Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104687 articles
Browse latest View live

Mama wa Kizungu Atoka Rwanda Kuja Bongo ili Diamond Amwimbie Happy Birthday (Video)

$
0
0

Kama Diamond Platnumz angekutana na Eiden usiku wa kuamkia Jumamosi ya leo, huenda angemfanya mwanamke huyo wa kizungu kuwa mwenye furaha kuliko watu wote duniani. Mwanamke huyo ambaye usiku huo alikuwa akisherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutimiza miaka 32, anadai alisafiri kutoka nchini Rwanda kuja jijini Dar es Salaam ili amtafute hitmaker huyo wa ‘Number One’ amuimbie wimbo maalum wa siku ya kuzaliwa.
Bahati mbaya, mara tu baada ya kutumbuiza kwenye show ya Road to MAMA, aliwahi ndege ya kwenda jijini London, Uingereza kuwahi show yake na Ommy Dimpoz na kuizima ndoto ya Eiden.

“Mimi ni shabiki mkubwa zaidi wa Diamond duniani,” Eiden aliiambia Bongo5. “I want him to sing me happy birthday cause I am his number one fan and I’m not married I have no kids and I am not ashamed. I just love him and I think I feel like he needs to meet me, If he doesn’t meet me his life is not gonna be the same. I am incredible, if he doesn’t know me he is just gonna be a poor person in the world.”

Kimenuka Yanga, Mastaa Wapukutishwa

$
0
0
YANGA iko kwenye taratibu za kuachana na wachezaji wake mahiri ambao kuna uwezekano mkubwa wakatua Simba kwani baadhi yao wameshafanya mazungumzo ya awali Msimbazi. Wachezaji hao ni kiungo mwenye nguvu Athuman Idd ‘Chuji’, David Luhende, Juma Abdul na Ally Mustapha ‘Barthez’.

Lakini cha kushtua zaidi kipa mwenye heshima kubwa na rekodi ya aina yake nchini, Juma Kaseja yuko katika mazungumzo na uongozi wa Yanga akiwashawishi kusitisha mkataba wake wa mwaka mmoja kwa kile alichodai kwamba hana bahati na timu hiyo kwa sasa.

Kaseja ambaye hakuwa na wakati mzuri msimu uliopita jana Ijumaa alifuzu kozi ya awali ya ukocha na kupata alama ya daraja A katika mafunzo yaliyoanza Mei 5 mwaka huu katika Manispaa ya Morogoro.

Habari za uhakika kutoka kwenye kamati ya usajili zinasema Chuji anaachwa kutokana na nidhamu ndogo ingawa baadhi wanapinga na kusema kwamba ni mbadala mzuri wa Frank Domayo aliyesaini Azam.

Mbali na Chuji pia klabu hiyo imewachomoa Luhende na Abdul ambao awali waliudengulia uongozi wa klabu hiyo kuongeza mkataba huku Luhende ikiripotiwa kuwa amefanya mazungumzo na Simba ingawa hawana mpango nae sana kwavile aliwaringia awali wakafanya mazungumzo na Abdi Banda wa Coastal Union. Uongozi wa Simba umekiri kufanya mazungumzo na Barthez na watamalizana muda wowote.

Habari kutoka kwenye kamati ya usajili ya Yanga zinasema kuwa zaidi ya nusu ya wachezaji inaowahitaji imeshawapa mikataba mipya ambapo mchezaji wa mwisho alikuwa Mbuyu Twite. Kamati hiyo imepanga kupeleka baadhi ya wachezaji wenye mikataba kwa mikopo kwenye klabu zingine za Bara.

“Luhende Simba walimuhitaji kwa ada ya usajili ya Sh 6 Milioni na aichezee klabu hiyo ya Msimbazi kwa miezi sita lakini akagoma, alitaka aongezewe dau zaidi na Yanga pia aligoma kusaini yeye na Juma Abdul wote walikuwa mkumbo mmoja na Frank Domayo na Didier Kavumbagu,” kilisema chanzo chetu.

