Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Majibu ya Serikali Kuhusu Mfungwa Mwanamke Kupata Mimba Akiwa Gerezani

$
0
0
BUNGE limeelezwa kuwa ni vigumu mfungwa mwanamke wa kifungo cha muda mrefu kupata mimba akiwa gerezani.

Hayo yalibainishwa jana bungeni na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum (CUF), Raisa Abdallah Mussa.

 Mbunge huyo alitaka kujua ni kwanini sehemu ya magereza inayoaminika kama ni sehemu salama, lakini wanawake wanapata mimba wakiwa gerezani.

 Akijibu swali hilo, Mwigulu alisema amezunguka katika magereza yote na hakuna eneo ambalo amefika na kukuta mwanamke aliyefungwa kifungo cha muda mrefu amegundulika kuwa na mimba akiwa kwenye kifungo hicho.

“Ni kweli unaweza kukuta wale wenye kifungo cha muda mfupi wakajifungua wakiwa gerezani, lakini kujifungua wakiwa gerezani haina maana kuwa mimba kaipatia gerezani,” alisema Mwigulu.

Alibainisha kutokana na sheria kali za majeshi likiwamo Jeshi la Magereza, haitawezekana mwanamke mfungwa apate mimba akiwa ndani ya gereza halafu taarifa zikafichwa.

Katika swali la msingi, Mbunge huyo alitaka kujua serikali imejipanga vipi katika kuwanusuru watoto ambao wanawake wamekuwa wakijifungua wakiwa magerezani.

“Je, serikali haioni kuwa inavunja haki za binadamu kwa kuwaweka magerezani watoto hao wasio na makosa, na je, inaweza kulipa Bunge takwimu za wanawake waliokinzana na sheria na kufungwa kwa miaka mitano iliyopita?” alihoji.

Akijibu swali hilo la msingi, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Yusuf Masauni, alisema kwa muda wa miaka mitano jumla ya wanawake 2,008 walikinzana na sheria na kufungwa magerezani.

Aidha, alisema kwa watoto kuwapo magerezani na wazazi wao ni kutokana na sheria ya mtoto ya kutaka mtoto kupata haki yake ya kunyonya maziwa ya mama.

Okoa Ndoa Yako Sasa, Ongeza Maumbile na Nguvu za Kiume Hata Kwa Wenye Kisukari Kwa Kutumia Products za Markson Beauty

$
0
0
OKOA NDOA YAKO SASA. ONGEZA MAUMBILE, NGUVU NA HAMU YA TENDO LA NDOA HATA KWA WENYE KISUKARI. Tatizo la maumbile madogo, nguvu za kiume na ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limekuwa likiwasumbua wengi na kusababisha kushindwa kujiamini ktk tendo hivyo kusababisha ndoa nyingi kuvunjika pamoja na mahusiano. Upungufu wa nguvu na hamu ya tendo husababisha mambo kama:-
(a)Uume kulegea wakati wa tendo (b)Kukosa hamu ya tendo la ndoa (C)Kuwahi kufika kileleni (D)Uume kuchelewa kusimama baada ya round ya kwanza. (E)Kuchoka sana baada ya round moja n.k @Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo kwa kutumia bidhaa zilizotengenezwa kwa mimea na matunda zisizo na kemikali wala madhara na kuthibitishwa kiafya. Pata hizi👇👇👇👇
🍉 🌿🍅🍒🍍🍓🍉🍎🍀
1.HANDSOME UP ni kifaa chenye uwezo wa 99 % kuongeza uume (size unayohitaji) na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200000@200,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130000@130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130000@130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo hata mara 3 @130000@130,000/= Kwa Bidhaa hizi na nyingine kama:-
5.Kupunguza unene na manyama uzembe @150000@150,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi @130000@130,000/=
7.Kutengeneza shepu (hips, makalio na mapaja) @200000@200,000/= 8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni @120000@120,000/=
9.Kuwa mweupe na soft mwili mzima bila kuacha sugu 120,000/=
10.Kurudisha usichana (bikra) @120000@120,000/=
11.Kupunguza au kuongeza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120000@120,000/=

Wasiliana nasi kwa (+255) 0767447444 au 0714335378.

NB: Matokeo ni uhakika na garantii na upate risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii. Follow us
@Markson_beauty_pr

Sherehe ya kula nyama ya mbwa Ilivyofanyika China

$
0
0
Sherehe ya kula nyama ya mbwa iliogubikwa na utata katika mji wa Yullin nchini China imeanza licha ya ripoti za awali kwamba ilikuwa imepigwa marufuku mwaka huu.

Sherehe hiyo hufanyika kila mwaka katika mkoa wa Guangxi.

Mapema mwaka huu ,wanaharakati walidai kwamba wafanyibiashara waliagizwa na mamlaka kutouza nyama ya mbwa.

Lakini wamiliki wa vibanda vinavyouza nyama hiyo waliambia BBC hawajasikia lolote kuhusu hatua hiyo kutoka kwa maafisa.

Mnamo tarehe 15 mwezi Mei, maafisa wa mji walithibitisha kwamba hakuna marufuku yoyote.

Siku ya Jumatano, ripoti kutoka Yullin zilisema kuwa mbwa waliokufa walionekana wakiwa wametundikwa katika ndoano za nyama katika vibanda ndani ya soko la Dongkou ambalo ndio kubwa mjini humo.

Mwanaharakati mmoja aliambia BBC kwamba alikatazwa na maafisa wa polisi kuingia katika soko la Dashichang ambapo inaaminika mbwa walikuwa wanauzwa.

Katika sherehe za miaka ya nyuma kumekuwa na mzozo kati ya wauzaji nyama ya mbwa na wanaharakati waliojaribu kuwaokoa mbwa waliopangiwa kuchinjwa.

Serikali Imesema Wanaume ndio Vinara wa Michepuko

$
0
0

Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla amefunguka na kusema kuwa wanaume wengi wamekuwa vinara wa michepuko jambo ambalo linapelekea kupata virus vya UKIMWI na kwenda kuwaambukiza wanawake.

