Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live

Taifa Stars Mmefanya Vizuri Ila Hongera Yangu Siwapi Leo

0
0
Leo Team ya Mpira ya Taifa ijulikanayo kama Taifa Stars ilikuwa inapambana na Team ya Taifa ya Nchi ya Zimbabwe na Matokeo ni Taifa Star imemaliza mechi na Ushindi wa Bao Moja Katika Mchezo huo wa kwanza ya raundi ya awali ya kugombea kwenda AFCON 2015 .Nadiriki kusema kuwa Taifa Star walikuwa na Nafasi kubwa sana ya kushinda Mechi ya Leo zaidi ya Mabao matatu kwa Kuwa walikuwa Nyumbani na jinsi nilivyouangalia Mpira lakini ilishindwa kuendeleza kasi waliyokuwa nayo mwanzo , Bao moja si baya ila kumbuka tuna mechi ya marudiano ambayo itafanyika Zimbabwe siku za Karibuni, So tungewafunga mengi tungejiweka nafasi nzuri ya Kushinda...Kule kwao tunahitajika tutoke Droo ama tuwafunge ...So Hongera yangu nitawapa siku nkiwafunga Zimbabwe kwao...
Toa Maoni yako 
Udaku Sports

Henry Kilewo:Sheikh Ponda Katibu wa UAMSHO Aachiliwe Huru na Mashtaka Yake Yote Yafutwe

0
0
Henry Kilewo Amefunguka Kuhusu Sheikh Ponda kwenye Ukurasa wake wa Facebook , Soma Hapa chini alichosema:

"Kama William Lukuvi,Janeth Mbene na Martha (Mkuu wa Wilaya ya Kiteto) bado wapo madarakani kuitumikia serikali inayojitangaza kulinda amani ya nchi basi Sheikh Ponda katibu wa UAMSHO aachiliwe huru na Mashtaka yake yote yafutwe.
Haiwezekani wabaguzi na wachochezi wa siasa za Udini na Ukabila kama hawa wawe madarakani achilia mbali kuwa huru huku Sheikh Issa Ponda akikandamizwa na kufunguliwa mashtaka ya uchochezi
Lukuvi alituhumiwa kufanya uchochezi Kanisani na kisha Bungeni hali kadhalika Janeth Mbene.Hawa nao ni Mawaziri.Anayefanya uchochezi Msikitini,kanisani au Hekaluni na kuhatarisha amani ya nchi kwa maslahi ya kisiasa na ya kidini wote wapimiwe kipimo kimoja bila kujali vyeo au hadhi.Tuwe wapenda haki.Tusiogope kusema ukweli.
Serikali imefanya uchochezi kwa kuwaacha watu hawa Huru huku Sheikh Issa Ponda akinyimwa uhuru.Taifa la Double Standard,Serikali inayopalilia unafiki kwa kuendekeza na kuchochea Chuki Miongoni mwa jamii.Hatuwezi kujenga umoja na kusonga mbele kwa tabia hizi na matendo haya yenye sura mbaya isiyotakiwa katika karne hii ya watu waliostaarabika
The Double Standard Policies of the claimants of Human Rights,Freedom of Worship,Freedom of Expression are further becoming exposed every passing day.
Ni jambo la ajabu kuwa kuna vijana wa CCM wametumika kwenda kumsanifu mama Maria Nyerere na kumlisha maneno ili kuficha aibu ya kauli za kibaguzi za akina Lukuvi
Mama Maria Nyerere aliwaambia ukweli kuwa watawala hawasikilizi wananchi na kisha kuonya kuwa Taifa litaingia kwenye machafuko
Alinukuliwa akilalamika pia kuwa kuna watu wanamchagulia hadi magazeti ya Kusoma? Jamani hiki si kinyume kabisa cha Tangazo la Kimataifa la Haki za Binadamu na kinyume kabisa na Sheria za nchi ambazo zimetungwa kwa mujibu wa Katiba ambayo imetoa haki ya kupata habari na pia uhuru wa maoni? Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inakanyagwa hadi kwa Mjane wa Baba wa Taifa?
Kikundi cha vijana wanaojiita wazalendo wa Chama cha Mapinduzi kilitumwa kwenda kumtumia Mama Maria kwa maslahi ya chama chao na baadhi ya kambi za Urais ndani ya chama
Ni jambo la ajabu vijana hao kutangaza kuwa watazunguka nchi nzima kueleza kuwa Mwalimu Nyerere ametukanwa.
Hawa ni vijana wasaliti kwa taifa na wanafiki wasiojua wanataka nini ndani ya nchi yao
Hawakumbuki historia kuwa kijana Mwenzao Sethi Benjamini alifariki akiwa safarini kwa matembezi ya kuunga mkono Azimio la Arusha lililojenga misingi ya utaifa na kujenga uadilifu kupitia miiko ya uongozi lakini yale aliyoyafia Sethi Benjamini ,yamepuuzwa na kutupiliwa mbali na watawala wenye nia ovu na taifa hili kisha vijana hawa wasaliti wa Sethi Benjamini na Mwalimu Nyerere wanakubali kutumika kuufunika uchafu huu.
Mwalimu Nyerere katika Hotuba zake amekua akikemea ubaguzi wa kidini na kikabila .Lukuvi na wenzake kuendelea kushikilia nyadhifa za serikali ni matusi makubwa kwa Mwalimu Nyerere na pia ni Kejeli kufanya ziara Nyumbani Kwa Mama Maria kabla ya Kushinikiza chama na serikali yao kuwachukulia hatua wabaguzi hawa na pia kufanya shinikizo la kisera ndani ya chama chao kurudia misingi ya Azimio la Arusha ambayo ilikua Kikwazo kwa Mafisadi"Hernry Kilewo

Tuhuma nzito Bajeti Nishati na Madini

0
0
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono wameingia katika mvutano baada ya ujumbe wa maandishi wa kutaka kukwamisha bajeti ya wizara hiyo kusambazwa kwa wabunge.

