Age yake sijajua bado, but hawezi kua zaidi ya 28.

Wadau, huyu binti anautesa sana mtima wangu siku hizi sijui yupo wapi nimemmisi sana,,,,akinikubalia namuoa kabisa huyu,

Naomba mwenye uwezo wa kupata contacts zake anisaidie please my

True Confession: 'I am Sleeping With My Sister'

$
0
0
I have been having an affair with my stepsister. I know it’s wrong but we love one another so much.

I am 26, she is 23. My mum married her dad 10 years ago and we got on from the moment we first met. She lived with her mum and we only met at birthdays and Christmas, then two years ago she finished school and got a job near where we live, so she came to stay with us.

My girlfriend and I have been dating for three years and everyone thinks we are going to get married and settle down soon. I thought so too until a few months ago.

Mum and my step-dad went away for the weekend when my girlfriend was at her sister’s party, so my stepsister and I were alone in the house.

We had a bottle of wine and watched a movie snuggled up together on the settee. It felt so comfortable, we turned to each other and kissed to say good night, but the kiss was electric.

Suddenly we were all over one another. It got very passionate and in the end we went upstairs and made love. It felt so natural and so right.

We expected to feel regrets in the morning but we had a wonderful day together, making love and acting like a real couple. Our relationship has carried on since though I’ve been feeling more and more uneasy about deceiving my girlfriend.

We decided we should tell my mum and her dad last week. We hoped they would be understanding and help us decide what to do but they were both very angry. They say unless we finish they will throw me out and tell my girlfriend.

Maalim Seif: Hatuna ugomvi na Lipumba

$
0
0

Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad amefunguka na kuweka wazi kuwa Chama Cha Wananchi ( CUF) hakina mgogoro wowote na Profesa, Ibrahim Lipumba na kudai kuwa kiongozi huyo si mwanachama wa CUF bali ni mwanachana wa Jaji Mutungi.

Maalim Seif Sharif Hamad amedai Lipumba si Mwenyekiti Chama cha Wananchi (CUF) na kudai kuwa mkutano Mkuu wa CUF ulishamuondoa siku nyingi lakini yeye mwenyewe alishajiuzulu nafasi hiyo.

"Wengi wanaulizia mgogoro huu na Lipumba sisi CUF hatuna mgogoro na Lipumba, Lipumba si mwanachama wetu kabisa kabisa, Lipumba ni mwanachama wa jaji Mutungi na Mwenyekiti wa jaji Mutungi lakini siyo mwanachama wala Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), Mkutano mkuu umeshamuondoa Mwenyekiti si Mwenyekiti kwani alishajiuzulu mwenyewe na Baraza Kuu lilimfukuza uanachama" alisisitiza Maalim Seif

Mbali na hilo Maalim Seif aliwapa mbinu wabunge na viongozi wa kisiasa hususani wapinzani, jinsi ambavyo wanaweza kukutana na watu wapiga kura wao na kuweza kufanya siasa katika mazingira hayo hayo watakayokutana nao. 

Maalim Seif amedai kuwa Lipumba ni mwanachama na Mwenyekiti wa jaji Mutungi kwa kuwa ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa nchini inamtambua Profesa, Ibrahim Lipumba kama Mwenyekiti CUF na mwanachama wa CUF.

Kamusi Kuu ya Kiswahili yazinduliwa Tanzania

$
0
0
Waziri mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema Serikali yake inatambua umuhimu wa lugha ya Kiswahili kwa ustawi wa taifa na katika kulinda umoja wa kitaifa.

Ametoa kauli hiyo alipozungumza na wabunge, viongozi wa Serikali na wananchi waliohudhuria uzinduzi wa Kamusi Kuu ya Kiswahili uliofanyika kwenye ukumbi wa Bunge mjini Dodoma.

"Serikali inatambua umuhimu wa lugha ya Kiswahili kwa ustawi wa nchi yetu na katika kulinda umoja wa kitaifa. Hakika lugha ya Kiswahili ndiyo inayotufanya tuwe Watanzania. Hivyo, tunaithamini na kwetu hii ni lulu na tunu ya Taifa," amesema.