Kigwangalla amesema hayo leo bungeni wakati akijibu swali lililoulizwa na Mbunge wa Viti maalum CHADEMA, Susan Lyimo ambaye alitaka kujua kwanini idadi kubwa ya wanawake ndiyo wamekuwa waathirika wa virus vya UKIMWI, akijibu swali hilo Naibu Waziri wa Afya alikiri kuwa ni kweli kuna utofauti japo si mkubwa sana na kudai kuwa wanawake wengi wanapata maambukizi haya kutokana na utofauti wa kibaolojia wa maumbile lakini pia kutokana na mienendo ya wanawake na wanaume.

"Maambukizi kati ya wanawake na wanaume kuna uwiano, lakini hili la wanawake kuwa wengi kuonekana wanapata virus vya UKIMWI ni kutokana na utofauti ya kimaumbile ya kibaolojia kati ya wanawake na wanaume, tabia za wanaume na wanawake. Lakini wanaume wengi wamekuwa na tabia za kuchepuka sana hivyo wao wanaweza kuvitoa virus huko na kuleta kwa wamama nyumbani, maana wanaume ndiyo chanzo cha michepuko ukilinganisha na wanawake" alisema Kigwangalla

Mbali na hilo Kigwangalla aliwataka wanaume kuachana na tabia za michepuko, na kujiwekea utaratibu wa kupima afya zao na wenza wao ili wame na uhakika na afya zao na kutopeleka virus hivyo kwa wake zao majumbani kwao.

"Mimi nawashauri wanaume waepukane na michepuko watulie kwenye ndoa zao, tujiwekee utaratibu wa kupima hali zetu na wenza wetu, kwa wale ndugu zangu waislam tumepewa fursa ya kuoa hata wake nne, hivyo ni bora upime hali za wenza wako wote hao kisha uoe wote na kuepukana na michepuko tunayoi

Spika Ndugai Afunguka Wapinzani Kususia Futari

$
0
0
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai ameonyesha kuumizwa na kitendo cha baadhi ya wabunge wa upinzani kutojumuika pamoja na wabunge wenzao katika masuala ya kijamii ikiwepo kususia futari iliyokuwa imeandaliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Kufuatia jambo hilo Ndugai amewaomba viongozi  na wabunge kwa pamoja kuachana na mambo ya kujitenda kwani yanaweza kuleta athari kubwa ambazo hakuna anayehitaji, na kudai kama kuna mambo ambayo yanakwaza basi viongozi hao wanapaswa kukaa pamoja na kumaliza mambo hayo.

"Tumekuwa tukiandaa baadhi ya hizi shughuli siku ile ya bajeti tulipata nafasi ya kupata futari iliyokuwa imeandaliwa na Waziri Mkuu na wageni wote waliokuwepo, mabalozi tulihudhuria pale na ilikuwa imeandaliwa kwa wema kwa kweli. Leo (jana) pia na mimi nimepata nafasi ya kuandaa kama nilivyowataarifu lakini nikajifunza kitu kimoja ambacho sikupenda kukisema lakini ngoja nikiseme hapa kidogo, kuna baadhi yetu wengine wamekatazana rasmi kutohudhuria shughuli kama hizi, sasa mimi sitaki kuingilia uhuru wao, wana haki kufanya hivyo kama wanaona ni sawa lakini mimi mwenzao ningependa kuwashauri tu hasa viongozi wanaofanya mambo hayo kutazama tena njia zao, yako mambo mengine ni ya kijamii tu, ukifika mahali kiongozi unaanza kuwazuia watu hata mambo ya kijamii ujue unaenda mbali kidogo" alisema Ndugai

Spika wa Bunge aliendelea kutoa malalamiko yake dhidi ya vitendo vya baadhi ya wabunge wa upinzani kususia shughuli hizo za kijamii ambazo zinawaweka pamoja na kusema

"Hili bunge linavyoendeshwa labda wabunge wa kambi mbalimbali mnaweza msielewe bunge hili linaendeshwa katika mawasiliano mbalimbali ya sisi kwa sisi endapo kuna jambo linakwaza mpaka linasababisha hata watu wasipate futari kwa pamoja basi ni vizuri viongozi wa pande zote tukakaa tuzungumze na kuondoa vikwazo hivyo kama vipo maana mimi sijui kama vipo lakini kama havipo ni vizuri tuwe tunajumuika kwa pamoja, maana sera hizo zikienea na hakika kabisa na pande zingine nazo zitaanza na hakika matokeo yake italeta mipasuko ambayo hakuna anayehitaji hapa" alisisitiza Job Ndugai

Ndugai alisema kuwa yeye anatambua kuwa wanamjibu na kufanya wanayoyafanya lakini Mungu anajua kuwa wanachokifanya si busara kwa kufanya hivyo na kusema kuwa katika mwezi huu mtukufu wanapaswa kusameheana, kuombeana, kutoa mikono upande wa pili na kufanya ibada kwani si mwezi wa chuki na kubaguana.

Soma List ya Marais 9 Matajiri Zaidi Barani Afrika

$
0
0
9. Robert Mugambe
rais wa Zimbabwe amekuwa madarakani kwa takribani miaka 25 richa ya chaguzi znazofanyika nnchini humo lakini hadi hii leo bado anashikilia madaraka, anautajiri wa dola million kumi 10 za kimarekani.


8. General Idrid Deby Itno
huyu ni mwanasiasa kutoka Chad ambae amekuwa madarakani toka mwaka 1990, mwezi October mwaka 2006 jarida la Forbes lilitaja Chad kuwa ndio nnchi inayoongoza kwa rushwa duniani.ruzuku Kutoka kwenye mradi wa mafuta wa Chad-Cameroon na bomba la mafuta ambapo fedha zake zilikusudiwa kupambana na njaa pamoja na kukuza miradi ya maendeleo badala yake alitumia fedha hizo kununua majeshi na kukuza nguvu ya Idris ambae anakadiliwa kuwa na utajiri wa dola milioni hamsini 50 za kimarekani.


