Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Mastaa Wengi ni Wasumbufu Kwenye Mapenzi – Amber lulu

$
0
0
Video vixen na mwanamuziki kutoka hapa Bongo Amber Lulu amebainisha kuwa mastaa wengi katika kiwanda cha burudani ni wasumbufu sana ukiingia nao katika mahusiano ya kimapenzi.



Amber mwenye Lulu zake amebainisha hayo kupitia Bongo Dot Home ya Time Fm kuwa ” Mastaa wengi bongo ni wasumbufu sana, mimi huko nyuma niliwahi kuwa katika mahusianio na hao mastaa nikaona aah basi bora niachane nao, naona walivyo kwa sasa na najua wanavyoishi ndio mana sina mpango nao.”

“Wastaa wengi hawako serious sana na hata kwenye maisha yao hawako serious, mie naona mastaa naoshindanao naona kabisa hata akiwa na mpenzi kuna kitu kinamiss , unakuta mtu anakaa na watu hata watano yani,” amesema Amber.

Kwa sasa mrembo huyo ameelekeza nguvu zake katika muziki na huwenda tusimuone mara kwa mara akitokea katika video za watu.

Diamond Platnumz Amkana Hamisa Mobeto

$
0
0
Msanii wa muziki Diamond Platnumz amekanusha taarifa ambazo zimekuwa zikizagaa katika mitandao ya kijamii kuwa Hamisa Mobeto ana mimba yake.


Aidha muimbaji huyo amekanusha pia kuwahi kutoka kimapenzi na video queen huyo ambaye anatikisa katika tasnia ya urembo.

Akiongea katika kipindi cha XXL cha Clouds Fm Jumatano hii wakati akiutambulisha wimbo wake mpya ‘I Miss You’, Diamond amedai tetesi za yeye kutoka kimapenzi na Hamisa zilianza baada ya kufanya naye kazi katika project ya wimbo, Salome.

“Toka nimeshoot na Hamisa Mobeto wimbo wa Salome, watu wamekua wakituhusisha pamoja, ujauzito wa Hamisa sio wangu,” alisema Diamond. “Jamani mwenye mimba si ajitokeze, si unajua hata mtu wake atakuwa anajisikia vibaya,”

Pia muimbaji huyo amedai wasichana wengi ambao anafanya nao kazi upakaziwa kuwa anatoka nao kimapenzi.

Askari Wawili wa Usalama Barabarani Wauawa Kwa Kupigwa Risasi Kibiti

$
0
0
Picha imefichwa kwa Maadili
Rufiji. Askari Polisi wawili wa kikosi cha usalama wa barabarani wilayani Kibiti ambao majina yao bado hayajatambulika wapigwa risasi na watu wasiojulikana katika Kijiji cha Msafiri,Kata ya Bungu wakiwa kazini.

Mbali na kupigwa risasi, pia watu hao wamechoma moto gari moja na pikipiki moja za askari hao kisha kutokomea kusikojulikana.

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Onesmo Lyanga amethibitisha kutokea kwa tukio na kusema anafuatilia.

Tukio hilo limetokea kilomita chache kutoka eneo ambalo waliuawa askari polisi wanane kwa kupigwa risasi katika eneo la Mkengeni walipokuwa wakitoka doria katika Kijiji cha Jaribu.

Maalim Seif Apata Pigo Kubwa zaidi Kutoka Kwa Lipumba, Bodi ya Lipumba Yasajiliwa na Ruzuku itakuwa yao

$
0
0
Kambi ya Cuf ya Ibrahim Lipumba imethibitisha bodi yao kupata usajili mpya kutoka RITA na sasa bodi ya wadhamini ya zamani imefutwa
Kwa sasa miamala yote ikiwemo ruzuku itakuwa inaingia kwenye akaunti na watakuwa wanachukua upande wa Lipumba na kutokana na bodi hiyo kufutwa wamesema kesi zilizokuwa zimefunguliwa dhidi yao na bodiya zamani watahakikisha zimefutwa.
Upande wa maalim seif wamesema kwa sasa hawana cha kuzungumza hadi watakapokaa
RITA walipopigiwa simu hawakupokea

Wazazi Wengi Huwakataza Watoto Wao Wasioe Wanyakyusa, Wachaga na Wahaya...Nini Sababu?