Waziri Mkuu katika taarifa iliyotolewa na ofisi yake amesema uzinduzi wa kamusi hiyo unaenda sambamba na azma ya Serikali ya kutumia Kiswahili kwenye shughuli zote za kitaifa kama vile mikutano, mijadala, semina na ufundishaji shuleni.

Majaliwa amempongeza Rais John Magufuli kwa kuhimiza matumizi ya Kiswahili kwenye mikutano na matukio muhimu ya kitaifa, kama vile dhifa za kitaifa anazowaandalia wageni wake kutoka nje.
"Hata alipokuwa kwenye mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika, Rais alitumia Kiswahili kuhutubia mkutano huo. Amekuwa akifanya hivyo, hata kwenye mikutano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki lengo lake ni kuitangaza lugha hii ya Kiswahili," amesema.

Waziri Mkuu , amewasihi wazazi wahakikishe watoto wao wanapata kamusi hiyo kama moja ya nyenzo zao za kujifunza lugha ya Kiswahili."Ninashauri makundi mengine kama vile waheshimiwa wabunge, wanahabari, wakalimani, wafasiri, waandishi na wahariri wa vitabu, maofisa mawasiliano wa kwenye ofisi zetu, muone umuhimu wa kununua kamusi hii ili iwasaidie kujiimarisha kwenye matumizi ya Kiswahili fasaha na sanifu," amesema.

Awali, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amesema Kiswahili ni lugha ya pili inayotumiwa na watu wengi zaidi barani Afrika lakini pia ni lugha ya 10 kati ya 6,000 zinazozungumzwa na watu wengi duniani.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa (Bakita), Dk Seleman Sewangi amesema kazi ya kuandaa kamusi hiyo ilianza Agosti 12, 2011 na kukamilika mwaka 2015 na toleo la kwanza lilichapishwa. Amesema kamusi hiyo imekusanya maneno mengi makuu (vidahizo) kuliko kamusi zilizotangulia na kwamba ya sasa ina maneno 45,500.
 Facebook  T

Vyeti vya Kuzaliwa Vilivyoandikwa Kwa Mkono Vyaandaliwa Mwongozo

$
0
0

Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi ameuagiza Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita) kuandaa miongozo itakayowezesha kuwaepusha Watanzania na usumbufu pindi wanapohitaji kutumia vyeti vya kuzaliwa vilivyoandikwa kwa mkono.

Akizungumza leo (Jumatatu) na wadau kuhusu usanifu mpango wa usajili wa matukio muhimu kwa binadamu na ukusanyaji wa takwimu (CRVS), Profesa Kabudi amesema amepokea malalamiko kutoka kwa watu kuhusu vyeti hivyo.

“Nimepokea malalamiko kuwa kuna baadhi ya taasisi za Serikali na sekta binafsi zinakataa kupokea vyeti  vilivyoandikwa kwa mkono na badala yake wanataka vilivyoandikwa kwa mashine,” amesema.

Profesa Kabudi amesema mwongozo huo utasaidia watu kutokata tamaa kutokana na usumbufu wanaoupata baada ya vyeti hivyo kukataliwa.

‘’Wanataka vile vya kompyuta, mbona vyeti vya ndoa na vifo huwa vinaandikwa kwa mkono, mtu wa kijijini anapata wapi kompyuta? Naomba mpokee na sitaki tena kusikia malalamiko kuhusu kukataa vyeti vinavyoandikwa kwa mkono,’ ’amesema.

Waziri amesema Serikali imeamua kuboresha mfumo wa usajili uliopo na kuanzisha utakaofanya kazi vizuri wa usajili wa matukio muhimu ya binadamu.

Mwenyekiti wa Bodi ya Rita, Profesa Hamis Dihengo amesema takwimu za sensa ya watu na makazi za mwaka 2012 zinaonyesha kuwa asilimia 13.4 ya wananchi ndio wamesajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa.

Profesa Dihengo amesema idadi hiyo ni ndogo na ni kiashiria kuwa Serikali haina taarifa za idadi kubwa ya wananchi.

