Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live

ROMA Afunguka Kutekwa Kwake.....Atoa Sababu Kwanini Ameamua Kukaa Kimya

0
0
Roma Mkatoliki amefunguka na kuweka wazi sababu kubwa zilizomfanya kutokusema nini kilichopelekea yeye kutekwa na nini kilikuwa kinaendelea wakati akiwa chimbo na kudai aliamua kutumia busara ya kutokusema ili mwisho siku aendelee na kazi ya muziki.

Roma Mkatoliki amesema hayo kupitia kipindi cha Friday Night Live (FNL) na kusema alitambua kuwa anaweza kuwakwaza baadhi ya watu kwa kutokusema na kuweka wazi lakini alifanya maamuzi hayo kwa lengo la kulinda sanaa yake na maisha yake kiujumla.

"Mimi najua nini kilipelekea wale jamaa kututeka ni zaidi ya muziki japo chanzo ni muziki ndiyo maana walikuja kututeka tukiwa studio na si kanisani, wala nyumbani unajua wananchi tayari walikuwa na video kichwani, wakijua Roma anakuja kuongea hiki na kile tunamaliza pale halafu usiku mwema, lile tukio lilikuwa linahitaji busara ili maisha yaweze kuendelea,labda ningesema ukweli pengine ungekuwa mwisho wa Roma kwenye muziki, mashabiki wangeshangilia lakini wadau mbalimbali mchongo ndiyo ungekuwa umekwisha" alisema Roma Mkatoliki.

Roma aliendelea kusisitiza kuwa kama angeweka wazi jambo hilo siku ile ambayo ametoka huko chimbo ingepelekea yeye kuacha muziki na kurudi Tanga kufanya mambo mengine kwani hakuna mtu ambaye angetaka kuwa karibu naye tena.

"Hata wewe hapo Dullah usingenipigia simu kunialika kwenye show hapa leo, nakwambia ungeniogopa, na mwisho wa simu Roma angerudi zake Tanga kushika jembe akalime, Je, mashabiki wangependa? Kwanini Roma sasa asiendelee kubaki halafu mashabiki wakaendelea kusikiliza ngoma zake na akaendelea kushusha dude kwa dude, kwa hiyo utaona kuwa yalihitajika maamuzi ya busara katika hili ila nashukuru sana wananchi na wabunge kwa kupaza sauti zenu mpaka tukaweza kutoka na kurudi mtaani kama hivi" alisema Roma Mkatoliki.

Mbali na hilo Roma Mkatoliki anasema toka ametoka mpaka sasa hataki hata kutazama video mbalimbali ambazo zinaonyesha jinsi watu walivyokuwa wakihangaika kuwatafuta ili waweze kupatikana anadai hataki kutazama sababu hataki kukumbuka kabisa, hali ambayo alikuwa nayo kipindi hicho huku akisema hapendi kuona mtu mwingine yoyote anakwenda huko chimbo ambako wao walikuwa wamewekwa wakipata mateso hayo.

Mwanzoni wa mwezi wa 4 mwaka huu msanii Roma Mkatoliki, Moni Cetrozone, Binladen na Emmanuel walitekwa na watu wasiojulikana katika studio za Tongwe Records na kukaa kusikojulikana kwa siku tatu na baadaye kuja kuonekana wakiwa na majeraha mbalimbali.

POLISI Hawataki Mchezo...Gusa Unate...Waua Sita Mwanza

0
0
Watu sita wanaosadikiwa kuwa majambazi wameuawa katika majibizano ya risasi na polisi katika mtaa wa Fumagila Mashariki Kata ya Igoma jijini Mwanza.

Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia leo baada ya watu hao kuzingirwa katikati ya majengo mtaani hapo na kufanya mashambulizi ya kujibizana risasi kwa muda mrefu.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo lakini akaomba alitolee ufafanuzi baadaye kwa kuwa hivi sasa bado anaendelea kukusanya taarifa zaidi.

 “Ni kweli hilo tukio hilo lipo, ila bado tunashughulikia naomba munipe muda nitataoa ufafanuzi baadaye,” alisema kwa ufupi Kamanda Msangi.

Shuhuda wa tukio hilo, ambaye ni diwani wa Kata ya Kishili iliyo jirani na kata hiyo, Sospeter Ndumi amesema kurushiana risasi baina ya watu hao na polisi kulianza usiku wa manane hadi majira ya asubuhi.

Amesema katika majibizano hayo polisi walifanikiwa kuwaua watu hao na kukamata silaha mbalimbali za kivita walizokuwa wanazitumia.

Katika mtaa huo huo ndipo lilipotokea tukio la Desemba 3 mwaka jana ambapo polisi waliwakamata watoto 11 wenye umri unaokadiriwa kuwa na miaka sita hadi 14 baada ya kuizingira nyumba moja kwa lengo la kuwakamata watu waliowahisi kuwa majambazi.

Mmoja kati ya watu watatu waliokutwa kwenye nyumba hiyo alikimbia baada ya kuwarushia polisi bumu la mkono, kabla ya polisi kuwadhibiti waliosalia kwa kushirikiana na wananchi wa mtaa huo.

Kadhalika katika tukio hilo, watu watatu waliosadikiwa kuwa ni majambazi waliuawa na bunduki mbili aina ya SMG na AK47, magazine saba, bastola moja na risasi 183 vilikamatwa na polisi.

Baada ya polisi kuondoka katika eneo hilo, wananchi waliiteketeza nyumba hiyo kwa moto.

KILA Ñapokaribia Kuko...... Anachomoa na Kuibana Kisha Ananidai vitu vya Thamani!