$
0
0
Habari wadau.... Topic hapo juu inajieleza huwa najiuliza hili swali bila majibu..coz wazazi wengi huishia kusema tuu nimesema usioe mnyakyusa,mhaya au mchaga..bila kutoa ufafanuzi..kwanini..hebu tujadiliane..kama unafahamu chochote kuhusu makatazo Haya Funguka Hapa Tafadhali. .
By kibona

Kutana na Maalim Fadhil Rashid Kutoka Komoro ni Mtaalam wa Tiba za Asili Anayetibu Magonjwa Yafuatayo

$
0
0
KUTANA NA MAALIM FADHIL RASHID KUTOKA KOMORO NI MTAALAM WA TIBA ZA ASILI

UNASHIDA NA MCHUMBA UNATATIZO PESA HAIKAI KURUDISHA MUME AU MKE KWA MUDA MFUPI MVUTO WA MAPENZI

MVUTO WA BIASHARA KUMSHIKA MUME AU MKE ASIKUSUMBUE

DAWA YA ( LIMBWATA )KUMTAWALA MPENZI WAKO KWA SABABU MAALUM

KUSAFISHA NYOTA ILI UWE NA MUONEKANO

NA PIA ANATOA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA PESA BILA MASHARTI

NA KUMILIKI MALI DAWA YA KUONGEZA UUME SAIZ UIPENDAYO

DAWA YA NGUVU ZA KIUME INAPATIKANA PIA ANAYO DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEP KUA NA UMBO BOMBA UMEIBIWA AU KUDHURUMIWA UTARUDISHIWA MALI YAKO NDANI YA MASAA 24 ANAFUNGA KESI NA KUPATA HAKI YAKO

DAWA YA MVUTO WA BIASHARA KUUZA MALI YAKO KWA HARAKA KUZUIA CHUMA ULETE

NA KUONDOA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI ACHA KUTESEKA ACHA KUHANGAIKA MAALIM FADHIL RASHID

YUPO TANZANIA KWA AJIALI YAKO. CALL...+255719362806/
+255763276239

WhatsApp IMO +255785786436

Nionavyo Mimi, Hakuna Haja ya Uchaguzi wa Urais 2020

$
0
0
Mie ni miongoni mwa Mamilioni ya watanzania ambao tunaamini hakuna haja ya kufanya uchaguzi wa Raisi mwaka 2020, kwani itakuwa ni kupoteza pesa tu.Hatuoni wa kushindana na Magufuli kwenye uraisi kutokana na kasi yake ya kiutendaji.

Hii ni kutokana na Uzalendo mkubwa na maono aliyonayo Muheshimiwa Raisi wetu Dr John P Magufuli. Ni mtu aliyedhamiria kupambana na rushwa, ufisadi, umasikini, maradhi na kukuza uchumi kwa vitendo.

Ndani ya muda mfupi tu ameweza kurejesha morali wa utendaji kazi serikalini kwa slogani yake ya HAPA KAZI TU na pia kufunga mirija ya upotevu wa mapato ya serikali.

HAKIKA ni raisi ambaye Tanzania ILIMUHITAJI. Kufanya uchaguzi wa Uraisi 2020 itakuwa ni kupoteza muda na resources zetu tu, na hakuna haja hiyo! Labda tufanye wa kutafuta madiwani na wabunge tu

Je Wewe Unaonaje Mdau?

By Kansigo From JF

Kila Mwanamke Anatamani Kutoka na Diamond – Amber Lulu

$
0
0
Msanii na Video Queen anaekuja kwa kasi kwenye kiwanda cha Bongo Fleva, Amber Lulu ameweka wazi hisia zake kwa msanii wa Bongo Fleva Diamond Platnumz kwa kusema kuwa yupo tayari kutoka kimapenzi na Baba Tiffah kama ikitokea.

Tokeo la picha la amber lulu
Amber Lulu

Amber Lulu amesema kwa sasa hapa Bongo anavutiwa sana na Diamond Platnumz sio tu kwa kazi zake bali hata ikitokea wakawa wapenzi yeye yupo tayari kwani hakuna mwanamke asiyependa kuwa nae.

