Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104690 articles
Browse latest View live

SAKATA la Makinikia laizika Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA)

$
0
0
Bunge  limepitisha sheria mpya ambayo sasa itatambua haki na dhamana ya serikali katika makinikia ambayo itakuwa ni marufuku kuchenjuliwa nje ya nchi na serikali itashiriki kwa asilimia kuanzia 16 hadi 50 katika shughuli zote za uchimbaji, uchakataji na uchejuaji madini na ununuzi wa hisa katika kampuni ya uchimbaji madini.

Aidha, Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA) umefutwa rasmi na sasa kunaanzishwa Kamisheni ya Madini, na kwamba kuanzia sasa umiliki wa leseni mbalimbali zinazotolewa kwa mujibu wa Sheria ya Madini, hautahamishwa kabla haujafanyiwa uendelezaji katika kitalu husika.

Akielezea mapendekezo ya Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2017 katika Sheria ya Madini ya Mwaka 2010, Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi alisema asilimia hizo za hisa ni kwa kuangalia thamani ya gharama ambazo serikali inahamia katika vituo vya uwekezaji na kodi aliyopewa mwekezaji.

Profesa Kabudi alisema muswada huo pia unatambua haki na dhamana ya serikali juu ya makinikia na kuweka utaratibu wa kuyahifadhi sehemu maalumu migodini chini ya uangalizi wa serikali.

“Kupitia marekebisho hayo, makinikia yanayotolewa nchini bila kufanyiwa uchunguzi wa kupata thamani halisi kabla ya kuchenjuliwa na uchenjuaji utafanyika nchini. Kuanzia sasa makinikia hayatauzwa nje ya nchi, yatauzwa kwenda kwa wachenjuaji wa ndani ya nchi yakiwa ni bidhaa ambayo itatozwa kodi,” alifafanua.

Alisema pia muswada unaipa serikali haki na dhamana juu ya usimamizi wa bidhaa zote na maliasili, zinazotokana na uchimbaji, uchakataji na uchejuaji wa madini yakiwamo makinikia au kwa jina maarufu mchanga wa dhahabu.

Aidha, alisema muswada umelenga kutambua na kuweka chini ya uangalizi wa serikali maeneo yote ya uchimbaji na madini kwa lengo la kuweka ulinzi na usimamizi madhubuti wa madini kwa lengo la kuweka ulinzi na usimamizi madhubuti wa maeneo ya uchimbaji.

 “Hii itasaidia kuwepo ulinzimahsusi wa maeneo yote ya uchimbaji wa madini, kuwepo kwa utaratibu wa serikali kufanya ukaguzi na udhibiti wa usambazaji wa madini, kuipa serikali uwezo wa kudhibiti na kutambua viwango vya madini yote yanayotolewa kwenye maeneo ya migodi na kupitia vyombo vya ulinzi na usalama vya serikali,” alieleza.

TMAA yazikwa rasmi
Alieleza kuwa kufutwa kwa TMAA kunatokana na majukumu yake, yaliyokuwa yakitekelezwa na wakala huyo kuhamishiwa kwa Kamisheni ya Madini ambayo itaanzishwa.

Akiwasilisha muswada huo, Profesa Kabudi alisema kutokana na kufanyiwa mapitio ya madaraka ya Waziri na Kamishna wa Madini kwa lengo la kuwapunguza baadhi ya majukumu na madaraka yatahamishiwa kwa Kamisheni ya Madini.

Alisema kamisheni inayopendekezwa kuanzishwa itakuwa na jumla ya makamishina tisa, na watu kati yao akiwamo Mwenyekiti watakuwa wa kudumu.

“Watashirikiana na watendaji wakuu kutekeleza majukumu yao ya Kamisheni ya kila siku, makamishna wengine watakuwa wa muda na watakutana katika vikao maalumu vya kamisheni kwa ajili ya kufanya maamuzi ya misingi na kufuatilia utekelezaji wake,” alifafanua na kuongeza kuwa makamishina wa muda watateuliwa kutokana na nafasi zao ambao ni Katibu Mkuu Hazina, Katibu Mkuu Tamisemi, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Katibu Mkuu wa Ulinzi na Katibu Mkuu Ardhi.

“Kamisheni inayopendekezwa kuundwa itachukua majukumu sehemu kubwa ya majukumu ya Kamishna wa Madini kwa sasa. Majukumu hayo ni pamoja na kutoa, kuhuisha au pale itakapolazimika kufuta leseni zote zinazotolewa kwa mujibu wa sheria ya madini, kusimamia shughuli za madini ikiwa ni pamoja na kufanya ukaguzi maeneo ya migodi.

"Pia majukumu yote yaliyokuwa yakitekelezwa na TMAA yatahamishiwa na kuwekwa chini ya Kamishna. Na kwa msingi huu TMAA inafutwa,” alibainisha.

Umiliki wa leseni
Kuhusu kutohamisha leseni, alisema hatua hiyo ni katika kuzuia watu kufanya biashara ya udalali wa leseni.

“Katika kuweka masharti yanayokusudia kuzuia watu kufanya biashara ya udalali wa leseni mbalimbali zinazotolewa kwa mujibu wa sheria ya madini, mmiliki wa leseni hataruhusiwa kuhamisha umiliki wa leseni kabla ya uendelezaji katka kitalu husika,” alieleza.

Aliongeza, “baada ya kumalizika kwa muda wake, leseni itahuishwa kwa kipindi kimoja tu, na baada ya hapo umiliki wa kitalu husika utarejeshwa serikalini.”

WANAUME za Watu Wamepanda Bei Sana Siku Hizi.......

