Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Kanuni Kumi '10' za Kuwa Mke Mwema Katika Ndoa

0
0
UHALISI WA MAISHA:
Maisha halisi ya mwanamke anayetarajia kuwa mke/ mke tayari hii ni kumaanisha kuwa wanawake mashujaa tunapaswa kuishi maisha ambayo yanatutambulisha kama mfano wa kuigwa ili tunapozungumza na kufundisha mabadiliko tuwe tunazungumza uhalisia wa maisha yetu ambao unajengwa na haya yafuatayo;

UVUMILIVU:
Kuwa mvumilivu katika maisha yake ya kila siku hasa ukizingatia kuwa tunakutana na mambo mbali mbali yasiyotuvutia katika mahusiano yetu, mengine ni magumu na yanayokwenda kinyume kabisa na matakwa yetu au mazoea yetu ya binafsi. Ifahamike kwamba wewe kama mwanamke shujaa inapotokea umekutana na mambo kama haya hupaswi kuonyesha hasira zako wazi wazi kama vile; chuki, kulaumu, ugomvi, vurugu, malalamiko, manung’uniko, machafuko, kulipa kisasi au aina yoyote ya uharibifu kutokea kwako au ndani mwako. Hivyo mwanamke shujaa huwa ni heri kila anapokuwa kwani hutunza amani ya eneo alipo.

UPENDO WA DHATI:
Maisha ya upendo wa halisi na sio wa kinafki kwa jamii inayomzunguka. Tabia ya upendo wa halisi ina thamani kubwa sana kuliko mali nyingi, pesa, elimu ya juu n.k. wewe unaweza kabisa kuwa na elimu ya juu sana na pesa nyingi sana lakini pasipo upendo wa halisi ni sawa na kusema kopo zuri kwa nje na ndani hamna kitu. Nguzo kuu ya maisha ya mwanamke shujaa ni Upendo wa dhati na uhalisia.

UTII KWA KWA JAMII:
Maisha halisi ya utii katika jamii inayokuzunguka  ili kuweza kuyafanyia kazi yale yote uliyojifunza na pia kuyatenda kwa ufasaha pasipo kupita kona yoyote. Utii  kwa jamii ni ufunguo mmoja wapo utakaokusaidia kufanikisha mambo yako na malengo yako kama mwanamke shujaa.

UAMINIFU KATIKA JAMII:
Kuishi maisha ya uaminifu wa kweli na uhalisia katika jamii inayomzunguka. Uaminifu wa kweli huonekana nyakati zote na siyo tu wakati mtu anapokuwa mbele za watu wanaomjua bali hata wale wasiomjua na hata anapokuwa mahali peke yake aweze kutunza uaminifu wake kwa faida ya jamii nzima. Mwanamke shujaa hujitahidi sana kutunza uaminifu wake katika sekta zote.

UNYENYEKEVU WA KWELI:
Kuishi maisha halisi kabisa ya unyenyekevu kwa jamii inayomzunguka, unyenyekevu ni kinyume kabisa na kiburi, majivuno, kujigamba, kujikweza, kujiinua, kujiona,na hata kjitanguliza mbele kwa kila jambo. Mwanamke shujaa huwa ni mnyenyekevu wakati wote na hana makuu daima.

UWAJIBIKAJI WA DHATI:
Maisha halisi ya uwajibikaji akiangalia majukumu yake yote yanayomkabili na kuhakikisha anafanya kwa moyo bila kuwa na tabia ya kusaidiwa majukumu yake. Mwanamke shujaa ni mfano wa kuigwa kutokana na uwajibikaji wake.

USHIRIKIANO WA DHATI:
Ushirikiano katika jamii inayomzunguka. Sisi wanawake mashujaa yatupasa kujua dhahiri kuwa kazi ya kubadili tabia na kufanya wengine wabadilike kwa lengo la kupata familia bora ni lazima kuwa na ushirikiano wa kweli ambao utajenga tabia ya kuaminiana na kunai mamoja katika harakati hizi za kuandaa/ kujenga familia bora.

UTARATIBU WA KAZI/MPANGILIO:
Katika utaratibu wa maisha yake, pamoja na mpangilio mzuri wa mambo yanayomzunguka hii itakusaidia kuwa na muda mzuri wa kufanya shughuli zako na pia kutekeleza majukumu yako ya kila siku kama mwanamke shujaa. Hakuna njia yoyote ya kukuwezesha kukua na kuendelea katika maisha yako bila kuwa na utaratibu na mpangilio wa mambo yako.

KUFANYA TATHIMINI:
Kuweza kufanya tathimini ya yale yote anayoyafanya katika maisha yake ya kila siku, pengine ni mfanyabiashara, mfanyakazi, mkulima n.k kama mwanamke shujaa yakupasa kutathimini shughuli zako kama zina leta faida/hasara kwa familia na jamii yako inayokuzunguka. Ukiona faida ni kubwa unaendelea na hiyo shughuli lakini kama hasara ni kubwa unajiweka katika nafasi ya kubadilisha aina ya shughuli mara moja bila kupoteza wakati.

Soma Nafasi Mbali Mbali za Kazi Zilizotangazwa leo

Wananchi Bukombe Waomba Rais Magufuli Aongezewe Muda wa Kukaa Madarakani

0
0
Wananchi wa vijiji vya Bulangwa na Katente mkoani Geita,wameliomba Bunge la Tanzania kufanya marekebisho ya muda wa ukomo wa urais kutoka miaka kumi ya sasa hadi miaka ishirini ili kumuwezesha Rais Dk.John Pombe Magufuli kuendelea kubakia madarakani.

Wananchi hao walitoa ushauri huo jana katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na mbunge wa jimbo la bukombe mh. Dotto biteko kwa ajili ya kumpongeza Rais Dk.John Pombe Magufuli kwa namna alivyosimamia sekta ya madini,mkutano ambao ulihudhuriwa na Mbunge wa Jimbo la Geita mjini Mh.Costantine Kanyasu.

