Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Kunani East Africa Radio...Watangazi Wazuri na Ma DJ Kuondoka......

$
0
0
Kwa muda mrefu nimekuwa nikifuatilia Eat Africa radio na Tv, wamekuwa ni walimu kwa watangazaji wanaotoka pale yaani watangazaji wanatoka wamekwiva ki maadili hadi utendaji.

Lakini ni kama swali najiuliza ni nini kunachowakimbiza hawa watu, ni Mshahara(maslahi), kujuana, unyanyasaji kazini au ni nini ambacho wanakikimbia na wanako kwenda wanakuwa dhahabu.

Orodha ni ndefu ya walioondoka tangu enzi za Bush baby, Steve ka fire, wale naweza sema labda waliona warudi nchini kwao wakaanze maisha ya huko. Hapa kati kati walioondoka ni wengi:
Dj AD aka Mafuvu baby, Anna Peter, Allan Lucky, Michael Lukindo, Sebastian Mwaikambo, Bahati Abdul, hivi karibuni wamepata pigo na si pigo dogo hasa kwa vijana waliowatengeneza kisha wakanyakuliwa ikiwa ni Kenedy the remedy, Dj sinyorita na Mammy Babby mara upepo haujatulia Dj ambae alionekana kuziba pengo la Mafuvu nae kaenda E-fm.

Tar 8 kwenye tamasha la Komaa concert jijini Mwanza alionekana Jukwaani akisimamia shoo kwa wasanii walio alikwa hakuwa mwingine ni Dj Ommy Crazy, ambae kwa muda amekuwa hasikiki redioni (Ea radio) na alikuwa akifanya yake nilihisi jambo ila nikasema acha muda uongee.

My take Ea radio kwa sasa mna Frida au Queen fifi na King smash ni kama hadhina mliobaki nayo ni watu ambao huchoki kuwasikiliza jaribuni kuwalinda kimaslahi na vinginevo waibebe redio, radio inakosa mvuto msipo kuwa makini hao hawana muda mrefu watawapokonya.

Program meneja wa Ea radio naamini atapita hapa



Ulimbukeni wa Wanaume Linapokuja Swala la Mapenzi na Uzuri wa Mwanamke

$
0
0
Leo inabidi tuambiane ukweli, kuna baadhi ya wanaume ambao sijui ndo tuite "nzi kufia kwenye kidonda" yani utakuta mwanaume anamfukuzia mwanamke kwa miaka 3, kisa ni nini? eti oh yule demu ni mzuri, oh i have a crush on her, ooh nimemzimia..utakuta huyo mwanamke anaefukuziwa wala hamuwazi huyo mwanaume tena usiku analala usingizi mnono na vijambo juu.

Mtu anakaa kwenye relationship isiomfaidisha wala kumpa furaha eti kisa demu ni mzuri, aise i advise ni bora kuwa single tu kuliko kupitia haya mateso ya kujitakia, sisemi mtu usiwe na crush kwa demu, ila wanaume (including me) tuwe tunajaribu kusoma upepo, mpende demu ukiona haeleweki na hakutilii maanani.. sepa fasta it will be good for ur emotional health, naamini ukitubu dhambi kiukweli na ukimuomba Mungu atakupa mke mwema.

Some of my friends wanaapa kutumia hela nyingi sana kwa demu wanaemuona kuwa ni mzuri, they're like yule demu bwana ni high status ngoja ntamchukua na prado, kumbe huyo demu anapigwa mate na muuza duka..just imagine mtu mwaka wa 4 bado anatajataja jina la demu ambae ana crush nae mm huwa mpaka nakereka, nawakataza wasitaje ovyo majina ya madem ambao hawana time nao..

Bora hata wanawake, akiona mwanaume hueleweki na hupendeki ..anafunga virago (labda cjui awe kwenye ndoa)

Nimemaliza.

Nafasi 20 za Ajira Zilizotangazwa na Tanzania Women's Bank Plc (TWB) Leo

JE Dada Unahitaji Kuwa Mrembo na Muonekano Bomba na Kaka Kuwa na Mvuto wa Kiume...Waone Hawa....