0
0
Jamani eeh naombeni msaada au tu munielekeze huyu mpenzi wngu ni wa namna gani.
Mtaani kwetu kuna demu nimempenda huu ni kama mwezi wa sita sasa,na yeye vilevile anaonyesha kunipenda lakini sina uhakika kwa hili ninalotaka kulitoa moyoni

Kiufupi tu mimi huwa ni mtu wa kupigwa mizinga karibia kila wiki nikimnunulia hiki wiki ijayo atataka hiki na kama unavojua maisha ya siku hizi hela yako tu vitu kama simu vinatoka matoleo kila siku,laptop ndo usiseme ,nguo na viatu kila asubuhi na jioni!sasa basi nilipoona huyu ni mtu wa mizinga kidogo siku hizi huwa na sitasita kutekeleza yani kiufupi nampenda sana sasa inabidi tu nipunguze mapenzi

Lakini cha ajabu kila ninapokuwa nae ndani ya sita kwa sita siku hizi yeye ka-change huwa ninapokaribia kutoa wareno( pale wakuu si mnajua tena shughuli yake pale) huwa anaichomoa na kuibana na kukumbushia ahadi zake za vitu alivyoniomba!!sasaa kwa sababu mimi nakuwa nmezidiwa nataka kumaliza(orgasm) huwa naitikia tu" yes ntakupa"!!kisha ndo anairudishia tena ndani!

Sasa jaman naombeni ushauri wanajamvi wenzangu wake kwa waume hapo napendwa au naibiwa tu?na nifanyeje mie kuli solve hili suala

Jina la Malinzi lafutwa kugombea Urais TFF

0
0

Jumamosi ya July 8 2017 kamati ya uchaguzi ya shirikisho la soka Tanzania TFF ilikutana kwa mara ya kwanza baada ya kuvunjwa na kuundwa upya na kikao cha kamati ya utendaji ya TFF.


Kamati ya uchaguzi ya TFF leo imekaa na kikao chake kimemalizika jioni ya leo na kufanya usahili wa wagombea wa nafasi zote na kuchuja, list ya wagombea waliyochujwa nafasi ya Urais ni pamoja na Rais wa sasa wa TFF Jamal Malinzi ambaye amechujwa kwa kukosekana katika usahili.


Malinzi amekosekana katika usahili kutokana na kuwa rumande kwa kesi ya tuhuma ya makosa 28 kati ya hayo 25 yana muhusu yeye ikiwemo tuhuma ya utakatishaji fedha ambayo imesababisha kukosa dhamana kwa mujibu wa sheria.

ACT-Wazalendo watema Cheche sakata la Halima Mdee

0
0

Ni siku nne tu zimepita tangu Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi kuagiza kukamatwa kwa Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (CHADEMA) akidaiwa kutoa kauli za kumkashifu Rais.


Leo July 8, 2017 Ngome ya Vijana wa Chama cha ACT Wazalendo imelaani na kupinga walichodai tabia ya baadhi ya viongozi wateule wa Rais kuwaweka kizuizini viongozi wa kisiasa.


Mwenezi wa Ngome hiyo, Karama Kaila amesema hadi sasa kuna viongozi kadhaa wa kisiasa wameshikiliwa katika vituo vya Polisi kwa sababu ya amri za Wakuu wa Mikoa na Wilaya.


“Ngome ya Vijana wa Chama cha ACT Wazalendo inalaani na kupinga vikali tabia ambayo inaonekana kuzidi kumea mizizi siku za hivi karibuni ya baadhi ya viongozi wateule wa Rais hususan Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kutumia vibaya Sheria ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa kwa kumrisha kukamatwa na kuwekwa kizuizini kwa saa 48 viongozi wa kisiasa ambao wanaonekana kuwa na maoni tofauti na viongozi hao.” – Karama Kaila.

JE Una Tatizo la Nguvu za Kiume , kukosa Hamu ya Tendo, Kushindwa Kurudia Tendo au Maumbile Madogo ya Uume?

0
0
JE, UNA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? SOMA HAPA 👇👇👇👇
Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, sio Tanzania tu bali duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo sio ugonjwa ila ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili.

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME HUSABABISHA MAMBO KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
@Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye kisukari kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @220,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kurudia tendo hata mara 3 bila kuchoka @130,000/=
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr.
Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no (+255)
0767447444 na 0714335378
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara kwa mtumiaji. Zimethibitishwa kiafya.

HALI Bado Mbaya Kwa Halima Mdee..Ahamishiwa Central Police Baada ya Masaa 72

0
0

Taarifa kwa Wanachama wa Chadema na Wananchi wa Jimbo la Kawe, Mhe Halima Mdee Mbunge wa Kawe aliyekuwa akishikiliwa na Jeshi la Police Kituo cha Osterbay tokea siku ya Jumanne jioni mpaka sasa Amehamishiwa Central Police.
Kwa wale wote mnaotaka kumjulia hali Mbunge kwasasa tuelekee Central Police....

BY HENRY KILEWO
KATIBU CDM DSM

WATU Wengi Hawamuelewi NYOKA Ndio Maana Wanapanic ,Chukua Tahadhari Hizi Pindi Uking'atwa

0
0
Wengi wakimuona nyoka wanaanza kukimbia ,kupiga makelele.Nani kakuambia kuna nyoka ambaye akimuona mtu anaanza kumkimbiza.

Nyoka sio simba au chui ambao tabia zao wakimuona mtu ambaye ni kitoweo kwao wanaanza kumkimbiza kwa nia ya kumla.Kwa nyoka la hasha hakuna nyoka wa aina hiyo awe venomous au non venoumous.Nyoka huwakimbiza rodents tu kama panya sababu ni kitoweo chao.



Watu hawamtizami nyoka kama kiumbe wa porini Bali humtizama kama vile kitu kibaya hilo ndio tatizo.

