Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104747 articles
Browse latest View live

Arusha Kunani?? Kiongozi Mwingine wa CHADEMA Ajivua Uanachama na Kuhamia CCM Leo...Wengine Kufuata!!

$
0
0
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa FFU kata ya Muriet jijini ndugu Anacletus Edward Arusha ameamua kuachia uwenyekiti na kujivua uanachama wa CHADEMA na kuhamia CCM.

Huu ni muendelezo wa viongozi wa CHADEMA kuachana na Chama hicho na kuamua kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli katika kupambana na ufisadi, kusimamia maendeleo na Rasilimali za nchi huku CHADEMA ikionekana kukinzana na kila jambo jema kwa maslahi ya nchi.

Tetesi kutoka Arusha zinaeleza kuwa bado kunatarajiwa wimbi kubwa la viongozi wa CHADEMA kuachia ngazi.

Mbunge Joseph Msukuma (CCM) Aonyesha Mahaba Niue Kwa Rais Magufuli...Adai yupo Radhi Kufanya Kazi Bure

$
0
0
Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Msukuma (CCM) amemtaka Rais Magufuli kutosikiliza kelele za baadhi ya viongozi hususani wapinzani na kusema anapaswa kushikilia hapo hapo aliposhikilia kwani anafanya vizuri na mambo anayotenda yameanza kuonekana.

Msukuma alisema hayo juzi wakati wa makabidhiano ya nyumba 50 zilizojengwa na taasisi ya The Benjamin William Mkapa Foundation (BMF) na kusema wao Geita wapo mstari wambele kuhakikisha wanaunga mkono kila jambo ambalo linafanywa na Rais Magufuli.

"Mhe. Rais sisi huku Geita tunakuunga mkono na tupo tayari kujitolea hata bure katika mambo unayofanya katika nchi hii, nakuomba tu usisikilize zile kelele za watubali wewe fanya kazi kwa ajili ya Watanzania, maana kuna watu wengine wanasimama bungeni na kuanza kupiga kelele tu, wengine wanasimama bungeni na kusema eti unajenga uwanja wa ndege Chato, usiwasikilize na wala kelele zao zisikukatishe tamaa, ukiona kitu kingine kizuri chochote usiusahau mkoa wa Geita" alisisitiza Msukuma

Mbali na hilo Msukuma alikuwa na ombi kwa Rais Magufuli pindi wawekezaji waliokuwa wakisafirisha makinikia kwenda nje ya nchi wakilipa deni hilo basi awakumbuke watuwa Geita japo kwa barabara za lami kwani barabara anadai zimekuwa hazina kiwango kizuri na ni mbovu.

"Sahizi ukizinguka sehemu ukisema tumetoka Geita kidogo tunakuwa na heshima kwa ajili yako Rais Magufuli, tunakuomba uendelee hivyo hivyo ombi letu watu wa Geita, mgodi huu hatufadiki nao, kwa kuwa tulipitisha asilimia 6 tunaomba asilimia 1 tubaki nayo, lakini ombi letu la pili tumekusikia mara nyingi unasema wawekezaji wakubwa wamekuwa na maeneo makubwa maeka na maeka, tunaomba vijana wako waruhusu wawekezaji wapunguze maeneo ili vijana wachimbaji wadogo wakachimbe madini," alimalizia Msukuma

Mbali na hilo Rais Magufuli alimsifu sana mbunge msukuma na kusema hata bungeni huwa anamsikia anasimamia sana chama chake (CCM) na kusema kuwa yupo vizuri sana kwa jambo hilo, kwani anawakilisha vizuri sana.

Ukweli Mchungu....Wanawake 556 Kati 1000 Hufariki kwa Uzazi..Sababu Hizi Hapa

$
0
0
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Aga Khan, Eunice Pallangyo amefanya utafiti katika wilaya ya Ilala na kubaini kwamba vifo vya akinamama wilayani humo husababishwa na mambo mbalimbali, ikiwamo kutokuwepo huduma ya uangalizi baada ya kujifungua.

Akizungumzia utafiti huo leo , Dk Pallangyo amesema amebaini hayo, baada ya kutembelea vituo vya afya na hospitali 27 za wilaya hiyo na kuwa  huduma hiyo haitolewi ipasavyo licha ya mwongozo wa wizara ya afya kuagiza hivyo.

Dk Pallangyo amesema takwimu za wizara zinaonyesha kwamba wanawake 556 kati 1000 hufariki kwa sababu ya matatizo wakati wa kujifungua
“Wanawake huondoka hospitali saa chache baada ya kujifungua bila kufanyiwa uchunguzi wa mara kwa mara,” alisema Pallangyo
Mbali na hilo Pallangyo amedai mwongozo wa wizara unataka mwanamke aliyejifungua kuchunguzwa mara kwa mara katika kipindi cha siku 42 za mwanzo. Amesema watoa huduma aliozungumza nao wamesema hawatoi huduma hiyo kwa sababu ya upungufu wa wafanyakazi na ufinyu wa nafasi katika vituo vya afya.