‘’Pamoja na takwimu hizi wapo wananchi ambao huzaliwa na kufa bila hata taarifa zao kuonekana katika kumbukumbu zozote za serikali, hivyo tunaomba Watanzania wajitokeze kupatiwa vyeti vya kuzaliwa,’’ amesema.

Marekani iliwapora Wanadiplomasia Wetu - Korea Kaskazini

$
0
0
Korea kaskazini imelaumu mamlaka nchini Marekani kwa kuwapora wanadiplomasia wake katika uwanja wa ndege mjini New York.

Msemaji wa taifa hilo lilijitenga alisema kuwa maafisa wake waliporwa mizigo yao katika uwanja wa ndege wa JF Kenedy siku ya Ijumaa.

Shirika la habari nchini Korea Kaskazini KCNA, lilisema kuwa kisa kilionyesha kuwa marekani ni taifa jambazi.

Ikulu ya Marekani hata hivyo haijasema lolote.

Wanadiplomasia wa Korea Kaskazini wanadaiwa kurejea kotoka mkutano wa Umoja wa Mataifa wakati kisa hicho kilitokea

Kisa hichi cha hicho huenda kikawa msumari wa moto kwenye kidonda kwa uhusiano ulioharibika kati ya nchi hizo mbili.

Wiki iliyopita Korea Kaskazini ilimrejesha mwanafunzi raia wa Marekani Otto Wambier kwa afamilia yake, baada ya zaidi ya mwaka moja tangu hukumiwe kifungo cha miaka 15 na kazi ngumu.

Bwana Warmbier alikuwa amepoteza fahamu na alikuwa na madhara makubwa kwenye ubongo.

Marekani Yaitungua Ndege ya Kijeshi ya Syria

$
0
0
Marekani imeitungua ndege ya kijeshi ya Syria iliyokuwa ikijiandaa kuwashambulia wanamgambo wa IS ambao wamekuwa wakihatarisha maisha ya wananchi wa nchi hiyo huku umoja wa mataifa ukitaka kuwepo na usuluhishi.

Aidha, Marekani imesema kuwa imefikia hatua hiyo mara baada ya jeshi la Syria kuvishambulia vikosi vya Syrian Democratic Force SDF, vinavyoungwa mkono na Marekani  kwa lengo la kupambana na wanamgambo wa Islamic State.

Kwa upande wa Serikali ya Syria imesema kuwa ndege yake ilikuwa katika maandalizi ya kuwashambulia wanamgambo wa Islamic State na si vikosi vya Syrian Democratic Force vinavyoungwa mkono na Marekani.

Vikosi vya Syrian Democratic Force (SDF ) vinaungwa mkono na umoja unaoongozwa na Marekani kwaajili ya kupambana na wanamgambo wa Islamic State ambao wamekuwa tishio katika ukanda huo.

Staa Mwingine wa Tatu wa Soka Duniani Yupo Tanzania Kwa Utalii

$
0
0
List ya mastaa wa soka barani Ulaya kuja Tanzania kutalii inazidi kuongezeka, baada ya wiki kadhaa nyuma kuja kwa David Beckham na familia yake, wiki moja baadae akatua staa wa Liverpool Mamadou Sakho kutalii katika hifadhi ya Ngorongoro.

Baada ya mastaa hao kuja Tanzania taarifa ikufikie kuwa kuna staa wa Tottenham Hotspurs amewasili Tanzania kwa ajili ya utalii, kiungo wa timu ya taifa ya Denmark anayeichezea Totteham Hotspurs ya England  Christian Dannemann Eriksen ametua Tanzania.

Chris Eriksen amekuwa tofauti kidogo kama ilivyokuwa kwa Mamadou Sakho ambaye alikuwa haoni tatizo kupost na kuonesha kuwa yupo Tanzania, Eriksen amekuwa akipost picha bila kutaja mahali alipo ila kimuonekano yupo Ngorongoro Crater Tanzania.

