Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live

DIAMOND Azungumzia Zilipoishia Headphone za Chibu Beats....Adai Jina lilileta Matatizo...

0
0
Baada ya ukimya wa muda mrefu tangu msanii wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz atangaze ujio wa bidhaa zake za headphone ‘Chibu Beats’, msanii huyo ameelezea kinachochelewesha.


Muimbaji huyo ameiambia XXL ya Clouds FM kuwa bidhaa hizo zimechelewa kutokana na mchakato wa usajili wa jina.

“Katika usajili wa Chibu Beats jina lilileta matatizo kidogo, ilikwamisha hapo kwa sababu neno beats mtu kashalisajili dunia nzima mtu mwingine asilitumie neno la beats, siunajua ni la Dre. Kwa hiyo tunaweka namna nyingine ambayo itakuwa nzuri, zitatoka zimeshakuwa tayari mpaka sampo, tumeshasikiliza ni fresh sound hatari” amesema Diamond.

UGANDA yapiga Marufuku Kufuga Kucha na Kujipodoa

0
0
Kama ulikuwa una ndoto za kufanya kazi nchini Uganda hasa kwa watoto wa kike wenye kupenda kujipodoa na kuvaa nguo zinazoonyesha maumbile basi jua hautaweza kudumu wala kupata kazi nchini humo.



Hii ni kutokana na sheria mpya iliyopo, Kwa mujibu wa mtandao wa edaily wa Kenya, umeripoti kuwa serikali ya Uganda imepiga marufuku uvaaji wa nguo fupi makazini, upakaji make up uliozidi, kubandika kucha ndefu na bandia, kuweka nywele bandia na kuzipaka rangi, kuvaa nguo inayobana kama vile Tshirt na magauni pamoja na kuvaa vivalio.

Miaka 2013 nchi hiyo ilitunga sheria ya kukataza kuvaa nguo fupi, sheria ambayo ilizua mijadala nchini humo na sehemu zingine.

Na Laila Sued

NGUVU Kuu 7 Alizonazo Mwanamke Hizi Hapa...Wengi Hawajui Kuhusu Nguvu Hizi......

0
0
Nguvu kuu 7 alizonazo mwanamke

1. Uwezo wa kuona na kugundua ya mbeleni (anawezakuona kisichosemwa au kitakachokuja).               Anatumia mlango wa sita wa fahamu unaoitwa EPS
2. Ananguvu ktk kinywa chake kuliko nguvu za mwili kwa mwanaume. Athari za kutotumia kinywa       chake vema ni kubwa zaidi.
3. Nguvu na uwezo wa kuendeleza uumbaji
4. Nguvu ya ushawishi
5. Nguvu na uwezo wa kustahimili. Kuvumilia. Kubeba mazito.
6. Nguvu na uwezo wa kujadili bei (bargaining power)
7. Uwezo wa kuwaathiri watoto (positively or negatively)

ILI NGUVU HII ITENDE KAZI
1. Tumia vema kinywa chako
2. Tumia vema ushawishi wako

TABIA Mpya Inayokera Mjini ya Wanawake Kujipiga Picha Ovyo Ovyo.......

0
0
Aisee hii tabia inanikera sana, tabia ya kupiga piga picha kila wakati wahanga wa kubwa wa hii tabia ni wanawake, unaenda na mtu sehemu  ile mmefika tu unaona mdada ametoa kasimu kake anaanza kupiga picha, sio kama anapiga picha moja, atapiga picha kama 20 katika eneo moja na wakati huo huo.

Huwa najiuliza hii mipicha yote huwa mnafanyia kazi gani? Wengine kila wakati wa kula wanapiga picha, kwenye simu kuna mapicha ya aina moja kibao hii tabia mwanzoni alikuwa nayo girl wangu ameacha baada ya kumchana kuwa hizo mambo sizizimikii, sasa imebaki kwa watu ambao nafanya nao kazi na watu wangu wa karibu mpaka imekuwa kero, wakiwa ofisini picha, wakienda kula picha. Napataga hasira natamani nichukue visimu vyao nivitupilie mbali.

Kama una tabia hii acha mara moja haipendezi kabisa, au kama unapiga picha piga moja au mbili inatosha sio unapiga picha kama 20 mpaka unasahau kilichokuleta, inakera sana!

JACK Wolper Aweweseka Juu ya Mpenzi Wake Mpya.....

0
0

KWA kuonyesha ni kumpa dongo mpenzi wake wa zamani, staa mwenye mvuto wa kipekee Bongo Muvi, Jacqueline Wolper amesema kuwa katu hawezi kumuweka hadharani mpenzi wake mpya kwa kuogopa kuibiwa tena na wazungu.

Staa huyo alituma dongo hilo kupitia mtandao wake wa Snapchat, ambapo alikuwa akisema kuwa, anatamani sana kumuweka hadharani mpenzi wake huyo mpya lakini anaogopa kunyakuliwa tena na wakware wa kizungu kama alivyofanyiwa kwa mpenzi wake aliyepita ambaye ni mwanamuziki wa Bongo Fleva.

Star Mix hili lilimtafuta Wolper ambaye baada ya kubanwa kutaka kujua jina la bwana huyo aliyenaye alianza kwa kuangua kicheko na kusema kuwa kuna wakati mwingine mtu anazungumza kufurahisha watu wacheke lakini si kwamba kuna mtu kweli kwa sasa.

“Jamani kuna kipindi mtu unawafanya watu wafurahi na kucheka sio kila unachozungumza mtu kiwe cha kweli.”

SERIKALI Yaendelea Kumkaba Koo Freeman Mbowe....

0
0

Serikali imetoa siku 30 kwa wawekezaji 50 waliopewa maeneo ya kujenga viwanda na kushindwa kuvijenga, kuwasilisha mipango ya ujenzi vinginevyo watanyang’anywa.

Serikali imetoa orodha ya watu hao na taasisi zilizopewa maeneo katika eneo la Weruweru karibu na kiwanda cha Kilimanjaro Machine Tools, akiwamo mbunge wa Hai (Chadema), Freeman Mbowe.

Katika orodha hiyo, Mbowe ambaye pia ni mwenyekiti wa Taifa wa Chadema anaonekana kumiliki viwanja viwili; kimoja kikiwa na ukubwa wa hekta 1.88 na kingine na hekta 2.17.

Akizungumzia uamuzi huo mpya wa Serikali na sababu za kushindwa kuendeleza eneo hilo kwa miaka 13 tangu yeye na wenzake walipomilikishwa mwaka 2004, Mbowe alisema alikuwa hajapata taarifa hizo, lakini kwa vile yuko njiani kuelekea mkoani Kilimanjaro akifika atafuatilia.

Ataja sababu

Mwanasiasa huyo alisema Serikali inapaswa kulaumiwa kwa kutofikisha miundombinu muhimu katika eneo hilo ikiwamo umeme na badala kutarajia wawekezaji wabebe gharama hizo.