Akiwahutubia wananchi,Mbunge wa Jimbo la Bukombe ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya Nishati na Madini Mh. Dotto Biteko,alisema kazi ya kupigania rasilimali za taifa inayofanywa na Rais Dk. John Pombe Magufuli si ya lelemama,huku Mbunge wa Jimbo la Geita mjini Mh. Kanyasu akisema serikali ya awamu ya tano haiwachukii wawekezaji, bali inawachukia waporaji wa raslimali za nchi.

Ripoti ya kamati ya pili ya mchanga wa madini wa Makinikia,iliyowasilishwa Juni 12 mwaka huu kwa Rais Magufuli na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Prof.Nehemiah Ossoro ilibaini taifa kupoteza shilingi Trilioni 252 kupitia usafirishaji wa mchanga wa madini ya makinikia nje ya nchi kuanzia mwaka 1998 hadi kufikia mwaka huu,huku ikiwahusisha baadhi ya mawaziri wa zamani wa nishati na madini waliohusika kuingia mikataba mibovu iliyoisababishia serikali hasara.

Kutana na Maalim Fadhil Rashid Kutoka Komoro ni Mtaalam wa Tiba za Asili Anayetibu Magonjwa Yafuatayo

0
0

KUTANA NA MAALIM FADHIL RASHID KUTOKA KOMORO NI MTAALAM WA TIBA ZA ASILI

UNASHIDA NA MCHUMBA UNATATIZO PESA HAIKAI KURUDISHA MUME AU MKE KWA MUDA MFUPI MVUTO WA MAPENZI

MVUTO WA BIASHARA KUMSHIKA MUME AU MKE ASIKUSUMBUE

DAWA YA ( LIMBWATA )KUMTAWALA MPENZI WAKO KWA SABABU MAALUM

KUSAFISHA NYOTA ILI UWE NA MUONEKANO

NA PIA ANATOA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA PESA BILA MASHARTI

NA KUMILIKI MALI DAWA YA KUONGEZA UUME SAIZ UIPENDAYO

DAWA YA NGUVU ZA KIUME INAPATIKANA PIA ANAYO DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEP KUA NA UMBO BOMBA UMEIBIWA AU KUDHURUMIWA UTARUDISHIWA MALI YAKO NDANI YA MASAA 24 ANAFUNGA KESI NA KUPATA HAKI YAKO

DAWA YA MVUTO WA BIASHARA KUUZA MALI YAKO KWA HARAKA KUZUIA CHUMA ULETE

NA KUONDOA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI ACHA KUTESEKA ACHA KUHANGAIKA MAALIM FADHIL RASHID

YUPO TANZANIA KWA AJIALI YAKO. CALL...+255719362806/
+255763276239

WhatsApp IMO +255785786436

Magufuli Alichowafanyia Vigogo Hawa Haijawai Kutokea

0
0
Ikiwa ni siku 593 kamili tangu Rais Dk. John Pombe Magufuli (pichani) aingie madarakani Novemba 5, 2015, serikali yake imevunja utaratibu na mazoea ya miaka mingi, baada ya kuchukua maamuzi magumu ambayo hayakuangalia sura, cheo, hadhi wala utajiri wa mtu katika kulinda na kutetea masilahi ya taifa, UWAZI, limegundua.

Kamishna Mkuu Mstaafu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya (katikati) sambamba na Waliokuwa Wafanyakazi wa Benki ya StanBic Tanzania, Sioi Sumari (kushoto) na Shose Sinare (kulia) wakiwa mahakamani.

ILIVYOKUWA HAPO AWALI

Kabla ya Rais Magufuli kuingia madarakani, kulikuwa na mazoea ya kuamini kuwa watu wenye nyadhifa nzito katika mashirika ya umma, serikalini au matajiri wasingeweza kuonja shubiri za vyombo vya dola, kutokana na kukithiri kwa tabia ya kulindana kutegemea na cheo au hadhi ya mtu.

Mgawe na wenzake watatu wakifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
“Unanijua mimi ni nani?” Haya yalikuwa ni maneno ya kawaida kutamkwa na mabosi wengi walipohitaji kuwatisha watendaji wa serikali katika kutimiza majukumu yao, kama vile kudai kodi, kuhimiza utekelezaji wa matakwa ya kijamii na mambo mengine kadha wa kadha.

Aidha, halikuwa jambo la kawaida kwa kigogo wa taasisi kubwa, mathalan meneja,mkurugenzi au tajiri, kushikiliwa na vyombo vya dola kwa muda mrefu, kwani simu zingepigwa kutoka ‘juu’ na mara moja mtu angekuwa huru uraiani, kitu ambacho kilichangia sana kuwepo kwa jeuri miongoni mwa wenye fedha, vyeo na hadhi huku wananchi wa kawaida wakiishi kinyonge na kuweka mazingira ya kuonewa na kudhulumiwa.

JPM SASA ALIVYOMALIZA ‘MAZOEA’

Ujio wa Rais Magufuli umeleta mabadiliko mengi yenye tija kwa wananchi wa kawaida, kwani siyo tu utu na haki yao imewekwa mbele, bali mazoea ya watu kutumia majina, hadhi na utajiri wao yamefikia mwisho, kwani sheria imekuwa ni msumeno unaokata pande zote.

Aidha, ile tabia ya viongozi wa serikali, walioharibu huku kuhamishiwa kule nayo imekoma, kwani mara kadhaa, amechukua maamuzi magumu kiasi cha kuwashangaza wengi.

WATEULE WAKE WAONJA JOTO YA JIWE

Tofauti na ilivyozoeleka katika uongozi wa marais Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete, katika utawala wake Rais Magufuli amewatoa kazini viongozi walioaminika kuwa ni watu wake wa karibu, huku akisisitiza kuwa katika masilahi ya taifa, hana urafiki.

Kiongozi wa kwanza kuonja joto ya jiwe ni aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, ambaye alitolewa katika nafasi yake kwa makosa ya kimaadili, baada ya kudaiwa kuingia bungeni kufanya kazi ya serikali akiwa amelewa.