Hata wazazi waliohojiwa wengi walionyesha kutokuwa na elimu sahihi ya masuala ya uzazi. "Kwa hiyo serikali imeweka miongozo ambayo watendaji wake hawaitekelezi kwa sababu ya changamoto zilizopo."Alidai Pallangyo

VIDEO: Tazama Jinsi Timu ya Everton ilivyowasili Tanzania Akiwemo Wayne Rooney

$
0
0
Klabu ya Everton tayari imewasili Jijini Dar es Salam dakika chache zilizopita ikiwa inatokea nchini Uingereza huku ikiwakosa wachezaji wake watatu muhimu katika kikosi hicho kutokana na majeruhi waliyokuwa nayo.

Waziri mwenye dhamana ya Michezo Dk harrison Mwakyembe akisalimiana na Wayne Rooney.
Pamoja na hayo, timu ya Everton imeongozwa na mchezaji nyota Wayne Rooney pamoja na Davy Klaassen na Michael Keane ambao pia wamejiunga na klabu hivi karibuni.

Kikosi kamili cha Everton kilichotua leo ni Maarten Stekelenburg, Mateusz Hewelt, Chris Renshaw, Tom Davies, Phil Jagielka, Ashley Williams, Callum Connolly, Jonjoe Kenny, Michael Keane, Muhamed Besic, Leighton Baines, Morgan Schneiderlin, James McCarthy, Davy Klaassen.


Nafasi za Ajira 105 Zilizotangazwa na Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS)

Kutana na Maalim Fadhil Rashid Kutoka Komoro ni Mtaalam wa Tiba za Asili......

$
0
0
KUTANA NA MAALIM FADHIL RASHID KUTOKA KOMORO NI MTAALAM WA TIBA ZA ASILI

UNASHIDA NA MCHUMBA UNATATIZO PESA HAIKAI KURUDISHA MUME AU MKE KWA MUDA MFUPI MVUTO WA MAPENZI

MVUTO WA BIASHARA KUMSHIKA MUME AU MKE ASIKUSUMBUE

DAWA YA ( LIMBWATA )KUMTAWALA MPENZI WAKO KWA SABABU MAALUM KUSAFISHA NYOTA ILI UWE NA MUONEKANO

NA PIA ANATOA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA PESA BILA MASHARTI

NA KUMILIKI MALI DAWA YA KUONGEZA UUME SAIZ UIPENDAYO

DAWA YA NGUVU ZA KIUME INAPATIKANA PIA ANAYO DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEP KUA NA UMBO BOMBA UMEIBIWA AU KUDHURUMIWA UTARUDISHIWA MALI YAKO NDANI YA MASAA 24 ANAFUNGA KESI NA KUPATA HAKI YAKO DAWA YA MVUTO WA BIASHARA KUUZA MALI YAKO KWA HARAKA KUZUIA CHUMA ULETE

NA KUONDOA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI ACHA KUTESEKA ACHA KUHANGAIKA MAALIM FADHIL RASHID

YUPO TANZANIA KWA AJIALI YAKO. CALL...
+255719362806/
+255763276239/

WhatsApp IMO +255785786436/

Kortini Kwa Kugonga Twiga wa Milioni 33/-

$
0
0
DEREVA wa basi la abiria la AM Coach, Andrea Jafari (42) amefi kishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Mlele mkoani Katavi kwa kosa la kuumua twiga anayekadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya Sh milioni 33 baada ya kumgonga kwa uzembe.

Mshtakiwa huyo ambaye ni mkazi wa mkoani Tabora alifikishwa jana mbele ya Hakimu wa wilaya hiyo, Teotimus Swai ambako alikana kosa hilo hivyo hakimu aliamuru arudishwe rumande hadi Julai 14, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

Jafari amerejeshwa rumande baada ya kushindwa kukidhi vigezo vya dhamana ambavyo vilimtaka aache mahakamani hapo nusu ya thamani ya twiga aliyetuhumiwa kumuua ambayo ni zaidi ya Sh milioni 16.5, na pia awe na hati ya mali isiyohamishika ambayo imethibitishwa na mtathmini yenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 16.5.

Aidha, mahakama hiyo ilimwamuru asalimishe hati zake za kusafiria na endapo akikidhi vigezo hivyo vya dhamana, asitoke nje ya Wilaya ya Mlele bila idhini ya mahakama. Kwa mujibu wa hakimu Swai, mshitakiwa huyo anashtakiwa kwa mujibu wa Kifungu cha Sheria Namba 148, (5) (b) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai sura ya 20 kama iliyofanyiwa Marekebisho 2002, pia kifungu cha 146 cha sheria hiyo.

Awali Mwendesha Mashtaka, Mkaguzi wa Polisi, Baraka Hongori alidai mahakamani hapo kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo Aprili 18, 2017 saa mbili asubuhi ambako akiendesha basi la abiria akiwa katika mwendo wa kasi, alimgonga twiga katika miinuko ya milima ya Kanono iliyopo katika Pori la Hifadhi la Rukwa – Lukwati wilayani Mlele. Alidai mshtakiwa huyo baada ya kumgonga na kumuua twiga huyo, alikimbia kusikojulikana hadi Julai 8, mwaka huu alipokamatwa mkoani Tabora na kurejeshwa Mlele.