Nyoka pekee ni kiumbe namba moja ambaye watu humuelewa sivyo ndivyo Africa,hivyo ni mnyama anayeongoza kuuliwa kikatili

Nyoka hupata attention mbaya sababu ya stori ambazo watu husikia pale mtu anapong'atwa

Kung'atwa kwingi panatokea pale mtu anapojaribu kumzuru nyoka na kiumbe huyo anajaribu kujitetea

Majira ya kiangazi nyoka hujificha sana chini ya mawe,miamba majani au kwenye miti kukaa mbali na joto la jua

Mida ya jioni hujitokeza kwa wingi na usiku wakati hali ya joto ipo chini hushamili kwa wingi

Nyoka wadogo sumu yao sio hatarishi sana kama nyoka wakubwa.Mfano Brown snake kila akiwa mzee sumu yake ndio inakuwa kali zaidi


Njia nzuri ya kufanya pindi ukimuona nyoka mwache pekee yake usimbughudhi labda kama atahatarisha maisha ya watoto

Utajiingiza kwenye matatizo pindi ukimsogelea na kuanza kumrushia fimbo ,nyoka ataamua kujilinda na kujilinda kwao ni kutafuta timing ya kukugonga ila kabla ya kufanya hivyo atakupa alarm ya kufungua mdomo wake na kurudi nyuma.

Endapo mtu aking'atwa na nyoka yafuatayo ni yakufanya.

1.Mtulize mgonjwa awe katika hali ya utulivu,asipanic sababu akipanic atasababisha moyo uende mbio hivyo msukumo wa damu utakuwa wa kasi na hivyo kurahisha usambaaji wa sumu kwenda kwenye moyo

2.Kama nyoka yupo sehemu husika usimuue au kumkamata

3.ondoa vitu vyote kwenye mwili wa mgonjwa ambazo zinazuia mzunguko wa damu kama saa,mkanda ,Pete, viatu sababu vitaweza kumletea matatizo

4.safisha eneo lililong'atwa ila usichue au kusugua sababu itaweza kusababisha sumu iliyo nje iweze kuingia.

5.Mzuie ngonjwa asitembee hovyo na mbebe mgonjwa sababu ukimuacha atembee sumu itasambaa kwa kasi sana

6.Funga bandage na weka pressure kwa juu


7.Mchukue mgonjwa na mpeleke kwenye hospitali ya karibu haraka iwezekanavyo lakini kwa kipando


Usimpe chakula chochote au maji mgonjwa haswa pombe

Usiweke barafu kwenye sehemu iliyong'atwa

Usikate sehemu iliyong'atwa na kufyonza hakuna uthibitisho wa kisayansi unaosema hivyo pia hiyo njia inaweza kumletea madhara anayefonza

Usimpe pain killers mgonjwa au dawa yeyote ilei


Mwisho itolewe elimu kwa wachungaji na wakulima na haswa watoto wanaotumwa kuchunga mifugo

Kuna stori ya kusikitisha ilitokea Zimbabwe miaka 3 iliyopita kijana mmoja wa umri wa miaka 13 alikuwa anasoma darasa la 7 moja ya masiku alikuwa anachunga mifugo pamoja na wadogo zake 2 ,katika hali ya taharuki Nyoka aina ya black mamba alimgonga kijana yule mkononi sababu kijana yule alikatiza kwenye mti ambao black mamba alikuwa amejituliza baada ya kung'atwa wadogo zake walimuambia waende nyumbani wakawaeleze wakubwa wao kilichotokea lakini kijana yule alikataa alisema ni nyoka wa kawaida na hali ni ya kawaida akachukua kitambaa na kujifunga na wakaendelea kuchunga.Haikupita muda mrefu 30mins kijana yule akawa anasikia kizunguzungu na kudai haoni na anasikia ugumu kupumua na inavyoelezwa ngozi ya kijana yule ikawa inabadilika rangi na kuwa nyeusi wale wadogo Zake wakambeba kumrudisha nyumbani lakini ikawa too late .kifo cha mtoto yule kilivuta hisia ya watu wengi

Hivyo elimu kubwa itolewe kwa wakazi wa vijijini ,wakulima ,wafugaji njia ya kutumia mawe asilimia ,kukata na kuanza kufyonza sio sahihi.

By undefine

MWAKA 2019 Ipigwe Kura ya Maoni, Rais Magufuli Aruhusiwe Akae Hadi 2035...Sababu Hizi Hapa

0
0
Raisi John Joseph Pombe Magufuli bado anaendelea na kazi yake ya kuisafisha nchi yetu ambayo haikuwa safi katika kila idara.

Nchi iliharibiwa kuanzia serikalini kwenyewe hadi katika ngazi ya mwananchi wa kawaida kiasi cha kuona kwamba rushwa ni jambo la kawaida wakati ukweli upo wazi kwamba rushwa ni aduai wa haki.

Mheshimiwa raisi Magufuli alizaliwa mwaka 1959 na sasa ana umri wa miaka 57 umri ambao katika duru za siasa na uongozi ni umri sawasawa wa kuendelea kuchapa kazi khasa ukiwa kiongozi wa nchi.

Ni dhahiri kwamba nchi sasa imeanza kunyooka si tu katika kuweka nidhamu kwenye idara za serikali bali pia katika sehemu nyingine muhimu zikiwemo idara ya mapato na vyanzo vingine vya mapato.

Tokea achaguliwe mwaka 2015 hadi sasa raisi John Magufuli amefanikisha kwa kiasi cha asilimia 100 mambo yafuatayo:

Hadi mwaka 2016

Hostel za Chuo cha UDSM.
Hostel za Askari Magereza.
Ununuzi wa Ndege 2 (Nyingine 3 ziko mbioni kuja).
Ujenzi wa Flyover Tazara na Ubungo
Upanuzi wa Airport Mwanza
Upanuzi barabara ya Morocco pale kinondoni Dsm
Upanuzi wa Kisasa Airport Dar
Kupambana na Rushwa
Kurejesha nidhamu Makazini.

Hivyo basi kwa maoni yangu ni kwamba wakati umefika sasa wa kuandaaa utaratibu wa kupigwa kwa kura ya maoni ili kuwauliza wananchi kama wanaridhia kufanyiwa mabadiliko kwa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kubadili kipindi cha uongozi wa raisi kutoka miaka 5 hadi miaka ishirini ikiwa ni miongo miwili ya kuijenga nchi.

