Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

Simu za Mabinti Kuharibika Mnapoanza Uhusiano

$
0
0
Bandugu,

Imekuwa kama fashion siku hizi ukianza uhusiano na binti, ile mmebadilishana namba na kesho ndo first date, tarajia kuambiwa 'simu imeingia maji, imechukuliwa na mwenyewe' na upuuzi kama huo.

Nime experience kwa mabinti kama watatu hasa under 25s! Sasa sijui kwanini hawaambiani kuwa hii trick imegundulika wabadili gia.

Haitham Atoboa Siri kwanini Wema Sepetu Hakutokea Kwenye Video yake

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva, Haitham amefafanua sababu ya Wema Sepetu kutoonekana katika video ya ngoma yake mpya ‘Play Boy’ ambayo amemshirikisha mrembo huyo.



Haitham amesema kulikuwa na mipango ya kufanya video na Wema na script ilikuwa tayari imeshaandikwa ila alipokosekana ilibidi wabadilishe.

“Na script ambayo tumefanya sasa inayoonekana kwenye video wasichana watatu ilibadilishwa fasta baada ya Wema kutokutokea kwenye video, so script ya mwanzo ambayo Wema alipaswa kuwepo aliandika yeye director na baada ya mabadiliko kutokea akabadilisha scrip,” ameiambia E-News ya EATV.

Kuhusu athari zilizojitokeza baada ya Wema kutokuwepo kwenye video,  amesema “kwa upande wingine yameathiri kidogo sio sana kwa sababu kuna baadhi ya mashabiki wa Wema walitamani kumuona kwenye video, kwa hiyo ameathiri kidogo kwa wale mashabiki walikuwa wanatamani kumuona,” amesisitiza.

Play Boy ni ngoma ya pili kwa Wema Sepetu kushirikishwa na msanii wa Bongo Flava baada ya ile ya mwanzo ‘Shoga Yake Mama’ aliyopewa shavu na Snura, lakini hizo zote hakuna hata moja Wema ametokea kwenye video.

Kimenuka....Baada ya Mkuu wa Wilaya ya Hai Kuharibu Shamba Lake, Mbowe amfikisha Mahakamani

$
0
0
Kampuni ya Kilimanjaro Veggies Ltd inayomilikiwa na Freeman Mbowe, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imefungua kesi katika Mahakama Kuu, Kanda ya Moshi dhidi ya Mkuu wa Wilaya ya Hai, Gelasius Byakanwa.

Imefungua kesi hiyo dhidi ya mkuu huyo wa wilaya kwa kuwa ndiye anayedaiwa kushiriki uharibifu wa miundombinu ya shamba la mbogamboga inalolimiliki wilayani Hai, Mkoa wa Kilimanjaro.

Kesi hiyo ambayo iko chini ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Moshi, Aishael Sumari, ilifunguliwa Juni 30, mwaka huu na Kampuni ya Uwakili ya D’ Souza& co ya jijini Arusha kwa niaba ya kampuni hiyo.

Kesi hiyo ina mashauri mawili ambayo ni shauri la ardhi namba 20/2017 na maombi madogo namba 51/2017.

Maombi hayo madogo namba 51/2017, yaliletwa kwa hati ya dharura ambapo mdai anaomba zuio la muda liweze kutolewa dhidi ya mdaiwa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Hai asiweze kufanya chochote katika eneo la shamba la hekari 2.7 lililopo katika Kijiji cha Nshara, Kata ya Machame Kaskazini, wilayani Hai, Mkoa wa Kilimanjaro.

Aidha, katika kesi hiyo, madai ya msingi ni zuio dhidi ya mdaiwa na wafanyakazi au mtu yeyote asiweze kuingilia eneo husika, mdaiwa aombe radhi kwa vitendo alivyovifanya ikiwa ni pamoja na kulipa fidia ya Sh milioni 549.3 kama hasara aliyoipata mlalamikaji.

Mashauri hayo yamepangwa kusikilizwa Julai 13, mwaka huu.

Bongo Hakuna Kama Ali Kiba Wengine Wote Takataka....Harmorapa Afunguka....

$
0
0
RAPA chipukizi ambaye haishiwi vituko Harmorapa, amefunguka na kusema Alikiba ni msanii ambaye amekosa mfano hapa Tanzania kutokana kazi zake na namna ambavyo amekuwa akifanya mambo yake nje ya muziki.

Harmorapa amesema hayo siku chache baada ya Alikiba kudondoka wino na kampuni ya usimamizi wa kazi za wasanii RockStar4000 na kuwa Mkurugenzi wa muziki na vipaji  wa kampuni hiyo, pia kuwa sehemu ya wamiliki wa kampuni ya Rockstar4000 Music Entertainment Co & Rockstar Television.