Baadaye akafuata Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga wakati huo, Anna Kilango Malecela ambaye alijikuta akipoteza nafasi yake baada ya kutoa tamko kuwa katika mkoa huo, hakukuwa na wafanyakazi hewa, jambo ambalo halikumridhisha kiongozi huyo wa nchi. Baadaye kulibainika kuwepo kwa watumishi kadhaa hewa, akatumbuliwa.

Mteule wa karibuni kabisa kukosa kazi ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, ambaye alijikuta akipoteza kazi kufuatia ripoti ya kamati ya kuchunguza sakata la usafirishaji mchanga wa madini. Rais Magufuli alisema pamoja na kuwepo kwa urafiki kati yao, jambo hilo halikubaliki na anastahili kuwajibika.

MABOSI KIBAO SERIKALINI WALALA SELO

Tofauti kabisa na miaka ya nyuma, serikali ya awamu ya tano, imekuwa haina mchezo linapofika suala la maadili ya kazi na ofisi za umma. Hadi sasa, makumi ya watumishi katika nafasi mbalimbali wamejikuta wakilala selo, kitendo ambacho kilikuwa ni nadra kufanyika miaka ya nyuma.

“Ni kweli hata katika tawala zilizopita kuna vigogo walikuwa wanafanya makosa na wanafikishwa katika vyombo vya dola, lakini ilikuwa ni kwa muda tu, kwani wengi walitoka nje hata kwa makosa ambayo walistahili kusubiri mahabusu wakati kesi zikiendelea, au wengine kesi zao zilifutwa katika mazingira ya kutatanisha na kwa ujumla, mahabusu hakukuwa sehemu ya mabosi na matajiri,” alisema Enock Masulungu alipoombwa kuoanisha utendaji wa serikali hizo tatu (awamu ya pili, tatu, nne na tano).

“Hiki anachokifanya Magufuli ni jambo zuri na kilishatabiriwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, mzee Yusufu Makamba mjini Dodoma wakati anamkampenia urais kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa chama hicho aliposema, Jakaya Kikwete alibatiza kwa maji lakini Magufuli atabatiza kwa moto,” alisema Masulungu.

Akaongeza kuwa ilikuwa ni vigumu kwa serikali zilizopita kuona wakurugenzi wakuu au makamishna kufikishwa mahakamani lakini serikali ya Magufuli imefanya hayo, hivyo kuandika rekodi kwa marais wa Tanzania waliopita.

HII HAPA ORODHA YA VIGOGO MATATANI

Tangu aingie madarakani Novemba 5, 2015 vigogo walioshitakiwa ni wengi na baadhi yao ni hawa wafuatao.

Maofisa nane wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), wakiongozwa na Kamishna wa Forodha, Tiagi Masamaki wapo matatani baada ya kufikishwa mahakamani Desemba 4, 2015 kwa tuhuma za kutoa makontena 329 bandarini bila ya kulipiwa kodi na kuisababishia serikali hasara ya sh. bilioni 12.7.

Vigogo wengine waliopandishwa kortini pamoja na Masamaki ambao tangu wakati huo wako mahabusu ni Habibu Mponezya, (Meneja wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja) na Bulton Mponezya.

Kamishna Mkuu Mstaafu wa TRA, Harry Msamire Kitilya na wenzake wawili, Miss Tanzania mwaka 1996, Shose Mori Sinare na Sioi Graham Solomon nao wapo mahabusu wakiendelea na kesi yao tangu walipopandishwa kizimbani Aprili Mosi, 2016 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaamu.

BANDARINI HAWAKUACHWA

Katika Bandari ya Dar es Salaam, moja kati ya milango ya uchumi nchini, moto wa Rais Magufuli umewawakia mkurugenzi wa zamani wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Ephraim Mgawe na naibu wake, Hamadi Koshuma wakajikuta wakikabiliwa na kesi na kutakiwa kujibu mashitaka ya kesi ya matumizi mabaya ya madaraka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Januari 16,2016.

Washitakiwa hao walidaiwa kuwa katika utendaji wao wa kazi kwa makusudi walitumia madaraka yao vibaya kwa kusaini mkataba wa kibiashara bila kuitisha zabuni.

NIDA NAO HAWAKUBAKI SALAMA

Serikali ya Rais Magufuli pia imemburuza mahakamani aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dickson Maimu na maofisa wengine saba waandamizi Agosti 17, 2015, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakikabiliwa na mashitaka 27 yakiwamo madai ya matumizi mabaya ya ofisi na kusababisha hasara ya zaidi ya Sh bilioni 1.2.

Washitakiwa wengine ni Mkurugenzi wa Huduma za Kibiashara, Avelin Momburi, Meneja wa Fedha na Uhasibu, Benjamini Mwakatumbula, Meneja wa Bajeti na Miliki, Joseph Makani, Ofisa Usafirishaji, George Ntalima na Mkurugenzi wa Sheria, Sabina Raymond.

Wengine ni Xavery Kayombo ambaye wadhifa wake haukutajwa, na Astery Ndefe ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Aste Insurance Brokers Company Limited.

PEDESHEE NDAMA

Mwingine aliyekumbana na ‘mkono’ wa dola ya Magufuli ni mfanyabiashara Ndama Shaabani ‘Pedeshee Ndama Mutoto ya Ng’ombe’ ambaye alifikishwa katika Mahakama ya Kisutu kwa tuhuma za kughushi, kutakatisha fedha na kujipatia dola za Marekani 540,390 kwa njia ya udanganyifu. Kwa muda wote wakati kesi yake ikiendelea, amekuwa mahabusu. Moja ya mashtaka yake ametiwa hatiani na amelipa faini ya shilingi milioni 200. Kesi bado inaendelea.

Licha ya vigogo hao, wapo pia vigogo mbalimbali katika ngazi za wilaya na mikoa ambao wanashikiliwa kwa tuhuma mbalimbali, kitu ambacho huko nyuma, kilionekana kuwa si cha kawaida.

Hata hivyo, enzi za Jakaya Kikwete, serikali yake ilimudu kuwapeleka mahakamani na kuwakuta na hatia mawaziri wawili wa zamani, Daniel Yona na Basil Mramba huku vigogo waliohusika na sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow nao wakipelekwa mahakamani.