Habari za ndani zinadai kwamba Yanga ipo mbioni kuingia mkataba na Kelvin Edward wa JKT Ruvu na pia imepanga kuibomoa Mtibwa Sugar ingawa bado haijawekwa wazi ni kifaa gani.

Katika hatua nyingine, Mwanaspoti linajua kwamba mpaka jana Ijumaa Yanga ilikuwa imebaki na majina ya makocha watatu ambao ni kutoka katika nchi za Brazil, Uholanzi na  Ujerumani. Habari zinasema kwamba majina ya makocha hao yapo kwa Mwenyekiti Yusuf Manji ambaye ndiye atakayefanya uamuzi wa mwisho kwani tayari kocha Hans Pluijm ameshatoa sifa za makocha hao kabla hajaondoka alfajiri ya leo Jumamosi.

Makocha hao imeripotiwa kwamba mmoja wao anafanya kazi nchini Ghana na ana uzoefu mkubwa na mazingira ya Kiafrika ambapo atatua nchini na mchezaji mmoja anayecheza nafasi ya kiungo.

Afia Kaburini Baada ya Kunaswa na Kitu Akijaribu Kufukua ili Aibe Fuvu

$
0
0
Vyombo vya habari vya Nigeria vimeripoti habari ya mtu mmoja aliyekutwa amefia kaburini kwamba  alikubwa na umauti wakati akifanya jaribio la kufukua kaburi ili aibe fuvu la marehemu kwa ajili ya matumizi ya mambo ya kishirikina.

Kwa mujibu wa Saturday Tribune la Nigeria, tukio hilo limetokea katika mji wa Ilobu eneo oa Osun ambapo mtu huyo alikutwa akiwa amekufa huku nusu ya mwili wake ukiwa umeingia kaburini.

Mmoja wa wakazi wa eneo hilo ameeleza kuwa kijana huyo alikuwa na marafiki zake wengine waliokuwa wanafanya tukio hilo kwa lakini baada ya kuona mwenzao amenaswa ndani ya kaburi wakakimbia na kumuacha huku wao wakiwa salama.

“Mwili wake ulikutwa majira ya saa kumi na mbili na nusu asubuhi na kichwa chake kilikuwa kimefunikwa na tope. Wakazi wa eneo hili waliripoti polisi na walikuja baadae wakautoa mwili wake na kuuweka kwenye gari lao na kuondoka nae.” Alisema mkazi wa eneo hilo.

Saturday Tribune iliongea na kamishina wa Jeshi la Polisi wa eneo la Osun, Ibrahi Maishanu ambaye alieleza kuwa polisi watafanya uchunguzi wa kina kufuatia tukio hilo kufahamu nini hasa kilikuwa chanzo cha kifo chake. Na kwamba polisi hawajathibisha kuwa tukio hilo linatokana na masuala ya kishirikina

Producer Mtanzania Anaedaiwa Kuwa Mpenzi Mpya wa Nazizi Aeleza Jinsi Walivyokutana

$
0
0
Suala la 'nani ni mpenzi mpya wa Nazizi baada ya kuachana na mmewe' lilipata jibu pale ambapo mtayarishaji wa muziki wa Homeboyz records, mtanzania Hery Sappy alipotuma picha zilizojieleza kuwa yeye ndiye.

Hata hivyo, jibu hilo liliingiwa shaka Nazizi alipoulizwa kuhusu hilo; alikanusha na kudai kuwa wao ni marafiki tu na walipiga picha kawaida na kwamba zipo picha nyingi hata zaidi ya hizo.

Nina marafiki wengi wa kiume, tunapiga picha kila mahali. Hivyo ndivyo uhusiano wangu na marafiki zangu ulivyo.” Nazizi aliiambia Nairobi News  March mwaka huu.

Producer Sappy amefunguka kuhusu jinsi walivyokutana na First Lady wa Necessary Noise.