$
0
0
BLACK BEAUTY COMPANY
JE Dada unahitaji kuwa Mrembo na ule muonekano bomba wa kisuperstar👌🔥,kaka unahitaji kuwa mtanashati na mvuto zaidi wa KIUME?fika black beauty company utatimiza ndoto zako,hawakosei hata siku moja kwa products original na zenye matokeo yaharaka sana,bila madhara,ni kampuni yenye uzoefu wa hali ya juu sana🔥
1)kuongeza hips,makalio,mapaja@150000
(b)kuongeza hips,makalio,mapaja na miguu@200000/=
2)kuongeza miguu ,kuondoa vigimbi@120000/=
3)kuwa mweupe mwili mzima (Rangi moja)@150000/=
4)Kupungua mwili mzima@150000/=
5)kupunguza tumbo@100000/=
6)kupunguza au kuongeza matiti@100000/=
7)kukuza nywele@100000/=
8)kuondoa michirizi @100000
9)kuondoa madoa,mabaka na chunusi sugu@100000/=
10)kuongeza uume na nguvu za kiume@150000/=
Dawa zetu niuhakika sana100%na utaletewa popote ulipo,mikoani tunatuma,nje ya nchi tunatuma DHL,ofic zetu zipo kariakoo msimbazi police,🔥karibuni kwa mawasiliano zaidi WhatsApp+255657778924,au call0743534406 au unaweza kutufollow
👇👇👇👇👇👇
@black_beauty_company

Mpasuko Kanisa la Anglicana Waendelea....Mwanza Kimenuka

$
0
0
KANISA la Anglikana Dayosisi ya Victoria Nyanza jijini Mwanza, limeingia katika mgogoro mkubwa baada ya Wazee wa Nyumba ya Walei kumwandikia barua Askofu Mkuu, Dk. Jacob Chimeledya na baraza lake la maaskofu wakitaka wamuondoe madarakani Askofu Boniface Kwangu wa dayosisi hiyo.
Katika maelezo yao, waumini hao walisema kuwa, wamechukua uamuzi huo ili kumaliza mgogoro uliodumu katika kanisa hilo kwa zaidi ya miaka miwili sasa wakimtuhumu kiongozi huyo kutumia madaraka vibaya na kufuja mali za kanisa.

Baada ya ibada ya wiki iliyopita katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Nicholaus jijini hapa, Mwenyekiti wa Baraza la Walei Dayosisi ya Victoria Nyanza, Osoro Nyawanga alisema kuwa, barua hiyo inamuomba Askofu Dk. Chimeledya katika kikao cha baraza lake mgogoro huo uwe moja ya ajenda katika mkutano mkuu wa baraza la maaskofu uliotarajiwa kufanyika mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Dodoma.



“Nyumba ya walei tulishamkataa Askofu Kwangu baada ya kushindwa kuliongoza kanisa. Tunaiomba mamlaka kuchukua hatua haraka zaidi kulinusuru kanisa na mali zake,” alisema Nyawanga.

Askofu Kwangu alipopigiwa simu baada ya mwandishi kujitambulisha alijibu kifupi: “Nipo kwenye shughuli nyingine zaidi, naomba unitafute siku nyingine.”

Askofu Dk. Chimeledya alipoulizwa kuhusu barua hiyo alisema hajaiona, lakini akafafanua kuwa kama ipo, kuna utaratibu wa kupitia makao makuu ya ofisi iliyopo Dodoma.

Alipoulizwa kama suala hilo litakuwa kwenye ajenda alisema: “Kama tukiona jambo hilo liwe ajenda, sawa, itategemea na zitakazokuwepo ila hawawezi wao kututengenezea ajenda.”
Mgogoro huo katika kanisa hilo una zaidi ya miaka miwili na tayari uongozi wa kanisa hilo umemfungulia kesi polisi Askofu Kwangu na wenzake wanne, tangu mwaka 2016 na kupewa jalada la kesi namba MW/ RB/265/2016 ambalo ni jalada la uchunguzi kwa watuhumiwa.

UWAZI

Mshuhudie Mtanzania Mrefu Kuliko Wote na Mateso Anayopata

$
0
0
JULIUS Charles, huenda ndiye Mtanzania mrefu kuliko wote kwa sasa, akiwa na urefu wa futi saba na nchi mbili, ambapo ameleza kwa kina juuu ya adha na mateso anaayokutana nayo ikiwa ni pamoja na kuogopwa na baadhi ya watu kiasi cha wengine kumkimbia husasan wanapokutana naye nyakati za usiku.

Katika mahojiano maalum na Global TV Online, Julius ambaye anajulikana zaidi kama Mr. Shinda Nyumba, kufuatia ushiriki wake kwenye kampeni ya uhamasishaji wa shindano hilo kwa wasomaji wa Magazeti ya Uwazi, Ijumaa, Risasi, Amani na Championi, alisema kiasili ni mkazi wa Mwanza, akiwa mtoto wa pili kati ya saba waliozaliwa kwenye familia yao ambapo kwa sasa ana miaka 21.

Julius alianza kujiona tofauti akiwa Darasa la Sita, kwani alianza kujigonga mara kwa mara mlangoni huku watu wakiwemo ndugu zake wakianza kushangazwa na aina ya ukuaji wake na nyakati zingine kugeuka kivutio na mshangao kwa wanafunzi wenzake na watu wengi waliokutana naye.

