Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Jinsi Coco Beach Ilivyofurika Jana Jijini Dar es Salaam

$
0
0
Hivi ndivyo Ufukwe wa Coco (Coo Beach) ulivyofurika watu wa aina mbalimbali hapo jana jioni, katika kusherehekea sikukuu ya Iddi pili,Mabasi/Daladala kutoka kona kadhaa za jiji la Dar zilionekana zikishusha watu kwa wingi katika ufukwe huo ambao ulisheheni pia vyakula vya kila aina ikiwemo Mihogo,Chips mayai na wengine walikutwa na Camera ya Blogu ya jamii wakiwa wemebeba vyakula vyao na kujibweda kando kando ya ufukwe,ama kwa hakika ilikuwa burudani kwa wakazi wa jiji la Dar.

 

 Foleni ya kuingia kando kando ya ufukwe nayo ilikuwa kubwa kiasi ambacho magari mengine yalipita kwa taabu kuendelea na safari zake.



Chopa ya Jeshi la polisi nayo ilikuwa na kazi ya ziada kama hivi ya kukagua meneo mbalimbali yaliyokuwa na mkusanyiko mkubwa wa watu,Pichani chini Chopa ikionekana kwa mbali ilipokuwa ikikatiza maeneo hayo.

Mapacha Wafa Maji, Mama Ajitupa Baharini Siku ya Eid

$
0
0
MAPACHA wawili waliokuwa wakiishi kata ya Kashai katika Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera walikufa maji juzi kwenye ufukwe za Ziwa Victoria wakati wakiogelea kusherehekea Eid, katika siku ambayo mama mmoja alijitupa baharini kutoka kwenye pantoni Feri, jijini Dar es Salaam kwa wivu wa mapenzi.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kagera, Agustino Ollomi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Kamanda Ulomi alisema juzi majira ya saa 11:30 jioni, mapacha hao walikuwa wakiogelea ziwani katika eneo la Kiloyela lililopo katika Manispaa ya Bukoba mkoani humo.

Marehemu mapacha hao walitajwa kuwa ni Hussein Hamis (12) na Hassan Hamis(12), na kwamba walikuwa wanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya Msingi Kashai.

“Watoto hao walikuwa wa askari mwenzetu(wa) kitengo cha Usalama Barabarani," alisema Kamanda Ollomi na kwamba "walikuwa wakisoma darasa la saba.”
Alisema sababu ya kifo cha marehemu hao ni kuzidiwa na nguvu ya maji na kupelekea kuzama ambapo waliopolewa wakiwa wamefariki.

"Watoto wenzao baada ya kuona wenzao wakiendelea kuzama walipiga kelele ili kuomba msaada, lakini jitihada za kuwaokoa wakiwa hai zilishindikana," alisema.

"Tayari watoto hawa wamezikwa Juni 27 mwaka huu (jana) katika makaburi ya Kishenge, yaliyoko katika Manispaa ya Bukoba.

“Tunaendelea kuwasihi wazazi, kuendelea kuangalia usalama wa watoto wao hasa katika siku za sikukuu ili kuepusha madhara kama haya."

Jijini Dar es Salaam, mwanamke aitwaye Asha Yahya(30), mkazi wa Zanzibar anadaiwa kujirusha baharini akiwa katika kivuko cha MV Magogoni kwa lengo la kujiua, lakini wananchi waliwahi kumuokoa.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Temeke, Andrew Satta alisema tukio hilo lilitokea majira ya 2:10 asubuhi wakati akitokea Kigamboni kuelekea Ilala na kwamba sababu za kutaka kujiua ni wivu wa kimapenzi.

"Baada ya kumhoji alituambia kwamba sababu ya kutaka kujiua, eti mume wake anataka kuoa mwanamke mwingine," alisema Satta.

Katika tukio jingine katika kipindi cha sikukuu, Jeshi la Polisi jana liliokota mwili wa mtumishi wa Mamlaka ya Bandari (TPA), Masoud Abdulrahman(27) katika ufukwe wa Kisiwa cha Mbutu, kilichopo Kigamboni.

Kamanda Satta alisema marehemu kabla ya kukutwa na umauti huo alikuwa na wafanyakazi wenzake 20 ambao walikwenda katika ufukwe huo kwa ajili ya kufurahia sikukuu ya Eid, lakini wakati wakiogelea wimbi kubwa la maji liliwapiga na hivyo wote kupotea.

Alisema hata hivyo, baada ya Jeshi la Polisi kufanya msako baada ya kugundua kwamba kuna watu waliosombwa na maji, waliwapata wenzake 20 ambao waliokolewa na kukimbizwa hospitali.