7. Goodluck Ebele Jonathan
huyu ni rais wa Nigeria anautajiri wa dola milioni 100 mia moja  za kimarekani.



6. King Mswati III
Huyu ni mflame kutoka Swaziland anayesifika kwa kuwa na wake wengi akiwa anamiliki utajiri wa Dollar za kimarekani $100 MILLION


5. Poul Biya
huyu ni mwanasiasa kutoka Cameroon ambae amekuwa akiingoza nchi hiyo toka November 6 mwaka 1982 rekodi inayomfanya kuwa miongoni mwa marais walioongoza kwa muda mrefu duniani kwa kipindi cha miaka 31, anamiliki kiasi cha dola milioni 200 za kimarekani inasemekana Poul Biya ndiye tajiri mkubwa huko Cameroon lakini pia imeripotiwa kuwa msafara wake ndio msafara wa gharama kuliko kiongozi yeyote duniani hata rais wa marekani kwa kutumia sio chini ya dola elfu 40 za kimarekani


4. Uhuru Kenyatta
Uhuru Muigai Kenyata huyu ni rais wa Kenya alizaliwa octoba 26 mwaka 1961 akiwa kama rais wanne wa Kenya na wasasa.

Ameanza rasmi kazi hiyo ya urais april 9 2013, pia ni moja katio ya vijana matajiri huko Kenya anakadiliwa kuwa na dola za kimarekani milioni 500, utajili huu umetokana na kumiliki zaidi ya heka 500000 kwenye ardhi ya Kenya lakini pia akiwa mwanahisa wa makampuni ya habari, hoteli pamoja na benki.



3. Teodoro Obiang Nguema mbasongo
huyu amekuwa akiiongoza equatoliar Guinea kwa miaka 34 baada ya kumuangusha mjomba wake 1979 kwa mapinduzi ya kijeshi, inasemekana chini ya uongozi wake kwenye taifa hilo lenye utajiri wa mafuta wananchi hawanufaiki kabisa na utajili huo na kuishi chini ya dola moja kwa siku, mototo wake wa kiume anafuata nyayo zake kwa kuishi kwenye bangaloo lenye thamani ya dola milioni 34 za kimarekani huko Malibu na gari aina ya Bugatti veyrons yenye thamani ya dola milioni 1.7 za kimarekani.


2. Mohamed wa VI wa Morocco
huyu aliwahi kuwa mfalme wa Morocco miaka 15 iliyopita kutoka kwenye familia ya ktajili aliweka ahadi za kuongeza ajira na kupunguza umaskini pamoja na rushwa na baadae kufanikiwa hii ilimfanya apendwe saana kuwa kiongozi mkweli kwa raia wake anautajiri wa dola billion 2.5 za kimarekani.


1. Jose Eduardo Dos Santos
amekuwa madarakani kwa takribani miaka 34 kama rais wa Angola anautajili wa dola bilioni 20 za kimarekani kama utajili binafsi, huku mwanae Isabel Dos Santos akitajwa kuwa mwanamke tajiri Afrika na dunia kama mwanamke mweusi tajiri kwa kumiliki zaidi ya dola bilioni 3.4 za kimarekani kama utajiri binafsi

Mambo 11 Aliyoyapinga Baba wa Taifa Hayati Mwl. JK. Nyerere

$
0
0
Mwalimu Nyerere ni Rais wa kwanza na ni muasisi aliyeliletea taifa hili uhuru wa kweli toka katika makucha ya mkoloni 9 December, 1961.

Mwalimu Nyerere alizaliwa April 13, 1922 katika kijiji kidogo cha mwitongo huko Butihama, kasikazini mwa Tanzania karibu kabisa na ziwa Victoria.

Alikuwa ni mototo wa chifu Burito Nyerere wa kabila dogo la wazanaki

Nyerere alifariki dunia kwa ugonjwa wa kansa ya damu, siku ya Alhamisi Oktoba 14, 1999 saa 4:30 asubuhi (kwa saa za Afrika Mashariki), katika hospitali ya Mtakatifu Thomas London, Uingereza akiwa amezungukwa na timu ya madaktari bingwa.

Ndipo wananchi wote tulipigwa na butwaa kwa kumpoteza kiongozi mwenye msimamo thabiti na busara duniani.

Mambo 11 aliyoyapinga baba wa taifa.

1. Ujinga
2. Ubinafsi Na Ufisadi
3. Ubepari
4. Ukabila Na Usehemu
5. Ubinafsishaji Holela Wa Mali Za Umma
6. Kuongozwa Kwa Rimoti Na Nchi Matajiri
7. Ubabe Na Vitisho Katika Uongozi
8. Umangimeza Na Ukiritimba
9. Usiri Wa Mikataba Na Makampuni Ya Kigeni
10. Rushwa
11. Uchu Wa Madaraka

Ukiona Haya, Fahamu Muda wa Kubadilisha Betri la Simu yako Umefika!

$
0
0
Ingawa betri la simu limetengenezwa na uwezo wa kuchajiwa mara kwa mara ila inafika muda ambao lazima libadilishwe tuu. Hasa inategemea utumiaji na utunzaji wa betri husika ila mara nyingi betri linaweza kuwa zima kabisa kati ya miezi 6 hadi miaka miwili ya kutumiwa.

Haya ndiyo ya kuangalia ili kutambua muda wa kubadilisha betri lako.

1.Muda wa betri kukaa na chaji umepungua na ata zaidi ya nusu ya mwanzo
Itakapofika muda ambao kiwango cha kupoteza chaji kimepungua kufikia hadi nusu au chini zaidi ukilinganisha na mwanzoni ulipoinunua kwa mara ya kwanza basi ujue haifai tena.

Muda mwingine utakuta simu inaonesha inakiwango cha asilimia nyingi tuu ya chaji alafu ghafla unashtukia imezima, ukiwasha inasema ‘battery low’, badilisha tuu betri.

Betri lisilofanya kazi kwa ufanisi linaathiri ata vitu vingine kwenye simu yako.