Aliongeza kuwa ni vigumu wawekezaji kufanya hivyo na ni lazima soko lijulikane kwanza na pawepo na mazingira rafiki ya uwekezaji ndipo wawekeze.

“Huwezi tu kukurupuka kujenga kiwanda, ni lazima ujue utazalisha bidhaa gani na soko liko wapi.
Serikali bado haijalinda viwanda vya ndani na kusababisha ushindani usio sawa wa bidhaa kutoka nje,” alisema mbunge huyo ambaye pia ni kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni.

Mbowe aliongeza kuwa ni lazima ufanyike utafiti wa kina hasa katika kipindi hiki ambacho uwezo wa wananchi kununua bidhaa unazidi kushuka siku hadi siku.

“Miundombinu hilo eneo hakuna, kuna ushindani usio sawa na bidhaa za nje, masoko na pia uhakika wa umeme. Zote hizi ni changamoto zinazohitaji utatuzi wa Serikali. Unajengaje kiwanda katikati ya changamoto hizo?” alihoji.

Agizo la DC

Akizungumza na baadhi ya wawekezaji hao juzi, mkuu wa Wilaya ya Hai, Gelasius Byakanwa alisema mipango ya ujenzi wa viwanda katika eneo hilo iwe imemfikia kabla ya Agosti 10.

“Mlikuja kuomba mkisema ninyi ni wawekezaji wa viwanda ambao pengine mliidhinishwa na TIC (Kituo cha Uwekezaji Tanzania). Kuanzia mwaka 2004 mpaka leo 2017 kwa nini hatuvioni viwanda pale?” alihoji na kuongeza;

“Nimeamua kuwaita si jukumu la kisheria kwamba nitawaita watu wanaomiliki maeneo na kuwauliza kwa nini hamyaendelezi. Si jukumu langu ningeweza kuchukua hatua.”

“Hamjaonyesha nia ya kujenga viwanda. Nataka niwatangazie wawekezaji wengine kuwa Hai lipo eneo la kujenga viwanda ila liko mikononi mwa watu ambao hawapo tayari kujenga viwanda.”

Mkuu huyo wa wilaya alisema ndani ya muda wa mwezi mmoja kuanzia juzi, wawekezaji hao wawe wamewasilisha mipango ya kujenga viwanda, vinginevyo watanyang’anywa maeneo hayo.

“Msipofanya hivyo, tutamuomba mheshimiwa Rais (John Magufuli) abatilishe miliki zenu wapewe watu wengine watakaokuja kujenga viwanda ili Hai nayo iwe ya viwanda,” alisema Byakanwa.

Alisema, “Wamiliki wengi wa viwanja hawasomi masharti ya umilikaji. Wengi waliomilikishwa viwanja miaka ya 1980 kwa sasa hawana ardhi wana makaratasi tu, umiliki wao ulishamalizika na hawajahuisha.”

Mmoja wa wawekezaji katika kikao hicho, Peter Naya alisema alikwama kujenga kiwanda kutokana na gharama za kuvuta umeme kuwa juu na kwamba aliambiwa ni zaidi ya Sh56 milioni.

“Niliwasiliana na Tanesco (Shirika la Umeme Tanzania) wakasema lile eneo halina kipaumbele tugharamie wenyewe. Nimetafuta gharama inaenda hadi Sh50 milioni,” alisema mwekezaji huyo.

Kwa mujibu wa mwekezaji huyo, ili kuweza kukusanya mtaji wa kujenga kiwanda cha kati inachukua kati ya miaka mitano na 10, na kusisitiza kuwa changamoto kubwa ni umeme na upatikanaji wa mtaji.

Misukosuko ya Mbowe

Endapo Mbowe atashindwa kuwasilisha mipango ya ujenzi wa viwanda katika eneo hilo na Serikali kumnyang’anya litakuwa ni pigo lake la nne tangu awamu ya tano iingie madarakani.

Pigo la kwanza lilikuwa la kunyang’anywa jengo la Club Billicanas jijini Dar es Salaam ambalo alilitumia kama ukumbi wa starehe na baadaye lilivunjwa.

Kubomolewa kwa jengo hilo lililokuwapo katika barabara ya Mkwepu na Indira Gandhi kulitokana na mgogoro wa umiliki kati yake na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

Mbali na tukio hilo, Januari 21, Serikali wilayani Hai ilimpa siku 14 kulipa Sh13.5 milioni alizokuwa akidaiwa kama kodi ya huduma ya hoteli yake ya Aishi Protea.

Ukiacha misukosuko hiyo, mwezi Februari alikuwa miongoni mwa watu waliotajwa kujihusisha na dawa za kulevya na kutakiwa kuripoti kituo kikuu cha polisi jijini Dar es Salaam.

Haikuishia hapo, ila mwezi Juni, Serikali iling’oa miundombinu ya umwagiliaji katika shamba lake la kilimo cha kisasa cha umwagiliaji (green house) lililopo Machame wilayani Hai, kwa madai ya kuharibu mazingira.

 Mbali na kung’oa miundombinu hiyo, pia Mamlaka ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (Nemc), ilimtoza faini ya Sh18 kwa kuendesha kilimo ndani ya mita 60 kutoka kilipo chanzo cha maji.

Sheria Mpya za Madini Mfupa mgumu kwa wawekezaji

0
0

Wakati Serikali ikiendelea kutafuta njia za kudhibiti kikamilifu rasilimali za nchi baada ya kupitisha sheria mpya ya maboresho ya Sheria ya Madini iliyopendekeza mambo kadhaa, wawekezaji katika sekta hiyo wameanza kutishika na kuanza kujiondoa.

Baada ya kupitishwa kwa sheria hiyo, tayari mwekezaji mmoja kutoka Australia, Ian Middlemas kupitia kampuni yake ya Cradle Resources, amekosa dili la dola 55 milioni za Marekani (Sh121 bilioni) kupitia mradi wa uchimbaji wa madini ya niobium Panda Hill, uliopo nchini.

Kufuatia hatua hiyo, wataalamu kadhaa wa masuala ya uchumi wamesema ni lazima sheria hizo zitakuwa zimewashtua wawekezaji.

Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Utafiti wa Kupunguza Umaskini (Repoa), Dk Abel Kinyondo alisema watakimbia kwa muda mfupi tu.

Profesa Haji Semboja wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema kutaibuka baadhi ya kampuni ambazo zitafanya hivyo ili kutishia Serikali ili ichanganyikiwe na kubadilisha uamuzi wake.

JE Una Tatizo la Nguvu za Kiume , kukosa Hamu ya Tendo, Kushindwa Kurudia Tendo au Maumbile Madogo ya Uume?

0
0

JE, UNA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? SOMA HAPA 👇👇👇👇
Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, sio Tanzania tu bali duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo sio ugonjwa ila ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili.