Akiongea na Pulse, Sappy amesema kuwa walikutana October mwaka jana  baada ya Nazizi kufika Homeboyz kukutana na mtayarishaji maarufu ambaye alikuwa anapika hits kadhaa pale.

Ikiwa ni mara ya kwanza kukutana Sappy anaeleza kuwa walizungumza kuhusu kumtayarishia albam nzima na kwamba baada ya hapo hawakukutana hadi February.

"We met back in October when she came to Homeboyz to meet a famous producer who had been churning out hits. We met and talked about her intentions to have me produce her album. We did not meet again as she was still relocating to Kitengela from Lamu. We hooked up again in February and it has been bliss ever since." Amesema Sappy.

Sappy alikazia wakati anajibu swali kuwa Nazizi ameteka umakini na mizuka yake.

Source: Ghafla

Ndoa ya Kanye West na Kim Kardashian sasa Kufungwa Italia na si Ufaransa

$
0
0

Ripoti mpya zinadai kuwa harusi ya rapper Kanye West na mama wa mwanaye Kim Kardashian sasa itafanyika Italia na sio Paris, Ufaransa kama ilivyodhaniwa awali.

Entertainment Tonight imeripoti kuwa wageni waalikwa watakusanyika pamoja Paris, Ufaransa May 23 kwaajili ya chakula cha usiku ‘Pre wedding dinner’, na baada ya hapo couple hiyo itawasafirisha wageni wote kwa ndege binafsi tofauti kuwapeleka Florence, Italy ambako sherehe rasmi ya ndoa yao itafanyika.

Kumekuwa na habari mbalimbali kuhusu ndoa ya Kanye na Kim, huku wengine wakidai kuwa couple hiyo tayari imeshafunga ndoa, habari ambazo Kim Kardashian amezikanusha hivi karibuni kupitia twitter kuwa bado hawajafunga ndoa.

Diamond Mpaka Sasa Anaongoza Kwa Kura BET Awards..Piga Kura Hapa Sasa Hivi

$
0
0
Ni siku chache tu zilizopita toka Diamond Platnumz ametangazwa kuwania tuzo za kituo cha Television cha Marekani BET akiwa ni msanii pekee kutoka Afrika Mashariki kuchaguliwa kuwania tuzo hiyo huku wengine wakitoka Nigeria, Ghana na Togo. (Best International Act: Africa )
Good news ni kwamba katika mchakato wa kura sasa hivi Diamond ameshika nafasi ya Kwanza katika list ya Wasanii wote sita ambapo kama Watanzania wataendelea kumpigia kura kwa kasi na kumzungumzia kwenye mitandao ya kijamii basi anaweza Kushinda Tuzo Hiyo..

Msimamo Upo Hivi Kwa Sasa 

Ukitaka Kumuongezea Kura Diamond Basi na wewe Piga Kura Hapa: Bonyeza <<BET>>

Picture of The Day..Studio Time With My Producer

$
0
0
Can you Guess who is This Gal ? Tip: Ni Mbongo Flava Akiwa Studio Akifanya Yake..

"Jose Mourinho is a fool for questioning my age' - Samuel Eto'o

$
0
0
Well, Sameul Eto'o can talk now because his contract with Chelsea is finished. He's finally responded to his former coach Jose Mourinho's comments about him being older than 33. Speaking with reporters in Abidjan yesterday, the 3-time African footballer of the year called Mourinho a fool for questioning his age
"I am 33 years old. And it is not because a fool called me an old man that you must believe it. And you may have noticed that the old man was better than the youngsters.'
Eto'o also hinted that he will play for a European club next season rather than sign a lucrative deal in the Middle East. "Some believe I am going to retire in the US or the Middle East, but I have regained the joy of the Champions League and I am going to carry on playing in the Champions League."

VIDEO: Masogange Ayatikisa Makalio Yake Kwa Makusudi Mbele ya Wazungu

$
0
0
Kwa mara nyingine tena mwanadada Agnes Masogange amerekodiwa na watu wake akiwa anatembea kwa kuyatingisha makalio yake akiwa nchi za mbele....Hii sio mara ya kwanza kufanya hivi...alishafanya VIDEO kadhaa akiwa hapa bongo [
Hii yasasa hivi ndio funga kazi kwani amebadilisha mitembeo kama mitatu hivi ....Nouma kweli!!!