2. Simu inapata joto sana
Je unasikia simu inakuwa yamoto sana hasa hasa joto hilo likitokea eneo la betri? Epuka hatari, badili betri mara moja. Pia mara nyingi ikitokea hivi kwa simu utagundua pia ata betri halikai na chaji sana ukilinganisha na zamani.

3. Linachukua muda mrefu zaidi kujaa
Betri linatakiwa kuchukua masaa machache tuu kujaa, mara nyingi kwa simu za kisasa ni kati ya dakika 30 hadi masaa mawili hivi.

Ukiona kuna tofauti ya masaa kadhaa ukilinganisha na lilivyokuwa zamani basi ujue tayari ndani mwake mambo hayaposawa na hivyo uanze maandalizi ya kununua jipya kuepusha usumbufu wa kuchaji kwa muda mrefu kitu ambacho ni hatari.

4. Umbo limebadilika: Kuvimba
Hili jambo maarufu kwa watu wengi. Betri zuri si kwa simu ata bali ata kwenye magari, ni betri ambalo pande zote zimenyooka.

Kuonesha uvimbe katika pande yeyote ni dalili ya kwamba betri limeshachoka…yaani limetumika sana au limewekwa katika mazingira mabovu. Ukiona hivi ufanye haraka kununua jipya kwani betri lililovimba huwa na hatari ya kupata milipuko.

Hatua Za Kufanya Kama Mwanamke Hataki Kujibu Texts Zako

$
0
0
Unafukuzia mwanamke mzuri mnaanza kuzungumza. Mnachukua muda wa dakika 20 hadi 30 kuongea na yeye mara ya kwanza. Anapendeza na kuvutia, na unaona kama ni mwanamke ambaye ni yule aliyekuwa ndotoni mwako maishani mwako. Mazungumzo yenu yanaenda vizuri mpaka ukwamwomba namba yake.

Baadaye unajaribu kumtumia text na hazijibu. Labda mnaeza kuchat kwa madakika halafu baada ya hapa anakataa kujibu texts zako. Unabaki ukijiuliza maswali ni kitu gani ambacho umefanya ambacho umekosea. Ok labda anaweza kuwa yupo buzy unampa muda kiasi ajibu text zako...unangojea masaa, siku, wiki mpaka inafikia wakati unagundua kuwa amekupuuza. Kwa nini hajajibu text zako?

So kwa nini hakujibu text zako?
Katika situation nyingi ni kuwa sababu kuu ambayo amekataa kujibu texts zako ni kuwa haukumpendeza mara ya kwanza ulipokutana naye. Ok labda sababu nyingine inaweza ni kuwa ameibiwa simu yake wakati alipokuwa akitext na wewe barabarani ama kitu kingine kama hicho, lakini hapa acha tumakinike na hatua ya kwanza uliokutana naye...yaani first impression ambayo unakudana na mwanamke yeyote.

1. Hakikisha unampendeza mara ya kwanza unapokutana naye
Anaweza kuwa hana muda mrefu wa kukaa na wewe ili akutambue zaidi so kile kitu ambacho unahitaji kufanya ni kuwa lazima uuonyeshe upendo wako kwa kuwa mpole, mkarimu na mtulivu. Hii itamfanya yeye kumakinika na labda kutaka kukufahamu. Hakikisha kuwa wakati unapoongea na yeye tumia mbinu za kuonyesha kuwa ungependa kukutana na yeye wakati mwingine. Kama hakuonyesha dalili zozote za kukuelewa basi hata kama atakupatia namba yake ya simu fahamu ya kwamba itakuwa ni kazi bure.

2. Taja sababu zako za kuongea na yeye
Mfano: Nimefurahia sana kuongea na wewe. Kusema kweli nimependa maonezi yetu machache. Nataka kwenda lakini naonelea wikendi nitakutext tukutane ili tuongee tena. Hapa utakuwa umeeleza ajenda yako kwake hivyo ukianza kuchat na yeye baadae haitakuwa vigumu kwake kukujibu.

3. Hakikisha kuwa unamtumia text wakati ufaao
Ukiomba namba ya simu kwa mwanamke inamaanisha kuwa wewe umeonyesha intrest kwake vilevile mwanamke akikupatia namba yake ya simu inamaanisha kuwa labda itakuwa amependezwa na wewe. Lakini je, ni muda upi unaotakikana hadi umtext mwanamke huyo.

Wanawake wanapenda kuona wanababaikiwa na kufukuziwa. So usijaribu kumtext hapo hapo wakati amekupatia namba yake. Hakikisha umejibatia shughli nyingi ili usahau kabisa kama uchukua namba kwa mwanamke. Masaa mazuri ambayo yangekuwa sawa ya kumtext ni baada ya masaa 24 baada ya kuchukua namba yake. Hii itamfanya mwanamke yeyote kujiuliza maswali ya kwa nini umechukua muda mrefu kumtext. Itamfanya kuingiwa na maswali ya kama: kwani hajapenda chat yangu? yuko na mwingine? nk. Ukichukua muda huu mrefu hadi kumtext, itakuwa rahisi kwake kukujibi.

ONYO: Hakikisha ya kwamba haupitishi zaidi ya siku tatu kwani anaweza kukusahau kwa haraka ama kuona unampotezea wakati wake.

4. Kitu cha kuandika kwa text yako ya kwanza
Messages za kwanza ambazo utazituma kwa mwanamke zitachangia pakubwa kuona kama wewe uko uko interesting ama unaboa. Unaweza kuuharibu mchezo mzima kama iwapo utaanza kumtext na mambo ambayo hayana manufaa kwake. Kile kitu unachohitajika kufanya hapa ni kuonekana hauna haraka na ujaribu kutumia lugha za kirafiki. Mfano unaweza kujaribu kumtext swala ambalo aliligusia kwa chat iliyopita. Labda aliongea kuhusu kwenda shopping na nduguyake, so swali lakini linaweza kuwa: Je ile shopping yenu na nduguyako iliendaje?. Hii itamfanya kuwa interested na wewe manake ataona ya kuwa ulikuwa umemakinika wakati mlipokuwa pamoja. Hii itamfanya kujibu text zako mara kwa mara bila yeye kuchoshwa.