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME HUSABABISHA MAMBO KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
@Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye kisukari kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @220,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kurudia tendo hata mara 3 bila kuchoka @130,000/=
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr.
Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no (+255)
0767447444 na 0714335378
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara kwa mtumiaji. Zimethibitishwa kiafya.

Mdee Kusota Lupango mpaka Juma Tatu

0
0

Mbunge wa Jimbo la Kawe Jijini Dar es Salaam Halima Mdee alikamatwa na jeshi la polisi hivi karibuni, kwa kile kinachodaiwa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi kuwa alitoa maneo ya uchochezi yenye kumtusi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli katika hotuba yake aliyoitoa kwa waandishi wa Habari Julai 4.

Ambapo Mkuu wa Wilaya kwa mujibu wa sheria aliagiza Mbunge huyo ashikiliwe na ahojiwe kwa masaa 48 yaliyotajwa kisheria na kumpa mamlaka Mkuu wa Wilaya kufanya hivyo.


Siku ambayo Mbunge huyo inabidi aachiwe na Jeshi la Polisi imeangukia kwenye sikukuu ya Saba Saba, jambo ambalo linapelekea Mbunge huyo kuendelea kusota rumande mpaka siku ya Jumatatu.

HAMISA Amchokonoa Zari, Ajiita 'Mama Dee...'

0
0
Mrembo Hamisa Mobetto anazidi kuzichukua headlines tangu ilipojulikana kuwa ni mjamzito mpaka ujauzito wake kuhusishwa na Diamond Platnumz mpenzi na mzazi mwenzake na Zari The BossLady na raundi hii amepost picha akiwa Nairobi na kuandika Mama Dee..?

Wanasema mwenye macho haambiwi tazama..

WAZIRI Mwakyembe Alivyomuacha mkewe 'ICU' akaenda kwa Saida Karoli

0
0
Usiku wa July 7 2017 mwimbaji wa mziki wa asili, Saida Karoli alikutana na mashabiki wake kwenye miaka 15 ya kusimama kuanguka na kuamka tena ya Saida Karoli ambapo wasanii mbalimbali, watu maarufu pamoja na mashabiki walijumuika naye Escape one Jijini DSM huku mgeni rasmi akiwa waziri wa Sanaa Mh Harisson Mwakyembe.

Kwenye kusalimia watu Mh. Mwakyembe alisema kuwa mkewe alikuwa na hali mbaya hospitali ICU ila kwa kuheshimu mchango wa Saida Karoli kwenye muziki wa Tanzania yeye na mkewe waliona ni vyema ahudhurie kwenye tamasha hilo.

MAMA Kiba Atoa 'Povu' Zito Kwa Binti Anayedai Kuzaa na Alikiba

0
0
SKENDO ‘hot’ inayomhusu staa wa Muziki wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ‘Ali Kiba’ ya kudaiwa kuzaa na msichana mmoja kutoka Kenya aliyefahamika kwa jina la Nuru Hatim kisha kumtimua, imechukua sura mpya baada ya mama wa msanii huyo kuzungumza na gazeti hili na kutema cheche, Ijumaa linakujuza.

Mwishoni mwa wiki iliyopita, Nuru alitua Bongo akitokea nchini Kenya na kwenda kwenye Kituo cha Polisi cha Msimbazi na pia Ubalozi wa Kenya nchini Tanzania kwa ajili ya kuomba msaada wa kumpata Kiba sambamba na kuomba msaada wa kisheria akidai amezaa na staa huyo kisha kuachwa kwenye mataa.

Baada ya hayo yote kujiri, waandishi wetu walifunga safari hadi nyumbani kwa wazazi wa Kiba na kufanikiwa kuzungumza na mama yake kuhusiana na mjukuu wake huyo mpya kutoka Kenya. Mahojiano yalikuwa hivi:

IJUMAA: Mama bila shaka umesikia juu ya huyu dada ambaye amekuja nchini na kusema amezaa na mwanao lakini amemtelekeza. Una lipi la kuongea?

MAMA KIBA: Nimesoma hiyo habari kwenye gazeti leo (Jumanne), wakati natoka kwenye shughuli zangu lakini nilikuwa sijazisikia kabisa.

IJUMAA: Haya, kwa kuwa umezisikia utachukua hatua gani ili kuhakikisha huyo dada na mwanaye wanapata msaada?

MAMA KIBA: Hakuna hatua nitakazochukua, ingekuwa Ali mwenyewe kaniambia kuwa huyo ni mwanaye, ningeweza kufanya lolote. Lakini katika hili siwezi kufanya lolote kwa sababu kwanza sina uhakika kuwa ni mwanaye na ni jambo ambalo halinihusu.

IJUMAA: Halikuhusu kwa sababu hujashirikishwa na mwanao ama halikuhusu kivipi? Hebu fafanua kidogo.

MAMA KIBA: Kwa sababu Ali hajaniambia kitu kama hicho. Unajua masuala haya ya wanawake kuibuka na kusema wamezaa na hawa watoto huwa yanajitokeza mara kadhaa.

Hata kwa Abdu (Abdu Kiba), alishawahi kuja mwanadada sijui anatokea Dubai sijui wapi na kusema amezaa naye lakini haikuwa kweli, ni kama alikuwa ametengenezwa tu ili kufanikisha vitu ambavyo hakuna anayeweza kuvielewa ama kuvielezea vikaeleweka.

IJUMAA: Sawa mama. Lakini Kiba ana watoto kadhaa ambao wamekuwa wakiandikwa na kusemwa kwenye vyombo vya habari, vipi kwa upande wako umewahi kuwasikia ama kuwaona?

MAMA KIBA: Ni mtoto mmoja tu aitwaye Samir ndiye nina taarifa naye sahihi. Huyu mimi ndiye nilimdai baada ya kumuona kwenye Laptop ya Ali wakati ananionyesha picha za shoo aliyoifanya Paris.

Baada ya kumuona moyo ulinilipuka maana mtoto huyo alikuwa anafanana na Ali wakati yupo mdogo. Ikabidi nimdai na nikaletewa.

Watoto wengine nimekuwa nikiwasikia tu, kuna mkubwa ana miaka nane wa kike na mwingine mdogo, lakini sijawa na taarifa nao sawasawa.

IJUMAA: Na kuhusu mama zao na hao watoto pamoja na wapenzi wengine ambao amekuwa akitoka nao, kuna hata mmoja ambaye amewahi kukutambulisha kuwa atamuoa?

MAMA KIBA: Hapana. Kwanza wanangu sijawalea kwenye maadili mabaya kiasi hicho kiasi kwamba wanihalalishie zinaa. Kwa hiyo sijatambulishwa mwanamke yeyote yule.

IJUMAA: Vipi kuhusu Jokate?

MAMA KIBA: Amefanya nini?

IJUMAA: Hujawahi kufahamu kuwa anatoka kimapenzi na mwanao?

MAMA KIBA: Ninachofahamu ni rafiki yake na walikuwa wanashirikiana kwenye kazi, basi!