Habarileo

Shadrack Nsajigwa Apewa Ulaji Yanga.......

$
0
0
Nahodha na mchezaji wa zamani wa Yanga, Shadrack Nsajigwa, rasmi ni kocha msaidizi wa timu hiyo.

Nsajigwa aliyekuwa anaifundisha timu ya vijana ya U20 anakuwa kocha wa timu hiyo akichukua nafasi ya Juma Mwambusi aliyekuwa anakinoa kikosi hicho.

Yanga inaachana na Mwambusi baada ya mkataba wa kuendelea kuifundisha timu hiyo kumalizika mwishoni mwa msimu uliopita wa Ligi Kuu Bara.

Nsajigwa alikuwa kwenye mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika asubuhi kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, jana.

Nsajigwa alionekana akitoa baadhi ya maelekezo kwa wachezaji wa timu hiyo akisaidiana na kocha wa viungo wa timu hiyo, Mzambia, Noel Mwandila.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo gazeti hili limezipata, kabla ya mazoezi hayo kuanza Nsajigwa alitambulishwa kwa wachezaji wa timu hiyo.

“Nsajigwa rasmi ni kocha msaidizi wa Yanga atakayekuwa anasaidiana na Lwandamina, Mwandila na Mwambusi hatakuwepo na timu hiyo tena,” alisema mtoa taarifa huyo.

Baada ya mazoezi hayo kumalizika, Nsajigwa alipoulizwa ili kuthibitisha hilo, akasema: “Mimi sina taarifa rasmi juu ya hilo suala la kuwa kocha msaidizi, tusubirie kwanza kama ikiwa hivyo basi nitatoa taarifa rasmi.”

Eti Anasema Ana Mimba Yangu !..Wataalam Nisaidieni Pliz

$
0
0
Ni kweli nilifanya nae mapenzi siku ya 6 tangu kuanza bleeding,leo ananiambia ujauzito wangu,nimemtoa nduki kwanza....nifanye utafiti kwanza kama inawezekana.....

Eti wadau,siku ya 6 inawezekana kweli?? kwa elimu yangu ya baiolojia kwa vidato sita,,,,,sioni uwezekano kwa kweli....nahisi nataka kubambikiwa mzigo hapa...

Kwa wataalamu wanaofahamu zaidi kuhusu huu utaratibu naomba wanisaidie ufahamu...

Jumba Lazidi Kumwangukia Mbunge Halima Mdee...Hichi Hapa Kibano Kingine Kinachomkabila

$
0
0
Siku moja baada ya Mbunge wa Kawe Halima Mdee kuachiwa kwa dhamana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah, amesema Mdee, atafikishwa mbele ya Kamati ya Maadili ya bunge, pindi utaratibu utakapokamilika.

Mdee alikamatwa Julai 4 kwa amri ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi akidaiwa kutoa lugha ya kumkashifu Rais John Magufuli. Hapi aliagiza Mdee awekwe mahabusu kwa saa 48 lakini alikaa siku sita.

Juzi Mbunge huyo aliachiwa kwa dhamana mahakamani hapo baada ya kutimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili waliosaini hati yenye thamani ya Sh10 milioni na yeye mwenyewe. Alisomewa shitaka moja ya kumkashifu Rais.

Baada ya kuachiwa kwa mbunge huyo jana, Mwananchi Digital lilihitaji kufahamu ni lini mbunge huyo atafikishwa mbele ya kamati ya maadili ya bunge kama agizo la Spika lilivyotaka.

Dk Kashilila amesema alikuwa hafahamu kama mbunge huyo ameachiwa kwa dhamana lakini muda utakapofika na ratiba ikapangwa kamati itayatekeleza yale maagizo ya Spika.

“Sidhani kama nina sababu ya kukuambia mimi jambo ambalo hata kamati yenyewe bado haijakutana kufanya hiyo kazi, kamati itakapokutana sisi tutatoa hiyo taarifa,” amesema Kashililah.

Baada ya kupiga simu ya Mdee kwa muda mrefu bila kupokewa tulizungumza na Katibu wa Chadema wa Mkoa, Henry Kilewo juu ya suala hilo na kusema ingawa taarifa ya Spika ilitolewa mbele ya wabunge lakini Mbunge huyo hawezi kufika mbele ya kamati ya maadili hadi taratibu zitakapofuatwa.

“Kuna taratibu za kibunge zinazotakiwa kufuatwa endapo unamuhitaji mtu kufika mbele ya kamati yoyote. Kwa kawaida hutumiwa wito unaoonyesha ni lini anahitajika ili aweze kusikiliza alichoitiwa,” amesema Kilewo.

Kifo cha Bikira wa Kisukuma Kimegusa Wengi...Zamaradi Mketema Afunguka Mazito.....