Vigogo hao ni Meneja wa Mamlaka ya Kodi Tanzania (TRA), Kyabukoba Mutabingwa, Mkurugenzi wa Fedha Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Julius Angello pamoja na Mwanasheria Mwandamizi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco),Steven Urassa.

Audio: Haruna Niyonzima kwenda Simba? Mwenyewe Afunguka Haya

0
0


Sintofahamu ya Mchezaji Nionzima Kuchezea timu gani msimu huu bado yaendelea huku pakiwa na tetesi kuwa amewakacha Yanga na Kusign Simba....Embu Msikilize Mwenye Hapa Akiongea:

Sumaye Acharuka Aitaka Serikali itambue CHADEMA ipo Kisheria, Wasitake Vurugu Bila Sababu'

0
0
Heshima kwenu wakuu,

Sumaye ameiomba Serikali iache kuwafanyia fujo CHADEMA. wanayo haki ya kutembelea Sehemu walizoshinda ili kuona kama kweli Madiwani wao wanafanya kazi walizowaahidi wananchi.

Hapa Ubungo kuna diwani wa CHADEMA, sisi kama Viongozi wake tumekuja kuona utendaji wake je anafanya kazi kweli au hafanyi. Sasa kosa lipo wapi?

Polepole na Bulembo wa CCM wanazunguka kila Halmashauri nchi wala hawakatazwi na haiwi nongwa. Lakini chadema wakitembelea pale wanapoongozwa wanakamatwa wanatiwa ndani.

Tunaomba Serikali ituache tuwatumikie wale waliotuchagua sababu hii miradi tunayoitembelea sio ya Chadema tu bali itatumiwa na Vyama vyote.

"Tunaomba tu Serikali ituvumilie, CHADEMA ni chama halali kisheria na kinafanya kazi yake yake kwa mujibu wa sheria na Katiba ya nchi" Mjumbe Kamati Kuu CHADEMA na Waziri Mkuu mstaafu, Mhe. Frederick Sumaye.

MY TAKE:

Mjusi ukimkimbiza sana akifika ukingoni ambapo mbele hakuna njia tena, hugeuka nyoka na kuanza kukukimbiza wewe. Siasa CCM wanazofanya hazijawahi kufanikiwa sehemu yoyote Duniani. Kwamba mshindani wako unamfunga mikono kwa nyuma halafu unataka mpande ulingoni kupambana kisha unajisifu umeshinda. Ni kutojitambua na ni aibu.

By Figganigga

VIDEO: Maajabu, Mwanaume Ajifungua Mtoto Nchini Marekani Kwa Kupitia Uume Wake

0
0
Karibu siku zinavyozidi kwenda, dunia I napata uvumbuzi mwingi sana

Amepatikana mwanaume aliezaa huko nchi ni marekani

Huyu hapa kwenye video muone

Install APP ya Blog Hii ya UDAKU SPECIAL Kwenye Simu yako Kutoka Google Play Kusoma Habari Kirahisi

0
0

Download  Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE 


Au Kama Unayotayari Bonyeza HAPA Ku Update Uweze Kupata Ikiwa na Muonekano Mpya

Tamko Kali la Kubenea Kuhusu Kukamatwa Kwa Meya wa Ubungo Boniface

0
0
TAARIFA KWA UMMA*

NIMEPOKEA kwa masikitiko makubwa taarifa kuwa Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Yakoub amekamatwa na jeshi la polisi kwa amri ya "wanaodai wako madarakani."

Kukamatwa kwake kunatokana na hatua yake ya kumpokea Mwenyekiti wa Chadema, Kanda ya Pwani, waziri mkuu mstaafu, Frederick Sumaye.

Mhe. Sumaye alikuwa na ziara ya kikazi ya kukagua shughuli za Manispaa za Dar es Salaam ambazo ziko chini ya vyama vinavyounda umoja wa UKAWA.

Napenda kuufahamisha umma kuwa amri; na au maelekezo yoyote yaliyotolewa iwe na polisi au mkuu wa mkoa ama wilaya juu ya kukamatwa kwa Meya ni batili na haikubariki.

Hivyo basi, ni jukumu letu kuhakikisha kuwa tunapigana kufa na kupona kutetea haki za wananchi waliotuchagua na kuhakikisha Meya wetu anakuwa huru kwa gharama yoyote ile.

Ninawaomba wanachama, viongozi na wananchi wa jimbo la Ubungo na Kanda ya Pwani kusimama nasi, pamoja na Meya wetu katika kipindi kigumu cha kudai demokrasia ya kweli ndani ya Nchi yetu.

Ninaahidi kuwa mstari wa mbele kutetea wananchi na kuhakikisha haki zao zinapatikana.

Ni jukumu letu sote kuhakikisha "udikteta ulioanza kuingia nchini taratibu," unatokomezwa.

Taifa hili siyo mali ya CCM. Ni letu sote.

*Saed Kubenea*
Mbunge wa Ubungo, M/M- Kanda ya Pwani.

Wanafunzi wa Kitanzania Wang'ara Marekani Aliwemo Rashid Jakaya Kikwete

0
0

Baadhi ya wanafunzi wa shule ya kimataifa Feza wakiwa na furaha nchini Marekani baada ta kushinda medali za dhahabu kwenye mashindano ya Genius Olympiad. Kushoto ni Abdulrazak Juma Mkamia wa pili Rashid Jakaya Kikwete na watatu ni Abdalah Rubeya yaliyoshirikisha nchi zaid 63 duniani huko Marekani juzi.

Kwanini CHADEMA Wanakwepa Kuulizia Hoja ya Richmond Kipindi Hiki cha Magufuli?

0
0
Katika kuchangia hoja zao haswa mitandaoni wafuasi wa chadema wanajitahidi sana kukwepa kuiongelea au kuiulizia kashfa ya Richmond.

Yaani katika mambo ambayo hawataki kumkumbusha Magufuli ni ufisadi wa Richmond.

Katika mambo ambayo Chadema hawataki kumuwekea mkono Magufuli apute ni kuhusu swala la Richmond.

Hivi hofu ya Chadema ni ipi kwenye hili?