Habari za uhakika zilizopatikana jana zilieleza kuwa kiini cha mgogoro huo ni ujumbe mfupi (SMS) ambao unamtuhumu Mkono kula njama za kutaka kukwamisha bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini.

Gazeti hili limedokezwa kuwa, SMS hiyo inadaiwa kutumwa na Waziri Muhongo kwenda kwa baadhi ya wabunge akimtuhumu Mkono kuwahonga baadhi ya wabunge Sh3 milioni kila mmoja ili kukwamisha bajeti hiyo.

Ujumbe huo unasomeka ”Mhe Spika wa Bunge la Jamhuri, Sisi wabunge waadilifu tunakiri kwamba Mhe Mkono ametufuata na kutupatia fedha kila mmoja milioni 3 ili tukwamishe bajeti ya Nishati na Madini.

Ujumbe huo umeanza pia kusambaa kwenye mitandao ya kijamii ikiwamo Jamii Forums .

Mkono

Mkono ambaye pia ni Mwanasheria mashuhuri nchini, alipoulizwa jana kama ni kweli amelalamika kwa Spika juu ya jambo hilo, alikiri na kusema alichofanya ni kulalamika kwa Spika na amemwachia alishughulikie.

“Ni kweli nimelalamika kwa Spika. Unajua taratibu za Bunge ni kuna any complaint (lalamiko) unaliwasilisha officially (rasmi) kwa Spika… hilo jambo lipo nimelifikisha kwa Spika wao ndiyo watafuatilia kwa taratibu zao,”alisema.

Profesa Muhongo

Alipotafutwa kwa njia ya simu ili alitolee ufafanuzi suala hilo, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alituma ujumbe kwa simu ukisema:

“Tutavuka tukiwa na ushindi wa maskini na wanyonge wa nchini mwetu. Tutaendelea kujenga uchumi imara utakaotoa ajira mpya na matumaini mapya kwa vijana, maskini na wanyonge wa nchini mwetu. Watanzania wamechoshwa na wizi, udalali, ubabaishaji na rushwa.”

Mkurugenzi wa shughuli za Bunge, John Joel alipotafutwa jana alisema yeye hana taarifa juu ya jambo hilo akisema kama lipo, basi huenda likawa mikononi mwa Spika mwenyewe.

Isabela Mpanda Hamnazo, Aonyesha Nguo yake ya Ndani Live Live

0
0
Mbovumbovu za staa! Miss Ruvuma 2006, Isabela Mpanda amedhihirisha jinsi alivyo hamnazo baada ya kuvua nguo hadharani na kuacha nyeti nje bila kujali watu waliokuwa wakimshangaa.

Tukio hilo la kushangaza lilitokea Alhamisi iliyopita kwenye Ukumbi wa Mawela uliopo Sinza, Dar ambako kulikuwa na kitchen party ya mwigizaji, Vanita Omary ambapo Isabela aliwashangaza watu baada ya kuacha nyeti nje.

Bila chembe ya aibu, Isabela akivalia gauni fupi akiwa tilalila, alikuwa akicheza muziki huku akilinyanyua gauni juu na kuacha sehemu nyeti za makalio nje na kusababisha ‘kufuli’ yenye muundo wa bikini kuonekana.

Ishu hiyo ilizua minong’ono kwa baadhi ya wageni waalikwa na kubaki wakimshangaa kwa kitendo hicho na kudai kuwa ni hamnazo.

Akiwa anafanya tukio hilo la kujifunua alisikika akisema amepania sherehe hiyo kwani yeye ndiye wifi wa Vanita na kama mwigizaji Jacqueline Wolper aliacha kufuli lake kubwa wazi na yeye aliamua kuonyesha lake aina ya bikini nje ili lionekane kwani ni la bei kubwa.

“Mh, kweli huyu Isabela hamnazo yaani anajifunua mbele za watu, hata haogopi, ukweli anatia aibu lakini afadhali wanaume hawapo maana wangekuwepo ingekuwa aibu zaidi,” walisikika wasanii wawili wakijadiliana huku wakimkodolea macho mwanadada huyo.
GPL

Mpenzi Wa Christan Ronaldo Ashambuliwa Baada Ya Kupost Picha Akiwa Utupu Na Bango Lililoandikwa "Bring Back Our Girls"

0
0
Tangu wasichana 276 wa Nigeria walipotekwa nyara na kundi la Boko Haram, watu mbalimbali maarufu duniani wamepost picha kwenye mitandao ya kijamii wakiwa na mabango yaliyoandikwa ‘Bring back Our Girls’, ikimaanisha wanajiunga na kampeni ya raia wa Nigeria.

Mwana mitindo Irina Shayk ambaye ni mpenzi wa mchezaji wa mpira wa miguu Christian Ronaldo yeye amepost picha kwenye twitter na Instagram akiwa amepoz mtupu huku akiwa ameshikilia bango linaloonesha amejiunga na kampeni hiyo, na bango hilo ndilo lililofunika kifua chake.
Hata hivyo kitendo chake hakikuungwa mkono na baadhi ya followers wake ambao walionesha moja kwa moja hisia kwa kumshambulia kuwa ameenda kinyume na maadili.

“Pretty tasteless and disrespectful. No class. This is exactly the justification terrorists are probably using to prevent women from receiving 'western education.” Aliandika mtu mmoja.

Mwingine aliona kama amefanya dharau kwa kuwa tatizo hilo sio la nchi kubwa kama Marekani na kuhoji kama angediriki kufanya hivyo siku ya tukio kubwa la shambulizi la kigaidi la September 11 nchini Marekani.

“Would you stand there n*ked wishing sorrow on the 9/11 victims? Would you do it for the tsunami? This is a tasteless attitude to 200 missing girls.”
Hata hivyo sio wote waliomshambulia, wengine walimsapoti na kueleza kuwa alikuwa na nia njema ya kuvuta umakini zaidi wa watu kuifuatilia kampeni hiyo kwenye mitandao ya kijamii.

