Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Huu Ndio Mpunga Anaoingiza Ronaldo Kupitia Istagram tu

$
0
0
Cristiano Ronaldo ana watu milioni 104 wanaomfuatilia katika mtandao wa Instagram.

Ronaldo anawatumia watu hao kujiingizia pauni 310,000 (zaidi ya Sh milioni 888) kwa vitu kadhaa ambavyo amekuwa akitupia kwenye mtandao huo kama sehemu ya biashara.

Ronaldo ndiye mwanasoka pekee aliye katika 10 Bora ya wale wenye wafuatiliaji wengi zaidi katika Instagram.


MASTAA WENYE WAFUATILIAJI WENGI ZAIDI

1. Selena Gomez – 122 million followers – £425,000 per post

2. Kim Kardashian – 100 million followers –  £387,000 per post

3. Cristiano Ronaldo – 104 million followers – £310,000 per post

4. Kylie Jenner – 95 million followers – £310,000 per post

5. Kendall Jenner – 81.7 million followers – £286,000 per post

6. Khloe Kardashian – 68 million followers – £193,000 per post

7. Kourtney Kardashian – 57.8 million followers – £193,000 per post

8. Cara Delevingne – 40.4 million followers – £116,000 per post

9. Gigi Hadid 34.7 million followers – £93,000 per post

10. Lebron James – 30.7 million followers – £93,000 per post

WALINZI 28 wa Acacia ‘wakwama’ mgodini kwa siku nne

$
0
0
Waliokuwa walinzi 28 wa mgodi wa dhahabu wa Buzwagi unaomilikiwa na Kampuni ya Acacia, wameshindwa kutoka ndani ya eneo la mgodi huo kwa siku nne mfululizo kuanzia Julai mosi, baada ya vitambulisho vyao vinavyotumika kufungulia milango kufutwa kwenye mfumo wa ulinzi.

Hatua ya kufuta vitambulisho vya walinzi hao ambao ajira zao zilikoma tangu Juni 30, kutokana na kampuni hiyo kufuta idara ya ulinzi na kukabidhi jukumu hilo kwa kampuni binafsi ya G4S, kunatokana na wao kugoma kusaini mikataba mipya wa kuajiriwa na kampuni hiyo mpya.

Ingawa uongozi wa mgodi wa Buzwagi haukuwa tayari kuzungumzia suala hilo licha ya awali, Meneja Rasilimali watu, Ivo Masanja kuahidi kulitolea ufafanuzi, Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Fadhil Nkurlu alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo.

Akizungumza ofisini kwake jana baada ya kuonana na walinzi hao, Nkurlu alisema Serikali ngazi ya wilaya na uongozi wa mgodi wamekubaliana walinzi hao waendelee kupata huduma zote muhimu ikiwamo chakula ambazo awali zilizuiwa. Alisema katika msafara wake uliohusisha maofisa kutoka idara ya kazi, alisikiliza maoni ya walinzi na uongozi wa mgodi na kubaini uhalali wa kampuni hiyo ya kuchimba madini wa kukabidhi jukumu la ulinzi kwa kampuni binafsi, lakini akaushauri uongozi kuendelea kuwahudumia waliokuwa watumishi hao hadi suala lao litakapopatiwa ufumbuzi kwenye baraza la ushuluhishi, Julai 10.

“Pia, tumekubaliana na hoja ya walinzi kuwa walikuwa na haki ya kugoma kusaini mkataba mipya kwa sababu suala hilo liko kwenye mchakato wa majadiliano yanayotarajiwa kukamilika Julai 10,” alisema Nkurlu.

Akizungumzia sakata la walinzi hao, Ofisa Uhamasishaji Taifa wa Chama cha Wafanyakazi wa Migodini na Nishati Tanzania (Numet), Shigela Aloyce alisema chama hicho kimekuwa kikifuatilia suala hilo bila mafanikio, kabla ya kuamua kulifikisha baraza la usuluhishi kwa uamuzi.

Mgodi huo ulikuwa na walinzi 107, kati yao, 52 walikubali mabadiliko na kusaini mkataba wa ajira kwenye kampuni mpya, 28 waligoma huku wengine 27 waliokuwa likizo nao wakijikuta vitambulisho vyao havina kazi.

Alipopigiwa simu jana ili kuzungumzia suala hilo, Msemaji wa Acacia, Nector Foya aliahidi kutoa majibu ifikapo saa 6:00 mchana ahadi ambayo hakuitekeleza hadi saa 11:00 jioni baada ya kudai kuwa yuko kwenye kikao.

LIPUMBA Akutana na Upinzani Mkali

$
0
0
Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba ameendelea kupata pigo baada ya madiwani 18 kati ya 21 wa Mkoa wa Dar es Salaam kuungana na wabunge 40 kumpinga.

Lipumba ndani ya Bunge anaungwa mkono na wabunge wawili, Magdalena Sakaya (Kaliua) na Maftah Nachuma (Mtwara Mjini) kati ya jumla ya wabunge wa CUF 42, kwa upande wa madiwani wa Mkoa wa Dar es Salaam Profesa Lipumba anaungwa mkono na madiwani wawili wa kata za Buguruni na Kiburugwa na mmoja wa viti maalumu.