“Katika vitu ambavyo tunatakiwa kujivunia ni kuwa na wasanii ambao wanatangaza taifa letu mbele na kujivunia juhudi zao. Naimani heshima, busara na juhudi ndiyo nyenzo pekee zilizowafanya wazungu kumwaga wino na kumkaribisha Alikiba meza moja na kumkabidhi kampuni kubwa ya Rockstar4000 kuwa mmiliki mmoja wapo na Director” alisema Harmorapa

Mbali na hapo Harmorapa aliwataka wasanii wengine kujifunza na kujivunia uwepo wa Alikiba kwani amekuwa akiutendea haki muziki wa bongofleva na kuipeperusha vizuri bendera ya Tanzania nje ya nchi.



“Wasanii wa Tanzania inabidi tujifunze na kujisifu kwa kuwa na King Alikiba maana anautendea haki mziki wetu wa bongo fleva, hongera zangu zizidi kutiririka kwa King wewe uliokosa mfano hapa bongo” alisisitiza Harmorapa

Harmorapa ni kati ya wasanii ambao wamekuwa na mapenzi sana na Alikiba kwani mara kadhaa amekuwa mstari wa mbele kuonyesha mapenzi yake hayo kwa msanii huyo na kuonyesha jinsi gani anamkubali, kiasi cha kuhangaika sana japo aweze kufanya naye collabo, Harmorapa alishawahi kusema uongozi wake unahangaika kuona kama wanaweza kupata fursa ya kufanya kazi na Alikiba.

Dunia Imekwisha...Mwalimu wa Kiume Abakwa na Wanawake Watatu Wakitaka Mbegu zake za Kiume

$
0
0

 MWALIMU mmoja wa kiume, mwenye umri wa miaka 39, amelazwa hospitalini nchini Zimbabwe baada ya genge moja ya wanawake watatu kumteka, kumlewesha kwa madawa na kufanya naye ngono kabla ya kumtekeleza kando ya barabara.

Mtu huyo kutoka sehemu ya Makoni, Wilaya ya Chitungwiza, nchini humo aliachwa akiwa na majeraha na michubuko kwenye sehemu zake za siri ambapo madaktari wa hospitali ya Waza waligundua alikuwa pia amenyanyaswa kingono.


Polisi wanawatafuta wanawake watatu wanaodaiwa kuwa sehemu ya “genge la manii” ambapo huwanasa watu wanaokutwa barabarani pake yao au wasafiri na kuwashambulio ili kuchukua manii yao (nguvu za kiume) kwa ajili ya kuyatumia kwa kile kiitwacho “bahati njema”.

Mtu huyo aliiambia polisi kwamba wakati akisubiri basi kituoni Julai 2 mwaka huu, alipewa lifti katika gari dogo la rangi ya bluu aina ya BMW likiwa na namba za usajili za Afrika Kusini lililokuwa linaendeshwa na mwanamme.

Ndani ya gari hilo kulikuwa na wanawake watatu. Baada ya hapo, alisema alipewa kinywaji cha kawaida akiwa ndani ya gari hilo na baadaye kukinywa alijisikia kizunguzungu na kulala.

JE Wajua Kwanini Wanaume Huishiwa na Nguvu za Kiume na Kushindwa Kupiga Game Kisawasawa?

$
0
0
KUISHIWA nguvu za kiume ni jambo la kawaida kwa wanaume wengi hasa wenye umri mkubwa. Hatari ya kupungukiwa nguvu za kiume huongezeka kutokana na umri. Kulingana na tafiti za kitabibu, wanaume wenye umri kuanzia miaka 60 tatizo hili ni kubwa kwao kuliko wanaume wenye umri wa miaka 40.

Wanaume wenye elimu ndogo juu ya utendaji kazi wa mwili na afya ndiyo wanaokabiliwa sana na tatizo hili. Hii ni kwa sababu wanashindwa kuelewa aina ya chakula kinachoongeza nguvu za kiume na za mwili kwa ujumla, mtindo wa maisha wanayotakiwa kuishi ili kupunguza hatari hiyo, wanakunywa pombe na hawafanyi mazoezi ya viungo.

Mazoezi ya mwili hupunguza hatari ya kupungukiwa nguvu za kiume. Tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume linaweza kuwa na sababu za kihisia (emotional causes) lakini sababu nyingine hutokana na maradhi kama vile kisukari na shinikizo la juu la damu. Inakadiriwa kuwa asilimia 50 hadi 60 ya wanaume wenye maradhi ya kisukari wana tatizo hili.

Watu wanaosumbuliwa na kiharusi na ulevi nao wana hatari kubwa sana kwa sababu ya uharibifu wa korodani yaani testicles kutokana na ulevi sugu na kupoteza testerone. Pombe hupunguza kwa kiasi kikubwa uzalishaji wa manii au mbegu za kiume.