$
0
0
Ikiwa bado Watanzania wapo kwenye majonzi mazito ya kuondokewa na Mtangazaji wa Kituo cha Radio EFM, Seth Katende maarufu kwa jina la Bikira wa Kisukuma aliyefariki dunia Jumapili ya Julai 9, 2017, watu maarufu nchini wakiwemo wasanii na watangazaji wameonyesha hisia za kuguswa na msiba huo.

Miongoni mwao, yupo mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha Clouds Tv, Zamaradi Mketema ambapo kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram ameandika ujumbe ambao umegusa mioyo ya watu wengi na kuamsha simanzi kwa mashabiki wa Bikira wa Kisukuma, ujumbe wenyewe unasomeka hivi:

“Kuna WENGI lakini MUNGU ameamua kukuchukua wewe kwanza, AMEKUCHAGUA WEWE KWA SABABU, kupitia wale tunaowaamini na kuona kitu ndani yao MUNGU huamua kuonesha UKUBWA na utukufu wake, kupitia WEWE MUNGU ametuonesha ufalme wake, MUNGU ametukumbusha kuwa tunarudi kwake, MUNGU anataka tujue DUNIA NI YAKE, pamoja na sababu nyingi za kibinaadamu zinazoweza kutuonesha ulistahili kupewa muda kidogo lakini bado amekuchukua, AMEFANYA MAAMUZI MAGUMU, hakutaka kuangalia hata mtoto wako mdogo aliekuwa bado akikuhitaji, yeye haangalii hayo, na hili ni funzo kwetu, haangalia ni nani una nini ama una kipi hujatimiza, ikifika siku akikuita utaitika tu sababu lazima Dunia iendelee, leo umeondoka wewe kesho hatujui ni ya nani, MUNGU AMETENDA!! Safari yako umeimaliza Seth.

Kupitia mitandao nilianza kukujua kabla hatujafahamiana, na ni kutokana na kile alichokubariki nacho MUNGU, Na kama nilivyokujua kuna wengi uliweza kugusa maisha yao kwa namna moja ama nyingine, na hiyo ikakufanya ujulikane ndani ya muda mfupi, ulikuwa na NDOTO nyingi, ulikuwa na mipango mingi, na zaidi hata juhudi katika kufukuza ndoto zako, lakini MUNGU HAKUTAKA ZITIMIE, Leo UMELALA ukiwa hujatimiza nusu ya ndoto zako labda, huenda ulijua kesho itakuwepo utaamka, utapigana tena lakini MUNGU akasema hapana, muda umefika, na hata ungefanikiwa kuzitimiza leo pia bado nawaza na kujiuliza ukiwa umelala zingekusaidia vipi huko uendako ambako hakuna anaepajua kati yetu panafananaje, tukumbuke kuna KESHO, na kuitengeneza ni matendo yetu na kufata Dini zetu zinavyotaka, Dunia sio rafiki, na maamuzi ni yetu bado kuamua kuibeba au kuidharau.

Instagram imetikisika leo, na hiyo inaonesha ulikuwa ni nani na ulikuwa na mchango mkubwa kiasi gani, Seth Umeniumiza lakini umenifundisha kitu kikubwa sana, Kapumzike kaka.
.ALLAHU AKBAR!!

Hatma ya IPTL Ipo Mikononi Mwa JPM....Zimebaki Siku Mbili

$
0
0
ZIKIWA zimebaki siku mbili kufika Julai 15 ambao ndio ukomo wa leseni ya Kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), imeelezwa kuwa hatima yake sasa ipo mikononi mwa Ikulu.

Wakati Ikulu ikisubiriwa kuijibu wizara husika, endapo Julai 15 itapita bila IPTL kuongezwa muda wa leseni yake, haitaweza kuendelea tena na uzalishaji wa nishati hiyo.

Juni 11, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, alimsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Felix Ngamlagosi, ikiwa ni siku chache tangu mamlaka hiyo itoe taarifa kwa umma ya kuanza kukusanya maoni baada ya ombi la IPTL la kuongezewa leseni ya uzalishaji umeme kwa miezi 55.

Mara baada ya taarifa ya kusimamishwa kazi kwa Ngamlagosi iliyohusishwa na hatua ya Ewura kutoa tangazo kwa umma kuutarifu juu ya kutoa maoni yao kufuatia ombi la IPTL kuongezewa muda wa leseni yao ya uzalishaji umeme, mamlaka hiyo ilitoa taarifa nyingine kwa umma ikitaarufu kusimamisha ukusanyaji huo wa maoni.

“Taarifa inatolewa kwa umma kwamba kufuatia maombi ya kampuni ya uzalishaji umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) (“Mwombaji”)
kuomba kuongezewa muda wa leseni yake ya kuzalisha umeme kwa kipindi cha miezi 55 kutokea tarehe 15 Julai 2017.

“Ewura zaidi ya hatua nyingine za kiudhibiti, iliwasiliana na Wizara ya Nishati na Madini ili kupata maoni yake kwa mujibu wa kifungu cha 7 (3) cha Sheria ya Ewura, sura ya 414 ya sheria za Tanzania.