Polisi DSM Wazungumzia Tukio la Walemavu Kupigwa Mabomu

$
0
0
Jeshi la Polisi DSM limekutana na Waandishi wa Habari na kutolea ufafanuzi mambo mbalimbali yaliyojiri na moja kati ya mambo hayo ni issue ya Walemavu waliotawanywa kwa mabomu ya machozi baada ya kuziba Barabara ya Sokoine June 16, 2017 wakiandamana kwenda kwa Mkurugenzi wa Manispaa.

Naibu Kamishna wa Polisi ambaye pia ni Mkuu wa Operation za Kipolisi Kanda Maalumu ya DSM anayekaimu nafasi ya Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya DSM Lucas Mkondya amesema:
”Hatujatumia nguvu ya kupita kiasi. Tumetumia nguvu kulingana na hali ya watu ambao walikuwa wanafanya maandamano hayo.

“Ulemavu, nataka nitoe rai kwa wananchi ulemavu sio kibali cha wewe kuvunja sheria wala ulemavu haukupi wewe kibali cha kuvunja sheria za nchi. Sheria za nchi zipo kwa mtu yeyote yule – mzima au mlemavu na hasa ambaye anazifunja kwa makusudi akijua.

“Hawa walemavu walifanya makosa, wamevamia Ofisi ya Mkurugenzi  wa Manispaa lakini pamoja na hivyo wakaziba njia. Tumejaribu kuongea nao kuwasihi kwamba wafungue njia lakini pia wateue viongozi wao kwenda kushughulikia matatizo yao lakini walikaidi. Kwa hiyo, ikabidi tutumie nguvu kidogo tukaenda kuwaondosha tukafungua barabara na wananchi wengine wakaendelea na shughuli zao.” – Kaimu Kamanda Lucas Mkondya

Hizi Ndio Siku za Hatari za Mwanamke Kushika Mimba

$
0
0

HABARI za leo wasomaji wangu? Kabla ya kuanza mada hii ya leo napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mungu kwani ameniwezesha kufika siku hii.Mada leo inahusu siku za hatari ambazo mwanamke  akifanya ngono bila kinga basi anakuwa katika hatari ya kushika mimba.


Nimeamua kutoa mada hii baada ya kugundua kuwa ongezeko la matukio ya utoaji mimba na kutupa watoto  na hata kuwa na watoto wa mitaani yanasababishwa  zaidi na mimba ambazo hazikutarajiwa.
Mimba nyingine zinaingia kwa sababu mzazi kutokujua siku yake ya hatari ili kujikinga asipate.


Ni muhimu sana kwa mwanamke kujua mzunguko wake wa hedhi, mizunguko hiyo iko katika makundi makuu matatu ambayo: Mzunguko mfupi wa siku 25 kurudi nyuma, mzunguko wa kawaida wa siku 28 na mzunguko mrefu wa siku30-35.


Wanawake wengi mzunguko wao  huwa  ni wa kawaida yaani siku 28 hawa ndiyo leo nitawaongelea zaidi.

Ili kutambua mzunguko wako ni wa siku ngapi unatakiwa kuhesabu kuanzia siku ya kwanza kuona damu ya hedhi hadi siku ya kwanza ya kuona damu ya hedhi ya mwezi unaofuata. Kwa mfano ukiona damu ya hedhi tarehe 15 Oktoba  basi hiyo ndiyo siku yako ya kwanza.


Kwa mtu mwenye mzunguko huo wa siku 28 siku zake za hatari za kuweza kushika mimba ni siku ya kumi na nne 14, hivyo kuanzia siku ya 12 hadi siku ya 16 kama atafanya ngono bila kinga anaweza kushika mimba.


Najua mtu anaweza akajiuliza kama siku ya hatari ni ya 14 sasa kwa nini akifanya ngono siku ya 12 anaweza akapata mimba?Hii ni kwa sababu mbegu za kiume zina uwezo wa kudumu kwa masaa 24 hadi

48 baada ya kujamiiana hivyo kama mwanamke atafanya ngono tarehe 12 na yai likatoka tarehe14 bado litakuta zile mbegu zikiwa hai hivyo zitarutubishwa.