“Kibongo Bongo sijaona mwanaume zaidi ya Diamond kwanza ana ni inspire na maisha yake yaani anajiweka kazi na kila kitu na sio kwamba na wish ku’date nae tuu bali kufanya nae kazi pia,” amesema Amber Lulu huku akisisitiza kuwa kila mwanamke ana ndoto za kuwa nae.

“Kama ikitokea kutembea nae is ok….sio mimi peke yangu kila mwanamke anawish kuwa nae…kila mtu mimi naamini wachache sana ambao hawamuhitaji,” amesema Amber Lulu kwenye mahojiano yake na Times FM.

Hata hivyo mrembo huyo amesema Diamond Platumz kwa sasa ni Baba na ana familia yake hivyo hafikirii sana kuwa nae kimapenzi zaidi ya kufanya nae kolabo.

Rais Magufuli: Hata Kama Ikulu Hawajalipa Bili ya Maji, Katani

$
0
0
Rais John Magufuli amesema taasisi yoyote ambayo haitalipa bili za maji, hata kama ni Ikulu ikatiwe maji.

Aliyasema hayo  jana Jumatano katika ziara yake ya siku tatu mkoani Pwani na kusisitiza kuwa miradi ya maji na ulipaji wa bili za maji ni muhimu.

“Mtu asipolipa bili, iwe taasisi yoyote hata kama ni Ikulu, narudia kusema kata,” alisema na kuongeza:

“Kwa sababu tumezoa kudekezana, kwenye mawizara haya nafahamu, fedha za OC na hata fedha za bajeti wanazo, lakini suala la bili ya maji linakuwa si la lazima.”

Alisema unamkuta kiongozi ana faili la kwenda Ulaya, anaenda kwanza Ulaya, ana semina analipa kwanza semina maji anaona si lazima.

 “Lakini pale hakuna maji, na wale hawajalipia bili, kwa hiyo fundisho la hapa ni kukata,” alisema.

Alisema hata kama ni hospitali wakatiwe kama hawajalipa kwa sababu wana bajeti.

Alisema kama Mkurugenzi wa wilaya yupo na maji yamekatwa, basi hafai kuwa mkurugenzi.

“ Tukifukuza wakurugenzi kama 10, 20 hivi wale wengine watawahi kwenda kulipa bili za maji,” alisema.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Siku ya Leo Alhamisi

BREAKING: Mkuu wa Majeshi aahirisha ziara yake Kibiti

$
0
0

Pwani. Mkuu wa Majeshi nchini, Jenerali Venance Mabeyo ameahirisha kufanya mazungumzo na wazee wa Kibiti.


Mkuu wa Wilaya ya Kibiti, Gullamuhusein Kifu amesema ni kutokana na mkuu huyo kupangiwa majukumu mengine ya kikazi.


Awali, Mabeyo alitarajiwa kufika Kibiti kufanya mazungumzo na wazee kwa ajili ya kuimarisha hali ya usalama mkoani humo ambamo kumekuwa na mfululizo wa mauaji hasa ya viongozi wa vijiji.

Baada ya vigogo wa Ecrow Takukuru yahamia kwenye Kashfa nyengine

$
0
0

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imesema itawafikisha mahakamani kutegemeana na ushahidi watuhumiwa wote waliojihusisha na jinai,-


ikiwamo kashfa nyingine nje ya Akaunti ya Tegeta Escrow ambayo wahusika wake wakuu walinyimwa dhamana na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mwanzoni mwa wiki.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, Ofisa Uhusiano na Mawasiliano wa Takukuru Makao Makuu, Mussa Misalaba, alisema kuna tuhuma mbalimbali zinazofanyiwa kazi, ikiwamo zilizoainishwa na Bunge.

Nipashe ilitaka kujua hatua zinazochukuliwa katika utekelezaji wa maazimio ya Bunge nje ya akaunti ya Tegeta Escrow, ikiwamo utoroshaji wa mabilioni ya fedha kwenda Uswisi, Richmond, Operesheni Tukomeza na North Mara.