Watu wanaosumbuliwa na shinikizo la damu, magonjwa ya tezi, majeraha kama vile kutokana na upasuaji wa  viungo vya uzazi, matumizi ya dawa zenye kemikali bila mpangilio au ushauri wa wataalamu na maradhi ambayo hudhoofisha mtiririko wa damu kwenye uume. Hata hivyo, upungufu wa nguvu za kiume unatibika katika umri wa rika zote.

Vipengele ambavyo daktari atahitaji kuvifahamu kabla ya kuanza kukutibu tatizo la kuishiwa nguzu za kiume ni;Umri wa mgonjwa, jumla ya afya aliyonayo kwa sasa, utendaji wa tendo la ndoa zamani na sasa, migogoro ya ndoa, kifamilia, kazi nk.

TIBA Ni muhimu wewe kujisikia vizuri na kumwamini daktari wako, kisaikolojia utakuwa umepiga hatua ya kwanza ya kupata nafuu ya tatizo linalokukabili, nenda akakupime na anaweza kukupa dawa kama ataona inafaa. Kwa ushauri wa bure piga au tuma ujumbe namba zilizopo hapo juu.

TCAA yapiga Marufuku Kununua, Kurusha ‘Drones’ Bila Kibali Maalum

$
0
0

Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imepiga marufuku urushwaji angani wa vifaa vya kieletroniki visivyo na rubani (drones) bila kupata kibali maalum.


Kupitia tangazo lake kwa umma, TCAA imesema kuwa kwa taasisi au mtu binafsi kufanya majaribio au kurusha drones, ni lazima apate idhini ya Wizara ya Ulinzi na Usalama pamoja na Mamlaka hiyo.


“Ifahamike kuwa kuanzia sasa, taasisi au mtu binafsi anayetaka kununua, kufanya majaribio au kurusha angani vifaa hivyo visivyotumia rubani anapaswa kupata idhidi ya Wizara ya Ulinzi na Usalama pamoja na kibali kutoka TCAA,” imeeleza taarifa ya Mamlaka hiyo.


Taarifa hiyo iliyosainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Hamza Johari imefafanua kuwa uendeshaji wa shughuli zote za anga nchini uko chini ya Mamlaka hiyo kwa mujibu wa sheria na kanuni zilizopo.


Tangazo hilo linakuja wakati ambapo kumekuwa na urushwaji wa drones unaofanywa na watayarishaji wa video za muziki kwa lengo la kuchukua picha za juu, pamoja na taasisi mbalimbali zinazochukua matukio husika hasa yanapofanyika katika maeneo ya wazi.


Drones zilitumika zaidi katika uchaguzi wa mwaka 2015 ambapo mikutano ya kampeni za wanasiasa ilikuwa ikipigwa picha za juu kuonesha umati uliohudhuria.

Chadema Yapata Pigo Jingine...Diwani Ahamia CCM

$
0
0

Diwani wa Ngabobo (Chadema), Solomon Laizer ameandika barua ya kujiuzulu udiwani na kujiunga na CCM kwa maelezo kwamba anamuunga mkono Rais John Magufuli.

Laizer ni diwani wa tano katika Halmashauri ya Meru kujiuzulu kwa kutoa sababu kuwa anamuunga mkono Rais Magufuli.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Christopher Kazeri amethibitisha leo (Julai 11) kupata taarifa za kujiuzulu kwa Ngabobo.

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari amesema kujiuzulu kwa diwani huyo ni mchezo mchafu akidai  amenunuliwa.

Amesema tayari walipata taarifa za diwani huyo kushawishiwa kujiuzulu na kwamba, alifuatwa na viongozi wa wilaya na kanda wa chama hicho aliowaeleza kuwa ameshawishiwa.

“Baadaye alieleza hataondoka lakini naona wamefanikiwa kumshawishi, tunashangaa viongozi wa Serikali badala ya kufanya kazi za maendeleo wanafanya kazi za kushawishi madiwani wa upinzani kuhama,” amesema.

Hata hivyo, madiwani wanaohama wanapinga kuwa wameshawishiwa kufanya hivyo.

Hadi sasa madiwani watano wa Chadema waliojiuzulu ni Credo Kifukwe wa Kata ya Murieti jijini Arusha.

Wengine waliojiuzulu katika Jimbo la Arumeru Mashariki na kata zao kwenye mabano ni Anderson Sikawa (Leguruki), Emmanuel Mollel (Makiba), Greyson Isangya (Maroroni) na Josephine Mshiu (Viti Maalumu).