$
0
0
Waume za watu bwana siku hizi watamu kama wametiwa sukari ya dubai! Ukiwaonja hunasuki! Yaani kama sumu isivolambwa. Haramu lakini tamu! Na hii inatoakana na Mabachelor kuchushaaa! Sifa kuu za waume za watu wengi ni hizi (Yaani mambo yao kama universal vile! utazani kuna standardiztion ilifanyika)

1. Wanahonga Balaaaaaaa! Kwa wale wasitaarabu mtaita wanajali! Yaani wanajua kujikombaga mweeeeee! Wala huna shida ya kumkumbushia shida yako! Mwenyewe tu anakujali. Akiona huna usafiri atakujali hata kwa tax, pesa ni kiunganishi, kodi atatoa tu wala si mbishi. Ndo maana ma Miss Tz wengi wamefanya mapinduzi ama wamejiweka kwa waume za wenzao.

2. Wamepevuka kiakili na wanajua kumhandle mwanamke. After yrs of constant nagging and endless bettles na wifey lazima akili zimkae fresh. Yaani the wife did all the coaching, so ukimpa weye anajua what he better does or else......! Sio mabachelor manshindana kama mtu na mke mwenzie. Chezea kujikuta situation ya No Way Out all you can do is make up with the ubavu wa pili.

3. Mahusiano yanakua open na hamna drama drama za kipuuzi! Kila mtu anajua ule uhusiano ni special kwa kula bata, mikasi, na kumwagiana pesa! Baaaaaaaaaaaass! Drama za kujipima unapendwa hupendwi hazimo. Mambo ya kuchungulia simu na u spy na nini unamuachia Wifey. Mkikutana ni bata mtindo mmoja na kufanya maovu tu.

4. Adventureous yaani hujui mwisho utakuwaje? Kama ndo utachanwa na viwembe ama utamwagiwa tindi kali! On the bright side hujui kama utavuna mijumba mingapi na ndinga ngapi? Yaaani balaaaa!

5. Mwanaume anakuwa in constant devotion ya kukurizisha coz anajua akileta upuuz tupa kule, anajitumaje sasa! Sio kwa simu, sms, lunch, dates ili mradi kujirizisha yupo kwenye ratiba yako.


DISCLAIMER!

Huu sio msimamo wangu, Im just people! It is what it is and i said it as it is!

Argument za Wake za watu
Ni tabia mbaya Mungu hapendi, na ukimtendea mwenzio hivo nawe utatendewa. Anakutumia tu, he loves me the wifey.

Argument ya Wezi wa waume za watu
Utajiju bibi wee, mi sina mume nina kasoro gani? Tutabanana hapo hapo. Kwanza sina uhakika kama nitaolewa. Hanitumii tunatumiana, kwani anaondoka nayo? Na hizi pesa anazonihonga kwa raha zangu! Angekuwa anakupenda kweli asingekuja kwangu! FYI ndo pia inavunjika vile vile kutangulia sio kufika.

MI SIMOOOOOOOOOOOO!!!!!!!!!!!!!!! !!!!!!!!!

Haya mvua ya mawe ianze!!!!!!!!!!!!!

ACACIA yatafuta Nafuu Marekani, Yatangaza Kufungua Kesi

$
0
0
Baada ya Serikali ya Tanzania kuweka zuio la kutosafirisha Makinikia Kampuni  ya Acacia, jana ilitangaza kufungua 'kesi' ya kuomba upatanishi wa mgogoro unaoendelea baina yake na serikali.

Taarifa iliyotolewa jana na Acacia ilisema kampuni hiyo imewasilisha taarifa hiyo ya kutafuta upatanishi kwa niaba ya kampuni zake tanzu za Bulyanhulu Gold Mine Limited (BGML) na Pangea Minerals Limited (PML), inayomiliki mgodi wa Buzwagi.

Kampuni hiyo ya Uingereza inamiliki pia mgodi wa dhahabu wa North Mara, lakini ni miwili hiyo ambayo mali yake huhusisha uchenjuaji wa makinikia.

Migogoro ya kimataifa ya kiuwekezaji hutatuliwa na ama Kituo cha Kimataifa cha Utatuzi wa Migogoro ya Uwekezaji (ICSID) au Chemba ya Kimataifa ya Biashara (ICC).

Ingawa taarifa ya Acacia haikueleza imefungua wapi ombi lake la kutaka upatanishi wa mgogoro wa makinikia, chanzo cha kuaminika kiliiambia pande hizo mbili zitaketishwa pamoja ICSID yenye makao yake makuu Washington DC, Marekani.

"Taarifa za kusudio hili zinahusu mgogoro wa sasa kati ya Serikali ya Tanzania na kila moja kati ya BGML na PML kusuluhishwa," ilisema Acacia katika taarifa yake iliyowekwa kwenye tovuti yake na kuongeza:

"Hii ni kuendana na mchakato wa utatuzi wa migogoro uliokubaliwa na Serikali ya Tanzania katika Makubaliano ya Uendelezaji Madini na BGML and PML.

"Uwasilishaji wa taarifa ya kutafuta upatanishi kwa wakati huu ni muhimu kwa ajili ya kuilinda kampuni. Pamoja na hatua hii, Acacia bado ina mtazamo kuwa mazungumzo nje ya vyombo rasmi ndiyo njia bora ya utatuzi wa migogoro iliyopo na kampuni itaendelea kufanya jitihada kufanikisha hili."

Acacia ilisema serikali pia imeiarifu Barrick, kampuni yake mama, kuwa kwa sasa ingependa kuendelea na mazungumzo yao, hivyo, "Acacia haitashiriki moja kwa moja kwenye mazungumzo hayo yatakapoanza."