"Kosa la jinai haliishi hadi mhusika afariki," alisema Misalaba. "Kama kuna kikwazo, ni suala la muda... uchunguzi ni mchakato mrefu."

"Kesi ya jinai inapokuwapo inachukua muda mrefu. Tunaendelea nayo hadi ushahidi wa kuturidhisha kuwafikisha mahakamani ukamilike.

"Maadamu (mtu) alishatenda jinai, (jambo hilo) halitakwisha hivyo tutawatafuta kokote waliko na hatua stahiki zitachukuliwa.
"Kila tuhuma tunaifanyia kazi."

Jumatatu wafanyabiashara Harbinder Singh Sethi na James Rugemarila walifikishwa mahakamani kwa makosa ya uhujumu uchumi, kwa matendo yanayotokana na uchotwaji fedha za akaunti Tegeta Escrow.

Mwaka 2013 Kamati ya Maliasili, Ardhi na Mazingira iliwasilisha ripoti ya uchunguzi wa Operesheni Tokomeza na kupendekeza Serikali iwachukulie hatua stahiki za kinidhamu wasaidizi wakuu wote wa Wizara ya Maliasili na Utalii, walioshiriki katika mpango kazi huo.

Kamati hiyo pia ilibaini kuwapo mchezo mchafu unaofanywa na baadhi ya maofisa wanyamapori, maofisa misitu katika mapori ya akiba, misitu ya serikali na katika baadhi ya hifadhi za taifa kwa kupokea rushwa, kutesa wananchi, kuwabambikia kesi na kujihusisha na ujangili.

Kufuatia ripoti hiyo, mawaziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Maliasili na Utalii na Mambo ya Ndani ya Nchi walijiuzulu nyadhifa zao.

Maazimio ya Bunge kuhusu akaunti ya Tegeta Escrow yalifuata mwaka mmoja baadaye.

Katika maazimio hayo ya 2014, Bunge lilitaka Takukuru, Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kuchukua hatua stahiki dhidi ya watu wote waliotajwa na taarifa maalum ya kamati kuhusika na vitendo vyote vya jinai kuhusiana na miamala ya akaunti ya Tegeta Escrow.

Mei 11, mwaka huu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alimuuliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ni kwa nini maazimio mbalimbali ya Bunge kuhusu uchukuliwaji wa hatua za kisheria kwa watuhumiwa hayatekelezwi.

Katika swali lake, mbali na kashfa hizo mbili, Mbowe ambaye ni Mbunge wa Hai (Chadema) alitaja pia kashfa ya ufichwaji wa mabilioni ya fedha katika akaunti za siri nchini Uswisi.

Lakini sasa, Misalaba amesema masuala yote hayo yapo chini ya uchunguzi wa Takukuru na ushahidi ukipatikana wahusika watafikishwa mahakamani.

Prof.Muhongo atoweka

$
0
0

Mei 24, mwaka huu, Rais John Magufuli alitengua uteuzi wa Prof. Muhongo katika baraza la mawaziri, ikiwa muda mfupi baada ya kukabidhiwa ripoti ya kamati ya kwanza ya uchunguzi wa mchanga wa dhahabu (makinikia).

Hata hivyo, uchunguzi wa Nipashe umebaini kuwa mtaalamu huyo wa jiolojia wa kimataifa hakuwapo bungeni wakati uteuzi wake wa uwaziri ukitenguliwa, huku taarifa zikidai alirudi nyumbani kwao, Musoma mkoani Mara, kuhudhuria mazishi ya dada yake.

Simu ya Prof. Muhongo iliita bila kupokewa alipotafutwa na Nipashe kwa siku tofauti, ikiwamo jana, kuzungumzia sababu za utoro bungeni.

Kutokana na kutoonekana bungeni kwa Prof. Muhongo, Nipashe jana ilizungumza na Katibu wa Bunge kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma, Dk. Thomas Kashililah, ambaye alisema ofisi yake haina taarifa za Mbunge huyo wa Musoma Vijijini (CCM) jambo ambalo ni kinyume cha utaratibu.

Kiongozi huyo wa Bunge pia alisema ofisi yake haijui aliko tangu alipoachishwa nafasi ya uwaziri mwishoni mwa mwezi uliopita.

