Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live

Tetesi: TCRA: Tangazo la Jaza Ujazwe linakiuka maadili

$
0
0
Baada ya TCRA kufanikiwa kuwaondolea wananchi KERO ya kusikilizishwa matangazo kwa lazima pindi wanapopiga simu, kuna taarifa kuwa wameitaka pia Kampuni ya Simu ya tiGO kufuta tangazo lake la JAZA UJAZWE kwa sababu linaenda kinyume na maadili na utamaduni wa kitanzania. Kuna tetesi watu wengi wameripoti kukerwa na tangazo hilo la kuudhi, hivyo TCRA wameitaka kampuni hiyo kulifuta mara moja kutoka kwenye mabango na matangazo ya sauti (televisheni, redio, yutube, santuri, nk).

MAONI YANGU
Kama kweli TCRA wamefikia uamuzi huo mimi nawaunga mkono kwa 101%. Ni ukweli usiopingika kuwa lugha iliyotumika kuandaa tangazo lile inakosa staha na adabu. Hata ikitokea baba na familia yake wanatazama TV sebuleni, tangazo hilo linapoanza tu baba huzima TV mara moja au kubadilisha chaneli.

Nawapongeza TCRA kwa uthubutu huu wa kuwaondolea kero wananchi hivyo kwenda sambamba kabisa na sera ya serikali ya “Tanzania ya Viwanda”. Nchi haiwezi kufikia malengo ya kuanzishwa viwanda wakati wananchi wanakwazwa na vitu kama hivi. Aidha, wananchi wataenda kinyume na maagizo ya Rais ikiwa tangazo hili litaendelea kuruka hewani na kutazamwa na watu wengi.

Kumbuka kwamba Rais ameagiza wasichana wanaopata mimba wasiruhusiwe kuendelea na masomo katika mfumo rasmi wa elimu; na watu wanaosababisha mimba hizo imeagizwa wafungwe jela miaka 30! Kwa kuwa tangazo la tiGO linachochea mafataki kuwajaza wanafunzi wa kike chips kuku na kisha kuwajaza mimba (JAZA UJAZWE), kusitishwa kwa tangazo hili kutapunguza idadi ya wasichana wanaojazwa mimba na mafataki. Vilevile, katazo la tangazo hili kutapunguza idadi ya mafataki wanaofungwa jela kwa sababu ya kuwapa mimba wanafunzi, hivyo kupunguza msongamano wa wafungwa katika mahabusu na magereza zetu.

Viva TCRA

By Tpaul/JF

Donald Trump: Muda wa Uvumilivu Umeisha Korea kaskazini

$
0
0
Rais wa Marekani Donald Trump anasema muda wa uvumilivu wa kimikakati kwa Korea Kaskazini umekamilika sasa.

Katika hotuba ya pamoja na rais wa Korea Kusini Moon Jae, kwenye ikulu ya White house, Trump amesema kwamba vitisho vya Korea Kaskazini vinafaa kupata majibu ya kijasiri.

Hata hivyo, Trump amesema ni muhimu kuwe na ushirikiano katika kugawana mzigo wa kuhakikisha usalama.

Rais wa Korea Kusini amesema kwamba taifa lake litaweka marekebisho ya kiuslama na kujenga msingi dhabiti wa kujikinga.

Rais Moon pia amesema ni muhimu kuendelea na majadiliano na viongozi wa Korea Kaskazini.

Ukiwa na Tabia hizi 7, Lazima Mwanaume Akukimbie

$
0
0
1. CHOKOCHOKO
Wanaume wengi huwa hawapendi chokochoko. Hawapendi mwanamke ambaye yeye kila wakati ni kuanzisha chokochoko ambazo zinazalisha ugomvi. Wanaume wengi hawapendi mabishano. Hawapendi ugomvi hivyo mwanamke anapokuwa hodari wa kuleta chokochoko, huepukwa.

Ni vyema basi mwanamke akachunga kauli. Akawa si mtu wa kuchimbachimba vitu ambavyo havina kichwa wala miguu. Asiwe na kisirani. Kinywa chake kitawaliwe na maneno matamu, yatakayomtia moyo mpenzi wake, yatakayomfariji na yatakayomfanya apende kuzungumza naye.

Mara nyingi mwanaume akiona mke au mpenziwe ni mtu wa kupenda chokochoko, mara nyingi humuepuka. Anajitahidi kadiri ya uwezo wake kukaa naye mbali. Ataona ni bora achelewe kurudi nyumbani akakutane na marafiki baa, wapige stori ili muda uende na akirudi nyumbani asiwe na muda wa kuzungumza na mwenzi wake, yeye ni kula na kulala.

2. KUTORIDHIKA
Wanaume wengi wanachukia kuwa na wanawake wasioridhika. Baadhi ya wanawake hata uwape nini huwa hawaridhiki. Wanawasumbua wapenzi wao kwamba hawawatimizii mahitaji. Mwanaume anajitoa kumpa zawadi mpenzi wake, haridhiki tu.

Anaanza kuikosoa. Anasema haifanani na yeye, eti si ya hadhi yake. Akipewa fedha anasema hazitoshi. Kila siku ni malalamiko. Hampi nafasi mpenzi wake ya kufurahia uhusiano wao.  Anamfanya kila anapokutana naye awaze atapigwa mzinga.

Bahati mbaya sasa kila atakachopewa haridhiki. Anatamani kikubwa zaidi. Wanaume wengi siku hizi wanaichukia tabia hiyo. Hawapendi kuwa na mwanamke ambaye haridhiki na kile kidogo walichojaliwa. Wanaume wengi wakiona hivyo huwa wanaanza kumuepuka mwanamke wa ‘sampuli’ hiyo.

Kwake kunakuwa hakuna jema. Badala ya kumshauri mpenzi wake mbinu za kujikwamua kiuchumi yeye ni lawama tu. Kila siku analalamika kwamba wanaume wengine wanawapa wapenzi wao mahitaji muhimu lakini wa kwake hamtimizii.

Mwanaume akiona kila analofanya kwa mpenzi au mkewe haridhiki, hatoi shukurani ni rahisi kupunguza mapenzi kwa mtu wake. Taratibu anaanza kujitoa na hata kuhamishia mapenzi kwa mtu mwingine ambaye atakuwa anaridhika kwa kidogo anachopewa. Ni muhimu kuridhika.

3. KULINGANISHA
Hii nayo ni tabia isiyopendwa na wanaume wengi. Wanaume wanapenda kuishi maisha yao. Wanapenda kuheshimiwa na wapenzi wao. Wanapenda kumsikia mwanamke akisema; ‘hakuna mwanaume mwingine wa kufanana na wewe.’

Mwanaume anapenda kuhakikishiwa kwamba hakuna mwanaume mwingine kama yeye. Yeye ndiye mzuri au bora kuliko wanaume wengine hivyo mwanamke anapoanza kuonesha tabia za kumlimnganisha na mwanaume mwingine linakuwa tatizo kubwa.

Mwanaume anakasirika. Anaona ni rahisi mwanamke wake kumtamani mtu mwingine baki kuliko yeye. Sifa anazozitoa kwa mwanaume mwingine ni nzuri hivyo zinamvutia. Kama zinamvutia siku yoyote anaweza kushawishika kumfuata yule anayemvutia.

Wanawake wanapaswa kuwa makini katika eneo hilo. Hata kama umeona kuna kitu kizuri kimekuvutia kutoka kwa mwanaume mwingine, kamwe usije kumwambia mwenzi wako. Baki nalo moyoni. Jipe moyo kwamba mwanaume uliyenaye ndiye bora kuliko wanaume wote duniani.