Madiwani hao wameungana kupinga jitihada za Profesa Lipumba za kukubaliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa na uamuzi wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini ((Rita) wa kuisajili Bodi ya Wadhamini aliyoiunda na kumhakikishia kupata ruzuku ya Serikali.

Akitoa maazimio mbele ya wanahabari jana kwa niaba ya wenzake, diwani wa Kiwalani, Mussa Kafana alisema wanaunga mkono msimamo uliotolewa na Maalim Seif Juni 28, kupinga bodi ya Lipumba.

Kafana ambaye ni Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam, alisema Maalim Seif alikuwa sahihi kueleza umma sababu za kutokukubaliana na hatua ya Rita.

Alisema wanaazimia kuipinga Rita mbele ya Mahakama Kuu kwa kufungua kesi dhidi yake kwa mujibu wa kifungu cha 26 kwa kukiuka taratibu za Sheria za Wadhamini.

JE Una Tatizo la Nguvu za Kiume, Kukosa Hamu ya Tendo, Kushindwa Kurudia Tendo au Maumbile Madogo ya Uume?

$
0
0

JE, UNA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? SOMA HAPA 👇👇👇👇
Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, sio Tanzania tu bali duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo sio ugonjwa ila ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili.

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME HUSABABISHA MAMBO KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
@Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye kisukari kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @220,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kurudia tendo hata mara 3 bila kuchoka @130,000/=
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr.
Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no (+255)
0767447444 na 0714335378
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara kwa mtumiaji. Zimethibitishwa kiafya.

Hii ndio simulizi ya maisha ya Ebitoke

$
0
0

KOMEDIANI wa kike Bongo, Anastazia Exavery ‘Ebitoke’ (19) anayefanya vizuri zaidi kupitia mitandao ya kijamii alipitia mambo mengi ikiwemo kufanya kazi za ndani ‘house girl’ huku dada yake akiwa kikwazo cha yeye kutoboa kisanaa. Showbiz Xtra imefanya mahojiano maalum na Ebitoke kuhusu maisha yake kabla na baada ya kuwa staa.

MAISHA YAKE
Ebitoke anafunguka: “Mimi ni Mkerewe ila nimezaliwa Kijiji cha Kiuwani Wilaya ya MulebaVijijini mkoani Kagera.

ELIMU YAKE
“Nilianza darasa la kwanza mwaka 2006 ambapo nilimaliza darasa la saba mwaka 2013 katika Shule ya Msingi Kalema iliyoko Chato mkoani Geita. Baada ya kumaliza shule ya msingi sikufanikiwa kuendelea na masomo hivyo nikajikuta nikiwa sina hili wala lile pale kijijini kwetu.

UGUMU WA MAISHA WAMTIMSHA
“Nilipoona maisha yanazidi kuwa magumu pale kijijini, nilikimbilia jijini Mwanza kwa ajili ya kutafuta kazi za ndani, nilifanikiwa kupata kazi nikiwa na dada yangu.



ALIVYOFIKA DAR
“Nilifanya kazi zile za ndani kwa muda, baadaye mjomba wangu ambaye anaishi MbeziBeach (Dar), aliniita Dar ili nimsaidie kulea watoto wake na huo ndiyo ukawa mwanzo wa kulijua Jiji la Dar nikiamini huko ndiko ndoto yangu ya kuwa mwigizaji ingetimia.

ASEPA KWA MJOMBA’KE
“Baada ya kuona siwezi kutimiza ndoto zangu za kuigiza nikiwa kwa mjomba, mwaka 2015, niliondoka kwa mjomba na kwenda kwa rafiki yangu mmoja kule Kibaha, Pwani.

MAISHA YAMCHAPA, AKUMBUKA KWA MJOMBA
“Nikiwa kwa rafiki yangu, maisha yalinichapa sana kutokana na kuwa magumu kiasi cha kunifanya nikumbuke kwa mjomba. Ukizingatia sikufukuzwa wala sikuondoka kwa mabaya bali kwa lengo la kufikia malengo yangu.

AANZA KUUZA MGAHAWA
“Kutokana na ugumu wa maisha, nilianza kufanya kazi kwenye mgahawa kama Mama-lishe ili niweze kujikimu na kuepuka vishawishi vya hapa na pale.


ATAFUTIWA KAZI ZA NDANI TENA
“Nilifanikiwa kupata rafiki mwingine kule Kibaha aliyenitafutia kazi za ndani maeneo ya Mikocheni (Dar) ambapo nikafanya kazi miezi sita.

APATA SIMU NA KUJIUNGA MITANDAONI
“Baada ya kufanya kazi kwa muda, nilipata simu ya kisasa ambayo niliweza kujiunga kwenye mitandao ya kijamii.

AKUTANA NA TANGAZO

“Nikiwa naperuzi kwenye mitandao ya kijamii, nilikutana na tangazo kuwa Kampuni ya Timamu African Media inahitaji wasanii. Nikaamua kuomba nafasi, nikaitwa kwenye usaili, nikapita.

AAMSHA DUDE KWA BOSI WAKE

“Niliposhinda usaili, nikawa ninatakiwa niende mazoezini, lakini ikawa ni ngumu kwa bosi wangu kunikubalia. Niliamua kuliamsha dude kwa kusudi ili nifukuzwe. Nikawa nikipewa kazi na bosi ninakataa, hapo ndipo nikafuzwa. Nilifanya vile ili nipate sehemu ambayo inaweza kunipa nafasi ya kwenda kufanya mazoezi.