Wema, Diamond Wachafua Hali ya Hewa

0
0
JAMBO limezua jambo. Pamoja na kuanza kwa kishindo safari yake ya kuelekea Afrika Kusini ‘Sauz’ kwa ajili ya fainali za kuwania Tuzo za MTV Africa (MAMA), mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na baby wake, Wema Isaac Sepetu wamechafua hali ya hewa, Ijumaa Wikienda lilikuwa linarandaranda ndani ya nyumba.

Pamoja na kufanya makamuzi ya kufa mtu kwenye shoo ya kuwatambulisha wasanii wanaowania tuzo hizo kwenye Ukumbi wa Bilicanas uliopo Posta, Dar, Diamond hakumpandisha Wema stejini kama kawaida yake, jambo lililozua kizaazaa.

Kuna muda mashabiki wake walipiga kelele wakimtaka Wema apande stejini lakini hakufanya hivyo.
Awali Diamond alipanda stejini mishale ya saa 8:00 akipishwa na msanii kutoka Sauz, Jigger ambaye alikuwepo kwa ajili ya kutoa sapoti kwa Mbongo Fleva huyo.

Msauz huyo alifanya shoo ya dakika 20 kisha akampisha Diamond ambaye aliingia na Kibao cha Uswazi Take Away Remix, ambacho ndani yake amemfagilia Halima Haroun ‘Kimwana’ ambaye ni hasimu wa mpenzi wake, Wema.

Baada ya kumaliza wimbo huo ndipo baadhi ya mashabiki wakasikika wakimwambia Diamond ampandishe Wema la sivyo watakinukisha.

Ishu hiyo iliendelea hadi jamaa aliposhuka stejini hapo.
Wakati Diamond akiendelea kufanya makamuzi yake hayo, Wema na Halima Kimwana wote walikuwepo ukumbini hapo na kwa bahati nzuri kama si mbaya walijikuta wote wakimshangilia Diamond, tena wakiwa VIP ya juu ambapo walikuwa wakiingia watu maalum.
Mwanahabari wetu aliwashuhudia wawili hao walipogeukiana kila mmoja alionekana kumwekea mwenzake uso wa mbuzi.

Hali hiyo ilidumu hadi Diamond alipomaliza shoo yake na Wema kushuka na kumuacha Halima Kimwana.

Baada ya shughuli za shoo Diamond alibaki na Halima Kimwana wakicheza disco. 
Kufuatia hali hiyo kwenye mitandao ya kijamii usiku huohuo, kuliibuka maneno mengi kutoka kila upande kuwa shoo ya Diamond ilichafuliwa na Wema na Halima Kimwana ambaye alidaiwa alijipanga kwenda kumfanyia fujo Wema kwa kuwa yupo upande wa Penniel Mungilwa ‘Penny’.
Stori: Musa Mateja na Shakoor Jongo

Homa ya Dengue Yaibua Tafrani Jijini Dar

0
0

TAARIFA isiyo sahihi ya maambukizi ya homa ya dengue inayoenezwa na mbu aina ya aedes, imesababisha baadhi ya madereva teksi jijini Dar es Salaam, kujilinda kwa kuvaa glovu za mikononi, soksi ndefu miguuni na kujifungia muda wote katika magari yao hata ambayo hayana viyoyozi.

Uchunguzi wa gazeti hili wiki hii, umebaini madereva hao wamekuwa wakivaa soksi miguuni hata kama wamevaa kandambili, huku wakiwa na glovu viganjani kwa madai kuwa wanaogopa kuumwa na mbu mwenye virusi hivyo.

Wakizungumza na gazeti hili, baadhi ya madereva wa kituo cha mtaa wa Mindu Upanga, walikiri kuvaa mavazi hayo kujikinga na ugonjwa huo ambao hauna tiba.

“Kwa kweli ugonjwa huu ni hatari kama hauna tiba , unafikiri tutapona kweli, ni heri tuvae hivi, au tujifungie ndani ya gari wakati tunasubiri wateja,” alisema Juma Hassan mmoja wa madereva teksi hao.

Hassan alimruhusu mwandishi kuzungumza naye akiwa amejifungia ndani ya gari huku jasho likimtoka na kulowanisha shati lake, kwa hofu kwamba akifungua madirisha, mbu wataingia na kumwambukiza ugonjwa huo.

Baraka Joseph dereva teksi wa kituo hicho, yeye alikuwa amevaa koti na miguuni amevaa soksi pamoja na kandambili, na alisema taarifa alizonazo zinaonesha ugonjwa huo unatisha kwani unaua muda mfupi na hauna tiba, hivyo sio ugonjwa wa kuudharau hata kidogo.

“Ugonjwa huu unatisha na tumesikia hapa mjini watu wengi wameupata, sasa kazi yetu hii tuko vijiweni tangu alfajiri hadi muda huu (saa mbili usiku), ni lazima tujikinge vinginevyo tutautapa na hatujui kama tutapona,” alisema Joseph.

Hali kwenye kituo cha kona ya Muhimbili, ambako taksi huwa zinapaki hapo, ilikuwa tofauti ambapo kulikuwa na dereva mmoja tu, ambaye naye alisema wenzake wameondoka kwa kuwa maeneo hayo kuna mbu wengi wanahofu ya kuumwa na kupata homa ya dengue.

“Nimebaki mimi ,lakini hata hivyo naondoka, nimejipaka dawa ya kuzuia mbu ila bado nina wasiwasi huenda mbu mwenye virusi hivyo akaniuma nikaupata, sasa itakuwa shida, kwa kweli ugonjwa huo unatutisha,” alisema Rashid Muhammed, ambaye ni dereva wa teksi eneo la Kona ya Muhimbili.