Kwa upande wa mkoa wa kipolisi wa Ilala, mtu mmoja ambaye jina lake halikujulikana mara moja aligongwa na basi la mwendokasi katika Barabara ya Uhuru na kufariki papohapo juzi pia.

Kamanda wa Polisi wa Ilala, Salum Hamdani, alisema mtu huyo aligongwa na gari hilo baada ya kuingilia barabara ya mwendokasi na kwamba mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Nay Wa Mitego Awachana Vibaya Young Killer, Barakah Da Prince

$
0
0
‘MDUNGUAJI’ bei mbaya kwenye kilinge cha Hi-hop, Emmanuel  Elibariki ‘Nay wa Mitego’ amekoleza moto bifu lake na wasanii chakaramu, Baraka Andrew ‘Da Price’ na Young Killer, ambapo pamoja na mambo mengine, amefafanua kwa kina mistari aliyowaimba kenywe wimbo wake mpya wa Moto.

Katika mahojiano maalum na Global TV Online, Nay au The True Boy ameweka wazi bila kutafuna maneno, kuwa Young Killer na Baraka  wamepoteza mweleko kwenye ramani ya muziki na kwamba kuna mahali walikosea, hivyo wajirekebishe vinginevyo watarudi Mwanza kuvua samaki.


Katika kuonesha amedhamiria kuwawashia moto, prezidaa huyo wa lebo ya Free Nation, amesema Da Prince arudi ampigie magoti prodyuza Kid Bway, kwani ndiye alimuonesha mwanga wa muziki lakini malipo ya dogo ni dharau na mateke ya punda, ndiyo chanzo cha kuporomoka kwake kimuziki.


Kuhusu Young Killer, Nay alisema ni lazima amuangukie Mona Ganstar kwani amemtoa kikazi, lakini amemlipa matusi na dharau. Nay amesema watu hao ‘wamekunja’ hivyo ni ngumu kwa wasanii hao kufika mbali kimuziki. Huku akiwakumbusha kuwa na nidhamu, kuandika mashairi na kuimba havitoshi.

Je, Wajua Majina ya Pombe na Magufuli yalipotoka?

$
0
0
Majina mawili ya Dk. John Pombe Joseph Magufuli yana historia yake ya jinsi yalivyopatikana.

Majina hayo mawili ‘Pombe’ na ‘Magufuli’ yalitokana na bibi na babu wazaa baba yake Magufuli.

Jina la ‘Pombe’ alipewa na bibi yake kwani wakati anazaliwa bibi yake alikuwa amepika pombe siku
hiyo.

Jina la ‘Magufuli’ lilitokana na babu yake ambaye alikuwa shujaa wa kucheza ngoma za asili aliyepewa jina Magufuli kwani kila alipokuwa akicheza ngoma alikuwa anawashinda wengine hivyo kitendo hicho kilifananishwa na kufuli linavyofungwa mlangoni.

Mpenzi Wangu Anataka Niwe na Wapenzi Wawili yeye na Rafiki yake

$
0
0
Nashindwa kuelewa ana maana gani..Huyo mpenzi wangu amekuwa na rafiki yake wanapendana sana kila mahali wako wote na siku zingine huwa nikitoka na mpenzi wangu out analazimisha na rafiki yake awepo...Sasa siku za hivi karibuni amekuwa akiniambia kuwa its ok kuwa naye na huyo rafiki yake...week iliyopita alikuja nyumbani kututembelea usiku ulipofika akaamua kulala japo tuna chumba kimoja tu, mie kwa aibu nikalala sebuleni japo mpenzi wangu alikuwa ananishawishi tulale naye kitanda kimoja..na its ok tukifanya theresome ila mimi nilikataa...Naomba ushauri wana udaku hii ni Halali ?

Je niendelee kuwa na wote ama nisimamie msimamo wangu wa kuwa na mmoja?

CCM inahitaji Upinzani Mpya, Huu wa Sasa ni Upinzani Chakavu na Uliozeeka

$
0
0

Chama tawala cha CCM ni chama ambacho kimepita katika safari ndefu sana mpaka kufikia hapa kilipo leo.Safari hiyo imekua ya furaha huzuni , machozi na jasho.

Katika miaka yote imekua ikikabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa vyama vingine vya siasa (Wapinzani) hususani katika uchaguzi lakini mara zote imekua inaibuka na ushindi wa kishindo katika kila uchaguzi.
Mathalani mwaka 1995 tulishuhudia upinzani mkali ambao mpaka leo haujapata kutokea tena.

Lakini leo mambo yamebadilika,upinzani ule ninaoujua mimi haupo tena , upinzani ule ulioweza kutingisha nchi umetoweka , upinzani ulioweza kulitikisa bunge la Jamhuri na kung'oa mawaziri umeyeyuka mithiili ya barafu kwenye jua.
Aina ya upinzani tulio nao sasa ni mwepesi sana kuwahi kutokea .