AISHI GETO

“Baada ya kufukuzwa kwa yule bosi wa Mikocheni, nilikwenda Mabibo kwa dada yangu aliyekuwa anaishi geto na wasichana wenzake wanne. Maisha hayakuwa mazuri kwa sababu tulimtegemea mtu mmoja aliyekuwa anafanya biashara.

AZINGUANA NA DADA YAKE

“Pale kwa dada nilipata nafasi ya kufanya mazoezi, lakini dada yangu hakuwa anapenda. Alikuwa akinigombeza kila siku.

APATA KAZI BAA

“Nilipoona dada yangu hapendi niigize, niliamua kuhamia kwa rafiki yangu mwingine maeneo ya Tegeta (Dar) niliyekuwa ninaigiza naye. Alinitafutia kazi ya baa ambayo ilikuwa hainibani kwani nilipata nafasi ya kwenda kufanya mazoezi.

ALIVYOSHINDWA KAZI YA BAA

“Nilifanya kazi ya baa kwa miezi mitatu, nikaacha kwa sababu wanaume wengi walikuwa wananisumbua halafu wenzangu karibu wote walikuwa wanakwenda kwa mabwana zao. Nikaona ninaweza kushawishika.

KUWAPIKIA WAJENZI

“Niliondoka pale na kwenda kukaa kwa dada yangu kwenye nyumba nyingine ya mjomba. Nikapata kibarua cha kuwa ninawapikia wajenzi halafu wananilipa shilingi elfu tano kwa siku. Ilikuwa ni kazi ngumu sana kupika ugali wa watu 12.

APITA KWENYE USAILI TENA

“Baadaye Timamu Media walifanya usaili wa mtu ambaye anaweza kuigiza kishamba, nikafanikiwa kupita, kila mtu akasema ninaiweza vizuri nafasi hiyo.

APEWA JINA LA EBITOKE

“Nikiwa mazoezini bosi wangu wa Timamu African Media, Timoth Kachumia aliniona ninavyocheza, ikabidi anipe jina la Ebitoke.

SINI ZA USHAMBA ZAMSUMBUA

“Mwanzoni nilisumbuka sana kuzoea kwani kuvaa nguo zile za kishamba na kupaka mafuta mengi ilikuwa inanipa shida, lakini sasa nimezoea.

MASHABIKI WAMPOKEA

“Kilichonifanya niendelee kuipenda sini (kipande cha kuigiza) ya ushamba ni vile mashabiki walivyonipokea na kunikubali.

TIMAMU WAMPA NAFASI

“Kabla sijatoka, kampuni ilianza kuwatoa Mkali Wenu, Mama Ashura, Mjeshi kisha mimi ndiyo nafuata, hapo ndipo nikapata nafasi ya kuwa Ebitoke.

MAFANIKIO YAKE

“Sijapata mafanikio makubwa kihivyo kwa sababu ndiyo nimeanza, ila ninaweza kujihudumia baadhi ya vitu na nimefahamika. Mashabiki wangu wategemee mambo mazuri kutoka kwangu na kama kuna wadau na makampuni wanakaribishwa.

TRCA Imetoa masharti 4 kwa mitandao simu kuanzia leo Julai 6

$
0
0


Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA imetoa masharti na vigezo ambavyo mtoa huduma za mawasiliano anatakiwa kuzingatia ikiwa ni siku chache tangu Mamlaka hiyo kutoa angalizo kwa watoa huduma baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wadau wa mawasiliano kukerwa na huduma za matangazo ya watoa huduma.


Akizungumza na Waandishi wa Habari leo July 6, 2017 Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Mhandisi James Kilaba amesema utaratibu huo ni kinyume cha matakwa ya Kanuni za Huduma za Ziada (VAS Regulations) za 2015 na Kanuni za Kumlinda Mtumiaji (Consumer Protection Regulations) za mwaka 2011.


Aidha, TCRA imesema kuwa, kwa mujibu wa Kanuni za Huduma za Ziada, baadhi ya masharti na vigezo ambavyo mtoa huduma (service provider) anatakiwa kuzingatia katika kutoa huduma ni pamoja na:-


1: Watioa huduma wanatakiwa kutoa taarifa kwa ukamilifu, (kwa Kiingereza na, au kwa Kiswahili), kuhusu huduma lengwa kwa kuendana na wakati na kwa lugha rahisi nay a kueleweka.


2: Watoa huduma wanatakiwa kuzingatia matakwa ya Sheria na Kanuni za Kumlinda Mtumiaji wa Huduma za Mwaka 2001.


3: Watoa huduma wanaweza kutoa matangazo na taratibu za kujiunga na huduma mbalimbali za ziada wakati:


-wa kumjibu mteja anapouliza salio la muda wa maongezi;
-mteja anapopokea taarifa baada ya kuongeza salio;
-mteja anapoingia kwenye orodha ya huduma za mtoa huduma.

4: Mtoa huduma haruhusiwi kutoa matangazo mengine yoyote kwa njia za mawasiliano ya simu au kwa njia yoyote ya kielektroniki bila kuzingatia vigezo vilivyowekwa kisheria.