“Nimeanza kuonekana mara kwa mara kwa siku za hivi karibuni tu, nilikuwa najificha ndani muda mwingi nikiogopwa kushangaliwa na watu, nakumbuka kuna siku nilikuwa naelekea nyumbani majira ya usiku nikakutana na jamaa, aliponiona alianza kukimbia huku akipiga mayowe, nikajitahidi kumuelewesha kuwa mimi ni binadamu wa kawaida, lakini bado akazidi kukimbia, huwa najisikia vibaya ni kama mateso kwangu.

“Lakini pia kwa upande wa faida ni kwamba nilisomeshwa bure na mzee mmoja ambaye ni Meja wa Jeshi, Idd Kipingu baada ya kuvutiwa na urefu wangu hivyo akanisajiri kwenye timu ya basketball, malengo yangu ni kwenda nchini Marekani kutimiza ndoto yangu ya kucheza kikapu, Hashim Thabeet huwa ananifariji sana, tunafahamiana,” alisema Julius au Mr. Shinda Nyumba. VIDEO:

JPM: Naujua Umaskini, Nimeuza Maziwa na Furu

$
0
0
Rais John Magufuli, amesema ataendelea kuwatetea Watanzania maskini na wenye kipato cha chini kwa sababu hata yeye ameishi maisha duni.

Magufuli ameyasema hayo leo Jumatatu, Julai 10 wilayani Chato wakati wa uzinduzi wa nyumba 50 zilizojengwa na Taasisi ya Mkapa Foundation.

“Nimeuza maziwa, nimeuza furu, nimechunga ng’ombe. Sitaki nisahahu nilipotoka, sitaki nisahau maisha ya Watanzania, sitaki Watanzania wenye maisha ya chini waonewe,” amesema.

Sababu za Ngeleja Kurejesha Fedha zabainishwa

$
0
0
MBUNGE wa Jimbo la Sengerema, William Ngeleja amesema moja ya sababu za kurudisha fedha za mgawo wa kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwa katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ni kugundua aliyempa fedha hizo, amehusishwa na kashfa ya kuzipata kinyume cha sheria.

Waziri huyo wa zamani wa Nishati na Madini, amerudisha serikalini kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Sh milioni 40.4 alizopewa kama msaada na mfanyabiashara James Rugemalira wa Kampuni ya VIP Engineering and Marketing Ltd ya Dar es Salaam. Aliwaambia waandishi wa habari Dar es Salaam jana kwamba alipokea fedha hizo bila kujua kuwa zilikuwa zinahusishwa na kashfa ya Tegeta Escrow kama ilivyo sasa.

Alisema fedha hizo alizipokea kwa nia njema kama msaada au mchango ili zimsaidie katika kutimiza majukumu yake ya kibunge hususan kusaidiana na wananchi wa jimbo lake kutekeleza shughuli za kijamii ikiwemo kujenga misikiti, makanisa na kusaidia wanafunzi wasiojiweza na kusaidia miradi ya maendeleo ambayo haipo kwenye Bajeti ya Serikali.

“Fomu ya tamko langu kama kiongozi wa umma kuhusu rasilimali na madeni kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Namba 13 ya mwaka 1995 kwa kipindi kilichoishia Desemba 31, 2014 niliyoiwasilisha ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Desemba 24, 2014 ilijumuisha msaada huu,” alieleza. Aidha, Ngeleja alisema Januari 15, 2015 alilipa kodi kwa TRA kiasi cha Sh 13,138,125 ikiwa ni sawa na asilimia 30 ya msaada huo aliopewa kama ilivyoelekezwa na TRA.

“Nilipokea msaada huu kama wapokeavyo wabunge wengine kwa nia njema, bila kujua kwamba Rugemalira baadaye angekuja kuhusishwa na kashfa ya fedha za akaunti ya Escrow kama ilivyo sasa,” alisema Ngeleja akirejea kufikishwa mahakamani mwezi uliopita kwa Rugemalira na mshirika wake wa kibiashara, Habinder Sethi wakihusishwa na utakatishaji wa fedha hizo zilizotokana na Akaunti ya Tegeta Escrow.

