Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live

FAHAMU Matumizi ya Gia L, 2 na 3 Katika Gari ya Automatic

$
0
0
FAHAMU MATUMIZI YA GIA L, 2 NA 3 KATIKA GARI AUTOMATIC


Katika gari za Automatic kuna gia za L, 2, na 3. Watu wengi hawafahamu kiundani matumizi ya gia hizi hivyo mara nyingi hujikuta wanakosea wapi na namna ya kuzitumia. Katika maelezo haya hapa chini, tumekufafanulia namna ya kutumia gia hizo.

Kwanza kabisa ujue katika hali ya kawaida gari lako linapaswa kuwa katika D (Drive) na hii inategemeana na mazingira ya barabara na hali ya hewa kama ni nzuri. Lakini 2, 3, hutumika tu pale unapokuwa aidha unateremka au unapanda mlima mkali na unataka ushuke au upande kwa spidi isiyozidi 40/60, hapo ndipo unaruhusiwa kutumia 2, na 3.

Namba 2, 3 na L ina maana kuwa unalock giaboksi (gearbox) ili gia zisibadilike (+/-) kama ambavyo zinabadilika ukiweka D. Itambulike kuwa unaweza kubadili kutoka D kwenda 2 au 3 wakati wowote gari inapokuwa katika mwendo ila hakikisha usiwe katika mwendokasi wa zaidi ya 40/60. Maana kinachofanyika ni kwamba D inasababisha sahani (disk) zilizomo ndani ya gearbox kufanya kazi na hii husababisha ile hydrolick iliyomo kupata joto linalotoka katika zile sahani ambalo joto lile husababisha gearbox kutokuwa na nguvu ile ile (Constant velocity) na ndiyo maana ukiweka 2, 3 au L, Gearbox inakuwa kwenye lock na sahani hazisuguani maana inakuwa inatumika sahani (Disk) moja tu.

Hii inasaidia hydrolick kupoa pia na ndiyo maana gari huongeza nguvu kwa ghafla.

Gia L inatumika pale unapokuwa aidha umekwama au unavuta gari jingine au tela, lakini inapaswa itumike kwa muda mfupi sana maana ina nguvu na inaongeza ulaji wa mafuta. Kama ukishatoka katika mkwamo na unaona bado barabara siyo nzuri labda utelezi au unavuta mzigo kwa mwendo mrefu basi unaweka 2 au 3 na wakati huo huo unaweza kuweka hata D kama hali ya njia na mzigo vinaruhusu na unaweza kuongeza walau spidi 40/60 au zaidi kama utaweka D.

Kwa maana rahisi zaidi ni kwamba, gia 2, 3 na L zinafanya kazi kama gari ya manual transmission na hii inakuwa rahisi kwa yeyote ambaye anafahamu kuendesha manual.

-MWANANCHI

MASKINI...Baada ya Kunyimwa Dhamana JAMAL Malinzi Apata Pigo Jingine Akiwa Jela

$
0
0
Viongozi wa ngazi ya juu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) huenda wanaoshitakiwa kwa jumla ya makosa 28 huenda wakawa katika wakati mgumu baada ya wakili wa kujitegemea, Jerome Mswemwa aliyekuwa anawawakilisha, kujitoa rasmi.

Msemwa alikuwa akiwawakilisha Rais wa TFF, Jamal Malinzi, Katibu MKuu wa TFF, Selestine Mwesigwa na  Mhasibu wa TFF, Nsiande Mwanga katika kesi namba 213 ya mwaka 2017.

Kielezea uamuzi wake wa kujiuzulu kupitia barua aliyoandika kwenda kwa Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Wilbard Mashauri, Msemwa alisema ameomba kujiondoa katika kesi hiyo baada ya kutokuopewa taarifa sahihi kutoka kwa wateja wake anaowawakilisha.

Jamal Malinzi (57), Katibu Mkuu wake, Mwesigwa Celestine (46) na Mhasibu, Nsiande Mwanga (27) walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka mbalimbali ikiwamo ya kughushi na kutakatisha fedha dola za Marekani 375,418 (Sh840 milioni).

HAYA Hapa MAKOSA Makubwa Yanayofanywa na Watu Wakienda Haja Kubwa Chooni

$
0
0
Picha A inaonesha jinsi watu wengi wanavyotumia vyoo vya kukaa wakiwa wanajisaidia haja kubwa. Wanasayansi wanasema kuwa mkao wa aina hii si sahihi kwakuwa unakunja utumbo na kufanya kiasi kikubwa cha uchafu kubaki tumboni.

Picha B ni jinsi utumbo unavyokunjwa kwa sababu ya kukaa kama inavyooneshwa kwenye picha A.

Picha C inaonesha mfano wa mtu anayejisaidia haja kubwa akiwa amechuchumaa. Hii ni aina ya asili ya kujisaidia haja kubwa ambapo utumbo haukunjwi. kwahiyo, wataalamu wanashauri kwamba hata unapotumia vyoo vya kukaa, inatakiwa mkao wako uendane na mkao wa asili wa kujisaidia haja kubwa (yaani uendane na kuchuchumaa).

Picha D inaonesha jinsi utumbo hasa sehemu ya mlango wa kutokea haja kubwa inavyokuwa ipo huru tofauti na inavyoonekana kwenye picha B


Kifupi, usahihi wa kujisaidi haja kubwa ni kama ifuatavyo:

1: Magoti yainuliwe juu zaidi ya mapaja

2: Inama mbele kidogo na uweke viwiko vya mikono magotini mwako

3: Tunisha tumbo lako na unyooshe (uti wa) mgongo

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika

Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo..

anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa  PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp/Calls +255 710 279 458
 Call+255 710 279 458

Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

FULL VIDEO: Mashtaka 7 Aliyosomewa Yusuf MANJI Akiwa Kitandani Hospitalini

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo July 5, 2017 ilihamia kwa muda katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kumsomea mashtaka saba ya uhujumu uchumi, mfanyabiashara maarufu Yusufu Manji na wenzake watatu.