Aidha TCRA imewataka watoa huduma wote kusitisha mara moja utoaji wa matangazo kwenye hduma za mawasiliano yasiyozingatia Kanuni za Huduma za Ziada (VAS Regulations) za mwaka 2015 kuanzia July 6, 2017.

Jaji aliyeomba kustaafu, alitajwa kwenye Escrow

$
0
0

Jaji wa Mahakama Kuu, Prof. Ruhangisa aliyeomba kustaafu kabla ya muda ni miongoni mwa wanaotuhumiwa kufaidika na fedha za Tegeta Escrow.



Leo Julai 6, Rais Magufuli ameridhia maombi ya kustaafu mapema kwa Jaji wa Mahakama Kuu Tanzania, Prof. John Eudes Ruhangisa, alikua Kanda ya Shinyanga.

SOMA Hii Story Unaweza Ukajifunza Kitu Katika Maisha

$
0
0

Kijana mmoja alisafiri kwa meli na rafiki zake,
wakiwa katikati ya safari yao meli ilianza
kuzama. Watu wengi pamoja na rafiki wa yule
kijana walikufa maji wakati wanajaribu kujiokoa
kwa kuogelea, lakini yule kijana alifanikiwa
kushika ubao ulioelea majini akaanza kuelea nao,
maji yalimpeleka hadi kisiwa cha mbali sana
ambako hakukuwa na watu wala wanyama
isipokuwa wadudu tu! Alifika ufukweni amechoka
sana na asiyeamini tukio lililotokea, akaishi huko
kwa kula matunda. Aliweza kujenga ka-kibanda
kwa shida sana maana hakuwa na shoka wala
panga, hatimaye akaanza maisha mapya.
Aliishi muda mrefu kisiwani na tayari alishazoea
mazingira yale ya shida japo shida haizoeleki.
Mara zote nyakati za jioni aliwasha moto kwa
kupekecha vijiti. Siku moja kama kawaida yake
aliwasha moto nje karibu na kibanda chake, aliota
moto muda mrefu hatimaye akapitiwa na usingizi.
Alilala hapo hapo hadi usiku wa manane
aliposhtushwa na joto kali lisilo la kawaida.
Kumbe moto ulishika nyasi za kibanda chake na
kibanda chote kikaungua moto.Alilia sana na
kumlaani sana Mungu kwa mateso hayo akisema
"Hivi Mungu nimekukosea nini mpaka unitese
hivi? Pamoja na shida zote hizi bado
unaniongezea shida nyingine, umeteketeza makazi
yangu ilhali nimejenga kwa shida, Hukuridhika
kunitenga mbali na familia yangu nilipoishi kwa
raha? Hukuridhika kuwaua rafiki zangu wote
baharini? Kwanini Mungu umekuwa mkatili hivi?
Bora nife tuu maana nimeshachoshwa na hizi
shida!" akaendelea kulalamika na kumlaani Mungu
hadi kukapambazuka.
Ilipofika asubuhi aliiona meli ikija kwa mbali
kuelekea alipo, alishangaa maana hakuna meli
yoyote inayoweza kwenda kisiwa kile labda kama
imepotea njia. Meli ilipofika ufukweni yule kijana
akaifuata, alienda moja kwa moja hadi kwa
kapteni.Kapteni akamwambia "tuliona moto mkali
sana usiku tukahisi ni meli inawaka moto
tukasema tuje ili tutoe msaada..kwa kweli
tumetembea masaa mengi sana hadi kufika hapa,
mshukuru Mungu maana ametumia moto kutuleta
hapa" yule kijana kusikia hivyo alilia sana,
akajilaumu kwa jinsi alivyo mnung'unikia Mungu.
Akaelewa kuwa Mungu ana njia nyingi za kuleta
msaada kwa mtu. Akapiga magoti akatubu huku
akimshukuru Mungu.

MKATABA wa TICTS na TPA Wafumiliwa....Sasa TICTS itailipa Serikali Dola Milioini 14 badala ya Dola..........

$
0
0
TPA, TICTS wasaini mkataba mpya, Majadiliano yachukua miezi 7 kufikia muafaka.

Mamlaka ya usimamizi wa bandari Tanzania TPA na kampuni ya kimataifa ya kuhudumia makasha Tanzania TICTS zimesaini mkataba mpya baada ya majadiliano yaliyochukua miezi saba kufikiwa kwa makubaliano.

Akizungumza katika hafla hiyo waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amesema mkataba huu mpya umeondoa masharti hasi ambayo yalikuwa yanabana maslahi kwa Tanzania, ambapo kwa sasa TICTS watalipa kodi ya mwaka ya dola milioni 14 kutoka dola milioni saba za kwenye mkataba wa awali, kodi ambayo itakuwa ikiongezeka kwa asilimia tatu kila mwaka.

Vile vile kodi ya makasha itakuwa dola ishirini kutoka dola kumi na tatu za kwenye mkataba wa awali ambayo pia itakuwa ikiongezeka kila mwaka kwa asilimia 4.