Alisema ameamua kurudisha fedha hizo, kwa kuwa imedhihirika kwamba aliyempa msaada anatuhumiwa kwenye kashfa ya akaunti ya Escrow, hivyo amepima na kutafakari na hatimaye kuamua kwa hiari yake kurejesha fedha hizo serikalini bila kujali kwamba alishazilipia kodi ya mapato. “Nimeamua kurejesha fedha hizi hata kama aliyenipa msaada bado ni mtuhumiwa tu, kwa vile hajathibitika kupatikana na hatia, kwa sababu sitaki kuwa sehemu ya kashfa na tuhuma hizi,” alieleza mbunge huyo na kuongeza: “Nina zaidi ya miaka kumi na miwili nikiwa kiongozi wa umma na pia niliwahi kuitumikia Wizara ya Nishati na Madini… lakini sijawahi kukumbwa na kashfa ya rushwa au ufisadi.

Kwa hiyo nimesononeka na kufadhaika sana kuona kuwa msaada niliopewa sasa unahusishwa na tuhuma.” Ngeleja alisema, “nimerudisha fedha hizi ili kulinda heshima na maslahi ya nchi yangu, chama changu CCM, serikali yangu, jimbo langu la Sengerema, familia yangu na heshima yangu mwenyewe.” Alisema kupokea msaada ni jambo la kawaida, ila ikibainika msaada unaopewa una harufu ya uchafu hata kama haujathibitishwa na vyombo husika ni vyema kujiepusha nao.

Pia alimpongeza Rais John Magufuli kwa kazi kubwa anayoendelea kuifanya kwa maslahi ya Taifa na kwamba anaungana na Watanzania wazalendo kumuombea kwa Mungu na kuahidi kuendelea kumuunga mkono kwa kupigania maendeleo ya nchi. Hata hivyo, alipoulizwa kuhusu suala la makinikia, alisema hawezi kulizungumzia suala hilo kwa kina kwa kuwa lipo katika uchunguzi kwa sasa.

Mjadala wa Kijinga wa Kingereza cha Kocha Mayanga na Ulimbukeni Wetu

$
0
0
INAWEZEKANA ikawa ni vizuri sana kuwa mtu ambaye unajivunia sana kujua lugha ya wenzako wakati ya kwako huijui vizuri? Mtu gani ambaye angeweza kufurahia kukijua Kingereza wakati akiwa debe tupu unapozungumzia lugha yake ya Kiswahili! Hivi karibuni, Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Salum Mayanga alionekana kushindwa kujibu maswali ya Kingereza aliyoulizwa na mtangazaji wa SuperSport ya Afrika Kusini.

Mara baada ya mechi ya mshindi wa tatu ya michuano ya Cosafa ambayo Tanzania iliing’oa Lesotho kwa mikwaju ya penalti 4-2 na kushika nafasi ya tatu, ndipo alipohojiwa na kuonekana kweli alipishana na maswali. Kwa hali ya kawaida ilionekana Mayanga anaweza kuwa anajua Kingereza cha kubabia kama Watanzania wengi tulivyo.

Lakini kasi ya uzungumzaji ya mtangazaji huyo mwanadada ambaye kawaida anaangalia muda wa runingani, ilimfanya ashindwe kuelewa ameulizwa nini.
Baada ya hapo, baadhi ya Watanzania ambao ninaamini hawakijui Kingereza hata zaidi ya Mayanga walianza kukisambaza kipande cha video ya Mayanga akishindwa kujibu swali hilo na kutaka kuamsha mjadala.

Mjadala ambao mimi hakika nauona ni wa kijinga sana, usio na maana hata kidogo na ambao unatufanya tuonekane ni watu tusiokua kwa kuwa bado tunaamini Kingereza ndiyo kila kitu katika maisha ya mtu aliyefanikiwa. Siku chache kabla, Elius Maguri aliulizwa Kingereza akajibu Kiswahili.

Mjadala tena ukazushwa, wengi wakaanza kuhoji kwa nini ajibu kwa Kiswahili wakati aliulizwa kwa Kingereza. Sisi Watanzania tunataka nini hasa? Aliyejibu kwa Kiswahili tumemuamshia mjadala tukiamini anakosea sana.

Aliyejibu kwa Kingereza cha kubabia, naye anaonekana alikosea sana na wengine wanasema angejibu kwa Kiswahili! Itafikia tupeleke maombi ya kupeleka walimu wa Kingereza katika shule za sekondari kuwa makocha ili waweze kujibu Kingereza baada ya mechi. Nenda Ujerumani, utashangaa wasivyo na habari na hicho Kingereza, nenda Hispania ndiyo utashangaa kabisa. Kweli wao ni wakubwa kimaendeleo.