Baada ya cheche hizo za mama, waandishi wetu pia walitaka kujua mwanadada Jokate Mwegelo aliyewahi kuwa na uhusiano na Kiba hadi kufikia hatua ya kusema atamzalia mtoto, ana lipi la kusema juu ya kuibuka kwa Nuru na kudai amezaa na X-boyfriend wake.

Katika hali ya kushangaza, Jokate alitoa povu kamainavyoonekana kwenye mahojiano haya hapa chini.

Ijumaa: Kuna madai ya mpenzi wako, Ali Kiba kuzaa na binti kutoka Mombasa, unaliongeleaje hilo?

Jokate: Inanihusu nini sasa mimi?

Ijumaa: Wewe kama uliyekuwa mpenzi wa Ali Kiba.

Jokate: Mwandikeni yeye (Ali Kiba) na huyo mwenye mtoto wake.

Ijumaa: Nilijua povu litatoka lakini ungesema lolote basi jamani.

Jokate: Sitoi povu nakueleza tu. Msinihusishe kwenye vitu vichafuchafu.

MTANZANIA Anayeigiza Kama 'YESU' Asimulia yanayomkuta

0
0
Msanii wa kuigiza Ayoub ambaye katika tamthilia ya 'Jambo na vijambo' anaigiza kama Yesu amefunguka na kusema kuigiza kama Yesu katika tamthilia hiyo inamletea shida kwa baadhi ya watu ambao siyo waelewa.

Ayoub alisema hayo alipokuwa akihojiwa katika kipindi cha eNewz na kudai kuwa kuna wakati hata majirani waligombana na mkewe na hawakutaka kusemeshana naye kwa kuwa mumewe anamuuigiza 'Yesu'

"Hata mke wangu kishagombana na watu kwa sababu tu ya mimi kuigiza kama Yesu, wanamwambia mumewe anamgeza mtume wetu Yesu wetu kwa hiyo usinisemeshe, mke wangu akaja kunipa mimi hizo habari nikabaki kucheka tu, lakini katika ule u serious zaidi sijaona kama kumetokea tatizo kubwa mimi ni muislam lakini yapo makanisa yananiita nikawasaidie kutengeneza kazi ya sanaa baada ya kuniona kwenye kile kipindi, kwa hiyo wenyewe wakristo ambao wamezama kwenye imani kuniona naigiza kama Yesu hawafikirii vibaya sababu hata nachoigiza mle ndani kinaendana na yale aliyokuwa anatenda Yesu, hivyo huwezi kuona amefanya jambo lolote baya yule muhusika wa Yesu ambaye ni mimi" alisema Ayoub

Mbali na hilo Ayoub anasema watu ambao wanakuwa na mtazamo hasi juu ya uhusika wake kama Yesu ni wachache sana ukifananisha na wale ambao wanafurahia kwani mambo mengi ambayo anafanya muhusika ni mambo ya msingi.

"Hata ukiangalia kwenye ukurasa wa facebook wa EATV tukiweka post akitokea mtu ambaye atazungumza vibaya juu ya 'character' Yesu wapo watu wengine wanakuja kumsema sana na kumuelewesha vizuri juu ya uhusika wa Yesu, kwa hiyo utaona watu wanaozungumza uzuri wanashinda kutokana na mazuri ambayo muhusika amefanya" alisema Ayoub

Kipindi cha Jambo na Vijambo kinaruka kila Jumapili kuanzia saa 12:30 jioni katika ting'a namba moja kwa vijana EATV

Ijue Mipaka ya RC/DC Kuamuru MTU Kuwekwa Rumande Kwa Saa 48

0
0

Tangu kuingia madarakani kwa Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli ambaye amekuja na kasi ya kutumbua na kurekebisha mfumo wa ufanyaji kazi kwa watumishi wa serikali, baadhi ya wateule wake wameonekana wakishindana katika kuweka watu rumande kwa saa 48, watu wanaowatuhumu kufanya makosa mbalimbali, hasa viongozi wa kisiasa wa vyama vya upinzani.

Matukio haya yamekuwa yakizua malalamiko mengi kutoka vyama vya upinzani na wanaharakati nchini na manung’uniko ya chini kwa chini kutoka kwa wananchi wanaofatilia siasa za nchi hii.

Pengine wengi wanatoa manung’uniko hayo kwa kutumia akili ya kawaida tu ya kibinadamu (common sense) ambayo wanadhani ingetumika kabla hata ya kutoa amri husika.

Ifuatayo ni tafsiri ya Sheria inayompa mamlaka Mkuu wa Mkoa na Wilaya kutoa amri ya mtu yeyote kukamatwa na kuwekwa rumande kwa muda usiozidi saa 48. Pamoja na mamlaka hayo, pia Sheria hii imeeleza mipaka ya Mkuu wa Mkoa na Wilaya juu ya amri hiyo. Soma zaidi upate kuielewa:

Ibara ya Saba (7)

Mamlaka ya Mkuu wa Mkoa

(1) Kwa malengo ya kutimiza majukumu yake kwa ufanisi kwa mujibu wa Sheria hii, Mkuu wa Mkoa anayo Mamlaka ya kuamrisha mtu yeyote akamatwe ambaye (Mkuu wa Mkoa) anaona kuwa amefanya kosa lolote ambalo litamfanya mtu akamatwe na kushtakiwa.

(2) Pamoja na yaliyoelezwa kwenye kifungu cha (1), endapo Mkuu wa Mkoa atakuwa na sababu za kuamini kuwa mtu yeyote ana uwezekano wa kusababisha uvunjifu wa amani au kuondoa utulivu kwenye jamii, au kufanya jambo lolote ambalo kwa namna yoyote linaweza kusababisha uvunjifu wa amani au kusababisha vurugu, na vurugu au uvunjifu huo wa amani hauwezi kuzuilika kwa njia nyingine yoyote zaidi ya kumuweka kizuizini anayesababisha hali hiyo, anaweza kumuamuru ofisa wa Polisi yeyote kwa maneno au kwa maandishi – amkamate mtu huyo.

(3) Mtu aliyewekwa kizuizini kutokana na mamlaka yaliyotolewa kwenye ibara hii, mapema iwezekanavyo, na kwa namna yoyote ile katika kipindi kisichozidi saa arobaini na nane tangu kukamatwa kwake, anatakiwa kufikishwa mahakamani ili asomewe mashtaka yanayomkabili kwa mujibu wa Sheria kwa makosa anayotuhumiwa.

(4) Kama mtu aliyekamatwa kwa amri ya Mkuu wa Mkoa kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa na Ibara hii hajafikishwa mahakamani na Mkuu wa Mkoa ndani ya saa arobaini na nane tangu kukamatwa kwake, anatakiwa, muda huo wa saa arobaini na nane utapokwisha, aachiwe huru na asikamatwe tena kwa amri ya Mkuu wa Mkoa huyo akimtuhumu tena mtu huyo kwa kosa kama hilo.