Tundu Lissu Afunguka" Kumkamata Seth na James Rugemalila ni Sawa Lakini Haitoshi"

$
0
0

Anaandika Mhe: Tundu Lissu
KUMKAMATA HARBINDER SINGH NA JAMES RUGEMALILA NI SAWA LAKINI HAITOSHI!!!! Na Tundu Lissu
Harbinder Singh Seth na James Rugemalila walikuwa ni sehemu muhimu ya mtandao uliokwapua shilingi bilioni 306 zilizokuwa Benki Kuu.
Ni sawa, kwa hiyo, wakifunguliwa mashtaka ya jinai ya uhujumu uchumi.

Hata hivyo, tusije kusahau kwamba walikuwa ni sehemu tu ya mtandao wa ufisadi. Vipande vingine vya chain hiyo viko wapi??? Ili bilioni 306 zitoke Benki Kuu ilikuwa lazima Gavana wa BoT Prof. Benno Ndullu na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Paymaster General, Dr. Servacius Likwelile watoe ridhaa yao.

Gavana Ndullu bado yuko ofisini kama Gavana. Dr. Likwelile ametumbuliwa ili kumpisha mpwa wa Bwana Mkubwa kuwa Katibu Mkuu na Paymaster General.
Ili bilioni 306 zitoke BoT ilikuwa lazima Waziri wa Fedha Saada Mkuya ajue na aridhie. Vinginevyo alikuwa ni Waziri wa Fedha wa aina gani asiyejua jambo kubwa kama hilo ndani ya Wizara yake.

Saada Mkuya sio Waziri wa Fedha tena lakini bado ni mbunge na yuko huru hadi sasa.

Ili bilioni 306 za umma zitoke ilikuwa lazima Rais Jakaya Kikwete afahamu na atoe ridhaa yake.
In fact, ripoti ya Kamati ya PAC ilionyesha ushahidi kwamba Prosper Mbena, wakati huo Msaidizi wa Rais Kikwete na sasa mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, aliandika dokezo kwa Gavana Ndullu kwamba Rais ameridhia mabilioni hayo yatoke.
Prosper Mbena sasa ni mheshimiwa mbunge na Kikwete ni mzee ambaye tumeambiwa tusimzungumzie bungeni wala magazetini, tumwache apumzike.

Nje ya hawa niliowataja, wapo wale waliopokea mgawo wa mapato ya udhalimu wa mabilioni hayo.

Wapo waliothibitika kuchukua tuhela twa mboga kama Prof. Anna Tibaijuka na Andrew Chenge (bilioni 1.6 kila mmoja); majaji wa Escrow, watumishi wa serikali na hata wa Ikulu ya Kikwete kama Shabani Gurumo, mapadre na maaskofu, n.k.
Wote hawa ni wahalifu kwa mujibu wa sheria za jinai za nchi hii. Karibu wote bado wako huru na wengine, kama Chenge, wamepanda vyeo na kuwa Mwenyekiti wa Bunge.

Pia kuna taasisi inayoitwa Simba Trust ambayo PAC ilisema inamiliki 50% ya IPTL. Serikali ya Kikwete ilikataa katakata kusema hawa Simba Trust ni akina nani.

JE Wajua Mayai Yanaweza Kukusaidi Uishi Umri Mrefu? Soma Stori ya Huyu Mama Mwenye Miaka 117

$
0
0
Mwanamke aliyekuwa mtu mwenye umri mkubwa zaidi duniani (kabla hajafariki akiwa na umri wa miaka 117 na siku 137), aliwahi kutoa sababu iliyomuwezesha kuishi umri mkubwa kiasi hicho.

Emma Morano alikuwa ni raia wa Italia aliyezaliwa mwaka 1899, alipohojiwa na Shirika la Habari la Ufaransa (AFP) alipokuwa nyumbani kwake, alieleza alielezea chakula chake cha kila siku.

“Ninakula mayai mawili tu kila siku, basi,” Emma alinukuliwa akisema.