Ikiwa raisi John Magufuli atapewa miaka 20 ya kuongoza nchi yetu kufika katika kule tunakokusudia kwamba anapata nafasi kwa uwazi zaidi wa kupanga mipango mingine zaidi ya maendeleo ya taifa letu.

Sasa tukiangalia na kupiga picha jinsi nchi yetu ya Tanzania itakapokuwa ifikapo mwaka 2035.

1. Umeme utakuwa umeenea nchi nzima.

Kwa kuendelea kutumia rasilimali ambazo nchi yetu inazo kama gesi serikali ya raisi Magufuli inaweza kabisa kuwezesha umeme kuwa umesamba nchi nzima ifikapo mwaka 2035.

2. Rushwa na Ufisadi vitaanza kuwa historia.

Hadi kufikia mwaka 2035 watanzania watakuwa wakielewa madhara ya kupokea na kutoa rushwa na pia kuendekeza masuala ya kifisadi.

Idadi ya wanafunzi wa vyuo vikuu watakuwa wamejiriwa katika sehemu mbalimbali nchini khasa katika idara kama TRA, viwanja vya ndege na bandari zetu kubwa za Dar-es-Salaaa, Tanga, Zanzibar na Mtwara.

3. Watanzania watakuwa ni wachapa kazi.

Kufikia mwaka 2035 biashara ya madawa ya kulevya na idaidi ya vijana waso na kazi itakuwa imedhibitiwa hivyo kuwepo na vijana wengi ambao ni waajiriwa katika nyanja mbalimbali. Watanzania watakuwa wakichapa kazi katika kuitikia kwa bidii kauli mbiu ya raisi Magufuli ya "Hapa Kazi Tu"

Pia watanzania watakuwa wakithamini kazi zao na kuanza kupata uwezo hata wa kujenga nyumba za kuishi na uwezo wa kupata mikopo kutpka katika mabenki mbalimbali nchini katika viwango vya riba vinavyokubalika.

4. Uchumi wa viwanda kukua pamoja na Miundombinu.

Kwa mujibu wa machapisho mbaimbali kutoka wizara ya viwanda na biashara, sera ya viwanda haijaanzishwa na serikali ya raisi Magufuli. Sera hii ilianzishwa mwaka 1996 na waziri wa wakati ule wa viwanda na biashara marehemu Dr Abdalah Kigoda ambae aliita Sustainable industrial development policy 1996-2020.

Sera hiyo ililenga katika kuhakikisha kwamba hadi kufikia mwaka 2020 Tanzania itakuwa inatumia mtaji wa ndani yaani "Domestic Capital" kuwekeza katika viwanda vya kutengeneza bidhaa ndogondogo au "basic capital good industries".

Tayari leo Serikali ya awamu ya tano imewezesha kufunguliwa kwa viwanda kadhaa vya kusindika chakula, maziwa Simiyu kujengwa kwa viwanda vya kutengeza vyuma na kile cha kutengeza vigae mkoani Pwani.

Pia Miundombinu mbalimbali itapata nafasi ya kukamilishwa kwa ujenzi wake na kufikia mwaka huo wa 2035, kutakuwa na reli ya kati ya kiwango cha standard gorge na miundombinu mingine kana barabara za lami za kueleweka.

5. Viashiria vikuu vya uchumi kukua na kuimarika.

Viashiria hivyo ambavyo vimo katika maeneo ya Madini, nishati, Mawasiliano na usafirishaji vitakuwa vimeimarika kutokana na wenye makampuni kuwa wameorodhesha biashara zao katika soko la hisa ambalo litaloa fursa kwa wananchi kuweza kuwa na hisa katika makapmuni hayo na hivyo kuimarisha mzunguko wa fedha wa ndani.

Viashiria vingine kama mabenki watakuwa na uwezo wa kukopesha fedha kwa wananchi ambao wengi watakuwa ni waajiriwa katika sehemu mbalimbali.

Ni wazi kabisa sasa kwamba kero za wananchi ambazo walikuwa wakizipigia kelele zimekuwa zinatatuliwa na serikali ya awamu ya tano.

Katika nchi yoyote ile kunapotokea kiongozi ambae atajitolea kufanya usafi wa aina yake na kwa kutumia mtindo wake wa kipekee, wananchi wana budi kumuunga mkono kiongozi huyo.

Hatufahamu ikiwa wagombea wa UKAWA wangeanza na sera ya hapa kazi tu au wangekuja kivingine lakini ni wazi wananchi tuling'amua hilo na kuamua kuwapa madaraka serikali ya raisi John Magufuli.

Raisi John Magufuli bado anaendelea kupingwa jitihada zake za kuonyoosha nchi yetu na baadhi ya wale wanaompinga ni walewale walotaka mtu wa aina ya raisi John Magufuli. Ikiwa raisi Magufuli ataishia katikati na kumwachia mtu mwingine aendeleze yake aloyaanza ni wazi kuwa kila kitu kitarudi kama mwanzo nai huenda ikawa mbaya zaidi.

Mashine za Scanners zitazimwa katika viwanja vya ndege na bandarini na kuendeleza utoroshaji wa madini na nyara za serikali na pia biashara ya madawa ya kulevya itashamiri waziwazi kama ilivyokuwa mwanzo.

Fedha za umma zitaibiwa kwa safari za nje ya nchi na pia mishahara hewa itarudiwa kulipwa kwa watumishi hewa. Kuna kila dalili kwamba hali ambayo Tanzania ilikuwa nayo kabla ya kuapishwa kwa raisi John Magufuli mwezi November mwaka 2015 itarudia kama ilivyokuwa mara tu atakapomaliza uongozi wake na hiyo itakuwa ni mapema sana.