Hatua ya Mahakama kuhamia JKCI ilikuja baada ya Manji kushindwa kuhudhuria Mahakamani kwa ajili ya kusomewa mashtaka hayo kutokana na kuugua na kulazwa katika Taasisi hiyo.

Jopo la Mawakili wa Serikali likiongozwa na Mutalemwa Kishenyi, Nassoro Katuga na Tulumanywa Majigo ilisomwa hati ya mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.

1: Kujipatia bidhaa isivyo halali

Mnamo June 30, 2017 katika maeneo ya Chang’ombe A Temeke DSM walikutwa na askari Polisi wakiwa na mabunda 35 ya vitambaa vinavyotumika kutengeneza sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) zenye thamani ya Tsh. 192.5m ambazo zilipatikana isivyo halali.

2: Mabunda manane ya vitambaa

Wakili Majigo alidai kuwa washtakiwa hao walikutwa na Maofisa wa Polisi katika eneo la Chang’ombe A Temeke DSM wakiwa na bidhaa za mabunda manane ya vitambaa vya kutengrneza sare za JWTZ zenye thamani ya Tsh. 44m.

3: Kukutwa muhuru wa Serikali

June 30, 2017 Washtakiwa hao walikutwa na muhuri wa Serikali wa JWTZ isivyo halali ambao umeandikwa “Mkuu wa Kikosi 121 kikosi cha JWTZ” bila ya kuwa na uhalali na kwamba kitendo hicho kinahatarisha uchumi na Usalama wa nchi.

4: Kukutwa na muhuri wa Serikali

Katika shtaka la nne Washtakiwa wanadaiwa kukutwa na muhuri wa Serikali wa JWTZ isivyo halali ambao umeandikwa “Kamanda Kikosi 834 KJ Makutupola Dodoma” bila kuwa na uhalali na kwamba kitendo hicho kingeweza kuhatarisha Usalama wa nchi.

5: Kukutwa na muhuri wa Serikali

Alidai, washtakiwa hao wanadaiwa kukutwa na muhuri wa serikali uliandikwa “Commanding Officer 835 KJ Mgambo, P.O. Box 224, Korogwe kinyume na sheria.

6: Mali iliyopatikana isivyo halali

Katika shtaka la sita, katika maeneo hayo hayo wanadaiwa kukutwa na Mali inayodhaniwa kupatikana isivyo halali ambayo ni namba ya gari zinazosomeka SU 383 mnamo July 1, 2017.

7: Kukutwa na Namba ya gari kinyume na sheria

Shtaka la saba ambalo washtakiwa hao wanakabiliwa nalo ni kukutwa na namba ya gari inayosomeka SM 8573, kinyume na sheria.

Washtakiwa hawakutakiwa kujibu mashtaka kwa sababu makosa hayo hapo chini ya Uhujumu Uchumi na Usalama wa Taifa huku upande wa mashtaka ukiwasilisha hati ya pingamizi la dhamana kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP).

Hii VIDEO ina kila kitu…bonyeza PLAY kutazama!!!

ABDU Kiba Amtupia Dongo Jokate Kiaina...Adai Bongo Hakuna Mrembo Anayeweza Kuwa Mapenzini na ALI KIBA

$
0
0
Leo July 5, 2017 kupitia 255 ya XXL ya Clouds FM mwimbaji wa Bongofleva Abdukiba ambaye ni mdogo wa mwimbaji Alikiba amefunguka akisema hajaona staa yeyote wa kike ambaye anaweza kuwa mapenzini na kaka yake Alikiba.

kuhusu msichana staa wa bongo anayeweza kuwa na uhisiano wa kimapenzi na kaka yake baada ya kuulizwa swali na kujibu kuwa hajaona msichana anaye weza kuwa na mtu kama kaka yake Alikiba.

Abdukiba amesema Bongo wapo wasichana warembo ambao hawana kasoro lakini hawajafikia vigezo vya kuwa na Alikiba ambaye amedai kuwa ni mtu mwenye busara, mcheshi na mpenda amani hivyo anahitaji mwanamke mpenda dini sana ndio maana anadiriki kusema hajamuona bado.

Unazungumzia star wa kike? Sijamuona bado huyo star ambaye nitasikia Alikiba anatoka naye halafu ndio nikafurahi. Bado sijamuona Kibongo Bongo. Bila shaka naweza kusema sijamuona atakayemfaa Alikiba. Nasema kwa sababu naona ila siwezi kuzungumzia tunakoenda. Waliopo hawana kasoro, ni wasichana wazuri na warembo ila haijafikia hatua ya wao kuwa na mtu kama Alikiba.

“Alikiba ni mtu wa kawaida: kwanza ni mpenda busara, mpenda amani na mcheshi, so anahitaji mtu ambaye anaipenda sana dini. Kwa hiyo mimi naweza kusema sijamuona, japo ni kweli mtu anaweza kuvaa baibui au mtandio lakini undani wake huujui. Naweza kusema u-smart huficha vitu vingi.” – Abdukiba. 

UTEUZI Mwingine wa Rais Magufuli leo July 6, 2017

$
0
0
Rais Magufuli amemteua Bw. Waziri Waziri Kindamba kuwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuziwa Bw. Waziri Waziri Kindamba umeanza July 4, 2017.

Kabla ya uteuzi huo, Bw. Waziri Waziri Kindamba alikuwa akikaimu nafasi hiyo.

GODZILLA Njoo Nikusaidie Kwa Stress Ulizonazo Usije Kula UNGA – Nay wa Mitego

$
0
0
Msanii wa Bongo Flava, Nay wa Mitego amezidi kuwasha moto kama inavyoeleza kwenye ngoma yake mpya ‘Moto’.