(5) Iwapo Mkuu wa Mkoa ataamrisha kukamatwa kwa mtu yeyote kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa na ibara hii, (Mkuu wa Mkoa huyo) anatakiwa wakati anatoa amri hiyo au mapema iwezekanavyo baada ya kutoa amri hiyo, atoe taarifa ya maandishi akieleza sababu zake za kumkamata au kutoa amri ya kukamatwa kwa mtu husika; na anatakiwa kuwasilisha nakala ya sababu hizo, (au hiyo) kwa Hakimu katika muda ambao mtu huyo anafikishwa mahakamani, au, iwapo mtu huyo atakuwa ameachwa huru kabla hajafikishwa mahakamani, (nakala hii iwasilishwe) mapema iwezekanavyo baada ya kuachiwa kwa mtu huyo; na kwa kuondoa mashaka, Hakimu atakuwa na mamlaka ya kuamuru kuachiwa na kuwekwa huru kwa mtu yeyote aliyefikishwa mahakamani bila kutolewa sababu rasmi za kukamatwa kwake, na kuamuru amri hiyo (ya Mkuu wa Mkoa) ifutwe kimaandishi na Mkuu wa Mkoa mwenyewe au na mtu mwingine kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huyo.

(6) Pamoja na yaliyoelezwa kwenye kifungu cha (5), kuwasilishwa kwa nakala ya sababu ya kutolewa kwa amri hiyo kwa mujibu wa mamlaka yaliyotolewa na ibara hii hakumuamrishi Hakimu kusimamia/kutekeleza amri hiyo ya Mkuu wa Mkoa bali Hakimu atamtaka (Mkuu wa Mkoa) atoe nakala hiyo chini ya kiapo.

(7) Hakimu ambaye mtuhumiwa huyo atapelekwa mbeye yake kutokana na kutumika kwa mamlaka hii, anaweza, atakapoona inafaa, kumuweka rumande mtu huyo mpaka kukamilika kwa uchunguzi kwa mujibu wa ibara ya 79 ya Sheria ya Makosa ya jinai bila chuki dhidi yake au anaweza kwa mamlaka ya Mahakama, kumpa dhamana mtuhumiwa huyo kama akiona inafaa.

(8) Kila Mkuu wa Mkoa na kila polisi au mtu yeyote aliyehusika kutekeleza amri hiyo ya Mkuu wa Mkoa kama alivyopewa kwenye ibara hii anatakiwa pia kutekeleza amri yoyote itakayotolewa na Hakimu kwa mujibu wa ibara hii endapo ataamua kumuachia huru mtu huyo aliyekamatwa kwa kutumia mamlaka yaliyotolewa na ibara hii, na kushindwa au kudharau kutekeleza amri hiyo atakuwa amefanya kosa la kuidharau Mahakama na ataadhibiwa kisheria kwa mujibu wa ibara ya 114 ya Sheria ya Adhabu.

(9) Endapo Mkuu wa Mkoa atatumia nguvu aliyopewa na ibara hii vibaya, kwa kutumia vibaya mamlaka ya ofisi yake, hivyo basi yeye, pamoja na mtu yeyote yule aliyehusika kumpa Mkuu wa Mkoa taarifa zilizosababisha matumizi mabaya ya madaraka, atakuwa na hatia ya kufanya kosa hili na anaweza kushtakiwa kwa mujibu wa ibara ya 96 ya Sheria ya Adhabu.



Ibara yaKumi na tano (15)

Mamlaka ya Mkuu wa Wilaya

(1) Kwa malengo ya kutimiza majukumu yake kwa ufanisi kwa mujibu wa Sheria hii, Mkuu wa Wilaya anayo mamlaka ya kuamrisha mtu yeyote akamatwe ambaye anaona kuwa amefanya kosa lolote ambalo litamfanya mtu akamatwe na kushtakiwa.

(2) Pamoja na yaliyoelezwa kwenye kifungu cha (1), endapo Mkuu wa Wilaya atakuwa na sababu za kuamini kuwa mtu yeyote ana uwezekano wa kusababisha uvunjifu wa amani au kuondoa utulivu kwenye jamii, au kufanya jambo lolote ambalo kwa namna yoyote linaweza kusababisha uvunjifu wa amani au kusababisha vurugu, na vurugu au uvunjifu huo wa amani hauwezi kuzuilika kwa njia nyingine yoyote zaidi ya kumuweka kizuizini anayesababisha hali hiyo, anaweza kumuamuru ofisa wa Polisi yeyote kwa maneno au kwa maandishi – amkamate mtu huyo.

(3) Mtu aliyewekwa kizuizini kutokana na mamlaka yaliyotolewa kwenye ibara hii, mapema iwezekanavyo, na kwa namna yoyote ile katika kipindi kisichozidi saa arobaini na nane tangu kukamatwa kwake, anatakiwa kufikishwa mahakamani ili asomewe mashtaka kwa mujibu wa makosa anayotuhumiwa kuyafanya.

(4) Kama mtu aliyekamatwa kwa amri ya Mkuu wa Wilaya kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa na Ibara hii hajafikishwa mahakamani na Mkuu wa Wilaya ndani ya saa arobaini na nane tangu kukamatwa kwake, anatakiwa, muda huo wa saa arobaini na nane utapokwisha, aachiwe huru na asikamatwe tena kwa amri ya Mkuu wa Wilaya huyo akimtuhumu tena mtu huyo kwa kosa kama hilo.

(5) Iwapo Mkuu wa Wilaya ataamrisha kukamatwa kwa mtu yeyote kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa na ibara hii, (Mkuu wa Wilaya huyo) anatakiwa wakati anatoa amri hiyo au mapema iwezekanavyo baada ya kutoa amri hiyo, atoe taarifa ya maandishi akieleza sababu zake za kumkamata au kutoa amri ya kukamatwa kwa mtu husika; na anatakiwa kuwasilisha nakala ya sababu hizo, (au hiyo) kwa Hakimu katika muda ambao mtu huyo anafikishwa mahakamani, au, iwapo mtu huyo atakuwa ameachwa huru kabla hajafikishwa mahakamani, (nakala hii iwasilishwe) mapema iwezekanavyo baada ya kuachiwa kwa mtu huyo; na kwa kuondoa mashaka, Hakimu atakuwa na mamlaka ya kuamuru kuachiwa na kuwekwa huru kwa mtu yeyote aliyefikishwa mahakamani bila kutolewa sababu rasmi za kukamatwa kwake, na kuamuru amri hiyo (ya Mkuu wa Wilaya) ifutwe kimaandishi na Mkuu wa Wilaya mwenyewe au na mtu mwingine kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya huyo.

(6) Pamoja na yaliyoelezwa kwenye kifungu cha (5), kuwasilishwa kwa nakala ya sababu ya kutolewa kwa amri hiyo kwa mujibu wa mamlaka yaliyotolewa na ibara hii hakumuamrishi Hakimu kusimamia/kutekeleza amri hiyo ya Mkuu wa Wilaya bali Hakimu atamtaka (Mkuu wa Wilaya) atoe nakala hiyo chini ya kiapo.