Madhara ya CCM kufanya mageuzi makubwa katika taasisi hiyo chini ya falsafa ya "CCM MPYA NA TANZANIA MPYA" yameanza kuonekana katika vyama vyote vya upinzani Tanzania.
Upinzani umekosa mashiko na hoja mujarab kutokana na kasi ya CCM MPYA katika kuisimamia serikali kutekeleza kwa vitendo Ilani ya mwaka 2015.

Ajenda kubwa ambayo walikua wanaitumia sana wapinzani ilikua ni ajenda ya ufisadi na hii ndio ilikua kete yao pekee iliyokua inawapa umaarufu.Lakini tokea serikali hii ya awamu ya 5 iingie madarakani ni kama vile vyama hivyo vimepigwa ganzi, havisikiki tena vikizungumzia ufisadi, na hii ni kwa sababu kuu mbili.

1.Uamuzi wao wa kumchukua ndugu Edward Lowassa kua mgombea urais umewafunga midomo kabisa kuzungumzia sakata la ufisadi maana kila Mtanzania anakumbuka miaka ya nyuma jinsi chadema kilivyokua kinazunguka nchi mzima kwa magari na helkopta kumtangaza Lowassa kua ni fisadi mkubwa (Fisadi nyangumi) na sehemu pekee anayostahili kuishi ni gerezani tu.
Leo hii wapo naye wanakunywa chai pamoja.

2.Kasi ya Mh Rais Magufuli katika kushughulika na wala rushwa na mafisadi.
Hatua ya ujenzi wa mahakama ya mafisadi ,utumbuaji na ukamataji wa watuhumiwa wa vitendo vya rushwa na ufisadi (Mf.Escrow Scandal) vimewatia ubaridi wapinzani hawa kuongelea tena kwa sababu kazi nzuri inafanyika ya kudhibiti na kufuta kabisa rushwa na ufisadi.Wamekosa points za kuongelea katika muktadha huo.

Serikali ya awamu ya 5 imefanya mambo makubwa na mazuri sana tangu iingie madarakani na tena mambo hayo yamefanywa kwa namna bora zaidi kupita matarajio ya wengi wakiwamo wapinzani ambao hawakutegemea kama yatafanyika. Mambo hayo yameleta tija na kufufua matumaini mapya kwa wananchi na Taifa zima.

Serikali inafanya mambo hayo kwa umakini mkubwa kuhakikisha haifanyi makosa na ndio maana kila wapinzani wakijaribu kuchungulia kuona labda wataona makosa wanaambulia patupu , wanaishia katika kuzusha uwongo usiwaosaidia wananchi na tena usio na hata lepe la ukweli.

Matokeo yake ni kwamba hoja zao za kitoto zinakosa ladha kwenye masikio ya wananchi zinadumu kwa kipindi kifupi sana kisha zinatoweka.

Ni wazi dhahiri kwamba upinzani wa Tanzania unatereka na umeshazeeka , na CCM inahitaji ladha mpya ya upinzani utakaotoka kwenye chama kipya kabisa.
Upinzani huu sasa uliojielekeza katika kusaliti rasrimali za taifa lao na kuwatetea mabwanyenye, wanyonyaji na makabaila wa kizungu umefikia hitimisho lake.
Upinzani huu uliofikia hatua ya kupinga hata yale mambo (Issues) ambayo walikua wanayapigia kelele kwa miaka mingi ni upinzani mzee.

Uzee na uchakavu wa vyama vya upinzani umeonekana pia katika chaguzi za marudio hivi karibuni , ambapo katika nafasi za madiwani,wenyeviti wa mitaa, vitongoji na vijiji ambapo kwa ujumla yake Chama Cha Mapinduzi kimeshinda kwa zaidi ya asilimia 99%.
Pia kasi kubwa ya viongozi na wanachama wa vyama hivyo kujiunga na Chama Cha Mapinduzi ni mfano mwingine wa uzee na uchakavu wa upinzani vya Tanzania kwa mfano tumeshudia madiwani kutoka kule Wilayani Arumeru Mkoani Arusha na mikoa mingine wakikihama chama hicho na kujiunga na CCM achilia mbali aliyekua Makamu Mwenyekiti (Taifa,) wa chadema Said Arfi ni ishara mojawapo kwamba CCM MPYA imekidhi matarajio mengi ya wananchi wakiwamo hao wapinzani walioamua kwa hiari yao kurudi CCM na kumuunga mkono Rais Mh. Dr John Pombe Magufuli.