Sahau kuhusu Vera Sidika, Corazon Kwamboka, Risper Faith na hata Agnes Masogange...Kutana na Jey'nel Dorothy

$
0
0

Hapa East Africa kuma ma Model wasiozidi wa tano ambao wanatikisa mitandaoni.....ambao ni Vera Sidika, Corazon Kwamboka, Risper Faith hawa wote kutoka nchini Kenya...Nakwahapa bongo tunajivunia Agnes Masogange......

Sasa believe me or not! ujio wa huyu model mpya Jey'nel Dorothy kutoka Kenya amekuwa tishishio kwa hawa wote.

Daktari Asahau Kitambaa Tumboni Wakati Akimfanyia Mzazi Operation..Kizazi Chaoza

$
0
0
MKAZI wa wilaya ya Urambo mkoani Tabora, Mwamini Adamu ametolewa mfuko wa kizazi na kukatwa sehemu ya utumbo baada ya mganga wa idara ya upasuaji katika wilaya hiyo kusahau kitambaa tumboni kwa mwanamama huyo wakati akijifungua.

Kutokana na kumsababishia ulemavu huo kwa uzembe, Mwamini ameifikisha Halmashauri ya wilaya ya Urambo kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Magharibi akidai fidia ya Sh milioni 500.

Mwamini ambaye anadai kuwa alipwe kiasi hicho cha fedha kutokana na uzembe wa uliofanywa na Dk Jacob Kamanda aliyemfanyia upasuaji wakati wa kujifungua na kumsababishia aondolewe mfuko wa kizazi pamoja na kukatwa utumbo.

Mwamini pamoja na mumewe Idrisa Jafari katika madai yao wametaka walipwe fedha hizo kutokana na makosa ya uzembe uliofanywa na wataalamu wa upasuaji kwa kuacha kitambaa tumboni mwa mama huyo.

Akitoa ushahidi wake mbele ya Jaji Amir Mruma jana, mama huyo alidai kuwa Januari 6 mwaka 2011 alijifungua kwa upasuaji baada ya hapo hali yake ilizidi kuwa mbaya huku akitokwa usaha ukeni na sehemu ya tumbo kwenye mshono.

Huku akiongozwa na wakili wa kujitegemea Mussa Kwikima, mama huyo aliiambia mahakama kuwa hali hiyo ilifanya apelekwe hospitali ya mkoa wa Tabora Kitete bila mafanikio ndipo ikamlazimu kwenda Itigi kwa matibabu zaidi.

Katika uchunguzi wa kitaalamu uliofanywa na madaktari bingwa, Haile Sales ambaye ni raia wa Italia pamoja na Anatole Lukonge wa hospitali hiyo ya Itigi, waligundua kuwa kuna kitu tumboni kama uvimbe hivyo wakalazimika kumfanyia upasuaji mwingine.

Baada ya upasuaji huo walikuta kitambaa cha rangi ya kijani ambacho kilikuwa kimeozesha mfuko wa uzazi pamoja na utumbo kugandana na kitambaa hicho ikabidi kitambaa hicho kutolewa na kusababisha kupasuka kwa utumbo ili kumnusuru maisha yake.

Naye daktari bingwa wa magonjwa ya akinamama na ambaye ni mganga mkuu wa hospitali ya Itigi, Anatory Lukonge katika ushahidi wake ameiambia mahakama hiyo kuwa alimpokea mlalamikaji akiwa anatokwa na usaha ukeni na sehemu iliyoshonwa.

Dk Lukonge amebainisha kwamba walipomfanyia upasuaji mama huyo, walikuta utumbo umeshikana na mfuko wa uzazi huku kukiwa na kitambaa kimeng’ang’ania juu yake.