800x800_560ccc8b7a464.jpg

Kwa upande wake waziri wa katiba na sheria Profesa Paramagamba Kabudi, ambaye ameshuhudia utiwaji saini wa mkataba huo mpya, amesema mkataba huu ni miongoni mwa mikataba iliyosaidia kujua kwamba kuna umuhimu wa kupitiwa kwa mikataba mingi ambayo imeonekana kutokuwa na manufaa kwa Tanzania na kutoa rai kwa wenye dhamana nchini.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya agizo la rais Dkt John Pombe Magufuli alipotembelea bandari ya Dar es Salaam na kutaka kupitiwa kwa mkataba huo wa TPA na TICTS. Aidha mkataba huu unasainiwa huku Bunge likiwa limepitisha sheria ya kupitia mikataba yote yenye masharti hasi, sheria ambayo inasubiri kusainiwa na Raisi ili kuanza kufanya kazi.

JUA Majina ya Kiume ya Kikristo yenye Hasara na Faida Katika Ndoa

$
0
0

Majina yenye faida katika Ndoa na Ndoa zao hudumu pia ni haya:

Charles
Kelvin
Ian
Moses
Lucas
Alex
Robert

Majina yenye hasara katika Ndoa na kama ukiolewa nao jua imekula Kwako kimoja ni haya:

Frank
George
Kenneth
Benjamin
John
Walter
James
Nawasilisha na ' alamsiki ' nyote.

HATIMAYE Utabiri wa Afande SELE Juu ya Saida Karoli Umetimia.........

$
0
0
Hatimaye unabii wa Afande Sele juu ya Saida Karoli umetimia.

“Mimi nilijua Saida Karoli ni mwanamuziki bora wa kike Afrika, mimi nafahamu sio Tanzania.Saida Karoli yupo juu ya dada yangu Jide, Saida Karoli anajua sijui kuliko Vanessa Mdee anakuwa msanii leo hii.

Unamuacha Saida Karoli unamuamini Vanessa Mdee ambaye anamuiga Beyonce sijui anamuiga Rihanna mimi nasema huu ni upumbavu wa aina yake, kwaiyo leo Vanessa Mdee anakuwa juu kuliko Saida Karoli ni Uchawi”. Hayo ni maneno ya Mfalme wa Afande Sele ambapo aliyazungumza Tarehe 23/4/2017 nyumbani kwake Mkoani Morogoro pale ambapo Team Tizneez tulifika na kupata fursa ya kuzungumza mengi yahusuyo muziki.
Baada ya kuweka mahojiano haya hoja nyingi zilizuka kutoka kwa mashabiki, wachambuzi wa muziki na wadau mbalimbali wa muziki.
Wapo ambao hawakuficha hisia zao na kuzionyesha hadharani kupinga kauli ya Afande Sele Iliyosema “Mimi nilijua Saida Karoli ni mwanamuziki bora wa kike Afrika, mimi nafahamu sio Tanzania.Saida Karoli yupo juu ya dada yangu Jide, Saida Karoli anajua sijui kuliko Vanessa Mdee anakuwa msanii leo hii.

Wengine walifika mbali na hoja ya kusema Afande Sele anachuki tena avuliwe ufalme wake.
Jambo hili sisi kama Team Tizneez lilitushangaza mno, kwa maana ni Tanzania pekee msanii akisema jambo Fulani kuhusu msanii mwingine huonekana anachuki, inaonyesha ni jinsi gani wengi hawajui maana ya neno mtazamo. (Maoni)

Miongoni mwa wale waliopinga kauli ya Afande Sele hawakuwa na hoja madhubuti za kuikosoa kauli hiyo bali walishinikizwa na mihemko na mahaba yao binasfsi kwa wasanii walioguswa na kauli ya Afande Sele.
Ingawa ukimsikiliza kwa makini Afande Sele alitete hoja yake ya ubora wa Saida Karoli.

Hivi karibuni umeibuka wimbo mpya wimbo unaozungumza ubora wa Saida Karoli, wimbo ambao awali Afande Sele aligusia kibwagizo tu ikawa shida na gumzo.

Wahenga wanasema atakayemlipa mpiga zumari ndiye atakayechagua wimbo. Safari hii Clouds Media Group wamemchagua Saida Karoli.
Mbiu zinasikika kila kona kuidhihilishia hadhira juu ya ubora, uwezo,ukongwe na mchango wa Saida Karoli katika Sanaa yetu.
Bado tunaishi juu ya maneno ya Afande Sele na kama angerudia Mtazamo hakika kungekuwa na mistari kuhusu Saida Karoli.

Zidume fikra sahihi za Mfalme Afande Sele.

By Mr gentleman

TANZANIA yapanda Viwango vya Mpira FIFA

$
0
0
Timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imepanda kwa nafasi 25 hadi nafasi 114 kutoka nafasi ya 139 kati ya mataifa 211 katika viwango vya ubora wa soka duniani vilivyotolewa na Shirikisho la Soka Duniani FIFA leo Julai 6, 2017.


Katika siku za hivi karibuni timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imekuwa ikicheza katika kiwango bora kabisa kilichoiwezesha timu hiyo kushinda katika michezo yake ikiwemo dhidi ya Burundi na Botswana katika mchezo wa kirafiki, Malawi pamoja na Afrika Kusini maarufu kama Bafana Bafana katika michezo ya COSAFA inayoendelea nchini Afrika Kusini.

Katika viwango hivyo vya mwezi Julai timu ya taifa ya Ujerumani inashika nafasi ya kwanza, Brazili ikishika nafasi ya pili, na timu ya Argentina ikishika nafasi ya tatu.