Nay kupitia mtandao wa Instagram ameendelea kuwashukia baadhi ya wasanii ambao amewataja katika ngoma yake hiyo. Haya ndio aliyoandika kuhusu, Godzilla na Bill Nass.

Ujinga Ni Kukasilika Pale unapo Ambiwa Ukweli. Una panic #Moto🔥Watag Walio Panic na Kubishana na Ukweli mi naanza na @kingzilla_tz 😂😂 🏃🏿🏃🏿 aiseh Yule Mwanamke nitakupa Number yake Mi Mwenyewe Japo Najua huto Muweza🔥. Ila @billnass Una Roho Mbaya sana Kijana Hutaki Kumpa ata Upenyo Kaka ako.!?, Njo Nikusaidie @kingzilla_tz Maana Stress Ulizo nazo Utaja kula Ngada Bureeeee. Karibu #FreeNation966 Tuta kurudisha kwenye Game.!, #Moto🔥

KAMANDA Sirro: Wametaka Ubaya Wataupata

$
0
0
MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali (IGP) Simon Sirro, amesema watu wanaotumwa kutekeleza mauaji Wilaya  za Kibiti, Mkuranga na Rujifi watajibiwa kwa ubaya na kwamba kuanzia sasa wametangaza vita dhidi yao.

Alisema watu hao ambao wanaua raia na askari walidhani watawachonganisha wananchi kirahisi bila kujua Watanzania wana umoja usioweza kugawanyika.

Sambamba na hilo, amesisitiza kuwa suala la ulinzi ni la watu wote na kwamba wananchi wa maeneo hayo wanapaswa kujilinda kwa kuanzisha vikundi vya ulinzi shirikishi.

IGP Sirro aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam, wakati akipokea msaada wa magari manne kila moja likiwa na thamani ya Sh. milioni 126.2 kutoka  kampuni ya Haval Great Wall Motors, yatakayosaidia kupatamba na uhalifu nchini.

“Sisi Tanzania hatujazoea vurugu za namna ile kwa hiyo wale ambao walikuwa wametumwa walifikiria Tanzania kama nchi nyingine wataona majibu yake,” alisema.

“Tangu zamani sisi ni wamoja na tunapendana kwa hiyo wale waliokuwa wametumwa vibaya vibaya na sisi tutawajibu kwa ubaya ubaya tu.”

Alisema Jeshi la Polisi linakwenda vizuri na suala la mauaji ya Kibiti na kwamba muda si mrefu kutakuwa na majibu mazuri.

IGP Sirro ambaye aliapishwa na Rais John Magufuli Mei 29, mwaka huu, akichukua nafasi ya Ernest Mangu aliyeondolewa, alisema wenyeviti wa vijiji wa Mkoa wa Pwani wana wajibu wa kuimarisha hali ya ulinzi katika maeneo yao.

“Maeneo hayapitiki, Kibiti, Ikwiriri, Mkuranga hata maeneo mengine ya nchi wananchi wanapaswa kujilinda kwa kuanzisha ulinzi shirikishi,” alisema IGP Sirro.

Alisema matukio ya uhalifu kwa miaka ya sasa yamekuwa magumu kuliko ya miaka ya nyuma, hivyo jeshi hilo linapaswa kwenda na wakati.

Kwa mujibu wa Sirro, Jeshi la Polisi linakabiliwa na changamoto  mbalimbali kama vile uhaba wa vitendea kazi, ufinyu wa bajeti na uwapo wa miundombinu mibovu ambayo ni kikwazo kwa polisi kufika sehemu ya tukio kwa haraka.

Naye Meneja wa kampuni iliyotoa magari hayo, Jianguo Liu, alisema wametoa msaada wa magari hayo kwa Jeshi la Polisi kwa lengo la kusaidia kupambana na uhalifu.

Mauaji katika wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji mkoani Pwani yalianza Januari, 2015 idadi ikitajwa kufikia 39 huku wanaotekeleza mauaji hao wakiwa hawafahamiki.

Mauaji ya mwisho kutekelezwa yalitokea Juni 27, mwaka huu, wilayani Kibiti baada ya watu wawili kuuawa kwa kupigwa risasi katika kijiji cha Mangwi, kata ya Mchukwu wilayani Kibiti usiku, huku mtu mmoja akijeruhiwa vibaya sehemu ya jicho.

Mauaji hayo yalitekelezwa ikiwa imepita wiki moja baada ya askari wawili wa usalama barabarani wilayani Kibiti mkoani Pwani kuuawa kwa kupigwa risasi katika kijiji cha Masafiri kata ya Bungu, huku askari mmoja akisalimika.

Moja ya matukio yaliyowahi kutokea wilayani Kibiti Mkoa wa Pwani na kuacha historia kwa Jeshi la Polisi ni lile lililotokea Aprili 13, mwaka huu, baada ya askari wanane kushambuliwa wakitoka kubadilishana lindo.

Katika shambulio hilo, majambazi hao walipora bunduki saba ambazo ni SMG nne na Long Range tatu zikiwa na risasi zake.

Kutokana na mwendelezo wa mauaji katika Wilaya hizo, IGP Sirro alipoingia madarakani alitangaza donge nono la Sh. milioni 10 kwa mtu yeyote atakayefanikisha kutoa taarifa za kukamatwa kwa watuhumiwa 12 wa mauaji.

Watuhumiwa hao ni pamoja na Abdurshakur Ngande Makeo, Faraj Ismail Nangalava, Anaf Rashid Kapera, Said Ngunde, Omary  Abdallah  Matimbwa, Shaban Kinyangulia,  Haji Ulatule, Hassan Uponda, Rashid Salim Mtulula, Hassan Nasri Mzuzuri na Hassan Njame.

IGP Sirro alitangaza bingo hiyo zikiwa zimepita siku chache tangu Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Onesmo Lyanga alipotangaza bingo ya Sh. milioni tano kwa yeyote atakayetoa taarifa zitakazowezesha kukamatwa kwa watu hao.