Wakati huo huo, Mkoa wa Shinyanga ulijikuta ukilazimika kukanusha uvumi ulioenea kuhusu kulipuka kwa ugonjwa wa dengue, baada ya kulazwa kwa mgonjwa mmoja mwenye viashiria vya ugonjwa huo katika hospitali ya mkoa.

Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake mjini hapa jana Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga, Dk Ntuli Kapologwe, alikanusha kulipuka kwa ugonjwa huo mkoani hapa, baada ya vipimo vya mgonjwa huyo vilivyopelekwa Dar es Salaam, kubaini hana ugonjwa huo.

“Ni kweli mtoto aliyelazwa katika hospitali ya mkoa alikuwa na viashiria vya kuambukizwa ugonjwa huo vya uchovu, kuishiwa nguvu, kutokwa na damu puani na homa kali, lakini hakuwa na ugonjwa wa dengue kwa kuwa vipimo vyake kuonesha anasumbuliwa na ugonjwa mwingine ambao unatibika kwa tiba sahihi,” alisema Dk Kapologwe.

Uvumi kuhusu kuibuka kwa ugonjwa huo, ulisababisha mkanganyiko uliowakumba baadhi ya wagonjwa waliofikia hatua ya kutaka kukimbia wadini ili kunusuru maisha yao wakihofia kuambukizwa ugonjwa huo.

Dk Kapologwe alisema, ili kuthibitisha kuwa mgonjwa aliyefika hospitali kupatiwa matibabu anasumbuliwa na maradhi ya dengue, ni lazima vipimo vyake vipelekwe kwenye Maabara Kuu jijini Dar es Salaam na majibu ya vipimo yathibitishe kuwa kweli mgonjwa huyo ameambukizwa ugonjwa huo.

Akizungumzia kinga ya ugonjwa huo, Dk Kapologwe aliwataka wananchi kuchukua tahadhari kwa kuchoma na kuangamiza mazingira yanayoweza kuwa chanzo cha mazalia ya mbu ambao husababisha ugonjwa huo.

Inakuwaje Video zinazofungiwa Kwenye TV za East Africa ni Deal Vituo vya TV vya Kimataifa

0
0
Hivi karibuni Tumesikia Video Mbali Mbali zikifungiwa na mamlaka husika kuchezwa kwenye Vituo vya TV hapa East Africa lakini cha kushangaza hizo hizo Video zilizofungiwa kwetu zinachezwa kwenye Vituo vikubwa vya kimataifa, Mfano mmoja wapo ni Video ya hivi karibuni ya kundi la Souti Soul ya wimbo unaitwa Nishike ilipigwa marufuku Kenya lakini cha ajabu inachezwa Channel O ya South Africa..Je Mamlaka Husika za Nchi zetu zimepitwa na wakati ?

Wakati huo huo kuna Swali nalojiuliza kila siku unakuta TV za Hapa ndani wanapiga nyimbo za nusu utupu za wanamuziki toka nje vizuri kabisa lakini za wasanii wa kwetu unakuta hata si za nusu uchi ila unakuta mdada kazungusha mauno kidogo tu eti Video inapigwa marufuku mbona hizo za kina Beyonce hamzizuiii?

Familia ni Kila Kitu-Baada ya Ugomvi Beyonce akaenda Kumtembelea Mdogo Wake

0
0
Baada ya Ugomvi wa Jay Z na Shemeji Yake Solange kurekodiwa na Kusambaa Mtandaoni kila kona watu mpaka leo wanajadili kuhusu ugomvi huo lakini wenyewe walishayamaliza na kuyasahau kabisa , Siku ya Pili tu Beyonce alikwenda kumtembelea Mdogo wake Kwake na kupiga picha hiyo hapo juu..Family Is Everything Bwana...Nyie kaeni kupiga Domo

Warembo wa Kenya Vs Warembo wa Tanzania...Wapi Zaidi?

0
0
Kati ya Tanzania na Kenya wapi Kunatoka Warembo Wazuri zaidi ?
Warembo wa Kenya Vs Warembo wa Tanzania...Wapi Zaidi? 

Bosi wa EWURA Akutwa Amefariki Hotelini

0
0
Meneja Biashara wa Petroli wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura) amekutwa amekufa hotelini katika mazingira ya kutatanisha muda mfupi baada ya kuwasili jijini Dar es Salaam akitoka Dodoma ambako alihojiwa na Kamati ya Bunge ya Bajeti.

Meneja huyo, Julius Gashaza, ambaye alikuwa na jukumu la kupanga bei za mafuta za kila mwezi, alihudhuria kikao hicho mjini Dodoma kwa siku mbili; Ijumaa na Jumamosi iliyopita kuhusu mambo mbalimbali, yakiwamo kiwango cha mafuta kinachoingizwa nchini, mgawo wa fedha unaotolewa na Ewura kwenda kuhudumia umeme vijijini (Rea) na fedha za mfuko wa barabara.

Jeshi la Polisi, Mkoa wa Temeke limethibitisha tukio hilo na kueleza kuwa meneja huyo alikutwa amejinyonga kwa kutumia tai kwenye hoteli ya Mwanga Lodge iliyopo Yombo Vituka wilayani Temeke.

Nyumbani kwa meneja huyo wa Ewura, kulikuwa na waombolezaji waliokuwa kwenye vikundi na kikao cha maandalizi ya mazishi kilifanyika ndani ya nyumba ya marehemu iliyopo Yombo Vituka na baadaye kuhamia nyumba ya jirani.

Kamati ya Bunge ya Bajeti, inayoongozwa na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, ilikutana na maofisa wa Ewura, akiwamo Gashaza na wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kugundua kuwapo kwa tofauti katika takwimu za kiwango cha mafuta kilichostahili kutozwa kodi.