Sasa Kiswahili kitakua lini kama tutaendelea kuzodoana kama mtu anayezungumza Kiswahili ataonekana hafai? Ukiwa Afrika Kusini, mara nyingi wenyeji wanakusisitiza kuzungumza Kizulu au Xhosa. Lugha mbili kubwa zaidi nchini humo hasa kama watakuona ni mweusi.
Wanataka Kingereza waachiwe Wazungu na wale wanaowaita ‘Makaladi’. Sasa shida iko wapi kujiamini katika lugha yetu? Tunachekana sana hadi inafikia Kiswahili kinaonekana ni kama ushamba kukizungumza runingani hasa inapokuwa katika michuano ya kimataifa! Huenda Mayanga naye alishindwa kujiamini kwa hofu ya kuonekana alizungumza Kingereza. Lakini alipaswa kuachana na hofu ya Kingereza chao, sahihi kabisa na mwisho kama akipata nafasi kama hiyo asiwe na hofu, atandike Kiswahili cha kutosha. Wengi waliomzodoa na kumbeza eti hakuongeza Kiswahili, hawakutumia njia nzuri zaidi ya kutaka kuonyesha kakosea sana huku wengi nawajua Kingereza pia kinawapiga chenga na hawawezi kuzungumza kwa majibizano ya zaidi ya dakika tano maana lazima “umeme utakata”. Waandaaji wa michuano yoyo
te kama Cosafa nao wanatakiwa kuweka nafasi kwa mahojiano ya Kiswahili. Safari nyingine kama Stars itaalikwa, basi Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) inapaswa kuonyesha inakithamini Kiswahili na kuhakikisha kunakuwa na wakalimani.

Mimi sitamzodoa yeyote aliyezungumza Kingereza cha kubabia, badala yake nitampongeza na kumsisitiza kuzungumza Kiswahili safi mbele ya wanaoweza kukisikia na siku moja wajifunze. Tuachane na zile hisia kwamba anayezungumza Kiswahili hawezi kuwa msomi, mjanja au mtu anayejitambua. Siku hizi mambo yamebadilika, kujivunia Kingereza kupita kiasi nao ni ushamba tu. Kwa wanaopata bahati ya kusafiri wataungana nami. Vizuri kujifunza Kingereza na lugha nyingine, lakini Kiswahili kiwe nembo ya Mtanzania. Badilikeni.

Stori: Saleh Ally Simu: +255 654 948888 Email: salehkubwa@gmail.com

Watu 16 Waaga Dunia Kwa Ajali ya Ndege

$
0
0
Watu 16 wamefariki kwenye ajali ya ndege ya jeshi la Marekani aina ya C-130 Hercules kwenye Jimbo la Mississipi nchini Marekani, ambayo imetokea katika eneo la LeFlore karibu kilomita 160 Kusini mwa mji mkuu wa jimbo hilo, Jackson.

Taarifa zimeeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mlipuko mkubwa uliotokea ndani ya ndege hiyo yenye injini nne.

Kwa mujibu wa jarida la Jimbo la Mississipi, ndege hiyo ilianguka katika shamba moja na mabaki yake yakatapakaa eneo hilo.

Aidha imeripotiwa kuwa miili ya marehemu 12 kati ya 16 wa ajali hiyo imepatikana katika eneo hilo ikiwa imeungua vibaya kwa moto.

C-130 Hercules ni ndege ya jeshi ambayo hutumika kusafirishia mizigo ya jeshi, kuzima moto na majanga ya aina mbalimbali.

Chanjo ya Ugonjwa wa Kisonono yapatikana

$
0
0
Gonorrhoea imekuwa taabu kutibika kwa sababu imezoea antibiotic

Wanasayansi nchini New Zealand wameonyesha kwa mara ya kwanza kwamba chanjo inaweza kutoa kinga dhidi ya ugonjwa wa kisonono.

Watafiti kutoka chuo kikuu cha Auckland wamegundua kuwa maambukizi ya ugonjwa huo wa zinaa yameshuka kwa takriban theluthi moja miongoni mwa watu ambao walipata chanjo dhidi ya homa ya manjano.

Watafiti hao wamefuatilia kutoka kwa vijana milioni moja waliopata chanjo hiyo pindi kulipotokea ugonjwa wa homa ya manjano nchini New Zealand.

Kisonono imekuwa taabu kutibika kwa sababu imezoea dawa za antibiotic.

Mwandishi wa BBC wa masuala ya afya anasema utafiti huu unaonyesha inawezekana kuwa na chanjo dhidi ya ugonjwa.

Maswali 5 Tata Kwa Ngeleja Baada ya Kutangaza Kurudisha Pesa za Escrow

$
0
0
Nikupongeze kwa hatua uliyoamua kuichukua ya kurejesha huo mgao wa Escrow......Lakini naomba ujibu haya maswali...

1.Ulichukua huo mgao kwa kazi gani?
2.Wewe na aliyekupa mlikua na mahusiano gani?
3.Kilicho kufanya urejeshe hizo fedha ni kipi? a) ni mali ya umma. b) Ulipokea kimakosa?
4.Je hizo fedha utarejesha kwenye akaunti ya nani?
5.Kutokana na swali la 3 upo tayari kutoa ushahidi mahakamani?