4. KUWA TEGEMEZI
Wakati mwingine hata kama huna kitu lakini mwanamke unashauriwa kutojionesha huna kitu. Jioneshe kwamba una kitu hata kama huna. Wanaume wa sasa hawapendi kuwa na mwanamke ambaye kila kitu anategemea kutoka kwa mwanaume.

Hata kama huna kazi lakini ni vyema basi mwanamke akajaribu kufanya biashara ndogondogo ambazo zitampunguzia mwanaume wake makali ya kuombwa fedha kila wakati. Wanaume wanapenda kuwapa wapenzi wao fedha lakini inapozidi kipimo inageuka kuwa kero.

Yani kuanzia mahitaji ya kila siku, saluni, mavazi, ada ya watoto na mengine mengi mwanamke anamtegemea mwanaume. Yeye hataki kujishughulisha hata kidogo. Anataka aletewe, kazi yake kubwa ni kulea familia nyumbani.

Mwanaume akigundua mwanamke ni tegemezi mkiwa katika hatua za mwanzoni, ni rahisi kumkimbia mwanamke na kwenda kwa mwanamke ambaye angalau atakuwa hamtegemei kwa kila kitu. Mwanamke anayejiongeza hata kwa kutoa wazo la kuanzishiwa biashara ambayo itamfanya asiwe tegemezi.

5. KUTOKUA MUELEWA
Mwanaume anapenda mwanamke muelewa. Hapendi mwanamke mbishi. Anatamani kuwa na mwanamke ambaye akimueleza kitu, anajiongeza na kufanya zaidi ya pale mwanaume alipofikiria. Mwanaume anapenda mwanamke atakayeanzisha wazo la kimaendeleo na kumshirikisha mpenzi wake ili walifanye.

Wanaume wanapenda wanawake wanaowaelewa. Kama mwanamke anakuwa si wa kumuelewa mpenzi wake, kumsaidia basi mara nyingi mwanaume humkimbia.

6. KUJITAPA KWA KUWA NACHO
Hakuna mwanaume anayependa kutawaliwa. Wanawake wenye fedha mara nyingi wanakuwa na tabia ya kutaka kuwatawala wanaume. Anataka mwanaume afanye kile ambacho yeye anataka. Fedha zinamvimbisha kichwa na kuona kwamba anaweza kuwa na mamlaka ya kumuamrisha mumewe.

Anatumia fedha zake kama fimbo ya kumchapia mpenzi wake. Ni vigumu sana wanaume kumvumilia mwanamke wa aina hiyo, mara nyingi wanajiepusha naye. Kwa kutumia fedha zake anaweza kupata mwanaume mwingine lakini pia watashindwana katika suala la kumtawala.

7. KUWA BIZE SANA
Wanaume wengi hawapendi mwanamke tegemezi lakini pia wanaume haohao wanachukia mwanamke akiwa bize sana na kazi zake. Mwanaume hapendi kuona mwenzi wake anakuwa bize na kazi au biashara zake kiasi ambacho kitamfanya hata akose muda na mwenzi wake.

Unachotakiwa kufanya hapo mwanamke ni kujigawa. Hakikisha unakuwa bize na kazi lakini si ya kupitiliza maana itamfanya mwanaume akose muda wa kuwa na wewe pale anapokuhitaji, badala yake anaweza kwenda kwa mwanamke mwingine ambaye hayupo bize.

Mama kuwa makini House Girl Yaweza Kuwa Mke Mwenzio

$
0
0
Ndugu msomaji wa Muungwana Blog, karibu kwenye makala hii maalumu, nimeamua kuandika habari hii ili kujaribu kupunguza mifarakano kwenye familia zetu especially familia zenye wafanyakazi wa ndani wanaojulikana kama house girl.

Katika mada hii nimekuwa nikikutana na maswali mengi sana ambayo mda mwingine yalikuwa yakituchanganya hata sisi wenyewe katika kuwajibu wahusika, maswali haya malanyingi yalikuwa yakiulizwa na akina mama.

Na kwa upande wa akina baba maswali yao sio mengi ukilinganisha na akina mama, sasa napenda nianze kwa kusema mambo yafuatayo ili wote twende sawa.

WAJIBU WA MWANAUME KATIKA FAMILIA: 
Mwanaume anawajibu wa kutimiza mahitaji yote ya msingi katika familia yake, moja ya majukumu hayo ni pamoja na kutoa pesa za matunzo ya familia yake kadri ipasavyo, kuonyesha upendo wa dhati kwa mama pamoja na watoto wake, na mambo mengineyo nk.

WAJIBU WA MWANAMKE KATIKA FAMILIA: 
Mwanamke ndiye mtendaji mkuu wa familia kwa upande wa nyumbani ukiachilia mbali ya kwamba baba ndiye kichwa cha familia, mwanamke anamajukumu mengi kwa upande wa nyumbani moja ya majukumu yake ni pamoja na kupika chakula cha familia, kufua nguo za mumewe pamoja na nguo za watoto, kuakikisha nyumba pamoja na eneo linaloizunguka nyumba ni safi, kuonyesha upendo wa dhati kwa mumewe pamoja na watoto wake, nk.

Ndugu msomaji wa makala hii, nadhani mpaka hapo tayari umeisha anza kupata mwanga kuhusu jibu la swali la makala yetu, sasa twende kuona wajibu wa mfanya kazi wa ndani kama house girl.

House girl wajibu wake ni kuakikisha anafanya usafi wa kuizunguka eneo la  nyumba kwa nje na kufanya usafi huo kwa upande wa ndani kwa baadhi tu ya maeneo ya nyumba hiyo pamoja na kuwaogesha watoto, kufua nguo za watoto, na kufanya kazi ndogo ndogo za nyumbani.

House girl hatakiwi kufanya usafi chumbani kwa mume wa mama mwenye nyumba, house girl hatakiwi kufua au kupiga pasi nguo za mume wa mama mwenye nyumba, house girl hatakiwi kumuandalia chakula au chai mume wa mama mwenye nyumba, nk.

Sasa ukiona house girl anafanya kazi zote nilizosema kuwa hatakiwi kuzifanya pindi awapo nyumbani kwako, ukiwa kama mama mwenye akili timamu jua kabisa tayari umeamua kumuletea mumeo mke mdogo na pia usipige kelele wala kulaumu maana jitihada zote za kumuandaa mke mwenzio umezifanya wewe mwenyewe.

Ushauri wangu kwenu akina mama na akina dada nikwamba, hatukatai kuwa wafanyakazi wa ndani hawafai, ila jitaidi mfanyakazi wako awe na mipaka ya kazi, mwanaume anaamua kumuoa house girl kwa sababu yeye amechukua majukumu yote ya mama mwenye nyumba, sasa wewe mama usianze kumtupia maneno mtoto wa watu pamoja na mumeo maana yote hayo umeyataka wewe mwenyewe.

Kanuni Kumi '10' za Kuwa Mke Mwema

$
0
0
UHALISI WA MAISHA:
Maisha halisi ya mwanamke anayetarajia kuwa mke/ mke tayari hii ni kumaanisha kuwa wanawake mashujaa tunapaswa kuishi maisha ambayo yanatutambulisha kama mfano wa kuigwa ili tunapozungumza na kufundisha mabadiliko tuwe tunazungumza uhalisia wa maisha yetu ambao unajengwa na haya yafuatayo;

UVUMILIVU:
Kuwa mvumilivu katika maisha yake ya kila siku hasa ukizingatia kuwa tunakutana na mambo mbali mbali yasiyotuvutia katika mahusiano yetu, mengine ni magumu na yanayokwenda kinyume kabisa na matakwa yetu au mazoea yetu ya binafsi. Ifahamike kwamba wewe kama mwanamke shujaa inapotokea umekutana na mambo kama haya hupaswi kuonyesha hasira zako wazi wazi kama vile; chuki, kulaumu, ugomvi, vurugu, malalamiko, manung’uniko, machafuko, kulipa kisasi au aina yoyote ya uharibifu kutokea kwako au ndani mwako. Hivyo mwanamke shujaa huwa ni heri kila anapokuwa kwani hutunza amani ya eneo alipo.