Dk. Kashililah aliongeza kuwa kwa kawaida mbunge anapokuwa na udhuru, humwandikia Spika kumwelezea hatakuwa bungeni kwa muda fulani na ofisi ya Katibu wa Bunge hupewa nakala.

"Sijapata nakala yoyote ya udhuru wa Profesa Muhongo na wala sijui alipo tangu siku ile," alisema Dk. Kashililah.

Katibu wa Bunge huyo alisema hii ni mara ya pili kwa Muhongo kuondoka bungeni kwa muda mrefu bila ya ruhusa kwani hata alipomwandikia barua ya kujiuzulu Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete, hakuhudhuria Bunge kwa muda mrefu.

Prof. Muhongo alijiuzulu nafasi ya Waziri wa Nishati na Madini Januari 24, 2015 kwa shinikizo la Bunge, kutokana na taarifa ya kamati moja ya chombo hicho juu ya kashfa ya uchotwaji fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow.

KUFUKUZWA UBUNGE
Alipoulizwa hatua ambazo Bunge linaweza kuchukua dhidi ya mbunge mtoro, Dk. Kashililah alisema mhusika anaweza kufukuzwa ubunge.

"Hilo liko wazi kwenye Katiba, mbunge asipohudhuria mikutano mitatu ya Bunge, anapoteza sifa ya kuwa mbunge, lakini ni nadra sana mbunge kutohudhuria mikutano mitatu," alisema.

Ibara ya 71(1)(c) cha Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 kinasema: "Mbunge atakoma kuwa mbunge na ataacha kiti chake katika Bunge ikiwa mbunge atakosa kuhudhuria vikao vya mikutano ya Bunge mitatu mfululizo bila ya ruhusa ya Spika."

Mbunge wa Misungwi, Charles Kitwanga (CCM) naye hakuhudhuria vikao vingi vya Bunge baada ya uteuzi wake katika nafasi ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kutenguliwa na Rais Magufuli mwanzoni mwa mwaka jana.

Aidha, Septemba 16, mwaka jana, alipokuwa akihitimisha mkutano wa nne wa Bunge la 11, Spika Job Ndugai aliwakaripia mawaziri wasioshiriki vikao vya Bunge na vya kamati za kadumu za chombo hicho cha kutunga sheria na kuweka wazi kuwa anakusudia kuwashtaki kwa Rais John Magufuli ili wachukuliwe hatua.

Kiongozi huyo wa Bunge pia aliwaonya wabunge watoro na kutahadharisha kuwa atawashtaki kwa wananchi na vyama vyao vya siasa iwapo wataendelea na tabia hiyo.

Alisema kadhia ya utoro miongoni mwa mawaziri na wabunge imekuwa ikiathiri utendaji kazi wa Bunge na kamati zake.

"Mahudhurio kwenye kazi za kamati, ukiondoa kamati ya PAC (Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali), kamati nyingi zilizobaki mahudhurio yake si mazuri sana. Si mazuri kwa mawaziri, si mazuri kwa wabunge baadhi," alisema. "Ninaomba kule tunakokwenda tuzingatie sana mahudhurio kwa pande zote mbili.

"Tumetengeneza orodha ya watoro. Mawaziri watoro, wabunge watoro kwenye kamati, lakini nimesema niitunze tuangalie na kwenye kikao kijacho.

"Kama watoro hao wataendelea, basi tutawaambia waajiri wao kwa maana ya wapigakura wenu, kwa maana ya vyama vyenu, kwamba mbunge huyu na mbunge huyu kazi zetu kwenye kamati za Bunge hafanyi, ili hivyo vyama vijue.

"Na kwa upande wa mawaziri, basi tutamwambia 'Namba Moja' kwamba hawa hawawajibiki. Kwa hiyo, natoa nafasi kwa mawaziri na wabunge kuhakikisha mnapanga ratiba zenu mapema."

*Imeandikwa na Joseph Mwendapole (DODOMA) na Sanula Athanas

Maalum kwa kina Dada, Sheria 5 za Kumridhisha mwanaume wako kimapenzi!