Gashaza alikwenda Dodoma kutoa ripoti ya Ewura kwenye kamati hiyo ya Bunge akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Felix Ngamlagosi.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya kamati hiyo, takwimu za Ewura ziliashiria kuwa fedha zilizopatikana ni nyingi zaidi ya zile zilizoelezwa na TRA, lakini Wizara ya Fedha ilisisitiza zifuatwe takwimu za mamlaka ya mapato.

Habari hizo, zinasema baada ya kurejea Dar es Salaam juzi majira ya saa tatu usiku, Gashaza hakwenda nyumbani kwake na badala yake alikwenda kwenye hoteli iliyo karibu na nyumbani ambako mkewe na ndugu yake mmoja walimfuata na akawaeleza kuwa anahisi kutishiwa maisha yake.

Baadaye walifanya maombi maalumu kabla ya kuachana naye.

Inadaiwa kuwa marehemu aliomba akalale hotelini kwa sababu hakuona kama ana amani kulala nyumbani kwake na ilipofika asubuhi alikutwa ‘amejinyonga’ ndani ya chumba alicholala hotelini humo.

Nyumbani kwa marehemu waombolezaji walikusanyika katika makundi, lakini baada ya kukaa katika kikao cha familia walitoka na kauli moja kuwa hawatasema chochote na kwamba jukumu hilo libaki mikononi kwa polisi.

Kamanda wa polisi wa Kanda ya Dar es Salaam, Seleiman Kova hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo akidai kuwa anayetakiwa kulizungumzia ni Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Temeke, Engbert Kiondo.

Alipotafutwa, Kamanda Kiondo alisema kulingana na taarifa zilizopo Gashaza aliitwa bungeni Mei 14 na akarejea Dar es Salaam Mei 17. Alisema aliporejea, Gashaza aliaga nyumbani kwake kuwa hajisikii vizuri na kuelekea Hoteli ya Mwanga Lodge iliyopo Yombo ambako alichukua chumba Namba 113.

Kamanda Kiondo alisema akiwa hotelini, Gashaza alimpigia simu rafiki yake mmoja anayejulikana kwa moja la Silipwango akimweleza kuwa yupo hotelini hapo kujipumzisha kwa sababu bungeni aliulizwa mambo ambayo hayakumpendeza na kwamba alihitaji kupumzika.

Rafiki huyo, kwa mujibu wa Kiondo, alimpigia simu mkewe anayeitwa Judith akamweleza alivyoelezwa na mumewe na baadaye kwa pamoja wakamfuata hotelini ambako baada ya kuzungumza nao kwa muda mfupi, aliwaomba wamuache apumzike na ndipo walipoondoka.

Asubuhi, Silipwango alipigiwa simu na mkewe kumueleza kuwa Gashaza hakurudi nyumbani na akaamua kupitia kwenye hoteli waliyomuacha na alipofika akakuta watu wamejaa. Alipouliza akaelezwa kuwa kuna mtu amejinyonga chumbani.

Kamanda Kiondo alisema Gashaza alijinyonga kwa kutumia tai aliyoifunga kwenye bomba la maji ambalo pia lilikatika na hivyo kuukuta mwili wake ukiwa sakafuni.

Kilichojiri kamati ya bajeti

“Kisheria kodi ya mafuta ni Sh263 kwa lita inakwenda mfuko mkuu Hazina na Sh50 inakwenda kwa Wakala wa Umeme Vijijini (Rea), lakini takwimu za mafuta yaliyouzwa inayostahili kutozwa kodi kati ya TRA na Ewura zinatofautiana,” alisema mmoja wa wajumbe.

“Kwa hiyo Kamati ya Bajeti iliwaita wote (Ewura na TRA) na kwa kweli wajumbe wa kamati tulikuwa wakali sana, hatutaki mchezo tulitaka kujua nani anasema ukweli,” alidokeza mjumbe huyo.

“Uko ugomvi mkubwa tu kati ya TRA na Ewura kuhusu nani hasa mwenye takwimu halisi,” alisema mjumbe huyo na kudokeza kuwa meneja huyo alisema kila kitu kwa uwazi.

Habari kutoka ndani ya kikao hicho zimeeleza kuwa baada ya vuta nikuvute ndani ya kamati hiyo, iliamuliwa watendaji wa vyombo hivyo viwili wakafanye ulinganisho na kupeleka jibu kwa kamati hiyo. Ewura waliwasilisha takwimu zao Jumamosi.

“Tension (mvutano) ni kubwa kwa sababu kuna watu wizarani hawazitaki takwimu za Ewura na wanataka za TRA ambazo sisi kama wajumbe tunaziona hazina uhalisia kunaweza kukawa na ufisadi,” alisisitiza mjumbe mwingine.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, Andrew Chenge alipoulizwa jana, alikiri kufanyika kwa kikao kilichomuhusisha meneja huyo na kwamba taarifa alizotoa zilionekana tofauti na zile za TRA.

“TRA ni chombo cha Serikali na Ewura ni chombo cha Serikali, kwanini wawe na takwimu zinazotofautiana? Hilo tu ndio tumewaagiza wakae pamoja watuambie zipi ni takwimu halisi,” alisema Chenge.

Alipoelezwa kuwa mmoja kati ya maofisa wa Ewura waliofika mbele ya kamati yake amejinyonga, Chenge alionyesha kushtushwa na kuhoji kama taarifa hizo zina ukweli.

“Una uhakika kwamba amejinyonga? lini? Kama ni kweli basi ni jambo la kusikitisha sana, lakini hiyo sasa ni kazi ya polisi. Mimi nisingependa sana kuzungumza, tuwaachie wao wachunguze sababu za kifo chake,” alisema Chenge.

Serikali inaelezwa kuwa katika hali mbaya kifedha na kamati hiyo ya Bajeti imekuwa ikifanya kila linalowezekana kuinusuru kwa kukutana karibu kila siku na Hazina na wadau wengine wanaochangia fedha katika mfuko wake.