(7) Hakimu ambaye mtuhumiwa huyo atapelekwa mbeye yake kutokana na kutumika kwa mamlaka hii, anaweza, atakapoona inafaa, kumuweka rumande mtu huyo mpaka kukamilika kwa uchunguzi kwa mujibu wa ibara ya 79 ya Sheria ya Makosa ya jinai bila chuki dhidi yake au anaweza kwa mamlaka ya Mahakama, kumpa dhamana mtuhumiwa huyo kama akiona inafaa.

(8) Kila Mkuu wa Wilaya na kila polisi au mtu yeyote aliyehusika kutekeleza amri hiyo ya Mkuu wa Wilaya kama alivyopewa kwenye ibara hii anatakiwa pia kutekeleza amri yoyote itakayotolewa na Hakimu kwa mujibu wa ibara hii endapo ataamua kumuachia huru mtu huyo aliyekamatwa kwa kutumia mamlaka yaliyotolewa na ibara hii, na kushindwa au kudharau kutekeleza amri hiyo atakuwa amefanya kosa la kuidharau Mahakama na ataadhibiwa kisheria kwa mujibu wa ibara ya 114 ya Sheria ya Adhabu.

(9) Endapo Mkuu wa Wilaya atatumia nguvu aliyopewa na ibara hii vibaya, kwa kutumia vibaya mamlaka ya ofisi yake, hivyo basi yeye, pamoja na mtu yeyote yule aliyehusika kumpa Mkuu wa Wilaya taarifa zilizosababisha matumizi mabaya ya madaraka, atakuwa na hatia ya kufanya kosa hili na anaweza kushtakiwa kwa mujibu wa ibara ya 96 ya Sheria ya Adhabu.

INAUMA SANA...Hatimaye Dogo Mshabiki wa Mpira Aliyekuwa anaumwa Kansa Afariki Dunia

0
0
Shabiki wa klabu ya Sunderland wa umri wa miaka sita Bradley Lowery, ambaye tatizo lake la kiafya liligusa nyoyo za wengi amefariki dunia.
Bardlay alikuwa anaugua ugonjwa ambao wa Kiingereza hufahamika kama neuroblastoma – aina nadra ya saratani – tangu alipokuwa na umri wa miezi 18.



Bradley alifanywa kuwa kibonzo-nembo wa klabu hiyo na akaunda urafiki wa karibu na mshambuliaji wa klabu hiyo Jermain Defoe.
Aidha, aliongoza wachezaji wa England kuingia uwanjani Wembley wakati wa mechi ya kufuzu kwa Kombe la Dunia dhidi ya Lithuania.
Kifo chake kimethibitishwa na wazazi wake kwenye mitandao ya kijamii.
“Kijana wetu mkakamavu ameenda kuwa na malaika leo.



“Alikuwa shujaa wetu na alipigana sana lakini alihitajika kwingine. Hatuna maneno ya kueleza jinsi tulivyohuzunishwa na kifo chake.”
Bradley alipewa matibabu lakini saratani yake ikaibuka tena mwaka jana.


Wahisani walichangisha zaidi ya £700,000 kulipia matibabu yake New York mwaka 2016, lakini madaktari waligundua kwamba saratani yake ilikuwa imeenea sana na hangeweza kutibiwa.
Wazazi wake Gemma na Carl, kutoka Blackhall Colliery, Durham, waliambia Desemba kwamba alikuwa amesalia na “miezi kadha tu ya kuishi”.
Miezi minne baadaye, walifahamishwa kwamba jaribio la mwisho kabisa la kumtibu lilikuwa limefeli.

SHOCKING..JAY Z na Mama Yake Waushtua Ulimwengu Kwa Kuanika Ukweli Huu

0
0

SIKU kadhaa zilizopita, nguli wa Muziki wa Hip Hop duniani, Shawn Carter ‘Jay Z’ aliachia albamu yake mpya, 4:44 kupitia mtandao anaoumiliki wa Tidal, ikiwa ni albamu yake ya kumi na tatu na kuvunja ukimya mrefu wa tangu mwaka 2013 alipotoa albamu yake ya Magna Carta Holly Grail.


Katika albamu hiyo, Jay Z ambaye pia ni mume wa staa Beyonce Knowles, wakiwa wamejaaliwa kupata watoto watatu, Blue Ivy na wadogo zake mapacha, Rumi na Sir amefanya jambo ambalo ama kwa hakika limeushangaza ulimwengu (shocking).
Muda mfupi baada ya kuachiwa kwake, gumzo kubwa liliibuka kuhusu mashairi yaliyomo kwenye moja kati ya nyimbo kumi zilizopo kwenye albamu hiyo. Wimbo wa Smile ambao Jay Z amemshirikisha mama yake mzazi, Gloria Carter ndiyo ulioibua utata kutokana na mashairi yake kubeba ujumbe mzito ambao pengine hakuna ambaye alitegemea kuusikia.

“…Mama had four kids, but she’s a lesbian, had to pretend so long that she’s a thespian…” (Mama ana watoto wanne lakini ni msagaji, kwa kipindi kirefu amekuwa akijifanya ni mwigizaji wa tamthiliya…).
Haya ni miongoni mwa mashairi yaliyoibua gumzo kubwa dunia nzima, hasa kutokana na ukweli kwamba mama yake Jay Z, Gloria pia anao watoto wanne, akiwemo Jay Z mwenyewe ambaye ni wa mwisho. Watoto wengine ni kaka yake Jay Z, Eric na dada zake, Andrea na Michelle.
Kwa lugha nyepesi, baada ya tetesi za chini kwa chini za muda mrefu, Jay Z amevunja ukimya na kutangaza hadharani kwamba mama yake anajihusisha na mapenzi ya jinsia moja.
“…Don’t matter to me if it’s a him or her, I just wanna see you smile through all the hate,” (Kwangu haijalishi kama ni mwanaume au mwanamke, ninachotaka ni kukuona ukitabasamu katikati ya chuki) Jay Z anazidi kufunguka kwenye wimbo huo.

Yote tisa, kumi ni kipande cha mwisho ambapo Gloria anasikika kwa sauti yake mwenyewe, akikiri kwamba amekuwa akiishi kwenye maisha ya kujificha gizani kwa muda mrefu akihofia kusema hadharani kwamba yeye ni msagaji lakini muda umefika wa kutabasamu na kuwa huru kwa vile alivyo.

“Living in the shadows. Can you imagine what kind of life it is to live? In the shadows people see you as happy and free. Because that’s what you want them to see… But life is short, and it’s time to be free. Love who you love, because life isn’t guaranteed,”
(Kuishi gizani. Unaweza kuvuta picha ni aina gani ya maisha? Gizani watu wanakuona una furaha na upo huru. Kwa sababu hicho ndicho ulichotaka wakione… Lakini maisha ni mafupi, ni wakati wa kuwa huru. Mpende yule unayempenda kwa sababu maisha ni kigeugeu.)