“Wizara ya Nishati na Madini imetoa mapendekezo ya kuwapo na mashauriano zaidi kati ya Wizara, Ewura na wadau mbalimbali wa sekta ndogo ya umeme kabla ya kuendelea na mchakato wa maombi ya mwombaji.

“Kutokana na maoni hayo, Ewura inasitisha mchakato wa kushughulikia maombi ya leseni ya mwombaji ikiwa ni pamoja na upokeaji wa maoni/mapingamizi dhidi ya maombi hayo mpaka hapo yatakapotolewa maelekezo mengine,” ilisema taarifa hiyo.

Jana Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa Ewura, Titus Kaguo, alipotafutwa na gazeti hili ili kuzungumzia hatima ya IPTL, alisema mashauriano na Serikali bado yanaendelea na ikifika Julai 15 ataweza kuwa na jambo la kusema.
“Kwenye tangazo letu tulisema mashauriano na Serikali yanaendelea na wadau wengine yanaendelea, kwa hiyo kwa sasa siwezi kusema kitu ila subiri hiyo Julai 15 nitakuwa na cha kusema,” alisema Kaguo.

MTANZANIA pia ilimtafuta Kamishina wa Nishati, Innocent Luoga, ili kujua mazungumzo ya suala hilo yalipofikia.
“Natamani kama ningeweza kukujibu, lakini suala hili msemaji wake ni Katibu Mkuu ambaye hayupo, lakini tu nikwambie ukweli kwamba kwa sasa lipo kwa Katibu Mkuu Kiongozi, kwa hiyo siwezi kusema chochote,” alisema Luoga.
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa, alipotafutwa ili kuthibitisha kama kweli suala hilo limefika mezani kwa Katibu Mkuu Kiongozi, alisema: “Hili suala ni la Wizara ya Nishati, kama wamewaambia kuwa wamelipeleka kwa Katibu Mkuu Kiongozi, basi watakachojibiwa watawaeleza.”

Kwa upande wao, Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) walipoulizwa baada ya leseni ya IPTL inayozalisha umeme megawati 110 (MW) kwa kutumia mafuata mazito itakapofika kikomo Julai 15 ni hatua gani itafuata, walisema hawawezi kusema lolote kwa sasa.

“Kwa sasa siwezi kuzungumza chochote juu ya suala hilo,” alisema msemaji wa shirika hilo, Leila Muhaji.
Makubaliano ya kuuziana umeme (Purchase Agreement-PPA) kati ya IPTL na Tanesco, yalisainiwa mwaka 1995 kwa miaka 20, huku leseni ya sasa ya IPTL ikiwa imetolewa na Wizara ya Nishati na Madini mwaka 1996 kwa kipindi cha miaka 21.

CHIMBUKO LA IPTL

Chimbuko la IPTL ni uhaba wa umeme mwaka 1994, ilipoonekana kuna uhitaji wa kuwa na umeme wa dharura.

Agosti 19, 2014, Mkurugenzi wa Kampuni ya Mechmar, iliyokuwa ikimiliki asilimia 70 ya hisa za IPTL, Datuk Baharuden Majid, aliongoza ujumbe kutoka Malaysia kuja kuzungumza na Serikali ya Tanzania.

Septemba 1994, Mkataba wa Maelewano (MOU) ulifikiwa, licha ya tahadhari kutoka kwa washauri wa Tanesco ambao ni kampuni za Acres (Canada) na Hunton and Williams (Uingereza), kwamba uwekezaji huo ulikuwa ni janga kwa sekta ya umeme na kwa uchumi wa taifa.

Kampuni hiyo ambayo wamiliki wake ni Mechmar ya Malaysia mwenye asilimia 70 na VIP ya Tanzania yenye asilimia 30 ilisaini mkataba wa miaka 20 (1995-2015) na Serikali ya Tanzania.

7.92 kwa mwezi kama ada ya huduma za mtambo. Mwaka 2002 IPTL ikaanza kuiuzia umeme Tanesco, lakini ilipofika 2004 ikabainika kuwa ilidanganya kuhusu mtaji.

Awali IPTL ilisema asilimia 30 ya mtaji ilikuwa nao sawa na Dola milioni 36 na kwamba asilimia 70 ilikopa.
Baada ya ukaguzi ikabainika IPTL haikuweka dola milioni 36 kama mtaji, bali iliweka dola 50 ambazo kwa wakati huo zilikuwa sawa na Sh 50,000.

Kutokana na kasoro hiyo, Tanesco ikataka gharama ya umeme ishuke.
Mabishano yakaendelea hadi mwaka 2006, ikaamuliwa kufunguliwa kwa akaunti maalumu (Tegeta Escrow) ili Tanesco iwe inaweka huko fedha hadi pale mwafaka utakapopatikana.

Mwaka 2008, IPTL ilishindwa kujiendesha, hivyo ikawekwa chini ya usimamizi wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA).
Hukumu ya Mahakama Kuu iliyotoka Septemba 2013 chini ya Jaji John Utamwa, iliamua IPTL iondolewe chini ya usimamizi wa Rita na mali zake zote ipewe Kampuni ya Pan Africa Power Solutions Ltd (PAP) ya Harbinder Singh Sethi.