UPENDO WA DHATI:
Maisha ya upendo wa halisi na sio wa kinafki kwa jamii inayomzunguka. Tabia ya upendo wa halisi ina thamani kubwa sana kuliko mali nyingi, pesa, elimu ya juu n.k. wewe unaweza kabisa kuwa na elimu ya juu sana na pesa nyingi sana lakini pasipo upendo wa halisi ni sawa na kusema kopo zuri kwa nje na ndani hamna kitu. Nguzo kuu ya maisha ya mwanamke shujaa ni Upendo wa dhati na uhalisia.

UTII KWA KWA JAMII:
Maisha halisi ya utii katika jamii inayokuzunguka  ili kuweza kuyafanyia kazi yale yote uliyojifunza na pia kuyatenda kwa ufasaha pasipo kupita kona yoyote. Utii  kwa jamii ni ufunguo mmoja wapo utakaokusaidia kufanikisha mambo yako na malengo yako kama mwanamke shujaa.

UAMINIFU KATIKA JAMII:
Kuishi maisha ya uaminifu wa kweli na uhalisia katika jamii inayomzunguka. Uaminifu wa kweli huonekana nyakati zote na siyo tu wakati mtu anapokuwa mbele za watu wanaomjua bali hata wale wasiomjua na hata anapokuwa mahali peke yake aweze kutunza uaminifu wake kwa faida ya jamii nzima. Mwanamke shujaa hujitahidi sana kutunza uaminifu wake katika sekta zote.

UNYENYEKEVU WA KWELI:
Kuishi maisha halisi kabisa ya unyenyekevu kwa jamii inayomzunguka, unyenyekevu ni kinyume kabisa na kiburi, majivuno, kujigamba, kujikweza, kujiinua, kujiona,na hata kjitanguliza mbele kwa kila jambo. Mwanamke shujaa huwa ni mnyenyekevu wakati wote na hana makuu daima.

UWAJIBIKAJI WA DHATI:
Maisha halisi ya uwajibikaji akiangalia majukumu yake yote yanayomkabili na kuhakikisha anafanya kwa moyo bila kuwa na tabia ya kusaidiwa majukumu yake. Mwanamke shujaa ni mfano wa kuigwa kutokana na uwajibikaji wake.

USHIRIKIANO WA DHATI:
Ushirikiano katika jamii inayomzunguka. Sisi wanawake mashujaa yatupasa kujua dhahiri kuwa kazi ya kubadili tabia na kufanya wengine wabadilike kwa lengo la kupata familia bora ni lazima kuwa na ushirikiano wa kweli ambao utajenga tabia ya kuaminiana na kunai mamoja katika harakati hizi za kuandaa/ kujenga familia bora.

UTARATIBU WA KAZI/MPANGILIO:
Katika utaratibu wa maisha yake, pamoja na mpangilio mzuri wa mambo yanayomzunguka hii itakusaidia kuwa na muda mzuri wa kufanya shughuli zako na pia kutekeleza majukumu yako ya kila siku kama mwanamke shujaa. Hakuna njia yoyote ya kukuwezesha kukua na kuendelea katika maisha yako bila kuwa na utaratibu na mpangilio wa mambo yako.

KUFANYA TATHIMINI:
Kuweza kufanya tathimini ya yale yote anayoyafanya katika maisha yake ya kila siku, pengine ni mfanyabiashara, mfanyakazi, mkulima n.k kama mwanamke shujaa yakupasa kutathimini shughuli zako kama zina leta faida/hasara kwa familia na jamii yako inayokuzunguka. Ukiona faida ni kubwa unaendelea na hiyo shughuli lakini kama hasara ni kubwa unajiweka katika nafasi ya kubadilisha aina ya shughuli mara moja bila kupoteza wakati.

Masauni: Lazima Tushinde vita ya Kibiti

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Hamad Masauni amesema kuwa Suala la kumaliza uhalifu kibiti na Mkuranga ni jambo ambalo halina mjadala kwani ni lazima lidhibitiwe.

Mhe. Masauni amesema hayo wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu mauaji yanayoendelea maeneo ya Kibiti, Rufiji na Mkuranga.

“Suala la kumaliza uhalifu Kibiti na Mkuranga ni suala ambalo halina mjadala, ni suala la lazima lakini, suala ni lini uharaka wake ndio maana tumejadili changamoto zinazokabili ili tuweze kukaa kwa pamoja tuweze kuzifanyia kazi. Tuweze kuharakisha zoezi hili ambalo kwa hakika kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu kwa sisi tunaosimamia haki na uhai wa raia wasio kuwa na hatia hii vita lazima tushinde inshaallah,” alisema Masauni.

Okoa Ndoa Yako Sasa, Ongeza Maumbile, Nguvu na Hamu ya Tendo la Ndoa Kwa Hata Wenye Kisukari

$
0
0
OKOA NDOA YAKO SASA. ONGEZA MAUMBILE, NGUVU NA HAMU YA TENDO LA NDOA HATA KWA WENYE KISUKARI. Tatizo la maumbile madogo, nguvu za kiume na ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limekuwa likiwasumbua wengi na kusababisha kushindwa kujiamini ktk tendo hivyo kusababisha ndoa nyingi kuvunjika pamoja na mahusiano. Upungufu wa nguvu na hamu ya tendo husababisha mambo kama:-
(a)Uume kulegea wakati wa tendo (b)Kukosa hamu ya tendo la ndoa (C)Kuwahi kufika kileleni (D)Uume kuchelewa kusimama baada ya round ya kwanza. (E)Kuchoka sana baada ya round moja n.k @Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo kwa kutumia bidhaa zilizotengenezwa kwa mimea na matunda zisizo na kemikali wala madhara na kuthibitishwa kiafya. Pata hizi👇👇👇👇
🍉 🌿🍅🍒🍍🍓🍉🍎🍀
1.HANDSOME UP ni kifaa chenye uwezo wa 99 % kuongeza uume (size unayohitaji) na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200000@200,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130000@130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130000@130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo hata mara 3 @130000@130,000/= Kwa Bidhaa hizi na nyingine kama:-
5.Kupunguza unene na manyama uzembe @150000@150,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi @130000@130,000/=
7.Kutengeneza shepu (hips, makalio na mapaja) @200000@200,000/= 8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni @120000@120,000/=
9.Kuwa mweupe na soft mwili mzima bila kuacha sugu 120,000/=
10.Kurudisha usichana (bikra) @120000@120,000/=
11.Kupunguza au kuongeza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120000@120,000/=

Wasiliana nasi kwa (+255) 0767447444 au 0714335378.

NB: Matokeo ni uhakika na garantii na upate risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii. Follow us
@Markson_beauty_pr

Rais Magufuli Amuweka Njia Panda Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo na Biashara Nchini Christopher Chiza

$
0
0
Rais John Magufuli  ameshangazwa na kauli ya Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo na Biashara nchini Christopher Chiza kuwa na mipango ya kujenga majengo mapya kwa ajili ya wafanyabiashara badala ya viwanda vitakasaidia nchi.

Akizungumza leo wakati wa ufunguzi wa Maonyesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa, Rais Magufuli amesema kwamba ameshangazwa sana na mipangio ya kujenga mahoteli pamoja na kufanyia ukarabati wa majengo kwani hajui mahali pesa hizo zitakapopatikana.