Wimbo wa Smile unakuja kumaliza ubishi uliokuwepo kwa muda mrefu, tangu mwaka 2013 tetesi zilipoanza kuzagaa kwamba mama yake Jay Z, alikuwa akijihusisha na mapenzi ya jinsi moja na aliyekuwa mwalimu ambaye kwa sasa anafanya kazi kwenye mfuko wa kusaidia jamii wa Jay Z na mama yake, The Shawn Carter Foundation, Dania Diaz.
Smile umethibitisha kwamba Gloria na Dania wamekuwa wapenzi kwa muda mrefu sasa, huku kukiwa na picha zinazomuonesha mwanadada huyo akiwa na Jay Z. Gloria na Dania walianza kuandamwa na waandishi wa habari za uchunguzi baada ya kuwepo kwa ukaribu unaotia shaka kati yao ambapo sasa Gloria mwenyewe ameamua kuuweka wazi.
Wawili hao, kwa mujibu wa Jarida la Enstar, wamekuwa wakizisaidia jamii za watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsi moja (LGBTQ- Lesbian, Gay, Bisexual, Transgender and Queer) jijini New York.
Yote kwa yote, ujasiri waliouonesha Jay Z na mama yake, Gloria umewashangaza watu wengi mno duniani. Kwa tamaduni za Kiafrika, mtoto kuzungumzia ishu kama hiyo ya mzazi wake, ni utovu mkubwa wa nidhamu lakini Jay Z ameweza, na inaonesha walikubaliana ndiyo maana hata studio waliingia pamoja.
Kwa tamaduni za wenzetu, vitendo vya mapenzi ya jinsia moja vinaonekana kuwa vya kawaida na vinakubalika na baadhi ya mataifa, hasa Ulaya yamepitisha sheria za kutambua ndoa za jinsia moja. Kwa Tanzania, uhusiano wa namna hiyo HAUKUBALIKI kisheria wala kijamii.

IMEANDIKWA NA HASHIM | IJUMAA

MANJI Aondolewa Muhimbili Usiku Apelekwa Keko, Adaiwa Kuchukuliwa Chini ya Ulinzi Mkali

0
0
Mfanyabiashara maarufu, Yusuf Manji, ameondolewa chini ya ulinzi mkali wa Polisi katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), alikokuwa akipatiwa matibabu na kupelekwa Gereza la Keko, lililopo jijini Dar es salaam.

Taarifa za uhakika na ambazo zimethibitishwa na wakili wake, zinaeleza kuwa, Manji, ambaye anakabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi na Usalama wa Taifa ambayo kimsingi hayana dhamana, aliondolewa hospitalini hapo juzi saa moja jioni.

Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali ndani ya gereza la Keko na ndani ya Taasisi ya JKCI, vililithibitishia Mtanzania jumamosi juu ya taarifa hizo za Manji.

"Ni kweli Manji walimwondoa jana usiku, alipelekwa moja kwa moja Gereza la Keko", alisema mmoja wa watoa taarifa.

Katika kuthibitisha hilo Mtanzania Ijumaa jana lilifika JKCI, lakini halikuwaona askari magereza waliokuwapo hapo kwa ajili ya kutoa ulinzi kwa siku zote ambazo Manji alikuwa amelazwa.

Gazeti hili lilimtafuta kwa njia ya simu Mkurugenzi Mkuu wa JKCI, Profesa Mohamed Janab, ambaye hata hivyo alikataa kuthibitisha taarifa hizo, kwa madai kuwa, hawezi kutoa taarifa za mgonjwa kwa kuwa si utaratibu.

"Si utaratibu wetu kutoa taarifa za mgonjwa... labda nikuambie tu jambo la msingi na kubwa sisi leo tupo katika viwanja vya Sabasaba, tumewapima watu takribani 420 hivi magonjwa ya moyo na wapo ambao walikuwa hawajui wanaumwa na tumewaambiwa waanze dawa", alisema Profesa Janabi.

Mtanzania lilimtafuta kwa njia ya simu mmoja wa mawakili wa Manji, Alex Mgongolwa, ambaye alisema alikuwa hospitali akimuuguza mama yake, hivyo hakuwa na taarifa hizo.

Wakili Mgongolwa alimtaka mwandishi wa gazeti hili kumtafuta Wakili Hudson Ndusyepo, ambaye ni miongoni mwa wanaomtetea Manji, ili kupata taarifa za kina.

Mtanzania liliwasiliana na Ndusyepo, ambaye alithibitisha taarifa za kukamatwa kwa mfanyabiashara huyo.

"Ninaweza kuthibitisha ni kweli amekuwa discharged (ameruhusiwa) kutoka hospitali na ninaweza kuthibitisha kuwa ni kweli tupo Keko, ila suala la kama ametoka jana au juzi kupelekwa Keko silijui, kwa sababu leo ni mapumziko", alisema Wakili Ndusyepo.

HAIJAWAHI Tokea...Kishindo cha Rais Magufuli Migodini Chalipa

0
0
KISHINDO cha Rais John Magufuli kuzuia kusafirishwa nje ya nchi mchanga wa madini maarufu kama ‘makinikia’ kisha kupeleka bungeni miswada mitatu kwa lengo la kubadili sheria ili kunufaisha taifa, kimeanza kuzaa matunda baada ya kuungwa mkono hadi ughaibuni.

Hali hiyo imetokana na mabilionea wa kampuni mbili za Australia na Canada zenye kujihusisha na shughuli za madini nchini kueleza namna zinavyomuunga mkono Magufuli (maarufu JPM), huku pia zikimpongeza na kuita hatua alizochukua kuwa ni za kizalendo.

Hivi karibuni, Magufuli aliunda kamati mbili zilizochunguza usafirishaji wa makinikia kwenda ughaibuni ambazo ripoti zake zilifichua upotevu mkubwa wa mapato kwa taifa.

Aidha, kutokana na matokeo ya ripoti hizo na mapendekezo yaliyotolewa, Serikali ilipeleka bungeni miswada mitatu iliyopitishwa kwa kishindo kuridhia mabadiliko kadhaa ya sheria, lengo likiwa ni kulinufaisha taifa na rasilimali tele ilizojaaliwa na siyo wawekezaji pekee.

Juni 29, mwaka huu, serikali iliwasilisha bungeni miswada mitatu inayohusu rasilimali za nchi ukiwamo muswada wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa mwaka 2017, Muswada wa Sheria ya Mapitio na Majadiliano kuhusu Masharti hasi katika Mikataba ya Maliasili za nchi wa mwaka 2017, na Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Nchi kuhusiana na Umiliki wa Maliasili wa mwaka 2017.