$
0
0

Mtaalam wa mapenzi, Bi. Layla Quinn, anasema wamaume ni viumbe rahisi sana kuridhishwa tunapokuja katika suala la unyumba. Mwanzoni, kitu kinachomhamasisha mwanaume kujamiiana ni muonekano wako (mwanamke) tu wakimahaba, lakini kadri siku zinavyokwenda ndani ya mahusiano, inakuwa ngumu kupandisha munkari wake, hata kama wewe ni mwanamke mrembo barabara!

Bi. Layla anaendelea kusema kuwa, kumridhisha mwanaume wako kitandani inaweza ikawa rahisi kama tu utakumbuka kuweka mambo katika hali ya mvuto ( Remember to keep things intereting!). Tafuta namna ya kuleta hamasa, iliyokuwepo siku za mwanzo mwanzo, na kwa hakika utakamata usukani. Sasa swali linakuja…..Nini unatakiwa kufanya, ili kumridhisha mwanaume wako kitandani? Kujibu swali hilo, Bi. Layla amekuja na sheria 10 zifuatazo, ambazo kama zitazingatiwa kwa makini, basi mwanamke hatokuwa na shida ya kumridhisha mwanaume wake kitandani na nyanja nyingine muhimu za mahaba.


# 1 Vaa vizuri. Utamu wa kujamiiana unaweza ukawa kwenye tendo lenyewe, lakini matamanio ya kufanya tendo hilo, yanategemeana na mambo mengine mengi. Vaa vizuri wakati wa kulala wakati wote, na sio tu wakati wa usiku, ambao unataka kufanya mapenzi. Vaa nguo nyororo, yenye mtelezo unaomwagika mwilini. Kwa vazi hili na mtembeo wa kimahaba chumbani, mwanaume wako hatotaka kutoa mikono yake mwilini mwako.


#2 Usiwe mtu wa aibu aibu linapokuja suala la kujamiiana. Mwaume anaweza akakupenda kwa mapozi yako na aibu kwanza (lugha iliyotumika hapa ni “innocence”), lakini hamna mwanaume atakaye endelea kuvumilia mwanamke, ambaye anastushwa kirahisi na kila kitu (mitindo ya kujamiiana), isipokuwa mtindo wa kifudi fudi, maarufu kama “Kifo cha Mende”. Wanaume wanapenda wanawake, ambao ni wataalam kitandani. Wanaume wanapenda wanawake, ambao wanajiamini na wanabuni manjonjo mbalimbali wakati wa shughuli. Kama unataka kumridhisha mwanaume wako kitandani, basi soma mbinu mbalimbali, ambazo zinatumiwa na wapenzi mbalimbali.


#3 Fanya mazoezi na onekana Bomba. Wanaume ni watu wakujali sana muonekano wa mwanamke. Kwahiyo, sio lazima kuonekana kama walimbwende wa vichupi, lakini mtazamo wa karibu na hapo, utakuongezea mvuto zaidi kitandani. Ndio, mwanaume wako “anakupenda kama ulivyo” na tila lila nyingiiiii…..lakini lazima tuukabili ukweli kwamba watu wenye kufanya mazoezi wanaonekana na mvuto zaidi, hakuna kupinga hilo. Hata kwetu Bongo katika nyakati hizi za utandawazi, wakina kaka wengi wanawaona wanawake kama wakina Naomi Campbell na Jennifer Lopez, ambao wanatamani kuwa nao. Lakini hauhitaji kuwa kama wakina Naomi na Jennifer kumridhisha mwanaume wako, bali hakikisha tu upo katika umbo zuri la kumpelekesha kirahisi kitandani, Basi!


#4 Kuwa Mchokozi. Hapa haimaanishi ule uchokozi wa kuleta ugomvi, lahasha! Bali, ni ule uchokozi, ambao kwa lugha ya kingereza unafahamika kama “Tease”, kwa maana hiyo basi tunasema “Tease him”. Cheza nae michezo mbalimbali na burudika nae ipasavyo, na michezo isiwe ya kitandani tu, kama karata na kadhalika, bali michezo ya hata nje ya kitanda kama kukimbia na kucheza kidali po! Kama unataka kuwa mjuzi kitandani, basi unatakiwa umfanye mwanaume wako akutake wakati wote na popote pia. Kujamiiana sio kitasa ambazo unawasha na kuzima mnapokuwa chumbani tu. Mchokoze chokoze wakati mnasakata muziki jukwaani, na mchokoze chokoze (katika mitindo ya kimahaba, bila kuvuka mipaka) wakati yupo na marafiki zake.