Kwa bajeti ya mwaka 2013/2014 iliyopitishwa na Bunge, Serikali imejikuta ikiwa na upungufu wa Sh1.8 trilioni hali ambayo kamati ya bajeti inatafuta kila njia ikiwamo kushauri vyanzo vipya vya mapato ili kunusuru bajeti ya mwaka huu wa 2014/2015.

Bajeti ambazo zinaelezwa kuiumiza kichwa Serikali ni ya Maji, Miundombinu na Nishati na Madini ambazo zinaelezwa kupata mgawo kidogo mwaka jana na kuzifanya zishindwe kutekeleza miradi mbalimbali.

Mkurugenzi wa Petroli wa Ewura, Godwin Samwel alisema alipata taarifa jana saa 3:00 asubuhi.

Alithibitisha kuwa marehemu alikuwa Dodoma kikazi kwenye vikao na kamati ya Bunge tangu Alhamisi iliyopita.

Baada ya kumaliza kazi ndiyo ndiyo jana (juzi) alichelewa sana kurudi ndipo alipoamua kujipumzisha kwenye nyumba ya wageni (iliyopo karibu na nyumbani kwake) ambako alikutwa amefariki,” alisema Samwel.

Alisema marehemu alikuwa mwadilifu, mchapa kazi na asiye na tatizo lolote kazini na kuondoka kwake kumeacha pengo kubwa.

Nguo ya Ndani ya Shemeji Yangu Imenishangaza Sana

0
0
Jana nimeshudia kitu cha ajabu sana na cha kushangaza nimejizuia kucheka lakini kiukweli nimeshindwa
Nina swaiba wangu tupo ofisini pamoja na ni marafiki sana leo tumekubaliana kukutana Bar moja ipo hapo kwa remmy ila ghafla jamaa akanipigia simu nipite kwake kwanza tupate baraka ya pamoja kutoka kwa shemeji (mke wa mshikaji)poa mimi nikafanya hivyo kufika kama kawaida mke wa jamaa alinipa juice tukiwa tunapiga stori moja mbili ghafla mtoto wa jamaa katokea chumbani kwao na CHUPI ya mke wake akijaribu kuivaa
Chupi ilikuwa chafu sana maana ilikuwa nyeupe na inaonekana ilikuwa haijafuliwa 
Kha mke kuona hivyo haraka akampokonya mtoto na kuikimbiza chumbani
Ki ukweli nilijizuia kucheka lakini nilishindwa
Baadae tulisepa na jamaa nipo naye hapa miller tunapiga moja mbili na stori
Kaona noma sana ila kwa pamoja tumekubaliana tumejifunza kitu
Unapokuwa na watoto wadogo hivi vitu tuwe tunaweka sehemu wasiyoweza kufikia

Wasichana Wapiga Mizinga, Mnajiaibisha Mbele ya Wanaume

0
0
Unakutana na msichana mrembo anavutia kwa muonekano na angalau mnaendana mfano dini etc. Unaamua kuanzisha uhusiano nae kwa malengo ya kuwa mwenzio wa maisha (Mke).

Sasa kidogo anaanza kukuambia naomba uninunulie simu yenye whatsapp, mara naomba hela ya mchango wa kitchen party, mara naomba kod ya nyumba, mdogo wangu kafukuzwa shule hana ada, twende Zanzibar holiday.

Zote hizi ni hela daah! hapo hamna hata wiki mbili. Kwa style hii aisee mtatukosa. Sikatai kukusadia lakin isiwe too much jamani kumbuka na mimi nina dhiki na ndugu kama wewe!

Ukija Kipesa Pesa Nitatumia Pesa Siku mbili tatu nikikuchoka Tupa Kule na Uzuri Wako ! Ubaki ukisema Huna Bahati na Wanaume!! Kubaf

Kenya Investors Cry Foul as Tourists Flee Country

0
0
Nairobi. Tourism investors in Kenya cried foul over a massive airlift of hundreds of foreign tourists from the country by Britain, Australia and France who cited insecurity concerns.

The traders think there was more than meets the eye, and have pointed to “economic sabotage over Kenya’s changing foreign policy since President Uhuru Kenyatta came to power in 2013.”

The developing crisis in Kenya is, however, partly blamed on the al-Qaeda linked Al-Shabaab whose stronghold inside Somalia was yesterday pounded by fighter jets in the latest push by African Union troops to root out the insurgents.

The air strikes on the town of Jilib are understood to be part of the offensive by the 22,000-strong UN-backed AU force, who launched in March a fresh bid to wrest remaining towns from the Al-Shabaab.

Kenyan forces are also in Somalia ever since they were ordered in by the previous regime to fight Al-Shabaab fighters who had masterminded several attacks on its soil and abducted tourists among other hostages. “I heard two heavy explosions, military jets were flying over the city,” said Osman Mohamed, a resident of Jilib. The impoverished town is a key Al-Shabaab hub in southern Somalia’s Middle Juba region, some 320 kilometres southwest of Mogadishu.

Senior Al-Shabaab commander Sheikh Ibrahim Abu Hamze said war planes had struck the town, but denied any casualties.

“The mujahedeen fighters have managed to repel the enemy with anti-aircraft weaponry, they have fled,” claimed Abu Hamze in a telephone interview with AFP.

It was not immediately clear where the jets were from, but Kenya is part of the AU force and has used its air planes to strike Al-Shabaab bases before.

Hardline Al-Shabaab insurgents once controlled most of southern and central Somalia.

After withdrawing from fixed positions in the capital Mogadishu nearly three years ago, they have lost most large towns to the AU and government soldiers. However, they still regularly launch guerrilla raids and its fighters are linked to ongoing sporadic bomb attack inside Kenya that have killed hundreds of people. The insecurity situation was however was not being seen by tourist players as the main reason why western countries at the weekend issued travel advisories cancelling holiday bookings for its citizens to deal a blow to the struggling industry.  (AFP)

Simba Msipokuwa Makini, Mtalia miaka Minne

0
0
MAANDALIZI ya Uchaguzi Mkuu wa Simba sasa yameshika kasi huku wagombea 41 wakiwa wamechukua na kurudisha fomu za kuwania uongozi kwa ngazi mbalimbali. Uchaguzi huo utafanyika Juni 29.