CCM MPYA ya sasa imejizatiti katika masuala mazima ya uadilifu, uaminifu, uwajibikaji,weledi, uchapakazi na kujishughulisha kutatua kero za wanyonge wa Tanzania.Pia CCM ina maono mapana katika kujenga chama bora kitakachozaa serikali bora na ndio maana iko mbioni kuanzisha chuo cha kuandaa viongozi wa hapo baadae.Hii ni tofauti na vya upinzani

Miaka 25 ya mfumo wa vyama vingi vya siasa vyama hivyo vimeshindwa kuandaa viongozi wake.
Vyama huokoteza okoteza watu wasio waadilifu na weledi au kusubiria rehema za makada wa CCM waliokengeuka na kujiunga na vyama hivyo ambao huwapachika katika nafasi za uongozi ambao mwisho wa siku huishia kuharibu mambo.
Upinzani unaoshindwa kuandaa viongozi katika miaka yote hiyo ni upinzani usio makini ,chakavu na mzee.

Kasi ya CCM MPYA chini ya Serikali adilifu na imara ya Mh Dr .Magufuli imefifisha uwezo wa kujenga hoja wa wapinzani,imekata miguu waliyokua wanatumia wapinzani kusimamamia na kubwa zaidi imezeesha vyama vya upinzani kwa kutekeleza Ilani ya CCM2015-2020 kwa spidi kubwa na ya ajabu.

Ile kauli ya Mh Rais ya kwamba mpaka kufikia mwaka 2020 vyama vya upinzani vitakua vimejifuta vyenyewe, inaenda kutimia.

Upinzani huu uliokosa msimamo,uadilifu, uaminifu, uwajibikaji ,weledi na maono umeshazeeka tunahitaji kuundwa kwa vyama kipya vitakavyotoa changamoto kwa CCM ,lakini chadema cuf, nccr ni muda wao wa kupumzika siasa kwa kua vimeshazeeka kihoja, kimkakati na kisera.

Vijana wote walio katika vyama hivyo au wanaotarakia kujiunga na vyama hivyo hawana tofauti na watu waliopanda boti iliyotoboka boriti kwani muda wowote itazama.

Maalim Seif asema Wajumbe wa Bodi CUF waliosajiliwa na RITA ni feki

$
0
0

Katibu Mkuu wa Chama Cha wananchi CUF amesema kuwa wajumbe wa Bodi ya wadhamini waliosajiliwa na Rita ni feki.

Maalimu Seif amesema kuwa wajumbe hao walipandikizwa na Mwenyekiti anayetambulika na Msajili wa Vyama vya siasa nchini profesa Ibrahim Lipumba.

Maalimu Seif pia ameeleza mbinu zilizosukwa   kumpindua, Mbinu  zilizotumika kutaka kumpindua na kumuondoa ndani ya Chama hicho.

Maalimu Seif amesema kuwa njama hizo ni pamoja na kufoji nyaraka za Usajili wa Bodi ya wadhamini.

Amesema kuwa mipango hiyo imeratibiwa na Msajili wa Vyama vya siasa pamoja na Mwenyekiti wa Chama hicho anayetambulika na Masajili wa Vyama ambapo mbinu hizo amedai kuzigundua.

Zitto Kabwe Achoshwa na Tambo za IGP na Amiri Jeshi Mkuu Mauaji ya Kibiti..Adai ni Maneno Matupu tuu

$
0
0

Watu 2 wanahofiwa kuuawa kwa kupigwa risasi katika kijiji cha Mangwi wilayani Kibiti kuamkia leo, Kamanda Lyanga amesema wanafuatilia tukio hilo ili kujua ukweli wake.

Kufuatia taarifa hizo za kuuawa kwa watu wawili Mbunge wa Kigoma mjini Mhe. Zitto Kabwe amefunguka juu ya mauaji yanayoendelea kutokea mkoa wa Pwani eneo la Kibiti kwa kuitaka serikali itazame jambo hilo kwa mtazamo mpana kwa kuwa wananchi wana haki ya kujua nini kinachoendelea juu ya mauaji hayo.

Zitto amebainisha hayo kupitia ukurasa wake Facebook huku akidai kuwa Usiku wa kuamkia leo yameweza kutokea mauaji mengine ambayo yamepelekea kuuwawa Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Mangwi kata ya Mchukwi na Mwenyekiti wake kwa kupigwa risasi na baadaye kuchomwa moto nyumba zao.

Wabunge Wanawake Watengewa Chumba Maalum cha Kunyonyeshea

$
0
0
Wabunge Wanawake Watengewa Chumba Maalum cha Kunyonyeshea
Bunge limetenga chumba maalum kwa ajili ya wabunge wenye watoto wachanga kunyonyesha watoto wao wakati vipindi vya bunge vinaendelea.