Bodi ya Mikopo yawazidi mbinu wadaiwa sugu

$
0
0

Bodi ya Mikopo ya Mikopo ya Elimu ya Juu  limefanikiwa kwa asilimia 46 kukusanya Mikopo kwa wadaiwa sugu hadi kuvuka makadiro yao

hayo yameelezwa naMkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Bwana Abdulrazak Badru alipokuwa akizungmza na  waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, kuhusiana na hali ya makusanyo ya mikopo kwa wanufaika wa elimu ya juu, ambapo walilenga kukusanya Shilingi Bilioni 76 lakini wamekusanya Shilingi Bilioni 116 ikiwa ni kiwango cha marejesho cha asilimia 46.

Bwana Badru amesema, hataacha kutumia mbinu ya ufuatiliaji mahala pa kazi huku akiwakumbusha wale ambao wanashindwa kurejesha mikopo kwa hiari sheria itafuata mkondo dhidi yao kwani fedha hizo hutumika kwa wanafunzi wa awamu mpya ya masomo.

Aidha, Bwana Badru ametoa onyo kali kwa waajiri ambao wameshindwa kuwasilisha majina ya waajiriwa wao ndani ya siku 28 kwa bodi hiyo, kuchelewesha makato baada ya kuwakata waajiriwa ama kuficha taarifa kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

JE Wajua Wanaume Waliochelewa Kuoa Wana Msongo wa Mawazo Kuliko Wanawake?

$
0
0

Kuna utafiti nilikuwa nafanya baada ya kufwatilia baada ya kuona topic nyingi zinazowasema single mother's na wanawake waliofika miaka 30s bila kuolewa.

Nilichokigundua;

1. Wanawake waliochelewa kuolewa na na single mother wengi wana amani ya moyo kuliko wanaume waliochelewa kuowa na single dads ndomana awaishi kujaza JF topic za kuwazungumzia wanawake hiyo yote nikujipa moyo ili kupunguza maumivu.

2. Wanaume wengi waliochelewa kuoa mpaka kufika miaka 35 na kuendelea wengi walitegemea kuchelewa kuoa kutawafanya wawe na pesa na maisha mazuri lakini imekuwa tofauti wengi wamefika umri huo wakiwa hawana kitu tofauti na wenzao waliooa mapema wana faraja ambayo ni watoto na wengine wamepata baraka maisha yamewanyookea,asila za kukosa vyote vinawatesa wanajikuta na asila muda wrote poleni kwa hilo.

3. Wanaume wengi waliochelewa kuoa wanatabia zisizovumilika bila kusahau maneno mengi bila vitendo ujuaji mwingi na dharau kwa wanawake wanasahau walizaliwa na mwanamke poleni, mwanamke yoyote anatakiwa kuheshimiwa.

NB; Jirekebisheni tabia njema si kwa mwanamke mtu hata mwanaume unatakiwa ujitambue labda ujitahidi uwe na mapesa kama Mengi ndo utapata mtoto mzuri wakutuliza moyo wako ukifika 40s maana huwa mnajipa moyo wanaume amzeeki.

Tafiti: Maji ya Mtu Msimbazi yana Sumu

$
0
0

MAJI ya Mtu Msimbazi yamebainika Kuwa yana 'sumu' ambayo hayawezi kuwa Makazi salama kwa viumbe hai

Serikali imechukua sampuli ya maji ya Mto huo kwa ajili ya kayafanyia Tafititi ili kubaini kiwango cha sumu na ubora wa maji yake kwa matumizi ya binadamu.

Emanuel Gwae, Meneja wa  Maabara ya Mazingira  wa Ofisi ya Mkemia Mkuu, amsema kuwa maji hayo hayana oksijeni ya kiwango cha  milimita3.3  alipokuwa akitoa matokeo ya awali kwa wandishi wa habari leo, 

Amesema  kuwa maji  hayo sio salama kwa viumbe hai

Ommy Dimpoz Atoboa Siri ya Kukaa Muda Mrefu Uarabuni

$
0
0

Baada ya tetesi zilizovuma karibia mwezi wote wa Marchi mwaka huu kuwa Msanii wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz anakula bata Dubai kwa pesa za kupewa na Tajiri mmoja hapa Nchini, hatimaye msanii huyo anaetamba na ngoma yake ya Cheche amefunguka A-Z siri ya yeye kukaa Dubai kwa kipindi kirefu.


Ommy Dimpoz amesema wakati anafika Dubai akitokea Marekani ambako alikuwa na AliKiba mwezi wa Marchi aliposti picha kwenye mtandao wa Instagram mapema alivyotua Dubai na kuweka Hashtag ya #HelloDubai hapo ndipo dili lilipoanza kwani alianza kutafutwa na Bodi ya Utalii ya Dubai kwa lengo la kufanya nae kazi.