Kwa nini hatuoni makala za kumtaka Magufuli ashughulikie Richmond?

Hatuoni makala zinazosema kwamba sisi wapinzani tulipigia kelele sana swala la Richmond.

Hofu ya Chadema ni nini?

Kwa nini Ufisadi unaongelewa kwa vipande vipande?

By Jingalao/JF

Mhe.Kaimu Jaji Mkuu, Prof. Ibrahim Juma, Naomba Usiruhusu Udhalilishaji Huu Ndani ya Mahakama Zetu!

0
0
Wanabodi,

Tanzania ni nchi yenye katiba inayoendeshwa kwa misingi ya haki, the rule of law kwa kufuata misingi ya sheria, taratibu na kanuni. Kwenye kila jambo linatekelezwa kwa mujibu wa sheria taratibu na kanuni, mahakamani ni mahali pa kutoa haki, tunaomba usiruhusu vyumba na maeneo ya mahakama kutumika kuwa ni sehemu ya udhalilishaji wa watuhumiwa!. Status ya Watuhumiwa wowote mbele ya sheria ni innocent until proven guilt!. Kwa nini watuhumiwa wadhalilishwe tena mbele ya kamera huku wakipigwa picha na video?!.

Tanzania inafuata mfumo wa sheria wa ya Uingereza, common law, ambapo mtuhumiwa huhesabiwa not guilt until proven guilt. Mfumo huu hauruhusu kuwapiga picha watuhumiwa wowote wakiwa mikononi mwa polisi au ndani ya vyumba vya mahakama. Lengo la kuzuia ni ili kuwaepushia watuhumiwa kuhukumiwa na media, "media trial".

Kitendo walichofanyiwa watuhumiwa hawa wawili, Rugemalila na Sing kuchuchumalishwa chini mbele ya camera za waandishi, ni udhalilishaji wa hali ya juu ya haki za watuhumiwa na ni kinyume cha sheria, taratibu na kanuni!.

Lengo la watuhumiwa kuchuchumalishwa, ni wale watuhumiwa wanaoshikwa kwa kufanya fujo, hivyo huchuchumalishwa ili kuwazuia wasitoroke chini ya ulinzi, hivi kweli Rugemalila na umri ule, na Singasinga na unene ule, walikuwa na tishio lolote la kutoroka chini ya ulinzi hadi kuwa chuchumalisha?!.

Sio mara moja au mbili, watuhumiwa wanafolenishwa na kupigwa picha mikononi mwa polisi. Watuhumiwa wanapigwa picha ndani ya vyumba vya mahakama!. Huu ni ukiukwaji wa haki za watuhumiwa!.

Tanzania – Code of Ethical Practice for media photographers and ...

"Contravene laws or lawful orders prohibiting the taking for pictures in the precincts for courts. The law prohibits the taking of pictures of any person (Judges, jurors and witnesses) involved in a proceeding before the court, whether civil or criminal; or to publish any photograph taken in contravention of the order. It could be in the courtroom, in the precincts of the building in which the court is held, or the persons leaving or entering the precincts". 

Kwa msio fahamu, hata watuhumiwa nao ni binadamu na haijalishi wamefanya kosa gani, nao wanastahili heshima na utu wa ubinaadamu wao na sio kudhalilishwa. Watuhumiwa wana haki zao ambao zinapaswa ziheshimiwe.

Hata wahalifu wanaohukumiwa kunyongwa, pia wana haki zao zinazopaswa kuheshimiwa. Mfano mtu aliyehukumiwa kunyongwa mpaka kufa, japo lengo ni afe, kabla adhabu hiyo haijatekelezwa kwanza daktari ataitwa na kumpima akikutwa na ugonjwa wowote, adhabu ile haitekelezwi hadi atibiwe apone kabisa akiwa fit ndipo anyongwe hadi kufa. Kumnyonga mtu mgojwa ni kumuonea!. Kabla ya kunyongwa viongozi wa dini huitwa kumsalisha sala ya toba, kumuungamisha na kumuombea dua na kama ni Muislamu hutazamishwa kibla ndipo hunyongwa!. Lengo la kueleza haya ni kuonyesha kuwa hata wahalifu wana haki.

Hivyo ni ombi maalum kwa Kaimu Jaji Mkuu wetu, Dr. Ibrahim Juma, tunakuomba please usiruhusu maeneo ya mahakama na vyumba vya mahakama kutumika kama sehemu ya udhalilishaji utu wa watuhumiwa huu unaofanywa wanapokuwa mikononi kwa polisi na ndani ya vyumba vya mahakama zetu!.

Ndani ya vyumba vya mahakama za Uingereza, India na Afrika Kusini, watuhumiwa hawaruhusiwi kupigwa picha wakiwa ndani ya vyumba vya mahakama, au mikononi mwa polisi. Kama sisi tumerithi sheria za Uingereza, kwa nini tuende kinyume cha wenzetu, unless kwa kufanya hivyo, ndio maendeleo yenyewe!.

Kitendo cha kuwapiga picha watuhumiwa ndani ya vyumba vya mahakama, huku kamera za video zikiwamulika, ni kama kuwahukumu kupitia kitu kinachoitwa "media trial", mtu akiishaonyeshwa kwenye TV ni jambazi, hata akijakukutwa hana hatia, mtaani kila apitapo, watu watanyoosheana vidole, "jambazi yule!"

Naamini polisi wanajua kumpiga picha mtuhumiwa mikononi mwa polisi ni kinyume cha kanuni, kumpiga picha mtuhumiwa akiwa ndani ya chumba cha mahakama ni kinyume cha kanuni, kwa nini haya yanafanyika na tunayanyamazia wakati sheria, taratibu na kanuni zipo wazi?!.

Wanasheria mliopo jf mtatusaidia kwa hili kama tulibadilishwa kutoka kufuata the common law or English Law into American law.

Nimetokea kumfahamu Prof. Ibrahim Juma kwa karibu na sina mashaka kabisa na uadilifu wake katika kutenda haki na kutoa haki ili tuu sio haki itendeke bali pia haki kuonekana imetendeka, "Justice must not only be done but must be seen to be done".