Uamuzi huo umetangazwa leo (Jumatano) bungeni na Naibu Spika Dk Tulia Ackson mara baada ya kipindi cha maswali na majibu bungeni.

"Ofisi ya Bunge inataarifu kuwa imetenga chumba maalum kwa ajili ya kunyonyeshea kwa wabunge wenye watoto wachanga,"amesema.

Amewasihi wabunge wenye watoto wachanga kuwanyonyesha watoto wao angalau miaka miwili kama inavyoshauriwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

VIDEO:Maalimu Seif Ahadithia Njama zilizopangwa Kumuhujumu

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUFMaalimu Seif Sharifu Ahmadi   ametaja Njama zinatumiwa na watu wenye nia ovu naye kumuhujumu pamoja na kumpindua kwenye nafasi yake

Maalim amezitaja mbinu mbinu hizo na maamuzi ya chama hicho kufuatia hofu hiyo ndani ni kukabiliana na njama hizo.

Hata Hivyo Katibu Mkuu huyo amesema kuwa Haki ya Wanzzibar ya kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar itapatikana sio muda mrefu.

Tazama Video

TAKUKURU yafunguka Baada ya Kuwakamata Jamal Malinzi, Mwesigwa

$
0
0
TAKUKURU yafunguka Baada ya Kuwakamata Jamal Malinzi, Mwesigwa
 
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania, (Takukuru) imethibitisha kumshikiria Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na katibu wake, Mwesigwa Silentine kwa mahojiano ambayo hakuyaweka wazi.

Ofisa Uhusiano wa Takukuru, Mussa Misalaba amethibisha kuwa viongozi hao walikamatwa kwa ajili ya uchunguzi ambapo amesema kuwa Jamal Malinzi na wengine wanaendelea kuhojiwa kwa tuhuma mbalimbali.

Kuhusu ufafanuzi wa tuhuma hizo, ofisa huyo alikataa kuzitaja kwamba ni suala la kiuchunguzi.

Pia alipoulizwa sasa ni lini viongozi hao watafikishwa mahakamani alisema hawezi kusema kwani inawezekana kama watuhumiwa hao wakitoa ushirikiano kwa Takukuru wa ushahidi wanaweza wasifikishwe mahakamani.

Tambwe kuongeza mkataba Yanga

$
0
0

UONGOZI wa Yanga upo kwenye hatua za mwisho za kufanikisha kumuongezea mkataba mwingine mshambuliaji wao tegemeo raia wa Burundi, Amissi Tambwe.

Yanga wanamuongezea mkataba Mrundi huyo, baada ya ule wa awali kumalizika mwishoni mwa msimu uliopita.

Wachezaji wengi walio kwenye mazungumzo nao kwa ajili ya kuwaongezea mikataba ni Deus Kaseke, Deogratius Munishi ‘Dida’, Thabani Kamusoko na Donald  Ngoma.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Championi Jumatano, mshambuliaji huyo juzi alikutana na viongozi na kufikia muafaka mzuri wa kuongeza mkataba huo mpya wa miaka miwili.

“Tambwe ameonyesha nia kubwa ya kubaki kuendelea kuichezea Yanga, ni baada ya mazungumzo mazuri tuliyoyafanya kati yetu viongozi na yeye mchezaji.

“Makubaliano tuliyoyafikia ni kwamba ataongeza mkataba mwingine wa miaka miwili ya kuendelea kuichezea Yanga, hivyo wakati wowote tutamalizana,” alisema mtoa taarifa huyo.

Alipotafutwa katibu mkuu wa timu hiyo, Boniface Mkwasa, kuzungumzia hilo, alisema: “Ni kweli kabisa Tambwe tulikutana naye juzi (Jumamosi iliyopita) na kikubwa tulijadiliana hatima yake, na amekubali kubaki na tupo kwenye makubaliano mazuri.”

Alipoulizwa Tambwe kuhusiana na suala hilo, alisema:
“Ni kweli nimeshazungumza nao lakini bado kuna baadhi ya mambo hayajakaa sawa na atakapokamilika, basi kila kitu kitakuwa wazi ila ninaamini nitabakia Yanga.”

Tabia Nne za Mpenzi asiyekuwa na penzi la kweli

$
0
0

WIKI iliyopita tuliona baadhi ya dalili ambazo zinaweza kukupa mwelekeo wa kujua kama mpenzi huyo ameumbwa kwa ajili yako, ama la, lakini wiki hii tunaangazia na kuzijua walau dalili Nne za Mpenzi ambaye hana mapenzi ya dhati nawe.