Application ya UDAKU SPECIAL Ndio Mpango Mzima...Fanya Kudownload Upate Habari za Udaku, Siasa na Mahusianio

$
0
0
Download  Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE 


Au Kama Unayotayari Bonyeza HAPA Ku Update Uweze Kupata Ikiwa na Muonekano Mpya

JE Una Tatizo la Nguvu za Kiume , kukosa Hamu ya Tendo, Kushindwa Kurudia Tendo au Maumbile Madogo ya Uume?

$
0
0
JE, UNA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? SOMA HAPA 👇👇👇👇
Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, sio Tanzania tu bali duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo sio ugonjwa ila ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili.

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME HUSABABISHA MAMBO KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
@Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye kisukari kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @220,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kurudia tendo hata mara 3 bila kuchoka @130,000/=
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr.

Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no (+255)
0767447444 na 0714335378

NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara kwa mtumiaji. Zimethibitishwa kiafya.

Rais Magufuli Awaonya Wakuu wa Wilaya na Mikoa

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewaonya wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa kote nchini na kuwataka kuwa na nidhamu ya pesa na kutumia fedha za serikali vizuri.

Rais Magufuli amesema hayo leo wilayani  Chato mkoani Geita alipokuwa akihutubia wananchi katika makabidhiano ya nyumba 50 zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa, ambapo mbali ya kushukuru kwa msaada huo Rais Magufuli alizungumzia juu ya tabia ya baadhi ya viongozi wa serikali kuiba fedha za wananchi na kutumia katika mambo yao wenyewe nje ya malengo ya serikali.
"Hapa penyewe Chato kuna fedha zaidi ya bilioni moja za pembejeo zimeliwa na viongozi, hivyo natoa wito kwa viongozi wote wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa kote nchini kuwa na nidhamu na fedha za serikali, tujifunze kutumia fedha vizuri  za serikali asitokee mchwa huko kula pesa za serikali. Maana hili lililotokea hapa Chato najua limetokea sehemu nyingi na hivyo saizi tunaanza kufanya ukaguzi kila sehemu" alisema Rais Magufuli

Mbali na hilo Rais Magufuli aliwataka wananchi wa hali ya chini kuwa na amani kwani katika kipindi chote ambacho yeye atakuwa madarakani hataki kuona wala kusikia wananchi wa hali ya chini wakinyanyaswa sababu na yeye ametokea katika maisha hayo hivyo anatambua jinsi wanavyopata shida watu wa kipato cha chini.

"Serikali haiwezi kufanya biashara na masikini, inawaacha matajiri inawasumbua masikini, mimi nimekuwa katika maisha ya shida nimechunga ng'ombe, nimeuza maziwa kwa hiyo najua maisha ni nini. Najua Tanzania watu wengi wanaishi maisha ya chini na katika kipindi changu sitaki kuona watu wa hali ya chini wanapata shida, wanapata taabu ndiyo maana tunajitahidi kuhangaika kuleta maendeleo ili wanufaike na wao" alisisitiza Magufuli

Rais Magufuli akuziacha taasisi ambazo zimekuwa zikitetea wanafunzi kupata mimba na kusema yeye taasisi hizo hazipendi na ameziwekea kizingiti kuwa ikiwezekana zisipewe msaada bali taasisi zinazofanya mambo ya kimaendeleo kama taasisi ya Mkapa Foundation ndiyo zinatakiwa kupewa msaada sana kwa kuwa zinarudi kuleta maendeleo kwa wananchi.

Umesikia Walichokisema Yanga Kuhusu Dida?

$
0
0
UONGOZI wa Klabu ya Yanga umesema kuwa bado nafasi ya aliyekuwa mlinda mlango wa timu hiyo, Deogratius Munishi ‘Dida’, ipo japokuwa ameondoka klabuni hapo.

Dida amekataa kuongeza mkataba mwingine wa kuitumikia Yanga kufuatia mchakato wake wa kwenda kucheza soka la kulipwa Afrika Kusini.

Akizungumza na Championi Jumatatu, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa Yanga, Hussein Nyika, ameeleza kuwa, licha ya kuondoka kwa Dida katika timu hiyo, bado atakuwa na nafasi yake iwapo atahitaji kurejea kikosini hapo.

“Dida siyo mchezaji wetu kwa sasa kwani mkataba wake umeisha mwezi huu wa saba na sasa anakwenda Afrika Kusini kufanya majaribio, tulitaka kumuongeza mkataba mwingine lakini amekataa.