Paskali.

Tundu Lissu Sasa ni "Liability" na Aibu ya Karne Kwa Mawakili Nchini

0
0
Ameandika Tundu Lissu kuwa kukamatwa Harbinder Singh Seth na James Rugemalila hakutoshi. Mwanasiasa huyu na mwanasheria huyu kwa sasa anatekeleza mradi maalum ambapo kila hatua inayochukuliwa na Serikali hukurupuka kuipinga.

Alipinga kila kitu Serikali ilipoanza kuchukua hatua dhidi ya uporaji wetu katika raslimali za madini hata pale alipooneshwa kuwa anakipinga alichokipigania hata katika maandiko yake ya nyuma ndio akaishiwa nguvu.

Alianza kupotosha umma kuwa tutashitakiwa lakini alipooneshwa ushahidi kuwa huko MIGA anakotaja vipo vifungu mkataba huo haulindi wezi na watoa rushwa akanywea.

Alipoumbuliwa kuwa alijenga ukaribu wa mashaka na Acacia na upo ushahidi wa nguvu walizompa na wenzake kuropoka na kwamba siku moja utaanikwa na ataanikwa na atapigwa butwaa akanywea.

Sasa amekurupuka kuanza kubeza hatua za mwanzo tu za Serikali kumkamata mfanyabiashara ambaye hata yeye Lissu alitokwa povu huko nyuma kutaka akamatwe.

Mbia wake katika ukaribu na Acacia na kutumika kubeza mambo Zitto Kabwe katika hili amekataa kugeuka jiwe-walau kapongeza juhudi hizi za Serikali.
Lissu anataja majina ya watu weeeengi akisema nao wakamatwe. Sipingani naye lakini mwanasiasa huyu ajue kuwa hoja si kukamata tu hoja kisheria ni ushahidi.

Kesi hizi kubwa ni wazi kuwa Serikali inapambana na watu wenye nguvu na watakaoweka mawakili wengi kuwatetea. Serikali ninavyoiona ina akili kuliko Lissu anavyodhani na ndio maana katika hili nataka kuamini hakuna atakayesalimika hata Lissu mwenyewe.Ipo siku.

Katika sheria kumpeleka mtu mahakamani sio suala la mbwembwe wala kiki za siasa wala hasira bali ushahidi. Lakini kama alivyoropoka mwenywe ushahidi tu hautoshi lazima uwe na ushahidi mzito na wa kuthibitisha kosa husika bila kuacha shaka ya maana (proof beyond reasonable doubt).

Mwanachama mwandamizi wa Chadema na mwalimu wa Lissu katika sheria Prof. Abdallah Saffari ameandika kwa kina dhana hii katika kitabu chake "Mashtaka ya Jinai na Utetezi" Ndio maana naamini hata Prof huyu atakuwa anashangaa ukurupukaji wa Lissu

Ninavyowaona watendaji makini wa JPM wanatimiza kanuni hii ya kisheria na maoni haya ya wasomi watulivu kama Prof. Safari kwa kukusanya ushahidi na wanapoupata wanaoamini unatosha (maana mwisho wa siku Mahakama ndiyo inaamua) ndipo wanakwenda kortini.

Lissu anajua pia kuwa kesi haishindwi kwa mtu kuwahi mahakamani asbh au mchana bali unaishinda pamoja na mambo mengine kuandaa ushahidi kujiridhisha na vifungu vya sheria utakazotumia na mwisho hoja utakazozijenga kortini.

Mimi nakubaliana naye kwamba kuwakamata hawa wawili hakutoshi na wala hata aliowataja hawatoshi na hata Serikali haijasema imetosha! Wapo watu wengi wamelikosea Taifa hili tena wengi Lissu akikwepa kuwataja na baadhi yeye ndio sasa anakuwa wakili wao kuwatetea.

Lipo kundi lililoamua kuhujumu Taifa kwa kuwatumikia mabepari wa nje...hawa nao bado. Nashangaa Lissu hawaoni.Wapo. Wapo wanasiasa ambao huvuta mabilioni kwa watu wanaoliibia Taifa na kuanza kuzuia juhudi za Serikali.Wapo ila Lissu hakuwataja.

Wapo wanasiasa wamekuwa katika kilele cha kashfa kubwa za nchi hii kama vile Richmond Lissu anawajua na yuko nao lakini hakuwataja wala hataki kuona kuwa hao nao bado.

Nilikuwa namkumbusha tu kuwa kama ni dhana ya bado, bado wengi ila aweke orodha yake vyema, asibague.Namhakikishia kwa spidi hii ya kazi wapo pia ambao atakwenda Mahakamani kujaribu kuwatetea.Wapo.Asubiri tu.

Lakini la msingi analopaswa kujua ni kwamba mtu hapelekwi Mahakamani kwa sababu tu kalalamikiwa au katajwa na flani. Ndio maana namuona Lissu kama Rais wa kwanza wa Chama cha Wanasheria Nchini ambaye kwa kweli ni "liability."

Mpaka sasa kaondoka kabisa kwenye kazi hiyo ya kushauri kitaalamu hadi kuwa mropokaji na mtu anayetishia Serikali isichukue hatua au akibeza kila hatua zinapochukuliwa hata katika mambo aliyoyatafiti katika thesis zake na kutaka yafanyiwe kazi.

Ni Rais wa kwanza wa wanasheria ambaye ofisi ya Urais wa TLS imekuwa ya kisiasa rasmi-hana lolote la kuzungumzia taaluma ya sheria wala kujadili utatuzi wa changamoto za taaluma lakini anasubiri Serikali ya JPM iamue kitu tu apayuke.

Ni Rais wa kwanza wa TLS, walau mpaka sasa tangu achaguliwe, huwezi kuona ana vision na mission gani katika kukiongoza chama hicho cha watu makini na wenye utulivu mkubwa. Ni mtazamo wangu kuwa Lissu anaweza kuwa asset lakini so far kwa sasa ni "liability."