"Suluhusho lolote litakaloweza kubainishwa kutokana na mazungumzo hayo litalazimika kupitishwa na Acacia, na kampuni itashirikiana na Barrick kwa hali na mali kusapoti mazungumzo hayo.

KULIPA FEDHA
Juni 14, Mwenyekiti wa Barrick Gold Corporation ya Canada ambayo ni mmiliki mkubwa wa Acacia, Prof. John Thornton alifanya mazungumzo na Rais John Magufuli na kukubali kulipa fedha ambazo Tanzania imezipoteza kutokana na udanganyifu ambao umegundulika kwenye biashara ya makinikia nchini.

Mazungumzo hayo yalifanyika ikiwa zimepita siku tatu tangu Rais akabidhiwe ripoti ya kamati maalum ya pili iliyochunguza masuala ya sheria na kiuchumi kuhusiana na mchanga wa madini unaosafirishwa nje ya nchi.

Ripoti iliyowasilishwa na mwenyekiti Prof. Nehemia Osoro, ilisema nchi inaweza kuwa imepoteza mpaka Sh. trilioni 489 katika kodi na mali (madini) kwa miaka 19 iliyopita kwenye biashara hiyo ya madini inayofanywa na Acacia.
Kati ya fedha hizo, kiwango cha kodi kilitajwa kuwa Sh. trilioni 108.

Taarifa ya Ikulu ilisema baada ya mazungumzo hayo, Prof. Thornton alisema kuwa kampuni yake ipo tayari kufanya mazungumzo yatakayozingatia maslahi ya pande zote mbili na kwamba ipo tayari kulipa fedha zote ambazo inapaswa kulipa kwa Tanzania.

Acacia imejikuta katika wakati mgumu baada ya kamati ya kwanza iliyoteuliwa na Rais Magufuli Machi 29, ikiwa na wajumbe nane wenye taaluma za jiolojia, kemia, uhandisi kemikali na uhandisi uchenjuaji madini, kuchunguza kiwango cha madini kwenye makontena yenye makinikia kuonyesha kuwapo kwa udanganyifu.

Acacia ndiyo msafirishaji mkuu wa makinikia nchini.

Kamati hiyo maalumu ilikuwa chini ya uenyekiti wa Profesa wa masuala ya miamba, Abdulkarim Mruma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Baada ya kamati ya kwanza kumkabidhi ripoti ya uchunguzi Mei 24, Rais Magufuli alichukua uamuzi wa kusitisha upelekaji mchanga nje ya nchi mpaka itakapoelezwa vinginevyo baadaye.

Na baada ya Kamati ya pili ya Rais kuchunguza masuala ya kisheria na kiuchumi kuhusiana na makinikia yanayosafirishwa nje ya nchi tangu mwaka 1998 kugundua Acacia haijasajiliwa kwa mujibu wa sheria, Rais Magufuli alisitisha moja kwa moja usafirishaji huo.

Akizungumzia Acacia kukosa usajili, Rais Magufuli aliwashangaa viongozi walioiacha ifanye bishara za ma-trilioni ya shilingi.
"Tujiulize sisi viongozi ni mara ngapi Watanzania wenzetu wasiposajiliwa tunawashughulikia kwa mitutu ya bunduki?" Aliuliza Rais kwa masikitiko.

"Mmachinga akienda bila kusajiliwa anafukuzwa kwenye maeneo yao, mara ngapi wafanyabiashara wadogowadogo wasio na leseni wanashughulikiwa?

"Huyu tumemuacha tangu mwaka 1998 hadi sasa.

"Tuna wanasheria wengi na wengine wanatisha utashtakiwa. Mali ni yangu, nimeamua kuiangalia mwenyewe halafu unishtaki uendelee kuchimba? Kukulinda nakulinda mimi, napeleka polisi wanalinda migodi yote, halafu unishtaki na uendelee kuchimba?

"Kwa kisingizio kwamba umetengeneza ajira, nikiruhusu watu si nitatengeneza ajira mamilioni? Tatizo litakuwa wangapi watakufa wakigombea dhahabu.

"Tumechezewa vya kutosha, haiwezekani tukawa sisi ndiyo wa kuibiwa tu."

Serikali ya CCM na Kutumia Nguvu na Vitisho vya Polisi.....

$
0
0
Ukiona Baba akiulizwa swali anakuwa mkali ujue hana jibu,
Hajui akujibu nini,
Hajui anakifanya kitamfukisha wapi,
Amepoteza mwelekeo anatafuta pa kutokea.
CCM sasa hivi Polisi ndio kimbilio lao,

Mwananchi akihoji kitu Jela,
Mwaandishi wa Habari akiandika kitu kuhusu Serikali Jela,
Vyama vya Siasa haviruhusiwi kufanya Siasa, Vikifanya Jela,
Na tena hii ni mbaya maana CCM wao kila siku wanafanya mikutano ya Kisiasa kupia Raisi, wakuu wa mikoa, Wakuu wa Wilaya, kiujumla CCM inafanya Siasa peke yake

Ukiishiwa Sera ndio nguvu hutumika...