Ifahamike kuwa hakuna asiyehitaji mapenzi ya kweli ingawa kuna wapenzi wanaothamini penzi wmenzi wake anapokuwa na pesa au kazi Fulani na baada ya hapo hujitoa katika mahusiano hayo hali ambayo huleta kwikwi katika mtima wa moyo wa anayefahamu kupenda.
I

1.      Muongo

Hakuna asiyefahamu athari za mtu muongo katika jamii, vivyo hivyo ndivyo ilivyo katika mapenzi uongo ni sumu mbaya na nidalili moja wapo ya kuonyesha kuwa mpenzi wako hana penzi la dhati nawe na huyo aweza kukuletea athari za kufikiri hapo baadae endapo hautakuwa makini nae. 

Hivi karibuni nilikuwa mjini Mbeya nikipata chakula katika moja ya mgahawa uliopo mkabala na Posta, katika mgahawa huo nilikutana na vijana wawili na msichana mmoja wakiwa wanakula chakula ambapo kati ya kijana mmoja alionekana kuwa ni mpenzi mpya wa yule binti ambaye alisikika akisema kiwa ‘’ukija kwangu atakalia sofa ambazo hujawahi kuziona maishani’’ hali iliyonishtua na kuelewa mara moja kati ya tabia alizonazo kijana yule ambaye anaonekana ni mcha Mungu.

Hivi utajisikiaje Mpenzi wako akigundua kuwa ulikuwa ukimdanganya na hatimaye yeye akajua ukweli wa suala ulilokuwa ukimpiga fiksi? Lakini ushauri wangu si kumacha bali jaribu kumshauri kwa hekima na akiendelea na tabia hiyo ujue kuwa hana mapenzi ya kweli kwako.

2.     Kupenda pesa

Ukiona mpenzi wako wa kike ama kiume anapenda sana kupata pesa kutoka kwako tambua ni moja ya dalili ambazo zinajieleza kuwa hana mpango nawe bali analazimika kuwa nawe kutokana na pesa ama kipato chako. Mpenzi wa namna hiyo ili kujihakikishia dalili hii siku moja akikuomba pesa hata kama ameziona mwambie kuwa huna, hapo yupo tayari kuvunja hata mahusiano kwasababu kitu muhimu kwake hajapata na wala wewe si muhimu tena kwake.

Nieleweke kuwa sisemi pesa ni mbaya katika mapenzi, la hasha bali pesa na mapenzi ni sawa na trafiki na kondakta katika mambo Fulani yale………ya kuchafua mifuko kwenye nguo nyeupe……………na ni muhimu wapenzi mkapenda kupeana maarifa ya kufanya kazi halali ili kujipatia vipato kwa ajili ya kuepukana na hili.

3.     Hajali kutokuwa jirani na wewe.

Mpenzi anaye kupenda muda mwingi hutamani kuwa nawe karibu na inapotokea hamjaonana hata masaa sita au matatu hujisikia shida ambapo kwa wengine hufikia kupiga simu na ukimuuliza anasemaje atakuuliza maswali yaliyoshonana kama ushanga mara upo wapi? Umekula? Na upo na nani? Na maswali mengi ya namna hiyo ili mradi moyo wake utulie.

Endapo Mpenzi wako mkiwa mbali naye kwa muda wa masaa mengi na yeye akaonyesha kuwa hakukosa chochote kutokuwa nawe karibu ama kuwasiliana nawe basi ujue kuwa mpenzi huyo ni kimeo yaani hana mapenzi ya dhati kwako.

4.     Anapenda kukuudhi

Dalili ya Nne ya mpenzi asiyekuwa na mapenzi ya dhati nawe ni yule anayependa kukuudhi mara kwa mara kana kwamba anatafuta sababu ya kuachana nawe lakini anashindwa kutamka bayana kuwa haitaji tena kuwa nawe.

Maudhi hayana budi kutokea pale inapobidi kwa bahati mbaya sana na si kwa makusudi, lakini wapo wapenzi wanaowaudhi wenzao kwa makusudi huku wakiendelea kusisitiza maudhi hayo kama utani na kujua kwa makusudi kuwa anamuumiza mwenzi wake bila kuomba msamaha. Ingawa kuomba msamaha ni kipaji na hasa katika mfumo dume ambao unaonesha kuwa mwanaume anapoomba msamaha basi ujue katumia njia nyingi za kumaliza tatizo hilo zimeshindikana hivyo kaomba msamaha kwa kulazimika sana na kwa siri.

Mpenzi msomaji wa safu hii, baada ya kuona dalili hizo za mpenzi asiyemwaminifu kwako, je wajua kuwa tendo la ndoa lina faida kubwa katika afya yako? wiki ijayo jiandae kujua faida nane za kufanya ngono kiafya.