Lakini inawezekana siri haipo kwenye mayai anayokula, inawezekana siri kubwa imo katika jinsi ya anavyoyaandaa ― au kwa upande wake, kwa kutoyaandaa. Morano alisema kuwa amekuwa akila mayai mawili mabichi kila siku kwa miaka mingi sana tangu daktari wake alipomwambia kuwa yatamsaidia katika ugonjwa uliokuwa unaomsumbua wa upungufu wa damu.

Zaidi ya hilo, mwanamke huyu aliyekuwa na umri mkubwa zaidi alisema ameishi umri mkubwa na anashukuru kwa “kutotawaliwa”  na mtu yeyote na kwa kuishi peke yake tangu alipoachana na mumewe alipokuwa na umri wa miaka ya 30.

Daktari wake, Carlo Bava, anasema kwamba sio tu kuishi kwake kwa muda mrefu, bali hata afya yake na uimara alionao ni wa kushangaza.

“Mbali na magonjwa yanayompata lakini mara zote anarudi kwenye afya yake kama kawaida,” alisema kuliambia AFP. “Akisema yupo vizuri au anajisikia vizuri, ni kweli anakuwa vizuri kweli kweli.”

Viongozi Watatu wa Chadema Matatani

$
0
0
Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Patrick Ole Sosopi alikamatwa na jeshi la polisi  kwa tuhuma za kufanya mkutano bila  kibali chao.
Kaimu kamanda wa polisi mkoani Iringa, John Kauga ameliambia gazeti hili kuwa Sosopi alitenda kosa hilo Juni 16 mwaka huu katika vijiji vya Mlowo na Kinyika vilivypo tarafa ya Idodi.

“Ni kweli tunamshikilia hapa kituoni na tunaendelea na uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili, mtuhumiwa alifanya mikutano katika vijiji vya Mlowo na Kinyika bila kibali cha polisi,”alisema Kauga na kuongeza:

“Kwa sasa tunaendelea kumhoji na pindi tutakapokamilisha tutaendelea na hatua nyingine ila kwa sasa tunaendelea kumhoji kwanza,”alisema.

Akieleza jinsi Sosopi alivyokamatwa, Katibu wa Bavicha Mkoa wa Iringa, Jackson Mnyawami alisema juzi mwenyekiti huyo akiwa katika ziara ya siku saba katika Jimbo la Isimani alitumiwa ujumbe mfupi wa maneno na polisi ukimtaka kusitisha ziara na mikutano hiyo.

Alisema ujumbe huo pia ulimtaka jana aripoti katika ofisi ya RCO mkoani Iringa saa mbili asubuhi jambo ambalo alitekeleza.

Alisema Sosopi aliwasili katika ofisi hiyo muda huo mara baada ya hapo alipelekwa kituo kikuu cha polisi ambako alihojiwa kwa muda wa saa moja na kisha kupelekwa rumande.

“Aliwasili kituoni tukiwa wote na alipofika alihojiwa kwa muda wa saa hivi na walipomaliza kumhoji walimpeleka rumande na kutueleza kuwa kama tunataka kumwekea dhamana tukamuone RCO, tumeenda kwa RCO ametuambiwa tufike kesho (leo) asubuhi,” alisema Mnyawami.

Akizungumzia ziara ya Sosopi, Mnyawami alisema ilikuwa ni vikao vya ndani na ilianza Juni 9 mwaka huu na kwamba hadi anazuiwa kuendelea na mikutano yake alikuwa ametembelea kata sita kati ya 13 jimboni humo.

Wakati Sosopi akijikuta katika mshikemshike huo, jijini Dar es Salaam Meya wa Ubungo, Boniface Jacob naye alijikuta akiangukia mikononi mwa polisi kwa kosa ambalo halijajulikana alipokuwa akijianda kwenda na waziri mkuu mstaafu, Frederick Sumaye kukagua miradi ya maendeleo ya Manispaa ya Ubungo.

Tukio hilo lilitokea jana saa sita mchana katika Makao Makuu ya Manispaa ya Ubungo yaliyopo Kibamba wakati Jacob akiwa katika msafara wa kuelekea kukagua miradi ya maendeleo akiwa na viongozi wenzake wa Chadema.