5. Jaribu kuhepa stori ambazo hazitafikia popote
Mara ya kwanza anaweza kukujibu lakini itafikia pahali atanyamaza. KUMBUKA: Siri kuu ya kumfanya mwanamke ajibu texts zako ni uwe makini kwake, yaani unamtext vtu ambavyo unajua yuko intrested navyo.

6. Weka wazi kuwa unataka mkutano
Acha stori za kumzungusha huku na huku kama wanaume wengine. Ukitaka akujibu text zako hakikisha ya kuwa unadhihirisha azma yako kwa kumwambia kuwa unataka kukutana naye.

7. Usikate tamaa
Kuna wanaume wengine kama wamekataliwa kujibiwa texts zao mara moja basi wanakasirika na wanaachana kabisa na kushungulika tena. Tatizo labda linaweza kuwa mwanamke anakupima akili aone bidii yako kwake. Kama tujuavyo tabia za wanawake ni kuwa hawapendi kuonekana kama ni watu wa kukubaliana na kila kitu hivyo basi wakati mwingine wanakuwa hawaeleweki.
Ukiona mwanamke amekataa kujibu text yako kwa siku tatu, fanya kumtext tena huku ukionyesha kuwa hauna intrest naye sana vile halafu achana naye. Hii itamfanya yeye kuona una interest na yeye lakini hauna haraka. Baadaye anaweza kuanza chat yeye mwenyewe.

KUMBUKA: Kuna sababu tofauti tofauti ambazo zinaweza kumfanya mwanamke kukataa kujibu texts zako. Labda umemtusi, hujampendeza, ni mwanamke mwenye haya nk. So hizi hatua zitategemea na vile imetokea katika situation yako

Walimu wa Vyuo Marekani Waruhusiwa Kubeba Bunduki Wakiwa Chuoni....Kisa Hichi Hapa

$
0
0
Walimu wanapewa mafunzo ya kubeba bunduki wakiwa shuleni katika jimbo la Colorado nchini Marekani ili kuwalinda watoto kama hatua baada ya mauaji ya watoto mwaka 2012.

Mafunzo hayo ya siku tatu yanayohusu bunduki na ya kutoa matibabu yalianza siku ya Jumanne katika kaunti ya Weld..

Watu 17 ambao watapewa bunduki hizo tayari wameshiriki mafunzo hayo.

Mpango huo ni wa kuruhusu watu wa kujitolea kuingia shuleni wakiwa na bunduki chini ya sheria ya Marekani ya kubeba bunduki.

Walimu walipelekwa kwa majiribio ya kupiga risasi karibu na Denver ambapo walijaribiwa uwezo wao wa kutumi bunduki.

Lakini hatua hiyo imekasirisha makundi kama ya Safe Campus Colorado, ambayo yanawashauri wafuasi kushinikiza mamlaka kusaidia kuondoa bunduki shuleni

Gigy, Amber Lulu wamlipua Msanii Mwenzao Baby Madaha

$
0
0
Kufuatia kauli ya Mbon­go Fleva, Baby Joseph Madaha maarufu kama Baby Madaha, aliyoitoa hivi karibuni kwamba ma-video queen wanaojaribu kuimba ndiyo wanaharibu heshima ya Muz­iki wa Kizazi Kipya, baadhi yao wameibuka na kumlipua vilivyo mwanadada huyo.
Bila kuwataja majina, Baby Madaha alisema kwamba wauza sura kwenye video mbalimbali za wanamuziki wa Bongo Fleva, ambao wanaingia kwenye muz­iki kwa mgongo huo, wanaharibu
 muziki ambao wao wameujenga kwa muda mrefu.



“Ma-video queen wanaoingia kwenye muziki ilimradi tu, ndiyo wanaotuharibia huu muziki ambao tumehangaika na kuhaso nao kwa muda mrefu, kwa sababu wao wanaingia tu kirahisi ili­mradi wanajifunza jinsi ya kuimba basi bila ku­jua kwamba kuna watu tumepata nao shida,” alisema Baby Ma­daha.
Kutokana na kauli hiyo warembo ambao wanafanya u-video queen huku wakiwa ni wanamuziki pia wamemjia juu Baby
 Madaha na kumtolea maneno makali huku wakimtaka awe na heshima.
Warembo waliok­erwa na kauli hiyo ni Amber Lulu, Lulu Diva na Gigy Mon­ey ambapo mapo­vu yao waliyatoa kama ifuatavyo;


AMBER LULU
“Huyo Baby M a ­daha ni msham­ba, ame­shachoka hana kitu kipya kwenye muziki, siyo mbunifu kwa hiyo wivu wa kuona vipaji vipya na wasichana wazuri kama sisi Amber Lulu, Gigy Money na Lulu Diva ambao tumepitia video queen. tulimkuta kwenye gemu na tumempita, Baby Madaha ni ‘very cheap’ kwa kweli.”


“Kwanza huyo Baby Madaha simfahamu vizuri na ningekuwa mimi ndiye yeye nimetokea BSS, ungekuta sasa hivi niko staa mkubwa Afrika lakini kwa kuwa hajiongezi ndiyo maana yupo hivyo alivyo, atuambie ana nyimbo gani inayovuma sana au amefanya kitu gani kwenye muziki ambacho tunakiharibu? Aache dharau maana hata yeye anadanga tu kwenye muziki.”


LULU DIVA
“Huo ni mtazamo wake, kwanza simfahamu Baby Ma­daha hivyo nashindwa kumzun­gumzia sana, ila angetuambia kitu gani cha maana alichokifan­ya kwenye tasnia ya muziki, vid­eo queen ni kazi kama nyingine ila watu wamekuwa wakiidharau tu.
“Nilifanya kazi hiyo kama daraja la kuniwezesha kufikia malengo ya kuwa mwanamuziki na nimefanikiwa kwa hilo, hivyo Baby Madaha anatakiwa kuan­galia upya muziki wake yaani ni wapi alipokosea ili aparekebishe na siyo kusingizia watu.”
GLADNESS MALLYA, RISASI MCHANGANYIKO

Yanga Wamekubali Yaishe Kuhusu Haruna Niyonzima..Simba Yawazidi Kete

$
0
0
Baada ya headlines za muda mrefu kuhusiana na hatma ya kiungo wa kimataifa wa Rwanda anayeichezea Dar es Salaam Young Africans Haruna Niyonzima kuhusishwa kuhama Yanga na kujiunga na Simba baada ya mkataba wake kumalizika.