“Nafasi bao ipo wazi kwake aende kufanya majaribio na iwapo atarejea basi nafasi yake ipo, ila hatujui anakwenda timu gani,” alisema Nyika.

Hauhitaji Elimu Kubwa Sana Ili Kufanikiwa

$
0
0
Hauhitaji elimu kubwa sana ambayo haina uwezo wa kubadilisha maisha yako, elimu bora ambayo unaihitaji au  unatakiwa uipate ni elimu ya kubadilisha maisha yako, elimu ambayo itakunyanyua au kukutoa sehemu moja na kukupeleka sehemu nyingine kimaisha. Mafanikio yako makubwa yanakuja kwa kujipatia elimu inayotoa thamani ya maisha yako na sio vinginevyo.

Kwa hiyo kama kwa namna moja au nyingine umekosa elimu kubwa ya darasani na kufika mahali unajilaumu kwamba ningesoma ningefika mbali sana kimafanikio, unakosea, huu sio wakati wa kusikitika. Jifunze kutafuta elimu yenye thamani itakayobadilisha maisha yako. na habari njema ni kwamba elimu hiyo haipatikani darasani, inatafutwa mtaani kwa watu sahihi.

Ni mzigo mkubwa sana kwako na kwa jamii kwa ujumla kuwa umesoma halafu hauna mafanikio makubwa. Kama iko hivyo kwako, jiongeze kidogo tu, anza kuisaka elimu sahihi, elimu ambayo itakupa thamani sahihi ya maisha yako na kukubadilisha na kuwa mtu wa mafanikio. Maisha ya mafanikio hayaji kwa kusoma saana, bali ni kwa kujifunza vitu sahihi ambavyo vina uwezo wa kubadilisha maisha yako.

Aina 10 za Waume Ambao Wake zao Wanakereka Kuwa nao

$
0
0
1. Wanaojiona Kama Wafalme (King Husband).
HIi ni aina ya wanaume ambao hutaka kusujudiwa kama wafalme na hupenda kuwafanya wake zao kuwa kama watumwa. Hawafanyi chochote ndani ya nyumba kazi yao ni kutumatuma hata kama mke anaumwa atapaswa kuamka na kupika, wanataka waheshimiwe wao tu na mwanamke akikosea kidogo ni maneno au kipigo. Mwanamke hana kauli ndani na mume akiingia nyumbani ni kama bosi anavyoingia ofisini, wote kimya hakuna hata kuongea.

2. Wanaume Wanaojihisi Bado Hawajaoa (Bachelor Husband).
Hii ni aina ya wanaume ambao hawawashirikishi wake zao kwa chochote. Hufanya mambo kama vile bado hawajaoa, hutumia muda wao mwingi na marafiki zao wakifanya mambo ambayo mke hata hayajui mke anaweza kustukizia tu mume kanunua gari bila kumshirikisha na mume haonyeshi hata kujali kuweza kumshirikisha. Hajali kama ana mke na mda mwingi huutumia akiwa na marafiki kufanya mambo yasiyo na msingi ambayo hayana mnanufaa yoyote katika ndoa yake.

3. Wanaume Wenye Gubu (Acidic Husband).
Hawa hukasirika kila mara tena bila kua na sababu ya misngi, mambo hayaishi, kosa la mwaka juzi anaweza kukukasirikia leo. Wamemuudhi kazini hataki kusemeshwa na mnanuniwa nyinyi, mwanamke akiomba hela ya chakula ni shida ni kununa kutwa nzima, wanahasira na nirahisi kumpiga mke.

4. Mume Wa Kila Mtu (Genarel Husband).
 Hawa wanajifanya wasamaria wema, wanajali kila mwanamke, wanajali marafiki wakike wa mke na wakwao kuliko wanavyowajali wake zao. Mke anaweza kuwa na shida akasema hana hela lakini rafiki akampa. Wana marafiki wengi wakike na mara nyingi huwa hawaachani kabisa na ma X wao, wakiwalalamikia wanawasaidia kuliko hata wanavyowasidia wake zao wakati wakiwa na shida.

5. Wanaume Wanaojifanya Wagumu (Dry Husband).
Hawa wanajifanya wagumu sana, hawana yale mambo ya kimahaba na wao hujua kuwa ndoa ni kuleta chakula tu na kushughulika kitandani. Hakuna kuongea na hawajali hata hisia za mke, mke akiongea kwao wala hawajali wanajifanya ni vidume sana na wanaona mambo kama vizawadi, kupiga simu, kutuma sms, kusema nakupenda, kununua maua ni mambo ya kike, yaani hawaonyeshi juhudi yoyote kuwafurahisha wekea zao.