Maoni ya Mahweso/JF

NB: Wahenga Walisema "Mwanamke Hapigwi, Bali Hupigwa na Kanga....na  Ukiona Mwanamume anampiga Mke wake jua Kaishiwa na Sera"


VIDEO: Mbunge Musukuma kuhusu wanaoikosoa Serikali

$
0
0
Wabunge waliosimama Bungeni Dodoma ili kuchangia muswada wa merekebisho ya sheria za maliasili na utalii ni pamoja na Mbunge wa Geita Joseph Musukuma ambaye kati ya vitu alivyozungumzia zaidi ni kuhusu watu wanaomkosoa Rais Magufuli na serikali yake… VIDEO:

MAMENEJA Sallam SK, Babu Tale, Mkubwa Fella, Wamesusa Wasanii wao Wanabanana WCB Kwa Diamond

$
0
0
MAMENEJA Sallam SK, Babu Tale, Mkubwa Fella, Wamesusa Wasanii wao Wanabanana WCB Kwa Diamond
Nakumbuka babu tale ndie mwanzilishi na meneja wa tip top connection kina madee, keisha, tunda, dogo janja etc... naona amekimbia lebo yake anabanana WCB.

sallam nakumbuka ni meneja wa AY naona kamkimbia anabanana na WCB.

Mkubwa fella nakumbuka ni meneja wa Yamoto band, kina temba, chege etc naona nae amekimbia lebo yake anabanana WCB.

WCB patamu kuna safari za ulaya nyingi na Diamond ana hela ndefu wanyonyaji wote wameamua wakomae nae..

Ofisi ya WCB kila kitu ni gharama za Diamond.

recruitment ya wasanii WCB ni diamond yaani diamond akisema chochote mameneja wanasema Yess boss

Sio majungu wadau ni maoni tu..

kama hawa mameneja ni wazuri wanaupenda mziki wetu why wasiwamanage wasanii wao nao wawe kama diamond..

madee anapigia video posta barabarani siku ya jumapili maskini kuepuka msongamano.. meneja kakimbilia nyumba ndogo WCB.

Sallam, Babu tale na fella msikimbie nyumba zenu wasaniii wenu wanawahitaji muwakomboeeee...

Diamond ana familia inamtegemea sio kisa ameshatusua mkomae nae,,,, msimnyonyeeee sana

KWELI, Inahitaji Uume Mkubwa Kumridhisha Mwanamke?

$
0
0

Nimetana na jamaa angu mmoja analala mika ana uume mdogo sana kwa ukisimaa ni inch 4 wakati ye kikawaida anajua inabid uwe inch6 so jamaa anahisi anaweza achwa na mke wake ......swali does the size of P*nis matter?

UKISIKIA Kutakatisha Fedha na Kuhujumu Uchumi, Hii Ndio Maana yake

$
0
0
Tumekuwa tukisikia watu wanafungwa kwa kutakatisha fedha, wengine kuhujumu uchumi, sasa leo tumempata mtaalamu kutoka Bank Kuu ya Tanzania (BoT), Meneja Msaidizi Idara ya Uendeshaji kesi na uchunguzi Ganga Mlipano kwenye huu ufafanuzi.

“Nchi yoyote inatakiwa kuwa na uchumi imara vitendo vyovyote vinavyofanya uchumi usiwe imara ni vitendo vinavyofanya uchumi uhujumiwe ndio maana Serikali yetu ilitunga sheria ya uhujumu uchumi mwaka 1984.

“Vitendo vyote vinavyofanywa ambavyo vimeelezewa kwenye hiyo sheria vinavyopelekea kuhujumu uchumi vinaitwa vitendo vya kuhujumu uchumi na mtu yeyote akifanya hivyo vitendo anapelekwa Mahakamani na kushtakiwa.

“Ili uchumi uendelee lazima kuwe na mtiririko wa fedha, mtu anapochukua fedha akaweka nyumbani au akachukua bidhaa nyingi za kiasi kikubwa akazihifadhi nyumbani na wananchi wakakosa maana yake kutatokea mfumuko wa bei. Vitendo kama hivyo ndio hupelekea uchumi uyumbe.

“Vitendo vinavyopelekea masuala haya ndio vinaitwa vitendo vya kuhujumu uchumi. Na hukusu kutakatisha fedha…fedha kwa kawaida inatakiwa kutumika kama ilivyopangwa. Mtu anaweza kupata fedha kwa njia sio ya halali na akaitakatisha…” – Ganga Mlipano. 
VIDEO:

MSIWALAUMU Kina Zari Hassan, Jack Wolper, Wema Sepetu na Shilole...Kuhusu Dogo Dogo

$
0
0
Wengi husema na kulaumu kuwa eti hawa wanawake hutembea na wanaume wadogo mfano

  • Zarina na daimond
  • Wolper-harmonize
  • Wema-idris
  • Shilole-nuhu

Hawa wamewazidi wapenzi wao miaka mingi mfano zari anamzidi daimond kama miaka 10 au zaidi
Nilichogundua ni hivi sio wao tu kina zari hata kina mama wakubwa hupenda vitoto kwa sababu eti vinajua sana mapenzi yaan havina utani katika swala la ngono tunasugua haswa na kuhakikisha kila angle ya mwili imelegea halaf havichokii,,,tofauti na hawa wakubwa kimoja tu hoi na wanasingizia eti ooh haya mambo tushayazoea wakati kumbe nguvu zishaisha...
Kiukweli hivi vitoto vinapanda mlima haswaa 25 kushuka chin mpaka 18 ni balaa ati,so tusiwalaumu ni utamu tu

By Stargirl

GIGY Money Afunguka Kutoa Mimba Mbili

$
0
0
MUUZA sura kwenye video za wasanii Bongo, ambaye mwili wake ‘umepukutika’ ghafla, Gift Stanford maarufu kama Gigy Money, amekiri kutoa mimba mbili mfululizo ambazo ndizo zilizosababisha hali hiyo.

Akizoza na Za Motomoto News, muuza nyago huyo ambaye awali alionekana kuwa na kalio lililotesa mioyo ya wakware wengi, alisema kitendo cha kutoa mimba hizo kilimfanya kuwa taaban na chupuchupu akumbwe na mauti.