Uchaguzi huo unafanyika baada ya kupita miaka minne tangu ule wa mwisho ulipofanyika na kuuingiza madarakani kwa mbwembwe uongozi wa Ismail Aden Rage ambao sasa unamaliza muda wake bila ya kukidhi matarajio ya wanachama.

Kwa miaka mitatu mfululizo sasa, Simba haijatwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara huku uwezo wa kikosi chake wakati mwingine ukitiliwa shaka kwani wachezaji wanaonekana kucheza kwa kufuata maelekezo mengine nje ya yale ya kocha.

Hata katika masuala mengine ya maendeleo ya klabu, Simba imeendelea kuwa na mambo yale yale yaliyojaa ubabaishaji.

Hilo ndilo soka la Tanzania, utegemezi wa klabu unakuwa shubiri wakati mwingine, tena katika wakati muhimu ambao timu inahitaji pointi za kutwaa ubingwa pengine.

Siku zote chaguzi za klabu kongwe za Simba na hata Yanga, hutawaliwa na makundi. Katika Simba inaelezwa kuna itikadi kali za makundi hayo yanayotajwa kuwa mawili. Inaelezwa kuwa ndani ya klabu hiyo, kundi moja likishinda basi jingine hujiweka kando na kutazama washindi wanafanya kitu gani.

Mbaya zaidi wakati Simba ikiwa katika mchakato wa uchaguzi, kuna kamati ya siri imeundwa ili kufanya usajili wa msimu ujao wa Ligi Kuu Bara. Usajili huo unafanyika kwa mikakati binafsi zaidi hasa katika utoaji fedha.

Hii inamaanisha kama Simba ilikuwa na tatizo la wachezaji kucheza chini ya kiwango kwa makusudi wakifuata maelekezo ya kiongozi fulani, basi hali hiyo bado itaendelea.

Kuna mfano wa kiongozi mmoja aliyekuwa akijitolea kuisaidia timu hiyo kwa kufanya usajili na kuiweka timu kambini kisha anajirudishia fedha zake kupitia mapato ya mechi za timu.

Alinogewa hadi akaingia katika uongozi, lakini akasahau kutimiza wajibu wa kuiwezesha klabu kuwa na mbinu zake za kupata fedha, pale wanachama walipobaini kuigeuza klabu mtaji, hakuwa na namna ikabidi atoke.

Simba haihitaji kuongozwa na mtu anayetaka yeye jinsi ya kuiendesha, inapaswa kuwa na uongozi wenye mipango ya maendeleo isiyo tegemezi kwa mtu au taasisi yoyote.

Hata siku moja wanajiita ‘wajanja wa mjini’ hawataweza kuisaidia klabu hiyo yenye rekodi ya pekee Tanzania na Afrika Mashariki. Viongozi wa aina hiyo wamekuwa wakiwapa kazi makocha asubuhi, jioni wanawafukuza.

Mambo Ambayo Wanawake Wanafanya ili Kuleta Mvuto Lakini Hayashtukiwi na Wanaume Kivile

0
0
1. Kubadili mtindo wa kujikwatua.

Mwanamke anaweza kuwa amezoea kujikwatua kwa namna fulani lakini baada ya muda akaamua kubadili muonekanao wake kwa kubadilisha aina mpya ya kujikwatua kwa kuongeza vikorombwezo fulani fulani akitegemea mwenzi wake ata notes lakini asijue kwamba wanaume kwenye jambo hilo wala haliwagusi kabisa mpaka wafanye kushtuliwa.

Kwa hiyo nawashauri tu msije mkaumia bure pale mnapoona wenzi wenu hawa notice mabadiliko mliyoyafanya ndivyo tulivyo....

2. Kubadili mtindo wa nywele.

Kwa kawaida wanawake hutumia muda wao mwingi kutengeneza nywele zao ili kujipa mwonekano mpya na pia wakitarajia kwamba wenzi wao watapenda, lakini cha kushangaza wenzi wao wala haiwagusi na wala hawa notice mabadiliko hayo ya nywele mpaka wafanye kushtuliwa na wenzi wao. jambo hilo huwa linawakwaza sana wanawake, lakini labda tu niwape ushauri wa bure, msiweke matarajio makubwa ya kudhani kwamba mabadiliko ya nywele mnayoyafanya yatawavutia wenzi wenu, si kweli utafadhaika bure bora tu mfanye kwa utashi wenu 

3. Kubadili rangi za kucha

Wanaume wengi hawajui tofauti ya rangi, kwa hiyo hata mwanamke abadili rangi yake ya kucha kwa ajili ya ku match na mavazi fulani aliyonunuliwa na mwenzi wake au hata aliyonunua mwenyewe anaweza kushangaa mwenzi wake asishtukie jambo hilo. Ajabu eh!

4. Mkoba mpya.

Unaweza kukuta mwanamke kajinasibu na kununua mkoba mpya wa gharama baada ya kujinyima sana akitegemea mwenzi wake atauona na kumsifia lakini atashangaa mwenzi wake wala haulizi anaona tu kama ni mkoba wa kawaida. Lakini pia hata kama mkoba wenyewe ume match na mavazi bado ni ngumu kwa mwanaume ku notice na ndiyo maana inawauma sana wanawake wengi. Mtuhurumie tu, ndivyo tulivyo....
5. Kiatu kipya

Viatu navyo ni eneo lingine ambalo wanaume hawa notice kabisa, mwanamke anaweza kununua kiatu kipya akitarajia mwenzi wake atakiona na kumsifia lakini wala, labda tu kama mwanaume huyo anapenda aina hiyo ya kiatu na aliwahi kukisifia baada ya kumuona mwanamke mwingine amekivaa na kikampendeza, lakini kama si mpenzi wa viatu wala mwanamke asitarajie kusifiwa, ni mpaka pale atakapomshtua mwenzi wake kwa kumuuliza kama kiatu alichovaa kimempendeza au la na sije akashangaa akijibiwa kwa kifupi tu, "ndiyo" bila comments.
Kwa kawaida wanawake wanapenda ukiwasifia kuhusu jambo fulani utoe na comments japo kidogo tena kwa undani kabisa....