Mataifa mengine ambayo timu zao zipo katika kumi bora nikama zifuatazo

4.Ureno

5.Uswisi

6.Poland

7.Chile

8.Colombia

9.Ufaransa

Na nafasi ya kumi inashikiliwa na timu ya taifa ya Ubelgiji

Barani Afrika Misri inaongoza ikiwa nafasi ya 24 ikifuatiwa na Senegal katika nafasi ya 27, Congo DR nafasi ya 28, Tunisia nafasi ya 34, Cameroon nafasi ya 36, Nigeria nafasi ya 39 huku Burkina Faso akiangukia nafasi ya 44.

Kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, Uganda imeporomoka nafasi tatu mpaka kufikia 74, ikifuatiwa na Kenya kuanguka nafasi 10 mpaka 84, Tanzania imepanda katika viwango hivyo kwa nafasi 25 juu mpaka kufikia 114, Burundi ikipanda nafasi 27 na kufikia 121, Rwanda imepanda nafasi moja na kufikia 127, Ethiopia ikidondoka kwa nafasi 11 na kufikia 136.

IKWIRIRI: Jeshi la Polisi Lawaua Watuhumiwa Wawili wa Uhalifu Kibiti

$
0
0
Dar es Salaam. Jeshi la Polisi nchini limewaua watu wawili wanaodaiwa kufanya mauaji katika Wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji, mkoani Pwani.

Akielezea tukio hilo jana (Alhamisi Julai 6) , Mkuu wa Operesheni Maalumu za Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Liberatus Sabas amesema tukio hilo lilitokea jana saa nne usiku katika msitu wa Ngomboroni Kata ya Ikwiriri, Wilaya ya Ikwiriri.

Wahalifu hao waliuawa na askari wa operesheni maalumu wakiwa katika doria za ufuatiliaji wahalifu sugu wanaojihusisha na mauaji yanayoendelea katika kanda hiyo ya kipolisi.

Alisema askari wakiwa na mtuhumiwa mmoja muhimu anayeshiriki katika mauaji hayo ambaye alikamatwa, alikubali kwenda kuwaonyesha polisi mahali ambapo ni maficho ya wenzake.

“Baada ya kufika eneo la msitu wa Ngomboroni kikundi cha watu wanaokadiriwa kufikia watano walikurupuka kutoka kwenye kichaka na kuanza kukimbia ndipo polisi kwa tahadhari kubwa walianzisha mashambulizi na kufanikiwa kumjeruhi mhalifu mmoja kwa risasi, katika mashambulizi hayo mtuhumiwa aliyekuwa mkononi mwa polisi naye alijaribu kutoroka na hivyo kupelekea kumjeruhi kwa risasi hivyo idadi yao kufikia wawili,” amesema.

Ameongeza; “majeruhi hao wawili walifariki dunia njiani wakati wakipelekwa hospitali kwa matibabu kutokana na kuvuja damu nyingi iliyosababishwa na majeraha ya risasi waliyoyapata. Miili ya marehemu imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.”

Kamishna Sabas amesema katika tukio hilo wamefanikiwa kupokonya silaha mbili aina ya SMG na Shotgun moja pamoja na risasi tisa.

Kamishina Sabas amewataka wananchi kutoa taarifa zitakazowezesha kupatikana kwa wahalifu wengine waliosalia na kwamba zawadi nono bado ipo pale pale na itatolewa kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa sahihi kuhusiana na wahalifu wanaojihusisha na mauaji katika kanda maalumu ya Rufiji.

Install APP ya Blog Hii ya UDAKU SPECIAL Kwenye Simu yako Kutoka Google Play Kusoma Habari Kirahisi

$
0
0
Download  Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE 


Au Kama Unayotayari Bonyeza HAPA Ku Update Uweze Kupata Ikiwa na Muonekano Mpya

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika

Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo..

anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa  PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp/Calls +255 710 279 458
 Call+255 710 279 458

Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

HAKIMU Kesi ya Lema Ajitoa, Kisa ‘Ushosti’ na Mke wa Lema.....

$
0
0
HAKIMU wa Mahakama ya Wilaya Arusha, Patricia Kisinda amejitoa kwenye kesi namba 441/2016 ya uchochezi dhidi ya Rais John Magufuli inayowakabili Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Akizungumza jana mahakamani hapo, Hakimu Kisinda alisema amekubali ombi la Wakili wa Serikali, Sabina Silayo la kumwomba ajitoe kutokana na urafiki na mke wa ndoa wa Lema.

“Ili kutendeka kwa haki pande zote mbili kwenye kesi hii, nakubaliana na ombi lililotolewa mahakamani hapa na najitoa, lakini haki ya kukata rufaa ipo wazi kwa asiyeridhika na uamuzi huu wa kujitoa,” alisema hakimu Kisinda.

Kabla ya kujitoa, Wakili Silayo aliomba hakimu ajitoe kwa sababu upande wa Jamhuri hawana imani naye, hivyo bora ajiondoe sababu ana uhusiano na mke wa ndoa wa mshitakiwa Lema na ushahidi wanao na halina pingamizi, “hivyo hatutatendewa haki, itakuwa busara hakimu akijiondoa”.

Akijibu ombi hilo, Wakili wa mshitakiwa, Sheck Mfinanga alisema Lema anaumwa na alikuwa anarejea Arusha akitokea bungeni Dodoma na alipofika Dar es Salaam alijisikia vibaya na kuwasilisha nakala ya hati ya matibabu, huku akidai nakala halisi atawasilisha.