“Roho inaniuma sipendi kuongea haya, lakini ni kweli nilinasa ujauzito mara mbili mfululizo, kutokana na vipigo vya mwanaume niliyekuwa naye,… (anamtaja jina) mimba zikawa zinatoka, ya mwisho hadi kizazi kilitoka nje nikaumwa sana hadi nilijua nakufa nikalazwa hospitali siku mbili,” alisema msanii huyo.

YUSUPH Manji Afumwa na Jora 43 za Nguo za Jeshi na Mihuru 39

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam  linamshikilia Mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuf Manji kwa mahojiano baada ya kukutwa na jora 43 za sare za Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) pamoja na mihuri 39 ya kampuni tofauti tofauti.


Akithibitisha taarifa hizo Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam, Kamanda Lucas Mkondya amesema Manji anashikiliwa na jeshi hilo tangu Julai mosi baada ya kukutwa na vitu hivyo katika ghala lake la Quality Motors, lililopo Chang’ombe jijini Dar es Salaam.

“Ni kweli tunamshikilia tangu Jumamosi tunaendelea kumhoji kwa vitu alivyokutwa navyo ili atuambie alivipataje na anavyo kwa madhumuni gani wakati yeye sio mwanajeshi na amekaa navyo kwake,” amesema Kamanda Mkondya.

Akizungumzia endapo Manji atafikishwa mahakamani baada ya mahojiano, Kaimu Kamanda Mkondya amesema baada ya kukamilisha mahojiano na kupata taarifa kamili, wataangalia kama atapelekwa mahakamani kutokana na majibu yake.

“Tunasubiri tumalize mahojiano tupate na maelezo yake ili tuone yamekwendaje na kama atafikishwa mahakamani kulingana na mahojiano yatakavyokwenda,” amesema Kamanda Mkondya.

Hii sio mara ya kwanza kwa Manji kushikiliwa na Jeshi la polisi kwa mahojiano kwani mwezi Februari mwaka huu, alishikiliwa kwa mahojiano baada ya kudaiwa kujihusisha na matumizi ya madawa ya kulevya.

Chanzo:HabariLeo

MARUFUKU Siasa za Matusi na Uchochezi Kinondoni – DC Ally Hapi

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi amewapiga marufuku Wanasiasa kutoa lugha za matusi na uchochezi kwenye wilaya yake huku akiwataka wachunge vinywa vyao wakati wanaongea .

Tokeo la picha la DC kinondoni ally hapi
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mh. Ally Hapi

DC Hapi amesema kila mwanasiasa anayetaka kufanya siasa kwenye wilaya yake ni lazima achunge mdomo wake kabla ya kuongea.

“Ni marufuku siasa za matusi na uchochezi katika wilaya ya Kinondoni.Kila anayetaka kufanya siasa Kinondoni na achunge kinywa chake,”ameandika DC Ali Hapi kwenye ukurasa wake wa Twitter.

Jana DC ally Hapi alitoa tamko la kukamatwa kwa Mbunge wa jimbo la Kawe Mh. Halima Mdee kwa kile alichodai kuwa kwenye moja ya mikutano yake aliyoifanya kwenye wilaya yake alitoa kauli za kichochezi na kejeli kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh Dkt John Pombe Magufuli.

VIDEO: Kauli ya Serikali kuhusu Watanzania 21 waliotekwa DR Congo

$
0
0
Serikali kupitia Wizara yake ya Mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika mashariki imethibitisha Waasi na kikundi cha waasi cha Mai-Mai nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) wamewateka madereva 24, wakiwamo Watanzania 21 wanaofanya kazi kwenye kampuni ya malori ya mizigo ya Alistair ya nchini. VIDEO:

NAIBU Spika Tulia Ackson Aanza Kukubali Hoja za Wapinzani.....

$
0
0
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson.

Naibu spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt.  Tulia Ackson  amefunguka na kusema wabunge wa upinzani muda mwingine huwa wanaleta hoja nzuri kwa serikali lakini serikali inashindwa kuzipokea hoja hizo kutokana na uwasilishaji wao.

Naibu Spika amesema hayo leo Dodoma wakati akifanyiwa mahojiano katika kipindi cha bunge, ambapo alikuwa akitoa mtazamo wake juu ya bajeti kuu ya serikali kwa mwaka 2017/2018
"Wabunge wa upinzani muda mwingine wanaleta hoja nzuri sana bungeni lakini tatizo kubwa linakuja katika lugha inayotumika inakuwa si lugha ya staha ndiyo maana unaona hata serikali inakuwa haikubali. Bunge ni jumba la kisiasa, hivyo kila mwamba ngoma huvutia kwake, upande wa chama kinachoongoza ndiyo chenye serikali wana namna yao ya kuishauri serikali, ila wale ambao wanataka kuingia madarakani nao wana namna yao ya uchangiaji bungeni ndiyo maana kuna kuwa na mvutano wa hapa na pale" alisema  Tulia Ackson

Mbali na hilo Naibu Spika alidai serikali muda mwingine imekuwa inashindwa kufanyia kazi kwa haraka baadhi ya ushauri wa wabunge utolewao bungeni kutokana na ukweli kwamba serikali kabla ya kuleta jambo bungeni huwa inakuwa imefanya utafiti wa kutosha, hivyo linapoibuka jambo jipya inakuwa changamoto, inabidi ilichukue na kuja kulifanyia kazi siku za mbeleni.

Kuhusu upendeleo bungeni Naibu Spika amesema wabunge wote wale wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wapinzani wamekuwa wakipewa nafasi sawa lakini wabunge wa upinzani wamekuwa wakilalamika kutokana na kuwa na dhana ya kuonewa.