POLISI KUWEZESHWA
Wakati huo huo, Serikali imesema imeongeza doria na vitendea kazi kwa Askari wa Mkoa Maalum wa Kipolisi wa Rufiji unaoundwa na wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji mkoani Pwani.

Katika hotuba yake ya kuahirisha Bunge jana, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema pia tayari Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo maalum ameshateuliwa na kutoa rai kwa wananchi wa maeneo hayo kutoa ushirikiano kwa serikali ili kuwezesha watuhumiwa wote kukamatwa.

Majaliwa alisema dhamira ya serikali ni kuhakikisha kila raia wa Tanzania, wakiwamo wananchi wa wilaya hizo, wanakuwa huru kufanya shughuli zao za maendeleo bila kuhofia usalama wa maisha yao.

“Serikali inaendelea kuchukua hatua za muda mfupi na za muda mrefu ili kurejesha hali ya usalama katika maeneo hayo. Tumeongeza doria na vitendea kazi kwa askari,” alisema Majaliwa.

Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo TRA na Makampuni Mengine

MTOTO Amkata Ulimi wa Shangazi ya Kuung'ata

$
0
0
Mwanamke mmoja (21) mkazi wa Kisiwa cha Bulubi wilaya ya Ukewe mkoani Mwanza anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kumng'ata ulimi shangazi yake hadi kipande kukatika chini


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Naibu Kamishna DCP Ahmed Msangi amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Edina Deus anayedaiwa kutenda tukio hilo dhidi ya shangazi yake Rose Marwa (31) mkazi wa Bulubi

Inadaiwa kuwa mtuhumiwa alifanya hivyo baada ya kufokewa na shangazi kwa kosa la kukojoa kitandani wakati wamelala ndipo ugomvi ukazuka na hatimaye Edina alikwenda kumkaba kwa nguvu shingoni majeruhi Bi. Rose hadi kutoa ulimi nje kisha akaung'ata mpaka ukakatika.

Inasemekana baada ya kutokea tukio hilo waliweza kujitokeza ndugu wa majeruhi na kuweza kumpatia huduma ya kwanza na kuamua kuficha tatizo hilo ili iwe siri lakini hali ilivyozidi kuwa mbaya ndipo walipoamua kutoa taarifa kituo cha polisi na kuanza kufanya ufuatiliaji wa haraka eneo la tukio na kufanikiwa kumkata mtuhumiwa.

Pamoja na hayo, DCP Msangi amesema kuwa polisi wapo katika mahojiano na mtuhumiwa pindi uchunguzi utakapokamilika, mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani huku majeruhi akiendelea kupatiwa matibabu kwenye hospitali aliyolazwa na hali yake inaendelea vizuri.

TANZIA....Msanii Shaaban Dede Afariki Dunia

$
0
0
Mwanamuziki mkongwe kutoka Msondo Ngoma Music Band, Shaaban Dede amefariki dunia leo saa mbili asubuhi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa matibabu.

Taarifa hizo zimethibitishwa na mtoto wake wa kiume aliyetambulika kwa jina la Hamad Dede na kusema mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa marehemu Mbagala jijini Dar es salaam, na kwamba ratiba na taratibu zote zitatangazwa mara zitapokamilika kupangwa.

Marehemu Dede atakumbukwa kama mmoja wa wanamuziki nguli kutokea nchini Tanzania kwa uwezo wa kucheza na sauti yake pamoja na kuwa mtunzi mahili wa nyimbo mbalimbali  enzi za uhai wake alipokuwa anaimbia bendi tofauti tofauti ni Jazz, Bima Lee, Tabora Mlimani Park na Msondo Ngoma ambako alikuwa anatumikia hadi mauti yanamkuta.

KITANDA Hakizai Haramu...Ila Kwa Huyu Mwanamke Hii ni Zaidi ya Haramu...Soma Hii Stori

$
0
0
Huko Nigeria mwanamke mmoja aliolewa na mwanaume wa kwanza akaachika,akaenda kwa mume mwingine ambaye alikaa nae kwa miezi 8 na wakafanikiwa kupata mtoto mmoja. Mtoto alipofikisha miaka mitatu mume wa kwanza akasema ni wake na mume wa pili hivyo hivyo lakini walipopimwa vinasaba (DNA) ikaonekana mtoto hawahusu wote wawili.

Ungekutwa kwenye hali kama hii ungechukua hatua gani?

ILIPOFIKIA Kesi ya Mmiliki wa Shule ya Lucky Vincent Baada ya Basi Kuuwa Wanafunzi

$
0
0
Tunakumbuka ajali ya basi la Wanafunzi wa Lucky Vincent iliyotokea Karatu, Arusha na kuua 32 na kuacha Majeruhi watatu ambao wanatibiwa kwenye Hospitali ya Mercy, Sioux City Iowa, Marekani huku Mmiliki wa shule hiyo na Makamu Mkuu wa Shule wakishikiliwa na Polisi.

Sasa new story jana July 5, 2017 ni kwamba Mahakama ya Wilaya Arusha imesema kuwa Upelelezi wa kesi inayomkabili mmiliki wa Shule ya Lucky Vincent, Innocent Mosha na Makamu Mkuu wa Shule hiyo Longino Vincent umekamilika na kesi hiyo itaanza kusikilizwa July 26, 2017 wakikabiliwa na mashtaka matano.

Mashtaka wanayokabiliwa nayo pamoja na Mmiliki huyo kuruhusu Dereva kuendesha gari la abiria bila kuwa na leseni ya usafirishaji, kutumia gari bila kuwa na BIMA pamoja na kushindwa kuingia mkataba na Mwajiriwa.