"Mh. Chiza amezungumza kubadilisha majengo na kujenga mapya, mawazo mazuri lakini najiuliza hizo hela zimetoka wapi , haingii akilini wao ndio wanatusisitizia mambo ya biashara na viwanda na 'theme' ya mwaka huu inazungumzia kukuza biashara na maendeleo ya viwanda sasa wao badala ya kuzungumza juu ya maendeleo ya viwanda wanataka wajenge Hotel hapa, watengeneze majengo mapya sasa. Sijaelewa, sasa kama hizo hela zipo basi mzipeleke mkajenge kiwanda cha mfano

Aidha Rais magufuli amesisitiza kwamba  "Haya majengo yaliyopo ambayo mnayaona yamechakaa hawa wanaokuja kuonesha bidhaa zao wapeni bure wajenge ili kila mwaka wawe wanaonesha, hiyo Hoteli kwani mkijenga lazima walale hapa hapa? Mnaweza kujenga hoteli hapa bado wakaenda mjini.  Mimi nilifikiri badala ya  kujenga jenga majengo fikirieni zaidi katika kujenga viwanda kwa ajili ya mfano wa kuonesha Wizara kweli iko mbele kwa ujenzi wa viwanda.

Katika kuonyesha nia ya kufikia Tanzania ya viwanda inafikiwa Rais ameitaka wizara pamoja na bodi hiyo kutofikiria ujenzi wa majengo.

"Mwenyekiti nimekuteua juzi umeshaanza kufikiria majengo hapa pamoja na Bodi yako mnanifanya nifikirie zaidi. Haya majumba yanaweza yakawa siyo mazuri sana lakini ni mazuri kwa watu wa Tanzania ambao wanataka kuona bidhaa. Yanayowaleta hapa siyo majumba Watanzania wanakuja hapa kuangalia Teknolojia na vifaa vilivyomo.Inawezekana mimi nipo tofauti mnisamahee lakini katika muelekeo wangu ninaona hizo hela mnataka kuzitumia vibaya" Rais alisisitiza.

Pamoja na hayo Mh. Rais amewaomba waandaji wa maonyesho hayo pamoja na Waziri wa viwanda na biashara Mh. Charles Mwijage  kuongeza siku zaidi katika maonesho ili watanzania waweze kupata muda mzuri wa kununua na wafanyabiasha kuuza ambapo ombi lake lilikubaliwa hapo hapo na kuongezwa siku tano mbele.

Install APP ya Blog Hii ya UDAKU SPECIAL Kwenye Simu yako Kutoka Google Play Kusoma Habari Kirahisi

$
0
0
Download  Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE 


Au Kama Unayotayari Bonyeza HAPA Ku Update Uweze Kupata Ikiwa na Muonekano Mpya

Mabinti Siri Ishafichuka Wanaume Hupenda Wanawake Wenye Tabia Hizi

$
0
0

Wanaume wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mwingi kuchunguza mambo mengi juu ya wake ambao wanadhani kwamba wanaweza kuwa pamoja kwa kipindi chote cha maisha. 


Wanawake wengi wanajisahau na kudhani kwamba kitu kinachoweza kuwafanya wakapata wachumba ni uzuri hivyo kupoteza muda wao kujichubua na kujiremba ili wawavutie wanaume bila kujua kwamba kuolewa ni zaidi ya uzuri.

Hali sasa hivi imebadilika ni tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ukiwa na sura nzuri na umbo la kuvutia basi una asilimia 100 za kuolewa. Utafiti ambao nimeufanya unaonesha kwamba zaidi ya uzuri wa tabia na umbo, kuna kuna sifa nyingine za msingi ambazo mwanamke anatakiwa kuwa nazo ili aweze kuwa katika mazingira mazuri ya kupata mchumba wa kumuoa kiasi kwamba asipokuwa nazo ataishia kuchezewa tu lakini haitatokea mtu kumtakiwa kwamba anataka kumuoa.

MWEYE MAPENZI YA KWELI

Lengo kubwa la mwanaume kuoa ni kutaka kupata mapenzi ya kweli kutoka kwa mwanamke na ikiwezekana waweze kupata watotoa ambapo watoto mara ndio wamekuwa furaha ya ndoa. Wapo wanawake wengine ambao wanonesha wazi kutokuwa na mapenzi ya kweli bali wanakuwa na mapenzi ya kuzuga. Wanachotaka wao aidha kupata umaarufu tu kwamba yuko na mtu fulani ama kuweza kupata pesa alizonazo mwanaume lakini sio kwamba ana mapenzi ya dhati kutoka moyoni mwake. Mwanamke asiye na mapenzi ya dhati utamgundua tu, muda mwingi utamuona macho yake yako kwenye mfuko wa mwanaume. Akiona kwamba mfuko umetuna utaona anaonesha mapenzi ya hali ya juu lakini pindi hali inapokuwa kubwa mbaya kifedha mapenzi yanaanza kufifia.

Kwanini wanaume wanapenda wana wake wenye mapenzi ya dhati kutoka mioyoni mwao na si kutokana na fedha walizonazo? Hii inatokana na ukweli kwamba maisha siku zote yanabadilika, kama waswahili wanavyosema, kuna kupanda na kushuka.Sio kwamba kila siku utakuwa na maisha mazuri na kama itatokea hivyo basi ushukuru mungu.Hivyo basi mwanamke wa kuoa lazima afahamu hivyo na awe tayari kuonesha mapenzi yake ya dhati wakati wote wa maisha yao na si kwa kipindi fulani tu cha neema.

Si hivyo tu pia asilimia kubwa ya maisha ya ndoa yanatawaliwa na mapenzi, kwa hiyo nyanja hiyo inakuwa ya msingi sana kwa wanaume wengi kuiangalia ili wasije wakajikuta wanaoa mwanamke ambaye baada ya muda mapenzi yanakwenda likizo hali ambayo inaweza kuwafanya wasiishi maisha ya raha mustarehe.

WENYE TABIA NZURI

Tabia njema ndio silaha ya maisha, ukiwa na tabia nzuri kila mtu atakupenda, hiyo ni katika maisha ya kawaida. Lakini linapokuja suala na kuoa tabia inakuwa kitu cha awali sana kungaliwa na hiyo inaweza kuwa na ukweli kwa sababu wapo wasichana wazuri wenye mvuto wa aina yake na maumbile mazuri, lakini wanakosa wanaume wa kuwaoa, ukiuliza kwani utaambiwa anatabia mbaya. Naweza kusema hilo ndilo limekuwa tatizo kubwa kwa baadhi ya wanawake kukosa wanaume wa kuwaona. Hakuna mwanaume hata mmoja kati ya wale ambao nimejaribu kuongea naye ambaye ameonesha kulidharau suala hilo la tabia.
Si hivyo tu wapo wanaume ambao wameingia kichwa kichwa na kuoa kwa kuangalia sura tu bila kujali tabia, matokeo yake baada ya siku chache yanatokea machafuko ya aina yake hali ambayo imepelekea kuvunjika kwa ndoa kutokana na tabia mbaya alizonazo mwanamke.

WENYE UCHU NA MAENDELEO

Hivi karibuni kumekuwepo na mabadiliko ya aina yake kwa wanaume, wengi sasa hivi hawapendi kabisa kuoa mwanamke ambaye hana kazi yaani 'golikipa'. Kama atakuwa hana kazi basi awe na uchu wa maendeleo kwa kujituma kufanya kazi mbalimbali za kimaendeleo kama vile kilimo kwa wale walio vijijini na biashara ndogondogo kwa wale ambao wako mijijini na hata vijijini. Ile dhana ya kusema mwanamke ni mama wa nyumbani wa kukaa na kujipodoa akimsubiria mwnaume arudi amstarehesha, sasa hivi imepitwa na wakati. Wanaume wengi wanapenda wanawake ambao ni wahangaikaji, wenye ndoto za maendeleo katika maisha yao. Hata kama watakuwa si wafanyakazi lakini wawe wenye kutoa ushauri kwa waume zao juu ya jinsi gani wafanye ili wafanikiwe.