6. Wanaume Wanaopenda Kutumia Wake Zao (Panadol Husband).
Hawa huwa wanaume pale tu wanapokuwa na shida, wanakuwa na wake wazuri wanaowajali lakini wao wala hawajali. Wanapomhitaji mwanamke, wanapotaka mwanamke awafanyie kitu flani basi huja na maneno mazuri na hata kuleta vizawadi, wanajua udhauifu wa wake zao na huutumia kuwalaghai kuwatimizia mahitaji yao lakini wanapotimiziwa tu basi husahau hata kama wanawake, hawajali tena.

7. Wanaume Ambao Hawataki Kukua (Baby Husband).
 Bado wanatabia za kitoto, hawawezi kufanya maamuzi yao wenyewe mpaka kuuliza kwa ndugu zao, mtu kaoa lakini kila siku humpigia simu Mama yake kuuliza hiki na kile. Yaani wakiongea kitu na mke nilazima aulize ndugu kwanza ndiyo kipitishwa na mke akifanya kosaa kidogo kazi nikulinganisha mke na ndugu zake, mbona flani alifanya hivi, flani anaweza fanya zaidi na mambo kama hayo. Kwakifupi hawawezi kufanya maamuzi na mkewe, ndugu zake hasa Mama yake anakuwa kama shemeu ya ndoa.

8. Mume Mtalii (Visiting Husband).
Hawa wanakuja nyumbani kama wageni vile, mume ataihudumia familia yake kwa kila kitu lakini hawezi kuipa muda wake. Akirudi mke na watoto wamelala ni kugonga na hana sababu za msingi za kuchelewa, hata mwisho wawiki hupenda kutumia na marafiki au ndugu lakini si na mke. Hakuna kitu cha pamoja ambacho anafanya na mkewe au watoto wake, kila akiingia tu anakua na safari ya kutoka yaani hata atoke akakae nnje tu lakini si kukaa na mke au watoto.

9. Wanaume Wanaofuatilia Kila Kitu (Stalking Husband). 
Hii ni aina ya wanaume ambao hufuatilia kila kitu, huchunguza kila kitu mwanamke anachofanya na hawampi pumzi. Akienda sehemu atachunguza anaenda na nani na alikutana na nani, huwa na wivu wa ajabu ajabu na kila saa huhisi wake zao ni wasaliti. Kila mtu mwanamke anayeongea naye wa jinsia tofauti huhisi ni mchepuko na hata marafiki wa mke wakike pia huhisi wanamkuwadia, kwakifupi hampi pumzi mwanamke.

10. Mwanaume Mbahili (Miserly Husband).
Huyu anaweza kuwa na hela lakini mbahili ajabu. Akimpa mwanamke hela atafuatilia matumizi yake mpaka senti ya mwisho, anafuatilia mpaka mambo ya jikoni. Sukari ikiisha naataka ajue iliisha ishaje na kila mara huhisi mke anamuibia hela labda akajenge kwao, huwa msumbufu sana na mgumu kutoa hela. Mwanamke akifikiria mchakato wa kuomba hela kwa mume hukata tamaa na wakati mwingine kuamua tu kukaa kimya na matatizo yake.

Diamond Platnumz Aweka Wazi Ufreemanson Wake......

$
0
0
Nyota wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’ ameendelea kuzua maswali kuwa ni memba wa jamii ya siri inayodaiwa kumwabudu shetani, Freemason au La? tetesi hizo zilianza kitambo lakini sasa zimeshika kasi baada ya kuonekana amevaa cheni za misalaba kwenye moja ya video yake aliyotoa hivi karibuni ya 'ENEKA', Kwamujibu wa wataalamu wa mambo wanadai msalaba pia umo kwenye listi ya alama za Freemason

Tazama picha hapo chini...

Simba Wanne Watoroka Mbugani South Africa

$
0
0
Simba wanne watoroka mbuga ya taifa Afrika Kusini

Walinzi wa mbuga nchini Afrika Kusini wanawattafuta simba wanne waliotoroka kutoka mbuga ya kitaifa.

Simba hao walitoroka kutoka mbuga ya Kruger siku ya Jumapili na mara ya mwisho walionekana katika kijiji cha Matsulu.

Usimamizi wa mbuga hiyo sasa umewataka wenyeji kuchukua tahadhari

Haijabainika vile simba hao walifanikiwa kutoroka kutoka mbuga hiyo inayozungukwa na ua.

Mbuga ya kitaifa ya Kruger ni moja ya mbuga kubwa zaidi barani Afrika ikiwa na ukubwa wa kilomita 19.485 mraba.

Kisa hiki kinatokea baada ya simba wengine watano kutoroka mbuga hiyo mwezi Mei. Wanne walipatikana lakini mmoja bado hajulikani aliko.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images