Alisema wakati walipojaribu kukiondoa kitambaa hicho kibofu cha mkojo kilipasuka wakalazimika kumuwekea mpira ili uweze kumsaidia kutolea uchafu.

Kesi hiyo ya madai namba 13/2011 imeahirishwa hadi Agosti tatu mwaka huu itakapoendelea kusikilizwa kwa upande wa utetezi kuleta mashahidi wake.

Wanaouza na Kuwafanyisha Biashara ya Umalaya Wasichana China Wanaswa

$
0
0
BAADA ya kuwepo malalamiko ya wasichana wadogo wa nchini kusafirishwa kwenda China kutumikishwa katika biashara ya ngono pamoja na dawa za kulevya, sasa serikali imenasa mtandao huo.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe alitoa taarifa hiyo juzi bungeni wakati akihitimisha michango kuhusu bajeti yake kwa mwaka wa fedha 2014/15 iliyopitishwa.

Chikawe ambaye hata hivyo hakufafanua kwa undani wa mtandao huo ulivyokamatwa, alieleza Bunge namna watoto hao wanavyopatikana kabla ya kufikishwa nchi hiyo ya nje.

Kwa mujibu wa Waziri, watu hao wamekuwa wakichukua watoto wadogo na kuwaambia kwamba wanawapeleka China hususani mji wa Guanzhou kuwaajiri kwenye saluni na maduka.

Alisema kinara wa usafirishaji amekuwa akitambuliwa kwa jina la ‘Mama’ ambaye baada ya kufika nchini humo, huwanyang’anya watoto hao hati zao za kusafiria. Imebainika zipo hata wakala zinazojihusisha na biashara hiyo haramu ya binadamu.

“Wakifika, Mama anawanyang’anya pasipoti zao. Anawaambia ili kuwarudishia, lazima watimize masharti ya kumpa kati ya dola 8,000 na 10,000 baada ya kutumika katika vitendo vya ngono,” alisema Waziri Chikawe.

Aliendelea kueleza kuwa wanaposhindwa kutimiza masharti hayo, hukutana na Wanigeria ambao huwapa hati bandia za kusafiria na kisha kuwaingiza katika biashara ya kusafirisha dawa za kulevya kwenda nchi mbalimbali.

“Tumenasa mtandao huu…polisi imenasa mtandao,” alisema Waziri na kutoa mfano kwamba hivi karibuni, alikamatwa mtu akiwa na hati ya kusafiria akimpelekea binti mmoja. Alisema binti huyo alipoulizwa juu ya hati hiyo, alikuwa hafahamu anakokwenda.

Awali, taarifa juu ya kuwepo usafirishaji wa wasichana wadogo kwenda China kwa ajili ya kutumikishwa katika ngono, ilitolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe baada ya kutoka ziarani nchini humo.

Membe alisema serikali inashirikiana na ubalozi wa China katika kubaini wahusika wa biashara hiyo sanjari na mkakati wa kuhakikisha wasichana hao wanarudishwa nchini.

Akielezea mikakati ya serikali katika kukabili biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu, Waziri Chikawe alisema katika mwaka wa fedha 2013/2014 Sekretarieti ya kupambana na biashara hiyo imeratibu vikao vinne vya Kamati ya kupambana nayo.

Aidha imeandaa kitabu cha anuani na majina ya watoa huduma kwa waathirika wa biashara haramu ya usafirishaji binadamu na vilevile kutengeneza rasimu ya kanuni za sheria ya kupambana na biashara hiyo nchini.

Katika mwaka wa fedha 2014/2015 sekretarieti itakamilisha kutengeneza kanuni za Sheria ya kupambana na biashara hiyo ya mwaka 2008. Pia itatoa elimu na kuimarisha mikakati ya kupambana na biashara hiyo ya kusafirisha binadamu.

Watanzania zaidi ya 100 wakiwemo wasichana 20 wamedaiwa wapo gerezani nchini China wakijihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Kufa kufaana, Tanzania itumie Wakati Huu wa Machafuko Kenya Kujitangaza Utalii.