6. Lebasi za ulimbwende na makochokocho mengine

Hereni, bangili na kishaufu au kipini cha puani kinaweza kumpa mwanamke muonekano mpya, lakini muonekano huo hauwezi kumshangaza mwanaume kama mwanamke anavyotarajia, jambo hilo huwa linawakera sana wanawake lakini ukweli ndiyo huo wanaume hawasumbuliwi na vitu vidogo vidogo. 
7. Pambo jipya chumbani au kitandani

Mwanamke anaweza kubadili mwonekano wa nyumba au wa chumba cha kulala akidhani kwamba jambo hilo litamvutia mwenzi wake. si kweli wanaume hawako hivyo anaweza akafika nyumbani na kuona kama vile hakuna kilichofanyika mpaka afanye kushtuliwa na mwenzi wake kwa kuulizwa kama ameionaje nyumba au chumba chao cha kulala. haishangazi mwanaume akiuliza kwani kuna nini....!

Kwa mwanamke jibu hili anaweza hata kutamani kumtwanga mwanaume na flower verse kwa hasira, lakini mianaume ndivyo tulivyo, mtuhurumie tu.


Mume Wangu Kwa Wiki Mara Moja Tu, Ndoa ina Miezi Miwili

0
0
Nimeolewa miezi miwili iliyopita. Kabla sijaolewa huyu jamaa tulikuwa tunakutana mara chache chache sana. Na tulijuana miaka mitatu kabla ya ndoa. 

Na pia kwa kipindi chote tulikuwa tukis3x akipiga moja ya km dk 10 akimwaga ndio imekwisha hajawahi kurudia, ni mpaka labda kesho tena au baada ya siku kadhaa.

Sasa mara nyingi sifiki kunako huwa ananiacha na nye'e, nikiwa peke yangu najisugua na mto hadi nafika mwenye na nimeshazoea hivyo wakati mwingine siku hizi hata simsumbui nataka. Kwa sababu kipindi cha nyuma nilikuwa namsumbua anasema subiri mpaka asubuhi.

Mara subiri nilale kidogo full majanga, hivi nauliza huyu atakuwa anaupungufu wa nguvu za kiume au ni nini?

Zaidi ni mdogo tu kijana hata 30 hajafikisha.

Post Ya Kwanza Ya Monalisa Baada Ya Kupata Taarifa Kuwa Baba Wa Mtoto Wake Amefariki Katika Ajali.

0
0
Post ya kwanza ya Monalisa baada ya kupata taarifa kuwa mume wake wa zamani na baba wa mtoto wake amefariki.

Aliweka picha hiyo ya mareheu Tyson akiwa na mwanae na kisha kuandika maneno haya hapa chini


Kifo Cha Tyson Chamliza Mboni Mwasimba zaidi, AY Aokoa Jahazi

0
0
Mtangazaji wa kipindi cha Mboni Show, Mboni Masimba akilia kwa uchungu akiwa nje ya Hospitali ya Mkoa wa Morogoro wakati wakisubiri kusafirisha maiti kuelekea Dar. Marehemu Tyson ndiye alikuwa Mtayarishaji wa kipindi chake na walikuwa wote katika safari hiyo, ingawa walikuwa magari tofauti.
Katika hatua nyingine, msanii wa Hip Hop nchini, Ambwene Yessaya 'AY' (anayehesabu pesa) aliamua kujitole kununua jeneza la kusafirishia mwili w marehemu, jeneza hilo liligharimu kiasi cha shilingi laki sita ambazo AY alizitoa cash!

Wakisaidiana kubeba jeneza hilo kuelekea hospitalini baada ya kulinunua

Taarifa Kutoka Jeshi la Polisi Kuhusu Tuhuma za Ubakaji Dhidi ya Mume wa Flora Mbasha

0
0

Jeshi la Polisi limethibisha kupokea tuhuma za ubakaji dhidi ya mume wa mwimbaji wa injili Flora Mbasha anayefahamika kwa jina la Emmanuel Mbasha.

Akiongea na Tovuti ya Times Fm, kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi wa Ilala, Marietha Minangi ameeleza kuwa jeshi hilo limepokea tuhuma hizo kutoka kwa mlalamikaji ambaye ni binti mwenye umri wa miaka 17 na kwamba binti huyo alifika katika kituo cha polisi akiwa na ndugu zake.

“Taarifa zimepokelewa na zinachunguzwa. Taarifa zilizokuja ni za kubaka sasa tunazichunguza tufike mwisho tujue ni nini.” Kamanda Minangi ameimbia tovuti ya Times Fm.

Ameeleza kuwa baada ya kupata taarifa hizo kutoka kwa mlalamikaji polisi walienda nyumbani kwake ambapo hawakumkuta yeye na mkewe na kwamba hadi sasa hawajapatikana.

Tovuti ya Times Fm ilitaka kupata ufafanuzi kuhusu uhusiano uliopo kati ya mlalamikaji na mtuhumiwa kwani taarifa za awali zinadai kuwa ni shemeji wa mtuhumiwa.

“Hayo yote yanachunguzwa, mimi siwezi kusema ni shemeji yake kabla hatujafikia mwisho wa uchunguzi. Tutakapofikia mwisho wa uchunguzi ndipo tutakapoweza kusema wana mahusiano gani.” Kamanda Minangi ameeleza.


Viewing all 104414 articles
Browse latest View live




Latest Images