Ila ni wazi kuwa raisi John Magufuli anafaa kuendelea kuwepo kwa miongo miwili ili aweze kurekebisha kila kasoro ambazo zilikuwepo kabla ya uongozi wake na kujenga mizizi ya kuheshimu kazi na matumizi ya hekima ya fedha za umma.

Halitakuwa jambo jema kwa yeye kuishia katikati katika mipango yake ambayo inaonekana ikiwa hataimaliza basi inaweza kuishia katikati na nchi yetu isifike katika ile nchi ya ahadi ya kila mtanzania kufaidi keki ya taifa.

Ni wakati basi, wa kuibadili katika yetu kwa kuitisha kura ya maoni ili raisi John Magufuli aongezewe muda wa kuongoza Tanzania hadi mwaka 2035.

Je Mdau una maoni gani?

NB:

Jaribu kutoingiza sana siasa za vyama katika maoni yako tuangalie zaidi utendaji wa raisi John Magufuli ingawa anatoka katika chama cha CCM.

Karibu.

Maoni ya Richard/Jamii Forums

SOMA Nafasi za Ajira Mbali Mbali zilizotangazwa Week Hii

JUA Aina ya Watu Wasionuka Vikwapa Wala Kuitaji Kutumia Deodorant......

0
0
Je wewe ni miongoni mwa wachache wenye bahati hii?

Kwa jinsi joto linavyoongezeka na msimu wa kiangazi ukiwa unakaribia, wengi wetu tunafikiria jinsi ya kukabiliana na kutoka jasho na harufu inayoambatana nayo. Lakini kama wewe ni miongoni mwa watu wachache wenye bahati zao ambaye una vinasaba (DNA) vinavyoitwa ABCC11, huna haja ya kuwa ma wasiwasi wa kutafuta deodorant ilipo.

Kwa mujibu wa tovuti ya LiveScience, uwepo wa kinasaba hicho inamaanisha kwamba vinyweleo vyako vya makwapa vinakosa kemikali ambayo ikichanganyika na jasho kinakuwa chakula cha bakteria na mwisho kutengeneza harufu mbaya mwilini.

Mwezi Januari 2013, wataalamu wa vinasaba vya ngozi katika Chuo Kikuu cha Bristol, Ian Day na Dkt. Santiago Rodriguez, walishirikiana kufanya utafiti kuhusu viondoa harufu ambapo walifanya utafiti kwa wanawake 6,495. Wataalamu hao waligundua kuwa asilimia 2 ya washiriki (wanawake 117) walikutwa na kinasaba cha ABCC11. Kati ya wanawake hao 117, asilimia 78 walikuwa wanaendelea kutumia deodorant ingawa hata hawakuwa wakilazimika kufanya hivyo kama wenzao.

Ingawa utafiti huu wa Day na Rodriguez haukuhusisha wanaume, Day aliiambia LiveScience kuwa anadhani matokeo ya utafiti huo yanaweza kutumika kwa wanaume pia na kutoa matokeo yanayofanana. Pia, katika mahojiano aliyofanyiwa, alikadiria kuwa asilimia mbili ya Wazungu na karibia watu wote wa Mashariki mwa Bara la Asia na Wakorea wana vinasaba vya aina hii.

“Matokeo haya yanaweza kumuongoza mtu kutumia Elimu ya vinasaba vya mwili wake kutambua na kuchagua aina ya vipodozi na bidhaa za usafi wa mwili wake,” alisema Rodriguez alipokuwa anazungumzia umuhimu wa matokeo ya utafiti huo. “Kipimo cha kawaida cha vinasaba kinaweza kukuongezea hali ya kujijua zaidi na kukuepushia gharama zinazotokana na matumizi yasiyo na ulazima wowote na pia kukuepusha na matumizi ya kemikali zilizopo kwenye bidhaa zinazozuia harufu.”

Kwa wenzetu ambao huwa wanatokwa jasho sana likiambatana na harufu mwilini, jaribu kufuata ushauri huu:


  • Jaribu kutumia kitoa harufu (deodorant) aina ya ‘Rx-strength,’ ambayo inawasaidia sana kwa watu wanaotokwa jasho jingi kwenye makwapa, viganja vya mikono au kwenye nyayo za miguu.
  • Hakikisha unapaka kitoa harufu chako nyakati za usiku, kwakuwa itakusaidia kuviweka vizuri zaidi vinyweleo vinavyotoa jasho kwa muda huo kuliko unapoipaka au kujipulizia asubuhi.
  • Jaribu pia kutumia sindano aina ya ‘Botox’ ambazo zinasaidia kuzuia mtiririko wa taarifa zinazoruhusu mwili kutoka jasho kutoka kwenye ubongo sizifike sehemu iliyochomwa sindano.

MANENO Machache ya Prof Jay Baada ya Kufunga Ndoa......

0
0
Msanii wa muziki, Professor Jay amefunga ndoa katika Kanisa la Mtakatifu Joseph la Posta jijini Dar es salaam leo Jumamosi Julai 08, 2017 na mpenzi wake wa siku nyingi Grace Mgonjo.

Cherekochereko za tukio kubwa la Mbunge wa Jimbo la Mikumi kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Joseph Haule almaarufu Profesa Jay limetikisa Jiji La Dar baada ya kufuatiliwa na watu wengi. Ndoa ya Profesa Jay na mpenzi wake wa muda mrefu.

Kabla ya ndoa hiyo iliyoibua shangwe kwa ndugu, jamaa na marafiki waliofurika kanisani hapo, msafara wa kuelekea kanisani ulianzia nyumbani kwa Profesa Jay, Kimara-Temboni jijini Dar.

Ndoa hiyo ilifuatiwa na sherehe ya kukata na shoka iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar ambapo waalikwa walipata nafasi ya kula, kunywa hadi kusaza huku shughuli nzima ikipambwa na mahudhurio ya mastaa kibao wa Bongo.

“Namshukuru Mungu nimetimiza ahadi ya ndoa kwa mchumba wangu ambaye tumepitia mabonde na milima,” alisema Profesa Jay baada ya kutoka kanisani hapo.