Mashtaka mengine ni kuzidisha abiria 13 kwenye gari pamoja Kaimu Mkuu wa Shule kuratibu safari na kuruhusu gari kuzidisha abiria

MBOWE Alaani Wabunge wa CHADEMA Kukamatwa......Aiomba Mahakama Itende Haki

$
0
0
Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Mh. Freeman Mbowe amelaani kitendo cha wabunge 8 wa upinzani kukamatwa na jeshi la polisi kwa madai yakutaka kumpiga mbunge wa CCM Juliana Shonza, na kusema hawajapeleka mabondia bungeni.

Freeman Mbowe aliyasema hayo  jana mjini Dodoma baada ya kutoka mahakamani na kudai kuwa wao wanaamini kuwa mahakama itatenda haki kwa wabunge hao.

"Kama ambavyo mnajua kwa masaa zaidi ya 48 wabunge wa CHADEMA wameshinda polisi, jana siku nzima wameshinda polisi na leo wameshinda polisi mpaka mchana huu.

"Kwa maana hiyo wawakilishi hawa wa wananchi wameshindwa kuwajibika kwa ajili ya wananchi kwa makosa ambayo kimsingi kabisa hayakutakiwa kupewa uzito huu yanaopewa.

"Inasemakana kuwa wabunge hawa walimfanyia fujo Mbunge wa viti maalum (CCM) Juliana Shonza, jambo hili linafedhehesha sana, sisi tuna wabunge ambao wanajiheshimu na kuheshimu sheria za nchi, hatukupeleka wapiganaji bungeni bali tumepeleka viongozi wa kutunga sheria" alisisitiza Freeman Mbowe

Mbali na hilo Mbowe anasema kitendo cha Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai kulivalia njuga suala hilo ni jambo ambalo yeye limemsikitisha.

"Kitendo cha kuwapeleka polisi na kuwashtaki wabunge wetu na Spika wa Bunge kushadadia jambo hili limenisikitisha sana

" Spika kusema ametoa ruhusa wahukumiwe kwa kesi za jinai ni mwendelezo wa kutaka kutunyamazisha, ila hatutayumba na tunaamini kuwa jopo la majaji litatenda haki katika jambo hili, maana hakuna mbunge yoyote wa CHADEMA wala UKAWA ambaye amemshambulia mbunge yoyote yule bungeni" alisisitiza Mbowe.

Katika watuhumiwa wote nane, mtuhumiwa mmoja ambaye ni Mbunge wa jimbo la Ubungo, Mbunge Saed Kubenea jana  alipandishwa mahakamani na kushtakiwa kwa kosa moja la shambulio la kawaida hivyo alidhaminiwa na shauri hilo upelelezi wake bado haujakamilika hivyo kesi itatajwa tena tarehe 26, Julai 2017 Dodoma.

MAMBO 10 Yaliyolivuruga Bunge la Bajeti....

$
0
0

Kuhitimishwa kwa Bunge la bajeti kumeacha kumbukumbu kumi muhimu ambazo kama ulikuwa hufuatilii kilichokuwa kikiendelea kwa siku hizo 92, leo tunakukumbusha.

Yapo mengi; yaliyofurahisha, yaliyotia simanzi na hata kufikirisha. Hayo yote yalijiri tangu Aprili 4, Bunge hilo lilipoanza mpaka jana Julai 5 lilipoahirishwa. Yalikuwapo mambo ya kisheria, kiuchumi na kijamii ambayo yaliibuka na kushughulikiwa ipasavyo na chombo hicho cha kutunga sheria.

Adhabu za wabunge

Katika Bunge hilo, adhabu ya kihistoria ilitolewa kwa wabunge wawili wa Chadema; Halima Mdee (Kawe) na Ester Bulaya (Bunda Mjini) ambao ‘wamehukumiwa’ kukaa nje ya vikao vya Bunge kwa mwaka mzima.

Adhabu hiyo ilitolewa baada ya kutiwa hatiani kwa kudaiwa kuvunja kanuni za Bunge wakati Spika Job Ndugai alipoamuru Mbunge wa Kibamba, John Mnyika atolewe nje ya ukumbi kwa kosa la kubishana naye. Katika tukio hilo, Mnyika aliadhibiwa kutohudhuria vikao vya Bunge kwa wiki moja. Kutokana na adhabu kwa wabunge wake wawili, Chadema imeliwasilisha shauri Mahakama Kuu ikiomba itengue hukumu hiyo kwa maelezo kwamba ipo nje ya uwezo wa Bunge.

Nusura wabunge wazichape

Hukumu waliyopewa Mdee na Bulaya ilichangiwa na maazimio yaliyotolewa na Mbunge wa Viti Maalumu mkoani Songwe, Juliana Shonza.

Kwa kile kinachoonekana kuwapo kwa visasi baina yao, wakati vikao vikikaribia kumalizika, wabunge wanane wa upinzani wanaidawa kumshambulia Shonza na sasa wanakabiliwa na kesi na moja wa wabunge hao wa upinzani, Saed Kubenea jana alifikishwa mahakamani kutokana na sakata hilo lililotokea Jumatatu wiki hii.

Miswada

Katika wiki za mwisho za Bunge hilo, miswada minne ilipitishwa ikiwamo mitatu iliyowasilishwa kwa hati ya dharura ambayo kwa kiasi kikubwa ilizungumzia mabadiliko ya sekta ya madini. Mmoja, ni wa sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali namba moja wa mwaka 2017, uliojadiliwa na kupitishwa jana.

Miswada hiyo imehitimisha hoja ya siku nyingi ya wapinzani waliotaka kufanyika kwa marekebisho kwenye sheria, sera na mikataba ya madini ambayo ilionekana hailinufaishi Taifa kama inavyotakiwa.

Hata hivyo, miswada hiyo iliyowasilishwa kwa hati ya dhahura, ilipingwa na kambi ya upinzani kwa maelezo kwamba muda uliotolewa haukutosha kuwashirikisha wadau wote hasa wachimbaji wadogo na wananchi waliopo kwenye maeneo yenye machimbo au migodi ya madini.