Katika taarifa iliyochapishwa jana na gazeti dada la Nipashe la The Guardian, Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Royalty Exploration ya Canada inayofanya kazi zake nchini, James Sinclair, alisema uamuzi wa serikali wa kuwasilisha miswada kwa hati ya dharura bungeni ili kubadili sheria mbovu zilizopo ni hatua ya kupongezwa.

"Mapendekezo ya mabadiliko ya sheria yanalenga kuleta usawa katika rasilimali zinazopatikana nchini lakini tunaamini sheria hizo hizo pia zitaweka vitu vitakavyowavutia wawekezaji,” alisema.

Kampuni ya Tanzania Royalty Exploration Corporation, yenye makao makuu Toronto, Canada, inamiliki asilimia 55 ya hisa katika mradi wa Buckreef Gold Mine nchini na Shirika la Madini la Taifa (Stamico) linamiliki asilimia 45.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Sinclair akiwa nchini Canada, kampuni yake ya Buckreef Gold inaunga mkono mabadiliko hayo ya sheria yanayokusudiwa kufanyika nchini.

Aliwahakikishia wanahisa wake kuwa kupitishwa kwa miswada hiyo na hatimaye kuwa sheria baadaye hakutaathiri uendeshaji wa kampuni hiyo.

Alisema dhamira yake ni kushiriki kwenye maendeleo ya uchumi wa mataifa ya kigeni katika misingi ya usawa kwenye mikataba inayoingiwa.

Katika miswada iliyopitishwa bungeni wiki hii, serikali imeongeza tozo ya mrabaha kwenye dhahabu, fedha, shaba na platinum kufikia asilimia sita kutoka iliyokuwa asilimia nne na kupandisha hisa za serikali kwenye umiliki wa kampuni za madini kufikia asilimia 16.

Nayo Kampuni ya Australia ya Cradle Resources, ilisema kwenye taarifa yake kuwa mabadiliko ya sheria yatokanayo na miswada iliyopitishwa bungeni hayawezi kuwaathiri kwa kiasi kikubwa, ingawa mpango wake wa kutoa dola za Marekani milioni 55 zilizokuwa zimependekezwa zichukuliwe na wabia wake Kampuni ya Tremont Investments, umezimika kutokana na mabadiliko hayo.

Kampuni mbili zilizoko kwenye Soko la Hisa la Australia (ASX), zilisema kwenye taarifa yao kuwa zina imani kuwa uwekezaji wanaoufanya nchini Tanzania utakuwa wa manufaa licha ya mabadiliko hayo ya sheria za madini.

Walkabout Resources Limited ya Australia, ilisema mabadiliko hayo hayawezi kusababisha athari mbaya kwenye uendeshaji wa shughuli zao.

Ilisema kwa kushirikiana na wanasheria wa ndani na wa nje walifanyia upembuzi wa miswada iliyopitishwa na Bunge na kubaini kuwa itakuwa na manufaa hata kwenye mradi wake wa Lindi Jumbo.

“Tumepitia kwa makini mabadiliko hayo, tumeangalia athari zake kwenye miradi yetu na baada ya kusikiliza maoni ya wanasheria wa ndani na wa nje ya kampuni hakuna mabadiliko yoyote yaliyofanyika ambayo yatasababisha kampuni kupunguza au kusitisha uwekezaji wake nchini Tanzania,” ilisema taarifa hiyo.

Chanzo: Nipashe

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa

0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika

Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo..

anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa  PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp/Calls +255 710 279 458
 Call+255 710 279 458

Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

KIMENUKA Tena...Chenge, Tibaijuka, Kilaini walipuliwa mabilioni ya IPTL

0
0
Dar es Salaam. Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imewataja vigogo wa serikali, wanasiasa na viongozi wa dini watatu walionufaika na uchotwaji wa Sh306 bilioni katika Akaunti ya Tegeta Escrow na jinsi baadhi walivyotumia mifuko ya plastiki kuzibeba.

Akisoma maoni ya kamati hiyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Zitto Kabwe aliwataja waliochukua fedha hizo kutoka kwa mkurugenzi wa VIP, James Rugemalira na kiwango walichopokea katika mabano kuwa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti na Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge (Sh1.6 bilioni) na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka (Sh1.6 bilioni).

Wengine ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini ambaye pia ni mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (Sh40.4 milioni), aliyewahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona (Sh40.4 milioni), Mbunge mstaafu wa Sumbawanga (CCM), Paul Kimiti (Sh40.4 milioni), aliyekuwa mjumbe wa Bodi ya Tanesco, Dk Enos Bukuku (Sh161.7 milioni).

Alisema majaji walioingiziwa fedha ni Jaji Profesa Eudes Ruhangisa (Sh404.25 milioni) na Jaji A.K Mujulizi (Sh40.4 milioni).

Kwa upande wa watumishi wa umma, Zitto alisema kuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usajili wa Vizazi na Vifo (Rita), Philip Saliboko (Sh40.4 milioni), aliyekuwa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji (TIC), Emmanuel Daniel Ole Naiko (Sh40.4 milioni) na ofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Lucy Appollo (Sh80.8 milioni).

Askofu Kilaini atajwa
Zitto alisema, “Kwa upande wa viongozi wa dini ambao waliingiziwa fedha na Benki ya Mkombozi ni Askofu Methodius Kilaini (Sh80.9 milioni), Askofu Eusebius Nzigirwa (Sh40.4 milioni) na Padri Alphonce Twimannye Simon (Sh40.4 milioni).

Aliongeza, “Kamati ya PAC ilithibitishiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru kuwa baadhi ya watu walienda kugawana fedha kwenye benki tajwa (Mkombozi) wakiwa na mifuko ya rambo, sandarusi, maboksi, magunia na lumbesa.”

Mkurugenzi Rugemalira
Zitto alisema Mkurugenzi Mtendaji wa VIP Engeneering, James Rugemalira alipata mgawo wa Dola za Marekani Sh75 milioni kutoka katika fedha zilizokuwa kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow na kuzigawa kwa watu mbalimbali.

Rugemalira ambaye alikuwa na hisa 3 kati ya 10 za kampuni ya IPTL, alichukua kiasi hicho cha fedha na kukipeleka katika Benki ya Mkombozi inayomilikiwa na Kanisa Katoliki.

Zitto alisema Rugemalira alionekana kuhusika na IPTL pale alipofungua shauri mahakamani kuomba kuiondoa IPTL kwenye ufilisi na kisha kuuza hisa zake kwa kampuni ya PAP.

Alisema baada ya uamuzi wa Kahakama Kuu kutolewa Septemba 5, 2013, fedha za Escrow zilitolewa kwa haraka na kupelekwa katika benki hiyo baadaye kugawiwa kwa vigogo hao.

Kamati hiyo imekabidhiwa taarifa za Benki za Stanbic na Mkombozi ambazo zimeonyesha namna ambavyo fedha zilichukuliwa na watu na kampuni mbalimbali.

Ripoti hiyo ya PAC iliyosomwa jana ilikuwa na kurasa 116 na maneno 16,979.
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live




Latest Images