Leo June 21 2017 Katibu Mkuu wa Yanga Charles Boniface Mkwasa ametangaza na kuweka wazi kuwa Haruna Niyonzima ambaye mkataba wake na Yanga unamalizika July, wameshindwa kufikia makubaliano ya kumuongezea mkataba mpya.


Hivyo ni rasmi sasa baada ya Haruna Niyonzima kuitumikia Yanga kwa misimu sita mfululizo, atakuwa nje ya Yanga kuanzia msimu ujao wa 2017/18, bado haijajulikana rasmi Niyonzima atajiunga na timu gani lakini kwa tetesi zinazoenea ni kuwa Niyonzima atajiunga na Simba.

Diamond: Nlipigiwa simu na Psquare pamoja na Fally Ipupa kuhusu ishu ya Zari

$
0
0

Nasseb Abdul maarufu kama Diamond Platnum amefunguka juu ya post ya Instagram aliyoiandika wiki chache zilizopita na baadae kuifuta baada ya picha ya mzazi mwenza Zari akiogelea na mwanaume mwingine.

Muimbaji huyo amedai baada ya tukio hilo kutokea, alipigiwa simu na mastaa mbalimbali kutaka kujua nini kimetokea.

“Baada ya post yangu ya insta wasanii wengi walinipigia simu, Psquare na Fally Ipupa walinicheki kutaka kujua nini kimenikuta,” alisema Diamond.

Diamond amesema baada ya kupost picha pamoja na ujumbe ambao haukuwa mzuri kwa Zari, mrembo huyo wa bosi wa WCB alionyesha kutofurahishwa na ujumbe huo.

“Baada ya Zari kuona post yangu Insta alikuwa ofisini na alirudi nyumbani na aliponielewesha nilikuwa mpole na nikamuelewa,” alisema Diamond.

Hata hivyo shemeji yake ambaye ni binamu wa marehemu Ivan, alikanusha tuhuma za kutoka na mrembo na kusema hawezi kufanya hivyo na kwani anamuheshimu.

Kila Ninachoongea na Mchumba Wangu Anaenda Kudiscuss na Mama Yake..Sipendi , Nifanyaje?

$
0
0

Jambo moja linalonitatiza ni huu:-Mpenzi wangu anaongea na mama yake saana.kwa nini ninaudhika?

kwa sababu anamwambia mambo yote ya kisiri ambayo bwana na bibi inafaa waongee.

kwa mfano...last time tulivyogombana ilikuwa hivi:-nilimuuliza :kwa nini ulienda town jana,ukaniambia unaenda kununua frem ya spectacles

na leo ukaniambia unaenda kuona customers town pia?akanijibu mimi nilienda kuona customers leo.jana nilienda kuleta frems nikamuuliza si ungeenda siku moja kuleta frem na kuona customers?

alivyofika nyumbani tukagombana...baadaye akampigia mamake, akamwambia

"ananiambia nilikuwa nimeenda kupeana dyudyu"

nilishangaa sana nikajiuliza, kwani mpenzi yangu anaongea maneno haya chafu na
mammake ,, kila kitu anasema, kwanini?
hebu nishauri vile nitakavyoendelea...

Naomba Niongee na Ninyi Waajiriwa Makazini Mnaomwamini Mungu..

$
0
0

NAOMBA NIONGEE NA NINYI WAAJIRIWA MNAOMWAMINI MUNGU..!!

Ndugu mpendwa mwajiriwa,
Nakusalimu kwa salamu za kiuchumi.

Sina chai ya kuuza leo, bali ninaenda chapchap kwenye points na kiini cha waraka wangu.

TWENDE...

Naomba unitajie mtu yeyote unaemfahamu katika Biblia kuanzia Mwanzo hadi Ufunuo ambae alibarikiwa kiuchumi na hakuwa mjasiriamali ama mfanyabiashara. Mtaje tu, nami nikufunulie Biblia na notisi zangu "nikusute" na "umbumbumbu" wako.

Unaniumiza sana ninapoona unasubiri Mungu akubariki kiuchumi, halafu huchukui hatua zozote kujifunza ama kujishughulisha na ujasiriamali ama biashara japo hata kuanza na kidogo ulichonacho. Hilo pepo linalokuaminisha kwamba wewe uliumbwa spesho kwa ajili ya kuajiriwa kiasi kwamba ujasiriamali na biashara unaona havikuhusu, ninalikemea kwa Jina la Yesu, maana ndilo linalomzuia Mungu kukupeleka mbali kiuchumi zaidi ya ulipo.

Tarehe 1 hadi 30, Januari hadi Desemba, unachokumbuka ni kuwahi kazini na kusubiri mshahara, baaaasiiii, halafu unataka Mungu akubariki zaidi kiuchumi. How? Ni kweli unatoa sadaka kwa uaminifu, ni kweli unasali sana, lakini kwa uzembe huo wa kutojiongeza kiujasiriamali, its impossible kwa wewewe kuja siku uwe "financially free". Utamlaumu Mungu kwa kupendelea wengine kumbe shida ni wewe mwenyewe maana Mungu hana upendeleo.