Na kwa kweli kwa uliability huo na uasset wa Serikali ya sasa ya JPM, namuona Lissu atakuwa na kazi ngumu sana duniani ya kupayuka na kuna siku atalazimika kujisahau na kupayuka "bado mimi."

Wasalaam
Political Jurist-Udom lakini aliyeko mapumzikoni Nang'ombe, Mtwara
Maramla

Watoto wa Bosi wa Freemason Wafunguka haya baada ya miezi miwili ya kifo cha baba yao

0
0
Takriban miezi miwili baada ya kifo cha aliyewahi kuwa Bosi wa Jamii ya Siri (Secret Society) ya Freemason kwa Afrika Mashariki, Jayantilial Andy Chande ‘Sir Chande’, aliyefariki dunia Aprili 7, mwaka huu, watoto wake wawili wamefunguka mazito juu ya jamii hiyo.
Kabla ya kupata neno la watoto hao, kufuatia kifo cha Sir Andy, kumekuwa na maswali mengi juu ya nini kinaendelea kwenye jamii hiyo kwa sasa hivyo Wikienda lilijipa kazi ya kutafuta majibu ya maswali.

NINI KINAENDELEA FREEMASON?

Katika nusanusa yake, Wikienda lilifika kwenye Hekalu la Freemason lililopo Mtaa wa Sokoine, mkabala na Hoteli ya Hyatt Regency, The Kilimanjaro jijini Dar, jirani na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na kutaka kujua kinachoendelea kwa kujigeuza mhitaji wa kujiunga na jamii hiyo.

Gazeti hili lilipofika mahali hapo mishale ya mchana, hakukuwa na pilikapilika nyingi zaidi ya mama ntilie aliyekuwa akisubiria wateja wa msosi.

Baada ya kuona kimya, ‘pandikizi’ wetu alijaribu kuzama ndani, lakini kabla ya kuvuka geti ambalo lilikuwa wazi kwenye mlango mdogo, alikutana na mlinzi aliyemhoji alikokuwa anakwenda.



Mlinzi: Haloo unakwenda wapi?

Wikienda: Samahani, nataka kuingia ndani kuulizia ‘process’ za kujiunga na Freemason, kwani hapa si ndilo hekalu lao?

Mlinzi: Ndiyo ni hapa, lakini hakuna shughuli ya watu kujiunga kwani nani amekuambia watu wanajiunga?

Wikienda: Sasa kwa mtu anayehitaji kujiunga inakuwaje?

Mlinzi: Hapa hakuna hilo zoezi na wala hakuna mtu aliyewahi kuja hapa akaunganishwa na Freemason. Kama yupo, huyo alitapeliwa tu maana mjini shule.

Wikienda: Inamaana wenyewe hawapo au?

Mlinzi: Wenyewe hawapo, mara ya mwisho sikumbuki vizuri labda ilikuwa mwezi wa tatu, lakini kuanzia mwezi ujao (wa saba) watakuwepo.

Wikienda: Sasa kama hivi nataka kujiunga, inakuwaje?

Mlinzi: Kwanza unataka kujiunga na nini na ili iweje?

Wikienda: Nataka kujiunga na Freemason. Nasikia watu waliojiunga wanapata pesa nyingi na mimi ninazitaka bwana au wewe hutaki pesa ndugu yangu?

Mlinzi: Kweli wajinga ndiyo waliwao, yaani pamoja na ujanja wote unaamini kuna pesa za hivihivi bila kufanya kazi? Nimekuambia hapa hakuna ishu ya watu kujiunga wala sijawahi kuona watu wanakuja tu na kuunganishwa. Kama nilivyokuambia, kama kuna mtu aliunganishwa kwa kuja tu hapa ujue alitapeliwa.


Wikienda: Sasa, mbali na hapa, naweza kujiungia wapi kwingine?

Mlinzi: Mimi kwa hapa sijui, lakini nasikia makao yao makuu kwa Afrika Mashariki yapo Mombasa (Kenya). Sasa kama unataka uende huko kama una uwezo, lakini kwa hapa hakuna kitu kama hicho. Kwanza ninavyojua mimi, hayo ni mambo ya siri. Huwezi kuja hapa tu, ukasema unataka kujiunga, kivipi?

Baada ya mazungumzo hayo, mlinzi huyo alitaka kuwa mkali kwa kumuona pandikizi wetu kuwa ni ‘bogas’ hivyo pandikizi huyo aliondoka kwa maelezo kwamba, hakuna zoezi la watu kuunganishwa mahali hapo.

TURUDI KWA WATOTO WA SIR CHANDE

Katika mazungumzo yao na waandishi wetu, watoto wa Sir Chande, Manish Jayantilial na Rupean Jayantilial walieleza kinachoendelea kwenye jamii hiyo.

Manish alisema kuwa, kwa upande wake, yeye ni muumini wa Jumuiya ya Freemason kwa muda mrefu na malengo yake ni siku moja kuwa kiongozi mkubwa wa jamii hiyo.

“Ni jambo zuri mno, ni jamii ya watu wanaosaidiana duniani, nimekuwa member (mwanachama) wake kwa muda mrefu sana na ninatamani siku moja niwe kiongozi wake mkubwa,” alisema Manish kwa lafudhi ya Kihindi.

MIAKA MITATU BILA MAFANIKIO

Kwa upande wake, Rupean alikiri jamii hiyo kuendelea na shughuli zake mbalimbali duniani ikiwemo hapa nchini na kwamba anatamani mno kujiunga na Freemason.

Rupean alisema kuwa, kwa muda wa miaka mitatu sasa, amekuwa akifanya maombi ya kujiunga bila mafanikio lakini anaamini ipo siku naye atafuzu kama ndugu yake, Manish.

Alisema kuwa, sababu ya kushindwa kufuzu ni kwamba, bado hajatimiza masharti yanayotakiwa lakini anaamini siku akiyatimiza atakuwa mwanachama wake.

WALIVUTIWA NA BABA YAO

Manish na Rupean walisema kuwa, baba yao ndiye aliyewavutia kujiunga na Freemason kwa kuwa ni jambo zuri kuwa na jamii ya kusaidiana na kuwasaidia wenye shida mbalimbali kwa kujitolea.