$
0
0
Kama mjuavyo, majirani zetu wanasumbuliwa na magaidi wa alshabaab ambao wako bize kulipua mabomu kila sehemu Kenya na kuifanya nchi hiyo kutokuwa salama tena.

Inasikitisha sana, lakini nadhani ni wakati sasa tutumie mwanya huu kudumisha amani yetu na kujitangaza kwa nguvu zote kwenye sekta ya utalii.

Tanzania ina vivutio vingi na vikubwa vya utalii zaidi ya Kenya, na kwa sasa nchi zote za magharibi zinawaonya raia wake wasiende Kenya. Kipindi cha holidays kwa nchi za magharibi ni kuanzia july, badala ya kwenda Kenya tuwavute kwetu.

Lakini serikali ibabidi idhibiti vidumu vya tindikali kule kwa wazee wa urojo...

Dr Slaa: 2015 Upinzani Tutamsimamisha Mgombea Mmoja Urais

$
0
0
Akihutubia maelfu ya wakazi wa jiji la arusha mapema jana katika mkutano wa [ukawa]katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo,chadema,dr wilbod slaa, alisema,tumefikia makubaliano kama [ukawa] 2015 kumsimamisha mgombea 1 katika nafasi ya urais,lengo letu sio kutafuta vyeo bali kuwakomboa wananchi watanzania waliopigika na mfumo wa chama cha mapinduzi,nilifarijika sana niliposikia maneno haya kutoka kinywani mwake,maana ndio mwisho wa chama cha mapinduzi umewadia,kimsingi ni kujipanga bara bara kusuka kikosi kazi kitakacho fanya kazi ya ziada kuhakikisha ccm haifurukuti kabisa,bg up [ukawa] pa1tutashinda,

Mpenzi Wangu Ananinyonya Nyuma..Sipendi Nashindwa Nimzuie Vipi..Ushauri Please

$
0
0
Mimi nimeolewa miaka 8 iliyopita
nna watoto watu na mume wangu
nnampenda na yeye ananipenda
niliolewa nikiwa na miaka 19 ni
hadith ndefu naomba uchukuwe
muda kuisoma, aliniona through
family friend akanipenda na mimi
sikuona vibaya kuolea naye japo
amenizidi umri kidogo nilikubali
na kusema ndoa siyo jela
ntajaribu nikishindwa ntarudi
kwetu.
siku ya harusi ikafika ndoa
ikapita usiku ule wa ndoa
tukaenda hotel tulipofika
akaniuliza kabla hajaniingili kama
nilikuwa bikira au kazi
nimeshaianza yeye kanipenda
miye na siyo bikira yangu
itakavyo kuwa nimeshakuwa
mkewe, na mimi I was just 19 at
the time na nilikuwa sijawahi
kufanya hilo tendo ni msichana
nnae penda dini yangu nikawa
nasubiri the right man na the
right man akaja, basi
nikamuambia sijawahi,
alinikumbatia for more than
10min akiniambia pole sana
ndon't worry every thing will be
ok kutokea hapo to cut the story
short ilimchukuwa two week
kuniingilia hakutaka niumie ni
mwanaume mwenye huruma sana
na mahaba.
lakini kinachoniumiza kitchwa ni
hiki mapenzi anayonifanyia
kitandani ni ya ajabu sana akitaka
kuniinigilia atachukuwa zaidi ya
saa moja kunichezaa wich I don't
complain ila anavyonichezea ndio
hatari akinianza kuninyonya ----
huwa anapenda kuninyonya na
nyuma kunitia ulimi wake au
vidole na wakati akinifanya hivyo
ni mimi raha zimehsanikolea
nikiogopa siku za mwanzo lakini
akaniambia wewe mke wangu na
mimi ni mumeo naomba niamini
sintokufanya tendo baya kinyume
na matakwa yako kama unasikia
raha enjoy kwani mimi ndio raha
zangu naona raha hivi nnanavyo
kuchezea naomba na wewe
starehe basi Rosemary mpaka
nimezowea na nnaona raha mno
kutiwa ulimi ndani ya ------ na
vidole na akinitia vidole huwa
anatumia special oil ambayo
inanifanya nione raha.
Sasa aliponiowa hakuniingialia for
two weeks alikuwa akinichezea tu
mpaka siku nilipomuambia anipe
yote ndipo alipo nibikiri sasa na
huu mchezo wake nnaona lengo
lake lile kuwa raha nnazo zipata
kwa chezewa mbele na nyuma
kwa wakati mmoja mwisho wake
kama siyo mzuri japo kuwa mimi
mwenyewe nikitu ambacho
sikitaki wala sikipendi lakini
kilipoanzi na kufukia hapa
nnaogopa, sijuwi nta ki stopisha
vipi.