VIDEO: Suprise ya Diamond Platnumz Kwenye Harusi ya Profesa J na Grace

0
0
Rapper na Mbunge wa Mikumi Joseph Haule ‘Profesa Jay’ July 8, 2017 alifunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu Grace ambaye walidumu katika uchumba kwa miaka 13 ambapo watu mbalimbali wakiwemo wanasiasa na wasanii walialikwa.

Moja ya mambo yaliyofurahisha katika tukio hilo ni surprise ya mwimbaji staa wa Bongofleva Diamond Platnumz ambaye alitumbuiza…bonyeza PLAY kwenye VIDEO hii kutazama!!!

Ridhiwani Kikwete amuomba msamaha Prof Jay

0
0

USIKU wa kuamkia leo ilikuwa ni shangwe kwenye Ukumbi wa Mlimani City wakati wa sherehe ya Rapper nguli wa Bongo ambaye pia ni Mbunge wa Mikumi Joseph Haule ‘Profesa Jay’ aliyefunga ndoa jana hiyohiyo Julai 8, 2017  na mpenzi wake Grace katika Kanisa la St. Joseph lililopo Posta ya Zamani Dar.

Licha ya Sherehe hiyo kuhudhuriwa na watu mashuhuri wakiwemo wabunge, Basi Ridhiwani Kikwete ameandika maneno haya kupitia ukurasa wake wa Instagram...


"hata Ubuyu ulianza kama Jay Mwisho ukakatika." Prof. Jeezy nawe umeaga kambi ya Mabachela na umejiunga na kambi ya Wastaarabu. Hongera sana Brother. Nisamehe kwa kushindwa kuhudhuria kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wangu. Nakujali sana bro.@professorjaytz"

TUKANENI ila Nasimama Kwenye Haki ‘Cheche ni Wimbo Wangu’- Ommy Dimpoz

0
0
Baada ya tetesi kuwa Msanii wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz ameiba wimbo wa Cheche kutoka kwa Msanii mchanga ajulikanaye kwa jina la Modala, Hatimae Ommy Dimpoz amejibu tuhuma hizo kwa kusema wimbo wa Cheche ni wake huku akiweka wazi kuwa amenunua mashairi ya wimbo huo kutoka kwa Mtunzi/Muandaaji wa muziki Lolipop.


Ommy Dimpoz amesema alinunua Wimbo huo kutoka kwa Lolipop mwaka jana ingawaje amechelewa kuuachia kutokana na muingilio wa ratiba lakini hakuwahi kuusikia wimbo wa Cheche wa Modala na hata wakati ananunua wimbo huo alimuamini Lolipop kwani ni mtunzi mzuri wa nyimbo na hakuambiwa kwamba wimbo huo tayari ulikuwa umenunuliwa.

“Mimi naamini Lolipop ni mwandishi mzuri pengine kuliko mimi…Kwahiyo mimi nina haki na wimbo wa Cheche na nilinunua kutoka kwake kwasababu ni mwandishi ambaye amewaandikia Wasanii wengi nyimbo.. Mimi nimewekwa mtu kati, kati ya Lolipop na Abby Dady lakini watu wajue wimbo huu ni wangu soo hata mkitukana tukaneni ila nasimama kwenye haki yangu wimbo wa Cheche ni wangu”,amesema Ommy Dimpoz kwenye mahojiano yake na Times FM.

Ommy Dimpoz amesema kama angekuwa ni yeye amesharekodi wimbo huo halafu anakuja kusikia kuna Msanii mwingine ameachiwa wimbo alioununua basi angeenda moja kwa moja kwa mtu aliyemuuzia na kumtaka amrudishie pesa yake badala ya kulalamika kuibiwa.

“Ningekuwa matatizo haya yametokea kwangu kuwa nimewapa pesa halafu nasikia wimbo wangu umeachiwa na msanii mwingine mimi ningemfuata Lolipop anirudishie hela yangu nisingeachia wimbo“,amesema Ommy Dimpoz.

Hata hivyo Ommy Dimpoz amesema kama kuna mtu anaona kaibiwa wimbo huo basi atafute haki yake ila anachojua yeye wimbo wa Cheche ni wake pia amewaomba Mashabiki waendelee kumpa sapoti kwenye kazi zake huku akiwataka waache matusi mitandaoni kwani sio ustaarabu.

sikiliza ngoma zote mbili hapa chini Cheche ya Ommy Dimpoz na Modala, kisha toa maoni yako

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa

0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika

Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo..

anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa  PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp/Calls +255 710 279 458
 Call+255 710 279 458

Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

BLACk Chyna Kumpeleka Rob Kardashian Mahakamani..Kisa Picha za Utupu

0
0
Mwanamitindo na mfanyabiashara Angela Renee White a.k.a Blac Chyna, amemfungulia mashtaka mpenzi wake Rob Kardashian.
 

Blac Chyna ambaye amezaa mtoto mmoja na Rob, wiki hii amejikuta akipokea mvua ya matusi na udhalilishaji pamoja na picha zake za utupu alizokuwa akimtumia mpenzi wake kuwekwa hadharani katika mtandao wa Instagram na mwanaume, ambaye anamtuhumu mpenzi wake huyo kuwamsaliti kwa kuwa na wanaume wengine kuwa mtumiaji wa madawa ya kulevya.

Mwanasheria wa mrembo huyo, Lisa Bloom ametumia ukurasa wake wa twitter, kutweet kwa kumjulisha Rob kuwa anatakiwa kufika mahakamani jumatatu kujibu tuhuma zinazomkabili za kumdhalilisha mpenzi wake huyo wa zamani.

“I represent Blac Chyna. I just gave Rob Kardashian notice that we’ll be in court Monday seeking restraining orders against him. More to come,” ameandika mwanasheria wa Blac

NJIA Anazotumia Mungu Kukujulisha Kuwa Mpenzi/Mchumba Uliye Nae si sahihi

0
0
Habari za jumapili ndugu wote.! ni siku nyingine ambayo Mungu ametupa nafasi ya kukutana hapa na kujulishana machache ambayo kwa hayo tunaweza kupiga hatua katika eneo hili la kimahusiano.