Ommy Dimpoz amesema alitumiwa E-mail na Bodi ya Utalii ya Dubai wakimtaka kuongeza siku za kukaa Dubai kutoka siku tatu ambazo alipanga mpaka mwezi mmoja huku akitembezwa maeneo yote muhimu ya Utalii ndani ya Dubai na kupigwa picha na kuposti kwenye mtandao wake wa Instagram.

Kwa maelezo ya Ommy Dimpoz amesema likes na Komenti nyingi zilizotolewa kwenye picha hiyo ziliwaogopesha watu wa Bodi ya Utalii mpaka kutamani kufanya nae kazi.

“Wakati natoka Marekani kwenye Tour ya Ali nilipofika Dubai nilipiga picha  na kuweka Hashtag ya #HelloDubai ambayo ilipata likes kibao so bodi ya utalii ikaona ile Hashtag na wakanitumia Email wakitaka kufanya kazi na mimi“,amesema Ommy Dimpoz kwenye mahojiano yake na East Africa Radio.

Ommy Dimpoz amesema Bodi hiyo ilimtaka atembezwe kwa helkopita kwenye maeneo muhimu ya Dubai na kuposti picha akiambatanisha na Hashtag ya #VisitDabai ikabidi aingie mkataba nao wa kibiashara uliomuweka kwa mwezi mmoja Dubai.

Hata hivyo, Ommy Dimpoz ameishauri Serikali kutumia wasanii wa ndani kuweza kuitangaza nchi yetu kimataifa kwani wana wafuasi wengi kwenye mitandao ya kijamii.

“Unajua watu wengi huwa wanapenda kujaji maisha kwenye picha mimi napenda hata kuishauri Serikali yetu kufikiria mara mbili suala la kuwatumia Wasanii wa ndani kuitangaza nchi kwenye sekta ya utalii kwani wana followers wengi,“amesema Ommy Dimpoz.

Fungu la Kumi Au Zaka Sadaka ya Ajabu Kuliko Zote..Usipoitoa Kwa Hiyari Utakutoka Kwa Lazima...

$
0
0

Shalom watu wa Mungu!

Mtumishi mmoja kaandika hapa juu ya zaka: unaweza usimuelewe sana ama usimpende, lakini ana ujumbe wa muhimu...Soma Hapa;

SADAKA YA AJABU KULIKO ZOTE:-

Kuna sadaka inaitwa Fungu la kumi (Zaka/Tithe) ambayo unatakiwa kutoa asilimia 10 ya mapato yako yote. Sadaka hii umaajabu wake uko hapa:- usipoitoa kwa HIARI itakutoka kwa LAZIMA.

KIMSINGI....

Hii sadaka unapoitoa inafanya kazi kubwa mbili:-

1). Inalinda na kuhifadhi usalama wa mambo yako yote:- (biashara yako, afya yako, ndoa yako, watoto wako, afya za wanaokutegemea, usalama wa mali zako n.k)

2). Inafungua madirisha ya baraka:- (yaani unakuwa na ideas nyingi useful, unakuwa na uwezo wa kubuni na kutekeleza, unakuwa na nguvu ya pekee kufanya kazi, unakuwa na maono, unakuwa na kibali kwa kila ulifanyalo). [MALAKI 3:8-12]

CHA AJABU....

Kwa kuwa kazi ya sadaka hii ni kukulinda, usipoitoa kwa hiari tena kiukamilifu, maana yake ni kwamba ule ulinzi unakuwa haupo. Ndio utashangaa umeuchuna kutoa hilo fungu la kumi let say elfu themanini (katika laki nane unayolipwa), halafu unapigiwa simu kwamba mzazi anaumwa kijijini na unakwenda kutumia laki mbili!

Ama ndio ile unagoma kutoa fungu la kumi then unashangaa kila mshahara ukitoka ama kila ukishika fedha, matatizo yanaongozana msururu, kufumba na kufumbua unakuta hela zimeisha bila hata kujielewa elewa! Kama una tatizo katika ndoa yako, kabla hujaomba ama kuombewa hebu kagua ikiwa unatoaga fungu la kumi kiuaminifu.

Huwezi kuacha kutoa fungu la kumi kwa uaminifu halafu uchumi wako ukabaki salama. Huwezi ukaacha kutoa fungu ka kumi halafu uwe na garantii ya kwamba ndoa yako itakuwa ni, "heat free marriage", "stress free marriage", ama "Haeaven on Earth" marriage. Haiwezekani!

Na kama huwa hutoi fungu la kumi na unadhani kuwa uko salama, huenda hujajua kwamba kutotoa kwako ndio kunasababisha mambo yako yawe magumu kifedha ama yawe yanaenda kwa jasho jingi sana. Kama unatoa fungu la kumi kiuaminifu hutakiwi kuwemo katika orodha ya wanaopambana na joto la fedha kuwa ngumu mtaani. Nakuona unajitetea moyoni kutokana na kutotoa kwako. Pleaseee hebu jaribu kuitoa hii sadaka kwa uaminifu ujionee inavyothibitisha kile anachosema Mungu kuhusu sadaka hii.