Hukumu hiyo ilitoka huku mmiliki wa asilimia 70 ya IPTL (Mechmar) akiwa mufilisi nchini Malaysia na zaidi ICSID kukiwa na kesi inayohusu mgogoro wa IPTL na Serikali uliofunguliwa na Standard Chartered Bank, ambayo ilinunua deni la kampuni hiyo mwaka 2005 na ikaruhusiwa kuishtaki Serikali ya Tanzania kwenye baraza hilo lenye mamlaka ya mwisho.

Februari 2014, ICSID ilifanya uamuzi wa awali kwamba ni kweli IPTL inaitoza zaidi Tanesco na kuelekeza pande mbili zikafanye hesabu upya ndani ya siku 90 zilizoisha Mei 2014 kwa lengo la kujua ni kwa kiasi gani kampuni hiyo imelipunja shirika hilo katika bei tangu 2002 hadi 2013.

Hata hivyo, Tanesco na Serikali hawakutoa ushirikiano ndani ya siku hizo 90 kutekeleza uamuzi huo.
Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuhusu ukaguzi wa Akaunti ya Tegeta Escrow na umiliki wa Kampuni ya IPTL iliyowasilishwa bungeni Novemba 2014, ilionyesha kuwa fedha zilizokuwa kwenye akaunti hiyo ni Sh bilioni 306 na zilitakiwa kurudishwa Tanesco.

Kutokuwapo kwa umakini kwa Serikali kulisababisha Kampuni ya PAP kujimilikisha fedha za IPTL kwa asilimia 70 bila kuwa na ushahidi wowote kwamba iliinunua IPTL ikiwamo malipo ya kodi kama ilivyofanya kwa VIP yenye asilimia 30 za hisa.


IPTL INAVYOINYONYA TANESCO

Moja ya taarifa za Ewura kuhusu kampuni zinazoiuzia Tanesco umeme, zinaonyesha kuwa IPTL inaiuzia kila uniti kwa Dola za Marekani senti 23.1 na kila mwezi inalipwa Capacity Charge ya Dola za Marekani 2,655,786.
Ukikokotoa kiasi hicho kwa wastani wa kila Dola moja kwa Sh 2,238, inafanya kila mwezi IPTL kulipwa Sh bilioni Sh bilioni 5.943 ambayo kwa mwaka inakuwa wastani wa Sh bilioni 71.316.

Source: Mtanzania

Makubwa!! Alietobolewa Macho na Scorpion Amtosa Mkewe na Kusepa!

$
0
0
Kumbukumbu zikiwa bado mbichi vichwani mwa watu juu ya tukio la kutobolewa macho kwa kijana Said Mrisho linalotajwa kufanywa na Salum Njwete ‘Scorpion’, mapya yameibuka yakiihusu familia hiyo kwa kile kinachoelezwa kuwa Said amemtekeleza mkewe na watoto.

Katika mahojiano Exclusive kupitia Global TV Online, mke wa Said, Stara Soud alisema kisanga hicho kinadaiwa kutokea hivi karibuni siku chache baada ya wawili hao kuhamia kwenye nyumba ya kupanga maeneo ya Majichumvi, wakitokea Mabibo-Hosteli Ubungo na likifuatiwa na varangati la aina yake ambapo soo hilo lilitinga polisi kabla ya kuamriwa kuhamia Ustawi wa Jamii.

“Baada ya kuhamia Majichumvi, siku hiyohiyo Said akaniambia anatarajia kusafiri usiku, hivyo nimuandalie nguo na mimi bila kusita wala kuwa na wasiwasi nilifanya kama alivyoniagiza, akaja akachukua nguo na kusema tena atalala kwa rafiki yake ili wadamke usiku, akaondoka lakini baadaye alinipigia simu na kuniuliza kama nilikuwa bado naweka vitu sawa na kunijulisha kuwa kuna mahali amekaa akipata chakula.

“Alipomaliza kuniambia hivyo, akadhani simu imekatika lakini bado ilikuwa hewani akawa anasema yaani huyu anadhani ninasafiri, nitamkimbia taratibu hadi tuachane kabisa, hakika niliumia na kuanza kulia kujua kumbe mume wangu ananifanyia uhuni wakati nina watoto wanne wengine wakiwa wachanga wa mwezi mmoja,” alisema Stara na kumalizia;

“Kuna nyumba ya zamani ambayo tulitaka kuhamia kabla ya huku Majichumvi na kuna baadhi nya vitu vyetu vilikuwa huko, nikampigia simu mama na hapohapo mimi na dada yangu tukaenda huko kubahatisha kama tutamkuta, kweli tulimkuta na alianza kufanya fujo akampiga mtoto na dada yangu, baadaye kesi ikahamia polisi, akiwa amenisingizia kwamba mimi na ndugu zangu tumemfanyia fujo na kumuibia shilingi milioni mbili, tukashauriana suala hilo lifike Ustawi wa Jamii ambapo kesho tutafanya hivyo,” alisema Stara.