WASIOPENDA MAKUU

Kuna wanawake wengine wanakuwa na tabia za ajabu sana kiasi kwamba yaweza kuwa kero kwa wanaume. Wapo wanawake ambao wanapenda makuu bila kujali hali halisi ilivyo. Kuna wanawake naweza kusema wana tamaa, kila wikiendi utamsikia "leo tunakwenda wapi dear?" Akimuona rafiki yake kanunua simu ya laki tatu na yeye utamsikia akisema, ‘na mimi naomba uninunulie simu kama ya Grace’. Ukienda naye Pub anakuambia, "mimi sinywi pombe za chupa natumia za kopo tena Heineken’. Yeye hajali kiasi cha pesa mwanaume alicho nacho na usipotekelezea anachukia na anaweza hata kupunguza mapenzi.


Wanawake kama hawa wako katika mazingira magumu sana ya kuweza kupata wanaume wa kuwaoa. Mara nyingi katika maisha fedha huzungumza, kama mwanaume atakuwa na pesa ya kutosha itakuwa rahisi sana kwa mwanamke kupata kila atakachopenda lakini si kwa kumwambia mimi nataka kitu fulani.Mwanaune mwenyewe utamsikia akisema, ‘unataka nikununulie simu ya aina gani, au leo unataka twende wapi?’ hapo ndipo utakuwa na nafasi ya kusema, ‘mimi nataka uninunulie simu kama ya fulani ama leo nataka twende sehemu fulani.’

Wanaume ni warahisi sana wa kuwapatia wale ambao wanatarajia kuwaoa chochote ambacho watahitaji kama tu pesa haitakuwa tatizo. Kitu ambacho kinawaudhi wanaume wengi ni ile tabia ya mwanamke kupenda mambo makubwa bila kuangalia uwezo uliopo kwa mwanume.
Kuna wanawake wengine wao si wasemaji kabisa, yeye anasubiri leo amemletea hiki, anapokea na kushukuru, kesho akiambiwa twende beach anakubali. Au wengine wanasubiri mpaka waulizwe wanataka nini, ndio wanasema.

Sisemi kwamba uwe mkimya tu hata kama una shida ya kitu fulani na unafahamu kwamba ukimweleza mwenza wako anaweza kukusaidia, hapana! kama unaona kwamba uwezekano wa kupata kile ambacho unakihitaji upo mweleze kwa utaratibu naamini atakuelewa na kukutimizia.Tabia ambayo hawaipendi wanaume wengi ni ile ya kulazimisha ufanyiwe kitu fulani wakati inawezekana uwezekano haupo.

WAVUMILIVU

Wapo wanawake ambao sio wavumilivu kabisa katika maisha.Tunajua kwamba maisha siku zote hayatabiriki, yanaweza kutokea matatizo ya kiafya ama kifedha.Huu ndio wakati wa kuona uvumilivu wa mtu.Kama mwanamke anatarajia kwamba siku zote ni za raha tu na pindi matatizo yanapotokea anachukua uamuzi wa kumtoroka mwanume, huyo siyo mwanamke wa kuoa.Wangapi leo hii huwatoroka waume zao pindi inapotea kuumwa, kufilisika ama kupatwa na tatizo lolote ambalo kwa namna moja ama nyingine yanaweza kuwafanya maisha yao kutingishika?

Uvumilivu kwa mwanamke utakuwepo kama tu atakuwa na mapenzi ya dhati kama nilivyozungumza hapo awali. Mwanamke mweye mapenzi ya dhati ni lazima atakuwa mvumilivu na atakuwa tayari kuishi katika maisha ya aina yoyote, yawe ya raha ama ya starehe.Hawa ndio wale ambao wanaume wengi wengependa kuwa nao maishani mwao.

Licha ya kupenda kuoa wanawake amabo wana tabia hizo nilizozitaja hapo juu, wanachukizwa sana na wanawake ambao wanavijitabia vidogo vidogo ambavyo kimsingi havikubaliki katka jamii.Tabia hizo ni kama wambea, wasio wakweli na wawazi, wasioridhika, wagumu kusamehe na wapesi wa kuchukia, wagomvi na wenye roho ya kwanini.

Utafiti huu umefanyikwa kwa baadhi ya wanaume ambao wanatarajia kuoa wanawake ambao wanaoishi katika maeneo mbalimbali jijini Dar-es-Salaam. Kwa maana hiyo basi hiyo iwe changamoto kwa wanawake. Wajue kwamba wanaume wanafurahi kuwa na wanawake wa aina gani. Hata kama utakuwa umeshaolewa, kama kuna wakati kunakuwa na kutokuelewana baina yenu, chunguza yawezekana kwamba unakosa mojawapo ya tabia ambazo nimezitaja hapo juu. Waweza kubadilika kwani inawezekana.

Prof. Kabudi: Watanzania Tuache Uoga, Hakuna Atakayeshitakiwa na ACACIA

$
0
0
Hayo yamesemwa na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi wakati akiwasilisha hoja na kujibu maswali mbali mbali kwenye Kamati nne za kudumu za bunge kuhusu miswada mitatu inayohusu raslimali za Taifa.

Prof. Kabudi amesema Serikali sio naive na inafahamu dunia ilivyo kuhusu economic order. Tunajua we are fighting giants but we cannot be afraid of giants. Tunatumia akili nyingi, hekima na busara katika vita hii.

Aliendelea kusema, ‘’We know there will be an attempt to sabotage, definitely na kama tuki-succumb kwamba we are fight a giant busi tukae, tutakuwa hatulitendei haki Taifa’’.

‘’This country has survived sabotage, miaka mingi tu, na sisi lazima tujaribu kuliko kukaa chini na ku-succumb’’ alisema.

Aliendelea kusema‘’Hatuwezi kuwa na wawekezaji ambao hatufaidiki nao nani bora madini tuyaache badala ya kuyachimba ili tusubiri hao kizazi kijacho watakaokuwa na busara na akili kwa sababu sisi tumeshindwa. Madini huwa hayaozi’’

‘’Sheria hii tutakayotunga haiwafukuzi bali inawakaribisha kwa mazungumzo, waje tuongee, tutaelewana na uzuri mambo tunayoyadai yamo ndani ya sheria za kimataifa, hatuyazui wenyewe. Mikataba ya sasa itaangaliwa, tutajadiliana nao. Hatufukuzi mtu na hawawezi kufunga migodi kwa sababu tunafahamu wanapata faida’’.

‘’Yes, we fighting giant, biashara ya dhahabu inafahamika nani ana control lakini huyo giant unapomfikisha anarusha ndege kuja nchini kujadiliana, hayo ni mafanikio’’

‘’Kama Botswana yenye wananchi milioni 2 inaweza ku-flex its muscles kwenye maliasili zake, sisi Watanzania ambao ni 50 millions, we are lame ducks and toothless bulldog. It's incredible’’.

‘’Tusisahau kuwa nchi hii ime survive kwa vitisho vikubwa kuliko leo. Mwaka 1964, Mwalimu angetetereka kwa Wajerumani waliokuwa wanatupa hela nyingi, akawasikiliza, Tanzania isingekuwepo kama Jamhuri ya Muungano. Kwa msimamo wa Mwalimu, tulipoteza Deutsche Mark milioni 35 lakini Mwalimu akawaambia pack and go’’.

‘’Mwaka uliofuata, 1965 kulitokea Unilateral Declaration of Independence (UDI) in Rhodesia ambapo nchi zote za Afrika zilikubaliana lazima Uingereza imuondoe Prime Minister, Ian Smith ama sivyo nchi zote zitavunja uhusiano wa kibalozi na Uingereza. Baada ya Uingereza kukataa, nchi mbili za Tanzania na Ghana ndizo zilivunja uhusiano wa kibalozi ambapo gharama yake ilisababisha Rais wa Ghana kupinduliwa huku Tanzania tukikosa msaada wa pound milioni 5’’.