"Bunge hili limekuwa na wabunge zaidi ya 300 na walio wengi zaidi ni wabunge kutoka chama tawala, hivyo wale wa upinzani kwa kuwa wapo wachache hivyo wanaweza kuona kama wanaonewa hivi, wanaweza kuona kama hawasikilizwi, wanaona kama hawapewi muda zaidi, lakini unakuta mtu ukiwa kwenye kile kiti unawaza hili na kufanya utende kwa usawa tena kwa kuwasaidia walio wachache ili dhana hiyo isiwepo" alisisitiza Tulia Ackson

Kwa kumalizia  Tulia Ackson  aligusia jambo la mbunge kulishtaki bunge mahakamani na kusema kuwa hakuna mbunge anaweza kulishtaki bunge kama taasisi

"Bunge kama taasisi likifanya jambo huwezi kulipeleka mahakamani, bunge likiwa limefanya maamuzi juu ya jambo fulani na ukaona bunge halijafanya sawa kuna utaratibu wa kibunge lakini huwezi kuchukua maamuzi ya bunge ukapeleka mahakamani, kwa hiyo kuna utaratibu wake, lakini uamuzi wa bunge huwezi kuupeleka mahakamani kikanuni" alimalizia  Tulia Ackson

JAY-Z athibitisha mamake ni mpenzi wa jinsia moja

$
0
0
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson.

Naibu spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt.  Tulia Ackson  amefunguka na kusema wabunge wa upinzani muda mwingine huwa wanaleta hoja nzuri kwa serikali lakini serikali inashindwa kuzipokea hoja hizo kutokana na uwasilishaji wao.

Naibu Spika amesema hayo leo Dodoma wakati akifanyiwa mahojiano katika kipindi cha bunge, ambapo alikuwa akitoa mtazamo wake juu ya bajeti kuu ya serikali kwa mwaka 2017/2018
"Wabunge wa upinzani muda mwingine wanaleta hoja nzuri sana bungeni lakini tatizo kubwa linakuja katika lugha inayotumika inakuwa si lugha ya staha ndiyo maana unaona hata serikali inakuwa haikubali. Bunge ni jumba la kisiasa, hivyo kila mwamba ngoma huvutia kwake, upande wa chama kinachoongoza ndiyo chenye serikali wana namna yao ya kuishauri serikali, ila wale ambao wanataka kuingia madarakani nao wana namna yao ya uchangiaji bungeni ndiyo maana kuna kuwa na mvutano wa hapa na pale" alisema  Tulia Ackson

Mbali na hilo Naibu Spika alidai serikali muda mwingine imekuwa inashindwa kufanyia kazi kwa haraka baadhi ya ushauri wa wabunge utolewao bungeni kutokana na ukweli kwamba serikali kabla ya kuleta jambo bungeni huwa inakuwa imefanya utafiti wa kutosha, hivyo linapoibuka jambo jipya inakuwa changamoto, inabidi ilichukue na kuja kulifanyia kazi siku za mbeleni.

Kuhusu upendeleo bungeni Naibu Spika amesema wabunge wote wale wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wapinzani wamekuwa wakipewa nafasi sawa lakini wabunge wa upinzani wamekuwa wakilalamika kutokana na kuwa na dhana ya kuonewa.

"Bunge hili limekuwa na wabunge zaidi ya 300 na walio wengi zaidi ni wabunge kutoka chama tawala, hivyo wale wa upinzani kwa kuwa wapo wachache hivyo wanaweza kuona kama wanaonewa hivi, wanaweza kuona kama hawasikilizwi, wanaona kama hawapewi muda zaidi, lakini unakuta mtu ukiwa kwenye kile kiti unawaza hili na kufanya utende kwa usawa tena kwa kuwasaidia walio wachache ili dhana hiyo isiwepo" alisisitiza Tulia Ackson

Kwa kumalizia  Tulia Ackson  aligusia jambo la mbunge kulishtaki bunge mahakamani na kusema kuwa hakuna mbunge anaweza kulishtaki bunge kama taasisi

"Bunge kama taasisi likifanya jambo huwezi kulipeleka mahakamani, bunge likiwa limefanya maamuzi juu ya jambo fulani na ukaona bunge halijafanya sawa kuna utaratibu wa kibunge lakini huwezi kuchukua maamuzi ya bunge ukapeleka mahakamani, kwa hiyo kuna utaratibu wake, lakini uamuzi wa bunge huwezi kuupeleka mahakamani kikanuni" alimalizia  Tulia Ackson

JAY-Z athibitisha mamake ni mpenzi wa jinsia moja

$
0
0
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson.

Naibu spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt.  Tulia Ackson  amefunguka na kusema wabunge wa upinzani muda mwingine huwa wanaleta hoja nzuri kwa serikali lakini serikali inashindwa kuzipokea hoja hizo kutokana na uwasilishaji wao.

Naibu Spika amesema hayo leo Dodoma wakati akifanyiwa mahojiano katika kipindi cha bunge, ambapo alikuwa akitoa mtazamo wake juu ya bajeti kuu ya serikali kwa mwaka 2017/2018
"Wabunge wa upinzani muda mwingine wanaleta hoja nzuri sana bungeni lakini tatizo kubwa linakuja katika lugha inayotumika inakuwa si lugha ya staha ndiyo maana unaona hata serikali inakuwa haikubali. Bunge ni jumba la kisiasa, hivyo kila mwamba ngoma huvutia kwake, upande wa chama kinachoongoza ndiyo chenye serikali wana namna yao ya kuishauri serikali, ila wale ambao wanataka kuingia madarakani nao wana namna yao ya uchangiaji bungeni ndiyo maana kuna kuwa na mvutano wa hapa na pale" alisema  Tulia Ackson

Mbali na hilo Naibu Spika alidai serikali muda mwingine imekuwa inashindwa kufanyia kazi kwa haraka baadhi ya ushauri wa wabunge utolewao bungeni kutokana na ukweli kwamba serikali kabla ya kuleta jambo bungeni huwa inakuwa imefanya utafiti wa kutosha, hivyo linapoibuka jambo jipya inakuwa changamoto, inabidi ilichukue na kuja kulifanyia kazi siku za mbeleni.