HALAFU...

Huo unaoufanya ni utoto ujue! Yaani Mungu anakupa milioni moja unakuwa mchoyo kumpa laki moja?!!?!!? Hivi unajua kwamba Mungu hafanyagi madili makubwa/ya maana na watoto? Unajichelewesha na kujiangamiza ujue?

Hakuna maombi wala matamko ya kinabii yatakayokufanikisha kiuchumi, kindoa, kiuzazi, kikazi ikiwa hautoi fungu la kumi kwa bidii, kwa furaha na uaminifu. Hata kama unatafuta mtoto, mume, ajira (n.k) unapoendelea na maombi ama kuombewa tafadhali zingatia sana fungu la kumi. Sadaka zote unazotoa zinaanza kuwa na maana ukishakuwa umemalizana na Mungu katika kipengele cha fungu la kumi.

Na kama hutoagi fungu la kumi wala hata usijichoshe kumuomba Mungu kwamba akubariki kiuchumi. Tena uelewe kwamba suala sio kiwango, suala ni moyo. Kama unaona ni ngumu kutoa fungu la kumi katika laki moja unayopata sasa, usifikiri ukishika milioni utaweza kutoa, kinachokuzuia sasa na laki moja ndicho kitakuzuia mbeleni na milioni kumi.

USISAHAU...

Mimi sikuelezi habari nilizozisoma ama kujifunza tu, hapana! Ninakueleza uzoefu halisia kutoka katika maisha yangu. Ninarekodi ya majanga na misala iliyonipata kwa kupuuza fungu la kumi ama kutotoa kwa uaminifu na ninazifahamu baraka za kuzingatia fungu la kumi kwa uaminifu. Nilishaweka agano na Mungu ya kwamba sitakaa nicheze na habari ya fungu la kumi, maana kibano chake sio cha hapa! Kama unabisha, shauri yako, endelea kuhanya hanya hivo hivo!

Baraka The Prince Amkana Katu Katu Ali Kiba......

$
0
0

Msanii Baraka The Prince ambaye yupo chini ya usimamizi wa kampuni ya RockStar4000 amefunguka na kusema kuwa yeye ni msanii aliye chini ya usimamizi wa RockStar4000 na si msanii aliye chini ya Alikiba.


Baraka The Prince amesema hayo kupitia kipindi cha 5 Selekt na kusema yeye anatambua kuwa Alikiba sasa amekuwa Director wa kampuni hiyo na anaamini anaweza kufanya vizuri lakini yeye hana taarifa zozote juu ya mchongo huo ambao ameupata Alikiba kwenye uongozii wake huo.

"Mimi sitaki sana kuzungumzia sana juu ya Alikiba kuwa Director wa RockStar4000 kwani kipindi ambacho yeye anaingia mikataba mimi nilikuwa Nairobi na wao walikuwa Afrika Kusini na sijapata nafasi kusikia chochote hivyo kwa sasa bado sijui vizuri hilo jambo, siwezi kulizungumzia japo nafahamu maana naweza kuzungumzia nikazungumza nikasema jambo lisilo la kweli. Ila nimefurahi sababu Alikiba ni kaka yangu na naishi naye vizuri na najua kuwa kazi itakwenda vizuri". Amesema

Mbali na hilo Baraka The Prince alitoa ufafanuzi kuwa yeye ni msanii anayesimamiwa kazi zake na kampuni ya RockStar4000 na si kusimamiwa na Alikiba kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakidhani au wakihisi hivyo.

"Mimi ni msanii wa RockStar4000 na si msanii wa Alikiba hilo watu naomba waelewe" alisema Baraka The Prince

Kwa kumalizia Baraka The Prince alisema watu wengi wanamchukia kutokana na misimamo yake katika kazi yake ya muziki na kudai wasanii wengi wa bongo wamekuwa wakifanya kazi zao kienyeji sana ndiyo maana anapishana nao, kwani yeye anataka kazi ambayo anashiriki iweze kuwekewa mipango na iende katika viwango.

JE Una Tatizo la Nguvu za Kiume , kukosa Hamu ya Tendo, Kushindwa Kurudia Tendo au Maumbile Madogo ya Uume?

$
0
0
JE, UNA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? SOMA HAPA 👇👇👇👇
Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, sio Tanzania tu bali duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo sio ugonjwa ila ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili.

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME HUSABABISHA MAMBO KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
@Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye kisukari kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @220,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kurudia tendo hata mara 3 bila kuchoka @130,000/=
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr.

Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no (+255)
0767447444 na 0714335378

NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara kwa mtumiaji. Zimethibitishwa kiafya.