‘’Malengo ya mifano yangu sio kwamba turudie hayo bali kuonyesha kuwa Taifa hili limepita vipindi vigumu kwa sababu lilikuwa na uongozi unaothubutu na kusimamia maslahi ya watu ili liweze kuvuka. Hiki ni kipindi kingine cha kuvuka’’.

‘’Tusiogope na kuanza kuulizana kuwa tutaweza au hatutaweza? Wawekezaji watatishia kuwa wataondoka lakini ninasema hawataondoka’’.

Prof. Kabudi amesema watu wa ACACIA kinachowasumbua siyo sheria bali ni integrity yao kwa sababu kampuni inayovunja integrity pledge hupelekea kushitakiwa kwa kosa la fraud. kampuni inayofanya fraud na ikadhibitika kisheria, mali zake hutaifishwa. Hiki kinafanyika hata kwenye nchi zao za Ulaya na Marekani’’.

Alisema, ‘’Ukiona ACACIA wanavyohangaika ambapo mara ya kwanza waliomba kuonana na Rais ambaye maombi yao aliyakataa. Wakaomba tena mara ya pili na kukubaliwa kupitia Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambaye ni mmiliki mkubwa wa hisa 63.9 wa Kampuni ya Acacia Mining, Profesa John Thorton’’.

‘’Kwao integrity ni muhimu sana kutokana na heshima ya kampuni ambayo wajumbe wa bodi ni viongozi wastaafu wenye heshima kubwa duniani’’.

Alimaliza kwa kusema, Watanzania tunatakiwa tujiamini kwa sababu nchi yetu ime train watu wengi katika fani mbali mbali pamoja na fani ya madini lakini tatizo lililopo ni kutowathamini, kuwadharau na kutowatambua. Hatukuwatumia na wameondoka kwenda kusaidia nchi nyingine. Kwa mfano, Nchi ya jirani tunayoisifu kuwa miji yake imepangwa vizuri, wataalam waliochora ramani ya miji hiyo wametoka Tanzania. Director of finance wa Air Tanzania ndio alikuwa Director of finance wa Air Rwanda. Ndiye ameiwezesha Air Rwanda kufika hapo ilipo. Key staff wa Air Rwanda ni Watanzania ambao baadhi yao wamekubali kurudi. Tatizo letu watanzania tunajidharau wenyewe wakati uwezo tunao’’.

Kwa maelezo zaidi angalia video.

Top 10 ya Madictator Waliouwa Watu Wengi zaidi Duniani....

$
0
0

10. Yakubu Gowon
Nigeria : 1966 - 1975
Total kills : 1.1 Million


9.  Mengistu Haile Mariam
Ethiopia : 1974 - 1991
Total kills : 1.5 million


 8. Kim II Sung
North Korea : 1948 - 1994
Total killing : 1.6 million


 7. Pol Pot
Cambodia : 1963 - 1981
Total kills : 1.7 million


6. Ismail Enver Pasha
Turkey : 1913 - 1919
Total kills : 2.5 million


 5. Hideki Tojo
Japan : 1941 - 1944
Total klls : 5 million


 4. Leopold II of Belgium
Belgium : 1865 - 1909
Total kills : 15 million


 3. Adolf Hitler
German : 1934 - 1945
Total kills : 17 million


 2. Jozef Stalin
The Sovjet : 1922 - 1953
Total kills : 23 million


1. Mao Ze Dong
China : 1943 - 1976
Total kills : 78 million

Zuma na Makamu Wake Walazimishwa Kusalimiana

$
0
0
Aliyekuwa mke wa rias wa kwanza wa Afrika Kusini Nelson Mandela,
Winnie Madikizela Mandela aliwalazimisha viongozi wawili maaruf nchini humo rais Jacob Zuma na makamu wa rais Cyril Ramaphosa kusalimiana.

Wawili hao walikuwa katika mkutano wa chama cha ANC mjini Johannesburg.

Bwana Ramaphosa anataka kumrithi rais Zuma na amekuwa akimkashifu rais huyo kwa uhusiano wake na familia ya Gupta.

Mojawapo ya mambo yaliobanikika katika barua pepe zilizotajwa kuwa 'Guptaleaks', ni kwamba rais Zuma alikuwa amepanga kwenda kuishi katika miliki za Kiarabu UAE.

Madai ambayo yamekanwa.

Mengine yalionyesha kuwa familia hiyo ya Gupta imekuwa na ushawishi mkubwa serikalini.

Huku Jamali Malinzi Akiendelea Kusota Selo...TFF Yamchagua Huyu Kuwa Kaimu Wake

$
0
0
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imekutana jana Jumamosi Julai 01, 2017 kwenye ofisi za TFF, Dar es Salaam imempitisha Wallace Karia kuwa Kaimu Rais wa shirikisho hilo huku Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Salum Madadi kuwa Kaimu.

Viongozi hao watakaimu nafasi tajwa hapo juu hadi mahakama itakapotoa maamuzi kuhusu kesi zinazowakabili kwa sasa ambaye ni  Rais wa TFF, Jamal Malinzi na Katibu Mkuu, Mwesigwa Selestine.

Kamati ya Utendaji ya TFF, imekutana kwa dharura kwa mujibu wa Ibara ya 35 (1) inayosomwa pamoja na Ibara ya 35 (6) na kufanya uamuzi huo.

Katika hatua nyingine, Karia amesema ujumbe wa FIFA unakuja nchini kufuatilia sakata zima la viongozi hao wa TFF kufikishwa kwenye vyombo vya dola.

Tundu Lissu Afunguka...Adai Serikali Ina Mkakati wa Kuminya Uhuru wa TLS ili Kuwadhibiti Wanasheria..

$
0
0
Chama cha Wanasheria cha Tanganyika (TLS) kimekutana kujadili na kutoa msimamo wao juu ya mapendekezo ya Serikali kuanzisha Bodi ya Usajili wa Mawakili huku kikiwataka mawakili wake kusimamia maadili ya taaluma yao ili kutimiza majukumu kwa haki.

Akizumza kwenye mkutano huo Rais wa TLS, Tundu Lissu amesema mapendekezo yaliyotolewa ni hatari kwa uhuru wa TLS na kada ya sheria kwa ujumla iwapo siasa itaingia kwenye kazi zao sheria.
Amesema bodi hiyo ikianzishwa itakuwa chini ya waziri wa sheria na katiba na ndiyo itakuwa na nguvu ya kusajili au kuwafuta wanasheria kadri itakavyoona inafaa.

"Mabadiliko haya ni hatari sana kwa uhuru wa wanasheria nchini, tumekutana hapa kuelezana na kupokea maoni ya wanachama kisha tutaweka msimamo wetu baada ya baraza la TLS kukaa Huo ni mkakati wa Serikali kuminya uhuru wa TLS ili kuwadhibiti wanasheria kuingia kwenye siasa, jambo ambalo  linatakiwa kupingwa na kila mtu kwa sababu matokeo yake ni mabaya" alisema Mh. Tundu Lissu.

Mbali na hayo Lissu amewaasa wanasheria kuwa endapo watashindwa kusimamia taaluma yao vizuri na kuruhusu siasa ikaingia ndani yake basi haitokuwa na maana ya  kuwepo kwa chama hicho.

Miujiza ya Maalim Khatibu Kutoka Kigoma Kusini Sasa Yupo Bagamoyo Mkoa wa Pwani

$
0
0

MIUJIZA YA MAALIM KHATIBU KUTOKA KIGOMA KUSINI SASA YUPO BAGAMOYO MKOA WA PWANI.