Askari wapatao wanne wakiwa katika gari aina ya Land Cruiser walifika katika eneo hilo kisha kuzuia msafara wa viongozi wa Chadema waliokuwa tayari kuanza ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya manispaa hiyo.

Baada ya kuzuia msafara huo, mmoja wa maofisa wa polisi alimfuata Jacob na kumweleza anamuhitaji kuambatana naye hadi Kituo cha Polisi Mbezi.

“Tunakuomba uongozane na sisi hadi kituoni, tuna maongezi na wewe yasiyozidi dakika 10 tukiridhika tunakuachia uendelee na shughuli zako,” alisema.

Ofisa huyo aliyejitambulisha kuwa Mkuu wa Kituo cha Polisi Mbezi alikwenda moja kwa moja hadi katika gari la Sumaye na kumweleza kuwa wanamuhitaji meya kwa dakika 10, kisha watamuachia.

Baada ya Jacob kuchukuliwa na polisi, Sumaye na viongozi wa Chadema waliendelea na ziara hiyo kwa kuanzia Shule ya Sekondari ya Matosa iliyopo Kata ya Goba.

Akiwa katika shule hiyo, Sumaye alisikitishwa na hatua hiyo na kusema huo ni mwendelezo wa uonevu dhidi ya viongozi wa upinzani na kwamba hatua hiyo inalenga kuwafanya baadhi ya watu kutojisikia huru katika nchi yao.

“Hili siyo jambo jema Serikali ivumilie, upinzani siyo uhalifu na wajue kuwa Chadema na viongozi wake ni chama halali na kinafanya kazi kama CCM. Habari ya kuwaandama watu wa Chadema kila mahali kitu hiki kinatusikitisha sana,” alisema Sumaye.

Alipotafutwa Kamanda wa Polisi wa Kinondoni, Suzan Kaganda simu yake ilipokelewa na msaidizi wake aliyejibu kamanda huyo yupo likizo na kwamba kaimu wake alikuwa zahanati.

Hayo yakitokea Iringa na Dar es Salaam kwa upande Kilimanjaro katika Wilaya ya Hai, kikao cha baraza la madiwani wa wilaya hiyo kiliendeshwa chini ya ulinzi wa polisi kutokana na amri ya kukamatwa kwa mwenyekiti na halmashauri hiyo, Helga Mchomvu (Chadema).

Kikao hicho kiliendeshwa chini ya ulinzi wa polisi baada ya polisi wa kituo cha polisi Bomang’ombe kumpelekea mwenyekiti wa halmashauri hiyo ujumbe wa kumtaka atoke nje kwa lengo la kumkata kumfikisha kituo cha polisi

Kufuatia hali hiyo, kikao hicho kiliendeshwa huku askari wa polisi wakiwa nje, wengine katika mlango wa kuingilia ukumbi wa halmashauri ambapo kikao hicho kilikuwa kikiendelea na ajenda zake za kawaida.

Kikao hicho kilichoanza saa 5:00 asubuhi na kumalizika saa 10:00 jioni kilimalizika huku polisi wakiendelea kumsubiria mwenyekiti huyo na kumtaka afike kituo cha polisi cha Bomang’ombe hali ambayo ilizua taaruki kwa madiwani na wananchi waliohudhuria kikao hicho.

Hali hiyo ilidumu kwa takribani dakika 20 kutokana na mwenyekiti huyo kutaka kujulishwa kosa la kutakiwa kufika kituo cha polisi, kitu ambacho askari hawakutaka kuweka wazi sababu ya kutakiwa kwake.

“Kama ni suala la kuharibiwa kwa miundombinu kwenye shamba la mbunge wa Hai sitanyamaza na huyo DC afanye maamuzi anayotaka lakini kama ni makosa nimefanya mtaani niko tayari kwenda polisi,”alisikika akisema.

Baada ya kikao hicho mwenyekiti huyo alichukuliwa na kupelekwa kituo cha polisi.