swali langu ni hili ni mimi
nnamfikiria vibaya au na wewe
unamuonaje mtu huyu kwani ni
mwanaume wa kwanza kuniingilia
na sijapatapo kutoka nje kuona
wengine wanafanya vipi, na hapa
tulipofikia ntamstopisha vipi
kwani nna muona anavyo
hangaika na ku -enjoy wakati
akinichezea nyuma mungu anajua.
Naomba ushauri wako kwani
alipoanza alianza kidogo kidogo
tena huwa ananiuliza unasikia
raha na kweli nasikia raha tena
kwa muda mwinigine anaongeza
sehemu nyingine kunitekenya na
kuniuliza kama nasikia raha na
kweli raha ipo mpaka hapa
tulipofikia naona kama tunaenda
kubaya kwani anavyonichezea
huwa kunatekenya mbele na
nyuma utamu naomba misaada
wako nifanye nini miye.

Lowassa Alipigwa Marufuku Kuendesha Harambee, Sitta Anagawa Pikipiki na Baiskeli Anaangaliwa Tu

$
0
0
Mh. EL alipigwa stop na chama chake shughuli mbalimbali za kijamii ikiwamo ya kuendesha harambee kwa tafsiri kuwa, ni dalili za rushwa kwa ajili ya kusaka uraisi. Je mbunge wa Irambo, Waziri wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa BMK pamoja na mkewe kugawa pikipiki 16 na baiskeli 95 kwa viongozi wa chama chake ni nini?

Nayo ni kama ya Lowassa na wenzake tu. Kitu kimoja kinachonishangaza ni kuwa CCM iliona kuanzia lini kuwa ile ni rushwa. mbona wote wamefanya hayo hayo? Mbona wamekuwa wanagawa uji, pombe, unga na wali kwa miaka mingi tu? Mbona wana tabia ya kugawa nguo na hela ndogondogo? Au inakuwa siyo rushwa wakati wa uchaguzi ukifika, ila sasa ndiyo rushwa?

Mi nadhani waache unafiki tu. Kama jini umelinunua mwenyewe usilalamike likianza kula wanao! Vinginevyo my concern wananchi,ambao kila siku wanahongwa uji, wali na vichenji vichache, ili wauze kura zao. Unanunuliwa kwa sahani ya wali ya mlo mmoja,halafu unavumilia maumivu ya maisha duni kwa miaka 5!

Nadhani Watanzania ni watu wa ajabu sana! Nadhaninikiwa namalizia masters itabidi research iwe ni "mentality ya Tanzania"
Source:JF

Marekani Kuhamishia Shughuli Zake Tanzania Kutoka Kenya!

$
0
0

Serikali ya Marekani imesema itapunguza wafanyakazi katika ubalozi wake nchini Kenya kutokana na kitisho cha ugaidi.


Marekani imechukua hatua hiyo baada ya vitisho na mashambulizi ya kigaidi kuzidi kupamba moto nchini Kenya, ambapo jana watu 10 walikufa na wengine wengi kujeruhiwa kutoana na bomu lililolipuka jijini Nairobi.

Marekani imesema itahamishia baadhi y shughuli zake nchini Tanzania au Ethiaopia.