#5 Jiamini na Jipende. Ndio, utaonekana vizuri zaidi ukipunguza maunene, lakini hiyo haimaanishi kwamba haupo bomba. Hakuna kinacho kera wanaume, kama mwanamke, ambae anauonea aibu mwili wake mwenyewe wakati anafanya mapenzi. Jiamini kuhusu mwili wako wakati upo mtupu, na jaribu mambo mbalimbali na mwanaume wako. Usikose muendelezo wa sheria 5 za mwisho juma lijalo

Ujumbe wa Vanessa Mdee kwa Jux, Atupa Dongo Gizani

$
0
0
Ni jambo zuri ukiona mtu wako wa karibu amefanikisha moja ya ndoto zake katika maisha yake. Ni muhimu kumpatia ujumbe ambao utakaomtia moyo katika kufanikisha mambo yake mengine aliyoyapangilia.


Vanessa Mdee ameamua kutumia vizuri fursa hiyo katika kumpongeza mpenzi wake Jux ambaye amehitimu masomo yake huko nchini China. Lakini katika ujumbe huo pia Vee amewapiga dongo watu waliokuwa wakimkejeli mwenza wake huyo kutokana na muimbaji huyo kutoonyesha picha yoyote akiwa na wanafunzi wenzake.

Kupitia mtandao wa Instagram, Vanessa ameandika:

Congratulations @juma_jux U finally done ✅ and you done did it well. Hapo watu walikuwa wakiombaga picha za wewe darasani nadhani hii picha jibu la kutosha. Umeweza kufanya yote, MZIKI, BIASHARA NA SHULE… now that’s exceptional. Muda wa vibunda babaaa. Keep inspiring the YUTEEEEE 🙌🏾👌🏾🎊

USAJILI:Mashabiki wa Yanga SC Wachoma Jezi ya Niyonzima

$
0
0
Kuondoka kwa mchezaji Haruna Niyonzima ndani ya klabu ya Yanga SC, kumeonyesha kuwaumiza mashabiki wa klabu hiyo ambapo moja kati ya kundi la mashabiki wameamua kuchoma jezi ya mchezaji huyo.

Mashabiki wakionekana kuichoma moto jezi yenye jina la Niyonzima na namba 8 mgongoni namba ambayo hutumia mchezaji huyo uwanjani

Hapo jana Klabu ya soka ya Yanga ilitoa taarifa ya kuachana na aliyekuwa mchezaji wake wa kimataifa raia wa Rwanda, Haruna Niyonzima baada ya kushindwa kuafikiana.

kupitia kwa Katibu Mkuu Boniface Mkwasa alisema Niyonzima bado ana mkataba mpaka mwezi Julai na Yanga Sc, lakini hawataweza kuendelea kuwa nae kwa msimu ujao kutokana na kushindwa kkuafikiana katika mazungumzo.

JPM Aagiza Watu Hawa Wakamatwe na Wawekwe Gerezani

$
0
0
Pwani. Rais John Magufuli amemwagiza Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage, kuwanyang’anya viwanda wamiliki ambao wameshindwa kuviendeleza.

Ameyazungumza hayo leo (Alhamisi) akiwa katika ziara yake ya siku tatu mkoani Pwani ambako amezindua viwanda saba.

“Kipindi cha nyuma tulipofanya makosa ni pale tulipouza viwanda kwa watu binafsi, sasa  kuna  viwanda 197 vimeshakufa waliouziwa hawajishughulishi na vingine vipo kama magofu,” amesema.

Kutokana na hilo, Rais amesema; "natoa wito kwa wote waliouziwa viwanda kipindi cha nyuma na sasa wameshindwa kuviendeleza , naagiza sasa basi mrudishe  na wewe Waziri Mwijage tumia hata nguvu kama kuwaweka ndani weka tu siku akitoka huko atakuta kiwanda kimeanza kazi."