Katika mchakato wa mijadala hiyo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aliweka pembeni tofauti zake na msaidizi wake mwandamizi wa zamani ambaye sasa ni Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe akimuunga mkono kuhusu hoja yake ya kutaka uwepo muundo wa uzalishaji wa madini akisema ndicho kitu muhimu cha kuzingatiwa kwenye sheria mpya.

Kamati ya Tanzanite

Wakati wa mjadala wa makadirio ya Wizara ya Nishati ya Madini, Kamati ya Nishati na Madini iliwasilisha ripoti ya ziara yake na kupendekeza kufanyika kwa mabadiliko ya usimamizi katika machimbo ya Tanzanite yaliyo chini ya Kampuni ya Tanzanite One (TML). Mwenyekiti wa kamati hiyo, Dotto Biteko alisema kampuni hiyo imekuwa ikitoa taarifa za uongo na kwamba imebaini udanganyifu inaofanya dhidi ya mwekezaji mwenza, Stamico na kuiokosesha Serikali mapato stahili.

Kutokana na mapendekezo ya kamati, Spika Ndugai aliunda kamati ya watu tisa itakayoanza kazi Julai 10 kuchungua suala hilo. Kubwa litakalofanywa ndani ya siku 30 ilizopewa ni kuuchambua mkataba kati ya Shirika la Taifa la Uchimbaji wa madini (Stamico) na TML na kubainisha faida na hasara kutokana na ubia uliopo.

Pia itatathmini mfumo wa uchimbaji, usimamizi na udhibiti wa biashara ya tanzanite na inavyoweza kuchangia zaidi katika uchumi wa Taifa. Kwenye ripoti, inatakiwa kubainisha na kushauri utaratibu bora unaoweza kutumika kusimamia uchimbaji na biashara hiyo.

Kukosekana kwa Waziri wa Nishati

Tangu kutenguliwa kwa uwaziri wa Profesa Sospeter Muhongo, aliyekuwa anaongoza Wizara ya Nishati na Madini mwishoni mwa Mei, wizara hiyo imeendelea kubaki bila kiongozi.

Muhongo aliondolewa baada ya kamati iliyoundwa na Rais John Magufuli kuibua madudu kadhaa katika biashara ya madini nchini. Wakati uamuzi huo unafanywa na Rais John Magufuli, makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo yalikuwa bado hayajawasilishwa bungeni hivyo, hoja zake ama zilijibiwa na naibu waziri au mawaziri wengine.

Muswada wa fedha

Baada ya kupitisha bajeti ya Sh31.7 trilioni, Bunge pia lilipitisha Muswada wa Sheria ya Fedha wa mwaka 2017 ili kuwezesha ukusanyaji wa mapato kufanikisha matumizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Katika marekebisho yaliyofanywa, wafanyabiashara wadogo wanaofanya biashara katika maeneo yasiyo rasmi wametambuliwa na kuanzia sasa watakuwa na vitambulisho rasmi.

Muswada huo pia unawagusa wachimbaji wadogo wa madini, kampuni zinazopata hasara, taasisi zisizo za Serikali (NGO), wasafirishaji wa maua nje ya nchi na wachimbaji wadogo ambao kuanzia mwezi huu, wataanza kulipa kodi. Kwenye mabadiliko yaliyopendekezwa, kodi ya majengo iliyokuwa chini ya halmashauri sasa inakusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Kutenguliwa na kuteuliwa mawaziri

Wiki moja kabla ya vikao vya Bunge kuanza, Rais Magufuli alifanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri. Alimuengua aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye na kumwingiza Profesa Palamagamba Kabudi bungeni akiwa Waziri wa Katiba na Sheria.

Profesa Kabudi alichukua nafasi ya Dk Harrison Mwakyembe aliyemrithi Nape ambaye sasa anabaki kuwa Mbunge wa Mtama.

Profesa Kabudi ndiye aliyesimamia mabadiliko ya sheria kadhaa ambazo miswada yake iliwasilishwa, kujadiliwa na kupitishwa na Bunge.

Miswada iliyopitishwa imependekeza kuvunjwa kwa Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA), kupunguzwa kwa mamlaka ya waziri wa nishati na madini na kamishna wa madini huku ikianzishwa taasisi nyingine ya usimamizi.

Mengine ni kuanzishwa kwa kamisheni ya madini itakayokuwa na wajumbe tisa, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuanza kutunza dhahabu na vito kama sehemu ya akiba ya Serikali na kuimarisha ulinzi kwenye migodi na machimbo yote na kujengwa kwa maghala na kuanzishwa kwa masoko maalumu ya madini.

Wabunge wa Chadema Eala

Miongoni mwa matukio yatakayokumbukwa katika Bunge safari hii ni mshikemshike wakati Bunge lilipowachagua wabunge tisa kuliwakilisha Taifa, Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (Eala).

Hata hivyo katika uchaguzi wa kwanza, majina mawili yaliyowasilishwa na Chadema; Ezekeah Wenje na Lawrence Masha yalipigwa chini baada ya kuzidiwa na kura nyingi za ‘hapana’.

Hata hivyo, chama hicho kilipopeleka majina kwa mara ya pili, waliochaguliwa kuhitimisha idadi ya wabunge tisa ni Josephine Lemoyan na Pamela Massay.

Awali, wabunge waliochaguliwa kuiwakilisha Tanzania kwa upande wa CCM ni Fancy Nkuhi, Happines Legiko, Maryam Ussi Yahya, Dk Abdullah Makame, Dk Ngawaru Maghembe na Alhaj Adam Kimbisa. Kwa upande wa CUF ni Habib Mnyaa.

Makinikia

Baada kukabidhiwa kwa ripoti ya pili ya uchunguzi wa usafirishaji wa mchanga wa dhahabu nje ya nchi na kamati ya Rais, mjadala mkubwa wa makinikia ulitawala bungeni.