Wengi wamepata tiba na kutatuliwa MATATIZO yao wewe unasubiri nini?

✨Kwanini umapata pesa haikai? Na haufanyi kitu cha maana?
✨Kwanini mapenzi yakutese?
Kwanini uachwe na Mke! Mme au mpenzi wako?
✨Kwanini hamuelewani katika familia yenu kwaaji ya kugombea mali?

Majibu yote utayapata kwa MAALIM KHATIBU, mwenye kubri kubwa kutoka kwa Allah,✔

MAALIM KHATIBU ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili na nimtambuzi wa nyota za binadamu, pia nimtatuzi wa matatizo yote yanayo watesa binadamu,

MAALIM KHATIBU anatibu kwa kutumia kitabu cha quran dawa za asili dawa za kiarabu, na majini, Anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango kwa kina mama, ngiri maji na n.k, anakuvutia mali zilizo potea au kudhulumiwa, pia anatoa Pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali, Wenye matatizo ya uzazi, jini mahaba, mapepo ya kichawi, vifungo vya kimaisha, ndoto mbaya za usiku, uelewa mdogo wa ufahamu shuleni kwa watoto wote, pia anauwezo mkubwa wa kumaliza kazi zilizoachwa na wataalamu wengine ndani ya masaa 48 tu,Pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo.

WASILIANA NAE KWA SIMU NA WhatsApp
Tigo - No:+255 710 -332103
Voda - No:+255 766-705404,
Insta follow @maalim_khatibu

USHAURI: ni vyema kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate huduma kwa haraka.

Rais Magufuli: Tanzania ni Yetu, Selous Iko Tanzania......Tuna Uhuru wa Kuamua Mambo Yetu maana Tumechoka Kuchezewa

$
0
0

Rais  John Magufuli amesema ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler’s Gorge) mkoani Pwani lazima ufanyike, akiapa kuwa inyeshe mvua au liwake jua, lazima utajengwa.


Alisema hayo jana alipokuwa akifungua Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere (Sabasaba), barabara ya Kilwa.


Aliwaeleza wawekezaji kuwa changamoto ya umeme wa uhakika itakwisha, kwani Tanzania itakuwa na umeme wa megawati kati ya 4,000 na 5, 000 utakapokamilika mradi huo.


“Inyeshe mvua, liwake jua Stiegler’s Gorge itajengwa, tumeamua kuchukua juhudi za makusudi kuifufua na ninawahakikishia wawekezaji tunaifufua... na tunaanza kwa fedha yetu,” alisema Rais Magufuli.


Aliwahakikishia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwa Tanzania imejipanga vizuri, kuweka mazingira mazuri kutatua changamoto za sekta ya viwanda. 


“Moja ya changamoto kubwa ni suala la umeme, kama serikali tumeamua kuchukua jitihada za makusudi kutekeleza ahadi za Mwalimu Nyerere ya kuendeleza Stiegler’s Gorge kwa kujenga bwawa kubwa,” alisema.


Alisema ameshatoa maelekezo kwa wizara husika, pia imeundwa timu ya wataalamu wa kufuatilia na kwamba zabuni itakapotangazwa, watu wajitokeze kwa ajili ya ujenzi. 


Alisema ujenzi wa bwawa hilo, utawezesha kupatikana umeme wa megawati 2,100, ikimaanisha kuwa ni umeme utakaotosheleza mahitaji mengi, yakiwemo ya matumizi ya kawaida, viwandani na mengineyo.


“Najua wapo watakaojiuliza fedha kweli wanazo? Nataka kuwaambia fedha tunazo, haiingii akilini tunazungumzia viwanda wakati umeme hatuna,” alisema. 


Aliongeza kuwa, Serikali ikiomba fedha za mradi huo kwa wafadhili, wataweka masharti makubwa na kuambiwa mradi huo una matatizo ya kimazingira.


“Nataka kuwaambia kuwa hatutasikiliza suala la environmental impact (athari za kimazingira), Selous iko Tanzania, tunawajibu wa kuamua jambo la kufanya ambapo,” alisema Rais na kuongeza kuwa mradi huo, utatumia asilimia tatu tu ya hifadhi hiyo.


Alisema kwa watu ambao wanazingatia mambo ya kimazingira, wataona kwamba Tanzania inatunza mazingira, kwani yatapatikana maji kwa ajili pia ya uvuvi, viumbehai wengine watatumia pia maji hayo kwa kilimo.


Rais Magufuli aliwaomba wadau wa maendeleo ambao wana nia ya kuisaidia Tanzania, wajitokeze ili Watanzania wanufaike na maliasili zao. 


Alisema umeme unaopatikana sasa hapa nchini ni megawati 1,460, lakini jitihada mbalimbali zimefanyika katika kuongeza kiwango hicho, ambapo ni pamoja na kuongeza umeme katika miradi ya Kinyerezi I, II na III iliyopo Dar es Salaam, itakayoongeza upatikanaji wa umeme nchini.


Rais Magufuli waliwaomba pia mabalozi wa nchi zote zenye uwakilishi hapa nchini, kuisaidia Tanzania kupitia nchi zao katika miradi mikubwa ambayo ina tija kwa taifa zima.


 “Kwa sababu tukishaweza kuzalisha megawati 2,100 watu wengi watakuwa na umeme, nina uhakika Waziri wa Mambo ya Nje atakuwa amechukua hiyo, na pia nawaomba mabalozi wote tunahitaji msaada katika miradi mikubwa,” alisema.


Rais Magufuli alipongeza maandalizi ya maonesho hayo, ambapo baada ya kuhutubia alipita kuangalia baadhi ya mabanda na kupata maelezo mbalimbali. 


Alisema maonesho hayo yana faida kubwa kwa wafanyabiashara, kwani huwakutanisha na wateja wao na pia kukutana na kampuni nyingine za nje na ndani ya nchi, kujifunza mambo mbalimbali na pia kubadilishana uzoefu na kuanzisha uhusiano wa kibiashara.


Alizipongeza pia kampuni za ndani na zile za nje takribani 3,000, zinazoshiriki katika maonesho hayo, zikiwemo 515 kutoka katika nchi 30 duniani. Rais Magufuli alisema Tanzania ni salama na ya amani na kwamba ipo kwa ajili ya wawekezaji.


Aliwataka Watanzania kutumia maonesho hayo, kama chachu ya kuibadili Tanzania. 


“Tumechoka, tumechezewa sana, lakini tulichezewa kwa sababu tuliamua sisi kuchezewa lazima tubadilike na moyo wa kubadili Tanzania tuanze sasa,” alisema Rais Magufuli.

Namna Rahisi na Salama ya Kupunguza Tumbo

$
0
0

Wengi wa wasomaji wamemtumia meseji za kutaka kujua njia ya kupunguza mafuta tumboni, wanawake kwa wanaume walituma maswali kwa wingi. Njia iliyosalama ya kupunguza mafuta katika tumbo au kupunguza tumbo kubwa ni ile ya kupangilia chakula na kufanya mazoezi. 