Source: DW Habari.

Ugaidi ni hatari sana. Haya makundi yanayozidi kuchanua kila siku sijui Dunia inaelekea wapi?

Majanga:Bango la Matangazo Barabarani Laangukia Gari Round About Kawe

$
0
0

Serikali ipige marufuku makampuni ya kutengeneza Mabango kuweka mabango karibu na Barabara ya wekwe mbali na barabara mita 20 kutoka Barabara kuu hili limeanguka Round about ya Royal Oven njia ya kwenda Lugalo Golf course (Avacado)Na hii siyo mara yakwanza mabango kuanguka kunasiku pale katika ya seilender bridge na Kinondoni lilianguka uzuri kulikuwa katika mikoko!

Updates: Kwanini Shabiki wa Diamond Platnumz Hutomwezesha Ashinde Tuzo za BET

$
0
0
Bila shaka umeshakutana na tweets au picha kwenye Instagram inayoonesha upigaji kura wa tuzo za BET ambapo kwenye kipengele cha Best International Act: Africa, Diamond anaonekana kuongoza. Well, ni good news kwa mashabiki wake lakini bad news ni kuwa kura hizo hazihusiki kabisa na kura zenyewe za BET kumpata mshindi.

Kituo cha redio cha V101.9 cha Marekani kimetengeneza utaratibu wake mwenyewe wa kuwapa nafasi wasikilizaji na wasomaji wake kumpigia kura msanii wanayempenda na kura hizo zitaishia kuwapa wao picha ya namna wasomaji wanapendekeza washindi wao. Kufanya hivyo ni rahisi sana na hata sisi tukiamua kutengeneza ballots systems kama hizi ingewezekana.

Utaratibu wa tuzo za BET upo tofauti kabisa na unaotumika kwenye tuzo zingine kama CHOAMVA ama MTV MAMA ambapo baada ya majina kutangazwa, mashabiki huwapigia kura wasanii wanaowapenda.

Kwenye tuzo za BET kuna jopo ama academy maalum yenye watu takriban 500 ambao ni wadau wa kiwanda cha muziki, habari na bloggers. BET huwataka watu hawa kupendekeza majina kwenye kila kipengele kwa mfumo wa kupiga kura ‘electronically’.

Kura hizi husimamiwa na kundi liitwalo “Yangaroo” ambalo hufanya kazi kwenye tuzo zingine pia. Kundi hili hupunguza majina na kubakiza wasanii watano kwenye kila kipengele na kuyatuma tena majina hayo (ambayo hutagazwa sasa rasmi kama majina ya mwaka husika) na kuyarudisha tena kwenye academy hiyo itakayopiga kura za mwisho kupata mshindi.

Habari njema ni kuwa, Vanessa Mdee pia ni miongoni mwa member wa academy hiyo. Hivyo bila wasiwasi atampigia Diamond. Haijulikani kuna members wangapi Afrika Mashariki ambao kiuzalendo watatakiwa kumpigia kura Diamond.

Bongo5.com

Mapenzi ya Rihanna na Drake Yadaiwa Kwenda Likizo kwa Mara Nyingine

$
0
0
Imeripotiwa kuwa Drake na Rihanna ambao walionekana kurudisha mapenzi yao kwa miezi michache iliyopita, inasemekana wawili hao wamerudi tena likizo ya mapenzi.

Chanzo kimeiambia US Weekly kuwa Riri na Drizzy walikuwa na ugomvi mwingine tana hivi karibuni kutokana na Drake kuwa na mapenzi mengi kwa Rihanna, kilisema chanzo hicho.

Couple hiyo yenye historia ya kuwa On na Off kwa muda mrefu ilianza kuonesha uhai mpya wa mapenzi yao walipokutana Paris, Ufaransa mwezi February, ambapo Riri alihudhuria show ya Drake, na baada ya hapo wakawa wanaonekana pamoja mara kwa mara.
Viewing all 104687 articles
Browse latest View live




Latest Images