Imeandikwa na Geofrey Nyang’oro, Bakari Kiango na Fina Lyimo


Mbwana Samatta Afunguka Kuitajika na Timu Nyingine Ulaya...Lakini

$
0
0

Samatta akiri kuwa klabu kadhaa Ulaya zinamtaka lakini zitalazimika kusubiri hadi 2020 mkataba wake na KRC Genk utakapomalizika

Kimenuka IPTL...Dude Limeamshwa Patamu.....Magazeti ya Leo

JE Wajua Uzuri wa Mwanamke na Utamu Kwenye Tendo la Ngono si Chochote?

$
0
0
HUU NDIO USHAURI WANGU KWAKO
“UZURI WA MWANAMKE UNAWEZA UKAMPELEKEA MWANAUME AKATHUBUTU KUMUOA, LAKINI TABIA YAKE NDIO ITAKAYO MUAMURU ADUMU KWA MUDA GANI NA HUYU MWANAMKE KATIKA NDOA”.

Kuna Mambo Mengine Pesa Haiwezi Kununua Vitu Kama Heshima, Busara Na Upendo
NDUGU YANGU, “KUWA MTAMU KWENYE TENDO LA NGONO INAWEZA IKAMFANYA MWANAMUME ALALE NA WEWE USIKU KUCHA, LAKINI ASUBUHI AKAONDOKAZAKE, LAKINI KUWA MTAMU KWENYE TENDO LA TABIA, KUNAWEZA KUMFANYA MWANAMUME AKUOE NA ADUMU NA WEWE MPAKA KUFA.”

By Julius Peter Gontako

VIDEO:Tujikumbushe Kwa Ufupi Kuhusu Sakata la Kuchotwa Kwa Fedha Kutoka Katika Akaunti ya Tegeta Escrow Mwaka 2014.

$
0
0
Tujikumbushe kwa ufupi kuhusu sakata la kuchotwa kwa fedha kutoka katika akaunti ya Tegeta Escrow mwaka 2014.

Tazama hii VIDEO Inayoelezea Tukio zima la Tegeta Escrow Lilipoanzia"

Okoa Ndoa Yako Sasa, Ongeza Maumbile, Nguvu na Hamu ya Tendo la Ndoa Hata Kwa Wenye Kisukari

$
0
0

OKOA NDOA YAKO SASA. ONGEZA MAUMBILE, NGUVU NA HAMU YA TENDO LA NDOA HATA KWA WENYE KISUKARI. Tatizo la maumbile madogo, nguvu za kiume na ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limekuwa likiwasumbua wengi na kusababisha kushindwa kujiamini ktk tendo hivyo kusababisha ndoa nyingi kuvunjika pamoja na mahusiano. Upungufu wa nguvu na hamu ya tendo husababisha mambo kama:-

(a)Uume kulegea wakati wa tendo (b)Kukosa hamu ya tendo la ndoa (C)Kuwahi kufika kileleni (D)Uume kuchelewa kusimama baada ya round ya kwanza. (E)Kuchoka sana baada ya round moja n.k @Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo kwa kutumia bidhaa zilizotengenezwa kwa mimea na matunda zisizo na kemikali wala madhara na kuthibitishwa kiafya. Pata hizi:

1.HANDSOME UP ni kifaa chenye uwezo wa 99 % kuongeza uume (size unayohitaji) na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200000@200,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130000@130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130000@130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo hata mara 3 @130000@130,000/= Kwa Bidhaa hizi na nyingine kama:-
5.Kupunguza unene na manyama uzembe @150000@150,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi @130000@130,000/=
7.Kutengeneza shepu (hips, makalio na mapaja) @200000@200,000/= 8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni @120000@120,000/=
9.Kuwa mweupe na soft mwili mzima bila kuacha sugu 120,000/=
10.Kurudisha usichana (bikra) @120000@120,000/=
11.Kupunguza au kuongeza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120000@120,000/=

Wasiliana nasi kwa (+255) 0767447444 au 0714335378. 

NB: Matokeo ni uhakika na garantii na upate risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii. Follow us
@Markson_beauty_pr
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images