KIMENUKA...Ngeleja Abanwa Ajiuzulu Ubunge Baada ya Kurejesha Fedha za Ufisadi....Magazeti ya Leo Jumatano....

$
0
0

KIMENUKA...Ngeleja Abanwa Ajiuzulu Ubunge Baada ya Kurejesha Fedha za Ufisadi....Magazeti ya Leo Jumatano....

Zijue Huduma Saba Ambazo Unazipata Ndani ya Ndege Bila Kulipia Chochote.......

$
0
0
Jarida la Reddit liliwauliza wahudumu wa mashirika mbalimbali ya ndege kuhusu huduma zipi ambazo abiria wanaweza kuwa wanapatiwa lakini hawaziombi wawapo safarini.

Kuanzia pombe za bure mpaka dawa kama utaumwa ghafla, hivi ndio vitu nane ambavyo usisite kuomba ukiwa kwenye ndege kwa mara nyingine.

1. Chupa nzima ya soda

Wahudumu wa ndege huwa wanabania sana kutoa soda, kwa mara nyingi kukupa nusu tu ya chupa wakiichanganya na barafu ili ionekane nyingi lakini haitoshi kukata kiu. Kwahiyo mara nyingine ukifanyiwa hivi, agiza chupa nzima. Wahudumu wa ndege mara zote wanafanya utakachowaambia, na kama hawatakuwa na akiba ya kutosha, watajaza tena glasi yako.

2. Dawa na bandeji

Ingawa inategemea sana na taratibu za Shirika la Ndege husika, ndege nyingi zinakuwa na dawa za msingi kama vile za kutuliza maumivu na kutuliza kiungulia pamoja na bandeji. Hivi vyote hutolewa bure unapohitaji.

3. Chokoleti ya moto

Kama mbadala wa chai au kahawa, mashirika mengi yanakuwa na chaguo la kukupa chokoleti ya moto. Mashirika ya ndege ya Etihad, Virgin Atlantic, na Southwest Airlines ni baadhi tu ya yale yanayotia huduma hii hata kwa madaraja ya kati.

4. Pombe ya bure

Kwakuwa kimsingi nauli yako ya ndege siku hizi inajumuisha huduma zote utakazopatiwa, wengine hudhani hii inajumuisha na pombe pia. Hata hivyo, makampuni mengi ya ndege bado yanatoa pombe za bure mpaka sasa.

Kwa mfano Shirika la Ndege la Alaska bado linatoa huduma ya pombe za bure kwa baadhi ya safari zake; Shirika la Ndege la Marekani (US Airways) linatoa waini ya bure pamoja na chakula cha usiku kwa ndege zake zinazofanya safari za kimataifa; Mara nyingi hii inafanyika kwa ndege zinazofanya safari ndefu sana zinazochosha au kwa zile zinazofanya safari za kimataifa.

5. Mikoba yenye vifaa maalumu

Kwa ndege za masafa marefu, baadhi ya makampuni huweka kwenye akiba yao vitu kama vizuia sauti vya masikio, peni, chanuo za nywele na karata ambavyo utakopoomba utapatiwa mara moja. Ndege za kampuni ya Emirates ina mikoba yenye vifaa hivi ambapo wanaweka vifaa vya bure vya kunyoa, miswaki, soksi na karata kwa ajili ya kukufanya usichoke sana kwenye safari ndefu.

6. Kuongezewa vitafunwa

Vitafunwa kidogo vinavyotolewa kwa abiria kwenye ndege havitoshi na mara nyingi huwa havishibishi, vinakuacha ukiwa na njaa vile vile. Cha kufanya ni kuomba uongezewe tu — kama kuna vitakavyobakia baada ya abiria wote kuhudumiwa, wahudumu wa ndege mara zote huwa wanakuongezea kwa furaha kabisa ili mteja wao uridhike.

7. Kuangalia chumba cha marubani

Kwa kawaida chumba cha marubani kwenye ndege huwa kinafungwa muda wote na muda pekee wa abiria kumsikia rubani wenu ni mwanzo wa safari, mwisho wa safari au ikitokea hitilafu ya kiufundi au hali ya hewa ikiwa mbaya mnapokuwa angani. Lakini kama ukiwa unataka uone jinsi chumba hiki kilivyo, muombe mhudumu wa ndege na yeye ataomba ruhusa kwa rubani ili uweze kwenda kuangalia mitambo ya kuongozea ndege ilivyo kwenye chumba hicho maalumu.

Pongezi Kubwa Ziwaendee TRA Kwa Kufanikisha Jambo Hili Chini ya Uongozi wa JPM...

$
0
0
Mamlaka ya Mapato Tanzania imefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi Trilioni 14.4 kwa mwaka wa fedha 2016/17.