TAZAMA VIDEO:
Source:GPL

JE Dada Unahitaji Kuwa Mrembo na Muonekano Bomba na Kaka Kuwa na Mvuto wa Kiume...Waone Hawa....

$
0
0
BLACK BEAUTY COMPANY
JE Dada unahitaji kuwa Mrembo na ule muonekano bomba wa kisuperstar👌🔥,kaka unahitaji kuwa mtanashati na mvuto zaidi wa KIUME?fika black beauty company utatimiza ndoto zako,hawakosei hata siku moja kwa products original na zenye matokeo yaharaka sana,bila madhara,ni kampuni yenye uzoefu wa hali ya juu sana🔥
1)kuongeza hips,makalio,mapaja@150000
(b)kuongeza hips,makalio,mapaja na miguu@200000/=
2)kuongeza miguu ,kuondoa vigimbi@120000/=
3)kuwa mweupe mwili mzima (Rangi moja)@150000/=
4)Kupungua mwili mzima@150000/=
5)kupunguza tumbo@100000/=
6)kupunguza au kuongeza matiti@100000/=
7)kukuza nywele@100000/=
8)kuondoa michirizi @100000
9)kuondoa madoa,mabaka na chunusi sugu@100000/=
10)kuongeza uume na nguvu za kiume@150000/=
Dawa zetu niuhakika sana100%na utaletewa popote ulipo,mikoani tunatuma,nje ya nchi tunatuma DHL,ofic zetu zipo kariakoo msimbazi police,🔥karibuni kwa mawasiliano zaidi

WASILIANA NASI

WhatsApp+255657778924,au call0743534406 



Au unaweza kutufollow INSTAGRAM
👇👇👇👇👇👇
@black_beauty_company

Diamond Platnumz Amduwaza Yemi Alade

$
0
0
Eneka ni moja kati ya nyimbo ambazo Diamond ameziachia kwa kushtukiza na mapokezi yake yameonekana kuwa makubwa tofauti na alivyotarajia. Miongoni mwa walioonekana kuikubali ngoma hiyo ni Yemi Alade.

Kitendo cha Diamond kutumia baadhi ya maneno ya lugha ya nchini Nigeria ndio kimeonekana kumfanya Yemi kuupenda zaidi wimbo huo.

Muimbaji huyo kutoka huko Nigeria, ameshindwa kuzuia hisia zake kwa wimbo huo baada ya kucomment kwenye moja ya video ambayo Diamond ameiweka kwenye mtandao wa Instagram. “Omg !you are singing in IGBO 💃💃 @diamondplatnumz,” ameandika Yemi Alade.

TAKUKURU: Kurudisha Hela Hakukuondoi Kwenye Tuhuma, Sheria Kufuata Mkondo Wake

$
0
0
JF Jana  Wali- tweet kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa au TAKUKURU kwa kifupi imesema kuwa mtu kurudisha hela aliyopewa iliyotokana na ufisadi au utakatishaji pesa hakumuondoi kwenye mashitaka.

Mnakumbuka jana Ngeleja alirudisha hela aliyopewa na Rugemalira kwa madai kwamba hakujua kuwa hela hiyo inatokana na ufisadi.


Maskini...Soka Limesababisha Gabriel Batistuta Ashindwe Kutembea......

$
0
0

Mshambuliaji wa zamani wa timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya Argentina na klabu ya Fiorentina, Gabriel Batistuta ameweka wazi kwamba kwa sasa anapata shida kutembea baada ya kucheza mpira wa miguu kwa miaka 17.

Staa huyo mwenye umri wa miaka 48 sasa alistaafu soka mwaka 2005 baada ya kucheza kwa mafanikio makubwa sana, akiifungia klabu yake ya Fiorentina magoli 168 na magoli 56 kwa timu yake ya Taifa.

Lakini amekaririwa na mtandao wa Shirikisho la Mchezo wa Soka Ulimwenguni Fifa.com kwamba “sasa anapata shida kutembea ” kwa sababu ya juhudi kubwa alizokuwa akizielekeza kujiimarisha kisoka ujanani.

“Nilikuwa nafanya kazi kubwa sana zaidi hata ya nilivyotakiwa kufanya,” amekaririwa Batistuta.

Mwaka 2014, Batistuta alisema kuwa aliwaomba madaktari wamkate miguu yake yote kwa sababu ya maumivu makali aliyokuwa akiyapata.

Hali yake ilikuwa imara kwa baada ya kufanyiwa upasuaji wa kupunguza msuguano katika mifupa na vifundo vya miguu lakini imemuacha akiwa na tabu katika kutembea.

Jinsi Historia Inavyopinga MBOWE Kuwa Mtetezi wa Wanyonge

$
0
0
Mimi ni muumini wa Historia ya ukombozi, ninafahamu dunia nzima namna nchi zilizohitaji ukombozi namna zilivyopata ukombozi na namna ya viongozi wao waliowakomboa walivyojitokeza kwenye jamii.