Ripoti hiyo iliyowasilishwa Juni 13, ilibainisha upungufu kadhaa kwenye mkataba wa kampuni ya Acacia inayochimba na kumiliki dhahabu kwenye migodi ya North Mara, Bulyanhulu na Buzwagi. Moto uliongezeka zaidi baada ya Mwenyekiti ya Kampuni ya Barrick Gold inayoimiliki Acacia, Profesa John Thornton kuja nchini na kukutana na Rais Magufuli na kukubali kufanya mazungumzo ili kupata muafaka wa sakata hilo.

Acacia wamewasilisha mgogoro huo na Serikali kwenye mahakama ya usuluhishi.

Kamati ya almasi

Spika wa Bunge, Job Ndugai jana aliunda Kamati Maalumu ya ushauri kuhusu mfumo wa usimamizi, umiliki na udhibiti wa madini ya almasi ambayo inajumuisha wabunge tisa.

Kamati hiyo itaongozwa na Mbunge wa Ilala (CCM), Mussa Azzan Zungu. Akitangaza kamati hiyo muda mfupi kabla ya kuahirisha Bunge jana, Spika Ndugai alisema aliiteua kwa kuzingatia vigezo vya taaluma, uzoefu, pande za Muungano, jinsia na uwakilishi wa vyama vya siasa bungeni.

Alisema itakapobidi, kamati hiyo itafanya ziara katika maeneo mbalimbali kwa kuzingatia muda wake wa kazi, bajeti na ulazima wa kufanya hivyo.

“Katika kutekeleza majukumu yake, kamati itashauriwa kwa karibu na sekretarieti itakayoteuliwa na Katibu wa Bunge,” alisema Ndugai.

Aliwataja wajumbe wa kamati hiyo kuwa ni Dk Immaculate Sware (Viti Maalumu - Chadema), Shally Raymond (Viti Maalumu – CCM) na Rashid Ali Abdallah (Tumbe - CUF).

Wengine ni Allan Kiula (Iramba Mashariki - CCM), Restituta Mbogo, (Viti Maalumu -CCM), Ahmed Juma Ngwali, (Ziwani - CUF), Richard Ndassa ( Sumve – CCM) na Emmanuel Mwakasaka (Tabora Mjini - CCM).

“Kamati hiyo itafanya kazi kwa muda wa siku 30 kuanzia Julai 10, 2017. Kituo kikuu cha kazi kitakuwa katika Ofisi ya Bunge hapa Dodoma,” alisema.

Hadidu za rejea za kamati hiyo ni kuchambua taarifa za Tume na Kamati mbalimbali zilizowahi kuundwa na Serikali kwa ajili ya kushughulikia mfumo wa uchimbaji, usimamizi, umiliki na udhibiti wa madini ya almasi nchini na kuona mapendekezo yake na namna yalivyotekelezwa na Serikali.

Nyingine ni kutathmini mfumo uliopo wa uchimbaji, usimamizi na udhibiti wa biashara ya madini ya almasi nchini na kubainisha manufaa ambayo Serikali inapata kutokana na uwekezaji uliopo.

Nyingine alisema ni, “Kubainisha na kushauri kuhusu utaratibu bora unaoweza kutumika katika kusimamia uwekezaji, uchimbaji na biashara ya madini ya almasi nchini.”

Alisema kamati hiyo itatathimini mfumo wa uchimbaji, usimamizi, umiliki na udhibiti wa madini ya almasi nchini kisha kuandaa mapendekezo kwa ajili ya kuishauri Serikali kuhusiana na uendeshaji bora wa biashara ya madini hayo nchini. Alisema uamuzi huo umetokana na Rais John Magufuli kupendekeza Bunge liunde kamati ya kuchunguza na kufuatilia madini hayo.

MAMBO Yanayochangia Mume Kutembea na Hausigeli

$
0
0


Ndugu zangu, malalamiko ya baadhi ya mabinti wanaofanya kazi za ndani ‘mahausigeli’ kuwazidi kete baadhi ya wanawake kwa kuwachukulia waume zao yamekuwa yakiripotiwa kila mara.
Si ajabu hata wewe unayesoma makala haya aidha umeshawahi kumsikia rafiki kama siyo jirani yako akikorofishana na hausigeli wake au kushuhudia hausigeli akifumaniwa na bosi wake.

Hakika ni matukio ya aibu sana. Inafika wakati unajiuliza inakuwaje mume anamtongoza na hatimaye kutembea na hausigeli wake? Ameshawishiwa na kitu gani au amekosa nini kwa mkewe mpaka anafikia uamuzi huo?

Kimsingi linapotokea tukio kama hili, wengi hujiuliza maswali mengi sana na majibu yake huwa ni magumu kupatikana. Hii ni kwa sababu ni jambo lisilotarajiwa kufanywa na mtu aliyestaarabika. Hata hivyo, tuna kila sababu ya kujua chanzo cha tatizo hili.

Nitajaribu kuzungumzia kipengele kimoja baada ya kingine kuhusiana na yapi yanayotajwa kuwasukuma baadhi ya wanaume kutembea na mahausigeli wao.
Wanawake wanajitakia

Ni jambo ambalo limekuwa likilalamikiwa sana na baadhi ya watu kuwa, inakuwaje hausigeli anapewa majukumu ya kumhudumia mume wakati mke yupo?

Ni ukweli usiofichika kwamba, kuna baadhi ya wanawake ni malimbukeni wasiojua jinsi ya kuitunza ndoa. Hawajui namna ya kumshika mume na kumuepusha na vishawishi vinavyoweza kumfanya akamsaliti.

Ndugu zangu, kitendo cha mke kumruhusu hausigeli amfulie mumewe nguo zake za ndani, amuandalie chakula, ampelekee maji ya kuoga na mambo mengine kama hayo ndivyo vimekuwa vikichochea usaliti huu.