Hata hivyo, walimalizia kwa kusema kuwa, mbali na Tanzania, pia wanaishi nchini Canada na India.

Sir Chande ambaye mwili wake ulichomwa moto kwenye Makaburi ya Baniani yaliyopo Makumbusho jijini Dar aliacha watoto watatu na wajukuu watatu.

Source: Global Publisher

Wanasayansi Wagundua Sayari Nyingine 10 Zenye Uhai

0
0
Sayari hizo ambazo zinatoshana na dunia, zote zipo nje ya jua katika mkusanyiko huo wa nyota.

Wataalam wa maswala ya angani wametangaza ugunduzi wa sayari nyengine kumi angani ambazo huenda zinaweza kusaidia uhai.

Wanasayansi wa shirika linaloshughulikia maswala ya angani NASA wanasema kuwa data mpya iliochunguzwa kutoka kwa darubini ya Kepler inaonyesha sayari kumi zenye miamba ambazo zipo hatua chache kutoka kwa mkusanyiko wa nyota.

Sayari hizo ambazo zinatoshana na dunia, zote zipo nje ya jua katika mkusanyiko huo wa nyota.

Darubini hiyo ya Kepler sasa imegundua jumla ya sayari 50 katika maeneo tofauti yenye uhai angani.

Zijue Dalili Kuwa Mkeo au Mpenzi Wako Ameshakulisha Limbwata la Kutukuka

0
0
1. Ukiwa mtaani unakuwa mbabe ila ukiwa Kwako na Mkeo unakuwa Mpole sana

2. Hupendi Ndugu zako kuja Kwako ila wa Mkeo unawalazimisha waje

3. Ukiwa unaongea na Ndugu zako huwa unakuwa na Hasira ila wa Mkeo meno yote 32 nje

4. Unasikia uvivu kwenda kusalimia Kwenu ila kwa Mkeo unatamani uende kila siku

5. Ukiombwa Hela na Ndugu zako unawaambia subiri hadi uzungumze na Mkeo Kwanza

6. Ukipokea tu Mshahara lazima utamwambia hata kama hajakuuliza

7. Ukiwa nae Kitandani unaogopa kumwomba Mbunye hadi akuambie Yeye

Je kwa dalili hizo hapo juu kuna mwana JF yoyote ambaye ni Mume wa Mtu zimemhusu kwa 100%?

BY GENTAMYCINE/Jamii Forums

Nina Mika 20 Sijawahi Fanya Mapenzi ila Nahisi Bikira yangu Haipo Je ni Kawaida?

0
0

Naitwa Nancy Naishi Kijitonyama , mimi ni Msichana na Miaka 20 nimekuwa nikijitunza kwa muda mrefu ili kutunza Bikira yangu kwa mwanaume atakaye nioa mungu akijalia ...so sijawahi fanya mapenzi na mtu yoyote japo napata vishawishi vingi....Saa zingine nikisikia hamu huwa najisugua kwa vidole sehemu zangu ili kutoa hamu....

Sasa hivi karibuni nimehisi huku chini hapako tight kama zamani hata nikiingiza kidole kinaingia bila shida sasa naogopa je Bikira yangu imeshatoka au ni kawaida? na je kujishika kwa vidole sehemu hizo kunaondoa bikira?

Please naomba ushauri.

Habari ya Uongo ya TBC iliyomhusisha Rais Magufuli yatua Bungeni

0
0
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Harrison Mwakyembe amesema Serikali ilichukua hatua stahiki za kinidhamu dhidi ya watangazaji wa kituo cha runinga cha TBC waliorusha habari ya uongo iliyomhusisha Rais Trump wa Marekani akidaiwa amemsifia Rais Magufuli.



Waziri Mwakyembe ametoa kauli hiyo leo, Bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi aliyetaka kujua Serikali ilichukua hatua gani juu wa Watangazaji waliosoma habari hiyo huku akidai kuwa bado anawaona katika kituo hicho cha runinga.

“Tulichukua hatua za kinidhamu kwa kosa ambapo kila binadamu hapa duniani anaweza kulifanya, yametokea matatizo kama hayo hayo Kenya yamefanyika watangaji wamerudi, na sisi tulichokifanya kuchukua hatua ya muda mfupi ili wawe waangalifu zaidi ni kitu kinafanyika kila siku leo, Mwenyekiti nikikuletea mfano wa Magazeti yanayochapishwa kila siku nakuhakikishia asilimia 60 ndani kuna makosa kwahiyo ni makosa ya kibinadamu,”

Waliosimamishwa kazi kwa kipindi hicho ni pamoja na mtangazaji aliyeisoma habari hiyo, Gabriel Zakaria na wengine ni Elizabeth Mramba, Prudence Constantine, Dorothy Mmari, Ramadhan Mpenda, Leya Mushi, Alpha Wawa, Chunga Ruza na Judica Losai.

Tazama video ifuatayo nikukumbushe habari hiyo:


Ujumbe wa Diamond kwa Mzee Yusuph Kufuatia Kifo cha Mkewe na Mtoto Wake

0
0
Mzee Yusuph alimpoteza mke wake mdogo Chiku Khamis Tumbo na mwanawe mchanga ambao waliaga dunia usiku wa Jumamosi katika hospitali la Amani Dar es Salaam Tanzania.

Chiku alifariki akijifungua, mtoto wake wa kike pia aliaga dunia wakati huo. Mwenda zake alikimbizwa hospitalini na Mzee Yusuph usiku huo alipoanza kuskia uchungu wa kujifungua.

Mashabiki wa Mzee Yusuph wamekua wakitoa salamu za rambirambi kwenye mitendao za kijamii kufuatia kifo cha bibi yake.


Diamond Platnumz pia amemfariji Mzee Yusuph kwa ujumbe aliyoandika kwa Instagram; alimpa roho kwa kumwambia Mola ndo hupanga kila kitu duniani.

“Stay strong bro, Mwenyez Mungu ndio mpanga wa kila jambo… tumshukuru na kuwaombea waendapo wapumzike kwa Amani…Amin, Inshaallah🙏” Diamond aliandika.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images