Bunge Lashindwa Kutoa Adhabu Kwa Joshua Nassari Kwa Kudharau Mamlaka ya Bunge

$
0
0
Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge imelibebesha Bunge mzigo kuhusu shauri la Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari la kuidharau Mamlaka ya Spika na Bunge baada ya kutopendekeza adhabu kwa mbunge huyo.

Nassari anatuhumiwa kuidharau mamlaka hiyo wakati Bunge lilipokuwa likijadili bajeti ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Juni Mwaka jana.

Akisoma mapendekezo ya kamati hiyo leo (Jumatano) mbele ya Bunge, Mwenyekiti wa kamati hiyo, George Mkuchika amesema kamati hiyo imemtia hatiani kwa makosa ya kuidharau Mamlaka ya Spika.

"Joshua Nassari aliitika wito wa Kamati bila kuleta usumbufu wa aina yoyote na alipohojiwa na kamati alikiri wazi kosa lake na kuomba radhi kwa Mheshimiwa Spika na Bunge,"amesema.

Hizi ndizo Sababu za CUF kutaka kumfikisha Mahakamini Boss wa Rita

$
0
0
CHAMA cha Wananchi CUF Kimepanga Kumfikisha Mahakama Mkurugenzi wa Rita kutokana na madai ya kushiriki kukihujumu chama hicho.

akizungumza na Waandishui wa Habari leo Jijini Dar es Salaam Maalimu Seif Sharifu Ahmad Katibyu Mkuu wa Chama hicho amesema kuwa chama hicho kitafungua kesi zidi ya Mkuregenzi huyo kutokana na kushiriki kwenye kufoji nyaraka za kuhalalisha Bodi ya wadhamini bandia.

Maalimu Seif amesema kuwa wajumbe hao bandia wametengenezwa ila kujipatia fedha za chama hicho kwa udanganyifu.

Taarifa kuhusu utata wa Biashara ya Gesi Tanzania na Kenya

$
0
0
Taarifa iliyotumwa kwa umma kutoka Wizara ya Biashara na Uwekezaji inasema kwamba Tanzania itaendelea kuheshimiwa kwenye mikataba ya Kibishara na Nchi Kenya.

Tarehe 24 Aprili, 2017 magazeti nchini Kenya yalitoa taarifa ya kwamba Serikali ya Kenya itapiga marufuku uingizwaji wa gesi ya kupikia

Liquefied Petrolium Gas, LPG ) nchini humo kutokea Tanzania, na kwamba gesi itakayoruhusiwa kuingia Kenya ni ile itakayokuwa imepitia kwenye Bandari ya Mombasa peke yake. Baada ya kusoma taarifa hizi Serikali ya Tanzania iliwasiliana na Serikali ya Kenya ili kupata maelezo kuhusu hatua hii ambayo ni kinyume cha taratibu za kibiashara katika Jumuiya ya Afrika ya Mashariki. Tarehe 18 Mei, 2017 Serikali ya Kenya ilitekeleza uamuzi wake kwa kuzuia shehena ya gesi isiingie Kenya kutokea Tanzania. Hatua hii ina athari kubwa kwa wafanyabiashara wa gesi ya kupikia hapa nchini pamoja na watu wote ambao ajira zao zinategemea biashara hii. Wakati hatua hizi zinachukuliwa bado Serikali ya Kenya ilikuwa haijatoa maelezo rasmi kwa Tanzania kuhusu uamuzi wake huo. Katika kikao cha Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji la Jumuiya ya Afrika ya Mashariki kilichofanyika tarehe 2 Juni, 2017, suala la hatua ya Kenya kupiga marufuku uingizwaji wa gesi kutokea Tanzania lilizungumzwa kwa kirefu na kufanyiwa maamuzi. Kimsingi Serikali ya Kenya ilikubali kuondoa katazo la uingizaji wa gesi kupitia Tanzania mara moja, na makubaliano haya yaliingizwa kwenye kumbukumbu za Mkutano ambazo ziliafikiwa na nchi zote wanachama wa Jumuiya kwa kuweka sahihi. Pamoja na makubaliano haya, Kenya imeendelea kuzuia gesi isiingie nchini mwao kutokea Tanzania. Serikali ya Tanzania imewasilisha rasmi malalamiko yake Kenya kuhusu suala hili

Okoa Ndoa Yako Sasa, Ongeza Maumbile, Nguvu na Hamu ya Tendo la Ndoa Hata Wenye Kisukari.