Kwanza kabisa ni lazima nikueleze ya kuwa sisi sote ni watoto wa Mungu na Mungu anatupenda sana..! ndio sababu akamtoa Yesu kwa ajili yetu.. (Yohana 3:16)

Mungu anapoona tunafanya maamuzi ambayo si sahihi au hayapo katika mapenzi yake huwa anatujulisha mapema sana ili tusiweze kupata madhara ya maamuzi yetu hapo baadae, na moja ya maamuzi hayo ni kuamua kuwa na mpenzi au mchumba. Je.! nitajuaje kama mchumba/mpenzi niliye nae ni sahihi au si sahihi? Zipo njia kadhaa ambazo Mungu huzitumia kukujulisha kuwa mchumba/mpenzi uliye nae si sahihi na hayo mahusiano yataishia pabaya au kuwapeleka jehanamu kabisa... Njia hizo ni kama hizi zifuatazo;

1. Huzuni moyoni (kujihukumu/kujilaumu moyoni)
Hii ni njia mojawapo muhimu sana ambayo Mungu huitumia kukujulisha kuwa mtu uliye naye si sahihi, unakuta tangu umeanza mahusiano na huyo mtu kuna hali ya huzuni moyoni mwako inaendelea na wakati mwingine unajisikia kujilaumu kwa nini nilimkubalia huyu mtu au kwa nini nilishawishika kutongoza huyu msichana, na wengine wameenda mbali zaidi wanaanza kubadilika kimatendo kwa wapenzi wao ili kudhihirisha kile kinachoendelea mioyoni mwao, hebu tuangalie maandiko haya katika Biblia;

2. Wakorintho 7:9 inasema “Sasa nafurahi, si kwa sababu ya ninyi kuhuzunishwa, bali kwa sababu mlihuzunishwa, hata mkatubu. Maana mlihuzunishwa kwa jinsi ya Mungu, ili msipate hasara… maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti.”

Huyu ni Paulo anawaambia wakorintho kuwa huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu na lisilo na majuto.., kwa maana nyingine ukiona ndani yako unasikia huzuni au kujilaumu au kujihukumu juu ya huyo mpenzi wako basi ujue Mungu katika Roho mtakatifu anakuambia hivi.. "Fanya toba juu ya huyo mtu na uachane nae mara moja.!" la sivyo utapata hasara katika hayo mahusiano. Toba maana yake ni Repent (change your mindset) au badili msimamo wako juu ya huyo mtu. Mungu amekuletea hiyo huzuni moyoni kukujulisha kuwa utapata hasara juu ya mahusiano yenu na huyo mtu. Hata unaposoma haya maneno saivi na ukaona unajisikia hiyo hali ya kujihukumu inajitokeza basi ujue ni ishara Roho mtakatifu anakuthibitishia juu ya hili jambo ili ulifanyie kazi.


2. Njia ya Ndoto 
Hii ni njia nyingine ambayo Mungu huitumia kukujulisha kuwa mpenzi huyo uliye nae si sahihi na unahitaji kubadili msimamo wako. hebu tutazame maandiko haya katika Biblia;

Ayubu 33:14-15 inasema "Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. Katika ndoto, katika maono ya usiku, usingizi mzito huwajiliapo watu, katika usingizi kitandani."

Hapa nataka uone ya kuwa Mungu huwa anaongea na watu kwenye ndoto, mara ya kwanza, na anaweza kurudia mara ya pili lakini watu hawajali.. na ndio maana kuna ndoto nyingine unaota zinajirudiarudia lakini wewe hujali, ujue hufanyii kazi kile ambacho Mungu anakueleza katika ndoto, sasa hata katika mahusiano ni hivyo hivyo, kuna mambo ambayo huwa unaota juu ya mpenzi wako lakini wewe unayapuuzia na huyajali kumbe ni Mungu anakueleza juu ya huo uhusiano wenu ambao si mzuri, kwa mfano mtu anaota anakimbizwa na mpenzi wake, au anachomwa kisu na mpenzi wake au unagombana na mpenzi wako.. maana yake hiyo ni ishara Mungu anakupa kuwa huyo mtu si mzuri kwako na si mtu sahihi kwako, atakusababishia matatizo makubwa katika mahusiano yako, na wengine kwa kupuuzia huku wamejikuta wameingia kwenye matatizo makubwa na majuto makubwa wakati Mungu aliwaonyesha mapema katika ndoto.. mimi sijui huwa unaota ndoto gani juu ya huyo mpenzi wako au juu ya uhusiano wenu lakini naamini Mungu huwa anaongea na watu kwenye ndoto, hivyo uwe makini na ndoto unazoota juu ya mpenzi wako, sasa ukishaota hizo ndoto inakua rahisi kumueleza huyo mtu na kuamua kuachana la sivyo kile ulichokiona katika ndoto kitatokea...

Hizi ni baadhi ya njia chache ambazo Mungu huzitumia kukujulisha juu ya mahusiano yako na juu ya huyo mpenzi wako kama si sahihi kwako, lakini zipo njia nyingi mno! labda tukipata nafasi wakati mwingine tutashirikishana zaidi.

Mungu akubariki, na uwe na jumapili njema.!!

SABABU Tano(5) Kwanini Unapata Pesa Lakini Huna Maendeleo

0
0
Leo ningependa tujifunze kitu juu ya hili suala la nidhamu ya fedha na ninatumai mtapata mawili matatu ya kujifunza na hata kubadilika.

Kuna watu umeanza nao kazi, au hata biashara lakini ukiangalia walipofikia unashangaa, huamini unaona wana maendeleo mpaka unadhani labda wao wana kitu cha ziada, kuna sehemu nyingine ambayo inawapatia pesa.