Kama mke hataki kusalitiwa kirahisi basi ajitahidi sana kuchukua jukumu la kufanya yale ambayo kwa kiasi kikubwa yakifanywa na hausigeli huweza kujenga ukaribu wa kimapenzi kwa mumewe. Kamwe usibweteke, ukibweteka hausigeli wako atakupindua na itakuwa ni aibu kwako.
Mahausigeli micharuko

Hivi inaingiaje akilini mke kuridhia kumuajiri hausigeli ambaye kwa macho tu anaonekana hajatulia? Unamuajiri hausigeli ambaye siku ya kwanza tu anataka umpe sehemu ya mshahara wake akafanye ‘shopping’ halafu unakubali, unajitaka kweli?

KISIRANI Cha Mimba Chamtesa Asha Buhet

$
0
0
STAA wa sinema za Kibongo, Esha Buhet amefunguka namna anavyoteswa na kisirani cha mimba hivyo kuwaomba watu wamsamehe pindi atakapowakwaza.

Akizungumza na 3-Tamu, Esha alisema kuwa mimba aliyonayo inampa kisirani hivyo inawezekana akawa anawaudhi baadhi ya marafiki na ndugu zake, lakini ni vyema wakaelewa hali aliyonayo kuwa ni ya mpito hivyo wamsamehe.

“Hali niliyonayo ni ya mpito na huwa inakuja na mambo mengi, hivyo ndugu zangu na jamaa zangu nawaomba wanisamehe sana kama ikitokea nikawaudhi maana naona mimba inanipeleka puta,” alisema Esha.

VODACOM Tanzania Waichangamkia RED RLX Katika Maonyesho ya Saba Saba

$
0
0
Kampuni ya simu za mkononi inayoongoza nchini, Vodacom Tanzania inashiriki Maonesho ya 41 ya Viwanda na Biashara maarufu kama “Sabasaba” ambapo mamia ya wateja wameoneshwa kufurahishwa na kujiunga na huduma mpya inayojulikana kama “RED RLX” ikiwa ni miongoni mwa huduma nyingi zinatolewa bandani hapo. Huduma hii ni mpango unaojumuisha vifurushi na kulipa kadri mteja atumiavyo na lengo ni kuwafanya wateja wa Vodacom waishi bila wasiwasi linapokuja suala la mawasiliano. Vifurushi hivi vina dakika nyingi, MB za intaneti nyingi, SMS nyingi na pia dakika za kupiga simu nje ya nchi. Wakati mteja anaponunua kifurushi cha RED, anaweza kuchagua huduma ya kifurushi cha kujirudia (kujinunua tena) kila kinapoisha muda wake au kununua mara moja tu.


Mteja wa Vodacom akinunua bando ya RED, atapata nafasi na kipaumbele ya kuhudumiwa bila kukaa kwenye foleni wakati akitembelea duka lolote la kampuni hiyo, atapata huduma ya SOKONI App BURE, taarifa fupi ya M-Pesa BURE pindi anapohitaji na huduma ya kipekee pindi atakapowasiliana na huduma kwa wateja. Ili mteja ajiunge na kunufaika na kifurushi hiki anatakiwa kupiga *149*01# na Chagua RED na ataona vifurushi hivi vya RED.
Kifurushi cha Silver
TZS 30,000
600 Dakika (Mitandao Yote)
3GB Data
3,000 SMS
Kifurushi cha Gold
TZS 50,000
1,000 Dakika (Mitandao Yote)
7GB Data
7,000 SMS
Kifurushi cha Platinum
TZS 95,000
2,500 Dakika (Mitandao Yote)
30 Dakika (Kimataifa)
20GB Data
15,000 SMS

Jini Kabula Adaiwa Kuzua Timbwili Hotelini

$
0
0
MSANII wa filamu Bongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ juzikati alidaiwa kuzua timbwili la aina yake kwenye Hoteli ya Lamada iliyopo Ilala jijini Dar baada ya tatizo alilolipata siku chache zilizopita la kudata kiakili kudaiwa kujirudia.

Kwa mujibu wa chanzo chetu kilichokuwepo hotelini hapo, mwanadada huyo alienda Lamada kumfuata msanii mwenzake Esha Buheti ambaye ndiye shosti wake mkubwa kwa sasa lakini alipoambiwa hayupo, ndipo alipowaanzishia timbwili wahudumu.

“Alizua timbwili la aina yake, ikabidi watu waliokuwa eneo la tukio wafanye kazi ya ziada kumtuliza.

“Baadaye ikabidi wamdanganye kwamba Esha yupo Muhimbili kapelekwa kujifungua, ndipo akacharuka tena akitaka apelekwe hukohuko akamuone, hawakumpeleka ila waliamua kumpakiza kwenye gari na kumzungusha maeneo mbalimbali ya jiji ili awe sawa,” alidai sosi huyo. Ikazidi kudaiwa kuwa, baada ya kuona ana nafuu kidogo waliamua kumpeleka Mbagala ambako ndiko ndugu zake waliko.

Baada ya kuinyaka ishu hiyo, paparazi wetu alimvutia waya mtu wa karibu na Kabula ambaye ni mzazi mwenziye, Tuesday Kihangala `Mr. Chuz’ ambaye alieleza kuwa, amepewa taarifa na ndugu wa mwanadada huyo kwamba bado hayupo sawa kiakili na anatafakari jinsi ya kumsaidia ili aweze kupona kabisa. “Leo (juzi) hii ndugu zake wamenitaarifu kwamba bado hajawa sawa na hali yake inawachanganya sana, walinipa niongee naye ili niamini, yaani anaongea maneno mengi mfululizo, kwa kweli anahitaji matibabu ya kina kabla ugonjwa haujakolea,” alisema Chuz.

Jini Kabula hivi karibuni alilazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili akidaiwa kuchanganyikiwa akili lakini siku chache baadaye alipata nafuu na kuruhusiwa kurudi nyumbani kabla ya juzi mambo kudaiwa kuharibika tena.

Source: Global Publisher
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live




Latest Images