Hiyo bidii uliyonayo kazini ulikoajiriwa laiti ungeielekeza na kwenye kijibiashara japo cha genge tu, sasa hivi (mwaka wako wa saba kazini) ungekua unajenga nyumba yako ya tatu kule Chanika ama Bagamoyo Road. Mfanyakazi unaemwamini Mungu, iwe umeajiriwa serikalini ama private, ukifanya kazi miaka mitano mfululizo, pasipo kufanikiwa kujenga nyumba yako (nzuri) ya kuishi, trust me, unakua ume-under utilize uwezo wa Mungu kukubariki! Wake up! (Rudia mare nne hii paragraph hadi ikuingie kabisa)

Kama unalipwa laki nane kwa mwezi, usitegemee kwenda benki siku moja na kukuta zipo milioni tatu. Hivyo sivyo Mungu anavyobariki, na ukiona hela zilizozidi mshahara wako kwenye akaunti, nenda kazirudishe kwa mwajiri maana watakua wamekosea. Hivi unaelewa kwamba kuongezewa mshahara ama kupandishwa daraja sio mambo yatakayokusaidia kupata uhuru wa kiuchumi?

Hivi unajua kuwa hakunaga mshahara mdogo ama mshahara mkubwa ila ukubwa ama udogo unategemea akili inayoushika mshahara husika? Tatizo sio JPM. By the way kwani kwa JK ulifanya kipi cha maana kwa mshahara wako? Achana na mipigo na posho za kizembe mlizokuwa mnajipatia, maana vingine humo itabidi mkatubu:- hapa naongelea ulichofanyia mshahara wako na marupurupu halali. Utamuonea Magufuli wa watu bure kwamba kafanya maisha yako ya ajira kuwa magumu, kumbe shida ni akili yako na uzembe wako wa kutoji-position vizuri na Mungu ili akubariki kupitia namna unavyoutumia mshahara wako kama mbegu kwenye ishu za ujasiriamali na biashara.

Unalipwa laki sita kwa mwezi then unaniambia mshahara hautoshi. Whaaaaaat????? Hapo hapo kuna mama (tena la saba B) yupo mtaa wa pili anauza mboga gengeni, mtaji wake ni elfu hamsini lakini hadi sasa keshanunua kiwanja na tayari ameshajenga nyumba yake chumba na sebule:- wewe na "lilaki sita lako" na digrii juu, ukifika muda wa kulipa kodi chumba na sebule miezi sita, unatetemeka hadi jasho linafika kwenye nyayo! Kuna shida kubwa kwenye akili yako, sema tu hujajishtukia!

Mie ninakushangaa hadi unaniudhi ujue! Haya yataendelea maishani mwako mpaka lini? Leo kodi tu inakutoa jasho, je siku watoto wako wanne wakiwa English Medium Schools, ada milioni sita kwa term, utafanyaje? Ofcourse najua wengine mko level hiyo ya kusomesha na yanayowapata ni siri yenu na Mungu wenu, maana sio kwa kupaniki huko kila msimu wa ada unapofika!

I CAN SEE "CLEARLY"....

Something is wrong somewhere and you have to fix it haraka sana. Mshahara (even if wawe wanakulipa take home ya milioni nne) will never give you financial freedom my dear. Hebu anza serious kufanyia mambo huo mshahara hata kwa Online Investment au Network Marketing au ujasiriliamali mwingine wowote ili umpe Mungu nafasi ya kukubariki beyond measures. Acha woga, acha kujifanya ama kujisemesha eti ajira imekutinga sana, hebu jitoe sadaka pambana, fanya kitu cha kiujasiriamali. Usidhani ni sifa kusema eti ajira imekubana wakati unaendelea kuteketea kiuchumi.

Hebu acha ujinga bana, haaa! Ninakupenda ndio maana nimekuja kukueleza haya, otherwise ningetulia zangu maskani na wanangu niendelee na mishe zangu.

Kila nilichokuandikia hapa nimekitoa katika Neno la Mungu hata kama sijanukuu moja kwa moja maandiko. Kwa hiyo, naomba usinichukie mimi, na kama una kipaji cha kumaindi watu, basi m-maindi Mungu anaekuwazia mema na alienisukuma nizungumze na wewe kwa niaba yake. Najua huu ni waraka mgumu, so, hata ukiamua kuto-like, sitashangaa, ila ujumbe umefika, au sio? (Jibu hata kimoyo moyo, baaaaasi)

Ni mimi msemaji katika Ufalme wa Mungu,
Idara ya Uchumi.
#SmartMind

Mwanasheria Mkuu TBS akamatwa tena baada ya kuachiwa huru

$
0
0

Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemfutia kesi Mwanasheria Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Baptister Bitaho (54) aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka matatu ikiwamo kuishi na kufanya kazi nchini bila kibali.

Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa alimfutia mashtaka Mwanasheria huyo wa TBS leo (Jumatano) baada ya Mwendesha Mashtaka wa Uhamiaji, Method Kagoma kuiomba mahakama imfutie makosa hayo chini ya kifungu cha 98 (a) cha sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai (CPA).

Hata hivyo baada ya mshtakiwa huyo kuachiwa huru alikamatwa tena na yupo katika Idara ya Uhamiaji kwa ajili ya mahojiano.

Awali, Mwendesha Mashtaka wa Uhamiaji, Novatus Mlay akimsomea mashtaka mshtakiwa huyo, alidai kuwa Mei 19, 2017 huko Kinondoni katika ofisi ya uhamiaji, Bitaho akiwa raia wa Burundi alikutwa akiwa nchini bila ya kuwa na kibali.

Imedaiwa kuwa, Bitaho siku hiyo alikutwa akifanya kazi kama Mwanasheria Mkuu wa TBS bila ya kuwa na kibali kinachomruhusu kufanya kazi hapa nchini.

Kadhalika, inadaiwa kuwa, Julai 6 mwaka 2011 katika ofisi ya Uhamiaji ya Dar es Salaam iliyopo Wilaya ya Ilala, mshtakiwa huyo akiwa raia wa Burundi alitoa taarifa za uongo kuhusu maelezo yake binafsi wakati akijaza fomu ya kuomba hati ya kusafiria namba CT (5)(Ai).