Umekata tamaa na unaishia kujipa moyo kuwa wale ni mafisadi, au wanahongwa, wazazi wao wana pesa, lakini pia unasema wanaenda kwa waganga kwani wewe pesa yako huoni inaenda wapi.

Labda sasa nikuambie ni kwanini wewe pesa haionekani katika mambo ya maendeleo.

(1) Huna Malengo 
Hii ndiyo sababu ya kwanza na kukosekana kwa malengo basi kunasababisha mambo mengine yote ambayo nitayataja. Kwamba unapata pesa lakini hujapanga kuwa unataka uzitumie kwenye mambo gani, hii hukufanya kuwa na matumizi ya hovyo ambayo hayana misingi kwako.

Kuwa na pesa bila malengo ni sawa na kuwa na nauli ukiwa hujui unaenda wapi, utapanda kila basi lakini hutafika. Ni lazima uwe na malengo ili ukipata pesa kidogo tu unajua unazipeleka wapi, unailazimisha akili yako kutafuta pesa na kuzipeleka sehemu husika.

(2) Unataka Kufanya Kila Kitu Kwa Wakati Mmoja 
Ndiyo hili ni tatizo kubwa, una pesa kweli lakini kwakuwa huna malengo na unataka kufanikiwa basi unaangalia watu waliofanikiwa na unajaribu kufanya kama wao. Kila siku ukiona biashara mpya unafanya, ukiona flani kanunua gari na wewe unataka.

Ukiona flani anajenga unaanza kujenga, kanunua kiwanja na wewe unanunua. Yaani hutulii na kufanya kitu kimoja, unafanya biashara tano na zote hazina hata uelekeo. Yaani ni kama unataka mtoto wa Chuo Kikuu hivyo unazaa wengi ukidhani ndiyo watafika chuo kikuu mapema, unapoteza uelekeo na unakuta pesa zako zinaishia katikati kwa kila kitu.

(3) Unatoa Zaidi Kuliko Uwezo Wako
Kama wewe ni yule mtu ambaye kila mtu akipata shida basi mtu wa kwanza kukufikiria ni wewe basi una tatizo, inawezekana unaona ni jambo jema na ni kweli kiubinadamu ni jambo jema lakini kiuchumi nikuwa unawafanyia kazi wengine.

Inawezekana hata huwapi misaada, wanakopa lakini jua wao hukopa kufanyia mambo yao ina maana wakati huo wewe hufanyi ya kwako. Unakua kama benki lakini bila riba. Kwamba wewe huna kazi ya kuzifanyia pesa zako hivyo unawapa wakazifanyie, zipo tu, watakulipa lakini watakulipa zikiwa hazina maana tena kwako.

(4) Una matumizi Ya Hovyo
Ndiyo unanunua vitu vya hovyo, kwa kuwa huna malengo kwamba hujapanga nikipata pesa nazipeleka wapi, unajikuta unakua na pesa nyingi ambazo ni cash kila siku. Kisaikolojia unajiona kama una hela nyingi, unajikuta unanunua vitu ambavyo hata ulikua huvihitaji.

Sehemu ya kutembea unapanda Bajaji kwakua una buku ipo tu, umeshiba lakini una mia mbili unanunua karanga. Huhitaji shati lakini una laki mfukoni na huna pa kuipeleka, unanunua vitu vingiii ambavyo hata huvihitaji. Pesa yako inaenda huko, lakini ungekua na malengo ungezipeleka kwenye malengo yako na si kununua hivyo.

(5) Unabeba Majukumu Ya Watu
Ndiyo unachukulia matatizo ya watu kama vile ni yako na unajipa wajibu wa kuyasuluhisha, ndugu wakikwama unajitwisha, marafiki, na kila mtu. Hapa sizungumzii kusaidia hapana bali unafanya mambo kama vile ni yako.

Baada ya muda unajikuta una majukumu mengi kuliko uwezo wako, kuna mtoto wa mjomba, shangazi, sijui nani na kila mtu anakuangalia wewe. Kinachotokea ni kuwa wewe unayachukua yale majukumu, yanakua yako na yanakua ndiyo malengo yako, kuwasaidia wahusika kuyatatua.

Lakini wale ambao unawasaidia nao wanalemaa, kwakua upo wanazilazimisha akili zao kuamini kuwa sio msaada bali ni majukumu yako. Wanakua wavivu na kuacha kutimiza wajibu wao wakijua upo. Wakati mwingine hata ukikosa wanalaumu kana kwamba ni wajibu wako.

Kama una tabia hizi ni muhimu kuanza kubadilika. Anza kwa kutambua tatizo lako, weka malengo yako ya kimaisha. Kuwa na malengo kutakuzuia kufanya mambo mengine yote haya ya kukumalizia pesa. Kutakufanya kuwa na nidhamu ya pesa na kuzitumia kutokana na malengo uliyojiwekea.

It is your time now to stand alone(Ni muda wako wa kusimama peke yako)

By Joseverest

Breaking News: Mtangazaji wa EFM Bikira wa Kisukuma Afariki Dunia

0
0


Kituo cha Radio cha EFM Kimedhibitisha kifo cha Mtangazaji wao Bikira wa Kisukuma.....

From @efmtanzania - Kwa masikitoko makubwa E FM inapenda kuwajulisha kuwa mwenzetu Seth Katende maarufu" Bikira wa kisukuma"amefariki dunia Leo mchana katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kuugua kwa muda mfupi.Seth atakumbukwa sana kwa ucheshi wake kupitia kipindi cha Ubaoni alichokua akiendesha sambamba na Imma Kapanga na Mpoki au "mwarabu wa Dubai".Msiba upo nyumbani kwa baba yake mzazi Changanyikeni Dar es salaam.Endelea kupitia kurasa zetu na kusikiliza Efm na TVE kwa taarifa zaidi.Mungua ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi Amen.
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live




Latest Images