Kuhusu upendeleo bungeni Naibu Spika amesema wabunge wote wale wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wapinzani wamekuwa wakipewa nafasi sawa lakini wabunge wa upinzani wamekuwa wakilalamika kutokana na kuwa na dhana ya kuonewa.

"Bunge hili limekuwa na wabunge zaidi ya 300 na walio wengi zaidi ni wabunge kutoka chama tawala, hivyo wale wa upinzani kwa kuwa wapo wachache hivyo wanaweza kuona kama wanaonewa hivi, wanaweza kuona kama hawasikilizwi, wanaona kama hawapewi muda zaidi, lakini unakuta mtu ukiwa kwenye kile kiti unawaza hili na kufanya utende kwa usawa tena kwa kuwasaidia walio wachache ili dhana hiyo isiwepo" alisisitiza Tulia Ackson

Kwa kumalizia  Tulia Ackson  aligusia jambo la mbunge kulishtaki bunge mahakamani na kusema kuwa hakuna mbunge anaweza kulishtaki bunge kama taasisi

"Bunge kama taasisi likifanya jambo huwezi kulipeleka mahakamani, bunge likiwa limefanya maamuzi juu ya jambo fulani na ukaona bunge halijafanya sawa kuna utaratibu wa kibunge lakini huwezi kuchukua maamuzi ya bunge ukapeleka mahakamani, kwa hiyo kuna utaratibu wake, lakini uamuzi wa bunge huwezi kuupeleka mahakamani kikanuni" alimalizia  Tulia Ackson

MASKINI:Haya hapa Mashtaka Aliyosomewa Yusuf Manji Kitandani Muhimbili Alipolazwa

$
0
0

SERIKALI imemsomea Mashtaka saba Mwenyekiti wa Quality Group Yusuf Manji na wenzake watatu yakiwamo ya Uhujumu uchumi na usalama wa nchi

Kesi walisomewa Kwenye Hospitali ya Muhimbili Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete alipolazwa Mtuhumiwa namba moja Yusuph Manji Mbele ya Hakimu Mkazib wa mahakama ya Kisutu Huruma Shahidi Wakili wa Serikali Kishenyi Mitalemwa aliwaomea washtakiwa mashataka yao.

Watuhumiwa wengine ni Pamoja na Abdala Sangey,  Deogratias Kisimba, na Tobias Fwele

Shtka la Kwanza Tarehe 30 Juni 2017 eneo la Changombe  Temeke Jijini Dar es Salaam walikutwa na Askari Polisi  wakiwa na mabunda 35 ya vitambaa yanayotumika kutengenea Sare  za Polisi zenye Thamani ya Milioni 192.5

Shitka la Pili watuhumiwa wote Tarehe 30 Juni walikutwa na Mabando Manane ya vitaambaa zinazotumika kutengeneza JWTZ

Kosa la Tatu  watuhumiwa walikuwa kukutwa na mihuri ya serikali washtakiwa wote  kwa pamoja tarehe 1 July  walikutwa na mihuri ya jeshi la Tanzania iliyoandikwa  "Mkuu wa Kikosi 121 Kikosi cha jeshi JWTZ "bila kuwa na uhalali kitendo kinachohatatisha usalama wa nchi

Kosa Nne watuhumiwa walikutwa na Mhuri wa Serikali walikutwa na muhuri wa JWTZ  yenye maandishi  Kamanda kikosi 834 KJ makutupola Dodoma bila kuwa na uhalali kitendo


Shtka la tano kukutwa na Mhuri wa Serikali wenye maneno "COMMANDING Oficcer 835 kj Mgambo P.O.BOX..."

Shtaka la sita kukutwa na mali inayozaniwa kupatikana isivyo halali Tarehe 1 Julai Changombe Plat namba SU 383 ambayo ilipatakan isivyo halali.



wahtakiwa Hawakuruhusiwa kujibu mashtaka hayo kwa sababu wanastakiwa kwa sheria ya Uhujumu Uchumi na usalama wa taifa.

Hakimu Shahidi amesma  Kwamba masuala hayo yasikilizwe kwenye Mahakama yenye mamlaka.
kesi hiyo itatajwa tena Tarehe 19 mwezi Julai  upelelezi wa Kesi haujakamilika.  



                 

MBUNGE Waitara Ahojiwa Dodoma Kwa Futari Aliyoiandaa Dar

$
0
0

Dodoma. Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara amehojiwa na ofisa wa polisi katika viwanja vya Bunge kwa kile alichokieleza ni kutokana na futari aliyoiandaa jimboni kwake.

Mwita amesema mahojiano hayo yanatokana na futari ambayo alimwalika Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa, ambaye alitoa maneno yanayodaiwa  yalionyesha kuikera Serikali.

"Amejitambulisha kwangu kuwa ni polisi, lakini jana (Julai 4) pia nilipigiwa simu na ofisa upelelezi Mkoa wa Dodoma akinitaka niende kwa mahojiano," amesema Waitara.

Mahojiano kati ya Waitara na ofisa huyo yamefanyika eneo la mapokezi katika jengo la utawala la Bunge muda mchache baada ya mkutano wa saba wa Bunge kuahirishwa leo (Julai 5).