Pia alipinga Hakimu Kisinda kujitoa kwa madai kuwa Watanzania wote ni marafiki na ndugu na sababu lazima ipimwe uzito na waangalie sababu za hakimu kujitoa, hivyo hoja hizo hazina mashiko.

“Ningefurahi niletewe ushahidi wa urafiki wa mke wa Lema na hakimu huyu, ili tuone kama kuna ukweli, maana hoja hii haina mashiko,” alidai Mfinanga. Hata hivyo, Hakimu Kisinda alipanga kesi hiyo Agosti 2, mwaka huu.

ALI KIBA na Baraka The Prince Hapatoshi....Ali Kiba Afunguka Kuhusu Akili za Kitoto za Baraka The Prince

$
0
0
Muimbaji Alikiba ambaye hivi karibuni ametangazwa na RockStar4000 kuwa mmoja kati ya wamiliki wa label hiyo, amefunguka kwa kudai kuwa msanii wa label hiyo, Baraka The Prince ana akili za kitoto ndio maana kuna maadhi ya mambo yanaibuka kwamba haelewani na baadhi ya wasanii wenzake.


Hit maker huyo wa Aje amesema hayo baada ya kuulizwa kwamba kwa sasa hawaonekani kuwa karibu na Baraka kama zamani huku tetesi zikidai kwamba ukaribu wao umevunjika baada ya Alikiba kuwa karibu na Ommy Dimpoz.

“Mimi nadhani ni utoto tu, nadhani ni umri tu lakini Baraka yupo vizuri, ni mtu anayesikiliza na ana rekebishika. Muda mwingine labda umri ndio unampeleka lakini muda mwingine mtoto akifanya jambo unamwambia,” Alikiba alikiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM. “Ni mdogo wetu tutamwelimisha na sidhani kama anamchukia Ommy Dimpoz labda ni maneno tu ya mtaani,”

Kwa upande wa Ommy Dimpoz ambaye alitambulisha wimbo wake mpya Cheche, amedai yeye hajawahi kugombana na Baraka na wala hana tatizo na mtu yeyote.

Muimbaji hapo jana amesainiwa mkataba na label ya RockStar4000 na kuungana na Baraka The Prince pamoja na Lady Jay Dee ambao wapo kwa muda mrefu.

JE ni Utumuaji Vibaya wa 'MAMLAKA' Tanzania?

$
0
0
Kukamatwa kwa Mbunge wa upinzani nchini Tanzania Halima Mdee kwa madai ya kumtusi Rais John Magufuli kumeshutumiwa pakubwa huku wakosoaji wakisema kuwa ni ishara ya hivi karibuni kwamba serikali inatumia mamlaka yake vibaya ili kukandamiza uhuru wa kujieleza.

Msemaji wa chama cha upinzani CHADEMA, Tumaini Makene ameambia BBC kwamba chama hicho kitakwenda mahakamani dhidi ya hatua ya mkuu wa Wilaya ambae aliagiza kukamatwa kwake pamoja na makamishna wengine wote wanaokiuka sheria.

Bi Mdee ni mwanachama wa CHADEMA, chama kikuu cha upinzani katika Taifa hilo la Afrika Mashariki akipanda gari la polisi


Mbunge wa Kawe, Halima Mdee aliyewekwa rumande kwa amri ya Mkuu wa Wilaya
Alituhumiwa na Ally Hapi, mkuu wa Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam kwa kumtusi Rais na kuchochea ghasia baada ya kudai kwamba Rais anafikiri kwamba matamshi yake ni Sheria na kwamba siku moja atawaagiza Watanzania kukaa utupu.

Muungano wa mabadiliko na uwazi unaongozwa na Zitto Kabwe ulisema kuwa hatua hiyo ni uendelevu wa utumiaji mbaya wa mamlaka.

”Sheria inayompatia mkuu huyo wa Wilaya uwezo wa kuagiza kukamatwa kwa mtu, hailingani na sababu ya kukamatwa kwa bi Mdee,” alisema.



Watu kadhaa wamekamatwa katika siku za nyuma kwa kuchapisha ujumbe katika mitandao ya kijamii ambayo mamlaka inadai inaingilia kisiasa.

Mamlaka inaamini kwamba inafuata sheria na kuchukua hatua za kuhakikisha kwamba hakuna ”migogoro yoyote miongoni mwa wananchi” nchini Tanzania.

Bwana Magufuli alishinda uchaguzi wa urais wa mwaka 2015 na licha ya kukosolewa na upinzani pamoja na makundi ya wanaharakati anaungwa mkono na Watanzania wengi.

HT @ BBC Swahili

Wanaozani ni Kiki Wasubirie Ndoa Yangu na Ebitoke- Ben Pol

$
0
0

Mkali wa Miondoko ya RNB Bongo Ben Pol ambaye yupo kwenye penzi zito la Mwanadada Mchekeshaji Ebitoke amesema kuwa wanaodhani kuwa mapenzi ya wawili hao ni kiki wasubiri kuona ndoa imefungwa.

Hayo ameyasema Jana wakati wa show ya Miaka kumi  na tanoya Msanii Mkongwe Saida Kalori,Escape one Jijini Dar es Salaam.