Makusanyo haya ni sawa na ukuaji wa asilimia 7.67 ikilinganishwa na makusanyo ya mwaka 2015/16 ambayo yalikuwa ni kiasi cha Shilingi Trilioni 13.3.

Sambamba na Makusanyo, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa kodi TRA Bw. Richard Kayombo alisema Mamlaka imeendelea kukusanya kodi mbalimbali ikiwemo kodi ya majengo na muitikio wake umekuwa ni wa kiwango cha kuridhisha.

Mamlaka inapenda kuwashukuru walipakodi wote kwa muitikio huo na wengine wanaoendelea kujitokeza katika ofisi mbalimbali za Mamlaka nchi nzima ili kuweza kulipa kodi hiyo ambayo mwisho wa kulipa kodi hiyo ni tarehe 15 Julai, 2017.

Aidha, Mamlaka inapenda kutoa wito kwa wafanyabiashara wote kutoa risiti za EFD pindi wanapouza bidhaa au huduma na Wananchi wote kuhakikisha wanadai risiti pindi wanaponunua bidhaa au kupata huduma na kuwa, kinyume na hapo watakuwa wanatenda kosa kwa mujibu wa sheria ya usimamizi wa kodi.

Hivi sasa kuna zoezi la uhamasishaji na ukaguzi linaloendelea nchi nzima katika sehemu zote za biashara kukagua wafanyabiashara wasiotumia Mashine za Risiti za Kielektroniki za EFDs pamoja na wananchi wote wasiodai risiti baada ya kununua bidhaa au huduma.

 “Napenda kuwakumbusha wananchi wote kuhakiki risiti zao ili kuona usahihi wa tarehe na kiasi walicholipa kabla ya kuondoka na risiti hiyo” alisistiza Kayombo

 ‘Pamoja Tunajenga Taifa Letu’

Richard Kayombo

Sakata la Simba Kumnyima Kibali cha Kuondoka Mchezaji Abdi Banda Lafika Pabaya....Simba Wadai Hawafanyi Kazi Kwa Shinikizo la Mtu

$
0
0
Klabu ya Simba inapenda kutoa ufafanuzi kuhusiana na malalamiko ya mchezaji Abdi Banda ambae alilalalamika jana kupitia vyombo vya habari,kuwa klabu imemkatalia kumpa barua ya kumuacha (REALESE LETTER) ilhali yeye amepata Timu huko Afrika kusini na huku akiwa amemaliza mkataba wake.

Ni kweli Banda amemaliza Mkataba na klabu, na jana alikuja ofisini kwetu kutaka barua hiyo, lakini akakumbushwa kuwa,ukiwa umemaliza Mkataba haupaswi kupewa barua hiyo,wanaoandikiwa barua hiyo ni waajiriwa ambao bado wana mikataba na labda kwa sababu yoyote ile,klabu inaamua kuachana nao.

Lakini kwa kuwa Banda aliitaka hyo barua, akaambiwe aandike barua fupi tu ya kuomba Realese Letter, ili ibaki kumbukumbu kwa klabu, lakini kwa mshangao wa maafisa wa klabu aligoma kuiandikia barua klabu na kuamua kukimbilia kwenye vyombo vya habari na Blogs.

Klabu imesikitishwa sana na kitendo hicho kinachojirudia cha kutafuta huruma kupitia Media,huku akijua kuwa anaikosea heshima klabu na kuipaka matope bila sababu.

Simba inaamini sana utamaduni wake wa miaka mingi wa kuwaruhusu wachezaji wake kwenda nje ya nchi kucheza soka, pindi wapatapo nafasi hiyo,lakini inasisitiza sana suala la utaratibu,haijawahi kutokea kokote duniani,mchezaji aliyemaliza mkataba kudai Realise letter,na kiukweli tumeshangazwa pia na baadhi ya vyombo vya habari kulishupalia jambo hili bila hata kutusikiliza (kubalance story).

Na kwa kupitia barua hii, klabu inawaambia haitafanya kazi kwa shinikizo la mtu au chombo chochote kile huku tukifahamu ni kinyume na utaratibu na utamaduni wa mchezo huu unaopendwa duniani kote

Natafuta Mume wa Mtu...Nimechoka Kuhangaika na Masharobaro Kwani ni Kero tu....

$
0
0

Nimechoka kuhangaika na masharobaro kwani ni kero tu

1. Hawajui kujali
2. Hawajui mapenzi
3. wanapenda kutunzwa na kupewa hela


Nataka mume wa mtu mwenye uwezo wake na pia anaependa familia yake na kuijali sitaki jitu lakuja kuniletea malaana mimi.

Kama uko serious wacha email hapo chini nitakutafuta mwenyewe tuanze mchakato.
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live




Latest Images