Nilipata nafasi wiki hii ya kuzungumza na daktari mmoja katika hospitali ya mkoa wa Iringa ambaye sitamtaja kwa jina na alikuwa na mengi ya kuelezea jinsi hali hiyo inavyoanza na husababishwa ni nani. Alisema kuwa,kama unataka kupunguza tumbo kwa haraka basi punguza kula vyakula vyenye wanga na badala yake tumia mbogamboga na matunda kwa wingi. Vyakula kama viazi mviringo, wali mkate hukaa tumboni kwa zaidi ya siku tatu, pia ulaji wa nyama nyekundu inasababisha kuongezeka uzito na pia huongeza ukubwa wa tumbo,vyakulahivyo vinatakiwa kutumiwa kwa kiasi kidogo sana. "Kuna wakati tumbo linajitokeza na kuwa kubwa kuliko kawaida hali hiyo inasababishwa na kula vyakula vya wanga kwa wingi, kutokunywa maji ya kutosha na pia kula bila ya mpangilio maalum" anasema. Anasema kuwa kama ntu anataka kupunguza mafuta au kuondoa kitambi anatakuwa kula milo mitatu kwa siku na si kujinyima kula kwa kudhani kuwa unaweza kupungua uzito. "Vyakula vya wanga na mafuta ufanya mtu kunenepa, acha au kupunza kula vyakula vyenye wanga ili kupunguza mafuta yaliyozidi mwilini, mafuta yanaporundikana mwilini athari moja kubwa ni kuwa na tumbo kubwa." anasema. Anasema kuwa,tumbo kuwa kubwa ni dhahiri kuwa chakula unachokula hakifanyi kazi inayotakiwa, kumekuwa na ziada mwilini na hii ziada inafanyika mafuta ambayo hujiwekesha akiba katika maeneo mbalimbali ya mwili. "Kwa kuwa Chakula hiki cha ziada huwa hakitakiwi, mwili hukibadilisha na kuweka akiba katika mfumo wa mafuta kitaalamu kama glycogem.Unaweza kukabiliana na kuzidi kwa protini zinazoyeyushwa na kuwekwa katika akiba kwa mfumo huo wa mafuta" Daktari huyo anasema kuwa, mtu mwenye tatizo hilo ni bora akapangilia mlo wake kwa siku.


"Asubuhi pata kifungua kinywa kilichokamilika, pata mlo wa mchana kama kawaida na usiku kula matunda tu kunaweza kufanya mwili wako uwe katika hali inayotakiwa. "Watu wengi wanatumia wanga mwingi wakati wa usiku muda ambao unaenda kulala na ziada ya chakula haifanyi kazi vizuri zaidi ya kujikusanya, kujibadilisha na kuhifadhiwa katika maeneo mbalimbali ya mwili hasa tumboni" anasema Daktari. Je Mazoezi husaidia kupunguza uzito wa mwili na manyama uzembe? Mazoezi ya viungo yamethibitishwa kusaidia kuchoma mafuta ya ziada katika mwili. Kutokana na hali ya ulaji unaweza kutengeneza manyama uzembe katika kifua, mapaja na maeneo fulani ya tumbo ambayo yametengenezwa kupokea maeneo ya ziada yanayotokana na mafuta yenyewe au sukari iliyobadilishwa kuwa mafuta. Nishati inayotokana na nafaka ambayop haiwezi kutumika muda huo hutengenezwa kuwa mafuta na kupelekwa eneo husika. Wanaume huwa na asilimia 8 hadi 20 ya mafuta katika mwili na ni kawaida wakati kwa wanawake ni asilinia 13 hadi 25.


Unapofanya mazoezi ya viungo unaongeza hewa ya oksijeni kwa wingi katika mapafu yako na wakati huohuo mwili nao unaunguza mafuta ili kutoa nguvu kwa mwili. Mafuta yanayounguzwa kwanza ni yale ya kawaida kabla ya kuingia katika akiba. Kuna umuhimu wa kutambua kuwa mazoezi ni kitu cha bure na kama ukifanya kwa mpangilio na vizuri hutakuwa na shida ya kutengeneza shepu yako. Dk.Martica Heaner,M.A, M.Ed. ambaye hutoa mawaidha ya keep fit ndani ya MSN anasema ni jambo la heri kama mtu atakula kidogo kabla ya kuanza mazoezi ili kutoa nishati ya kutosha ya kufanyisha mazoezi. "Lakini kama unaenda mwendo fulani mdogo tu au unatembea kwa dakika 30 huenda usiwe na haja kabisa ya kula hata hicho kidogo na hasa ikiwa uliweka kitu kiogo saa tatu zilizopita" anasema.

Foleni za ulipaji kodi ya majengo zayeyuka Dar

$
0
0

Siku moja baada ya Mamlaka ya Mapato (TRA) kuongeza muda wa ulipaji kodi ya majengo, idadi ya watu wanaokwenda kuhakiki taarifa zao za kodi katika ofisi hizo imepungua.

TRA imeongeza muda wa ulipaji kodi juzi hadi Julai 15 badala ya Juni 30 kama ilivyokuwa awali.

Kupungua kwa watu katika ofisi hizo ni tofauti na juzi iliyokuwa siku ya mwisho, ambapo msongamano ulionekana katika ofisi za mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam.

Kutokana na hali ilivyokuwa katika ofisi mbalimbali jijini hapa kwa siku ya juzi, gazeti hili lilitembelea Temeke, Ilala na Kinondoni jana kuangali kama kungekuwa na msongamano au la. Hata hivyo, Mwananchi ilikuta ofisi hizo hazina idadi kubwa ya watu kama ilivyotegemewa licha ya TRA kufanya kazi hadi saa kumi jioni.

Mfanyakazi wa mamlaka hiyo eneo la Mbagala ambaye hakutaka jina lake litajwe kwa kuwa si msemaji alisema wanafanya kazi mpaka saa kumi jioni. “Hapa sisi tunatoa huduma mpaka jioni, Juni 29 na 30 tulikusanya fomu za watu 1,222 ambazo tunazifanyia kazi kwa leo kama hivi ulivyokuta,” alisema huku akionyesha boksi lililojaa fomu hizo.

Alisema kwa kuwa muda umeongezwa wanajitahidi kufanya kazi kwa kasi zaidi ingawa juzi mtandao ulikuwa chini.

Mkazi wa Mbagala aliyekuwa akisubiri kuingia katika ofisi hizo, Ally Mbwela alisema hakuwahi kulipa kodi hadi tarehe ya mwisho ilipotangazwa kuwa ni Juni 30 na baada ya kusikia muda umeongezwa amepata fursa ya kwenda kufanyiwa uhakiki.

Meneja wa TRA Mkoa wa Temeke, Gemalieli Mafie alisema wameongeza kituo eneo la Sabasaba ambapo wananchi wanaweza kufika kuhakiki taarifa zao na kupata fomu za malipo.

Pia, Mafie alisema wananchi wanaweza kupata taarifa za madai yao katika kituo hicho bila kujali walikojengea nyumba zao nchini.

Brazil: Mlanguzi maarufu wa madawa ya kulevya akamatwa

$
0
0

Polisi nchini Brazil wamamkamata mlanguzi wa madawa ya kulevya maarufu ambaye amefanyiwa upasuaji ili kukwepa kukamatwa kwa muda wa karibu miaka 30.

Luiz Carlos da Rocha ambaye pia anafahamika kama "White Head" anaamnika kuongoza genge kubwa la madawa ya kulevya barani America Kusini.

Polisi walisema kuwa hakuamu anayoweza kupewa Rocha inaweza kuwa ya karibu miaka 50 jela.
Rocha alikamatwa eno la Sorriso katika jimo la magharibu la Mato Grosson siku ya Jumamosi.

Amekuwa akiishi mjni humo akitumia jina Vitor Luiz de Moraes.

Polisi walilinganisha picha za zamani za Rocha na za mshukiwa ampya na kusema kuwa Luiz Carlos da Rocha na Vitor Luiz ni mtu mmoja.

Polisi wa Brazil wanasema kuwa genge lake lilitambuliwa kama lenye ghasia ambalo lilikuwa likitumia maghari yasiyopenya risasi na silaha nzito.

Genge hilo lilizalisha madawa ya Cocaine nchinin Bolivia, Peru na Colombia kabla ya kusafirisha madawa hayo hadi barani Ulaya na Marekani.
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live




Latest Images