$
0
0
OKOA NDOA YAKO SASA. ONGEZA MAUMBILE, NGUVU NA HAMU YA TENDO LA NDOA HATA KWA WENYE KISUKARI. Tatizo la maumbile madogo, nguvu za kiume na ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limekuwa likiwasumbua wengi na kusababisha kushindwa kujiamini ktk tendo hivyo kusababisha ndoa nyingi kuvunjika pamoja na mahusiano. Upungufu wa nguvu na hamu ya tendo husababisha mambo kama:-
(a)Uume kulegea wakati wa tendo (b)Kukosa hamu ya tendo la ndoa (C)Kuwahi kufika kileleni (D)Uume kuchelewa kusimama baada ya round ya kwanza. (E)Kuchoka sana baada ya round moja n.k @Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo kwa kutumia bidhaa zilizotengenezwa kwa mimea na matunda zisizo na kemikali wala madhara na kuthibitishwa kiafya. Pata hizi👇👇👇👇
🍉 🌿🍅🍒🍍🍓🍉🍎🍀
1.HANDSOME UP ni kifaa chenye uwezo wa 99 % kuongeza uume (size unayohitaji) na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200000@200,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130000@130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130000@130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo hata mara 3 @130000@130,000/= Kwa Bidhaa hizi na nyingine kama:-
5.Kupunguza unene na manyama uzembe @150000@150,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi @130000@130,000/=
7.Kutengeneza shepu (hips, makalio na mapaja) @200000@200,000/= 8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni @120000@120,000/=
9.Kuwa mweupe na soft mwili mzima bila kuacha sugu 120,000/=
10.Kurudisha usichana (bikra) @120000@120,000/=
11.Kupunguza au kuongeza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120000@120,000/=

Wasiliana nasi kwa (+255) 0767447444 au 0714335378.

NB: Matokeo ni uhakika na garantii na upate risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii. Follow us
@Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr

Mchezaji Donald Ngoma si wa Mchezo..Akata Mzizi wa Fitina...Yanga au Simba? Jibu Hili Hapa

$
0
0
Mshambuliaji wa  Yanga, Mzimbabwe Donald Ngoma ameongeza mkataba wa miaka miwili kuendelea kuitumikia timu hiyo katika Ligi Kuu Bara msimu ujao.


Kupitia kurasa rasmi za mitandao ya kijamii za timu hiyo wamethibitisha taarifa za usajili huo kwa kuandika “Donald Ngoma Raia wa Zimbabwe ni mali ya Yanga kwa mkataba wa miaka miwili.”

Ngoma ambaye alikuwa akihusishwa kujiunga wapinzani wa Yanga, Simba kabla ya kuzuka kwa taarifa za kujiunga na klabu ya Polokwane City inayoshiriki Ligi ya kuu ya Afrika Kusini ‘ ambapo alitua nchini usiku wa jana na  mchana  wa leo amesaini mkataba huo.

Huddah Monroe "Nachukia Sana Tendo la Ngono..Najuta Kujiingiza Huko"

$
0
0
Kila mtu ana mabaya na mazuri yake katika maisha. Mrembo Huddah Monroe ambaye anafahamka sana kwenye mitandao ya kijamii ameonyesha kujutia kuingia katika mahusiano.

Licha ya kuwa na mvuto hasa kwa wanaume, mrembo huyo ameonyesha kuchukia maisha yake ya kimahusiano na anatamani bora asingejiingiza katika tendo la ngono na mtu yeyote kwa sababu wakiachana na mtu huyo huwa anajutia kuingia naye kwenye mahusiano.

Huddah amepost kupitia Snap Chat yake ambayo inaelezea kuwa anajutia kitendo hicho na tena anakereka hasa anapoachana na mtu huo na  baadae  mtu huyo ambaye anamuoana mbaya kwa wakati huo anakuwa akimfua warudiane.

Kukamatwa Kwa Viongozi wa TFF na Takururu..Haji Manara Awatumia Pole ikiwa na Dongo Ndani yake

$
0
0
Baada ya taarifa za kukamatwa kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF, Jamal Malinzi na Katibu Mkuu wake Mwesigwa Celestine leo mapema msemaji mkuu wa klabu ya Simba (aliyesimamishwa), Haji Manara ametoa pole kwa viongozi hao.


Haji Manara amesema sisi kama wanadamu tunapitia changamoto nyingi sana hivyo ni bora tukafarajiana japo hata kwa kupeana pole pale mwenzio anavyopatwa na matatizo.

Poleni Viongozi wangu wa TFF,no matter wat!!ni challenges tu ktk life, bnadaam hatufai kuombeana mabaya,hata kama huwakukutendea haki, Mungu awasimamie kutendewa HAKI,“ameandika Haji Manara kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Haji Manara ambaye alipigwa ‘STOP’ na TFF ya kutokujihusisha na masuala ya soka kwa mwaka mmoja kwa makosa ya kinidhamu bado anaendelea na msimamo wake wa kuitumikia klabu yake ya Simba kama kawaida kwani alilitaka Shirikisho hilo limpe barua ya kumsimamisha.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images