Mbowe ndio mfanyabiashara pekee anayejiita mtetezi wa masikini duniani, tangu nimewahi kuifahamu historia ya ukombozi,

Hakujawahi kutokea Duniani labda ahera, Masikini wakatetewa na Tajiri, Haijawahi na Jaitawahi kutokea Mfanya biashara yoyote akapanga kupata hasarfa eti kwa maslahi ya Umma, wafanya biashara wote wanawaza faida, hata mbowe anawaza faida na sasa anatafuta faida kwa gharama yoyote.

Tunamsifia Mandela leo, Mandela hakuwa mfanyabiashara, Mandela hakuwa tajiri, Mandela alichangiwa na masikini wenzake kuikomboa Arika ya Kusini, Mandela hakuwahi Kuikopesha ANC pesa ili iwaondoe Makaburuu, Mandela alifanana na jamii aliyotaka kuikomboa na Mandela alifanikiwa kuikomboa.

Wote tunamsifia Nyerere Hapa Tanzania, Nyerere Hakuwa Mfanyabiashara, mwalimu Hakuwa Tajiri, mwalimu Hakuwahi kuikopesha TANU ili kumuondoa MKOLONI, nyerere alichangiwa na masikini wenzake, aliombewa na walalhoi wenzake na alilindwa na mafukara wenzake.

Mifano ni mingi, hivyo hivyo kwa Samora Machel, Kwame Nkuruma, Milton Obote, Robert Mugabe, Kamuzu Banda, Dkt Martin Lutherking, Mahatma Gandh, Mao Zedong, AmilicaCabra na wengineo wote, KAMWE KUNGURU WASIOFANANA HAWAWEZI KURUKA PAMOJA.
Nitaendelea kuwafundisha mengi ninayoyajua kuhusu MBOWE NA CHADEMA kwa kadri itakavyowezekana.

Jamii Forums

HESLB Yavuka Lengo, yakusanya Bilioni 116

$
0
0
Zoezi la utafutaji, ufuatiliaji na ukaguzi wa wadaiwa sugu na ambao wamenufaika na mikopo ya elimu ya juu mahala pa kazi iliyoendeshwa na Bodi ya Mikopo ya Mikopo ya Elimu ya Juu katika kipindi cha mwaka mmoja, limefanikiwa kwa asilimia 46

na kupelekea makusanyo ya mikopo hiyo kuvuka lengo lililokusudiwa.
Akiongea na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, kuhusiana na hali ya makusanyo ya mikopo kwa wanufaika wa elimu ya juu, Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Bwana Abdulrazak Badru amesema walilenga kukusanya Shilingi Bilioni 76 lakini wamekusanya Shilingi Bilioni 116 ikiwa ni kiwango cha marejesho cha asilimia 46.

Bwana Badru amesema, hataacha kutumia mbinu ya ufuatiliaji mahala pa kazi huku akiwakumbusha wale ambao wanashindwa kurejesha mikopo kwa hiari sheria itafuata mkondo dhidi yao kwani fedha hizo hutumika kwa wanafunzi wa awamu mpya ya masomo.

Aidha, Bwana Badru ametoa onyo kali kwa waajiri ambao wameshindwa kuwasilisha majina ya waajiriwa wao ndani ya siku 28 kwa bodi hiyo, kuchelewesha makato baada ya kuwakata waajiriwa ama kuficha taarifa kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Imevuja: Yanga Kumsajili Erasto Nyoni

$
0
0
KIUNGO anayeweza kucheza nafasi zote za ulinzi, Erasto Edward Nyoni yuko mbioni kujiunga na mabingwa wa Tanzania, Yanga baada ya kumaliza mkataba wake Azam FC.

Nyoni yupo kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars inayojiandaa kwa mchezo na Rwanda Jumamosi Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza kuwania tiketi ya Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN), michuano inayohusisha wachezaji wanaocheza ligi za nchini mwao pekee – na Yanga wanatarajia kumalizana naye kabisa baada ya mechi hiyo.

“Mazungumzo na Nyoni yamekwenda vizuri na wakati wowote tunaweza kumalizana naye, pengine baada ya mechi tu dhidi ya Rwanda,”kimesema chanzo kutoka Yanga.

Benchi la Ufundi la Yanga, chini ya Kocha Mkuu, Mzambia George Lwandamina kwa kushirikiana na Sekretarieti chini ya Katibu Mkuu, Charles Boniface Mkwasa ambaye kitaaluma ni kocha kwa pamoja wamejiridhisha Nyoni ni mchezaji ambaye wanamuhitaji kikosini.

Na hiyo ni kwa sababu huyo ni ‘kiraka’ anayeweza kucheza nafasi yoyote ya ulinzi kuanzia kiungo wa ulinzi – lakini uzoefu na weledi wake kisoka ni vitu vingine vinavyomuunganisha na Yanga katika siku za mwishoni za maisha yake ya uwanjani.
Viewing all 104747 articles
Browse latest View live




Latest Images