Wakili Mlay ameongeza kuwa, kitendo hicho cha kutoa taarifa za uongo kilimuwezesha Bitaho kupata hati ya kusafiria ya Tanzania yenye namba AB 474856 huku akijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria za nchi.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, mshitakiwa aliyakana na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Mshitakiwa yupo nje kwa dhamana baada ya kukamilisha masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika ambao kila mmoja alisaini bondi ya Sh 20 milioni.

Ndege ya Nato yakimbizwa na ndege ya Urusi

$
0
0

Ndege ya jeshi la NATO imeikaribia ndege ya Urusi iliyokuwa imembeba waziri wa ulinzi wa Urusi lakini ikafukuzwa na ndege ya jeshi la Urusi iliyokuwa ikiisindikiza ndege hiyo.

Vyombo vya habari vilisema kuwa kisa hicho kilitokea katika anga ya kimataifa eneo la Baltic, wakati Sergei Shoigu alikuwa akisafiri kuenda himaya ya Urusi ya Kaliningrad.

Nato baadaye ilisema ilifuatilia ndege za Urusi lakini haakujitambulisha.

Mapema Marekani ilisema kuwa ndege ya jeshi la Urusi iliikaribia ndege ya ujasusi ya Marekani umbali wa mita 1.5.

Lakini Urusi ilisema kuwa ndege hiyo ya ujasusi ilikuwa imefanya uchokozi.

Visa kadhaa kama hivo vimeripotiwa miaka michache iliyopita huku Nato na Urusi wakilaumiana.

Kulingana na mashirika ya habari ya Urusi ndege ya F16 ilipita karibu na ndege ya Shoigu.

Yanasema kuwa kisha ndege ya Urusi ya Su-27, ikaingilia kati na kutoa ishara kuonyesha kuwa ilikuwa imejihami.

Kisha ndege ya Nato ikaondoka.

Rungu la Magufuli Lahamia Dawasa....Amtaka Mkuu wa Mamlaka Hiyo Ndugu Mtalemwa Ajitumbue

$
0
0

Pwani. Rais John Magufuli amemtaka Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (Dawasa) Archado Mtalemwa ajiandae kustaafu kutokana na mapungufu mengi ambayo Rais amesema ameyaona katika mamlaka hiyo.

Rais ameyasema hayo leo(Jumatano) akiwa katika ziara yake ya siku tatu mkoani Pwani na alitumia fursa hiyo kuzungumzia miradi ya maji na ulipaji wa maji kwa taasisi za serikali.

“Ndugu yangu Mtalemwa, naongea kwa lugha nzuri hapa, nikuombe tu kuwa ustaafu mapema, inawezekana Waziri wa Maji ni rafiki yako, kama ilivyo kwa mawaziri wengine, lakini nadhani huu ni wakati mzuri,” amesema na kuongeza;

“Pamoja na kazi zako nzuri, it’s your time to go.”

 Amezungumzia kero mbalimbali za maji na kusema kuna upotevu mkubwa wa maji.

Okoa Ndoa Yako Sasa, Ongeza Maumbile na Nguvu za Kiume Hata Kwa Wenye Kisukari Kwa Kutumia Products za Markson Beauty

$
0
0
OKOA NDOA YAKO SASA. ONGEZA MAUMBILE, NGUVU NA HAMU YA TENDO LA NDOA HATA KWA WENYE KISUKARI. Tatizo la maumbile madogo, nguvu za kiume na ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limekuwa likiwasumbua wengi na kusababisha kushindwa kujiamini ktk tendo hivyo kusababisha ndoa nyingi kuvunjika pamoja na mahusiano. Upungufu wa nguvu na hamu ya tendo husababisha mambo kama:-
(a)Uume kulegea wakati wa tendo (b)Kukosa hamu ya tendo la ndoa (C)Kuwahi kufika kileleni (D)Uume kuchelewa kusimama baada ya round ya kwanza. (E)Kuchoka sana baada ya round moja n.k @Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo kwa kutumia bidhaa zilizotengenezwa kwa mimea na matunda zisizo na kemikali wala madhara na kuthibitishwa kiafya. Pata hizi👇👇👇👇
🍉 🌿🍅🍒🍍🍓🍉🍎🍀
1.HANDSOME UP ni kifaa chenye uwezo wa 99 % kuongeza uume (size unayohitaji) na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200000@200,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130000@130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130000@130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo hata mara 3 @130000@130,000/= Kwa Bidhaa hizi na nyingine kama:-
5.Kupunguza unene na manyama uzembe @150000@150,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi @130000@130,000/=
7.Kutengeneza shepu (hips, makalio na mapaja) @200000@200,000/= 8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni @120000@120,000/=
9.Kuwa mweupe na soft mwili mzima bila kuacha sugu 120,000/=
10.Kurudisha usichana (bikra) @120000@120,000/=
11.Kupunguza au kuongeza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120000@120,000/=

Wasiliana nasi kwa (+255) 0767447444 au 0714335378.

NB: Matokeo ni uhakika na garantii na upate risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii. Follow us
@Markson_beauty_pr

G Nako Afunguka ishu ya Kulala Kwenye Jeneza

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva kutoka kundi la Weusi, G Nako ameelezea issue yake ya kulala kwenye jeneza kama inavyoonekana kwenye video ya wimbo ‘Lucky Me’.


G Nako amesema baada ya video hiyo kutoka kuna watu wameogopa na kuwa na hofu lakini baada ya kuwaelewesha walielewa.
“Sijavuka mipaka nilichokuwa najaribu kukifanya ni sanaa, na sanaa haina mipaka na kuna baadhi ya watu wamepokea vizuri asilimia ndogo wamepokea kidogo lakini wakieleweshwa wanaelewa,” ameiambia E-Newz ya EATV.

“Watu wanaingia kwenye majeneza kila siku, watu wanauliwa kwenye movie kila siku, sio kitu kigeni sana ni kwa sababu tumechelewa kuingia kwenye tasnia ya muziki. Jeneza lilikodishwa, kununua kidogo itakuwa ngumu, actually walikuwepo wenye mali yao kwa hiyo baada ya kumaliza kulitumia wakalichukua kwenda kufanyia shughuli nyingine,” ameongeza G Nako.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images