FAHAMU Wanawake Wenye Hips na Shida Wanazokabiliana Nazo Kila Siku!

$
0
0

Wanawake wengi wenye hips , ni wanawake ambao si kwa mwanaume tu hata kwa wanawake wenzie husifia kuwa fulani kajaliwa, ki maumbile, ni kweli wana mvuto wapekee, humwagiwa sifa nyingi za urembo, lakini pia kwa upande mwingine wa shillingi nimatatizo tupu.

Sifa:

1. Huwatesa sana wakina baba wanapokuwa katika vyombo vya usafiri kama daladala, treni, meli na ngalawa, mababa wengi hujawa na hisia kali za mahaba kiasi kwamba hupata mfadhaiko.

2. Hawana haraka sana kwani mwendo wao, hutembea kwa maringo, hata daladala likisimamia mbali hawawezi kukimbia kuwahi.

3. Hutongozwa wanaume watano kwa siku, hata wanaume wasiposema kitu angalau ukonyeza.

4. Ni wasikivu sana wakati wa kudatemaana wengi ni warefu hupenda sana kukuinamia kusikia zaidi uliongealo.

Matatizo.

5. Kwa kuwa huwa wanavutia sana nirahisi kurubuniwa kwani mwanamke yeye duniani hawezi kutongozwa watu elfu 2000 asimpendemmojawapo.

6. Hawana raha kwani ukodolewa sana machona watu, si wanawake wala wanaume.

7. Upata magonjwa sana asa fungus kwani sehemu zao za siri hazipati hewa ya kutosha kufatana na kubanana kwa nyama na msuguano kila watembeapo.

8. Wana gharama sana kuwatunza kwa sababu hawatakiwi kutembea kwa muda mrefu kuogopa msuguanahivyo umuoapo ni lazima ughalimike usafiri au unatakiwa kumunulia skin taiti kila mara kwa kuwa zinahariibikamuda mfupi sehemu ya mapaja.

TAIFA Stars Yafa Kiume Mbele ya Chipolopolo......

$
0
0
TANZANIA itawania nafasi ya tatu katika Kombe la COSAFA Castle baada ya leo kufungwa mabao 4-2 na Zambia katika mchezo wa Nusu Fainali Uwanja wa Uwanja wa Moruleng mjini Rusternburg, Afrika Kusini.

Zambia inatangulia fainali na Julai 9 itamenyana na mshindi kati ya Lesotho na Zimbabwe zinazomenyana kuanzia Saa 2:00 usiku wa leo.

Mkongwe Erasto Nyoni alianza kuifungia Taifa Stars kwa shuti zuri la mpira wa adhabu dakika ya 14 na bao hilo lilikaribia kudumu hadi kipindi cha pili, kama si Zambia kupata mabao mawili ya haraka haraka mwishoni mwa kipindi hicho.

Brian Mwila alianza kuifungia Chipolopolo bao la kusawazisha dakika yaa 44, kabla ya Justin Shonga kufunga la pili dakika ya 45 na Zambia ikaenda kupumzika inaongoza 2-1.

Jackson Chirwa akaifungia Zambia bao la tatu kwa mkwaju wa penalti dakika ya 55, baada ya mpira kumgonga mkononi kwa nyuma beki wa kushoto, Gardiel Michael na la nne dakika 67 kwa shuti la mpira wa adhabu.

Simon Msuva akaipunguzia macungu Tanzania kwa kufunga bao la pili dakika ya 84 akimalizia mpira uliorudi baada yaa krosi ya Gardiel Michael.  Taifa Stars wakaongeza kasi ya mashambulizi baada ya bao hilo, lakini bahati mbaya ‘muda haukuruhusu’.

Taifa Stars inapoteza mechi ya kwanza chini ya kocha Salum Mayanga aliyeanza kazi Machi mwaka huu akimpokea Charles Boniface Mkwasa, baada ya kucheza mechi saba bila kupoteza, ikishinda tatu na kutoa sare nne.

Zambia leo imeifunga Tanzania kwa mara ya 17 katika mechi 31 walizokutana, wakifungwa tano  na sare tisa.

Tanzania ilianzia hatua ya mchujo kwenye Kundi A ambako iliongoza kwa pointi zake tano sawa na Angola baada ya sare mbili 0-0 na Angola, 1-1 na Mauritius na ushindi wa 2-0 dhidi ya Malawi, hivyo kutengeneza wastani mzuri wa mabao na kuwapiku wapinzani kusonga Nusu Fainali.

Zambia yenyewe ilianzia moja kwa moja hatua ya Robo Fainali sawa na Afrika Kusini, Botswana,
Namibia, Lesotho na Swaziland huku Zimbabwe ikiongoza Kundi B. Lesotho na Zimbabwe zitamenyana katika Nusu Fainali ya pili Saa 2:00 usiku.

Kikosi cha Tanzania kilikuwa; Aishi Manula, Shomary Kapombe, Gardiel Michael, Abdi Banda/Nurdin Chona dk69, Salim Mbonde, Himid Mao, Erasto Nyoni/Raphael Daudi dk45, Muamil Yassin, Elias Maguri/Thomas Ulimwengu dk80, Simon Msuva na Shiza Kichuya.

Zambia; Alan Chibwe, Lawrence Chungu, Adrian Chama, Diamond Chikwekwe/Lubinda Mundia dk61, Justin Shonga/Godfrey Ngwenya dk90, Donashano Malama, Mike Katiba, Jackson Chirwa, Webster Mulenga, Isaac Shamujompa na Brian Mwila/Chitia Mususu dk82.
Viewing all 104690 articles
Browse latest View live


Latest Images