VIDEO: Serikali yashauriwa izuie simu ya Prof Muhongo, Chenge, Tibaijuka

$
0
0
Jumuiya ya Kupambana na Kuzuia Rushwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ivitaka vyombo vya dola kuzuia Mawasiliano ya watuhumiwa wa kashfa  wa Escrow.

Akizungumza na Muungwana Blog Rais wa Jumuiya hiyo Abdul Nondo amewataja viongozi hao wa wa Umma  ni pamoja na Professa Anna Tibaijuka , Andrew Chenge , Sospiter Muhongo na wengine wanatakiwa kichunguzwa na kushikiliwa Mawasilino yao kisha kupelekwa Mahakamani kwa vigogo hao.
TAZAMA FULL VIDEO HAPO CHINI

3 Things Men Can’t Resist in a Woman

$
0
0
A Woman Who Smiles (more powerful than you might realize)

A woman who smiles makes it easier for a man to approach her by conveying an attitude of confidence, warmth and playfulness. Since many women are fearful of giving men the wrong impression, they frequently guard their smiles. If the only knew that smiling is one of the things men can’t resist. While this approach is safer, it inadvertently sends the wrong message that she is someone who is overly cautious because she has been hurt. In addition, smiling is a sign of acceptance. Men often need some signal that it is safe to approach a woman before they’re willing to risk introducing themselves (unless they are intoxicated).

A Woman Who Listens (instead of dominating the conversation)

Women are generally perceived as rarely really listening to men, at least not beyond a few minutes. Most of the time, a few minutes is all men really need. But since most men hate to be rejected, it is easier for them to keep conversations superficial. Men expect most women to want to talk, rather than be willing to listen. If they happen to meet a woman who listens with her eyes (looks at him while he’s talking) as well as her ears, they are intrigued. If she continues to listen and not take over the conversation, she’s the kind of woman that men can’t resist and want to spend more time getting to know her better. If fact, this is one of the best things you can do on a first date.

A Woman Who Dresses Feminine (men are really visual)

Everyone knows that men are visual. However, women often forget just how helpless men are to what they see. The right visual stimulation can hypnotize any man. Unfortunately, women hear this and often become fearful. They mistakenly believe that men only notice perfect women. Forget perfect! In spite of what you read about in magazines, men don’t expect a woman to be perfect. If you really want to be noticed by men, think colors, dresses which highlight your curves. Men basically like any woman who has that adorable quality that men can’t resist. It isn’t that men don’t find women attractive in pants or when they are dressed comfortably – they just don’t notice them as easily. It doesn’t catch their eye like sparkly earrings, pretty colors or flowing dresses and long hair does. Conversely, a powerfully dressed woman (think lots of red) makes most men think of s*x, or not notice her at all. She may have a soft side, but if men can’t see it, they often don’t know it exists. The more feminine (softer) a woman dresses, the more men she will attract.

Rais Magufuli Adanganywa Mbele ya Kadamnasi

$
0
0
Chama cha ACT Wazalendo kimemkana Isihaka Karanda aliyedai kuwa ni mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Pwani ambapo juzi alitangaza kukihama chama hicho na kujiunga na Chama cha Mapainduzi mbele ya Rais Magufuli.

Taarifa hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Mkoa wa Pwani, Mrisho Swagara alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ambapo alisema kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani wameamua kumdanganya Rais Dkt Magufuli.

Kiongozi huyo wa ACT Wazalendo alisema kuwa Isihaka alikuwa ni mwanamchama wao wa kawaida ambaye hakuwa tegemeo kwenye chama hivyo madai kuwa alikuwa mwenyekiti mkoa Pwani si za kweli na kwamba ni propaganda za CCM dhidi ya chama hicho.

Rais Magufuli akizungumza na mamia ya wananchi waliojitokeza katika viwanja wa Mjini Kibaha, Isihaka alitangaza kukihama chama hicho ambapo alipokelewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole. Alipokuwa akitambulishwa, ilielezwa kuwa ni Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Mkoa wa Pwani ambapo yeye mwenyewe alikiri hilo na kusema hata kwenye uchaguzi mkuu alimchagua John Pombe Magufuli.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images