 

Yusuf Manji Kibanoni ,Serikali Imekamilisha Upelelezi Kesi ya Dawa za Kulevya dhidi yake

$
0
0

Upande wa Jamhuri  Umekamilisha  upelelezi  dhidi ya mfanyabiashara Yusuf Manji kuhusu tuhuma za Matumizi ya Dawa za Kulevya.


Awali Wakili wa utetezi, Alex Mgongolwa alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi, Cyprian Mkeha, kwamba mshtakiwa ni mgonjwa na amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

"Mheshimiwa mteja wangu ameshindwa kuja mahakamani kusikiliza kesi yake kwa sababu mgonjwa na amelazwa katika Hospitali ya Muhimbili," alidai Mgongolwa mahakamani hapo.

Kabla ya kutolewa taarifa ya ugonjwa wa mshtakiwa huyo, Wakili wa Serikali Mkuu, Timon Vitalis, alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kwamba upande wa Jamhuri unaomba tarehe nyingine ya kusikiliza maelezo ya awali.

Hakimu Mkeha alisema kwa kuwa mshtakiwa ni mgonjwa, kesi hiyo itaanza kusikilizwa Agosti 10, mwaka huu.

Katika kesi ya msingi, Manji ambaye pia ni Diwani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kata ya Mbagala Kuu jijini Dar es Salaam na mfanyabiashara maarufu nchini, anakabiliwa na mashtaka ya kutumia dawa za kulevya.

Ilidaiwa kuwa kati ya Februari 6 na 9 mwaka huu, eneo la Upanga Sea View jijini Dar es Salaam, Manji alitumia dawa za kulevya  aina ya heroin.

Mshtakiwa alikana mashtaka hayo na yuko nje kwa dhamana.

Hata hivyo, wakati Manji akiwa nje kwa dhamana katika kesi hiyo ya tuhuma za utumiaji dawa za kulevya, mfanyabiashara huyo alikosa dhamana juzi katika kesi nyingine inayohusiana na uhujumu uchumi.

Katika kesi hiyo ambayo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ilihamishia shughuli zake Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikolazwa Manji kwenye Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Manji na wenzake watatu walikosa dhamana baada ya upande wa Jamhuri kuwasilisha hati ya kuzuia dhamana kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), akiomba washtakiwa wasipewe dhamana kwa usalama wao na maslahi ya taifa.

Pia DPP alieleza sababu nyingine ya Manji kunyimwa dhamana kuwa ni mahakama hiyo kutokuwa na mamlaka ya kushughulikia dhamana dhidi ya kesi hiyo. Washtakiwa wengine ni Ofisa Rasilimaliwatu Deogratias Kisinda (28), Mtunza Stoo, Abdallah Sangey (46) na Mtunza Stoo msaidizi, Thobias Fwele (43).

Ilidaiwa katika shtaka la kwanza kuwa Juni 30, mwaka huu eneo la Chang'ombe Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, Manji na wenzake walikutwa na askari polisi wakiwa na mabunda (majora) 35 ya vitambaa vinavyotengezea sare za JWTZ vyenye thamani ya Sh. milioni 192.5 na kwamba vilipatikana isivyo halali.

Katika shtaka la pili, ilidaiwa kuwa Julai Mosi, mwaka huu eneo la Chang'ombe 'A' Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, washtakiwa wote kwa pamoja walikutwa na askari polisi wakiwa na mabando nane ya sare za JWTZ zenye thamani ya Sh. milioni 44.

Upande huo wa Jamhuri uliendelea kudai kuwa, Juni 30, mwaka huu eneo la tukio la kwanza, washtakiwa walikutwa na mhuri wa JWTZ uliokuwa na maandishi 'Mkuu wa Kikosi 121 Kikosi cha Jeshi JWTZ' bila kuwa na uhalali, kitendo ambacho kinahatarisha usalama wa nchi.

Katika shtaka la nne, ilidaiwa kuwa siku ya tukio la tatu, washtakiwa wote kwa pamoja walikutwa na mhuri wenye maandishi "Kamanda Kikosi 834 KJ Makutupora Dodoma" bila uhalali kitendo ambacho kinahatarisha usalama wa nchi.

Katika shtaka la tano, ilidaiwa siku ya tukio la tatu na la nne, mshtakiwa alikutwa na mhuri wenye maandishi "Comanding Officer 835 KJ Mgambo P.O BOX 224 Korogwe" bila kuwa na uhalali kitendo ambacho kinahatarisha usalama wa nchi.

Ilidaiwa katika shtaka la sita, Julai Mosi, mwaka huu eneo la Chang'ombe 'A', washtakiwa wote walikutwa na namba za gari zenye usajili wa SU 383 iliyopatikana isivyo halali.

Katika shtaka la saba, eneo la tukio la sita, washtakiwa walikutwa na namba za gari zenye namba ya usajili SM 8573 iliyopatikana isivyo halali.

Kwa mujibu wa mashtaka hayo yaliyofunguliwa chini ya Sheria ya Uhujumu Uchumi na Usalama wa Taifa, washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi yao.

Hakimu Mkazi Huruma Shaidi alisema kesi hiyo itatajwa Julai 19 na washtakiwa watatu walipelekwa mahabusu ya Keko huku Manji akiwa chini ya ulinzi wa polisi wodini hapo.
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images